Kimeidhinishwa na KICD
Longhorn
Umilisi
wa
Kiswahili
Mwongozo wa Mwalimu
Gredi ya 4
John Kobia
iii
ii
Kimeidhinishwa na KICD
Kimechapishwa na:
Longhorn Publishers PLC,
Barabara ya Funzi, Eneo la Viwandani,
S.L.P. 18033 00500,
Nairobi, Kenya.
Simu: +254 02 6532579/81, +254 02 558551,
+254 708 282 260, +254 722 204 608
Baruapepe: enquiries@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Uganda) Ltd.,
Plot 4, Barabara ya Vubyabirenge,
Eneo la Ntinda,
S.L.P. 24745,
Kampala, Uganda.
Simu: +256 414 286 093
Baruapepe: ug@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Tanzania) Ltd.,
Barabara ya Bagamoyo/Barabara ya Garden,
Mikocheni B, Plot No. MKC/MCB/81,
S.L.P. 1237,
Dar es Salaam, Tanzania.
Simu: +255 714 184 465
Baruapepe: longhorntz@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Rwanda) Ltd.,
Remera, mkabala wa Benki ya COGE,
S.L.P. 5910,
Kigali, Rwanda.
Simu: +250 784 398 098
Baruapepe: rwanda@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
© J. Kobia, 2019
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupigisha
chapa, kutafsiri au kukitoa kitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila idhini,
kwa maandishi, ya kampuni ya Longhorn Publishers PLC.
Chapa ya kwanza, 2019
Msanifu wa Jalada: Tu Mulokwa
ISBN 978 9966 64 225 7
Kimepigwa chapa na English Press Ltd., Barabara ya Enterprise,
Eneo la Viwandani, S.L.P. 30127-00100, Nairobi, Kenya
iii
ii
Kimeidhinishwa na KICD
UTANGULIZI ...................................................................................................................v
NYUMBANI......................................................................................................................1
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 4
Kusoma............................................................................................................................................. 14
Kuandika .......................................................................................................................................... 18
Saru................................................................................................................................................. 20
NIDHAMU MEZANI........................................................................................................28
Kusikiliza na kuzungumza............................................................................................................. 30
Kusoma............................................................................................................................................. 33
Kuandika .......................................................................................................................................... 36
Saru................................................................................................................................................. 39
MAVAZI ............................................................................................................................45
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 48
Kusoma............................................................................................................................................. 51
Kuandika .......................................................................................................................................... 55
Saru................................................................................................................................................. 58
DIRA..................................................................................................................................67
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 72
Kusoma............................................................................................................................................. 75
Kuandika .......................................................................................................................................... 78
Saru................................................................................................................................................. 81
USHAURI NASAHA .........................................................................................................87
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 91
Kusoma............................................................................................................................................. 93
Kuandika .......................................................................................................................................... 96
Saru................................................................................................................................................. 99
YALIYOMO
v
iv
Kimeidhinishwa na KICD
BENDERA YA TAIFA .......................................................................................................106
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 109
Kusoma............................................................................................................................................. 112
Kuandika .......................................................................................................................................... 115
Saru................................................................................................................................................. 118
MATUNDA NA MIMEA...................................................................................................128
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 131
Kusoma kwa Mapana ..................................................................................................................... 134
Kuandika .......................................................................................................................................... 137
Saru................................................................................................................................................. 140
WANYAMA WA PORINI .................................................................................................146
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 150
Kusoma............................................................................................................................................. 153
Kuandika .......................................................................................................................................... 158
Saru................................................................................................................................................. 161
AFYA BORA......................................................................................................................167
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 172
Kusoma............................................................................................................................................. 175
Kuandika .......................................................................................................................................... 179
Saru................................................................................................................................................. 182
KUKABILIANA NA UHALIFU........................................................................................186
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 191
Kusoma............................................................................................................................................. 194
Kuandika .......................................................................................................................................... 197
Saru................................................................................................................................................. 200
MAPATO ...........................................................................................................................206
Kusikiliza na Kuzungumza ............................................................................................................ 210
Kusoma............................................................................................................................................. 213
Kuandika .......................................................................................................................................... 217
Saru................................................................................................................................................. 220
v
iv
Kimeidhinishwa na KICD
Utangulizi wa mtaala wa kiumilisi
Umilisi ni uwezo wa kufahamu na kutumia maarifa, ujuzi na stadi ili kufanya shughuli
kwa mafanikio makubwa. Mtaala wa kiumilisi ni mtaala unaomlenga mwanafunzi
na utendaji wake darasani, nje ya darasa, nyumbani na katika maisha ya kila siku.
Mtaala huu unafuata mfumo wa elimu wa 2-6-3-3-3. Katika mfumo huu, wanafunzi
katika shule ya chekechea watasoma kwa miaka miwili, shule ya msingi ya awali miaka
mitatu, shule ya msingi daraja la juu, miaka mitatu, shule ya sekondari daraja la chini,
miaka mitatu, shule ya sekondari daraja la juu, miaka mitatu na angalau miaka mitatu
katika taasisi za elimu ya juu kama vile vyuo anuwai, vyuo vya kiufundi na vyuo vikuu.
Matarajio ya mtaala wa kiumilisi ni kumwezesha kila Mkenya kushirikishwa,
kuwezeshwa na kuwa mwananchi mwenye kuzingatia maadili. Mwalimu katika
mtaala wa kiumilisi ni mwezeshaji, kiongozi na mwelekezi wa mwanafunzi katika
shughuli mbalimbali za kiutendaji katika ujifunzaji wa vipengele mbalimbali vya lugha
ya Kiswahili.
Sifa bainifu za mtaala wa kiumilisi
1. Mtaala wa kiumilisi husisitiza ubora na ushindani ufaao katika shughuli
mbalimbali miongoni mwa wanafunzi.
2. Unasisitiza zaidi matumizi ya maarifa na ujuzi kupitia stadi, ubunifu, uvumbuzi
na kutatua changamoto au tatizo halisi.
3. Mwalimu humsaidia mwanafunzi kujenga na kukuza maarifa na ujuzi wake
akishirikiana na wengine kwa kuzingatia hali na mazingira yenye changamoto na
uzoefu wake.
4. Una uhuru mwingi, ufaraguzi unakubalika, uko wazi na unasaidia katika
kukubali mahitaji na uwezo tofautitofauti wa wanafunzi katika mchakato wa
ujifunzaji.
5. Hushirikisha wazazi, walezi na jamaa wengine katika ujifunzaji kupitia
uwezeshaji na huruhusu kuchangia kwa washikadau katika uwajibikaji wa
pamoja katika ngazi na viwango vyote vya elimu.
6. Hudhamiria kufungamanisha mambo muhimu ya kisasa na kujifunza shughuli
za huduma za kijamii ambayo hufungamanisha wanaojifunza darasani na hali
halisi ya maisha.
UTANGULIZI
vii
vi
Kimeidhinishwa na KICD
7. Msisitizo uko kwenye tathmini endelevu katika shughuli mbalimbali ambapo
kuna tathmini za mara kwa mara ingawa kuna tathmini tamati mwishoni kwa
kila kiwango cha elimu.
8. Husisitiza ujifunzaji unaomlenga zaidi mwanafunzi hasa kukuza umilisi wake
katika ujuzi na stadi mbalimbali.
9. Unajikita katika matumizi ya vyambo vya kidijitali ili kwenda na wakati wa
dunia ya leo ambapo sayansi na teknolojia imepewa kipaumbele katika nyanja
mbalimbali za maisha ya binadamu.
10. Husisitiza mwingiliano na mahusiano ya masomo mbalimbali ili kukuza uelewa,
maarifa na stadi za mwanafunzi.
Malengo ya elimu ya taifa
Malengo ya elimu ya taifa ni matarajio ya muda mrefu ya elimu katika nchi ya Kenya.
Kulingana na mtaala wa kiumilisi, elimu ya taifa nchini Kenya inalenga kufanikisha
malengo yafuatayo:
1. Kukuza utaifa, uzalendo na kujenga umoja wa kitaifa
Nchini Kenya, kuna jamii zenye mila, dini na tamaduni mbalimbali. Elimu ina jukumu
la kuziunganisha jamii kwa kujenga utaifa na uzalendo. Elimu inapaswa kukuza amani
na utangamano miongoni mwa watu mbalimbali.
2. Kukuza mahitaji ya kijamii, kiuchumi, kiteknolojia na kiviwanda kwa ajili ya
maendeleo ya kitaifa
Elimu inapaswa kumwandaa mwanafunzi kutekeleza wajibu wa kuleta ufanisi na
uzalishaji katika maendeleo ya nchi.
(a) Mahitaji ya kijamii
Elimu inapaswa kumkuza na kumwandaa mwanafunzi ili aweze kukabiliana na
changamoto zinazotokana na mabadiliko ya kijamii na kuweza kujitegemea na
kutegemewa na taifa.
(b) Mahitaji ya kiuchumi
Elimu inapaswa kumwandaa mwanafunzi kuwa na umilisi ufaao wa kuchangia katika
maendeleo ya kiuchumi ya kisasa kwa kutumia teknolojia inayoenda na wakati. Hili
litachangia katika kuboresha hali ya maisha ya watu katika jamii.
(ch) Mahitaji ya kiteknolojia na kiviwanda
Elimu inapaswa kumsaidia mwanafunzi kuwa na umilisi ufaao wa kiteknolojia na
kiviwanda kulingana na mabadiliko ya kiteknolojia yanayokwenda kwa kasi duniani.
vii
vi
Kimeidhinishwa na KICD
3. Kukuza nafasi ya kujiendeleza na kujitosheleza
Elimu inapaswa kumwezesha mwanafunzi kujiendeleza kikamilifu. Hii ni kupitia
kutambua, kupalilia, kukuza na kuimarisha kipawa chake ili aweze kujiendeleza na
kujitosheleza na kutoa mchango wake katika jamii.
4. Kukuza maadili mema ya kijamii na kidini
Elimu inakusudiwa kukuza maadili ya kitaifa na utangamano miongoni mwa wanajamii.
Inapaswa kukuza mwananchi mwenye nidhamu na mwadilifu, anayezingatia maadili
ya kijamii na kidini.
5. Kukuza usawa wa kijamii na uwajibikaji
Elimu inapaswa kuimarisha na kukuza usawa wa kijamii na uwajibikaji.
6. Kukuza heshima kwa ajili ya maendeleo ya tamaduni mbalimbali za Kenya
Elimu hutoa nafasi kwa mwanafunzi kuelewa, kuthamini, kuheshimu, kukuza na
kudumisha tamaduni faafu za jamii yake na za watu wengine ili kuakia maendeleo
na kujenga jamii dhabiti.
7. Kuimarisha utambuzi wa uhusiano wa kimataifa na kukuza mwelekeo chanya
kuhusu mataifa mengine.
Kenya ni sehemu ya jamii ya kimataifa. Elimu inapaswa kumsaidia mwanafunzi
kutambua, kuheshimu na kuthamini mahusiano ya kimataifa kwa kushiriki katika
nafasi zinazopatikana katika jamii ya kimataifa. Elimu inapaswa kumwezesha
mwanafunzi kushiriki katika jamii ya kimataifa kwa kuzingatia mikataba, uwajibikaji,
haki na manufaa yanayoambatana na ushirika huo.
8. Kukuza mwelekeo chanya kuhusu afya bora na uhifadhi wa mazingira
Elimu inakusudiwa kujenga mielekeo ifaayo kuhusu udumishaji wa afya bora na
utunzaji wa mazingira kwa kujiepusha na mienendo inayoweza kudhuru afya na
kukuza ulinzi na uhifadhi wa mazingira hasa utunzaji wa wanyama kwa minajili ya
maendeleo endelevu.
Malengo ya kijumla yanayotarajiwa katika shule ya msingi, daraja la juu
Kukia mwisho wa kiwango cha shule ya msingi, daraja la juu, mwanafunzi anatarajiwa:
1. Kuwasiliana kikamilifu katika miktadha mbalimbali.
2. Kutumia stadi za kusoma, kuandika, Hisabati na uwazaji kimantiki katika
kujieleza ipasavyo.
3. Kudhihirisha stadi za kijamii, kidini na kimaadili ili kuishi na wenzake kwa
amani na utangamano katika jamii.
4. Kuzingatia usa wa mwili, mazingira na lishe bora ili kudumisha afya bora.
ix
viii
Kimeidhinishwa na KICD
5. Kutumia ujuzi wa kidijitali ipasavyo katika mawasiliano na ujifunzaji.
6. Kudhihirisha maadili na uraia kama njia ya uwajibikaji.
7. Kuthamini, kukuza na kudumisha utajiri wa tamaduni mbalimbali za Kenya ili
kuishi kwa amani na utangamano katika jamii.
8. Kushughulikia kikamilifu masuala mtambuko na ya kisasa katika jamii.
Matokeo ya kijumla ya somo la Kiswahili yanayotarajiwa katika shule ya msingi
daraja la juu
Kukia mwisho wa shule ya msingi, daraja la juu, katika somo la Kiswahili, mwanafunzi
anatarajiwa:
1. Kusikiliza kwa makini na kuitikia ipasavyo kwa Kiswahili katika miktadha
mbalimbali ya mawasiliano.
2. Kuzingatia kanuni za lugha kuwasiliana kiubunifu kwa njia ya mazungumzo na
maandishi.
3. Kujieleza kwa ufasaha katika miktadha mbalimbali.
4. Kusoma kwa ufasaha na kufahamu matini mbalimbali yaliyochapishwa na ya
kidijitali na kutumia maarifa anayoyapata katika mazingira tofauti maishani.
5. Kutumia hati za kimaandishi na mfumo wa kidijitali kuwasiliana ipasavyo kwa
kuzingatia mitindo na miundo husika katika miktadha mbalimbali.
6. Kuchangamkia matumizi ya Kiswahili kama lugha rasmi na ya taifa katika
mawasiliano ya kila siku.
Mpangilio wa mwongozo wa mwalimu
Mwongozo huu wa mwalimu umepangwa katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ni
ya utangulizi wa kijumla kuhusu masuala ya ufunzaji na sehemu ya pili inaeleza kwa
kina mwendelezo wa kila kipindi katika kila sehemu kama ilivyo katika Kitabu cha
Mwanafunzi. Sehemu hii inaeleza kwa undani mambo yafuatayo:
1. Sehemu na utangulizi
2. Kipindi
3. Matokeo maalumu yanayotarajiwa
4. Maswali dadisi
5. Shughuli za ufunzaji na ujifunzaji
6. Nyenzo
7. Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
8. Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
9. Uhusiano na masuala mtambuko
10. Uhusiano na maadili
11. Uhusiano na masomo mengine
12. Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalumu
13. Shughuli za huduma za kijamii
14. Mapendekezo ya mbinu za
kutathmini
15. Mifano ya tathmini
ix
viii
Kimeidhinishwa na KICD
Njia za ufunzaji katika shughuli za Kiswahili
Baadhi ya njia ambazo mwalimu anaweza kufanikisha mchakato wa ufunzaji na
ujifunzaji katika mtaala wa kiumilisi katika somo la Kiswahili ni:
1. Kutega na kutegua vitendawili
2. Kuimba nyimbo
3. Kukariri mashairi
4. Maigizo
5. Kusimulia hadithi
6. Maswali na majibu
7. Kazi mradi
8. Kusakura
9. Majadiliano katika vikundi
10. Ufundishaji kikoa
11. Maonyesho
12. Ziara nyanjani
13. Kazi ya nyumbani
14. Kufanya mazoezi
15. Kutafakari
16. Matumizi ya vifaa vya kidijitali
Stakabadhi za kitaaluma
Hivi ni vitu ambavyo mwalimu anahitaji ili kutayarisha, kutekeleza na kutathmini
ufunzaji na ujifunzaji. Mwalimu anahitaji stakabadhi hizi ili kuweka rekodi ya kazi
yake na ya wanafunzi wake na pia kufanikisha ufunzaji. Stakabadhi hizi ni:
i. Maazimio ya kazi
ii. Mpangilio wa somo
iii. Rekodi ya kazi
iv. Rekodi ya utathmini
Maazimio ya kazi
Haya huandaliwa kutokana na silabasi inayoeleza sehemu zinazotakiwa kufunzwa
katika darasa fulani kwa mwaka mzima. Hupangwa kwa kuzingatia sehemu, malengo
ya somo kwa kutegemea mihula na wiki.
Kielelezo cha maazimio ya kazi
Jina la Shule Gredi Somo Muhula Mwaka Jina la Mwalimu
Shule ya
Msingi ya
Bondeni
4 Kiswahili 1 2020 Kipembe Korosho
xi
x
Kimeidhinishwa na KICD
Wiki Kipindi Sehemu kuu Mada Mada
ndogo
Matokeo
maalumu
yanayotarajiwa
Shughuli za
ujifunzaji
Maswali dadisi Nyenzo Tathmini Maoni
1 2 NYUMBANI Kusoma Kusoma
Hadithi
‘Nyumbani
kwa Akina
Akinyi’
Kukia mwisho
wa kipindi,
mwanafunzi
aweze:
1. Kutambua
msamiati wa
nyumbani
katika kifungu
cha hadithi.
2. Kutumia
msamiati wa
nyumbani
katika
sentensi kwa
usahihi.
3. Kusoma
kifungu
cha hadithi
‘Nyumbani
kwa Akina
Akinyi kwa
ufasaha.
4. Kujibu
maswali
kutokana na
kifungu cha
hadithi.
5. Kusoma
msamiati wa
nyumbani
kwa ufasaha.
Mwanafunzi:
asome
maneno yenye
msamiati wa
nyumbani.
ajadili na
wenzake
maneno ya
msamiati wa
nyumbani.
asome kifungu
cha hadithi.
atunge sentensi
akitumia
msamiati wa
nyumbani.
ajibu maswali
kutokana na
kifungu cha
hadithi.
1. Ni vifaa gani
vya nyumbani
unavyofahamu?
2. Vifaa vya
nyumbani
hutumiwa
kufanya kazi
gani?
Kitabu cha
Mwanafunzi,
ukurasa wa
8-9
Kadi zenye
maneno ya
msamiati wa
nyumbani
Michoro
au picha za
msamiati wa
nyumbani.
Mwongozo
wa Mwalimu
ukurasa wa
14-16
Kusoma
maneno
Kusoma
hadithi
Kutunga
sentensi
akitumia
msamiati wa
nyumbani
Kujibu
maswali
xi
x
Kimeidhinishwa na KICD
Mpangilio wa somo
Huu hutayarishwa kutoka kwenye maazimio ya kazi. Mpangilio wa somo ndio
humwongoza mwalimu wakati wa kufundisha darasani. Humwongoza mwalimu kwa
kuzingatia muda uliotengewa kila kipindi na shughuli za kutekelezwa katika kipindi
husika. Mpangilio wa somo ndio humwelekeza mwalimu katika vifaa vya kutumia
darasani na jinsi ya kuvitumia.
Kielelezo cha mpangilio wa somo
Shule: Shule ya Msingi ya Bondeni Jina la mwalimu: Kipembe Korosho
Muhula Gredi Somo Tarehe Mada Kipindi Muda Idadi ya
Wanafunzi
Idadi ya
wanafunzi
wenye
majitaji
maalumu
1 4 Kiswahili 14/01/2020 Kusoma 2 Dakika 35 40 2
NYUMBANI
Kusoma: Nyumbani kwa akina Akinyi
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua msamiati wa nyumbani katika kifungu cha hadithi.
2. Kutumia msamiati wa nyumbani katika sentensi kwa usahihi.
3. Kusoma kifungu cha hadithi ‘Nyumbani kwa akina Akinyi’ kwa ufasaha.
4. Kujibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi.
5. Kusoma msamiati wa nyumbani kwa ufasaha.
Nyenzo
1. Kitabu cha Mwanafunzi
2. Mwongozo wa Mwalimu
3. Kadi maneno
4. Michoro na picha
xiii
xii
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa kipindi
Hatua Shughuli ya ujifunzaji Muda
Utangulizi
Hatua ya 1
Wanafunzi wasome maneno kwenye mti
maneno katika Kitabu cha Mwanafunzi wakiwa
watatuwatatu.
Dakika 2
Uwasilishaji
Hatua ya 2
Wanafunzi wakiwa katika vikundi wataje vitu
vinavyopatikana nyumbani.
Dakika 5
Hatua ya 3 Wanafunzi wasome kifungu cha hadithi, ‘Nyumbani
kwa akina Akinyi wakiwa wawiliwawili.
Dakika 5
Hatua ya 4 Wanafunzi watambue msamiati wa nyumbani
uliotumika katika kifungu cha hadithi wakiwa
wawiliwawili.
Dakika 5
Hatua ya 5 Wanafunzi watunge sentensi wakitumia msamiati
wa nyumbani waliotambua kutokana na kifungu
cha hadithi wakiwa wawiliwawili.
Dakika 5
Hatua ya 6 Wanafunzi wajibu maswali kutokana na kifungu
cha hadithi wakiwa wawiliwawili.
Dakika 5
Hitimisho
Hatua ya
Mwisho
Wanafunzi wataje msamiati wa nyumbani
wanaofahamu.
Dakika 3
Kazi ya ziada
Waambie wanafunzi wataje msamiati wa nyumbani uliojadiliwa darasani kisha
uwape kazi mradi ya kuandika vifaa vya nyumbani vinavyopatikana nyumbani
kwao.
Tathmini ya kipindi
Tumia maswali haya kutathmini jinsi kipindi kilivyoeleweka:
1. Ni stadi gani ambayo imewatatiza baadhi ya wanafunzi wakati wa kipindi?
2. Je, wanafunzi waliweza kushiriki na kuchangia msamiati wa nyumbani katika
vikundi?
3. Katika kuwasilisha kipindi, wanafunzi wameuliza na kujibu maswali kuhusu
nyumbani barabara?
4. Je, nyenzo zilizokuwa zimetayarishwa zilifaulisha kipindi?
5. Je, ni wapi ninahitaji kuboresha ili kipindi kieleweke kwa wanafunzi ili
washiriki katika shughuli mbalimbali kikamilifu?
xiii
xii
Kimeidhinishwa na KICD
Rekodi ya kazi
Hii ni stakabadhi ambayo mwalimu huweka ili kuonyesha kazi ambayo amefundisha
katika kila kipindi cha somo lake. Rekodi ya kazi hujazwa kila siku na mwalimu ili
kuonyesha uwajibikaji wa mwalimu, maendeleo ya ufundishaji na pia husaidia iwapo
mwalimu mwingine atahitajika kufundisha darasa husika, ataweza kujua ni sehemu
gani ilifundishwa mwisho.
Kielelezo cha rekodi ya kazi
Rekodi ya kazi
Shule : Bondeni
Somo : Kiswahili
Mwalimu : Kombo
Gredi : 4
Tarehe Wiki Kazi Maoni Sahihi
3/7/2020 3 Kuandika
insha ya
masimulizi
Malengo ya
somo yalitimia
Rekodi ya tathmini
Hii ni stakabadhi inayotumika kuweka rekodi ya jinsi wanafunzi walivyofanya katika
somo husika. Rekodi ya tathmini hufanywa kwa mwanafunzi binafsi. Kwa hivyo,
mwalimu huandaa rekodi ya tathmini kwa kutegemea idadi ya wanafunzi katika
darasa lake. Rekodi hii huonyesha viwango vya tathmini.
Kielelezo cha rekodi ya tathmini ya maendeleo ya wanafunzi
Jina: Silvia Adava
Shule: Shule ya Msingi ya Bondeni
Gredi: 4
Somo: Kiswahili
1
xiv
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika tathmini: Kuzidi matarajio (4) Kukia matarajio (3)
Kukaribia matarajio (2) Mbali na matarajio (1)
Mada Vigezo
Viwango vya kutathmini mwanafunzi
Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Maoni
Matamshi
bora:
sauti /p/
na /b/
Kutambua
na
kutamka
sauti /p/
na /b/ kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
na kutamka
silabi za sauti
/p/ na /b/
kwa ufasaha
na urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
na kutamka
silabi za
sauti /p/
na /b/ kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
na kutamka
silabi za /p/
na /b/.
Mwanafunzi
anatambua
na kutamka
baadhi ya
silabi za
sauti /p/ na
/b/.
Mwanafunzi
anatambua
na kutamka
silabi za
sauti /p/
na /b/ kwa
usahihi.
Kusoma
kifungu
cha
Hadithi
Kutambua
na
kuchora
vifaa vya
nyumbani.
Mwanafunzi
anatambua
na kuchora
vifaa vya
nyumbani
vizuri, kwa
ufasaha na
sahihi.
Mwanafunzi
anatambua
na kuchora
vifaa vya
nyumbani
kwa sahihi.
Mwanafunzi
anatambua
na kuchora
vifaa vya
nyumbani.
Mwanafunzi
anatambua
na kuchora
baadhi ya
vifaa vya
nyumbani.
Mwanafunzi
anatambua
na kuchora
vifaa vya
nyumbani.
Kuandika Kuandika
insha ya
wasifu
kwa
kuzingatia
ujumbe,
muundo
na mtindo.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya
wasifu
akizingatia
ujumbe
ufaao,
muundo
na mtindo
sahihi kwa
ufasaha na
usahihi.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya
wasifu
akizingatia
ujumbe,
muundo na
mtindo kwa
ufasaha na
usahihi.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya
wasifu
akizingatia
ujumbe,
muundo na
mtindo.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya
wasifu
akizingatia
baadhi ya
vipengele
vya
muundo.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya
wasifu
akizingatia
ujumbe,
muundo
na mtindo
sahihi.
Saru
Aina za
maneno
Nomino
Kutumia
nomino
kwa njia
sahihi
katika
sentensi.
Mwanafunzi
anatumia
nomino
katika
kutunga
sentensi kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatumia
nomino
katika
kutunga
sentensi
ipasavyo.
Mwanafunzi
anatumia
nomino
katika
kutunga
sentensi.
Mwanafunzi
anatumia
baadhi ya
nomino
katika
kutunga
sentensi.
Mwanafunzi
anatumia
nomino
katika
kutunga
sentensi
ipasavyo.
1
xiv
Kimeidhinishwa na KICD
NYUMBANI
1
Nyenzo
Shughuli ya ujifunzaji na ufunzaji hufanikiwa kutokana na uteuzi, maandalizi na
matumizi ya nyenzo. Hakikisha kuwa umeandaa nyenzo mwafaka ili kufanikisha
shughuli ya ufunzaji na ujifunzaji wa sehemu ya nyumbani. Unaweza kutumia
nyenzo zifuatazo:
Vifaa halisi: saa, stuli, redio, runinga, meza na kiti.
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, tabuleti, rununu na projekta.
Kinasasauti
Mtandao wa intaneti
Picha
Michoro
Chati
Kadi
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wafanye mazoezi na shughuli mbalimbali kwa kushirikiana katika
vikundi. Wanaweza kutamka sauti au kusoma makala kwa pamoja. Mijadala baina
ya wanafunzi kuhusu vifaa vya nyumbani itaimarisha mawasiliano na kukuza
Utangulizi
Nyumbani ni mahali ambapo watu huishi. Nyumbani kuna watu, wanyama, ndege,
vyumba, sehemu na vifaa mbalimbali. Sehemu hii ina sehemu ndogo zinazohusu:
matamshi bora, kusoma kwa ufahamu, kuandika insha, nomino, vitenzi na vivumishi.
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutamka sauti, silabi, maneno na vitanzandimi ipasavyo.
2. Kusoma maneno ya hadithi kwa ufasaha.
3. Kuandika insha ya wasifu kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
4. Kutunga sentensi kwa kutumia nomino, vitenzi na vivumishi kwa njia ifaayo.
3
2
Kimeidhinishwa na KICD
ushirikiano. Mawasiliano yatimizwe wanafunzi wakisambaza habari kuhusu vifaa vya
nyumbani kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Hakikisha kuwa umeshirikisha matumizi ya tarakilishi,
video, tabuleti, projekta, intaneti na tovuti ili mwanafunzi ajifunze shughuli za
nyumbani.
(ch) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia wanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
shughuli za nyumbani.Umilisi huu utawapa wanafunzi hamu ya kukariri silabi na
vitanzandimi. Pia, watatafakari maswali ya ziada ambayo wataulizwa. Unaweza
ukawauliza maswali kuhusu vifaa vinavyopatikana nyumbani kwao. Kupitia maswali
kama haya, kila mwanafunzi anaweza kuwa na hamu ya kutaka kutumia vyombo vya
kidijitali na atafakari zaidi kuhusu shughuli za nyumbani.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika insha ya wasifu kuhusu mama,
baba, walimu, mlezi, mzazi, darasa au shule. Pia ubunifu ukuzwe na kuimarishwa kwa
kutunga vitanzandimi na sentensi. Ubunifu utadhihirika mwanafunzi akibuni hadithi
kuhusu nyumbani kwao.
(e) Kujiamini
Umilisi huu unakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kutamka sauti, silabi, maneno na vitanzandimi. Pia, kujiamini kunakuzwa
kupitia mwanafunzi kutambua aina za maneno kama vile: nomino, vivumishi na
vitenzi na kutunga sentensi sahihi akitumia aina hizo za maneno.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu unakuzwa kupitia kumpa mwanafunzi swali la kutafakari, kukiria na
kutafuta jawabu lake ambalo halimo kwenye matini. Kwa mfano, unaweza ukawauliza
wanafunzi: unataka kupika ugali lakini hakuna gesi kwenye mtungi wa gesi nyumbani.
Utafanyaje?
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Kujitambua na kujithamini
Kunadhihirika kupitia kukariri vitanzandimi, kutunga sentensi na kutunga
vitanzandimi.
3
2
Kimeidhinishwa na KICD
(b) Stadi za maisha
Stadi hizi zinakuzwa kupitia mwanafunzi kujieleza, kushiriki katika vikundi,
kuchangia mijadala na kutunza vitu vya nyumbani.
(ch) Uraia
Uraia unadhihirika kupitia wanafunzi kufanya kazi pamoja na kudhihirisha
upendo katika familia.
(d) Utunzaji wa mazingira
Stadi hii inadhihirika kupitia kutunza mazingira ya nyumbani kwa kufyeka
nyasi, kupanda maua, mimea na miche.
(e) Afya bora
Stadi hii itadhihirika kupitia wanafunzi kushiriki kula lishe bora nyumbani na
kufanya shughuli zinazofanikisha afya bora kama vile: kuosha vyombo, kula
matunda na kupanda mboga nyumbani.
(f) Utunzaji wa wanyama
Wanafunzi watadhihirisha stadi hii kwa kutunza wanyama wanaopatikana
nyumbani.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu kwa watu nyumbani kama baba, mama, mlezi, babu au
nyanya inakuzwa wanafunzi wanapofanya kazi katika shughuli za vikundi kwa
kuheshimu maoni ya wenzao na kusikiliza wenzao wakizungumza.
Uaminifu unakuzwa wanafunzi wanapofanya kazi wanazopewa nyumbani.
Wanafunzi wanajifunza kuonyesha upendo kwa watu wote nyumbani
kutokana na jinsi wanavyotangamana nao katika shughuli zao za kila siku.
Wanafunzi wanasisitiziwa kushabikia uzalendo kwa kupenda, kuenzi na
kufurahia nyumbani kwao.
Kwa kuzingatia utulivu na uhusiano mwema na watu nyumbani, wanafunzi
wanajifunza umuhimu wa amani.
Shughuli za huduma za kijamii
Kushiriki katika kutunza mazingira ya nyumbani kwa: kufyeka nyasi, kuokota
taka, kufagia na kupiga deki.
Kutunza wanyama wanaopatikana nyumbani kwa kuwapa chakula na maji.
Kunyunyizia mimea na matunda maji.
Kusaidia wazazi au walezi katika kufanya shughuli za nyumbani kama vile
kupika na kuosha vyombo.
Kuwasaidia majirani au wakongwe walio karibu na nyumbani kwao.
Kuimarisha matamshi bora kwa kuzungumza na watu akiwa nyumbani.
5
4
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
1. Environmental Activities: somo la Kiswahili linangiliana na somo
hili kupitia matumizi ya msamiati kuhusu mimea, wanyama na vifaa
vinavyopatikana nyumbani.
2. English Activities: somo hili lina sehemu kuhusu vitanzandimi, sauti,
silabi na maneno. Mada hizi zinafunzwa ili kukuza stadi ya kusikiliza
na kuzungumza. Katika saru kuna mada kuhusu nomino, vitenzi na
vivumishi.
3. Indigenous Languages Activities: vitanzandimi, sauti, silabi na maneno
hufundishwa katika Kiswahili na somo hili. Uhusiano huu unasaidia
katika kukuza stadi ya kusikiliza na kuzungumza.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Sehemu hii inahusu sehemu nne kuu, kusikiliza na kuzungumza, kusoma, kuandika na
saru. Kwa somo linalohusu kusoma na kusikiliza, hakikisha kuwa wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona wamepata mashine za breli darasani ili ziwasaidie katika kutambua maneno.
Kwa wanafunzi wenye matatizo ya kusikia na kuzungumza, unaweza kumwalika mfasiri
wa lugha ishara ili awasaidie wanafunzi hao katika kushiriki kwenye somo kikamilifu. Pia,
unaweza ukatumia vifaa vya kiteknolojia kama vile: projekta ili kuwaonyesha wanafunzi
baadhi ya picha zinazohusu nyumbani kutoka mtandaoni. Ili kuwahusisha wanafunzi
wenye matatizo katika baadhi ya viungo vyao vya mwili kama vile, miguu na mikono,
hakikisha kuwa wakati wa kuigiza wanafunzi hawa wameangaliwa ili wasijiumize au
kuumizwa kwenye viungo vilivyoathirika.
Kusikiliza na Kuzungumza
Matamshi bora: Silabi na vitanzandimi vya p/b, t/d, k/g na ch/j
Kipindi cha 1
Sauti /p/ na /b/
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 1-3
Utangulizi
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaagize
watambue vitu vinavyopatikana nyumbani kama ilivyo kwenye picha iliyo
kitabuni.
5
4
Kimeidhinishwa na KICD
ü Waongoze wanafunzi katika kuandika kile wanachoona kwenye picha hiyo.
Hakikisha kuwa wanafunzi wanataja na kuandika vitu hivyo. Wanaweza
wakataja:
(a) Nyumba
(b) Sebule
(ch) Meza
(d) Kuku
(e) Ua
(f) Kochi
(g) Kabati
(h) Mtu
(i) Fyekeo
(j) Maua
(k) Zulia
(l) Nyasi
Kwa wanafunzi wasioona, mwalimu anaweza kupata msaada ili majina ya
vifaa hivyo yaandikwe kwa breli.
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sauti, silabi na maneno yenye sauti /p/ na /b/.
2. Kutamka sauti, silabi na maneno yenye sauti /p/ na /b/.
3. Kutamka vitanzandimi vya sauti /p/ na /b/.
4. Kutunga vitanzandimi vilivyo na sauti /p/ na /b/.
5. Kuchangamkia kutamka sauti /p/ na /b/ na kukariri vitanzandimi vilivyo na sauti
/p/ na /b/.
Swali dadisi
Ni silabi zipi zinazorudiwa katika vitanzandimi ulivyosoma?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwalimu atambue sauti /p/ na /b/ katika maneno.
Mwalimu atamke sauti /p/ na /b/.
Mwanafunzi asikilize na atamke baada ya mwalimu.
Mwalimu atamke silabi na maneno yaliyo na sauti /p/ na /b/.
Wanafunzi wasikilize na watamke silabi na maneno hayo baada ya mwalimu.
Wanafunzi wasikilize maneno yakitamkwa kupitia vyombo vya kidijitali hasa
kanda ya sauti.
Wanafunzi watamke maneno waliyosikia kwenye kanda ya sauti.
Wanafunzi watamke vitanzandimi wakiwa wawiliwawili.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 2-3
Kadi za sauti, silabi na maneno
Chati ya sauti, silabi na maneno
Rununu
Kanda ya sauti
7
6
Kimeidhinishwa na KICD
Tarakilishi Breli
Maandalizi ya mwalimu
Andaa kadi za sauti, silabi na maneno yenye sauti /p/ na /b/.
Rekodi maneno yenye sauti /p/ na /b/ kwenye kanda ya sauti.
Rekodi silabi zenye sauti /p/ na /b/ kwenye rununu au tabuleti yako.
Rekodi vitanzandimi vilivyo na sauti /p/ na /b/ kwenye rununu au tabuleti.
Andaa chati yenye silabi na maneno yaliyo na sauti /p/ na /b/.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame picha kwenye ukurasa
wa kwanza katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Mwanafunzi awaeleze wenzake anaona vitu gani nyumbani. Kubali majibu
yanayohusiana na nyumbani.
Andika sauti /p/ na /b/ kwenye ubao.
Tamka sauti /p/ na /b/ kwa sauti. Wanafunzi wasikize kwa makini.
Waelekeze wanafunzi watamke sauti /p/ na /b/. Teua mwanafunzi mmoja
mmoja kutamka sauti hizi kisha baadaye watamke wakiwa wawiliwawili.
Ongoza kila mwanafunzi kutamka sauti /p/ na /b/ akiwa peke yake.
Tamka kwa sauti silabi za sauti /p/ na /b/ huku wanafunzi wakisikiliza.
Waonyeshe wanafunzi kadi za silabi zenye sauti /p/ na /b/. Unaweza pia
ukawapa wanafunzi rekodi ya utamkaji wa sauti hizi. Waongoze wanafunzi
kutamka silabi zenye sauti /p/ na /b/ wakiwa wawiliwawili.
Toa kanda ya sauti iliyo na maneno yenye sauti /p/ na /b/. Wanafunzi
wasikilize maneno yakitamkwa kwenye kanda ya sauti yenye sauti /p/ na /b/.
Waongoze wanafunzi katika kutamka maneno yenye sauti /p/ na /b/ wakiwa
darasa zima. Waonyeshe kadi za maneno yenye sauti /p/ na /b/. Maneno
yenyewe ni:
ü buba/pupa
ü beba/pepo
ü beni/peni
ü bana/pana
ü bima/pima
ü baa/paa
Waelekeze wanafunzi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 2 kisha
uwaambie wasikilize kwa makini mwanafunzi mwenzao akitamka maneno
yaliyo na sauti /p/ na /b/. Hakikisha kuwa matamshi hayo ni sahihi.
Warekebishe wanapokosea katika matamshi.
Waweke wanafunzi wako katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaelekeze
katika kutamka vitanzandimi vilivyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Watamke vitanzandimi kwa sauti, kwa kasi na kwa makini.
Waongoze wanafunzi katika kufanya zoezi la kwanza katika vikundi.
7
6
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 2-3
1. Hakikisha wametamka vitanzandimi kwa kuzingatia matamshi sahihi ya
sauti /p/ na /b/.
2. Maneno yenye sauti /p/ na /b/ ni:
(a) baba, papa, bata, sikumpata
(b) bango, pango, limebomolewa
(ch) punda, bunda, mkubwa
(d) baa, paa, hawakukubalia
3. Hakikisha wametunga vitanzandimi kwa kutumia maneno hayo yenye
sauti /p/ na /b/.
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha funzo kwa kuwaambia wanafunzi watamke maneno
yenye sauti /p/ na /b/ kwa usahihi na haraka. Kwa mfano: baba na papa.
Kipindi cha 2
Sauti /t/ na /d/
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 3-4
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sauti, silabi na maneno yenye sauti /t/ na /d/.
2. Kutamka sauti, silabi na maneno yenye sauti /t/ na /d/.
3. Kutamka vitanzandimi vya sauti /t/ na /d/.
4. Kutunga vitanzandimi vilivyo na sauti /t/ na /d/.
5. Kuchangamkia kutamka sauti /t/ na /d/ na kukariri vitanzandimi vilivyo na sauti
/t/ na /d/.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwalimu atambue sauti /t/ na /d/ katika maneno.
Mwalimu atamke sauti /t/ na /d/.
Mwanafunzi asikilize na atamke saut/t/ na /d/ baada ya mwalimu.
Mwalimu atamke silabi na maneno yaliyo na sauti /t/ na /d/.
9
8
Kimeidhinishwa na KICD
Mwanafunzi asikilize na atamke silabi na maneno hayo baada ya mwalimu.
Wanafunzi wasikilize maneno yakitamkwa kupitia vyombo vya kidigitali hasa
kanda ya sauti.
Wanafunzi watamke maneno waliyosikia kwenye kanda ya sauti.
Wanafunzi watamke vitanzandimi wakiwa wawiliwawili.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 3
Kadi za maneno, sauti na silabi
Chati ya maneno
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Kinasasauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha na yatakayofunzwa.
Soma mwongozo wa mwalimu ili kupata mwelekeo.
Andaa kadi za sauti, silabi na maneno yenye sauti /t/ na /d/.
Rekodi maneno yenye sauti /t/ na /d/ kwenye kanda ya sauti.
Rekodi silabi zenye sauti /t/ na /d/ kwenye rununu au tabuleti yako.
Rekodi vitanzandimi vilivyo na sauti /t/ na /d/ kwenye rununu au tabuleti.
Andaa chati yenye silabi na maneno yaliyo na sauti /t/ na /d/.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tamka sauti /t/ na /d/ kwa sauti. Wanafunzi wasikize kwa makini.
Ongoza mwanafunzi kutamka sauti /t/ na /d/ akiwa peke yake.
Tamka kwa sauti silabi za sauti /t/ na /d/ huku wanafunzi wakisikiliza.
Waonyeshe wanafunzi kadi za silabi zenye sauti /t/ na /d/. Waongoze
wanafunzi kutamka silabi zenye sauti /t/ na /d/ wakiwa wawiliwawili.
Toa kanda ya sauti iliyo na maneno yenye sauti /t/ na /d/. Wanafunzi
wasikilize maneno yakitamkwa kwenye kanda ya sauti yenye sauti /t/ na /d/.
Waongoze wanafunzi kutamka maneno yenye sauti /t/ na /d/.
Waongoze wanafunzi kutamka maneno yenye sauti /t/ na /d/ wakiwa darasa
zima. Waonyeshe kadi za maneno yenye sauti /t/ na /d/. Maneno yenyewe ni:
(a) damu/tamu
(b) dubu/tubu
(c) dada/tata
(d) dua/tua
(e) toa/doa
(f) taka/daka
Waelekeze wanafunzi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 3.
Waambie wasikilize kwa makini mwanafunzi akitamka maneno yaliyo
9
8
Kimeidhinishwa na KICD
na sauti /t/ na /d/. Hakikisha matamshi ya wanafunzi ni bora na sahihi.
Warekebishe panapohitajika.
Waweke wanafunzi wako katika vikundi vya wawiliwawili. Wakiwa
wawiliwawili, waelekeze katika kutamka vitanzandimi vilivyo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi. Watamke vitanzandimi hivi kwa sauti, kwa kasi na kwa
makini.
Waongoze wanafunzi katika kufanya zoezi katika Kitabu cha Mwanafunzi
kwa vikundi.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 4
1. Hakiki vitanzandimi watakavyotunga. Vizingatie sauti /t/ na /d/
ipasavyo.
2. Wanafunzi wasome ipasavyo wakizingatia sauti /t/ na /d/.
3. Maneno yenye sauti /t/ na /d/ ni:
(a) Dada, matata, Tata, utata
(b) Daka, alitaka, kudaka, taka
(ch) Tunda, dunda
(d) Ndoa, Toa, doa, alitoa
(e) Alimdunga, akatunga
(f) Mtundu, dundu, tundu
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha funzo kwa kuwaambia wanafunzi watamke vitate
kadhaa.
Kipindi cha 3
Sauti /k/ na /g/
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 4-5
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sauti, silabi na maneno yenye sauti /k/ na /g/.
2. Kutamka sauti, silabi na maneno yenye sauti /k/ na /g/.
3. Kutamka vitanzandimi vya sauti /k/ na /g/.
4. Kutunga vitanzandimi vilivyo na sauti /k/ na /g/.
5. Kuchangamkia kutamka sauti /k/ na /g/ na kukariri vitanzandimi vilivyo na sauti
/k/ na /g/.
11
10
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwalimu atambue sauti /k/ na /g/ katika maneno.
Mwalimu atamke sauti /k/ na /g/.
Mwanafunzi asikilize na atamke sauti/k/ na /g/ baada ya mwalimu.
Mwalimu atamke silabi na maneno yaliyo na sauti /k/ na /g/. Mwanafunzi
asikilize na atamke silabi na maneno hayo baada ya mwalimu.
Mwanafunzi asikilize maneno yakitamkwa kupitia vyombo vya kidijitali hasa
kanda ya sauti.
Wanafunzi watamke maneno waliyosikia kwenye kanda ya sauti.
Wanafunzi watamke vitanzandimi wakiwa watatuwatatu.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 4-5
Kadi za sauti, silabi na maneno
Chati ya maneno
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Kinasasauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 4-5 ili kujifahamisha na
yatakayofunzwa.
Soma mwongozo wa mwalimu ili kupata mwelekeo.
Andaa kadi za sauti, silabi na za maneno yenye sauti /k/ na /g/.
Rekodi maneno yenye sauti /k/ na /g/ kwenye kanda ya sauti.
Rekodi silabi zenye sauti /k/ na /g/ kwenye rununu au tabuleti yako.
Rekodi vitanzandimi vilivyo na sauti /k/ na /g/ kwenye rununu au tabuleti.
Andaa chati yenye silabi na maneno yaliyo na sauti /k/ na /g/.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tamka sauti /k/ na /g/ kwa sauti. Wanafunzi wasikize kwa makini.
Waelekeze wanafunzi katika kutamka sauti /k/ na /g/ baada yako.
Ongoza kila mwanafunzi kutamka sauti /k/ na /g/ akiwa peke yake.
11
10
Kimeidhinishwa na KICD
Tamka kwa sauti silabi za sauti /k/ na /g/ huku wanafunzi wakisikiliza.
Waonyeshe wanafunzi kadi za silabi zenye sauti /k/ na /g/. Waongoze
wanafunzi katika kutamka silabi zenye sauti /k/ na /g/ wakiwa wawiliwawili.
Toa kanda ya sauti iliyo na maneno yenye sauti /k/ na /g/. Wanafunzi
wasikilize maneno yakitamkwa kwenye kanda ya sauti yenye sauti /k/ na /g/.
Waongoze wanafunzi kutamka maneno yenye sauti /k/ na /g/.
Waongoze wanafunzi kutamka maneno yenye sauti /k/ na /g/ wakiwa
wawiliwawili. Waonyeshe kadi za maneno yenye sauti /k/ na /g/. Maneno
yenyewe ni:
(a) gaidi/kaidi
(b) kuku/gugu
(ch) kuni/guni
(d) kesi/gesi
(e) koti/goti
(f) kuna/guna
Waambie wasikilize kwa makini mwanafunzi akitamka maneno yaliyo
na sauti /k/ na /g/. Hakikisha matamshi ni bora na sahihi. Warekebishe
panapohitajika.
Wapange wanafunzi wako katika vikundi vya wawiliwawili. Wakiwa
wawiliwawili, waelekeze katika kusoma vitanzandimi vilivyo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi. Watamke vitanzandimi kwa sauti, kwa kasi na kwa makini.
Waongoze wanafunzi kufanya zoezi katika Kitabu cha Mwanafunzi kwa
vikundi.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa wa 5
1. Hakiki namna watakavyotamka vitanzandimi wakizingatia sauti /k/ na
/g/.
2. Maneno yenye sauti /k/ na /g/ ni:
(a) Gatia, aliketi, kigoda, geti.
(b) Kiptoo, koti, linalomkia, goti.
(ch) Kesi, kuhusu, gesi, itasikizwa
(d) Gundi, ilikwama, kwenye,
kia, jibwa.
3. Wanafunzi watunge vitanzandimi ipasavyo wakizingatia sauti /k/ na /g/.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watamke maneno
koti na goti kwa kasi mara nyingi.
13
12
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 4
Sauti /ch/ na /j/
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 5-6
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sauti, silabi na maneno yenye sauti /ch/ na /j/.
2. Kutamka sauti, silabi na maneno yenye sauti /ch/ na /j/.
3. Kutamka vitanzandimi vya sauti /ch/ na /j/.
4. Kutunga vitanzandimi vilivyo na sauti /ch/ na /j/.
5. Kuchangamkia kutamka sauti /ch/ na /j/ na kukariri vitanzandimi vilivyo na
sauti /ch/ na /j/.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwalimu atambue sauti /ch/ na /j/ katika maneno.
Mwalimu atamke sauti /ch/ na /j/.
Mwanafunzi asikilize na atamke sauti/ch/ na /j/ baada ya mwalimu.
Mwalimu atamke silabi na maneno yaliyo na sauti /ch/ na /j/. Mwanafunzi
asikilize na atamke silabi na maneno hayo baada ya mwalimu.
Mwanafunzi asikilize maneno yakitamkwa kupitia vyombo vya kidigitali hasa
kanda ya sauti.
Wanafunzi watamke maneno waliyosikia kwenye kanda ya sauti.
Wanafunzi wasome vitanzandimi wakiwa wawiliwawili.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 5-6
Kadi za sauti, silabi na maneno
Chati ya maneno
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Kinasasauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ili kujifahamisha yatakayofunzwa.
Soma mwongozo wa mwalimu ili kupata mwelekeo.
13
12
Kimeidhinishwa na KICD
Andaa kadi za sauti, silabi na za maneno yenye sauti /ch/ na /j/.
Rekodi maneno yenye sauti /ch/ na /j/ kwenye kanda ya sauti.
Rekodi silabi zenye sauti /ch/ na /j/ kwenye rununu au tabuleti yako.
Rekodi vitanzandimi vilivyo na sauti /ch/ na /j/ kwenye rununu au tabuleti.
Andaa chati yenye silabi na maneno yaliyo na sauti /ch/ na /j/.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tamka sauti /ch/ na /j/ kwa sauti. Wanafunzi wasikilize kwa makini.
Waelekeze wanafunzi katika kutamka sauti /ch/ na /j/ wakiwa wawiliwawili.
Ongoza kila mwanafunzi kutamka sauti /ch/ na /j/ akiwa peke yake.
Tamka kwa sauti silabi za sauti /ch/ na /j/ huku wanafunzi wakisikiliza.
Waonyeshe wanafunzi kadi za silabi zenye sauti /ch/ na /j/. Waongoze
wanafunzi katika kutamka silabi zenye sauti /ch/ na /j/ wakiwa wawiliwawili.
Toa kanda ya sauti iliyo na maneno yenye sauti /ch/ na /j/. Wanafunzi
wasikilize maneno yakitamkwa kwenye kanda ya sauti yenye sauti /ch/ na /j/.
Waongoze wanafunzi katika kutamka maneno yenye sauti /ch/ na /j/.
Waongoze wanafunzi katika kutamka maneno yenye sauti /ch/ na /j/ wakiwa
darasa zima. Waonyeshe kadi za maneno yenye sauti /ch/ na /j/. Maneno
yenyewe ni:
(a) chumba/jumba
(b) chungu/jungu
(c) chana/jana
(d) chuma/juma
Waelekeze wanafunzi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 6 na
uwaambie wasikilize kwa makini mwanafunzi akitamka maneno yaliyo na
sauti /ch/ na /j/. Hakikisha kuwa matamshi ni bora na sahihi. Warekebishe
panapohitajika.
Waweke wanafunzi wako katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaelekeze
kusoma vitanzandimi vilivyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Watamke
vitanzandimi kwa sauti, kwa kasi na kwa makini.
Warekodi wanafunzi wakisoma vitendawili hivyo.
Wanafunzi wasikilize jinsi walivyorekodiwa na mwalimu. Wajikosoe
panapohitajika.
Waelekeze wanafunzi kutambua maneno yote yenye sauti /ch/ kwenye
vitanzandimi walivyosoma. Maneno haya ni:
(a) alichora
(b) Gucha, kucha
(c) mchi
(d) chumba
(e) Pacha
(f) chenga
15
14
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi kutambua maneno yote yenye sauti /j/ kwenye
vitanzandimi walivyosoma. Maneno haya ni:
(a) jora
(b) alipokuja
(c) mjini
(d) jumba
(e) paja
(f) Njenga alijenga
Waongoze wanafunzi kufanya zoezi katika Kitabu cha Mwanafunzi kwa
vikundi.
Majibu
Zoezi la 4, ukurasa wa 6
1. Waongoze wanafunzi katika kujigawa katika vikundi vya wannewanne
na kutunga vitanzandimi vitano kisha wavisome darasani. Waambie
washindane kuvitamka kwa kasi. Kikundi kitakachoibuka na ushindi
kituzwe.
2. Waelekeze katika kuandika maneno yote yenye sauti /ch/ kwenye
vitanzandimi walivyotunga. Hakiki maneno ya wanafunzi wako.
3. Waongoze katika kuandika maneno yote yenye sauti /j/ kutoka kwenye
vitanzandimi walivyotunga. Hakiki maneno ya wanafunzi wako.
4. Waambie wapige taipu vitanzandimi walivyotunga kisha wawasambazie
wenzao kupitia kwa mtandao wa intaneti.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha funzo kwa kuwaambia wanafunzi watamke maneno
chora na jora kwa kasi na mara nyingi wawezavyo.
Kusoma
Kipindi cha 1
Ufahamu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 7-9
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua msamiati wa nyumbani katika kifungu cha hadithi.
2. Kutumia msamiati wa nyumbani katika sentensi kwa usahihi.
3. Kusoma kifungu cha hadithi ‘Nyumbani kwa Akina Akinyi’ kwa ufasaha.
15
14
Kimeidhinishwa na KICD
4. Kujibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi.
5. Kusoma msamiati wa nyumbani kwa ufasaha.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi asome maneno yenye msamiati wa nyumbani kwenye mti maneno.
Mwanafunzi ajadili na wenzake maneno ya msamiati wa nyumbani.
Mwanafunzi asome kifungu cha hadithi.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia msamiati wa nyumbani.
Mwanafunzi ajibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi katika usomaji wa maneno na kifungu cha
hadithi.
Nyenzo
Kadi
Mti maneno
Kinasasauti
Breli
Mfasiri wa lugha ishara
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 7-9 ili kuelewa sehemu hii.
Tafuta kadi za maneno ya msamiati wa nyumbani.
Andaa mchoro wa mti maneno wenye msamiati wa nyumbani.
Soma kifungu cha hadithi kabla ya uwasilishaji darasani.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya
watatuwatatu. Waambie wasimame mbele ya wanafunzi darasani. Waelekeze
katika kusoma maneno yaliyo kwenye mti maneno.
Wanafunzi wasome kwa zamu. Waulize ni vitu gani vya nyumbani ambavyo
wamewahi kutumia miongoni mwa vitu walivyosoma.
Waongoze kueleza matumizi ya vifaa vinavyopatikana nyumbani walivyotaja.
Kwa mfano: kitanda- kulalia, maga-kuinjika chungu, neti-kuzuia mbu, saa-
kujua wakati, kinu- kutwangia nafaka, sebule- sehemu ya kupumzika.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili.
Waongoze wanafunzi katika kusoma hadithi kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 8 ili wasome kifungu cha hadithi: Nyumbani kwa Akina Akinyi
wakiwa wawiliwawili.
Waongoze wanafunzi katika kutambua maneno ya msamiati wa nyumbani
kutoka kwa kifungu hicho cha hadithi.
Waelekeze wanafunzi katika kujibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi
walichosoma.
17
16
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 8-9
1. Wanafunzi watoe muhtasari wa kifungu cha hadithi waliyosoma.
2. Akinyi
3. Akinyi alikuwa jikoni akichochea kuni kwenye meko.
4. Kinu na mchi
5. Kiyoyozi
6. Kabatini
7. Kitanda, godoro, foronya, blanketi, chandarua na patipati.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi majina ya vyombo
vinavyopatikana nyumbani kwao. Wanafunzi wataje vifaa vya nyumbani kama: kochi,
meza, kiti, sahani, televisheni, miongoni mwa vingine.
Kipindi cha 2
Wimbo
Nyumbani kuna Nyumba
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 9-10
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kuimba wimbo ulio na msamiati wa nyumbani.
2. Kusoma maneno ya msamiati wa nyumbani yaliyo kwenye wimbo huo kwa
usahihi.
3. Kutunga sentensi akitumia msamiati wa nyumbani.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kuimba wimbo.
Wanafunzi kuchora vifaa vya nyumbani kwenye chati.
Wanafunzi kupaka rangi michoro ya vifaa vya nyumbani.
Wanafunzi kusoma maneno ya vifaa vya nyumbani yaliyo kwenye wimbo.
Wanafunzi kutunga sentensi wakitumia maneno yenye msamiati wa
nyumbani.
17
16
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha
Mwanafunzi
Wimbo
Rangi ya kupaka
Karatasi za manila
Penseli
Gundi
Brashi
Breli
Kinasasauti
Maandalizi ya mwalimu
Hakikisha una nyenzo zinazohitajika kama rangi, penseli, karatasi za manila,
gundi na rekodi ya wimbo ulio kwenye kitabu.
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 9.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje vyombo vya
nyumbani wanavyofahamu. Wataje vifaa hivyo wakiwa wawiliwawili.
Waelekeze wanafunzi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 9. Wakiwa
darasa zima, waongoze katika kuimba wimbo wa ‘Nyumbani kuna Nyumba.
Unaweza ukawapa mahadhi ya kufuata wakiimba na pia uwape uhuru wa
kuimba kwa mahadhi yao wenyewe.
Washirikishe katika kutambua msamiati wa nyumbani uliotumiwa katika
wimbo huo.
Waelekeze wanafunzi katika kujadili matumizi ya vyombo vya nyumbani
vilivyotajwa kwenye wimbo huo.
Waambie wachore na kuvipaka rangi vifaa vya nyumbani kwenye chati
wakiwa wawiliwawili.
Waelekeze wanafunzi ili waweke michoro hiyo kwenye kuta za darasa.
Waambie wasome maneno ya michoro hiyo wakiwa wawiliwawili.
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia msamiati wa
nyumbani. Kwa mfano: Sebule yetu inapendeza. Kikombe kimewekwa ndani
ya kabati. Lango limefunguliwa. Akello anatumia mchi kutwanga mahindi.
Yeye alinunua foronya nyeupe.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 10
1. Wimbo unahusu vyombo vinavyopatikana nyumbani na matumizi yake.
2. Meza, kiti, kitanda, kochi, sahani, bilauri, sufuria, godoro, blanketi,
panga, shoka, jembe
3. Tathmini namna wanafunzi wanavyojadili matumizi ya vifaa vya
nyumbani.
19
18
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi zoezi la ziada la
kuchora vifaa vya nyumbani kwao.
Kuandika
Insha ya wasifu
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 10-11
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua muundo wa insha ya wasifu.
2. Kuandika insha ya wasifu kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue muundo wa insha ya wasifu.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika kuandika insha ya wasifu.
Wanafunzi waandike insha ya wasifu kuhusu: Raki Yangu na Mlezi Wangu.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi
Insha kielelezo (insha ya wasifu)
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Tayarisha insha kielelezo (insha ya wasifu)
Tafuta tarakilishi au tabuleti
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yaliyomo.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaweka wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili.
Waambie watoe maelezo kuhusu wanafunzi wenzao.
Washirikishe wanafunzi wawiliwawili katika kusoma maelezo kuhusu insha
ya wasifu.
Washirikishe wanafunzi katika zoezi la kujibu maswali kuhusu Raki Yangu
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Waelekeze katika kuandika majibu ya maswali kuhusu Raki Yangu
kimfululizo kwenye madaari yao.
19
18
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi ili waandike majibu yao kwenye tarakilishi kama aya
moja.
Washirikishe katika kusoma majibu waliyoandika kuhusu Raki Yangu
kwenye tarakilishi.
Wasaidie wanafunzi kusambaza aya hiyo kupitia mtandao wa intaneti.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 11
Tathmini jinsi wanafunzi wanavyoshiriki katika zoezi la kueleza kuhusu raki
na kuandika majibu kwenye tarakilishi.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kwa kuteua wanafunzi wawili waje mbele ya darasa
na kusoma kwa zamu aya kuhusu Raki Yangu.
Kazi ya ziada
Waambie wanafunzi waandike sentensi saba kuhusu: Nyumbani Kwetu.
Kipindi cha 2
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya wasifu kwa kuzingatia muundo.
2. Kuandika insha ya wasifu kwa kutumia vidokezo alivyopewa.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi aandike vidokezo kuhusu insha ya wasifu.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika kuandika muundo wa insha ya wasifu.
Mwanafunzi aandike insha ya wasifu kuhusu Mlezi Wangu kwa kuzingatia
vidokezo alivyopewa.
Mwanafunzi asome insha ya wasifu aliyoandika kwa ufasaha.
Nyenzo
Insha kielelezo (insha ya wasifu)
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 11-12
21
20
Kimeidhinishwa na KICD
Maandalizi ya mwalimu
Andaa maelezo mafupi na vidokezo vya insha bora ya wasifu.
Andaa muundo wa insha ya wasifu.
Tafuta au andika insha kielelezo (insha ya wasifu).
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje sifa za mwalimu wao.
Waelekeze katika kujadili vidokezo vya insha bora ya wasifu kama anwani,
muundo, mpangilio wa mawazo, hati, saru, uakishaji, saru na ubunifu.
Waongoze wanafunzi katika kuandika hoja hizo kwenye daari.
Waambie wanafunzi waandike insha ya wasifu kuhusu Mlezi Wangu.
Washirikishe katika kutumia vidokezo vilivyoteuliwa katika Kitabu cha
Mwanafunzi.
Hitimisho: Hitimisha kwa kumwuliza mwanafunzi mmoja asimame mbele ya
wanafunzi darasani na kuwasomea wanafunzi wenzake insha aliyoandika.
Saru
Aina za maneno
Nomino
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 12-14
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika kundi la maneno na sentensi.
2. Kueleza maana ya nomino.
3. Kutunga sentensi sahihi akitumia nomino.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino kati ya maneno mengine.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia
nomino zinazohusu nyumbani.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika kueleza nomino ni nini.
21
20
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wasikilize mwalimu akisoma kifungu kilicho na nomino.
Wanafunzi waandike nomino zinazohusu nyumbani.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 12-14
Chati yenye nomino
Michoro
Vifaa halisi kama: saa, kijiko, mchi, mwiko, kiti na meza
Mti maneno
Maandalizi ya mwalimu
Soma maelezo yaliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Waambie wanafunzi waje na vifaa halisi vya nyumbani kama: vijiko, vikombe
na sahani.
Andaa chati yenye nomino.
Tafuta michoro.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaonyesha wanafunzi michoro ya nomino
mbalimbali kama: bilauri, ua, lango, mchi au kinu.
Waelekeze katika kutambua majina ya michoro hiyo. Waeleze kuwa majina ni
nomino.
Waongoze wanafunzi katika kutazama mti maneno kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi. Washirikishe ili wasome maneno kwenye mti maneno huo.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu. Waambie watazame
michoro iliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 13.
Waambie wanafunzi waelezane wanachoona kwenye michoro hiyo.
Wasomee wanafunzi kifungu hiki:
Hili ni darasa letu. Mwalimu ameingia darasani. Yeye anaitwa Mutiso. Mwalimu
anafundisha Kiswahili. Anafundisha kwa tabuleti.
Waambie wanafunzi waandike kifungu hicho kisha uwaelekeze katika
kutambua nomino katika kifungu hicho.
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaambie
wajadiliane maana ya nomino na watambue nomino katika kifungu
ulichowasomea.
Hitimisho: Hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wakienda nyumbani wataje
na wachore vitu vinavyopatikana huko.
23
22
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 14-15
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika kundi la maneno.
2. Kutumia nomino katika sentensi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi ashirikiane na wanafunzi wenzake kutoa mifano ya nomino.
Mwanafunzi aweze kutunga sentensi sahihi akitumia nomino.
Kusambaza nomino mtandaoni ili wanafunzi wenzake wasome nomino hizo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 14-15
Chati ya nomino
Michoro na picha za nomino
Tarakilishi au rununu
Maandalizi ya mwalimu
Andaa chati iliyo na nomino.
Tafuta picha na michoro yenye nomino.
Hakikisha kwamba una tarakilishi au tabuleti au rununu.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaomba wanafunzi kutaja nomino walizosoma hapo
awali.
Waelekeze katika kutazama kapu maneno lililo kwenye kitabu na kusoma
maneno kwenye kapu hilo.
Waongoze katika kutambua nomino katika kapu maneno.
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie wasome
kifungu kilicho kitabuni.
Washirikishe katika kutambua nomino katika kifungu walichosoma.
Waongoze katika kutunga sentensi wakitumia nomino za vitu vya nyumbani
kama: mboga, godoro, shuka, bakuli, kijiko, kabati, uwanja na ua. Kwa mfano:
Bakuli imewekwa ndani ya kabati.
Waongoze wanafunzi kuchora vifaa vya nyumbani kwenye daari na
kuandika majina ya vifaa hivyo.
23
22
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: Unaweza kuteua mwanafunzi mmoja mmoja ili asimame mbele ya darasa
na kuwaonyesha wenzake michoro yake. Wape wanafunzi kazi mradi kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi.
Vitenzi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 15-16
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya vitenzi ili kuvitofautisha na aina nyingine za maneno.
2. Kutambua vitenzi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia vitenzi ipasavyo katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Wanafunzi wajadili vitenzi mbalimbali.
Mwanafunzi atambue vitenzi katika maneno na sentensi.
Wanafunzi waandike vitenzi.
Wanafunzi wasome vitenzi mbalimbali.
Wanafunzi waigize vitendo mbalimbali.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 15-16
Michoro
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 15-16
Tafuta michoro yenye vitenzi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi baadhi ya vitendo wanavyofanya.
Waambie watazame michoro katika kitabu cha wanafunzi wakiwa
wawiliwawili.
Waongoze kujadili vitendo vya watu kwenye michoro. Wanaweza kujibu:
Nyanya ameketi. Msichana anaandika. Mvulana amesimama. Baba anasoma
gazeti. Mama anapika chakula.
Waeleze kuwa maneno ya vitendo kama ameketi, anaandika, amesimama,
anasoma, anapika ni vitenzi.
25
24
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kutambua vitenzi katika sentensi za zoezi la,
ukurasa wa 16. Watambue vitenzi vifuatavyo:
1. anaandika
2. alifagia
3. amesimama
4. anafyeka
5. analilia
6. ameinjika
Waambie waandike vitenzi hivyo kwenye madaari yao.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi ya ziada ya kuandika vitenzi
kumi kwenye tarakilishi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 16-17
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vitenzi kutoka kwa maneno mengine.
2. Kutunga sentensi sahihi akitumia vitenzi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atunge sentensi sahihi akitumia vitenzi.
Wanafunzi watambue vitenzi kati ya maneno waliyopewa.
Wanafunzi wapige taipu vitenzi kwenye tarakilishi na kuvisambaza kupitia
mtandao wa intaneti.
Nyenzo
Kadi za maneno yenye vitenzi
Kitabu cha Mwanafunzi
Tarakilishi
Kadi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 16-17
Andaa kadi za vitenzi
Tafuta tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwatolea kadi za vitenzi ili wasome wakiwa
wawiliwawili.
Waongoze wanafunzi katika kusoma maneno yaliyo kwenye kadi wakiwa
wawiliwawili.
25
24
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze kutambua vitenzi kati ya maneno waliyosoma kwenye kadi.
Waelekeze katika kutunga sentensi fupi wakitumia vitenzi walivyotambua.
Waongoze katika kutunga sentensi wakitumia vitenzi vilivyo katika kitabu cha
wanafunzi.
Washirikishe wanafunzi katika kupiga taipu sentensi walizotunga kwenye
tarakilishi kwa zamu.
Waelekeze wanafunzi katika kusambaza sentensi walizotunga kwenye
mtandao wa intaneti.
Waambie wajaze mapengo katika sentensi zilizo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 17 kwa kuchagua jibu sahihi.
Wagawe wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi wannewanne ili washiriki
katika kuigiza vitenzi vinavyohusiana na nyumbani. Majibu ya zoezi la 2,
ukurasa wa 17
1. alipika
2. amesuka
3. ametaga
4. alijenga
5. alifua
6. ameoka
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kutaja kikundi kilichoigiza
vyema. Unaweza ukawatuza wanafunzi kwa kuwapigia mako au kwa zawadi.
Vivumishi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa17-18
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kivumishi ili kukitofautisha na aina nyingine za maneno.
2. Kutambua vivumishi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia vivumishi kutunga sentensi sahihi.
4. Kuandika aya fupi akieleza kuhusu mchoro kwa kutumia vivumishi sahihi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Wanafunzi wajadili vivumishi ni nini.
Mwanafunzi atambue vivumishi katika sentensi na kifungu.
Wanafunzi waandike aya fupi wakitumia vivumishi.
27
26
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 17-18
Michoro
Vifaa halisi: chaki, kalamu, kitabu n.k.
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi
kabla ya kipindi.
Tafuta michoro ya vivumishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wewe ni mrefu au mfupi.
Waulize kuhusu rangi ya vifaa vya darasani kama: ubao, kuta, meza na vitabu.
Waongoze wanafunzi katika kutazama michoro iliyo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 17-18 wakiwa wawiliwawili. Wanafunzi wawaambie
wenzao wanachoona kwenye michoro husika.
Waulize michoro hiyo ina sifa gani? Wanafunzi watoe majibu kama vile:
(a) Msichana huyu ni mrefu.
(b) Mvulana huyu ni mfupi.
(c) Hicho ni kiti chekundu.
(d) Paka huyu ni mweupe.
(e) Huo ni mpira mweusi.
(f) Mkoba huu ni mwepesi.
Waelekeze katika kufahamu kuwa maneno kama mweupe, mweusi,
chekundu, mwepesi, mfupi na mrefu ni vivumishi. Vivumishi hueleza sifa
kuhusu nomino au kiwakilishi cha nomino.
Waongoze wanafunzi katika kutambua vivumishi katika sentensi zilizo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 18.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 18
1. kizuri
2. jeusi
3. nyepesi
4. kubwa
5. ndefu
Hitimisho: Kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi kuwa wakienda nyumbani
watazame na waandike nyumba yao ina sifa gani. Waambie waeleze vitu vilivyo
nyumbani kwao vina sifa gani.
27
26
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 19-20
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vivumishi katika kundi la maneno na sentensi.
2. Kutumia vivumishi ipasavyo katika sentensi na kifungu.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Wanafunzi watambue vivumishi katika kundi la maneno.
Wanafunzi watunge sentensi sahihi wakitumia vivumishi.
Wanafunzi waandike kifungu kifupi wakitumia vivumishi ifaavyo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 19-20
Mti maneno
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Tafuta michoro mwafaka ya vivumishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi iwapo darasa lao ni kubwa au
dogo. Kubali majibu yoyote ya wanafunzi mradi yawe sahihi.
Waelekeze katika kusoma maneno yaliyo kwenye mti maneno katika Kitabu
cha Mwanafunzi, ukurasa wa 19 wakiwa watatuwatatu.
Waongoze kutambua vivumishi kwenye mti maneno huo. Wanaweza
kutambua vivumishi kama vile: kikubwa, mzuri, mifupi, vibaya, nyekundu,
kirefu na chembamba.
Washirikishe wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia vivumishi walivyopewa
katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 19. Pia, wape fursa ya kushiriki katika
shughuli ya kikundi inayohusu kwelezana maana ya vivumishi.
Waambie watazame mchoro ulio katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 20. Waulize wanachoona katika mchoro huo. Wanaweza kusema: kijana
aliyevaa suti nzuri. Amevaa shati lenye mauamaua na tai nyeusi. Ana viatu
vyeusi. Amevaa miwani. Ana bahasha kwenye mkono wake wa kulia na mkono
wa kushoto ameshika rununu.
Hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie wakiwa nyumbani
waulize mzazi au mlezi maswali yaliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Tathmini kazi
hiyo baadaye. Wanaweza kujibu: jiko jeusi, meza ndogo, kinu kirefu, vitabu vizuri na
mbwa mkali.
29
28
Kimeidhinishwa na KICD
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutumia aina mbalimbali za maamkuzi na maagano katika mawasiliano.
2. Kutumia kamusi ipasavyo kutafuta maana za maneno ili kukuza msamiati wake.
3. Kuandika insha ya masimulizi akizingatia mada, ujumbe, mtindo na muundo
ufaao.
4. Kutumia viwakilishi ipasavyo katika sentensi.
5. Kutumia vielezi ipasavyo katika sentensi.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa kupitia wanafunzi kushirikiana katika maigizo ya
maamkuzi na maagano wakiwa darasani au nyumbani.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Huu unakuzwa kupitia matumizi ya vifaa vya kidijitali kama: tarakilishi, rekoda,
vinasasauti na runinga wakati wa kujifunza.
NIDHAMU MEZANI
2
Utangulizi
Nidhamu ni adabu, kuwa na heshima na ustaarabu. Nidhamu mezani ni kuwa na
adabu wakati wa kula chakula au kunywa vinywaji mbalimbali. Nidhamu mezani
inaonyesha kuwa mtu anafanya mambo yanayostahili wakati wa kiamshakinywa,
chamcha, chajio au wakati wowote ule. Kuna mambo ambayo yamekubaliwa na
mengine yamekatazwa ili kufanikisha nidhamu mezani. Kwa mfano, usiongee
unapokula, pakua kiasi cha chakula unachohitaji, unapotaka kupewa kifaa mezani,
itisha kifaa hicho kutoka kwa aliye karibu nacho.
Sehemu ya nidhamu mezani imeshughulikiwa katika mada ndogo tano. Mada hizo
ni: maamkuzi na maagano, matumizi ya kamusi, kuandika insha ya masimulizi na
saru kuhusu viwakilishi na vielezi.
29
28
Kimeidhinishwa na KICD
(ch) Kujiamini
Kupitia kutumia maamkuzi na maagano ipasavyo, wanafunzi watakuwa na
ujasiri wa kuzungumza na watu kwa kuanza na kuwaamkua kwanza.
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Elimu ya amani
Wanafunzi wanajifunza kuishi na wenzao nyumbani na hata kutangamana kwa
amani kwa kusalimiana na kuagana ipasavyo.
(b) Umoja wa kijamii
Huu unakuzwa wanafunzi wanapotumia maamkuzi na maagano ipasavyo.
Uhusiano na maadili
(a) Heshima upendo na umoja ni maadili yanayokuzwa na kuimarishwa kupitia
maamkuzi na maagano sahihi.
Uhusiano na masomo mengine
Somo kuhusu nidhamu mezani linaingiliana na masomo mengine kama vile English
na Indigenous Languages kwa kuwa masomo haya yana sehemu zinazofunza kuhusu
maamkuzi.
Shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji.
Wanafunzi wahamasishane kuhusu jinsi ya kuamkuana, kuagana na umuhimu wa
maamkuzi na maagano.
Utangulizi
Waelekeze wanafunzi kutazama picha katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 21.Tena mwanafunzi mmoja asimame mbele ya darasa na awaambie
wenzake ameona nini katika picha hiyo.
Waongoze wanafunzi kueleza watu walioona kwenye picha hiyo wanafanya
nini.Wanafunzi wanaweza kutoa majibu kama vile: wanakunywa chai au
wanakula mkate.
Wakirishe wanafunzi kwa kuwauliza wanakiria familia hiyo inakula na
kunywa saa ngapi? Waambie wathibitishe kutoka kwa picha.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Wanafunzi walio na changamoto au udhaifu wa viungo vya mwili wanaweza kupewa
vifaa vya kidijitali vya kisasa ambavyo vinaweza kushughulikia mahitaji yao. Pia,
wanafunzi kama hawa wanaweza kuongezewa muda wakati wa kufanya shughuli au
kupewa shughuli mbadala.
31
30
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi walio na ndaro ya kusikia wanaweza kushauriwa waketi karibu na mwalimu.
Inapendekezwa mwalimu atumie lugha ya ishara inapobidi ili kuwasiliana na wanafunzi
wenye upungufu wa kusikia. Hata hivyo, lugha ishara itumiwe kwa uangalifu ili
isiwapotoshe wanafunzi. Vilevile unapotumia nyenzo, unashauriwa utumie vifaa halisi
ambavyo wanafunzi wanavielewa.
Kuna wanafunzi walio na changamoto ya kuona. Kuna wale ambao wana uwezo
wa kuona kiasi na kuna wale wasioona kabisa. Wale ambao wana uwezo wa kuona
kiasi, wanaweza kuhimizwa kukaa karibu na ubao ama mbali na ubao kutegemea
changamoto yake. Unashauriwa kuepuka nyenzo ambazo zinatatiza uwezo wa
wanafunzi wa kuona. Unaweza ukapendekeza kwa wazazi wa watoto walio na uwezo
wa kuona kiasi, wawapeleke kwa daktari wa macho ili wapimwe. Daktari anaweza
kushauri wavae miwani. Kwa wanafunzi wasioona kabisa, inapendekezwa wawe na
breli Wanafunzi hawa waongezewe muda zaidi wa kufanya shughuli darasani. Katika
tathmini kuwe na ukadiriaji unaozingatia mahitaji maalumu ya mwanafunzi.
Kuna wanafunzi mahiri darasani ambao wana kasi ya kufanya shughuli au zoezi kwa
upesi kuliko wengine. Hawa pia wanahitajika kushughulikiwa. Wanafunzi hawa huelewa
dhana, mada au jambo kwa haraka. Wanafunzi hawa wanapaswa kupewa shughuli za
ziada. Hakikisha una kazi ya ziada katika kila kipindi ili kuwashughulikia walio hodari
zaidi darasani. Wanafunzi hawa huhitaji kupewa shughuli ambazo ni pevu kuliko
wengine. Mwalimu awahimize kutia bidii kwa kuwapa kazi ya ziada. Mwalimu
anapaswa kutambua talanta za wanafunzi wake darasani. Waongoze kukuza talanta
zao ili wafanikiwe maishani.
Kusikiliza na kuzungumza
Maamkuzi na maagano
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 22-23
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua aina za maamkuzi na maagano katika mawasiliano.
2. Kutumia maamkuzi na maagano katika miktadha mbalimbali.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Wanafunzi wasome maamkuzi na maagano.
31
30
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wajibu maamkuzi na maagano.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua maamkuzi kwenye vifaa vya
kidijitali.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika mjadala kuhusu maamkuzi na
maagano.
Wanafunzi watazame, wazungumze na wajibu maamkuzi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 22
Michoro ya maamkuzi na maagano mbalimbali
Picha
Video ya maamkuzi
Rununu au tarakilishi
Kanda za sauti
Kinasasauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi.
Tafuta vifaa vya kidijitali kama: rununu au tarakirishi.
Rekodi maamkuzi na maagano.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaamkua wanafunzi darasani. unaweza ukawaambia
wanafunzi: Hamjambo? Wanafunzi nao wajibu: Hatujambo.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma maamkuzi kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 22.
Waonyeshe video ya watu wakiamkuana katika miktadha mbalimbali kama:
nyumbani, shuleni au hospitalini.
Washirikishe katika kuigiza maamkuzi hayo wakiwa wawiliwawili darasani.
Waongoze katika kuamkuana na kuagana kulingana na nyakati na miktadha
mbalimbali. Kwa mfano: makiwa, alamsiki, habari ya asubuhi? Habari ya
jioni? Umeamkaje? Umelalaje?
Wanafunzi waigize kuamkuana kulingana na umri. Kwa mfano: Shikamoo?
Marahaba.
Waelekeze wanafunzi katika kuambatanisha maamkuzi na maagano pamoja
na majibu yake kwa kutumia tarakilishi.
33
32
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 22-23
1. Tathmini majibu ya wanafunzi.
2. Habari yako raki?
3. Kwaheri.
4. (a) Shikamoo?__Marahaba
(b) Hamjambo?__Sijambo
(ch) Habari yako?__Njema
(d) U hali gani?__Nzuri/Njema
(e) Alamsiki?__Binuru
Hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wawaamkue wazazi au walezi wao
wakika nyumbani. Pia, waambie wawaage wazazi au walezi wao kutoka nyumbani
wakija shuleni. Mwisho, waambie wawaage wanafunzi wenzao kwa kuwaambia:
kwaheri nao wajibu: kwaheri ya kuonana.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 23-24
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutumia maamkuzi na maagano katika mawasiliano ipasavyo.
2. Kueleza namna maamkuzi na maagano hutumika katika miktadha mbalimbali.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kuamkuana.
Kuagana.
Kujadili maamkuzi na maagano.
Kushiriki maamkuzi na maagano.
Kutazama video ikionyesha watu wakiagana na kuamkuana.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 23-24
33
32
Kimeidhinishwa na KICD
Michoro
Video iliyo na maamkuzi na maagano
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kumwita mwanafunzi mmoja aje mbele ya
darasa na kuwaamkua wenzake kisha awaage kabla ya kuketi.
Wagawe wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili.
Waelekeze katika kuigiza maamkuzi na maagano kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 23.
Wateue wanafunzi wawili ili waje mbele ya darasa na kuwaambia wenzao
maamkuzi na maagizo waliyoigiza hutumika wakati gani.
Waongoze kutazama video iliyo na maamkuzi na maagano. Waulize
wanafunzi walichosikia na kuona kwenye video. Waulize watu wanapoagana
wanatumia maneno gani. Wanaweza kutaja maneno kama: kwaheri, alamsiki
na makiwa.
Wagawe wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu ili wajadili maagano
yaliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi hutumika wakati gani. Wanaweza
kutoa majibu kama vile:
(a) Alamsiki- usiku
(b) Makiwa- wakati mtu amewa
(c) Kwaheri- wakati wowote wakiagana
(d) Lala unono- usiku
Hitimisha kwa kuwaambia wanafunzi wawaage wanafunzi wenzao wakitoka shuleni
wakienda nyumbani.
Kusoma
Ufahamu
Matumizi ya kamusi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 24-25
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
35
34
Kimeidhinishwa na KICD
1. Kueleza maana ya kamusi ili kuitofautisha na vitabu vingine.
2. Kutumia kamusi ipasavyo kutafuta maana za maneno
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Wanafunzi kujadiliana maana na matumizi ya kamusi.
Kutumia kamusi kutafuta maana za maneno.
Kushirikiana kutafuta maana za maneno katika kamusi.
Nyenzo za ufunzaji na ujifunzaji
Kamusi ya kawaida
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 24-25
Maandalizi ya mwalimu
Kutafuta kamusi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza somo kwa kuja na kamusi darasani kisha uwaulize
wanafunzi umebeba nini.
Waongoze wanafunzi katika kujadili kamusi ni nini. Waulize watoe kamusi
kwenye mikoba yao.
Washirikishe wakiwa wawili wawili katika kusoma makala kuhusu matumizi
ya kamusi kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Waongoze katika kueleza kamusi ni kitabu cha aina gani.
Washirikishe katika kujadili matumizi ya kamusi kama vile: kutafuta maana
ya maneno, kuonyesha aina za maneno na kuonyesha matumizi ya maneno
katika sentensi.
Waambie wanafunzi wataje aina za maneno yanayopatikana kwenye
kamusi. Wanafunzi wataje: nomino, kivumishi, kiwakilishi, kitenzi, kielezi,
kiunganishi, kihisishi ama kihusishi.
Unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi maneno ambayo
watatafuta maana yake kwenye kamusi.
Wape maneno yafuatayo:
i. Nidhamu
ii. Kamusi
iii. Alamsiki
iv. Shikamoo
v. Maamkuzi
vi. Kwaheri
35
34
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 25-26
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutumia kamusi ipasavyo kutafuta maana za maneno.
2. Kupanga maneno namna yanavyotokea kwenye kamusi.
3. Kutumia mtandao kusikiliza na kusoma maana za maneno.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma maneno na maana yake kwenye kamusi.
Kupanga maneno jinsi yanavyofuatana katika kamusi.
Kutafuta maana ya maneno kwenye kamusi ya mtandao.
Nyenzo za ufunzaji
Kamusi ya kawaida
Tarakilishi, tabuleti au rununu
Kamusi ya mtandao
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 25-26
Mchoro wa kamusi
Maandalizi ya mwalimu
Tafuta kamusi ya kawaida.
Tafuta tarakilishi, tabuleti au rununu.
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi waeleze maana
ya maneno uliyowapa waangalie kwenye kamusi katika kipindi kilichopita
kuhusu kamusi. Wanafunzi wawaeleze wenzao darasani kwa kuzungumza.
Waelekeze wanafunzi katika kutazama ukurasa wa kamusi katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 25.
Wanafunzi washirikiane wakiwa wawiliwawili katika kusoma maneno yaliyo
kwenye ukurasa huo.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma maelezo ya maneno yaliyo kwenye
ukurasa wa kamusi hiyo.
37
36
Kimeidhinishwa na KICD
Waambie watazame picha iliyo kwenye ukurasa wa kamusi hiyo. Waongoze
kueleza inahusu nini na iwapo imechorwa vizuri.
Waambie wanafunzi wasimuliane kuhusu namna ya kula kwa nidhamu.
Waelekeze katika kuandika yale waliyowasimulia wenzao. Hiyo ni insha ya
masimulizi.
Unaweza kuhitimisha kwa kuwaambia wanafunzi wasimuliwe kisa fulani
nyumbani na mzazi au mlezi kisha wawasimulie wenzao darasani. Hatimaye,
waandike masimulizi hayo kwenye daari
Kuandika
Insha ya masimulizi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 27-29
Kipindi cha 1
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
2. Kuandika insha ya masimulizi akizingatia ujumbe, mada, mtindo na muundo
ufaao.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma masimulizi.
Kueleza masimulizi.
Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
Kuandika insha ya masimulizi.
Kusikiliza maelezo ya insha ya masimulizi.
Kuandika vidokezo vya insha ya masimulizi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 27
Insha za masimulizi
Tarakilishi
Kanda za sauti kuhusu insha ya masimulizi
Michoro
37
36
Kimeidhinishwa na KICD
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Tafuta mifano ya insha za masimulizi.
Uwe na tarakilishi.
Andaa kanda ya sauti kuhusu insha ya masimulizi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame picha iliyo katika
Kitabu cha Mwanafunzi kisha waambiane wanachoona wakiwa katika vikundi
vya wawiliwawili.
Waongoze kujadiliana kuhusu wanachoona kwenye picha kisha waandike
walichoambiana ndani ya madaari yao
Waulize wanafunzi waeleze jinsi wanavyoshiriki chakula cha jioni nyumbani
kwao. Wanafunzi watoe masimulizi hayo wakiwa wawiliwawili. Mmoja aende
mbele ya darasa na asimulie wengine wakisikiliza.
Kipindi cha 2
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kujua jinsi ya kuandika insha ya masimulizi.
2. Kuandika insha ya masimulizi akizingatia ujumbe, mada, mtindo na muundo
ufaao.
3. Kuwasomea wenzake insha yake ya masimulizi.
4. Kuandika insha ya masimulizi kwenye tarakilishi.
5. Kuhifadhi insha ya masimulizi kwenye tarakilishi.
6. Kusambaza insha aliyoandika kupitia mtandao wa intaneti.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma masimulizi.
Kueleza masimulizi.
Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
Kuandika insha ya masimulizi.
Kusikiliza maelezo ya insha ya masimulizi.
Kuandika vidokezo vya insha ya masimulizi.
39
38
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 28-29
Insha za masimulizi
Tarakilishi
Kanda za sauti kuhusu insha ya masimulizi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Tafuta mifano ya insha za masimulizi.
Uwe na tarakilishi.
Andaa kanda ya sauti kuhusu jinsi ya kuandika insha ya masimulizi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwagawa wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili
ili wasome mfano wa insha ya masimulizi kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 28.
Waombe wanafunzi kuambiana masimulizi waliyosoma yanahusu nini.
Wape wanafunzi fursa ya kuandika kwenye madaari yao kuhusu jinsi
wanavyoshiriki chakula cha jioni.
Washirikishe wanafunzi katika kusikiliza maelezo kuhusu insha ya masimulizi
kwa kutumia kanda ya sauti. Maelezo ya insha ya masimulizi yazingatie
yafuatayo:
Maana ya insha ya masimulizi
Kusimulia ni kutoa habari au maelezo kuhusu jambo au tukio fulani. Insha ya
masimulizi ni insha inayoeleza namna tukio, jambo ama kisa kilivyotokea. Kisa
kinaweza kuwa cha ukweli au cha kubuni. Hata kama kisa ni cha ukweli, ni
muhimu kiwe na ubunifu ili kimvutie msomaji.
Insha ya masimulizi huwa na muundo ufuatao:
i. Kichwa- hutokana na mada. Kichwa kiwe chenye mvuto na kiwe na maneno
machache aghalabu yasiyopita sita. Kichwa huandikwa kwa heru kubwa na
kupigiwa mstari.
ii. Utangulizi - hueleza kisa kinahusu nini. Utangulizi huandikwa kwa njia ya
kumvutia msomaji kuendelea kusoma kisa. Wahusika wakuu hutajwa.
iii. Mwili - katika sehemu hii kisa huelezwa vizuri na kwa mpangilio mwafaka.
Lugha inayoeleweka, rahisi na yenye mvuto hutumiwa. Wahusika hutengana
katika mandhari iliyoelezwa vizuri. Tamathali za usemi hutumiwa.
iv. Hitimisho - msimulizi hutoa muhtasari wa kisa katika aya ya mwisho.
Hitimisho linaweza kutoa funzo fulani kwa msomaji.
39
38
Kimeidhinishwa na KICD
Waulize wanafunzi wamesikiliza nini kwenye kanda uliyowafungulia.
Wanafunzi watoe hoja za insha ya masimulizi kwa muhtasari.
Gawa wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi watatuwatatu kisha uwaelekeze
katika kusoma vidokezo kumi vilivyoorodheshwa kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 29.
Waambie wapange vidokezo hivyo kumi kwa utaratibu mwafaka.
Agiza kila mwanafunzi aandike insha ya masimulizi kuhusu jinsi ya kuwa na
adabu mezani kutokana na vidokezo kumi alivyopanga ipasavyo.
Teua mwanafunzi mmoja mmoja ili aje mbele ya wanafunzi wengine darasani
na awasomee insha ya masimulizi aliyoandika.
Waambie wanafunzi waandike insha zao kwenye tarakilishi na wazihifadhi
humo.
Waelekeze wanafunzi katika kusambaza insha ya masimulizi waliyoandika
kwenye mtandao wa intaneti kwa wenzao na wakutumie nakala.
Hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi waandike insha ya masimulizi
kuhusu tukio lililotendeka nyumbani kwao wakiwa nyumbani.
Saru
Aina za maneno
Viwakilishi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 30
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kiwakilishi ili kukibainisha ipasavyo.
2. Kutambua viwakilishi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia viwakilishi ipasavyo katika sentensi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua viwakilishi katika kundi la maneno na sentensi.
Kueleza viwakilishi ni nini.
Kutunga sentensi akitumia viwakilishi.
41
40
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 30
Tarakilishi
Chati
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Andaa chati ya sentensi zenye viwakilishi.
Andaa tarakilishi za kutumika darasani.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwaambia wanafunzi wataje majina
yao kisha watunge sentensi wakitumia majina hayo.
Waelekeze wanafunzi kusoma sentensi zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 30.
Waongoze wanafunzi katika kutambua viwakilishi katika sentensi
walizosoma.
Waeleze maneno yaliyokolezwa rangi kwenye sentensi hizo yanatumika
badala ya nomino. Waulize iwapo wanajua maneno hayo huitwaje.
Waelekeze katika kutumia maneno mengine badala ya yale yaliyokolezwa
rangi.
Kipindi cha 2
Tanguliza kipindi kwa kuwagawa wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili
ili wasome maneno yaliyo kwenye mti maneno.
Waambie waandike viwakilishi vyote vilivyo kwenye mti maneno huo.
Waambie wanafunzi watunge sentensi sahihi wakitumia viwakilishi
walivyoandika hapo juu. Hakikisha kuwa wanafunzi wanatunga sentensi
sahihi.
Washirikishe katika kutunga sentensi wakitumia viwakilishi walivyotambua.
Waelekeze katika kupiga taipu na kuhifadhi sentensi walizotunga kwenye
tarakilishi.
Waambie wasambaze sentensi hizo kwenye mtandao kwa wanafunzi wenzao.
41
40
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 31
1. Sisi
2. Wewe
3. Ye y e
4. Wao
5. ki
6. a
7. li
Unaweza kuhitimisha mada hii kwa kuwapa wanafunzi sentensi zenye
nomino na wazigeuze ziwe na viwakilishi. Wape wanafunzi zoezi hili:
Tumia kiwakilishi mwafaka badala ya nomino katika sentensi zifuatazo
1. Kiti kimevunjika.
2. Verisa anasoma kwa bidii.
3. Wanafunzi wataka kesho.
4. Watoto hula kwa adabu.
5. Chungu kitaletwa kesho.
Vielezi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 32-33
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho mwa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kielezi ili kukibainisha.
2. Kutambua vielezi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia vielezi ipasavyo katika mawasiliano.
4. Kuonea fahari matumizi ya vielezi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kueleza maana ya kielezi.
Kutambua vielezi katika sentensi.
Kutunga sentensi akitumia vielezi.
Kujaza mapengo wakitumia vielezi mwafaka.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 32-33
Michoro
43
42
Kimeidhinishwa na KICD
Chati ya vielezi
Video ya watu wakifanya vitendo kwa namna tofauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Tafuta video ya watu wakifanya vitendo kwa namna tofauti.
Andaa michoro ya kufafanua vielezi.
Andaa chati yenye vielezi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuingia darasani polepole. Waulize
wanafunzi umeingia darasani kwa namna gani. Wanafunzi wanaweza kusema
polepole au kimya. Kubali jawabu lolote sahihi.
Waambie wanafunzi watazame picha zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 32 wakiwa wawiliwawili. Mwanafunzi amwambie mwenzake
namna swara anavyokimbia na kobe anavyotembea. Wanaweza kusema:
swara anakimbia haraka, mbio, kasi au sana. Kobe anatembea polepole.
Waulize namna vitabu vimepangwa na namna meza imepangwa.
Waambie wanafunzi kuwa: vizuri, vibaya, mno, polepole na haraka ni
vielezi. Waeleze kuwa vielezi ni maneno yanayotoa habari kuhusu vitenzi,
vivumishi ama vielezi vingine.
Waelekeze wanafunzi kusoma vilelezi kwenye chati utakayokuwa
umetayarisha na kuingia nayo darasani. Wape nafasi ya kutunga sentensi
wakitumia vielezi hivyo. Vielezi hivi viwe: jana, sana, haraka, jikoni, vizuri.
Waongoze wanafunzi kujaza mapengo kwenye sentensi katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 33 wakitumia vielezi mwafaka.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 33
1. vizuri
2. sebuleni
3. haraka
4. jikoni
5. kisheria
Waonyeshe wanafunzi video ya watu wakifanya vitendo kwa namna tofauti
na mahali mbalimbali. Video hii inaweza kuwa ya watu: kulima shambani,
kutembea polepole, kukimbia kasi au kula taratibu.
Waelekeze katika kutunga sentensi wakitumia vielezi walivyotambua.
43
42
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisha kwa kuwapa zoezi au shughuli katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 33. Baadaye pitia kazi yao na uhakiki majibu yao.
Kipindi cha 2
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vielezi katika kundi la maneno na sentensi.
2. Kutumia vielezi ipasavyo katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kuandika vielezi.
Kutambua vielezi kwenye kapu maneno.
Kusoma sentensi zenye vielezi.
Kutunga sentensi zilizo na vielezi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 34-35
Kapu maneno
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi ili kujiandaa ipasavyo.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza somo kwa kuwaelekeza wanafunzi wakiwa wawiliwawili, kusoma
maneno yaliyo kwenye kapu maneno katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waongoze kutambua vielezi kwenye kapu la maneno na uwaambie waandike
vielezi hivyo kwenye daari.
Waelekeze katika kutunga sentensi wakitumia vielezi walivyotambua na
kuandika katika daari.
Teua mwanafunzi mmoja asimame mbele ya wanafunzi darasani. Mwambie
awasomee wanafunzi wenzake darasani. Wanafunzi watathmini sentensi hizo,
wanaweza kusema ni sahihi, si sahihi ama kurekebishana.
Washirikishe wanafunzi katika kuigiza vitendo vya zoezi la 3. Wanafunzi
waigize vitendo hivi darasani wanafunzi wengine wakitazama.
Washirikishe wanafunzi katika kutambua vielezi katika sentensi.
45
44
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 34
1. sana
2. jana
3. taratibu
4. polepole
5. vizuri
6. harakaharaka
Hitimisha kipindi hiki kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Kazi mradi
inahusu kutazama vitendo vya wazazi au walezi wao nyumbani wakati
wa kula chajio kisha kueleza wazazi au walezi wao wanafanyaje vitendo
mbalimbali.
45
44
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Hakikisha umeandaa nyenzo mwafaka ili kufanikisha shughuli ya ufunzaji na ujifunzaji
wa mada ya mavazi. Unaweza kutumia nyenzo zifuatazo:
Vifaa halisi: sare, shati, blauzi, kaptura na sweta.
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, vipakatalishi, tabuleti, rununu na projekta
Kinasasauti
Redio
Mtandao
Picha
Michoro
Chati
Kadi maneno
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
Miti maneno
MAVAZI
3
Utangulizi
Vazi ni kitu kinachovaliwa mwilini. Mavazi huvaliwa ili kufunika mwili wa binadamu.
Mavazi hutumiwa kujikinga kutokana na baridi, joto au mvua. Mavazi yanaweza
kutumiwa kuonyesha mtu yuko katika kundi fulani katika jamii. Kwa mfano, wanaovaa
kilemba hujitambulisha na dini fulani. Jezi huvaliwa na timu ya mpira kujitambulisha.
Kuna mavazi ya aina mbalimbali kama vile: kaptura, boshori, kizibao, njuti na sidiria.
Kuna mavazi yanayovaliwa na wanawake na kuna yale ambayo huvaliwa na wanaume.
Mavazi huvaliwa kutegemea hali ya mazingira. Mavazi mepesi kama fulana huvaliwa
wakati wa joto ilhali mavazi mazito kama sweta huvaliwa wakati wa baridi.
Sehemu ya mavazi imeshughulikiwa katika mada sita. Mada hizo ni: matamshi bora
(vitendawili), kusoma kwa ufahamu, kuandika kwa kutumia tarakilishi, viunganishi,
vihusishi na vihisishi.
Mada hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutega na kutegua vitendawili ili kujenga matamshi bora.
2. Kusoma kifungu kuhusu mavazi kwa ufasaha ili kupata ujumbe uliolengwa.
3. Kuandika kuhusu mavazi kwa kutumia tarakilishi.
4. Kutumia viunganishi, vihusishi na vihisishi kwa njia sahihi katika mawasiliano.
47
46
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mada ya mavazi inakuza umilisi wa kimsingi. Baadhi ya umilisi huo ni:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wafanye mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika vikundi
kama kutega na kutegua vitendawili au kusoma makala kwa pamoja. Mijadala baina
ya wanafunzi kuhusu aina za mavazi na mavazi yepi huvaliwa na nani huimarisha
mawasiliano na kukuza ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi wakisambaza
habari kuhusu mavazi mbalimbali kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi, video,
tabuleti, projekta, intaneti na tovuti mbalimbali ili mwanafunzi ajifunze aina za mavazi,
picha za mavazi, wakati na mahali panapovaliwa mavazi mbalimbali. Mwanafunzi pia
ataweza kutumia tarakilishi kuandika na kuhifadhi kazi yake kuhusu mavazi kwenye
faili.
(ch) Hamu ya Ujifunzaji
Umilisi huu utamsaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
mavazi. Umilisi huu utampa mwanafunzi hamu ya kutega na kutegua vitendawili vipya
katika jamii yake. Pia, atafakari maswali ya ziada mavazi yanayovaliwa na wafanyakazi
mbalimbali kama: nesi, daktari, mekanika na wengine. Mwanafunzi anaweza kuwa na
hamu ya kutaka kutumia vyombo vya kidijitali ili atafute habari zaidi kuhusu mavazi
mbalimbali na asili ya mavazi hayo.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika kuhusu mavazi kwa kutumia
tarakilishi, tabuleti au simu ya mkononi. Pia, ubunifu ukuzwe na kuimarishwa kupitia
kuunda vitendawili vipya kulingana na mazingira na kuvitega ili wanafunzi wenzake
wavitegue. Ubunifu utadhihirika mwanafunzi akifunga na kufungua tarakilishi.
(e) Kujiamini
Umilisi huu unakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kutega na kutegua vitendawili. Pia, kujiamini kunakuzwa kupitia mwanafunzi
kutambua aina za maneno kama: viunganishi, vihusishi na vihisishi.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu unakuzwa kupitia kumpa mwanafunzi swali la kutafakari, kukiria na
kutafuta jawabu lake ambalo halimo kwenye matini. Kwa mfano: mavazi yana umuhimu
gani?
47
46
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Kujitambua na kujithamini
Huku kunadhihirika kupitia kutega na kutegua vitendawili, kutunga sentensi na
kufungua tarakilishi kwa kufuata hatua zote zinazohitajika.
(b) Stadi za maisha
Zinakuzwa kupitia mwanafunzi kujieleza, kushiriki katika vikundi, kuchangia
mijadala na kutunza mavazi yake.
(ch) Uraia
Uraia unakuzwa kwa kufanya kazi pamoja na kuwaheshimu watu
(d) Elimu ya maendeleo endelevu
Kupitia ujuzi wa kutumia teknolojia ya kisasa hasa tarakilishi, wanafunzi
wanapata maarifa mengi mapya na wanaweza kuyatumia katika kuleta
maendeleo.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu kupitia kuvaa mavazi yanayostahili.
Ushirikiano kupitia kwa kazi za vikundi, mijadala darasani na kazi mradi
kuhusu mavazi.
Uwajibikaji kupitia mwanafunzi kutunza na kuhifadhi vyombo vya kidijitali
kama tarakilishi.
Shughuli za huduma za kijamii
Kushiriki katika kutunza mavazi.
Kuwahamasisha wenzake nyumbani na shuleni kuhusu umuhimu wa kutumia
teknolojia kama tarakilishi.
Kuwahimiza watu kutumia kanuni za kisaru ili kufaulisha mawasiliano.
Kuwasaidia wasiojiweza katika jamii kwa mavazi.
Uhusiano na masomo mengine
Sehemu hii inaingiliana na masomo mengine kama vile:
1. Science and Technology Activities: inahimiza matumizi ya tarakilishi.
2. English Activities: vitendawili vinazofunzwa ili kukuza stadi ya kusikiliza na
kuzungumza. Stadi za kusoma na kuandika hufunzwa katika English Activities.
Saru, hasa viunganishi, vihusishi na vihisishi hufundishwa.
3. Indigenous Language Activities: vitendawili vinazofunzwa ili kukuza stadi ya
kusikiliza na kuzungumza.
49
48
Kimeidhinishwa na KICD
Jinsi ya Kuwashughulikia Wanafunzi Wenye Mahitaji Maalumu
Mada hii inahusu sehemu nne kuu. Kuna sehemu ya kusikiliza na kuzungumza,
kusoma, kuandika na saru. Kwa somo linalohusu kusoma na kusikiliza, hakikisha
kuwa wanafunzi wasio na uwezo wa kuona wamepata mashine za breli darasani ili
ziwasaidie katika kutambua maneno. Kwa wanafunzi wenye matatizo ya kusikia na
kuzungumza, unaweza kumwalika mfasiri wa lugha ishara ili awasaidie wanafunzi hao
katika kushiriki kwenye somo kikamilifu. Pia, unaweza ukatumia vifaa vya kiteknolojia
kama vile: projekta ili kuwaonyesha wanafunzi baadhi ya picha zinazohusu nyumbani
kutoka mtandaoni. Ili kuwahusisha wanafunzi wenye matatizo katika baadhi ya
viungo vyao vya mwili kama vile, miguu na mikono, hakikisha kuwa wakati wa
kuigiza wanafunzi hawa wameangaliwa ili wasijiumize au kuumizwa kwenye viungo
vilivyoathirika.
Utangulizi
Waelekeze wanafunzi katika kutazama picha kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 36. Waongoze katika kutambua mavazi yaliyo kwenye picha.
Wanafunzi wajadili mavazi hayo huvaliwa na nani. Wanaweza kujibu kwa
kusema: blauzi huvaliwa na wanawake na shati huvaliwa na wanaume.
Washirikishe wanafunzi katika kujadili mavazi wanayovaa. Wanaweza kutaja
mavazi kama vile: rinda, buibui, kizibao, blauzi, suti, shati, sweta, suruali,
kilemba, chupi,viatu, koti, tai na ndara. Kubali majibu yoyote mradi yawe ni
mavazi ya kiwango cha wanafunzi.
Kusikiliza na Kuzungumza
Matamshi bora: Vitendawili
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 36-38
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vitendawili vyenye uradidi kwenye orodha.
2. Kutamka maneno yenye sauti radidi katika vitendawili lengwa.
3. Kutega na kutegua vitendawili vyenye sauti radidi ili kujenga matamshi bora.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue vitendawili vyenye uradidi kwenye orodha.
49
48
Kimeidhinishwa na KICD
Mwanafunzi atamke maneno yenye sauti radidi katika vitendawili.
Mwanafunzi atege na kutegua vitendawili.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 36
Vifaa halisi: yai, mwavuli, kiatu na mshipi
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Michoro
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha na unayostahili kufunza
kuhusu vitendawili.
Soma mwongozo wa mwalimu ili kupata mwelekeo.
Tafuta ama uwaulize wanafunzi waje na vifaa halisi darasani kama vile: yai,
mwavuli, kiatu na mshipi.
Andaa vitendawili vyenye sauti radidi vikishirikisha sauti p/b, t/d, k/g, ch/j na w/y.
Rekodi vitendawili vyenye p/b, t/d, k/g, ch/j na w/y kwenye kanda ya sauti,
tabuleti ama rununu.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi, Kitendawili’. Sikiliza iwapo
watajibu: Tega. Waambie watoe vifaa halisi kama vile: yai, mshipi na mwavuli.
Tega kitendawili: nyumba yangu haina mlango. Waambie wanafunzi wategue
kitendawili hicho kwa kutazama vifaa halisi ulivyo navyo darasani.
Waulize wanafunzi iwapo wanajua kitendawili ni nini. Waongoze katika
kutega na kutegua vitendawili.
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili. Waelekeze kutega na
kutegua vitendawili vilivyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa
38-39. Washirikishe kutambua vitendawili ambavyo majibu yake ni aina za
mavazi. Pia, waongoze kutambua vitendawili ambavyo hutaja aina za mavazi.
Tega vitendawili vilivyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi huku wanafunzi
wakitegua wakiwa darasani.
Wakiwa wanafunzi wawiliwawili, washirikishe katika kusoma kwa zamu
vitendawili kwenye Kitabu cha Mwanafunzi . Waongoze kutambua sauti p/b,
t/d, k/g, ch/j na w/y katika vitendawili walivyosoma.
Waelekeze katika kutegua vitendawili walivyosoma. Majibu yatategemea
mazingira ya jamii ya mwanafunzi. Kubali jibu lenye mantiki.
51
50
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha funzo kwa kuwaambia wanafunzi wakika nyumbani
waulize wazazi au walezi wao watege na kuwategulia vitendawili vitano. Vitendawili
vinaweza kuwa hata katika lugha za kiasili. Mwalimu atafanya juhudi kutafsiri kwa
Kiswahili ili wanafunzi wote wafaidike darasani.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vitendawili vyenye uradidi.
2. Kutamka maneno yenye sauti radidi katika vitendawili.
3. Kutega na kutegua vitendawili vyenye sauti radidi ili kujenga matamshi bora.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue vitendawili vyenye uradidi kwenye orodha.
Mwanafunzi atamke maneno yenye sauti radidi katika vitendawili.
Mwanafunzi atege na kutegua vitendawili.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 38-39
Rununu
Tabuleti
Kanda ya sauti
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha kuhusu vitendawili
utakavyofundisha.
Soma mwongozo wa mwalimu ili kupata mwelekeo.
Andaa vitendawili vyenye sauti radidi vikishirikisha sauti p/b, t/d, k/g, ch/j na w/y.
Rekodi vitendawili vyenye p/b, t/d, k/g, ch/j na w/y kwenye kanda ya sauti au
tabuleti ama rununu.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Mteue mwanafunzi mmoja aje mbele ya wanafunzi wengine darasani.
Mwambie awategee wanafunzi wenzake kitendawili chochote anachojua.
Wanafunzi wategue kitendawili watakachotegewa. Wakishindwa, aliyetega
kitendawili hicho akitegue.
Teua mwanafunzi mwingine ake mbele ya wanafunzi wenzake darasani.
51
50
Kimeidhinishwa na KICD
Mwambie awategee wanafunzi vitendawili vilivyo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi.
Wanafunzi washirikiane katika kujadili majibu ili kutegua vitendawili hivyo.
Kubali majibu yenye matinki.
Panga wanafunzi wawe katika vikundi vya wawiliwawili ili washiriki katika
kutega na kutegua vitendawili vilivyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 38-39. Mmoja atege na mwingine ategue. Kubali majibu ya
wanafunzi kulingana na mazingira ya jamii wanamotoka.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 38-39
1. njia
2. njiti za viberiti
3. kobe
4. yai
Wanafunzi wasikilize kwa makini kanda ya sauti, rununu au tabuleti.
Wasikilize vitendawili vikiteguliwa. Vitendawili ni:
1. Ajifungua na kujifunika. - Mwavuli
2. Bak bandika, bak bandua. - Nyayo
3. Tega nikutegue. - Mwiba
4. Ninakwenda naye na kurudi naye. - Kivuli
5. Chakula kikuu cha mtoto. - Usingizi
Washirikishe wanafunzi katika kutegua vitendawili walivyosikiliza
kwenye kanda ya sauti, tabuleti ama rununu.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha funzo kwa kuwauliza wanafunzi vitendawili vina
umuhimu gani. Wanaweza kujadili nje ya darasa wakati wa kwenda nyumbani au
wakiwa nyumbani.
Kusoma
Ufahamu
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 39-41
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
53
52
Kimeidhinishwa na KICD
1. Kutambua msamiati wa mavazi katika kifungu cha hadithi.
2. Kutumia msamiati wa mavazi katika sentensi kwa usahihi.
3. Kusoma kifungu cha hadithi ‘Duka la Mavazi kwa ufasaha.
4. Kujibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi.
5. Kusoma msamiati wa mavazi kwa ufasaha.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi asome maneno yenye msamiati wa mavazi.
Mwanafunzi ajadili na wenzake mavazi mbalimbali na umuhimu wake.
Mwanafunzi asome kifungu cha hadithi.
Mwanafunzi atoe muhtasari wa hadithi.
Mwanafunzi atazame vibonzo vikiwa mavazi mbalimbali.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia msamiatti wa mavazi.
Mwanafunzi ajibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi katika usomaji wa maneno na kifungu cha
hadithi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 39-41
Kadi zenye maneno ya msamiati wa mavazi
Michoro au picha za mavazi
Vibonzo
Penseli za rangi
Manila
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kuelewa kipindi hiki.
Tafuta kadi za maneno yaliyo na msamiati wa mavazi.
Andaa michoro au picha za mavazi mbalimbali.
Tafuta vibonzo vilivyovaa mavazi mbalimbali.
Soma kifungu cha hadithi kabla ya uwasilishaji darasani.
Tafuta tarakilishi.
Uwe na penseli za rangi na manila.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya
watatuwatatu. Waelekeze katika kutazama mchoro ulio kwenye Kitabu
53
52
Kimeidhinishwa na KICD
cha Mwanafunzi, ukurasa wa 39 kisha uwaulize waeleze wenzao ni nini
kinachoendelea katika mchoro huo. Wanaweza kusema kuwa hilo ni duka la
kuuza nguo, watu mbalimbali wananunua.
Waambie wanafunzi wakutazame. Waulize umevaa nini? Watoe majibu
yao kulingana na mavazi uliovaa. Waweke wanafunzi katika vikundi vya
wannewanne kisha uwaambie watazamane na waseme wamevaa nini. Kubali
majibu yaliyo sahihi.
Wakiwa katika vikundi vya wannewanne, washirikishe kujadili umuhimu
wa kuvaa mavazi. Zunguka darasani kuhakikisha kuwa wanashiriki katika
majadiliano. Mmoja anaweza kuwa mwenyekiti (kiongozi) na mwingine
anakili hoja zao.Wanaweza kutoa majibu kama: ili kucha uchi, kujikinga
na baridi, kuwa nadhifu, kusali, ni kanuni ya dini, kwenda kuoga, kulala na
kuzuia miale ya jua.
Waongoze wanafunzi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 40 ili
wasome kifungu cha hadithi: Duka la Mavazi wakiwa wawiliwawili.
Wanafunzi watoe muhtasari wa kifungu cha hadithi waliyosoma.
Waongoze wanafunzi katika kutambua maneno ya msamiati wa mavazi
kutoka kwa kifungu cha hadithi.
Waelekeze wanafunzi katika kujibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi
waliyosoma.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 40
1. Mavazi
2. Sketi, rinda, blauzi na chupi
3. Koti, suruali, shati, kizibao, tai na soksi
4. Kanchiri, rinda, gaguro na shela
5. Suti na shati
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili. Washirikishe
wanafunzi hao katika kuchora mavazi na kuyapaka rangi wapendazo.
Waongoze kutathmini ni michoro ipi ya mavazi inayopendeza zaidi.
Kubali maoni ya wanafunzi wako.
Waelekeze wanafunzi kutumia tarakilishi kuchora michoro ya
mavazi. Waongoze kusambaza michoro hiyo kupitia mtandao wa
intaneti.
55
54
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wakienda
nyumbani, wataje mavazi yanayovaliwa na watu wa familia yao. Wanafunzi wataje
msamiati wa mavazi kama vile: kikoi, sweta, chepeo, kanzu, buibui, kilemba, koti, njuti
na soksi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 41-43
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua aina mbalimbali za mavazi.
2. Kusoma kifungu cha hadithi: ‘Umuhimu wa Mavazi kwa ufasaha.
3. Kujibu maswali kutokana na kifungu cha hadithi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi asome kifungu cha ufahamu.
Mwanafunzi ajibu maswali.
Wanafunzi wajadili umuhimu wa mavazi.
Wanafunzi wataje mavazi ya kiasili na ya kisasa.
Watazame video ya vibonzo vikiwa na mavazi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli mbalimbali.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 41-43
Michoro
Video
Maandalizi ya mwalimu
Hakikisha kuwa una nyenzo zinazohitajika kama vile: video. Tayarisha
video ya vibonzo vikiwa vimevaa mavazi kama vile: rinda, blauzi, viatu na
kitambaa. Vibonzo vingine viwe vimevaa suruali, shati, tai, soksi na viatu.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi mavazi
wanayofahamu. Wataje mavazi hayo wakiwa wawiliwawili.
Waelekeze wanafunzi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 41-42 na
wakiwa katika vikundi vya wanafunzi wawiliwawili. Waongoze katika kujadili
55
54
Kimeidhinishwa na KICD
ni mavazi ya aina gani ambayo yako kwenye michoro. Wanafunzi wataje:
shuka, buibui, fulana, ovaroli/surupwenye, rinda, tai, sketi na soksi.
Waelekeze katika kujadili mavazi hayo huvaliwa na nani, lini na huvaliwa wapi.
Waongoze wanafunzi ili wasome kifungu, ‘Umuhimu wa Mavazi kisha
wajibu maswali.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 43
1. Mavazi ya kiasili ni: shuka, kanzu na leso.
2. Mavazi ya kisasa ni: suruali, tai, shati, rinda na koti.
3. Ovaroli
4. Mavazi yana umuhimu kama vile: kucha uchi, kuzuia uchafu mtu
anapofanya kazi, kuzuia baridi, kujikinga dhidi ya hatari na kuonekana
nadhifu.
Waonyeshe wanafunzi video ya vibonzo vikiwa vimevaa mavazi
mbalimbali. Waambie wanafunzi watazame video hiyo. Waongoze
kujibu maswali na utathmini majibu ya wanafunzi kwa kutegemea
video waliyotazama.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi wakienda
nyumbani wachore mavazi yanayovaliwa na wazazi ama walezi wao.
Kuandika
Kuandika kwa kutumia tarakilishi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 44
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sehemu mbalimbali za tarakilishi zinazotumika kupigia chapa.
2. Kuchora tarakilishi akionyesha sehemu mbalimbali.
57
56
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue sehemu mbalimbali za tarakilishi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika kuchora tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi
Tarakilishi
Mchoro wa tarakilishi.
Maandalizi ya mwalimu
Tafuta tarakilishi
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha na yaliyomo kabla ya kipindi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Leta tarakilishi darasani. Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kifaa
hicho kinaitwa nini. Wanafunzi wataje. Waambie kinaitwa tarakilishi au
kompyuta. Waulize kazi yake ni nini? Waeleze kwamba tarakilishi ni chombo
au mashine ya kielektroniki yenye uwezo wa kupokea, kukusanya, kuhariri,
kuhifadhi na kutuma habari ama taarifa. Mtu anaweza kupiga taipu kazi na
kuihifadhi kwenye tarakilishi. Tarakilishi ikiunganishwa na intaneti ina uwezo
wa kupeana habari kwa urahisi kuhusu mambo mbalimbali kama vile: mavazi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne kisha uwaambie
watazame mchoro ulio kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 44. Waelekeze katika kujibu maswali wakiwa na wenzao. Majibu
yaliyopendekezwa ni:
1. Mchoro huu ni wa tarakilishi/kompyuta.
2. Watoe majibu kulingana na ufahamu wao. Kuna watakaosema la na
wengine ndio. Kwa watakaosema ndio, waulize waeleze jinsi walivyotumia
tarakilishi.
3. Watoe majibu kulingana na ufahamu wao. Kuna watakaosema hakuna
sehemu wanayojua na kuna wengine watasema chache na wengine
wanajua sehemu zote. Kwa wale wanaojua, wape nafasi wataje huku
wasiojua wakisikiliza.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili. Waambie watazame
na wasome sehemu za tarakilishi kwenye kadi za maneno kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 44.
Waonyeshe tarakilishi wakiwa darasa zima. Waambie waje mbele
wawiliwawili ili waitazame kwa karibu tarakilishi hii.
Waambie wachore tarakilishi kwenye daari. Zunguka darasani kuona
57
56
Kimeidhinishwa na KICD
namna wanavyochora tarakilishi. Waambie waonyeshe na kuandika majina
ya kila sehemu ya tarakilishi. Waambie wataje sehemu za tarakilishi kwa
wanafunzi wenzao. Waambie sehemu ni za tarakilishi ni kama:
ü Kipanya au puku
ü Kiwambo au skrini
ü Kiibodi au baobonye
ü Kitufe
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kwa kuwaambia wanafunzi waonyeshane tarakilishi
walizochora. Wajitathmini ni yupi aliyechora tarakilishi ya kuvutia zaidi. Waliochora
vizuri zaidi na kuonyesha majina ya kila sehemu watuzwe kwa njia rahisi na ifaayo.
Kipindi cha 2
Kufungua na kufunga tarakilishi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 45-47
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi , mwanafunzi aweze:
1. Kufungua na kufunga tarakilishi ili kuandika kazi na kuihifadhi.
2. Kuandika aya kuhusu mavazi kwenye tarakilishi na kuihariri.
3. Kuhifadhi kazi kwenye faili ya tarakilishi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi aandike aya kuhusu mavazi kwenye tarakilishi
Mwanafunzi afungue na afunge tarakilishi.
Kuhifadhi kazi kwenye tarakilishi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufungua na kufunga tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 44-47
Tarakilishi Mchoro
Maandalizi ya mwalimu
Tafuta tarakilishi nyingi, ikiwezekana wanafunzi watatu watumie tarakilishi
moja.
Hakikisha kuna soketi na nguvu za umeme au jenereta.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame mchoro kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 45. Waambie waseme wanafunzi kwenye
59
58
Kimeidhinishwa na KICD
mchoro wanafanya nini. Wanaweza kusema wanafunzi wanatumia tarakilishi,
wanafunzi wanafungua tarakilishi, wanafunzi wanaandika kwa tarakilishi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu. Waelekeze katika
kufungua tarakilishi. Waambie kwanza wasome na waelewe hatua za
kufungua tarakilishi kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 45.
Fungua tarakilishi wanafunzi wakitazama. Wanafunzi katika kikundi
wafungue tarakilishi jinsi ulivyowaonyesha.
Baada ya kufungua, waelekeze wanafunzi katika kufungua ukurasa ili
waandike aya. Waongoze katika kusoma hatua za kufuata katika Kitabu cha
Mwanafunzi.
Waambie wanafunzi watazame ukifungua ukurasa katika tarakilishi yako.
Waelekeze katika kufuata hatua za kufungua ukurasa. Wakishafungua,
waongoze ili waweze kuandika mada Mavazi’.
Waelekeze kupiga taipu jina la faili. Faili hiyo iitwe: Mavazi Yetu.
Wapige chapa aya moja kuhusu: Mavazi Yetu. Unaweza kuwasomea aya hii:
Kuna mavazi ya aina nyingi. Kuna mavazi yanayovaliwa na wanaume na yale
yanayovaliwa na wanawake. Mavazi ya wanaume ni: shati, fulana na tai. Mavazi
ya wanawake ni: rinda, sketi, blausi na sidiria. Mavazi mengine huvaliwa na
wanawake na wanaume. Mavazi hayo ni: viatu, mshipi, suruali ndefu, kaptura,
koa na sweta. Mimi ninapenda mavazi yetu.
Waongoze ili wahariri aya hiyo. Zunguka darasani ili uwasaidie walio na
matatizo.
Waelekeze katika namna ya kuhifadhi kazi waliyopiga chapa na kuhariri.
Washirikishe wanafunzi katika kufanya shughuli katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 46-47.
Hitimisho: Hitimisha kwa kuwaambia wanafunzi wahakikishe kuwa wamefunga
tarakilishi kwa kufuata hatua sahihi.
Saru
Viunganishi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 47-48
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
59
58
Kimeidhinishwa na KICD
1. Kueleza maana ya kiunganishi ili kukibainisha.
2. Kutambua viunganishi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia viunganishi kwa njia sahihi katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue viunganishi kati ya maneno mengine.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia
viunganishi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika kueleza kiunganishi ni nini.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 47-48
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi
Michoro ya mavazi mbalimbali
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaonyesha wanafunzi michoro ya mavazi.
Waonyeshe: shati na bombo. Waulize michoro hiyo ni ya nini. Wajibu kwa
kutaja shati na bombo. Waambie watunge sentensi wakitumia neno shati’
pekee. Waambie watunge sentensi wakitumia neno ‘bombo pekee. Wanafunzi
watunge sentensi kama:
1. Bombo ni vazi.
2. Shati ni vazi.
Waambie watunge sentensi moja ikiunganisha bombo na shati. Wanaweza
kutunga sentensi kama vile:
1. Shati na bombo ni mavazi.
2. Utavaa shati au bombo?
3. Vaa bombo lakini usivae shati.
4. Nitavaa bombo pia shati.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua kuwa: na, au, lakini na pia ni maneno
yanayounganisha sentensi mbili au zaidi. Wafahamishe kuwa maneno hayo
huitwa viunganishi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaongoze ili
wasome sentensi zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 47 .
waambie wanafunzi waambiane jukumu la maneno yaliyokolezwa rangi.
Wakiwa wawiliwawili, waeleze kuwa kazi ya maneno hayo ni kuunganisha
au kuweka pamoja maneno au sentensi.
61
60
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia maneno: na,
ama, lakini, kwa sababu, au ingawa na pia. Wanafunzi wajitathmini na
kujirekebisha.
Hitimisho: Hitimisha kwa kuwaambia watumie maneno na na au kwenye sentensi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 48-49
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kiunganishi ili kukibainisha.
2. Kutambua viunganishi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia viunganishi kwa njia sahihi katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue viunganishi kati ya maneno mengine.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia viunganishi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kueleza kiunganishi ni nini.
Wanafunzi waandike viunganishi kwenye tarakilishi.
Wanafunzi wahifadhi viunganishi kama faili kwenye tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 48-49
Kapu maneno
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi Tafuta tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie watazame
makapu maneno kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 48. Wanafunzi
wasome maneno yote kwenye makapu maneno. Waongoze katika kutambua
viunganishi kati ya maneno yaliyo kwenye kapu maneno. Maneno hayo ni:
ili, au, ilhali, pia, ama, isitoshe, lakini, wala,na, ila, ingawa na bali.
Wanafunzi wakiwa katika vikundi vyao, washirikishe katika kuandika
viunganishi walivyotambua kwenye makapu maneno kwenye tarakilishi.
Wahifadhi maneno hayo kwenye faili na waiite ‘VIUNGANISHI’.
61
60
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia viunganishi vilivyo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 49. Warekebishe wanapokosea.
Waelekeze wanafunzi ili waweze kusambaza sentensi zilizo na viunganishi
kwa wenzao kupitia mtandao wa intaneti ili wazisome. Pia wanafunzi
waelezane maana ya viunganishi huku ukitathmini namna wanavyoshiriki
katika shughuli hiyo.
Hitimisha kwa kuwaelekeza kufanya zoezi la 2 katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 49.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 49
1. ama
2. lakini
3. wala
4. kwa sababu
5. bali
Vihusushi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 49-50
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kihusishi ili kukitofautisha na aina nyingine za maneno.
2. Kutambua vihusishi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia vihusishi ipasavyo katika sentensi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue vihusishi katika sentensi.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia vihusishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 49-50
Michoro
Vifaa halisi
63
62
Kimeidhinishwa na KICD
Maandalizi ya mwalimu
Tafuta michoro inayobainisha vihusishi.
Tafuta vifaa halisi kama boksi, mpira, meza na chaki.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaonyesha wanafunzi vifaa mbalimbali kama vile:
boksi, chaki na mpira.
Unaweza kumwita mwanafunzi mmoja aje mbele ya wengine darasani kisha
aweke mpira ndani ya boksi. Waulize wanafunzi mpira uko wapi. Watajibu
kuwa mpira uko ndani ya boksi.
Teua mwanafunzi mwingine aje mbele ya darasa kisha umwambie atoe mpira
kwenye boksi na auweke nje ya boksi. Waulize wanafunzi mpira uko wapi.
Wanafunzi sharti waweze kujibu kuwa mpira uko nje ya boksi.
Waeleze wanafunzi maneno: ndani ya na nje ya ni vihusishi. Waongoze katika
kutoa maana ya kihusishi.
Waambie wanafunzi watazame picha kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 49. Unaweza kumwita mwanafunzi mmoja aje asimame mbele ya
darasa kisha awaambie wenzake mahali kitu kiko katika picha ya kwanza.
Waongoze wanafunzi katika kuigiza baadhi ya vihusishi. Vihusishi hivi ni
kama vile:
1. Kusimama nje ya darasa.
2. Kuketi ndani ya darasa.
3. Kusimama chini ya mti.
4. Kusimama katikati ya watu
wawili.
5. Kusimama mbali na darasa.
6. Kuketi karibu na ubao.
Hitimisha kwa kuwaelekeza wanafunzi katika kufanya zoezi katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 50.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 50
1. nje ya
2. zaidi ya
3. ndani ya
4. miongoni mwa
5. kabla ya
6. kando ya
63
62
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 50-51
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vihusishi katika kundi la maneno na sentensi.
2. Kutumia vihusishi ipasavyo katika sentensi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue vihusishi katika sentensi.
Mwanafunzi atunge sentensi sahihi akitumia vihusishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 50-51
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi mbeleni
Tafuta tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje vihusishi wanavyofahamu.
Wataje: ndani ya, nje ya, mbele ya na nyuma ya.
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaongoze katika kusoma
kwa zamu sentensi zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 50-51.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua vihusishi katika sentensi walizosoma.
Vihusishi hivyo ni:
1. chini ya
2. kando ya
3. ndani ya
4. juu ya
5. badala ya
6. nje ya
7. katikati ya
8. chini ya
9. mbali na
10. kabla ya
Waambie wanafunzi watazame mti maneno ulio kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 51. Waongoze katika kutambua vihusishi na
kuviweka kwenye mti maneno huo.
Washirikishe wakiwa wawiliwawili kutunga sentensi sahihi wakitumia
vihusishi: nyuma ya, nje ya, juu ya, kando ya, kati ya na baina ya.
Waambie wanafunzi waandike sentensi walizotunga kwenye tarakilishi
65
64
Kimeidhinishwa na KICD
kisha wazisambaze kwa wenzao na kwa baruapepe yako kupitia mtandao wa
intaneti.
Hitimisha kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya vihusishi.
Vihisishi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 52-54
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kihisishi ili kukitofautisha na aina nyingine za maneno.
2. Kutambua vihisishi katika kundi la maneno na sentensi.
3. Kutumia vihisishi ipasavyo katika sentensi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue vihisishi katika sentensi.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia vihisishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 52-53
Michoro
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Tafuta michoro inayobainisha vihisishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame mchoro kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 52 kisha uwaulize wanachoona.
Wanaweza kusema wanaona muuzaji na mnunuzi. Waulize maoni yao kuhusu
wanachofanya watu kwenye mchoro huo. Wanafunzi wanaweza kusema
kuwa watu hao wananunua na kuuza viatu. Waulize kama wamewahi kufanya
shughuli kama hiyo kwenye mchoro. Wanaweza kusema kuwa wamewahi
kununua viatu lakini hawajawahi kufanya kazi ya kuviuza. Wengine wanaweza
kuwa wameshirika katika kuuza wakiwa na wazazi, walezi au watu wa familia.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili. Waambie wasome kwa
zamu mazungumzo kati ya muuzaji na mnunuzi.
Waongoze katika kutamka maneno yaliyowekwa rangi katika mazungumzo
65
64
Kimeidhinishwa na KICD
hayo. Waambie maneno hayo ni vihisishi. Waelekeze katika kusoma maana ya
vihisishi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 52-53. Waeleze kwamba
vihisishi hudhihirisha hisia mbalimbali kama: furaha, kilio, kukataa, kukubali,
kushangilia na kuchukia.
Waelekeze wanafunzi katika kuigiza mazungumzo hayo.
Wajadili kuhusu jukumu la maneno yaliyokolezwa rangi. Baadhi ya wanafunzi
wanaweza kusema maneno hayo hutumika:
ü Kuonyesha mshangao
ü Kuitikia
ü Kushtuka
ü Kuashiria furaha
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia vihisishi vilivyo
kwenye mazungumzo hayo.
Wanafunzi wasome sentensi walizotunga ili kujitathmini na kujirekebisha.
Hitimisha kipindi kwa kuwapa zoezi lifuatalo:
Mtu atatumia kihisishi kipi kudhihirisha hisia zifuatazo:
1. Kushangaa
2. Kuitikia
3. Kushangilia
4. Kukashifu
5. Kukataa
6. Kukasirika
Tathmini majibu ya wanafunzi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 53-54
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vihisishi katika kundi la maneno na sentensi.
2. Kutumia vihisishi ipasavyo katika sentensi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue vihisishi katika sentensi.
Mwanafunzi atunge sentensi sahihi akitumia vihisishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 53-54
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi mbeleni
Tafuta tarakilishi
67
66
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje vihisishi wiwili
wanavyofahamu. Wanaweza wakataja: Oyee! Lo!
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaongoze katika
kusoma kwa zamu sentensi zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 53.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua vihisishi katika sentensi walizosoma.
Vihisishi hivyo ni:
1. Oyee!
2. Salaaale!
3. La hasha!
4. Wallahi
5. Mama eeeh!
6. Enhe!
7. Pole!
8. Aha!
Waelekeze katika kujaza nafasi zilizoachwa wazi wakitumia vihisishi mwafaka.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 54
1. (a) Aha!
(b) Toba!
(ch) Hata!
(d) Pole!
(e) Hata!
(f) Ala!
2. Tathmini sentensi za wanafunzi. Hakikisha kuwa ni sahihi na zimetumia
vihisishi.
3. Taib! Hee! Kumbe! We! Ala! Afanalek! Lahaula! Harambee! Ata!
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi sahihi wakitumia
vihisishi. Tathmini sentensi hizo na uwarekebishe panapohitajika.
Hitimisha kipindi kwa kuwapa kazi ya ziada kwa kuwaambia
wanafunzi waonyeshe vihisishi katika sentensi hizi na wajadili nje ya
darasa zinawakilisha hisia gani.
67
66
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Sehemu hii inakuza umilisi wa kimsingi. Baadhi ya umilisi huo ni:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi watafanya mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika vikundi
kama vile: kujadili maneno ya upole au kueleza pande za dira. Mijadala baina ya wanafunzi
kuhusu mambo watakayoandika kwenye barua ya kiraki itamarisha mawasiliano na
kukuza ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi wakisambaza barua za kiraki
walizoandika kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi,
DIRA
4
Utangulizi
Dira ni chombo kinachofanana na saa ambacho huonyesha pande za dunia. Dira
humwelekeza mtu anayesari hasa nahodha na rubani. Dira huwa na pande nne
kuu: Kaskazini, Kusini, Mashariki na Magharibi.
Sehemu hii ya Dira ina mada tano. Mada hizo ni: heshima, adabu na vyeo (Maneno
ya upole), kusoma kwa mapana (Matini ya kidijitali), kuandika barua ya kiraki,
ngeli za nomino (umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya A-WA), na ngeli za
nomino (umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya A-WA).
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutumia maneno ya upole katika mawasiliano.
2. Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata habari muhimu.
3. Kuandika barua ya kiraki akizingatia mada kwa kufuata kanuni zifaazo.
4. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya A-WA akizingatia upatanisho
wa kisaru.
69
68
Kimeidhinishwa na KICD
video, projekta, intaneti, mitandao na tovuti ili wanafunzi wajifunze pembe kuu za
dira na kusakura habari muhimu kwenye tovuti.
(ch) Hamu ya Ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia wanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
dira. Umilisi huu utawapa mwanafunzi hamu ya kujua pande zote za dira na matumizi
ya dira katika maisha ya kila siku ya binadamu katika jamii yake. Pia, wanafunzi
watatafakari wakijibu maswali tekelezi kuhusu dira. Wanafunzi watakuwa na hamu ya
kutaka kutumia vyombo vya kidijitali ili kutafuta habari zaidi kuhusu dira.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika barua ya kiraki kwa kutumia
tarakilishi, tabuleti au simu ya mkononi. Pia, ubunifu ukuzwe na kuimarishwa kupitia
kutunga sentensi sahihi wakitumia nomino mbalimbali katika ngeli ya A-WA. Ubunifu
hudhihirika wanafunzi wakitafuta maana za maneno wakitumia mtandao wa intaneti.
(e) Kujiamini
Umilisi huu unakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kuwasomea barua ya kiraki aliyoandika. Pia, kujiamini kunakuzwa kupitia
wanafunzi kuigiza matukio mbalimbali kuonyesha pande za dira na kutumia maneno ya
adabu na heshima.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu unakuzwa kupitia kuwapa wanafunzi maswali ya kutafakari, kukiria na
kutafuta majibu ambayo hayapo kwenye matini. Kwa mfano, dira ina umuhimu gani?
Uhusiano wa masuala mtambuko
Sehemu hii ina uhusiano na masuala mtambuko yafuatayo:
(a) Kujitambua na kujithamini
Kupitia kuigiza vitendo vya upole, kutunga sentensi, na kufungua na
kufunga tarakilishi wanafunzi wanaweza kujitambua na kujithamini.
(b) Stadi za maisha
Stadi hii inakuzwa kwa kujieleza, kushiriki katika vikundi, kuchangia
mijadala na kuutumia dira kuelekeza mahali.
(ch) Uraia
Kupitia kufanya kazi pamoja kwa kutumia dira na kuheshimu watu kwa
kutumia maneno ya upole na adabu.
(d) Elimu ya maendeleo endelevu
Kupitia ujuzi wa kutumia teknolojia ya kisasa hasa tarakilishi.
69
68
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Sehemu hii ina uhusiano na maadili kwa njia zifuatazo:
Heshima na adabu kwa kujua msamiati wa adabu na heshima na kuutumia
maishani mwake.
Ushirikiano kupitia kwa kazi za vikundi.
Uaminifu kwa kuelekeza mtu kupitia dira na kuwa mwaminifu na mwenye
kusema ukweli.
Upendo kwa watu waliowa au wenye huzuni katika jamii kwa kuwaambia
pole.
Umoja kupitia shughuli za vikundi kama kufungua na kufunga tarakilishi.
Uwajibikaji kupitia wanafunzi kutunza na kuhifadhi vyombo vya kidijitali
kama vile tarakilishi, vinasasauti na rekoda.
Shughuli za huduma za kijamii
Katika sehemu hii, mwanafunzi anaweza kushiriki katika shughuli za huduma za
kijamii zifuatazo:
Kushiriki katika kuandika barua ya kiraki.
Kuwahamasisha wenzake nyumbani na shuleni kuhusu umuhimu wa kutumia dira.
Kuhimiza watu kutumia kanuni za kisaru hasa nomino za ngeli ya A-Wa
ipasavyo ili kufanikisha mawasiliano.
Uhusiano na masomo mengine
Sehemu hii inaingiliana na masomo mengine kama vile:
Social Studies: mafunzo ya dira hufunzwa katika somo hili kuonyesha sehemu
mbalimbali za dunia.
Religious Activities: lugha ya upole hufunzwa.
English Activities: kuna mada kama vile lugha ya upole zinazofunzwa ili
kukuza stadi ya kusikiliza na kuzungumza.
Indigenous Language Activities: kuna mada kama vile lugha ya upole
zinazofunzwa ili kukuza stadi ya kusikiliza na kuzungumza.
Shughuli na huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Wanafunzi washiriki katika kutazama jua lichomozapo asubuhi na jua
linapozama jioni.
Wanafunzi washiriki katika kuwafariji waliowa katika jamii kwa kuwapa pole.
Washiriki katika kuwapongeza wenzao katika mashindano kama vile riadha
na kabumbu.
71
70
Kimeidhinishwa na KICD
Kushiriki katika kuandika barua za kiraki halisi hasa kwa wazazi au walezi
wao.
Mapendekezo ya mbinu za kutathmini
Tathmini inaweza kufanywa kwa:
Kuhakiki jinsi wanafunzi wanavyosoma maneno ya upole.
Kuchunguza jinsi wanafunzi wanavyotumia msamiati wa upole.
Kuhakiki jinsi wanafunzi wanavyoandika barua ya kiraki.
Kusikiliza majadilano ya wanafunzi.
Kuchanganua namna wanafunzi wanavyojibu maswali kutokana na kifungu
walichosoma.
Kuhakiki namna wanafunzi wanavyotamka maneno, kutunga sentensi na
kujaza mapengo katika sentensi.
Kuchunguza namna wanafunzi wanavyotumia msamiati wa dira kama:
Kaskazini, Kusini, Magharibi na Mashariki katika mawasiliano.
Nyenzo
Nyenzo zifuatazo zinaweza kutumika:
Vifaa halisi
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi,
tabuleti, rununu na projekta
Kinasasauti
Redio
Mtandao
Tovuti
Picha
Michoro
Chati
Kadi maneno
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
Shughuli za ujifunzaji
Mwanafunzi atambue maneno ya upole katika mazungumzo.
Mwanafunzi atumie maneno ya upole katika sentensi.
Mwanafunzi aigize matumizi ya maneno ya upole katika miktadha
mbalimbali.
Mwanafunzi atoe muhtasari wa matini aliyosoma.
Mwanafunzi ajibu maswali katika maandishi au mazungumzo.
Mwanafunzi atambue sehemu za kimuundo za barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki kwa muundo na mtindo ufaao.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki mtandaoni na kuisambaza kwa wenzake.
71
70
Kimeidhinishwa na KICD
Mwanafunzi awasomee wenzake barua ya kiraki.
Kusikiliza usomaji wa nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
kwenye kinasasauti.
Kuandika mafungu ya maneno yenye nomino za ngeli ya A-WA.
Kujaza mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa nomino
katika ngeli ya A-WA.
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Kushiriki katika mchezo wa kuchopoa kadi za sentensi zenye nomino za ngeli
ya A-WA katika umoja na wingi na kuzisoma.
Maswali dadisi
1. Dira ina umuhimu gani katika maisha ya binadamu?
2. Ni maneno gani yanayotumiwa katika miktadha mbalimbali kuonyesha upole
katika mazungumzo?
3. Je, ni hatua zipi za kiusalama ambazo unapaswa kuzingatia unapotumia
mtandao?
4. Ni mambo gani unayozingatia unapoandika barua ya kiraki?
5. Ni nomino zipi zinazorejelea viumbe hai?
6. Je, unafahamu nomino zipi za ngeli ya A-WA?
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Unaweza kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kupitia mikakati
ifuatayo:
Wape wanafunzi wenye hitilafu za viungo fulani vya mwili kama vile: miguu
na mikono shughuli mbadala. Kwa mfano, badala ya kusimama wanaweza
kuketi na kuonyesha pande za dira.
Watengee wanafunzi wanaotatizika kuelewa vipindi fulani muda maalumu wa
kurudia shughuli baada ya ujifunzaji darasani.
Tumia mbinu na nyenzo tofauti kufunza vipengele mbalimbali. Tumia video,
michoro, picha au rekodi za kinasasauti.
Kwa wasioona, unaweza kushirikisha vifaa halisi ili waguse na kushika.
Kwa wanafunzi wanaochukua muda mrefu kuelewa na kufanya shughuli
darasani, uwe na subira nao wanaposoma, wanapoandika, wanapozungumza
au wanaposhiriki katika shughuli mbalimbali darasani.
Wale ambao wana uwezo wa juu darasani, wape kazi ya ziada na changamano
kama vile: kuchora dira na kutunga sentensi zaidi.
73
72
Kimeidhinishwa na KICD
Kusikiliza na Kuzungumza
Heshima, Adabu na Vyeo: Maneno ya Upole
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 55-57
Utangulizi
Iwapo ni asubuhi, waambie wanafunzi watoke nje ya darasa. Waambie
watazame jua. Waulize jua liko upande gani. Wanaweza kusema Mashariki au
pia wakaonyesha kwa mikono yao upande ambao jua liko. Waeleze kuwa jua
huchomoza upande wa Mashariki. Waambie watazame vivuli vyao na waseme
upande ambao vivuli hivyo viko.
Waelekeze wanafunzi katika kutazama michoro kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 55. Waulize waseme wanachoona kwenye michoro
hiyo.
Waongoze katika kutaja sehemu kuu za dira kama vile Kaskazini, Kusini,
Mashariki na Magharibi. Waeleze kuwa kuna pande zaidi ya nne katika dira.
Waongoze katika kusoma maelezo kuhusu dira katika kitabu.
Waambie wachore dira katika madaari yao na waonyeshe sehemu za dira.
Waongoze katika kutambua pande nne kuu za dunia.
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua maneno ya upole yanayotumiwa katika mawasiliano.
2. Kutumia maneno ya upole katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Ni maneno gani yanayotumiwa kuonyesha upole katika mazungumzo?
2. Maneno ya upole hutumiwa katika miktadha ipi ya mawasiliano?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue maneno ya upole.
Mwanafunzi ashiriki katika matumizi ya maneno ya upole .
Mwanafunzi atumie maneno ya upole katika sentensi.
73
72
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 55-57
Rununu
Tabuleti
Kanda ya sauti
Video
Kinasasauti
Mti maneno
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yatakayofunzwa kuhusu
maneno ya adabu.
Tafuta video iliyo na watu wakizungumza wakitumia maneno ya upole.
Tayarisha mti maneno wenye maneno ya upole.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje maneno ya vyeo kama
vile: Bwana, Bi, Daktari, Kasisi na Profesa.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwashirikishe
katika kusoma maneno yaliyo kwenye mti maneno katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 56.
Waongoze katika kutambua maneno hayo hutumika wakati gani. Kwa mfano,
kuendesha ni wakati tumbo la mtu lina matatizo na anaenda haja kubwa mara
kwa mara.
Wanafunzi waeleze wenzao kama wamewahi kutumia maneno ya upole.
Washirikishe wanafunzi katika mjadala wa ni kwa nini kuna umuhimu wa
kutumia maneno ya upole katika mawasiliano. Wanaweza kutoa hoja kama
vile:
ü Kucha aibu.
ü Kuwa na adabu.
ü Kuheshimiana.
ü Kufuata kaida za jamii.
ü Kupunguza ukali katika
mawasiliano.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wafanye zoezi la 1.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 57
(a) Ameaga dunia- amekufa
(b) Karibu- kukaribisha
(ch) Naomba msamaha- kunyenyekea ili kusamehewa kosa ulilofanya
(d) Anaendesha- ana matatizo ya tumbo: anahara
(e) Alijifungua- alipata mtoto
75
74
Kimeidhinishwa na KICD
(f) Tafadhali- kuomba kwa kunyenyekea
(g) Pole- kumhurumia mtu kwa dhiki iliyompata
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia maneno ya
upole waliojadili. Kwa mfano: Ninaomba msamaha kwa kuka nikiwa
nimechelewa.
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje maneno
mengine ya upole wanayofahamu. Waambie watunge sentensi wakitumia maneno
hayo.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 57
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua maneno ya upole yanayotumiwa katika mawasiliano.
2. Kutumia maneno ya upole katika miktadha tofauti.
Maswali dadisi
1. Ni maneno gani yanayotumiwa kuonyesha upole katika mazungumzo?
2. Maneno ya upole hutumiwa katika miktadha ipi ya mawasiliano?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue maneno ya upole.
Mwanafunzi ashiriki katika matumizi ya maneno ya upole.
Mwanafunzi aigize matumizi ya maneno ya upole katika miktadha
mbalimbali.
Mwanafunzi atumie maneno ya upole katika sentensi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 57
Rununu
Tabuleti
Kanda ya sauti
Video
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yatakayofunzwa kuhusu
maneno ya adabu.
75
74
Kimeidhinishwa na KICD
Andaa video iliyo na mazungumzo na kutumia maneno ya upole.
Tafuta video iliyo na watu wakizungumza wakitumia maneno ya upole.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wanakumbuka maneno ya
upole. Waulize wataje baadhi ya maneno ya upole waliojifunza.
Waelekeze wanafunzi katika kutazama video wakiwa darasa zima. Video hiyo
iwe na mazungumzo ya watu wakitumia maneno ya upole.
Waongoze katika kutambua maneno ya upole yaliyotumiwa katika video.
Teua mwanafunzi mmoja asimame mbele ya wanafunzi wenzake darasani.
Mwambie awatajie na awaeleze wanafunzi maneno ya upole yaliyotumiwa
katika video hiyo. Mwanafunzi apongezwe iwapo atataja maneno sahihi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili waigize vitendo kama
vile: kuomba ruhusa ili kwenda msalani na kuomba msamaha. Wanafunzi
watumie maneno ya upole na adabu katika maigizo yao.
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi
wasome kwa sauti sentensi zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa
57. Waongoze katika kutambua maneno ya upole kwenye sentensi hizo.
Kusoma
Kusoma kwa Mapana: Matini ya Kidijitali
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 58-59
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi hiki, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua na kufungua faili iliyo na kifungu cha kusoma.
2. Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata vifungu vya kusoma kuhusu dira.
3. Kutumia vyombo vya kidijitali kupata matini.
Maswali dadisi
1. Ni hatua gani za kiusalama unazofaa kuzingatia unapotumia mtandao?
2. Unaweza kufanya nini ili uweze kukia matini ya kusoma kwenye mtandao?
77
76
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue hatua za kiusalama kwenye mtandao.
Mwanafunzi ajadili na wenzake msamiati kuhusu dira.
Mwanafunzi atambue faili lenye matini iitwayo, DIRA.
Mwanafunzi atafute maana za maneno yanayohusiana na Dira
Mwanafunzi asikilize matamshi na maelezo mtandaoni.
Mwanafunzi atoe muhtasari wa matini aliyosoma.
Mwanafunzi ajibu maswali katika maandishi au mazungumzo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 58-59
Mchoro Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi
kabla ya kipindi.
Tafuta tarakishili.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi maswali kuhusu mchoro ulio
kwenye kitabu. Waulize watu katika mchoro huo wanafanya nini.
Andaa darasa liwe na tarakilishi
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaelekeze katika
kusoma kwa zamu maelezo kuhusu jinsi ya kufungua faili kwenye tarakilishi.
Waambie wafungue faili iitwayo, ‘DIRA kwa kufuata hatua zilizo katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 58-59.
Washirikishe wanafunzi wakiwa wawiliwawili katika kusoma matini ya
kidijitali kuhusu, ‘Sehemu za Dira.
Waongoze ili waweze kusoma maelezo ya kufunga faili yaliyo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi.
Waambie wafunge faili iitwayo ‘DIRA kwa kufuata hatua zilizo katika kitabu.
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha kwa kuwapa zoezi la kutafuta maana ya maneno
yanayohusu dira kwenye kamusi mtandaoni.
77
76
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 59-61
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya kidijitali.
2. Kutumia vyombo vya kidijitali kupata matini.
3. Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata vifungu vya kusoma kuhusu dira.
Maswali dadisi
1. Ni hatua gani za kiusalama unazofaa kuzingatia unapotumia mtandao?
2. Unaweza kufanya nini ili uweze kukia matini ya kusoma kwenye mtandao?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue hatua za kiusalama kwenye mtandao.
Mwanafunzi matini ya kidijitali na kuyasoma kwa ufasaha.
Mwanafunzi atafute maana za maneno yanayohusiana na dira
Mwanafunzi atoe muhtasari wa matini aliyosoma.
Mwanafunzi ajibu maswali katika maandishi au mazungumzo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 59-61
Mchoro
Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje vyombo vya
kidijitali wanavyofahamu. Wataje vyombo hivyo wakiwa wawiliwawili.
Waelekeze wanafunzi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 59-60 ili
wasome matini.
Washirikishe wanafunzi kujadili umuhimu wa kutoa habari kwa mwalimu,
mlezi au mzazi endapo wamepata ujumbe wa kidijitali kutoka kwa watu
wasiowajua. Zingatia hoja kama vile:
ü Ili asitapeliwe.
ü Kuepuka kuibiwa.
ü Kuepuka ulanguzi wa watoto.
ü Kuepuka kuingizwa katika mtego wa dawa za kulevya.
ü Wanaweza kuingizwa katika masuala ya wizi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne na uwaambie wasakure
matini za kidijitali kwenye tovuti kuhusu dira na maneno ya upole.
Waelekeze katika kuandika msamiati wa dira na maelezo yake na waipige
chapa matini hiyo kwenye tarakilishi.
79
78
Kimeidhinishwa na KICD
Waambie wanafunzi wasome kwa sauti maneno waliyoandika na kuhifadhi
matini hayo na kuyaita, Msamiati wa Dira
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi ya nje ya
darasa ya kuandika msamiati wa upole, kuupiga chapa kwenye tarakilishi, kuwasomea
wenzake na kuhifadhi faili kwenye tarakilishi.
Kuandika
Barua ya Kiraki
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 61-62
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia muundo wake.
2. Kuandika barua ya kiraki akizingatia mada na kanuni zifaazo.
Maswali dadisi
1. Unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
2. Ni masuala gani yanayoshughulikiwa katika barua ya kiraki?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue sehemu za kimuundo za barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki kwa muundo na mtindo ufaao.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki mtandaoni na kuisambaza kwa
wenzake.
Mwanafunzi awasomee wenzake barua ya kiraki.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 61-62
Tarakilishi
Barua ya kiraki halisi
Mchoro wa muundo wa barua ya kiraki
Maandalizi ya mwalimu
Andaa mchoro ulio na muundo wa barua ya kiraki.
Tafuta barua ya kiraki halisi.
79
78
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaonyesha wanafunzi barua ya kiraki halisi.
Unaweza kuwauliza hiyo ni nini. Teua mwanafunzi mmoja ili asome mbele ya
wanafunzi wengine darasani anwani ya mwandishi na mwanzo wa barua hiyo.
Pia anaweza kusoma mwisho wa barua hiyo.
Wakiwa darasa zima, waambie wanafunzi watazame mchoro ulio kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 61 kisha uwaelekeze katika kutambua
muundo wa barua ya kiraki kwa kuwaonyesha sehemu zifuatazo:
1. Anwani ya mwandishi
2. Tarehe
3. Mwanzo wa barua
4. Kiini cha barua
5. Mwisho wa barua
Wakiwa katika vikundi vya wannewanne, waulize wanafunzi iwapo
wamewahi kuandika au kuandikiwa barua. Iwapo wamewahi, waeleze
walimwandikia nani kuhusu nini. Wanafunzi wajadiliane huku mmoja
akinakili hoja zao.
Waongoze katika kujadili barua ya kiraki ni nini na ina sehemu gani.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika barua ya kiraki wakieleza ndugu yao
yale yanayoendelea katika darasa lao.
Teua mwanafunzi mmoja kisha umwambie aisome kwa sauti barua
aliyoandika.
Waambie wanafunzi wapige taipu na kuzihifadhi barua zao kwenye tarakilishi.
Waelekeze wanafunzi kuisambaza barua hiyo kwa wenzao kupitia mtandao
wa intaneti.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kwa kuwaambia wanafunzi wataje sehemu kuu za
barua ya kiraki.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 62-64
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
3. Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia muundo wake.
4. Kuandika barua ya kiraki akizingatia mada na kanuni zifaazo.
Maswali dadisi
1. Unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
2. Ni masuala gani yanayoshughulikiwa katika barua za kiraki?
81
80
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue sehemu za kimuundo za barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandae vidokezo vya kuandika barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki kwa muundo na mtindo ufaao.
Mwanafunzi ajadili na wanafunzi wenzake mada ya barua ya kiraki.
Mwanafunzi atumie msamiati wa dira katika barua ya kiraki.
Mwanafunzi awasomee wenzake barua ya kiraki.
Wanafunzi wajadili umuhimu wa barua za kiraki katika mawasiliano.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi
Tarakilishi
Barua ya kiraki halisi
Bahasha
Stempu
Mfano wa barua ya kiraki
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje sehemu kuu za barua
ya kiraki. Waulize sehemu hizo zinahusu nini. Waulize wanafunzi barua
huwekwa wapi iwapo inatumwa kwa njia ya posta. Waonyeshe bahasha na
stempu na uwaeleze namna ya kutuma barua kwa posta.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasome mfano
wa barua ya kiraki ulio katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 63.
Waongoze katika kutambua sehemu za barua ya kiraki. Waelekeze ili wajadili
barua hiyo inahusu nini.
Waongoze wanafunzi katika kusoma mambo muhimu kuhusu barua ya
kiraki katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 64. Wape nafasi wajadili
hoja hizo wakirejelea mfano wa barua ya kiraki waliyosoma.
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi wawiliwawili na
uwashirikishe katika kujadili umuhimu wa barua ya kiraki. Waelekeze kwa
kuzingatia hoja zilizo katika Kitabu cha Mwanafunzi. Zunguka darasani
kuhakikisha kuwa mijadala inaendelea vizuri na kusaidia palipo na tatizo.
Waambie wanafunzi wanakili hoja zao na kuzieleza.
Waelekeze wanafunzi kuandika barua kwa mzazi au mlezi wakimwarifu
ahudhurie mkutano wa wazazi shuleni. Waongoze wanafunzi katika kuandaa
vidokezo vya kuandika barua ya kiraki. Waambie wazingatie mambo
muhimu kama vile: anwani na tarehe, mpangilio mwafaka wa mawazo,
maamkuzi, kiini cha barua (mkutano wa wazazi shuleni), hati nadhifu, tahajia,
kanuni za kisaru, uakishaji ufaao, lugha ya kuvutia na mwisho wa barua.
Teua mwanafunzi mmoja ili awasomee wenzake barua aliyoandika.
Wanafunzi wampongeze kwa usomaji mzuri.
81
80
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kwa kuwaambia wanafunzi kuwa wakati mwingine
barua huwekwa katika bahasha. Anwani ya anayeandikiwa huandikwa juu ya bahasha.
Waambie kuwa iwapo barua itatumwa kwa njia ya posta, bahasha huwekwa stempu.
Wape shughuli ya kufanya nje ya darasa ya kujadili vipengele muhimu katika barua ya
kiraki.
Saru
Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya A-WA
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 65-66
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya ngeli za nomino ili kuzibainisha.
2. Kutambua nomino katika ngeli ya A-WA.
3. Kuandika umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya A-WA.
Maswali dadisi
1. Ni nomino gani zinazorejelea viumbe hai?
2. Nomino zinazorejelea viumbe hai hutambuliwa na nini?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya A-WA.
Mwanafunzi aeleze maana ya ngeli za nomino.
Mwanafunzi aandike nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi
Mti maneno
Vifaa halisi
Chati
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya nomino.
Kubali mifano ambayo wanafunzi watatoa.
Waongoze katika kusoma maneno yaliyo kwenye mti maneno katika kila tawi.
Waulize wamegundua nini kuhusu maneno hayo. Wanaweza kujibu kuwa
83
82
Kimeidhinishwa na KICD
maneno hayo ni nomino na yamegawanywa katika nomino za watu, ndege na
wadudu.
Wakiwa katika vikundi vya wanafunzi wawiliwawili, waelekeze kupanga
maneno kwenye kila tawi katika mti maneno katika umoja na wingi
wakitumia majedwali. Zunguka darasani kuhakikisha kuwa wanafunzi
wanayapanga maneno hayo. Wasaidie kutambua maneno hayo
panapohitajika.
Hitimisho: Hitimisha kwa kuwaambia kuwa maneno yaliyo kwenye mti maneno ni
nomino. Nomino hizo zote ziko katika ngeli ya A-WA. Waambie kuwa ngeli ni vikundi
vya majina na majina katika ngeli ya A-WA ni ya viumbe wenye uhai pekee.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 66-67
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya ngeli za nomino ili kuzibainisha.
2. Kutambua nomino katika ngeli ya A-WA.
3. Kuandika umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya A-WA.
Maswali dadisi
1. Ni nomino gani zinazorejelea viumbe hai?
2. Nomino zinazorejelea viumbe hai hutambuliwa na nini?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kuandika nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Kusikiliza usomaji wa nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
kwenye kinasasauti.
Kuandika mafungu ya maneno yenye nomino za ngeli ya A-WA.
Kujaza mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa nomino
katika ngeli ya A-WA.
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 66-67 kabla ya kipindi.
Tafuta kinasasauti.
Rekodi mtu akisoma nomino za ngeli ya A-WA katika wingi na umoja.
83
82
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wajibu kwa kuzungumza umoja
na wingi wa maneno yafuatayo:
(a) mtu
(b) kijana
(ch) kiroboto
(d) kuku
(e) tausi
(f) kifaru
Wakiwa wawiliwawili, waelekeze wanafunzi kuandika umoja na wingi wa
nomino zilizo katika swali la kwanza. Wazingatie idadi iliyowekwa kwenye
mabano. Waeleze kuwa hayo ni mafungu ya maneno ya ngeli ya A-WA yaani:
mkulima mmoja na wakulima kumi.
Waongoze wanafunzi katika kujaza mapengo kwa kutumia viambishi vya
umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya A-WA. Wajaze jedwali lililo katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 66. Kwa mfano, mchuuzi - wachuuzi.
Waambie wanafunzi wasikilize kinasasauti kama darasa zima. Wasikilize kwa
makini nomino za ngeli ya A-WA zikisomwa katika umoja na wingi. Nomino
hizo zilizorekodiwa ni:
1. mbuzi-mbuzi
2. muuguzi-wauguzi
3. kipepeo-vipepeo
4. kasuku-kasuku
5. kunguni-kunguni
6. mtoto-watoto
7. kifaru-vifaru
8. kupe-kupe
9. mkulima-wakulima
10. kiroboto-viroboto
Hitimisho: Hitimisha kwa kuwateua wanafunzi wawiliwawili ili mmoja ataje nomino
kwa umoja na mwingine aseme wingi wa nomino iliyotajwa. Nomino zenyewe ni:
1. kuku
2. mvuvi
3. kiwavi
4. farasi
5. mjomba
6. mzalendo
Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya A-WA
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 67-69
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya A-WA katika
umoja na wingi.
2. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
85
84
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutaja nomino za ngeli ya A-WA.
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Mwanafunzi aandike nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 67-69
Majedwali
Chati
Tarakilishi
Vifaa halisi
Maandalizi ya mwalimu
Andaa majedwali yenye nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Tayarisha chati yenye sentensi zilizo na nomino za ngeli ya A-WA katika
umoja na wingi.
Tafuta tarakilishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya nomino za
ngeli ya A-WA. Kubali mifano ambayo wanafunzi watatoa. Mifano kama vile:
mtu-watu, mwalimu-walimu, ng’ombe-ngombe na kipepeo-vipepeo.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uaelekeze katika
kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
kwenye jedwali.
Waongoze wanafunzi katika kutambua viambishi a na wa katika vitenzi
kwenye sentensi walizosoma. Mwanafunzi amwambie mwenzake
alichogundua katika sentensi walizosoma. Washirikishe katika mjadala ili
wagundue nomino hizi ziko katika ngeli ya A-WA.
Kwa usaidizi wako, wanafunzi waelekezane kugundua viambishi vya
nomino za ngeli ya A-Wa katika umoja na wingi. Kwa mfano, anachakura -
wanachakura.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika sentensi za nomino za ngeli ya A-WA
zilizo katika umoja ziwe katika wingi.
85
84
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 67
(a) Viongozi watawasili kesho.
(b) Mbuzi wanakula nyasi.
(ch) Watoto walilia jana.
(d) Vyura wanakoroma majini.
(e) Viwavi waliuawa jana.
(f) Watoto wanaelekea Kusini.
Waongoze wanafunzi katika kuandika sentensi za nomino za ngeli ya A-WA
katika umoja na wingi kwenye tarakilishi. Wanafunzi warejelee sentensi zilizo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 67-68.
Waambie wanafunzi wazisambaze sentensi walizoandika kwa wenzao kupitia
mtandao.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uaelekeze katika
kusoma sentensi kutoka kwenye tarakilishi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi watatuwatatu na
uwashirikishe katika kutunga sentensi za nomino katika ngeli ya A-WA
katika umoja na wingi. Wanafunzi warejelee sentensi zilizo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 67-68.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kutoa muhtasari kuwa sentensi zenye nomino katika
ya ngeli ya A-WA huwa na kiambishi a katika umoja na kiambishi wa katika wingi ili
kubainisha upatanisho wa kisaru.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 68-69
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya A-WA katika
umoja na wingi.
2. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
87
86
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Kushiriki katika mchezo wa kuchopoa kadi za sentensi zenye nomino za ngeli
ya A-WA katika umoja na wingi
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 68-69
Boksi au kikapu
Kadi
Maandalizi ya mwalimu
Tafuta boksi au kikapu cha kuwekea kadi zenye sentensi.
Andaa kazi za kuandikia sentensi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi watunge sentensi mbili zenye
nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaelekeze katika
kuandika sentensi zenye nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
kwenye kadi. Warejelee sentensi zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 68-69.
Wape wanafunzi boksi au kikapu kimoja ili waweke kadi zenye sentensi ndani.
Waongoze wanafunzi katika kuchopoa kadi moja moja kwa zamu na kusoma
sentensi zilizoandikwa kwenye kila kadi.
Hitimisho: kuhitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa sentensi za
nomino za ngeli ya A-WA huwa na kiambishi a katika umoja na kiambishi wa katika
wingi ili kubainisha upatanisho wa kisaru.
87
86
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Unaweza kutumia nyenzo zifuatazo:
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, rununu na projekta
Kinasasauti
Redio
Mtandao
Picha
Michoro
Chati
Kadi
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
Vibonzo
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Baadhi ya umilisi unaokuzwa ni:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Yanakuzwa kwa wanafunzi kufanya mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano
USHAURI NASAHA
5
Utangulizi
Ushauri nasaha ni mawaidha yanayotolewa kwa mtu kabla ya tatizo kutokea. Ushauri
nasaha ni huduma inayohitaji watu wawili ambao ni mshauri na mshauriwa. Mshauri
ni mtu anayetoa mawaidha ilhali mshauriwa ni yule anayepokea mawaidha ili afaulu
maishani. Katika muktadha wa shuleni, mara nyingi, mwalimu huwa mshauri na
mwanafunzi ni mshauriwa.
Sehemu hii imeshughulikiwa katika mada nne. Mada hizo ni: methali zinazohusu
malezi, kusoma kwa ufahamu, kuandika insha ya maelezo na saru kuhusu ngeli ya
U-I.
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutumia methali zinazohusu malezi katika mawasiliano.
2. Kusoma shairi kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
3. Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
4. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
89
88
Kimeidhinishwa na KICD
katika vikundi. Shughuli hizi ni kama vile: kukamilisha methali au kusoma makala
kwa pamoja. Mijadala baina ya wanafunzi kuhusu ushauri itaimarisha mawasiliano na
kukuza ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi wakisambaza habari kuhusu
mawaidha mbalimbali kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi,
video, projekta, intaneti na tovuti ili mwanafunzi ajifunze masuala mbalimbali ya
ushauri-nasaha. Kutumia tarakilishi kuandika na kuhifadhi kazi kuhusu ushauri-
nasaha kwenye faili.
(ch) Hamu ya Ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
ushauri-nasaha. Umilisi huu utampa mwanafunzi hamu ya kukamilisha methali. Pia,
atafakari maswali ya ziada yanayohusu ushauri-nasaha. Mwanafunzi anaweza kuwa na
hamu ya kutaka kutumia vyombo vya kidijitali ili atafute habari zaidi kuhusu ushauri-
nasaha na methali.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika insha ya maelezo kuhusu ushauri-
nasaha kwa kutumia tarakilishi, tabuleti au simu ya mkononi. Pia ubunifu ukuzwe na
kuimarishwa kupitia kusakura mtandaoni ili kutafuta methali.
(e) Kujiamini
Umilisi huu utakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kuwapa ushauri. Pia, kujiamini kutakuzwa kupitia mwanafunzi kutunga
sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu utakuzwa kupitia kumpa mwanafunzi swali la kutafakari, kukiria na
kutafuta jawabu lake ambalo halimo kwenye matini. Kwa mfano, mwanafanzi anataka
kusoma somo kuhusu lugha za kiasili. Mshauri mwanafunzi jinsi somo hili litamsaidia
maishani.
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Kujitambua na kujithamini kupitia:
ü kukamilisha methali.
ü kutunga sentensi.
ü kufungua na kufunga
tarakilishi.
89
88
Kimeidhinishwa na KICD
(b) Stadi za maisha zitakuzwa kupitia:
ü mwanafunzi kujieleza.
ü kushiriki katika vikundi.
ü kuchangia mijadala.
ü kuwapa wanafunzi ushauri.
(ch) Uraia utakuzwa kupitia:
ü kufanya kazi pamoja. ü kuheshima watu.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu kupitia kusikiliza kwa makini na kutilia maanani ushauri
anaopewa mwanafunzi.
Ushirikiano kupitia kwa kazi za vikundi na kazi mradi.
Uaminifu kwa kusema ukweli wakati wa kupokea ushauri.
Upendo kupitia kwa kuwasaidia wanafunzi wengine wanaohitaji ushauri ama
usaidizi.
Uwajibikaji kupitia mwanafunzi kutunza na kuhifadhi vyombo vya kidijitali
kama vile: tarakilishi.
Shughuli za huduma za kijamii
Kushiriki katika kutoa ushauri.
Kuwahamasisha wanafunzi wengine nyumbani na shuleni kuhusu umuhimu
wa ushauri-nasaha.
Kuhimiza watu kutumia kanuni za kisaru ili kufaulisha mawasiliano.
Uhusiano na masomo mengine
Sehemu ya ushauri-nasaha inaingiliana na masomo mengine kama vile:
1. Science and Technology Activities: inahimiza matumizi ya tarakilishi.
2. English Activities: methali zinafunzwa ili kukuza stadi ya kusikiliza na
kuzungumza.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Kwa somo linalohusu kusoma, hakikisha kuwa wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wamepata mashine za breli darasani ili ziwasaidie katika kutambua maneno. Kwa
wanafunzi wenye matatizo ya kusikia na kuzungumza, unaweza kumwalika mfasiri
wa lugha ishara ili awasaidie wanafunzi hao katika kushiriki kwenye somo kikamilifu.
Pia, unaweza ukatumia vifaa vya kiteknolojia kama vile: projekta ili kuwaonyesha
wanafunzi baadhi ya picha zinazohusu nyumbani kutoka mtandaoni. Ili kuwahusisha
wanafunzi wenye matatizo katika baadhi ya viungo vyao vya mwili kama vile, miguu
na mikono, hakikisha kuwa wakati wa kuigiza wanafunzi hawa wameangaliwa ili
wasijiumize au kuumizwa kwenye viungo vilivyoathirika.
91
90
Kimeidhinishwa na KICD
Kusikiliza na Kuzungumza
Methali
Methali zinazohusu malezi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 71-72
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua methali katika matini.
2. Kutaja methali zinazohusu malezi.
3. Kueleza maana za methali.
4. Kutumia methali zinazohusu malezi katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue methali kwenye matini.
Mwanafunzi ataje methali zinazohusu malezi.
Mwanafunzi aeleze maana za methali mbalimbali.
Mwanafunzi akamilishe methali ifaavyo.
Mwanafunzi atunge kifungu au atoe masimulizi akitumia methali kuhusu
malezi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 71-72
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Chati
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha na yatakayofunzwa kuhusu
methali zinazohusu malezi.
Rekodi methali zinazohusu malezi kwenye kanda ya sauti au tabuleti ama
rununu.
Tafuta tarakilishi.
Andika methali kuhusu malezi kwenye chati.
91
90
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi methali nyepesinyepesi ili
wazikamilishe.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma methali zilizoorodheshwa kwenye chati
kitabuni wakiwa wawiliwawili. Hakikisha kuwa wamesoma kwa usahihi.
Unaweza ukawaonyesha wanafunzi methali zaidi zilizoandikwa kwenye chati.
Waongoze wanafunzi katika kujadili miongoni mwao maana ya methali
pamoja na matumizi yake.
Waelekeze katika kusoma maelezo kuhusu methali kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 71.
Waulize wanafunzi swali la kutafakarisha linalohusu ni kwa nini methali
hutumiwa katika mawasiliano. Wanaweza kutoa majibu kama:
ü Kushauri
ü Kuonya
ü Kutoa tahadhari
ü Kuelimisha
ü Kuburudisha
ü Kuongeza ladha katika lugha
ü Kuadilisha
Waweke wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili. Waelekeze kutazama
picha iliyo kitabuni. Wanafunzi wanastahili kutambua kuwa hiyo ni picha ya
ukurasa wa intaneti kuhusu methali.
Waelekeze wanafunzi kwenye mtandao wa intaneti na uwaongoze katika
kusakura methali zilizoorodheshwa kitabuni. Waelekeze katika jinsi ya kupata
maana ya methali hizo kwenye mtandao. Waambie wanafunzi waandike
majibu yao kwenye madaari.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wakika nyumbani
wawaulize wazazi au walezi wao methali wanazofahamu. Waandike methali hizo
kwenye madaari na wakuletee ili uzitathmini.
Kipindi cha 2
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua methali zinazohusu malezi.
2. Kueleza maana za methali ili kuzibainisha.
3. Kutumia methali zinazohusu malezi katika mawasiliano.
93
92
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue methali zinazohusu methali kutoka kwa orodha.
Mwanafunzi aeleze maana za methali mbalimbali zinazohusu malezi.
Mwanafunzi akamilishe methali ifaavyo.
Mwanafunzi atunge kifungu au atoe masimulizi akitumia methali kuhusu
malezi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 72-73
Rununu
Tarakilishi
Tabuleti
Kanda ya sauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yatakayofunzwa kuhusu
methali zinazohusu malezi.
Rekodi methali zinazohusu malezi kwenye kanda ya sauti, tabuleti ama
rununu.
Tafuta tarakilishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu kisha
uwaambie wasome methali zilizo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 72.
Kwa kutumia kinasasauti, waongoze katika kujirekodi na kuhifadhi kanda ya
sauti. Wanafunzi wasikilize namna walivyotamka methali hizo baadaye.
Waongoze kutambua methali zinazohusu malezi kati ya orodha waliojirekodi
wakisoma. Majibu yaliyopendekezwa ni kama:
1. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.
2. Mwana wa kuku hufunzwi kuchakura.
3. Mtoto wa nyoka ni nyoka.
4. Mtoto hutazama kisogo cha nina.
5. Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.
Waelekeze katika kujadili na kuandika maana ya methali zozote tatu za malezi
walizotambua.
Waambie wawasomee wanafunzi wenzao methali zinazohusu malezi na
maana zake walizojadili na kuandika. Wanafunzi wengine wasikilize kwa
makini.
Waongoze wanafunzi kukamilisha methali zinazohusu malezi kwa kutafuta
jibu mwafaka kutoka kwa maneno yaliyo kwenye mabano.
93
92
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 73
(a) Baba wa kambo si baba.
(b) Kulea mimba si kazi, kazi kulea mtoto.
(ch) Mwana wa kuku hafunzwi kuchakura.
(d) Uchungu wa mwana aujuae mzazi.
(e) Mwana wa nyoka hafunzwi kuuma.
Hitimisho: hitimisha funzo kwa kuwapa wanafunzi zoezi la kibinafsi lililo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 73 kama kazi ya ziada.
Majibu
Zoezi la kibinafsi, ukurasa wa 73
1. Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.
2. Mtoto wa nyoka ni nyoka.
3. Mtoto hutazama kisogo cha nina.
4. Mama wa kambo si mama.
5. Teke la kuku halimuumizi mwanawe.
Kusoma
Ufahamu
Ujumbe na Lugha katika Ushairi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 73-74
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya shairi, ubeti na mshororo ili kuvibainisha.
95
94
Kimeidhinishwa na KICD
2. Kusoma shairi kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
3. Kutambua beti na mishororo katika shairi.
4. Kutambua shairi kutokana na umbo lake.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua shairi, beti na mishororo katika matini.
Kusoma shairi akizingatia msamiati wa mada.
Kukariri shairi kwa mahadhi mbalimbali akizingatia ujumbe.
Kushiriki katika kujadili maana ya shairi, beti na mishororo.
Kujibu maswali kutokana na shairi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 73-74
Mashairi Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili.
Waambie wanafunzi, katika vikundi vyao, wasimame mbele ya wenzao
darasani. Waelekeze kwenye shairi, Mtu ni Utu’ kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 73-74 na uwaambie wakariri shairi kwa zamu: kila
mwanafunzi ubeti mmoja. Wasisitizie umuhimu wa kutumia mahadhi ya
kupendeza wakati wa ukariri.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi wawiliwawili na
uwaongoze katika kujadili na kujibu maswali kutokana na shairi hilo.
Waelekeze wanafunzi kufahamu maana ya: shairi, ubeti na mshororo
kutokana na maelezo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 74. Waambie
wasome maelezo hayo kwa sauti.
Waongoze katika kujadili shairi linahusu nini, lina beti ngapi na lina
mishororo mingapi katika kila ubeti.
Mwisho, waongoze katika kutambua kibwagizo katika shairi hilo.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie wajadili ni
kwa nini mshairi anasema mtu ni mwenye utu.
95
94
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 75-76
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kukariri shairi kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
2. Kutambua beti na mishororo katika shairi.
3. Kutambua shairi kutokana na umbo lake.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua shairi, beti na mishororo katika matini.
Kukariri shairi kwa mahadhi mbalimbali akizingatia ujumbe.
Kujibu maswali kutokana na shairi.
Kusikiliza mashairi yanayokaririwa kwenye vifaa vya kidijitali.
Kusoma mashairi kwenye mtandao.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 75-76
Mashairi
Tarakilishi
Rekoda au simu
Kinasasauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Tafuta mashairi kuhusu ushauri-nasaha.
Soma shairi kabla ya uwasilishaji darasani.
Tafuta tarakishili, rekoda na simu.
Rekodi shairi likikaririwa kwa kutumia simu au tabuleti.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili
kisha uwaambie wasimame mbele ya wanafunzi wenzao darasani na kukariri
shairi, Maradhi ya Saratani kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 75.
Waambie wakariri shairi hilo huku wakijirekodi kwa kutumia simu au rekoda.
Waongoze wanafunzi katika kujadili ujumbe wa shairi hilo. Waulize shairi
hilo linahusu nini. Waambie watumie kamusi kwenye mtandao kupata maana
ya neno saratani.
97
96
Kimeidhinishwa na KICD
Wakiwa katika vikundi vyao, waelekeze katika kujibu maswali ya kutafakari
na kuwaza kwa kina kama vile:
1. Ni nini dalili ya saratani?
2. Ugonjwa wa saratani unaweza kuwapata watu gani?
3. Saratani inaweza kuepukwa kwa njia gani?
Wakiwa darasa zima, waambie wanafunzi wasikilize shairi likikaririwa
kwenye simu au tabuleti. Wanafunzi watambue shairi hilo lina beti ngapi na
kila ubeti una mishororo mingapi.
Waongoze wanafunzi katika kueleza shairi hilo linahusu nini. Wakishirikishe
katika kujadili ujumbe unaotolewa na kibwagizo. Baada ya kusoma, waongoze
katika kukariri shairi hilo kwa mahadhi mwafaka.
Wanafunzi wote wakariri shairi walilosikia likikaririwa kwa mahadhi yao.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie wasome
mashairi kwenye mitandao na wajadili ujumbe unaotolewa na shairi hilo.
Kuandika
Insha ya Maelezo
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 76-77
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vifungu vya maelezo katika matini.
2. Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma maelezo kuhusu insha ya maelezo.
Kutambua vifungu vya maelezo kwenye matini au tarakilishi.
Kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya maelezo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 76-77
Insha kielelezo
Tarakilishi
97
96
Kimeidhinishwa na KICD
Maandalizi ya mwalimu
Tayarisha insha kielelezo (insha ya maelezo).
Tafuta tarakilishi au tabuleti.
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yaliyomo kabla ya kipindi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wasome maelezo ya insha ya
maelezo yaliyo katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Washirikishe wanafunzi katika kuandaa vidokezo vitakavyowaongoza
kuandika insha ya maelezo. Vidokezo hivyo vihusishe:
ü Utangulizi- maelezo mafupi kuhusu mada.
ü Mwili/kiini- hoja zote hujadiliwa hapa.
ü Hitimisho- mwisho wa insha ya maelezo. Hutoa kauli kuhusu mada.
Wapange wanafunzi katika vikundi wawiliwawili ili wasome maelezo kuhusu
insha ya maelezo. Waongoze wanafunzi watakapokuwa wakisoma huku
mkijadili kila hoja.
Teua mwanafunzi mmoja ili ake mbele ya wanafunzi wenzake darasani
na ataje sehemu za insha ya maelezo. Ataje huku wengine wakimsikiliza.
Wanaweza kumtathmini na kumrekebisha anapokosea.
Teua mwanafunzi mwingine ake mbele ya wanafunzi wenzake darasani.
Mwambie aeleze kwa ufupi mambo matatu ya kuzingatia wakati wa kuandika
insha ya maelezo. Ataje na afafanue huku wengine wakimsikiliza. Wanaweza
kumtathmini na kumrekebisha anapokosea.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa kazi ya nje ya darasa. Waambie wakiwa
nyumbani, wawaulize wazazi au walezi wao wawape ushauri wa namna ya kufaulu
maishani. Waambie wanakili hoja zitakazotolewa na wazazi au walezi wao. Baadaye,
waandike hoja hizo kama aya mbili za kimaelezo. Wakuletee darasani ili utathmini
kazi yao.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 77-78
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vifungu vya maelezo katika matini.
2. Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
99
98
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma maelezo kuhusu insha ya maelezo.
Kutambua vifungu vya maelezo kwenye matini au tarakilishi.
Kuandaa vidokezo vya kuandikia insha ya maelezo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 77-78
Insha kielelezo (insha ya maelezo)
Tarakilishi au tabuleti
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kurejelea kipindi walichojifunza awali kuhusu insha ya
maelezo. Waulize wanafunzi insha ya maelezo ina sehemu gani kuu. Waambie
wataje sehemu hizo na watoe maelezo kuhusu kila sehemu.
Waelekeze wanafunzi katika kutaja mambo muhimu yanayozingatiwa wakati
wa kuandika insha ya maelezo.
Teua mwanafunzi mmoja mmoja ili aje mbele ya wanafunzi wenzake darasani
kisha asome aya mbili za kazi ya nyumbani aliyoandika wakati wa kipindi cha
awali kuhusu insha ya maelezo.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaambie wasome
mfano wa insha ya maelezo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 77-
78.
Waulize insha hiyo inahusu nini. Wakiwa wawiliwawili, washirikishe katika
kuandika insha ya maelezo kuhusu umuhimu wa malezi mema, waandike
insha hii kwenye tarakilishi. Kabla ya kuandika insha, waongoze wanafunzi
katika kujadili mada hiyo na muundo wa insha hiyo.
Washirikishe katika kutoa vidokezo kuhusu umuhimu wa malezi mema.
Vidokezo vinaweza kuwa:
ü Malezi mema ni nini?
ü Kutii wazazi, walezi na watu wote.
ü Kuheshimu watu.
ü Kuwa na mwelekeo chanya kuhusu maisha.
ü Kuwa na nidhamu.
ü Kuishi kwa ushirikiano na watu.
Wanafunzi waandike insha ya maelezo kisha uteue mwanafunzi mmoja ili aje
mbele ya wanafunzi wenzake darasani na kusoma kwa sauti insha ya maelezo
kuhusu umuhimu wa malezi mema. Wanafunzi wamsikilize kwa makini.
99
98
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kuitathmini insha hiyo. Mwanafunzi apongezwe
baada ya kusoma insha.
Waelekeze wanafunzi ili wasambaze insha za maelezo walizoandika kwenye
mitandao ili wanafunzi wenzao na wewe mzisome.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa kazi ya nje ya darasa. Waambie wakiwa
shuleni, wakati wa gwaride, wamsikilize kwa makini mwalimu mkuu akiwapa
wanafunzi wote ushauri kisha wanakili hoja zitakazotolewa na mwalimu mkuu katika
gwaride. Baadaye, waandike hoja hizo kimaelezo. Waandike insha ya maelezo wakiwa
nyumbani na wakuletee darasani ili utathmini kazi zao.
Saru
Umoja na wingi wa nomino
Ngeli ya U-I
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 79-80
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika ngeli ya U-I.
2. Kuandika nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
3. Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya U-I.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya U-I.
Mwanafunzi aandike nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
Mwanafunzi asikilize usomaji wa nomino za ngeli ya U-I katika umoja na
wingi kwenye kinasasauti.
Mwanafunzi aandike mafungu ya maneno katika ngeli ya U-I katika umoja na
wingi.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya U-I kwa hati ya mkono ama tarakilishi.
101
100
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 79-80
Kinasasauti
Tarakilishi
Vifaa halisi: mifuko, mikate, mlango, mishipi na miti.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kutoa baadhi ya vifaa halisi na kuwaonyesha
wanafunzi. Unaweza ukawaonyesha mshipi kisha uwaambie wataje jina la
kifaa hicho. Baadaye, waonyeshe mishipi miwili nao wataje kuwa ni mishipi
miwili.
Teua mwanafunzi mmoja aje mbele ya wanafunzi wenzake darasani.
Mwambie aunyooshe mkono wake mmoja na wenzake wataje sehemu hiyo
ya mwili. Pili, anyooshe mikono yake yote na wenzake waseme ni nini
alichonyoosha. Waseme mikono miwili.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaongoze katika
kusoma maneno yaliyo kwenye miti maneno. Maneno hayo yanahusu mimea,
vitu na sehemu za mwili.
Waulize wanafunzi walichogundua kuhusu maneno hayo. Wanaweza kusema
yanahusu mmea, na sehemu za mwili, yameandikwa kwa umoja na ni
nomino. Pia, wanaweza kusema ni maneno katika ngeli ya U-I.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika wingi wa maneno yaliyo kwenye miti
maneno.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 79-80
1. Miti
2. Michungwa
3. Miwa
4. Miembe
5. Mitama
6. Migomba
7. Mihogo
8. Mifuko
9. Miavuli
10. Miamba
11. Misitu
12. Miiba
13. Mikeka
14. Midomo
15. Mishipa
16. Mikono
17. Miguu
18. Miundi
1. miko mikubwa
2. miaka mirefu
3. mikate midogo
4. milango wazi
5. mipera mifupi
6. mioyo mipana
101
100
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: hitimisha kwa kuwaambia kuwa maneno katika ngeli ya U-I huchukua
kiambishi u katika umoja na i katika wingi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 80-81
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika ngeli ya U-I.
2. Kuandika nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
3. Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya U-I.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya U-I.
Mwanafunzi asikilize usomaji wa nomino za ngeli ya U-I katika umoja na
wingi kwenye kinasasauti.
Mwanafunzi aandike mafungu ya maneno katika ngeli ya U-I katika umoja na
wingi.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya U-I kwa hati ya mkono ama tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 80-81
Kinasasauti
Tarakilishi
Vifaa halisi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi yale waliojifunza kuhusu
nomino katika ngeli ya U-I. Watoe mifano kama vile:
ü mshipi-mishipi
ü muwa-miwa
ü mkate-mikate
ü mlango-milango
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasome maneno
yaliyo kwenye jedwali.
Waongoze katika kujaza mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi
katika katika ngeli ya U-I. Wambie wapige chapa kazi hiyo kwenye tarakilishi
na waihifadhi faili hiyo kwa kuiita: ‘Nomino za Ngeli ya U-I’.
103
102
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi katika kutambua nomino katika ngeli ya U-I kwenye
kadi maneno. Nomino zenyewe ni:
1. Mche
2. Miavuli
3. Mifupa
4. Mtambo
5. Mitego
6. Mitihani
7. Mbuyu
8. Moyo
9. Mikoba
Toa kinasasauti na ucheze rekodi ya usomaji wa nomino. Waambie wanafunzi
wasikilize usomaji wa nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
Wanafunzi wasikilize kwa makini. Nomino zenyewe ni:
1. mchango-michango
2. mti-miti
3. mpapai-mipapai
4. msumari-msumari
5. mpera-mipera
6. mzizi-mizizi
7. mfereji-mifereji
8. msaada-misaada
9. mfenesi-mifenesi
10. mzabibu-mizabibu
Wakiwa wawiliwawili, waongoze wanafunzi kutamka nomino walizosikia
kwenye kinasasauti.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia kuwa maneno katika ngeli ya U-I
huchukua kiambishi u katika umoja na i katika wingi katika mafungu.
Umoja na wingi wa sentensi
Ngeli ya U-I
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 81-82
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya U-I katika
umoja na wingi.
2. Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutaja nomino za ngeli ya U-I.
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
103
102
Kimeidhinishwa na KICD
Mwanafunzi asome sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na
wingi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 81-83
Majedwali
Chati
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Andaa majedwali na chati yenye sentensi zilizo na nomino za ngeli ya U-I.
Tafuta tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi mifano ya nomino za ngeli ya
U-I. Kubali mifano ambayo wanafunzi watatoa mradi iwe sahihi. Wanafunzi
wanaweza wakataja:
ü mti-miti
ü mpira-mipira
ü mbuni-mibuni
ü mtego-mitego
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu ili wasome sentensi
zenye nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi kwenye jedwali. Wasome
huku wengine wakisikiliza.
Waulize wanafunzi walichogundua kuhusu sentensi hizo. Wanaweza kusema
zinahusu nomino za ngeli ya U-I.
Waongoze katika kutaja nomino nyingine zilizo katika ngeli ya U-I.
Wanaweza kutoa mifano kama vile:
ü mswaki-miswaki
ü mti-miti
ü mwembe-miembe
ü mguu-miguu
Waambie wanafunzi watunge sentensi katika umoja na wingi wakitumia
nomino watakazotaja. Sentensi ziwe katika umoja na wingi.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 82 la kuandika sentensi katika umoja au wingi.
105
104
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 82
1. Mizizi ilingolewa.
2. Mti ulianguka.
3. Misumari itapigiliwa.
4. Mswaki unapendeza.
5. Mfereji unavuja.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie watunge
sentensi wakitumia nomino walizopewa kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Waambie waandike upya sentensi walizotunga katika wingi.
Wakiwa katika vikundi vyao, waelekeze katika kupiga chapa sentensi zilizo
katika Kitabu cha Mwanafunzi kwenye tarakilishi.
Waambie wanafunzi wawatumie wenzao sentensi walizopiga chapa kupitia
mtandao ili wazisome.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwakumbusha kuwa sentensi za nomino za ngeli
ya U-I huwa na kiambishi u katika umoja na kiambishi i katika wingi ili kubainisha
upatanisho wa kisaru.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 83
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizotungwa kutokana na nomino za ngeli ya U-I katika
umoja na wingi.
2. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
Kushiriki katika mchezo wa kuchopoa kadi za sentensi zenye nomino za ngeli
ya U-I na kusoma sentensi hizo katika umoja na wingi.
105
104
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 83
Kadi maneno
Vikapu au Maboksi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watunge sentensi zenye nomino
za ngeli ya U-I katika umoja na wingi. Wanaweza kutunga sentensi kama vile:
ü Mto umefurika. ü Mito imefurika.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaelekeze
katika kusoma sentensi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 83.
Wakumbushe kuwa baadhi ya sentensi hizo ziko katika hali ya umoja na
nyingine katika hali ya wingi. Waambie zile ambazo ziko katika umoja,
ziandikwe kwa wingi na zile zilizo katika wingi ziandikwe kwa umoja. Hivyo
basi, zitakuwa sentensi kumi na mbili.
Waongoze wanafunzi katika kuandika sentensi zenye nomino za ngeli ya U-I
katika umoja na wingi kwenye kadi. Warejelee sentensi zilizo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi.
Wape wanafunzi katika kila kikundi kikapu kimoja au boksi moja na
uwaambie waweke kadi zote zenye sentensi kwenye kikapu au boksi hiyo.
Waongoze wanafunzi katika kuchopoa kadi moja moja na kusoma sentensi
zilizoandikwa kwenye kila kadi. Wasome sentensi hizi kwa zamu.
Waelekeze wanafunzi katika kupanga sentensi zilizo katika umoja pamoja na
za wingi pamoja.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa sentensi za nomino
za ngeli ya U-I huwa na kiambishi u katika umoja na kiambishi i katika wingi.
107
106
Kimeidhinishwa na KICD
BENDERA YA TAIFA
6
Nyenzo
Unaweza kutumia nyenzo zifuatazo:
Vifaa halisi: bendera.
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, tabuleti, rununu na projekta
Kinasasauti
Picha
Michoro
Chati
Kadi maneno
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
Vibonzo
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Sehemu ya bendera ya Taifa inakuza umilisi wa kimsingi. Baadhi ya umilisi huo ni:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wakifanya mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika
Utangulizi
Bendera ni kitambaa chenye rangi na nembo, ambacho hutumiwa kama alama ya
utambulisho na mawasiliano. Bendera ya taifa hutambulisha taifa moja kutoka kwa
jingine. Kila taifa lina bendera yake. Bendera hupandishwa na kushushwa wakati
maalumu. Bendera ya Kenya hutumika shuleni, osini na katika taasisi nyingine.
Bendera ya Kenya ilianza kutumika tarehe 12 Disemba 1963 Kenya ilipopata uhuru.
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kukariri au kuimba shairi kwa kuzingatia matamshi na mahadhi mbalimbali.
2. Kusoma na kutambua umuhimu wa ujumbe wa makala husika.
3. Kuandika insha ya wasifu kwa kufuata kanuni zifaazo akizingatia vivumishi na
vielezi.
4. Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
5. Kutumia nomino za ngeli ya KI-VI katika mawasiliano.
107
106
Kimeidhinishwa na KICD
vikundi kama kukariri shairi au kusoma makala kwa pamoja, wanakuza ushirikiano
na mawasiliano. Mijadala baina ya wanafunzi kuhusu bendera ya taifa itaimarisha
mawasiliano na kukuza ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi
wakisambaza habari kuhusu bendera kwenye mitandao wakitumia vyombo vya
kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi,
kipakatalishi, video, tabuleti, projekta, intaneti, mitandao na tovuti ili mwanafunzi
ajifunze masuala ya bendera na aweze kutumia tarakilishi kuandika na kuhifadhi kazi
yake kuhusu bendera kwenye faili.
(ch) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi
kuhusu bendera. Umilisi huu humpa mwanafunzi hamu ya kukamilisha sentensi. Pia,
atatafakari maswali ya ziada kuhusu bendera ya taifa. Mwanafunzi anaweza kuwa na
hamu ya kutaka kutumia vyombo vya kidijitali ili atafute habari zaidi kuhusu asili ya
bendera ya Kenya.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kutunga sentensi kwa kutumia tarakilishi,
tabuleti au simu ya mkononi. Pia ubunifu ukuzwe na kuimarishwa kupitia kusakura
mitandao ili kutafuta habari kuhusu bendera. Ubunifu utadhihirika mwanafunzi
akiandika insha ya wasifu.
(e) Kujiamini
Umilisi huu utakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kukariri ama kuimba shairi. Pia, kujiamini kutakuzwa kupitia mwanafunzi
kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu utakuzwa kupitia kumpa mwanafunzi swali la kutafakari, kukiria na
kutafuta jawabu lake ambalo halimo kwenye matini. Kwa mfano, mwanafunzi anaweza
kuulizwa: Bendera ya Kenya hupandishwa lini?
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Kujitambua na kujithamini kupitia kukariri au kuimba mashairi na
kufungua na kufunga tarakilishi.
(b) Stadi za maisha zinazohusisha mwanafunzi kujieleza, kushiriki katika
vikundi na kuchangia katika mijadala.
109
108
Kimeidhinishwa na KICD
(ch) Uraia utakuzwa kupitia wanafunzi kufanya kazi pamoja, kushiriki kikamilifu
katika kuheshimu bendera ya Kenya kwa kusimama wima inapopandishwa
na kushushwa.
Uhusiano na maadili
Heshima itakuzwa kwa wanafunzi kukariri na kujadiliana kwa vikundi.
Kupitia shughuli hii, wanafunzi watajifunza kuwasikiliza wenzao
wanapozungumza.
Uwajibikaji utadhihirika kupitia wanafunzi kutunza na kuhifadhi vyombo vya
kidijitali, kuwajibikia majukumu katika vikundi na kufuata mafunzo katika
shairi.
Shughuli za huduma za kijamii
Kushiriki katika kupandisha na kushusha bendera ya taifa.
Kuwahamasisha wenzake kuipenda na kuiheshimu bendera ya taifa na pia
kutumia mashairi katika mawasiliano.
Wanafunzi watawakariria watu mashairi katika haa mbalimbali.
Uhusiano na masomo mengine
Sehemu ya bendera inaingiliana na masomo mengine kama vile:
1. Katika somo la English Activities kuna mada kuhusu ushairi ambazo hufunzwa ili
kukuza stadi ya kusikiliza na kuzungumza.
2. Somo la Music lina shughulikia nyimbo za mahadhi mbalimbali sawia na
wanavyojifunza kuimba wimbo wa taifa.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Unaweza kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kwa kutumia baadhi
ya mbinu hizi:
Wape wanafunzi wenye hitilafu za viungo fulani vya mwili kama vile: miguu
na mikono shughuli mbadala. Kwa mfano, badala ya kusimama wakishiriki
katika kupandisha na kushusha bendera, wanaweza kuketi na kuwatazama
wenzao wakipandisha bendera baada ya wao kukunja bendera hizo.
Watengee wanafunzi wanaotatizika kuelewa vipindi fulani muda maalumu wa
kurudia shughuli baada ya ujifunzaji darasani.
Tumia mbinu na nyenzo tofauti kufunza vipengele mbalimbali. Tumia video,
michoro, picha au rekodi za kinasasauti.
Kwa wasioona, unaweza kushirikisha vifaa halisi ili waguse na kushika.
Kwa wanafunzi wanaochukua muda mrefu kuelewa na kufanya shughuli
darasani, uwe subira nao wanaposoma, wanapoandika, wanapozungumza au
waposhiriki katika shughuli mbalimbali darasani.
109
108
Kimeidhinishwa na KICD
Wale ambao wana uwezo wa juu darasani, wape kazi ya ziada na changamano
kama vile: kuchora na kuipaka rangi bendera kwenye tarakilishi na kutunga
sentensi zaidi.
Kusikiliza na Kuzungumza
Methali: Kujieleza kwa ufasaha
Ushairi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 84-85
Waelekeze wanafunzi kutazama picha kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 84
wakiwa wawiliwawili kisha uwaongoze katika kutambua picha hiyo ni ya nini. Waongoze
ili waweze kutaja rangi zilizo kwenye bendera. Waelekeze wanafunzi kutambua bendera
ya taifa hupatikana katika maeneo gani mbali na shuleni. Wanaweza wakataja: kwenye
vituo vya polisi, osi za utawala, osi za ubalozi na magari ya viongozi wa ngazi za juu
katika taifa.
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kukariri au kuimba shairi kwa kuzingatia matamshi na mahadhi mbalimbali.
2. Kueleza maana ya msamiati uliotumiwa katika shairi.
3. Kutumia msamiati uliotumiwa katika shairi kuboresha mawasiliano.
4. Kueleza ujumbe wa shairi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi akariri au aimbe shairi.
Mwanafunzi asikilize shairi likikaririwa au likiimbwa.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kukariri au kuimba shairi.
Mwanafunzi atambue msamiati uliotumika katika shairi.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kujadili ujumbe katika shairi.
Mwanafunzi ajibu maswali kutokana na shairi alilosikia, aliloimba au alilokariri.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 84-85
Bendera
Shairi
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
111
110
Kimeidhinishwa na KICD
Maandalizi ya mwalimu
Rekodi shairi kwenye kanda ya sauti au rununu.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi hiki kwa kuwaonyesha wanafunzi bendera ya Kenya na
kuwauliza kifaa hicho ni nini. Wanaweza kusema ni bendera ya Kenya.
Waulize wanafunzi rangi za bendera ya Kenya. Wanafunzi wataje kwa
ufupi. Waulize wazalendo hufanya nini bendera ya taifa inapopandishwa au
kushushwa nao wajibu kuwa wazalendo husimama kama ishara ya heshima
kwa bendera ya taifa.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaelekeze katika
kukariri shairi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 85. Waongoze
katika kutafakari shairi linazungumzia nini. Wanafunzi waweze kugundua
kuwa shairi linazungumzia uzalendo kwa kuheshimu bendera ya Kenya na
maana za rangi za bendera ya Kenya.
Waongoze kueleza maana ya maneno kama yalivyotumika katika shairi.
Waelekeze katika kutambua kibwagizo cha shairi. Kibwagizo ni: Asante
kipenzi chetu, bendera yetu ya Kenya. Wafafanue maana ya kibwagizo hicho.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje sehemu zingine
ambazo wamewahi kuona bendera ya Kenya mbali na shuleni.
Majibu ya zoezi la 1, ukurasa wa 85
1. Shairi linahusu bendera ya Kenya.
2. Tathmini majibu ya wanafunzi kwa kusoma maelezo waliyotoa kuhusu maneno
yaliyotumika kwenye shairi.
3. Asante kipenzi chetu, bendera yetu ya Kenya.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 86
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kukariri au kuimba shairi kwa kuzingatia matamshi na mahadhi mbalimbali.
2. Kueleza maana ya msamiati uliotumiwa katika shairi.
3. Kutumia msamiati ulio katika shairi kuboresha mawasiliano.
4. Kueleza ujumbe wa shairi.
111
110
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi akariri au aimbe shairi.
Mwanafunzi asikilize shairi likikaririwa au likiimbwa.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kukariri au kuimba shairi.
Mwanafunzi atambue msamiati uliotumika katika shairi.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kujadili ujumbe katika shairi.
Mwanafunzi ajibu maswali kutokana na shairi alilosikia, aliloimba au
alilokariri.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 86
Shairi
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Kinasasauti
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yatakayofunzwa.
Rekodi shairi kwenye kanda ya sauti au tabuleti ama rununu.
Tafuta tarakilishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi ili wasikilize shairi
lililorekodiwa likikaririwa kutoka kwa tepurekoda au kinasa sauti.
Shairi lenyewe ni:
BENDERA TUNAKUPENDA DAIMA
Bendera tunakuenzi, kipenzi chetu daima,
Kiwakilishi cha mapenzi, ya taifa letu daima,
Upandishwapo kipenzi, tunasimama kwa heshima,
Bendera ya tangu enzi, tunakupenda daima.
Tunapokupandisha juu, husimama kwa heshima,
Kwetu sisi kuwa huru, kweli umehakikisha,
Ishara tosha ya uhuru, uzalendo wa dhamana,
Bendera ya tangu enzi, tunakupenda daima.
113
112
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha funzo kwa kuwauliza wanafunzi kueleza kibwagizo
ni nini katika shairi.
Kusoma
Kusoma kwa kina
Makala
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 86-88
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kusoma makala kwa ufasaha.
2. Kutambua ujumbe wa makala.
3. Kujibu maswali kutokana na makala.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma makala.
Kujadili na wenzake kuhusu makala.
Kutumia kamusi kupata maana za msamiati uliotumika kwenye makala.
Kujibu maswali kutokana na makala.
Kitambulisho cha taifa, hili kwa kila daraja,
Weusi rangi twapenda, wakilisho la Wakenya,
Wekundu uliojitenga, kuwakilisha uhuru tosha,
Bendera ya tangu enzi, tunakupenda daima.
Ngao yetu twakupenda, ulinzi wako twatambua,
Utajiri dhihirika, kijani kibichi tosha,
Weupe huonekana, amani tele ishara,
Bendera ya tangu enzi, tunakupenda daima.
113
112
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 86-88
Kamusi
Tarakilishi
Tabuleti
Rekoda au simu
Maandalizi ya mwalimu
Soma makala kabla ya uwasilishaji darasani.
Tafuta tarakishili, rekoda na simu.
Tafuta kamusi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu.
Waambie wasome kwa zamu mchezo wa kuigiza, ‘Kaugua Augua kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 86-87.
Waelekeze katika kuigiza mchezo huo waliousoma huku wanafunzi wengine
wakitazama. Vikundi vya wanafunzi vifanye hivi kwa zamu.
Waongoze wanafunzi katika kujadili ujumbe wa mchezo huo wa kuigiza.
Ujumbe ni kuwa: tunapokuwa na dalili zozote za ugonjwa, twende hospitalini
ili kupata matibabu.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua wahusika walio katika mchezo huo.
Wanafunzi wataje: Kaugua, mamake na Daktari Tiba kama wahusika katika
mchezo huo wa kuigiza.
Waongoze katika kutambua ugonjwa aliougua Kaugua. Sharti watambue
kuwa Kaugua aliugua ugonjwa wa homa ya mafua.
Washirikishe katika kutambua msamiati wa adabu na heshima katika mchezo
huo. Maneno ya adabu au upole yaliyotumika ni kama vile:
ü Karibu ü Asante ü Tafadhali
Waongoze wanafunzi katika kueleza maana ya maneno waliyoulizwa.
Unaweza kuwaelekeza kutafa maana ya maneno hayo kwenye kamusi.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi nafasi ya kuigiza mchezo
waliousoma. Tathmini jinsi wanafunzi wanavyoshiriki katika maigizo. Wapongeze
wanafunzi watakaoigiza vyema kwa kuwapa zawadi ndogondogo ama kuwapigia
mako.
115
114
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 88-89
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kusoma makala kwa ufasaha.
2. Kutambua ujumbe wa makala.
3. Kujibu maswali kutokana na makala.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma makala.
Kujadili kuhusu ujumbe na msamiati kwenye makala.
Kutumia kamusi kupata maana za msamiati uliotokana na makala.
Kujibu maswali kutokana na makala.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 88-89
Kamusi
Mchoro
Kijiti
Kitambaa
Rangi
Brashi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame mchoro ulio kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi na waseme wanachoona. Huo ni mchoro wa
wanariadha wa Kenya wakisherehekea ushindi wao kwa kupeperusha bendera
ya Kenya.
Teua mwanafunzi mmoja ili aje mbele ya wanafunzi wenzake na kusoma aya
ya makala. Mbali na kuja mbele ya darasa, wanafunzi wanaweza wakasoma
wakiwa wameketi kwenye madawati yao hasa wale wenye matatizo katika
viungo vyao vya mwili. Sisitiza kusoma kwa sauti na kwa usahihi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaongoze katika
kujadili ujumbe unaojitokeza katika makala: ‘Ushindi wa Bendera ya Kenya.
Waelekeze katika kutaja maeneo ambamo bendera ya Kenya hupatikana.
Maeneo haya ni kama vile:
ü shuleni,
ü osi za serikali,
ü kwenye baadhi ya magari ya viongozi wa taifa,
ü kwenye makao makuu ya osi za kibalozi.
115
114
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kutaja rangi za bendera ya Kenya. Hakikisha
kuwa wanazingatia mfuatano wa rangi za bendera kutoka juu hadi chini.
Waeleze rangi hizo huashiria nini. Waambie kuwa:
ü Nyeusi huashiria rangi ya Wakenya.
ü Nyekundu ni ishara ya damu iliyomwagika wakati wa kupigania uhuru.
ü Kijani ni rangi ya maliasili, utajiri na kilimo chetu.
ü Nyeupe huashiria amani tuliyo nayo nchini mwetu.
Wanafunzi wajadili ni kwa nini watu husimama wima wakati wa kupandisha
na kushusha bendera. Sharti waseme kuwa kusimama wima ni kutoa heshima
kwa bendera ya taifa.
Waelekeze wanafunzi katika kutafuta maana ya maneno hayo kwenye kamusi.
Watafute maana ya: mabepari, ngao na taifa.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie wakiwa
wannewanne watafute kitambaa cheupe kisha wachore bendera ya Kenya na kuipaka
rangi. Pia, wakiwa nje ya darasa, watumie uzi na kijiti kupandisha na kushusha bendera.
Kuandika
Insha ya wasifu
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 89-90
Matokeo maalum yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya wasifu kwa kuzingatia muundo.
2. Kuandika insha ya wasifu kwa kufuata kanuni zifaazo akizingatia vivumishi na
vielezi.
3. Kuchangamkia utunzi mzuri wa kuandika insha ya wasifu ili kukuza ubunifu.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue muundo wa insha ya wasifu.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kuandika insha ya wasifu.
Mwanafunzi aandike insha ya wasifu.
117
116
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi
Insha kielelezo (insha ya wasifu)
Tarakilishi au tabuleti
Maandalizi ya mwalimu
Tayarisha insha kielelezo (insha ya wasifu)
Tafuta tarakilishi au tabuleti
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yaliyomo kabla ya kipindi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuhusu insha ya wasifu.
Waambie wanafunzi wajigawe katika vikundi vya wannewanne kisha
uwaongoze katika kujadili kuhusu insha ya wasifu. Mambo yafuatayo
yazingatiwe katika mjadala:
ü Insha ya wasifu hutoa maelezo kuhusu sifa za mtu, kitu au mahali. Insha
ya wasifu hufafanua namna mtu, mahali au kitu kilivyo. Unapoandika
insha ya wasifu unapaswa kutoa habari kamili kuhusu mtu, kitu au eneo.
ü Zingatia mambo haya uandikapo insha ya wasifu:
(a) Umbo
(b) Sura
(ch) Tabia
(d) Vitendo
(e) Mazingira
(f) Rangi
(g) Vipimo
(h) Hali
(i) Kimo
ü Insha ya wasifu inaweza kuwa kuhusu mtu, darasa, mnyama, kaunti,
ndege, nchi, kitu, shule au shamba.
Wanafunzi wajadili muundo wa insha ya wasifu ambao ni:
ü Utangulizi ü Mwili/kiini ü Hitimisho
Kipindi cha 2
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya wasifu kwa kuzingatia muundo.
2. Kuandika insha ya wasifu kwa kufuata kanuni zifaazo akizingatia vivumishi na
vielezi.
3. Kuwasambazia wenzake insha ya wasifu aliyoandika kupitia mtandao wa
intaneti.
117
116
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue muundo wa insha ya wasifu.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kuandika insha ya wasifu.
Mwanafunzi aandike insha ya wasifu.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 90-91
Insha kielelezo (insha ya wasifu)
Tarakilishi au tabuleti
Mchoro wa bendera ya Kenya
Maandalizi ya mwalimu
Tayarisha insha kielelezo (insha ya wasifu)
Tafuta tarakilishi au tabuleti
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yaliyomo kabla ya kipindi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi insha ya wasifu inahusu
nini.
Waongoze katika kujadili kuhusu insha ya wasifu.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie watazame
mchoro kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 90 kisha wawaeleze
wenzao wanachoona.
Waongoze katika kutaja rangi za bendera ya Kenya zilizo kwenye mchoro.
Waeleze mbali na rangi ni vitu gani vingine vinavyopatikana katika bendera
ya Kenya.
Wagawe wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi watatuwatatu na uwaongoze
katika kuandika insha ya wasifu kuhusu ‘Bendera ya Kenya.
Waelekeze kwenye vidokezo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 90.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi inayohusu kuandika
insha ya wasifu kuhusu bendera ya taifa kwa kuzingatia vidokezo vilivyoorodheshwa
kitabuni. Wape wanafunzi kazi ya zoezi la 1 ili waandike insha za wasifu na kuzisambaza
kwa wenzao kupitia mtandao wa intaneti.
119
118
Kimeidhinishwa na KICD
Saru
Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya LI-YA
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 91-92
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika ngeli ya LI-YA.
2. Kuandika nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
3. Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-YA.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya LI-YA.
Mwanafunzi aandike nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Mwanafunzi asikilize usomaji wa nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na
wingi kwenye kinasasauti.
Mwanafunzi aandike mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-YA katika umoja
na wingi.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya LI-YA kwa hati ya mkono ama tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 91-92
Kinasasauti/rekoda
Tarakilishi
Vifaa halisi: jani,ua,dirisha,chungwa
Wanafunzi
Chati
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kutoa vifaa halisi na kuwaonyesha wanafunzi. Kwanza,
waonyeshe jani moja. Waambie waseme jina la kifaa hicho. Watasema hilo ni
jani. Waonyeshe majani matatu nao wataje kuwa ni majani matatu.
119
118
Kimeidhinishwa na KICD
Teua mwanafunzi mmoja aje mbele ya wanafunzi wenzake darasani.
Mwambie afunge jicho moja kisha awaulize wanafunzi sehemu hiyo ya
mwili inaitwaje. Wakisema jicho, mwenzao afunge macho yake yote. Waulize
wanafunzi mwenzao amefunga nini.
Waambie wanafunzi wote wasome maneno kwenye kapu maneno lililo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 91. Waambie watumie rekoda
kunasa sauti zao wakisoma.
Waelekeze katika kugundua kuwa maneno yaliyo kwenye kapu maneno hilo
ni nomino katika ngeli ya LI-YA.
Waongoze wanafunzi katika kuweka maneno hayo kwenye jedwali katika
umoja na wingi.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 92
Umoja Wingi
embe maembe
jani majani
sikio masikio
gari magari
dirisha madirisha
ua maua
yai mayai
chungwa machungwa
tunda matunda
jino meno
Waelekeze wanafunzi kukamilisha jedwali kwa kutumia mafungu ya
nomino za ngeli ya LI-YA.
Umoja Wingi
sikio linalouma masikio yanayouma
tunda langu matunda yangu
ua limechomwa maua yamechomwa
dirisha kubwa madirisha makubwa
daraja pana madaraja mapana
darasa lao madarasa yao
121
120
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: Hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa maneno katika
ngeli ya LI-YA huchukua kiambishi li katika umoja na ya katika wingi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 93-94
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika ngeli ya LI-YA.
2. Kuandika nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
3. Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-YA.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya LI-YA.
Mwanafunzi asikilize usomaji wa nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na
wingi kwenye kinasasauti.
Mwanafunzi aandike mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-YA katika umoja
na wingi.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya LI-YA kwa hati ya mkono ama tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 93-94
Kinasasauti
Tarakilishi
Vifaa halisi
Wanafunzi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu
na uwaongoze katika kusoma maneno yaliyo kwenye mti maneno.
Waongoze kutambua nomino zilizo katika ngeli ya LI-YA kwenye mti maneno
huo. Watambue nomino kama vile:
ü Jiwe
ü Jani
ü Jiko
ü Swali
ü Darasa
ü Jicho
ü Madebe
ü Masoko
ü Chungwa
ü Godoro
ü Jumba
Waambie wanafunzi wapige chapa nomino hizo kwenye tarakilishi, wahifadhi
faili hiyo na waiite, ‘Nomino za Ngeli ya U-I
121
120
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi ili waweze kuandika nomino za ngeli ya LI-YA katika
wingi.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 93-94
Umoja Wingi
Tawi Matawi
Tangazo Matangazo
Jicho Macho
Jitu Majitu
Gazeti Magazeti
Waelekeze wanafunzi kuandika nomino katika umoja. Majibu ni:
Wingi Umoja
Mawe Jiwe
Matunda Tunda
Majembe Jembe
Majengo Jengo
Masanduku Sanduku
Waongoze wanafunzi wote darasani ili wasikilize nomino za ngeli ya LI-YA
katika umoja na wingi zikisomwa kwenye tepurekoda. Nomino zenyewe ni:
1. jina -majina
2. kufuli-makufuli
3. shati -mashati
4. bwawa-mabwawa
5. mpera-mipera
6. zulia-mazulia
Waambie wanafunzi wakiwa peke yao, waandike nomino hizo kwenye
madaari yao. Tathmini kazi ya kila mwanafunzi.
Hitimisho: wape wanafunzi zoezi katika Kitabu cha Mwanafunzi. Zoezi hili ni la
kujaza mapengi kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa nomino katika ngeli
ya LI-YA. Wakumbushe kuwa maneno katika ngeli ya LI-YA huchukua kiambishi li
katika umoja na ya katika wingi. Wanakili hilo kwenye madaari.
123
122
Kimeidhinishwa na KICD
Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya LI-YA
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 94-96
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-YA katika
umoja na wingi.
2. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutaja nomino za ngeli ya LI-YA.
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Mwanafunzi asome sentensi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja
na wingi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 94-96
Majedwali
Chati
Tarakilishi
Kikapu
Kadi
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi kabla ya kipindi.
Andaa majedwali yenye sentensi zenye nomino katika ngeli ya LI-YA.
Tayarisha chati yenye sentensi zilizo na nomino za ngeli ya LI-YA katika
umoja na wingi.
Tafuta tarakilishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya nomino za
ngeli ya LI-YA. Kubali mifano ambayo wanafunzi watatoa mradi ni sahihi.
Wanaweza wakataja:
ü jina -majina
ü kufuli-makufuli
ü shati -mashati
ü bwawa-mabwawa
ü mpera-mipera
ü zulia-mazulia
123
122
Kimeidhinishwa na KICD
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwelekeze katika
kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Wasome huku wengine wakisikiliza.
Waongoze katika kutunga sentensi wakitumia nomino za ngeli ya LI-YA
katika umoja. Unaweza kuwauliza wanafunzi watathmini majibu ya wenzao.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika sentensi walizotunga kwa umoja ziwe
katika wingi. Waambie wanafunzi watathmini majibu ya wenzao. Tathmini
kazi za wanafunzi. Wapongeze wanafunzi kwa kazi nzuri itakayofanywa.
Kwa wale ambao watapata matatizo katika shughuli hii, waongoze ili wafanye
shughuli hii ifaavyo.
Waongoze wanafunzi kuandika sentensi zenye nomino za ngeli ya LI-YA
katika umoja na wingi kwenye kadi. Warejelee sentensi zilizo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi, ukurasa wa 95-96.
Tafuta kikapu kimoja na uwaambie wanafunzi waweke kadi zote zenye
sentensi kwenye kikapu hicho.
Waongoze wanafunzi katika kuchopoa kadi moja moja zenye sentensi na
kuzisoma sentensi hizo. Waulize iwapo sentensi wanazosoma ni za umoja au
wingi.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwakumbusha kuwa sentensi za
nomino ya ngeli ya LI-YA huwa na kiambishi li katika umoja na kiambishi ya katika
wingi ili kubainisha upatanisho wa kisaru.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 96-97
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-YA katika
umoja na wingi.
2. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Kushiriki katika mchezo wa kuchopoa kadi za sentensi zenye nomino za ngeli
ya LI-YA katika umoja na wingi.
125
124
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 96-97
Kikapu Kadi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watunge sentensi zenye nomino
za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi. Wanaweza kutunga sentensi kama
vile:
ü Dawati limenunuliwa. ü Madawati yamenunuliwa.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaelekeze katika
kusoma sentensi katika jedwali kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa
96. Waeleze kwamba sentensi zimeparaganywa katika umoja na wingi.
Waelekeze wanafunzi katika kupanga kila sentensi kwenye jedwali na sentensi
yake sahihi katika umoja na wingi. Jedwali hilo lionekane hivi:
Umoja Wingi
Daraja lililobomoka litajengwa. Madaraja yaliyobomoka yatajengwa.
Jiko jipya limenunuliwa. Majiko mapya yamenunuliwa.
Chungwa lililoiva litamenywa. Machungwa yaliyoiva yatamenywa.
Lango kubwa litafunguliwa. Malango makubwa yatafunguliwa.
Shimo kubwa litachimbwa. Mashimo makubwa yatachimbwa.
Waongoze wanafunzi katika kutaja nomino nyingine zilizo katika ngeli ya LI-
YA, katika umoja na wingi. Wataje nomino kama vile:
ü jicho-macho
ü hindi-mahindi
ü neno-maneno
ü lori-malori
ü nanasi-
mananasi
ü jina-majina
ü shati-mashati
ü tawi-matawi
ü godoro-
magodoro
ü duka-maduka
ü jiwe-mawe
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi sahihi wakitumia nomino za
ngeli ya LI-YA. Tathmini kazi za wanafunzi ukiwakosoa pale wanapokosea.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaelekeze
katika kutumia tarakilishi kupiga chapa sentensi zilizo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 97. Waambie wawatumie wanafunzi wenzao
sentensi hizi kupitia mtandao wa intaneti.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa zoezi fupi la kutunga sentensi katika umoja
kutokana na nomino walizopewa katika kazi mradi. Baadaye, waambie watunge
sentensi hizo katika wingi. Wakumbushe kuwa sentensi za nomino ya ngeli ya LI-YA
huwa na kiambishi li katika umoja na ya katika wingi.
125
124
Kimeidhinishwa na KICD
Umoja na Wingi wa Nomino katika Ngeli ya KI-VI
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 97-98
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika ngeli ya KI-VI.
2. Kuandika nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
3. Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya KI-VI.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya KI-VI.
Mwanafunzi aandike nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
Mwanafunzi asikilize usomaji wa nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na
wingi kwenye kinasasauti.
Mwanafunzi aandike mafungu ya maneno katika ngeli ya KI-VI katika umoja
na wingi.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya KI-VI kwa hati ya mkono ama tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 97-98
Kinasasauti
Rekoda
Tarakilishi
Vifaa halisi: kiti, kitabu, kikombe, kikapu na kiazi
Wanafunzi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kutoa vifaa halisi na kuwaonyesha wanafunzi. Kwanza,
waonyeshe kitabu kimoja kisha uwaambie waseme jina la kifaa hicho.
Watasema, ‘kitabu’. Waonyeshe vitabu viwili nao wataje kuwa ni vitabu viwili.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasome maneno
yaliyo kwenye kadi. Waongoze katika kusoma maneno hayo kwa kuhakikisha
kuwa wanayatamka kwa usahihi.
Waongoze wanafunzi ili waweze kupanga maneno yaliyo kwenye kadi kwenye
jedwali katika umoja na wingi. Wanafunzi wapange maneno hayo hivi:
127
126
Kimeidhinishwa na KICD
Umoja Wingi
cheo vyeo
kitumbua vitumbua
chombo vyombo
kitanda vitanda
kidole vidole
kijiti vijiti
chumba vyumba
kisima visima
chuma vyuma
kitanda vitanda
Waambie wanafunzi wakamilishe jedwali kwa kutumia mafungu ya nomino
za ngeli ya KI-VI.
Umoja Wingi
Chakula kimeiva. Vyakula vimeiva.
Kitabu chako. Vitabu vyako.
Chama kikuu. Vyama vikuu.
Chuma chake. Vyuma vyake.
Kisu kikali. Visu vikali.
Hitimisho: Hitimisha kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa maneno katika nomino
za ngeli ya KI-VI huchukua kiambishi ki katika umoja na vi katika wingi. Pia, nomino
katika ngeli ya KI-VI ni za vitu vya kawaida na visivyo na uhai.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 98-99
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika ngeli ya KI-VI.
2. Kuandika nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
3. Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya KI-VI.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya KI-VI.
Mwanafunzi asikilize usomaji wa nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na
wingi kwenye kinasasauti.
Mwanafunzi aandike mafungu ya maneno katika ngeli ya KI-VI katika umoja
na wingi.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya KI-VI kwa hati ya mkono ama tarakilishi.
127
126
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 98-99
Kinasasauti
Tarakilishi
Vifaa halisi
Wanafunzi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watambue nomino zilizo katika
ngeli ya KI-VI kwenye chati. Watambue nomino kama vile: visu, cherehani,
kitana, vijiko, kioo, kitabu, chungu, vyuo, vyura, chombo na chama.
Waongoze wanafunzi katika kuandika nomino za ngeli ya KI-VI zilizo katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 99 kwenye tarakilishi.
Waelekeze katika namna ya kukoleza rangi viambishi vya ngeli ya KI-VI
katika maneno waliyoandika kwenye tarakilishi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie watunge
sentensi katika umoja na wingi wakitumia nomino walizopewa katika Kitabu
cha Mwanafunzi.
Waongoze wanafunzi ili waweze kujaza mapengo kwenye jedwali kwa
kutumia viambishi vya ngeli ya KI-VI. Wanafunzi watathmini majibu ya
wenzao. Tathmini kazi za wanafunzi na kuwatuza wanaofanya kazi yao
ipasavyo.
Hitimisho: hitimisha kwa kuwakumbusha wanafunzi kwamba maneno katika ngeli ya
KI-VI huchukua kiambishi ki katika umoja na vi katika wingi. Waambie kuwa nomino
nyingi katika ngeli ya KI-VI huanza kwa viambishi ki au ch katika umoja na vi au vy
katika wingi.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 99
1-3. Tathmini jinsi wanafunzi wanavyoshiriki katika shughuli ya kupiga
chapa, kuhariri na kuhifadhi kazi zao kwenye tarakilishi na kutunga sentensi.
Hakikisha kuwa wamezingatia upatanisho wa kisaru wakati wa kutunga
sentensi.
Umoja Wingi
kiazi Viazi
Chakula Vyakula
Kisogo Visogo
Kituo Vituo
Kicheko Vicheko
129
128
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Shughuli ya ujifunzaji na ufunzaji hufanikiwa kutokana na uteuzi, maandalizi na
matumizi ya nyenzo. Hakikisha umeandaa nyenzo mwafaka ili kufanikisha shughuli
ya ufunzaji na ujifunzaji wa mada ya matunda na mimea. Unaweza kutumia nyenzo
zifuatazo:
Mimea na matunda: papai, tufaha, chungwa na embe
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, vipakatalishi, tabuleti, rununu na projekta
Kinasasauti
Mtandao
Tovuti
Picha
Michoro
Chati
Kadi
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
MATUNDA NA MIMEA
7
Utangulizi
Mmea ni kitu kinachoota, chenye uhai kilicho na mzizi, shina na majani ambacho
aghalabu hutokana na mbegu au tawi. Mimea huwapa binadamu matunda na
mazao mbalimbali. Mifano ya mimea ni: mbuni, mpera, mbuyu, mpapai, mgomba,
mzabibu na mwembe.
Tunda ni zao la mmea ambalo aghalabu huhifadhi mbegu. Mifano ya matunda ni:
chungwa, nanasi, papai, zabibu, tufaha, ndizi na embe.
Mada hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutumia nahau za maadili na uraia katika mawasiliano.
2. Kusoma matini kwa ufasaha ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumika.
3. Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
4. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli za KI-VI na LI-LI katika umoja
na wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
129
128
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wafanye mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika vikundi
kama kusoma kwa zamu nahau za maadili au kusoma makala kwa pamoja. Mijadala
baina ya wanafunzi kuhusu matunda na mimea itaimarisha mawasiliano na kukuza
ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi wakisambaza habari kuhusu mimea
na matunda mbalimbali kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi,
kipakatalishi, video, tabuleti, projekta, intaneti, mitandao na tovuti ili mwanafunzi
ajifunze masuala mbalimbali ya matunda na mimea. Mwanafunzi ataweza kutumia
tarakilishi kuandika na kuhifadhi kazi yake kuhusu matunda na mimea kwenye faili.
(ch) Hamu ya Ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
matunda na mimea. Utampa mwanafunzi hamu ya kufahamu mimea na mazao. Pia,
atatafakari maswali ya ziada kuhusu matunda na mimea. Mwanafunzi anaweza kuwa
na hamu ya kutaka kutumia vyombo vya kidijitali ili atafute habari zaidi kuhusu mada
ya matunda na mimea.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika majina ya matunda na mimea kwa
kutumia tarakilishi, tabuleti au simu ya mkononi. Pia ubunifu ukuzwe na kuimarishwa
kupitia kusakura mitandao ili kutafuta matunda mbalimbali. Ubunifu utadhihirika
mwanafunzi akiandika insha ya maelezo.
(e) Kujiamini
Umilisi huu utakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kutaja na kutoa maelezo kuhusu mimea na matunda. Pia, kujiamini
kutakuzwa kupitia mwanafunzi kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli za KI-VI
na LI-LI.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu unakuzwa kupitia wanafunzi kukiria kuhusu maana za nahau na
matumizi yake.
131
130
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano wa masuala mtambuko
(a) Kujitambua na kujithamini kupitia kutunga sentensi akitumia nahau za
maadili na uraia
(b) Stadi za maisha kupitia kutumia nahau kujieleza kwa njia ya upole, kushiriki
katika mijadala ya vikundini n.k.
Uhusiano wa maadili
Nahau za maadili na uraia zinakuza heshima na umoja hasa katika kufanya
kazi kwa vikundi na wanafunzi wanaposhirikiana katika majadiliano.
Uwajibikaji kupitia mwanafunzi kutunza na kuhifadhi vyombo vya kidijitali
anavyotumia katika ujifunzaji.
Shughuli za huduma za kijamii
Kushiriki katika kutunza mimea katika jamii kwa kuinyunyizia maji na
kuipalilia.
Kuwahamasisha wenzake nyumbani na shuleni kuhusu umuhimu wa
matunda na mimea.
Uhusiano na masomo mengine
1. Science and Technology activities: somo hili linafundisha kuhusu mimea na
matunda kwa mapana.
2. English Activities: nahau zinafunzwa katika somo hili ili kukuza stadi ya kusikiliza
na kuzungumza.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Sehemu hii inahusu sehemu nne kuu. Kuna sehemu ya kusikiliza na kuzungumza,
kusoma, kuandika na saru. Kwa somo linalohusu kusikiliza na kuzungumza,
hakikisha kuwa wanafunzi wasio na uwezo wa kuona wamepata mashine za breli
darasani ili ziwasaidie katika kutambua maneno. Kwa wanafunzi wenye matatizo
ya kusikia na kuzungumza, unaweza kumwalika mfasiri wa lugha ishara ili awasaidie
wanafunzi hao katika kushiriki kwenye somo kikamilifu. Pia, unaweza ukatumia
vifaa vya kiteknolojia kama vile: projekta ili kuwaonyesha wanafunzi baadhi ya picha
zinazohusu nyumbani kutoka mtandaoni. Ili kuwahusisha wanafunzi wenye matatizo
katika baadhi ya viungo vyao vya mwili kama vile, miguu na mikono, hakikisha kuwa
wakati wa kuigiza wanafunzi hawa wameangaliwa ili wasijiumize au kuumizwa kwenye
viungo vilivyoathirika.
131
130
Kimeidhinishwa na KICD
Kusikiliza na Kuzungumza
Nahau: Nahau za maadili na uraia
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 101-102
Utangulizi
Waelekeze wanafunzi kutazama michoro kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 100. Waambie watambue michoro hiyo ni ya nini.Wanafunzi
watambue mimea: mharage, mwembe, mpapai, mgomba na muhogo. Pia
watambue kuwa kuna matunda: papai, maembe na ndizi.
Teua mwanafunzi mmoja mmoja ili awatajie wenzake majina ya michoro iliyo
kitabuni.
Mwambie aambatanishe michoro ya mimea na matunda au mazao yake.
Mwanafunzi ataje ni matunda yapi kati ya yaliyo kwenye mchoro amewahi
kula. Aeleze ladha ya matunda hayo. Wanafunzi wafanye hivi kwa zamu.
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nahau za maadili na uraia katika matini.
2. Kueleza maana za nahau mbalimbali za maadili na uraia katika mazungumzo.
3. Kutumia nahau za maadili na uraia katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nahau za maadili na uraia kwenye matini.
Mwanafunzi ashiriki katika kujadili maana za nahau za maadili na uraia.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia nahau za maadili na uraia.
Mwanafunzi atazame vibonzo vikijibizana kuhusu nahau za maadili na uraia
na maana zake.
Mwanafunzi ashiriki katika kuteua nahau za maadili na uraia kutoka kwenye
kundi la nahau.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 101-102
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Vibonzo
Kamusi ya misemo na nahau
133
132
Kimeidhinishwa na KICD
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yatakayofunzwa kuhusu
nahau za maadili na uraia.
Rekodi nahau za maadili na uraia kwenye kanda ya sauti au rununu.
Tafuta tarakilishi.
Tafuta kamusi ya misemo na nahau.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili.
Waambie watazame mchoro ulio kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 101. Waelekeze katika kutambua mvulana katika mchoro anafanya nini.
Wajibu kwa kusema kuwa anapiga hodi. Waambie kupiga hodi ni nahau
inayomaanisha kubisha ili kuruhusiwa kuingia mahali.
Waulize ni kwa nini mvulana huyo anafanya hivyo. Sikiliza majibu ya
wanafunzi mbalimbali ili kujua ni vipi wanavyokiria.
Wanafunzi wajadili kama wamewahi kufanya kitendo kama hicho ama
vitendo vingine vya kuonyesha heshima. Waseme wamewahi kufanya wapi.
Waelekeze wanafunzi wakiwa wawiliwawili katika kusoma kwa zamu maneno
na sentensi katika jedwali lililo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 101.
Washirikishe wanafunzi katika kujadili nahau na maana zake. Watunge
sentensi wakitumia nahau walizosoma. Hakikisha kuwa wametunga sentensi
sahihi.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma maelezo kuhusu nahau.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wafanye zoezi katika Kitabu
cha Mwanafunzi.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 102
1. aliona njaa
2. kulaza damu
3. alipigwa kalamu
4. alishika adabu
5. kupiga deki
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 103-104
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
133
132
Kimeidhinishwa na KICD
1. Kutambua nahau za maadili na uraia katika matini.
2. Kueleza maana za nahau mbalimbali za maadili na uraia katika mazungumzo.
3. Kutumia nahau za maadili na uraia katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nahau za maadili na uraia kwenye matini.
Mwanafunzi ashiriki katika kujadili maana za nahau za maadili na uraia.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia nahau za maadili na uraia.
Mwanafunzi atazame vibonzo vikijibizana kuhusu nahau za maadili na uraia
na maana zake.
Mwanafunzi ashiriki kuteua nahau za maadili na uraia kutoka kwenye kundi
la nahau.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 103-104
Rununu
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Chati
Projekta
Vibonzo
Kamusi ya misemo na nahau
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yatakayofunzwa kuhusu
nahau za maadili na uraia.
Rekodi nahau za maadili na uraia kwenye kanda ya sauti au rununu.
Tafuta tarakilishi.
Tafuta kamusi ya misemo na nahau.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Waelekeze wanafunzi katika kusoma nahau zilizo kwenye kapu maneno
wakiwa wawiliwawili.
Washirikishe wanafunzi katika kutaja na kuandika nahau za maadili na uraia
kutoka kwa zile zilizo kwenye kapu maneno.
Waongoze wanafunzi ili waweze kuandika maana ya kila nahau walizosoma
na kuandika.
Waelekeze katika kutunga sentensi sahihi wakitumia nahau za maadili na
uraia walizotambua kwenye kapu maneno.
Waambie waandike sentensi zao kwenye chati. Waelekeze wanafunzi katika
kupachika chati hizo kwenye ukuta na kuzisoma sentensi walizotunga.
Tathmini sentensi za wanafunzi ili uwakosoe pale ambapo wamekosea.
135
134
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi katika kutazama vibonzo vikizungumza kupitia kwa
projekta. Vibonzo hivyo vitumie nahau katika mazungumzo yavyo. Waongoze
katika kutambua nahau za maadili na uraia zilizotumiwa na vibonzo.
Waongoze wanafunzi katika kuandika maana ya nahau walizosikia
zikitumiwa na vibonzo.
Hitimisho: Unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wafanye zoezi
katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 104.
Majibu ya zoezi la 2, ukurasa wa 104
1. kufa kuzikana
2. eleza kinaganaga
3. Kula mlungula
4. kwenda haja
5. kula jasho lako
Kusoma kwa Mapana
Matini
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 104-106
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua matini ya aina mbalimbali na kusoma kisha kuchagua yanayomvutia.
2. Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
3. Kufurahia usomaji wa aina mbalimbali za matini.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua ni matini ya aina gani.
Kusoma matini.
Kusimulia kuhusu matini aliyosoma.
Kujadili matini aliyosoma.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 104-106
Tarakilishi
Mchoro
Tabuleti
Rekoda au simu
135
134
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili
ili wasome kifungu kilicho kwenye ukurasa wa 104-105.
Waongoze wanafunzi katika kueleza kwa muhtasari matini hayo yanahusu
nini.
Waelekeze wanafunzi kutaja matunda yaliyotajwa kwenye matini.
Waongoze wanafunzi katika kutaja vitu ambavyo nyanya huuza.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua nyanya huuza viazi vyake wapi.
Waongoze wanafunzi katika kujadili ni kwa nini msimulizi anampenda
nyanyake. Kubali majibu mwafaka ya wanafunzi.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi.
Waambie wasome matini yanayowavutia maktabani au mtandaoni. Wanafunzi
wawaeleze wenzao kile walichosoma baadaye.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 106
1. Kifungu kinahusu mimea ambayo inapatikana nyumbani kwa nyanya.
2. Matunda hayo ni: maparachichi, maembe, mapapai, mapera, matomoko
na mazaituni.
3. Nyanya huuza: viazi vitamu, mboga, matunda na asali.
4. Nyanya huuza viazi sokoni, shuleni na maduka makuu.
5. Tathmini majibu ya wanafunzi. Kubali majibu mwafaka ya wanafunzi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 106-108
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua matini ya aina mbalimbali na kusoma na kuchagua yanayomvutia.
2. Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
3. Kufurahia usomaji wa aina mbalimbali za matini.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua ni matini ya aina gani.
Kusoma matini.
137
136
Kimeidhinishwa na KICD
Kusimulia kuhusu matini aliyosoma.
Kujadili matini aliyosoma.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 106-108
Tarakilishi Mchoro Rekoda au simu
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili.
Waambie watazame michoro na kusoma matini yaliyo kando ya kila mchoro
katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 106-108.
Waongoze wanafunzi kutaja mmea na zao lake.
Waelekeze wanafunzi katika kutoa masimulizi kuhusu mmea wowote mmoja
kutokana matini waliyosoma. Tathmini majibu ya wanafunzi wako.
Waongoze wanafunzi ili wajibu maswali ya matini.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 108
1. Mmea unaokua kwenye maeneo kame ni mkonge.
2. Tui ni maji yanayopatikana kwa kukamua nazi iliyokunwa ambayo
hutumika kama kiungo cha chakula.
3. Mkonge hutumika kuunda kamba na mikeka.
4. Aina za vitunguu ni kitunguumaji na kitunguusaumu.
5. Tathmini majibu ya wanafunzi kuhusu mboga.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie watoke
nje ya darasa kisha watazame mimea iliyopo na kuitaja. Baadaye, waambie wachore
mimea miwili kati ya ile waliyoona kisha waipake rangi.
Kipindi cha 3
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 109-110
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kukariri au kuimba shairi kwa kuzingatia matamshi na mahadhi mbalimbali.
137
136
Kimeidhinishwa na KICD
2. Kueleza maana ya msamiati uliotumiwa katika shairi.
3. Kutumia msamiati uliotumiwa katika shairi kuboresha mawasiliano.
4. Kueleza ujumbe wa shairi.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi akariri au aimbe shairi.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kukariri au kuimba shairi.
Mwanafunzi atambue msamiati uliotumika katika shairi.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kujadili ujumbe katika shairi.
Mwanafunzi ajibu maswali kutokana na shairi alilosikia, aliloimba au alilokariri.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 109-110
Shairi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watano watano na uwaelekeze katika
kukariri shairi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 109. Waongoze
katika kujadili ujumbe katika shairi. Wanafunzi waweze kugundua kuwa
shairi linazungumzia faida za matunda.
Waongoze wanafunzi ili waeleze maana za baadhi ya maneno yaliyotumika
katika shairi.
Waelekeze katika kutambua kibwagizo cha shairi na kujibu maswali ya shairi.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wawakaririe wazazi au
walezi wao shairi hilo watakapoenda nyumbani.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa wa 110
1. Neno ‘tutuliyeni limetumiwa kuashiria kuwa na utulivu ili kujua zaidi.
2. Shairi linahusu faida za matunda.
3. Nazi, parachichi, limau, tikiti, zambarau na pesheni.
4. Matunda hupunguza kisukari, hukinga magonjwa, hukinga uchovu,
hufanya ngozi kuwa laini, hutupa madini na kututia nguvu.
139
138
Kimeidhinishwa na KICD
Kuandika
Insha ya maelezo
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 110-111
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vifungu vya insha ya maelezo katika matini.
2. Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
3. Kuchangamkia utunzi mzuri wa insha ya maelezo ili kukuza ubunifu.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma maelezo kuhusu insha ya maelezo.
Kutambua vifungu vya maelezo kwenye matini au tarakilishi.
Kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya maelezo.
Kuandika insha ya maelezo kwa kuzingatia mada.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 110-111
Insha kielelezo (insha ya maelezo)
Tarakilishi
Maandalizi ya mwalimu
Tayarisha insha kielelezo (insha ya maelezo).
Tafuta tarakilishi au tabuleti.
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yaliyomo kabla ya kipindi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kurejelea kipindi walichojifunza awali kuhusu insha ya
maelezo. Waulize insha ya maelezo ni nini?
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watano watano na uwaambie wajadili
sehemu za insha ya maelezo.
Waongoze kujadili muundo wa insha ya maelezo. Hakikisha kuwa wanafunzi
wanaeleza kuhusu muundo huo kwa namna inayofaa.
Waelekeze wanafunzi katika kutaja mambo muhimu yanayozingatiwa wakati
wa kuandika insha ya maelezo.
139
138
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kusoma maelezo yaliyo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 110 kuhusu insha ya maelezo. Watoe mifano ya
mada za insha za maelezo.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma insha za maelezo walizoandika hapo
awali.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa insha. Waambie waandike insha ya
maelezo kuhusu utunzaji wa mimea.Waandike insha ya maelezo wakiwa nyumbani
na wakuletee darasani ili utathmini kazi zao.
Kipindi cha 2
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vifungu vya maelezo vilivyoandikwa kwenye matini mbalimbali.
2. Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma maelezo kuhusu insha ya maelezo.
Kutambua vifungu vya maelezo kwenye matini au tarakilishi.
Kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya maelezo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 111
Insha kielelezo (insha ya maelezo)
Tarakilishi au tabuleti
Maandalizi ya mwalimu
Tayarisha insha kielelezo (insha ya maelezo).
Tafuta tarakilishi au tabuleti.
Soma Kitabu cha Mwanafunzi ili kujifahamisha yaliyomo kabla ya kipindi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wasome insha ya maelezo
waliyoandika katika mada ya 5 kuhusu, Jinsi ya Kuhifadhi Mazingira.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu kisha uwaambie
waandike insha kuhusu utunzaji wa mimea.
Waelekeze wanafunzi katika kujadili vipengele muhimu vya kuzingatia wakati
wa kuandika insha hiyo. Wape vidokezo hivi:
1. Utunzaji wa mimea ni nini? 2. Ni mimea ipi hutunzwa?
141
140
Kimeidhinishwa na KICD
3. Mimea hiyo hutunzwa vipi?
4. Kwa nini tunatunza mimea?
5. Ni nini hasara ya kutotunza
mimea?
Waongoze wanafunzi katika kujadili hoja muhimu katika kila kidokezo.
Hakikisha kuwa wananakili hoja hizo kwenye madaari yao.
Waelekeze katika kuandika insha ya maelezo wakitumia vidokezo na hoja
walizonakili.
Teua mwanafunzi mmoja ake mbele ya wanafunzi wenzake darasani.
Mwambie awasomee wenzake insha yake. Wanafunzi wengine wasikilize.
Wateue wanafunzi hawa kwa zamu. Hakikisha kuwa wanafunzi
wanapongezwa ili kuwapa hamu ya kutaka kushiriki zaidi katika uandishi wa
insha na kuwasomea wenzao darasani.
Hitimisho: wakumbushe wanafunzi kuwa insha ya maelezo hueleza suala jinsi lilivyo.
Mwanafunzi anahitajika kutoa hoja nzito na tele kuhusiana na mada husika. Kila hoja
ielezwe kwa kutoa mifano halisi.
Saru
Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya KI-VI
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 111-112
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya KI-VI katika
umoja na wingi.
2. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
3. Kufurahia matumizi ya nomino za ngeli ya KI-VI katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutaja nomino za ngeli ya KI-VI.
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 111-112
Majedwali Chati Tarakilishi
141
140
Kimeidhinishwa na KICD
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 111-112
Andaa majedwali yenye sentensi za nomino katika ngeli ya KI-VI.
Tayarisha chati yenye sentensi zilizo na nomino za ngeli ya KI-VI katika
umoja na wingi.
Tafuta tarakilishi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya nomino za
ngeli ya KI-VI. Kubali mifano ambayo wanafunzi watatoa, mradi ni sahihi.
Wanaweza kutaja:
ü kiatu-viatu
ü chakula-vyakula
ü choo-vyoo
ü kioo-vioo
ü kisu-visu
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasome sentensi
zenye nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi kwenye jedwali.
Hakikisha kuwa wanafuzni wanashiriki kikamilifu katika shughuli hii.
Waulize wanafunzi walichogundua kuhusu sentensi hizo. Wanaweza kusema
sentensi hizo zinahusu nomino za ngeli ya KI-VI.
Waongoze katika kutaja nomino nyingine zilizo katika ngeli ya KI-VI.
Wanafunzi wanaweza kutoa mifano kama vile:
ü kisogo-visogo
ü kipenga-vipenga
ü kiazi-viazi
ü kijumba-vijumba
ü kitoto-vitoto
Waambie wanafunzi watunge sentensi katika umoja na wingi wakitumia
nomino watakazotaja. Waonyeshe wanafunzi viambishi vya upatanisho wa
kisaru katika kila sentensi.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya kazi mradi katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 112. Wapange katika vikundi vya watatuwatatu na
uwaambie wapige chapa sentensi zilizopo kwenye tarakilishi.
Waambie wanafunzi wazihifadhi sentensi hizo kisha wawatumie wenzao
sentensi walizopiga chapa kwenye mtandao ili wazisome.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa
sentensi zenye nomino katika ngeli ya KI-VI huwa na kiambishi ki katika umoja na
kiambishi vi katika wingi ili kubainisha upatanisho wa kisaru.
143
142
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya KI-VI katika
umoja na wingi.
2. Kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma sentensi zenye nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
Kutunga sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI, katika umoja na
wingi.
Kufurahia matumizi ya nomino za ngeli ya KI-VI katika mawasiliano.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 112
Chati
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili
kisha uaelekeze katika kuandika sentensi zilizo katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 112 kwa umoja au wingi. Waambie watumie hati mkono kuandika
sentensi hizo kwenye chati.
Waelekeze wanafunzi katika kuweka sentensi kwenye chati ukutani. Waambie
wanafunzi katika kila kikundi wasome sentensi zao walizoandika kwenye
chati.
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi kwa kutumia nomino
walizopewa kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Wanafunzi watathmini sentensi
za wanafunzi wenzao. Na kuwarekebisha wenzao wanapokosea. Hakikisha
kuwa wanafunzi wanashiriki katika shughuli hii kwa njia ifaayo.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kwa kuwakumbusha kuwa sentensi za nomino ya
ngeli ya KI-VI huwa na kiambishi ki katika umoja na kiambishi vi katika wingi ili
kubainisha upatanisho wa kisaru.
143
142
Kimeidhinishwa na KICD
Umoja na wingi wa nomino ngeli ya LI-LI
Kipindi cha 1
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino katika ngeli ya LI-LI.
2. Kuandika nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na wingi.
3. Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-LI.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya LI-LI.
Mwanafunzi aandike nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na wingi.
Mwanafunzi asikilize usomaji wa nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na
wingi kwenye kinasasauti.
Mwanafunzi aandike mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-LI katika umoja
na wingi.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwa kutumia viambishi vya umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya LI-LI kwa hati ya mkono ama tarakilishi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
wa 113
Kinasasauti/rekoda
Tarakilishi
Wanafunzi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaonyesha wanafunzi mchoro wa jua. Waambie
wataje jua kwa umoja na wingi. Hakikisha kuwa wameweza kutambua kuwa
jua hubaki hivyo tu katika umoja na wingi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi wawiliwawili kisha
uwaambie wasome maneno yaliyo kwenye kadi.
Waongoze wanafunzi katika kujirekodi wakisoma maneno hayo kwa kutumia
rekoda.
Waelekeze katika kusikiliza sauti zao wakisoma maneno hayo.
Waambie waandike umoja na wingi wa maneno hayo waliyosoma.
Waelekeze katika kugundua kuwa maneno katika ngeli ya LI-LI hayabadiliki
katika umoja na wingi.
Waongoze wanafunzi katika kukamilisha jedwali katika Kitabu cha
Mwanafunzi.
145
144
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 113
Umoja Wingi
Chaguo limekataliwa. Chaguo limekataliwa.
Giza linatisha sana. Giza linatisha sana.
Huba limea. Huba limea.
Jasho linatiririka. Jasho linatiririka.
Pendo limeshabikiwa. Pendo limeshabikiwa.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa maneno katika
nomino za ngeli ya LI-LI huchukua kiambishi li katika umoja na li katika wingi.
Kiambishi hakibadiliki katika umoja na wingi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 114
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-LI.
2. Kutunga sentensi sahihi akitumia nomino katika ngeli ya LI-LI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
3. Kufurahia matumizi ya nomino za ngeli ya LI-LI katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue nomino katika ngeli ya LI-LI.
Mwanafunzi asome sentensi zenye nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na
wingi.
Mwanafunzi aandike sentensi zenye nomino katika ngeli ya LI-LI katika
umoja na wingi.
Mwanafunzi atunge sentensi kwenye tarakilishi akirejelea ngeli ya LI-LI kisha
azisambaze kwa wenzake mtandaoni ili wachangie kuziboresha.
145
144
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 114
Tarakilishi Boksi Kadi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili
kisha uwaongoze katika kutunga sentensi wakitumia nomino walizopewa.
Waambie waandike sentensi walizotunga katika wingi.
Waelekeze ili wapige chapa sentensi hizo kwenye tarakilishi.
Waongoze wanafunzi katika kusambaza sentensi walizotunga kupitia kwa
mtandao wa intaneti.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu. Waambie waandike
sentensi katika Kitabu cha Mwanafunzi kwenye kadi.
Waelekeze ili waweke kadi hizo zenye sentensi kwenye boksi moja.
Washirikishe kwenye mchezo wa kuchopoa kadi za sentensi zenye nomino za
ngeli ya LI-LI kutoka kwa boksi na kuzisoma mbele ya wanafunzi wenzake.
Hitimisho: hitimisha kwa kuwakumbusha kuwa sentensi katika ngeli ya LI-LI
huchukua kiambishi li katika umoja na li katika wingi.
147
146
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Nyenzo zifuatazo zinaweza kutumika katika kufundisha mada kuhusu wanyama wa
porini.
Vifaa halisi: barua, pesa, bendera ili kufunza visawe.
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, vipakatalishi, rununu na projekta
Kinasasauti
Mtandao
Tovuti
Picha
Michoro
Chati
Kadi
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
WANYAMA WA PORINI
8
Utangulizi
Wanyama wa porini ni wanyama wanaoishi msituni. Wanyama hawa ni wa aina
mbalimbali. Kuna walao nyama, wanaokula nyasi na pia kuna wengine wanaokula
nyasi na nyama. Wanyama wa porini ni raslimali muhimu ya taifa la Kenya kwa
kuwa wao huwavutia watalii kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Watalii huiletea
nchi ya Kenya pesa za kigeni. Wanyama wa porini ni njia mojawapo ya nchi kujipatia
mapato. Kuna wanyama wa porini kama vile: simba, ndovu, chui, si, ngiri, swara
na twiga.
Sehemu hii imeshughulikiwa katika mada nne. Mada hizo ni: kusikiliza na
kuzungumza (visawe vya maneno mawili), kusoma kwa ufahamu (mchezo mfupi
wa kuigiza), kuandika insha ya masimulizi na saru (mnyambuliko wa vitenzi).
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutumia visawe vya maneno ipasavyo katika mawasiliano.
2. Kuigiza mchezo wa kuigiza kwa kuzingatia maelekezo.
3. Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
4. Kutumia vitenzi katika kauli za kutenda, kutendea na kutendwa ipasavyo
katika mawasiliano.
147
146
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji katika sehemu hii
Mwanafunzi atambue visawe vya maneno mawili katika kundi la maneno.
Mwanafunzi atumie visawe vya maneno ifaavyo katika mawasiliano.
Mwanafunzi atambue wahusika na maelekezo katika mchezo wa kuigiza.
Mwanafunzi aigize mchezo kwa kuzingatia maelekezo.
Mwanafunzi atoe muhtasari wa mchezo wa kuigiza aliosoma.
Mwanafunzi aandike insha ya masimulizi.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki mtandaoni na kuisambaza kwa wenzake.
Mwanafunzi atambue vitenzi katika kauli za kutenda, kutendea na kutendwa.
Mwanafunzi atumie vitenzi katika kauli za kutenda, kutendea na kutendwa
katika mawasiliano.
Maswali dadisi
Maswali yafuatayo yatamwongoza mwanafunzi katika kuakia malengo ya mada
kuhusu wanyama wa porini:
1. Je, unajua maneno yapi ya Kiswahili yaliyo na maana sawa au maana
inayokaribiana?
2. Mhusika katika mchezo wa kuigiza ni nani?
3. Je, unaweza kupata ujumbe vipi katika mchezo wa kuigiza?
4. Insha ya masimulizi inahusu nini?
5. Unazingatia nini unapoandika insha ya masimulizi?
6. Vitenzi vinaweza kubadilika vipi mwishoni ili kuleta mabadiliko?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Sehemu ya Wanyama wa Porini’ inakuza umilisi wa kimsingi ufuatao:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wafanye mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika vikundi
kama vile kuambatanisha neno na kisawe chake au kueleza sifa za wanyama wa porini.
Mijadala baina ya wanafunzi kuhusu mambo watakayoandika kwenye insha ya masimulizi
itaimarisha mawasiliano na kukuza ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi
wakisambaza insha za masimulizi walizoandika kwenye mitandao wakitumia vyombo vya
kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi,
149
148
Kimeidhinishwa na KICD
kipakatalishi, video, projekta, intaneti na tovuti ili mwanafunzi ajifunze aina mbalimbali
za wanyama wa porini na kusakura habari muhimu kwenye tovuti kuwahusu wanyama
wa porini. Wanaweza kutumia tarakilishi kuandika na kuhifadhi kazi kuhusu wanyama
wa porini na visawe vya maneno kwenye faili.
(ch) Hamu ya Ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
wanyama wa porini. Mwanafunzi anaweza akachochewa kutaka kujua wanyama wa
porini hula nini, huishi wapi na vipi. Umilisi huu humpa mwanafunzi hamu ya kujua
maisha ya wanyamapori na umuhimu wao katika maisha ya binadamu katika jamii yake.
Pia, mwanafunzi atatafakari akijibu maswali tekelezi kuhusu wanyamapori. Mwanafunzi
anaweza kuwa na hamu ya kutaka kutumia vyombo vya kidijitali ili atafute habari zaidi
kuhusu wanyama wa porini.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika insha ya masimulizi kwa kutumia
tarakilishi. Pia, ubunifu ukuzwe na kuimarishwa kupitia kutunga sentensi akitumia
vitenzi katika kauli mbalimbali. Ubunifu utadhihirika mwanafunzi akitafuta visawe
vya maneno akitumia mtandao wa intaneti.
(e) Kujiamini
Umilisi huu unakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kuigiza nafasi ya mhusika fulani katika mchezo wa kuigiza. Pia, kujiamini
kunakuzwa kupitia mwanafunzi kuigiza sauti na miondoko ya wanyama mbalimbali
wa porini.
Uhusiano wa masuala mtambuko
Sehemu hii ina uhusiano na masuala mtambuko yafuatayo:
(a) Kujitambua na kujithamini kupitia kuigiza vitendo vya wanyama wa porini,
kuigiza katika michezo ya kuigiza, kutunga sentensi akitumia vitenzi katika
kauli mbalimbali.
(b) Stadi za maisha kupitia wanafunzi kujieleza, kushiriki katika vikundi,
kuchangia katika mijadala na kubainisha umuhimu wa wanyama wa porini
kwa nchi ya Kenya.
(ch) Uraia unakuzwa kupitia kufanya kazi pamoja, kulinda wanyama wa porini
na kuwaripoti wawindaji haramu wa wanyama wa porini.
(d) Elimu ya maendeleo endelevu inakuzwa kupitia ujuzi wa kutumia teknolojia
ya kisasa hasa tarakilishi katika kutafuta sifa bainifu za wanyama wa porini
na kupata maarifa kuhusu jinsi ya kuwatunza wanyama wa porini.
149
148
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano wa maadili
Sehemu hii ina uhusiano na maadili kwa njia zifuatazo:
Heshima inadhihirika kupitia wanafunzi kuheshimu wanyama wa porini
kama raslimali ya nchi na pia kupitia kuendeleza shughuli za vikundi.
Umoja, uzalendo na upendo unakuzwa wanafunzi wanapofanya kazi ya
vikundi.
Uwajibikaji kwa wanafunzi kuwalinda na kuwaheshimu wanyama wa porini
na kuripoti hatari yoyote kwa idara ya wanyama wa porini.
Shughuli za huduma za kijamii
Katika sehemu hii mwanafunzi anaweza kushiriki katika shughuli za huduma za
kijamii zifuatazo:
Kuwalinda wanyama wa porini.
Kuwa mwanachama wa vyama vinavyotetea wanyama wa porini.
Kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa wanyama wa porini.
Kuwahamasisha wanafunzi wenzake kutembelea mbuga za wanyama
Kuhimiza watu kutumia vitenzi katika kauli mbalimbali ipasavyo ili
kuboresha mawasiliano.
Uhusiano na masomo mengine
Sehemu hii inaingiliana na masomo mengine kama vile:
Social Studies: kupitia mada kuhusu wanyama wa porini na mbuga za
wanyama.
English Activities: visawe vya maneno hufunzwa ili kukuza stadi ya kusikiliza
na kuzungumza. Saru hasa vitenzi na sentensi hufundishwa katika somo hili.
Indigenous Language Activities: visawe vya maneno hufunzwa ili kukuza stadi
ya kusikiliza na kuzungumza. Stadi za kusoma na kuandika hufunzwa katika
Indigenous Language Activities.
Mapendekezo ya mbinu za kutathmini
Tathmini inaweza kufanywa kwa:
Kuhakiki jinsi mwanafunzi anavyosoma visawe vya maneno.
Kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyotumia msamiati wa wanyama wa porini.
Kuhakiki jinsi mwanafunzi anavyoandika insha ya masimulizi. Azingatie
muundo na mtindo wa kuandika insha ya masimulizi.
Kusikiliza majadiliano ya wanafunzi kuhusu sifa za wanyama wa porini.
151
150
Kimeidhinishwa na KICD
Kuchanganua namna mwanafunzi anavyojibu maswali kutokana na kifungu
alichosoma kuhusu wanyama wa porini.
Kuhakiki namna mwanafunzi anavyotamka visawe vya maneno.
Kutunga sentensi akitumia vitenzi katika kauli mbalimbali.
Kujaza mapengo katika sentensi.
Kuchunguza namna mwanafunzi anavyotumia msamiati wa wanyama wa
porini katika mawasiliano.
Kuhakiki jinsi anavyokamilisha jedwali.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Unaweza kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kupitia mikakati
ifuatayo:
Wape shughuli mbadala wanafunzi wenye hitilafu katika baadhi ya viungo
vyao vya mwili kama vile mikono na miguu. Kwa wanafunzi hawa, badala ya
kuigiza mchezo wa kuigiza darasani, wanaweza kusoma mchezo huo wakiwa
wameketi.
Watengee wanafunzi wanaopata matatizo katika kuelewa baadhi ya masomo
muda maalumu wa kurudia shughuli husika.
Tumia mbinu na nyenzo kama vile: video, picha au kinasasauti kufunza
vipengele mbalimbali na kuwafanya wanafunzi kufurahia ujifunzaji.
Kwa wanafunzi wasioona, unaweza kushirikisha sauti wakati wa ufundishaji
ili wajifunze kupitia kusikia.
Uwe na subira na wanafunzi walio na matatizo ya kuzungumza kama
vigugumizi kwa kuwapa muda zaidi wanaposoma.
Kwa wanafunzi wenye uwezo wa juu darasani, wape kazi ya ziada na
changamano kama vile kuchora wanyama wa porini au kutunga sentensi
zaidi.
Kusikiliza na Kuzungumza
Visawe vya maneno mawili
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 116-117
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
151
150
Kimeidhinishwa na KICD
1. Kueleza maana ya kisawe ili kukibainisha.
2. Kutambua visawe vya maneno mawili katika kundi la maneno.
3. Kutumia visawe vya maneno ifaavyo katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Kisawe ni nini?
2. Ni maneno gani ya Kiswahili yaliyo na maana sawa?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi aeleze maana ya kisawe.
Mwanafunzi atambue visawe vya maneno.
Mwalimu aambatanishe visawe.
Mwanafunzi ahusishe visawe na vifaa halisi.
Mwanafunzi ashiriki katika kujadili visawe mbalimbali.
Mwanafunzi atumie kisawe kimoja kuchukua nafasi ya kingine katika sentensi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 116-117
Michoro Kamusi Mti maneno
Utangulizi
Waelekeze wanafunzi katika kutazama michoro katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 115. Mwambie mwanafunzi mmoja asimame mbele
ya wengine darasani na awaambie ameona nini katika michoro hiyo.
Waongoze wanafunzi ili waeleze aina mbalimbali za wanyama ambao
wamewahi kuwaona.
Wakirishe wanafunzi kwa kuwauliza mahali wanyama hao hupatikana.
Waelekeze katika kutaja umuhimu wowote wa wanyama wowote kwenye
picha hizo.
Waongoze wanafunzi ili wasome maelezo yaliyo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 116. Wakumbushe kuwa wanyama wa porini huishi
msituni na hawafugwi nyumbani.
Waeleze kuwa kuna wanyama wa pori wanaokula nyama pekee, wengine nyasi
pekee na wengine hula nyama na nyasi. Waelekeze katika kutaja wanyama wa
porini kama vile: simba, ndovu, swara, tohe na chui.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame picha kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi, ukurasa wa 116 kisha uwaongoze katika kusoma maelezo
kuhusu ndovu. Waelekeze kutambua kuwa tembo ni kisawe cha ndovu.
153
152
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi katika kufanya shughuli ya kusoma maneno kwenye mti
maneno wakiwa katika vikundi vya wawiliwawili.
Waelekeze wanafunzi katika kuambatanisha neno lililo na maana sawa na
jingine.
Waongoze wanafunzi kutaja methali zinazowataja wanyama wa porini.
Methali zinazowataja wanyama wa porini ni kama vile:
ü Mtoto wa nyoka ni nyoka.
ü Nyani haoni kundule.
ü Paka akiondoka panya hutawala.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi kuwa visawe ni maneno
yaliyo na maana sawa. Waambie watoe mifano kama vile: kinyonga-lumbwi.
Kipindi cha 2
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kisawe ili kukibainisha.
2. Kutambua visawe vya maneno mawili katika kundi la maneno.
3. Kutumia visawe vya maneno ifaavyo katika mawasiliano.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue visawe vya maneno.
Mwalimu atunge sentensi sahihi akitumia visawe.
Mwanafunzi aandike upya sentensi akitumia visawe.
Mwanafunzi atafute visawe katika kamusi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 118-119
Chati Kamusi Mraba maneno
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje visawe vya maneno
yafuatayo:
1. lumbwi - kinyonga
2. nyati - mbogo
3. kilimo - zaraa
4. televisheni - runinga
Waongoze wanafunzi kusoma maneno kwenye chati wakiwa watatuwatatu.
Wanafunzi wasome kila neno na kisawe chake kwa kutamka kwa usahihi.
153
152
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia maneno yaliyo
kwenye kitabu.
Waelekeze wanafunzi ili watumie kamusi kutafuta visawe vya maneno yaliyo
kwenye kitabu.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 118-119
1. Tathmini sentensi ambazo wanafunzi watatunga.
2. (a) uzembe-uvivu
(b) jaji-hakimu
(c) tajiri-bwanyenye
(d) maskini-mlalahoi/mkata
(e) maringo-majivuno/madaha
3. (a) Mwanafunzi alihitaji hela/njenje nyingi.
(b) Fisi ni mnyama wa porini.
(c) Mama alininunulia zawadi.
(d) Usipokee hongo/mlungula.
(e) Nilipata ruhusa ya kutembelea mbuga ya wanyama.
(f) Mama atanunua simu.
(g) Akinyi amefua sare.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaongoze katika
kutafuta majina ya wanyama wa porini kwenye mraba. Wanafaunzi wafanye
hivi kwa kuviringa maneno hayo kwenye mraba watakaojichorea.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi kuwa visawe ni maneno
yaliyo na maana sawa. Waambie watoe mifano zaidi ya visawe wanavyofahamu.
Kusoma
Mchezo wa Kuigiza
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 120
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi hiki, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya mchezo wa kuigiza, mhusika na maelekezo.
155
154
Kimeidhinishwa na KICD
2. Kutambua mchezo wa kuigiza katika matini.
3. Kutambua wahusika na maelekezo katika mchezo wa kuigiza.
4. Kuigiza mchezo wa kuigiza kwa kuzingatia maelekezo.
Maswali dadisi
1. Mhusika katika mchezo wa kuigiza ni nani?
2. Maelekezo ni nini katika mchezo wa kuigiza?
3. Ujumbe unapatikana vipi katika mchezo wa kuigiza?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue mchezo wa kuigiza, mhusika na maelekezo katika
mchezo wa kuigiza.
Mwanafunzi ashiriki katika majadiliano kuhusu mchezo wa kuigiza.
Mwanafunzi atazame mchezo wa kuigiza ukiigizwa darasani.
Aigize mchezo mfupi kwa kuzingatia maelekezo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 120
Rekoda
Kinasasauti
Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya wannewanne.
Waambie wataje wanyama wanne wa porini wanaofahamu. Sikiliza majibu
ya wanafunzi kwa makini ili kuhakikisha kuwa wanataja wanyama wa porini.
Wanafunzi wataje wanyama wa porini kama vile: sungura, simba, ndovu,
swara na pundamilia. Wanafunzi wengine wanaweza wakawakosoa wenzao
ambao hawatataja wanayama wa porini.
Ambia kila mwanafunzi achague kuwa mnyama mmoja wa porini kisha
waigize mazungumzo kati ya wanyama wa porini.
Waongoze katika kuigiza mazungumzo hayo ili kuhakikisha kuwa wanafunzi
wanashiriki ipasavyo katika shughuli hiyo. Mazungumzo ya wanafunzi
yalenge ukame porini. Baadhi ya hoja wanazoweza kuzungumzia ni:
ü Ukame umesababishwa na nini?
ü Ukame utawaathiri wanyama vipi?
ü Wanyama wanaweza kufanya nini kuzuia ukame?
Waelekeze wanafunzi katika kurekodi mchezo wao wa kuigiza. Unaweza
ukateua wanafunzi watakaoshika rekoda au pia urekodi mazungumzo hayo.
155
154
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wengine wasikilize na watazame maigizo hayo ambayo yatakuwa
yakifanyika kwa zamu darasani.
Waambie wanafunzi kuwa mazungumzo waliyoshiriki ni mchezo wa kuigiza.
Waelekeze wanafunzi ili wasome maelezo kuhusu mchezo wa kuigiza kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi mchezo wa kugiza ni nini?
Wahusika hufanya kazi gani katika mchezo wa kuigiza. Mwisho, wape wanafunzi
shughuli ya nje ya darasa. Waambie wachore wanyama wa porini walioigiza nafasi
zao.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 121-123
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi hiki, mwanafunzi aweze:
1. Kusoma mchezo wa kuigiza kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
2. Kutambua mchezo wa kuigiza katika matini.
3. Kutambua wahusika na maelekezo katika mchezo wa kuigiza.
4. Kuigiza mchezo wa kuigiza kwa kuzingatia maelekezo.
Maswali dadisi
1. Wahusika ni nani katika mchezo wa kuigiza?
2. Maelekezo ni nini katika mchezo wa kuigiza?
3. Mchezo wa kuigiza una ujumbe gani kwa watazamaji na wasomaji?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi asome mchezo wa kuigiza akizingatia maelekezo na ujumbe.
Mwanafunzi ajibu maswali yanayotokana na mchezo wa kuigiza aliosoma.
Mwanafunzi atambue wahusika na maelekezo katika mchezo wa kuigiza.
Mwanafunzi ashiriki katika majadiliano kuhusu mchezo wa kuigiza.
Mwanafunzi atazame mchezo wa kuigiza ukiigizwa kwenye vifaa vya kidijitali.
Mwanafunzi asome mchezo wa kuigiza kwenye mtandao.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 121-123
Rekoda
Kinasasauti
Tarakilishi
Mchoro
157
156
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame mchoro kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 121 na wataje wanyama walio kwenye
mchoro huo. Wanafunzi wataje ndovu, sungura na kobe.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne na uwaambie wasome
mchezo wa kuigiza ulio baada ya mchoro kwa sauti na kwa usahihi.
Mwanafunzi mmoja asome maelekezo na wengine wachukue nafasi ya
Sungura, Ndovu na Kobe.
Waongoze katika kuigiza mchezo waliosoma. Waigize huku wakifuata
maelekezo na mandhari. Wanaweza kurekodi maigizo hayo kwa kutumia
rekoda au kinasasauti.
Waelekeze katika kujadili ujumbe katika mchezo wa kuigiza. Wape wanafunzi
nafasi ya kukiria kwa kina.
Waongoze katika kutambua wahusika katika mchezo huu. Wahusika hao ni:
Kobe, Sungura na Ndovu.
Waelekeze wanafunzi ili waweze kutambua wahusika katika mchezo wa
kuigiza waliamua vipi. Wanafunzi watambue kuwa wanyama waliamua kuwa
wa ushirikiano ili kukabiliana na adui wa wanyama wa porini ambaye ni
binadamu.
Waongoze kutambua sifa za wahusika katika mchezo wa kuigiza waliosoma
kisha uwaulize mhusika waliyempenda kwenye mchezo wa kuigiza. Kumbuka
kuwauliza pia sababu za kupenda wahusika hao. Kubali majibu ya wanafunzi
kulingana na namna watakavyotetea hoja vyake.
Hitimisho: hitimisha kwa kuwaambia wanafunzi waigize mchezo huo wakiwa nje ya
darasa. Wape kazi mradi ya kuwataka watembelee mbuga ya wanyama kisha wataje
wanyama watakaowaona katika mbuga hiyo ya wanyama. Waigize namna wanyama
hao walivyokuwa wakiishi kwenye mbuga hiyo.
Kipindi cha 3
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 123
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi hiki, mwanafunzi aweze:
1. Kutazama mchezo wa kuigiza kwenye vifaa vya kidijitali.
2. Kutambua mchezo wa kuigiza katika matini.
3. Kutambua wahusika na maelekezo katika mchezo wa kuigiza.
4. Kuigiza mchezo wa kuigiza kwa kuzingatia maelekezo.
157
156
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atazame mchezo wa kuigiza ukiigizwa kwenye video.
Mwanafunzi ajibu maswali yanayotokana na mchezo wa kuigiza aliotazama
kwenye video.
Mwanafunzi atambue wahusika na maelekezo katika mchezo wa kuigiza
aliotazama.
Mwanafunzi ashiriki katika majadiliano kuhusu mchezo wa kuigiza.
Mwanafunzi asome mchezo wa kuigiza kwenye mtandao.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 123
Tarakilishi Video
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje vipengele muhimu
katika mchezo wa kuigiza. Sikiliza majibu ya wanafunzi kwa makini huku
ukiwakosoa popote wanapokosea. Wanafunzi wataje: wahusika, maelekezo,
mandhari na ujumbe.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne. Waongoze katika
kutazama mchezo wa kuigiza kwenye video. Mchezo huo unaweza kuwa
kuhusu wanyama wa porini.
Waelekeze katika kujadili ujumbe katika mchezo wa kuigiza waliotazama kwenye
video. Wape wanafunzi nafasi ya kukiria kwa kina na kutoa majibu yao.
Waongoze katika kutambua na kutaja wahusika katika mchezo huo.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua ni mhusika yupi aliyewafurahisha.
Mwanafunzi apewe nafasi ya kujieleza ni kwa nini amechagua mnyama huyo.
Waongoze wanafunzi katika kusoma na kutazama mchezo wa kuigiza kwenye
mtandao. Mchezo unaweza kuhusu utunzaji wa wanyama wa porini au
kukabiliana na wawindaji haramu.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wasakure mitandao
iliyo na video kuhusu wanyama wa porini. Waambie wawaombe wazazi au walezi
wao kuwakubalia kutazama video kuhusu wanyama wa porini wakiwa nyumbani.
Wakika darasani, wanafunzi wawaeleze wenzao kuhusu wanyama waliotazama na
walichokuwa wakifanya.
159
158
Kimeidhinishwa na KICD
Kuandika
Insha ya masimulizi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 124
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
2. Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
3. Kuchangamkia utunzi mzuri wa wa insha ya masimulizi ili kujenga ubunifu wake.
Maswali dadisi
1. Insha ya masimulizi inahusu nini?
2. Unazingatia nini ili kuandika insha nzuri ya masimulizi?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
Kuandika insha ya masimulizi.
Kushiriki na wenzake kujadili mada ya insha na muundo wa insha ya masimulizi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 124
Insha za masimulizi halisi
Tarakilishi
Kanda za sauti kuhusu insha ya masimulizi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi waeleze wanachojua kuhusu
insha ya masimulizi. Sikiliza majibu ya wanafunzi kwa makini huku
ukiwakosoa popote wanapokosea.
Waambie wasome mifano ya insha ya masimulizi waliyosoma katika mada ya
pili kisha warejelee maelezo kuhusu insha ya masimulizi kwenye mada hiyo
hiyo.
159
158
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kujadili insha ya masimulizi ni nini. Wanafunzi
wajadili na watoe maelezo kuihusu. Wakumbuke kuwa: kusimulia ni kutoa
habari au maelezo kuhusu jambo au tukio fulani.
Waelekeze katika kujadili muundo wa insha ya masimulizi. Wakumbushe
kuwa insha ya masimulizi huwa na muundo ufuatao:
ü Kichwa- hutokana na mada. Kichwa sharti kiwe chenye mvuto na kiwe
na maneno machache aghalabu yasiyopita sita. Kichwa huandikwa kwa
heru kubwa na kupigiwa mstari.
ü Utangulizi- hutoa maeleo kuhusu kisa kizima. Utangulizi huandikwa
kwa njia ya kumvutia msomaji ili aweze kuendelea kusoma kisa.
ü Mwili- katika sehemu hii, kisa huelezwa vizuri na kwa mpangilio
mwafaka. Lugha inayoeleweka, rahisi na yenye mvuto hutumiwa.
Wahusika hutengana katika mandhari yaliyoelezwa vizuri. Tamathali za
usemi hutumiwa.
ü Hitimisho- msimulizi hutoa muhtasari wa kisa katika aya ya mwisho.
Hitimisho linaweza kutoa funzo fulani kwa msomaji.
Waongoze wanafunzi kujadili mambo muhimu yanayozingatiwa wakati wa
kuandika insha ya masimulizi.
Wanafunzi warejelee kazi zao za awali kuhusu insha ya masimulizi. Kila
mwanafunzi asome insha yake ya awali kuhusu masimulizi.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia waandike insha ya masimulizi kuhusu
tukio muhimu lililotendeka walipokuwa wametembelea mbuga ya wanyama. Insha hii
iandikwe wanafunzi wakiwa nyumbani.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 124-125
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo na mtindo.
2. Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
Maswali dadisi
1. Insha ya masimulizi inahusu nini?
2. Je, unazingatia nini unapoandika insha ya masimulizi?
161
160
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
Kuandaa vidokezo vya insha ya masimulizi.
Kuandika insha ya masimulizi.
Kushiriki na wenzake katika kujadili mada ya insha na muundo wa insha ya
masimulizi.
Kusikiliza insha ya masimulizi ikisomwa.
Kuandika insha ya masimulizi mtandaoni na kuisambaza kwa wenzake.
Kuwasomea wenzake insha ya masimulizi aliyoaiandika.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 124-125
Insha za masimulizi halisi
Tarakilishi
Kanda za sauti kuhusu insha ya masimulizi.
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie wasome
maelezo kuhusu insha ya masimulizi kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Waongoze wanafunzi katika kujadili mambo wanayopaswa kuzingatia katika
uandishi wa insha ya masimulizi. Wanafunzi wasome na kizijadili hoja zilizo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi katika Kitabu cha Mwanafunzi
kuhusu matembezi katika mbuga ya wanyama.
Waongoze ili waweze kuandaa vidokezo watakavyozingatia katika kuandika
insha ya masimulizi kuhusu mnyama wa porini waliyemwona mbugani.
Waelekeze katika kujadili kuhusu mnyama huyo. Wanaweza kuzingatia
maumbile yake, makao yake, sifa zake, chakula chake, uhusiano wake na
wanyama wengine na mengineyo.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika insha ya masimulizi kuhusu mnyama
huyo kwenye tarakilishi. Tathmini insha za wanafunzi.
Waongoze wanafunzi ili waweze kuisambaza insha hiyo kwenye mtandao
ili wanafunzi wengine waisome. Waambie wanafunzi waisome insha ya
masimulizi waliyosambaziwa.
Hitimisho: waambie wanafunzi, wakiwa nyumbani, waandike insha ya masimulizi
kuhusu mnyama mwingine wa porini na vitendo vyake walipotembelea mbuga ya
wanyama.
161
160
Kimeidhinishwa na KICD
Saru
Mnyambuliko wa vitenzi
Kipindi cha 1
Kauli ya kutenda
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 125-126
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya mnyambuliko wa vitenzi ili kuubainisha.
2. Kutambua vitenzi katika kauli ya kutenda katika matini.
3. Kutumia vitenzi katika kauli ya kutenda ipasavyo katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Mnyambuliko wa vitenzi unahusu nini?
2. Vitenzi katika kauli ya kutenda huisha kwa viambishi gani?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kueleza maana ya mnyambuliko wa vitenzi.
Kutambua vitenzi katika kauli ya kutenda.
Kutunga sentensi kwa kutumia vitenzi katika kauli ya kutenda.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 125-126
Chati Kadi Boksi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kwa kuwaambia wanafunzi wakiwa wannewanne, waandike
vitenzi wanavyofahamu kwenye kadi kisha waweke kadi hizo kwenye boksi.
Wanaweza kuandika vitenzi kama vile: cheka, ruka, imba, keti na soma.
Wateue wanafunzi, mmoja baada ya mwingine ili watende baadhi ya vitendo
watakavyoonyeshwa kwenye kadi.
Waambie wanafunzi kuwa baadhi ya mambo walivyofanya mbele ya darasa
ni vitendo na vikifanywa katika hali yake ya kawaida, huwa katika hali ya
kutenda.
163
162
Kimeidhinishwa na KICD
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie wasome
maneno yaliyo kwenye chati katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waongoze katika kutambua vitenzi katika kauli ya kutenda kutoka kwa
orodha iliyo kwenye chati. Watambue vitenzi kama vile:
ü panda
ü imba
ü tambua
ü chagua
ü iva
ü tazama
ü beba
ü ruka
ü tafuta
ü lia
ü funga
ü tunga
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia vitenzi vilivyoorodheshwa
katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 126. Tathmini sentensi ambazo wanafunzi
watatunga. Wanaweza wakatunga sentensi kama:
1. Mwalimu ameingia darasani.
2. Mwanafunzi ametoka shuleni.
3. Askari analinda wanyama wa porini.
4. Juma anatembea darasani.
5. Mwalimu alitusimulia kisa.
Waelekeze wanafunzi kutunga upya sentensi ili ziwe katika kauli ya kutenda.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 126
1. Mkulima alilima shamba.
2. Akinyi alisoma kitabu.
3. Mwalimu atakagua vyeti vyao.
4. Otoyo aliondoa nyasi.
5. Duma amemfukuza swara.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi kwamba vitenzi vingi katika
kauli ya kutenda huishia kwa irabu a. Watolee mifano michache: andika, soma,
zungumza, sikiliza, ruka, tembea, kula na hitimisha. Wape kazi ya ziada ya kuandika
vitenzi vitano katika kauli ya kutenda wakiwa nyumbani. Waambie watunge sentensi
wakitumia vitenzi walivyoandika.
163
162
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kauli ya kutendea
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 127-128
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vitenzi katika kauli ya kutendea.
2. Kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendea.
3. Kutunga sentensi sahihi kwa kutumia vitenzi katika kauli ya kutendea.
Maswali dadisi
1. Vitenzi katika kauli ya kutendea hunyambuliwa vipi?
2. Vitenzi katika kauli ya kutendea huisha kwa viambishi gani?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua vitenzi katika kauli ya kutendea.
Kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendea.
Kuigiza vitendo mbalimbali.
Kutumia vitenzi katika kauli ya kutendea katika mawasiliano.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 127-128
Chati Jedwali Mti maneno
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaongoze ili waigize
vitendo mbalimbali vilivyotajwa katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waelekeze wanafunzi katika kusema ni nini walichowafanyia wenzao katika
shughuli iliyotangulia. Majibu ni:
(a) Kupikia
(b) Kusomea
(ch) Kukimbilia
(d) Kuandikia
(e) Kuimbia
Waambie wanafunzi wasome maelezo ya kauli ya kutendea katika Kitabu cha
Mwanafunzi. Wasome na mifano zaidi ya vitenzi katika kauli ya kutendea
kwenye jedwali.
Waongoze wanafunzi ili waweze kutambua vitenzi katika kauli ya kutendea kati ya
maneno yaliyo kwenye mti maneno ulio katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 128
165
164
Kimeidhinishwa na KICD
Vitenzi katika kauli ya kutendea ni:
(a) rukia
(b) bebea
(ch) kimbilia
(d) waliwashonea
(e) pikia
(f) somea
(g) songea
(h) vulia
(i) bomolea
(j) Chimbia
Waelekeze wanafunzi katika kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendea.
Majibu
(a) pikia
(b) semea
(c) vunjia
(d) pimia
(e) ombea
Washirikishe wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia vitenzi katika
kauli ya kutendea. Mwanafunzi atunge sentensi sahihi kama vile:
1. Baba alimbebea nyanya kuni.
2. Mwajuma atamlimia mkulima shamba lote.
3. Amemtupia mbwa mfupa.
4. Nitakusomea sentensi ukinisikiliza.
5. Tutaenda kumtembelea nyanya wakati wa likizo.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi kwamba vitenzi vingi katika
kauli ya kutendea huisha kwa viambishi -ia, ‘-ea au -lia. Watolee mifano michache
kama vile: andikia, somea, zungumzia, sikilizia, rukia, tembelea na hitimishia. Wape
kazi ya ziada ya kuandika vitenzi vitano katika kauli ya kutendea wakiwa nyumbani.
Waambie watunge sentensi wakitumia vitenzi katika kauli ya kutendea walivyoandika
awali.
Kipindi cha 3
Kauli ya kutendwa
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 129-130
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vitenzi katika kauli ya kutendwa.
2. Kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendwa
3. Kutunga sentensi sahihi kwa kutumia vitenzi katika kauli ya kutendwa.
165
164
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Je, vitenzi katika kauli ya kutendwa hunyambuliwa vipi?
2. Vitenzi katika kauli ya kutendwa huisha kwa viambishi gani?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua vitenzi katika kauli ya kutendwa.
Kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendwa.
Kuigiza vitendo mbalimbali katika kauli ya kutendwa.
Kutumia vitenzi katika kauli ya kutendwa katika mawasiliano.
Kuandika sentensi upya kwa kutumia vitenzi katika kauli mbalimbali.
Kushirikiana na wengine katika kujaza mapengo katika jedwali la
mnyambuliko wa vitenzi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 129-130
Jedwali la mnyambuliko wa vitenzi.
Tarakilishi
Chati
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasome sentensi
katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waelekeze wanafunzi kutambua vitenzi vyenye kauli ya kutendwa katika
sentensi walizosoma .
Waongoze wanafunzi katika kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendwa.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa wa 129
1. (a) ilijengwa
(b) kilipikwa
(ch) umepakwa
(d) imeshonwa
(e) amefukuzwa
(f) alikimbizwa
(g) lililimwa
2. (a) shonwa
(b) tuzwa
(ch) pikwa
(d) andikwa
(e) chorwa
(f) okwa
(g) pendwa
(h) uzwa
3. 3-6. Tathmini majibu ya wanafunzi.
167
166
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia vitenzi
vilivyonyambuliwa katika kauli ya kutendwa.
Waambie waandike sentensi walizotunga kwenye tarakilishi. Wanaweza pia
kuandika sentensi hizo kwenye chati.
Waambie wanafunzi wawasambazie wenzao sentensi walizoandika kwenye
tarakilishi na chati ili wazisome.
Waelekeze wanafunzi katika kujaza mapengo katika jedwali la mnyambuliko
wa vitenzi. Majibu yanayotarajiwa ni:
Kutenda Kutendea Kutendwa
imba imbia imbwa
oka okea okwa
pika pikia pikwa
chora chorea chorwa
andika andikia andikwa
funga fungia fungwa
weka wekea wekwa
lima limia limwa
sugua sugulia suguliwa
suka sukia sukwa
fuma fumia fumwa
Waongoze wanafunzi katika kuandika upya sentensi ili ziwe katika kauli ya
kutendwa. Majibu yanayotarajiwa ni:
(a) Barua itaandikwa na Ali.
(b) Muwa unakatwa na Musalia.
(ch) Nywele zimenyolewa na kinyozi.
(d) Chakula kilipikwa na Odhiambo.
(e) Nguo itashonwa na Fundi.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuweka chati ukutani na kuwaambia wanafunzi
wasome sentensi walizotunga katika kauli ya kutendwa. Wakumbushe kuwa vitenzi
vingi katika kauli ya kutendwa huisha kwa kiambishi wa’.
167
166
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Shughuli ya ufunzaji na ujifunzaji wa mada ya afya bora inaweza kufanikishwa kwa
kutumia nyenzo zifuatazo:
Vifaa halisi
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, vipakatalishi, tabuleti, rununu na projekta
Kinasasauti
Mtandao
Tovuti
Picha
Michoro
Chati
Kadi maneno
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
Shughuli za ujifunzaji katika sehemu hii
Mwanafunzi atambue mazungumzo yasiyo rasmi.
AFYA BORA
9
Utangulizi
Afya bora ni hali ya binadamu kuwa na mwili sa, mwili usio na magonjwa, mazingira
sa na akili iliyo sawa. Afya bora humsaidia binadamu kuishi maisha marefu. Ili kuwa
na afya bora ni muhimu kuzingatia kanuni fulani maishani. Kwa mfano, kula mlo
kamili kwa wakati ufaao, kula chakula chenye virutubisho, usa wa mazingira, usa
wa mwili, kunywa maji sa na ya kutosha, kupumzisha akili na kuwa na mwelekeo
chanya kuhusu maisha.
Sehemu hii imeshughulikiwa katika mada nne. Mada hizo ni: mazungumzo katika
miktadha isiyo rasmi, kusoma kwa mapana, kuandika insha ya maelezo na vinyume
vya nomino.
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutumia lugha katika miktadha mbalimbali ya mawasiliano.
2. Kusoma matini ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
3. Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
4. Kutunga sentensi kwa kutumia vinyume vya nomino ipasavyo.
169
168
Kimeidhinishwa na KICD
Mwanafunzi asome matini ili kufaidi ujumbe kuhusu afya bora na lugha
inayotumiwa.
Mwanafunzi atambue vinyume vya nomino.
Mwanafunzi aandike insha ya maelezo
Mwanafunzi atunge sentensi kwa kutumia vinyume vya nomino.
Maswali dadisi
1. Je, watu hutumia lugha isiyo rasmi wakati gani?
2. Ni nini kinachokuvutia unaposoma matini?
3. Je, ni vitu gani vinavyoweza kuandikiwa insha ya maelezo?
4. Je, ni mambo gani unayopaswa kuzingatia unapoandika insha ya maelezo?
5. Unafahamu nomino gani na vinyume vyake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Afya Bora inakuza umilisi wa kimsingi. Baadhi ya umilisi huo ni:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wafanye mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika vikundi
kama vile: kuigiza mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi. Mijadala baina ya wanafunzi
kuhusu mambo watakayoandika kwenye insha ya maelezo itaimarisha mawasiliano na
kukuza ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi wakisambaza insha za maelezo
walizoandika kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Shirikisha matumizi ya tarakilishi, kipakatalishi, video, tabuleti, projekta, intaneti,
mitandao na tovuti ili mwanafunzi ajifunze vipengele mbalimbali vya afya bora na
kusakura habari muhimu kwenye tovuti kuwahusu afya bora. Wanaweza kutumia
tarakilishi kuandika na kuhifadhi kazi yake kuhusu afya bora na vinyume vya maneno
kwenye faili.
(ch) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
afya bora kama vile: kupata lishe bora, usingizi wa kutosha, kufanya mazoezi ya mwili
na kunywa maji. Umilisi huu utampa mwanafunzi hamu ya kujua vipengele vya
afya bora na umuhimu wake katika maisha ya binadamu katika jamii. Pia, atafakari
akijibu maswali tekelezi kuhusu mambo fulani yanayohusiana na afya bora kama vile:
utengenezaji wa sharubati. Mwanafunzi anaweza kuwa na hamu ya kutaka kutumia
vyombo vya kidijitali ili atafute habari zaidi kuhusu afya bora. Habari hii inaweza kuwa
kuhusu: kujikinga na magonjwa, kufanya mazoezi ya mwili n.k.
169
168
Kimeidhinishwa na KICD
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika insha ya maelezo kwa kutumia
tarakilishi, tabuleti au simu ya mkononi. Pia, ubunifu ukuzwe na kuimarishwa kupitia
kutunga sentensi akitumia vinyume vya maneno mbalimbali. Ubunifu utadhihirika
mwanafunzi akitafuta vinyume vya maneno na maana zake akitumia mtandao wa
intaneti.
(e) Kujiamini
Umilisi huu unakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wenzake darasani na
kuigiza mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi kama: nyumbani, hotelini, sokoni
na dukani.
Pia, kujiamini kunakuzwa kupitia mwanafunzi kutengeneza sharubati kutoka kwa
matunda.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu unakuzwa kupitia kumpa mwanafunzi swali la kutafakari, kukiria na
kutafuta jawabu lake ambalo halimo kwenye matini. Kwa mfano, ni kwa nini tunapaswa
kula matunda?
Uhusiano na masuala mtambuko
Masuala mtambuko katika sehemu hii ni pamoja na:
(a) Kujitambua na kujithamini kupitia kuigiza vitendo vya watu wakizungumza
katika miktadha isiyo rasmi na kutunga sentensi akitumia vinyume vya
maneno. Kutengeneza sharubati pia ni njia ya kujithamini na kujitambua
kwa kushiriki katika shughuli za kulinda afya.
(b) Stadi za maisha ambazo mwanafunzi anapata ni kupitia kujieleza, kushiriki
katika vikundi, kuchangia mijadala na kubainisha umuhimu wa afya bora
katika maisha ya binadamu.
(ch) Elimu ya maendeleo endelevu inakuzwa kupitia ujuzi wa kutumia teknolojia
ya kisasa hasa tarakilishi katika kutafuta habari muhimu kuhusu afya bora.
Uhusiano na maadili
Sehemu hii inakuza maadili yafuatayo:
Heshima: mwanafunzi aheshimu watu wengine katika mazungumzo yasiyo
rasmi. Kutumia maneno ya adabu, heshima na upole katika mazungumzo.
Ushirikiano wakati wa mazungumzo sharti watu wawe wa ushirikiano ili
kuelewana,
Upendo: mwanafunzi atajifunza kuwa na upendo kwa watu wengine katika
mazungumzo.
171
170
Kimeidhinishwa na KICD
Umoja katika shughuli za vikundi kupitia kufungua na kufunga tarakilishi.
Uwajibikaji kupitia kwa mwanafunzi kufanya mazoezi ya mwili, kula
matunda, kulala usingizi wa kutosha na kupata lishe bora.
Shughuli za huduma za kijamii
Katika sehemu hii mwanafunzi anaweza kushiriki katika shughuli za huduma za
kijamii zifuatazo:
Kusasha mazingira kama vile ya sokoni kunakouzwa matunda.
Kuwa mwanachama wa chama cha mijadala shuleni.
Kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa afya bora.
Kuwahamasisha wanafunzi wenzake kula chakula kiasi.
Kuhimiza watu kutumia vinyume vya maneno mbalimbali ipasavyo.
Uhusiano na masomo mengine
Mada ya afya bora inaingiliana na masomo mengine kama vile:
Sayansi na Teknolojia ambayo hutoa mafunzo kuhusu afya bora
English Activities hufunza vinyume vya maneno.
Mapendekezo ya mbinu za kutathmini
Tathmini inaweza kufanywa kwa:
Kuhakiki jinsi mwanafunzi anavyosoma vinyume vya maneno.
Kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyotumia msamiati wa afya bora.
Kuhakiki jinsi mwanafunzi anavyoandika insha ya maelezo kwa kuhakikisha
amezingatia muundo na mtindo wa kuandika insha ya maelezo.
Kusikiliza majadilano na wanafunzi kuhusu afya bora.
Kuchanganua namna wanafunzi wanavyojibu maswali kutokana na kifungu
alichosoma kuhusu afya bora.
Kuhakiki namna mwanafunzi anavyotamka vinyume vya maneno.
Kutunga sentensi akitumia vinyume vya maneno mbalimbali.
Kujaza mapengo katika sentensi.
Kuchunguza namna wanafunzi wanavyotumia msamiati wa afya bora katika
mawasiliano.
Kukadiria ushiriki wa mwanafunzi katika shughuli za darasani.
171
170
Kimeidhinishwa na KICD
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Unaweza kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kupitia mikakati
ifuatayo:
Wape shughuli mbadala wanafunzi wenye hitilafu katika baadhi ya viungo
vyao vya mwili kama vile mikono na miguu. Kwa wanafunzi hawa, badala ya
kuigiza mchezo wa kuigiza darasani, wanaweza kusoma mchezo huo wakiwa
wameketi.
Watengee wanafunzi wanaopata matatizo katika kuelewa baadhi ya masomo
muda maalumu wa kurudia shughuli husika
Tumia mbinu na nyenzo kama vile: video, picha au kinasasauti kufunza
vipengele mbalimbali na kuwafanya wanafunzi kufurahia ujifunzaji.
Kwa wanafunzi wasioona, unaweza kushirikisha sauti wakati wa ufundishaji
ili wajifunze kupitia kusikia.
Uwe na subira na wanafunzi walio na matatizo ya kuzungumza kama
vigugumizi kwa kuwapa muda zaidi wanaposoma.
Kwa wanafunzi wenye uwezo wa juu darasani, wape kazi ya ziada na
changamano kama vile kuchora wanyama wa porini au kutunga sentensi
zaidi.
Utangulizi
Waelekeze wanafunzi katika kutazama picha katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 131 wakiwa darasa zima.
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya darasa kisha awaambie
wenzake alichoona kwenye picha hiyo. Wanafunzi wataje: matunda, maji,
maziwa, juisi, keki, peremende na dawa
Waongoze wanafunzi katika kueleza vitu walivyoona kwenye picha hiyo vina
faida gani katika mwili wa binadamu.Wanafunzi wanaweza kutoa majibu
kama: kutia nguvu au kujenga mwili.
Wakirishe wanafunzi kwa kuwauliza mawazo yao kuhusu wakati ambao
vyakula hivyo huliwa.
Waongoze wanafunzi katika kutambua vitu vinavyoboresha afya kwenye
picha. Vitu hivi ni kama: maji, matunda, mboga na maziwa.
Waongoze wanafunzi katika kutambua vitu vinavyodhoosha afya ya
binadamu. Vitu hivi ni kama peremende,keki na juisi
Waelekeze wanafunzi katika kusoma maelezo kuhusu afya bora.
173
172
Kimeidhinishwa na KICD
Kusikiliza na Kuzungumza
Mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 132-133
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi mwanafunzi aweze:
1. Kutambua miktadha ya mazungumzo isiyo rasmi.
2. Kutumia lugha ipasavyo katika miktadha isiyo rasmi.
Maswali dadisi
1. Lugha isiyo rasmi hutumiwa lini?
2. Ni maneno gani ya upole yanayotumiwa katika mazungumzo yasiyo rasmi?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue mazungumzo yasiyo rasmi.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kutaja miktadha ya mazungumzo
yasiyo rasmi.
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake kuigiza mazungumzo yasiyo rasmi.
Mwanafunzi atambue umuhimu wa nidhamu ya lugha katika mazungumzo
yasiyo rasmi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 132-133
Picha
Rununu au tarakilishi
Kanda za sauti
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wataje mahali ambapo mazungumzo
yasiyo rasmi hufanyika. Wanaweza kutaja: sokoni, dukani, nyumbani, hotelini
au mtaani.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu kisha uwaambie
wasome mazungumzo yaliyo katika Kitabu cha Mwanafunzi.
173
172
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kujadili mada inayozungumziwa katika
mazungumzo hayo. Wanafunzi watambue kuwa mada inayozungumziwa ni
afya bora.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua maneno ya adabu na heshima
yaliyotumiwa katika mazungumzo hayo. Wanafunzi watambue maneno kama
vile: bee! na asante.
Waongoze wanafunzi katika kujadili afya bora inahusu nini. Wanaweza
wakajadili wajadili hoja kama vile:
ü Usa wa mwili
ü Akili tulivu
ü Kufanya mazoezi ya mwili
ü Kupata usingizi wa kutosha
ü Kupata mlo kamili kwa wakati ufaao
Washirikishe wanafunzi katika kuigiza mazungumzo kati ya Imani na Amani
wakizingitia wahusika, maelekezo na matumizi ya viziada lugha.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa mazungumzo
katika miktadha isiyo rasmi ni kama yale ya: nyumbani, jikoni, sokoni, dukani au
hotelini. Wape wanafunzi kazi ya nyumbani. Waambie wazungumze na ndugu, wazazi
au walezi wao wakika nyumbani. Pia, waambie watumie maneno ya heshima kama
vile: kwaheri, karibu, samahani, pole na asante.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 133
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi mwanafunzi aweze:
1. Kutambua maneno ya upole yanayotumiwa katika miktadha ya mazungumzo
isiyo rasmi.
2. Kutumia lugha ipasavyo katika miktadha isiyo rasmi.
Maswali dadisi
1. Ni maneno gani ya upole yanayotumiwa katika mazungumzo yasiyo rasmi?
2. Je, ni muhimu kutumia maneno ya upole katika mazungumzo yasiyo rasmi?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue mazungumzo yasiyo rasmi.
Mwanafunzi asikilize mazungumzo yaliyorekodiwa kati ya mtoto na nyanya.
175
174
Kimeidhinishwa na KICD
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake katika kuigiza mazungumzo yasiyo rasmi.
Mwanafunzi ataje maneno ya upole katika mazungumzo yasiyo rasmi.
Mwanafunzi atambue umuhimu wa nidhamu ya lugha katika mazungumzo
yasiyo rasmi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 133
Picha
Rununu au tarakilishi
Rekoda
Kanda za sauti
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mahali ambapo
mazungumzo yasiyo rasmi hufanyika. Wanaweza kutaja: sokoni, dukani,
nyumbani, hotelini au mtaani.
Waongoze wanafunzi katika kusikiliza mazungumzo yaliyorekodiwa kwenye
rekoda. Wanafunzi wasikilize kwa makini mazungumzo hayo. Mazungumzo
yenyewe ni haya:
(Ni nyumbani kwa nyanya. Nyanya ameandaa mayai, ndizi na viazi vitamu.)
Egara: Nyanya, mimi nitakula mayai matatu. Mayai ya kuku wako ni
matamu sana.
Nyanya: La hasha mjukuu wangu! Kila mtu atakula yai moja pekee. Kula
mayai mengi kila siku ni hatari. Mayai yanaweza kusababisha mtu
kuwa na uzani kupita kiasi.
Egara: Samahani! Sikujua hilo!
Nyanya: (Akiwapa maziwa.) Mwili unahitaji chakula kiasi tu.
Babu: (Akivaa miwani yake.) Maziwa ni muhimu pia. Maziwa humsaidia
mtu kuwa na meno imara. Meno imara husaidia kutafuna vyakula.
Egara: Asante kwa kiamshakinywa nyanya na babu! Nimeshiba sana.
Nyanya: Karibu mjukuu wangu.
Waongoze wanafunzi katika kujibu maswali kutokana na mazungumzo
waliyosikiliza.
Waelekeze ili waweze kutambua maneno ya upole na adabu yaliyotumiwa
katika mazungumzo. Maneno hayo ni kama vile:
ü Samahani ü Karibu ü Asante
175
174
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze katika kujadili umuhimu wa kutumia maneno ya upole na heshima
katika mazungumzo.
Waelekeze wanafunzi katika kuigiza mazungumzo waliyosikiliza kwenye
rekoda. Wanafunzi waigize darasani nafasi ya Egara, Nyanya na Babu.
Wengine watazame maigizo hayo.
Hitimisho: kamilisha kipindi hiki kwa kuwakumbusha wanafunzi kuhusu sifa za
mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi. Wape wanafunzi hao kazi ya nyumbani.
Waambie wakiwatembelea nyanya, babu au jamaa wengine, wazungumze nao kuhusu
jambo lolote wanalopenda. Wanaweza kujirekodi kwa kutumia rununu na baadaye,
wasikilize mazungumzo hayo wakiwa nyumbani au darasani.
Kusoma
Kusoma kwa Mapana
Matini
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 134-135
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua matini yanayovutia.
2. Kusoma matini ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
3. Kufurahia usomaji wa matini ili kupanua mawazo yake.
Maswali Dadisi
1. Kwa nini unapenda kusoma?
2. Kwa nini ulichagua matini fulani?
3. Ni nini hukuvutia unaposoma matin
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua matini maktabani.
Kusoma matini.
Kusimulia yanayohusu matini hiyo.
Kujadili na wenzake kuhusu matini hiyo.
177
176
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo za ufunzaji na ujifunzaji
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 134-135
Matini
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi afya bora inahusu nini.
Waongoze kusoma matini kuhusu, Afya ni Uhai kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi. Kila mwanafunzi asome matini haya peke yake. Tembea
darasani ili kuhakikisha kuwa wanasoma kwa ufasaha.
Washirikishe wanafunzi katika kujibu maswali kutokana na matini waliyosoma.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 135
1. Matini haya yanahusu afya bora.
2. Virutubishi muhimu katika vyakula ni vitamini, protini na wanga.
3. Vyakula vya kiasili ni: yugwa, viazi vitamu na mihogo.
4. Miti humsaidia binadamu kwa hewa sa na upepo mwanana.
5. Mwanafunzi ataje kile ambacho yeye hufanya ili kuwa na afya bora.
Anaweza kutaja hoja kama vile:
ü Kupata usingizi wa kutosha.
ü Kunywa maji sa.
ü Kula vyakula vifaavyo kwa wakati ufaao.
ü Kufanya mazoezi.
Unaweza kuhitimisha kwa kuwaambia wanafunzi kuwa afya bora
ni msingi wa maisha ya binadamu. Wape kazi ya ziada. Waambie
watafute maana ya maneno yafuatayo kwenye kamusi:
(a) afya
(b) kirutubishi
(ch) lishe
(d) wanga
Wape wanafunzi kazi ya nyumbani. Waambie wakienda nyumbani
wawaulize wazazi wao vyakula vya kiasili wanavyofahamu. Waandike
majina ya vyakula hivyo. Kazi hiyo itasahihishwa wanafunzi
watakaporejea kutoka nyumbani.
177
176
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 135
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua matini yanayovutia kwenye mtandao.
2. Kusoma matini kutoka kwa mtandao ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
3. Kufurahia usomaji wa matini kwenye mtandao ili kupanua mawazo yake.
Maswali dadisi
1. Kwa nini ni muhimu kunywa maji?
2. Ni nini kinaweza kufanyika mtu akikataa kunywa maji?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusakura matini kuhusu kunywa maji kwenye mtandao.
Kusoma matini kuhusu kunywa maji kwenye mtandao.
Kusimulia yanayohusu matini hiyo.
Kujadili kuhusu matini hiyo.
Nyenzo za ufunzaji na ujifunzaji
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 135
Tarakilishi
Matini kuhusu umuhimu wa kunywa maji
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi afya bora inahusu
nini. Wanafunzi wakirie na wajibu. Wanaweza kutaja kunywa maji ya
kutosha miongoni mwa mengine.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu. Waambie wasakure
kwenye mtandao, ‘umuhimu wa kunywa maji.
Waambie wasome matini waliyopata kwenye mtandao wakiwa watatuwatatu.
Waongoze katika kusimulia wenzao yale waliosoma kwenye mtandao.
Waelekeze wanafunzi ili wajadili ujumbe katika matini hayo. Wanaweza
kusema yalihusu umuhimu wa kunywa maji. Umuhimu wenyewe unaweza
kuwa:
ü Kuzuia magonjwa.
ü Kuondoa sumu mwilini.
179
178
Kimeidhinishwa na KICD
ü Kusaidia katika kupunguza uzani.
ü Kuboresha na kuimarisha ngozi.
ü Kuhamasisha ukuaji wa nywele bora zenye afya.
ü Kuongeza na kuimarisha kinga ya mwili.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu ili wajadili hoja hizo.
Waandike hoja zao na maelezo.
Waambie wanafunzi waandike matini hayo kwenye tarakilishi kisha
wawasambazie wanafunzi wenzao darasani.
Waongoze wanafunzi katika kusoma matini waliyosambaziwa na wenzao.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwambia wanafunzi kuwa: maji ni uhai. Wahimize
kunywa maji kila asubuhi. Wape kazi ya nyumbani. Waambie wakienda nyumbani
wawaambie wazazi au walezi wao kuwa maji ni muhimu sana katika mwili wa
binadamu. Binadamu anahitaji maji ili awe na afya bora.
Kipindi cha 3
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 135-137
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kusoma matini ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
2. Kufurahia usomaji wa matini ili kupanua mawazo yake.
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma matini.
Kujibu maswali kutokana matini ya, Utamu wa Sharubati.
Kusimulia ujumbe katika matini hayo.
Kujadili na wenzake kuhusu matini hayo.
Nyenzo
Matunda mbalimbali: ndizi, nanasi, parachichi na chungwa
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 35-136
Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuja na matunda darasani. Tafuta: maembe,
machungwa, ndizi, pera au papai ili uwaonyeshe wanafunzi. Wanafunzi wataje
majina ya matunda hayo.
179
178
Kimeidhinishwa na KICD
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaambie wasome
matini yenye anwani, ‘Utamu wa Sharubati kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 135-136.
Waongoze wanafunzi katika kujibu maswali ya matini waliyosoma.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 137
1. Matunda yaliyokuwa sokoni ni maembe, mapapai, mananasi,
machungwa, ndizi, maparachichi, mapera, matikitimaji, peasi na
matomoko.
2. Musa alitaka kupanda mwembe ili apate maembe.
3. Matunda yaliyonunuliwa yaligharimu shilingi mia tatu na themanini.
4. Musa hawakununua ndizi kwa sababu walikuwa na ndizi tamu zaidi
nyumbani.
5. Matunda yaliyotumika kuunda sharubati ni ndizi, machungwa, mapapai
na tikitimaji.
Hitimisho: waambie wanafunzi wakienda nyumbani wawaitishe wazazi au walezi wao
matunda yanayopatikana nyumbani au sokoni. Wasashe matunda hayo na kuyala.
Baadaye, waandike majina ya matunda hayo. Pia, wachore matunda hayo kwenye
madaari.
Kuandika
Insha ya Maelezo
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 137
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya maelezo kwa kuzingatia muundo.
2. Kuandika insha ya maelezo akizingatia ujumbe, mada, mtindo na muundo ufaao.
3. Kuchangamkia utunzi wa insha ya maelezo ili kujenga ubunifu.
Maswali dadisi
1. Ni mambo gani yanayoweza kutungiwa insha ya maelezo?
2. Unazingatia nini unapoandika insha ya maelezo?
181
180
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma maelezo kuhusu insha ya maelezo.
Kutambua vifungu vya maelezo kwenye matini au tarakilishi.
Kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya maelezo.
Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 137
Insha za maelezo Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi warejelee mada ya saba sehemu
ya kuandika insha ya maelezo. Wajikumbushe insha ya maelezo ni nini.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne na uwaongoze katika
kukumbushana kuhusu insha ya maelezo. Wanaweza kusema kuwa: Insha ya
maelezo husimulia namna tukio, jambo ama kisa kilivyotokea.
Waelekeze katika kujadili muundo wa insha ya maelezo. Wanafunzi wajadili
hoja kama vile:
ü Insha ya maelezo huwa na muundo ufuatao:
i. Kichwa- hutokana na mada. Kichwa kiwe chenye mvuto na kiwe na maneno
machache aghalabu yasiyopita sita. Kichwa huandikwa kwa heru kubwa na
kupigiwa mstari.
ii. Utangulizi- hueleza kisa kinahusu nini. Utangulizi huandikwa kwa njia ya
kumvutia msomaji kuendelea kusoma kisa.
iii. Mwili- katika sehemu hii, kisa huelezwa vizuri na kwa mpangilio mwafaka.
Lugha inayoeleweka, rahisi na yenye mvuto hutumiwa.
iv. Hitimisho- msimulizi hutoa muhtasari wa kisa katika aya ya mwisho.
Hitimisho linaweza kutoa funzo fulani kwa msomaji.
Washirikishe wanafunzi katika kujadili mambo yanayozingatiwa katika
kuandika insha ya maelezo. Jadili: mambo hayo yanahusu nini, nani, wapi,
lini na kwa nini.
Waongoze wanafunzi katika kuandika insha ya maelezo kuhusu: ‘Lishe Bora.
Waelekeze katika kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya maelezo kuhusu
insha hiyo. Wanaweza kuzingatia vidokezo vifuatavyo:
ü Lishe bora ni nini?
ü Lishe bora hupatikana vipi?
ü Vyakula gani hutupatia lishe bora?
181
180
Kimeidhinishwa na KICD
ü Lishe bora ina umuhimu gani?
ü Kuna madhara katika kutozingatia lishe bora?
Tathmini insha ya maelezo ambayo wanafunzi wataandika.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie wasakure
kwenye mtandao na kisha waandike insha ya maelezo yenye anwani: Umuhimu wa
usingizi’.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 137-138
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya maelezo kwa kuzingatia muundo.
2. Kuandika insha ya maelezo akizingatia vidokezo na mtindo ufaao.
3. Kuchangamkia utunzi wa insha ya maelezo ili kujenga ubunifu.
Maswali Dadisi
1. Ni mambo gani yanayoweza kutungiwa insha ya maelezo?
2. Unazingatia nini unapoandika insha ya maelezo?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua vifungu vya maelezo kwenye matini au tarakilishi.
Kushiriki katika kujadili mada ya insha ya maelezo.
Kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya maelezo.
Kuandika insha ya maelezo mtandaoni kwa kufuata kanuni zifaazo.
Kusambaza insha ya maelezo mtandaoni.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 137-138
Insha za maelezo
Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi warejelee kipindi kilichotangulia
kuhusu kuandika insha ya maelezo.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaongoze katika
kujadili kuhusu insha ya maelezo yenye anwani: Jinsi ya Kudumisha Afya Bora
183
182
Kimeidhinishwa na KICD
Washirikishe katika kujadili vidokezo walivyopewa kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi.
Waongoze wanafunzi katika kuandika insha ya maelezo kuhusu jinsi ya
kudumisha afya bora wakizingatia vidokezo walivyojadili. Wanaweza
kuandika kwenye chati ama kwenye tarakilishi.
Waambie wanafunzi wawasomee wenzao insha walizoandika. Tathmini insha
za maelezo ambazo wanafunzi wataandika.
Waelekeze katika kusambaza insha walizoandika kupitia mtandao ili wafunzi
wenzao wasome. Wanafunzi wasome insha za maelezo walizosambaziwa
kwenye mitandao.
Kwa walioandika kwenye chati, waongoze kuziweka chati kwenye ukuta.
Waambie wawe wakizisoma insha hizo mara kwa mara.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi iliyo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi, ukurasa wa 138. Kila mwanafunzi aandike insha ya maelezo kuhusu
umuhimu wa maji katika afya ya binadamu kisha waisambaze kwa wanafunzi wenzao
ili waisome na kuitathmini.
Saru
Vinyume vya nomino
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 138-139
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya kinyume cha nomino ili kukibainisha ipasavyo.
2. Kutambua vinyume vya nomino katika matini.
3. Kutunga sentensi akitumia vinyume vya nomino ipasavyo.
Maswali dadisi
1. Je, nomino zote zina vinyume?
2. Ni nomino gani zina vinyume?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua vinyume vya nomino.
Kushirikiana na wenzake kutafuta vinyume vya nomino.
Kutalii mazingira yake na kuunda orodha ya vinyume vya nomino.
183
182
Kimeidhinishwa na KICD
Kutunga sentensi akitumia vinyume vya nomino akizingatia upatanisho wa
kisaru.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 138-139
Chati ya vinyume vya nomino
Jedwali la vinyume vya nomino
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje nomino
mbalimbali. Wanafunzi wataje nomino kama: baba, dada, mama, kaka, babu
au nyanya.
Waongoze wanafunzi katika kugundua kuwa baba ni kinyume cha mama,
kaka ni kinyume cha dada na babu ni kinyume cha nyanya.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaelekeze katika
kusoma maneno yaliyo kwenye jedwali katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 138. Waambie wasome kwa sauti.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua kuwa maneno waliyosoma ni vinyume
vya nomino. Kwa mfano: usiku - mchana.
Waongoze wanafunzi katika kutaja maneno mengine ambayo ni vinyume vya
nomino. Wanaweza kutaja maneno kama vile:
ü giza-nuru
ü kicheko-kilio
ü Kusini-Kaskazini
ü kushoto-kulia
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia maneno waliyotaja.
Waongoze wanafunzi ili waweze kusoma maelezo kuhusu vinyume vya
nomino katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waelekeze katika kufanya zoezi la kutafuta vinyume vya nomino katika
Kitabu cha Mwanafunzi.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 139
(a) kaka
(b) nyanya
(ch) baba
(d) mwalimu
(e) Uchafu
(f) Shibe
(g) Mwisho
(h) shangazi
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watalii mazingira ya
darasa lao. Waambie watambue nomino na vinyume vyake. Kwa mfano, mwalimu-
185
184
Kimeidhinishwa na KICD
mwanafunzi. Wanafunzi waandike orodha ya vinyume vya nomino zinazopatikana
katika darasa lao. Wape wanafunzi kazi ya ziada ili waifanye wakiwa nyumbani.
Wanafunzi watafute na waandike vinyume vya nomino: Majibu yanayotarajiwa ni:
1. utajiri - umaskini
2. usiku - mchana
3. mwanzo - mwisho
4. muuzaji - mnunuzi
5. ardhi - mbingu
6. Mashariki - Magharibi
7. tajiri - maskini
8. asubuhi - jioni
9. furaha - huzuni
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua vinyume vya nomino katika matini.
2. Kutunga sentensi akitumia vinyume vya nomino ipasavyo.
Maswali Dadisi
1. Je, nomino zote zina vinyume katika sentensi?
2. Ni nomino gani zina vinyume katika sentensi?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua vinyume vya nomino.
Kushirikiana katika kutafuta vinyume vya nomino.
Kutalii mazingira na kuunda orodha ya vinyume vya nomino.
Kutunga sentensi kwa kutumia vinyume vya nomino na kuzingatia
upatanisho wa kisaru.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 139-140
Chati ya vinyume vya nomino
Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje vinyume vya nomino
kama vile:raki, shujaa, kaka na mgeni. Wanafunzi wataje vinyume vya
nomino hizo. Wataje: adui, mwoga, dada na mwenyeji.
185
184
Kimeidhinishwa na KICD
Waambie watunge sentensi wakitumia maneno hayo.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma kwa sauti sentensi katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 139.
Waongoze wanafunzi katika kutambua kuwa maneno yaliyo katika heru za
italiki ni vinyume vya nomino.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika sentensi walizopewa katika kinyume.
Hakikisha kuwa wanaandika vinyume vya nomino.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa wa 140
1. Nomino zinabadilika na kuwa katika kinyume.
2. Maneno katika heru za italiki ni vinyume.
(a) Kaka ataamka jioni.
(b) Mfalme ameka kwenye kasri.
(ch) Adui yake amewasili salama.
(d) Uongo utadhihirika hivi karibuni.
(e) Nyanya ameketi kistaarabu.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wakiwa nyumbani watalii
mazingira ya nyumbani kwao kisha watambue nomino na vinyume vyake.Waambie
waandike kazi hiyo kwenye madaari yao na kwenye tarakilishi. Wahifadhi kazi hiyo
kwenye tarakilishi kwa faili iitwayo ‘Vinyume vya nomino.
187
186
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Uteuzi, maandalizi na matumizi ya nyenzo utafanikisha shughuli ya ujifunzaji na
ufunzaji. Hakikisha umeandaa nyenzo mwafaka ili kufanikisha shughuli hii. Unaweza
kutumia nyenzo zifuatazo:
Vifaa halisi
Vyombo vya kidijitali: tarakilishi, vipakatalishi, tabuleti, rununu na projekta.
Kinasasauti
Mtandao
Tovuti
Picha
Michoro
Chati
Kadi maneno
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
KUKABILIANA NA UHALIFU
10
Utangulizi
Kila jamii huwa na sheria ambazo huwaongoza wanajamii katika shughuli mbalimbali.
Uhalifu ni tendo la kuvunja sheria za jamii. Hata hivyo, kuna wale ambao huvunja
sheria kwa kujiingiza katika vitendo haramu katika jamii kama vile: wizi, mauaji au
ugaidi.
Sehemu ya Kukabiliana na Uhalifu imeshughulikiwa katika mada nne. Mada hizo ni:
kusikiliza na kuzungumza (tashbihi za kimo na umbo), kusoma kwa mapana, kuandika
insha ya masimulizi na saru (nyakati na hali).
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kutumia tashbihi za kimo na umbo kwa usahihi katika sentensi.
2. Kutambua na kufungua faili iliyo na kifungu cha kusoma katika tarakilishi.
3. Kusoma matini ili kupata ujumbe.
4. Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
5. Kutunga sentensi akitumia vitenzi katika nyakati mbalimbali, hali ya kuendelea.
187
186
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji katika sehemu hii
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia tashbihi za kimo na umbo.
Mwanafunzi asome matini kwenye tovuti salama ili kufaidi ujumbe na lugha
inayotumiwa.
Mwanafunzi atafute maana za maneno mapya kwenye kamusi mtandaoni.
Mwanafunzi aandike insha ya masimulizi.
Mwanafunzi atunge sentensi katika nyakati mbalimbali: hali ya kuendelea.
Maswali Dadisi
Katika sehemu hii, maswali dadisi yafuatayo yatamwongoza mwanafunzi:
1. Je, ni tashibihi zipi hutumiwa kueleza kimo na umbo?
2. Utafanya nini iwapo mtu usiyemfahamu atakutumia ujumbe kwenye mtandao?
3. Je, ni mambo gani unayopaswa kuzingatia unapoandika insha ya masimulizi?
4. Ni viambishi gani hutumiwa kuwakilisha nyakati na hali mbalimbali katika
vitenzi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Sehemu hii inakuza umilisi wa kimsingi. Baadhi ya umilisi huo ni:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wafanye mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika vikundi
kama vile: kutunga sentensi wakitumia tashbihi za kimo na umbo. Mijadala baina ya
wanafunzi kuhusu mambo watakayoandika kwenye insha ya masimulizi itaimarisha
mawasiliano na kukuza ushirikiano. Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi wakisambaza
insha za masimulizi walizoandika kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi,
kipakatalishi, video, tabuleti, projekta, intaneti, mitandao na tovuti ili mwanafunzi
ajifunze njia mbalimbali za kukabiliana na uhalifu na kusakura habari kuhusu nyakati
na hali. Wanaweza kutumia tarakilishi kuandika na kuhifadhi kazi kuhusu namna ya
kukabiliana na uhalifu na sentensi zilizo katika nyakati na hali mbalimbali kwenye
faili.
(ch) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
namna ya kuwaepuka wahalifu mtandaoni. Umilisi huu utampa mwanafunzi hamu ya
189
188
Kimeidhinishwa na KICD
kujua njia za kuwaepuka wahalifu. Mwanafunzi anaweza kuwa na hamu ya kutaka
kutumia vyombo vya kidijitali ili atafute habari kuhusu nyakati na hali katika lugha ya
Kiswahili.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika insha ya masimulizi kwa kutumia
tarakilishi, tabuleti au simu ya mkononi. Pia, ubunifu ukuzwe na kuimarishwa
kupitia kutunga sentensi akitumia nyakati na hali mbalimbali. Ubunifu utadhihirika
mwanafunzi akitafuta matini kwenye tovuti akitumia mtandao wa intaneti.
(e) Kujiamini
Umilisi huu unakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kutoa maelezo kuhusu michoro kitabuni.
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu unakuzwa kupitia kumpa mwanafunzi swali la kutafakari, kukiria na
kutafuta jawabu. Kwa mfano, unaweza kuwauliza wanafunzi: ni nini athari za kuharibu
misitu?
Uhusiano na masuala mtambuko
Sehemu hii ina uhusiano na masuala mtambuko yafuatayo:
(a) Kujitambua na kujithamini kupitia kusimama mbele ya wenzake darasani
na kueleza alichoona kwenye michoro kuhusu uhalifu. Kutunga sentensi
akitumia nyakati na hali ni njia ya kujithamini na kujitambua.
(b) Stadi za maisha kwa kujieleza, kushiriki katika vikundi, kuchangia mijadala
na kubainisha uhalifu unaokumba binadamu katika maisha yake.
(ch) Elimu ya mazingira kwa kufundisha kuhusu umuhimu wa kutunza na
kuhifadhi mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Uhusiano na maadili
Sehemu hii ina uhusiano na maadili kwa njia zifuatazo:
Heshima na adabu kwa mwanafunzi kuheshimu mazingira na kuyatunza.
Mwanafunzi pia awe na heshima katika mijadala na wengine.
Ushirikiano wakati wa mijadala kuhusu aina za uhalifu na namna ya
kukabiliana na uhalifu wa mitandao.
Upendo kwa kuwa na upendo kwa watu wengine katika mazungumzo.
Umoja katika shughuli za vikundi kama vile: kutunga sentensi wakitumia
nyakati na hali mbalimbali.
Uwajibikaji kwa mwanafunzi kuripoti watu wenye nia ya kufanya uhalifu.
189
188
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za huduma za kijamii
Katika sehemu hii, mwanafunzi anaweza kushiriki katika shughuli za huduma za
kijamii zifuatazo:
Kushiriki katika juhudi za kuhifadhi mazingira kama kupanda miti.
Kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuepukana na uhalifu kama wizi na
kutuma ujumbe usiofaa kwa watu wengine.
Kuwahamasisha wanafunzi wenzake kuripoti kwa wazazi, walezi au mwalimu
wanapotumiwa jumbe mtandaoni na watu wasiowajua.
Kuhimiza watu kutumia nyakati na hali mbalimbali katika sentensi ipasavyo.
Uhusiano na masomo mengine
Mada ya afya bora inaingiliana na masomo mengine kama vile:
Sayansi na Teknolojia: mada hii hutoa mafunzo kuhusu vifaa vya kidijitali.
English Activities kuna mada kuhusu tashbihi. Stadi za kusoma na
kuandika hufunzwa katika English Activities. Saru hasa vitenzi na sentensi
hufundishwa.
Indigenous Language Activities kuna mada kama vile tashbihi ambazo
hufunzwa.
Shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Wanafunzi watembelee maeneo ambapo miti imekatwa ili kupanda miti katika sehemu
hizo. Wanaweza kushiriki katika kuelimisha watu kuhusu hatari ya kujiingiza katika
uhalifu wa mtandaoni.
Mapendekezo ya mbinu za kutathmini
Tathmini inaweza kufanywa kwa:
Kuhakiki jinsi wanafunzi wanavyosoma sentensi katika nyakati mbalimbali.
Kuchunguza jinsi wanafunzi wanavyotumia msamiati wa kukabiliana na
uhalifu.
Kuhakiki jinsi wanafunzi wanavyoandika insha ya masimulizi. Sharti
wazingatie muundo na mtindo wa kuandika insha ya masimulizi.
Kusikiliza majadilano ya wanafunzi kuhusu namna ya kukabiliana na uhalifu.
Kuchanganua namna wanafunzi wanavyojibu maswali kutokana na kifungu
alichosoma kuhusu usalama wa kidijitali.
Kutunga sentensi kwa kutumia nyakati na hali mbalimbali.
Kujaza mapengo katika majedwali.
191
190
Kimeidhinishwa na KICD
Kuchunguza namna wanafunzi wanavyotumia msamiati wa kukabiliana na
uhalifu katika mawasiliano.
Kukadiria ushiriki wa wanafunzi katika shughuli za darasani.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Unaweza kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kupitia mikakati
ifuatayo:
Wape shughuli mbadala wanafunzi wenye hitilafu katika baadhi ya viungo
vyao vya mwili kama miguu na mikono. Badala ya wanafunzi hawa kusimama
wakati wa kueleza yaliyo kwenye michoro darasani, wanaweza kueleza wakiwa
wameketi.
Watengee wanafunzi wanaotatizika kuelewa muda maalumu wa kurudia
shughuli kama vile nyakati na hali katika sentensi baada ya ujifunzaji
darasani.
Tumia mbinu na nyenzo kama vile video, picha au kinasasauti kufunza
vipengele mbalimbali vya kukabiliana na uhalifu.
Uwe na subira na wanafunzi wanaposoma, wanapoandika, wanapozungumza
au wanaposhiriki katika shughuli mbalimbali darasani.
Wale ambao wana uwezo wa juu darasani, wape kazi ya ziada na changamano.
Utangulizi
Waelekeze wanafunzi katika kutazama picha zilizo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 141.
Teua mwanafunzi mmoja asimame mbele ya darasa na kuwaambia wenzake
alichoona katika picha hizo.
Waongoze wanafunzi katika kueleza mazingira kwenye picha a na b.
Waongoze wanafunzi katika kueleza uhalifu walioona katika picha a ni wa
aina gani. Wanafunzi wanaweza kusema kuwa huo ni uhalifu wa mazingira
kwa ukataji wa miti.
Wakirishe wanafunzi kwa kuwauliza ni vipi uharibifu wa mazingira
unaweza kukabiliwa. Waambie wataje juhudi wanazoweza kufanya ili kulinda
mazingira. Wanaweza kutaja: upanzi wa miti na kuwashtaki wanaokata miti
kiholela.
191
190
Kimeidhinishwa na KICD
Kusikiliza na Kuzungumza
Tashbihi za kimo na umbo
Kipindi cha 1
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya tashbihi ili kuibainisha.
2. Kutambua tashbihi za kimo na umbo katika matini.
3. Kutumia tashbihi za kimo na umbo kwa usahihi katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Tashbihi hutumiwa kufanya kazi gani?
2. Je, ni tashbihi zipi hutumiwa kueleza kimo na umbo la kitu au mtu?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kueleza maana ya tashbihi.
Kutambua tashibihi za kimo na umbo.
Kurejelea michoro ili kutumia tashbihi za kimo na umbo.
Kutunga sentensi kwa kutumia tashbihi za kimo na umbo.
Kukamilisha sentensi kwa kutumia tashbihi za kimo na umbo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 142-143
Picha
Michoro
Vifaa halisi kama sindano, nyundo
Video zenye wanyama
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watazame picha kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi, ukurasa wa 142 kisha waseme majina na wanyama au vitu
kwenye picha hizo.
Teua mwanafunzi mmoja aje mbele ya darasa na kutaja majina hayo. Ataje
twiga, nyundo, nguruwe na sindano.
193
192
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kutambua sifa za wanyama na vitu vilivyo
kwenye picha na kulinganisha sifa hizo na binadamu. Walinganishe kwa
kusema: mrefu kama twiga, mfupi kama nyundo, mnono kama nguruwe,
mwembamba kama sindano.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma maelezo kuhusu tashbihi kwenye kitabu
cha wanafunzi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaongoze katika
kusoma sentensi zilizo katika Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha kuwa
wanasoma kwa usahihi.
Waelekeze katika kutambua tashbihi katika sentensi walizosoma kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 143.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 143
1. kimestawi kama mgomba
2. mfupi kama mbilikimo
3. shujaa kama simba
4. nyeusi kama makaa
5. imesinyaa kama magome
6. walishonana kama ushanga
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi mpya kwa kutumia tashbihi
walizotambua. Hakiki sentensi za wanafunzi.
Waongoze wanafunzi ili wawasomee wenzao sentensi walizoandika.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha kuwa tashbihi ni msemo wa
kulinganisha sifa za mtu, mnyama au kitu na kingine. Tashbihi hutumia maneno, ‘kama,
au mfano wa kulinganisha. Tashbihi za kimo ni misemo ambayo hufananisha sifa za
mtu au kitu na kingine kwa kuzingatia urefu wake. Tashbihi za umbo hufananisha sifa
za mtu au kitu na kingine kwa kuzingatia mwonekano wake.
Wape wanafunzi kazi ya vikundi ya kutafuta tashbihi tano za kimo na umbo
katika kamusi ya tashbihi.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 144
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya tashbihi ili kuibainisha.
193
192
Kimeidhinishwa na KICD
2. Kutambua tashbihi za kimo na umbo katika matini.
3. Kutumia tashbihi za kimo na umbo kwa usahihi katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Tashbihi hufanya kazi vipi?
2. Ni tashbihi gani hutumiwa kuelezea kimo na umbo la kitu au mtu?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua tashibihi za kimo na umbo.
Kutunga sentensi akitumia tashbihi za kimo na umbo.
Kusambaza sentensi zilizo na tashbihi za kimo na umbo kupitia mtandao.
Kukamilisha sentensi akitumia tashbihi za kimo na umbo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 144
Chati Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya tashbihi za
kimo na umbo walizojifunza katika kipindi kilichotangulia.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaongoze katika
kusoma sentensi zilizo Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 144.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua tashbihi katika sentensi walizosoma
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Majibu yanayotarajiwa ni kama vile:
1. alinenepa kama nguruwe
2. mwembamba kama sindano
3. akonde kama ngonda
4. imara kama mwamba
Waongoze wanafunzi katika kukamilisha sentensi kwa kuchagua tashbihi
ifaayo.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 144
1. sindano
2. unyasi
3. mbuyu
4. mnara
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia tashbihi walizopewa
wanafunzi watunge sentensi hizo. Hakiki sentensi za wanafunzi.
195
194
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze katika kuandika sentensi walizotunga wakitumia tashbihi za kimo
na umbo kwenye chati kwa hati ya mkono. Wanafunzi waandike sentensi hizo
kwa makini.
Waambie wabandike chati zenye sentensi walizotunga ukutani kisha wasome
sentensi kwenye chati.
Waelekeze katika kuandika sentensi zenye tashbihi za kimo na umbo kwenye
tarakilishi. Waambie wazisambaze kwa wenzao kupitia kwa mtandao ili
wazisome.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi ya nyumbani. Waambie
wakika nyumbani watazame vitu halisi na watu nyumbani. Watunge sentensi
wakitumia tashbihi zinazohusiana na wanyama na vitu vya nyumbani.
Kusoma
Kusoma kwa mapana
Matini ya kidijitali
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 145
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua na kuzingatia hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya
kidijitali.
2. Kutambua na kufungua faili iliyo na kifungu cha kusoma kwenye tarakilishi.
3. Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata vifungu vya kusoma vyenye
mada lengwa.
4. Kusoma matini ili kupata ujumbe.
Maswali dadisi
1. Je, ni matini gani umewahi kusoma kutoka kwa mtandao?
2. Utafanyaje ukipata mtu usiyemjua amekutumia ujumbe mtandaoni?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua na kuzingatia hatua za kiusalama kutoka kwenye tarakilishi au mitandao.
Kutambua jina la faili kuhusu kukabiliana na uhalifu, kuifunga na kuifungua.
Kueleza umuhimu wa kutoa habari kwa mwalimu, mzazi au mlezi endapo
atapata ujumbe kutoka kwa mtu asiyemjua mtandaoni.
195
194
Kimeidhinishwa na KICD
Kutafuta maana za maneno kwenye kamusi mitandaoni.
Kusoma matini kwenye tovuti salama.
Kusikiliza matamshi ya maneno na maelezo mtandaoni.
Kutoa muhtasari wa matini aliyosoma na kujibu maswali kimaandishi au
kimazungumzo.
Nyenzo
Tarakilishi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 145
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne na uwaongoze katika
kutafuta matini kwenye mtandao. Waambie wasakure maneno kama
vile uhalifu’, ‘kukabiliana na uhalifu’, ‘kukabiliana na wawindaji haramu,
‘kukabiliana na ukataji miti’ au ‘kukabiliana na dawa za kulevya.
Wakumbushe wanafunzi kusakura tovuti salama.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma matini waliyopata kwenye mtandao.
Waambie watambue tovuti ambapo makala hayo hupatikana.
Waongoze katika kueleza kwa muhtasari habari waliyosoma inahusu nini.
Inaweza kuwa kuhusu kukabiliana na dawa za kulevya, kupambana na wakora
wa kimitandao, kukabiliana na wawindaji haramu, kukabiliana na ukataji miti
au kukabiliana na utoaji na upokeaji rushwa.
Waelekeze katika kutambua msamiati wa uhalifu kwenye matini waliyosoma.
Msamiati unaweza kuwa:
ü uhalifu
ü usalama
ü mtandao
ü mshukiwa
ü shahidi
ü jela
ü kortini
ü jaji
ü askari
ü sheria
Waongoze wanafunzi katika kutafuta maana ya maneno hayo na mengine
kwenye kamusi.
Waelekeze wanafunzi ili waweze kukiri kwa kina. Waongoze katika kutoa
mapendekezo ya njia zinazoweza kutumiwa kukabiliana na uhalifu. Baadhi ya
majibu yanayotarajiwa ni:
ü Kuwahamasisha watu kuhusu athari za uhalifu.
ü Utekelezaji wa sheria.
ü Kufunza watu kuwa na maadili.
ü Kutoa adhabu kali kwa wahalifu.
197
196
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Wakiwa nyumbani,
wanaweza kusakura kwenye mtandao matini kuhusu usalama wa kidijitali. Waambie
wasome matini hayo kwenye tovuti na kuwatolea wenzao nje ya darasa muhtasari wa
matini yenyewe.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa145-146
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua na kuzingatia hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya kidijitali.
2. Kusoma matini ili kupata ujumbe.
3. Kueleza muhtasari wa matini aliyosoma.
4. Kujibu maswali yanayotokana na matini waliyosoma.
Maswali dadisi
1. Je, usalama wa kidijitali unahusu nini?
2. Utafanyaje ukipata mtu usiyemjua amekutumia ujumbe mtandaoni?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma matini lengwa.
Kujibu maswali yanayotokana na matini waliyosoma.
Kutafuta maana za maneno kwenye kamusi.
Kusikiliza matamshi ya maneno na maelezo.
Kutoa muhtasari wa matini aliyosoma na kujibu maswali kimaandishi au
kimazungumzo.
Nyenzo
Tarakilishi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 145-146
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaongoze katika
kusoma makala yaliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi kwa zamu.
Waelekeze wanafunzi katika kutoa muhtasari wa matini waliyosoma.
Wape wanafunzi fursa ya kujibu maswali kuhusu matini.
197
196
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 146
1. Vyombo vya kidijitali ni kama vile:
(a) Tarakilishi
(b) Vipakatalishi
(ch) Tabuleti
(d) Simu
2. Umuhimu wa vyombo vya kidijitali unahusisha matumizi katika:
(a) Biashara
(b) Sayansi
(ch) Elimu
(d) Teknolojia
(e) Habari
3. Hatua za kiusalama kwenye tarakilishi na mitandao ni:
(a) Usitoe nenosiri kwa watu usiowajua.
(b) Funga faili kwenye tarakilishi.
(c) Fahamisha mzazi, mlezi au mwalimu kuhusu ujumbe kutoka
kwa watu usiowajua.
4. Kadiria maoni ya wanafunzi kuhusu wanachokiria kuhusu kutoa
habari kwa mzazi, mwalimu au mlezi.
5. Tathmini maelezo ya wanafunzi kuhusu maana za maneno
yaliyoorodheshwa kitabuni.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Wakiwa na wenzao
nje ya darasa, watafute maana ya maneno yafuatayo:
ü Teknolojia
ü Blogi
ü Propaganda
ü Benki
ü Kompyuta
Kuandika
Insha ya masimulizi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 147
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo.
2. Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
199
198
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali Dadisi
1. Je, insha ya masimulizi inahusu nini?
2. Unazingatia nini unapoandika insha ya masimulizi?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua insha ya masimulizi.
Kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya masimulizi.
Kushirikiana na wenzake katika kujadili mada ya insha na muundo wa insha
ya masimulizi.
Kuandika insha ya masimulizi kuhusiana na uhalifu.
Kusoma insha ya masimulizi iliyoandikwa.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 147
Tarakilishi
Mtandao wa intaneti
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwaambia wasome insha ya masimulizi
waliyoandika katika mada ya pili.
Waongoze wanafunzi katika kueleza maana ya insha ya masimulizi.
Waelekeze wanafunzi katika kufafanua muundo wa insha ya masimulizi.
Washirikishe wanafunzi katika kusoma mifano ya insha za masimulizi
walizoandika katika mada ya pili.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi watatuwatatu kisha
uwaambie watumie tarakilishi kuingia kwenye intaneti.
Waelekeze katika kusakura video kuhusu uwindaji haramu, ukataji miti
misituni, uchomaji wa makaa na uingizaji wa bidhaa ghushi nchini. Tazameni
video hizo.
Waongoze wanafunzi katika kusimulia kile walichoona kwenye video hizo.
Waambie waandike kile walichosimulia kwenye madaari yao.
Waambie wanafunzi wateue mmoja wao ili aje mbele ya darasa na kuwasomea
wanafunzi wengine kile mlichoandika.
Wanafunzi wengine wasikilize kwa makini mwanafunzi akisoma
kilichoonekana kwenye video na kuandika madaarini.
Waelekeze katika kupiga taipu yale waliyosoma. Waambie wawasambazie
wanafunzi wenzenu kwenye mtandao ili wasome insha hiyo.
199
198
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa insha ya
masimulizi hueleza mambo au matukio fulani.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 147-148
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo na vidokezo vilivyotolewa.
2. Kuchangamkia utunzi wa insha ya masimulizi ili kujenga ubunifu wake.
Maswali dadisi
1. Unazingatia nini unapoandika insha ya masimulizi?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kuandaa vidokezo vya kuandika insha ya masimulizi.
Kuandika insha ya masimulizi kuhusiana kukabiliana na utumiaji wa dawa za
kulevya.
Kusoma insha ya masimulizi
Kusambaza insha ya masimulizi kwenye mtandao.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 147-148
Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wasome insha ya
masimulizi waliyoandika katika kipindi kilichotangulia.
Washirikishe katika kusoma mifano ya insha za masimulizi walizoandika
katika kipindi kilichotangulia.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika insha kuhusu namna ya kukabiliana na
utumiaji wa dawa za kulevya. Fanya hivi kwa kujadili vidokezo katika Kitabu
cha Mwanafunzi. Waambie watumie vidokezo hivyo wakati wa kuandika
insha zao. Waeleze kisa au tukio ambapo mhusika alitumia dawa za kulevya,
akaathiriwa au akawauzia watu kisha akakamatwa na polisi, kushtakiwa,
kuhukumiwa, kutumikia kifungo na kuachiliwa akiwa amerekebisha tabia yake.
Wape wanafunzi fursa ya kuandika insha ya masimulizi kwa kutumia
vidokezo hivyo.
201
200
Kimeidhinishwa na KICD
Waambie wawasomee wenzao kwa sauti insha walizoandika.
Waelekeze katika kusambaza kwenye mtandao insha za masimulizi
walizoandika ili wanafunzi wenzao wazisome. Wanafunzi wazisome na
kuzitathmini.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa nsha ya masimulizi
hueleza mambo au matukio fulani. Masimulizi yanaweza kuwa kisa cha ukweli au kisa
cha kubuni. Wakumbushe kuwa hata kama kisa ni cha ukweli, kidhihirishe ubunifu wa
hali ya juu katika usimulizi.
Saru
Nyakati na Hali
Kipindi cha 1
Wakati uliopita, hali ya kuendelea
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 148-150
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua viambishi vya wakati uliopita hali, ya kuendelea kwenye vitenzi.
2. Kutambua vitenzi katika wakati uliopita, hali ya kuendelea kwenye matini.
3. Kutunga sentensi akitumia vitenzi katika wakati uliopita, hali ya kuendelea.
Maswali dadisi
1. Ni viambishi gani hutumiwa kuwakilisha wakati uliopita, hali ya kuendelea
kwenye vitenzi?
2. Vitenzi hudhihirika vipi katika matini ili kubainisha wakati uliopita hali ya
kuendelea?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue viambishi vinayobainisha wakati uliopita, hali ya kuendelea.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia vitenzi katika wakati uliopita, hali ya
kuendelea.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwenye sentensi kwa kutumia vitenzi katika
wakati uliopita, hali ya kuendelea.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 148-150
Jedwali Tarakilishi
201
200
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje vitenzi wanavyofahamu.
Wataje vitenzi kama soma, lima, cheza na andika.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaambie wasome
maneno na sentensi zilizo kwenye jedwali katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 148.
Waongoze wanafunzi katika kutambua sehemu tatu za jedwali zinaonyesha
nini. Wanafunzi watambue kuwa sehemu ya A ina vitenzi, sehemu B ina
vitenzi katika wakati uliopita na sehemu CH inaonyesha sentensi zenye vitenzi
katika wakati uliopita, hali ya kuendelea, katika umoja na wingi.
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi tano kama zilizo kwenye
jedwali. Tathmini sentensi za wanafunzi huku ukizingatia wakati uliopita, hali
ya kuendelea katika umoja na wingi.
Waongoze wanafunzi katika kusoma maelezo kuhusu nyakati katika Kitabu
cha Mwanafunzi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaelekeze ili
waandike vitenzi kwenye jedwali katika wakati uliopita. Tathmini majibu ya
wanafunzi.
Majibu ya zoezi la 1, ukurasa wa 149-150
Kitenzi Wakati uliopita (umoja- wingi
hukumu alihukumu walihukumu
lia alilia- walilia
lima alilima walilima
zungumza alizungumza-walizungumza
ruka aliruka- waliruka
Wakati uliopita Wakati uliopita: hali ya kuendelea
alisoma - walisoma alikuwa akisoma - walikuwa wakisoma
nilicheka - tulicheka nilikuwa nikicheka - tulikuwa tukicheka
uliingia - mliingia ulikuwa ukiingia - mlikuwa mkiingia
nilipika - tulipika nilikuwa nikipika - tulikuwa tukipika
alilala - walilala alikuwa akilala - walikuwa wakilala
203
202
Kimeidhinishwa na KICD
Wakati uliopita Wakati uliopita: hali ya kuendelea
Maria alikimbia sokoni. Maria alikuwa akikimbia sokoni.
Mgeni alibisha mlangoni. Mgeni alikuwa akibisha mlangoni.
Uji ulitokota sana. Uji ulikuwa ukitokota sana.
Vyombo vilioshwa. Vyombo vilikuwa vikioshwa.
Karani alipiga chapa. Karani alikuwa akipiga chapa.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi kuwa wakati uliopita
huonyesha kwamba kitendo kilitendeka kabla ya kutolewa kwa kauli. Wakati uliopita
hutambulishwa kwa kutumia kiambishi -li-. Hali ya kuendelea huonyeshwa kwa
kiambishi -ki- pamoja na neno -likuwa.
Kipindi cha 2
Wakati uliopo, hali ya kuendelea
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 150-152
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua viambishi vya wakati uliopo, hali ya kuendelea kwenye vitenzi.
2. Kutambua vitenzi katika wakati uliopo, hali ya kuendelea kwenye matini.
3. Kutunga sentensi akitumia vitenzi katika wakati uliopo, hali ya kuendelea.
Maswali dadisi
1. Ni viambishi gani hutumiwa kuwakilisha wakati uliopo, hali ya kuendelea
kwenye vitenzi?
2. Vitenzi hudhihirika vipi katika matini kubainisha wakati uliopo, hali ya
kuendelea?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue viambishi vinavyobainisha wakati uliopo, hali ya
kuendelea.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia vitenzi katika wakati uliopo, hali ya
kuendelea.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwenye sentensi kwa kutumia vitenzi katika
wakati uliopo, hali ya kuendelea.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 150-152
Jedwali Tarakilishi
203
202
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje vitenzi wanavyofahamu.
Hakikisha kuwa wanataja vitenzi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu. Waambie wasome
maneno na sentensi zilizo kwenye jedwali katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waongoze wanafunzi katika kutambua vitendo katika jedwali vilifanyika
lini. Wanafunzi watambue kuwa vitendo ni vya wakati uliopo kwa sababu ya
kiambishi na.
Waambie wanafunzi wasome maelezo kuhusu wakati uliopo katika Kitabu cha
Mwanafunzi.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaelekeze katika
kukamilisha jedwali katika wakati uliopo. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 151
Kitenzi Wakati uliopo (Umoja- Wingi)
1. sema anasema - wanasema
2. haribu anaharibu- wanaharibu
3. eneza anaeneza-wanaeneza
4. imba anaimba-wanaimba
5. inama anainama-wanainama
Wakati uliopo Wakati uliopo: hali ya kuendelea
1. Maria anaketi kwenye kivuli. Maria anaketi kwenye kivuli.
2. Wewe unacheza sana. Wewe unacheza sana.
3. Nani anazungumza leo? Nani anazungumza leo?
4. Mchezaji anainua gunia. Mchezaji anainua gunia.
5. Jaji anamhukumu mshatakiwa. Jaji anamhukumu mshtakiwa.
Waongoze wanafunzi katika kutambua kuwa wakati uliopo, hali ya kuendelea
huonyesha kuwa kitendo kinaendelea katika wakati uliopo.
Wape wanafunzi kazi mradi. Waambie watunge sentensi wakitumia vitenzi
walivyopewa kuonyesha wakati uliopo, hali ya kuendelea. Wanafunzi
waandike sentensi hizo. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Waongoze wanafunzi katika kuandika sentensi walizotunga kwenye tarakilishi
na uwaambie wasambaze sentensi hizo kwa wenzao kupitia mtandao.
205
204
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi kuzitathmini sentensi walizosambaziwa. Tathmini
maoni ya wanafunzi.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaeleza wanafunzi kuwa wakati uliopo huonyesha
kwamba kitendo kinatendeka wakati wa kutoa kauli. Wakati uliopo hutambulishwa
kwa kutumia kiambishi -na-. Wape wanafunzi kazi ya nyumbani. Watunge sentensi
wakitumia vitenzi hivi:
(a) anasoma
(b) wanafunga
(ch) analima
(d) wanasakura
(e) wanakula
Kipindi cha 3
Wakati ujao, hali ya kuendelea
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 152-152
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua viambishi vya wakati ujao, hali ya kuendelea kwenye vitenzi.
2. Kutambua vitenzi katika wakati ujao, hali ya kuendelea kwenye matini.
3. Kutunga sentensi akitumia vitenzi katika wakati ujao, hali ya kuendelea.
Maswali dadisi
1. Ni viambishi gani hutumiwa kuwakilisha wakati ujao hali ya kuendelea kwenye
vitenzi?
2. Vitenzi hudhihirika vipi katika matini kubainisha wakati ujao hali ya kuendelea?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue viambishi vinavyobainisha wakati ujao, hali ya
kuendelea.
Mwanafunzi atunge sentensi akitumia vitenzi katika wakati ujao, hali ya
kuendelea.
Mwanafunzi aandike upya sentensi katika wakati mmoja. Ziwe katika wakati
ujao, hali ya kuendelea.
Mwanafunzi ajaze mapengo kwenye sentensi kwa kutumia vitenzi katika
wakati ujao, hali ya kuendelea.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 152-153
Jedwali Tarakilishi
205
204
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje vitenzi katika nyakati
wanazofahamu.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili na uwaambie wasome
maneno na sentensi zilizo kwenye jedwali katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 152.
Waongoze wanafunzi katika kutambua vitendo katika jedwali vilifanyika lini.
Wanafunzi watambue ikiwa vilifanyika wakati ujao, kwa sababu ya kiambishi ta.
Waambie wanafunzi wasome maelezo kuhusu wakati ujao katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 153.
Wanafunzi wakiwa wangali katika vikundi vyao vya wawiliwawili, waelekeze
katika kuandika sentensi kwa kukamilisha jedwali katika wakati ujao, hali ya
kuendelea.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa wa 153
Wakati ujao Wakati ujao, hali ya kuendelea
1. Musa atasimulia hadithi. Musa atakuwa akisimulia hadithi.
2. Watoto wataimba wimbo wa
taifa jioni.
Watoto watakuwa wakiimba wimbo
wa taifa jioni.
3. Mimi nitasakura kwenye
mtandao.
Mimi nitakuwa nikisakura kwenye
mtandao.
4. Yeye atakusanya habari hizo. Yeye atakuwa akikusanya habari hizo.
5. Fundi atarekebisha
tarakilishi.
Fundi atakuwa akirekebisha
tarakilishi.
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia vitenzi kuonyesha
wakati ujao, hali ya kuendelea. Tathmini sentensi za wanafunzi.
Waongoze wanafunzi katika kuandika upya sentensi kutoka wakati uliopita
hadi wakati ujao, hali ya kuendelea.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi kuwa wakati ujao, hali ya
kuendelea huonyesha kwamba kitendo kitakuwa kikiendelea wakati ujao. Viambishi
-takuwa na -ki- hutumika.
207
206
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Hakikisha umeandaa nyenzo mwafaka ili kufanikisha shughuli ya ufunzaji na ujifunzaji
wa sehemu hii. Unaweza kutumia nyenzo zifuatazo:
Vifaa halisi kama vile: noti na sarafu
Vyombo vya kidijitali kama vile: tarakilishi, vipakatalishi, tabuleti, rununu na
projekta
Kinasasauti
Mtandao
Tovuti
Picha
Michoro
Chati
Kadi maneno
Video
Kamusi
Mgeni mwalikwa
Maswali dadisi
Katika sehemu hii, maswali dadisi yafuatayo yatamwongoza mwanafunzi:
1. Je, unazingatia nini unapotoa masimulizi?
Utangulizi
Mapato ni kitu kinachopatikana kutokana na biashara au kazi fulani. Watu wanaweza
kupata mapato kutokana na njia mbalimbali kama vile: biashara, ajira au kujiajiri.
Sehemu hii inalenga kumpa mwanafunzi uwezo wa:
1. Kusimulia tungo kwa kuzingatia mada, ubunifu na usanifu wa lugha mbele ya
wenzake.
2. Kusoma kifungu kwa ufasaha ili kuimarisha ufahamu.
3. Kuandika barua ya kiraki kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
4. Kukanusha maneno na sentensi kwa kuzingatia nafsi na wakati katika
mawasiliano.
5. Kutumia nomino katika hali ya ukubwa na udogo kwenye sentensi.
MAPATO
11
207
206
Kimeidhinishwa na KICD
2. Je, unafahamu shughuli gani za kujipatia mapato?
3. Unafahamu viambishi gani vya nafsi?
4. Unaweza kutaja ukubwa wa nomino gani?
5. Ni nomino zipi unazoweza kutaja udogo wake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mada ya Mapato inakuza umilisi wa kimsingi. Baadhi ya umilisi huo ni:
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wafanye mazoezi na shughuli mbalimbali kwa ushirikiano katika vikundi
kama vile: kusoma kwa zamu kifungu au kusoma makala kwa pamoja. Mijadala
baina ya wanafunzi kuhusu mapato itaimarisha mawasiliano na kukuza ushirikiano.
Mawasiliano yatatimizwa wanafunzi wakisambaza habari kuhusu mapato mbalimbali
kwenye mitandao wakitumia vyombo vya kidijitali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi wa kidijitali unanuia kumsaidia mwanafunzi kutumia vyombo vya kidijitali
kuwasiliana na kujifunza. Mwalimu anapaswa kushirikisha matumizi ya tarakilishi,
kipakatalishi, video, tabuleti, projekta, intaneti, mitandao na tovuti ili mwanafunzi
ajifunze njia za kupata mapato.
(ch) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu utasaidia mwanafunzi kuwa na kichocheo cha kutaka kujua mengi kuhusu
mapato. Umilisi huu utampa mwanafunzi hamu ya kufahamu njia za kupata mapato.
Pia, atafakari maswali ya ziada kuhusu mapato. Mwanafunzi anaweza kuwa na hamu
ya kutaka kutumia vyombo vya kidijitali ili atafute habari zaidi kuhusu mapato na
ukanushaji.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unapaswa kukuzwa kupitia kuandika sentensi za mapato kwa kutumia
tarakilishi, tabuleti au simu ya mkononi. Pia, ubunifu ukuzwe na kuimarishwa kupitia
kusakura mitandao ili kutafuta habari zaidi kuhusu mapato. Ubunifu utadhihirika
mwanafunzi akiandika barua ya kiraki.
(e) Kujiamini
Umilisi huu unakuzwa kupitia mwanafunzi kusimama mbele ya wanafunzi wenzake
darasani na kutaja au kutoa maelezo kuhusu mapato. Pia, kujiamini kunakuzwa kupitia
mwanafunzi kutunga sentensi akitumia ukubwa na udogo wa nomino.
209
208
Kimeidhinishwa na KICD
(f) Kukiria kwa kina na kutatua changamoto
Umilisi huu unakuzwa kupitia kumpa mwanafunzi swali la kutafakari, kukiria na
kutafuta jawabu lake ambalo halimo kwenye matini. Kwa mfano, mwanafunzi anawezaje
kuanzisha mradi wa kufuga sungura?
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Kujitambua na kujithamini kupitia kutunga sentensi akitumia ukubwa na
udogo wa nomino.
(b) Ujuzi wa matumizi ya fedha kupitia kusimulia kuhusu mapato.
(ch) Stadi za maisha zitakuzwa kwa mwanafunzi kujieleza, kushiriki katika
shughuli za vikundi, kuchangia katika mijadala na kuwapa wanafunzi
ushauri kuhusu jinsi ya kujipatia mapato.
(d) Uraia utakuzwa kupitia kufanya kazi pamoja, ujuzi wa matumizi ya
fedha mwanafunzi anapotumia msamiati wa mapato na kutunga sentensi
zinazolenga uraia mwema.
Uhusiano na maadili
Mada ya mapato inakuza maadili yafuatayo:
Uwajibikaji kupitia kukamilisha shughuli fulani za ujifunzaji.
Heshima, upendo na adabu hasa katika shughuli za vikundi na uandishi wa
barua ya kiraki.
Ushirikiano kupitia kufanya kazi za vikundi.
Shughuli za huduma za kijamii
Kuendeleza mawasiliano na wenzake pamoja na wazazi kwa kutumia barua ya
kiraki.
Kuwahamasisha wenzake nyumbani na shuleni kuhusu njia za kupata mapato
kupitia kwa masimulizi.
Kuwa kielelezo cha kutumia lugha kwa ufasaha shuleni na nyumbanni ili
kufaulisha mawasiliano.
Kuwasaidia wasijioweza katika jamii kutokana na faida uliyopata katika
biashara.
Kushiriki katika kutunza kuku, sungura au ndege wengine wa nyumbani ili
kujipatia mapato.
Kuwa mwanachama wa chama cha mazingira ili kunadhisha soko.
209
208
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
Mada hii inaingiliana na masomo mengine kama vile:
1. Science and Technology activities inahimiza matumizi ya tarakilishi.
2. English Activities: inashughulikia ufasaha wa kusema kwa ubunifu kupitia
masimulizi ili kukuza stadi ya kusikiliza na kuzungumza. Pia uandishi wa barua
unafunzwa katika somo hili.
3. Indigenous Language Activities: inashughulikia masimulizi kukuza stadi ya
kusikiliza na kuzungumza. Stadi za kusoma na kuandika hufunzwa katika
Indigenous Language Activities. Saru pia hufundishwa.
Mapendekezo ya mbinu za kutathmini
Tathmini inaweza kufanywa kwa:
Kuhakiki jinsi wanafunzi wanavyosoma ukubwa na udogo wa nomino.
Kusikiliza na kutazama namna wanafunzi wanatoa masimulizi kwa kutumia
viziada lugha.
Kuchunguza jinsi wanafunzi wanavyotumia msamiati wa mapato katika
mawasiliano.
Kuhakiki jinsi wanafunzi wanavyoandika barua ya kiraki. Wazingatie
ujumbe, muundo na mtindo wa kuandika barua ya kiraki.
Kusikiliza majadiliano ya wanafunzi kuhusu njia za kujipatia mapato.
Kuchanganua namna wanavyojibu maswali kutokana na kifungu walichosoma
kuhusu wa mapato.
Kuhakiki namna wanafunzi wanavyotamka maneno wakijieleza.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu
Unaweza kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kupitia mikakati
ifuatayo:
Kwa wanafunzi wenye matatizo ya kusikia na kuzungumza, unaweza kumwalika mfasiri
wa lugha ishara ili awasaidie wanafunzi hao katika kushiriki kwenye somo kikamilifu. Pia,
unaweza ukatumia vifaa vya kiteknolojia kama vile: projekta ili kuwaonyesha wanafunzi
baadhi ya picha zinazohusu nyumbani kutoka mtandaoni. Ili kuwahusisha wanafunzi
wenye matatizo katika baadhi ya viungo vyao vya mwili kama vile, miguu na mikono,
hakikisha kuwa wakati wa kuigiza wanafunzi hawa wameangaliwa ili wasijiumize au
kuumizwa kwenye viungo vilivyoathirika.
Utangulizi
Waelekeze wanafunzi katika kutazama mchoro kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 154. Waongoze katika kutambua mchoro huo
unahusu nini.Wanaweza kutambua kuwa ni duka la kisasa lenye bidhaa tele.
211
210
Kimeidhinishwa na KICD
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya wanafunzi wengine darasani
na kuwaambia anachoona kwenye mchoro. Muulize iwapo amewahi kuwa
mahali kama hapo na alichokuwa akifanya hapo. Mwanafunzi ajibu huku
wengine wakisikiliza.
Kusikiliza na Kuzungumza
Kuzungumza na kujieleza kwa ufasaha
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 154-155
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi mwanafunzi aweze:
1. Kusimulia tungo kwa kuzingatia mada, ubunifu na usanifu wa lugha mbele ya
wenzake.
2. Kutumia ishara zifaazo ili kuimarisha masimulizi yake
Maswali dadisi
1. Unazingatia nini unapotoa masimulizi kwa hadhira?
2. Ni ishara zipi za mwili zinazotumiwa wakati wa kutoa masimulizi?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atazame michoro.
Mwanafunzi ajadiliane na wenzake kuhusu michoro.
Mwanafunzi asimulie masimulizi kuhusu michoro.
Mwanafunzi atumie ishara za mwili kutoa masimulizi.
Mwanafunzi ashirikishwe katika mjadala kuhusu umuhimu wa biashara.
Mwanafunzi atazame, aigize na kujibu maswali.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 154-155
Picha
Video ya wauzaji
Rununu au tarakilishi
Kanda za sauti
211
210
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuingia darasani na bidhaa mbalimbali za duka na
kuwauliza wanafunzi maswali kuhusu bidhaa hizo.
Waelekeze wanafunzi katika mchoro ulio kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 155.
Waonyeshe video ya watu katika miktadha ya biashara.
Wape wanafunzi fursa ya kusikiliza masimulizi. Hakikisha kuwa umerekodi
masimulizi haya kwa kutumia rekonda au rununu. Washughulikie wanafunzi
wenye mahitaji maalum kama vile wasio na uwezo wa kusikia kwa kumwalika
mtaalamu wa lugha ishara atakayetafsiri sauti ya masimulizi.
Masimulizi:
Biashara ni njia moja ya kujipatia mapato. Kuna biashara za aina nyingi. Biashara
inaweza kuwa ya kibinafsi, kikundi, jamaa au ya kitaifa. Mtu anayefanya biashara
huitwa mfanyabiashara. Ili kupata mapato, mfanyabiashara hujitahidi sana. Anaweza
akawaajiri wafanyakazi wengi ili wamsaidie katika kuendeleza biashara yake. Pia,
wafanyabiashara wengine hutumia mashini za kiteknolojia ili kurahisisha kazi zao. Baada
ya kufanya biashara, mfanyabiashara hufanya hesabu ya mapato yake. Ni kutokana
na mapato haya ndipo mfanyabiashara atawalipa wafanyakazi wake. Mapato hayo
pia hutumika katika kuendeleza biashara na kuendesha shughuli za biashara. Shughuli
za biashara ni kama vile: kukarabati vifaa vya biashara, kufanya malipo mbalimbali
na pia kuweka akiba kwenye akaunti ili kupata mtaji. Baada ya kufanya hesabu hizi
zote, mfanyabiashara hupata faida yake. Tunaweza kujipatia mapato kupitia kilimo,
biashara, utalii au uchimbaji madini.
Wagawe wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasimuliane
walichosikia kwenye masimulizi.
Wape wanafunzi fursa ya kujadiliana umuhimu wa masimulizi waliyosikiliza.
Sharti wanafunzi waweze kutambua kuwa masimulizi hayo yanatoa elimu
ya ziada kuhusu kujiendeleza kiuchumi. Pia, masimulizi hayo yanawahimiza
kuwa wenye bidii maishani ili kuwa na mapato.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwaambia wazungumze na wauzaji jioni warudipo
nyumbani ili wajue namna ambavyo watu hao hupata na kutumia mapato yao.
Hakikisha kuwa umetathmini jinsi ambavyo wanafunzi walishiriki katika shughuli ya
kuzungumza na wauzaji watakaporudi shuleni.
213
212
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 155-156
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kusimulia tungo kwa kuzingatia mada, ubunifu na usanifu wa lugha mbele ya
wenzake.
2. Kutumia ishara zifaazo ili kuimarisha masimulizi yake.
3. Kuchangamkia masimulizi katika mazingira mbalimbali.
4. Kubuni masimulizi yanayohusiana na mada.
Maswali dadisi
1. Unazingatia nini unapotoa masimulizi kwa hadhira?
2. Ni ishara zipi za mwili zinazotumiwa wakati wa kusimulia?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atazame michoro.
Mwanafunzi ajadiliane na wenzake kuhusu michoro.
Mwanafunzi asimulie kuhusu michoro.
Mwanafunzi atumie ishara za mwili kutoa masimulizi.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 155-156
Rununu
Michoro
Tarakilishi
Kanda ya sauti
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwapanga wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu
na uwaambie watazame michoro iliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 155-156. Waelekeze katika kutambua watu kwenye michoro hiyo
hufanya kazi gani. Sharti wanafunzi waweze kutambua kuwa: daktari hutibu
wagonjwa, mchezaji hucheza kandanda, rubani huendesha ndege, mwalimu
hufunza na mpishi hupika.
Waongoze wanafunzi katika kueleza watu hao hupewa nini baada ya kazi ili
kujipatia mapato. Wanaweza kujibu kwa kusema mshahara au aina ya malipo
yoyote mwafaka.
Waelekeze katika kujadili wangependa kufanya kazi gani wakikamilisha
masomo yao. Wape nafasi ya kujadili ni kwa nini wanapenda kazi hizo.
213
212
Kimeidhinishwa na KICD
Teua mwanafunzi mmoja ake mbele ya wanafunzi wengine darasani.
Mwambie awasimulie wengine ni kwa nini anapenda kazi fulani
Waelekeze wanafunzi katika kutumia lugha kwa ufasaha. Waambie watumie
ishara za mwili kama mikono, uso, mabega na macho ili kueleza shughuli ya
upishi.
Waambie wanafunzi waandike majibu ya maswali ya kazi wanayoipenda
kwenye daari.
Waongoze wanafunzi katika kusoma majibu yaliyoandikwa. Teua mwanafunzi
mmoja ili aje mbele awasomee huku wanafunzi wengine wakisikiliza.
Waelekeze katika kuandika majina hayo kwenye chati na kuzitundika ukutani
ili wazisome baadaye.
Unaweza kuwaambia waandike majibu yao kwenye tarakilishi kisha
wawasambazie wenzao kwenye mtandao.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wakiwa nyumbani, watoe
masimulizi kwa wazazi au walezi wao kuhusu yale yaliyofanyika shuleni siku hiyo.
Kusoma
Ufahamu
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 157-158
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi mwanafunzi aweze:
1. Kusoma kifungu kwa ufasaha ili kuimarisha ufahamu.
2. Kujibu maswali kutokana na kifungu.
3. Kutambua msamiati wa mapato uliotumika katika hadithi ili kuimarisha
ufahamu.
4. Kutumia msamiati wa mapato kwa usahihi katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Unafahamu shughuli gani za kujipatia mapato?
2. Unakiri ni kwa nini mapato ni muhimu?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma kifungu.
215
214
Kimeidhinishwa na KICD
Kutoa muhtasari wa kifungu.
Kutambua msamiati wa mapato.
Kushiriki katika vikundi kujadili umuhimu wa mapato.
Kuigiza matukio kuhusu mapato.
Kutazama vibonzo katika shughuli za mapato kwenye tarakilishi
Kuuliza na kujibu maswali kuhusu mapato
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 157-158
Michoro Video Kamusi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuteua mwanafunzi mmoja ili aje mbele ya darasa na
kutaja aina za biashara anazofahamu.
Wagawe wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaambie wasome
kifungu kwa zamu.
Wateue wanafunzi wawili waje mbele ya darasa. Waambie wawaeleze wenzao
biashara zifanyikazo katika soko lao.
Waongoze wanafunzi katika kutazama video iliyo na watu wakifanya aina
mbalimbali za biashara. Unaweza ukatafuta video za: kuuza mboga, kuuza
kuku, kuuza mavazi na kuuza matunda.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua methali iliyotumika katika kifungu.
Methali hiyo ni: kinolewacho hupata.
Waongoze katika kutafuta maana ya maneno katika kamusi na kutunga
sentensi wakitumia maneno hayo.
Majibu
Majibu ya zoezi la 1, ukurasa wa 158
1. Mfanyabiashara na nesi
2. Akiba ya mshahara wake
3. Kufanya utati wa soko, kuzingatia mahitaji ya kufanya biashara na
kuweka mikakati ya usambazaji na mauzo.
4. Kinolewacho hupata.
5. Tathmini majibu ya wanafunzi kuhusu maana za maneno.
Hitimisho: kamilisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie wajadili
kuhusu umuhimu wa mapato wakiwa wawiliwawili.
215
214
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 158-160
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kusoma kifungu kwa ufasaha ili kuimarisha ufahamu.
2. Kujibu maswali kutokana na kifungu cha Pato Apata Mapato
3. Kutambua msamiati wa mapato uliotumika katika hadithi ili kuimarisha
ufahamu.
4. Kutumia msamiati wa mapato kwa usahihi katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Je, unajua shughuli zipi za kujipatia mapato?
2. Ni kwa nini mapato ni muhimu?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kusoma kifungu.
Kutoa muhtasari wa kifungu.
Kutambua msamiati wa mapato.
Kushiriki katika vikundi kujadili umuhimu wa mapato.
Kuigiza matukio kuhusu mapato.
Kutazama vibonzo katika shughuli za mapato kwenye tarakilishi.
Kuuliza na kujibu maswali kuhusu mapato.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 158-160
Tarakilishi
Mchoro
Vibonzo
Video
Rekoda au simu
Maandalizi ya mwalimu
Soma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa158-160.
Soma matini kabla ya uwasilishaji darasani.
Tafuta video ya vibonzo kuhusu shughuli za kujipatia mapato.
Tafuta tarakilishi, rekoda na simu.
217
216
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wasome kifungu kilicho katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 158-159 kimoyomoyo.
Waongoze wanafunzi katika kutoa muhtasari wa kifungu hicho kwa kueleza
kinahusu nini.
Waelekeze wanafunzi kutambua msamiati wa mapato uliotumika katika
kifungu hicho. Msamiati huo ni:
ü mtaji
ü kuanzisha
mradi
ü pesa
ü kununua
ü kuuza
ü faida
ü mauzo
ü mapato
ü akiba
ü biashara
ü riziki
ü kuwekeza
ü wateja
Waongoze katika kutunga sentensi wakitumia msamiati wa mapato
waliotambua.Waelekeze ili waweze kufahamu Pato alipata mapato kupitia
shughuli gani.
Waongoze wanafunzi katika kudadisi na kutafakari kuhusu shughuli
zinazoweza kumsaidia mtu kupata mapato. Kubali hoja yoyote mwafaka ya
wanafunzi wako.
Waelekeze wanafunzi katika kutazama video ya vibonzo kuhusu shughuli za
kujipatia mapato.
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya wanafunzi wenzake darasani
kisha awaeleze kuhusu yale aliyotazama kwenye video ya vibonzo.
Waongoze wanafunzi katika kujadili video ya vibonzo shughuli za kujipatia
mapato zilizo kwenye video hiyo.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika msamiati wa mapato waliosikia kwenye
video.
Waweke wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu kisha uwaambie waigize
yaliyotazama kwenye video.
Waongoze wanafunzi kutafuta msamiati wa mapato kwenye mraba. Maneno
hayo ni:
1. Nunua
2. Wekeza
3. Uza
4. Malipo
5. Mauzo
6. Mteja
7. Faida
8. Akiba
9. Mtaji
10. Bidhaa
11. Leseni
12. riziki
Waelekeze wanafunzi ili waandike msamiati huo kwenye tarakilishi au chati.
217
216
Kimeidhinishwa na KICD
Waambie waweke chati zenye maneno hayo kwenye ukuta na wasome
maneno yaliyo kwenye chati hizo baadaye.
Baada ya kuandika msamiati kwenye tarakilishi, waongoze wanafunzi ili
wawasambazie wenzao msamiati huo kwenye mtandao wa intaneti. Wasome
msamiati huo wa mapato kwenye mtandao wa intaneti.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi. Waambie watembelee
mtaa, kijiji au mji ulio karibu na shule yao na watazame na wanakili shughuli za
kujipatia mapato zinazoendeshwa na watu katika mtaa, kijiji au mji huo.
Kuandika
Barua ya kiraki
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 161
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia muundo wake.
2. Kusoma mfano wa barua ya kiraki.
3. Kuchangamkia umuhimu wa barua katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
2. Unakiri barua za kiraki zina umuhimu gani katika mawasiliano?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue sehemu za kimuundo za barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandae vidokezo vya kumwongoza kuandika barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki kwa muundo na mtindo ufaao.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki kwenye daari na mtandaoni na
kuisambaza kwa wenzake.
Mwanafunzi awasomee wenzake barua ya kiraki.
Mwanafunzi ajadili na wenzake umuhimu wa barua ya kiraki katika
mawasiliano.
219
218
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 162
Insha za barua ya kiraki
Tarakilishi
Kanda za sauti kuhusu insha ya barua
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi maswali machache
kuhusu barua ya kiraki.
Waongoze wanafunzi katika kujikumbusha mambo muhimu kuhusu barua ya
kiraki.
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya wanafunzi wenzake
darasani kisha awakumbushe wanafunzi wengine kuhusu barua ya kiraki.
Mwanafunzi azingatie vidokezo katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waongoze wanafunzi katika kuandika vidokezo vya barua. Waelekeze
katika kufanya zoezi la 1. Wanafunzi waandike barua kwa mzazi au mlezi
wakimweleza jinsi ya kupata mapato kupitia ufugaji wa wanyama wa
nyumbani kama sungura. Waelekeze katika kuandika vidokezo kwanza kabla
ya kuandika insha.
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya wanafunzi wenzake darasani
kisha awasomee barua ya kiraki aliyoandika. Wanafunzi wengine wasikilize
na kuitathmini insha hiyo.
Waelekeze wanafunzi katika kuandika barua ya kiraki kwenye tarakilishi na
kuihifadhi. Waambie waisambaze barua hiyo kwa wanafunzi wenzao kupitia
mtandao wa intaneti.
Waambie wanafunzi wasome barua za wenzao kwenye mtandao.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje sehemu
kuu za barua ya kiraki.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 162-163
Matokeo maalum yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia muundo wake.
2. Kuandika barua ya kiraki akizingatia mada na kanuni zifaazo.
219
218
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
2. Unakiri barua za kiraki zina umuhimu gani katika mawasiliano?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Mwanafunzi atambue sehemu za kimuundo za barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandae vidokezo vya kuandika barua ya kiraki.
Mwanafunzi aandike barua ya kiraki kwa muundo na mtindo ufaao.
Mwanafunzi ajadili na wanafunzi wenzake mada ya barua ya kiraki.
Mwanafunzi atumie msamiati wa mapato katika barua ya kiraki.
Mwanafunzi awasomee wenzake barua ya kiraki.
Wanafunzi wajadili umuhimu wa barua za kiraki katika mawasiliano.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 162-163
Tarakilishi
Barua ya kiraki halisi
Bahasha
Stempu
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje sehemu kuu za barua ya
kiraki. Wanafunzi wataje sehemu hizi kisha uwaulize sehemu hizo zinahusu
nini. Waulize wanafunzi barua huwekwa wapi iwapo inatumwa kwa njia ya
posta.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi wawiliwawili. Waambie
wasome mfano wa barua ya kiraki ulio katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 162 kisha uwaongoze kutambua sehemu za barua ya kiraki.
Waelekeze ili wajadili barua hiyo inahusu nini.
Waongoze wanafunzi katika kusoma mambo muhimu kuhusu barua ya
kiraki. Wape nafasi ili wajadili hoja hizo wakirejelea mfano wa barua ya
kiraki waliosoma.
Waulize wanafunzi iwapo wanakiri barua ya kiraki ina umuhimu wowote.
Waelekeze katika kujadili umuhimu wa barua ya kiraki katika mawasiliano.
Kubali hoja zozote muhimu za wanafunzi. Wanaweza kuzingatia hoja kama
vile:
ü Watu kujuliana hali
ü Kuliwazana
ü Kupongezana
ü Kufahamishana mambo
221
220
Kimeidhinishwa na KICD
ü Kuelezana jambo
ü Kuomba msamaha
ü Kualikana kwenye sherehe
Waambie wanafunzi wajifanye babake Adava na wajibu barua ya Adave.
Waongoze katika kuandaa vidokezo mwafaka kwa barua hiyo. Waandike
barua kwenye madaari yao.
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya wengine darasani na
kuwasomea barua aliyoandika. Wanafunzi wenzake wampongeze.
Waelekeze wanafunzi kupiga taipu barua waliyoandika kwenye tarakilishi.
Waambie waisambaze kwa wenzao kupitia mtandao wa intaneti. Waelekeze
wanafunzi kuisoma barua hiyo na waitathmini.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa kazi mradi au shughuli ya kufanya nje ya
darsasa ya kujadili umuhimu wa barua ya kiraki katika mawasiliano.
Saru
Ukanushaji wa maneno na sentensi
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 163-165
Ukanusho wa maneno na sentensi katika nafsi ya kwanza
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya ukanushaji ili kuubainisha.
2. Kutambua maneno yaliyokanushwa katika nafsi ya kwanza kwenye kundi la maneno.
3. Kutambua viambishi vya nafsi ya kwanza na wakati katika maneno na sentensi.
4. Kukanusha maneno na sentensi kwa kuzingatia nafsi ya kwanza na wakati katika
mawasiliano.
Maswali Dadisi
1. Unafahamu viambishi gani vya nafsi?
2. Unajua viambishi gani vya wakati?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kueleza maana ya ukanushaji.
Kutambua maneno yaliyokanushwa katika nafsi ya kwanza.
221
220
Kimeidhinishwa na KICD
Kutambua viambishi vya nafsi ya kwanza na wakati katika maneno na
sentensi.
Kukanusha maneno na sentensi akizingatia nafsi ya kwanza na nyakati.
Kusikiliza vipindi vya ukanushaji kwenye kanda zilizorekodiwa.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 163-165
Majedwali
Chati
Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya vitenzi.
Tathmini majibu ya wanafunzi ili kuhakikisha kuwa wanataja vitenzi pekee.
Waelekeze wanafunzi katika kutambua kuwa kukanusha ni kukataa.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaelekeze
katika kusoma maneno kwenye jedwali. Wanafunzi wasome huku wengine
wakisikiliza.
Waulize wanafunzi walichogundua nini kuhusu maneno hayo. Wanaweza
kusema maneno hayo yamekanushwa.
Waongoze katika kutambua kuwa viambishi vilivyokolezwa rangi ni viambishi
vya kukanusha. Waongoze wanafunzi katika kugundua kuwa maneno katika
nafsi ya kwanza huchukua kiambishi ni katika umoja na tu katika wingi.
Katika kukanusha, viambishi huwa si katika umoja na ha katika wingi.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Waongoze kujitathmini na uwatathmini.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 164
1. Sijanunua
2. Hatujaanza
3. Siuzi
4. Hakukopa
5. Hatupunguzi
6. Sikumaliza
7. Sitakodisha
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasome sentensi
kwenye jedwali. Wanafunzi wasome huku wengine wakiwasikiliza.
Waulize wanafunzi walichogundua kuhusu maneno hayo. Wanaweza kusema
kuwa viambishi vinabadilika kulingana na nafsi na wakati.
223
222
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi katika kutambua kuwa viambishi vilivyokolezwa rangi
ni viambishi vya kukanusha. Waongoze wanafunzi katika kugundua kuwa
sentensi hubadilika wakati wa ukanusho kulingana na nafsi.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi la 2 katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 164. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa wa 164
1. Mimi simalizi kupika.
2. Sisi hatutaanza biashara.
3. Mimi sijasikiliza rekodi.
4. Sisi hatukupewa mkopo.
5. Mimi sijaenda sokoni.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa maneno katika
nafsi ya kwanza huchukua kiambishi ni katika umoja na kiambishi tu katika wingi.
Katika kukanusha viambishi huwa si katika umoja na ha katika wingi.
Kipindi cha 2
Ukanusho wa maneno na sentensi katika nafsi ya pili
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua maneno yaliyokanushwa katika nafsi ya pili katika kundi la maneno.
2. Kutambua viambishi vya nafsi ya pili na wakati katika maneno.
3. Kukanusha maneno kwa kuzingatia nafsi ya pili na wakati katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unafahamu viambishi gani vya nafsi ya pili?
2. Unajua viambishi gani vya wakati?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua maneno yaliyokanushwa.
Kutambua viambishi vya nafsi na wakati katika maneno.
Kukanusha maneno akizingatia nafsi na nyakati.
Kusikiliza vipindi vya ukanushaji.
Nyenzo
223
222
Kimeidhinishwa na KICD
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 165-166
Majedwali Chati Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya maneno katika
nafsi ya pili. Wanafunzi wataje maneno kama vile: unacheka, mtalia, umefagia,
mlipata, utalima, mmenunua na unauza.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya watatuwatatu na uwaelekeze katika
kusoma maneno yaliyo kwenye jedwali. Hakikisha kuwa wanatamka maneno
hayo kwa usahihi.
Waulize wanafunzi walichogundua kuhusu maneno hayo. Wanaweza kusema
maneno hayo yamekanushwa.
Waongoze katika kutambua kuwa viambishi vilivyokolezwa rangi ni viambishi
vya kukanusha. Waongoze wanafunzi katika kugundua kuwa maneno katika
nafsi ya pili huchukua kiambishi u katika umoja na m katika wingi. Katika
kukanusha, viambishi huwa hu katika umoja na ham katika wingi.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi la 3 katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 165. Waongoze katika kujitathmini kisha
uwatathmini.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa wa 165
1. Hujalipa
2. Hamjanunua
3. Huagizi
4. Hamkusarisha
5. Hamharibu
6. Hukuleta
7. Hamtalipa
8. Hakukopa
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne na uwaelekeze katika
kusoma sentensi kwenye jedwali. Wanafunzi wasome huku wengine
wakisikiliza.
Waulize wanafunzi walichogundua kuhusu maneno hayo. Wanaweza kusema
kuwa viambishi vinabadilika kulingana na nafsi na wakati.
Waongoze wanafunzi katika kutambua kuwa viambishi vilivyokolezwa
rangi ni viambishi vya kukanusha. Waambie wanafunzi kuwa kiambishi u
hutumika katika umoja na ukanusho wake ni hu. Katika wingi, kiambishi m
hutumika na hukanushwa na kiambishi ham’.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi la 4 katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 166.
225
224
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 4, ukurasa wa 166
1. Wewe hujaagiza mizigo mingi.
2. Nyinyi hamkukopa pesa nyingi.
3. Wewe hutayarishi risiti.
4. Nyinyi hamtagharamika sana.
5. Nyinyi hamjapata faida.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kiambishi u hutumika
katika umoja na ukanusho wake ni kiambishi hu. Katika wingi, kiambishi m hutumika
na hukanushwa na kiambishi ham’.
Kipindi cha 3
Ukanusho wa maneno na sentensi katika nafsi ya tatu
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua maneno yaliyokanushwa katika nafsi ya tatu katika kundi la maneno.
2. Kutambua viambishi vya nafsi ya tatu na wakati katika maneno.
3. Kukanusha maneno kwa kuzingatia nafsi ya tatu na wakati katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unafahamu viambishi gani vya nafsi ya tatu?
2. Unajua viambishi gani vya wakati?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua maneno yaliyokanushwa.
Kutambua viambishi vya nafsi ya tatu na wakati katika maneno.
Kukanusha maneno akizingatia nafsi na nyakati.
Kusikiliza vipindi vya ukanushaji kutoka kwenye kanda zilizorekodiwa.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 167-169
Majedwali
Chati
Tarakilishi
225
224
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje mifano ya maneno katika
nafsi ya tatu. Wanafunzi wataje maneno kama vile: anacheka, atalia, amefagia,
alipata, atalima, amenunua na anauza.
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili ili wasome maneno
yaliyo kwenye jedwali. Wasome huku wengine wakisikiliza na kuwakosoa
wanapokosea.
Waulize wanafunzi walichogundua kutokana na maneno hayo. Wanaweza
kusema maneno hayo yamekanushwa.
Waongoze katika kutambua kuwa viambishi vilivyokolezwa rangi ni viambishi
vya kukanusha. Waongoze wanafunzi katika kugundua kuwa: katika nafsi
ya tatu: viambishi ni a katika umoja na wa katika wingi. Viambishi hivi
hubadilika na kuwa ha katika umoja na hawa katika wingi wakati wa
kukanusha.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi lililo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 167.
Majibu
Zoezi la 5, ukurasa wa 167
1. Hajakopa
2. Hawajapokea
3. Halipi
4. Hawakuwekeza
5. Hawakununua
6. Hawatapakia
Waelekeze wanafunzi katika kusoma sentensi kwenye jedwali. Mwanafunzi asome
akiwa peke yake huku wengine wakisikiliza.
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya darasa na kuwaambia wenzake
alichogundua kutokana na sentensi hizo. Wanafunzi watambue kuwa: katika
umoja, kiambishi a hutumika na ukanusho wake huwa ni kiambishi ha’.
Katika wingi, kiambishi wa hutumika na hukanushwa kwa kiambishi hawa’.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya zoezi la 6 katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 168.
Majibu
Zoezi la 6, ukurasa wa 168
1. Yeye hajasari leo.
2. Wao hawatatumia kadi kulipa.
3. Yeye hakuajiriwa tena.
4. Wao hawajasarisha bidhaa.
5. Yeye hatafuti kibanda.
227
226
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi katika kusakura mtandao ili wapate video kuhusu
ukanushaji. Waongoze ili wasikilize na kutazama video hizo kwa makini kisha
uwaelekeze katika kuandika sentensi zilizokanushwa kwenye video.
Waongoze wanafunzi katika kutambua viambishi vya nafsi na wakati katika
sentensi zilizokanushwa katika Kitabu cha Mwanafunzi. Tathmini majibu yao.
Waelekeze katika kuandika sentensi hizo kwenye vipakatalishi na uwaaambie
wazisambaze kwako kupitia mtandao ili uzisahihishe.
Hitimisho: unaweza kuhitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi mradi.
Ukubwa wa Nomino
Ukubwa wa Nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi
moja
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 170-171
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya ukubwa wa nomino ili kuubainisha.
2. Kutambua nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja.
3. Kutambua nomino katika hali ya ukubwa.
4. Kubadilisha nomino kutoka wastani kuwa hali ya ukubwa.
5. Kutumia nomino katika hali ya ukubwa kwenye sentensi.
Maswali dadisi
1. Ni nomino zipi unazoweza kutaja ukubwa wake?
2. Ukubwa wa nomino unaashiria nini?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja.
Kushiriki katika vikundi kubadilisha nomino kutoka hali ya wastani hadi hali
ya ukubwa.
Kushiriki katika mchezo wa vikundi.
Kuambatanisha nomino katika hali ya ukubwa.
Kutunga sentensi zinazorejelea nomino katika ukubwa.
227
226
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 170-171
Majedwali Chati Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya nomino
zinazoanza kwa m-. Baadaye, waambie wahesabu silabi katika maneno
waliyotaja. Waambie wanafunzi wataje nomino zenye mzizi wa silabi moja.
Wanafunzi wataje nomino kama vile
ü Mti ü Mto ü Mji
Waelekeze wanafunzi katika kusoma nomino zilizo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa wa 170.
Teua mwanafunzi mmoja ili asimame mbele ya darasa kisha awaonyeshe
wenzake silabi za kila neno kwenye maneno waliyosoma.
Waambie wanafunzi wataje maneno mengine yanayoanza kwa heru m- na
yenye mzizi wa silabi moja. Wataje maneno kama vile:
ü Mbu
ü Mto
ü Mche
ü Mvi
ü Mji
Waongoze wanafunzi katika kutafuta nomino zinazoanza kwa m- na
zenye mzizi wa silabi moja katika kapu la maneno lililo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 170-171
(a) Mto
(b) Mji
(ch) Mche
(d) Mchi
(e) Mvi
(f) Mbu
(g) Mtu
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaelekeze katika
kusoma nomino za kawaida na nomino za ukubwa katika jedwali.
Waongoze wanafunzi katika kubadilisha nomino za wastani ziwe katika hali
ya ukubwa katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 171.
229
228
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
1. mchi-jichi
2. mti-jiti
3. mtu-jitu
4. mji-jiji
5. mto-jito
6. mvi-jivi
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa nomino za
ukubwa huchukua kiambishi ji kisha mzizi wake kudondoshwa.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 171-173
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutumia nomino katika hali ya ukubwa kwenye sentensi.
2. Kufurahia kutumia nomino katika hali ya ukubwa kwa usahihi ili kuimarisha
mawasiliano.
3. Kubadilisha nomino kutoka wastani kuwa hali ya ukubwa.
Maswali dadisi
1. Ni nomino zipi unazoweza kutaja ukubwa wake?
2. Ukubwa wa nomino unaashiria nini?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja.
Kushiriki katika vikundi kubadilisha nomino kutoka hali ya wastani hadi hali
ya ukubwa.
Kushiriki katika mchezo wa vikundi.
Kuambatanisha nomino katika hali ya ukubwa.
Kutunga sentensi zinazorejelea nomino katika ukubwa.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 171-173
Majedwali Chati Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wabadilishe nomino za wastani
229
228
Kimeidhinishwa na KICD
zifuatazo ziwe katika hali ya ukubwa:
1. mti
2. mtu
3. mto
4. mji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne na uwashirikishe katika
mchezo wa kutaja nomino na kikundi kingine kutaja ukubwa wa nomino
zilizo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 171. Waongoze wanafunzi ili
waweze kuambatanisha nomino za wastani na ukubwa katika jedwali kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma sentensi zilizo na nomino wastani kisha
wasome zilizo na nomino katika ukubwa.
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia nomino zilizo katika
Kitabu cha Mwanafunzi kwa ukubwa wake. Tathmini sentensi za wanafunzi.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwapa wanafunzi kazi ya ziada ya kutunga sentensi
wakitumia nomino zifuatazo:
1. mchi
2. mche
3. mlo
4. msu
5. mke
6. mja
Udogo wa nomino
Udogo wa nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja
Kipindi cha 1
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 173-174
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kueleza maana ya udogo wa nomino ili kuubainisha.
2. Kutambua nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja.
3. Kutambua nomino katika hali ya udogo.
4. Kubadilisha nomino kutoka wastani kuwa hali ya udogo.
5. Kutumia nomino katika hali ya udogo kwenye sentensi.
Maswali Dadisi
1. Ni nomino zipi unazoweza kutaja udogo wake?
2. Udogo wa nomino unaashiria nini?
231
230
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja.
Kushiriki katika vikundi kubadilisha nomino kutoka hali ya wastani hadi hali
ya udogo.
Kushiriki katika mchezo wa vikundi.
Kuambatanisha nomino katika hali ya udogo.
Kutunga sentensi zinazorejelea nomino katika udogo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 173-174
Majedwali Chati Tarakilishi
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mifano ya nomino
zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja. Wanafunzi wataje nomino
kama vile:
ü Mti ü Mto ü Mji
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wawiliwawili kisha uwaelekeze katika
kusoma nomino za kawaida na za udogo katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa wa 173.
Waelekeze wanafunzi ili waweze kuwaonyesha wenzao silabi za kila neno.
Waonyeshe kwa kutenganisha silabi katika maneno hivi:
(a) M-ti
(b) M-to
(ch) M-ji
(d) M-vi
(e) M-che
Waongoze wanafunzi katika kutaja maneno mengine yanayoanza kwa m- na
yenye mzizi wa silabi moja. Wanafunzi wataje maneno kama vile:
(a) Mti
(b) Msu
(ch) Mto
(d) Mvi
(e) Mchi
(f) Mke
(g) Mja
(h) Mlo
Waelekeze wanafunzi katika kusoma nomino za kawaida na nomino za udogo
zilizo katika jedwali kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Wanafunzi wasome
kisha watambue tofauti kati ya nomino za watani na za udogo. Katika udogo,
nomino huongezwa kiambishi ki katika hali yake ya ukubwa katika umoja
umoja na kiambishi vi’ katika wingi.
Waongoze wanafunzi katika kubadilisha nomino za wastani ziwe katika hali
ya udogo katika kitabu cha wanafunzi.
231
230
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa wa 173
(a) mchi-kijichi
(b) mti-kijiti
(ch) mtu-kijitu
(d) mji-kijiji
(e) mto-kijito
(f) mvi-kijivi
Hitimisho: hitimisha kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa katika udogo nomino
huongezwa kiambishi ki katika hali yake ya ukubwa.
Kipindi cha 2
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 174-176
Matokeo maalumu yanayotarajiwa
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja.
2. Kutambua nomino katika hali ya udogo.
3. Kubadilisha nomino kutoka wastani kuwa hali ya udogo.
4. Kutumia nomino katika hali ya udogo kwenye sentensi.
Maswali dadisi
1. Ni nomino zipi unazoweza kutaja udogo wake?
2. Udogo wa nomino unaashiria nini?
Shughuli za ujifunzaji na ufunzaji
Kutambua nomino zinazoanza kwa m- na zenye mzizi wa silabi moja.
Kushiriki katika vikundi kubadilisha nomino kutoka hali ya wastani hadi hali
ya udogo.
Kushiriki katika mchezo wa vikundi.
Kuambatanisha nomino katika hali ya udogo.
Kutunga sentensi zinazorejelea nomino katika udogo.
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 174-176
Majedwali Chati Tarakilishi
PB
232
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji na ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wabadilishe nomino za wastani
zifuatazo ziwe katika hali ya udogo:
1. mti - kijiti
2. mtu - kijitu
3. mto - kijito
4. mji - kijiji
5. mlo - kijilo
Wapange wanafunzi katika vikundi vya wannewanne na uwashirikishe katika
mchezo wa kutaja nomino na kikundi kingine kutaja udogo wa nomino hizo.
Waongoze wanafunzi katika kuambatanisha nomino za wastani na udogo
wake katika jedwali kwenye ukurasa wa 174.
Waelekeze wanafunzi katika kusoma sentensi zilizo na nomino wastani kisha
wasome zilizo na udogo wa nomino zizo hizo.
Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia nomino zilizo katika
Kitabu cha Mwanafunzi kwa udogo wake.Tathmini sentensi za wanafunzi
huku majibu ya sentensi yawe na nomino zifuatazo:
1. kijibwa
2. kijitu
3. kijifu
4. kijiji
5. kijito
Waongoze wanafunzi kubadilisha nomino za wastani ziwe katika hali ya
udogo katika kitabu cha wanafunzi. Majibu ya kazi mradi:
(a) Mti-kijiti
(b) Mche-kijiche
(ch) Mchi-kijichi
(d) Mji-kijiji
(e) Mtu-kijitu
(f) Mto-kijito
Waelekeze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia nomino za udogo
walizobadilisha.
Waongoze katika kuandika sentensi hizo kwenye chati. Watumie hati mkono
na wabandike chati zenye sentensi za nomino za udogo ukutani ili wanafunzi
wengine wazisome.
Hitimisho: hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuwa katika udogo,
nomino huongezwa kiambishi ki katika hali yake ya ukubwa.