Kimeidhinishwa na KICD
Mwanga
wa
Kiswahili
Mwongozo wa Mwalimu
Gredi ya 5
Kenan Ngere
Mary Kikwanuu
Hellen N. Kangai
Wallah bin Wallah
Kimeidhinishwa na KICD
Kimechapishwa na:
Longhorn Publishers PLC,
Barabara ya Funzi, Eneo la Viwandani,
S.L.P. 18033 00500,
Nairobi, Kenya.
Simu: +254 02 6532579/81, +254 02 558551,
+254 708 282 260, +254 722 204 608
Baruapepe: enquiries@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Uganda) Ltd.,
Plot 4, Barabara ya Vubyabirenge,
Eneo la Ntinda,
S.L.P. 24745,
Kampala, Uganda.
Simu: +256 414 286 093
Baruapepe: ug@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Tanzania) Ltd.,
Light Industry, Wilaya ya Kinondoni,
Mikocheni, Ploti No. 92,
S.L.P. 1237,
Dar es Salaam, Tanzania.
Simu: +255 714 184 465
Baruapepe: longhorntz@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Rwanda) Ltd.,
Remera, mkabala wa Benki ya COGE,
S.L.P. 5910,
Kigali, Rwanda.
Simu: +250 784 398 098
Baruapepe: rwanda@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
© K. Ngere, M. Kikwanuu, H. N. Kangai, Wallah bin Wallah 2022
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupigisha
chapa, kutafsiri au kukitoa kitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila idhini,
kwa maandishi, ya kampuni ya Longhorn Publishers PLC.
Chapa ya kwanza, 2022
Msanifu wa Jalada: Longhorn Publishers PLC
ISBN 978-9966-64-316-2
Kimepigwa chapa na Printing Services Ltd.,
Factory Street, Eneo la Viwandani,
S.L.P 32197-00600, Nairobi, Kenya.
iii
Kimeidhinishwa na KICD
Yaliyomo
Utangulizi.................................................. v
MAPISHI
............................................1
Kusikiliza na Kuzungumza: Matamshi
bora
............................................................1
Kusoma kwa ufahamu
............................. 8
Kuandika
.................................................11
Insha ya wasifu
.......................................12
Saru: Aina za nomino
..........................14
Nomino za pekee
....................................15
Nomino za kawaida
...............................18
HUDUMA YA KWANZA
...................20
Kusikiliza na Kuzungumza
...................20
Maamkuzi na maagano
.........................22
Kusoma kwa kina
................................... 24
Matumizi ya kamusi
..............................25
Kuandika
.................................................27
Insha za masimulizi
...............................29
Saru: Aina za nomino
..........................30
Nomino za wingi
.................................... 31
Nomino za vitenzi-jina
..........................34
MAPAMBO
........................................ 37
Kusikiliza na Kuzungumza: Matamshi
bora
...........................................................37
Vitendawili
...............................................39
Kusoma kwa ufahamu
............................40
Kifungu cha hadithi
................................42
Kuandika
...................................................43
Kuandika kwa tarakilishi:Uchapaji
.......44
Saru: Aina za nomino
...........................46
Nomino za makundi
...............................47
Nomino ambata
.......................................50
Nomino za dhahania
............................... 52
Saru: Uakishi
.......................................54
Heru kubwa, koma (,), kikomo (.) na
kiulizi (?)
...................................................55
SAA NA MAJIRA
..............................58
Kusikiliza na Kuzungumza: Heshima,
adabu na vyeo
........................................ 58
Maneno ya heshima
................................60
Kusoma kwa mapana
.............................61
Matini ya kidijitali
...................................63
Kuandika
...................................................64
Baruapepe
...............................................66
Saru: Umoja na wingi wa nomino
..... 67
Umoja na wingi wa nomino: Ngeli ya
I-ZI
........................................................... 69
Umoja na wingi wa sentensi: Ngeli ya
I-ZI
........................................................... 71
KUKABILIANA NA UMASKINI
......74
Kusikiliza na Kuzungumza: Methali
....74
Methali zinazohusu bidii
.......................76
Kusoma kwa ufahamu
...........................77
Lugha katika ushairi
..............................78
Kuandika
.................................................80
Insha ya maelezo
....................................81
Saru: Umoja na wingi wa nomino ....
83
Umoja na wingi wa nomino: Ngeli ya
U-ZI
.........................................................84
Umoja na wingi wa sentensi: Ngeli ya
U-ZI
.........................................................87
iv
Kimeidhinishwa na KICD
MAADILI ...........................................89
Kusikiliza na Kuzungumza: Matamshi
bora............................................................89
Matamshi bora: Ushairi...........................91
Kusoma kwa mapana...............................92
Kuandika: Insha za wasifu.......................95
Saru: Ngeli ya U-YA...............................98
Umoja na wingi wa nomino: Ngeli ya
U-YA..........................................................99
Umoja na wingi wa sentensi: Ngeli ya
U-YA........................................................102
ELIMU YA MAZINGIRA..................104
Kusikiliza na Kuzungumza: Nahau
za usa na mazingira.............................104
Kusoma kwa mapana.............................107
Kusoma matini.......................................109
Kuandika: Insha ya maelezo...................111
Saru: Ngeli ya KU-KU..........................114
Umoja na wingi wa nomino: Ngeli ya
KU-KU.....................................................115
Umoja na wingi wa sentensi: Ngeli ya
KU-KU.....................................................118
NDEGE WA PORINI .......................121
Kusikiliza na Kuzungumza: Visawe.....121
Visawe vya maneno matatu ..................123
Kusoma kwa ufahamu............................125
Mchezo wa kuigiza ...............................127
Kuandika..................................................129
Insha za masimulizi................................131
Saru: Mnyambuliko wa vitenzi..........132
Kauli za kutendewa, kutendeka na
kutendana ...............................................134
MAGONJWA .................................. 138
Kusikiliza na Kuzungumza: Mazungumzo
ya kimuktadha......................................138
Mazungumzo katika miktadha rasmi ......
.................................................................140
Kusoma kwa mapana........................... 142
Kuandika: Insha za maelezo ...............146
Saru: Vinyume....................................150
Vinyume vya vitenzi ............................152
KUDHIBITI ITIKADI ZA KIDINI NA
ZA KIJAMII..................................... 155
Kusikiliza na Kuzungumza:
Tashbihi .................................................155
Tashbihi za tabia................................... 157
Kusoma kwa mapana: Matini ya kidijitali
................................................................160
Kuandika: Insha ya masimulizi ..........164
Saru: Nyakati na hali .........................167
Hali ya mazoea .....................................169
Hali timilifu ..........................................170
UWEKEZAJI...................................172
Kusikiliza na Kuzungumza: Kutoa
masimulizi............................................. 172
Kusoma kwa ufahamu .........................176
Kuandika insha: Baruapepe ................179
Saru: Ukanushaji wa maneno na
sentensi ..................................................182
Saru: Ukubwa na udogo wa
nomino zinazoanza kwa heru m-
na zenye mzizi wa silabi mbili ............185
Saru: Ukubwa na udogo wa nomino
zinazoanza kwa heru n- ....................189
v
Kimeidhinishwa na KICD
UTANGULIZI
Taarifa kuhusu mtaala
wa umilisi
A.
Lengo kuu la mabadiliko ya mtaala wa
elimu ya msingi nchini Kenya lilikuwa
kumwezesha kila mwanafunzi kuwa raia
ambaye ameshirikishwa, amewezeshwa,
ametambulika, ameihudumia
jamii na ameadilika. Mambo haya yote
yatawezekana kwa kumpa kila mwanafunzi
Mkenya kaida zinazofaa kuboresha uwezo
na ujuzi wanaohitaji ili kufaulu maishani.
Kitabu cha mwongozo huu kimeandaliwa
kwa makini kwa minajili ya kufaulisha
jukumu la mwalimu anayefunza mtaala
wa umilisi. Mwalimu katika mtaala wa
umilisi ni mshirikishaji, ni mwezeshaji, ni
mwadilifu, ni kiongozi na ni mwelekezi
wa mwanafunzi katika shughuli anuwai za
kiutendaji katika ujifunzaji wa vipengele
mbalimbali vya lugha ya Kiswahili.
Mwongozo huu unamwezesha mwalimu
kuwa na mbinu za kutambua na kukuza
vipawa na mahitaji ya wanafunzi mapema
ili kuwaandaa vilivyo kwa ulimwengu wa
kufanya kazi, kujiendeleza kimaisha na
kuwa na maendeleo endelevu. Mtaala wa
umilisi humfanya mwanafunzi kuwa kiini
cha mchakato mzima wa kusoma.
Malengo ya Kitaifa ya
Elimu
B.
Mtaala mpya umekitwa kwenye malengo
ya kitaifa ya elimu nchini Kenya ambayo
ni:
1. Kukuza utaifa, uzalendo na kuendeleza
umoja wa kitaifa.
2. Kuendeleza ujenzi wa taifa kiuchumi,
kiteknolojia na kijamii.
3. Kujiendeleza na kujiajiri binafsi.
4. Kuendeleza uadilifu na amali za kidini.
5. Kuhimiza usawa wa kijamii na
uwajibikaji.
6. Kukuza, kuhifadhi na kuthamini
tamaduni za jamii mbalimbali
nchini Kenya.
7. Kuendeleza uhusiano wa kimataifa na
kudumisha mwelekeo ufaao kwa
mataifa mengine ulimwenguni.
8. Kuendeleza uhifadhi wa afya bora na
mazingira.
Malengo ya kijumla,
kiwango cha shule ya
msingi daraja la juu
C.
Kukia mwisho wa shule ya msingi
daraja la juu, mwanafunzi aweze:
1. Kusikiliza kwa makini na kuitikia
ipasavyo kwa Kiswahili katika
miktadha mbalimbali ya mawasiliano.
2. Kuzingatia kanuni za lugha kuwasiliana
kiubunifu kwa njia ya mazungumzo na
maandishi.
3. Kujieleza kwa ufasaha katika miktadha
mbalimbali.
4. Kusoma kwa ufasaha na kufahamu
matini mbalimbali yaliyochapishwa
na ya kidijitali na kutumia maarifa
anayoyapata katika mazingira tofauti
maishani.
vi
Kimeidhinishwa na KICD
5. Kutumia hati za kimaandishi na mfumo
wa kidijitali kuwasiliana ipasavyo kwa
kuzingatia mitindo na miundo husika
katika miktadha mbalimbali.
6. Kuchangamkia matumizi ya Kiswahili
kama lugha rasmi na ya taifa katika
mawasiliano ya kila siku.
7. Kuwa na usa wa binafsi, usa wa
mazingira na lishe ili kuendeleza
afya.
Muundo wa mwongozo
huu wa mwalimu
D.
Mwongozo huu wa mwalimu una
sehemu zifuatazo:
1. Masuala lengwa
Suala lengwa ni muktadha mpana ambao
unatumiwa kufunzia lugha. Kwa mfano,
katika Gredi ya Tano tuna masuala
lengwa kama vile: Mapishi, Huduma
ya Kwanza, Mapambo, Saa na Majira,
Kukabiliana na Umaskini, Maadili, Elimu
ya mazingira, Ndege wa porini, Magonjwa,
Kudhibiti itikadi za kidini na kijamii na
Uwekezaji.
2. Matokeo maalum yanayotarajiwa
Haya ni matokeo maalum ya ujifunzaji
katika mada ndogo tofauti zilizomo
kwenye masuala lengwa.
3. Maswali dadisi
Maswali dadisi ni mbinu sahili ambapo
mwalimu huuliza maswali ili kujenga
stadi za uwazaji wa kina sana na utafutaji
suluhu wa kiwango cha juu. Pia, huupa
ujifunzaji na ufunzaji mwelekeo au
mkondo wa kufuata.
Maswali dadisi yaliyo kwenye mwongozo
huu ni mapendekezo tu. Una uhuru wa
kubuni na kuongeza maswali yako katika
kila kipindi. Unapobuni swali dadisi:
Zingatia lengo la matarajio yako ya
somo na mada kama ilivyotolewa
kwenye mfumo wa mtaala.
Chunguza suala lengwa au dhana
muhimu katika mtaala ambayo
inapaswa kuzingatiwa.
Zingatia maswali sita ya kawaida:
Nani? Nini? Wapi? Lini? Kwa nini?
Vipi?
4. Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Umilisi wa kimsingi unakuzwa kutokana
na miktadha ya mada mbalimbali ambazo
zinafundishwa kwa kutimiza malengo yote
ya somo. Mifano ya umilisi wa kimsingi
ambao kila mwanafunzi anahitajika kupata
ni: Mawasiliano na ushirikiano, kujiamini,
uwazaji kina na utatuzi wa matatizo,
ubunifu, uraia, ujuzi wa kidijitali na hamu
ya ujifunzaji.
5. Uhusiano na masuala mtambuko
Wanafunzi hukumbana na changamoto
nyingi kama ilivyo kwa watu wazima.
Hii ni kutokana na mabadiliko ya
kisheria, kiteknolojia, kijamii, kidini,
kitamaduni na kiuchumi katika jamii.
Katika mtaala huu mpya wa umilisi,
changamoto zinazowakumba watoto
na watu wazima zimeshughulikiwa
kama masuala mtambuko. Mifano
ya masuala mtambuko ni: Uraia wa
kimataifa, elimu ya afya, stadi za maisha
na elimu ya maadili, elimu ya maendeleo
endelevu, mipango mizuri ya kuwasaidia
wanafunzi, usomaji unaohusisha huduma
kwa jamii na kushirikishwa kwa wazazi.
6. Uhusiano na maadili
Maadili ni vigezo ambavyo humwongoza
mtu yeyote katika maongezi na vitendo
vinavyokubalika katika jamii. Kufunza
maadili kutasaidia kutimiza malengo ya
kuibua wananchi waadilifu. Mifano ya
vii
Kimeidhinishwa na KICD
maadili ya kimsingi yaliyosisitizwa katika
mwongozo huu ni: upendo, uwajibikaji,
heshima, umoja, amani, uzalendo, haki za
kijamii na uadilifu.
7. Uhusiano na masomo mengine
Ni muhimu sana kwa wanafunzi kuelewa
uhusiano uliopo baina ya masomo tofauti ili
usomaji wa kila somo utiliwe mkazo katika
mtaala mzima.
8. Mapendekezo ya shughuli za
huduma za kijamii zinazochangia
ujifunzaji
Usomaji ambao unashirikisha huduma
kwa jamii ni mbinu ya kiutendaji ambayo
hushirikisha usomaji darasani na nje ya
darasa. Shughuli za usomaji unaohusisha
huduma kwa jamii zimependekezwa
ili wanafunzi watumie ujuzi na stadi
ambazo wamepata katika miktadha
rasmi katika jamii zao wakati uo huo
wakisoma kutokana na jamii. Wanafunzi
watapata stadi za kuwawezesha kuajiriwa
na wakati uo huo kuendeleza ukuaji
wa binafsi kwa mahusiano thabiti na
fanikifu katika jamii.
9. Namna ya kuwashughulikia
wanafunzi wenye mahitaji maalum
Sehemu hii inaonyesha namna mwalimu
anavyoweza kuwashughulikia wanafunzi
ambao wana mahitaji maalum katika
ufunzaji na ujifunzaji.
10. Mapendekezo ya nyenzo za
ujifunzaji
Nyenzo zitakazotumika kufundishia
shughuli mbalimbali zimependekezwa
kwa kila somo. Mwalimu awe huru
kubuni nyenzo zake kulingana na uwezo
wake, mazingira yake na muda alio nao.
11. Mapendekezo ya shughuli za
ujifunzaji
Utaratibu wa kufundisha shughuli zote
katika kitabu hiki umeangaziwa katika
kila somo. Hii ni kumwelekeza mwalimu
kufuata mpangilio sahili sana kuanzia
kwa kile wanachokijua wanafunzi hadi
kwa wasichokijua ambacho watajifunza
kwa kujigundulia.
12. Tathmini
Sehemu hii ya tathmini imeonyesha
mbinu mbalimbali ambazo mwalimu
anaweza kutumia kutathmini maendeleo
ya wanafunzi darasani.
Stakabadhi za kikazi
E.
Hizi ni stakabadhi ambazo zinatumiwa
na mwalimu katika kuandaa, kutekeleza
na kutathmini ufunzaji na ujifunzaji wa
somo lake. Stakabadhi hizi ni muhimu
kwa mwalimu. Sharti awe nazo.
Stakabadhi hizi ni:
a) Maazimio ya kazi
b) Mpangilio wa somo
c) Rekodi ya ufunzaji
d) Rekodi za maendeleo ya
wanafunzi
a) Maazimio ya kazi
Maazimio ya kazi ni stakabadhi ambayo
mwalimu huwa anatayarisha kutokana na
mfumo wa mtaala husika. Maazimio ya
kazi huonyesha namna yaliyomo katika
mtaala yatafundishwa kwa muda ambao
umetengewa sehemu fulani ya vipindi.
Maazimio ya kazi humsaidia mwalimu:
Kupanga vifaa ambavyo vitahitajika.
Kuchagua mbinu ambazo zitatumiwa
kufundishia.
Kupanga kazi kwa ajili ya tathmini.
viii
Kimeidhinishwa na KICD
Jina la Shule Gredi Somo Muhula Mwaka Jina la Mwalimu
Shule ya Msingi ya Bidii 5 Kiswahili 1 2021 Juma Kahawa
Kielelezo cha maazimio ya kazi
Wiki Kipindi Mada kuu Mada Mada
ndogo
Matokeo
maalum
yanayotarajiwa
Shughuli za
ujifunzaji
Maswali
dadisi
Nyenzo Tathmini Maoni
4 1
Huduma
ya
Kwanza
Kusikiliza na
kuzungumza:
Maamkuzi na
maagano
Maana ya
maamkuzi
na
maagano
Kukia mwisho
wa mada ndogo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kutambua
aina mbalimbali
za maamkuzi na
maagano katika
mawasiliano.
b) Kueleza
maamkuzi
na maagano
yanayotumika
katika miktadha
mbalimbali.
ch) Kutumia
aina mbalimbali
za maamkuzi
na maagano
katika
mahusiano.
Wanafunzi
wakiwa katika
vikundi
waongozwe
kujadiliana
kuhusu
maamkuzi
na maagano
ambayo wao
hutumia
nyakati
mbalimbali.
Wanafunzi
wakiwa katika
vikundi wajadili
michoro iliyo
kitabuni mwao
inayoonyesha
maamkuzi
na maagano
mbalimbali.
1. Je, unajua
maamkuzi
na maagano
gani katika
jamii yenu?
2. Je, wewe
huagana
vipi na
wenzako
shuleni na
nyumbani?
Kapu lenye
maamkuzi
mbalimbali.
Kitabu cha
Mwanafunzi,
ukurasa 16.
Breli.
Michoro ya
watu
wanaoamkuana.
Rekodi ya
maamkuzi
na maagano
mbalimbali.
Maswali ya
moja kwa
moja:
Wanafunzi
watambue
maamkuzi
mbalimbali.
Matokeo:
Wanafunzi
waamkuane.
Tathmini ya
vikundi:
Wanafunzi
waigize
maamkuzi
waliyotambua.
ix
Kimeidhinishwa na KICD
b) Mpangilio wa somo
Mpangilio ulio bora wa somo humsaidia mwalimu:
Kupanga yatakayofunzwa awali kwa kuzingatia wazi yaliyomo na namna
yatakavyofunzwa hivyo kuondoa uvulivuli na mambo yasiyofaa.
Kupanga, kutayarisha na kukusanya vifaa vya ufunzaji/ujifunzaji.
Kuwasilisha dhana na stadi kwa utaratibu mwafaka kwa kutumia mbinu stahiki
ili kuakia matokeo yanayotarajiwa yaliyotajwa.
Kutumia muda vizuri wakati wa somo.
Kuteua na kuandaa mbinu mwafaka za kupima ili kutathmini mchakato wa
ufunzaji na ujifunzaji.
Kujenga uhusiano baina ya vipengele.
Vipengele vya mpangilio wa kazi:
a) Mpangilio wa ufunzaji
b) Utangulizi
c) Maendelezo ya somo
d) Hitimisho
Mfano wa kazi ya ziada
Mwambie kila mwanafunzi ashirikiane na mzazi au mlezi wake kujadili umuhimu
wa kuamkuana na kuagana. Pia, wasikilize rekodi iliyoambatanishwa na kitabu cha
mwanafunzi inayohusisha maamkuzi na maagano mbalimbali.
Tathmini ya kipindi
Tumia maswali haya ili kutathmini jinsi kipindi kilivyoeleweka:
1. Ni maamkuzi gani yalitatiza baadhi ya wanafunzi wakati wa kipindi?
2. Je, wanafunzi waliweza kushiriki katika maigizo ya maamkuzi katika vikundi?
3. Je, nyenzo nilizokuwa nimetayarisha zilifaulisha kipindi?
4. Je, ni wapi ninahitaji kuboresha ili kipindi kieleweke kwa wanafunzi ili washiriki
katika shughuli mbalimbali kikamilifu?
Kielelezo cha mpangilio wa somo
Shule Gredi Somo Tarehe Muda Darasa
Bidii 5 Kiswahili 19/04/2021 Dakika 35 Gredi 5 Nyota
x
Kimeidhinishwa na KICD
Suala Lengwa: Huduma ya Kwanza
Mada: Kusikiliza na kuzungumza
Mada Ndogo: Maamkuzi na maagano
Matokeo maalum yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa mada ndogo, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua aina mbalimbali za maamkuzi na maagano katika mawasiliano.
2. Kueleza maamkuzi na maagano yanayotumika katika miktadha mbalimbali.
3. Kutumia aina mbalimbali za maamkuzi na maagano katika mawasiliano.
4. Kuchangamkia maamkuzi na maagano katika mahusiano.
Maswali dadisi:
Je, unajua maamkuzi gani katika jamii yenu?
Je, watu mbalimbali husalimiana vipi wanapokutana katika jamii yenu?
Je, wewe huagana vipi na wenzako shuleni na nyumbani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
Mawasiliano na ushirikiano - Umilisi huu unakuzwa wanafunzi
wanaposhirikiana katika vikundi kuigiza maamkuzi na maagano mbalimbali.
Ujuzi wa kidijitali - Ujuzi huu unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa
vya kidijitali kusakura mtandaoni ili kupata mafunzo kuhusu njia za kutoa
huduma ya kwanza hivyo kujifunza.
Kujiamini na kujithamini - Kunakuzwa mwanafunzi anapotumia maamkuzi
na maagano ipasavyo katika jamii bila woga.
Uhusiano na maadili:
Heshima - Maamkuzi na maagano huimarisha heshima baina ya wanajamii.
Pia, huchochea matumizi ya maneno ya adabu na heshima.
Umoja - Hukuzwa mwanafunzi anapotangamana na wenzake kutoa huduma
ya kwanza katika vikundi mbalimbali.
Amani na upendo - Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi anapokubali
kuwaamkua wanafunzi wenzake na kufanya shughuli mbalimbali katika
vikundi bila ugomvi.
Uhusiano na masuala mtambuko:
Uraia - Unakuzwa mwanafunzi anapoweza kuwaamkua wenzake kwa usahihi
na anapotangamana nao kutoa huduma ya kwanza shuleni.
Afya bora - Inakuzwa mwanafunzi anapoweza kufahamu njia mbalimbali za
kutoa huduma ya kwanza hivyo kupunguza maafa na kuboresha afya.
Stadi za maisha - Zinakuzwa mwanafunzi akifahamu njia mbalimbali za
kutoa huduma ya kwanza na hata kujiunga na vikundi na taasisi ambazo
hutoa huduma ya kwanza nchini.
xi
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo:
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16
Kadi zilizoandikwa maamkuzi na maagano mbalimbali
Kanda yenye maamkuzi na maagano yaliyorekodiwa
Breli
Mpangilio wa somo:
Hakikisha umefanya utati kuhusu maamkuzi na maagano mbalimbali katika
jamii mbalimbali. Pia, andaa kadi zilizoandikwa maamkuzi na maagano
mbalimbali pamoja na rekodi yenye maamkuzi na maagano mbalimbali.
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi waamkuane na kuagana kwa
kutumia maamkuzi na maagano mbalimbali ambayo wao hutumia kila siku.
Uwasilishaji wa somo
Waelekeze wanafunzi kujadili michoro iliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 16. Wanafunzi waeleze maamkuzi na maagano yanayoweza kutumika
kwa michoro husika.
Wachezee wanafunzi rekodi yenye maamkuzi na maagano mbalimbali kisha
wayajadili na kujifunza.
Waelekeze wanafunzi wakiwa katika vikundi wajadili miktadha ya maamkuzi
na maagano mbalimbali yaliyoandikwa kwenye kadi zilizo kapuni kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 17.
Waongoze wanafunzi kuigiza maamkuzi na maagano mbalimbali ambayo
wao hutumia shuleni na nyumbani. Maigizo hayo yataboresha mawasiliano
yao na kukuza ujasiri wao wa kusimama na kuzungumza mbele ya watu.
Hitimisho
Tathmini iwapo:
Mwanafunzi amefahamu maamkuzi na maagano mbalimbali.
Mwanafunzi amefahamu miktadha mbalimbali ya maamkuzi na maagano.
Mwanafunzi amefahamu umuhimu wa maamkuzi na maagano.
Hakikisha kila mwanafunzi amefanya kazi ya ziada iliyo kitabuni mwake
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Tafakuri
Mwanafunzi apewe muda wa dakika tano hivi wa kufanya tafakuri kuhusu
mambo aliyojifunza kuhusu maamkuzi na maagano mbalimbali.
xii
Kimeidhinishwa na KICD
c) Rekodi za ufunzaji
Hii ni stakabadhi ambayo huhifadhiwa na mwalimu ili kuonyesha kazi ambayo imefanywa
mwishoni mwa kila kipindi, mada au mada ndogo. Mwalimu mahususi hujaza kazi aliyofanya
kila siku. Stakabadhi hii husaidia katika:
• Uwajibikaji na uwazi wa kazi iliyofanywa na mwalimu.
• Mwendelezo wa ufunzaji wa darasa.
• Ili mwalimu mgeni ajue mahali pa kuanzia kufundisha darasa.
• Kutathmini maazimio ya kazi baada ya kipindi fulani.
• Kuleta usawa wa ufunzaji wa mada mahali ambapo kuna madarasa kadha.
Rekodi hii huonyesha kufanikiwa kwa matokeo maalum yaliyotarajiwa na umilisi alioupata
mwanafunzi. Rekodi hii inaweza kumwonyesha mwalimu iwapo ufunzaji wake umefanikiwa
katika kushughulikia mahitaji ya ujifunzaji wa wanafunzi binafsi.
Sehemu za Rekodi ya Ufunzaji
a) Maelezo kuhusu shule: Haya ni pamoja na: jina la shule, mwalimu husika, somo na gre-
di mahususi.
b) Muda: Huonyesha tarehe na wiki ambayo kazi husika ilishughulikiwa.
c) Kazi iliyofanywa: Mada na mada ndogo kama zilivyotolewa kwenye matokeo maalum
yanayotarajiwa.
d) Maoni: Hii ni sehemu ya maoni inayoonyesha ufanisi na changamoto za somo husika
pamoja na mapendekezo.
e) Maelezo kuhusu mwalimu: Haya ni pamoja na: jina, saini au ufupisho wa majina ya
mwalimu husika ili kuonyesha uwajibikaji.
Utawala wa shule unapaswa kutia sahihi rekodi za ufunzaji mara kwa mara.
Kielelezo cha Rekodi ya Ufunzaji
Shule: ________________________
Somo: ________________________
Jina la Mwalimu: _______________
Gredi: _________________________
Tarehe Wiki Kazi iliyofanywa Maoni Saini
d) Rekodi ya maendeleo ya mwanafunzi
Hii inaweza kuandaliwa kwa utaratibu-elekezi. Utaratibu-elekezi ni namna ya kutathmini
maendeleo ya mwanafunzi kwa vigezo vilivyoelezwa kwa kina. Utaratibu-elekezi huonyesha
sehemu kadha muhimu wakati wa kukadiria kazi ya binafsi. Humpa mwalimu chombo
ambacho kinahakikisha kuwa ukadiriaji ni wa haki na unafanana kwa wanafunzi wote.
Matokeo ya ujifunzaji yanahitaji mbinu tofauti za kutathmini.
xiii
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu-elekezi ni chombo kilichoandaliwa na mwalimu ambacho huonyesha matokeo
maalum yanayotarajiwa ambayo hudhihirisha utendaji, viwango vya ufanisi na uelewa
wa matokeo. Taratibu-elekezi hunuia kukusaidia katika kupima matokeo, mchakato na
maendeleo ya ujifunzaji. Isitoshe, utaratibu-elekezi humhusisha mwanafunzi katika kuunda
na kuelewa vigezo vya tathmini ambavyo vinawaruhusu kushiriki vilivyo katika mchakato
unaotakikana ili kukia lengo.
Amua kuhusu viwango ya tathmini, kwa mfano: Vizuri sana, Vizuri, Anaendelea, Anahitaji
msaada.
Mfumo wa mtaala umetumia kuzidi matarajio, kukia matarajio, kukaribia matarajio na mbali
na matarajio. Huu ni mfano wa utaratibu-elekezi:
Kigezo Kuzidi matarajio Kukia matarajio Kukaribia matarajio Mbali na matarajio
Kutambua
maamkuzi
na maagano
mbalimbali
na kuyatumia
katika
miktadha
tofautitofauti
kwa ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
maamkuzi na
maagano mbalimbali
na kuyatumia
katika miktadha
tofautitofauti kwa
ufasaha na urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
maamkuzi na
maagano mbalimbali
na kuyatumia
katika miktadha
tofautitofauti kwa
ufasaha.
Mwanafunzi anatambua
baadhi ya maamkuzi na
maagano na kuyatumia
katika miktadha
tofautitofauti kwa ufasaha.
Mwanafunzi anatambua
baadhi ya maamkuzi na
maagano na kutumia
baadhi ya maamkuzi
hayo kwa ufasaha.
Kielelezo cha Rekodi ya Maendeleo ya Mwanafunzi
Jina la Mwanafunzi: Shane Abedino
Gredi ya 5 Mwaka 2021 Muhula 1 Umri: Miaka 11
Mada
Zilizofunzwa
Mbinu Ishara za kufaulu
Maamkuzi
na maagano
ya nyakati
mbalimbali
Kutambua aina
mbalimbali za
maamkuzi na maagano
katika mawasiliano.
Mwanafunzi anaweza kutambua aina
mbalimbali za maamkuzi na maagano
katika mawasiliano
Kueleza maamkuzi na
maagano ya nyakati
mbalimbali
Mwanafunzi anaweza kueleza baadhi
ya maamkuzi na maagano ya nyakati
mbalimbali kwa ufasaha.
Kuigiza maamkuzi na
maagano ya nyakati
mbalimbali
Mwanafunzi anaweza kuigiza
maamkuzi na maagano ya nyakati
mbalimbali.
Kutumia maamkuzi na
maagano mbalimbali
katika mawasiliano.
Mwanafunzi anaweza kutumia baadhi
ya maamkuzi na maagano mbalimbali
katika mawasiliano.
xiv
Kimeidhinishwa na KICD
Hitimisho
Mwongozo huu umeandikwa ili kukusaidia kuwaelekeza wanafunzi kujifunza Kiswahili
kwa njia ambayo inavutia na kusisimua zaidi. Unakumbushwa kuamsha hamu ya wanafunzi
unapofunza. Mambo ambayo unaweza kufanya kabla ya kwenda darasani kufunza ni kama
vile:
• Kupitia matokeo yanayotarajiwa hii itakusaidia kuongoza namna ya kufunza.
• Kupitia somo ili kupata taswira ya yaliyomo yatakayoshughulikiwa.
• Kujenga taswira akilini ya shughuli za ufunzaji na namna ambavyo utawasilisha somo
hilo.
• Tangamana na wanafunzi unapozingatia shughuli zilizopendekezwa.
• Kusanya vifaa vitakavyohitajika katika somo kabla ya somo lenyewe.
Kumbuka: Shughuli za ujifunzaji ambazo zimependekezwa humu ni kielelezo tu. Si lazima
uzifuate zote. Uko huru kushirikisha mbinu nyingine za kiuvumbuzi za ufunzaji ambazo
zitasaidia kuwasilisha yaliyomo yaliyokusudiwa kwa ufanisi zaidi.
1
Kimeidhinishwa na KICD
MAPISHI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1-15)
Utangulizi
Mapishi ni shughuli za kuandaa
vyakula. Ili kutayarisha vyakula,
mpishi huhitaji vifaa vya kupikia
pamoja na aina mbalimbali za viungo
vya kupikia kulingana na chakula
anachoazimia kuandaa. Mapishi mazuri
sharti yazingatie usafi na lishe bora
inayodumishwa kwa kuwa na aina
mbalimbali za vyakula kama vile vyakula
vyenye protini, wanga na vitamini. Kuna
njia mbalimbali za mapishi. Kila njia
ya upishi hutegemea aina ya chakula
kinachopikwa.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na Kuzungumza
(Matamshi bora: Silabi na vitanzandimi
- Sauti f/v, s/z, l/r na th/dh), Kusoma kwa
ufahamu (Kifungu cha hadithi), Kuandika
insha ya wasifu, Sarufi (Aina za nomino:
nomino za pekee na nomino za kawaida).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1-6)
Matamshi bora
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua silabi za sauti
zinazokaribiana katika maneno.
b) Kutamka silabi za sauti zinazotokana
na sauti zinazokaribiana kimatamshi.
c) Kutamka vitanzandimi
vinavyoundwa kwa silabi za sauti
zinazokaribiana kimatamshi ili
kuimarisha mawasiliano.
d) Kuunda vitanzandimi vyenye maana
kutokana na sauti zinazokaribiana
kimatamshi.
e) Kuchangamkia kukariri
vitanzandimi vinavyoundwa kwa
silabi za sauti zinazokaribiana
kimatamshi ili kuimarisha
matamshi yake.
Maswali dadisi
1. Je, unajua maneno gani yenye silabi
zinazokaribiana kimatamshi?
2. Je, unajua vitanzandimi gani
vilivyo na silabi zinazokaribiana
kimatamshi?
3. Je, unaweza kuunda vitanzandimi
gani vyenye maana kwa kutumia
vitate?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Unakuzwa kupitia kwa mwanafunzi
kufanya shughuli mbalimbali kwa
kushirikiana na wenzake katika
vikundi. Mwanafunzi atamke
silabi husika, atunge na akariri
vitanzandimi akishirikiana na
wenzake katika vikundi.
2
Kimeidhinishwa na KICD
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa kupitia kwa
mwanafunzi kutunga na kuandika
vitanzandimi kwenye tarakilishi
pamoja na kujirekodi akikariri
vitanzandimi hivyo kwa kutumia
rekoda au rununu. Pia, atawatumia
wanafunzi wenzake na mwalimu
vitanzandimi alivyounda mtandaoni
ili wavitathmini na kujifunza.
(c) Ubunifu
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotunga vitanzandimi mbalimbali
vyenye maana akitumia silabi za sauti
husika bila kunakili vya wenzake.
(d) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kutunga na kukariri
vitanzandimi akiwa shuleni na nje
ya shule. Anapata hamu ya kutunga
na kukariri vitanzandimi zaidi akiwa
peke yake na akiwa na wengine
mahali popote.
(e) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutamka silabi za sauti lengwa kwa
usahihi, kutunga vitanzandimi na
kuvikariri mbele ya wenzake bila
woga. Pia, kujiamini kunakuzwa
mwanafunzi anapotunga
vitanzandimi vyenye maana kwa
kutumia silabi husika na kuwatumia
wenzake pamoja na mwalimu ili
wavitathmini.
(f) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiri kuhusu maswali dadisi
kuhusu vitanzandimi pamoja na
kufikiri kuhusu vitanzandimi vyenye
maana atakavyotunga.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utunzaji wa mazingira
Suala mtambuko hili linadhihirika
mwanafunzi anapotunga
vitanzandimi vinavyohusu mazingira
yake akitumia sauti husika.
Ujuzi wa matumizi ya fedha
Mwanafunzi anapotunga vitanzandimi
vinavyohusu msamiati wa fedha kama
vile kununua vyakula.
Afya bora
Afya bora inajitokeza mwanafunzi
anapotunga vitanzandimi vyenye
maana vinavyohusu mapishi, lishe
bora na afya bora.
Ajira kwa vijana na usalama
Kutokana na ustadi wa kukariri
vitanzandimi, mwanafunzi anaweza
kujitosa katika sanaa ya uimbaji na
ukariri wa mashairi. Vijana wakipata
ajira bila shaka usalama utaimarika.
Uhusiano na maadili
Heshima na umoja
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotunga na kukariri vitanzandimi
akiwa na wengine katika vikundi na
kuweza kutumia maneno ya heshima
kuwasiliana.
Upendo
Mwanafunzi anajifunza kuwapenda
wenzake wanapotangamana katika
vikundi wakifanya shughuli za
kutunga na kukariri vitanzandimi.
Uaminifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
3
Kimeidhinishwa na KICD
vitanzandimi vyake mwenyewe bila
kunakili vya wenzake au kutoka
kwenye matini yoyote.
Uzalendo
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
vitanzandimi vyenye ujumbe kuhusu
uzalendo. Ujumbe ambao unamfanya
kuipenda nchi yake.
Amani na haki za kibinadamu
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotunga vitanzandimi vyenye
maana akishirikiana na wenzake
kwa amani na kupewa nafasi ya
kuwasilisha maoni yake.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza - somo hili lina mafunzo
kuhusu sauti ambazo zinakaribiana
kimatamshi pamoja na uundaji wa
vitanzandimi vyenye maana.
Lugha za kiasili sauti na silabi
hufundishwa katika lugha hizi.
Muziki - somo hili hurejelea matamshi
bora. Mwanafunzi anaweza kutunga na
kuimba vitanzandimi kuhusu mapishi
wakati wa somo la Muziki na ataweza
kuchangamkia ujifunzaji.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawashirikisha wenzake
shuleni na nyumbani katika kutunga
vitanzandimi vyenye maana na kuvikariri
kwa usahihi. Kufanya hivi kutaimarisha
matamshi bora katika mawasiliano
pamoja na uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Ili kuweza kufanikisha ujifunzaji wa
wanafunzi wasioweza kuzungumza
au kusikia, unaweza kumhusisha
mfasiri/mtaalamu wa lugha ishara ili
kuwasiliana nao.
Hakikisha kuwa wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona wana mashine za
breli ili kufanikisha ujifunzaji wao.
Wanafunzi ambao wanajifunza na
kuvielewa vitanzandimi kwa haraka
na wepesi wanaweza kushirikishwa
kuwafunza wenzao wanaojifunza na
kuelewa polepole.
Hakikisha una rekodi za wanafunzi
walio na changamoto za kiafya ili ujue
jinsi ya kuwashughulikia kwa dharura.
Pia, ni vyema uwe na stadi za kuwapa
wanafunzi hao huduma ya kwanza
iwapo watakabiliwa na tatizo wakiwa
darasani.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1-6)
Maandalizi ya mwalimu
Shughuli za ufunzaji na ujifunzaji
huimarishwa ikiwa mwalimu na
wanafunzi watakuwa wamejiandaa
ipasavyo kabla ya kipindi kuanza.
Hakikisha kila mwanafunzi ana vifaa
muhimu vya kujifunzia kabla ya kipindi
kuanza. Pia,
Andaa kadi zilizoandikwa sauti f/v,
s/z, l/r na th/dh.
Andaa kadi zenye maneno yaliyo na
silabi za sauti f/v, s/z, l/r na th/dh.
Andaa chati zilizoandikwa
sentensi zenye maneno yaliyo na
1.1 Silabi na vitanzandimi
vyenye sauti f/v, s/z, l/r
na th/dh (Vipindi 4)
4
Kimeidhinishwa na KICD
silabi za sauti f/v, s/z, l/r na th/dh.
Rekodi silabi na maneno yenye
sauti f/v, s/z, l/r na th/dh kwenye
rununu, tarakilishi, rekoda au
tabuleti.
Rekodi vitate na vitanzandimi
vyenye maneno yaliyo na silabi za
sauti f/v, s/z, l/r na th/dh.
Hakikisha mashine za breli zipo na
ziko katika hali nzuri ili zitumiwe
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara mapema kuhusu somo hili
ili aweze kujifahamisha kuhusu
anayofaa kufasiri na kuhudhuria
kipindi kwa wakati unaofaa.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1
2. Rununu, tarakilishi, breli, rekoda
3. Tarakilishi, breli, rekoda, intaneti
4. Chati zilizoandikwa maneno ya
silabi za sauti f/v, s/z, l/r na th/dh.
5. Kadi zenye maneno ya silabi za
sauti f/v, s/z, l/r na th/dh.
6. Kanda yenye vitanzandimi vya
maneno ya silabi za sauti f/v, s/z,
l/r na th/dh.
1.1.1 Silabi na vitanzandimi
vyenye sauti f na v
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1-2)
Utaratibu wa ujifunzaji (Kipindi 1)
Tanguliza kipindi kwa kuwachezea
wanafunzi rekodi ya matamshi
iliyoambatanishwa na kitabu hiki.
Wanafunzi watamke kwa usahihi
sauti na maneno kwenye rekodi hiyo.
Tamka kwa usahihi sauti f na v na
kuziandika ubaoni kisha uwaulize
wanafunzi wazitamke kwa usahihi
baada yako.
Katika shughuli ya 1, tamka silabi
za sauti f na v kwa usahihi na kwa
sauti. Kila mwanafunzi atamke
silabi hizo kwa usahihi baada
yako. Tathmini matamshi ya kila
mwanafunzi.Mwelekeze mwanafunzi
kutambua silabi za sauti f na v katika
maneno. Hakikisha kila mwanafunzi
anatambua kwa usahihi kwa kupigia
mistari silabi za sauti f na v katika
maneno aliyopewa.
Mwongoze mwanafunzi kutamka
maneno yaliyo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 1. Mwanafunzi
atamke maneno hayo kwa usahihi
na aeleze maana ya kila neno
alilotamka. Tathmini matamshi na
maelezo ya mwanafunzi. Mwongoze
mwanafunzi kutambua kuwa maneno
ambayo ametamka yanakanganya
kwa kuwa yanakaribiana kimatamshi
na yanaitwa vitate. Sentensi
zinazoundwa kwa kutumia vitate
zinaitwa vitanzandimi.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha
uwaongoze kuunda vitanzandimi
vyenye maana wakitumia vitate vya
sauti f na v. Mifano: 1. Alivaa vazi
lililomfaa. 2. Alivuta dawati kisha
akafuta ubao. 3. Alivaa veli akaabiri
feri. Kubali vitanzandimi vyovyote
vyenye maana vitakavyoundwa
kwa kutumia vitate vya sauti f na v.
5
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi kusoma na
kukariri vitanzandimi walivyounda
kwa zamu na kwa haraka.
Hitimisha kipindi hiki kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Tathmini iwapo kazi hii
imefanyika kabla ya kipindi kingine.
matamshi ya mwanafunzi.
Mwongoze mwanafunzi kutambua
silabi za sauti s na z kwa kuzipigia
mistari katika maneno yaliyo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 2.
Waongoze wanafunzi wote kutamka
maneno yenye silabi za sauti s na z
uliyoandika kwenye chati. Hakikisha
kila mwanafunzi anatamka maneno
hayo kwa usahihi.
Mwelekeze vyema mwanafunzi mmoja
ayarekodi matamshi ya wanafunzi
wenzake akitumia rununu yako,
rekoda au hata tarakilishi. Matamshi
sahihi yazingatiwe. Katika shughuli
ya 2, wapange wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na uwezo
wao kisha uwaongoze kutambua
vitate vya sauti s na z kwenye mraba
ulio katika kitabu chao. Majibu
tarajiwa: saba/zaba, suka/zuka, sisi/
zizi.
Waongoze wanafunzi wote waunde
vitanzandimi vyenye maana
wakitumia vitate walivyotambua
kutoka kwenye mraba. Mifano ya
vitanzandimi: 1. Polisi alimzaba
mwizi makofi saba. 2. Nilikuwa
nikisuka nywele kisa kile kilipozuka.
3. Sisi tutajenga zizi la ngombe.
Waelekeze wanafunzi wote wasome
vitanzandimi walivyotunga na
kuvikariri kwa zamu na kwa haraka.
Matamshi sahihi yazingatiwe.
Mwelekeze kila mwanafunzi kuhusu
atakavyoshirikiana na mzazi au mlezi
wake kufanya kazi ya ziada. Majibu
tarajiwa: 1. a) zizi, b) futa, c) suka,
d) kuvuta, e) zaba.
1.1.2 Silabi na vitanzandimi
vyenye sauti s na z
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 2-3)
Utaratibu wa ujifunzaji (Kipindi 1)
Katika shughuli ya 1, wachezee
wanafunzi rekodi ya matamshi
iliyoambatanishwa na kitabu hiki.
Wanafunzi watamke kwa usahihi
sauti na maneno kwenye rekodi hiyo.
Tamka kwa usahihi silabi za sauti s
na z kisha umwelekeze mwanafunzi
kuzitamka kwa usahihi. Tathmini
Tathmini
1. Sikiliza na utathmini iwapo kila
mwanafunzi anatamka silabi
zinazotokana na sauti f na v kwa
usahihi.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua silabi ambazo
zinatokana na sauti f na v katika
maneno.
3. Sikiliza na utathmini iwapo
mwanafunzi anatamka na kukariri
vitanzandimi vilivyoundwa kwa
silabi za sauti f na v.
4. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kuunda vitanzandimi
vyenye maana akitumia vitate
vyenye silabi za sauti f na v.
6
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anatamka silabi zinazotokana na
sauti s na z kwa usahihi.
2. Chunguza iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua silabi
zinazotokana na sauti s na z katika
maneno.
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anatamka na kukariri
vitanzandimi vyenye silabi za sauti
s na z.
4. Chunguza iwapo mwanafunzi
anaweza kuunda vitanzandimi
vyenye maana akitumia vitate
vilivyo na silabi za sauti s na z.
Iwapo huna uwezo wa kuandika
sentensi kwenye tarakilishi, unaweza
kuziandika ubaoni au hata kwenye
chati.
Katika shughuli ya 2, tamka kwa
usahihi vitate vilivyo kwenye jedwali
katika Kitabu cha Mwanafunzi
ukurasa 4 kisha uwaulize wanafunzi
wawiliwawili wavitamke baada yako.
Waongoze wanafunzi kujadili
maana ya kila kitate walichotamka
kisha watumie vitate hivyo kuunda
vitanzandimi sahihi vyenye maana,
wavikariri kwa zamu, kwa haraka na
kwa sauti. Mifano ya vitanzandimi:
1. Alipeleka mahari mahali mbali.
2. Nitapiga kura baada ya kula.
3. Alifeli mtihani wa kuendesha feri.
4. Sina swali kwa sababu kila kitu kiko
shwari.
Mteue na umwelekeze mwanafunzi
mmoja awarekodi wenzake wakikariri
vitanzandimi kwa kutumia rununu
yako au tarakilishi. Iwapo huna vifaa
hivi vya kidijitali, unaweza kuviazima
kutoka kwa walimu wenzako.
Waulize wanafunzi wasikilize na
kutamka kwa haraka na kwa usahihi
vitanzandimi vilivyorekodiwa na
mmoja wao.
Katika kazi ya ziada, mwulize kila
mwanafunzi amkaririe mzazi au mlezi
wake vitanzandimi vilivyo katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 4-5
na wajadili maana ya vitanzandimi
hivyo. Mwanafunzi awaeleze wenzake
darasani maana za vitanzandimi.
Tathmini iwapo kazi hii imefanyika
kabla ya kuanza kipindi kingine.
1.1.3 Silabi na vitanzandimi
vyenye sauti l na r
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 4-5)
Utaratibu wa ujifunzaji (Kipindi 1)
Katika shughuli ya 1, wachezee
wanafunzi rekodi ya matamshi
iliyoambatanishwa na kitabu hiki.
Wanafunzi watamke kwa usahihi
sauti na maneno kwenye rekodi hiyo.
Mwongoze mwanafunzi kutamka
silabi za sauti l na r kwa usahihi.
Hakikisha kila mwanafunzi anatamka
silabi hizo kwa usahihi.
Mwongoze mwanafunzi kutambua
silabi za sauti l na r kwa kuzipigia
mistari katika vitate vilivyo kitabuni
mwake. Tathmini utambuzi wa
mwanafunzi.
Mwelekeze mwanafunzi kutambua
silabi za sauti l na r katika maneno
ya sentensi zilizo kwenye tarakilishi.
7
Kimeidhinishwa na KICD
1.1.4 Silabi na vitanzandimi
vyenye sauti th na dh
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 5-6)
Utaratibu wa ujifunzaji (Kipindi 1)
Unaweza kutanguliza kipindi kwa
kuwachezea wanafunzi rekodi ya
matamshi iliyoambatanishwa na
kitabu hiki. Wanafunzi watamke
kwa usahihi sauti na maneno kwenye
rekodi hiyo.
Katika shughuli ya 1, tamka silabi
za sauti th na dh kwa usahihi na
kwa sauti. Kila mwanafunzi atamke
silabi za sauti th na dh baada yako.
Tathmini matamshi yao.
Mwongoze mwanafunzi kutambua
silabi za sauti th na dh kwa kuzipigia
mistari kwenye maneno yaliyo katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 5.
Tathmini uwezo wa mwanafunzi wa
kutambua silabi husika.
Andika sentensi zenye maneno yenye
silabi za sauti th na dh ubaoni na
umwongoze mwanafunzi kutambua
silabi za sauti hizo. Mifano ya
sentensi: 1. Dhahabu ni madini
yenye thamani kuu. 2. Aliona
fedheha kutembea kwenye theluji.
3. Serikali imethibitisha kumalizika
kwa dhiki kuu.
Katika shughuli ya 2, wanafunzi wote
wakusikilize ukisoma maneno yaliyo
vitabuni mwao kisha watamke maneno
hayo kwa usahihi baada yako.
Waelekeze wanafunzi kujadili maana
ya maneno waliyotamka. Wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao. Waelekeze
kutumia vitate vyenye sauti th na dh
kuunda vitanzandimi vinne vyenye
maana. Mmoja wao aviandike
kwenye tarakilishi. Wawatumie
wenzao mtandaoni ili wavisome na
kuvirekebisha.
Waulize wanafunzi wasikilize wenzao
wakisoma vitanzandimi walivyounda.
Wavikariri kwa zamu, kwa sauti na
kwa haraka.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya kazi
ya ziada iliyo kitabuni mwao.
Tathmini
1. Chunguza iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutamka silabi
zinazotokana na sauti l na r kwa
usahihi.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua silabi ambazo
zinatokana na sauti l na r katika
maneno.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anatamka na kukariri vitanzandimi
vyenye silabi za sauti l na r.
4. Chunguza iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuunda vitanzandimi
vyenye maana akitumia vitate
vilivyo na silabi za sauti l na r.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anatambua silabi zinazotokana na
sauti th na dh katika maneno.
2. Sikiliza na utathmini iwapo
mwanafunzi anatamka silabi
zinazotokana na sauti th na dh
kwa usahihi.
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anatamka na kukariri
8
Kimeidhinishwa na KICD
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 6-9)
Kusoma kwa ufahamu
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa suala
lengwa uliotumika katika kifungu
ili kuimarisha ufahamu.
b) Kutumia msamiati lengwa kwa
usahihi katika sentensi.
c) Kusoma kifungu cha hadithi kwa
kuzingatia ujumbe, matukio na
wahusika.
d) Kuonyesha uelewa wa kifungu kwa
kutoa muhtasari na kujibu maswali.
e) Kujenga mazoea ya usomaji bora
katika maisha ya kila siku.
Maswali dadisi
1. Je, maana ya mapishi ni ipi?
2. Kusoma kuhusu mapishi kuna
umuhimu gani?
3. Ni hadithi gani umewahi kuisoma
kuhusu mapishi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa kupitia kwa
wanafunzi kufanya shughuli za
ujifunzaji kwa kushirikiana katika
vikundi. Wanapotambua na kujadili
maana ya msamiati wa mapishi,
kutunga sentensi wakitumia msamiati
wa mapishi, kusoma ufahamu na
kutoa muhtasari wa vifungu hivyo.
Pia, wanapowasiliana na kufanya kazi
ya ziada pamoja na walezi wao.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Katika kazi ya ziada, mwanafunzi
atatarajiwa kupiga picha hatua za
kupika chakula anachopenda au
kuzirekodi hatua hizo. Itambidi
atumie vifaa vya kidijitali kutekeleza
shughuli hii.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kutafuta vifungu
zaidi kuhusu mapishi kwenye
makala mbalimbali na mtandaoni ili
kujifunza zaidi.
(d) Ubunifu
Unakuzwa kila mwanafunzi anapoweza
kusoma makala mbalimbali kuhusu
jinsi mbalimbali za kupika na kupakua
vyakula tofautitofauti. Pia, anaposoma
kuhusu njia mbalimbali za kuandika
meza wakati wa maakuli.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Wanafunzi wafanye shughuli za
ujifunzaji kwa ushirikiano katika
vikundi. Wakosoane na kukubaliana
bila fujo ili kuonyesha uraia mwema.
Wanafunzi wathamini vyakula
vinavyopendwa na jamii mbalimbali
ili kuleta utangamano mwema.
vitanzandimi vilivyoundwa kwa
silabi za sauti th na dh.
4. Tathmini ikiwa mwanafunzi anaunda
vitanzandimi vyenye maana akitumia
vitate vyenye silabi za sauti th na dh.
9
Kimeidhinishwa na KICD
Stadi za maisha
Stadi hizi zinadhihirika mwanafunzi
anapojifunza upishi wa vyakula
mbalimbali. Ataweza kujitegemea
baadaye kwa kujipikia chakula bora
au kwa kupika vyakula vya kuuza ili
kuyakimu mahitaji yake.
Afya bora
Suala hili linashughulikiwa
mwanafunzi anaposoma
vifungu vyenye ujumbe kuhusu
aina mbalimbali za vyakula
vinavyoiboresha afya.
Kutokana na kusoma huku, mwanafunzi
atafahamu mengi kuhusiana na lishe
bora, umuhimu wa vyakula vya wanga,
protini na vitamini hivyo kuboresha
afya.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Mwanafunzi atayaheshimu maoni ya
wenzake katika shughuli za ujifunzaji
wakiwa kwenye vikundi. Ashirikiane
na wanafunzi wenzake kwa kutumia
lugha ya adabu. Pia, aonyeshe uthamini
wa vyakula mbalimbali vinavyoliwa na
jamii mbalimbali nchini.
Amani na umoja
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake
katika shughuli za vikundi kwa amani
bila kuzua fujo yoyote.
Uwajibikaji
Mwanafunzi aweze kumsaidia
mlezi wake kupika vyakula akiwa
nyumbani. Pia, akamilishe kazi zake
kwa wakati ufaao na kuvitunza vifaa
vyake vya ujifunzaji.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hushughulikia usomaji
wa vifungu vya hadithi na upanuzi
wa msamiati.
2. Sayansi na Teknolojia
Somo hili hushughulikia aina
mbalimbali za vyakula pamoja na
upanzi wake.
3. Sayansi Kimu
Somo hili hushughulikia vifaa vya
kupikia, usafi wakati wa mapishi
pamoja na aina mbalimbali za
mapishi.
Mapendekezo ya shughuli za kijamii
zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake
shuleni na nyumbani kuhusu suala la
mapishi. Ashirikiane na mlezi wake
kupika. Anapojua kupika ataweza
kuwapikia watu katika jamii hasa
wasiojiweza kama vile watu wagonjwa
na wazee. Pia, mwanafunzi ataweza
kuwahamasisha watu katika jamii
kuhusu umuhimu wa lishe bora ili
kuboresha afya.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Ili kuweza kuwahusisha wanafunzi
wasioweza kuona katika ujifunzaji,
hakikisha wana mashine za breli zilizo
katika hali nzuri ili waweze kutambua
msamiati mbalimbali wa mapishi. Pia,
wanaweza kupewa vifaa mbalimbali
halisi vya mapishi, viungo mbalimbali
vya vyakula na vyakula mbalimbali ili
waviguse, wavinuse na kuvitambua.
10
Kimeidhinishwa na KICD
Ili kuwahusisha wanafunzi wasio
na uwezo wa kuzungumza au
kusikia katika ujifunzaji, unaweza
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara ili kuwasiliana nao. Pia,
unaweza kuwaeleza maana ya
msamiati wa mapishi pamoja na
aina mbalimbali za mapishi kwa
kuziandika na wakazisoma.
Unaweza kuwashirikisha wanafunzi
wanaong’amua wanayojifunza
haraka katika kuwafunza wenzao
wanaojifunza polepole.
Mwalimu awashughulikie wanafunzi
wengine walio na matatizo
mbalimbali ya kiafya au kisaikolojia
kadri ya uwezo wake.
2.1 Kifungu cha hadithi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 6-7)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Hakikisha kuwa nyenzo za ujifunzaji
kama vile tarakilishi na breli zipo na
hazina hitilafu yoyote. Pia,
Andaa chati iliyoandikwa msamiati
mbalimbali wa mapishi.
Andaa kanda yenye maelezo kuhusu
njia mbalimbali za kupika.
Kusanya aina mbalimbali za vyakula
halisi.
Kusanya viungo halisi vya vyakula
mbalimbali.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 6
3. Kamera, projekta, tarakilishi, breli
4. Chati iliyoandikwa msamiati wa
mapishi
5. Kanda yenye maelezo kuhusu njia
mbalimbali za mapishi
6. Aina mbalimbali za vyakula halisi
7. Viungo halisi vya vyakula
mbalimbali.
Utaratibu wa ujifunzaji
Waongoze wanafunzi kusoma
kimyakimya ufahamu ulio vitabuni
mwao katika shughuli ya 1.
Waelekeze wanafunzi wasome
ufahamu huo tena wakiwa darasa
zima kisha wajibu maswali
waliyopewa. Tathmini majibu ya
wanafunzi kulingana na kifungu
husika.
Mwongoze mwanafunzi kuandika
muhtasari wa kifungu alichosoma
katika daftari lake. Wanafunzi
wabadilishane madaftari ili
watathmini kazi zao. Tathmini kazi
zao pia.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao. Waelekeze
kutambua vitendo vinavyoendelea
katika michoro iliyo vitabuni mwao
ukurasa 8 kisha wajibu maswali
waliyopewa. Majibu tarajiwa:
(a) Mpishi anaoka keki. (b) Mpishi
anapika/anasonga ugali. (c) Mpishi
anafunua sufuria ili kukoroga
chakula. (d) Mpishi anatengeneza
sharubati/juisi. Kubali majibu yoyote
sahihi yanayohusu vitendo kwenye
michoro husika. Katika kujibu
maswali kuhusu michoro husika,
tathmini majibu ya wanafunzi.
Washirikishe katika kuelezana
kuhusu vyakula mbalimbali ambavyo
wamewahi kupika.
11
Kimeidhinishwa na KICD
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 9-11)
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya wasifu kwa
kuzingatia mtindo na muundo
wake.
b) Kuandika insha ya wasifu kwa
ubunifu ili kujenga maelezo yenye
kutoa picha dhahiri.
c) Kufurahia kutunga insha bora ili
kuimarisha mazoea ya kuandika.
Maswali dadisi
1. Insha ya wasifu ni gani?
2. Unazingatia nini unapoandika
insha ya wasifu?
3. Insha ya wasifu huandikwa vipi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Unakuzwa wanafunzi wanapojadili
muundo, mtindo na mada
mbalimbali za insha za wasifu wakiwa
katika vikundi. Wanapoandika insha
na kuwasomea wenzao wanakuza
uwezo wao wa kuwasiliana.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoandika insha ya wasifu kwenye
tarakilishi na kuwatumia wenzake
pamoja nawe ili muitathmini. Pia,
anaweza kutumia intaneti kusakura
au kutafuta jinsi ya kupika vyakula
mbalimbali.
(c) Ubunifu
Unajengeka mwanafunzi
anapoandika insha ya wasifu kuhusu
mapishi mbalimbali kwa kubuni
matukio yake mwenyewe.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Unakuzwa wanafunzi wanapofanya
kazi kwa kushirikiana katika vikundi
licha ya tofauti zao anuwai.
Stadi za maisha
Kutokana na insha za wasifu kuhusu
mapishi mbalimbali, mwanafunzi
atapata ujuzi wa kupika vyakula
mbalimbali hivyo anaweza
kuendeleza ujuzi huu hadi kujiajiri
kuwa mpishi hodari.
Mwanafunzi ataweza kuwafundisha
wanajamii kuhusu mapishi mbalimbali.
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua na kutumia
msamiati wa mapishi katika kifungu
na mawasiliano kwa usahihi.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kusoma kifungu kwa
ufasaha akizingatia ujumbe,
matukio, wahusika pamoja na
matamshi sahihi.
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaonyesha uelewa wa kifungu
alichosoma kwa kutoa muhtasari na
kujibu maswali kwa usahihi.
4. Tathmini iwapo mwanafunzi anaweza
kupika vyakula mbalimbali.
Mwelekeze mwanafunzi jinsi
atakavyofanya kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
12
Kimeidhinishwa na KICD
Elimu ya afya
Mwanafunzi atafahamu lishe bora na
kuweza kudumisha afya bora kwake
na kwa wanajamii.
Uhusiano na maadili
Heshima na umoja
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotambua na kujadili insha ya
wasifu akiwa na wengine katika
vikundi na kuweza kutumia
maneno ya adabu kuwasiliana,
anapomheshimu mzazi nyumbani
wanapopika na kufuata maagizo ya
mwalimu anapojifunza.
Upendo
Insha ya wasifu inaweza kulenga watu
wanaojulikana kwa upendo hivyo
mwanafunzi kujifunza. Mwanafunzi
atakuza upendo kati yake na mlezi
wake wanaposhirikiana kupika
nyumbani.
Uaminifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
insha ya wasifu inayohusu mapishi
mbalimbali akiwa peke yake bila
kunakili insha za wenzake.
Uzalendo
Insha ya wasifu inaweza kuhusu watu
wanaojulikana kwa uzalendo hivyo
mwanafunzi kujifunza.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanashughulikia mada
ya kuandika.
2. Somo la Jamii
Somo hili linafundisha wasifu wa watu
mbalimbali mashuhuri katika nchi
hivyo mwanafunzi anaweza kujifunza.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake
shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu
wa uandishi bora katika mawasiliano.
Mwanafunzi atawaelekeza wanajamii
kuhusu mapishi mbalimbali pamoja
na umuhimu wa lishe bora.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa
kuona watambue maelezo kuhusu
muundo na mtindo wa kuandika
insha ya wasifu kwa kutumia breli.
Pia, unaweza kuwasomea maelezo
hayo wakayasikiliza na kujifunza.
Wanafunzi walio na changamoto
za viungo vya mwili kama vile
mikono wasaidiwe kuandika kwa
kutumia kiungo kingine cha mwili
walichozoea kutumia.
Unastahili kuwa mvumilivu ili uweze
kuwasaidia wanafunzi wanaochukua
muda mrefu kujifunza uandishi wa
insha ili waweze kujifunza bila kukata
tamaa.
Hakikisha kuwa unatambua hatua
yoyote inayopigwa na mwanafunzi
anayejifunza kuandika insha polepole
ili kumtia moyo.
3.1 Insha ya wasifu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 9-10)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Kusanya nakala za aina mbalimbali za
insha na uhakikishe kuna insha za wasifu
kati ya nakala hizo ambazo utawapa
wanafunzi darasani ili waweze kutambua
13
Kimeidhinishwa na KICD
insha za wasifu. Pia,
Andaa picha za aina mbalimbali za
vyakula.
Kusanya viungo mbalimbali vya
vyakula kama vile mdalasini, bizari,
vitunguu, iliki na chumvi.
Hakikisha kila mwanafunzi ana
vifaa vya kujifunzia kabla ya kipindi
kuanza.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Nakala za aina mbalimbali za insha
2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 9
3. Chati yenye insha kielelezo (insha
ya wasifu), tarakilishi
4. Viungo mbalimbali vya vyakula
5. Picha za vyakula mbalimbali
kwenye chati au tarakilishi.
Utaratibu wa ujifunzaji
Unaweza kutanguliza kipindi kwa
kuwauliza wanafunzi wataje aina za
insha walizojifunza katika gredi ya
nne.
Katika shughuli ya 1, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao na kuwauliza
watoe maelezo kuhusu insha ya
wasifu kutokana na waliyojifunza
katika gredi ya nne. Tathmini
maelezo yao.
Wape wanafunzi nakala za aina
mbalimbali za insha na uwaulize
watambue insha za wasifu kutoka
kwa nakala hizo. Waelekeze
wanafunzi kutambua insha hizo.
Waongoze kujadili mtindo na muundo
wa insha ya wasifu.
Katika shughuli ya 2, mwelekeze
mwanafunzi kutazama michoro
iliyo kitabuni mwake kisha achague
chakula kimoja anachojua kupika
pamoja na viungo vyake. Mwanafunzi
ataje viungo zaidi vya kupikia chakula
alichochagua.
Mwongoze mwanafunzi kuandika
vidokezo vitakavyomsaidia kuandika
insha ya wasifu kuhusu chakula
alichokichagua katika nambari 1.
Mwelekeze mwanafunzi kuandika
insha ya wasifu kuhusu chakula
alichochagua kwa kutumia vidokezo
alivyoandika. Mkumbushe azingatie
mtindo na muundo unaofaa. Insha
yake iwe na mada na isipungue
maneno 150.
Mwambie mwanafunzi aisome na
kuihariri insha aliyoandika. Aandike
insha hiyo kwenye tarakilishi na
akutumie pamoja na wenzake
darasani ili muisome na kuitathmini.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya kazi
ya ziada akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini iwapo kazi hii itafanyika
kabla ya kipindi kingine kuanza.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua insha ya wasifu
kwa kuzingatia mtindo na muundo
wake.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kuandika insha ya wasifu
kwa ubunifu akizingatia kanuni
zifaazo za lugha, mtindo, muundo
na mpangilio mzuri wa mawazo.
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kuandika vidokezo na
insha kwa kutumia michoro.
14
Kimeidhinishwa na KICD
4.1 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11-13)
Aina za nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino za pekee kwenye
sentensi au vifungu vya maneno.
b) Kutunga sentensi kwa kutumia
nomino za pekee ili kukuza
matumizi ya lugha sahihi.
c) Kuchangamkia kutumia nomino za
pekee katika utungaji wa sentensi na
kujaza mapengo kwenye vifungu.
Maswali dadisi
1. Je, maana ya nomino ni ipi?
2. Nomino za pekee zinahusu nini?
3. Unajua nomino za pekee gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi watafanya shughuli za
kutambua nomino za pekee na
kuzitungia sentensi wakiwa katika
vikundi. Wanafunzi watatunga
sentensi na kusomeana ili
kuzitathmini hivyo kuboresha uwezo
wao wa kuwasiliana.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Unakuzwa wanafunzi wanapotumia
vifaa vya kiteknolojia kama vile
tarakilishi kuandika kifungu na
kukoleza rangi nomino za pekee
zilizotumiwa katika kifungu hicho.
(c) Ubunifu
Unajengeka mwanafunzi anapotunga
sentensi na hata kifungu chake
mwenyewe kwa kutumia nomino za
pekee bila kunakili za wenzake.
(c) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapofaulu
kutambua nomino za pekee na
kuzitumia kutunga sentensi sahihi.
Pia, mwanafunzi anapoweza kutunga
sentensi sahihi na kuwasomea
wanafunzi wenzake.
(d) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
changamoto
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotunga sentensi kuhusu
masuala mbalimbali hasa mtambuko
akitumia nomino za pekee. Uwazaji
wa kina unajitokeza mwanafunzi
anapofikiri kuhusu nomino za pekee
atakazotumia kutunga kifungu.
Uhusiano na masuala mtambuko
Masuala mbalimbali kama vile:
lishe bora, utunzaji wa mazingira,
usalama, magonjwa mbalimbali
na utunzaji wa wanyama
yatashughulikiwa mwanafunzi
anapotunga sentensi akitumia
nomino za pekee kurejelea masuala
hayo.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Unadhihirika mwanafunzi
anapotunza vifaa vyake vya ujifunzaji.
Pia, kutekeleza majukumu yake
ifaavyo anaposhirikiana na wenzake
katika vikundi.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
15
Kimeidhinishwa na KICD
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutambua nomino za pekee
akitumia lugha ya adabu pamoja na
kuyaheshimu maoni ya wenzake.
Amani na umoja
Maadili haya yatalengwa katika
sentensi zitakazotungwa na
wanafunzi wakitumia nomino za
pekee. Pia, kupitia kwa wanafunzi
kutangamana kwa amani katika
vikundi bila kuzua fujo yoyote.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili -
masomo haya yanaangazia mada
kuhusu nomino za pekee.
Masomo mengine yote hutumia
nomino za pekee katika matini zao.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakapotumia sentensi
zenye nomino za pekee kwa usahihi
katika mawasiliano ataboresha lugha
katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Unaweza kurekodi video yenye
picha na maandishi ya maelezo
ya nomino za pekee pamoja
na mifano yake ili kuwasaidia
wanafunzi wenye changamoto
ya kusikia ili wajifunze. Pia,
mfasiri wa lugha ishara anaweza
kuhusishwa.
Hakikisha kuna mashine za breli
ili wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona wazitumie kujifunza.
Pia, wanafunzi hawa wanaweza
kutolewa maelezo kuhusu nomino
za pekee na wakayasikiliza na
kujifunza.
Jiandae kuwasaidia wanafunzi
wengine walio na matatizo
mbalimbali kadri ya uwezo wako.
4.1.1 Nomino za pekee
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11-13)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti zaidi kuhusu nomino za pekee kabla
ya kipindi ili kumwelekeza mwanafunzi
vyema. Pia,
Andaa chati zilizoandikwa nomino
za pekee mbalimbali.
Rekodi kanda yenye maelezo
kuhusu nomino za pekee.
Hakikisha tarakilishi na breli
zipo na ziko katika hali nzuri
ya kutumiwa na wanafunzi
wasioona.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11
2. Kanda yenye maelezo kuhusu
nomino za pekee
3. Tarakilishi, breli
4. Chati zilizoandikwa nomino za
pekee
Utaratibu wa ufunzaji
Tanguliza kipindi kwa shughuli ya
1 kwa kuwapanga wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na uwezo
wao na kuwauliza waeleze maana ya
nomino kwa kurejelea waliyojifunza
katika gredi ya nne.
Waongoze wanafunzi kutaja majina ya
16
Kimeidhinishwa na KICD
wanafunzi wenzao, majina ya kumtajia
Mungu, majina ya miji, mito, nchi,
milima, barabara, maziwa pamoja na
majina ya miezi ya mwaka na siku za
wiki.
Waelekeze wanafunzi kubaini kuwa
majina waliyotaja ni nomino za pekee
na lazima zianze kwa herufi kubwa.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 2 kwa kutambua
nomino za pekee kutoka kwenye
mti maneno ulio kitabuni mwake.
Majibu tarajiwa: Nairobi, Suleimani,
Kilimanjaro, Alhamisi, Mola, Juni.
Mwongoze mwanafunzi kutumia
nomino za pekee alizotambua
kutunga sentensi sahihi. Aziandike
sentensi hizo kwenye daftari lake na
apigie mistari nomino za pekee.
Mwambie mwanafunzi awasomee
wenzake sentensi alizotunga wakiwa
katika vikundi ili wazitathmini.
Katika shughuli ya 3, mwelekeze
mwanafunzi kusahihisha nomino
za pekee katika sentensi alizopewa.
Majibu tarajiwa:
1. Juma na Mueni walienda Thika
kununua samaki.
2. Ziwa Victoria na Ziwa Naivasha
hupatikana Kenya.
3. Wananchi walipanda miti ya
matunda karibu na Mlima Elgon.
4. Tulimwomba Mungu asubuhi ili
atuongoze tunapozuru Mto Tana.
5. Mwalimu alipowagawia wanafunzi
maembe, Naitore alipata mawili.
Mwongoze mwanafunzi kuandika
kifungu kilicho kitabuni mwake
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua nomino za
pekee katika sentensi na kifungu.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kutumia nomino za pekee
kutunga sentensi na kifungu kwa
usahihi.
kwenye tarakilishi. Hakikisha kila
mwanafunzi anaandika kwa usahihi.
Tathmini majibu sahihi ya nomino za
pekee ambazo mwanafunzi atatumia
kujaza mapengo ya kifungu hicho.
Akoleze rangi na kupigia mistari
nomino za pekee.
Iwapo huna tarakilishi, mwanafunzi
anaweza kuandika kifungu hicho
kwenye daftari lake.
Mweleze mwanafunzi afanye kazi ya
ziada akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Kubali sentensi zozote sahihi
zitakazotumia nomino za pekee
alizotajiwa na mzazi au mlezi wake.
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 13-15)
Aina za nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino za kawaida
kwenye sentensi au vifungu vya
maneno.
b) Kutunga sentensi kwa kutumia
nomino za kawaida ili kukuza
matumizi sahihi ya lugha.
17
Kimeidhinishwa na KICD
c) Kufurahia kutumia nomino
za kawaida katika utungaji wa
sentensi na kujaza mapengo
kwenye vifungu.
Maswali dadisi
1. Maana ya nomino ni ipi?
2. Ni vitu gani vinavyopatikana katika
mazingira yako?
3. Ni vitu gani vinavyotumiwa katika
mapishi mbalimbali?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
sentensi zake mwenyewe na kujaza
mapengo ya kifungu akitumia
nomino za kawaida zinazofaa akiwa
peke yake.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutaja nomino za kawaida
na kuzitungia sentensi. Kuwasomea
wanafunzi wenzake sentensi
alizotunga kutaboresha mawasiliano.
(c) Uwazaji wa kina
Unakuzwa mwanafunzi anapofikiri
kuhusu sentensi sahihi atakazotunga
akitumia nomino za kawaida katika
muktadha husika.
Uhusiano na masuala mtambuko
Masuala mtambuko kama vile: afya bora
na utunzaji wa mazingira yataangaziwa
kutokana na sentensi zitakazotungwa na
mwanafunzi.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapothamini maoni ya wengine
wakiwa katika vikundi na kusaidiana
kutambua nomino za kawaida kwa
kutumia lugha ya adabu.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa
mwanafunzi anapotangamana na
wanafunzi wenzake kwa amani
katika vikundi wanapotambua
nomino za kawaida na kuzitungia
sentensi sahihi.
Uzalendo na uaminifu
Maadili haya yanaweza kuhusishwa
na kujitokeza katika sentensi ambazo
mwanafunzi atatunga akitumia
nomino za kawaida.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanashughulikia mada
ya nomino za kawaida.
Masomo mengine pia hutumia nomino
za kawaida katika matini zao.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atarejelea nomino
mbalimbali za kawaida katika mazingira
yake na kuimarisha mawasiliano katika
jamii anapozitumia kutunga sentensi
sahihi. Pia, atawafundisha wanajamii
mawasiliano bora kwa kutumia nomino
za kawaida kwa usahihi.
18
Kimeidhinishwa na KICD
4.2.1 Nomino za kawaida
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi
waeleze maana ya nomino walizojifunza
katika kipindi kilichotangulia.
Katika kufanya shughuli ya 1, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi yao na uwezo wao kisha uwaulize
wataje vitu vinavyopatikana nyumbani
na shuleni mwao.
Pia, waelekeze wanafunzi wataje vifaa
vinavyopatikana jikoni.
Waambie wataje majina ya watu wa
familia, wanyama, vyakula, ndege
na wadudu. Majina ya watu wa
familia yasiwe majina halisi bali ya
kiuhusiano kama vile baba, mama na
kadhalika.
Mwambie mwanafunzi mmoja kutoka
katika kila kikundi asome maneno
waliyoandika ili wenzake katika
vikundi vingine wayatathmini na
kujifunza.
Katika shughuli ya 2, waelekeze
wanafunzi wawiliwawili wachague
nomino za kawaida kutoka kwenye
mchoro ulio vitabuni mwao. Majibu
tarajiwa: ukuta, chumvi, kalamu,
bizari, kuku, mwalimu, meza, mtu.
Waelekeze wanafunzi kutunga sentensi
sahihi wakitumia nomino za kawaida
walizochagua.
Mteue mwanafunzi mmoja awasomee
wenzake sentensi walizotunga ili
wazitathmini na kujifunza.
Katika shughuli ya 3, mwelekeze
mwanafunzi aandike sentensi
alizopewa kitabuni mwao katika
daftari lake kisha atambue nomino za
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasioweza kuona
watumie breli. Wanafunzi ambao
hawawezi kuona mbali wakae
karibu na ubao na wasioona
karibu wakae mbali kidogo na
ubao.
Wanafunzi wasioweza kusikia
watambue nomino za kawaida
kwa kutumia lugha ishara au
kwa kuzikoleza rangi kwenye
tarakilishi au kuzipigia mistari
kwenye daftari.
Wanafunzi wengine walio na
changamoto mbalimbali za kiafya
au kisaikolojia washughulikiwe
vilivyo kadri ya uwezo wako.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 13-15)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Andaa chati zilizoandikwa nomino
mbalimbali za kawaida. Pia,
Tafuta breli na uhakikishe ziko
katika hali nzuri.
Andaa sentensi zenye nomino za
kawaida utakazoandika ubaoni.
Mapendekezo ya nyenzo za
ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
13-15
2. Breli
3. Chati zilizoandikwa nomino za
kawaida
4. Vifaa halisi kama vile kalamu,
chaki, kijiko, sahani na kikombe.
19
Kimeidhinishwa na KICD
kawaida kwa kuzipigia mstari.
Majibu tarajiwa:
a) Mpishi alipika vyakula vingi.
b) Sisi hunawa mikono kabla ya kula
chakula.
c) Mimi ninaipenda nchi yangu.
d) Mazingira safi huzuia magonjwa.
e) Mjomba hula chakula cha wanga,
protini na vitamini.
Mwambie mwanafunzi afanye kazi
ya ziada akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Hakikisha mwanafunzi
amewasomea wenzake darasani
sentensi alizotunga ili wazitathmini
na kujifunza.
Mwisho, mwanafunzi ajaze mapengo
kwenye kifungu alichopewa kitabuni
mwao kwa kutumia nomino
za kawaida sahihi na mwafaka.
Mwalimu atathmini majibu ya
wanafunzi.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua nomino za
kawaida.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kutumia nomino za
kawaida kutunga sentensi sahihi
na kujaza mapengo kwenye
vifungu.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutofautisha nomino za
kawaida na nomino za pekee.
Wanafunzi wawatajie wauzaji viungo
mbalimbali vya kupikia wanavyovijua.
Wauzaji pia wawatajie na kuwaonyesha
wanafunzi viungo mbalimbali vya
kupikia wanavyoviuza. Waongoze
wanafunzi kutumia vifaa vya kidijitali
kupiga picha viungo mbalimbali
watakavyoonyeshwa na wauzaji.
Wanafunzi watakaporudi shuleni,
waandike insha ya masimulizi kuhusu
ziara hii. Ziara hii itaboresha
uhusiano wa wanafunzi na wanajamii
pamoja na kukuza uwezo wao wa
kujieleza hivyo mawasiliano na ujasiri
wao kuboreshwa.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Kubali vitanzandimi vyovyote sahihi
vilivyotumia sauti f/v, l/r, s/z au th/dh.
2. Tathmini hatua sahihi za kuoka
keki atakazoandika mwanafunzi.
Hakikisha mwanafunzi anawasomea
wenzake darasani ili wajifunze.
3. Tathmini sentensi atakazotunga
mwanafunzi akitumia maneno
aliyopewa kitabuni mwake.
Hakikisha ni sahihi kisarufi na
kimantiki.
4. Tathmini insha ya wasifu
atakayoandika mwanafunzi.
Hakikisha inazingatia kanuni za
sarufi zifaazo, mtindo, muundo
maalum na mada husika.
5. Tathmini sentensi atakazotunga
mwanafunzi kwenye tarakilishi.
Iwapo mwanafunzi hana tarakilishi,
anaweza kuziandika kwenye daftari
lake. Hakikisha ni sahihi kisarufi.
Shughuli ya nje ya darasa
Pakiwepo na muda, wapeleke
wanafunzi kwenye duka au soko lililo
karibu na shule yenu.
20
Kimeidhinishwa na KICD
HUDUMA YA KWANZA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16-24)
Utangulizi
Huduma ya kwanza ni msaada ambao
mtu hupewa anapopata majeraha au
matatizo akisubiri kupata matibabu au
suluhisho kamili. Huduma hii hutolewa
ili kumwokoa majeruhi kutokana na hali
hatari kabla ya kufikishwa hospitalini.
Baadhi ya vifaa ambavyo hutumiwa
kutoa huduma ya kwanza ni kisanduku
cha huduma ya kwanza ambacho
huwa na bendeji, dawa za kupunguza
maumivu, glavu, makasi n.k. Kila ofisi,
taasisi, sehemu za maabadi na biashara
zinafaa kuwa na visanduku vya huduma
ya kwanza. Ni muhimu kwa kila mtu,
mkubwa hata mdogo kupokea mafunzo
kuhusu njia mbalimbali za kutoa
huduma ili kuifaa jamii na kupunguza
vifo.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na Kuzungumza
(Maamkuzi na maagano), Kusoma kwa
kina (Matumizi ya kamusi), Kuandika
insha ya masimulizi, Sarufi (Nomino za
wingi na nomino za vitenzi-jina).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16-18)
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua aina mbalimbali za
maamkuzi na maagano katika
mawasiliano.
b) Kueleza maamkuzi na maagano
yanayotumiwa katika miktadha
mbalimbali.
c) Kutumia aina mbalimbali za
maamkuzi na maagano katika
mawasiliano.
d) Kuchangamkia maamkuzi na
maagano katika mahusiano.
Maswali dadisi
1. Je, unajua maamkuzi gani?
2. Je, watu mbalimbali husalimiana
vipi wanapokutana katika jamii
yenu?
3. Je, wewe huagana vipi na wenzako
shuleni na nyumbani?
21
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa wanafunzi
wanaposhirikiana katika vikundi
kuigiza maamkuzi na maagano
mbalimbali.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Unakuzwa wanafunzi wanapotumia
vifaa vya kidijitali kusakura
mtandaoni ili kupata mafunzo
kuhusu njia za kutoa huduma ya
kwanza hivyo kujifunza.
(c) Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapotumia
maamkuzi na maagano ipasavyo
shuleni, nyumbani na katika jamii
bila woga.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuwaamkua wenzake kwa usahihi na
anapotangamana nao kutoa huduma
ya kwanza shuleni.
Afya bora
Inakuzwa mwanafunzi anapoweza
kufahamu njia mbalimbali za kutoa
huduma ya kwanza hivyo kupunguza
maafa na kuboresha afya.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi akifahamu
njia mbalimbali za kutoa huduma ya
kwanza na hata kujiunga na vikundi
au taasisi ambazo hutoa huduma ya
kwanza nchini. Watu hupata ajira
kutokana na utoaji wa huduma ya
kwanza.
Uhusiano na maadili
(a) Heshima
Maamkuzi na maagano huimarisha
heshima baina ya wanajamii. Pia,
huchochea matumizi ya maneno ya
adabu na heshima.
Umoja
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake kutoa
huduma ya kwanza katika vikundi
mbalimbali.
Amani na upendo
Mwanafunzi anapokubali kuwaamkua
wanafunzi wenzake na kufanya shughuli
mbalimbali katika vikundi bila ugomvi.
Mwanafunzi kuwa tayari kutoa huduma
ya kwanza kwa wenzake kila wanapopata
majeraha ni kuonyesha upendo.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza
Somo hili hufundisha mada ya
huduma ya kwanza pamoja na jinsi
ya kuamkuana na kuagana.
2. Lugha za kiasili
Maamkuzi na maagano huwa somo
la kimsingi katika masomo ya lugha
za kiasili. Uhusiano wake na huduma
ya kwanza utamsaidia mwanafunzi
kuwasiliana vyema zaidi.
3. Sayansi na Teknolojia na Sayansi Kimu
Mada kuhusu huduma ya kwanza
hufundishwa katika masomo haya
ili kujenga uelewa wa huduma ya
kwanza ili kumwokoa mtu kwa
dharura.
22
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anatarajiwa
kuwaheshimu na kutangamana na
wenzake katika jamii.
Mwanafunzi anatarajiwa kusaidia
katika utoaji wa huduma ya kwanza
katika jamii pamoja na kuwafundisha
wanajamii njia mbalimbali za kutoa
huduma ya kwanza ili kupunguza
maafa na kuboresha afya.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi walio na uwezo wa
kung’amua wanayojifunza mara
moja baada ya kushirikishwa katika
shughuli za ujifunzaji wapewe fursa
ya kubuni sentensi zaidi zenye
maamkuzi na maagano mbalimbali.
Wanafunzi wanaochukua muda
zaidi kufahamu wanayofundishwa
washirikishwe katika shughuli
zaidi na kutengewa muda zaidi wa
kujifunza baada ya masomo jioni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusema au kusikia watambue
maamkuzi na maagano mbalimbali
katika sentensi kwa kuyapigia mistari.
Mfasiri wa lugha ishara anaweza
kushirikishwa.
Wale ambao hawana uwezo wa kuona
watumie breli au kusikiliza maneno ya
maamkuzi na maagano yakisomwa na
mwalimu, wanafunzi wenzao au kutoka
kwenye kanda iliyorekodiwa.
1.1 Maamkuzi na maagano
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16-17)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Shughuli za ufunzaji huimarishwa ikiwa
mwalimu na wanafunzi watakuwa
wamejiandaa ipasavyo kabla ya kipindi
kuanza.
Hakikisha kila mwanafunzi ana vifaa
muhimu vya ujifunzaji kabla ya kipindi
kuanza. Pia,
Fanya utafiti kuhusu maamkuzi
na maagano mbalimbali kutoka
kwa makabila mbalimbali ili
kuwaburudisha wanafunzi na
kuwafunza. Pia, fanya utafiti kuhusu
njia mbalimbali za utoaji wa huduma
ya kwanza.
Andaa maigizo yatakayoigizwa na
wanafunzi yanayohusu maamkuzi na
maagano mbalimbali.
Andaa kadi tofauti zilizoandikwa
maamkuzi na maagano mbalimbali.
Hakikisha mashine za breli zipo na
ziko katika hali nzuri ili zitumiwe na
wanafunzi wasio na uwezo wa kuona.
Hakikisha una sanduku la huduma ya
kwanza lenye vifaa muhimu.
Mfahamishe mapema mfasiri wa
lugha ishara kuhusu somo hili ili
aweze kujiandaa ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16
2. Kadi zilizoandikwa maamkuzi na
maagano mbalimbali
3. Kanda ya maamkuzi na maagano
yaliyorekodiwa
4. Breli, Sanduku la huduma ya
kwanza
23
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi hiki kwa kuwaelekeza
wanafunzi waamkuane na kuagana
kwa kutumia aina mbalimbali za
maamkuzi na maagano kutegemea
majira mbalimbali. Mifano ya maamkuzi
na maagano: hamjambo hatujambo,
safari njema - asante n.k. Unaweza
kuwachangamsha wanafunzi zaidi kwa
kuwaelekeza kuamkuana na kuagana
kwa kutumia lugha za makabila yao
mbalimbali. Mifano: Lugha ya Kikisii:
Bwakire? Bwakire buya. (Taf siri : Habari
ya asubuhi? - Njema.) Obotuko obuya
Naye bo. (Tafsir i: Usiku mwema Nawe
pia.)
Katika shughuli ya 1, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha
uwaelekeze kujadili michoro iliyo
vitabuni mwao.
Waongoze kutaja maamkuzi na
maagano ambayo yanaweza kutumika
katika michoro waliyojadili. Majibu
tarajiwa: hujambo daktari? sijambo,
habari ya asubuhi? njema/nzuri,
kwaheri kwaheri ya kuonana,
alamsiki binuru. Tathmini majibu
ya wanafunzi kulingana na michoro
husika.
Wachezee wanafunzi rekodi ya
maamkuzi na maagano mbalimbali
iliyoambatanishwa na kitabu hiki.
Wanafunzi wajadiliane maamkuzi na
maagano kwenye rekodi hiyo.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kisha
uwaongoze kueleza miktadha
ya maamkuzi na maagano
yaliyoandikwa kwenye kadi
zilizo kapuni kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 17. Mfano:
safiri salama hutumiwa kumuaga mtu
anaposafiri wakati wowote.
Katika shughuli ya 3, wanafunzi
katika vikundi waigize maamkuzi
na maagano mbalimbali ambayo
wao hutumia shuleni na hata
nyumbani. Maigizo haya yataboresha
mawasiliano yao na kukuza ujasiri
wao wa kusimama na kuongea
mbele ya watu. Mfano: Maigizo
kuhusu mwanafunzi na mwalimu
wakizungumza katika majilisi.
Maigizo kuhusu mama na mtoto wake
wakizungumza nyumbani.
Katika shughuli ya 4, waongoze
wanafunzi kujadili njia mbalimbali
za kutoa huduma ya kwanza kwa
wenzao wakijeruhiwa.
Hatimaye, mwambie mwanafunzi
afanye kazi ya ziada akisaidiwa na
mzazi au mlezi wake. Tathmini iwapo
mwanafunzi amefahamu umuhimu
wa maamkuzi na maagano, kwa
mfano: kujenga uhusiano mwema
baina ya wanajamii, kukuza msamiati
hivyo kuboresha mawasiliano. Pia,
mwanafunzi afahamu maamkuzi na
maagano mbalimbali yanayotumiwa
katika jamii yao.
Tathmini
1. Tathmini ikiwa mwanafunzi anaweza
kutambua maamkuzi na maagano
mbalimbali katika mawasiliano.
24
Kimeidhinishwa na KICD
vikundi kutafuta maana za maneno
kwenye kamusi ya Kiswahili na
kujadiliana.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia kamusi ya Kiswahili
mtandaoni kutafuta maana za
maneno kwa kutumia vifaa vya
kidijitali.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inajengeka mwanafunzi
anapoendelea kutumia kamusi ya
Kiswahili kutafuta maana za maneno
darasani, nyumbani na mahali popote
pale.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Suala mtambuko hili linakuzwa
mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake kutoka maeneo mbalimbali
katika vikundi kutafuta maana
za maneno kwenye kamusi ya
Kiswahili.
Stadi za maisha
Hizi zinakuzwa mwanafunzi
anapopata uwezo wa kujitegemea
katika kutumia kamusi ya Kiswahili
darasani na nyumbani. Mwanafunzi
anaweza kujifunza mambo mengine
kutoka kwenye kamusi ya Kiswahili
na kujiboresha.
Uhusiano na maadili
Uzalendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapothamini kushirikiana na
wenzake kutafuta maana za maneno
kwenye kamusi ya Kiswahili.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kueleza miktadha mbalimbali
ya maamkuzi na maagano
mbalimbali.
3. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia kwa usahihi aina
mbalimbali za maamkuzi na
maagano katika mawasiliano yake.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 18-20)
Kusoma kwa kina
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua mpangilio wa maneno
katika kamusi ili kupata maneno
lengwa kwa urahisi.
b) Kutumia kamusi ipasavyo
kutafuta maana za maneno
asiyoyajua yaliyo katika matini
teule ili kukuza msamiati wake.
c) Kuchangamkia kutumia kamusi
katika kukuza msamiati wake.
Maswali dadisi
1. Kamusi ya Kiswahili ina umuhimu
upi kwako?
2. Unatafuta vipi maana za maneno
kwenye kamusi ya Kiswahili?
3. Je, ni habari zipi ambazo tunaweza
kupata kwenye kamusi ya Kiswahili?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
25
Kimeidhinishwa na KICD
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutafuta maana za maneno
kwenye kamusi ya Kiswahili bila
kuzua ugomvi.
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuitunza vyema kamusi ya Kiswahili
anapoitumia kutafuta maana za
maneno bila kuirarua wala kuichafua.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazohusisha
matumizi ya Kamusi ili kuelewa maana
za maneno mbalimbali.
Masomo yote humhitaji mwanafunzi
kutumia kamusi ili kuelewa maana za
misamiati mbalimbali katika ujifunzaji
wake.
Mapendekezo ya shughuli za
huduma za kijamii zinazochangia
ujifunzaji
Mwanafunzi awasaidie wanajamii
kufahamu maana za misamiati
mbalimbali ili kuboresha mawasiliano
yao kwa lugha ya Kiswahili.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye uwezo wa
kung’amua wanayojifunza kwa
haraka wapewe fursa ya kutafuta
maana za msamiati zaidi katika
kamusi na kuyatungia sentensi
sahihi.
Wanafunzi wanaochukua muda
zaidi kuelewa na kufahamu
wanayojifunza washirikishwe
katika shughuli zaidi na
kutengewa muda zaidi wa
kujifunza.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuzungumza au kusikia watambue
maana za maneno kwenye sentensi
kwa kuyapigia mistari. Pia,
unaweza kumshirikisha mfasiri wa
lugha ishara katika funzo hili.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona watumie mashine za breli.
Pia, wanaweza kusikiliza maana za
maneno zikisomwa na mwalimu,
wanafunzi wenzao au kutoka
kwenye kanda iliyorekodiwa.
2.1 Matumizi ya kamusi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 18-19)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Shughuli za ufunzaji na ujifunzaji
huimarishwa ikiwa mwalimu na
wanafunzi watakuwa wamejiandaa
ipasavyo kabla ya kipindi kuanza.
Hakikisha una kamusi ya
Kiswahili. Ikiwa wanafunzi
hawana nakala za kamusi za
Kiswahili za kutosha unaweza
kuwaazimia nakala kutoka kwa
wanafunzi wa gredi au madarasa
mengine.
Pitia kamusi yako ya Kiswahili ili
kujifahamisha na mipangilio yake
ya maneno.
26
Kimeidhinishwa na KICD
Andaa chati yenye sampuli za
maneno yaliyopangwa kialfabeti
kama ilivyo kwenye kamusi ili
kuitundika ukutani kwa ujifunzaji
wa wanafunzi.
Hakikisha kuwa mashine za
breli ziko katika hali nzuri. Pia,
hakikisha mfasiri wa lugha ishara
amefahamishwa kuhusu somo hili
ili ajiandae ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 18
2. Kamusi ya Kiswahili
3. Chati yenye maneno yaliyopangwa
kialfabeti
4. Breli
5. Mfasiri wa lugha ishara
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi hiki kwa shughuli
ya 1 kwa kuwaelekeza wanafunzi
wajadiliane kuhusu vitabu ambavyo
watatumia iwapo wangetaka kupata
maana za maneno ya Kiswahili.
Tathmini majibu yao. Wanafunzi
wajikumbushe kuhusu waliyojifunza
kuhusiana na matumizi ya kamusi
katika gredi ya nne.
Wakumbushe wanafunzi kuhusu
alfabeti za Kiswahili. Kila
mwanafunzi amtajie mwenzake
alfabeti zote za Kiswahili. Tathmini
majibu yao. Hakikisha ni sahihi.
Wanafunzi wakiwa wawiliwawili
wapange maneno waliyopewa
vitabuni mwao kialfabeti. Majibu
tarajiwa: ambulensi, bendeji, chupa,
dawa, dunga, glavu, kitanda, machela,
muuguzi, nguo, pamba, sindano,
tapika, tembe, umia, wembe.
Waelekeze wanafunzi wawiliwawili
wajadiliane kuhusu maneno
yalivyopangwa kwenye kamusi ya
Kiswahili. Unaweza kuwapanga
wanafunzi katika vikundi kulingana
na nakala za kamusi za Kiswahili
walizo nazo au ulizo nazo. Wanafunzi
wabaini kuwa maneno katika kamusi
yamepangwa kialfabeti kuanzia A
hadi Z.
Katika shughuli ya 2, mwelekeze
mwanafunzi kutafuta maana za
maneno waliyopanga kialfabeti
katika shughuli ya 1. Mwanafunzi
atumie kamusi ya Kiswahili. Baadaye,
wanafunzi wajadiliane kuhusu maana
za maneno hayo na iwapo ilikuwa
rahisi kuyapata kwenye kamusi.
Katika shughuli ya 3, mwalimu
awaongoze wanafunzi kusoma matini
inayohusu huduma ya kwanza iliyo
vitabuni mwao kisha wajibu maswali
waliyopewa. Majibu tarajiwa:
1. Dawa, bendeji, tembe, kisanduku
cha vifaa vya huduma ya kwanza,
kipimajoto, makasi, sindano.
2. Kidonda chake kilisafishwa
na kupakwa dawa, kilifungwa
bendeji kisha akapewa tembe za
kumeza ili kupunguza maumivu.
3. Mwanafunzi atumie kamusi
ya Kiswahili kupata maana za
maneno yaliyokolezwa rangi
katika matini husika kisha
ayatungie sentensi sahihi.
Tathmini sentensi atakazotunga
mwanafunzi.
27
Kimeidhinishwa na KICD
Hakikisha ni sahihi na zinatumia
maneno husika.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Tathmini iwapo mwanafunzi alisoma
mtandaoni matini kuhusu utoaji
huduma ya kwanza kwa kuthibitisha
aliyoandika kwenye daftari lake. Pia,
awasomee wenzake aliyoandika.
c) Kuchangamkia utunzi mzuri wa
insha ya masimulizi ili kukuza
ubunifu wake.
Maswali dadisi
1. Je, insha ya masimulizi ni gani?
2. Je, unazingatia nini unapoandika
insha nzuri ya masimulizi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia vifaa vya kidijitali
kuandika insha, kuihariri na kuituma
mtandaoni kwa wenzake na kwako ili
muitathmini na kujifunza.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutoa masimulizi mbalimbali
na kuandika insha za masimulizi.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kuimarisha ujuzi wake
wa kuandika insha ya masimulizi
darasani na nyumbani. Pia,
anapoendelea kutumia tarakilishi
katika uandishi.
(d) Ubunifu
Unajengeka mwanafunzi anapoandika
insha ya masimulizi kwa kuwa mbunifu
wa matukio na miktadha mbalimbali.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Hukuzwa mwanafunzi anaposhirikiana
na wanafunzi wenzake kutoka maeneo
mbalimbali kufanya kazi kwa pamoja
nje na ndani ya darasa.
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua mpangilio wa
maneno katika kamusi ili kupata
maana za maneno kwa urahisi.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi
amefahamu umuhimu wa kamusi
kwake.
3. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia kamusi ipasavyo
ili kupata maana za maneno
asiyoyajua ili kukuza msamiati
wake.
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 20-21)
Kuandika insha
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi
kwa kuzingatia ujumbe, mtindo
na muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi kwa
kufuata kanuni zifaazo.
28
Kimeidhinishwa na KICD
Utunzaji wa mazingira
Huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake
katika vikundi kuandika insha
ya masimulizi kuhusu utoaji wa
huduma ya kwanza pamoja na
jinsi ya kuyatunza mazingira, kwa
mfano, kutotupa ovyoovyo vifaa
vilivyotumiwa kutoa huduma
ya kwanza bali kuvitupa kwenye
majalala.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Hukuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
wanapojadili mada mbalimbali
za kuandikia insha za masimulizi
na kutumia lugha ya adabu
anapowasiliana. Pia, anapowapa
wenzake fursa ya kuchangia katika
majadiliano yao.
Umoja na amani
Unakuzwa kutokana na mwanafunzi
kutangamana kwa amani na wenzake
katika vikundi wanapojadili na
kuandika insha za masimulizi bila
kuzua ugomvi wowote.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya mawili yana mada
zinazofundisha kuhusu uandishi
wa insha mbalimbali zikiwemo za
masimulizi.
2. Sayansi na Teknolojia na Sayansi Kimu
Masomo haya yana mada zinazoangazia
utoaji wa huduma ya kwanza.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake
shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu
wa uandishi bora katika mawasiliano.
Mwanafunzi awafundishe wanajamii
wenzake kuhusu njia mbalimbali za
kutoa huduma ya kwanza ili kuyaokoa
maisha ya wenzao katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia mashine za breli
kusoma maelezo kuhusu insha ya
masimulizi pamoja na kuandika insha
yenyewe. Pia, wanaweza kusikiliza
insha ya masimulizi ikisomwa nawe,
wanafunzi wenzao au kutoka kwenye
kanda iliyorekodiwa.
Wanafunzi wenye uwezo wa
kung’amua wanayojifunza kwa
haraka wapewe fursa ya kubuni insha
zaidi za masimulizi.
Wanafunzi wanaochukua muda zaidi
kabla ya kufahamu wanayojifunza
washirikishwe katika shughuli zaidi
za uandishi wa insha ya masimulizi
na kutengewa muda zaidi wa
kujifunza baada ya masomo jioni.
Mfasiri wa lugha ishara anaweza
kushirikishwa hapa iwapo kuna
wanafunzi ambao hawana uwezo
wa kusikia au kuzungumza.
Pia, wanafunzi hawa wanaweza
kuwasiliana nawe na wenzao kupitia
kwa maandishi.
29
Kimeidhinishwa na KICD
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 20-21)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti zaidi kuhusu uandishi wa
insha ya masimulizi pamoja na njia
mbalimbali za utoaji wa huduma ya
kwanza. Pia,
Andaa nakala za insha mbalimbali
zikiwemo insha za masimulizi
utakazowapa wanafunzi darasani
ili watambue insha za masimulizi.
Unaweza kutumia nakala za
insha mbalimbali kutoka kwa
wanafunzi wa gredi au madarasa
mengine.
Hakikisha mashine za breli zipo
na ziko katika hali nzuri ya
kutumika. Mfasiri wa lugha ishara
afahamishwe mapema ili ajiandae.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 20
2. Nakala za insha mbalimbali
3. Mfasiri wa lugha ishara
4. Mashine za breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaelekeza
wanafunzi kufanya shughuli ya 1
ambapo watajikumbusha kuhusu
waliyojifunza kuhusu uandishi wa
insha ya masimulizi katika gredi ya
nne. Waelekeze wanafunzi kujadili
sifa za insha ya masimulizi.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha
uwape nakala mbalimbali za insha
ulizoandaa. Waelekeze kusoma
nakala hizo za insha kisha watambue
nakala za insha za masimulizi kwa
kutumia sifa za insha ya masimulizi
walizojadili katika shughuli ya 1.
Wanafunzi wajadili insha za
masimulizi walizotambua kwa
kuzingatia ujumbe, mtindo na
muundo wa insha hizo. Watambue
iwapo sifa walizojadili zinafanana na
walizotaja kwenye shughuli ya 1.
Katika shughuli ya 3, waongoze
wanafunzi katika vikundi kuandika
insha za masimulizi kutokana na
matukio ya michoro iliyo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 20.
Mwanafunzi mmoja kutoka katika
kila kikundi awasomee wanafunzi
wengine insha ya masimulizi
waliyoandika katika kikundi chao.
Shughuli hii itakuza ubunifu wa
wanafunzi pamoja na kujiamini na
kuwa na ujasiri wa kusimama na
kuongea mbele ya watu.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada iliyo
kitabuni mwake.Tathmini insha
ya masimulizi atakayoandika na
kukutumia mtandaoni. Hakikisha
insha hiyo haipungui maneno 150,
imetumia lugha sahihi, ina ubunifu
na imezingatia mada aliyopewa.
3.1 Insha za masimulizi
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua insha ya
masimulizi kwa kuzingatia
30
Kimeidhinishwa na KICD
(b) Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapofaulu
kutambua nomino za wingi kwa
usahihi na kuzitungia sentensi. Pia,
anapoweza kuwasomea wenzake
sentensi zake sahihi.
(c) Kufikiri kwa kina
Kunakuzwa mwanafunzi anapofikiri
kuhusu sentensi sahihi atakazotunga
akitumia nomino za wingi na kuzijadili
na wenzake. Pia, anapotunga kifungu
sahihi akitumia nomino za wingi.
(d) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
sentensi zake mwenyewe zilizo sahihi
akitumia nomino za wingi. Pia,
anapoweza kubuni kifungu akitumia
nomino za wingi kwa usahihi bila
kunakili vya wenzake.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano na uraia
Hukuzwa mwanafunzi anaposhirikiana
na wenzake kutoka maeneo mbalimbali
katika vikundi kutambua nomino za
wingi na kuzitungia sentensi sahihi.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapoweza
kujieleza kupitia kwa utungaji wa
sentensi na vifungu vilivyo na
nomino za wingi.
Uhusiano na maadili
Heshima
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi wanapotambua nomino za
wingi wakitumia lugha ya adabu. Pia,
4.1 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 21-22)
Aina za nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino za wingi
katika matini mbalimbali.
b) Kutumia nomino za wingi katika
sentensi.
c) Kufurahia kutumia nomino za
wingi katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, unajua majina gani ambayo
yanahusisha vitu vinavyopatikana
katika wingi pekee?
2. Ni sifa zipi unazoweza kutambua
katika nomino hizi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutambua nomino za wingi
kutoka kwenye matini mbalimbali.
ujumbe, mtindo na muundo kati
ya insha mbalimbali.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutunga na kuandika insha
ya masimulizi kwa kufuata
kanuni zifaazo. Aweze kuandika
kwenye daftari lake na pia kwenye
tarakilishi na kuituma kwako na
kwa wanafunzi wenzake.
31
Kimeidhinishwa na KICD
anapoheshimu maoni ya wenzake
wanapotunga sentensi na vifungu.
Uwajibikaji
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi
anapokamilisha kazi zake za darasani
kwa wakati unaofaa.
Pia, anapovitunza vifaa vyake vya
ujifunzaji.
Amani, umoja na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa umoja na amani bila kuzua
ugomvi. Pia, mwanafunzi anapowapa
wenzake fursa ya kushiriki katika
majadiliano yao.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazoangazia
nomino za wingi katika sarufi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awafundishe wanajamii
kuhusu nomino za wingi ili
kuyaboresha mawasiliano yao.
Mwanafunzi awe kielelezo chema
katika kutumia lugha ya Kiswahili
ipasavyo katika mawasiliano.
Namna ya kuwashughulikia
wanafunzi wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia mashine za breli
kusoma maelezo kuhusu maana ya
nomino za wingi. Pia, unaweza kuleta
vitu halisi darasani ili waviguse na
kuvitambua. Vilevile, wanafunzi hawa
wanaweza kusikiliza maelezo kuhusu
nomino za wingi yakitolewa nawe au
wanafunzi wenzao na kujifunza.
Wanafunzi walio na matatizo ya
kifamilia au kisaikolojia wapewe
ushauri nasaha ili waweze kujifunza
bila usumbufu au taabu.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia
au kuzungumza wanaweza kujifunza
kwa kutumia maandishi. Mfasiri wa
lugha ishara anaweza kushirikishwa
katika somo hili.
4.1.1 Nomino za wingi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 20-21)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu nomino za wingi
ili kufahamu zaidi kuhusu shughuli za
ujifunzaji utakazowahusisha wanafunzi.
Pia,
Andaa vitu halisi mbalimbali
vinavyoashiria nomino za wingi
kutoka kwenye mazingira ya
kawaida ya mwanafunzi. Vitu
hivi halisi vitachangia pakubwa
katika kurahisisha ujifunzaji wa
mwanafunzi.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa.
Mfasiri wa lugha ishara
afahamishwe mapema ili ajiandae
ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 21
2. Breli
3. Chati zilizoandikwa mifano ya
nomino za wingi
4. Vitu halisi katika hali ya wingi.
32
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi
wataje aina za nomino mbalimbali ambazo
tayari wamejifunza pamoja na mifano ya
nomino hizo. Wanafunzi wataje mifano
ya nomino za pekee, nomino za kawaida,
nomino ambata na nomino dhahania.
Katika shughuli ya 1, waelekeze
wanafunzi wawiliwawili kusoma na
kutambua nomino za wingi kutoka
kwenye mchoro ulio vitabuni mwao.
Majibu tarajiwa: mate, usaha, damu,
maji, chumvi.
Wanafunzi wajadili umoja na wingi
wa nomino walizotambua. Waelekeze
kugundua kuwa nomino walizotambua
hazina wingi. Zinabaki vilevile. Baada
ya majadiliano haya, watunge sentensi
sahihi wakitumia nomino hizo katika
umoja na wingi. Tathmini sentensi
watakazotunga. Ziwe sahihi kisarufi.
Katika shughuli ya 2, wasomee
wanafunzi matini ifuatayo. Hakikisha
unaisoma kwa sauti na kwa matamshi
sahihi.Wanafunzi wakusikilize kwa
makini.
Lucy ni dada yangu. Yeye hupenda kupika
chai kila jioni. Nilimwomba anifundishe
kupika chai siku moja jioni. Alinieleza kuwa,
baada ya kuwasha jiko, nichukue sufuria
safi halafu nitie maji safi ndani. Alinishauri
kuwa sufuria hiyo yenye maji iinjikwe
kwenye jiko kwa uangalifu mkubwa. Baada
ya maji kuchemka aliniagiza kutia maziwa
ndani na kuongeza majani chai. Ili kupasua
pakiti ya maziwa, yeye hutumia makasi ili
kuzuia mate kuchanganyika na maziwa
mtu anapotumia meno kutoboa pakiti ya
maziwa. Mchanganyiko huo huachwa hadi
utokote ili kuunda chai. Ili kuongeza ladha,
sukari huongezwa wala sio chumvi.
Waongoze wanafunzi kutambua
nomino za wingi kutoka kwenye
matini uliyowasomea.
Katika shughuli ya 3, mwelekeze
mwanafunzi aandike kwenye daftari
lake nomino kumi za wingi anazojua.
Aziandike katika umoja na wingi.
Mwanafunzi atumie nomino za
wingi alizoandika kutunga kifungu
kifupi sahihi. Mwanafunzi ahakikishe
amezipigia mistari nomino za wingi
kwenye kifungu hicho. Shughuli hii
itakuza ubunifu na uwazaji kina wa
mwanafunzi.
Hatimaye, mwanafunzi awasomee
wenzake kifungu kifupi alichotunga.
Kusoma huku kutakuza ujasiri wa
mwanafunzi wa kuongea mbele
ya watu pamoja na kujiamini na
kujithamini.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada. Majibu
tarajiwa:
1. maji 2. chai 3. mate 4. chumvi
5. marashi.
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua nomino za
wingi katika matini mbalimbali.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia nomino za wingi
katika kutunga sentensi na vifungu
ili kuboresha mawasiliano yake.
33
Kimeidhinishwa na KICD
kutambua kwa usahihi nomino za
vitenzi-jina na kuzitungia sentensi
sahihi. Pia, mwanafunzi anapoweza
kuwasomea wenzake sentensi na
vifungu sahihi alivyotunga.
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Utangamano na uraia
Masuala mtambuko haya yanakuzwa
mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake wenye asili tofautitofauti
kutambua nomino za vitenzi-
jina wakiwa kwenye vikundi. Pia,
anaposhirikiana na wenzake kwenye
vikundi kutunga sentensi na vifungu
wakitumia nomino za vitenzi-jina.
(b) Masuala mengine kama vile
utunzaji wa mazingira, afya bora,
elimu ya fedha n.k. yatajitokeza
katika sentensi atakazotunga
mwanafunzi akitumia nomino za
vitenzi-jina.
Uhusiano na maadili
Upendo na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kufanya shughuli mbalimbali
kwa amani bila kuzua fujo.
Umoja na heshima
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutambua nomino za vitenzi-
jina kwa kutumia lugha ya adabu.
Pia, kwa kuyaheshimu maoni ya kila
mwanafunzi katika vikundi.
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 23-24)
Aina za nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino za vitenzi-jina
kwenye kifungu cha maneno au
sentensi.
b) Kutunga sentensi au vifungu vya
maneno akitumia nomino za
vitenzi-jina ili kukuza matumizi
bora ya lugha.
c) Kufurahia kutumia nomino za
vitenzi-jina katika utungaji wa
sentensi na kujaza mapengo.
Maswali dadisi
1. Je, ni matendo gani wewe hufanya
nyumbani?
2. Unapenda kufanya mambo gani
ukiwa shuleni?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Kufikiri kwa kina
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiri kuhusu sentensi na
vifungu atakavyotunga akitumia
nomino za vitenzi-jina na kuvijadili
na wenzake.
(b) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kujifunza kuhusu
nomino za vitenzi-jina shuleni na
nyumbani.
(c) Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapofaulu
34
Kimeidhinishwa na KICD
kukamilisha kazi zake za darasa kwa
wakati unaofaa. Pia, mwanafunzi
anapovitunza vifaa vyake vya
ujifunzaji pamoja na vifaa vya
kidijitali kama vile tarakilishi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada ambazo
zinashughulikia nomino za vitenzi-
jina katika sarufi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anaweza kuwahamasisha
wanajamii kuhusu nomino za vitenzi-
jina katika shughuli zao za kila siku
hivyo kuyaboresha mawasiliano yao.
Namna ya kuwashughulikia
wanafunzi wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye matatizo ya
kusikia watumie vifaa vya kuwasaidia
kuwasikia wenzao wanapotunga
sentensi wakitumia nomino za
vitenzi-jina. Wasio na uwezo wa
kusikia kabisa wanaweza kutumia
lugha ishara au wawasiliane na
wenzao kupitia kwa maandishi.
Mfasiri wa lugha ishara anaweza
kushirikishwa hapa.
Wanafunzi wenye matatizo ya
kuzungumza wanaweza kuhimizwa
kutumia lugha ishara.
Walio na ugumu wa kuona wanaweza
kuketi karibu na ubao na wasioona
kabisa watumie mashine za breli.
Wasiofahamu kwa urahisi
wanayofundishwa wapewe maelezo
zaidi na kutengewa muda zaidi baada
ya masomo jioni. Walio na uwezo
wa kung’amua wanayofundishwa
kwa wepesi na haraka washirikishwe
katika shughuli za ziada za kutunga
sentensi na vifungu wakitumia
nomino za vitenzi-jina.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 23-24)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu nomino za
vitenzi-jina ili kufahamu zaidi kuhusu
shughuli za ujifunzaji utakazowahusisha
wanafunzi. Vilevile,
Andaa kadi zilizoandikwa mifano
ya nomino za vitenzi-jina.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumika.
Mfahamishe mapema mfasiri wa
lugha ishara ili ajiandae ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 23
2. Breli
3. Kadi zilizoandikwa mifano ya
nomino za vitenzi-jina
4. Chati zilizoandikwa sentensi
zenye nomino za vitenzi-jina
vilivyopigiwa mistari.
Utaratibu wa shughuli za ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza
wanafunzi wataje mambo wanayopenda
kufanya wakiwa shuleni na nyumbani.
Majibu tarajiwa: kusoma, kucheza,
kulala, kula, kuoga, kuosha vyombo,
kufua nguo, kuandika, kuchora, kufuta
ubao n.k.
4.2.1 Nomino za vitenzi-jina
35
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya 1, wanafunzi
wajikumbushe waliyojifunza katika
gredi ya nne kuhusu vitenzi-jina.
Wataje mifano ya vitenzi-jina
wanavyokumbuka.
Mwelekeze mwanafunzi asome
kifungu kifupi kilicho kitabuni
mwake kisha atambue vitenzi-jina
vilivyotumika. Majibu tarajiwa:
kuchomeka, kutoa, kufundishwa,
kuharibika, kuumia, kuhamasishwa.
Wanafunzi wajadiliane kuhusu jinsi
wanavyoweza kukabiliana na janga la
moto shuleni mwao iwapo litatokea.
Tathmini maelezo ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi kucheza mchezo wa
kuchopoa kadi zilizoandikwa nomino
za vitenzi-jina kutoka kwenye kapu
la maneno. Unaweza kuandaa kadi
hizi na kuziweka ndani ya kapu au
chombo chochote kile ili wanafunzi
wazichopoe kwa urahisi.
Mwanafunzi mmoja achopoe kadi
moja kutoka kapuni na wenzake
watunge sentensi sahihi kwa kutumia
nomino hiyo. Mwanafunzi mwingine
aiandike sentensi iliyotungwa ubaoni
na apigie mstari kitenzi-jina ili
wenzake watathmini na kujifunza.
Mchezo huu uendelee hadi kadi
zote kapuni zichopolewe. Tathmini
sentensi za wanafunzi pamoja na
maandishi yao ubaoni. Hakikisha
ni sahihi kisarufi.Wanafunzi
washirikishwe kwa zamu.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada. Majibu
tarajiwa: Vitenzi vinavyohusu
huduma ya kwanza: dunga, safisha,
tibu, funga n.k. Vitenzi-jina kutokana
na vitenzi hivyo: kudunga, kusafisha,
kutibu, kufunga n.k. Mifano ya
sentensi:
a) Kudunga huku hakufai.
b) Kusafisha kuzuri husaidia
kidonda kupona haraka. c) Kutibu
kwake kuliwafurahisha wagonjwa.
d) Kufunga huku kumefanya jeraha
lipone haraka.
Tathmini kazi ya mwanafunzi.
Hakikisha anawasomea wenzake
darasani ili wajifunze.
Shughuli ya nje ya darasa
Kwa ushirikiano na viongozi wa eneo
lenu, waongoze wanafunzi kuunda
kambi ya kutoa huduma ya kwanza
katika eneo lililo karibu na shule yenu.
Wanafunzi watumie fursa hii
kuwafundisha wanajamii kuhusu njia
mbalimbali walizofundishwa za kutoa
huduma ya kwanza. Wataalamu wa kutoa
huduma ya kwanza wawafundishe njia
nyingine zaidi za kutoa huduma ya
kwanza, Wanafunzi watumie vifaa vya
kidijitali kurekodi hatua mbalimbali za
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua nomino za
vitenzi-jina kwenye matini.
2. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutumia nomino za
vitenzi-jina kutunga sentensi na
vifungu sahihi.
36
Kimeidhinishwa na KICD
kutoa huduma ya kwanza. Shughuli
hii itaimarisha ujuzi na maarifa ya
wanafunzi pamoja na wanajamii kuhusu
utoaji wa huduma ya kwanza ili
kuyaokoa maisha.
Pia, wanafunzi wataweza kutangamana
na wanajamii hivyo kuboresha
mawasiliano yao.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Tathmini majibu ya mwanafunzi.
Mifano: Kuosha jeraha kwa maji safi
na kupaka dawa, kupeana dawa za
kupunguza maumivu, kufunga jeraha
kwa kipande cha nguo safi au bendeji
n.k.
2. Tathmini majibu ya mwanafunzi.
Mfano: Kamusi hutoa maana na
matumizi ya maneno mbalimbali
hivyo kukuza msamiati wa
mwanafunzi katika mawasiliano.
3. Tathmini insha ambayo mwanafunzi
ataandika. Insha ilenge kisa chochote
kinachohusu huduma ya kwanza.
Insha itumie lugha sanifu na
sahihi pamoja na kufuata mtindo
na muundo wa kuandika insha ya
masimulizi.
4. Tathmini sentensi za mwanafunzi.
Mifano:
a) Marashi yaliyonunuliwa yanavutia.
b) Chumvi ilikuwa nyingi kwenye
mchuzi.
c) Mafuta yalitosha kupika mandazi.
d) Damu ilimtiririka alipokatwa na
bati.
e) Chai ya maziwa huwa tamu.
5. Tathmini kifungu atakachotunga
mwanafunzi. Sharti kitumie nomino
za vitenzi-jina na zipigiwe mistari.
Pia, atumie lugha sanifu na sahihi.
37
Kimeidhinishwa na KICD
MAPAMBO
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 25-41)
Utangulizi
Mapambo ni vitu ambavyo vinavaliwa au
kupakwa mwilini ili kumrembesha mtu
na kumfanya avutie machoni pa wengine
wanapomtazama. Mtu hupendeza
anapovalia mapambo. Watu wengi
hupenda kuvalia mapambo wanapoenda
kwenye sherehe mbalimbali.
Jamii mbalimbali huvalia mapambo
tofautitofauti. Kila mtu anafaa
kuyaheshimu mapambo ya jamii
nyingine ili kukuza uraia na utangamano
mwema. Sote tujivunie mapambo ya
jamii zetu. Ndiyo fahari ya jamii zetu.
Mifano ya mapambo ni kama vile: herini,
vipuli, vikuku, shanga, vipini n.k.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na Kuzungumza
(Matamshi bora - vitendawili), Kusoma
kwa ufahamu (Kifungu cha hadithi),
Kuandika (Kuandika kwa tarakilishi -
uchapaji), Sarufi (Nomino za makundi,
nomino ambata, nomino za dhahania
na uakifishi kwa kutumia herufi kubwa,
koma, kikomo na kiulizi).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 25-27)
Matamshi bora
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vitendawili vya
suala lengwa vyenye sauti
zinazokaribiana kwenye orodha.
b) Kutamka maneno yenye
sauti zinazokaribiana katika
vitendawili lengwa.
c) Kutega na kutegua vitendawili
vyenye sauti zinazokaribiana ili
kujenga matamshi bora.
d) Kuchangamkia matumizi
ya vitendawili vyenye sauti
zinazokaribiana kama njia
ya kujenga utamkaji bora wa
maneno.
Maswali dadisi
1. Maana ya kitendawili ni ipi?
2. Je, unajua vitendawili gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Mwanafunzi anaposhiriki katika
38
Kimeidhinishwa na KICD
kutega na kutegua vitendawili kwenye
vikundi anakuza ushirikiano pamoja
na kuboresha mawasiliano yake.
(b) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Unakuzwa mwanafunzi anapofikiri
majibu ya vitendawili mbalimbali
vinavyohusu mapambo.
(c) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutega na kutegua vitendawili kwa
usahihi. Pia, mwanafunzi anapoweza
kutamka kwa usahihi sauti ambazo
zinakaribiana kimatamshi.
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Umoja wa kijamii
Suala mtambuko hili linakuzwa
mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake katika vikundi kutega
na kutegua vitendawili pamoja na
kujadili kuhusu mapambo ya jamii
mbalimbali.
(b) Stadi za maisha
Zinakuzwa kutokana na maudhui
katika vitendawili mbalimbali vya
mapambo ambavyo mwanafunzi
atatega na kutegua. Kutokana na
kufahamu mapambo mbalimbali,
mwanafunzi anaweza kufuata
mkondo wa kazi ya kuwa mpambe
au muuza mapambo mbalimbali kote
nchini na hata ulimwenguni.
(c) Uraia
Unakuzwa mwanafunzi
anapothamini na kuheshimu
mapambo yanayovaliwa na watu
kutoka jamii mbalimbali nchini. Pia,
uraia unaweza kukuzwa kutokana
na maudhui ya vitendawili ambavyo
mwanafunzi atatega na kutegua.
Uhusiano na maadili
(a) Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
wanapotoa majibu ya vitendawili
mbalimbali na kujadili mapambo
mbalimbali katika vikundi. Pia,
kwa kutumia lugha ya adabu katika
mawasiliano yao.
(b) Umoja na amani
Wanafunzi wanapofanya shughuli
mbalimbali katika vikundi vyao
kwa amani bila kuzua fujo yoyote.
Kushirikiana kwa umoja katika
vikundi na darasani kwa jumla.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya huwa yanashughulikia
vitendawili mbalimbali kwa
kuzingatia maudhui tofautitofauti.
2. Sayansi Kimu
Somo hili huwa linaangazia mapambo
mbalimbali na jinsi ya kuyatengeneza,
kuyapanga na kuyavaa.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anatarajiwa kukabiliana
na masuala mbalimbali yanayohitaji
uwazaji wa kina katika jamii na katika
mawasiliano.
Mwanafunzi anaweza kuwafundisha
wanajamii kuhusu mapambo yao
mbalimbali pamoja na umuhimu na
dhamana yao.
39
Kimeidhinishwa na KICD
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye matatizo ya kusikia
watumie vifaa vya kuwasaidia kusikia
wenzao wanapotega na kutegua
vitendawili kuhusu mapambo.
Wanafunzi wenye matatizo
ya kuzungumza wanaweza
kuhimizwa kutumia lugha
ishara. Mfasiri wa lugha ishara
ashirikishwe iwapo huifahamu
lugha hiyo.
Walio na ugumu wa kuona wanaweza
kuketi karibu na ubao na wasioona
kabisa watumie mashine za breli.
Wasioweza kufahamu kwa urahisi
wanayofundishwa wapewe maelezo
zaidi na kutengewa muda zaidi baada
ya masomo jioni. Walio na uwezo
wa kung’amua wanayofundishwa
kwa wepesi na haraka washirikishwe
katika shughuli za ziada.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 25
2. Michoro au picha za mapambo
mbalimbali
3. Mapambo halisi
4. Breli, mfasiri wa lugha ishara
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa shughuli ya
1 kwa kuwakumbusha wanafunzi
walichosoma katika gredi ya nne
kuhusu vitendawili. Waongoze
wanafunzi kuyarejelea na kuyajibu
maswali dadisi husika.
Wapange wanafunzi kwenye vikundi
kulingana na idadi yao na uwezo wao
kisha waelekeze kutambua vitendawili
vyenye sauti f/v, l/r, /s/z, th/dh kutoka
kwenye orodha waliyopewa vitabuni
mwao. Watumie michoro waliyopewa
kutambua majibu ya vitendawili hivyo.
Watambue vitendawili ambavyo majibu
yao ni majina ya mapambo mbalimbali.
Majibu tarajiwa: b) Nikimvaa hunifaa
na kunifanya mfalme taji. d) Kina
uchungu kinapotiwa mwilini lakini raia
hupendeza chale/nembo. f) Ziwapo
siri za wawili hudumu daima pete.
g) Unga wangu nauthamini, hunipa
dhana mpya na kunifanya upya
kanta. h) Niguse nitikise, bila shaka
utashangilia kwa uzuri– njuga.
Unaweza kuwakumbusha wanafunzi
kuhusu utamkaji kwa kutamka sauti f/v,
l/r, /s/z, th/dh kwa usahihi wakikusikiliza
kwa makini kisha watamke baada yako
kwa haraka. Wazingatie matamshi sahihi
kutoka kwa vitendawili walivyoteua.
Hakikisha kila mwanafunzi anaweza
kutamka sauti hizo kwa usahihi.
1.1 Vitendawili
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 25-27)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tayarisha chati yenye michoro ya
mapambo mbalimbali. Pia,
Tafuta mapambo halisi mbalimbali.
Hakikisha una video inayoonyesha
mapambo mbalimbali katika harusi
(video imeambatanishwa na kitabu
hiki).
Kwa kutumia rununu, piga
picha mapambo mbalimbali ili
uwaonyeshe wanafunzi.
Fanya utafiti kuhusu mapambo ya
jamii mbalimbali.
40
Kimeidhinishwa na KICD
Waelekeze wanafunzi kujadili majibu ya
vitendawili walivyoteua. Wabaini kuwa
majibu hayo ni majina ya mapambo.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi viwili
kisha uwaelekeze kucheza mchezo
wa kutega na kutegua vitendawili
vyenye sauti f/v, l/r, /s/z, th/dh na
vinavyohusu mapambo. Mfano:
Kikundi cha kwanza - Kitendawili!...
Tega!...Nivaliwapo kiunoni
ninafaa ______. (sauti f/v). Jibu
tarajiwa: mshipi. Kikundi cha pili -
Kitendawili!...Tega!... Kamba yakaa
vizuri sana shingoni______. (sauti
s/z). Jibu tarajiwa: mkufu. Tathmini
vitendawili na majibu ya kila kikundi.
Zoezi hili litawawezesha wanafunzi
kupata ujasiri wa kuongea mbele ya
watu, kujiamini pamoja na kuboresha
mawasiliano yao.
Hitimisha kipindi kwa kuwaelekeza
wanafunzi namna ya kufanya kazi ya
ziada. Tathmini kufanyika kwa kazi ya
ziada kabla ya kipindi kingine kuanza.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada
1. a) mkufu b) mshipi c) saa
d) marashi
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutaja na kutambua
mapambo mbalimbali.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua na kuunda
vitendawili vya mapambo vyenye
sauti f/v, l/r, s/z na th/dh.
2. Sikiliza kwa makini sana iwapo
mwanafunzi anaweza kutamka sauti
f/v, l/r, s/z na th/dh kwa usahihi
katika vitendawili vya mapambo na
umtathmini.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 27-29)
Kusoma kwa ufahamu
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa mapambo
uliotumiwa katika kifungu.
b) Kueleza maana za msamiati
mbalimbali wa mapambo.
c) Kusoma kifungu cha hadithi ili
kupata ujumbe.
d) Kuonyesha uelewa wa hadithi kwa
kutoa muhtasari na kujibu maswali.
e) Kuonea fahari kusoma hadithi
kuhusu mapambo na kujibu
maswali.
Maswali dadisi
1. Mapambo ni nini? Unajua mifano
gani ya mapambo?
2. Kwa nini ni muhimu kusoma
kuhusu mapambo?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposoma kifungu kwa sauti na
kwa usahihi na kuwaeleza wenzake
kuhusu alichosoma. Kutokana na
hili, mawasiliano ya mwanafunzi
yataboreka. Pia, kufanya shughuli
41
Kimeidhinishwa na KICD
fujo yoyote. Kila mwanafunzi anapewa
fursa ya kujibu.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazofunza
kuhusu vitendawili mbalimbali.
2. Sayansi Kimu
Somo hili hufunza kuhusu mapambo
mbalimbali na jinsi ya kuyatengeneza
na hata kuyatunza au kuyahifadhi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake
shuleni na katika jamii kuhusu umuhimu
wa kukuza utamaduni wa kusoma
miongoni mwao. Hili litaboresha
mawasiliano kati ya wanajamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona watumie breli kusoma
au wakusikilize au wawasikilize
wenzao wakisoma kifungu husika.
Wanafunzi wenye changamoto za
kitabia wapewe ushauri nasaha na
mwalimu. Pia, mwalimu anaweza
kutunga sheria za kufuatwa na
wanafunzi hawa ili wasiwasumbue
wenzao wanaposoma darasani.
Wanafunzi walio na matatizo ya
kusoma wapatiwe kauli fupifupi
za kusoma ili kukuza uzoefu wao
wa kusoma. Mwalimu anaweza
kuwa kielelezo bora cha usomaji
huo.
katika vikundi kutaleta ushirikiano
na utangamano mwema.
(b) Kufikiri kwa kina
Mwanafunzi anapofikiri na kujibu
maswali kutokana na kifungu
alichosoma anakuwa na uwezo wa
kutatua matatizo katika jamii kwa
kutafuta suluhu.
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Elimu kwa maendeleo endelevu
Inakuzwa mwanafunzi anapotumia
msamiati wa mapambo mbalimbali
aliyojifunza kupitia kwa vifungu katika
mawasiliano yake ya kila siku katika
jamii.
(b) Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapoweza
kufahamu mapambo mbalimbali.
Ufahamu huu unaweza kutumika
kujikimu kimaisha baadaye kwa kuwa
muuzaji wa mapambo au hata mtu
anayewashauri na kuwapamba watu
wengine kwa malipo.
Uhusiano na maadili
(a) Heshima na umoja
Haya yanakuzwa anaposhirikiana
na wenzake katika vikundi na
kuyaheshimu maoni yao. Pia, kupitia
kwa kuwasikiliza wengine wakisoma
kifungu bila kuwatatiza.
(b) Upendo na amani
Unakuzwa mwanafunzi anapowasaidia
ama anaposhirikiana na wenzake katika
kujibu maswali ya kifungu bila kuzua
42
Kimeidhinishwa na KICD
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 27-28)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Rejelea maswali dadisi husika ili
upate ujumbe wa kufunza darasani.
Hakikisha umesoma kifungu husika
kabla ya kipindi ili kuweza kutafuta
na kuelewa maana za misamiati
mipya iliyotumika.
Unaweza kuandaa michoro ya
mapambo mbalimbali kwenye
chati. Pia, unaweza kutumia picha
za mapambo hayo.
Kusanya mapambo halisi tofauti ili
kuboresha uelewa wa wanafunzi.
Hakikisha video iliyoambatanishwa
na kitabu hiki inaweza kuonyeshwa
kwa wanafunzi darasani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 27
2. Gazeti la Kiswahili
3. Breli
4. Video ya harusi
5. Tarakilishi na intaneti
6. Mapambo halisi kama vile pete,
bangili, mkufu n.k.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwaelekeza
wanafunzi wajadili mchoro ulio
kitabuni mwao. Wanafunzi waelezane
yanayoendelea kwenye mchoro huo. Jibu
tarajiwa: Mchoro ni wa maharusi pamoja
na wasimamizi wao na wazazi wa bi
harusi.
Katika shughuli ya 1, waongoze
wanafunzi kusoma kimyakimya
na kwa makini kifungu kilicho
vitabuni mwao. Baada ya kusoma
huku, teua mwanafunzi mmoja
asome tena kifungu hicho kwa sauti
huku wenzake wakimsikiliza kwa
makini. Hakikisha mwanafunzi huyo
anazingatia matamshi bora na sahihi
na anasoma kwa sauti ya kusikika na
wanafunzi wote.
Waongoze wanafunzi kutoa
muhtasari wa kifungu walichosoma
ili kudhihirisha uelewa wao.
Shughuli hii itaboresha mawasiliano
yao na hata kukuza ujasiri wao
wa kuzungumza mbele ya watu.
Waelekeze wanafunzi kutambua
mapambo yaliyovaliwa na watu
walio kwenye michoro waliyotazama.
Majibu tarajiwa: vikuba, mikufu, tai,
saa, taji, shanga, bangili, vipuli, pete,
utepe n.k.
Hatimaye, waelekeze wanafunzi
kueleza maana za msamiati wa
mapambo uliotumiwa katika
kifungu walichosoma. Wanafunzi
wanaweza kutumia kamusi zao za
Kiswahili kutafuta maana. Waongoze
wanafunzi kutambua kuwa pambo
lililoonyesha kilele cha harusi katika
kifungu walichosoma ni pete.
Waongoze wanafunzi kujadiliana
kuhusu mapambo wanayopendelea
kuvalia wanapoenda kwenye sherehe.
Mwalimu atathmini maelezo ya
wanafunzi.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi kusakura mtandaoni au
kwenye gazeti la Kiswahili matini
yoyote inayohusu mapambo.
Wanafunzi wasome matini hiyo na
2.1 Kifungu cha hadithi
43
Kimeidhinishwa na KICD
kujadili ujumbe uliopo. Hii itaboresha
mawasiliano, ushirikiano, uwazaji
wa kina pamoja na uwezo wao wa
kutumia vifaa vya kidijitali. Pia,
hakikisha wanataja kwa usahihi
sehemu ambazo mapambo husika
huvaliwa mwilini.
Waongoze wanafunzi katika shughuli
ya 3 kujadili mapambo mbalimbali
yanayovaliwa na watu katika jamii
mbalimbali.
Hitimisha kipindi kwa kumhimiza
kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada
akisaidiwa na mlezi wake.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada:
1 a) hina –vidoleni b) ushanga
shingoni c) kipuli sikioni d) ndonya
mdomoni e) kishaufu puani
f) kipini puani. Tathmini iwapo
mwanafunzi alijadiliana na mzazi
au mlezi wake kuhusu mapambo
yanayovaliwa na watu katika familia
yake kwa kumwuliza awaeleze
wenzake darasani.
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 29-31)
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sehemu mbalimbali za
tarakilishi zinazotumika kupigia
chapa.
b) Kutumia tarakilishi ili kujenga
maarifa ya kidijitali.
c) Kujenga mazoea ya kutumia
tarakilishi kuandika na kuhifadhi
maandishi.
Maswali dadisi
1. Unajua sehemu gani za tarakilishi?
2. Umuhimu wa tarakilishi ni upi?
3. Ni hatua gani zinafaa kufuatwa
tunapotumia tarakilishi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kufanya
kazi za vikundi za kutaja na kujadili
sehemu za tarakilishi na kueleza
matumizi yazo.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia tarakilishi kupiga chapa
na kuhifadhi kazi yake.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapotumia tarakilishi kupiga chapa
maandishi akiwa nje ya darasa kama
vile maktabani au nyumbani.
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua msamiati wa
mapambo uliotumika kwenye
kifungu ili kuimarisha ufahamu.
2. Vilevile, tathmini ikiwa
mwanafunzi ana uwezo wa kueleza
maana za msamiati mbalimbali wa
mapambo.
3. Pia, tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kusoma kwa mfululizo na
kwa usahihi na kuelewa ujumbe
wa hadithi na kuweza kutoa
muhtasari wake.
44
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya maendeleo endelevu
Hii inakuzwa mwanafunzi
anapotumia tarakilishi kukuza ujuzi
wake wa kiteknolojia ili kufanikisha
uandishi na mawasiliano kwa jumla.
Uhusiano na maadili
(a) Umoja, amani na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa umoja na amani bila
kuzua ghasia au fujo. Pia, kupitia
kwa kutumia tarakilishi kwa pamoja
bila kuwanyima wenzake fursa ya
kuitumia.
(b) Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapokuwa
makini akitumia vifaa vya kidijitali
bila kuviharibu wala kuvichafua.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza
Somo hili lina mada inayofunza
kuhusu matumizi ya vifaa vya
kidijitali katika mawasiliano.
2. Sayansi na Teknolojia
Somo hili linafunza kuhusu jinsi
ya kutumia vifaa mbalimbali vya
kidijitali, jinsi ya kuvihifadhi na hata
kuvitengeneza vinapopata hitilafu
yoyote.
Pia, masomo mengine yanahusisha
matumizi ya vifaa vya kiteknolojia.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atapata uwezo wa kutumia
vifaa vya kidijitali shuleni na nyumbani
katika kufanyia mazoezi ya kuandika
akiwa na wenzake. Atawasaidia wanajamii
wenzake kuboresha mawasiliano yao
kupitia kwa matumizi ya vifaa vya kisasa
vya kidijitali.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Iwapo kuna wanafunzi ambao
hawana uwezo wa kuona, hakikisha
wana tarakilishi zinazotoa sauti
mtu anapopiga chapa au breli za
kuwasaidia kusoma na kuelewa
yanayofunzwa.
Wanafunzi walio na matatizo
mbalimbali ya kiafya au kisaikolojia
washughulikiwe vilivyo kadri ya
uwezo wako.
Wanafunzi ambao wanangamua
wanayofundishwa kwa wepesi na
haraka wapewe mazoezi zaidi ya
kuandika vifungu kwenye tarakilishi.
Wanafunzi wasioweza kungamua
wanayofundishwa kwa haraka
watengewe muda zaidi baada ya
masomo wa kufanya mazoezi ya
kutumia tarakilishi.
3.1 Kuandika kwa tarakilishi:
Uchapaji
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 29-31)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Andaa vifaa halisi kama vile
tarakilishi, vipakatalishi au
tabuleti ambavyo utatumia katika
somo hili. Hakikisha hali yao ni
nzuri.
Panga darasa vizuri ili uwe na
nafasi ya kutosha pamoja na meza
45
Kimeidhinishwa na KICD
ya kuwekea vifaa vyako.
Hakikisha kuna nguvu za umeme
au nishati za kutosha pamoja na
intaneti.
Unaweza kurekodi shairi
lolote kwenye rununu yako ili
wanafunzi walisikilize darasani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 29
2. Tabuleti, vipakatalishi, tarakilishi
3. Mfasiri wa lugha ishara, breli
4. Rekodi ya shairi lililokaririwa.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwauliza
wanafunzi iwapo wanakumbuka sehemu
za tarakilishi walizojifunza katika gredi
ya nne. Wanafunzi wataje sehemu hizo.
Katika shughuli ya 1, waelekeze
wanafunzi kujadili mchoro ulio
kitabuni mwao na kutaja sehemu
zilizoonyeshwa kwa nambari.
Majibu tarajiwa: mchoro ni wa
tarakilishi. Sehemu zilizoonyeshwa
kwa nambari ni: 1. kiwambo/mulishi/
skrini 2. kicharazio/bodidota/kiibodi
3. kitengo kikuu cha uchakataji
4. kipanya. Waelekeze wanafunzi
kujadili matumizi ya sehemu
walizotambua.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na uwezo wao na idadi ya tarakilishi
halisi unazoweza kupata. Wanafunzi
waruhusiwe kugusa na kutambua
sehemu mbalimbali za tarakilishi
hizo.
Waelekeze kutunga sentensi
wakitumia mapambo mbalimbali
kisha kila mwanafunzi afanye
mazoezi ya kuziandika sentensi
hizo kwenye tarakilishi. Mwalimu
azunguke katika kila kikundi
kuhakikisha kila mwanafunzi
anapiga chapa vizuri na kwa usahihi.
Wanafunzi wenye matatizo ya kupiga
chapa watengewe muda zaidi baada
ya masomo jioni ili wafanye mazoezi
zaidi na watiwe moyo.
Waongoze wanafunzi kufanya shughuli
ya 3 kwa kulisoma shairi walilopewa
vitabuni mwao na kutambua sehemu
mbalimbali za tarakilishi zilizotajwa.
Hakikisha kila mwanafunzi amelisoma
shairi husika. Majibu tarajiwa: kiibodi,
kipanya, kiwambo.
Pia, watambue mapambo yaliyotajwa
kwenye shairi hilo na kuyatumia
kutunga sentensi sahihi. Tathmini
sentensi za mwanafunzi. Hakikisha
zimetumia mapambo yaliyotajwa
kwenye shairi pekee. Mifano ya
sentensi: 1. Mwalimu amevaa herini
na pete. 2. Mama amenunua shanga
nzuri.
Hatimaye, kila mwanafunzi aliandike
shairi alilosoma kwenye tarakilishi na
kulihifadhi kwenye faili kwa jina lake
na kukutumia mtandaoni ili utathmini
uandishi wake.
Mhimize mwanafunzi afanye kazi
ya ziada akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake.Tathmini kifungu
atakachotunga mwanafunzi na
kukipiga chapa. Hakikisha kifungu
kinahusu sherehe ambayo amewahi
kuhudhuria pamoja na mapambo
mbalimbali aliyoona.
46
Kimeidhinishwa na KICD
4.1 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 31-33)
Aina za nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino za makundi
katika sentensi ili kuzibainisha.
b) Kueleza nomino za makundi kwa
kutoa mifano mwafaka.
c) Kutumia nomino za makundi kwa
usahihi katika sentensi.
d) Kuonea fahari matumizi ya
nomino za makundi katika
miktadha mbalimbali.
Maswali dadisi
1. Je, maana ya nomino ni ipi?
2. Unajua maneno gani yanayotumiwa
kutaja makundi ya watu na vitu?
3. Je, nomino za makundi hutumiwa
vipi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuyajibu maswali kuhusu nomino za
makundi kwa usahihi. Pia, kunakuzwa
mwanafunzi anapoweza kutambua
nomino za makundi kwa usahihi.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutambua na kutumia
nomino za makundi ili kuboresha
mawasiliano.
(c) Hamu ya kuendelea kujifunza
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anaporejelea maswali dadisi na
kutaka kujifunza zaidi kuhusu
nomino za makundi.
(d) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutumia vifaa vya
kidijitali kupiga chapa kwa kutunga
sentensi zenye nomino za makundi.
Pia, ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia mtandao kuwatumia
wenzake pamoja nawe kifungu
alichotunga.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Stadi hizi zinakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake katika
shughuli za vikundi na kujifunza
ukakamavu na kujiamini. Pia,
ufahamu wa matumizi ya vifaa
vya kidijitali unaweza kumpa
mwanafunzi ajira baada ya masomo
pamoja na kumwezesha kufahamu
maendeleo ya nchi yake na nchi
nyingine.
Uraia
Unakuzwa mwanafunzi anapojiunga
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua kwa usahihi
sehemu mbalimbali za tarakilishi
zinazotumiwa kupigia chapa.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia tarakilishi kuandika na
kuhifadhi maandishi kwenye faili,
kuyahariri kisha kuyatuma kwa
wenzake na mwalimu kwa kutumia
mtandao.
47
Kimeidhinishwa na KICD
na vikundi vya wanafunzi kutoka
maeneo na jamii mbalimbali
kiuhalisia au hata mtandaoni.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika shughuli za vikundi. Pia, kupitia
kwa matumizi ya lugha ya adabu.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutambua nomino za makundi
na kuzitungia sentensi bila kuzua fujo.
Uwajibikaji
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapokamilisha kazi yake kwa wakati
ufaao. Pia, unakuzwa mwanafunzi
anapovitunza vifaa vyake vya
ujifunzaji na kutoviharibu.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazoangazia
nomino za makundi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atumie lugha kwa ustadi
katika shughuli mbalimbali za kijamii.
Mwanafunzi awaeleze wanajamii
kuhusu nomino za makundi ili
kuboresha lugha yao na mawasiliano
yao.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona wanaweza kutumia breli
kusoma kuhusu nomino za
makundi na kuandika kazi zao.
4.1.1 Nomino za makundi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 31-33)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Unaweza kujifunza wimbo kuhusu nomino
za makundi na kuwaimbia wanafunzi ili
kutanguliza somo hili. Vilevile,
Andaa picha za nomino za makundi
mbalimbali.
Kusanya vifaa halisi vya nomino
za makundi na uvilete darasani.
Hivi vitasaidia katika ufunzaji wa
nomino za makundi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 31
2. Picha za nomino za makundi
3. Vifaa halisi vya nomino za makundi
4. Breli, mfasiri wa lugha ishara
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa shughuli ya
1 kwa kuwauliza wanafunzi iwapo
wanakumbuka nomino ambazo tayari
wamejifunza. Wataje nomino za pekee,
nomino za kawaida n.k.
Wanafunzi walio na matatizo ya
kuzungumza wanaweza kutumia
lugha ishara. Mfasiri wa lugha
ishara anaweza kushirikishwa.
Wanafunzi wasioweza kuelewa
wanayofundishwa kwa urahisi
wapewe muda zaidi wa ujifunzaji.
Wanaong’amua wanayofundishwa
haraka wapewe mazoezi zaidi
kuhusu nomino za makundi.
Wanafunzi wenye matatizo ya kiafya
au kisaikolojia washughulikiwe
vilivyo kulingana na uwezo wako ili
wasitatizike katika ujifunzaji.
48
Kimeidhinishwa na KICD
Waongoze wanafunzi kutaja majina
ya michoro iliyo vitabuni mwao
kisha watambue nomino za makundi
kutoka kwenye majina hayo. Majibu
tarajiwa: Nomino za makundi ni
mlolongo wa magari, chane ya ndizi
na bunda la noti. Baada ya utambuzi
wa nomino za makundi, mwanafunzi
azitumie kutunga sentensi sahihi.
Tathmini sentensi atakazotunga.
Katika shughuli ya 2, wanafunzi
wakiwa katika vikundi wajadili
maana ya nomino za makundi.
Waeleze kuwa nomino za makundi ni
nomino zinazotaja makundi ya watu
au vitu. Pia, huitwa nomino za jamii.
Waelekeze wataje mifano ya nomino
za makundi kama vile: genge la wezi,
kikoa cha waimbaji, baraza la wazee,
kundi la ng’ombe, tita la kuni, shungi
la nywele, shada la maua n.k.
Waongoze katika kutunga sentensi
wakitumia nomino za makundi
walizotaja. Tathmini sentensi ambazo
kila mmoja atatunga.
Mifano: 1. Bibi harusi alibeba shada
la maua. 2. Genge la wezi lilikamatwa
na kigaro cha polisi baada ya
kuiba mikufu ya dhahabu. 3. Rais
alihutubia umati wa watu. Wanafunzi
watathmini kazi za wenzao.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 3 kwa kukamilisha
sentensi zilizo kitabuni mwake kwa
kutumia nomino za makundi sahihi.
Tathmini kazi ya mwanafunzi.
Majibu tarajiwa: 1. mlolongo
2. bunda 3. mkungu
4. korija 5. genge 6. tita 7. doti
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua nomino za makundi
katika sentensi.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi wa
kutaja mifano mwafaka ya nomino
za makundi na kuzitungia sentensi
sahihi.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuipiga chapa kazi yake
na kuituma mtandaoni.
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 33-35)
Aina za nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino ambata katika
matini ili kuzitofautisha na aina
nyingine za nomino.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Tathmini sentensi
atakazotunga mwanafunzi na
kukutumia mtandaoni. Mifano
ya sentensi: a) Thurea ya nyota
ilionekana juu angani. b) Halaiki ya
watu ilifika shereheni kwa mapambo
teule. c) Pete yangu ilipotea pamoja na
kicha cha funguo. d) Mama aliyevalia
ushanga alinunua kishazi cha samaki.
e) Kikuba kilifungwa kwenye shungi la
nywele.
49
Kimeidhinishwa na KICD
b) Kutumia nomino ambata kwa
usahihi katika sentensi ili
kuimarisha mawasiliano.
c) Kuonea fahari matumizi ya nomino
ambata katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, nomino ni nini?
2. Je, unajua nomino gani ambazo
zinaweza kuunganishwa kuunda
nomino moja?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Hamu ya kuendelea kujifunza
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kujifunza mengi
kuhusu nomino ambata akiwa
shuleni na nyumbani.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili kuhusu nomino
ambata na kuzitofautisha na aina
nyingine za nomino.
(c) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutambua nomino ambata na
kuzitofautisha na nomino nyingine.
Pia, anapoweza kutunga kifungu
sahihi akitumia nomino ambata na
kuwasomea wenzake darasani na hata
nyumbani.
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Uraia
Huu unaweza kukuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
shughuli mbalimbali za vikundi.
Utangamano wa wanafunzi kutoka
maeneo mbalimbali kunaleta
kuthamini kila mtu.
(b) Stadi za maisha
Stadi hizi zinakuzwa mwanafunzi
anapojifunza kuhusu nomino ambata
na kuweza kuzitumia maishani katika
mawasiliano ya kila siku.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kufanya kazi kwa pamoja na
kwa kuheshimiana. Maoni ya kila
mwanafunzi yanaheshimiwa. Pia,
mwanafunzi anapotumia lugha ya
adabu.
Uwajibikaji
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapofanya kazi aliyopewa na
mwalimu na kuikamilisha kwa
wakati unaofaa. Pia, mwanafunzi
anapotunza vifaa vyake vya ujifunzaji.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapofanya kazi na wenzake katika
vikundi bila kuzua vurugu yoyote.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazohusu
nomino ambata.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapojifunza kuhusu nomino
ambata ataweza kuwahamasisha wenzake
shuleni na nyumbani kuhusu mawasiliano
yanayozingatia kanuni za sarufi.
50
Kimeidhinishwa na KICD
4.2.1 Nomino ambata
2. Kadi zilizoandikwa nomino
mbalimbali zikiwemo nomino
ambata
3. Kamusi ya Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi
wataje mifano ya nomino ambazo tayari
wameshajifunza. Wanafunzi wataje mifano
ya nomino za pekee, nomino za kawaida na
nomino za makundi.
Katika shughuli ya 1, waelekeze
wanafunzi kuchunguza nomino
mbalimbali zilizo kwenye mti
maneno ulio kwenye vitabu vyao.
Wanafunzi wachague nomino
zilizoundwa kwa maneno mawili.
Majibu tarajiwa: mkemwenza,
mwananchi, pundamilia,
simbamarara, batamzinga,
askarikanzu, mbwamwitu,
mwanasesere. Wanafunzi
wajadiliane kuhusu maana za
nomino walizochagua. Waruhusu
watumie kamusi ya Kiswahili.
Waelekeze kufahamu kuwa nomino
walizochagua huitwa nomino
ambata. Nomino ambata ni nomino
zinazoundwa kwa maneno mawili
huru.
Katika shughuli ya 2, mwelekeze
mwanafunzi aandike mifano mitano
ya nomino ambata na kuzitungia
sentensi sahihi. Waongoze wanafunzi
katika kutathmini sentensi za wenzao.
Hakikisha nomino ambata na
sentensi za wanafunzi ni sahihi.
Wapange wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na uwezo wao
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 33-35)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Andaa kadi zilizoandikwa nomino
mbalimbali zikiwemo nomino ambata ili
wanafunzi wazitambue darasani. Pia,
Fanya utafiti kuhusu mifano zaidi
ya nomino ambata pamoja na
maneno yanayotumiwa kuziunda.
Hakikisha una kamusi ya Kiswahili
itakayokusaidia kuelewa maana za
nomino ambata usizozifahamu.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 33
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana uwezo
wa kuona wanaweza kutumia
breli kusoma na kuandikia. Pia,
wanaweza kusikiliza maelezo kuhusu
nomino ambata yakitolewa nawe au
wanafunzi wenzao.
Wanafunzi wenye matatizo ya kitabia
au kisaikolojia wanaweza kupewa
ushauri nasaha ili waweze kujifunza
pamoja na wenzao bila usumbufu
wowote.
Wanafunzi ambao hawana
uwezo wa kuelewa kwa urahisi
wanayofundishwa watengewe muda
zaidi wa kujifunza baada ya masomo
jioni. Wanafunzi walio na uwezo wa
kung’amua wanayofundishwa kwa
wepesi waongezewe shughuli zaidi
za kufanya au wawasaidie wenzao
wanaojifunza polepole.
51
Kimeidhinishwa na KICD
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino za dhahania
katika matini mbalimbali.
b) Kueleza nomino za dhahania kwa
kutoa mifano mwafaka.
c) Kutumia nomino za dhahania kwa
usahihi katika sentensi.
d) Kuonea fahari matumizi ya nomino
za dhahania katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, unafahamu mifano ipi ya nomino za
dhahania?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadiliana kuhusu nomino
za dhahania na kuzitungia sentensi
sahihi.
(b) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapokuwa
na ukakamavu wa kutunga sentensi
sahihi akitumia nomino za dhahania
na kuwasomea wenzake darasani na
nyumbani. Pia, anapoweza kutambua
nomino za dhahania kwa usahihi.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutumia vifaa vya
kidijitali kuucheza wimbo
ulioambatanishwa na kitabu hiki
unaohusu nomino za dhahania.
(d) Hamu ya kuendelea kujifunza
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoweza kujibu maswali dadisi na
kuendelea kujifunza kuhusu nomino
za dhahania darasani na nyumbani.
kisha uwaelekeze kutunga na
kuhariri vifungu vifupi wakitumia
nomino ambata mbalimbali
katika shughuli ya 3. Wanafunzi
wasikilize na kutathmini vifungu
vilivyoandikwa na wenzao na
kuvitathmini na kujifunza. Shughuli
hii itawapa wanafunzi ujasiri wa
kusimama na kuzungumza mbele
ya watu, watajiamini na kuboresha
mawasiliano yao.
Hitimisha somo kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
iliyo kitabuni mwao ukurasa 37.
Majibu tarajiwa: 1. mwananchi
2. mjamzito 3. mbwamwitu
4. duaradufu 5. batamzinga
6. malighafi
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua nomino ambata
katika matini na kuzitofautisha na
nomino nyingine.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuunda nomino ambata
kwa kutumia maneno mawili huru.
3. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kutunga sentensi sahihi
akitumia nomino ambata ili
kuimarisha mawasiliano yake.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 35-37)
Aina za nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
4.3 Sarufi
52
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Stadi hizi zinakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi na kupewa majukumu
hivyo basi kupata stadi ya uongozi
maishani.
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anatangamana na wanafunzi kutoka
maeneo mbalimbali na kushirikiana
nao katika kufanya kazi za vikundi.
Uhusiano na maadili
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapofanya kazi katika vikundi kwa
kushirikiana na wenzake kwa amani
bila kuzua fujo.
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapovitunza
vifaa vya kidijitali vilivyotumiwa
kuchezea wimbo kuhusu nomino
za dhahania. Pia, kupitia kwa
mwanafunzi kuvitunza vifaa vyake
vya ujifunzaji akiwa darasani na
nyumbani.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni yanayotolewa
na wenzake wanaposhirikiana kufanya
kazi katika vikundi mbalimbali. Pia,
mwanafunzi anapotumia lugha ya
adabu.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada
zinazofundisha dhana ya nomino za
dhahania.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 35-37)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Andaa chati ambazo zimeandikwa
nomino kadhaa zikiwemo
nomino za dhahania. Wanafunzi
watatumia chati hizi kuweza
4.3.1 Nomino za dhahania
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake
shuleni na nyumbani kuhusu maana na
mifano ya nomino za dhahania hivyo
kuboresha mawasiliano yao.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia breli kusoma na
kuandika maelezo kuhusu nomino za
dhahania. Pia, wanaweza kuwasikiliza
wenzao na mwalimu wanapotoa
maelezo kuhusu nomino za dhahania.
Wanafunzi wasioweza kuona mbali
wakae karibu na ubao na wale
wasioweza kuona karibu wakae mbali
kidogo na ubao.
Wanafunzi walio na matatizo ya
kifamilia au kisaikolojia wapewe
ushauri nasaha ili kuwawezesha
kujifunza bila usumbufu wowote.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia wanaweza kutumia vifaa vya
kuwasaidia kusikia. Mfasiri wa lugha
ishara anaweza kushirikishwa katika
somo hili. Pia, wanaweza kusoma
maelezo kuhusu nomino za dhahania
na kuandika majibu au maoni yao.
53
Kimeidhinishwa na KICD
kutambua nomino za dhahania
mbalimbali na kuzitofautisha na
aina nyingine za nomino.
Hakikisha rekodi ya wimbo ulio
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 36 unachezeka
ili uwachezee wanafunzi
darasani. Rekodi ya wimbo huo
imeambatanishwa na kitabu hiki.
Unaruhusiwa kuuimba wimbo
huo kwa mahadhi yako.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 35
2. Chati zilizoandikwa nomino
mbalimbali zikiwemo nomino za
dhahania
3. Rekodi ya wimbo.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza
wanafunzi wataje nomino mbalimbali
ambazo tayari wamejifunza.
Wanafunzi wataje mifano ya nomino
za pekee, nomino za kawaida, nomino
za makundi na nomino ambata.
Hakikisha mifano wanayotaja ni
sahihi.
Katika shughuli ya 1, waelekeze
wanafunzi wachunguze maneno
yaliyo kwenye mchoro ulio vitabuni
mwao. Wataje majina ya vitu
visivyoweza kuonekana kwa macho
wala kugusika. Majibu tarajiwa:
wivu, ukali, uchoyo, upepo, urafiki,
upole, hewa.
Wanafunzi wakiwa katika vikundi,
wataje mifano zaidi ya nomino za
dhahania.
Tathmini majadiliano yao.
Waelekeze wanafunzi kujadiliana
kuhusu maana ya nomino za
dhahania. Nomino za dhahania
hutaja vitu visivyoweza kuonekana
kwa macho wala kugusika ila
huhisiwa tu.
Katika shughuli ya 2, wanafunzi
wakusikilize kwa makini ukiimba
wimbo ulio kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 36. Waelekeze
waimbe wimbo huo kwa sauti na
kwa mahadhi mengine tofautitofauti.
Shughuli hii itakuza ubunifu na
kujiamini kwa wanafunzi.
Waulize wanafunzi watambue
nomino za dhahania zilizotumiwa
katika wimbo huo. Waziandike katika
madaftari yao kisha wazitungie
sentensi sahihi. Tathmini sentensi
za mwanafunzi. Hakikisha ni sahihi
na zimetumia nomino za dhahania
zilizotajwa kwenye wimbo walioimba.
Unaweza kuhitimisha somo hili kwa
kumpa mwanafunzi kazi ya ziada.
Tathmini kazi hii kabla ya kipindi
kitakachofuata. Hakikisha kuwa
sentensi zitakazotungwa ni sahihi
na zimetumia nomino za dhahania.
Majibu tarajiwa: a) Mbwa huyu ana
ukali mwingi. b) Bawabu aliyevalia tai
amepatwa na usingizi. c) Waliovalia
njuga miguuni walituonea wivu.
d) Uongo wako hautakufaa maishani.
e) Hewa safi hupatikana tunapoyatunza
mazingira.
54
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua nomino dhahania
kutoka kwenye matini mbalimbali
na kuzitofautisha na aina nyingine za
nomino.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi ana
uwezo wa kueleza maana ya nomino
za dhahania, kutaja mifano sahihi na
kuzitungia sentensi sahihi.
4.4 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 37-40)
Uakifishi
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua herufi kubwa, alama
ya koma, kikomo na kiulizi katika
maandishi.
b) Kutumia herufi kubwa, koma,
kikomo na kiulizi ifaavyo katika
maandishi.
c) Kufurahia matumizi ya herufi
kubwa, koma, kikomo na kiulizi
katika maandishi.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadiliana kuhusu alama za
uakifishi (koma, kikomo, kiulizi na
herufi kubwa). Matumizi sahihi ya
alama hizi za uakifishi yataboresha
mawasiliano.
(b) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunga sentensi zake sahihi na
kuziakifisha ifaavyo bila kunakili za
wenzake.
(c) Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuwasiliana na kuelewana vyema na
watu katika jamii.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Suala mtambuko hili linakuzwa
mwanafunzi anapotangamana na
wenzake wa asili mbalimbali katika
vikundi na kuthamini maoni yao.
Pia, anapotunga sentensi kuhusu
mapambo mbalimbali yanayovaliwa
na jamii mbalimbali atathamini jamii
nyingine.
Umoja wa kijamii na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kuakifisha sentensi kwa
usahihi bila kuzua ugomvi.
Stadi za maisha
Stadi hizi zinakuzwa mwanafunzi
anapotumia alama za uakifishi katika
uandishi kuboresha mawasiliano yake
ya kila siku katika jamii.
Uhusiano na madili
Upendo na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapofanya kazi na wenzake katika
vikundi bila kuzua fujo. Pia, kuwapa
wanafunzi wenzake fursa ya kutoa
maoni katika vikundi vyao.
55
Kimeidhinishwa na KICD
Uwajibikaji
Huu unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kufanya kazi aliyopewa na kuikamilisha
kwa muda unaofaa. Pia, anapotunza
vifaa vyake darasani na nyumbani.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoheshimu hoja za wenzake katika
majadiliano kuhusu alama za uakifishi.
Pia, anapotumia lugha ya adabu.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada ambazo
zinafundisha alama za uakifishi.
Masomo yote hutumia sentensi
na vifungu vilivyoakifishwa kwa
kutumia alama za uakifishi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakuwa kielelezo shuleni
na nyumbani anapotumia lugha fasaha
na iliyoakifishwa vyema. Pia, ataboresha
mawasiliano yake katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana
uwezo wa kuelewa kwa haraka
wanayofundishwa watengewe
muda zaidi wa ujifunzaji baada ya
masomo jioni. Wanafunzi walio
na uwezo wa kuelewa kwa haraka
wanayofundishwa wapewe shughuli
zaidi za kufanya. Pia, wanafunzi
hao wanaweza kuwasaidia wenzao
wanaojifunza polepole.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia breli kuandika
na kusoma maelezo kuhusu alama za
uakifishi. Pia, wanaweza kusikiliza
maelezo kuhusu alama za uakifishi
yakitolewa nawe au wanafunzi
wenzao.
Wanafunzi wenye matatizo ya
kifamilia au kisaikolojia wapewe
ushauri nasaha ili kuwawezesha
kujifunza bila usumbufu.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia wanaweza kutumia vifaa vya
kuwasaidia kusikia. Pia, unaweza
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara katika somo hili.
4.4.1 Herufi kubwa, koma (,),
kikomo (.) na kiulizi (?)
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 37-40)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 4)
Fanya utafiti kuhusu matumizi mbalimbali
ya alama za uakifishi (koma, kikomo, kiulizi
na herufi kubwa). Rejelea maswali dadisi
ili upate uelewa zaidi wa yanayohitajika
kutimizwa katika funzo hili. Pia,
Andaa chati zilizoandikwa sentensi
kadhaa ambazo hazijaakifishwa ili
wanafunzi waweze kuziakifisha kwa
pamoja darasani na kujifunza.
Andaa chati zilizoandikwa sentensi
kadhaa zilizoakifishwa kwa kutumia
koma, kikomo, kiulizi na herufi kubwa
ili wanafunzi waweze kutambua alama
za uakifishi kwa pamoja darasani na
kujifunza.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 37
2. Chati zilizoandikwa sentensi
zilizoakifishwa
56
Kimeidhinishwa na KICD
3. Chati zilizoandikwa sentensi
ambazo hazijaakifishwa
4. Breli, mfasiri wa lugha ishara.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi
iwapo wanakumbuka alama zozote za
uakifishi walizowahi kujifunza. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 1, waelekeze
wanafunzi kujadili makosa yaliyopo
katika sentensi walizopewa kitabuni
mwao wakiwa katika vikundi. Majibu
tarajiwa: nomino za pekee zinafaa
kuanza kwa herufi kubwa, sentensi
zinafaa kuanza kwa herufi kubwa,
kikomo kinafaa kuwekwa mwishoni
mwa sentensi n.k. Waongoze
wanafunzi warekebishe sentensi hizo
kwa kuziandika upya kwa usahihi.
Waulize wanafunzi walichojifunza
kutokana na sentensi hizo. Wajadili
wakiwa katika vikundi. Hakikisha
wamejifunza matumizi ya herufi
kubwa na kikomo katika sentensi.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi kutunga sentensi sahihi
wakitumia herufi kubwa pamoja na
alama ya kikomo. Wabadilishane
madaftari ili watathmini sentensi
za wenzao. Hakikisha wanajadili
matumizi ya herufi kubwa na
kikomo. Herufi kubwa hutumiwa
mwanzoni mwa sentensi (Mfano:
Mwalimu anafundisha.), mwanzoni
mwa nomino za pekee (Mfano:
Anyango, Kenya), hutumiwa
kuonyesha ufupisho wa neno au
maneno (Mfano: bi. bibi, k.v.
kama vile), hutumiwa kuandika
tarehe (Mfano: 20.02.2021) n.k.
Waongoze wanafunzi wakiwa katika
vikundi wafanye shughuli ya 3 kwa
kujadili makosa yaliyopo kwenye
sentensi walizopewa vitabuni mwao.
Jibu tarajiwa: Sentensi hazikuakifishwa
ifaavyo kwa kutumia kiulizi na koma.
Wanafunzi warekebishe sentensi
ambazo wamepewa vitabuni mwao
kwa kuziakifisha kwa usahihi.
Wanafunzi wajadili kuhusu matumizi
ya kiulizi na koma. Kiulizi hutumiwa
mwishoni mwa sentensi ambayo ni
swali ili kupata jibu (Mfano: Kwa
nini umevaa bangili tano?). Koma
hutumiwa kuorodhesha vitu, viumbe
au mambo kwenye orodha (Mfano:
Mama alivalia herini, mkufu na saa
ya dhahabu). Pia, koma hutenganisha
mawazo kwenye sentensi ndefu
(Mfano: Alipofika njiani, alikutana
na wauzaji mapambo). Waeleze kuwa
koma pia huitwa kipumuo au kituo.
Katika shughuli ya 4, waongoze
wanafunzi watunge sentensi sahihi
wakitumia kiulizi na koma kwa
usahihi. Wabadilishane madaftari
na uwaelekeze wazitathmini na
kujifunza.
Katika shughuli ya 5, soma kwa sauti
na matamshi sahihi kifungu kilicho
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 39. Wanafunzi wakusikilize
kwa makini. Hakikisha unatumia
alama za uakifishi kwa usahihi.
Mwanafunzi akisome kifungu hicho
57
Kimeidhinishwa na KICD
kwa sauti baada yako akizingatia
alama zote za uakifishi zilizotumika.
Tathmini usomaji wa wanafunzi.
Waongoze wanafunzi wajadiliane
kuhusu herufi kubwa, kikomo, koma
na kiulizi kama zilivyotumika katika
kifungu walichosoma.
Mwanafunzi amsikilize mwenzake
akisoma kifungu husika. Atambue
mahali popote anapopumua na
anapotua kisha waelezane sababu za
kufanya hivyo.
Katika shughuli ya 6, waongoze
wanafunzi kutunga sentensi tano
zisizoakifishwa kisha wawape
wenzao waziakifishe kwa usahihi.
Waelekeze kuzitathmini sentensi zao.
Hakikisha sentensi hizo ni sahihi na
zimeakifishwa kwa usahihi.
Hitimisha somo hili kwa kuwapa
wanafunzi kazi ya ziada ya
kuakifisha sentensi kwa usahihi.
Majibu tarajiwa:
1. Baadhi ya vyombo vya
kiteknolojia ni kama vile redio,
simu, tarakilishi na tepurekoda.
2. Mbona hupendi kufunga tai
shingoni?
3. Ulikinunua kidani hiki pesa ngapi?
4. Rinda la Linda linamfaa
anapolivaa na taji kichwani./
Rinda la Linda linamfaa
anapolivaa na taji kichwani?
5. Wanakijiji walihamasishwa
kuhusu madhara ya mafuriko.
Tathmini
1. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
amefahamu matumizi ya herufi
kubwa, koma, kikomo na kiulizi
katika maandishi.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi anaweza
kutumia alama hizo kwa usahihi
katika maandishi kwa kutunga
sentensi na hata vifungu kwenye
daftari, tarakilishi au tabuleti yake.
Shughuli ya nje ya darasa
Mwelekeze kila mwanafunzi atengeneze
angalau mapambo mawili kutoka kwa
jamii yake. Wanafunzi wawauzie
wanafunzi wenzao shuleni mapambo
hayo. Pesa watakazopata kutokana na
mauzo hayo wazitoe kama mchango
wao kwa kituo chochote cha watoto
mayatima kilicho karibu na shule yenu.
Wanafunzi wawaonyeshe mayatima
hao jinsi ya kutengeneza mapambo
mbalimbali. Shughuli hii itaimarisha
utangamano, uraia na upendo.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Kubali kitendawili chochote sahihi
ambacho jibu lake ni jina la pambo.
2. Tathmini michoro ya mapambo.
Hakikisha ni michoro ya kikuba,
mkufu, shanga na bangili.
3. Kiwambo/skrini/mulishi, kipanya,
kiibodi/bodidota/kicharazio,
kitengo kikuu cha uchakataji n.k.
Tathmini matumizi ya sehemu
hizi atakavyoeleza mwanafunzi.
4. Tathmini usahihi wa sentensi
ambazo zitatungwa na
mwanafunzi akitumia nomino
husika.
58
Kimeidhinishwa na KICD
SAA NA MAJIRA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 42-54)
Utangulizi
Saa ni chombo maalum cha kuonyesha
muda au wakati. Pia, saa ni muda
unaokamilishwa kwa dakika sitini.
Majira ya siku ni nyakati katika siku.
Siku ina majira ya asubuhi, adhuhuri,
alasiri, jioni, usiku n.k. Binadamu
hupanga shughuli zake kwa kuzingatia
saa na majira.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Heshima, adabu na vyeo: Maneno ya
heshima), Kusoma kwa mapana (Matini
ya kidijitali), Kuandika baruapepe na
Sarufi (Umoja na wingi wa nomino
ngeli ya I-ZI na umoja na wingi wa
sentensi katika ngeli ya I-ZI).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 42-45)
Heshima, adabu na vyeo
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua maneno ya heshima
yanayohusiana na udugu ambayo
yanatumiwa katika mawasiliano.
b) Kutumia maneno ya udugu kwa
usahihi katika mazungumzo yake
ya kila siku.
c) Kuthamini kutumia maneno ya
udugu katika mawasiliano ya kila
siku.
Maswali dadisi
1. Unajua maneno gani ya heshima
ya kuwarejelea watu wa kike na
wa kiume?
2. Unatumia neno lipi la heshima
kumrejelea mwalimu wako wa
kike au wa kiume?
3. Kutumia maneno ya heshima
katika mawasiliano kuna
umuhimu gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kufanya
shughuli mbalimbali katika vikundi
kama vile maigizo na majadiliano
yanayohusisha maneno ya heshima.
(b) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
sentensi zake mwenyewe akitumia
maneno ya heshima yanayohusiana
na udugu. Pia, anapoandika maelezo
kuhusu jinsi anavyotumia muda wake
kuanzia asubuhi hadi usiku.
59
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano
Utangamano unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali kuigiza maigizo
mafupi yanayohusu matumizi ya
maneno ya heshima yanayohusiana
na udugu.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapotumia
maneno ya heshima yanayohusiana
na udugu katika mawasiliano shuleni,
nyumbani na katika jamii.
Uhusiano na maadili
Heshima na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotumia maneno ya heshima
kuwasiliana na wenzake shuleni na
nje ya shule. Pia, anaposhiriki katika
shughuli za vikundi kwa amani bila
vurugu.
Upendo
Unakuzwa mwanafunzi anapotumia
maneno ya udugu kwa wenzake na
kwa wakubwa wake anapowasiliana
nao shuleni na nje ya shule.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada
zinazofundisha matumizi ya lugha ya
heshima.
2. Somo la Dini
Lugha ya heshima na adabu hufunzwa
katika somo hili kama mojawapo ya
mambo yanayompendeza Mungu na
yanayomstahiki mcha Mungu.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahimize wenzake
shuleni na nje ya shule kutumia
maneno ya heshima na udugu ili
kukuza upendo na utangamano
mwema miongoni mwao.
Matumizi ya lugha ya heshima na
adabu yatayaboresha mawasiliano
ya wanajamii ambao watakuwa na
mlahaka mwema.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye changamoto
za viungo vya mwili
wapewe majukumu ambayo
hayatasababisha kuumia kwa
viungo vilivyoathirika hasa
wakati wa maigizo mafupi
kuhusu maneno ya heshima
yanayohusiana na udugu.
Wanafunzi wasioweza kuona
watumie breli kujifunza maneno
ya heshima yanayohusiana na
udugu. Pia, wanaweza kuyasikiliza
maelezo kuhusu maneno ya
heshima na udugu kutoka kwa
wenzao na mwalimu.
Wanafunzi wasioweza kusikia
au kuzungumza wanaweza
kuwasiliana kwa kutumia
maandishi. Pia, mwalimu anaweza
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara ambaye atawaelekeza
wanafunzi hao wanapojifunza.
60
Kimeidhinishwa na KICD
1.1 Maneno ya heshima
heshima yanayohusiana na udugu
3. Tarakilishi, projekta, rununu
4. Kamusi ya Kiswahili
5. Mfasiri wa lugha ishara, breli.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza
wanafunzi wataje jina la mwalimu
wao mkuu pamoja na walimu wao wa
masomo mengine katika shule yao.
Chunguza iwapo kuna wanafunzi
watakaotumia maneno bwana au bi kabla
ya kutaja majina ya walimu hao.
Katika shughuli ya 1, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha
uwaelekeze kuchagua maneno ya
udugu kutoka kwenye mti maneno
ulio vitabuni mwao. Majibu
tarajiwa: binti, bwana, kaka, bin,
mama, ndugu, mama mdogo, bibi, bi,
mjomba, dada, mama mkubwa.
Waelekeze wanafunzi kujadili maana za
maneno ya udugu waliyochagua huku
wakiwarejelea watu katika familia.
Waongoze kutaja majina ya heshima
wanayotumia kuwarejelea watu
mbalimbali katika swali la 3. Majibu
tarajiwa: a) bi b) bwana c) mama
d) mama mdogo e) mama mkubwa
f) mjomba g) bin h) binti i) dada.
Waongoze wanafunzi wakiwa
wawiliwawili wafanye shughuli ya
2, ambapo watatambua majina ya
heshima katika sentensi 1-5. Majibu
tarajiwa: 1. Shikamoo Bwana Musa?
2. Binti/Bi. Ole Sakuda 3. Bin Seko
4. Mama Juma 5. Baba Mariamu.
Mwelekeze mwanafunzi katika
shughuli ya 3 ambapo atatunga
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 42-45)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Shughuli za ufunzaji na ujifunzaji
hufanikishwa na maandalizi mema
ya mwalimu na mwanafunzi.
Unaweza kubuni shughuli zaidi ya
zilizopendekezwa katika mada ndogo hii.
Mfano, unaweza kutunga wimbo wenye
maneno ya heshima ili mwanafunzi
auimbe hata baada ya kipindi na kuweza
kujikumbusha aliyojifunza. Pia,
Unaweza kurekodi video yenye
maigizo mafupi kuhusu matumizi ya
maneno ya heshima yanayohusiana
na udugu. Video hiyo iwe na
maandishi yanayoeleza kila tukio ili
mwanafunzi asiyeweza kusikia ayaone
na kujifunza. Unaweza kuwatumia
wanafunzi wako au wa gredi nyingine
kurekodi.
Hakikisha vifaa vya kujifunzia kama
vile projekta na tarakilishi viko katika
hali nzuri ya kutumika.
Hakikisha breli za kutumiwa na
wanafunzi wasioweza kuona ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa.
Ikiwa huwezi kufasiri lugha ishara,
tafuta mfasiri wa lugha ishara na
umweleze kuhusu somo hili ili
afahamu atakayofasiri na kujiandaa.
Hakikisha una kamusi ya Kiswahili ili
kurejelea maana za baadhi ya maneno
ya heshima na udugu.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 42
2. Kanda yenye video ya maigizo
mafupi kuhusu maneno ya
61
Kimeidhinishwa na KICD
sentensi sahihi akitumia maneno ya
heshima aliyopewa kitabuni mwake.
Kubali sentensi zozote sahihi na
zenye maneno ya heshima husika.
Waongoze wanafunzi kufanya shughuli
ya 4 kwa kusoma mazungumzo ya watu
walio katika mchoro waliopewa vitabuni
mwao. Waelekeze waigize mazungumzo
hayo wakiwa wawiliwawili.
Pia, waongoze wakiwa katika vikundi
kuigiza mazungumzo mbalimbali
wakitumia msamiati wa heshima
unaohusiana na udugu kwa kutumia
lugha sahihi.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya zaida.
Tathmini iwapo kazi hii imefanyika
kabla ya kipindi kingine kuanza.
Umuhimu wa kutumia maneno
ya heshima ni: Kujenga uhusiano
mwema baina ya watu, kuonyesha
uhusiano wa kifamilia, kikazi ama
kirafiki kwa watu wawili au zaidi
wanaowasiliana, kuashiria kuwa mtu
ana adabu n.k.
Hakikisha sentensi atakazotunga
mwanafunzi ni sahihi na zimetumia
maneno ya heshima na udugu
aliyopewa pamoja na majina ya watu
katika familia yao.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anafahamu maana ya maneno
mbalimbali ya heshima na adabu
yanayohusiana na udugu na
kuyatumia kwa usahihi katika
mazungumzo yake ya kila siku.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua maneno ya
heshima yanayohusiana na udugu
yanayotumiwa katika mawasiliano.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anafahamu umuhimu wa kutumia
maneno ya heshima na udugu
katika mawasiliano.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 45-48)
Kusoma kwa mapana
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua na kuzingatia hatua
za kiusalama katika matumizi ya
vifaa vya kidijitali.
b) Kutambua msamiati wa suala
lengwa katika matini ya kidijitali.
c) Kusakura matini kwenye tovuti
salama ili kupata vifungu vya
kusoma vyenye suala lengwa.
d) Kuchangamkia matumizi ya vifaa
vya kidijitali katika kutafuta na
kusoma ujumbe ili kuimarisha
maarifa yake.
Maswali dadisi
1. Unajua vifaa gani vya kidijitali?
2. Ni njia zipi unazoweza kutumia
kupata matini za kusoma kwenye
vifaa vya kidijitali?
3. Ni hatua zipi za kiusalama unazofaa
kuzingatia unapotafuta matini za
kusoma mtandaoni?
62
Kimeidhinishwa na KICD
pamoja na kuzingatia mitandao
salama pekee.
Uaminifu na ukweli
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapohakikisha anasakura matini
kwenye tovuti salama pekee na
haingii kwenye mitandao isiyo salama
kwake hata pasipokuwa na mtu
mzima wa kumwona.
Amani na umoja
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kwa
amani kufanya shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana matini mbalimbali
zinazoweza kutafutwa kwenye mtandao
na kumhitaji mwanafunzi kuzingatia
usalama.
Masomo yote yanatakiwa kuzingatia
ujuzi wa kidijitali katika ufunzaji wao.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake
shuleni na katika jamii kuhusu usomaji
wa matini za kidijitali mtandaoni na
kuzingatia usalama mtandaoni.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia na kuzungumza, wajifunze
kwa usaidizi wa mfasiri wa lugha
ishara. Pia, wanaweza kujifunza kwa
kutumia maandishi.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona watumie breli au wasikilize
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadiliana kuhusu saa
na majira mbalimbali pamoja na
kutafuta mtandaoni matini salama za
kusoma.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia vifaa vya kidijitali
kusakura mtandaoni na kusoma
matini zinazohusu saa na majira
mbalimbali.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii itakuzwa mwanafunzi
atakapoendelea kutafuta matini za
kusoma mitandaoni na hata kwenye
magazeti na vyanzo vingine.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapozingatia
hatua za kiusalama akiwa mtandaoni.
Usalama wa mtandaoni
Huu unaendelezwa mwanafunzi
anapotambua hatari zinazoambatana
na mtandao na kufuata njia salama za
kutumia mtandao.
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anapotangamana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali wakisakura
mtandaoni matini salama za kusoma.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Unajitokeza mwanafunzi anapotunza
vifaa vya kidijitali bila kuviharibu
63
Kimeidhinishwa na KICD
5. Saa halisi
6. Mfasiri wa lugha ishara.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi
maswali yanayohusiana na saa kama vile:
Saa hii ni saa ngapi? Ulifika shuleni saa
ngapi? Wewe huenda nyumbani saa ngapi?
n.k. Tathmini majibu ya wanafunzi. Majibu
yahusu saa.
Katika shughuli ya 1, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi yao kisha uwaongoze
kujadili michoro iliyo vitabuni
mwao. Wajibu maswali waliyopewa.
Majibu tarajiwa: 2. Saa a) saa kumi
asubuhi/jioni b) saa nne asubuhi/
usiku c) saa saba adhuhuri/usiku 3.
d) jua linapochomoza asubuhi, e)
jua linapotua jioni f) usiku mwezi
unapong’aa. Tathmini majibu ya
wanafunzi kulingana na maswali 4
na 5. Wanafunzi watumie kamusi ya
Kiswahili kuelewa maana ya saa na
majira.
Unaweza kuwa na saa halisi ili
wanafunzi waitumie kujifunza
nyakati mbalimbali. Unaweza
kusogeza akrabu za saa hiyo ili
kuonyesha nyakati mbalimbali huku
wanafunzi wakizitaja. Unaweza
kumteua mwanafunzi mmoja
akasogeza akrabu za saa huku
wenzake wakisema ni saa ngapi.
Waongoze wanafunzi kufanya
shughuli ya 2 wakiwa katika vikundi.
Watumie tarakilishi kuingia kwenye
mtandao. Watafute matini yoyote
iliyo salama kwa kusoma inayohusu
msamiati wa suala lengwa ukisomwa
na kuelezwa nawe au na wanafunzi
wenzao darasani.
Wanafunzi walio na uwezo wa
kung’amua wanayojifunza kwa haraka
wapewe fursa ya kusoma matini zaidi
mtandaoni kuhusu matumizi mazuri
ya muda.
Wanafunzi wanaochukua muda
zaidi kufahamu wanayofundishwa
washirikishwe katika shughuli
zaidi na kutengewa muda zaidi wa
kujifunza baada ya masomo jioni.
2.1 Matini ya kidijitali
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 45-48)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu vifaa mbalimbali vya
kidijitali na matumizi yake kabla ya kipindi
ili kuwaelekeza wanafunzi vyema. Pia,
Hakikisha vifaa vya kidijitali
utakavyotumia viko katika hali
nzuri ya kutumika.
Ikiwa utahitaji usaidizi wa mfasiri
wa lugha ishara, mwarifu kuhusu
kipindi ili ajiandae ifaavyo.
Panga utakavyowashirikisha
wanafunzi katika shughuli za
ujifunzaji kulingana na idadi ya
vifaa vya kidijitali watakavyotumia
kujifunza.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 45
2. Vifaa vya kidijitali kama vile:
tarakilishi, rununu, saa ya kidijitali
3. Mashine za breli na intaneti
4. Kamusi ya Kiswahili
64
Kimeidhinishwa na KICD
saa na majira. Hakikisha unawapanga
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi ya tarakilishi zilizopo.
Wanafunzi wajadili hatua salama
walizofuata kupata matini waliyotaka.
Kubali maelezo yoyote yanayozingatia
hatua salama za kufuata ili kupata
matini salama mtandaoni.
Waelekeze wanafunzi wajadiliane
kuhusu hatua za kuchukua endapo
watapata jumbe kutoka kwa watu
wasiowajua mtandaoni. Kwa mfano,
mwanafunzi atoe habari kwa
mwalimu, mzazi au mlezi wake.
Pia asifanye anayoambiwa na watu
asiowajua mtandaoni.
Waongoze wanafunzi kufahamu
mambo ya kuepukana nayo wakati
wowote wanapotumia vifaa vya
kidijitali kama vile: Mtu asile
anapotumia vifaa vya kidijitali,
mikono yake isiwe na unyevunyevu
au maji, atumie kifaa cha kidijitali
kwa kazi yake maalum, asiache vifaa
vya kidijitali vikawa vichafu kwa
kutovipangusa vumbi, asicheze akiwa
anatumia vifaa vya kidijitali. Ikiwa
kifaa cha kidijitali kinatumia nguvu
za umeme, asiache nguvu za umeme
ziwake wakati hatumii kifaa hicho.
Pia, aepuke kujibu ujumbe wa mtu
asiyemjua mtandaoni ili kudumisha
usalama wake.
Mwelekeze mwanafunzi kusoma
kifungu katika shughuli ya 3 kisha
ajibu maswali aliyopewa. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
Katika swali la 5, waelekeze
wanafunzi kuandika kifungu
walichosoma kwenye tarakilishi. Kila
mwanafunzi apewe nafasi ya kupiga
chapa sehemu ya kifungu hicho.
Maneno yanayohusu saa na majira
katika kifungu hicho yakolezwe rangi
na kupigiwa mistari.
Baadaye, wafungue faili kwenye
tarakilishi kwa jina la mmoja wao
kisha wahifadhi kifungu hicho.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada.
Tathmini iwapo kazi hii ilifanyika
kabla ya kipindi kingine kuanza.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua hatua za
kiusalama za kuzingatia wakati wa
kutumia vifaa vya kidijitali.
2. Tathmini kama kila mwanafunzi
anaweza kutambua msamiati wa
saa na majira katika matini ya
kidijitali.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutafuta mtandaoni
matini salama za kusoma kuhusu
saa na majira.
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 48-50)
Aina za insha
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua baruapepe kwa
kuzingatia muundo wake.
65
Kimeidhinishwa na KICD
b) Kuandika baruapepe kwa
kuzingatia ujumbe, muundo na
mtindo.
c) Kuchangamkia uandishi wa
baruapepe katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unajua vifaa vipi vinavyoweza
kutumiwa kutuma baruapepe?
2. Je, unazingatia mambo gani
unapoandika baruapepe?
3. Ni mambo gani ambayo unaweza
kumweleza rafiki yako kupitia kwa
baruapepe?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
shughuli za vikundi na kujadiliana
kuhusu baruapepe.
(b) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi anapobuni
ujumbe wa baruapepe na kuuandika na
kuutuma kwa rafiki, mlezi, wanafunzi
wenzake au walimu.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia vifaa vya kidijitali
kuandika na kutuma baruapepe.
(d) Uwazaji wa kina
Unakuzwa mwanafunzi anapofikiri
kuhusu ujumbe wa kuandika kwenye
baruapepe, kuuandika na kuutuma.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anapotangamana na kushirikiana na
wenzake kutoka maneno mbalimbali
katika vikundi kujadili kuhusu insha
ya baruapepe.
Stadi za maisha
Kutokana na mwanafunzi kutumia
baruapepe kuwasiliana, atapata stadi
ya kujitegemea katika kuwasilisha
ujumbe wake.
Elimu kwa maendeleo endelevu
Mwanafunzi anapotumia teknolojia
kuwasiliana ataweza kuendeleza
uchumi wa jamii hasa anapoitumia
teknolojia kujipa mapato maishani.
Uhusiano na maadili
Upendo na amani
Upendo unakuzwa mwanafunzi
anapotuma baruapepe kwa marafiki
na mlezi wake kuwajulia hali.
Pia, kutokana na mwanafunzi
kushirikiana na wenzake katika
vikundi kuandika baruapepe bila
kuzua ugomvi kunakuza amani.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
wakati wa majadiliano kuhusu uandishi
wa baruapepe. Pia, anapotumia lugha
ya adabu na kuwajali wenzake.
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapotunza
vifaa vya kidijitali anavyotumia katika
uandishi wa baruapepe.
Uhusiano na masomo mengine
Katika mfumo mpya wa elimu, masomo
yote yanazingatia ujuzi wa kidijitali.
66
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake
shuleni na nyumbani kuhusu hatua
za kuandika baruapepe na kuituma ili
kuboresha mawasiliano yao.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana uwezo
wa kusikia ama kuzungumza
wasaidiwe kujifunza kwa lugha
ishara na mfasiri wa lugha hiyo.
Pia, wanaweza kuwasiliana kwa
kutumia maandishi.
Wanafunzi wenye changamoto
za viungo vya mwili wasaidiwe
kujifunza kwa utaratibu bila
kuumia.
Wahamasishe wanafunzi kuhusu
wenzao walio na mahitaji maalum
na jinsi ya kuwasaidia ili kutokuwa
na unyanyapaa kwa wenye mahitaji
maalum.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 48
2. Breli, rununu
3. Tarakilishi, intaneti
4. Mfasiri wa lugha ishara.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza
wanafunzi wataje vifaa vya kidijitali
wanavyojua. Wataje majina ya vifaa vya
kidijitali wanavyofahamu. Tathmini
majibu yao.
Waelekeze wanafunzi katika shughuli
ya 1, watazame michoro iliyo vitabuni
mwao, waijadili na kujibu maswali
waliyopewa. Majina ya vifaa a) na c)
ni kipakatalishi na tabuleti mtawalia.
Waambie wanafunzi wajadili
matumizi ya kipakatalishi na
tabuleti. Majibu tarajiwa: Vifaa hivi
hutumiwa kupiga chapa, kuwasiliana,
kuonyesha saa, siku, tarehe, kuchezea
michezo ya kidijitali, kupiga picha,
kunasa video na kuzihifadhi, kusoma
matini mtandaoni, kutuma baruapepe
n.k.
Waelekeze wanafunzi kutambua
kuwa watu katika michoro
waliyopewa wanatumia tarakilishi na
rununu (simu ya mkononi). Hakikisha
wanafunzi wanajadili matumizi ya
vifaa hivi.
Tathmini majibu ya wanafunzi
kuhusiana na matumizi ya tarakilishi
na rununu. Pia, tathmini majibu
yao kuhusiana na vifaa walivyowahi
kutumia kutoka kwenye michoro.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi kujadili jinsi vifaa vya
kidijitali vimerahisisha mawasiliano.
3.1 Baruapepe
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 48-50)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti kuhusu uandishi wa baruapepe
ili kuwaelekeza wanafunzi vilivyo bila
changamoto. Pia,
Hakikisha vifaa vya kidijitali
watakavyotumia wanafunzi viko
katika hali nzuri ya kutumiwa.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara kuhusu atakayofasiri kabla
ya somo hili ili ajiandae ifaavyo.
67
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu tarajiwa: Vifaa vya kidijitali
vimepunguza muda wa kutuma
ujumbe, vimepunguza kupotea kwa
ujumbe au kutomfikia mlengwa, watu
wengi wanaweza kupata ujumbe kwa
wakati mmoja n.k.
Waelekeze wanafunzi kufahamu kuwa
baruapepe ni barua inayotumwa kwa
kutumia mtandao na kurasa za yahoo
au gmail. Sharti mtumaji na mpokeaji
wawe na anwani maalum za kutumia.
Waelekeze wanafunzi katika shughuli
ya 3, waandike na kutuma baruapepe
kwa kuzingatia hatua zinazofaa.
Hakikisha wanafunzi wanazingatia
hatua salama za kutumia tarakilishi
kuandika na kutuma baruapepe.
Mhimize kila mwanafunzi aendelee
kufanya mazoezi ya kutuma, kusoma na
kupokea baruapepe kwenye mtandao.
Waongoze wanafunzi kujadili kuhusu
muundo na mtindo wa baruapepe.
Baruapepe huzingatia anwani ya
anayeituma, anwani ya mpokeaji,
salamu, mada ya ujumbe wa
baruapepe, mwili wa baruapepe na
mwisho.
Mhimize mwanafunzi afanye kazi
ya ziada akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Hakikisha mwanafunzi
anatunga baruapepe kuhusu safari ya
alfajiri akizingatia hatua alizopewa
kitabuni mwake kisha akutumie
mtandaoni ili uitathmini.
4.1 Sarufi: Umoja na wingi
wa nomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 50-52)
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya
I-ZI ili kuzitofautisha na nomino
katika ngeli nyingine.
b) Kuandika nomino za ngeli ya I-ZI
katika umoja na wingi.
c) Kuandika umoja na wingi wa
mafungu ya maneno katika ngeli
ya I-ZI.
d) Kuchangamkia kutumia nomino za
ngeli ya I-ZI katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, unajua nomino zipi ambazo
hazibadiliki katika umoja na wingi?
2. Je, unajua nomino zipi za ngeli ya
I-ZI?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Uwazaji wa kina
Huu unakuzwa mwanafunzi anapofikiri
kuhusu jinsi ya kutumia nomino za
ngeli ya I-ZI kutunga mafungu ya
maneno sahihi.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuandika baruapepe kwa
kuzingatia ujumbe, muundo na
mtindo na kuituma.
3. Tathmini ikiwa mwanafunzi anaweza
kutumia vifaa vya kidijitali kutuma
na kupokea baruapepe.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua baruapepe kwa
kuzingatia muundo na mtindo wake.
68
Kimeidhinishwa na KICD
anaposhirikiana na wenzake
katika vikundi kutambua nomino
mbalimbali za ngeli ya I-ZI.
(c) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi unapotunga
mafungu ya maneno yake mwenyewe
akitumia nomino za ngeli ya I-ZI bila
kunakili ya wenzake.
Uhusiano na masuala mtambuko
(a) Stadi za maisha
Mwanafunzi atajifunza kujitegemea
anapoweza kutambua nomino za ngeli
ya I-ZI na kuzitungia mafungu ya
maneno katika umoja na wingi akiwa
peke yake.
(b) Utangamano na uraia
Masuala mtambuko haya yanakuzwa
mwanafunzi anapotangamana na
wenzake kutoka maeneo mbalimbali
katika vikundi kutambua nomino za
ngeli ya I-ZI.
Uhusiano na maadili
Uzalendo
Uzalendo unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake wa asili
mbalimbali katika vikundi kutambua
nomino za ngeli ya I-ZI na kuzitungia
mafungu sahihi.
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuvitunza vifaa anavyotumia kujifunzia
bila kuviharibu.
Umoja na amani
Unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa amani bila kuzua fujo.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanajumuisha mafunzo
kuhusu ngeli mbalimbali za nomino.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atumie lugha kwa usahihi
ili kuimarisha mawasiliano shuleni,
nyumbani na katika jamii kwa jumla.
Mwanafunzi awahamasishe
wanajamii kuhusu nomino za ngeli ya
I-ZI ili kuboresha mawasiliano kwa
lugha sahihi na sanifu.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuelewa haraka washirikishwe
katika shughuli zaidi ili kutimiza
malengo ya ujifunzaji ya mada
ndogo hii.
Wanafunzi walio na mahitaji
ya kisaikolojia au kifamilia
kutokana na matukio katika jamii
wasaidiwe na mwalimu kujiamini
na kuchangamkia shughuli za
ujifunzaji.
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kusikia au kuzungumza,
watambue nomino za ngeli ya I–
ZI kwa kuzikoleza rangi kwenye
tarakilishi au kuzigusa ubaoni
kwa kutumia rula ikiwa utaandika
nomino mbalimbali ubaoni na
kuwauliza watambue nomino
za ngeli ya I-ZI. Pia, wanaweza
kuziandika madaftarini mwao.
Ikiwa mwanafunzi anaweza
kusikia lakini hawezi kuona,
69
Kimeidhinishwa na KICD
anaweza kusikiliza maelezo
kuhusu nomino za ngeli ya I –ZI
yakitolewa nawe au wanafunzi
wenzake. Pia, wanaweza kutumia
breli kufanikisha ujifunzaji wao.
tarakilishi, ngazi, picha, sabuni,
televisheni.
Waongoze wanafunzi kueleza maana za
nomino walizochagua kisha waandike
nomino hizo katika umoja na wingi.
Majibu tarajiwa: saa - saa, bahari
bahari, ngao ngao, tarakilishi
tarakilishi, ngazi ngazi, picha picha,
sabuni sabuni, televisheni televisheni.
Wanafunzi wajadili ugunduzi wao.
Katika shughuli ya 2, mwelekeze
mwanafunzi kujaza mapengo katika
umoja na wingi kwenye jedwali lililo
kitabuni mwake. Majibu tarajiwa:
1. ndizi 2. kalamu 3. nyumba 4. ndoo
5. nguo 6. simu 7. sahani 8. dakika
9. siku 10. rangi
Waongoze wanafunzi katika kufanya
shughuli ya 3 kwa kukamilisha jedwali
walilopewa vitabuni mwao kwa kufuata
mfano waliopewa.
Majibu tarajiwa: 1. Nyumba zetu
2. Ndizi yake 3. Sahani hizi 4. Saa
hizo. 5. Kengele ndogo 6. Ndizi ile
7. Dakika hizi 8. Pua safi
9. Baruapepe yako 10. Tarakilishi
kubwa.
Waongoze wanafunzi wakiwa katika
vikundi wajadili kuhusu mabadiliko
waliyoyaona katika umoja na wingi wa
mafungu ya maneno yenye nomino za
ngeli I-ZI waliyoandika. Wafahamu
kuwa nomino hizo hazibadiliki katika
umoja au wingi.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada.Tathmini
kufanyika kwa kazi hii kabla ya
kipindi kingine kuanza.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 50-52)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Hakikisha una nyenzo za ufunzaji na
ujifunzaji kama vile tarakilishi na kamusi
ya Kiswahili. Pia,
Rekodi maelezo kuhusu nomino za
ngeli ya I-ZI na mifano ya mafungu
ya maneno yenye nomino hizo
ili wanafunzi wasioweza kuona
wasikilize na kujifunza.
Fanya utafiti kuhusu ngeli ya I-ZI ili
kuwaelekeza wanafunzi ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kinasasauti, rekoda, rununu
2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 50
3. Kamusi ya Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwauliza
wanafunzi wataje nomino wanazojua
ambazo hazibadiliki katika umoja na
wingi. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 1, waelekeze
wanafunzi kujikumbusha kuhusu
ngeli ya I-ZI walivyofundishwa katika
gredi ya nne. Wanafunzi wataje
mifano ya nomino wanazokumbuka.
Wanafunzi wasome na kutambua
nomino za ngeli ya I-ZI kutoka
kwenye jedwali lililo vitabuni mwao.
Majibu tarajiwa: saa, bahari, ngao,
4.1.1 Umoja na wingi wa
nomino: Ngeli ya I-ZI
70
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua nomino katika
ngeli ya I-ZI.
2. Chunguza iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuandika nomino za ngeli
ya I-ZI katika umoja na wingi.
3. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kuandika umoja na wingi
wa mafungu ya maneno katika
ngeli ya I-ZI kwa usahihi.
nomino za ngeli ya I-ZI.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili upatanisho wa kisarufi
wa ngeli ya I-ZI na kutunga sentensi
sahihi.
(c) Kufikiri kwa kina
Kunakuzwa mwanafunzi anapowaza
kwa kina kuhusu sentensi sahihi ya
kutunga katika ngeli ya I-ZI.
(d) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu utakuzwa mwanafunzi
anapoandika sentensi katika umoja
na wingi kwenye tarakilishi na
kukoleza rangi nomino za ngeli ya
I-ZI pamoja na viambishingeli vyake
sahihi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia na utangamano
Utakuzwa kupitia kwa mwanafunzi
kushirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kutunga sentensi sahihi kwa kutumia
nomino za ngeli ya I-ZI.
Stadi za maisha
Zitakuzwa mwanafunzi anapojifunza
kuandika sentensi sahihi akitumia
nomino sahihi za ngeli ya I-ZI huku
akishirikiana na wenzake katika
vikundi.
Uhusiano na maadili
Umoja na amani
Maadili haya yatakuzwa mwanafunzi
anapofanya kazi na wengine katika
vikundi kwa amani bila kuzua fujo.
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 52-54)
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vipatanishi
vya ngeli ya I-ZI kwenye sentensi.
b) Kuunda sentensi akitumia nomino
za ngeli ya I-ZI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa
kisarufi.
c) Kuonea fahari matumizi ya ngeli ya
I-ZI katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Nomino za ngeli ya I-ZI huchukua
viambishi vipatanishi gani?
2. Nomino za ngeli ya I-ZI hubadilika
vipi katika wingi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
sentensi zake mwenyewe zilizo sahihi
katika umoja na wingi akitumia
71
Kimeidhinishwa na KICD
Uwajibikaji
Utakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunza tarakilishi atakayotumia
kukolezea rangi nomino za ngeli ya
I-ZI katika sentensi ambazo atatunga.
Uaminifu na ukweli
Utakuzwa mwanafunzi atakapotunga
sentensi zake mwenyewe zilizo sahihi
bila kunakili za wenzake.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mafunzo kuhusu
ngeli mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi ahimizwe kutumia lugha
kwa ufasaha shuleni na nje ya shule ili
kuimarisha mawasiliano katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana uwezo
wa kuona watumie breli kutambua
viambishi vipatanishi vya ngeli ya
I-ZI.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia wasome maelezo kuhusu
viambishi vipatanishi vya ngeli ya
I-ZI ubaoni au kwenye chati. Pia,
mwalimu anaweza kuwaeleza kwa
lugha ishara ikiwa anaifahamu
au amshirikishe mfasiri wa lugha
ishara.
Wanafunzi wenye uwezo wa
kung’amua wanayojifunza kwa
haraka wapewe fursa ya kutunga
sentensi zaidi wakitumia nomino
za ngeli ya I-ZI.
Wanafunzi wanaochukua muda
zaidi kuelewa na kufahamu
wanayojifunza washirikishwe
katika shughuli zaidi na
kutengewa muda zaidi wa
kujifunza baada ya somo.
4.2.1 Umoja na wingi wa
sentensi: Ngeli ya I-ZI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 52-54)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Andaa vifaa vya ujifunzaji hasa vile vya
kidijitali kwa kuhakikisha vinaweza
kutumika wakati wa kipindi hiki.
Vilevile,
Andaa chati zenye maelezo ya
viambishi vya upatanisho wa ngeli
ya I-ZI.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumika.
Andika mifano ya sentensi kadhaa
katika ngeli ya I-ZI zitakazokusaidia
katika ufunzaji.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 52
2. Chati zilizoandikwa maelezo ya
viambishingeli vya ngeli ya I-ZI
3. Mashine za breli, tarakilishi
4. Kamusi ya Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa shughuli ya 1
ambapo mwanafunzi ataandika nomino
kumi za ngeli ya I-ZI alizojifunza.
Tathmini nomino za wanafunzi.
72
Kimeidhinishwa na KICD
Mwelekeze mwanafunzi kutunga
sentensi sahihi katika umoja na wingi
akitumia nomino za ngeli ya I-ZI
alizoandika. Waelekeze wanafunzi
watathmini sentensi za wenzao.
Wanafunzi waelezane kuhusu
viambishi vipatanishi vya ngeli ya I-ZI
ambavyo ni i- katika umoja na zi-
katika wingi.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi ya tarakilishi zilizopo kisha
kila mwanafunzi aandike kwenye
tarakilishi sentensi mbili katika
ngeli ya I-ZI katika umoja na wingi.
Akoleze rangi nomino za ngeli I-ZI
katika sentensi hizo na apigie mistari
viambishi vipatanishi vya ngeli ya
I-ZI. Iwapo hakuna tarakilishi, kila
mwanafunzi aandike sentensi hizo
kwenye daftari lake na kupigia mistari
nomino za ngeli ya I-ZI pamoja
na viambishi vipatanishi vyake.
Viambishi vipatanishi vya ngeli ya
I-ZI ni i- na zi-.
Mwongoze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 3, ambapo ataandika
sentensi zilizo kitabuni mwake katika
umoja au wingi. Majibu tarajiwa:
a) Nyumba zao zilijengwa vizuri.
b) Saa yangu imenunuliwa. c) Nguo
hizi zilifuliwa asubuhi. d) Kalamu
zilianguka zikavunjika. e) Kamba
iliyokatika ilikuwa ndefu. f) Dakika
hii itanitosha kula. g) Ndizi zilizooza
zilitupwa jana usiku.
Wanafunzi wapigie mistari viambishi
vipatanishi vya ngeli ya I-ZI katika
sentensi walizoandika katika umoja
au wingi.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Kubali sentensi zozote sahihi
zilizoandikwa na mwanafunzi
akitumia nomizo za ngeli ya I-ZI.
Awasomee wenzake sentensi
alizotunga darasani ili wazitathmini
na kujifunza.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua viambishi
vipatanishi vya ngeli ya I-ZI
kwenye sentensi.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kuunda sentensi sahihi
zenye maana akitumia nomino
za ngeli ya I-ZI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa
kisarufi.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anashirikiana na kuwasiliana
vyema na wenzake darasani.
Shughuli ya nje ya darasa
Waongoze wanafunzi wakiwa kwenye
gwaride watambue majina ya walimu
wao wote pamoja na vyeo vyao. Pia,
waelekeze wanafunzi watambue majina
ya viranja wao wote pamoja na vyeo
vyao. Wasaidie wanafunzi watambue
majina ya viongozi wa eneo la
shule yenu pamoja na vyeo vyao.
Baadhi ya viongozi halisi wanaweza
kuhudhuria gwaride hiyo ili wanafunzi
wawaone na kuwatambua.
73
Kimeidhinishwa na KICD
Mwongoze kila mwanafunzi kuandika
insha ya wasifu kuhusu mwalimu,
kiranja au kiongozi yeyote
anayemfahamu vizuri.
Kila mwanafunzi aambatishe insha hiyo
kwenye baruapepe atakayokutumia ili
uitathmini na kuisahihisha. Shughuli hii
itawasaidia wanafunzi kufahamu vyeo
vya watu mbalimbali katika jamii
na kuimarisha utangamano na
uzalendo wao.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Kubali kifungu chochote sahihi
kilichotungwa kwa kutumia maneno
yanayohusiana na udugu.
2. Tathmini iwapo mwanafunzi anaweza
kutafuta mtandaoni matini salama
inayohusu jinsi ya kutumia muda
wake vizuri na kuandika muhtasari
wake kwenye daftari lake kwa
usahihi.
3. Sifa za baruapepe ni: huwa na anwani
ya anayeituma, anwani ya mpokeaji,
salamu, mada ya baruapepe, mwili
wa baruapepe, hitimisho/mwisho wa
baruapepe.
4. Kubali sentensi zozote sahihi
alizotunga mwanafunzi katika umoja
na wingi akitumia nomino alizopewa.
74
Kimeidhinishwa na KICD
KUKABILIANA NA
UMASKINI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 55-67)
Utangulizi
Umaskini ni hali ya mtu kukosa uwezo
wa kuyakimu mahitaji yake hasa
kutokana na changamoto za kiuchumi.
Umaskini huathiri mtu binafsi, familia
na taifa zima. Wananchi wenye umaskini
mara nyingi hukosa mahitaji ya kimsingi
kama vile chakula cha kutosha, nyumba
nzuri za kuishi na mavazi bora. Taifa
lenye umaskini linaweza kushindwa
kuwapa wananchi wake elimu bora,
miundomsingi, matibabu na mahitaji
mengine muhimu katika maisha. Ni
jukumu la kila mtu kufanya bidii ili
kukabiliana na umaskini nchini.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Methali: Methali zinazohusu bidii),
Kusoma kwa ufahamu (Lugha katika
shairi), Kuandika insha ya maelezo na
Sarufi (umoja na wingi wa nomino ngeli
ya U-ZI na umoja na wingi wa sentensi
katika ngeli ya U-ZI).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 55-57)
Methali
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua methali zinazohusu bidii
ili kuzitofautisha na aina nyingine
za methali.
b) Kueleza maana na matumizi ya
methali mbalimbali zinazohusu
bidii katika jamii.
c) Kutumia methali zinazohusu bidii
katika mawasiliano.
d) Kuchangamkia matumizi ya
methali katika kuhimiza bidii.
Maswali dadisi
1. Je, umuhimu wa methali ni upi
katika jamii?
2. Unajua methali zipi zinazohusu
bidii zinazotumiwa katika jamii?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Unakuzwa mwanafunzi anapofikiria
kuhusu maana na matumizi ya methali
zinazohusu bidii.
75
Kimeidhinishwa na KICD
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili maana na matumizi
ya methali zinazohusu bidii.
(c) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotumia
methali zinazohusu bidii katika
maandishi (kuandika insha au
vifungu) na maongezi yake.
(d) Ujuzi wa kidijitali
Unakuzwa mwanafunzi anapotumia
vifaa vya kidijitali kutafuta mtandaoni
maana za methali zinazohusu bidii.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Mwanafunzi atajifunza kuwa mwenye
bidii maishani kutokana na kujifunza
methali zinazohusu bidii.
Ushauri nasaha
Mwanafunzi atakuwa mwenye
maadili kutokana na kujifunza na
kutumia methali zinazohusu bidii
katika mawasiliano.
Uraia na utangamano
Utakuzwa mwanafunzi akishirikiana
na wenzake kutoka maeneo
mbalimbali katika vikundi kujadili
maana na matumizi ya methali
zinazohusu bidii.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake kwa
heshima wakati wa kujifunza methali
za bidii katika vikundi. Pia, kwa
kuyaheshimu maoni ya wenzake
kuhusiana na maana za methali
wanazojadili na kuwapa fursa ya
kuchangia katika majadiliano.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi wanapojifunza kuhusu
maana na matumizi ya methali
zinazohusu bidii bila kuzua fujo.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada ambazo
zinafundisha kuhusu methali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapojifunza methali
zinazohusu bidii anatarajiwa kuwa
kielelezo bora kwa jamii katika matumizi
ya lugha na kuwa mwenye ubunifu katika
mawasiliano.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Hakikisha kuwa wanafunzi wasio
na uwezo wa kuona wamepata
mashine za breli ili ziwasaidie
katika kutambua methali
zinazohusu bidii pamoja na
maana na matumizi yao.
Unaweza kumwalika mfasiri
wa lugha ishara ili kuwasaidia
wanafunzi wenye changamoto
ya kusikia na kuzungumza ili
washiriki katika ujifunzaji.
Wanafunzi wenye matatizo ya
viungo vya mwili washirikishwe
katika shughuli kwa kupewa
majukumu ambayo hayatawatia
76
Kimeidhinishwa na KICD
katika hatari ya kuumia hasa
wakiwa katika vikundi.
waliyojifunza kuhusu methali katika gredi
ya nne. Wanafunzi wakiwa katika vikundi
wataje mifano ya methali wanazokumbuka.
Pia, wataje mifano ya methali zinazohusu
bidii na kujadili maana na umuhimu wa
methali hizo. Mifano: Mchumia juani hulia
kivulini. Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.
Atafutaye hachoki, akichoka keshapata n.k.
Tathmini majibu ya wanafunzi. Waongoze
wajadili umuhimu wa methali za bidii
kama vile kuhimiza watu kuwa na bidii.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi wawili kusoma
mazungumzo kati ya mjomba na
mpwa yaliyo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 54-55.
Wanafunzi wengine wasikilize
mazungumzo hayo kwa makini
yakisomwa na wenzao darasani.
Waongoze wanafunzi kujibu maswali
waliyopewa. Majibu tarajiwa:
1. Yalitokea shambani. 2. Wote
wana maadili mema, wanapenda
kufanya bidii, wanawasiliana vyema,
wanatangamana vyema, mpwa ni
mtiifu kwa sababu yeye huzingatia
ushauri wa mwalimu wake. Mjomba
ana hekima, anamshauri mpwa wake
kuwa mwenye bidii.
Wanafunzi watambue na kueleza
maana za methali zinazohusu bidii
katika kifungu walichosoma.
Waelekeze wanafunzi katika kuigiza
mazungumzo waliyosoma kati ya
mjomba na mpwa wake.
Katika shughuli ya 3, waelekeze
wanafunzi kucheza mchezo wa
kukamilisha methali zinazohusu
1.1 Methali zinazohusu bidii
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 55-57)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu methali mbalimbali
zinazohusu bidii pamoja na maana na
matumizi yao ili kufanikisha ufunzaji na
ujifunzaji wa somo hili. Pia,
Andaa kapu lenye kadi ambazo
zimeandikwa methali mbalimbali
zinazohusu bidii na ambazo
hazijakamilishwa.
Andika methali mbalimbali
kamilifu zinazohusu bidii kwenye
chati.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara mapema kuhusu somo hili
ili aweze kujiandaa ifaavyo.
Hakikisha una kamusi ya methali
za Kiswahili.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 55
2. Kamusi ya methali za Kiswahili
3. Mashine za breli
4. Chati iliyoandikwa methali
zinazohusu bidii
5. Kapu lenye kadi zilizoandikwa
methali zinazohusu bidii zenye
nafasi za kukamilishwa
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa shughuli ya 1 kwa
kuwauliza wanafunzi ikiwa wanakumbuka
77
Kimeidhinishwa na KICD
bidii wakiwa katika vikundi viwili.
Tathmini majibu ya kila kikundi na
utoe jibu sahihi kwa methali ambayo
wanafunzi watashindwa kukamilisha.
Mhimize mwanafunzi afanye kazi
ya ziada akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Tathmini methali
atakazoandika mwanafunzi. Wenzake
darasani wataeleza maana na
umuhimu wa methali hizo. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
c) Kuchangamkia kusoma shairi
akizingatia mapigo ya sauti.
Maswali dadisi
1. Je, shairi ni nini?
2. Je, kuna tofauti gani kati ya mashairi
na maandishi mengine?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Unakuzwa mwanafunzi anapofikiria
kuhusu ujumbe unaojitokeza kwenye
shairi.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili msamiati uliotumika
katika ushairi.
(c) Ubunifu
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi
anapofafanua ujumbe wa shairi
kwa maneno yake mwenyewe bila
kunakili ya wenzake.
(d) Ujuzi wa kidijitali
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutafuta shairi mtandaoni kwa
kutumia vifaa vya kidijitali.
Uhusiano na masuala mtambuko
Ushauri nasaha
Unakuzwa kupitia kwa mafunzo
yanayotokana na ujumbe wa shairi
kuhusu bidii.
Stadi za maisha
Zitakuzwa kupitia kwa mwanafunzi
kujifunza kutumia lugha kwa ustadi
maishani.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua methali
zinazohusu bidii katika matini.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kueleza maana na
matumizi ya methali mbalimbali
zinazohusu bidii katika jamii.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutumia methali
sahihi zinazohusu bidii katika
mawasiliano.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 58-59)
Kusoma kwa ufahamu
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vina na mizani katika
shairi ili kuvibainisha.
b) Kusoma shairi akizingatia vina,
mizani na ujumbe ili kuimarisha
ufahamu.
78
Kimeidhinishwa na KICD
shairi na kutambua vina na
mizani katika shairi.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia na kuzungumza watazame
shairi kwenye vitabu vyao na
kulisoma kimoyomoyo kisha
watoe maelezo kwa maandishi.
Mfasiri wa lugha ishara anaweza
kushirikishwa.
Wanafunzi wasioweza kungamua
wanayojifunza upesi wapewe
mazoezi zaidi. Unaweza
kuwatumia wanafunzi ambao
wana uwezo wa kujifunza
upesi kuwasaidia wenzao
wanaong’amua mambo polepole
kutambua vina na mizani katika
shairi.
Uraia
Uraia unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali kufafanua ujumbe
wa shairi na kutambua vina na mizani ya
shairi.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi wanapojadili shairi
walilosoma. Pia, anapotumia lugha ya
adabu.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kukariri na kujadili shairi kwa
amani bila kuzua ugomvi wowote.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada ambazo
hushughulikia ufunzaji wa mashairi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anaweza kutumia ushairi
kuwahamasisha wanajamii kuhusu masuala
mbalimbali. Pia, anaweza kutumia ushairi
kuwatumbuiza wanajamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Tumia nyenzo mbalimbali
ili kukidhi mahitaji ya kila
mwanafunzi kulingana na mahitaji
maalum aliyo nayo. Wanafunzi
wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia breli kusoma
2.1 Lugha katika ushairi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 58-59)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu ushairi ili kufanikisha
ufunzaji wako. Vilevile:
Andaa chati yenye maelezo kuhusu
vina na mizani ya shairi.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara kuhusu somo hili ili
ajiandae ifaavyo.
Pia, unaweza kutafuta mashairi
mbalimbali mtandaoni au vitabuni
ili kufanikisha ufunzaji wako.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
79
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 58
2. Rununu, tarakilishi, breli
3. Rekodi ya shairi
4. Chati yenye maelezo kuhusu shairi.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa shughuli ya
1 kwa kuwauliza wanafunzi iwapo
wamewahi kukariri mashairi yoyote.
Wanaweza kuwakariria wenzao
mashairi wanayokumbuka. Tathmini
matamshi sahihi na bora.
Katika shughuli ya 2, wachezee
wanafunzi rekodi ya shairi
iliyoambatanishwa na kitabu hiki.
Waongoze wanafunzi kukariri kwa
sauti shairi walilosikiliza. Baadaye,
kila mwanafunzi asome shairi hilo
kimyakimya halafu ajibu maswali
aliyopewa.
Majibu tarajiwa:
1. Ujumbe unaojitokeza katika shairi hili
ni umuhimu wa bidii. Kubali jibu lolote
sahihi kulingana na ujumbe wa shairi.
2. Idadi ya silabi katika shairi zima ni 192.
Mstari wa 1 una silabi 16, mstari wa 2
una silabi 16, mstari wa 3 una silabi 16,
mstari wa 4 una silabi 16, mstari wa 5
una silabi 16, mstari wa 6 una silabi 16,
mstari wa 7 una silabi 16, mstari wa 8
una silabi 16, mstari wa 9 una silabi
16, mstari wa 10 una silabi 16, mstari
wa 11 una silabi 16, mstari wa 12 una
silabi 16.
3. Silabi za kati na mwisho wa mistari 1,
2 na 3 ni mu, ni, mstari wa 4 ni a, li,
mistari 5, 6 na 7 ni ni, ni, mstari wa 8
ni a, li, mistari 9, 10 na 11 ni ka, ka,
mstari 12 ni a, li.
Wanafunzi watambue kuwa silabi za
kati ya kila mstari katika kila ubeti
zinafanana. Silabi za mwisho wa kila
mstari wa kila ubeti zinafanana.
4. Shairi huwa na vina, mizani, beti
na huandikwa kwa mtindo maalum.
Maandishi mengine hupangwa katika
sentensi au aya. (Kubali maelezo
yoyote sahihi kuhusu tofauti ya shairi
na maandishi mengine).
Katika shughuli ya 3, mwongoze
mwanafunzi kuandika katika daftari
lake shairi alilosoma kisha ataje idadi
ya beti zake, idadi ya mizani katika
mshororo wa pili katika ubeti wa tatu.
Majibu tarajiwa: Beti tatu. Mizani
16.
Mwelekeze mwanafunzi kuonyesha
vina vya kati na vya mwisho katika kila
ubeti kwa kuvipigia mstari.
Waeleze wanafunzi kuwa ikiwa
kuna mshororo unaorudiwarudiwa
mwishoni mwa kila ubeti vina vyake
havitazingatiwa katika kutaja vina vya
kati na vya mwisho katika ubeti wa shairi.
Mhimize kila mwanafunzi afanye
kazi ya ziada katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 59. Tathmini
majibu ya mwanafunzi kulingana na
shairi atakaloandika.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua kwa usahihi
vina na mizani katika shairi.
2. Tathmini kama mwanafunzi
anaweza kusoma shairi akizingatia
vina, mizani na ujumbe ili
kuimarisha ufahamu.
80
Kimeidhinishwa na KICD
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 60-62)
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha za maelezo katika
matini mbalimbali.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa
kufuata kanuni zifaazo.
c) Kuchangamkia utunzi mzuri wa
insha ili kuimarisha uandishi.
Maswali dadisi
1. Je, insha ya maelezo huhusu nini?
2. Unazingatia nini unapoandika
insha nzuri ya maelezo?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia tarakilishi kuandika
insha ya maelezo.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadiliana kuhusu uandishi
wa insha ya maelezo pamoja na jinsi
ya kukabiliana na umaskini katika
jamii.
(c) Ubunifu
Huu unajengeka mwanafunzi
anapobuni na kuandika insha
ya maelezo kwa maneno yake
mwenyewe bila kunakili insha za
wenzake.
(d) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoyatafakari maswali dadisi
na anapoendelea kujifunza kwa
kuandika insha mbalimbali za
maelezo.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapojifunza
uandishi bora pamoja na utoaji bora
wa maelezo.
Uraia
Unakuzwa kutokana na mwanafunzi
kushirikiana na wenzake katika vikundi
wanapojifunza kuhusu uandishi wa
insha ya maelezo.
Elimu ya pesa
Inakuzwa mwanafunzi anapoandika
insha kuhusu njia mbalimbali za
kukabiliana na janga la umaskini
katika jamii.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu
Maadili haya yatakuzwa mwanafunzi
atakaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa heshima na adabu hata
kwa kutumia lugha ya adabu.
Umoja na amani
Maadili haya yatakuzwa kupitia kwa
mwanafunzi kushirikiana na wenzake
katika vikundi kwa amani bila kuzua
fujo.
3. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kusoma shairi akizingatia
mapigo ya sauti.
81
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hushughulikia stadi za
uandishi wa kila aina.
2. Somo la Jamii
Somo hili lina mada zinazofunza
kuhusu jinsi ya kupata mapato
kwa njia mbalimbali kama vile
kutokana na kilimo, utalii na biashara
mbalimbali na kuboresha uchumi
wa taifa ili kukabiliana na janga la
umaskini.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake
akiwa shuleni na nje ya shule kuhusu
umuhimu wa uandishi mzuri.
Kutokana na maelezo ya jinsi
ya kukabiliana na umaskini,
mwanafunzi atapata maarifa
ya kukabiliana na umaskini na
kuanzisha miradi ya kumpa mapato
nyumbani kama vile kufuga kuku,
sungura na kumsaidia mlezi
kutekeleza shughuli kama vile kulisha
mifugo.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona watumie mashine za breli
kujifunza muundo wa insha ya
maelezo. Pia, wasikilize maelezo
kuhusu uandishi wa insha ya
maelezo kutoka kwa mwalimu au
wanafunzi wenzao.
Wanafunzi wenye changamoto ya
kusikia na kuzungumza watazame
na kusoma kimoyomoyo insha ya
maelezo vitabuni mwao au kwenye
tarakilishi kisha wajibu maswali
kwa kuandika majibu au kutumia
lugha ishara ikiwa mwalimu
anaifahamu. Ikiwa mwalimu
haifahamu lugha ishara, anaweza
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara darasani ili kuwasaidia
wanafunzi hao.
Wanafunzi wenye changamoto
ya kuandika polepole waongezwe
muda wa kuandika ili waweze
kujieleza zaidi. Baadaye, mwalimu
awape wanafunzi hao mafunzo
ya ziada yanayohusu kuandika
maneno kwa kasi ili waweze
kuandika insha kwa muda
unaofaa.
3.1 Insha ya maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 60-62)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Hakikisha mwanafunzi ana vifaa muhimu
vya kuandikia insha kama vile penseli,
daftari na kifutio au raba ili kutumia muda
uliotengewa kila shughuli katika kipindi
ipasavyo. Pia,
Andaa nakala za aina mbalimbali
za insha zikiwemo nakala za insha
za maelezo ili wanafunzi waweze
kuzitambua na kuzitofautisha.
Unaweza kupata nakala hizi kutoka
kwa wanafunzi wa gredi nyingine.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
kuhusu funzo hili ili ajiandae ifaavyo.
Unaweza kuandaa michoro au picha
mbalimbali ambazo wanafunzi
wanaweza kutumia kutolea
82
Kimeidhinishwa na KICD
maelezo kuhusu njia mbalimbali za
kukabiliana na umaskini pamoja.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 60
2. Mashine za breli
3. Nakala zenye insha ya maelezo na
insha nyingine.
4. Michoro na picha kuhusu njia za
kukabiliana na umaskini.
Utaratibu wa ujifunzaji
Unaweza kutanguliza somo
hili kwa shughuli ya 1 kwa
kuwauliza wanafunzi waelezane
wanayokumbuka kuhusu uandishi wa
insha za maelezo waliyojifunza katika
gredi ya nne. Tathmini maelezo ya
wanafunzi.
Wapange wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na uwezo wao.
Waelekeze kujadiliana kuhusu
jinsi ya kukabiliana na umaskini.
Mwanafunzi mmoja katika kila
kikundi aandike maelezo ya wenzake
kisha mwingine ayasome maelezo
hayo mbele ya wanafunzi wengine.
Shughuli hii itawasaidia wanafunzi
kukuza ujasiri wao wa kuongea
mbele ya watu hivyo kujiamini na
kujithamini. Tathmini maelezo ya
wanafunzi pamoja na matamshi yao.
Waongoze wanafunzi kufanya
shughuli ya 2 kwa kusoma nakala
mbalimbali za insha utakazowapa.
Wanafunzi waweze kutambua insha
za maelezo kutoka kwa nakala
hizo. Waelekeze wanafunzi katika
kujadili ujumbe wa insha za maelezo
walizotambua. Hatimaye, wanafunzi
wajadili sifa za insha ya maelezo.
Katika shughuli ya 3, mwongoze
mwanafunzi kusoma kwa usahihi
insha ya maelezo iliyo kitabuni
mwake. Kosoa tabia isiyofaa wakati
wa usomaji na kumwelekeza
mwanafunzi ili kuboresha mbinu za
usomaji.
Wapange wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi yao kisha wajibu
maswali waliyopewa. Majibu
tarajiwa:
1. Tathmini majibu ambayo wanafunzi
watajadili kulingana na ujumbe wa
insha waliyosoma.
2. Sofia ni msichana mwenye bidii. Pia,
hakati tamaa maishani.Tathmini
majibu ya wanafunzi kuhusu tabia ya
Sofia kulingana na insha waliyosoma.
3. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Kwa mfano: a) Mgaagaa na upwa
hali wali mkavu. Mtu anayefanya
bidii hufanikiwa. b) Ukiona vyaelea
vimeundwa. Ufanisi huchangiwa na
bidii. c) Mtaka cha mvunguni sharti
ainame. - Mtu akitaka kufanikiwa
lazima afanye bidii. d) Atafutaye
hachoki akichoka keshapata. Ikiwa
mtu anatafuta ufanisi hafai kukata
tamaa hadi afaulu. e) Mchumia
juani hulia kivulini. Anayevumilia
changamoto hatimaye hufurahia
mafanikio.
4. Tathmini majibu ya wanafunzi
kuhusu mafundisho waliyopata
kutokana na insha waliyosoma. Kwa
mfano: kutokata tamaa maishani,
bidii huleta mafanikio n.k.
Katika shughuli ya 4, waongoze
wanafunzi kujadili mchoro ulio
83
Kimeidhinishwa na KICD
vitabuni mwao wakiwa katika
vikundi. Kubali jibu lolote sahihi
kulingana na matukio katika mchoro
huo. Mwanafunzi aandike vidokezo
kuhusiana na mchoro waliojadili
kisha atumie vidokezo hivyo kubuni
insha ya maelezo yenye mada.
Mpe mwanafunzi kazi ya ziada
ambayo atafanya akisaidiwa na
mzazi au mlezi wake. Tathmini
insha atakayokutumia mtandaoni
inayohusu jinsi ulipaji ushuru
husaidia katika kukabiliana na
umaskini. Pia, tathmini iwapo
mwanafunzi alifahamu njia
mbalimbali zinazotumiwa katika
familia yake kukabiliana na umaskini.
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya
U-ZI.
b) Kuandika nomino za ngeli ya U-ZI
katika umoja na wingi.
c) Kuandika umoja na wingi wa
mafungu ya maneno katika ngeli
ya U- ZI.
d) Kuchangamkia kutumia nomino za
ngeli ya U-ZI katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Ni nomino zipi hupatikana katika
ngeli ya U-ZI?
2. Je, nomino za ngeli ya U-ZI
hubadilika vipi katika umoja na
wingi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi
anapoandika mafungu ya maneno
sahihi akitumia nomino za ngeli ya
U-ZI akiwa pekee yake bila kunakili
ya wenzake.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutambua nomino za ngeli ya
U-ZI na kuziandikia mafungu sahihi.
(c) Uwazaji wa kina
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiria kuhusu nomino za ngeli
ya U-ZI na kuzitofautisha na nomino
nyingine.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano
Unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua insha
za maelezo katika matini
mbalimbali.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuandika insha ya
maelezo kwa kufuata mtindo,
muundo na kanuni zifaazo.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
amefahamu njia mbalimbali za
kukabiliana na umaskini katika
jamii.
4.1 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 63-64)
Umoja na wingi wa nomino
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
84
Kimeidhinishwa na KICD
vikundi kutoka maeneo mbalimbali
kutambua nomino za ngeli ya U-ZI
pamoja na kuzitungia mafungu
sahihi.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapofanya
kazi inayohusisha ngeli ya U-ZI darasani
akiwa pekee hivyo kumwezesha kukuza
stadi ya kujitegemea maishani.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuvitunza vifaa vyake vya kusomea na
kuandikia darasani na nyumbani.
Uzalendo
Uzalendo unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutoka maeneo mbalimbali
kufanya shughuli mbalimbali za
ujifunzaji.
Heshima na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi wanapojadili kuhusu
nomino za ngeli ya U-ZI na mafungu
yao. Pia, mwanafunzi anaposhirikiana
na wenzake bila kuzua ugomvi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada ambazo
hufundisha ngeli mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi ataimarisha mawasiliano
katika jamii anapojifunza kutunga
mafungu sahihi katika ngeli ya U-ZI kwa
kutumia lugha sahihi na fasaha. Anaweza
kuwafundisha wanajamii wengine.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kuzungumza au kusikia,
watambue nomino za ngeli ya
U-ZI kwa kuziandika kwenye
madaftari yao au kuzipigia mistari
kwenye tarakilishi. Pia, unaweza
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara.
Wanafunzi ambao hawana uwezo
wa kuona wanaweza kutumia breli
au wasikilize mafungu ya maneno
ya ngeli ya U-ZI yakisomwa na
mwalimu au wanafunzi wenzao.
Pia, wanaweza kugusa vifaa halisi
vinavyopatikana katika ngeli ya
U-ZI ili kuvitambua.
Wanafunzi wasiojimudu kufahamu
vipengele vyote walivyojifunza
kuhusu ngeli ya U-ZI waandaliwe
kipindi cha ziada cha kujifunza
zaidi baada ya masomo ya siku ili
kufikia matarajio ya mada.
4.1.1 Umoja na wingi wa
nomino: Ngeli ya U-ZI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 63-64)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu ngeli ya U-ZI ili
kumwelekeza mwanafunzi vyema.
Tafuta mapema vifaa halisi ambavyo
vinapatikana katika ngeli ya U-ZI kama
vile wembe (nyembe), uteo, uta, uzi,
ufunguo n.k. Vifaa hivi vitakusaidia
katika ufunzaji wa ngeli ya U-ZI.
Hakikisha mashine za breli zipo ili
wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wazitumie kujifunza.
85
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 63
2. Vifaa halisi katika ngeli ya U-ZI
kama vile: uzi, wembe, uteo, uta,
ufunguo n.k.
3. Mashine za breli
4. Kamusi ya Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi
wataje ngeli ambazo tayari wamejifunza.
Wataje mifano ya nomino katika ngeli hizo.
Katika shughuli ya 1, mwongoze
mwanafunzi kutambua michoro iliyo
kitabuni mwake na kuandika majina
yao. Majibu tarajiwa: a) ukuta
b) uzi c) uteo d) wembe e) ulimi
f) uta. Waelekeze wanafunzi kutambua
kuwa majina waliyoandika ni ya ngeli
ya U-ZI.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi wawiliwawili wakamilishe
jedwali lililo vitabuni mwao kwa
kuandika umoja au wingi wa nomino
walizopewa. Majibu tarajiwa: a) teo
b) uso c) ndevu d) mbao e) wakati
f) njiti g) unywele h) nyimbo.
Waelekeze wanafunzi katika vikundi
kuchunguza maneno waliyoandika.
Waongoze kutambua mabadiliko
ya nomino za ngeli ya U-ZI katika
umoja na wingi.
Katika shughuli ya 3, mwelekeze
mwanafunzi kutambua nomino za
ngeli ya U-ZI katika mchoro aliopewa
kitabuni mwake kisha aziandike
nomino hizo daftarini mwake katika
umoja na wingi. Majibu tarajiwa:
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua nomino katika
ngeli ya U-ZI pamoja na viambishi
vyake.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kuandika nomino za ngeli
ya U-ZI katika umoja na wingi.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuandika umoja na wingi
wa mafungu ya maneno katika
ngeli ya U-ZI.
4. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutumia nomino za
ngeli ya U-ZI kwa usahihi katika
mawasiliano.
uwanja nyanja, waraka nyaraka,
uzi nyuzi, ulimi –ndimi, uta
nyuta, uteo - teo. Tathmini majibu ya
mwanafunzi.
Katika shughuli ya 4, waongoze
wanafunzi wawiliwawili wasome
mafungu ya maneno yaliyo kwenye
vitabu vyao. Mwelekeze mwanafunzi
kuandika mafungu ya maneno
katika umoja na wingi akitumia
nomino alizopewa kitabuni mwake.
Wanafunzi wabadilishane madaftari
ili watathmini mafungu yao.
Mhimize mwanafunzi afanye kazi ya
ziada akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini usahihi wa nomino
za ngeli ya U-ZI atakazoandika katika
umoja na wingi za sehemu za mwili
na vitu vinavyopatikana nyumbani
kwao.
86
Kimeidhinishwa na KICD
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 65-67)
Umoja na wingi wa sentensi
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vipatanishi
vya ngeli ya U-ZI kwenye sentensi.
b) Kuunda sentensi akitumia nomino
za ngeli ya U-ZI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa
kisarufi.
c) Kufurahia matumizi ya ngeli ya
U-ZI katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, unajua nomino gani za ngeli ya
U-ZI?
2. Je, nomino za ngeli ya U-ZI
huchukua viambishi vipatanishi
gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutunga sentensi sahihi
kwa maneno yake mwenyewe katika
umoja na wingi akitumia nomino za
ngeli ya U-ZI.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotafuta mtandaoni picha
za nomino za ngeli ya U-ZI na
kuzitungia sentensi katika umoja na
wingi.
(c) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kutambua
viambishi vipatanishi vya ngeli ya
U-ZI.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapofanya
shughuli zinazohusu ngeli ya U-ZI
akiwa peke yake hivyo kujifunza
kujitegemea maishani.
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kuunda sentensi sahihi katika
ngeli ya U-ZI.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi
anapotunza vifaa vyake vya
ujifunzaji anavyotumia kama vile
tarakilishi, madaftari na vifaa halisi
vinavyopatikana katika ngeli ya U
ZI.
Uzalendo
Unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake wa asili
mbalimbali katika vikundi kuunda
sentensi katika ngeli ya U-ZI katika
umoja na wingi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazofunza
kuhusu nomino na ngeli.
87
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapojifunza kutunga
sentensi sahihi katika ngeli ya U-ZI
atatumia lugha kwa ufasaha hivyo
kuimarisha mawasiliano katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona wanaweza kutumia breli
kutambua viambishi vipatanishi
vya ngeli ya U-ZI katika sentensi.
Pia, wanaweza kusikiliza maelezo
kuhusu vipatanishi vya ngeli ya
U-ZI kutoka kwa mwalimu au
wanafunzi wenzao na kujifunza.
Wanafunzi wanaong’amua
wanayojifunza upesi wanaweza
kupewa mazoezi zaidi ya
kubuni na kuandika aya moja
au zaidi wakitumia sentensi
zenye vipatanishi vya ngeli ya
U-ZI. Wanafunzi wanaong’amua
wanayofundishwa polepole
watengewe muda zaidi wa
kuendelea kujifunza baada ya
masomo.
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kusikia au kuzungumza
wanaweza kusaidiwa na mfasiri
wa lugha ishara katika ujifunzaji
wao.
4.2.1 Umoja na wingi wa
sentensi: Ngeli ya U–ZI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 65-67)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu viambishi
vipatanishi vya sentensi katika ngeli
ya U-ZI ili kufanikisha ufunzaji wako.
Vilevile,
Andaa sentensi zenye vipatanishi vya
ngeli ya U-ZI.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kuweza kutumika
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona katika ujifunzaji wao.
Andaa vifaa halisi kama vile uteo, uzi,
wembe, ufunguo, uta n.k. Vifaa hivi
vitakusaidia katika ufunzaji wa mada
hii.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 65
2. Kamusi ya Kiswahili
3. Vifaa halisi kama vile uteo, uzi,
ufunguo, wembe, uta n.k.
4. Mfasiri wa lugha ishara, breli.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo kwa kuwauliza
wanafunzi wataje mifano ya nomino za
ngeli ya U-ZI ambazo walijifunza katika
kipindi kilichotangulia. Tathmini majibu
ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 1, waongoze
wanafunzi wawiliwawili kukamilisha
sentensi zilizo chini ya michoro iliyo
vitabuni mwao. Majibu tarajiwa:
a) ubao, mbao b) uteo, teo
c) uta, nyuta. Waelekeze wanafunzi
kuchunguza sentensi walizokamilisha
na kutambua kuwa viambishi
vipatanishi katika sentensi hizo ni u-
katika umoja na zi- katika wingi.
Mwelekeze mwanafunzi ajaze jedwali
lililo kitabuni mwake katika umoja
na wingi kwa usahihi katika shughuli
88
Kimeidhinishwa na KICD
ya 2. Majibu tarajiwa: 1. Nyuzi zetu
zimekatika. 2. Uta ule umevunjika.
3. Ukuta mkubwa utajengwa.
4. Pembe ndefu zimevunjika.
5. Nyaraka hizi zimeandikwa.
Katika shughuli ya 3, mwongoze
mwanafunzi kutunga na kuandika
kwenye daftari lake sentensi tano
katika umoja na wingi akitumia
nomino za ngeli ya U-ZI. Azingatie
upatanisho sahihi wa kisarufi na
apigie mistari viambishi vya ngeli
ya U-ZI katika sentensi alizotunga.
Wanafunzi wabadilishane madaftari
ili watathmini sentensi zao.
Mhimize mwanafunzi afanye kazi
ya ziada akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Tathmini sentensi
atakazotunga mwanafunzi. Hakikisha
ni sahihi na zimezingatia upatanisho
sahihi wa kisarufi.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua viambishi
vipatanishi vya ngeli ya U-ZI
kwenye sentensi.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuunda sentensi akitumia
nomino za ngeli ya U-ZI katika
umoja na wingi akizingatia
upatanisho sahihi wa kisarufi.
3. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kutumia sentensi za
ngeli ya U-ZI kwa usahihi katika
mawasiliano.
Shughuli ya nje ya darasa
Waongoze wanafunzi kutembelea
mtaa wowote wa mabanda ulio
karibu na shule yenu. Wanafunzi
wawaeleze wanajamii kuhusu njia
mbalimbali za kukabiliana na umaskini
walizofundishwa. Wanajamii pia
wawaeleze njia mbalimbali wanazotumia
kukabiliana na umaskini katika mtaa
wao. Mwongoze kila mwanafunzi
kuandika insha ya maelezo kuhusu
njia mbalimbali za kukabiliana na
umaskini walizojifunza kutoka kwa
wanajamii hao. Shughuli hii itakuza
utangamano, uzalendo, uwazaji kina na
ujasiri wa kujieleza.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Kubali methali zozote tano
zinazohusu bidii. Hakikisha maana
na matumizi ya methali hizo ni
sahihi.
2. Mwalimu akubali ubeti wowote wa
shairi linalohusu bidii lililotungwa na
mwanafunzi. Hakikisha mwanafunzi
ameonyesha vina, idadi ya mizani
na idadi ya mishororo katika ubeti
aliotunga.
3. Kubali insha ya maelezo inayohusu
jinsi mwanafunzi anavyoweza
kuweka pesa akiba ili kukabiliana
na umaskini. Insha hiyo izingatie
muundo, mtindo na kanuni zifaazo.
4. Majibu ya jedwali: a) nyayo b) ufa
c) nyimbo d) ubao e) udevu
5. Kubali sentensi zozote tano sahihi
zilizoandikwa katika umoja na wingi
zenye nomino za ngeli ya U-ZI.
89
Kimeidhinishwa na KICD
MAADILI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 68-78)
Utangulizi
Maadili ni tabia njema ya ubinadamu.
Mtu mwenye maadili huwa na utu.
Maadili humfanya mtu kuwa mwadilifu
katika kila shughuli anayotekeleza.
Maadili yatawasaidia wanafunzi kuwa
wazalendo na viongozi wa kutegemewa
nchini na watakuwa kielelezo kwa vizazi
vijavyo.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Matamshi bora: Ushairi), Kusoma kwa
mapana (Makala), Kuandika insha za
wasifu na Sarufi (umoja na wingi wa
nomino ngeli ya U-YA na umoja na
wingi wa sentensi katika ngeli ya U-YA).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 68-70)
Matamshi bora
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kukariri shairi kwa kuzingatia
matamshi na mahadhi mbalimbali.
b) Kueleza maana ya msamiati ambao
umetumiwa katika shairi.
c) Kutumia msamiati uliotumiwa
katika shairi kuboresha
mawasiliano.
d) Kuonyesha ufahamu wa ujumbe
katika shairi kwa kujibu maswali.
e) Kuchangamkia ushairi kama njia
ya kujieleza kwa ufasaha.
Maswali dadisi
1. Ushairi unatofautiana vipi na
maandishi mengine?
2. Ushairi unaweza kuboresha vipi
mazungumzo yako?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Kujiamini na kujithamini
Mwanafunzi atakuza umilisi huu kwa
kuweza kukariri shairi kwa mahadhi
mbalimbali na kujibu maswali kuhusu
shairi kwa usahihi.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu utakuzwa mwanafunzi
akishirikiana na wenzake katika
vikundi kukariri shairi, kutunga
shairi, kujadili ujumbe wa shairi na
kutambua vina na mizani katika
shairi.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu utakuzwa mwanafunzi
akiweza kutafuta shairi mtandaoni
na kulisoma na hata kuwasomea
wenzake darasani.
90
Kimeidhinishwa na KICD
(d) Ubunifu
Umilisi huu utakuzwa mwanafunzi
atakapoweza kutunga shairi akiwa
peke yake au akishirikiana na
wenzake katika vikundi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Kukariri mashairi kutamwezesha
mwanafunzi kuwasiliana kwa ufasaha
na ukakamavu hivyo kuyaboresha
mawasiliano yake. Pia, anaweza
kuibukia kuwa malenga au manju
stadi maishani.
Elimu ya mazingira
Hii itakuzwa kutokana na ujumbe katika
mashairi mbalimbali ambao unaweza
kuhusu utunzaji wa mazingira. Mtu
mwenye maadili huyatunza na kuyajali
mazingira yake.
Uraia
Uraia utakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kujadili mashairi yanayohusu
maadili.
Uhusiano na maadili
Kutokana na mafunzo na ujumbe
wa mashairi katika muktadha wa
maadili, mwanafunzi atajifunza
maadili mbalimbali kama vile
heshima, uwajibikaji, umoja, amani,
haki n.k.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanashughulikia mada
ya ushairi.
Muziki
Somo hili hushughulikia mashairi na
nyimbo za mahadhi mbalimbali.
Somo la Dini
Somo hili hushughulikia maadili
mbalimbali anayopaswa kuwa nayo
kila mcha Mungu.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapokariri
mashairi katika hafla mbalimbali
atawahamasisha wanajamii
kuhusu maadili na masuala ibuka
mbalimbali.
Mwanafunzi anapotunga shairi
anawaza kwa kina. Kutokana na hilo
atakuza ubunifu wake na hivyo kuwa
mbunifu katika kutatua changamoto
zinazomkumba na kuikumba jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
watumie mashine za breli kusoma
shairi. Pia, wanaweza kusikiliza shairi
likisomwa na kukaririwa na mwalimu
au wanafunzi wenzao.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza wanaweza
kutambua maana za msamiati wa
shairi kwa kuandika au kutumia
lugha ishara ikiwa mwalimu
anaifahamu. Mfasiri wa lugha ishara
anaweza kushirikishwa.
Wanafunzi walio na matatizo mengine
ya kiafya au kisaikolojia wasaidiwe ili
waweze kutekeleza ujifunzaji wao.
91
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wanaoelewa
wanayofundishwa upesi wapewe
mazoezi zaidi ya kufanya kama vile
kutunga shairi kuhusu maadili.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuelewa wanayofundishwa upesi
watengewe muda zaidi wa kujifunza
baada ya masomo jioni.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 68
2. Mashine za breli
3. Nakala za mashairi mbalimbali
4. Rekodi ya shairi
5. Kamusi ya Kiswahili
6. Rununu, tarakilishi au redio.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza
wanafunzi wakariri shairi lolote
ambalo wamewahi kujifunza. Tathmini
matamshi yao.
Katika shughuli ya 1, wachezee
wanafunzi rekodi ya shairi ambayo
imeambatanishwa na kitabu hiki.
Wanafunzi wasikilize kwa makini.
Wapange wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na uwezo wao kisha
wakariri shairi hilo kwa zamu na kwa
mahadhi mbalimbali wakiwa katika
vikundi.
Waongoze kujadili ujumbe wa
shairi hilo. Ikiwa kuna muda, kila
mwanafunzi akariri shairi hilo
akiwa peke yake huku mwenzake
wakimsikiliza na kutathmini
matamshi yake.
Waelekeze wanafunzi kujadili maana
za msamiati uliokolezwa rangi
kwenye shairi walilokariri. Wanaweza
kutumia kamusi ya Kiswahili.
Mwanafunzi atambue vina vya kati
na vya mwisho wa ubeti wa tatu. Jibu
tarajiwa: ko, ja.
Waongoze wanafunzi kujadiliana
kuhusu umuhimu wa maadili
maishani. Majibu tarajiwa: Maadili
1.1 Matamshi Bora: Ushairi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 68-70)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti zaidi kuhusu maadili mbalimbali na
jinsi ya kuandika na kuchambua shairi ili
kuwaelekeza wanafunzi ipasavyo. Vilevile,
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumika na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Andaa mashairi mbalimbali
yanayohusu maadili ambayo
wanafunzi watatumia katika
ujifunzaji wao. Unaweza
kuyatoa kwenye magazeti ya
Kiswahili, vitabu vya Kiswahili au
mtandaoni.
Hakikisha unafahamu mahadhi
mbalimbali ya kukariri mashairi
ili uwafunze wanafunzi kukariri
mashairi mbalimbali.
Unaweza kurekodi mashairi
mbalimbali yaliyokaririwa kwa
mahadhi tofautitofauti.
Hakikisha una simu, tarakilishi
au tepurekoda ambayo itatumiwa
na wanafunzi kurekodi mashairi
watakayotunga na kuyaimba
darasani.
92
Kimeidhinishwa na KICD
huongoza utaratibu wa shughuli
za kila jamii. Maadili huwezesha
watu kuishi kwa amani. Maadili
huzuia visa vya utovu wa nidhamu
katika jamii. Maadili husababisha
maendeleo ya kiuchumi katika jamii.
Maadili yanaweza kuzuia baadhi
ya magonjwa na ajali. Maadili
hutuwezesha kuwa na mazingira safi.
Mwalimu akubali jibu lolote sahihi.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi yao kisha uwaelekeze
kutunga shairi la beti mbili kuhusu
maadili. Wahakikishe mashairi
yao yanazingatia kanuni za ushairi
zifaazo. Wanafunzi watambue vina
vya kati na vya mwisho katika
beti walizotunga kisha wawaimbie
wenzao mashairi waliyotunga kwa
mahadhi mbalimbali. Mwalimu ampe
mwanafunzi mmoja simu au redio
ili awarekodi wenzake wakikariri au
wakiimba mashairi yao. Shughuli
hii itawasaidia wanafunzi kukuza
kujiamani na kujithamini kwao. Pia,
itakuza ujuzi wao wa kidijitali.
Katika kazi ya ziada, mwambie
mwanafunzi atafute shairi lolote
linalohusu maadili mtandaoni
au kwenye gazeti la Kiswahili
na aliandike katika daftari lake.
Amkaririe mzazi au mlezi wake
shairi hilo na wajadili ujumbe wake.
Tathmini kuwa kazi hii ilifanyika
kabla ya kipindi kingine.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kukariri shairi kwa
kuzingatia matamshi bora na
mahadhi mbalimbali.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kueleza maana ya
msamiati uliotumiwa kwenye
shairi na kuutumia kuboresha
mawasiliano yake.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kufahamu ujumbe katika
shairi.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 70-72)
Kusoma kwa mapana
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua makala ya kusoma
katika maktaba ili kuimarisha
uchaguzi bora wa makala.
b) Kusoma makala mbalimbali ili
kujenga ufasaha wa lugha.
c) Kufurahia kuyasoma makala
mbalimbali ili kujenga ufasaha wa
lugha.
Maswali dadisi
1. Unapenda kusoma makala ya aina
gani? Wewe huyapata wapi makala?
2. Ni ujumbe upi uliopata kwenye
makala uliyowahi kusoma?
3. Unazingatia nini unapochagua
makala ya kusoma?
93
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Kujiamini
Mwanafunzi anaposoma makala
na kusimulia aliyojifunza ataukuza
umilisi huu.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapojadiliana na wenzake katika
vikundi kuhusu makala aliyosoma.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Unakuzwa mwanafunzi anapotafuta
makala ya kusoma mtandaoni kwa
kutumia vifaa vya kidijitali.
(d) Hamu ya kujifunza zaidi
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapochangamkia kusoma makala
kuhusu maadili na kuendelea
kutafuta makala zaidi ili asome na
kujifunza shuleni na nje ya shule.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Mwanafunzi anapochagua makala ya
kusoma atapata uwezo wa kuongoza na
kuelekeza usomaji wake hivyo kuweza
kuwajibika na kujitegemea maishani.
Ushauri nasaha
Utakuzwa mwanafunzi akisoma
makala mbalimbali kuhusu maadili
yatakayomfaa maishani ili kuwa
mwadilifu.
Uhusiano na maadili
Mwanafunzi anaposoma makala
mbalimbali yanayohusu maadili
atajifunza na kuzingatia maadili kama
vile: uzalendo, upendo, uwajibikaji,
haki, usawa, heshima na amani.
Uhusiano na masomo mengine
1. Somo la Dini
Mwanafunzi hujifunza maadili
mbalimbali katika somo hili
linalompasa kila mcha Mungu kuwa
mwadilifu.
2. Somo la Jamii
Somo hili huangazia maadili katika
jamii ili kuwawezesha wanajamii
kuishi vyema.
3. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hulenga kukuza umilisi
wa kusoma kwa ustadi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atatumia mawazo na
maadili aliyopata kutokana na makala
mbalimbali aliyosoma hivyo kuweza
kuwaelekeza wenzake katika jamii.
Mwanafunzi akichangamkia usomaji
wa makala huenda akaanzisha mradi
wa maktaba kijijini au atakapoishi
baada ya kuhitimu masomo yake na
kukuza stadi ya kusoma katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kuona waletewe vifaa halisi
kama vile tarakilishi na magazeti
darasani ili waweze kuvitambua
kwa kuvigusa ili kutambua
makala hupatikana wapi. Pia,
wanaweza kutumia breli kusoma
makala mbalimbali.
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kusikia au kuzungumza
waelekezwe kutambua makala
kwa kutumia lugha ishara.
94
Kimeidhinishwa na KICD
6. Nakala za majarida yenye makala
yanayohusu maadili.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwapanga
wanafunzi katika vikundi kisha uwaulize
iwapo wamewahi kusoma makala yoyote.
Makala hayo yalihusu nini? Waliyapata
wapi? Walipata mafunzo gani?
Wanapenda kusoma makala gani? Kwa
nini wanapenda makala hayo? Tathmini
majibu ya wanafunzi.
Waelekeze wanafunzi wawiliwawili
kufanya shughuli ya 1 kwa kujadili
michoro iliyo vitabuni mwao.
Michoro hiyo ni ya gazeti, tarakilishi,
kitabu cha hadithi na kipakatalishi.
Waeleze wanafunzi kuwa makala
mbalimbali ya kusoma yanaweza
kupatikana kutoka kwenye vifaa hivi.
Wanafunzi wajadiliane kuhusu makala
waliyowahi kusoma, wanachozingatia
wanapotafuta makala ya kusoma na
makala wanayopenda kusoma.
Katika shughuli ya 2, mwelekeze kila
mwanafunzi kuchagua makala yoyote
kuhusu maadili katika maktaba na
ayasome. Somo hili linaweza kufanyikia
maktabani iwapo shule ina maktaba
yenye nafasi ya kutosha. Iwapo shule
haina maktaba, somo hili lifanyikie
darasani. Mwalimu anaweza kuwapa
wanafunzi makala tofauti tofauti ya
kusoma kisha wajadiliane kuhusu
mafunzo watakayopata.
Mwanafunzi atumie kamusi ya
Kiswahili kupata maana ya msamiati
mpya uliotumika katika makala
aliyosoma.
Mfasiri wa lugha ishara anaweza
kushirikishwa.
Wanafunzi wasioweza kusoma na
kung’amua yaliyo kwenye makala
wakati wa kipindi watengewe
muda maalum baada ya masomo
jioni ili waweze kujifunza zaidi.
Pia, mwalimu anaweza kubuni
shughuli nyingine tofauti na zile
alizotumia wakati wa kipindi ili
kuwafaa wanafunzi hao katika
ujifunzaji wao.
2.1 Kusoma kwa mapana:
Makala
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 70-72)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu umuhimu wa maadili
mbalimbali ili kuboresha ufunzaji kwa
kuwaelekeza wanafunzi vyema. Pia,
Hakikisha tarakilishi
utakayotumia ina makala
yanayohusu maadili unayotarajia
kutumia kuwafunzia wanafunzi.
Kusanya magazeti na vitabu
vyenye makala kuhusu maadili.
Hivi vitakusaidia kufanikisha
ufunzaji wako.
Hakikisha una mashine za breli
ili wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona wazitumie kujifunzia.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 70
2. Kamusi ya Kiswahili
3. Mashine za breli na tarakilishi
4. Nakala za magazeti yenye makala
yanayohusu maadili
5. Vitabu vya hadithi zinazohusu
maadili
95
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya 3, mwanafunzi
aelekezwe kusoma makala yaliyo
kitabuni mwake kisha ajibu maswali
aliyopewa. Tathmini majibu ya
mwanafunzi kulingana na makala
husika. Majibu tarajiwa:
1. Mtu mwenye maadili ni mpole, ni
mzalendo, anafanya kazi kwa hiari
yake mwenyewe, si mwizi, si fisadi na
anawaheshimu watu.
2. Wanafunzi watumie kamusi ya
Kiswahili kupata maana za maneno
yaliyokolezwa rangi kwenye makala.
3. Tathmini majibu ya wanafunzi. Kwa
mfano: Nchi yetu kuwa na amani,
kuwa na mazingira safi, wananchi
kuwa na afya njema, kupungua
kwa visa vya uhalifu na ajali za
barabarani, ufisadi utakwisha n.k.
4. Kubali kitendo chochote ambacho si
cha kimaadili.
Katika kazi ya ziada, mwanafunzi
asaidiwe na mzazi au mlezi wake
kutafuta makala ya kusoma
yanayohusu maadili. Ayasome na
kuandika muhtasari wa ujumbe
aliopata. Tathmini kazi ya kila
mwanafunzi.
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 73-74)
Insha za wasifu
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vipengele vya kimuundo
vya insha za wasifu.
b) Kuandika insha ya wasifu kwa
kuzingatia muundo na mtindo
ufaao.
c) Kufurahia uandishi wa insha
za wasifu ili kukuza stadi ya
kuandika.
Maswali dadisi
1. Ni nini maana ya insha ya wasifu?
2. Unazingatia nini unapoandika
insha ya wasifu?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Hamu ya ujifunzaji
Mwanafunzi anapoweza kuandika insha
ya wasifu inayohusu maadili atakuwa
na hamu ya kuendelea kujifunza hasa
baada ya kutambua mada mbalimbali
zinazoweza kutungiwa insha hiyo.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili vipengele vya
kimuundo vya insha ya wasifu, mada
zinazoweza kutungiwa insha za
wasifu na ujumbe wa insha ya wasifu.
Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi anapoweza
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua vizuri makala
yanayohusu maadili katika
maktaba kwa kuzingatia hatua
salama katika uchaguzi.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kusoma makala
mbalimbali na kueleza ujumbe
husika.
96
Kimeidhinishwa na KICD
kutunga insha ya wasifu kwa maneno
yake mwenyewe bila kunakili insha za
wenzake.
Kujiamini na kujithamini
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutunga insha ya wasifu
iliyo bora na kuwasomea wenzake
darasani.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Kutokana na kufahamu kuandika
insha, mwanafunzi atakuza uandishi
wake ambao unaweza kumpa mapato
baadaye hasa ikiwa atashiriki katika
uandishi wa makala mbalimbali
kwa malipo. Pia, atajifunza mengi
yanayohusu maisha anapotunga
insha za wasifu kuhusu watu, vitu na
mahali mbalimbali.
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kuandika na kujadili insha za wasifu.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoiandika
insha ya wasifu akiwa peke yake
na hivyo kujifunza kuwajibika na
kujitegemea. Pia, anapokamilisha kazi
yake kwa muda unaofaa na kuvitunza
vifaa vyake vya kujifunzia.
Umoja na amani
Maadili haya yatakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa amani bila kuzua
ugomvi.
Heshima na upendo
Maadili haya yatakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi na kumpa kila mmoja
wao fursa ya kuweza kuchangia katika
majadiliano yao.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada ambazo
huangazia uandishi wa insha.
2. Somo la Jamii
Somo hili lina mada zinazoangazia
maelezo kuhusu watu na mahali
mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wanajamii
kuhusu umuhimu wa kuwa na maadili
kutokana na vitendo vyake vya kimaadili
katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye changamoto ya
kutumia mkono kuandika wapewe
muda wa kutosha kuandika kwa
kutumia kiungo kingine cha mwili
walichozoea kutumia.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia wanaweza kutumia vifaa
vya kuwawezesha kusikia au
watazame na kusoma maelezo
kuhusu insha za wasifu vitabuni
na ubaoni. Mfasiri wa lugha
ishara anaweza kushirikishwa.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
97
Kimeidhinishwa na KICD
kuona watumie mashine za breli
ili kujifunza.
wasifu mbalimbali na uwaongoze
kutambua vipengele vya muundo
na mtindo vilivyotumiwa kuandika
insha hizo. Tathmini majadiliano ya
wanafunzi.
Katika shughuli ya 2, waelekeze
wanafunzi wasome wasifu ulio
kitabuni mwao kisha wajibu maswali
waliyopewa. Tathmini majibu ya
wanafunzi. Majibu tarajiwa:
1. Sikiliza maelezo ya mwanafunzi ili
utathmini iwapo wameelewa ujumbe
wa wasifu huo. 2. Tathmini majibu
ya wanafunzi. Kwa mfano: kuwepo
kwa mada kuhusu mtu, kitu, mnyama
au mahali, kuwepo kwa aya na
kuzingatia lugha sahihi. 3. Wanafunzi
watumie kamusi ya Kiswahili kuelewa
maana ya msamiati uliokolezwa rangi
kwenye wasifu.
Waongoze wanafunzi kujadili mada
mbalimbali zinazoweza kutungiwa
insha za wasifu. Hatimaye, wataje
maadili ambayo wangependa kiranja
wa darasa lao azingatie. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 3, mwongoze
mwanafunzi kuandika insha ya
wasifu kuhusu mtu yeyote anayemjua
mwenye maadili. Hakikisha insha
anayoandika mwanafunzi haipungui
maneno 150 na inazingatia mada,
muundo, mtindo wa kuandika insha
ya wasifu pamoja na lugha sahihi.
Mpe mwanafunzi kazi ya ziada
atakayofanya akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake.
Hakikisha kazi hii imefanyika kwa
3.1 Insha za wasifu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 73-74)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Andaa nakala mbalimbali za insha
za wasifu utakazowapa wanafunzi ili
kutambua vipengele vya muundo na
mtindo vya insha za wasifu. Vilevile,
Hakikisha una mashine za breli
zilizo sawa ili wanafunzi wasio
na uwezo wa kuona wazitumie
kujifunza.
Hakikisha wanafunzi wana vifaa
vya kuandikia insha kama vile
penseli, kifutio na kichongeo.
Tafiti kuhusu mada mbalimbali
ambazo zinaweza kutungiwa
insha za wasifu ili kuwaongoza
wanafunzi zaidi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 73
2. Kamusi ya Kiswahili
3. Nakala zenye insha ya wasifu
mbalimbali
4. Mashine za breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa shughuli
ya 1 kwa kuwaongoza wanafunzi
kujikumbusha kuhusu insha za wasifu
walizowahi kujifunza. Wanafunzi wajadili
sifa za insha hizo.
Wapange wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na uwezo wao
kisha uwape nakala zenye insha za
98
Kimeidhinishwa na KICD
kumwuliza mwanafunzi maswali
kuhusu wasifu wa mtu aliyeelezwa na
mzazi au mlezi wake.
3. Umoja na wingi wa mafungu ya
maneno katika ngeli ya U-YA
huandikwa vipi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Kujiamini na kujithamini
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutambua kwa usahihi
nomino za ngeli ya U-YA, kuziandika
katika umoja na wingi na kuzitungia
mafungu ya maneno kwa usahihi.
(b) Ubunifu
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi
anapotunga mafungu ya maneno
katika umoja na wingi akitumia
nomino za ngeli ya U-YA kwa
maneno yake mwenyewe bila
kunakili mafungu ya wenzake.
(c) Mawasiliano na ushirikiano
Mwanafunzi anaposhirikiana na
kuwasiliana na wenzake katika
vikundi kutambua nomino za ngeli
ya U-YA na kuzitungia mafungu ya
maneno sahihi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anapotangamana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kutambua nomino za ngeli ya U-YA
na kuzitungia mafungu sahihi.
Stadi za maisha
Mwanafunzi anapotambua nomino za
ngeli ya U-YA na kuzitungia mafungu
ya maneno katika umoja na wingi kwa
usahihi akiwa peke yake atakuza stadi
ya kujitegemea maishani.
4.1 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 74-76)
Ngeli ya U-YA
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya
U-YA ili kuzitofautisha na nomino
katika ngeli nyingine.
b) Kuandika nomino za ngeli ya U-YA
katika umoja na wingi.
c) Kuandika umoja na wingi wa
mafungu ya maneno katika ngeli
ya U-YA.
d) Kuchangamkia kutumia nomino za
ngeli ya U-YA katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, ni nomino zipi hupatikana
katika ngeli ya U-YA?
2. Nomino za ngeli ya U-YA
huandikwa vipi katika umoja na
wingi?
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua vipengele vya
kimuundo na kimtindo vya insha
ya wasifu.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kuandika insha ya wasifu
kwa kuzingatia muundo na
mtindo ufaao.
99
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutambua nomino za ngeli
ya U-YA na kuzitungia mafungu ya
maneno sahihi bila kuzua ugomvi.
Uzalendo
Uzalendo unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
asili mbalimbali katika vikundi
kutambua nomino za ngeli ya U-YA
na kuzitungia mafungu ya maneno
yaliyo sahihi.
Uwajibikaji
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi
anapovitunza vifaa anavyotumia
kujifunzia pamoja na kukamilisha
kazi yake kwa wakati unaofaa.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazofunza
ngeli za nomino.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapotambua nomino za
ngeli ya U-YA na kuzitungia mafungu
ya maneno yaliyo sahihi ataboresha
mawasiliano katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza wanaweza
kutambua nomino za ngeli ya
U-YA kwa kuzikoleza rangi
kwenye tarakilishi au kuzipigia
mistari kwenye madaftari yao.
Mfasiri wa lugha ishara anaweza
kushirikishwa.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona watumie breli kujifunza.
Wanafunzi wasioweza kutambua
nomino za ngeli ya U-YA kwa
urahisi wapewe shughuli zaidi
ili wajifunze. Unaweza kutunga
wimbo au shairi kwa kutumia
nomino za ngeli ya U-YA ili
kuwawezesha wanafunzi hao
kuimba au kukariri ili kutambua
nomino za ngeli ya U-YA kwa
urahisi.
4.1.1 Umoja na wingi wa
nomino - Ngeli ya U-YA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 74-76)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti zaidi kuhusu nomino za ngeli ya U-YA
ili kuwaongoza wanafunzi vyema wakati wa
ufunzaji. Vilevile,
Ikiwa wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza watatambua
nomino za ngeli ya U-YA kwa
kuzikoleza rangi kwenye tarakilishi,
hakikisha tarakilishi zipo na zinaweza
kutumika. Pia, unaweza kumwarifu
mfasiri wa lugha ishara ili awasaidie
wanafunzi hawa kufanikisha ujifunzaji
wao.
Wanafunzi wasioweza kungamua
wanayofunzwa upesi watengewe
muda wa kujifunza zaidi baada ya
masomo jioni au asubuhi kabla ya
masomo kuanza. Katika mafunzo
ya ziada, unaweza kuwapa shughuli
tofauti na ulizowapa darasani ili
100
Kimeidhinishwa na KICD
wajifunze vyema. Mfano, unaweza
kutunga wimbo au shairi kwa
kutumia nomino za ngeli ya U-YA
na wanafunzi hao wakauimba
wimbo huo au kukariri shairi hilo na
kutambua nomino za ngeli ya U-YA.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 74
2. Kamusi ya Kiswahili
3. Kapu lenye kadi zilizoandikwa
nomino za ngeli ya U-YA pamoja
na nomino za ngeli nyingine
4. Mashine za breli, tarakilishi
5. Mfasiri wa lugha ishara
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwauliza
wanafunzi wataje mifano ya nomino
za ngeli mbalimbali ambazo
wameshajifunza. Tathmini majibu ya
wanafunzi.
Katika shughuli ya 1, wapange
wanafunzi katika vikundi viwili
kulingana na uwezo wao. Waongoze
kusoma umoja na wingi wa nomino
za ngeli ya U-YA zilizo vitabuni
mwao. Wanafunzi wabaini kuwa
nomino za ngeli ya U-YA walizosoma
huanza kwa herufi u- katika umoja
na ma- katika wingi.
Waelekeze wanafunzi kujadili maana
za nomino walizosoma kwenye
jedwali. Wanaweza kutumia kamusi
ya Kiswahili. Tathmini majibu ya
wanafunzi.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 2, kwa kuchagua nomino
za ngeli ya U-YA kutoka kwenye
mchoro ulio kitabuni mwake.
Majibu tarajiwa: upishi, ulezi,
ugonjwa, ubele, manyoya. Mwongoze
mwanafunzi kuandika umoja au
wingi wa nomino za ngeli ya U-YA
alizoteua kutoka kapuni. Majibu
tarajiwa: mapishi, malezi, magonjwa,
mabele, unyoya.
Katika shughuli ya 3, waongoze
wanafunzi kusoma mafungu ya
maneno yaliyo vitabuni mwao na
wajadili waliyogundua.
Waongoze wanafunzi kutambua
kuwa vivumishi vinapotumiwa
pamoja na nomino za ngeli ya U-YA
huchukua m-/mw katika umoja na
ma-/me katika wingi: Ulezi mzuri -
malezi mazuri.
Mwelekeze mwanafunzi kutumia
nomino tano za ngeli ya U-YA
kutunga mafungu ya maneno
akitumia mfano aliopewa katika
nambari 1. Mwalimu atathmini
usahihi wa kila fungu la maneno
ambalo mwanafunzi atatunga.
Mhimize kila mwanafunzi afanye
kazi ya ziada ambapo anatarajiwa
kujaza kwa usahihi mapengo kwenye
kifungu alichopewa kitabuni mwake.
Majibu tarajiwa: Mapishi mazuri,
ulezi mwema, ubua mwembamba,
magonjwa mengi.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua nomino za
ngeli ya U-YA na kuzitofautisha na
nomino za ngeli nyingine.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
101
Kimeidhinishwa na KICD
akiwasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kutunga
sentensi sahihi akitumia nomino za
ngeli ya U-YA.
(c) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunga sentensi sahihi katika ngeli ya
U-YA kwa maneno yake mwenyewe
bila kunakili sentensi za wenzake.
(d) Uwazaji wa kina
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiria kuhusu sentensi sahihi
za kutunga katika ngeli ya U-YA
akizingatia muktadha wa maadili.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Mwanafunzi anapojifunza viambishi
vipatanishi vya ngeli ya U-YA
ataweza kutunga sentensi sahihi na
kuzungumza kwa ufasaha hivyo
kuyaboresha mawasiliano yake.
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
asili mbalimbali katika vikundi
kutunga sentensi sahihi katika ngeli
ya U-YA.
Uhusiano na maadili
Amani na umoja
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa amani kusoma sentensi za
ngeli ya U-YA katika umoja na wingi
na kutambua viambishi vipatanishi vya
ngeli hiyo bila kuzua vurugu.
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 76-78)
Ngeli ya U-YA
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vipatanishi
vya ngeli ya U-YA kwenye
sentensi.
b) Kuunda sentensi akitumia
nomino za ngeli ya U-YA katika
umoja na wingi akizingatia
upatanisho wa kisarufi.
c) Kufurahia matumizi ya ngeli ya
U-YA katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, ni nomino zipi hupatikana katika ngeli
ya U-YA?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunga sentensi kwa usahihi
katika ngeli ya U-YA na kuwasomea
wenzake.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaweza kuandika nomino za
ngeli ya U-YA katika umoja na
wingi.
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kuandika kwa usahihi
umoja na wingi wa mafungu ya
maneno katika ngeli ya U-YA.
102
Kimeidhinishwa na KICD
Uwajibikaji na uaminifu
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapojitungia sentensi zake
mwenyewe akitumia nomino za
ngeli ya U-YA na anapotunza
vifaa anavyotumia kujifunzia. Pia,
anapokamilisha kazi zake kwa wakati
unaofaa.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazofunza
kuhusu ngeli za nomino.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapotunga sentensi sahihi
akitumia nomino za ngeli ya U-YA
atatumia lugha ya Kiswahili kwa ufasaha
na kuimarisha mawasiliano katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona wanaweza kupewa vitu
halisi vinavyopatikana katika
ngeli ya U-YA kama vile unyoya,
ubua na mawele ili waviguse na
kuvitambua.
Wanafunzi wasioweza kuona mbali
wakae karibu na ubao na wasioweza
kuona karibu wakae mbali na ubao.
Ili kuboresha kumbukumbu
za anayojifunza mwanafunzi,
mwalimu atayarishe shughuli
maalum za ujifunzaji kulingana
na mahitaji ya kila mwanafunzi.
Kwa mfano, wanafunzi
wanaojifunza upesi kwa kutazama
wapewe picha za nomino za ngeli
ya U-YA ili waweze kuzitambua na
kujifunza.
Wanafunzi wanaojifunza vyema
kupitia kwa kusikia watungiwe
wimbo au shairi lenye nomino
za ngeli ya U-YA na viambishi
vipatanishi vyake sahihi.
4.2 Umoja na wingi wa
sentensi: Ngeli ya U-YA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 76-78)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti kuhusu ngeli ya U-YA ili kuwaelekeza
wanafunzi ipasavyo katika kutunga sentensi
sahihi. Pia,
Unaweza kutunga shairi au wimbo
wenye nomino za ngeli ya U-YA
kabla ya kipindi ikiwa utautumia
kuwafunzia wanafunzi.
Tafuta vifaa halisi kama vile
mabua, manyoya, mabele na
mawele ili uvitumie kutoa mifano
ya nomino katika ngeli ya U-YA.
Hakikisha umeandaa sentensi
kadhaa sahihi za ngeli ya U-YA
ambazo utatumia kuwafunzia
wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 76
2. Chati iliyoandikwa sentensi za
ngeli ya U-YA
3. Vifaa halisi kama vile: mabua,
mawele, mabele, manyoya
4. Kamusi ya Kiswahili
5. Wimbo au shairi lenye nomino za
ngeli ya U-YA.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa shughuli ya
103
Kimeidhinishwa na KICD
1 kwa kuwaambia wanafunzi wasome
sentensi zilizo kwenye jedwali lililo
vitabuni mwao katika umoja na wingi
wakiwa wawiliwawili. Wanafunzi wajadili
walichobaini baada ya kusoma sentensi
hizo. Jibu tarajiwa: Vitenzi kwenye
sentensi katika ngeli ya U-YA, huanza kwa
u- katika umoja na ya- katika wingi.
Mwongoze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 2 kwa kutunga sentensi
zenye upatanisho wa kisarufi katika
umoja na wingi akitumia maneno
ya ngeli ya U-YA aliyopewa kitabuni
mwake. Mwanafunzi atambue
viambishi vya ngeli ya U-YA katika
sentensi alizotunga ambavyo ni u-
katika umoja na ya- katika wingi.
Wanafunzi wabadilishane madaftari
ili watathmini sentensi zao. Waelekeze
wanafunzi ipasavyo.
Katika shughuli ya 3, mwelekeze
mwanafunzi kujaza kwa usahihi
nafasi kwenye sentensi alizopewa
kitabuni mwake. Majibu tarajiwa: 1.
Magonjwa, yatatibiwa 2. Ulezi
3. upishi 4. manyoya 5. mawele.
Mhimize mwanafunzi afanye kazi
ya ziada, akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Atunge kisa kifupi
sahihi akitumia nomino katika ngeli
ya U-YA kisha amsomee mzazi au
mlezi wake kifungu hicho. Tathmini
kifungu atakachotunga mwanafunzi.
Hakikisha anazingatia viambishi
vipatanishi vya ngeli ya U-YA kwa
usahihi.
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi anaweza
kutambua viambishi vipatanishi vya
ngeli ya U-YA kwenye sentensi.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kuunda sentensi sahihi
akitumia nomino za ngeli ya U-YA
katika umoja na wingi akizingatia
upatanisho sahihi wa kisarufi.
Shughuli ya nje ya darasa
Waongoze wanafunzi kutembelea
makao ya wakongwe iliyo karibu na
shule yenu. Wanafunzi wawakaririe
wakongwe hao mashairi yanayohusu
maadili waliyojifunza darasani.
Wakongwe nao wawakaririe wanafunzi
mashairi wanayofahamu hasa
yanayohusu maadili. Wanafunzi
watumie vifaa vya kidijitali kuwarekodi
wakongwe wakikariri mashairi yao.
Shughuli hii itakuza utangamano,
uthamini, uzalendo, upendo na
mawasiliano kuboreshwa.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Kubali majibu ambayo ni maadili.
2. Kubali insha yoyote iliyoandikwa na
mwanafunzi kuhusu mtu mwenye
maadili ya kuigwa. Hakikisha
imezingatia muundo na mtindo
wa kuandika insha za wasifu na
mwanafunzi akutumie insha hiyo
mtandaoni.
3. a) ugonjwa b) ubele c) unyoya
4. a) Uwele wa nyanya umekauka.
b) Upishi mzuri ulimvutia mgeni.
c) Ulezi huu utamkuza mtoto mwenye
maadili.
104
Kimeidhinishwa na KICD
ELIMU YA MAZINGIRA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 79-88)
Utangulizi
Mazingira ni vitu au maumbile ambayo
yanamzunguka kiumbe anapoishi. Elimu
ya mazingira ni muhimu sana katika
maisha ya binadamu. Ni mojawapo ya
masuala mtambuko yanayoangaziwa
na mtaala mpya wa elimu nchini
Kenya. Katika elimu hii, mwanafunzi
atafahamu njia mbalimbali za kuyatunza
na kuyahifadhi mazingira. Vilevile,
atapata kufahamu athari za kuyaharibu
mazingira. Kuyaharibu mazingira ni
kujidhuru mwenyewe na kuidhuru jamii.
Utunzaji wa mazingira ni jukumu letu.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Nahau: Nahau za usafi na mazingira),
Kusoma kwa mapana (Matini), Kuandika
insha ya maelezo na Sarufi (Umoja na
wingi wa nomino ngeli ya KU-KU na
umoja na wingi wa sentensi katika ngeli
ya KU-KU).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 79-80)
Nahau za usafi na mazingira
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua kwa usahihi nahau za
usafi na mazingira katika matini
mbalimbali.
b) Kufafanua maana ya nahau
mbalimbali za usafi na mazingira
kwa kutoa mifano.
c) Kutumia nahau za usafi na
mazingira katika mawasiliano.
d) Kuthamini matumizi ya nahau
za usafi na mazingira katika
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, nahau ni nini?
2. Je, unajua nahau zipi zinazohusu
usafi na mazingira?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Hamu ya kuendelea kujifunza
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kutafuta maana
za nahau na kuzitumia vyema
anapowasiliana na wenzake shuleni
na nje ya shule.
(b) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiria kwa undani kuhusu
maana ya nahau na hata matumizi
yake. Uwazaji huu utamwezesha
105
Kimeidhinishwa na KICD
kutatua changamoto zinazomkumba
maishani kadri ya uwezo wake.
(c) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kujadili
maana na matumizi ya nahau
zinazohusu usafi na mazingira.
(d) Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kujadiliana maana na matumizi ya
nahau za usafi na mazingira.
Uhusiano na masuala mtambuko
Umoja wa kijamii
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili kuhusu nahau za
usafi na mazingira.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapojiamini
na kutumia nahau za usafi na
mazingira katika kuyaboresha
mawasiliano katika jamii.
Elimu ya mazingira
Itakuzwa mwanafunzi anaposhiriki
katika majadiliano kuhusu umuhimu
wa kuyatunza mazingira na njia
mbalimbali za kuyahifadhi mazingira.
Uhusiano na maadili
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana kwa amani na wenzake
katika vikundi kujadili nahau za usafi
na mazingira bila kuzua ugomvi.
Upendo na heshima
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhiriki katika majadiliano
kuhusu nahau za usafi na mazingira
na njia mbalimbali za kuyatunza
mazingira kwa kuyaheshimu maoni
ya kila mwanafunzi. Pia, kwa kumpa
kila mwanafunzi fursa ya kutoa
mchango wake katika majadiliano.
Uwajibikaji
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi
anapoyahifadhi mazingira yake kwa
kutotupa takataka ovyoovyo, kutokata
miti n.k. Pia, kwa kuhifadhi vifaa
vyake vya kujifunzia na kukamilisha
kazi zake kwa wakati unaofaa.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya huangazia mada kuhusu
usafi na mazingira.
2. Sayansi na Teknolojia
Somo hili lina mada zinazoangazia
usafi, utunzaji wa mazingira na
umuhimu wake.
3. Sayansi Kimu
Somo hili lina mada zinazohusu usafi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapotumia nahau
ifaavyo katika mawasiliano yake
atakuwa kielelezo kwa wengine katika
jamii.
Mwanafunzi atatumia mafunzo
kuhusu elimu ya mazingira
kuihamasisha jamii yake kuhusu njia
mbalimbali za kuyatunza mazingira
pamoja na umuhimu wa kuyatunza
na athari za kutoyatunza.
106
Kimeidhinishwa na KICD
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza wanaweza
kutumia lugha ishara katika
mawasiliano yao. Pia, unaweza
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara pamoja na kutumia vifaa
vya kuwawezesha kusikia. Pia,
wanafunzi hawa wanaweza
kuwasiliana na wenzao kupitia
kwa maandishi.
Wanafunzi wenye matatizo ya
kitabia au kisaikolojia wapewe
ushauri nasaha na sheria za
kufuata ziwepo ili kuwawezesha
kujifunza bila usumbufu.
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kuona wanaweza kutumia
mashine za breli kusoma
maelezo kuhusu nahau za usafi
na matumizi yao. Pia, wanaweza
kusikiliza maelezo kuhusu nahau
hizi yakitolewa na mwalimu au
wanafunzi wenzao ili kujifunza.
Unaweza kuandaa picha
au michoro mbalimbali
inayoonyesha njia mbalimbali za
usafi pamoja na njia mbalimbali
za kuyatunza mazingira.
Unaweza kuandaa hadithi
au kifungu cha kuwasomea
wanafunzi darasani kinachohusu
utunzaji wa mazingira, madhara
ya kuyaharibu mazingira au
umuhimu wa usafi. Hivi vitasaidia
kufanikisha ufunzaji wako.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 79
2. Michoro au picha zinazoonyesha
usafi na utunzaji wa mazingira
3. Kamusi ya Kiswahili
4. Kamusi ya misemo na nahau
5. Mfasiri wa lugha ishara, breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo kwa kuwashirikisha
wanafunzi kufanya shughuli ya
1. Waongoze katika kukumbuka
waliyojifunza katika gredi ya nne kuhusu
nahau. Wanafunzi waelezane maana
ya nahau kisha wataje nahau zozote
wanazojua. Nahau ni usemi unaoundwa
kwa kitenzi na nomino wenye maana
isiyo ya moja kwa moja. Mifano ya
nahau: andika meza (kuweka vyakula
mezani kwa ajili ya kula), piga mswaki
(kusafisha meno kwa kutumia mswaki na
dawa maalum), piga deki (safisha sakafu
kwa maji, sabuni na dasta), fyata ulimi
(kunyamaza na kuacha kuongea), piga
kelele (kuongea kwa sauti) n.k. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
1.1 Nahau za usafi na
mazingira
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 79-80)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti zaidi kuhusu mifano ya
nahau za usafi na mazingira pamoja na
maana na matumizi yazo ili kufanikisha
ujifunzaji wa wanafunzi. Pia,
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumika na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona katika ujifunzaji wao.
107
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi wakiwa wawiliwawili
wajadili vitendo vya watu katika
michoro iliyo vitabuni mwao kisha
wajadili nahau zinazoweza kutumiwa
kwa michoro hiyo. Majibu tarajiwa:
a) piga mswaki b) piga deki c) futa
vumbi/pangusa vumbi. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
Waelekeze wanafunzi kutaja mifano
zaidi ya nahau za usafi na mazingira
kisha wajadili maana za nahau hizo.
Mifano: tandika kitanda (tandaza
shuka na blanketi juu ya godoro kwa
njia nadhifu), piga kelele (kuongea
kwa sauti) n.k. Wanafunzi watunge
sentensi sahihi kwa kutumia
nahau walizotaja. Mifano: Zawadi
anatandika kitanda chake.Wanafunzi
wanapiga kelele darasani.
Katika shughuli ya 3, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha wabuni
kifungu kifupi kwa kutumia nahau
za usafi na mazingira walizopewa
vitabuni mwao. Wanafunzi wanaweza
kutumia mifano zaidi ya nahau
za usafi na mazingira kando na
walizopewa vitabuni mwao.
Kila mwanafunzi apewe fursa
ya kuchangia katika utungaji wa
kifungu husika. Waongoze wanafunzi
kuvihariri vifungu vyao ili kuondoa
makosa ya kisarufi. Mwanafunzi
mmoja kutoka katika kila kikundi
awasomee wanafunzi wengine
kifungu walichobuni ili wakitathmini
na kujifunza. Shughuli hii itakuza
ujasiri wa wanafunzi wa kuzungumza
mbele ya watu hivyo kujiamani na
kujithamini.
Mwalimu ahitimishe somo hili kwa
kumhimiza mwanafunzi kufanya
kazi ya ziada akisaidiwa na mzazi
au mlezi wake. Tathmini maelezo
ya mwanafunzi anapowaeleza
wenzake darasani kuhusu namna
wanavyodumisha usafi nyumbani
kwao.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kueleza maana ya nahau
na kutambua nahau za usafi
na mazingira katika matini
mbalimbali.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kutaja mifano ya nahau
za usafi na mazingira, kufafanua
maana yake na kuzitumia katika
mawasiliano.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 80-83 )
Kusoma kwa mapana
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini anazotaka
kusoma kwenye maktaba.
b) Kusoma matini ili kufaidika na
ujumbe na lugha inayotumiwa.
c) Kufurahia usomaji wa matini
za aina mbalimbali ili kujenga
utamaduni wa kusoma.
108
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Unapenda kusoma matini za aina
gani? Kwa nini?
2. Unaweza kupata matini za
kusoma vipi na wapi?
3. Kusoma matini mbalimbali kuna
faida gani kwako?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kujadili njia
mbalimbali za kuyatunza mazingira.
(b) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kusoma matini
mbalimbali kuhusu uhifadhi wa
mazingira akiwa shuleni na nje ya
shule.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia vifaa vya kidijitali
kutafuta matini mbalimbali za
kusoma.
(d) Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anapotangamana na wanafunzi
wa asili mbalimbali katika vikundi
kusoma na kujadili matini
mbalimbali zinazohusu elimu ya
mazingira.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya afya
Inakuzwa mwanafunzi anaposoma
matini mbalimbali kuhusu elimu ya
mazingira na kufahamu magonjwa
mbalimbali yanayoweza kusababishwa
na mazingira machafu au mazingira
yasiyotunzwa.
Elimu na maendeleo endelevu
Masuala haya yanashughulikiwa
mwanafunzi anaposoma matini
mbalimbali kuhusu mazingira na
jinsi ya kuyahifadhi mazingira kwa
ajili ya vizazi vijavyo.
Utangamano
Utangamano unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wengine katika
vikundi darasani kujadili kuhusu
elimu ya mazingira.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapoweza
kupata matini mbalimbali na kuzisoma
hivyo kupanua uwezo wake wa kufikiri
na kuwajibika maishani.
Uhusiano na maadili
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana kwa amani na
wenzake katika kufanya kazi za
vikundi bila kuzua fujo.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
wanapojadiliana katika vikundi. Pia,
mwanafunzi anapowapa wenzake
fursa ya kuchangia katika majadiliano
kwenye vikundi.
Uwajibikaji
Huu unakuzwa mwanafunzi anapopata
elimu ya mazingira na kuwajibika kwa
kuyatunza mazingira na kuwaelimisha
wanajamii wengine.
109
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wanaositasita
wakisoma wasiharakishwe
kusoma bali wapewe muda zaidi
wa kufanya hivyo hadi wapate
uzoefu wa kusoma kwa ufasaha
na kujithamini.
Mshirikishe mfasiri wa lugha ishara
iwapo kuna wanafunzi wasio na
uwezo wa kusikia au kuzungumza
ili kufanikisha ujifunzaji wao.
Uhusiano na masomo mengine
1. Somo la Jamii
Somo hili lina mada zinazoangazia
elimu ya mazingira.
2. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hushughulikia usomaji
wa matini mbalimbali kuhusu mada
tofautitofauti.
3. Sayansi na Teknolojia
Somo hili linashughulikia elimu ya
mazingira.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapopata elimu ya
mazingira ataweza kuihamasisha jamii
kuhusu njia mbalimbali za kuyatunza
mazingira pamoja na madhara ya
kutoyatunza mazingira.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kuona wanaweza kutumia
mashine za breli kusoma matini
kuhusu elimu ya mazingira.
Pia, wanaweza kusikiliza matini
zikisomwa na mwalimu au
wanafunzi wenzao na kujifunza.
Wanafunzi ambao hawana
uwezo wa kuelewa kwa urahisi
wanayofundishwa watengewe
muda zaidi wa kusoma baada
ya masomo jioni ili kujifunza
zaidi. Wanafunzi wenye uwezo
wa kuelewa wanayofundishwa
kwa upesi wapewe mazoezi
zaidi ya kusoma. Pia, wanaweza
kuwasaidia wenzao wanaojifunza
polepole.
2.1 Kusoma matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 80-83)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 3)
Tafiti zaidi kuhusu matini mbalimbali za
kusoma zinazohusu elimu ya mazingira
ili kufanikisha ufunzaji wako. Unaweza
kufanya utafiti wako mtandaoni au
maktabani kwenye vitabu na majarida
mbalimbali. Vilevile:
Tafuta nakala za matini
mbalimbali zinazohusu elimu ya
mazingira ili wanafunzi wazisome
darasani na kujifunza. Matini
hizi mbalimbali zitasaidia katika
kuboresha ufunzaji wako.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumika na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara kuhusu somo hili ili
ajiandae kwa wakati.
Tafuta magazeti ya Kiswahili yenye
matini mbalimbali kuhusu elimu
ya mazingira ili kuwapa wanafunzi
darasani wazisome.
110
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 80
2. Breli
3. Magazeti ya Kiswahili yenye
matini kuhusu elimu ya mazingira
4. Nakala za matini mbalimbali
kuhusu elimu ya mazingira
5. Mfasiri wa lugha ishara
6. Kamusi ya Kiswahili.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwaongoza
wanafunzi kufanya shughuli ya
1. Wanafunzi watambue kwa
usahihi majina ya michoro iliyo
vitabuni mwao. Majibu tarajiwa:
kitabu, jarida, gazeti, simu. Matini
mbalimbali za kusoma hupatikana
maktabani.Waelekeze wanafunzi
kukumbuka kuhusu waliyojifunza
katika gredi ya nne kuhusu maktaba
na umuhimu wake.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha
uwaongoze kujadili umuhimu wa
miti kulingana na matini ambazo
wamewahi kuzisoma.Waelezane
waliyojifunza kutoka kwa matini
hizo. Wanafunzi waelezane
walikopata matini walizosoma.
Tathmini majibu ya wanafunzi.
Waongoze wanafunzi kusoma
kimyakimya matini zilizo vitabuni
mwao katika shughuli ya 3 kisha
wajibu maswali waliyopewa.
Wanafunzi wajadiliane kuhusu
usafi wa kibinafsi unavyodumishwa
(kupenga kamasi, kupiga mswaki,
kuchokonoa meno, kuzikata na
kuziangua kucha n.k.) na madhara
yanayotokana na mazingira machafu
(magonjwa, wadudu hatari, harufu
mbaya n.k.). Pia, wanafunzi wabaini
kuwa nahau za usafi na mazingira
zimetumiwa katika kifungu
walichosoma (futa vumbi, piga
deki, fyeka nyasi, angua kucha n.k.).
Hatimaye, waongoze wanafunzi
kuelezana wanavyodumisha usafi wa
mazingira yao. Tathmini maelezo ya
wanafunzi.
Katika shughuli ya 4, mwongoze
mwanafunzi kutafuta matini
maktabani kuhusu njia mbalimbali
za kuyatunza mazingira. Mwanafunzi
aisome matini hiyo na kuandika
mafunzo anayopata. Awasimulie
wenzake darasani kuhusu mafunzo
hayo. Shughuli hii itaukuza ujasiri
wa mwanafunzi wa kusimama na
kuongea mbele ya wanafunzi hivyo
kujiamani na kujithamini. Somo
hili linaweza kufanyika maktabani
au mwalimu anaweza kuleta matini
kadhaa darasani na wanafunzi
wakazisomea darasani.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
iliyo kitabuni mwake. Tathmini iwapo
kazi hii imefanyika kwa kumwuliza
mwanafunzi aeleze kuhusu magonjwa
yanayosababishwa na mazingira
machafu kama vile kipindupindu,
malaria, homa ya matumbo, homa,
kichocho, waba n.k. Pia, mwanafunzi
aeleze iwapo walishirikiana na mzazi
au mlezi wake kusafisha mazingira ya
111
Kimeidhinishwa na KICD
nyumbani kwao. Awaeleze wenzake
njia walizotumia kusafisha mazingira
yao nyumbani. Tathmini maelezo ya
mwanafunzi.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Mwanafunzi anapowasiliana na
kushirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili na kuandika insha za
maelezo atakuza umilisi huu.
(b) Ubunifu
Huu utakuzwa mwanafunzi anapoweza
kubuni insha za maelezo za kuvutia
kwa kuzingatia mada mbalimbali.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Mwanafunzi atakuza ujuzi huu
anapotumia vifaa vya kidijitali
kutafuta mtandaoni njia mbalimbali
za kuzuia mmomonyoko wa udongo
kama njia mojawapo ya kuyatunza
mazingira. Pia, anapoandika insha za
maelezo kwenye tarakilishi.
(d) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii itakuzwa mwanafunzi
atakapoendelea kujifunza kuhusu
uandishi wa insha ya maelezo pamoja
na njia mbalimbali za kuyatunza
mazingira akiwa shuleni na nje ya
shule.
Uhusiano ma masuala mtambuko
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali kufanya kazi za
vikundi kama vile kuandika insha za
maelezo na kujadili kuhusu utunzaji
wa mazingira.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua matini salama za
kusoma maktabani au mtandaoni.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kusoma matini na kufaidi
kutokana na ujumbe uliopo na
kuyaboresha mawasiliano yake.
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 83-84)
Insha ya maelezo
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha za maelezo katika
matini mbalimbali.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa
kuzingatia muundo na mtindo
ufaao.
c) Kuchangamkia utungaji wa insha
za maelezo ili kuimarisha uandishi
bora.
Maswali dadisi
1. Je, insha ya maelezo inatofautiana
vipi na insha nyingine?
2. Je, ni shughuli gani zinaweza
kuandikiwa insha za maelezo?
3. Ni mambo yapi yanayofaa
kuzingatiwa katika uandishi wa
insha za maelezo?
112
Kimeidhinishwa na KICD
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapojiamini
na kujithamini katika uandishi wa insha
akirejelea mazingira yake. Kufahamu
kuhusu njia mbalimbali za kuyatunza
mazingira kutamfaa maishani pamoja
na vizazi vijavyo.
Elimu ya mazingira
Mwanafunzi anapofahamu jinsi ya
kuyatunza mazingira na madhara ya
kutoyatunza ataweza kuwahamasisha
wanajamii wenzake. Atafahamu haya
kutokana na maudhui ya insha za
maelezo atakazoandika akiwa peke
yake au katika vikundi.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
wanapojadili na kuandika insha za
maelezo kuhusu elimu ya mazingira.
Pia, anapotumia lugha ya adabu na
kuwapa wenzake fursa ya kuchangia
katika majadiliano yao.
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapovitunza
vifaa vyake vya kujifunzia na
kumaliza kazi zake kwa wakati
unaofaa. Pia, mwanafunzi anapoweza
kuyatunza mazingira yake.
Uzalendo
Uzalendo huu unakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake wa asili
mbalimbali katika kufanya kazi za
vikundi za kuandika insha za maelezo
kuhusu elimu ya mazingira.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada zinazohusu
uandishi.
2. Sayansi na Teknolojia
Somo hili lina mada zinazoshughulikia
elimu ya mazingira.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawaeleza wenzake
shuleni na nje ya shule kuhusu
umuhimu wa uandishi bora katika
kuyaboresha mawasiliano.
Pia, mwanafunzi ataihamasisha jamii
kuhusu umuhimu wa kuyatunza
mazingira.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wanaochukua muda
mrefu kuandika kwa sababu ya
ulemavu fulani wapewe muda wa
kutosha wa kuandika.
Wanafunzi wenye matatizo ya
kisaikolojia wapewe ushauri
nasaha na kuwekewa sheria za
kufuata ili waweze kujifunza bila
usumbufu.
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kuona wanaweza kutumia
mashine za breli kusoma maelezo
kuhusu uandishi wa insha za
maelezo pamoja na kuandika
insha zao.
Mshirikishe mfasiri wa lugha
ishara iwapo una wanafunzi
darasani wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza. Pia,
113
Kimeidhinishwa na KICD
wanafunzi hawa wanaweza
kuwasiliana na wenzao na
mwalimu kwa maandishi hivyo
wanaweza kuandika insha
za maelezo kuhusu elimu ya
mazingira.
katika gredi ya nne. Tathmini maelezo
ya wanafunzi. Sifa za insha za maelezo ni
kama vile: huhusu maelezo ya jambo au
kitu fulani, huandikwa kwa lugha nathari,
huwa na mada n.k.
Katika shughuli ya 2, wape wanafunzi
nakala za insha mbalimbali ulizoandaa
ili waweze kutambua insha za maelezo.
Waongoze katika kuzisoma insha hizo.
Wajadili sifa zake (wakilinganisha na
sifa walizojadili katika shughuli ya 1)
na ujumbe unaojitokeza. Tathmini
majadiliano ya wanafunzi.
Wanafunzi wakiwa katika vikundi
washirikishwe katika shughuli ya 3.
Wayajadili matukio kwenye michoro
iliyo vitabuni mwao.
Waongoze wanafunzi kuandika
vidokezo kutokana na michoro
waliyojadili kisha uwaelekeze
kuandika insha ya maelezo
wakitumia vidokezo hivyo.
Wanafunzi wahariri insha zao kisha
mwanafunzi mmoja kutoka katika
kila kikundi awasomee wanafunzi
wengine insha yao ili waitathmini na
kujifunza. Shughuli hii itakuza ujasiri
wa wanafunzi wa kuongea mbele ya
watu hivyo kujiamini na kujithamini.
Tathmini insha za wanafunzi. Hakikisha
zinazingatia muundo na mtindo ufaao
pamoja na kanuni za kisarufi zifaazo.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini insha atakayoandika
mwanafunzi kuhusu njia mbalimbali
za kuzuia mmomonyoko wa udongo.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 83-84)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafuta nakala za insha mbalimbali
zikiwemo insha za maelezo ili kuzitumia
kuwafunzia wanafunzi darasani.
Unaweza kupata nakala hizi kutoka
kwa wanafunzi wa gredi nyingine au
ukaziandika mwenyewe. Vilevile,
Fanya utafiti zaidi kuhusu uandishi
wa insha za maelezo pamoja
na elimu ya mazingira. Kutafiti
huku kutakusaidia kufanikisha na
kurahisisha ufunzaji wako darasani.
Hakikisha mashine za breli
zitakazotumiwa na wanafunzi wasio
na uwezo wa kuona ziko katika hali
nzuri ya kutumika.
Mfahamishe mapema mfasiri wa
lugha ishara ili aweze kujiandaa
ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 83
2. Kamusi ya Kiswahili, breli
3. Nakala za insha mbalimbali
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza funzo hili kwa kuwaelekeza
wanafunzi kufanya shughuli ya 1. Wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi
na uwezo wao. Wajikumbushe kuhusu sifa
za insha ya maelezo kama walivyojifunza
3.1 Insha ya maelezo
114
Kimeidhinishwa na KICD
Njia za kuzuia mmomonyoko wa
udongo ni kama vile: upandaji wa
miti, nyasi, kutokata miti kwenye
vyanzo vya maji, kutolima karibu
na kingo za mito, kuchimba mitaro,
kutofuga mifugo wengi kwenye sehemu
ndogo ya malisho n.k. Mwanafunzi
anaweza kupiga chapa insha kwenye
tarakilishi au aiandike kwenye daftari
lake.
2. Je, ni nomino zipi zinapatikana
katika ngeli ya KU-KU?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kufanya
kazi za vikundi za kutambua na
kujadili nomino za ngeli ya KU-KU.
(b) Kufikiri kwa kina
Kunakuzwa mwanafunzi anapofikiria
kuhusu mafungu sahihi ya maneno
atakayotunga katika ngeli ya KU-KU
katika umoja na wingi.
(c) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapobuni mafungu ya nomino
kwa maneno yake mwenyewe bila
kunakili mafungu ya wenzake.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia na utangamano
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake wa
asili mbalimbali katika vikundi
kutambua nomino za ngeli ya KU-
KU na kuziandikia mafungu sahihi
ya maneno.
Stadi za maisha
Mwanafunzi anapofahamu kutunga
mafungu sahihi ya maneno katika ngeli
ya KU-KU atayaboresha mawasiliano
yake. Pia, anapoweza kujifanyia kazi
darasani.
Elimu endelevu
Inakuzwa mwanafunzi anapoendelea
kutumia nomino za ngeli ya KU-KU
pamoja na mafungu yake shuleni na
nje ya shule kuboresha mawasiliano.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua insha za maelezo
kwenye matini mbalimbali.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuandika insha ya
maelezo akizingatia mtindo na
muundo ufaao na mada lengwa.
4.1 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 84-86)
Ngeli ya KU-KU
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya
KU-KU.
b) Kuandika nomino za ngeli ya KU-
KU katika umoja na wingi.
c) Kuandika umoja na wingi wa
mafungu ya maneno katika ngeli
ya KU-KU.
d) Kuchangamkia kutumia nomino za
ngeli ya KU-KU katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, unajua vitenzi gani?
115
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Uzalendo
Unakuzwa mwanafunzi anapofanya
kazi na wenzake wa asili mbalimbali
katika vikundi darasani wakitambua
nomino za ngeli ya KU-KU na
kuzitungia mafungu sahihi.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa
mwanafunzi anapoyaheshimu maoni
yanayotolewa na wenzake katika
majadiliano kuhusu nomino za
ngeli ya KU-KU. Pia, mwanafunzi
anapowapa wenzake fursa ya
kuchangia majadiliano yao.
Uwajibikaji
Mwanafunzi anapohakikisha
amefanya mazoezi yaliyotolewa kwa
wakati unaofaa. Pia, anapovitunza
vifaa vyake vya kujifunzia darasani na
nyumbani.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hufunza kuhusu ngeli
za nomino.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Kutokana na kutumia nomino za ngeli ya
KU-KU kwa usahihi, mwanafunzi ataweza
kutumia lugha sanifu na fasaha hivyo
kuyaboresha mawasiliano katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye matatizo ya
kuona wanaweza kuketi karibu au
mbali na ubao. Wanafunzi wasio
na uwezo wa kuona watumie breli
katika ujifunzaji wao.
Wanafunzi wasio na uwezo
wa kusikia wanaweza kutumia
vifaa vya kuwawezesha kusikia.
Mshirikishe mfasiri wa lugha
ishara iwapo una wanafunzi wasio
na uwezo wa kusikia kabisa ili
kufanikisha ujifunzaji wao.
Wanafunzi wanaochukua muda
mrefu kuelewa wanayofundishwa
watengewe muda zaidi baada ya
masomo jioni ili wajifunze zaidi.
Wanafunzi wanaoelewa kwa haraka
wanayofundishwa wapewe shughuli
zaidi za ujifunzaji au wawasaidie
wenzao wanaojifunza polepole.
4.1.1 Umoja na wingi wa
nomino: Ngeli ya KU-KU
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 84-86)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti zaidi kuhusu ngeli ya KU-KU
ili kufanikisha ufunzaji wako. Vilevile:
Andaa kadi zilizoandikwa
nomino za ngeli mbalimbali
zikiwemo za ngeli ya KU-KU ili
wanafunzi waweze kutambua
nomino za ngeli ya KU-KU.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Mfahamishe mapema mfasiri wa
lugha ishara ili aweze kujiandaa
ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 84
2. Mfasiri wa lugha ishara
116
Kimeidhinishwa na KICD
3. Kadi zilizoandikwa nomino za
ngeli mbalimbali
4. Breli
5. Michoro au picha zinazoonyesha
vitendo mbalimbali.
Utaratibu wa ujifunzaji
Unaweza kutanguliza somo hili kwa
kuwashirikisha wanafunzi katika
shughuli ya 1. Waulize wanafunzi
iwapo wanakumbuka walichosoma
katika sura ya pili kuhusu nomino
za vitenzi-jina. Wanafunzi
wataje mifano ya vitenzi-jina
wanavyokumbuka. Mifano: kuimba,
kuandika, kucheza, kulala, kuoga,
kusafisha, kufyeka, kuokota, kutupa,
kuosha, kupanda n.k. Waelekeze
wanafunzi kutambua kuwa vitenzi-
jina ni nomino zilizo katika ngeli ya
KU-KU.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi kusoma na kuchagua
nomino za vitenzi-jina katika
mchoro waliopewa vitabuni mwao
kisha wazijadili. Majibu tarajiwa:
kupanda, kula, kupalilia, kunyunyizia.
Wanafunzi waelezane maana za
vitenzi-jina walivyochagua. Tathmini
maelezo ya wanafunzi.
Waongoze wanafunzi katika shughuli
ya 3 kuandika katika madaftari yao
nomino kumi za ngeli ya KU-KU katika
umoja na wingi.
Kila mwanafunzi awasomee wenzake
nomino alizoandika katika umoja na
wingi. Wanafunzi wajadiliane kuhusu
mabadiliko ya nomino za ngeli ya
KU-KU katika umoja na wingi.
Wabaini kuwa nomino za ngeli ya KU-
KU hazibadiliki katika umoja na wingi.
Mifano:
Umoja Wingi
1. kucheza kucheza
2. kupalilia kupalilia
3. kuosha kuosha
Katika shughuli ya 4, waelekeze
wanafunzi kuandika mafungu sahihi
ya maneno wakitumia nomino za
ngeli ya KU-KU. Wanafunzi watumie
nomino walizoandika katika shughuli
ya 3 swali la 1. Wafuate mfano
waliopewa vitabuni mwao. Majibu
tarajiwa:
Umoja Wingi
1. Kuoga kwako Kuoga kwenu
2. Kulima kwingi Kulima kwingi
3. Kusafisha kwake Kusafisha kwao
Tathmini mafungu ya maneno
yatakayoandikwa na wanafunzi.
Hakikisha ni sahihi.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
ataifanya akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Majibu tarajiwa:
Kubali vitenzi vyovyote vitano
vinavyohusu usafi na mazingira na
vilivyobadilishwa na kuwa nomino
katika ngeli ya KU-KU. Nomino hizo
ziwe zimeandikwa katika umoja na
wingi. Mfano: osha (kitenzi) kuosha
(nomino), kuosha (umoja) kuosha
(wingi).
117
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua nomino za
ngeli ya KU-KU na kuziandika
katika umoja na wingi kwa
usahihi.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kuandika umoja na wingi
wa mafungu ya maneno kwa
usahihi katika ngeli ya KU-KU.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunga sentensi sahihi katika umoja
na wingi kwa maneno yake mwenyewe
bila kunakili za wenzake.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi hii unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kutunga
sentensi sahihi katika ngeli ya KU-
KU na kuzijadili.
(c) Kufikiri kwa kina
Kunakuzwa mwanafunzi anapowaza
kwa kina kuhusu kutunga sentensi
sahihi katika ngeli ya KU-KU katika
umoja na wingi.
(d) Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anapotangamana na wenzake wa asili
mbalimbali katika vikundi kutunga
sentensi sahihi za ngeli ya KU-KU
katika umoja na wingi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano
Unakuzwa mwanafunzi anapofanya
kazi pamoja na wenzake katika vikundi
kutunga sentensi sahihi katika ngeli ya
KU-KU na kuzijadili.
Stadi za maisha
Mwanafunzi anapofanya kazi yake
mwenyewe ya kutunga sentensi sahihi
katika ngeli ya KU-KU katika umoja
na wingi, atakuza ukakamavu wake
na kujiamini.
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 86-87)
Ngeli ya KU-KU
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vipatanishi
vya ngeli ya KU-KU kwenye
sentensi.
b) Kuunda sentensi akitumia
nomino za ngeli ya KU-KU
katika umoja na wingi akizingatia
upatanisho wa kisarufi.
c) Kufurahia matumizi ya ngeli ya
KU-KU katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, sentensi katika ngeli ya
KU-KU huchukua viambishi gani
vya upatanisho?
2. Je, sentensi katika ngeli ya KU-
KU hubadilika vipi katika umoja
na wingi?
118
Kimeidhinishwa na KICD
Elimu endelevu
Mwanafunzi anapoendelea kutumia
nomino za ngeli ya KU-KU kwa
usahihi atayaboresha mawasiliano
yake shuleni na nje ya shule.
Uhusiano na maadili
Uzalendo
Unakuzwa mwanafunzi anapofanya
kazi pamoja na wenzake wa asili
mbalimbali kwenye vikundi kutunga
sentensi sahihi katika ngeli ya KU-
KU.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi wanapotunga sentensi
sahihi katika ngeli ya KU-KU. Pia,
anapotumia lugha ya adabu na
kuwapa wenzake fursa ya kuchangia
majadiliano yao.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hufunza umoja na wingi
wa sentensi kwa kuzingatia ngeli.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Kutokana na mwanafunzi kufahamu
matumizi ya ngeli kwa usahihi atatumia
lugha kwa ufasaha hivyo kuimarisha
mawasiliano katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye changamoto za
kusikia wanaweza kutumia vifaa
maalum vya kuwasaidia kusikia.
Wasio na uwezo wa kusikia
kabisa watumie lugha ishara
katika ujifunzaji wao. Mshirikishe
mfasiri wa lugha ishara hapa
iwapo huifahamu lugha hiyo.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona watumie mashine za
breli katika ujifunzaji wao. Pia,
wanaweza kusikiliza maelezo
kuhusu sentensi za ngeli ya KU-
KU yakitolewa na mwalimu au
wanafunzi wenzao na kujifunza.
Wanafunzi wasioelewa kwa
urahisi wanayofundishwa
watengewe muda zaidi wa
kujifunza baada ya masomo jioni.
Wanafunzi wanaong’amua kwa
upesi wanayofundishwa darasani
wapewe shughuli zaidi za kutunga
kifungu kifupi wakitumia nomino
za ngeli ya KU-KU. Pia, wanaweza
kuwasaidia wenzao wanaojifunza
polepole.
4.2.1 Umoja na wingi wa
sentensi: Ngeli ya KU-KU
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 86-87)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu ngeli ya KU-KU
ili kuweza kuwafaa wanafunzi darasani
wakati wa ujifunzaji. Vilevile,
Andaa kapu lenye kadi zilizoandikwa
nomino za ngeli ya KU-KU.
Hakikisha mashine za breli ziko katika
hali nzuri ya kutumiwa na wanafunzi
wasio na uwezo wa kuona.
Mshirikishe mfasiri wa lugha ishara ili
awasaidie wanafunzi wasio na uwezo
wa kusikia au kuzungumza.
119
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 86
2. Kapu lenye kadi zilizoandikwa
nomino za ngeli ya KU-KU
3. Breli
4. Mfasiri wa lugha ishara
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa
kuwashirikisha wanafunzi katika
shughuli ya 1. Waongoze wanafunzi
kutunga sentensi sahihi wakitumia
nomino za ngeli ya KU-KU
walizoandika katika kazi ya ziada
ya kipindi kilichotangulia. Tathmini
sentensi za wanafunzi. Hakikisha ni
sahihi kisarufi.
Waelekeze wanafunzi wapigie mistari
viambishi vya ngeli ya KU-KU katika
sentensi walizotunga kisha wavijadili.
Wanafunzi wabaini kuwa viambishi
vipatanishi vya ngeli ya KU-KU ni
ku- katika umoja na ku- katika wingi.
Mfano: 1. Kusoma kwingi kulimfanya
apite mtihani. Kusoma kwingi
kuliwafanya wapite mitihani.
2. Kulima kwake kunafaa katika
shamba hili. Kulima kwao kunafaa
katika mashamba haya.
Katika shughuli ya 2, waelekeze
wanafunzi katika kuucheza mchezo
wa kuchopoa kadi kutoka kapuni.
Hakikisha umeandaa kadi hizi
mapema kabla ya kipindi hiki ili
kuhifadhi wakati. Mwanafunzi
mmoja achopoe kadi iliyoandikwa
nomino ya ngeli ya KU-KU kutoka
kapuni kisha wanafunzi wengine
watunge sentensi katika umoja
na wingi wakitumia nomino
iliyoandikwa kwenye kadi hiyo.
Mwanafunzi mmoja aandike ubaoni
sentensi iliyotungwa na kupigia
mistari viambishi vya ngeli ya KU-
KU. Wanafunzi wengine wasome
sentensi hiyo na kuitathmini.
Tathmini sentensi za wanafunzi.
Hakikisha kuwa ni sahihi kisarufi na
zina maana.
Mchezo huu uendelee hadi kadi
zote kapuni ziishe. Mchezo huu
utawasaidia wanafunzi kuweza
kutunga sentensi sahihi katika ngeli
ya KU-KU na kutambua viambishi
vyake sahihi.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada.
Tathmini iwapo kazi hii imefanyika
kabla ya kipindi kingine kuanza.
Kubali vitenzi vyovyote vitano
vinavyorejelea usafi wa mtu binafsi.
Tathmini vitenzi vilivyobadilishwa
na kuwa katika ngeli ya KU-KU na
usahihi wa sentensi zilizotungwa
katika umoja na wingi. Mfano: oga
(kitenzi) kuoga (nomino), Kuoga
kwangu kulinisaidia. (sentensi katika
umoja) Kuoga kwetu kulitusaidia.
(sentensi katika wingi).
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua viambishi
vipatanishi vya ngeli ya KU-KU
kwenye sentensi.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
120
Kimeidhinishwa na KICD
wa kutunga sentensi sahihi
akitumia ngeli ya KU-KU katika
umoja na wingi akizingatia
upatanisho sahihi wa kisarufi.
Shughuli ya nje ya darasa
Shirikiana na mamlaka ya shule,
mamlaka ya eneo la shule yenu pamoja
na wanafunzi kupanda miti katika
eneo lililo karibu na shule yenu. Kila
mwanafunzi angalau apande mti mmoja.
Shughuli hii itakuza uthamini wao
wa mazingira pamoja na kufahamu
umuhimu wa kuyatunza mazingira.
Pia, unaweza kuwashirikisha
wanafunzi katika kulifagia soko lililoko
karibu na shule yenu. Hakikisha
wanafunzi wanazingatia usalama wao
wakati wa shughuli hii. Wanafunzi
wawaeleze wanajamii umuhimu wa
kuyatunza mazingira yao. Shughuli hii
itawahamasisha wanajamii kuyatunza
mazingira yao kwa manufaa yao
wenyewe.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Kubali nahau zozote tatu zinazohusu
usafi na mazingira na maana zao.
2. Tathmini maelezo ya mwanafunzi.
Kwa mfano: ili kujikinga na maradhi
mbalimbali, kuepuka hatari na ajali,
kupata hewa safi, kuepuka vifo vya
watu na wanyama n.k.
3. Mahali pa kupata matini za kusoma
ni kama vile: kwenye vitabu,
majarida, magazeti na mtandaoni.
4. Tathmini insha ya mwanafunzi.
Hakikisha imezingatia mada lengwa,
muundo na mtindo wa kuandika
insha ya maelezo. Pia, hakikisha
haijapungua maneno 150.
5. a) Kuoga kwao kulizuia harufu mbaya.
b) Kunyunyizia mimea maji kunafaa.
c) Kufagia huko kunatifua mavumbi.
d) Kunawa mikono kwao kulizuia
kipindupindu.
121
Kimeidhinishwa na KICD
NDEGE WA PORINI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 89-101)
Utangulizi
Ndege wa porini ni viumbe wenye
mabawa ambao hawaishi nyumbani.
Dini nyingi huamini kuwa Mungu ndiye
muumba wa viumbe hawa. Baadhi ya
ndege wa porini kama vile tai, mwewe,
bundi, kasuku, chiriku n.k. huishi mitini
na huweza kupaa juu angani. Ndege
hawa hujenga viota vyao mitini. Hawa
hula nafaka, wadudu wadogo wadogo,
mimea, mbegu na matunda mbalimbali.
Ndege wengine kama vile heroe na
korongo huishi majini. Ndege wa majini
hula samaki, wadudu wadogo wadogo na
mimea. Ndege huwa kivutio cha watalii
nchini kwetu. Watalii hutoka sehemu
mbalimbali kuja kuwaona ndege wetu
hivyo kuuboresha uchumi wa taifa letu.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Visawe: Visawe vya maneno matatu),
Kusoma kwa ufahamu (Mchezo wa
kuigiza), Kuandika insha za masimulizi
na Sarufi (Mnyambuliko wa vitenzi: Kauli
za kutendewa, kutendeka na kutendana).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 89-91)
Visawe
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua maneno matatu yenye
maana sawa katika kundi la
maneno.
b) Kutumia visawe ifaavyo katika
mawasiliano.
c) Kuthamini matumizi ya maneno
matatu yenye maana sawa katika
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, visawe ni nini?
2. Unajua visawe vipi katika
Kiswahili?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Umilisi huu utakuzwa kupitia kwa
mwanafunzi kufikiria sana kuhusu
maneno matatu yaliyo na maana sawa
pamoja na maana hiyo. Kufikiria
122
Kimeidhinishwa na KICD
huku kutamwezesha kutatua matatizo
yanayomkumba na yanayoikumba
jamii kadri ya uwezo wake.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu utakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kujadili
kuhusu maana za maneno matatu
yenye maana sawa.
(c) Ubunifu
Huu utakuzwa mwanafunzi
anapotunga sentensi sahihi kwa
maneno yake mwenyewe akitumia
visawe sahihi bila kunakili sentensi za
wenzake.
(d) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kutafuta maana za
visawe vya maneno matatu kwenye
kamusi au mtandaoni akiwa shuleni
na nje ya shule. Pia, anapoendelea
kutumia visawe katika kuyaboresha
mawasiliano yake.
(e) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutambua visawe vya maneno matatu
kutoka kwenye kundi la maneno na
kueleza maana yavyo. Pia, anapoweza
kutunga sentensi sahihi akitumia
visawe.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Mwanafunzi anapofahamu maana za
visawe mbalimbali ataweza kuvitumia
kuboresha mawasiliano yake.
Utunzaji wa mazingira
Utunzaji huu unadhihirika
mwanafunzi anapofahamu kuwa
makao ya ndege wengi wa porini
ni msituni kwenye miti hivyo
atahakikisha mazingira yanatunzwa
vilivyo.
Umoja wa kijamii na uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake wa asili
mbalimbali kufanya shughuli za
ujifunzaji katika vikundi kwa amani.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya
wenzake wakiwa katika vikundi
kuhusu ndege mbalimbali wa
porini. Pia, anapotumia lugha ya
adabu kuwasiliana na wenzake na
kuwapa fursa ya kuchangia katika
majadiliano.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake katika
vikundi kwa amani bila kuzua
ugomvi wanapojadili visawe vya
maneno matatu na ndege wa porini.
Uaminifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
sentensi kwa maneno yake mwenyewe
akitumia visawe vya maneno matatu
bila kunakili sentensi za wenzake.
Uzalendo
Uzalendo unakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake wa asili
mbalimbali katika vikundi kujadili
ndege wa porini na maana za visawe
vya maneno matatu.
123
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mafunzo kuhusu
visawe mbalimbali na majina ya
ndege wa porini.
2. Sayansi na Teknolojia
Somo hili lina mada zinazoangazia
ndege wa porini.
3. Somo la Jamii
Somo hili hushughulikia utalii
kutokana na ndege wa porini.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakuwa kielelezo kwa
wanajamii wenzake anapotumia lugha
kwa ufasaha na maneno tofauti yenye
maana moja kujieleza. Pia, ataifahamisha
jamii kuhusu utalii wa ndege wa porini
na jinsi ya kuyatunza mazingira.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Ili kuweza kufanikisha ujifunzaji wa kila
mwanafunzi,
Unaweza kumhusisha mfasiri wa
lugha ishara ili kuwasiliana na
wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia
na kuzungumza.
Washirikishe wanafunzi wote
wanaojifunza na kuvielewa visawe
vya maneno matatu kwa haraka na
wepesi katika kuwafunza wenzao
wanaojifunza na kuelewa polepole.
Hakikisha kuwa wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona wana mashine za
breli ili kufanikisha ujifunzaji wao.
Pia, wanaweza kusikiliza maelezo
kuhusu maana za visawe vya maneno
matatu yakitolewa na mwalimu au
wanafunzi wenzao.
Weka rekodi za wanafunzi wenye
changamoto za kiafya au kisaikolojia
ili ujue jinsi ya kuwashughulikia
nyakati za dharura. Pia, ni vyema
uwe na stadi za kuwapa wanafunzi
hao huduma ya kwanza iwapo
watakabiliwa na tatizo wakiwa
darasani.
1.1 Visawe vya maneno
matatu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 89-91)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Shughuli za ufunzaji pamoja na ujifunzaji
huimarishwa ikiwa mwalimu na wanafunzi
watakuwa wamejiandaa ipasavyo kabla ya
kipindi kuanza.
Unaweza kuandaa michoro au
picha za kuonyesha visawe vya
maneno matatu, kwa mfano: picha
za nyumba, barabara, pesa n.k. ili
zikusaidie katika ufunzaji wako.
Andaa michoro au picha za ndege
mbalimbali wa porini.
Hakikisha mashine za breli zipo na
ziko katika hali nzuri ili zitumiwe
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara mapema kuhusu somo hili
ili aweze kujiandaa ifaavyo.
Hakikisha kuwa una kamusi ya
Kiswahili na kamusi ya visawe
zitakazokusaidia katika ufunzaji.
124
Kimeidhinishwa na KICD
ya michoro hiyo yaliyo sahihi na
ambayo ni visawe. Mwanafunzi
atumie visawe hivyo kutunga
sentensi sahihi. Abadilishane daftari
na mwanafunzi mwenzake ili
watathmini na kusahihisha sentensi
zao. Tathmini sentensi za wanafunzi.
Mifano tarajiwa: 1. Mwewe anaishi
kwenye msitu/pori/mwitu. 2. Kiingilio
cha mbuga hii ni pesa/ngwenje/fulusi
kidogo. 3. Hii ni nyumba yangu./Haya
ni makao/maskani yangu.
4. Msichana/banati/binti huyu
anapenda kuwatazama heroe majini.
Tathmini sentensi atakazotunga
mwanafunzi.
Katika shughuli ya 3, mwelekeze
mwanafunzi kutambua visawe vya
maneno matatu kutoka kwenye
mti maneno ulio kitabuni mwake.
Majibu tarajiwa: Mungu/Mola/
Maulana, mja/binadamu/mtu,
mwandani/sahibu/rafiki, pori/
mwitu/msitu. Akiwa na mwanafunzi
mwenzake wajadili maana za maneno
waliyochagua. Wanaweza kutumia
kamusi ya Kiswahili kupata maana
hizo. Tathmini maana ambazo
wataeleza ili kuhakikisha ni sahihi.
Wapange wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na uwezo wao ili
wafanye shughuli ya 4. Wanafunzi
wataje mifano ya visawe vya maneno
matatu kisha wajadili maana za
visawe hivyo. Wanaweza kutumia
kamusi za Kiswahili. Tathmini
maelezo yao ili kuhakikisha ni sahihi.
Kila mwanafunzi atunge sentensi
sahihi kwa kutumia visawe
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 89
2. Picha au michoro ya kuonyesha
visawe vya maneno matatu
3. Picha au michoro ya ndege wa
porini
4. Kamusi ya Kiswahili, breli
5. Kamusi ya visawe
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwauliza
wanafunzi wataje ndege wowote wa
porini wanaowajua. Wanafunzi waeleze
ndege wa porini ambao wamewahi
kuwaona na walikowaona.
Katika shughuli ya 1, waulize
wanafunzi iwapo wanakumbuka
waliyojifunza katika gredi ya nne
kuhusu maana ya visawe. Wanafunzi
waelezane maana ya visawe na wataje
mifano miwili ya visawe vya maneno
mawili wanavyokumbuka. Tathmini
maelezo na mifano ya wanafunzi.
Visawe ni maneno yaliyo na maana
sawa, kwa mfano: kinyonga lumbwi,
ndovu tembo, ndege nyuni n.k.
Waelekeze wanafunzi wakiwa
wawiliwawili watambue visawe
katika shughuli ya 2. Wataje majina
ya michoro iliyo vitabuni mwao.
Waongoze wanafunzi kutambua
visawe vya maneno matatu kutokana
na michoro husika. Majibu tarajiwa:
msitu/pori/mwitu, pesa/ngwenje/
fulusi, nyumba/maskani/makao,
msichana/banati/binti.
Wanafunzi wawasomee wenzao
visawe walivyotaja ili wavitathmini
na kujifunza. Kubali majina yote
125
Kimeidhinishwa na KICD
walivyotaja na kuwasomea wenzake
katika kikundi chao. Wenzake
watathmini sentensi hizo na
wajifunze. Tathmini sentensi za
wanafunzi ili kuhakikisha ni sahihi
kisarufi.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada
atakayofanya akisaidiwa na mzazi
au mlezi wake. Tathmini sentensi za
mwanafunzi. Majibu tarajiwa:
1. Njia/baraste/ghurufa ya kwenda
sokoni huwa na kanga wengi.
2. Msichana/banati/binti huyu
anaogopa mlio wa bundi.
3. Mungu/Mola/Jalali/Maulana
aliumba ndege wa porini na wa
nyumbani.
4. Kasuku wengi wamejaa katika
msitu/mwitu/pori hii.
5. Mwewe amepaa juu ya nyumba/
makao/maskani/auta yao.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 91-93)
Kusoma kwa ufahamu
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua mchezo wa kuigiza
katika matini.
b) Kusoma mchezo mfupi wa
kuigiza kwa ufasaha.
c) Kueleza maana ya msamiati
uliotumiwa katika mchezo wa
kuigiza.
d) Kuonyesha ufahamu wa mchezo
wa kuigiza kwa kujibu maswali.
e) Kuigiza mchezo mfupi ili kukuza
uwezo wa kujieleza.
f) Kufurahia kusoma michezo na
kuigiza.
Maswali dadisi
1. Je, mchezo wa kuigiza ni nini?
2. Umewahi kusoma michezo ipi ya
kuigiza?
3. Unakumbuka nini katika mchezo
wa kuigiza uliowahi kuusoma au
kuutazama?
4. Kusoma michezo ya kuigiza kuna
umuhimu gani kwako?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Mawasiliano na ushirikiano
unakuzwa kupitia kwa wanafunzi
kufanya shughuli mbalimbali kwa
kushirikiana katika vikundi. Kusoma
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anafahamu maana ya visawe.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kutambua maneno
matatu yenye maana sawa katika
kundi la maneno.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kueleza maana za visawe
vya maneno matatu kwa usahihi.
4. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutumia visawe vya
maneno matatu kutunga sentensi
sahihi na katika mawasiliano.
5. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anafahamu ndege wa porini.
126
Kimeidhinishwa na KICD
Uraia
Huu unakuzwa wanafunzi wa asili
mbalimbali wanapofanya shughuli
za ujifunzaji kwa ushirikiano katika
vikundi kwa kuigiza na kubuni
michezo ya kuigiza. Wakosoane na
kukubaliana bila fujo ili kuonyesha
uraia mwema.
Elimu ya maendeleo endelevu
Suala hili linashughulikiwa
mwanafunzi anapowathamini
ndege wa porini na kuwahamasisha
wenzake kuyatunza mazingira.
Elimu ya mazingira
Suala hili linashughulikiwa
mwanafunzi anapofahamu kuwa
makao ya ndege wa porini ni mwituni
hasa mitini hivyo kuwahamasisha
wenzake na jamii kuyatunza
mazingira.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Mwanafunzi ayaheshimu maoni ya
wenzake katika shughuli za vikundi.
Ashirikiane na wanafunzi wenzake
kwa kutumia lugha ya adabu na
kuwapa wenzake fursa ya kuchangia
katika majadiliano yao. Pia, aonyeshe
uthamini wa ndege wa porini nchini.
Umoja na amani
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake
katika shughuli za vikundi za kusoma
na kuigiza michezo ya kuigiza kwa
amani bila kuzua fujo.
Uwajibikaji
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kuyatunza mazingira na
kuwahamasisha wenzake na jamii
michezo ya kuigiza na kuiigiza
darasani. Pia, kuwasiliana na kufanya
kazi ya ziada pamoja na walezi wao.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Katika kazi ya ziada, mwanafunzi
atatarajiwa kutafuta mtandaoni
au kwenye runinga mchezo wa
kuigiza unaoigizwa kwa Kiswahili
na kuujadili akiwa na mlezi wake.
Itambidi atumie vifaa vya kidijitali
kutekeleza shughuli hii hivyo kukuza
ujuzi wake.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kutafuta michezo
mingine ya kuigiza kwenye makala
mbalimbali, runingani au mtandaoni
ili kujifunza zaidi.
(d) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi anapoigiza
michezo ya kuigiza akiwa shuleni na
nje ya shule pamoja na kubuni michezo
ya kuigiza kwa kuzingatia miktadha na
mada mbalimbali.
(e) Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuigiza michezo ya kuigiza kwa
ustadi na kwa lugha sahihi na fasaha.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Stadi hizi zinadhihirika mwanafunzi
anapojifunza uigizaji hodari kwa
lugha fasaha. Ataweza kujitegemea
baadaye kwa kuwa mwigizaji
mashuhuri wa michezo ya kuigiza na
drama na kuyakimu mahitaji yake.
127
Kimeidhinishwa na KICD
kufanya hivyo ili kuhifadhi makao
ya ndege wa porini. Pia, avitunze
vifaa vyake vya kujifunzia pamoja
na kukamilisha kazi zake kwa wakati
ufaao.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya pia hushughulikia
kusoma na kuigiza michezo ya
kuigiza na upanuzi wa msamiati.
2. Sayansi na Teknolojia
Somo hili lina mada zinazoangazia
ndege wa porini.
3. Somo la Jamii
Somo hili hushughulikia ndege wa
porini kama kivutio cha watalii
nchini ili kuboresha uchumi wa taifa.
Mapendekezo ya shughuli za kijamii
zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakuwa kielelezo kwa
wenzake shuleni na nje ya shule
katika usomaji na uigizaji wa michezo
ya kuigiza.
Pia, mwanafunzi ataweza
kuwahamasisha watu katika jamii
kuhusu umuhimu wa kuyatunza
mazingira ili kuhifadhi makao na
lishe ya ndege wa porini.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Ili kuweza kufanikisha ujifunzaji wa kila
mwanafunzi,
Unaweza kumshirikisha mfasiri
wa lugha ishara ili kuwasiliana
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza. Pia, unaweza
kuwaeleza maana ya mchezo wa
kuigiza na wakawasikiliza wenzao
wakisoma mchezo wa kuigiza.
Hakikisha wanafunzi wasio na uwezo
wa kuona wana mashine za breli zilizo
katika hali nzuri ili waweze kusoma
na kubuni michezo ya kuigiza.
Washirikishe wanafunzi wanaong’amua
wanayojifunza haraka katika
kuwafunza wenzao wanaojifunza
polepole.
Mwalimu awashughulikie wanafunzi
wengine walio na matatizo
mbalimbali ya kiafya na kisaikolojia
kadri ya uwezo wake.
2.1 Mchezo wa kuigiza
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 91-93)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 3)
Fanya utafiti zaidi kuhusu michezo
mbalimbali ya kuigiza ili kufanikisha
ufunzaji wako. Pia,
Andaa nakala za matini
mbalimbali zilizo na michezo
ya kuigiza pamoja na maandishi
mengine ambazo utawapa
wanafunzi darasani ili watambue
matini zinazohusu michezo ya
kuigiza.
Unaweza kurekodi vipindi vya
Kiswahili ambavyo ni michezo
ya kuigiza na ukawaonyesha
wanafunzi darasani.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara mapema kuhusu somo hili
ili aweze kujiandaa ifaavyo.
128
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 91
2. Rekodi za vipindi vya Kiswahili
(michezo ya kuigiza)
3. Mfasiri wa lugha ishara
4. Projekta, breli na tarakilishi.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo kwa kuwaelekeza
wanafunzi washiriki katika
majadiliano katika shughuli ya 1.
Wapange katika vikundi kulingana
na uwezo na idadi yao kisha wajadili
kuhusu vipindi ambavyo wanapenda
kutazama kwenye vyombo vya
kidijitali. Wataje majina ya wahusika
kwenye vipindi hivyo, maudhui ya
vipindi hivyo na watoe sababu zao za
kuvipenda vipindi hivyo. Hakikisha
wanajadili vipindi vilivyo na maudhui
chanya. Tathmini majadiliano ya kila
kikundi.
Katika shughuli ya 2, wape wanafunzi
nakala za matini mbalimbali ulizoandaa
mapema zilizo na michezo ya kuigiza
na maandishi mengine ili wasome na
kutambua matini zinazohusu michezo
ya kuigiza.
Waelekeze wanafunzi kujadili tabia za
wahusika na ujumbe katika michezo
ya kuigiza waliyotambua. Tathmini
majadiliano ya wanafunzi katika
vikundi vyao. Wakosoe wanapokosea.
Wapange wanafunzi katika vikundi
viwili kisha uwaongoze kusoma
mchezo wa kuigiza ulio vitabuni
mwao katika shughuli ya 3. Kikundi
kimoja kiwakilishe mhusika Dennis
na kikundi cha pili kiwakilishe
mhusika Farida. Hakikisha wanafunzi
wanasoma kwa usahihi na ufasaha.
Rekebisha makosa yoyote ya
kimatamshi.
Wanafunzi wajadili ujumbe uliopo
katika mchezo wa kuigiza waliosoma.
Mchezo huo unahusu Dennis ambaye
amewahi kuwaona ndege wa porini
na Farida ambaye hajawahi kuwaona
ndege wa porini. Tathmini maelezo ya
wanafunzi.
Wanafunzi waeleze maana za maneno
yaliyokolezwa rangi nyeusi kwenye
mchezo wa kuigiza waliosoma.
Watumie kamusi za Kiswahili.
Waongoze wanafunzi kuandika
visawe vya maneno yaliyopigiwa
mistari katika mchezo waliosoma.
Majibu tarajiwa: Mungu/Rabana/
Maulana/Jalali, rafiki/mwandani,
pori/mwitu.
Wanafunzi wakiwa wawiliwawili
waigize mchezo wa kuigiza
waliosoma. Tathmini uigizaji wao na
mazungumzo yao.
Katika shughuli ya 4, wanafunzi
watunge michezo ya kuigiza
wakitumia ndege wa porini kuwa
wahusika na kuihariri. Tathmini
maendeleo yao katika vikundi vyao.
Waelekeze kuigiza michezo ya kuigiza
waliyobuni huku wanafunzi wenzao
wakiwatazama, wakiwasikiliza na
kutathmini maigizo yao. Tathmini
maigizo na mazungumzo ya kila
kikundi.
129
Kimeidhinishwa na KICD
Mwelekeze kila mwanafunzi
jinsi atakavyofanya kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Tathmini iwapo kazi hii ilifanyika
kabla ya kipindi kingine kuanza.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Unajengeka mwanafunzi
anapoandika insha ya masimulizi
kuhusu ndege wa porini kwa
kubuni matukio yake mwenyewe
kwa maneno yake mwenyewe bila
kunakili insha za wenzake.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa wanafunzi
wanaposhirikiana katika vikundi
kujadili muundo, mtindo na mada
mbalimbali za kuandika insha ya
masimulizi. Wanapoandika insha na
kuwasomea wenzao wanakuza uwezo
wao wa kuwasiliana.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu utakuzwa mwanafunzi
atakapofanya kazi ya ziada kwa
kuandika insha ya masimulizi
(kuhusu umuhimu wa ndege wa
porini) kwenye tarakilishi na
kuwatumia wenzake na mwalimu
mtandaoni ili waitathmini. Pia,
anaweza kutumia intaneti kutafuta
picha na maelezo kuhusu ndege
mbalimbali wa porini.
(d) Kujiamini
Unajengeka mwanafunzi anapoweza
kuandika insha ya masimulizi kuhusu
ndege wa porini kwa kubuni matukio
yake mwenyewe na kuwasomea
wenzake darasani na nyumbani.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Unakuzwa wanafunzi wa asili
mbalimbali wanapofanya kazi kwa
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kutambua mchezo wa
kuigiza katika matini mbalimbali.
2. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kusoma mchezo wa
kuigiza kwa ufasaha na kueleza
maana za msamiati mpya
uliotumiwa.
3. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kubuni mchezo wa
kuigiza na kuuigiza kwa ustadi
akiwa na wenzake.
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 94-96)
Kuandika insha
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kueleza sifa za insha ya masimulizi
ili kuibainisha.
b) Kuandika insha ya masimulizi kwa
kufuata kanuni zifaazo.
c) Kuchangamkia utunzi mzuri.
Maswali dadisi
1. Insha ya masimulizi ni ipi?
2. Unakumbuka jinsi ya kuandika
insha ya masimulizi?
3. Je, wewe huzingatia mambo gani
unapoandika insha ya masimulizi?
130
Kimeidhinishwa na KICD
kushirikiana katika vikundi licha ya
tofauti zao anuwai.
Stadi za maisha
Kutokana na insha za masimulizi
kuhusu ndege wa porini,
mwanafunzi atafahamu kuwatunza
na kuwathamini ndege wa porini.
Kwa hivyo, anaweza kufanya kazi
na serikali, mashirika ya kuhifadhi
ndege wa porini na katika mbuga
mbalimbali.
Mwanafunzi ataweza kuwafundisha
wanajamii kuhusu umuhimu wa
kuwathamini ndege wa porini.
Elimu ya mazingira
Mwanafunzi atafahamu umuhimu
wa kuyatunza mazingira kwani
ndiyo maskani ya ndege wa porini.
Pia, ataihamasisha jamii kuhusu
umuhimu wa kuyatunza mazingira
na kuwalinda ndege wa porini.
Uhusiano na maadili
Uzalendo
Maadili haya yatakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kujadili na kuandika insha za
masimulizi. Pia, kuwathamini ndege
wa porini pamoja na kuyatunza
mazingira ni ishara ya uzalendo.
Amani na umoja
Maadili haya yatakuzwa mwanafunzi
anapotambua na kujadili insha ya
masimulizi akiwa na wenzake katika
vikundi na kuweza kutumia maneno
ya heshima kuwasiliana bila kuzua
fujo.
Heshima na upendo
Mwanafunzi anapoyaheshimu maoni
ya wenzake katika vikundi kuhusu
ndege wa porini na kutumia lugha ya
adabu kuwasiliana. Pia, anapowapa
wenzake fursa ya kuchangia katika
majadiliano yao.
Uaminifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
insha ya masimulizi inayohusu
ndege wa porini akiwa peke yake bila
kunakili insha za wenzake.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanashughulikia mada
ya kuandika.
2. Somo la Jamii
Somo hili linafundisha kuhusu
ndege wa porini na umuhimu wao
kama kivutio cha watalii nchini. Pia,
uhifadhi wa mazingira hufundishwa
katika somo hili.
3. Sayansi na Teknolojia
Somo hili linafundisha kuhusu
utunzaji wa ndege wa porini,
umuhimu wao na mazingira yao.
Pia, utunzaji wa mazingira hufunzwa
katika somo hili.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha
wenzake shuleni na nyumbani
kuhusu umuhimu wa kuhifadhi
mazingira na kuwatunza ndege wa
porini.
131
Kimeidhinishwa na KICD
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa
kuona watambue maelezo kuhusu
muundo na mtindo wa kuandika
insha ya masimulizi kwa kutumia
breli. Pia, wanaweza kukusikiliza
ukiyasoma maelezo hayo au
yakisomwa na wenzao darasani ili
wajifunze.
Wanafunzi walio na changamoto
za viungo vya mwili kama vile
mikono wasaidiwe kuandika kwa
kutumia viungo vingine vya mwili
walivyozoea kutumia.
Mwalimu awe mvumilivu ili aweze
kuwasaidia wanafunzi wanaochukua
muda mrefu kujifunza uandishi wa
insha ili waweze kujifunza bila kukata
tamaa.
Mwalimu atambue hatua yoyote
inayopigwa na mwanafunzi
anayejifunza kuandika insha
polepole.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuongea au kusikia wanaweza
kusaidiwa na mfasiri wa lugha ishara
kujifunza.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona ili kujifunza.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara kuhusu funzo hili ili
ajiandae vilivyo.
Unaweza kuandaa chati yenye
insha ya masimulizi itakayokuwa
kielelezo kwa wanafunzi wakati
wa ufunzaji darasani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 94
2. Picha au michoro ya aina
mbalimbali za ndege wa porini
3. Chati yenye insha kielelezo (insha
ya masimulizi)
4. Mfasiri wa lugha ishara, breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwauliza
wanafunzi wataje aina mbalimbali za
insha wanazofahamu. Tathmini majibu
ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 1, waongoze
wanafunzi wakiwa wawiliwawili
wajadiliane kuhusu maana ya insha
ya masimulizi kama walivyojifunza
hapo awali. Insha ya masimulizi
huandikwa kwa mtindo na muundo
maalum wa kusimulia matukio fulani.
Wanafunzi wajadili sifa za insha ya
masimulizi pamoja na kueleza tofauti
zilizopo kati ya insha za masimulizi
na insha nyingine wanazofahamu.
Tathmini maelezo ya wanafunzi.
Insha za masimulizi huhusisha
kusimulia matukio kwa njia ya
kinathari.
3.1 Kuandika: Insha za
masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 94-96)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu uandishi bora wa
insha za masimulizi pamoja na ndege wa
porini. Pia,
Andaa picha au michoro ya aina
mbalimbali za ndege wa porini.
132
Kimeidhinishwa na KICD
Wapange wanafunzi katika vikundi
ili washiriki katika shughuli ya
2. Waelekeze wanafunzi kuelezana
kuhusu majina, sifa, vyakula na
upekee wa ndege walio vitabuni
mwao.
Majibu tarajiwa: a) bundi
anaaminiwa kuwa na mlio wa
kuleta msiba, ana macho makubwa,
anafanana na paka usoni, hula
wanyama na wadudu wadogo wadogo
b) mwewe ana kidona chenye
ncha kali, hupenda kula vifaranga,
wanyama wadogo wadogo, wadudu
na nafaka c) tai hupaa juu sana
angani, ana mabawa makubwa,
hula wanyama wadogo, wadudu na
samaki d) kasuku - yeye huvutia kwa
rangi zake mbalimbali, anajulikana
kwa uwezo wake wa kuiga sauti,
hula wanyama wadogo, wadudu,
nafaka, mabaki ya vyakula e) chiriku
anajulikana kwa kupenda kuimba
sana, hula wadudu na nafaka f)
njiwa - anajulikana kwa upole wake,
hula wadudu na nafaka.
Katika shughuli ya 3, waelekeze
wanafunzi kujadili matukio katika
michoro iliyo vitabuni mwao wakiwa
katika vikundi. Waandike vidokezo
kutokana na michoro hiyo kisha
wajadili muundo wa kuandika insha
ya masimulizi.
Kila mwanafunzi avitumie vidokezo
walivyoandika kutunga insha ya
masimulizi. Awasomee wenzake
insha aliyotunga ili waitathmini (kwa
kutumia vigezo vilivyotajwa vitabuni
mwao) na kujifunza. Tathmini insha
za wanafunzi.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
kazi ya ziada akisaidiwa na mzazi au
mlezi wake. Tathmini iwapo kazi hii
imefanyika kabla ya kipindi kijacho.
Mwanafunzi akutumie mtandaoni
insha aliyobuni kuhusu umuhimu
wa ndege wa porini. Pia, hakikisha
ameandika majina ya ndege wa
porini kwenye daftari lake kutokana
na picha za ndege hao alizoziona
mtandaoni.
4. Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 96-101)
Mnyambuliko wa vitenzi
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vitenzi katika kauli
za kutendewa, kutendeka na
kutendana katika matini.
Tathmini
1. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kueleza sifa za insha ya
masimulizi ili kuibainisha.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kuandika insha ya
masimulizi kwa ubunifu
akizingatia kanuni zifaazo za
lugha, mtindo, muundo na
mpangilio mzuri wa mawazo.
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kuandaa vidokezo na
kuandika insha ya masimulizi kwa
kutumia matukio ya michoro.
133
Kimeidhinishwa na KICD
b) Kutumia vitenzi katika kauli
za kutendewa, kutendeka
na kutendana ipasavyo
anapowasiliana.
c) Kuchangamkia matumizi ya
vitenzi katika kauli za kutendewa,
kutendeka na kutendana katika
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Mnyambuliko wa vitenzi ni nini?
2. Je, vitenzi vinaweza kubadilika
vipi mwishoni ili kuleta maana
mbalimbali?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
changamoto
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiri kuhusu jinsi ya
kunyambua vitenzi katika kauli za
kutendewa, kutendeka na kutendana.
Pia, katika kutunga sentensi sahihi
kuhusu masuala mbalimbali akitumia
vitenzi vilivyonyambuliwa katika
kauli hizo.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi watashirikiana
kunyambua vitenzi katika kauli za
kutendewa, kutendeka na kutendana
wakiwa katika vikundi. Wanafunzi
watatunga sentensi na kusomeana ili
kuzitathmini hivyo kuboresha uwezo
wao wa kuwasiliana.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Unakuzwa wanafunzi wanapotumia
vifaa vya kidijitali kama vile tarakilishi
kuandika kifungu na kupigia mistari
vitenzi vilivyo katika kauli ya kutendeka
vilivyotumiwa katika kifungu hicho.
(d) Ubunifu
Unajengeka mwanafunzi anapoweza
kutunga sentensi sahihi na vifungu
kwa maneno yake mwenyewe kwa
kutumia vitenzi katika kauli za
kutendewa, kutendeka na kutendana.
(e) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapofaulu
kunyambua vitenzi katika kauli za
kutendewa, kutendeka na kutendana
na kuvitumia kutunga sentensi sahihi.
Pia, mwanafunzi anapoweza kutunga
sentensi sahihi na kuwasomea
wenzake anajithamini zaidi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Masuala mbalimbali kama vile:
utunzaji wa mazingira, usalama,
lishe bora, magonjwa mbalimbali
na utunzaji wa wanyama
yatashughulikiwa mwanafunzi
anapotunga sentensi akitumia vitenzi
vilivyonyambuliwa katika kauli za
kutendewa, kutendeka na kutendana
kwa kurejelea masuala hayo.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Uwajibikaji unadhihirika mwanafunzi
anapovitunza vifaa vyake vya ujifunzaji.
Pia, anapotekeleza majukumu yake
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi.
Amani na umoja
Maadili haya yatakuzwa kupitia kwa
mwanafunzi kutangamana kwa amani
na wenzake katika vikundi bila kuzua
ugomvi wowote.
134
Kimeidhinishwa na KICD
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kunyambua vitenzi katika
kauli za kutendewa, kutendeka na
kutendana na kuheshimu maoni
yao. Pia, anapotumia lugha ya adabu
kuwasiliana na wenzake pamoja na
kuwapa wenzake fursa ya kuchangia
katika majadiliano yao.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yana mada
zinazoangazia mnyambuliko wa
vitenzi.
Masomo mengine yote hutumia
vitenzi vilivyonyambuliwa katika
matini zao.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakapotumia sentensi zenye
vitenzi vilivyonyambuliwa katika kauli za
kutendewa, kutendeka na kutendana kwa
usahihi katika mawasiliano ataboresha
lugha na mawasiliano katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Mshirikishe mfasiri wa lugha ishara
iwapo una wanafunzi wasio na
uwezo wa kusikia au kuzungumza.
Pia, wanaweza kusikiliza maelezo
kuhusu mnyambuliko wa vitenzi
kutoka kwako au wanafunzi wenzao
ili kujifunza.
Hakikisha kuna mashine za breli
zilizo katika hali nzuri ya kutumiwa
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona ili wajifunze. Pia, wanafunzi
hawa wanaweza kutolewa maelezo
kuhusu mnyambuliko wa vitenzi na
wakayasikiliza na kujifunza.
Wanafunzi wanaochukua muda
kuelewa yale wanayofundishwa
watengewe muda zaidi baada ya
masomo jioni ili wajifunze zaidi.
Wanafunzi wanaoweza kuelewa
wanayofundishwa kwa wepesi
wapewe shughuli zaidi za ujifunzaji
au watumiwe kuwasaidia wenzao
wanaojifunza polepole.
Mwalimu awe tayari kuwasaidia
wanafunzi wengine walio na
changamoto mbalimbali.
4.1 Kauli za kutendewa,
kutendeka na kutendana
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 96-101)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 3)
Tafiti zaidi kuhusu mnyambuliko wa
vitenzi katika kauli za kutendewa,
kutendeka na kutendana kabla ya kipindi
ili uweze kumwelekeza mwanafunzi
vyema. Pia,
Andaa chati iliyoandikwa vitenzi
mbalimbali vilivyonyambuliwa katika
kauli za kutendewa, kutendeka na
kutendana.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumika na
wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
ili wajifunze.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
ili aweze kujiandaa ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 96
135
Kimeidhinishwa na KICD
2. Mfasiri wa lugha ishara, breli
3. Chati ambayo imeandikwa vitenzi
vilivyonyambuliwa.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza
wanafunzi wataje vitenzi mbalimbali
wanavyofahamu. Tathmini majibu yao.
Hakikisha maneno wanayotaja ni vitenzi.
Waelekeze wanafunzi wote kufanya
shughuli ya 1 kwa kuwapanga katika
vikundi kulingana na uwezo na idadi
yao. Waulize wasome kisha wajadili
sentensi zilizo vitabuni mwao na
kuelezana ugunduzi wao. Vitenzi
katika sentensi hizo viko katika kauli
ya kutendewa. Kauli ya kutendewa
huonyesha kuwa kitendo kimefanyiwa
mhusika fulani.
Waelekeze wanafunzi kufahamu jinsi
ya kunyambua vitenzi katika kauli ya
kutendewa. Mifano: imba imbiwa,
andika andikiwa, soma somewa,
chora chorewa, fuga fugiwa n.k.
Katika shughuli ya 2, waongoze
wanafunzi kukamilisha jedwali
lililo vitabuni mwao kwa kuandika
vitenzi katika kauli ya kutenda na
kutendewa. Tathmini majibu ya
wanafunzi.
Majibu tarajiwa: c) kata d) abudiwa
e) jengewa f) fuliwa. Wanafunzi
wafahamu jinsi ya kunyambua
vitenzi katika kauli ya kutendewa.
Wajadiliane wakiwa wawiliwawili
mabadiliko kwenye vitenzi husika.
Mwelekeze mwanafunzi afanye
shughuli ya 3. Aandike sentensi
zilizo kitabuni mwake upya katika
kauli ya kutendewa. Wanafunzi
wabadilishane madaftari ili
watathmini sentensi zao. Tathmini
sentensi zao. Hakikisha vitenzi viko
katika kauli ya kutendewa. Majibu
tarajiwa:
1. Waumini wanaombewa na padri.
2. Kifaranga amenyakuliwa na
mwewe.
3. Maji yananywewa na bundi.
4. Nyama inaliwa na tai.
5. Babu amebebewa mizigo na
watoto.
6. Ndege wale wanatibiwa na
daktari wa wanyama.
Hitimisha kipindi hiki kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Mwanafunzi abuni kifungu
kifupi akitumia vitenzi katika kauli ya
kutenda na kutendewa.
Tanguliza kipindi cha pili kwa kumwuliza
mwanafunzi awasomee wenzake kifungu
alichotunga akitumia vitenzi katika kauli
ya kutenda na kutendewa katika kazi ya
ziada aliyopewa. Tathmini kifungu cha
mwanafunzi. Hakikisha ametumia vitenzi
katika kauli ya kutenda na kutendewa.
Waelekeze wanafunzi wote wafanye
shughuli ya 4. Wapange katika
vikundi kulingana na uwezo na idadi
yao. Wajadili sentensi zilizo vitabuni
mwao kisha waelezane ugunduzi
wao. Vitenzi katika sentensi hizo
viko katika kauli ya kutendeka.
Waelekeze wanafunzi watambue jinsi
ya kunyambua vitenzi katika kauli ya
kutendeka.
136
Kimeidhinishwa na KICD
Wafahamu kuwa kauli ya kutendeka
huonyesha vitendo ambavyo tayari
vishakamilika au vishatendeka.
Mifano: pika- pikika, andika
andikika, fua fulika, soma –someka,
chora choreka n.k.
Katika shughuli ya 5, waongoze
wanafunzi kukamilisha jedwali lililo
vitabuni mwao. Waandike vitenzi
katika kauli ya kutendeka. Tathmini
majibu yao. Majibu tarajiwa:
c) katika d) abudika e) jengeka
f) fulika. Wanafunzi wajadili mabadiliko
ya vitenzi katika kauli ya kutendeka.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 6 kwa kuandika sentensi
zilizo kitabuni mwake katika kauli ya
kutendeka. Wanafunzi wabadilishane
madaftari ili watathmini sentensi zao.
Hakikisha sentensi zao ziko katika
kauli ya kutendeka. Majibu tarajiwa:
a) Nyumba ya nyanya imejengeka.
b) Kifaranga amenyakulika.
c) Maji yamenyweka.
d) Nyama imelika.
e) Mizigo ya babu imebebeka.
f) Ndege wale wametibika.
Hitimisha kipindi cha pili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Atunge kifungu kifupi akitumia
vitenzi katika kauli ya kutenda,
kutendewa na kutendeka.
Tanguliza kipindi cha tatu kwa
kuwauliza wanafunzi wawasomee
wenzao vifungu walivyotunga katika
kazi ya ziada. Tathmini vifungu vyao.
Hakikisha vimetumia vitenzi katika kauli
ya kutenda, kutendewa na kutendeka.
Waongoze wanafunzi kufanya
shughuli ya 7 ambapo watajadili
sentensi zilizo vitabuni mwao kisha
waelezane ugunduzi wao wakiwa
katika vikundi. Waelekeze wanafunzi
kutambua kuwa vitenzi katika
sentensi hizo viko katika kauli ya
kutendana. Wanafunzi wafahamu
jinsi ya kunyambua vitenzi katika
kauli ya kutendana. Katika kauli hii,
watenda hufanyiana vitendo, mifano:
beba - bebana, soma somana, chana
chanana, suka sukana, penda
pendana n.k.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 8 kwa kukamilisha
jedwali lililo kitabuni mwake.
Tathmini majibu ya mwanafunzi.
Majibu tarajiwa:
b) chunga c) sukana d) oshana
e) jengana f) onana. Wanafunzi wajadili
mabadiliko ya vitenzi katika kauli ya
kutendeka.
Katika shughuli ya 9, mwelekeze
mwanafunzi aunganishe sentensi
zilizo kitabuni mwake ili ziwe
sentensi moja moja. Wanafunzi
wabadilishane madaftari ili
watathmini sentensi zao. Hakikisha
sentensi zao ni sahihi kisarufi na
zimetumia vitenzi katika kauli ya
kutendana. Majibu tarajiwa:
1. Baba na mtoto wanapendana.
2. Mwalimu na mwanafunzi
wameonana.
3. Fahali na punda wamepigana.
4. Dada na kaka wamebebana.
5. Rita na Anita wanaoshana.
137
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli ya nje ya darasa
Waongoze wanafunzi kuandaa mchezo
wa kuigiza kuhusu umuhimu wa
ndege wa porini. Waelekeze wanafunzi
kufanya mazoezi ya mchezo huo wa
kuigiza. Wanafunzi wapewe fursa ya
kuigiza mchezo huo wa kuigiza wakati
wa siku ya wazazi shuleni. Wanafunzi
wawahimize wazazi na wageni
watakaohudhuria siku hiyo umuhimu
wa kuwatunza na kuwathamini ndege
wa porini. Shughuli hii itakuza ujasiri wa
wanafunzi wa kuzungumza na kuigiza
mbele ya watu pamoja na kuboresha
mawasiliano yao. Pia, itakuza uzalendo
wao.
Majibu ya Zoezi la Mwisho wa
Sura
1. Kubali sentensi zozote zilizo sahihi
zilizotumia visawe vya maneno
matatu.
2. Kubali sifa zozote sahihi za korongo,
mbuni na heroe.
3. Tathmini mchezo wa kuigiza ambao
mwanafunzi atatunga. Hakikisha
unahusu ndege wa porini na ni sahihi
kisarufi na kimantiki.
4. Tathmini majibu ya mwanafunzi:
a) limiwa, limika, limana
b) fuga, fugika, fugana
c) nyoa, nyolewa, nyoana
d) tunza, tunziwa, tunzika
e) chora, choreka, chorana
Hitimisha kipindi hiki kwa
kumhimiza mwanafunzi afanye
kazi ya ziada iliyo kitabuni mwake
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Abuni kifungu kifupi akitumia vitenzi
katika kauli ya kutenda, kutendewa,
kutendeka na kutendana.
Wanafunzi wasomeane vifungu
walivyobuni ili kuvitathmini na
kujifunza kabla ya kipindi kingine
kuanza. Tathmini vifungu vyote vya
wanafunzi.
Hakikisha vifungu vyao vimetumia
vitenzi katika kauli ya kutenda,
kutendewa, kutendeka na kutendana.
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kunyambua vitenzi
kwa usahihi katika kauli za
kutendewa, kutendeka na
kutendana.
2. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kutunga sentensi na
vifungu kwa usahihi akitumia
vitenzi katika kauli za kutendewa,
kutendeka na kutendana.
3. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kubadilisha sentensi
kutoka kauli moja hadi kauli
nyingine kwa usahihi.
138
Kimeidhinishwa na KICD
MAGONJWA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102-110)
Utangulizi
Magonjwa ni hali inayoufanya mwili
wa kiumbe kudhoofika na kukosa afya
njema. Magonjwa pia huitwa maradhi
au ndwele. Magonjwa huwafanya viumbe
kuwa wanyonge na kutoweza kutekeleza
kazi zao za kuyakidhi maisha yao. Ni
muhimu kwa mwanafunzi kufahamu
kuhusu magonjwa mbalimbali na
namna ya kuyazuia. Ufahamu huu
utamwezesha kuyatunza mazingira yake,
kuhifadhi usafi na kupata lishe bora.
Kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali
kutamwezesha mwanafunzi kuwa na afya
njema shuleni na hata nyumbani.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Mazungumzo ya kimuktadha:
Mazungumzo katika miktadha rasmi),
Kusoma kwa mapana (Matini), Kuandika
insha za maelezo na Sarufi (Vinyume vya
vitenzi).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102-103)
Mazungumzo ya kimuktadha
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua miktadha rasmi
kunakotumiwa lugha rasmi ili
kukuza mawasiliano.
b) Kutumia lugha katika miktadha
rasmi ili kufanikisha mawasiliano.
c) Kuchangamkia matumizi ya lugha
katika miktadha rasmi.
Maswali dadisi
1. Ni wapi katika shughuli zetu za
kila siku tunaitumia lugha rasmi?
2. Je, unaweza kutambua lugha rasmi
katika mawasiliano?
3. Lugha rasmi ni lugha gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Ubunifu unakuzwa wakati ambapo
mwanafunzi anashiriki katika
maigizo ya mazungumzo katika
miktadha mbalimbali ili kubaini
miktadha rasmi.
139
Kimeidhinishwa na KICD
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kujadili
miktadha rasmi na kuigiza
mazungumzo katika miktadha
mbalimbali.
(c) Uwazaji wa kina
Uwazaji huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiria kuhusu lugha ya
kutumia katika miktadha rasmi na
miktadha isiyo rasmi ili kuitofautisha.
(d) Uraia na utangamano
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kujadiliana kuhusu miktadha rasmi
na kuiigiza.
(e) Kujiamini na kujithamini
Mwanafunzi atakuza umilisi
huu atakapoweza kuigiza
maigizo mbalimbali ya miktadha
tofautitofauti akitumia lugha rasmi
kwa usahihi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya afya
Inakuzwa mwanafunzi anapofahamu
magonjwa mbalimbali, njia za
kupata magonjwa hayo na jinsi ya
kujikinga dhidi yao. Ufahamu huu
utamwezesha mwanafunzi kujikinga
dhidi ya magonjwa mbalimbali
pamoja na kuwahamasisha
wanajamii wenzake. Pia, mwanafunzi
anapofahamu madhara ya matumizi
ya dawa za kulevya kwa afya pamoja
na umuhimu wa mazoezi ya viungo
vya mwili.
Elimu ya mazingira
Njia mojawapo ya kupata magonjwa
mbalimbali ni kutokana na mazingira
machafu. Elimu ya mazingira itakuzwa
mwanafunzi atakapoyatunza mazingira
yake ili kuzuia magonjwa mbalimbali
kama vile kipindupindu.
Stadi za maisha
Kuigiza kutamwezesha mwanafunzi
kuwasiliana kwa ufasaha na ukakamavu
hivyo kuyaboresha mawasiliano yake.
Pia, anaweza kuibukia kuwa mwigizaji
stadi wa kulipwa.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
wakati wa majadiliano na maigizo
mbalimbali. Pia, yanaweza kukuzwa
mwanafunzi anapotumia lugha
ya adabu kuwasiliana na kuwapa
wenzake fursa ya kuchangia katika
majadiliano na maigizo yao.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa wanafunzi
wanaposhirikiana katika vikundi
kwa amani bila kuzua ugomvi
wowote wanapojadiliana na kuigiza
mazungumzo katika miktadha rasmi.
Uwajibikaji
Utakuzwa mwanafunzi anapofahamu
jukumu lake katika maigizo
mbalimbali na kulitekeleza kwa
ustadi. Pia, mwanafunzi anapomaliza
kazi zake kwa wakati ufaao.
140
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hufunza matumizi ya
lugha rasmi katika miktadha rasmi.
Masomo mengine yote huangazia
miktadha rasmi na lugha itumikayo
kuyafunzia huwa rasmi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapotumia lugha kwa
ufasaha na heshima atakuwa kielelezo
cha jamii katika kuboresha mawasiliano
kwenye miktadha mbalimbali kwa
kutumia lugha ifaavyo.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Ili kuweza kufanikisha ujifunzaji wa kila
mwanafunzi:
Unaweza kumhusisha mfasiri
wa lugha ishara ili kuwasiliana
na wanafunzi wasioweza kusikia
au kuzungumza. Pia, wanafunzi
hawa wanaweza kusikiliza
maelezo kuhusu miktadha rasmi
kutoka kwako au wenzao ili
wajifunze.
Hakikisha kuwa wanafunzi
wasio na uwezo wa kuona wana
mashine za breli ili kufanikisha
ujifunzaji wao.
Washirikishe wanafunzi
wanaojifunza na kuelewa kwa haraka
na wepesi katika kuwafunza wenzao
wanaojifunza na kuelewa polepole.
Washugulikie wanafunzi wenye
changamoto nyingine kadri
ya uwezo wako ili kufanikisha
ujifunzaji wao.
1.1 Mazungumzo katika
miktadha rasmi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102-103)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti zaidi kuhusu miktadha mbalimbali
rasmi na lugha itumikayo ili kuwaelekeza
wanafunzi ipasavyo. Vilevile,
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumika na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Unaweza kuandaa video fupifupi
za mazungumzo ya watu wakiwa
katika miktadha mbalimbali
rasmi ili kukusaidia katika
ufunzaji wa mada hii.
Unaweza kurekodi kipindi kutoka
kwenye runinga kinachoigizwa kwa
Kiswahili katika miktadha rasmi na
kuwaonyesha wanafunzi darasani
ili kufanikisha ujifunzaji wao.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102
2. Rekodi za mazungumzo mbalimbali
rasmi na mashine za breli
3. Rekodi ya kipindi cha Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwachezea
wanafunzi rekodi ya mazungumzo
rasmi iliyoambatanishwa na kitabu
hiki. Waelekeze wanafunzi watazame
na kujadili michoro iliyo vitabuni
mwao katika shughuli ya 1. Majibu
tarajiwa:
a) Daktari anazungumza na mgonjwa
141
Kimeidhinishwa na KICD
akimtibu (muktadha rasmi).
b) Chifu anawahutubia wanakijiji
(muktadha rasmi). c) Mwalimu
mkuu anawahutubia wanafunzi
kwenye gwaride (muktadha rasmi).
d) Wanafunzi wawili wanazungumza
(muktadha usio rasmi). Waelekeze
wanafunzi kutambua miktadha rasmi
na isiyo rasmi kutokana na michoro
waliyojadili.
Wapange wanafunzi katika vikundi
vinne kisha kila kikundi kiigize
mazungumzo yanayoendelea katika
kila mchoro. Kila kikundi kiigize
mbele ya wanafunzi wenzao darasani.
Shughuli hii itakuza ujasiri wa
wanafunzi wa kuongea mbele ya watu
hivyo kujiamini na kujithamini zaidi.
Tathmini uigizaji wa kila kikundi.
Rekebisha matamshi na lugha isiyo
sahihi.
Katika shughuli ya 2, waelekeze
wanafunzi katika vikundi vyao
wajadili kuhusu magonjwa matano
wanayofahamu, dalili zao, kinga zao
pamoja na hospitali wanazofahamu
zilizo karibu na shule yao. Tathmini
majadiliano ya wanafunzi.
Waongoze wanafunzi wawiliwawili
kushiriki maigizo ya mazungumzo
katika miktadha waliyopewa
vitabuni mwao katika shughuli ya
3. Wanafunzi hawa waigize mbele ya
wenzao darasani. Tathmini uigizaji
na lugha yao. Hakikisha wanatumia
lugha rasmi kwa sababu miktadha
waliyopewa ni rasmi. Wanafunzi
wajadili maigizo ya wenzao pamoja
na lugha wanayotumia.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Mwanafunzi atafiti kuhusu njia za
kuambukizwa ugonjwa wa korona,
dalili zake, kinga yake na njia za
kuudhibiti ugonjwa huo. Mwanafunzi
awasomee wenzake darasani maelezo
yake ili wayatathmini na kujifunza.
Majibu tarajiwa:
1. Njia za kuambukizwa ugonjwa wa
korona ni kama vile: Mgonjwa wa
korona anapokohoa au kupiga chafya
karibu nawe (iwapo hujavaa maski ya
uso), kugusa sehemu zilizo na virusi
vya korona kisha kujigusa kwenye
macho, mdomo au pua, kumgusa
mgonjwa wa korona kisha kujigusa
kwenye macho, mdomo au pua n.k.
2. Dalili za ugonjwa wa korona ni
kama vile: kuwa na joto jingi mwilini,
kukohoa, kupiga chafya, kuumwa
na kifua, kuumwa na koo, kupata
matatizo ya kupumua n.k.
3. Kinga za ugonjwa wa korona ni kama
vile: kunawa mikono kila wakati kwa
kutumia maji safi na sabuni, kutumia
kieuzi (‘sanitaiza’), kuvalia barakoa
(maski ya uso), kujizuia kuyagusa
macho yako, mdomo na pua, kukaa
mbali na watu, kutotangamana na
makundi ya watu wengi n.k.
4. Njia za kudhibiti ugonjwa wa korona
ni kama vile: kufika kwenye kituo cha
afya haraka iwezekanavyo ili kupata
dawa za kusaidia kupumua na kudhibiti
joto mwilini, kujitenga (kujikarantini)
na watu ili usiwaambukize virusi vya
korona, kupata ushauri nasaha n.k.
142
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua miktadha rasmi
kunakotumiwa lugha rasmi.
2. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutumia lugha
rasmi katika miktadha rasmi
anapowasiliana na wengine.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapofanya shughuli mbalimbali
za ujifunzaji kwa kuwasiliana na
kushirikiana na wenzake katika
vikundi. Anapowasimulia wenzake
kuhusu matini anazopenda kusoma,
ujumbe na lugha ya matini hizo. Pia,
anapowasiliana na kufanya kazi ya
ziada pamoja na mlezi wake.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
atakapotumia vifaa vya kidijitali
kutafuta mtandaoni matini
za kusoma kuhusu magonjwa
mbalimbali.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kujitafutia matini
mbalimbali za kusoma maktabani au
mtandaoni ili kujifunza zaidi.
(d) Uwazaji wa kina na kutatua
matatizo
Kunakuzwa mwanafunzi anapofikiria
kuhusu ujumbe wa matini
mbalimbali atakazosoma na kuweza
kudondoa mafunzo muhimu.Pia,
mwanafunzi anapofikiria kuhusu jinsi
ya kujikinga kutokana na magonjwa
mbalimbali maishani.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Huu unakuzwa wanafunzi
kutoka maeneo mbalimbali
wanapofanya shughuli za ujifunzaji
kwa ushirikiano katika vikundi.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 104-106)
Kusoma kwa mapana
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini ya aina
mbalimbali ya kusoma na
kuchagua yanayomvutia.
b) Kusoma matini aliyochagua ili
kufaidika na ujumbe na lugha
iliyotumiwa.
c) Kufurahia usomaji wa aina
mbalimbali za matini ili kupanua
mawazo yake.
Maswali dadisi
1. Wewe hupata matini za kusoma
kutoka wapi?
2. Ni habari zipi unazopenda
kusoma kwenye matini?
3. Kwa nini unapenda kusoma
matini unayochagua?
143
Kimeidhinishwa na KICD
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi wanapojadiliana kuhusu
magonjwa mbalimbali na ujumbe wa
matini mbalimbali watakazosoma. Pia,
yanakuzwa mwanafunzi anapotumia
lugha ya adabu kuwasiliana na wenzake
katika vikundi na kuwapa wenzake
fursa ya kuchangia majadiliano yao.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake
katika vikundi bila kuzua fujo
wanapojifunza kuhusu magonjwa
mbalimbali na kujadili ujumbe wa
matini mbalimbali watakazosoma.
Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kusoma matini kwa ufasaha na
usahihi na kueleza ujumbe wake
pamoja na mafunzo anayopata.
Pia, anapoweza kutumia vifaa vya
kidijitali kutafuta mtandaoni matini
salama za kusoma.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hufunza kuhusu usomaji
wa matini mbalimbali.
2. Sayansi na Teknolojia na Sayansi
Kimu
Masomo haya huwa yana mada
zinazofundisha magonjwa
mbalimbali pamoja na umuhimu
wa usafi kama njia mojawapo ya
kujikinga dhidi ya magonjwa.
Wanafunzi wakosoane na
kukubaliana bila fujo ili kuonyesha
uraia mwema.
Elimu ya afya bora
Inakuzwa mwanafunzi anapojifunza
kuhusu magonjwa mbalimbali,
visababishi vyake, dalili zake, jinsi ya
kujikinga na matibabu yanayostahili.
Maarifa haya yatamfaidi katika
kuboresha afya yake maishani.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapopata
maarifa kuhusu magonjwa
mbalimbali na jinsi ya kujikinga
dhidi ya magonjwa hayo hivyo
kuiboresha afya yake maishani. Pia,
zinakuzwa mwanafunzi anapoweza
kusoma matini kwa ufasaha na
usahihi kwani usomaji mahiri
unaweza kumfungulia milango ya
heri ya kupata kazi za usomaji au
utangazaji siku za usoni.
Elimu kwa maendeleo endelevu
Inakuzwa mwanafunzi anapopata
maarifa kuhusu magonjwa
mbalimbali pamoja na dalili, kinga
na matibabu yake ambayo yatamfaidi
maishani.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapovitunza
vifaa vya kidijitali anavyotumia kutafuta
matini za kusoma mtandaoni. Pia,
unakuzwa mwanafunzi anapotekeleza
majukumu yake katika kazi za vikundi
pamoja na kukamilisha kazi zake kwa
wakati ufaao.
144
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakuwa kielelezo
kwa wanafunzi wenzake pamoja na
wanajamii katika kukuza utamaduni
wa usomaji fasaha na sahihi.
Mwanafunzi atayatumia maarifa
atakayopata kuhusu magonjwa
mbalimbali, visababishi vyake, dalili
zake, kinga zake na matibabu yake
kuihamasisha jamii ili kuboresha
afya zao.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Tumia nyenzo mbalimbali ili
kuweza kukidhi mahitaji ya
kila mwanafunzi kulingana na
changamoto zinazomkumba.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona wanaweza kutumia breli
kusoma matini kuhusu magonjwa
mbalimbali na mada nyingine ili
waweze kujifunza. Pia, wanaweza
kukusikiliza au kuwasikiliza
wanafunzi wenzo wakisoma matini
hizo na wakajifunza.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza waelekezwe
kusoma matini kimoyomoyo kisha
watoe maelezo kuhusu waliyojifunza
kwa maandishi kuhusiana na maswali
yaliyopo. Mfasiri wa lugha ishara
anaweza kushirikishwa ili kuwasaidia
katika ujifunzaji wao.
Wanafunzi wasioweza kungamua
wanayojifunza kwa upesi wapewe
mazoezi zaidi ya kusoma matini
nyingine.
Pia, unaweza kuwatumia wanafunzi
wanaoweza kujifunza kwa upesi
kuwasaidia wenzao wanaongamua
mambo polepole katika kusoma
vifungu, kujibu maswali na kufafanua
msamiati lengwa.
Washughulikie wanafunzi walio na
matatizo ya kiafya au kisaikolojia
kadri ya uwezo wako ili waweze
kujifunza bila usumbufu wowote.
2.1 Kusoma matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 104-106)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 3)
Tafiti kwa kina kuhusu matini
mbalimbali za kusoma hasa zenye mada
zinazohusiana na magonjwa na afya.
Unaweza kufanya utafiti wako kwenye
magazeti, majarida, vitabu au mtandaoni.
Utafiti huu utakusaidia katika
kufanikisha ufunzaji wako darasani. Pia,
Unaweza kuandaa nakala za matini
mbalimbali ambazo utawapa
wanafunzi wasome darasani ili
kufanikisha ujifunzaji wao.
Hakikisha mashine za breli zipo na
ziko katika hali nzuri ya kuweza
kutumiwa na wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona.
Unaweza kumfahamisha mapema
mfasiri wa lugha ishara kuhusu
somo hili ili aweze kujiandaa
ifaavyo.
Andaa chati ambazo zimeandikwa
magonjwa mbalimbali, visababishi
vyao, dalili zao na kinga zao.
145
Kimeidhinishwa na KICD
Unaweza kubeba vyanzo mbalimbali
vya matini za kusoma (kama vile
magazeti, majarida, vitabu n.k.) na
ukawaonyesha wanafunzi darasani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
104
2. Majarida, magazeti na vitabu
3. Chati zilizoandikwa maelezo
kuhusu magonjwa mbalimbali
4. Nakala za matini mbalimbali za
kusoma
5. Breli
6. Mfasiri wa lugha ishara
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa
kuwashirikisha wanafunzi kujadili
michoro iliyo vitabuni mwao katika
shughuli ya 1. Majibu tarajiwa: a)
Msichana anasoma matini kutoka
kwenye mtandao kwa kutumia
tarakilishi. b) Babu anasoma matini
kutoka kwenye gazeti. c) Mwanafunzi
anasoma matini kutoka kwa kitabu
maktabani. Wanafunzi waelezane
kuhusu vyanzo mbalimbali vya
matini za kusoma wanavyopendelea
kutumia kupata matini za kusoma.
Waelekeze kufahamu kuwa matini za
kusoma zinaweza kupatikana kutoka
kwa magazeti, majarida, vitabu na
kwenye mtandao.
Katika shughuli ya 2, mwongoze
mwanafunzi kusoma kimyakimya
matini iliyo kitabuni mwake kisha
ajibu maswali yaliyopo. Wape
wanafunzi wote fursa ya kujadiliana
kuhusu ujumbe wa matini
waliyosoma pamoja na mafundisho
waliyopata kutokana na matini hiyo.
Majibu tarajiwa:
1. Tathmini majibu ya mwanafunzi, kwa
mfano: kwenye magazeti, majarida,
vitabu, mtandao n.k.
2. Tathmini majibu ya mwanafunzi,
kwa mfano: Taifa Jumapili, Gazeti la
biashara, Gazeti la michezo.
3. Tathmini majibu ya wanafunzi
wakiwa katika vikundi, kwa mfano:
mtu hufahamu mambo asiyoyajua,
huburudika na kufurahishwa,
huonywa na kupata ushauri nasaha,
hukuza mbinu zake za usomaji bora
n.k.
4. Wanafunzi watumie kamusi za
Kiswahili kupata maana za maneno
yaliyokolezwa rangi katika matini
waliyosoma. Tathmini maana hizo.
5. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Kubali majibu yanayohusu shughuli
ambazo hutendeka maktabani.
6. Tathmini majibu ya wanafunzi,
kwa mfano: kusoma matini faafu
zisizopotosha.
Waelekeze wanafunzi katika kufanya
shughuli ya 3 wakiwa wawiliwawili
ambapo watasimuliana visa vyovyote
ambavyo wamewahi kusoma kuhusu
magonjwa. Wanafunzi waelezane
walikopata matini walizosoma na
mafundisho waliyopata kutokana
na matini hizo. Tathmini maelezo
ya wanafunzi. Hakikisha ni sahihi
kulingana na magonjwa husika.
146
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya 4, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha uwape
nakala za matini mbalimbali (ambazo
ulikuwa ushaandaa mapema kabla
ya funzo hili). Kila kikundi kichague
matini itakayowavutia na waisome.
Wanafunzi wajadili ujumbe na lugha
ya matini zao kisha mmoja wao
awaeleze wanafunzi wengine kuhusu
waliyojadili. Tathmini majadiliano
na mawasilisho ya wanafunzi kutoka
kwa kila kikundi. Shughuli hii
itaboresha usomaji wa wanafunzi
pamoja na kukuza ujasiri wao wa
kuzungumza kwa ufasaha mbele ya
watu.
Somo hili linaweza kufanyiwa
maktabani. Iwapo shule yako haina
maktaba, usijali, unaweza kufanyia
somo hili darasani na wanafunzi
wakajifunza.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Mwanafunzi atafute mtandaoni
matini itakayomvutia kuhusu
magonjwa yoyote manne. Aisome
kisha aandike muhtasari wa matini
hiyo katika daftari lake. Awasomee
wenzake muhtasari huo darasani ili
wautathmini na kujifunza. Tathmini
kazi za wanafunzi pamoja na
mawasilisho yao. Hakikisha matini
walizosoma zilihusu magonjwa
mbalimbali.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua aina mbalimbali za
matini salama za kusoma kutoka
kwa vyanzo mbalimbali salama.
2. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kusoma matini kwa
ufasaha na kufaidika na ujumbe
uliomo.
3. Tathmini ikiwa mwanafunzi
amejua magonjwa mbalimbali
pamoja na visababishi vyao, dalili
zao na kinga zao.
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 106-108)
Insha za maelezo
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vifungu vya maelezo
vilivyoandikwa kwenye matini
mbalimbali.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa
kufuata mtindo na muundo
ufaao.
c) Kuchangamkia utunzi mzuri wenye
ujumbe mahususi.
Maswali dadisi
1. Insha ya maelezo ni gani?
2. Je, ni mada gani inaweza
kuandikiwa insha za maelezo?
3. Ni mambo gani yanafaa
kuzingatiwa unapoandika insha
za maelezo?
147
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kubuni na kuandika
insha ya maelezo kwa maneno yake
mwenyewe bila kunakili insha za
wenzake. Pia, anapoweza kuandika
vidokezo vya kuandikia insha ya
maelezo.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa wakati
mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake katika vikundi kujadiliana
kuhusu uandishi wa insha ya
maelezo. Pia, anapojadiliana
na wenzake kuhusu magonjwa
mbalimbali, dalili zao, jinsi ya
kujikinga na jinsi ya kuyatibu.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia vifaa vya kidijitali
kuandika insha ya maelezo akisaidiwa
na mlezi wake katika kazi ya ziada.
(d) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoyatafakari maswali dadisi
husika na anapoendelea kujifunza
kuandika insha mbalimbali za
maelezo kwa kuzingatia mada
tofautitofauti.
(e) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunga na kuandika insha ya maelezo
kisha kuwasomea wenzake darasani
bila woga ili waitathmini na kujifunza.
(f) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiri kuhusu mada ya insha
aliyopewa, vidokezo atakavyotumia
pamoja na insha ya maelezo ambayo
atatunga kwa ufasaha. Uwazaji wa
aina hii utamwezesha mwanafunzi
kujitegemea maishani kwa kuweza
kupata suluhu kwa changamoto
zitakazomkumba.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Uraia unakuzwa wanafunzi wa asili
mbalimbali wanapofanya kazi kwa
kushirikiana katika vikundi licha ya
tofauti zao anuwai. Pia, mwanafunzi
anapofahamu kuwa ugonjwa haujui
kabila kwani huweza kumpata mtu
yeyote hivyo kuthaminiana katika
jamii.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapojifunza
uandishi bora na utoaji bora
wa maelezo. Pia, mwanafunzi
anapojitambua na kujithamini
anapoiandika insha ya maelezo.
Elimu ya afya bora
Elimu hii inakuzwa mwanafunzi
anapojadiliana na wenzake pamoja
na mlezi wake kuhusu magonjwa
mbalimbali, dalili zao, kinga zao
pamoja na tiba yao. Kutokana
na ufahamu huu, mwanafunzi
atafahamu jinsi ya kujikinga dhidi
ya magonjwa mbalimbali hivyo
kudumisha afya bora katika jamii.
148
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa heshima na adabu hata
kwa kutumia lugha ya adabu. Pia,
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
na kuwapa fursa ya kuchangia katika
majadiliano yao.
Uwajibikaji
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kuvitunza vifaa vyake
vya ujifunzaji. Pia, mwanafunzi
anapohakikisha kuwa amefanya
kazi yake ya uandishi wa insha
kama alivyoelekezwa na mwalimu
na kuikamilisha kwa wakati ufaao,
pamoja na kutekeleza majukumu
yake katika vikundi impasavyo.
Umoja na amani
Maadili haya yatakuzwa kupitia kwa
mwanafunzi kushirikiana na wenzake
katika vikundi kwa amani bila kuzua
fujo wanapojadili kuhusu uandishi wa
insha ya maelezo.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya hushughulikia mada za
uandishi.
2. Sayansi na Teknolojia
Somo hili lina mada zinazofunza
kuhusu magonjwa mbalimbali.
Masomo mengine yote hutumia
maelezo katika ufunzwaji wao.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha
wenzake shuleni na hata nyumbani
kuhusu umuhimu wa uandishi mzuri
hivyo kuyaboresha mawasiliano
katika jamii.
Kutokana na ufahamu wa magonjwa
mbalimbali, dalili zao, kinga zao na tiba
yao, mwanafunzi ataweza kuihamasisha
jamii kuhusu jinsi ya kujikinga dhidi ya
magonjwa mbalimbali hivyo kuboresha
afya zao.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
watumie mashine za breli kujifunza
muundo na mtindo wa kuandika
insha ya maelezo. Pia, wanaweza
kusikiliza maelezo kuhusu uandishi
wa insha ya maelezo yakisomwa nawe
au wanafunzi wenzao.
Wanafunzi walio na changamoto
ya kusikia ama kuzungumza
wanaweza kusaidiwa kujifunza kwa
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara darasani.
Wanafunzi wenye changamoto ya
kuandika polepole waongezwe muda
wa kuandika ili waweze kujieleza
zaidi. Baadaye, mwalimu awape
wanafunzi hao mafunzo ya ziada
yanayohusu kuandika maneno kwa
kasi ili waweze kuandika insha kwa
muda unaofaa.
Wanafunzi walio na uwezo wa
kung’amua wanayojifunza kwa
upesi baada ya kushirikishwa katika
shughuli za ujifunzaji wapewe fursa
ya kuandika insha za maelezo zaidi
katika mada husika.
Wanafunzi wanaochukua muda
149
Kimeidhinishwa na KICD
kufanya shughuli ya 1 ambapo
watajikumbusha kuhusu waliyowahi
kujifunza kuhusiana na uandishi
wa insha za maelezo. Wanafunzi
wakumbushane kuhusu mambo
muhimu ya kuzingatia wanapoandika
insha za maelezo. Tathmini maelezo
yao. Insha ya maelezo hufafanua zaidi
kuhusu kitu au jambo na huwa na
mada, utangulizi, mwili na hitimisho.
Katika shughuli ya 2, wape
wanafunzi matini mbalimbali
ulizoandaa mapema. Matini hizo
ziwe na mchanganyiko wa vifungu
vikiwemo vya maelezo ili wanafunzi
waweze kutambua vifungu vya
maelezo.
Waongoze kutambua vifungu
vya maelezo kisha wavisome na
kujadiliana kuhusu ujumbe, mada
na muundo wa vifungu hivyo.
Mwakilishi mmoja kutoka kwa
kila kikundi awaeleze wanafunzi
wengine waliyojadiliana. Hakikisha
umewapanga wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na
uwezo wao. Tathmini majadiliano ya
wanafunzi.
Washirikishe wanafunzi wakiwa
katika vikundi wajadili matukio
kwenye michoro iliyo vitabuni mwao
katika shughuli ya 3 kisha wajibu
maswali waliyopewa. Michoro hiyo
inaonyesha mtoto anayeumwa na
mbu, anakuwa mgonjwa, anapelekwa
hospitalini, anatibiwa na kushauriwa
kulala ndani ya chandarua.
Kutokana na matukio ya michoro
zaidi kuelewa wanayojifunza
washirikishwe katika shughuli
zaidi kuhusu uandishi wa insha za
maelezo na kutengewa muda zaidi
wa kujifunza wakati wa jioni.
3.1 Insha za maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 106-108)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu uandishi wa insha
za maelezo, muundo wake, mtindo wake
na lugha yake ili kufanikisha ufunzaji
wako darasani. Vilevile,
Tafuta matini mbalimbali zenye
mchanganyiko wa vifungu vikiwemo
vya maelezo (kutoka kwenye vitabu,
magazeti, majarida au mtandaoni)
utakazowapa wanafunzi darasani
ili waweze kuchagua vifungu vya
maelezo na kuwasaidia katika
ujifunzaji wao.
Hakikisha mashine za breli zipo na
ziko katika hali nzuri ya kutumiwa
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona ili waweze kuandika insha za
maelezo.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
kuhusu funzo hili mapema ili aweze
kujiandaa ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 106
2. Matini zenye vifungu mbalimbali
vikiwemo vya maelezo
3. Mfasiri wa lugha ishara na breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa
kuwaongoza wanafunzi wawiliwawili
150
Kimeidhinishwa na KICD
hiyo, wanafunzi waandike vidokezo.
Kila mwanafunzi atumie vidokezo
watakavyoandika kutunga insha ya
maelezo na kuiandika katika daftari
lake. Tathmini insha za wanafunzi.
Hakikisha zina mada, utangulizi,
mwili, hitimisho na zinazingatia
kanuni za kisarufi.
Katika shughuli ya 4, waongoze
wanafunzi kujadili mada, muundo,
ujumbe na mapambo waliyotumia
katika uandishi wa insha katika
shughuli ya 3. Tathmini majadiliano
yao.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini insha atakayoandika
mwanafunzi na kukutumia pamoja
na wanafunzi wenzake mtandaoni
ili muitathmini na kujifunza. Insha
hiyo iwe ya maelezo kuhusu ugonjwa
wowote unaoathiri watoto wadogo.
Pia, hakikisha insha hiyo inazingatia
kanuni zote za kuandika insha
za maelezo. Mifano ya magonjwa
ambayo huathiri watoto wadogo
ni: kifaduro, utapiamlo, surua,
kipindupindu/waba, choa, malaria
n.k.
3. Tathmini ikwa kila mwanafunzi
amefahamu kuhusu magonjwa
mbalimbali yanayowaathiri watoto
wadogo na jinsi ya kujikinga dhidi
yao.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua vifungu vya maelezo
kutoka kwenye matini mbalimbali.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuandika insha ya maelezo
kwa kufuata mtindo, muundo na
kanuni za kisarufi zinazofaa.
4. Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 108-110)
Vinyume
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vinyume vya vitenzi
katika matini.
b) Kuunda sentensi kwa kutumia
vinyume vya vitenzi.
c) Kuchangamkia matumizi sahihi
ya vinyume vya vitenzi katika
mawasiliano ya kila siku.
Maswali dadisi
1. Je, kuandika kinyume cha kitenzi
ni kufanya nini?
2. Je, ni vitenzi gani unavyoweza
kutambua vinyume vyake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutunga sentensi sahihi
akiwa peke yake akitumia vinyume
vya vitenzi bila kunakili sentensi za
wenzake.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kutambua
151
Kimeidhinishwa na KICD
vinyume vya vitenzi mbalimbali
kwa usahihi. Pia, anaposhirikiana
na wenzake kuunda sentensi sahihi
akitumia vinyume vya vitenzi.
(c) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapofikiri kuhusu jinsi ya kuandika
vinyume vya vitenzi na kuvitumia
kutungia sentensi sahihi. Uwazaji
huu utamsaidia mwanafunzi kuweza
kufikiri kuhusu jinsi ya kupata suluhu
ya matatizo yanayoweza kumkumba
maishani.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu endelevu
Hii inakuzwa mwanafunzi
anapopanua mawazo yake kuhusu
mazingira yake kwa kutambua
vinyume vya vitenzi anavyofanya
kila siku au kutokana na vitendo
anavyoshuhudia katika jamii yake.
Pia, anapoendelea kujifunza shuleni
na nje ya shule kuhusu vitendo
vifaavyo kutendwa.
Stadi za maisha
Zinakuwa mwanafunzi anapojifunza
kuhusu vitendo vinavyofaa kutendwa
katika maisha na jinsi ya kuishi
na wenzake. Pia, anapofanya kazi
inayohusisha kutunga sentensi
kwa kutumia vinyume vya vitenzi
darasani akiwa pekee hivyo
kumwezesha kukuza stadi ya
kujitegemea maishani.
Uraia
Uraia unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake wa asili
mbalimbali kutambua vinyume vya
vitenzi mbalimbali na kuvitungia
sentensi sahihi.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuvitunza vifaa vyake vya kusomea
na kuandikia darasani na nyumbani.
Pia, anapotekeleza majukumu yake ya
kuigiza vitenzi na vinyume vyao kwa
ufasaha na kukamilisha kazi zake kwa
wakati ufao.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi wanapoandika vinyume
vya vitenzi na kuvitungia sentensi
sahihi. Pia, anapowasiliana na wenzake
kwa lugha ya adabu na kuwapa fursa
ya kuchangia katika majadiliano yao.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kufanya
shughuli za vikundi kwa amani bila
kuzua ugomvi wowote.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya huwa yana mada
zinazoshughulikia vinyume vya
vitenzi.
Masomo yote kwa kiwango fulani
hutumia vitenzi na vinyume vyao
katika maelezo yao.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapoelewa matumizi
sahihi ya vitenzi pamoja na vinyume
vyao katika mawasiliano atakuwa
152
Kimeidhinishwa na KICD
kielelezo cha lugha fasaha katika jamii.
Atawahamasisha wanajamii kuhusu jinsi
ya kutumia lugha ya Kiswahili ipasavyo
katika kuboresha mawasiliano yao.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasioweza kusikia au
kuzungumza, watambue vitenzi
na vinyume vyao kwa kuviandika
kwenye madaftari yao au kuvipigia
mistari kwenye tarakilishi. Pia,
unaweza kumshirikisha mfasiri wa
lugha ishara ili kuwafaa wanafunzi
hawa katika ujifunzaji wao.
Wanafunzi ambao hawana uwezo
wa kuona wanaweza kutumia breli
au wakusikilize ukiyasoma maelezo
kuhusu vitenzi na vinyume vyao
au wawasikilize wanafunzi wenzao
wakiyasoma maelezo hayo.
Wanafunzi wasiojimudu kufahamu
vipengele vyote walivyojifunza
kuhusu vitenzi na vinyume vyao
waandaliwe kipindi cha ziada cha
kujifunza zaidi baada ya masomo ya
siku ili kuafikia matarajio ya mada.
Wanafunzi wanaojimudu kufahamu
vipengele vyote walivyojifunza
kuhusu vitenzi na vinyume vyao
wapewe mazoezi ziada ya kufanya
au wawasaidie wenzao wanaojifunza
polepole.
pamoja na vinyume vyao ili kuweza
kumwelekeza mwanafunzi vyema
darasani. Vilevile,
Unaweza kutafuta picha au
michoro inayoonyesha vitenzi
mbalimbali pamoja na vinyume
vyao ili kukusaidia katika ufunzaji
wako darasani na kurahisisha
uelewa wa wanafunzi.
Andaa kadi zilizoandikwa vitenzi
mbalimbali pamoja na vinyume
vyao ambazo zitatumika kucheza
mchezo wa kadi darasani. Mchezo
huu utarahisisha uelewa wa
wanafunzi kuhusu vinyume vya
vitenzi mbalimbali.
Hakikisha mashine za breli zipo
na ziko katika hali nzuri ya
kuweza kutumika na wanafunzi
wasio na uwezo wa kuona ili
kuwasaidia katika ujifunzaji wao.
Hakikisha umejiandaa vilivyo
ili kuwasaidia wanafunzi wenye
matatizo ya kiafya au kisaikolojia
kadri ya uwezo wako ili waweze
kujifunza bila usumbufu wowote.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
108
2. Mashine za breli
3. Michoro au picha za vitenzi
mbalimbali na vinyume vyao
4. Kadi zilizoandikwa vitenzi
mbalimbali pamoja na vinyume
vyao
5. Mfasiri wa lugha ishara
4.1 Vinyume vya vitenzi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 108-110)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu vitenzi mbalimbali
153
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwaongoza
wanafunzi wawiliwawili kujadili
vitendo katika michoro iliyo
vitabuni mwao katika shughuli ya 1.
Wanafunzi waelezane ugunduzi wao.
Waelekeze wanafunzi kubaini kuwa
vitenzi hivyo ni pamoja na vinyume
vyao: lala - amka, keti simama.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi viwili
kulingana na idadi na uwezo wao
kisha uandike ubaoni kitenzi kimoja.
Kikundi kimoja kisome kitenzi hicho
kisha kikundi cha pili kiigize kitendo
hicho. Kikundi cha pili kitoe kinyume
cha kitendo walichoigiza kisha
kikundi cha kwanza kiigize kinyume
hicho. Mchezo huu uendelee hadi
vitenzi vyote utakavyoandika ubaoni
visomwe na kuigizwa. Mifano
ya vitenzi vya kuandika ubaoni:
lia cheka, enda rudi, andika
futa, vaa vua, ficha fichua n.k.
Waelekeze wanafunzi kufahamu
kuwa vinyume vya vitenzi ni maneno
ambayo yanaonyesha vitendo vilivyo
tofauti kwa maana inayopingana au
kukinzana.
Mwongoze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 3, ambapo atatambua
kwa usahihi vitenzi pamoja na
vinyume vyao kutoka kwenye kapu la
maneno lililo kitabuni mwake kisha
aviandike daftarini mwake. Majibu
tarajiwa: pakia pakua, lia cheka,
andika futa, panga pangua, ficha
fichua, meza tema, enda - rudi,
vaa –vua.
Mwongoze mwanafunzi katika
utunzi wa sentensi sahihi akitumia
vitenzi pamoja na vinyume vyao
alivyotambua kutoka kwenye kapu
la maneno. Tathmini sentensi za
mwanafunzi. Hakikisha ni sahihi na
zinatumia vitenzi pamoja na vinyume
vyao kutoka kwenye kapu la maneno
husika.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada. Majibu
tarajiwa:
1. Habari hizo zilimfanya acheke wakati
wote.
2. Bahati alitabasamu alipomwona
ndugu yake.
3. Chifu alimkashifu mkulima yule.
4. Mwanafunzi alisimama chini ya mti
akisoma hadithi.
5. Mtoto yule alinyamaza sana.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua vinyume vya vitenzi
katika sentensi na matini.
2. Tathmini iwapo kila mwanafunzi
anaweza kuunda sentensi sahihi kwa
kutumia vitenzi pamoja na vinyume
vyao sahihi.
154
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli ya nje ya darasa
Waongoze wanafunzi kufanya kampeni
kwa wanajamii wanaoishi katika eneo
lililo karibu na shule yenu kuhusu
ugonjwa hatari wa korona. Wanafunzi
wawaeleze wanajamii kuhusu njia za
kupata maambukizi ya ugonjwa huo
na jinsi wanavyoweza kujikinga. Kwa
kushirikiana na mamlaka ya eneo lenu,
mnaweza kuwapa wanajamii sanitaiza
na barakoa za kuvaa usoni ili kujikinga
dhidi ya korona. Shughuli hii itakuza
utangamano, uzalendo, afya njema na
upendo.
3. Tathmini majibu ya mwanafunzi.
Mifano ya magonjwa yanayosababishwa
na mazingira machafu ni kama vile:
kipindupindu/waba, malaria, kichocho,
homa ya matumbo n.k.
4. Tathmini insha ya mwanafunzi.
Hakikisha inazingatia kanuni zote za
uandishi wa insha ya maelezo kama
vile: kuwa na mada, utangulizi, mwili
na hitimisho pamoja na kuzingatia
mtindo, lugha na muundo ufaao.
5. a) fumbua b) fumua c) funua
d) tawanya
6. Tathmini sentensi atakazotunga
mwanafunzi. Hakikisha ni sahihi
kisarufi, kimantiki na zinatumia
vinyume vya vitenzi alivyoandika.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Tathmini miktadha sahihi ambayo
mwanafunzi ataandika. Sharti iwe
miktadha rasmi pekee. Kwa mfano:
shuleni, mahakamani, hospitalini,
ofisini n.k.
2. Tathmini majibu ya mwanafunzi
kuhusu vyanzo vya matini ya kusoma.
Kwa mfano: magazetini, vitabuni,
majaridani, mtandaoni n.k.
155
Kimeidhinishwa na KICD
KUDHIBITI ITIKADI ZA
KIDINI NA ZA KIJAMII
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 111-122)
Utangulizi
Itikadi ni imani au mawazo fulani ambayo
huwa misingi ya nadharia na mfumo wa
dini au jamii fulani. Itikadi ndizo huipa
jamii au dini fulani namna ya kuendesha
shughuli zake za kila siku.
Itikadi za kidini ni jinsi mtu anavyoamini
na kufuata dini fulani. Nchini Kenya kuna
dini mbalimbali ambazo kila mwananchi
ana uhuru wa kuchagua ya kuamini na
kufuata mafundisho na sheria zake. Kila
mwananchi anapaswa kuheshimu dini za
wenzake kwa sababu imeandikwa kwenye
katiba ya nchi kuwa kila mwananchi ana
uhuru wa kuabudu.
Itikadi za kijamii ni imani, desturi za
maisha au mienendo ya watu katika
jamii. Itikadi hizi hujumuisha mavazi,
vyakula, sehemu za makao, marafiki n.k.
Kila jamii ina mienendo mbalimbali
ambayo wanajamii wake hupendelea
kufuata. Sharti itikadi za kidini na
kijamii zidhibitiwe ili zilindwe na
kuhifadhiwa bila kuvuka mipaka.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Tashbihi: Tashbihi za tabia), Kusoma
kwa mapana (Matini ya kidijitali),
Kuandika insha ya masimulizi na Sarufi
(Nyakati na hali - hali ya mazoea na hali
timilifu).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 111-113)
Tashbihi
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua tashbihi za tabia katika
matini.
b) Kutumia tashbihi za tabia kwa
usahihi katika sentensi.
c) Kufurahia matumizi ya tashbihi
za tabia katika mawasiliano ya
kila siku.
Maswali dadisi
1. Unafahamu maana ya tashbihi?
2. Taja mifano mbalimbali ya tashbihi
unazofahamu.
3. Ni tashbihi zipi hutumiwa kueleza
tabia?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa kupitia
kwa mwanafunzi kufanya shughuli
mbalimbali kwa kushirikiana na
wenzake katika vikundi. Mwanafunzi
156
Kimeidhinishwa na KICD
atafahamu maana ya tashbihi, mifano
ya tashbihi za tabia pamoja na maana
zao akiwa na wenzake katika vikundi.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposaidiwa na mlezi wake
kutafuta mtandaoni picha za viumbe
mbalimbali na kutunga tashbihi za
tabia akitumia sifa zao. Hivyo, atapata
ujuzi wa kutumia vifaa vya kidijitali.
(c) Hamu ya kujifunza
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anaposhiriki katika kusoma matini
mbalimbali na kutambua tashbihi za
tabia. Anapata hamu ya kuendelea
kutafuta tashbihi zaidi za tabia
pamoja na maana zao akiwa peke
yake shuleni na nje ya shule.
(d) Ubunifu
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutumia sifa za viumbe
mbalimbali kutunga tashbihi za tabia
zenye maana.
(e) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutambua na kueleza maana ya tashbihi
za tabia mbele ya wenzake bila woga.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Kutokana na ufahamu wa tashbihi
mbalimbali za tabia, mwanafunzi
atajifunza kuwa mwenye tabia
njema na kuepuka au kurekebisha
tabia zisizo njema maishani. Pia,
ataimarisha mawasiliano yake
atakapoweza kutumia tashbihi za
tabia kwa usahihi katika mawasiliano
shuleni na nje ya shule.
Utunzaji wa viumbe (wanyama,
ndege, wadudu n.k.)
Utunzaji huu unadhihirika kupitia
kwa tashbihi za tabia ambazo
mwanafunzi atatunga kuhusu viumbe
mbalimbali hivyo kuweza kutambua
umuhimu wa viumbe hao maishani
na kuwatunza na kuwahifadhi.
Ushauri nasaha
Mwanafunzi atakuwa mwenye tabia
njema kutokana na kujifunza na
kutumia tashbihi za tabia katika
mawasiliano. Mwanafunzi atatambua
tabia njema za kuiga na tabia zisizo
njema za kurekebisha au kuacha.
Uraia na utangamano
Utakuzwa mwanafunzi akishirikiana
na wenzake kutoka maeneo
mbalimbali katika vikundi kujadili
maana na matumizi ya tashbihi
mbalimbali za tabia.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na wenzake katika
vikundi kwa kutumia lugha ya adabu.
Pia, mwanafunzi anapoyaheshimu
maoni ya wenzake katika vikundi
wanapojadiliana kuhusu tashbihi za
tabia.
Amani na umoja
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoweza kushirikiana na wenzake
kwa amani katika vikundi wanapojadili
157
Kimeidhinishwa na KICD
maana za tashbihi mbalimbali za tabia
bila kuzua ugomvi wowote.
Upendo
Unakuzwa mwanafunzi
anapojifunza kuwapenda wenzake
wanapotangamana katika vikundi
kujadili tashbihi mbalimbali za tabia.
Pia, anapowapa wenzake fursa ya
kuchangia katika majadiliano yao
katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanafundisha mada
kuhusu tashbihi.
2. Sayansi na Teknolojia na Somo la
Jamii
Masomo haya yanafundisha mada
kuhusu viumbe mbalimbali (tabia
zao).
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Baada ya mwanafunzi kujifunza tashbihi
za tabia, anatarajiwa kuwa kielelezo
bora katika jamii katika kuwa na tabia
njema na kuzirekebisha au kuziacha
tabia zisizo njema.
Mwanafunzi atawashirikisha wenzake
shuleni na nyumbani katika kutumia
tashbihi mbalimbali za tabia kwa
usahihi. Kufanya hivi kutaimarisha
mawasiliano yao katika jamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi walio na uwezo wa
kung’amua wanayojifunza kwa
upesi baada ya kushirikishwa katika
shughuli za ujifunzaji wapewe fursa
ya kubuni sentensi zaidi zenye
tashbihi za tabia.
Wanafunzi ambao wanachukua
muda zaidi kabla ya kufahamu
wanayojifunza washirikishwe katika
shughuli zaidi za ujifunzaji wa
tashbihi za tabia na kutengewa muda
zaidi wa kujifunza baada ya masomo
jioni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuzungumza au kusikia waelekezwe
kutambua tashbihi za tabia katika
sentensi au matini kwa kuzipigia
mistari. Mfasiri wa lugha ishara
anaweza kushirikishwa katika funzo
hili.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia breli kujifunza au
kusikiliza tashbihi za tabia zikisomwa
na mwalimu, wanafunzi wenzao au
kutoka kwenye kanda iliyorekodiwa.
Mwalimu ajiandae kuwasaidia
wanafunzi wenye matatizo ya kiafya
au kisaikolojia kadri ya uwezo wake
ili kufanikisha ujifunzaji wao.
1.1 Tashbihi za tabia
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 111-113)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusu tashbihi mbalimbali
za tabia pamoja na maana na matumizi
yao ili kufanikisha ufunzaji na ujifunzaji
wa somo hili. Pia,
Andaa michoro au picha za viumbe
mbalimbali watakaotumika kubuni
tashbihi mbalimbali za tabia.
158
Kimeidhinishwa na KICD
Andaa matini iliyotumia tashbihi
za tabia ambayo utawasomea
wanafunzi darasani ili waweze
kutambua tashbihi za tabia
zilizotumika.
Pia, unaweza kuandika tashbihi
mbalimbali za tabia kwenye chati.
Tashbihi hizi zitakusaidia katika
ufunzaji wako darasani.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kutumiwa na
wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara mapema kuhusu funzo hili
ili aweze kujiandaa ifaavyo.
Hakikisha una kamusi za tashbihi
za Kiswahili.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
111
2. Michoro au picha za viumbe
mbalimbali
3. Breli
4. Mfasiri wa lugha ishara
5. Matini iliyotumia tashbihi za tabia
6. Chati zilizoandikwa tashbihi
mbalimbali za tabia
7. Kamusi ya tashbihi za Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa shughuli
ya 1 kwa kuwaomba wanafunzi
wajikumbushe kuhusu waliyojifunza
katika gredi ya nne kuhusu tashbihi.
Wanafunzi wawiliwawili waelezane
maana ya tashbihi na wataje mifano
ya tashbihi wanazojua. Tathmini
maelezo yao pamoja na mifano
watakayotaja.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na uwezo na idadi yao na uwaelekeze
wajadili tabia za wanyama walio
katika picha walizopewa vitabuni
mwao. Majibu tarajiwa: a) kobe ni
mwenda pole b) sungura ni mjanja
c) kinyonga ni kigeugeu d) simba-
ni mkali.
Waongoze wanafunzi kutambua
tashbihi zinazoweza kutumika
kueleza tabia za wanyama walio
kwenye picha walizopewa vitabuni
mwao. Majibu tarajiwa: a) Enda
polepole kama kobe b) Mjanja kama
sungura c) Kigeugeu kama kinyonga
d) Mkali kama simba.
Waelekeze wanafunzi wote kutunga
sentensi sahihi wakitumia tashbihi
zinazolinganisha tabia za watu na za
wanyama walio kwenye picha zilizo
vitabuni mwao. Majibu tarajiwa:
1. Nyanya yangu hutembea polepole
kama kobe.
2. Mwanafunzi huyu ni mjanja kama
sungura.
3. Mhalifu huyo ni kigeugeu kama
kinyonga.
4. Mjomba wangu ni mkali kama
simba.
Hakiki sentensi za wanafunzi. Hakikisha
ni sahihi na zinatumia tashbihi za tabia
kwa usahihi kulingana na wanyama
waliopewa vitabuni mwao.
Katika shughuli ya 3, wanafunzi
wakiwa katika vikundi wataje viumbe
159
Kimeidhinishwa na KICD
wengine ambao wanaweza kutumiwa
kuunda tashbihi za tabia.
Majibu tarajiwa: fisi, mkizi, kunguru,
njiwa, nguruwe, kiboko n.k. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
Mwongoze mwanafunzi kuunda
tashbihi sahihi za tabia akitumia
majina ya viumbe waliowataja.
Majibu tarajiwa: mlafi kama fisi,
hasira kama za mkizi, mwoga kama
kunguru, mpole kama njiwa, mchafu
kama nguruwe, mnene kama kiboko
n.k. Tathmini tashbihi ambazo
mwanafunzi ataunda. Hakikisha ni
sahihi na zinarejelea tabia za viumbe
aliowataja.
Mwelekeze mwanafunzi kutunga
sentensi sahihi akitumia tashbihi
alizounda.
Wanafunzi wasomeane sentensi
walizotunga wakiwa katika vikundi ili
wazitathmini wao kwa wao.
Majibu tarajiwa:
1. Mtu huyu ni mlafi kama fisi.
2. Jirani yetu ana hasira kama za
mkizi.
3. Dada yake ni mwoga kama
kunguru.
4. Babu yangu ni mpole kama njiwa.
5. Mwendawazimu yule ni mchafu
kama nguruwe.
6. Mwimbaji huyu ni mnene kama
kiboko.
Andaa mapema matini iliyotumia
tashbihi za tabia ambayo utawasomea
wanafunzi darasani katika shughuli
ya 4. Hakikisha unasoma matini hiyo
kwa ufasaha na kwa sauti ya kusikika
na wanafunzi wote darasani. Matini
hiyo isheheni tashbihi mbalimbali za
tabia. Wanafunzi watambue tashbihi
za tabia kutoka kwenye matini hiyo,
waziandike kwenye madaftari yao na
kuzitungia sentensi sahihi. Tathmini
sentensi za wanafunzi.
Washirikishe wanafunzi kujadiliana
jinsi watu wenye tabia zisizo njema
wanaweza kujirekebisha maishani.
Tathmini majadiliano ya wanafunzi
katika vikundi vyao.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini iwapo mwanafunzi
amefahamu sifa za njiwa, mkizi,
fisi na nguruwe kutoka mtandaoni.
Aunde tashbihi sahihi kwa kutumia
sifa za viumbe hao. Majibu tarajiwa:
Mpole kama njiwa, hasira kama za
mkizi, mlafi kama fisi, mchafu kama
nguruwe.
Tathmini sentensi ambazo
mwanafunzi atatunga akitumia
tashbihi za tabia alizounda.
Tathmini
1. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kutambua tashbihi za
tabia katika matini.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia tashbihi za tabia kwa
usahihi kutunga sentensi sahihi.
160
Kimeidhinishwa na KICD
kutafuta, kusakura na kusoma matini
mbalimbali kuhusu itikadi za kidini
na kijamii zilizo salama kwa kusoma
mtandaoni.
(b) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu utakuzwa kupitia kwa
mwanafunzi kufanya shughuli
mbalimbali kwa kuwasiliana na
kushirikiana na wenzake katika
vikundi. Kutafuta matini salama za
kusoma mtandaoni kuhusu itikadi
za kidini na za kijamii, kutambua na
kujadili maana ya msamiati katika
matini lengwa. Pia, kuwasiliana na
kufanya kazi ya ziada pamoja na
mlezi wake.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kutafuta matini zaidi za
kusoma mtandaoni kuhusu itikadi za
kidini na za kijamii ili kujifunza zaidi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Stadi hizi zinadhihirika mwanafunzi
anapojifunza kuhusu itikadi
mbalimbali za kidini na za kijamii
kutokana na matini atakazosoma
mtandaoni. Ataweza kufahamu dini
mbalimbali na desturi mbalimbali
za kimaisha hivyo kujifanyia uamuzi
mwema wa mwelekeo wake maishani.
Pia, zinakuzwa mwanafunzi
anapozingatia usalama akiwa
mtandaoni.
Uraia
Wanafunzi wafanye shughuli za
ujifunzaji kwa ushirikiano katika
vikundi. Wakosoane na kukubaliana
2. Kusoma kwa
mapana
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 113-116)
Matini ya kidijitali
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua na kuzingatia hatua za
kiusalama katika matumizi ya vifaa
vya kidijitali.
b) Kutambua na kufungua faili iliyo na
kifungu cha kusoma ili kuimarisha
umilisi wake wa kutumia tarakilishi.
c) Kusakura kwenye tovuti salama ili
kupata vifungu vya kusoma.
d) Kutumia vyombo vya kidijitali kwa
urahisi kupata matini zinazolengwa.
e) Kuchangamkia matumizi ya vifaa
vya kidijitali katika kutafuta na
kusoma ujumbe ili kuimarisha
maarifa yake.
Maswali dadisi
1. Unapenda kusoma matini kuhusu
nini mtandaoni?
2. Je, unakumbuka habari gani
uliyoisoma mtandaoni?
3. Je, ni hatua gani za kiusalama
unazozingatia unapotafuta matini
mtandaoni?
4. Unajua maana ya itikadi za kidini
na za kijamii?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia vifaa vya kidijitali
161
Kimeidhinishwa na KICD
bila fujo ili kuonyesha uraia
mwema. Pia, wanafunzi wafahamu
itikadi mbalimbali za kidini na za
kijamii na kuzithamini hivyo kuleta
utangamano mwema.
Ushauri nasaha
Huu unakuzwa kutokana na mafunzo
yanayotokana na dini na desturi
mbalimbali za wanajamii.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kuvitunza vifaa vya kidijitali
atakavyotumia kutafutia matini salama
ya kusoma mtandaoni. Pia, anapoweza
kukamilisha kazi zake kwa wakati
unaofaa pamoja na kuzingatia itikadi
za kidini na za kijamii za dini yake na
jamii yake.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wanafunzi
wenzake katika shughuli za vikundi
na kuwasiliana nao kwa kutumia
lugha ya adabu. Pia, kwa kuonyesha
uthamini wa itikadi za kidini na za
kijamii za wenzake kutoka kwenye
dini na jamii mbalimbali nchini.
Umoja na amani
Mwanafunzi ashirikiane na wenzake
katika kufanya shughuli za vikundi kwa
amani bila kuzua fujo yoyote.
Uhusiano na masomo mengine
1. Somo la Dini
Somo hili linaangazia itikadi za dini
mbalimbali nchini.
2. Somo la Jamii
Somo hili linaangazia itikadi za kijamii
za jamii mbalimbali nchini.
Funzo hili linahusiana na masomo
yote kwa sababu yanazingatia ujuzi
wa kidijitali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake
nyumbani na shuleni kuhusu usalama
mitandaoni na manufaa ya ujuzi wa
kidijitali katika kuimarisha usomaji
na kupata maarifa yanayohusu nyanja
mbalimbali.
Mwanafunzi awahamasishe wanajamii
kuhusu kuthamini itikadi za kidini na
za kijamii za dini na jamii mbalimbali
nchini ili kuleta utangamano mwema.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye uwezo wa kung’amua
wanayojifunza kwa haraka na wepesi
baada ya kushirikishwa katika shughuli
za ujifunzaji wapewe fursa ya kutafuta
matini zaidi za kusoma mtandaoni ili
kuimarisha ujifunzaji wao.
Wanafunzi wanaochukua muda zaidi
kabla ya kufahamu wanayojifunza
washirikishwe katika shughuli zaidi
za kutumia vifaa vya kidijitali na
kusoma matini salama mtandaoni
kwa kutengewa muda zaidi wa
kujifunza baada ya masomo jioni.
Ili kufanikisha ujifunzaji wa kila
mwanafunzi, unaweza kumshirikisha
mfasiri wa lugha ishara ili
kuwasiliana na wanafunzi wasioweza
162
Kimeidhinishwa na KICD
kusikia na kuzungumza. Pia, unaweza
kuwasomea matini salama kuhusu
itikadi za kidini na za kijamii kutoka
mtandaoni ili waweze kujifunza.
Ili kuwahusisha wanafunzi wasioweza
kuona katika ujifunzaji, hakikisha
wana mashine za breli zilizo katika
hali nzuri ili waweze kutafuta matini
salama mtandaoni kuhusu itikadi za
kidini na za kijamii ili kujifunza.
Unaweza kuwashughulikia wanafunzi
wengine walio na matatizo mbalimbali
ya kiafya au kisaikolojia kadri ya uwezo
wako.
kijamii za dini na jamii mbalimbali ili
kufanikisha ujifunzaji wa wanafunzi
walio na matatizo ya kuona au
kuzungumza. Wanaweza kusikiliza
matini hizo na kujifunza.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
kuhusu somo hili ili ajiandae vilivyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
113
2. Vifaa vya kidijitali kama vile,
tarakilishi
3. Breli
4. Mfasiri wa lugha ishara
Utaratibu wa ufunzaji
Mwelekeze mwanafunzi katika
shughuli ya 1 ambapo atatambua
vifaa vya kidijitali kutoka kwa
michoro ya vifaa iliyo kitabuni
mwake na kuandika majina yavyo.
Majibu tarajiwa: b) rununu/simu
d) tarakilishi. Waeleze wanafunzi
kuwa daftari, kalamu na kibanizi/
kibanio si vifaa vya kidijitali.
Waongoze wanafunzi kujadiliana
kuhusu matumizi ya rununu/simu
na tarakilishi. Majibu tarajiwa:
tarakilishi hutumiwa kuandika
na kuhifadhi matini mbalimbali,
kusakura matini ya kusoma kwenye
mtandao, kuhifadhi data mbalimbali,
kutazama video muhimu za kujifunza
n.k. Rununu hutumiwa kuwasiliana,
kutuma na kupokea pesa, kupiga
picha, kuhifadhi data mbalimbali,
kutafuta matini ya kusoma, kusikiliza
redio n.k. Tathmini majibu ya
mwanafunzi.
2.1 Matini ya kidijitali
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 113-116)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Shughuli za ufunzaji na ujifunzaji
huimarishwa ikiwa mwalimu na
wanafunzi watakuwa wamejiandaa
ipasavyo kabla ya funzo kuanza.
Hakikisha kuwa nyenzo za ujifunzaji
kama vile tarakilishi na breli zipo na
hazina hitilafu. Pia,
Tafiti kuhusu itikadi mbalimbali za
kidini na za kijamii za dini na jamii
mbalimbali ili kufanikisha ufunzaji
wako darasani.
Andaa mada mbalimbali za matini
kuhusu itikadi za kidini na za kijamii
za dini na jamii mbalimbali ambazo
utawapa wanafunzi. Pia, watafute
matini hizo mtandaoni na kuzisoma
ili kujifunza.
Andaa kanda yenye maelezo kuhusu
itikadi mbalimbali za kidini na za
163
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha
uwaelekeze katika hatua za kutumia
tarakilishi. Waongoze kujadili hatua
za kiusalama (kama vile, kuzingatia
mada lengwa, kusalia kwenye tovuti
lengwa, kutofungua matangazo
yanayojitokeza kwenye kiwambo
n.k.) katika matumizi ya mtandao.
Watafute matini kuhusu itikadi za
dini wanayoifahamu na waisome
kisha wajadili kuhusu itikadi hizo.
Wawaeleze wenzao wa vikundi
vingine kuhusu itikadi za dini
waliyoisoma. Hakikisha wanafunzi
wanaheshimu dini mbalimbali
watakazojadili. Wanafunzi wafungue
faili kwenye tarakilishi kisha
wahifadhi matini waliyosoma.
Hakikisha wanazingatia hatua
zifaazo.
Katika shughuli ya 3, waelekeze
wanafunzi kujibu maswali yaliyo
kwenye jedwali lililo vitabuni mwao
kwa kutumia neno sahihi au kosa.
Majibu tarajiwa: 1. sahihi 2. kosa
3. kosa 4. kosa 5. sahihi 6. kosa 7. kosa
8. sahihi 9. kosa 10. sahihi. Waelekeze
wanafunzi katika kujadili majibu
yao kisha waandike hatua salama za
kufuata wanapotumia mtandao.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 4 ambapo atasoma
kimyakimya matini aliyopewa na
kuuelewa ujumbe uliomo kisha
kujibu maswali aliyopewa kitabuni
mwake. Majibu tarajiwa:
1. Dini humwunganisha Mungu na
binadamu (mwalimu akubali majibu
mengine baada ya kutathmini).
2. Kwa sababu ya imani kuwa Mungu
ni yule yule mmoja aliyewaumba
wanadamu wote.
3. Tathmini majibu ya mwanafunzi.
Mwanafunzi atumie kamusi ya
Kiswahili.
4. Wasipopata mwongozo, maelekezo na
msisitizo kutoka kwa wazazi, wazee
katika jamii, viongozi wa kidini na wa
serikali.
5. Kwa kutoa mwongozo, maelekezo na
masisitizo yanayofaa.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini iwapo mwanafunzi
alisoma mtandaoni matini kuihusu
dini yao kwa kutazama aliyoandika
daftarini mwake. Pia, mwanafunzi
aweze kueleza tofauti zilizopo kati ya
dini yao na dini nyingine anazojua.
Tathmini maelezo ya mwanafunzi na
uhakikishe unaiheshimu dini yake na
kuwa anaziheshimu dini nyingine.
Tathmini
1. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
amefahamu na kuzingatia hatua za
kiusalama katika matumizi ya vifaa
vya kidijitali akiwa mtandaoni.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kufungua faili iliyo na matini ya
kusoma ili kuimarisha umilisi wake
wa kutumia tarakilishi.
3. Tathmini uwezo wa mwanafunzi wa
kutafuta mtandaoni tovuti salama
ili kupata matini salama ya kusoma.
164
Kimeidhinishwa na KICD
wenzake mtandaoni ili waitathmini.
Pia, anaweza kutumia intaneti
kusakura matini mbalimbali za
masimulizi kuhusu itikadi za kidini
na za kijamii za dini na jamii
mbalimbali nchini na kuzisoma ili
kujifunza.
(c) Ubunifu
Ubunifu unajengeka mwanafunzi
anapoandika insha ya masimulizi
kuhusu itikadi za kidini na za
kijamii za dini na jamii mbalimbali
nchini kwa kubuni matukio yake
mwenyewe.
(d) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kubuni na kuandika
insha za masimulizi akirejelea
mada mbalimbali. Pia, mwanafunzi
anapoendelea kutumia vifaa vya
kidijitali kutafuta matini mbalimbali
salama za kusoma mtandaoni.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Unakuzwa wanafunzi kutoka maeneo
mbalimbali wanapofanya kazi kwa
kushirikiana katika vikundi licha ya
tofauti zao anuwai. Pia, mwanafunzi
anapothamini dini na desturi za
maisha za wanajamii mbalimbali
hivyo kuleta utangamano mwema
katika jamii.
Stadi za maisha
Kutokana na insha za masimulizi
kuhusu itikadi za kidini na za kijamii
za dini na jamii mbalimbali nchini,
mwanafunzi atapata ufahamu
wa dini na desturi mbalimbali za
3. Kuandika
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 116-118)
Insha ya masimulizi
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa
kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi kwa
kufuata kanuni zifaazo.
c) Kuchangamkia utunzi mzuri wa
insha ya masimulizi ili kukuza
ubunifu wake.
Maswali dadisi
1. Unajua maana ya insha ya
masimulizi?
2. Unazingatia nini unapoandika
insha ya masimulizi?
3. Unawezaje kupata hoja za kusimulia
katika insha ya masimulizi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa wanafunzi
wanapojadili muundo, mtindo na
mada mbalimbali za kuandikia insha
za masimulizi wakiwa katika vikundi.
Wanapoandika insha na kuwasomea
wenzao wanakuza uwezo wao wa
kuwasiliana.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu utakuzwa mwanafunzi
atakapoandika insha ya masimulizi
kwenye tarakilishi na kufungua
faili na kuihifadhi kisha kuwatumia
165
Kimeidhinishwa na KICD
jamii hivyo kufanya uamuzi wa
busara utakaomfaidi maishani. Pia,
mwanafunzi ataweza kuwafundisha
wanajamii kuhusu kuthamini dini
na desturi za maisha za wanajamii
mbalimbali.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake
katika vikundi kujadili insha za
masimulizi akitumia lugha ya adabu.
Pia, anapowapa wenzake fursa ya
kuchangia katika majadiliano yao
katika vikundi na kuyaheshimu
maoni yao.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa amani bila kuzua
ugomvi wowote.
Uaminifu na uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunga insha ya masimulizi inayohusu
itikadi za kidini na za kijamii akiwa peke
yake bila kunakili insha za wenzake.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanafundisha uandishi
wa insha kama mojawapo ya stadi za
lugha.
2. Somo la Dini
Somo hili linafundisha kuhusu itikadi
za kidini.
3. Somo la Jamii
Somo hili linafundisha kuhusu itikadi
za kijamii.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake
shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu
wa uandishi bora katika kuboresha
mawasiliano.
Mwanafunzi atawahamasisha
wenzake katika jamii kuhusu
kuthamini itikadi za dini mbalimbali
na desturi mbalimbali za maisha za
wanajamii.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa
kuona watambue maelezo kuhusu
muundo na mtindo wa kuandika
insha ya masimulizi kwa kutumia
breli. Pia, unaweza kuwasomea
wanafunzi hao maelezo hayo
wakayasikiliza na kuelewa hivyo
kujifunza.
Wanafunzi walio na changamoto
za viungo vya mwili kama vile
mikono wasaidiwe kuandika kwa
kutumia kiungo kingine cha mwili
walichozoea kutumia.
Mwalimu awe mwenye uvumilivu ili
aweze kuwasaidia wanafunzi ambao
wanachukua muda mrefu kujifunza
uandishi wa insha ili waweze
kujifunza bila kukata tamaa.
Wanafunzi wenye changamoto ya
kusikia au kuzungumza wasaidiwe
kujifunza kwa kumshirikisha mfasiri
wa lugha ishara (ikiwa mwalimu
haifahamu lugha ishara).
166
Kimeidhinishwa na KICD
3.1 Insha ya masimulizi
awali katika sura ya 2. Wanafunzi
waelezane maana ya insha ya
masimulizi. Tathmini maelezo yao.
Insha ya masimulizi huandikwa ili
kueleza matukio yanayotokea katika
maisha kwa kuzingatia muundo,
mtindo na lugha maalum ya
kinathari.
Wape wanafunzi nakala mbalimbali
za insha ulizoandaa mapema. Nakala
hizo za insha ziwe mchanganyiko
wa insha mbalimbali zikiwemo
za masimulizi. Shughuli hii ni ya
kuwawezesha wanafunzi kutambua
insha za masimulizi na kuweza
kuzitofautisha na insha nyingine
kwa usahihi. Waongoze wanafunzi
kutambua na kujadili sifa za insha
za masimulizi. Insha za masimulizi
huzingatia kusimulia matukio fulani,
lugha ya nathari, mada lengwa,
matumizi ya lugha fasaha na sahihi
n.k.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha wajadili
kuhusu ndoa za lazima katika jamii
mbalimbali (kama vile jamii za
Wamaasai, Waturkana, Wasamburu).
Ndoa za lazima zinahusu msichana
au mwanamke kulazimishwa kuolewa
kabla ya kufikisha umri wa kuolewa
au bila ya hiari yake. Wanafunzi
waandike vidokezo ambavyo kila
mwanafunzi atavitumia kubuni
insha ya masimulizi kwa maneno
yake mwenyewe. Kila mwanafunzi
awasomee wanafunzi wa kikundi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 116-118)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti zaidi kuhusu uandishi wa insha za
masimulizi zinazohusu itikadi za kidini na
za kijamii. Pia,
Unaweza kukusanya nakala za aina
mbalimbali za insha na uhakikishe
kuna insha za masimulizi kati ya
nakala hizo ili wanafunzi waweze
kuzitambua na kuzitofautisha.
Unaweza kupata nakala hizi kutoka
kwa wanafunzi wa gredi nyingine.
Hakikisha mashine za breli ziko
katika hali nzuri ya kuweza kutumiwa
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona ili kufanikisha ujifunzaji wao.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
kuhusu funzo hili ili ajiandae ifaavyo.
Unaweza kuandaa michoro au picha
mbalimbali ambazo wanafunzi
wanaweza kutumia kutolea
masimulizi kuhusu itikadi za kidini
na za kijamii.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 116
2. Nakala za insha mbalimbali
zikiwemo za masimulizi
3. Mfasiri wa lugha ishara, breli
4. Michoro na picha zinazoonyesha
itikadi mbalimbali za kidini na
kijamii
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa shughuli
ya 1 kwa kuwaelekeza wanafunzi
kujikumbusha kuhusu insha za
masimulizi walizojifunza hapo
167
Kimeidhinishwa na KICD
chake insha aliyobuni ili waitathmini
na kujifunza.
Waelekeze wanafunzi kutathmini insha
zao kwa kuzingatia majibu ya maswali
waliyopewa vitabuni mwao.
Waongoze wanafunzi kufanya
shughuli ya 3 kwa kujadili michoro
waliyopewa vitabuni mwao wakiwa
katika vikundi. Michoro ni ya ibada
inayofanyika nje chini ya mti pamoja
na sherehe ya kuzaliwa kwa mtoto.
Waelekeze wanafunzi kusimuliana
kuhusu sherehe zozote za harusi
za kitamaduni au ibada za kidini
ambazo wamewahi kuhudhuria.
Tathmini masimulizi yao. Hakikisha
wanasimulia kwa ufasaha, ujasiri na
kwa lugha sahihi.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini ikiwa mwanafunzi
alitunga insha ya masimulizi kuhusu
harusi aliyowahi kuhudhuria.
Hakikisha insha hiyo haijapungua
maneno 150. Hakikisha kuwa
mwanafunzi ameituma insha hiyo
kwako na kwa wanafunzi wengine
kwa kutumia mtandao.
Tathmini
1. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kutambua insha ya
masimulizi kwa kuzingatia
ujumbe, mtindo na muundo katika
matini mbalimbali.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutunga insha za masimulizi
kwa kufuata kanuni zifaazo.
4. Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 118-122)
Nyakati na hali (Vipindi 3)
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vya hali ya
mazoea na hali timilifu kwenye
vitenzi.
b) Kutambua vitenzi katika hali ya
mazoea na hali timilifu kwenye
matini.
c) Kutumia vitenzi vya hali ya
mazoea na timilifu katika sentensi
ili kuimarisha mawasiliano.
d) Kufurahia matumizi ya hali
ya mazoea na timilifu katika
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, wewe hufanya shughuli gani
kila siku?
2. Unajua nyakati gani katika
Kiswahili?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi wataweza kuwasiliana
na kushirikiana kufanya shughuli
za kutambua hali ya mazoea na hali
timilifu katika vitenzi, sentensi na
matini wakiwa katika vikundi.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa wanafunzi
wanapotumia vifaa vya kiteknolojia
168
Kimeidhinishwa na KICD
kama vile tarakilishi kuandika
kifungu na kukoleza rangi vitenzi
vilivyo katika hali ya mazoea na hali
timilifu katika kifungu hicho.
(c) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoendelea kutunga sentensi na
vifungu kwa usahihi katika hali ya
mazoea na hali timilifu.
(d) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapotunga
sentensi katika hali ya mazoea na hali
timilifu.
Unajengeka mwanafunzi anapoweza
kutunga sentensi sahihi na hata vifungu
vyake mwenyewe katika hali ya mazoea
na hali timilifu bila kunakili kazi za
wenzake.
(e) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
changamoto
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutunga sentensi kuhusu
masuala mbalimbali hasa mtambuko
katika hali ya mazoea na hali
timilifu. Uwazaji wa kina unajitokeza
mwanafunzi anapofikiri kuhusu
vitenzi atakavyotumia kutunga
kifungu.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano
Utangamano unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kutoka maeneo mbalimbali
kutunga sentensi na vifungu kwa usahihi
katika hali ya mazoea na hali timilifu.
Stadi za maisha
Zinakuwa mwanafunzi anapoweza
kuwasiliana kwa usahihi katika hali
ya mazoea na hali timilifu hivyo
kuyaboresha mawasiliano yake.
Masuala mbalimbali kama vile:
lishe bora, utunzaji wa mazingira,
usalama, afya bora, utunzaji wa
wanyama n.k yatashughulikiwa
mwanafunzi anapotunga sentensi na
vifungu katika hali ya mazoea na hali
timilifu akirejelea masuala mtambuko
mbalimbali.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kujadili hali timilifu na hali
ya mazoea na kuyaheshimu maoni
ya wenzake. Pia, anapowapa wenzake
fursa ya kuchangia katika majadiliano
yao.
Amani na umoja
Maadili haya yatalengwa katika sentensi
zitakazotungwa na wanafunzi katika
hali timilifu na hali ya mazoea. Pia,
kupitia kwa wanafunzi kutangamana
kwa amani katika vikundi bila kuzua
ugomvi wowote.
Uwajibikaji
Unadhihirika mwanafunzi
anapovitunza vifaa vyake vya
ujifunzaji na kukamilisha kazi zake
kwa wakati ufaao. Pia, anapotekeleza
majukumu yake anaposhirikiana na
wenzake katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanaangazia mada
kuhusu hali timilifu na hali ya
mazoea.
169
Kimeidhinishwa na KICD
Masomo mengine yote hutumia hali
timilifu na hali ya mazoea katika
matini zake.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakapotumia kwa usahihi
sentensi zilizo katika hali timilifu na hali
ya mazoea katika mawasiliano ataboresha
lugha katika jamii.
Namna ya kuwashughulikia
wanafunzi wenye mahitaji maalum
Rekodi video yenye mifano ya
mambo ambayo wanafunzi hufanya
kila siku ili kuwasaidia wanafunzi
wenye changamoto ya kusikia au
kuzungumza ili wajifunze. Pia,
mfasiri wa lugha ishara anaweza
kuhusishwa.
Hakikisha kuna mashine za breli
ili wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona wazitumie kujifunza. Pia,
wanafunzi hawa wanaweza kutolewa
maelezo kuhusu hali timilifu na
hali ya mazoea na wakayasikiliza na
kujifunza.
Jiandae kuwasaidia wanafunzi wengine
walio na matatizo mbalimbali kadri ya
uwezo wako.
Unaweza kuandaa chati zilizoandikwa
vitenzi na sentensi katika hali timilifu
na hali ya mazoea.
wako darasani. Vilevile,
Unaweza kuandaa chati ambazo
zimeandikwa vitenzi na sentensi
zilizo katika hali timilifu na hali
ya mazoea ili kufanikisha ufunzaji
wa wanafunzi darasani.
Rekodi kanda yenye picha na
maelezo kuhusu mambo ambayo
wanafunzi hufanya kila siku
kama vile kupiga mswaki, kuoga,
kutandika kitanda, kusali n.k.
Hakikisha breli ziko katika hali
nzuri ya kutumika na wanafunzi
wasio na uwezo wa kuona ili
kuwasaidia katika ujifunzaji wao.
Unaweza kumfahamisha mapema
mfasiri wa lugha ishara ili aweze
kujiandaa ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
118, mashine za breli
2. Chati zilizoandikwa vitenzi na
sentensi katika hali ya mazoea na
hali timilifu.
3. Kanda iliyorekodiwa
inayoonyesha au kueleza mambo
ambayo wanafunzi hufanya kila
siku.
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kuwaelekeza
wanafunzi kufanya shughuli ya 1.
Wajibu maswali waliyopewa vitabuni
mwao. Waelekeze wanafunzi kugundua
kuwa mambo wanayofanya kila siku
yako katika hali ya mazoea. Kiambishi
hu- hutumika katika vitenzi kuonyesha
hali hii. Hali ya mazoea huonyesha
kitendo kilichozoeleka kutendeka au
4.1 Hali ya mazoea
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 118-120)
Maandalizi ya mwalimu
Fanya utafiti kuhusu nyakati na hali kwa
kujikita katika hali ya mazoea na hali
timilifu ili kuweza kufanikisha ufunzaji
170
Kimeidhinishwa na KICD
kinachotendeka kila mara. Tathmini
majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kwa
kuzingatia idadi na uwezo wao.
Wanafunzi wasome vitenzi vilivyo
katika jedwali lililo vitabuni mwao
na watambue viambishi vya vitenzi
vilivyo katika hali ya mazoea. Majibu
tarajiwa: husoma, huimba, hucheka.
Katika shughuli ya 3, tathmini ikiwa
mwanafunzi ametambua vitenzi
vya hali ya mazoea katika sentensi
zilizoko kitabuni mwake kwa
kuvipigia mistari. Majibu tarajiwa:
hucheza, husoma, hunisaidia, hula,
huenda, huwatibu. Waelekeze
wabadilishane madaftari ili
watathmini sentensi zao.
Mwelekeze mwanafunzi kusoma
kifungu kilicho katika shughuli ya
4 kitabuni mwake. Tathmini iwapo
mwanafunzi anatambua vitenzi
vya hali ya mazoea katika kifungu
alichosoma kwa kuvipigia mistari.
Majibu tarajiwa: huamka, husali,
huoga, huniandalia, huwa amelala,
hunywa, huenda. Tathmini majibu ya
mwanafunzi.
Mshirikishe mwanafunzi katika
kufanya kazi ya ziada iliyo kitabuni
mwake. Tathmini majibu ya
mwanafunzi. Majibu tarajiwa:
1. Watoto hucheza kila siku uwanjani.
2. Mimi huomba kila siku.
3. Wanafunzi hufika shuleni kila siku
asubuhi.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 120-122)
Utaratibu wa ujifunzaji
Unaweza kutanguliza somo hili kwa
kuwashirikisha wanafunzi kusoma na
kujadili maana za sentensi walizopewa
vitabuni mwao katika shughuli ya 1.
Waelekeze kugundua kuwa sentensi
hizo ziko katika hali timilifu. Kiambishi
–me hutumika katika vitenzi kuonyesha
hali hii. Hali timilifu huonyesha kuwa
kitendo kimetendeka muda mfupi
uliopita. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya 2, wanafunzi
wakiwa katika vikundi wasome vitenzi
vilivyo katika jedwali lililo vitabuni
mwao na watambue viambishi vya
vitenzi vilivyo katika hali timilifu.
Majibu tarajiwa: nimelala, nimepika,
ameomba.
Mshirikishe mwanafunzi kusoma
kifungu kilicho katika shughuli ya
3 kitabuni mwake. Tathmini iwapo
mwanafunzi anaweza kutambua
vitenzi vya hali timilifu katika kifungu
hicho kwa kuvipigia mistari. Majibu
tarajiwa: ameingia, wameketi,
wametulia, wamekula, wameshiba,
wamesubiri. Tathmini majibu ya
wanafunzi.
Hitimisha kipindi hiki kwa kumpa
mwanfunzi kazi ya ziada iliyo
kitabuni mwake. Tathmini majibu ya
mwanafunzi. Majibu tarajiwa:
4.2 Hali timilifu
4. Mgonjwa humeza dawa asubuhi
na jioni.
5. Wewe hula chakula gani kila jioni?
171
Kimeidhinishwa na KICD
1. a) Mtoto amenyonya maziwa.
b) Wazazi wamewasaidia watoto wao.
c) Wewe umesoma Kurani Tukufu
vizuri sana.
d) Mama amenipa chakula kitamu.
e) Sisi tumecheza uwanjani.
2. a) Wakulima huvuna mahindi mengi.
b) Mazingira hutunzwa vizuri sana.
c) Maharusi huanza safari alfajiri.
d) Wewe hula ugali wangu.
e) Dada hunifulia nguo zangu.
Katika swali la 3, tathmini kifungu
ambacho mwanafunzi atabuni.
Hakikisha anatumia vitenzi vilivyo
katika hali timilifu na hali ya mazoea.
Pia, hakikisha sentensi za kifungu
hicho ni sahihi kisarufi. Mwanafunzi
awatumie wanafunzi wenzake pamoja
nawe kifungu hicho mtandaoni ili
mkitathmini.
Shughuli ya nje ya darasa
Waongoze wanafunzi kutengeneza
orodha ya sheria ambazo mwanafunzi
anastahili kufuata kila mara anapoingia
mtandaoni kutafuta matini ya kusoma.
Waelekeze wanafunzi wazijadili sheria
hizo, wakubaliane nazo, wazihariri kisha
waziweke mtandaoni ili zitumike na
mwanafunzi yeyote anayetaka kuingia
mtandaoni kutafuta matini ya kusoma.
Shughuli hii itawahamasisha wanafunzi
wote kuzingatia usalama wakiwa
mtandaoni. Pia, itakuza ujuzi wao wa
kidijitali.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. a) Maria ni mwoga kama kunguru.
b) Kasisi huyu ni mpole kama njiwa.
c) Mbwa wetu ana hasira kama za
mkizi.
2. Tathmini majibu ya mwanafunzi
kulingana na kitabu tukufu ambacho
kinatumika katika dini yao. Hakikisha
mwanafunzi alijadiliana na mlezi
wake kuhusu ujumbe wa mistari
michache kutoka kwenye kitabu chao
tukufu.
3. Tathmini insha ya masimulizi
ambayo mwanafunzi ataandika
kuhusu sherehe yoyote ya kitamaduni
aliyowahi kuhudhuria. Hakikisha
inazingatia mtindo, muundo na
kanuni za kisarufi zifaazo.
4. Tathmini sentensi za mwanafunzi.
Hakikisha ziko katika hali ya mazoea
kisha kubadilishwa na kuwa katika
hali timilifu. Ziwe sahihi kisarufi.
Tathmini
1. Tathmini ikiwa kila mwanafunzi
anaweza kutambua viambishi vya
hali ya mazoea na hali timilifu
katika vitenzi na sentensi.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua hali ya mazoea na
hali timilifu katika vifungu au
matini.
3. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia vitenzi katika hali ya
mazoea na hali timilifu kutunga
sentensi na vifungu sahihi kisarufi.
172
Kimeidhinishwa na KICD
UWEKEZAJI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 123-135)
Utangulizi
Uwekezaji ni hali ya kutumia rasilimali
kama vile pesa katika miradi au biashara
ili kupata faida. Hii ni njia mojawapo ya
mtu kuweza kujipatia riziki ya kila siku.
Kutokana na uwekezaji, mtu anaweza
kuibukia kuwa tajiri sana katika jamii. Watu
huwekeza katika miradi tofautitofauti k.v.:
ujenzi wa majumba ya kupangisha, ufugaji,
ukulima, usafiri wa umma, kufungua
maduka makubwa na madogo, hoteli,
masuala ya utalii, hospitali, masoko pamoja
na kuanzisha biashara mbalimbali zilizo na
faida. Mara nyingine miradi hii au biashara
hizi zinaweza kuleta hasara kwa mwekezaji.
Mtaji wa kutumia katika uwekezaji huweza
kutokana na pesa ambazo mtu ameweka
akiba au mikopo kutoka kwa mashirika
mbalimbali ya utoaji mikopo kama vile
mabenki. Kila mtu anahitaji kuwa na
njia ya kuziwekeza pesa zake ili tuweze
kujitegemea maishani.
Suala lengwa hili litashughulikia mada
zifuatazo: Kusikiliza na kuzungumza
(Kutoa masimulizi), Kusoma kwa
ufahamu (Kifungu cha hadithi), Kuandika
insha ya baruapepe na Sarufi (Ukanushaji
wa maneno na sentensi Viambishi
vya nafsi na wakati katika sentensi,
ukubwa na udogo wa nomino nomino
zinazoanza kwa herufi m- na n-).
Kusikiliza na
Kuzungumza
1.
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 123-125)
Kutoa masimulizi
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kusimulia tungo mbele ya
wenzake kwa kuzingatia mada,
ubunifu na usanifu wa lugha.
b) Kutumia ishara zifaazo kuimarisha
masimulizi yake.
c) Kuchangamkia masimulizi katika
mazingira mbalimbali.
Maswali dadisi
1. Je, masimulizi ni nini?
2. Wewe huzingatia nini unapotoa
masimulizi?
3. Je, unapenda kusikiliza masimulizi
kutoka kwa nani? Kwa nini?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
173
Kimeidhinishwa na KICD
vikundi kujadiliana, kubuni na kutoa
masimulizi kuhusu njia mbalimbali
za kuhifadhi na kuwekeza pesa.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu utakuzwa katika kazi ya
ziada ambapo mwanafunzi akisaidiwa
na mlezi wake atasakura mtandaoni
kuhusu watu mashuhuri waliowekeza
nchini na kujifunza kutokana na
jinsi walivyowekeza. Katika shughuli
hii, mwanafunzi atapata ujuzi wa
kutumia vifaa vya kidijitali.
(c) Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kusimulia visa kuhusu uwekezaji
mbalimbali mbele ya wenzake bila
woga.
(d) Ubunifu
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi
anapotunga visa mbalimbali kuhusu
uwekezaji kwa maneno yake
mwenyewe bila kunakili visa vya
wenzake na kuvisimulia kwa ustadi.
(e) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Unakuzwa mwanafunzi anapofikiria
kuhusu namna ya kuweka pesa akiba
na njia ya kuwekeza pesa hizo ili
kuweza kujitegemea maishani na
kuihamasisha jamii.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya fedha
Kutokana na mada hii, mwanafunzi
atapata ujuzi wa matumizi mema ya
fedha anaposimulia visa mbalimbali
kuhusu uwekezaji. Pia, atapata ujuzi
wa njia mbalimbali za kuweka pesa
zake akiba kidogo kidogo na jinsi ya
kuziwekeza.
Uraia
Huu utakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kusimuliana kuhusu njia za kuweka
pesa akiba na uwekezaji mbalimbali.
Ajira kwa vijana na usalama
Kutokana na mada hii, vijana
watapata maarifa kuhusu uwekaji
pesa akiba na njia mbalimbali za
uwekezaji hivyo kuweza kuanzisha
miradi au biashara mbalimbali za
kuwawezesha kujitegemea maishani.
Vijana wakipata riziki, uhalifu
utapungua hivyo kuwepo kwa
usalama nchini.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kuweka pesa akiba kidogo
kidogo kwa ajili ya mradi wa baadaye.
Pia, anapokamilisha kazi zake kwa
wakati unaofaa.
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapotangamana na wenzake katika
vikundi kwa amani bila kuzua ugomvi
wakisimuliana kuhusu uwekezaji.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya
wenzake katika majadiliano kuhusu
uwekezaji wakiwa kwenye vikundi.
174
Kimeidhinishwa na KICD
Pia, anapowapa wenzake fursa ya
kuchangia katika majadiliano yao
kwenye vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza
Somo hili linafundisha ufasaha wa
kusema au kusimulia kwa ubunifu
katika miktadha mbalimbali.
2. Somo la Jamii
Somo hili hufundisha uwekezaji.
Masomo mengine pia kwa kiwango
fulani yanamhitaji mwanafunzi
kusema kwa ufasaha hata anapojibu
maswali kwa kujieleza.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapoweza kuyatoa
masimulizi kwa ufasaha
ataihamasisha jamii kutumia lugha
kwa ufasaha hivyo kuboresha
mawasiliano yao.
Mwanafunzi ataihamasisha jamii
kuhusu umuhimu wa kuweka pesa
akiba na kuwekeza ili kujitegemea
maishani na kuukuza uchumi wa
nchi.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye uwezo wa
kung’amua wanayojifunza mara
moja baada ya kushirikishwa
katika shughuli za ujifunzaji
wapewe fursa ya kubuni
masimulizi zaidi kuhusu njia
mbalimbali za uwekezaji. Pia,
wanaweza kuwasaidia wenzao
wanaochukua muda zaidi kuelewa
wanayofundishwa.
Wanafunzi hawa wanaweza
kutengewa muda zaidi wa
kujifunza baada ya masomo jioni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kuzungumza au kusikia wanaweza
kusaidiwa na mfasiri wa lugha
ishara ili kuweza kujifunza kama
wenzao.
Wanafunzi ambao hawana uwezo
wa kuona watumie mashine za
breli au kusikiliza masimulizi
kuhusu uwekezaji yakitolewa na
mwalimu, wanafunzi wenzao
au kutoka kwenye kanda
iliyorekodiwa.
Wanafunzi wenye matatizo ya
viungo vya mwili washirikishwe
katika shughuli za ujifunzaji
kwa kupewa majukumu ambayo
hayatawatia katika hatari ya
kuumia hasa wakiwa katika
vikundi.
1.1 Kutoa masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 123-125)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Shughuli zote za ufunzaji na ujifunzaji
huimarishwa ikiwa mwalimu na
wanafunzi watakuwa wamejiandaa
ipasavyo kabla ya kipindi kuanza.
Hakikisha kila mwanafunzi ana vifaa
muhimu kama vile daftari na kalamu
kabla ya kipindi kuanza. Pia,
Fanya utafiti kuhusu njia mbalimbali
za kuweka pesa akiba na uwekezaji ili
kufanikisha ufunzaji wako darasani.
Andaa masimulizi mbalimbali
yanayohusu uwekezaji ambayo
175
Kimeidhinishwa na KICD
yatakusaidia katika ufunzaji wako
na uelewa wa wanafunzi wa mada
husika.
Hakikisha mashine za breli zipo na
ziko katika hali nzuri ya kutumiwa na
wanafunzi wasioweza kuona.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
kuhusiana na funzo hili ili ajiandae
ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
123
2. Picha au michoro ya miradi
mbalimbali kama vile: maduka,
majengo ya kifahari, vyumba/
nyumba za kupangisha, shamba la
mimea, mifugo n.k.
3. Mfasiri wa lugha ishara, breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi hiki kwa kuwapanga
wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi na uwezo wao kisha uwaongoze
kufanya shughuli ya 1. Wanafunzi
wajadili mchoro ulio vitabuni mwao.
Wanafunzi waeleze ishara za mwili
anazotumia babu katika masimulizi
yake. Majibu tarajiwa:
Babu anawasimulia wajukuu wake
kuhusu jinsi alivyowekeza kwa kufungua
dukakuu lenye bidhaa nyingi.
Hatimaye, wanafunzi wajadiliane
iwapo wamewahi kusimuliwa kuhusu
uwekaji akiba na waliyojifundisha.
Tathmini maelezo yao.
Katika shughuli ya 2, wanafunzi
wakiwa katika vikundi wajadili njia
mbalimbali za kuweka pesa akiba
na kuwekeza. Majibu tarajiwa:
Njia mbalimbali za kuweka pesa
akiba: kwenye benki, kwenye vyama/
mashirika, kwenye akaunti za
simu, akiba za nyumbani n.k. Njia
mbalimbali za kuwekeza ni kama vile:
kujenga hoteli, maduka, nyumba za
kupangisha, kuuza bidhaa sokoni,
kutoa huduma muhimu, usafiri,
kilimo, ufugaji, kununua hisa n.k.
Waelekeze wanafunzi kusimuliana
kuhusu mtu yeyote wanayemfahamu
ambaye aliweka pesa akiba na
kuziwekeza baadaye. Hakikisha kuwa
wanafunzi wanafahamu jinsi ya
kutumia ishara za viungo vya mwili
kutoa masimulizi kuhusu uwekezaji
kama vile: ishara za mikono, ishara za
nyuso, miondoko ya mwili n.k.
Katika shughuli ya 3, waongoze
wanafunzi katika kubuni masimulizi
yanayohusu uwekezaji kwa kutazama
michoro iliyo vitabuni mwao.
Hakikisha kuwa kisa kinahusu
msichana aliyehifadhi pesa mkebeni
nyumbani ambazo alitumia kununua
kuku/vifaranga wachache ambao
baadaye walikuwa wengi. Kuku
wakaanza kutaga mayai ambayo
waliyauza. Usimulizi huu uzingatie
lugha fasaha na ishara za mwili
zinazofaa.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini ikiwa mwanafunzi
amefahamu umuhimu wa uwekezaji
na njia mbalimbali za kuwekeza kwa
kutathmini maelezo yake kuhusu
wawekezaji wawili mashuhuri.
176
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kusimulia tungo mbele ya
wenzake kwa kuzingatia mada ya
uwekezaji, ubunifu na usanifu wa
lugha.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia ishara zifaazo
kuimarisha masimulizi yake.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi wanaposoma
kifungu na kujadiliana.
(b) Kufikiria kwa kina na kutatua
changamoto
Kunakuzwa mwanafunzi anapofikiria
kuhusu majibu sahihi ya maswali ya
kifungu alichosoma. Pia, mwanafunzi
anapofikiria kuhusu njia mbalimbali za
kuweka pesa akiba na kuwekeza.
(c) Ubunifu
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kubuni masimulizi kuhusu uwekezaji
na kuwasimulia wenzake. Pia,
anapobuni njia ya kuweka pesa zake
akiba kwa urahisi na iliyo salama na
jinsi ya kuziwekeza hapo baadaye.
(d) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutafuta mtandaoni
maelezo kuhusu watu wanaofanya
biashara mbalimbali kama vile: kuuza
samaki, usafiri wa barabarani na
kuuza vitabu. Kutokana na shughuli
hii, ataweza kupata ujuzi wa kutumia
vifaa vya kidijitali.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu kwa maendeleo endelevu
Inakuzwa mwanafunzi anapojifunza
kuhusu elimu ya fedha hususan
uwekezaji ambayo itamfaidi siku zote
maishani.
2. Kusoma
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 125-127)
Kusoma kwa ufahamu
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa mada
lengwa uliotumika katika kifungu.
b) Kueleza maana za msamiati lengwa
uliotumika katika kifungu.
c) Kutumia msamiati ulio katika
kifungu kwa usahihi katika
sentensi.
d) Kusoma kifungu kwa ufasaha ili
kupata ujumbe.
e) Kuonyesha uelewa wa kifungu kwa
kutoa muhtasari na kujibu maswali.
f) Kuchangamkia usomaji wa kifungu
ili kujenga maarifa ya ufahamu.
Maswali dadisi
1. Je, ni mambo gani hukuvutia
unaposoma kifungu cha hadithi?
2. Wewe hujua vipi maana ya msamiati
uliotumiwa katika kifungu?
3. Unapenda kusoma vifungu gani
vya hadithi?
177
Kimeidhinishwa na KICD
2. Somo la Jamii
Somo hili linafundisha mada kuhusu
uwekezaji.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anatarajiwa
kuwahamasisha wenzake katika jamii
kuhusu kusoma kwa ufasaha hivyo
kuyaboresha mawasiliano yao.
Mwanafunzi ataweza kuwahamasisha
wanajamii kuhusu umuhimu
wa uwekezaji ili kuwawezesha
kujitegemea.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Tumia nyenzo mbalimbali ili
kukidhi mahitaji ya kila mwanafunzi
kulingana na aina ya changamoto
zinazomkumba. Wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona wanaweza kutumia
breli kusoma vifungu kuhusu
uwekezaji na kujifunza.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia na kuzungumza watazame
kifungu kwenye vitabu vyao na
kukisoma kimoyomoyo kisha watoe
maelezo kwa maandishi kuhusiana na
maswali yaliyopo. Mfasiri wa lugha
ishara anaweza kushirikishwa.
Wanafunzi wasioweza kungamua
wanayojifunza kwa upesi wapewe
mazoezi zaidi. Unaweza kuwatumia
wanafunzi wanaoweza kujifunza
kwa upesi kuwasaidia wenzao
wanaong’amua mambo polepole
kusoma vifungu, kujibu maswali na
kufafanua msamiati lengwa.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapopata
maarifa ya kujitegemea anapoweza
kuweka pesa zake akiba, kuandaa
bajeti na kuwekeza vyema.
Uraia
Huu unakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake wa
asili mbalimbali katika vikundi
kujadiliana kuhusu uwekezaji.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji
Huu unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuweka pesa zake akiba na kuwekeza
hapo baadaye. Pia, anapokamilisha kazi
zake kwa wakati unaofaa.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi wanapojadiliana
kuhusu uwekezaji. Pia, anapotumia
lugha ya heshima kuwasiliana na
wenzake katika vikundi na kuwapa
fursa ya kuchangia katika majadiliano
yao.
Kujiamini na kujithamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuweka akiba pesa zake na kuziwekeza
hapo baadaye. Pia, anapoweza kubuni
masimulizi na kuwasimulia wenzake
kwa ujasiri nao wakajifunza.
Uhusiano na masomo mengine
1. Kiingereza
Somo hili linafundisha mada ya
kusoma vifungu vya hadithi na kutoa
masimulizi.
178
Kimeidhinishwa na KICD
Washughulikie wanafunzi
walio na matatizo ya kiafya au
kisaikolojia kadri ya uwezo wako.
kifungu hicho ambao mwanafunzi
atamtolea mwenzake darasani. Kifungu
kinahusu uwekezaji. Tathmini lugha
yao kwa kuhakikisha ni fasaha na
sahihi.
Waongoze wanafunzi kujadili
maana za maneno yaliyokolezwa
rangi kwenye kifungu walichosoma.
Wanaweza kutumia kamusi ya
Kiswahili. Baadaye, wayatungie
sentensi maneno hayo. Tathmini
sentensi za wanafunzi ili kuhakikisha
ni sahihi.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na uwezo wao kisha
uwaelekeze kujadili maswali
waliyopewa vitabuni mwao kuhusu
ushauri nasaha ambao wangetoa.
Mifano ya majibu tarajiwa: Ratemo
aweke akiba ya asilimia fulani ya
mshahara wake kwa kipindi fulani ili
apate mtaji wa kuanzisha biashara ya
kuuza viatu. Milka anaweza kupanda
pikipiki au gari kwa umbali unaoweza
kugharimu kiasi kidogo cha pesa kama
shilingi thelathini na kuweka akiba ya
shilingi ishirini. Tathmini majibu ya
wanafunzi na kutoa ushauri nasaha.
Waelekeze wanafunzi kufanya
shughuli ya 3 ambapo watajadiliana
kuhusu watu wanaofanya biashara
mbalimbali kama vile kuuza samaki,
usafiri wa barabarani, kuuza vitabu
n.k. Wanafunzi wasome kuhusu
biashara hizi kutoka mtandaoni
au kutoka kwa watu wa familia
zao au watu wengine wanaowajua
2.1 Kifungu cha hadithi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 125-127)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti kwenye magazeti, majarida, vitabu
na mtandaoni kuhusu uwekezaji, msamiati
wake, umuhimu wake, changamoto zake
pamoja na maelezo kuhusu njia mbalimbali
za kuwekeza. Utafiti huu utakusaidia katika
kufanikisha ufunzaji wako darasani. Pia:
Andaa vifungu mbalimbali vya
hadithi vinavyohusu uwekezaji
ambavyo unaweza kuwapa
wanafunzi wakavisoma darasani
ili kujifunza.
Hakikisha mashine za breli zipo ili
zitumiwe na wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona.
Unaweza kumfahamisha mfasiri
wa lugha ishara kuhusu funzo hili
ili aweze kujiandaa ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
125
2. Vifungu vinavyohusu uwekezaji
3. Kamusi ya Kiswahili
4. Mfasiri wa lugha ishara, breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo hili kwa kumwelekeza
mwanafunzi kusoma kifungu cha
hadithi kilicho kitabuni mwake katika
shughuli ya 1. Mwanafunzi asome
kifungu hicho kimyakimya na kuelewa
ujumbe wake. Tathmini muhtasari wa
179
Kimeidhinishwa na KICD
wanaofanya biashara hizi. Tathmini
maelezo ya wanafunzi.
Himiza mwanafunzi afanye kazi ya
ziada akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini iwapo mwanafunzi
amefahamu kuhusu uwekaji akiba na
kuwekeza.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kuandika na
kutuma baruapepe kwa wenzao na kwa
mwalimu.
(b) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotumia vifaa vya kidijitali
kuandika na kutuma baruapepe kwa
wenzake na mwalimu.
(c) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi anapobuni
ujumbe wa baruapepe na kuuandika
kisha kuutuma kwa kutumia vifaa vya
kidijitali.
(d) Hamu ya ujifunzaji
Hamu hii inakuzwa mwanafunzi
anapoyatafakari maswali dadisi na
anapoendelea kujifunza kuandika na
kutuma baruapepe.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapoweza
kuandika na kutuma baruapepe ili
kuboresha mawasiliano yake shuleni
na nje ya shule.
Elimu kwa maendeleo endelevu
Hii inakuzwa mwanafunzi anapotumia
teknolojia kuwasiliana kwa kutumia
baruapepe.
Uraia
Unakuzwa kutokana na mwanafunzi
kushirikiana vyema na wenzake
wa asili mbalimbali katika vikundi
Tathmini
1. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kusoma kifungu kwa
ufasaha na kufafanua msamiati wa
mada lengwa.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutumia msamiati wa uwekezaji
ipasavyo katika kutunga sentensi,
vifungu na masimulizi ili kukuza
msamiati wake.
3. Kuandika insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 127-129)
Baruapepe
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua baruapepe kwa
kuzingatia muundo wake.
b) Kuandika baruapepe kwa
kuzingatia ujumbe, muundo na
mtindo.
c) Kuchangamkia uandishi wa
baruapepe katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Baruapepe ni nini?
2. Wewe huzingatia vipengele gani
unapoandika baruapepe?
3. Baruapepe hutumwa vipi?
180
Kimeidhinishwa na KICD
wanapojifunza kuhusu uandishi wa
baruapepe.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa heshima na adabu
hata kwa kutumia lugha ya adabu
kuwasiliana. Pia, anapoyaheshimu
maoni ya wenzake katika kikundi na
kuwapa fursa ya kuchangia katika
majadiliano yao.
Upendo
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutuma baruapepe kwa wazazi au
marafiki zake ili kuwajulia hali.
Uwajibikaji
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kuvitunza vifaa vya
kidijitali kama vile tarakilishi
anavyotumia katika uandishi
na utumaji wa baruapepe. Pia,
anapokamilisha kazi zake kwa wakati
ufaao.
Uhusiano na masomo mengine
Masomo yote yanashughulikia ujuzi wa
kidijitali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapofahamu jinsi
ya kutumia vifaa vya kidijitali
kuwaandikia wazazi na marafiki
zake baruapepe pamoja na kupokea
baruapepe kutoka kwao.
Mwanafunzi anapowashirikisha
wenzake shuleni na nje ya shule
katika uandishi, utumaji na upokeaji
wa baruapepe.
Jinsi ya kuwashughulikia wanafunzi
wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wenye uwezo wa
kung’amua wanayojifunza kwa
upesi baada ya kushirikishwa katika
shughuli za ujifunzaji wapewe fursa
ya kuandika baruapepe zaidi katika
mada husika.
Wanafunzi wanaochukua muda
zaidi kuelewa wanayojifunza
washirikishwe katika shughuli zaidi
kuhusu uandishi wa baruapepe na
kutengewa muda zaidi wa kujifunza
baada ya masomo jioni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
watumie mashine za breli kujifunza
uandishi wa baruapepe. Pia,
wanaweza kusikiliza maelezo kuhusu
uandishi wa baruapepe kutoka kwa
mwalimu au wanafunzi wenzao.
Wanafunzi wenye changamoto ya
kusikia au kuzungumza watambue
baruapepe katika matini ambazo
mwalimu atawapa.Unaweza
kumshirikisha mfasiri wa lugha
ishara darasani ili kuwasaidia
wanafunzi hao.
Wanafunzi wenye changamoto ya
kuandika polepole waongezwe muda
wa kuandika ili waweze kujieleza
zaidi. Baadaye, mwalimu awape
wanafunzi hao mafunzo ya ziada
yanayohusu kuandika maneno kwa
kasi ili waweze kuandika insha kwa
muda unaofaa.
181
Kimeidhinishwa na KICD
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza funzo hili kwa
kuwashirikisha wanafunzi katika
majadiliano ya shughuli ya 1 wakiwa
katika vikundi. Wajikumbushe
kuhusu insha za baruapepe
walizowahi kujifunza katika mada
ya hapo awali. Tathmini majadiliano
ya wanafunzi. Waelekeze kujadili
sifa za insha za baruapepe, kwa
mfano: anwani ya baruapepe ya
mwandishi, anwani ya baruapepe ya
anayetumiwa, mada, mwili/ujumbe
na hitimisho.
Katika shughuli ya 2, wape
wanafunzi nakala mbalimbali za
insha za baruapepe ulizoandaa
mapema kutoka mtandaoni kisha
uwaelekeze kuzisoma na kuchunguza
iwapo zina sifa walizojadili katika
shughuli ya 1. Waongoze kujadili
ujumbe na muundo wa insha za
baruapepe ulizowapa. Pia, wajadili
tofauti zilizopo kati ya insha za
baruapepe na insha nyingine
wanazofahamu.
Waongoze wanafunzi kufanya
shughuli ya 3 ya kuandika insha
za baruapepe hatua kwa hatua.
Washirikishe katika hatua za
matumizi ya tarikilishi, kufungua
akaunti ya kuandika na kutuma
baruapepe, kuandika baruapepe,
kuituma kwa wenzao wa vikundi
vingine na kupokea majibu yao.
Hakikisha kila mwanafunzi anaendelea
kufanya mazoezi zaidi ya kuandika
na kutuma baruapepe akisaidiwa na
3.1 Insha ya baruapepe
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 127-129)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Fanya utafiti kuhusiana na uandishi wa
baruapepe, muundo wake, mtindo wake,
lugha yake na jinsi ya kuituma na kuipokea
ili kufanikisha ufunzaji wako darasani.
Vilevile.
Andaa sampuli mbalimbali za insha
za baruapepe kutoka kwenye matini
mbalimbali mtandaoni utakazowapa
wanafunzi darasani ili kuwasaidia
katika ujifunzaji wao.
Andaa vifaa vya kidijitali kama vile
tarakilishi ambazo zitatumiwa na
wanafunzi kuandika na kutuma
baruapepe darasani. Iwapo shule
yenu ina chumba cha tarakilishi,
unaweza kufanyia somo hili humo.
Iwapo shule yenu haina chumba cha
tarakilishi, unaweza kuleta tarakilishi
kadhaa darasani ili wanafunzi
wazitumie katika ujifunzaji wao.
Hakikisha mashine za breli zipo ili
zitumiwe na wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona ili waandike na
kutuma baruapepe.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
kuhusu funzo hili ili aweze kujiandaa
ifaavyo
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 127
2. Nakala za insha za baruapepe ambazo
zimetolewa kwenye tarakilishi
3. Tarakilishi, breli
4. Mfasiri wa lugha ishara panapofaa
182
Kimeidhinishwa na KICD
mlezi wake au wanafunzi wenzake. Pia,
unaweza kumsaidia baada ya masomo
wakati wa jioni.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Tathmini ikiwa mwanafunzi alibuni
na kuandika insha ya baruapepe
kwenye tarakilishi. Tathmini iwapo
aliituma kwa mlezi wake, kwako na
kwa wanafunzi wenzake ili waisome,
waitathmini na kujifunza. Hakikisha
insha hiyo ya baruapepe ilizingatia
muundo, mtindo na lugha inayofaa.
a) Kutambua viambishi vya nafsi na
vya wakati katika sentensi.
b) Kukanusha viambishi vya wakati
na nafsi katika maneno na
sentensi kwa usahihi.
c) Kutunga sentensi sahihi zenye
viambishi vya nafsi na wakati na
kuzikanusha.
d) Kufurahia ukanushaji wa viambishi
vya nafsi na wakati katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Je, viambishi vya nafsi katika vitenzi
ni vipi?
2. Je, viambishi vya wakati katika
vitenzi ni vipi?
3. Wewe hutumia viambishi gani
kukanusha vitenzi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kutambua
viambishi vya nafsi na wakati katika
sentensi. Pia, anaposhirikiana na
wenzake kukanusha viambishi vya
nafsi na wakati katika sentensi.
(b) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
matatizo
Huu unakuzwa mwanafunzi anapofikiri
jinsi ya kukanusha viambishi vya nafsi
na wakati katika vitenzi na sentensi
kwa usahihi.
(c) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kutunga kwa usahihi sentensi akiwa
peke yake akitumia viambishi vya nafsi
4.1 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 129-131)
Ukanushaji wa maneno
na sentensi
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
Tathmini
1. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutambua baruapepe kwa
kuzingatia mtindo na muundo
wake.
2. Tathmini uwezo wa mwanafunzi wa
kuandika baruapepe kwa kuzingatia
ujumbe, muundo na mtindo ufaao.
3. Hakikisha mwanafunzi anafahamu
kutumia vifaa vya kidijitali
kuandika na kutuma kwa
baruapepe.
183
Kimeidhinishwa na KICD
na wakati na kuzikanusha kwa usahihi
bila kunakili sentensi za wenzake.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapokuza
uwezo wake wa kukubali au kukataa
mambo mbalimbali maishani. Pia,
matumizi ya viambishi vya nafsi
na wakati kwa usahihi yataboresha
mawasiliano yake.
Uraia
Uraia unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kutambua viambishi vya nafsi na
wakati katika vitenzi na kuvikanusha
kwa usahihi.
Uhusiano na maadili
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kufanya
shughuli za vikundi kwa amani bila
kuzua ugomvi.
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi wanapokanusha
viambishi vya nafsi na wakati katika
vitenzi. Pia, mwanafunzi anapowapa
wenzake fursa ya kuchangia katika
majadiliano yao.
Uwajibikaji
Unakuzwa mwanafunzi anapoweza
kukamilisha kazi zake kwa wakati
unaofaa. Pia, anapoweza kuvitunza
vifaa vyake vya ujifunzaji akiwa
darasani na nyumbani.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanashughulikia mada
ya sarufi kuhusu viambishi vya nafsi
na wakati katika maneno na sentensi
pamoja na ukanushaji.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapoelewa matumizi
sahihi ya viambishi vya nafsi na wakati
atakuwa kielelezo cha lugha fasaha
katika jamii. Atawahamasisha wanajamii
kuhusu jinsi ya kutumia lugha ya
Kiswahili ipasavyo katika kuboresha
mawasiliano.
Namna ya kuwashughulikia
wanafunzi wenye mahitaji maalum
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa
kuzungumza au kusikia, watambue
viambishi vya nafsi na wakati kwa
kuviandika kwenye madaftari yao au
kuvipigia mistari kwenye tarakilishi.
Pia, unaweza kumshirikisha mfasiri
wa lugha ishara.
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa
kuona watumie breli au wakusikilize
ukiyasoma maelezo kuhusu viambishi
vya nafsi na wakati na ukanusho
wake au yakisomwa na wanafunzi
wenzao.
Wanafunzi wasiojimudu kufahamu
vipengele vyote walivyojifunza kuhusu
viambishi vya nafsi na wakati na
ukanusho wake waandaliwe kipindi
cha ziada cha kujifunza zaidi baada ya
masomo ya siku ili kufikia matarajio
ya mada.
184
Kimeidhinishwa na KICD
4.1.1 Viambishi vya nafsi na
wakati
Herufi zilizokolezwa rangi nyekundu
(ni, tu, a, wa, u, m) ni viambishi vya
nafsi. Herufi zilizokolezwa rangi ya
kijani (na, li, ta) ni viambishi vya
wakati. Tathmini sentensi ambazo
wanafunzi watatunga kwa kutumia
viambishi vya nafsi na wakati
walivyojadili.
Waelekeze wanafunzi kutambua kuwa:
kiambishi ni- huonyesha nafsi ya kwanza
umoja (ninasoma, ninauza), kiambishi
tu- huonyesha nafsi ya kwanza, wingi
(tunasoma, tunauza), kiambishi u-
huonyesha nafsi ya pili umoja (unasoma,
unauza), kiambishi m- huonyesha nafsi
ya pili, wingi (mnasoma, mnauza),
kiambishi a- huonyesha nafsi ya tatu
umoja (anasoma, anauza) na kiambsihi
wa- huonyesha nafsi ya tatu wingi
(wanasoma, wanauza). Kiambishi -na-
huonyesha wakati uliopo, kiambishi -li-
huonyesha wakati uliopita na kiambishi
-ta- huonyesha wakati ujao.
Katika shughuli ya 2, waelekeze
wanafunzi wawiliwawili wasome
sentensi zilizo kwenye vitabu
vyao. Waongoze kufahamu jinsi ya
kukanusha vitenzi katika sentensi
walizopewa. Majibu tarajiwa:
a) Siendi dukani. b) Hatuendi madukani.
c) Mteja hakulipa deni lake. d) Wateja
hawakulipa madeni yao. e) Hutaandika
bajeti yako? f) Hamtaandika bajeti
zenu?
Mwongoze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 3. Akanushe kwa usahihi
vitenzi na sentensi alizopewa kitabuni
mwake. Majibu tarajiwa:
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 129-131)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 3)
Fanya utafiti kuhusu viambishi vya nafsi na
wakati pamoja na ukanushaji wake kwenye
maneno na sentensi ili kufanikisha ufunzaji
wako. Pia,
Andaa chati ambazo zimeandikwa
vitenzi mbalimbali na kuonyesha
viambishi vya nafsi na wakati
pamoja na ukanusho wao. Chati
hizi zitakusaidia katika ufunzaji
wako darasani.
Hakikisha mashine za breli zipo na
ziko katika hali nzuri ya kutumiwa
na wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona.
Hakikisha umemfahamisha mfasiri
wa lugha ishara kuhusu funzo hili
kwa wakati ili ajiandae ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
129
2. Chati zilizoandikwa vitenzi na
kuonyesha viambishi vya wakati
na nafsi pamoja na ukanusho wao.
3. Mfasiri wa lugha ishara, breli
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza somo kwa kuwashirikisha
wanafunzi katika shughuli ya 1.
Waulize watambue vitenzi kwenye
sentensi zilizo vitabuni mwao.
Waelekeze wanafunzi kujadili herufi
zilizokolezwa rangi nyekundu na
rangi ya kijani. Majibu tarajiwa:
185
Kimeidhinishwa na KICD
1. a) Hauzi b) Hukunikopesha
c) Hawatanunua d) Hakuwekeza
e) Hamtahifadhi f) Sihesabu
2. a) Mfanyabiashara hasomi gazeti
la biashara. b) Mteja wangu
hakunitembelea nyumbani. c) Wewe
hutanunua bidhaa mpya kutoka
ngambo? d) Mimi sifagii duka langu.
e) Kwa nini huuzi bidhaa hii?
3. Tathmini sentensi atakazoandika
mwanafunzi katika wingi. Hakikisha
ni sahihi kisarufi. Majibu tarajiwa:
a) Wafanyabiashara hawasomi
magazeti ya biashara. b) Wateja
wetu hawakututembelea nyumbani.
c) Nyinyi hamtanunua bidhaa mpya
kutoka ng’ambo? d) Sisi hatufagii
maduka yetu. e) Kwa nini hamuuzi
bidhaa hizi?
Katika shughuli ya 4, wapange
wanafunzi katika vikundi viwili
kulingana na uwezo wao kisha
uwaelekeze kucheza mchezo wa
kutunga na kukanusha sentensi
kwa usahihi. Hakikisha sentensi
zao zinatumia viambishi vya nafsi
na wakati kwa usahihi. Tathmini
ukanusho wa sentensi zao.
Hitimisha somo hili kwa kumpa
mwanafunzi kazi ya ziada ambayo
atafanya akisaidiwa na mzazi au mlezi
wake. Tathmini kifungu ambacho
mwanafunzi atabuni kuhusu duka
analojua akitumia viambishi vya
nafsi na wakati kwa usahihi kisha
akikanushe kifungu hicho. Iwapo
kutakuwa na muda, mwanafunzi
awasomee wenzake darasani ili
watathmini vifungu vyake.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua viambishi vya nafsi
na wakati katika sentensi.
2. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kukanusha viambishi vya
nafsi na wakati katika maneno na
sentensi kwa usahihi.
3. Tathmini ikiwa mwanafunzi
anaweza kutunga sentensi sahihi
zenye viambishi vya nafsi na wakati
na kuzikanusha kwa usahihi.
4.2 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 131-132)
Ukubwa na udogo wa
nomino zinazoanza
kwa herufi m- na zenye mzizi
wa silabi mbili
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino zinazoanza kwa
herufi m- na zenye mzizi wa silabi
mbili.
b) Kutambua nomino zinazoanza kwa
herufi m- katika hali ya ukubwa na
udogo.
c) Kubadilisha nomino zinazoanza
kwa herufi m- katika hali wastani
kuwa katika hali ya ukubwa na
udogo.
d) Kutumia nomino zinazoanza kwa
herufi m- katika hali ya ukubwa na
186
Kimeidhinishwa na KICD
udogo katika sentensi.
e) Kufurahia kutumia nomino
katika hali ya ukubwa na udogo
kwa usahihi ili kuimarisha
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unajua nomino gani zinazoanza
kwa herufi m-?
2. Ni nomino gani unazoweza kutaja
ukubwa wake?
3. Ni nomino gani unazoweza kutaja
udogo wake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapowasiliana na kushirikiana na
wenzake katika vikundi kutambua
ukubwa na udogo wa nomino
zinazoanza kwa herufi m- zenye
mzizi wa silabi mbili.
(b) Ubunifu
Huu unakuzwa mwanafunzi
anapoweza kutunga sentensi sahihi
kwa maneno yake mwenyewe bila
kunakili za wenzake akitumia
ukubwa na udogo wa nomino
zinazoanza kwa herufi m- zenye
mzizi wa silabi mbili.
(c) Ujuzi wa kidijitali
Ujuzi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotafuta mtandaoni picha za
nomino zinazoanza kwa herufi
m- zenye mzizi wa silabi mbili na
kuzitungia sentensi katika ukubwa na
udogo.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia
Huu unakuzwa wakati mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake kutoka
maeneo mbalimbali katika vikundi
kutunga sentensi sahihi katika
ukubwa na udogo akitumia nomino
zinazoanza kwa herufi m- zenye
mzizi wa silabi mbili. Pia, sentensi
hizo zinaweza kulenga uraia mwema.
Stadi za maisha
Zinakuzwa mwanafunzi anapofanya
shughuli zinazohusu ukubwa na
udogo wa nomino zinazoanza kwa
m- zenye mzizi wa silabi mbili katika
sentensi akiwa peke yake hivyo
kujifunza kujitegemea maishani.
Uhusiano na maadili
Umoja na amani
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi kwa amani bila kuzua fujo.
Uwajibikaji
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi
anapotunza vifaa vyake vya ujifunzaji.
Pia, anapokamilisha kazi zake kwa
wakati ufaao.
Upendo na heshima
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anapoyaheshimu maoni ya wenzake
katika vikundi kuhusiana na ukubwa
na udogo wa nomino zinazoanza kwa
herufi m- zenye mzizi wa silabi mbili
katika sentensi. Pia, anapotumia lugha
ya heshima kuwasiliana na wenzake na
hata kuwapa fursa ya kuchangia katika
majadiliano yao.
187
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanashughulikia mada
ya nomino katika sarufi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakuwa kielelezo chema
anapotumia lugha kwa ufasaha shuleni
na nje ya shule hivyo kuboresha
mawasiliano yake na ya wanajamii.
Namna ya kuwashughulikia
wanafunzi wenye mahitaji maalum
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia breli kutambua
ukubwa na udogo wa nomino
zinazoanza kwa herufi m- zenye
mzizi wa silabi mbili na kuzitungia
sentensi sahihi. Pia, wanaweza
kusikiliza maelezo kuhusu ukubwa
na udogo wa nomino zinazoanza kwa
herufi m- zenye mzizi wa silabi mbili
kutoka kwa mwalimu au wanafunzi
wenzao na kujifunza.
Wanafunzi ambao wanangamua
wanayojifunza upesi wanaweza
kupewa mazoezi zaidi ya kubuni
kifungu cha aya moja wakitumia
nomino zinazoanza kwa herufi m-
zenye mzizi wa silabi mbili katika
udogo na ukubwa.
Wanafunzi ambao wanangamua
wanayofundishwa polepole
watengewe muda zaidi wa kuendelea
kujifunza baada ya masomo jioni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia au kuzungumza wanaweza
kusaidiwa na mfasiri wa lugha ishara
katika ujifunzaji wao.
4.2.1 Nomino zinazoanza kwa
herufi m- zenye mzizi wa
silabi mbili
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 131-132)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti zaidi kuhusu ukubwa na udogo
wa nomino zenye mizizi ya silabi
mbili zinazoanza kwa herufi na m- ili
kufanikisha ufunzaji wako darasani.
Vilevile,
Unaweza kuandaa chati zilizoandikwa
nomino zinazoanza kwa herufi m-
zenye mzizi wa silabi mbili katika
ukubwa na udogo ili kuwasaidia
wanafunzi katika ujifunzaji wao.
Hakikisha mashine za breli zipo ili
zitumiwe na wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona ili kuwasaidia katika
ujifunzaji wao.
Mfahamishe mfasiri wa lugha ishara
kuhusu somo hili ili ajiandae ifaavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 131
2. Mfasiri wa lugha ishara, breli
3. Chati zenye nomino zinazoanza kwa
herufi m- zenye mzizi wa silabi mbili
katika ukubwa na udogo
4. Kamusi ya Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa shughuli ya
1. Waulize wanafunzi wakiwa katika
vikundi wataje nomino zinazoanza kwa
herufi m- zenye mizizi ya silabi moja
walizojifundisha katika gredi ya nne.
Mifano: mti, mtu, mto, mke, mji n.k.
188
Kimeidhinishwa na KICD
Wakumbushe wanafunzi kuwa mzizi
wa neno ni sehemu ya neno isiyobadilika
neno hilo linapoandikwa katika wingi,
umoja, ukubwa au udogo.
Waelekeze wanafunzi kutaja nomino
zozote zilizo na mizizi ya silabi mbili
kisha watambue nomino zinazoanza
kwa herufi m- kati ya walizotaja.
Mifano: mkwaju mikwaju, mkoba
mikoba, mkanda mikanda, mshipi
mishipi n.k. Tathmini majibu ya
wanafunzi.
Katika shughuli ya 2, mwelekeze
mwanafunzi kuonyesha mizizi ya
nomino alizopewa kitabuni mwake.
Majibu tarajiwa: m+pira, m+keka,
m+kono, m+kia, m+koba. Sehemu
zilizopigiwa mistari ndizo mizizi.
Mwanafunzi ahesabu idadi ya silabi
katika mizizi ya nomino aliyoonyesha.
Mizizi hiyo yote ina silabi mbili mbili.
Waongoze wanafunzi kujikumbusha
kuhusu ukubwa na udogo wa nomino
katika shughuli ya 3 walivyojifunza
katika gredi ya nne. Tathmini maelezo
yao. Wanafunzi waandike ukubwa
na udogo wa nomino zilizotajwa
katika shughuli ya 2. Majibu tarajiwa:
Ukubwa pira, keka, kono, kia, koba.
Udogo kipira, kikeka, kikono, kikia,
kikoba. Tathmini majibu ya wanafunzi.
Washirikishe wanafunzi katika kutaja
mifano zaidi ya nomino zinazoanza
kwa herufi m- zenye mizizi ya silabi
mbili. Waandike udogo na ukubwa
wa nomino hizo. Tathmini majibu ya
wanafunzi.
Katika shughuli ya 4, mwongoze
mwanafunzi kujaza jedwali lililo
kitabuni mwake kwa nomino sahihi
katika udogo na ukubwa. Majibu
tarajiwa: a) guu, kiguu b) rija, kirija
c) domo, kidomo, d) pini, kipini
e) shipi, kishipi f) dudu, kidudu.
Tathmini majibu ya mwanafunzi.
Waelekeze wanafunzi kutunga
sentensi sahihi kwa kutumia nomino
walizoandika katika ukubwa na
udogo kwenye jedwali. Sentensi hizo
ziandikwe ubaoni ili wanafunzi wote
wazitathmini na kujifunza.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Tathmini orodha ya nomino za vitu
vinavyopatikana nyumbani ambazo
mwanafunzi ataandika katika ukubwa
na udogo.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua nomino zinazoanza
kwa herufi m- zenye mizizi ya
silabi mbili.
2. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kuandika ukubwa na
udogo wa nomino zinazoanza kwa
herufi m- zenye mizizi ya silabi
mbili.
3. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kubadilisha nomino zinazoanza
kwa herufi m- zenye mizizi ya
silabi mbili katika hali wastani
kuwa katika hali ya ukubwa na
udogo.
189
Kimeidhinishwa na KICD
4.3 Sarufi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 133-134)
Ukubwa na udogo wa
nomino zinazoanza kwa
herufi n-
Matokeo maalum yanayotarajiwa
Kufikia mwisho wa mada ndogo hii,
mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino zinazoanza
kwa herufi n- ili kuzitofautisha na
nomino nyingine.
b) Kutambua nomino zinazoanza kwa
herufi n- katika hali ya ukubwa na
udogo.
c) Kubadilisha nomino zinazoanza
kwa herufi n- katika hali ya
wastani kuwa katika hali ya
ukubwa na udogo.
d) Kutumia nomino zinazoanza kwa
herufi n- katika hali ya ukubwa na
udogo kwenye sentensi.
e) Kufurahia kutumia nomino
katika hali ya ukubwa na udogo
kwa usahihi ili kuimarisha
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unajua nomino gani zinazoanza
kwa herufi n-?
2. Ni nomino gani unazoweza kutaja
ukubwa wake?
3. Ni nomino gani unazoweza kutaja
udogo wake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
(a) Mawasiliano na ushirikiano
Wanafunzi watafanya shughuli
za kutambua nomino zinazoanza
kwa herufi n- katika ukubwa na
udogo na kuzitungia sentensi
wakiwa katika vikundi. Wanafunzi
watatunga sentensi na kusomeana ili
kuzitathmini hivyo kuboresha uwezo
wao wa kuwasiliana.
(b) Ubunifu
Unajengeka mwanafunzi anapoweza
kutunga sentensi na hata kifungu
kifupi kwa maneno yake mwenyewe
akitumia nomino zinazoanza kwa
herufi n- katika ukubwa na udogo
bila kunakili kazi za wenzake.
(c) Kujiamini
Kunakuzwa mwanafunzi anapofaulu
kutambua kwa usahihi nomino
zinazoanza kwa herufi n- katika
ukubwa na udogo. Pia, mwanafunzi
anapoweza kutunga sentensi sahihi
akitumia nomino hizo na kuwasomea
wanafunzi wenzake.
(d) Uwazaji wa kina na utatuzi wa
changamoto
Umilisi huu unakuzwa mwanafunzi
anapotunga sentensi kuhusu masuala
mbalimbali hasa mtambuko akitumia
nomino zinazoanza kwa herufi n-
katika ukubwa na udogo. Pia, uwazaji
wa kina unajitokeza mwanafunzi
anapofikiri kuhusu ukubwa na udogo
wa nomino zinazoanza kwa herufi n-
atakazotumia kutunga kifungu.
4. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutunga sentensi sahihi
akitumia nomino zinazoanza kwa
herufi m- katika hali ya ukubwa na
udogo.
190
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Masuala mbalimbali kama vile uraia,
lishe bora, utunzaji wa mazingira na
usalama yatashughulikiwa mwanafunzi
anapotunga sentensi akitumia nomino
zinazoanza kwa herufi n- katika ukubwa
na udogo akirejelea masuala hayo.
Uhusiano na maadili
Heshima na upendo
Maadili haya yanakuzwa mwanafunzi
anaposhirikiana na wenzake
katika vikundi kutambua nomino
zinazoanza kwa herufi n- katika
ukubwa na udogo na kuyaheshimu
maoni yao. Pia, anapotumia lugha
ya adabu kuwasiliana na wenzake na
kuwapa fursa ya kuchangia katika
majadiliano yao.
Uwajibikaji
Unadhihirika mwanafunzi
anapotunza vifaa vyake vya ujifunzaji.
Pia, anapotekeleza majukumu yake
anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi pamoja na kukamilisha kazi
zake kwa wakati ufaao.
Amani na umoja
Maadili haya yatalengwa katika
sentensi zitakazotungwa na
wanafunzi wakitumia nomino
zinazoanza kwa herufi n- katika
ukubwa na udogo. Pia, kupitia kwa
wanafunzi kutangamana kwa amani
katika vikundi bila kuzua ugomvi
wowote.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili
Masomo haya yanashughulikia mada
ya nomino katika sarufi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma
za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakapotumia sentensi zenye
nomino zinazoanza kwa herufi n- kwa
usahihi katika mawasiliano ataboresha
mawasiliano na lugha katika jamii.
Namna ya kuwashughulikia
wanafunzi wenye mahitaji maalum
Unaweza kurekodi video yenye
picha na maandishi ya maelezo
ya nomino zinazoanza kwa herufi
n- ili kuwasaidia wanafunzi wenye
changamoto ya kusikia ili wajifunze.
Pia, mfasiri wa lugha ishara anaweza
kuhusishwa.
Hakikisha kuna mashine za breli ili
wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wazitumie kujifunza. Pia, wanafunzi
hawa wanaweza kutolewa maelezo
kuhusu ukubwa na udogo wa
nomino zinazoanza kwa herufi n- na
wakayasikiliza na kujifunza.
Jitayarishe kuwasaidia wanafunzi
wengine ambao wana matatizo
mbalimbali kadri ya uwezo wako.
4.3.1 Ukubwa na udogo wa
nomino zinazoanza
kwa herufi n-
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 133-134)
Maandalizi ya mwalimu (Vipindi 2)
Tafiti zaidi kuhusu nomino zinazoanza
kwa herufi n- katika ukubwa na udogo
kabla ya kipindi ili kuweza kumwelekeza
mwanafunzi vyema. Pia,
Andaa chati zilizoandikwa
nomino zinazoanza kwa herufi
191
Kimeidhinishwa na KICD
n- katika ukubwa na udogo ili
uzitumie kuwafunza wanafunzi
darasani.
Unaweza kurekodi video au kanda
yenye picha au maelezo kuhusu
nomino zinazoanza kwa herufi n-
katika ukubwa na udogo.
Hakikisha mashine za breli zipo
ili zitumiwe na wanafunzi wasio
na uwezo wa kuona ili waweze
kutambua nomino zinazoanza
kwa herufi n- katika ukubwa na
udogo.
Mfahamishe mfasiri wa lugha
ishara kuhusu funzo hili ili
ajiandae vilivyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
133
2. Chati zilizoandikwa nomino
zinazoanza kwa herufi n- katika
ukubwa na udogo.
3. Kanda au video iliyorekodiwa
yenye maelezo ya nomino
zinazoanza kwa herufi n- kwa
manufaa ya wanafunzi wasio na
uwezo wa kuona.
4. Mfasiri wa lugha ishara, breli
5. Kamusi ya Kiswahili
Utaratibu wa ujifunzaji
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza
wanafunzi wawiliwawili watambue
na kuandika majina ya michoro
waliyopewa vitabuni mwao. Majibu
tarajiwa: a) ngoma b) dawati c) ndoo
d) nyumba e) chura f) ng’ombe.
Wanafunzi watambue kwa usahihi
majina yanayoanza kwa herufi n-
kati ya waliyotaja. Majibu tarajiwa:
ngoma, ndoo, nyumba, ngombe.
Katika shughuli ya 2, wapange
wanafunzi katika vikundi kulingana
na uwezo na idadi yao kisha
waandike mifano ya nomino
zinazoanza kwa herufi zifuatazo:
a) Herufi nd -: ndizi, ndume, ndoo
b) Herufi ny-: nyumba, nyoka, nyasi
c) Herufi ng’-: n g’o mb e
d) Herufi ng-: ngoma, ngamia, ngazi
e) Herufi nj-: njia, njuga
Wanafunzi waandike ukubwa
na udogo wa nomino walizotaja.
Tathmini majibu yao. Majibu
tarajiwa:
a) Herufi nd -: dizi - kidizi, dume -
kidume, doo - kidoo
b) Herufi ny-: jumba - kijumba, joka
- kijoka, jasi - kijasi
c) Herufi ng’-: gombe - kigombe
d) Herufi ng-: goma - kigoma, gamia
- kigamia, gazi - kigazi
e) Herufi nj-: jia - kijia, juga - kijuga
Waongoze wanafunzi kujadiliana
ugunduzi wao kutokana na ukubwa
na udogo wa nomino walizoandika.
Tathmini maelezo yao.
Mwelekeze mwanafunzi kufanya
shughuli ya 3 kwa kujaza kwa
usahihi jedwali lililo kitabuni mwake
kwa kutumia nomino zinazoanza kwa
herufi n- katika ukubwa na udogo.
Majibu tarajiwa: goma kigoma, dizi
–kidizi, doo –kidoo, dama kidama,
gombe –kigombe.
Tathmini majibu ya mwanafunzi.
192
Kimeidhinishwa na KICD
Shughuli ya nje ya darasa
Waongoze wanafunzi kutembelea
baadhi ya wawekezaji walio katika eneo
lililo karibu na shule yenu. Wanafunzi
wawaeleze wawekezaji hao njia
mbalimbali za uwekezaji walizojifunza
darasani. Wanafunzi wawape wawekezaji
hao fursa wawaeleze njia walizotumia
kuwekeza na matokeo yake. Wanafunzi
watakaporudi shuleni, waandike insha
ya maelezo kuhusu njia mbalimbali
za uwekezaji walizoelezwa. Shughuli
hii itakuza utangamano, uwazaji kina,
uzalendo, na hamu ya kujitegemea
maishani.
Majibu ya Zoezi la Mwisho
wa Sura
1. Kubali majibu yoyote yanayohusu
njia za uwekezaji, kwa mfano:
kufungua biashara itakayoleta faida,
kujenga vyumba vya kupangisha,
kuanzisha biashara ya usafiri,
kununua mashamba ili kukuza
mimea itakayouzwa na kuleta faida
n.k.
2. Kubali sifa zozote za baruapepe,
kwa mfano: anwani ya baruapepe
ya mwandishi, anwani ya baruapepe
ya mwandikiwa, mada, mwili na
hitimisho.
Waelekeze wanafunzi kutunga
sentensi sahihi wakitumia nomino
walizoandika katika ukubwa na
udogo kwenye jedwali. Sentensi hizo
ziandikwe ubaoni ili wanafunzi wote
wazitathmini na kujifunza.
Hitimisha somo hili kwa kumhimiza
mwanafunzi afanye kazi ya ziada
akisaidiwa na mzazi au mlezi wake.
Tathmini orodha ya nomino za vitu
au viumbe wanaopatikana nyumbani
ambazo mwanafunzi ataandika katika
wingi.
Tathmini
1. Tathmini uwezo wa mwanafunzi
wa kutambua nomino zinazoanza
kwa herufi n- ili kuzitofautisha na
nomino nyingine.
2. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kuandika ukubwa na
udogo wa nomino zinazoanza kwa
herufi n-.
3. Tathmini uwezo wa mwanafunzi wa
kubadilisha nomino zinazoanza kwa
herufi n- zilizo katika hali ya wastani
na kuwa katika hali ya ukubwa na
udogo.
4. Tathmini iwapo mwanafunzi
anaweza kutumia nomino
zinazoanza kwa herufi n- katika
hali ya ukubwa na udogo kutunga
sentensi sahihi.
193
Kimeidhinishwa na KICD
3. Tathmini insha ya baruapepe
atakayoandika mwanafunzi. Sharti
izingatie mtindo, muundo na lugha
inayofaa na mada ya umuhimu wa
kuweka pesa akiba.
4. Tathmini sentensi ambazo
mwanafunzi atatunga. Hakikisha
ni sahihi kisarufi na zinatumia
viambishi vya nafsi na wakati pamoja
na maneno aliyopewa kitabuni
mwake. Mifano: a) Nilinadi bidhaa
sokoni. b) Baba atawekeza pesa zake.
c) Utalipa deni lako lini? d) Tunauza
mayai dukani. e) Mlinunua makochi
wapi?
5. Tathmini majibu ya mwanafunzi.
a) kebe kikebe
b) dama kidama
c) gombe kigombe
d) lima kilima