Kusoma na Kuandika
katika Kiswahili
Mwongozo wa Mwalimu
Gredi ya 2
Hezekiel Gikambi
Henry T. Indindi
Danson Khasiani
Rachael Maina
ii
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Kimechapishwa na:
Longhorn Publishers (Kenya) Ltd.,
Barabara ya Funzi, Eneo la Viwandani
S.L.P. 18033–00500
Nairobi, Kenya
Longhorn Publishers (Uganda) Ltd.,
Ploti 4, Eneo la Vubyabirenge, Ntinda,
S.L.P 24745
Kampala, Uganda.
Longhorn Publishers (Tanzania) Ltd.
Barabara Mpya ya Bagamoyo/Garden,
Mikocheni B, Ploti Namba: MKC/MCB/81
S.L.P 1237, Dar es Salaam, Tanzania
Longhorn Publishers (Rwanda) Ltd.,
Remera mkabala na Benki ya COGE
S.L.P 5910
Kigali, Rwanda.
© H. Gikambi, H. T. Indindi, D. Khasiani, R. Maina, 2018
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupigisha chapa, kutafsiri au
kukitoa kitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila idhini, kwa maandishi ya Longhorn Publishers
Ltd.
Chapa ya kwanza 2018
ISBN 978-9966-64-018-5
Kimepigwa chapa na Ramco Printing Works Ltd,
Unit 2, Ramco Industrial Complex,
Barabara ya Mombasa, Eneo la Viwandani,
S. L. P. 27750 - 00506, Nairobi.
iii
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi .............................................................................................................................v
Mbinu za kufundisha ......................................................................................................... vi
Vifaa vya kufundisha .........................................................................................................vii
Sehemu 1: Kwenye kivuko cha barabara...........................................................................1
Sehemu 2: Lenana na Kantai wapata maji.......................................................................33
Sehemu 3: Adhuhuri ya mvua..........................................................................................52
Sehemu 4: Mutulu amkasirisha mama yake...................................................................77
Sehemu 5: Fatuma aumia goti lake...................................................................................98
Sehemu 6: Treni mpya ....................................................................................................117
Yaliyomo
iv
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
v
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
UTANGULIZI
Lugha ya Kiswahili imepita mipaka ya Uswahilini, kusambaa na kutambaa katika
Afrika Mashariki, Kati na kwingineko. Ni wajibu wa mwalimu kuwahamasisha
wanafunzi wake kuipenda lugha ya Kiswahili kwani ina matumaini ya siku za usoni.
Mwalimu awahimize wanafunzi wake kuwa wanaweza kujiendeleza katika somo la
Kiswahili katika bahari pana ya maisha kama vile: redio, runinga, magazeti, ualimu,
tafsiri miongoni mwa nyanja anuwai.
Jukumu la lugha ya taifa ni kuweza kutambulisha watu wa taifa moja na kuwatia
hisia kuwa wanaungana na kutambulika. Lugha ni kitambulisho muhimu sana cha
watu wa jamii fulani. Lugha ya Kiswahili kwa sababu ya kusambaa kwake kama moto
nyikani, msamiati wake ulio mzuri, utati uliofanyiwa lugha hii na idadi kubwa ya
watu wanaoizungumza ni thibitisho tosha kuwa lugha hii inapaswa kupewa nafasi
mwafaka kwani ndiyo lugha ya kutambulisha bara la Afrika katika ramani ya dunia.
Isitoshe, lugha ya Kiswahili inao wajibu wa kuleta mabadiliko ya kijamii, kisiasa
na kiuchumi katika bara la Afrika, ingawa Afrika ni bara ambalo limekumbwa na
matatizo si haba yakiwemo usadi, Ukimwi, ukabila, madeni ya kimataifa, umaskini
na kadhalika.
Malengo ya kufundisha Kujifunza kusoma na kuandika na mazoezi
katika lugha za kiasili
Malengo haya katika shule za msingi kama yanavyofafanuliwa na silabasi mpya
ni kumwezesha mwanafunzi:
1. Kusikiliza na kuitikia vilivyo kwa lugha ya Kiswahili.
2. Kuongea lugha ya Kiswahili kwa ufasaha.
3. Kusoma na kuelewa lugha ya Kiswahili.
4. Kujieleza kikamilifu kwa lugha ya Kiswahili kwa kuandika.
5. Kutunga kazi za kisanii kulingana na kiwango cha mwanafunzi.
6. Kuimarisha mazoea ya usomaji bora.
7. Kupenda na kujiendeleza katika somo la Kiswahili baada ya shule ya msingi.
8. Kuionea fahari na kuikuza lugha ya Kiswahili katika mawasiliano.
9. Kutukuza na kuendeleza Kiswahili sanifu maishani.
10. Kutathmini, kufurahia na kujivunia Kiswahili kama lugha ya taifa na kimataifa.
11. Kutambua na kushiriki katika kupata suluhisho la masuala ibuka yanayohusu
na kuathiri jamii kama vile: afya na Ukimwi, uadilifu, jinsia, mazingira na
teknolojia.
Jukumu la mwalimu katika kutimiza malengo haya
Ili kutimiza malengo haya, mwalimu wa Kiswahili ana wajibu muhimu. Mwalimu
vi
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
azingatie mazingira ya shule na kutoa mifano halisi ya vitu au watu wanaopatikana
katika mazingira ya shule. Kuna mazingira ya mjini na ya mashambani.
Mwalimu ana wajibu wa kujitayarisha mapema kabla ya somo lake kwa kuhakikisha
ana vifaa vya kutumia darasani ili kufanikisha somo lake. Vifaa hivi viwe vinapatikana
kwa urahisi au kwa bei rahisi iwapo ni vya kununuliwa.
Mwalimu anapaswa kutumia mwongozo huu na kitabu cha wanafunzi na rasilimali
yoyote itakayofanikisha kipindi chake. Mwalimu asitumie mwongozo huu kisisisi bali
awe mbunifu kulingana na uwezo wa wanafunzi wake na vifaa vinavyopatikana.
Mwalimu aanze kwa kufundisha dhana sahili kabla ya kufundisha zile changamano
zaidi. Si lazima afuate ukurasa hadi ukurasa. Lazima azingatie uwezo wa wanafunzi
wake.
Mwalimu anapaswa kuwashirikisha wanafunzi wake kadiri iwezekanavyo katika
somo la Kiswahili. Kwa kuwashirikisha, watakuza stadi zao za kusikiliza, kuongea,
kusoma na kuandika. Nyakati za kufundisha lugha ya Kiswahili ikiwa kavu zimepita
na yamkini hazitarudi!
Mifano anayotoa darasani, iwe rahisi, sahihi, ya hali ya kila siku na inayoeleweka
kwa wanafunzi kuhusu mazingira yao na kuihusisha na masuala ibuka kama vile:
uadilifu, haki za watoto, Ukimwi, jinsia na teknolojia. Jukumu kubwa la mwalimu
ni kuwahamasisha wanafunzi kuongea, kusoma na kuandika lugha ya Kiswahili kwa
ufasaha. Hili ni jukumu ambalo mwalimu yeyote wa Kiswahili hawezi kuepuka.
Lazima mwalimu awe kielelezo kwa wanafunzi wake kwa sababu wanafunzi
hupenda sana kuiga. Awe ni mtu anayeipenda lugha ya Kiswahili na kuionea fahari
ili awatie ari wanafunzi wake kuipenda lugha ya Kiswahili.
Mwalimu mwema ni yule anayejaribu kuwa katika kiwango cha wanafunzi.
Kama ni kuimba, wote wanaimba, kama ni kuigiza naye anaigiza. Mwalimu sharti
awe mchangamfu ili awachangamshe wanafunzi wake. Asifunze mambo au mada
kidhahania tu. Ataje matukio halisi maishani mwa wanafunzi huku akiwahusisha
katika kila hatua darasani. Mwongozo huu ni kama dira kwa mwalimu katika
kutekeleza mambo haya.
Mwalimu ajaribu kutumia rekodi za redio pamoja na video ili kuwavutia
wanafunzi mbali na kuendeleza stadi za kusikiliza na matamshi bora. Mwalimu
awahusishe wanafunzi katika kuchora picha, kuigiza darasani, kuimba, mijadala ili
somo la Kiswahili liwe hai. Mwalimu anaweza kuwaalika shuleni watu waliobobea
katika Kiswahili ili kuwahamasisha wanafunzi kuipenda na kuionea fahari lugha ya
Kiswahili.
Mbinu za kufundisha somo hili
Kuna mbinu kadhaa zinazoweza kutumiwa kufundisha somo la Kiswahili. Mwalimu
anashauriwa atumie mbinu kulingana na kiwango cha wanafunzi wake, uwezo wao,
vii
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
mazingira, rasilimali na vifaa vinavyopatikana. Kuna mbinu kama kuigiza, mjadala,
kuwaalika watu wenye ujuzi wa lugha ya Kiswahili (kama waandishi wa habari,
wahadhiri, malenga, watangazaji) na kadhalika. Mbinu ya jadi ni maswali na majibu
lakini bado inatumiwa hasa kutathmini wanafunzi darasani. Michoro au kuunda
picha za vitu mbalimbali na kuwapanga wanafunzi katika vikundi ni mbinu nyingine.
Mwalimu akumbuke kuwa kila mbinu ina faida na upungufu wake. Mwalimu atumie
mbinu inayofaa zaidi na rahisi kwa wanafunzi ili kueleza dhana inayohusika.
Kazi za wanafunzi
Sharti mwalimu awashirikishe wanafunzi katika somo la Kiswahili. Baadhi ya
shughuli za wanafunzi ni:
Kujibu na kuuliza maswali darasani.
Kusoma makala katika kitabu.
Kujadiliana darasani, kusimuliana hadithi na kukariri mashairi.
Kuchora vifaa mbalimbali.
Kuigiza watu mbalimbali.
Kusikiliza wenzao wakisoma, wakiongea au wataalamu walioalikwa.
Kuandika majibu ya maswali mbalimbali.
Vifaa vya kufundisha
Mwalimu anaweza kutumia vifaa kama vile:
Kadi Mabango Vifaa halisi vinavyoweza kupatikana
kwa urahisi
Michoro Picha Tarakilishi
Redio Vitabu
Tathmini
Kutathmini ni mfanyiko unaoendelea katika mfumo wa elimu. Kutathmini ni
jambo lisiloepukika katika elimu kwa sababu ufundishaji hauwezi kuwa kamilifu
bila kutathmini. Kupitia tathmini mwalimu anaweza kuelewa udhaifu na uwezo
wa wanafunzi wake. Kuna mbinu kadhaa za kutathmini kama kuuliza na kujibiwa
maswali darasani, kusoma, kuandika na kusimulia hadithi. Katika kutathmini,
mwalimu atumie mbinu inayofaa wanafunzi wake ili kupima stadi husika kama
kusoma, kuandika, kusikiliza, ufahamu, saru na kuzungumza.
Tunatarajia kuwa mwongozo huu utakuwa dira mui kwa mwalimu anapowaongoza
wanafunzi katika safari ya kuiendeleza na kuikuza lugha ya Kiswahili.
viii
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
1
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Sehemu
1
Kwenye kivuko cha barabara
Somo Kusikiliza
maagizo na
maswali
Somo Kujibu
maswali na
maagizo
Somo Kusoma
katika jozi
Somo Miundo ya
maneno na sentensi
Kukia mwisho wa
somo mwanafunzi
aweze:
a) Kusilikiza kwa
makini maagizo
mepesi yenye
mfululizo.
b) Kutumia
vidokezo
mwafaka vya
mawasiliano
yasiyo ya uneni
(viziada-lugha)
kuashiria welewa
wa maswali na
maagizo.
Kukia mwisho wa
somo mwanafunzi
aweze:
a) Kujibu kwa
ukakamavu
maswali na
maagizo
kuhusu mada
mbalimbali.
b) Kutumia
vidokezo vya
uneni na visivyo
vya uneni katika
kujibu ifaavyo
maswali na
maagizo.
Kukia mwisho wa
somo mwanafunzi
aweze:
a) Kujitathmini
kuhusu kasi
na ufasaha wa
usomaji wake.
b) Kutoa maoni na
majibu kuhusu
usomaji wa
mwenzake.
ch) Kuuliza
maswali ili
kuthibitisha na
kupanua uelewa
wa matini
iliyosomwa.
Kukia mwisho wa
somo mwanafunzi
aweze:
a) Kutumia maneno
na virai vya
kawaida kuandika
sentensi sahili.
b) Kutumia miundo
ifaayo ya nomino
na vitenzi katika
kutunga sentensi.
2
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
ch) Kudhihirisha
uelewa wa
fungu la
maagizo
kupitia majibu
mwafaka.
d) Kudhihirisha
kaida za kutoa
maagizo
na kuuliza
maswali.
ch) Kuuliza
maswali ili
kupata ubayana
kuhusu
maagizo.
d) Kudhihirisha
hamu ya
kujibu maswali
na kufuata
maagizo.
d) Kufanya
ubashiri kabla
na baada ya
kusoma.
e) Kutambua
umuhimu
wa kusoma
kwa zamu na
kuwasikiliza
wenzake
wanaposoma.
ch) Kutambua
na kuandika
ipasavyo heru
kubwa na ndogo
katika maneno na
sentensi.
d) Kuendeleza hamu
ya kuandika kwa
starehe.
Umilisi mkuu unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano
Wanafanya mazoezi ya kupokea na kutoa maagizo mepesi katika vikundi vidogo
vidogo au wakiwa wawili wawili.
Uwazaji wa kina na usuluhishaji wa matatatizo
Wanafunzi wanafanya mazoezi ya kukiria na kujibu maswali. Kwa mfano
wanapoeleza wanachostahili kufanya kwenye kivuko cha barabara, wanakuza uwezo
wao wa kukiri na kutatua matatizo.
Umilisi wa ubinifu
Wanakuza ubinifu wao katika kutunga sentesi na hadithi mbalimbali za kusimulia
wanazaogizwa.
Ujuzi wa kidijitali
1. Wanafunzi wanakuza umilisi wao wa kidijitali kwa kutumia vifaa vya kidijitali
kama vile simu, kijirekodi na kurekodi shughuli mbalimbali wanazotekeleza.
2. Aidha, wanaposoma kuhusu baadhi ya vyombo vya usari kama vile ndege, treni
na vyombo vya mawasiliano wanakuza umilisi wao wa kiteknolojia.
Kujiamini na kuwajibika
1. Uwezo wa kujiamini unakuzwa katika kujieleza kwa wanafunzi mbele ya wenzao
na vilevile wanaposimulia hadithi zao.
2. Uwajibikaji unafunzwa wanapojifunza kutekeleza kazi wanayopewa na mwalimu.
3
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Uhusiano na maswala ya matambuko
a. Stadi za maisha zinaendelezwa wanapojifunza kujithamini na kuwa jasiri.
Aidha, wanajifunza kuthaminiana na kuheshimiana wanapofanya kazi na
wenzao katika vikundi.
b. Wanafunzi wanafanya mazoezi mbalimbali yanayokusaidia kimarisha viungo
vyao vya mwili na hivyo kimarisha afya yao.
Uhusiano na thamani za kitaifa
a. Heshima inakuzwa wanafunzi wanapothaminiana kwa kufanya kazi wakishirikiana
katika vikundi.
b. Uwajibikaji unaendelezwa wanaposaidia kwa kazia mbali mbali nyumbani
kama vile kupanga na ktandika vitanda au malazi yao. Aidha, wanadhihirisha
uwajibikaji kwa kuzingatia na kufanya kazi wanaopewa na mwalimu.
ch. Umoja unakuzwa kushirikiana na kufanya kazi pamoja katika vikundi.
d. Elimu kwa maendeleo endelevu inadumishwa katika ushirikiano wa kijinsiaa
darasani au michezoni. Aidha, inadhihirishwa kutokana na utumizi wa mifano
mipya ya kiteknolojia/kidijitali, mawasiliano na usari.
Uhusiano na masomo mengine
a. Mathematical Activities wanajigawa katika vikundi vya idadi maalum za
wanafunzi.
b. Environmental Activities wakitumia mazingira mbalimbali katika ujifunzaji
wa mada mbalimbali.
ch. Psychomotor Activities wakifanya mazoezi mbalimbali ya maundo ya mwili
pamoja na kutembea.
Shughuli zingine zisizo rasmi zinazoweza kuchangia ujifunzaji
1. Wanafunzi wanatoa maoni na masuala yanayowatatiza kwa kujieleza kwa wenzao
au wakubwa wao.
2. Wanafunzi wanashiriki katika mwasilisho ya kisimulizi kwa wazazi au walezi
wao.
3. Wanafanya mazoezi ya kuelezana au kusoma wakiwa katika jozi ndani na nje ya
darasa.
4. Wanafunzi wanafana mazoezi ya kuandika ndani na nje ya darasa,
Mapendekezo ya huduma za kijamii katika ujifunzaji
1. Wanafunzi kukasiri maoni ya masuala ya mtambuko.
2. Wanafunzi kufanya mazoezi ya kutumia lugha katika shughuli za kijamii.
3. Wanafunzi kufanya mazoezi ya kusoma wakiwa katika jozi na maraki wao.
4
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
4. Wanafunzi watengenezea orodha za vitu k.v. bidhaa za kununua na kuwapa wazazi
wao. Aidha, wanajaribu kutoa maombi mepesi katika orodha zilizoandikwa.
Nyenzo za kujifunzia
Vifungu vya ufahamu vya kusikiliza, vifaa vya kusikiliza na kuona/rekoda, vielelezo,
picha za matukio tofautitofauti, vitabu vya hadithi, magazeti, majarida, vifaa vya
kuandika, stenseli, kadi na michoro ya kuonyesha namna maneno yalivyotumika
katika mti wa maneno.
Tathmini zinazopendekezwa
1. Mwalimu atoe mada ambazo zitakuwa msingi wa mazungumzo.
2. Maswali/jibu na kuonyesha uwezo wa kufuata maagizo.
3. Wanafunzi wasimulie upya kile walichosoma, kuuliza au kujibu maswali.
4. Tathmini ya wenza, maswali/majibu, kusimulia upya hadithi iliyosomwa.
5. Andika aya fupi kuhusu mada yenye maudhui mahsusi.
Kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalum
Usaidizi kwa usomaji wa wenye uwezo
wa viwango tofauti
Usaidizi kwa usomaji wa wenye mahitaji
ya kipekee
Himiza wanafunzi wenye uelewa wa chini
kushiriki katika mazungumzo kama vile
uigizaji na usimulizi wa hadithi.
Wape wanafunzi wenye uelewa wa haraka
mazoezi ya ziada ili kuepuka kuwachosha
na kuzubaa darasani.
Wape wanafunzi wa viwango vyote viwili,
chini na juu, nafasi sawa za kushiriki
katika shughuli za darasani. Ni jukumu
lako kuhakikisha kwamba wanafurahiana
na kufurahia kukaa pamoja licha ya tofauti
zao.
Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
kabisa, wape breli, picha za kugusa na kwa
wale wasioweza kuona vizuri, wape matini
zenye maandishi makubwa.
Kwa wanafunzi wenye matatizo ya kusikia
tumia lugha ya ishara au ushirikishe
mkalimani wa lugha ya ishara.
Waruhusu wanafunzi ambao hawaoni mbali
waketi mbele darasani na wale wenye
uwezo wa kuona mbali waketi sehemu ya
nyuma.
Wape wanafunzi wenye ulemavu wa
viungo nafasi ambazo wanaweza kuigiza
kama za mwalimu mkuu au mzee wa kijiji.
Wape msaada wa kutosha na uhakikishe
wanafunzi wenzao wamefanya hivyo, kama
kwa kusukuma kitimaguru cha mwanafunzi
mwenye ulemavu.
5
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Wiki ya 1
Mpangilio wa masomo
Somo la 1: Kusikiliza maagizo
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kusilikiza maagizo mepesi yenye
mfululizo kwa makini.
Habari za kimsingi
Somo hili litawawezesha wanafunzi kufanya mazoezi ya kusikiliza na kujibu ifaavyo
katika mazungumzo. Haya yatachangia stadi za kusikiliza, hasa zilizo katika Somo
la 1 (Kusikiliza maagizo na maswali). Mwalimu anapaswa kuwaeleza wanafunzi
umuhimu wa kusikiliza kwa makini ili waelewe dhana ya kutumia vidokezo visivyo
vya kiuneni, kuwasiliana kwa kuangaliana na kupishana zamu katika mawasiliano.
Baadaye, wanafunzi wanapaswa kumsikiliza mwalimu na kufuata maagizo
waliyopewa. Tia juhudi kuingiza matumizi ya kanda za rekodi za sauti na picha ili
wanafunzi wasikie waziwazi ujumbe unaotolewa.
Nyenzo za kufunzia
Video au kanda za sauti
Picha
Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 1-3
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi wasikilize unapoimba wimbo ulio kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1 kuhusu viungo vya mwili. Uliza darasa zima
kushiriki kuimba wimbo pamoja. Kwa utaratibu ufaao, mwalimu anapaswa kuigiza
vitendo katika wimbo kwa kugusa viungo mahususi vya mwili. Waongoze wanafunzi
katika jozi kuimba wimbo ulio katika Zoezi la 1, ukurasa wa 1; Kichwa, mabega,
magoti na vidole... Washirikishe wanafunzi katika mjadala wa namna mtu anaweza
kutoa maagizo kwa wengine kutekeleza tendo fulani. Hatua kwa hatua, toa majibu na
maoni kuhusu yale yanayopaswa kufanywa na maendeleo ya utendaji wa wanafunzi.
Ikiwa unaweza kutumia kanda iliyorekodiwa, wachezee ili wanafunzi wasikilize
maagizo mbalimbali yanayotolewa katika gwaride, wakati wa upishi nyumbani au
katika mazoezi uwanjani.
6
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Waelekeze wanafunzi kuchunguza picha ilivyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 2. Wanafunzi wajadili katika makundi yale wanayoona na kukisia kile
wale watu wawili wanazungumzia. Zoezi hili litaendeleza uwezo wa wanafunzi
kutumia utungaji na ubunifu. Waelekeze katika kupata maagizo na majibu kutoka
kwenye picha. Hili litachangia stadi za kimsingi kama mawasiliano na ushirikiano.
2. Waulize wanafunzi kusema kwa nini wanadhani ni lazima Juma amuage mamake.
Waongoze wanafunzi katika kujibu maswali ya kujibu kwa mdomo ambalo
ni zoezi la ziada la kusikiliza maagizo/maswali na kujibu ipasavyo. Zoezi hili
litachangia uwazaji makinifu na usuluhishaji wa matatizo.
3. Waelekeze wanafunzi katika uigizaji wa mazungumzo baina ya Juma na mamake.
Hili litaendeleza umoja na ushirikiano.
Majibu yanayotarajiwa, ukurasa 3
1. Kwenda shuleni bila kusimama mahali popote.
2. Usipigane.
3. Usipige kelele darasani.
4. Kamilisha kazi yako ya darasani kwa wakati ufaao.
5. Tii walimu.
6. Rudi nyumbani moja kwa moja utokapo shuleni.
4. Washirikishe wanafunzi katika kufanya mazoezi ya kusikiliza maagizo na kujibu
ipasavyo kwa wakubwa wao ili kuendeleza mawasiliano fanikifu.
5. Simamia maigizo na kuwahimiza wanafunzi kuuliza maswali panapofaa, jambo
linalokuza ari ya kufanya kazi pamoja
6. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki vilivyo. Hili litakuza mawasiliano na
ushirikiano miongoni mwa wanafunzi na kukuza maadili kama vile matumizi ya
maneno ya adabu, heshima na ushirikiano wanapotangamana ndani na nje ya
darasa.
Hitimisho
Waulize wanafunzi kutaja baadhi ya mambo ambayo sharti wayafanye wanapomsikiliza
mtu akiwapa maagizo. Panua majibu yao kwa kuuliza zaidi au kuunda upya jibu. Huku
ukitumia mifano mwafaka, waeleze kuwa baadhi ya ishara zisizo za kiuneni hutumiwa
kuwasilisha au kusisitiza ujumbe. Kusikiliza huhitaji kuwa makini na kuangaliana.
Tathmini
Katika jozi, wanafunzi wafanye mazoezi ya kusikiliza maagizo na kujibu ipasavyo.
7
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 2: Kuelewa ujumbe wa kiuneni na usio wa kiuneni
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia mawasiliano ya kiuneni na
yasiyo ya kiuneni katika mazungumzo.
Habari ya kimsingi
Somo hili linapaswa kuwaonyesha wanafunzi taarifa mbalimbali za kiuneni na
zisizo za kiuneni katika mazungumzo. Washirikishe wanafunzi katika kutoa mifano
ya taarifa mbalimbali za kiuneni na zisizo za kiuneni ambazo wanaweza kutumia
kujieleza katika mazungumzo yao ya kila siku. Shirikisha hapa kauli za adabu ambazo
hutumiwa katika mawasiliano yoyote mwafaka. Vidokezo visivyo vya kiuneni ni
kama vile kutikisa kichwa, kuashiria kukubali kwa kichwa, kukunja uso, kufunga
macho na kuinua kidole cha gumba vitumike. Wape wanafunzi muda wa kutosha wa
kufanya mazoezi ya kutumia ishara mbalimbali na kuwakosoa inapostahili. Ingawa
somo hili litachangia stadi za kusikiliza katika Mada ya Somo la 1.1 (Kusikiliza),
juhudi zifanywe kushirikisha stadi za kuzungumza, kuandika na kusoma katika somo
kwa kutumia miktadha faafu.
Nyenzo za kujifunzia
Chati
Picha
Rekodi
Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 3-5
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuuliza wanafunzi kama wamewahi kumsikia mtu yeyote akitoa
maagizo shuleni au nje ya shule.
Wanafunzi waelezane waliyowahi kusikia, katika kundi dogo. Waelekeze wanafunzi
mahsusi kufafanua taarifa za kiuneni na zisizo za kiuneni kutokana na mjadala.
Orodhesha majibu yao ubaoni.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waongoze wanafunzi katika kuchunguza michoro iliyo katika Kitabu cha
Mwanafunzi ukurasa 3.
8
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
2. Wape wanafunzi mazoezi mbalimbali yasiyo ya kiuneni na uwaombe waonyeshe.
3. Waombe wanafunzi wanne, mmoja baada ya mwingine kusema wanachoona katika
picha zilizo katika Kitabu cha Wanafunzi ukurasa 3. Waombe wanafunzi kueleza
kuhusu miktadha, ambapo stadi kama kujiamini katika utekelezaji huendelezwa.
4. Katika jozi, wanafunzi waonyeshe baadhi ya ishara kisha wajaribu kubashiri zina
maana gani. Hili litachangia uwazaji kwa makini na usuluhishaji wa matatizo.
5. Ili kuendeleza ari ya kuwa pamoja na kujiamini katika utekelezaji, sikiliza majibu
anuwai ya wanafunzi ukihakikisha kuwa kila mwanafunzi ameshiriki. Wapongeze
kwa majibu sahihi ili kuwahamasisha na utamke bayana kwa darasa ili wapate
majibu sahihi.
Majibu;
Zoezi la 1, ukurasa 3-4
1. Mvulana akilia kwa sababu ya maumivu ya tumbo.
2. Msichana akiendesha gari.
3. Msichana akionyesha namna ya kupika chakula katika chungu.
4. Mvulana akionyesha namna ya kusherehekea baada ya kushinda shindano la
mbio.
Zoezi la 2, ukurasa 4-5
1. Wanafunzi wacheze mchezo wa lugha ya ishara wakiwa katika makundi
madogo.
2. Katika jitihada za kuendeleza thamani za uwajibikaji na heshima, wanafunzi
wasimame, mmoja baada ya mwingine, kuonyesha ishara huku wengine
wakikisia anachosema mwenye kutoa ishara.
Majibu
a. Salamu, kwaheri
b. Kimya
c. Kukubali
d. Kuwaza
3. Mwalimu atathmini matendo ya wanafunzi
4. Mwalimu atathmini uigizaji wa wanafunzi
6. Waelekeze wanafunzi watoe ishara nyingine na kuonyeshana katika jozi. Ishara
hizi ni kama vile;
1. Kufungua kinywa (woga)
2. Kutikisa kichwa (kukataa katakata)
3. Kuzungusha kidole cha shahada (harakisha/maliza)
4. Kushika pua (harufu)
9
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi zaidi
1. Waulize wanafunzi wawili waonyeshe ishara zilizoelezwa hapo juu. Wanafunzi
wengine watazame na kutoa maoni au kuuliza maswali kuhusu maonyesho ya
wenzao. Zoezi lote litachangia umoja na ushirikiano miongoni mwa wanafunzi.
2. Somo hili litaendeleza stadi za maisha za kujuana na kuishi na wanafunzi wengine
kupitia mawasiliano fanikifu. Hivyo, hakikisha kila mwanafunzi anashiriki katika
zoezi hili ili kuchangia katika mawasiliano, utangamano na umoja.
Hitimisho
Wanafunzi wataje taarifa za kiuneni na zisizo za kiuneni ambazo wamejifunza.
Waeleze kuwa mtu anapotumia taarifa zisizo za kiuneni anapaswa kuwa makini ili
asieleweke visivyo. Waonyeshe kuwa ni muhimu kuteua na kutumia maneno yenye
adabu wanapozungumza na watu wengine.
Zoezi la kufanyia nyumbani, ukurasa 5
1. Mwalimu atathmini uigizaji wa wanafunzi.
2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
3. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 3: Kukisia majibu yanayotolewa
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kukisia majibu yaliyotarajiwa kutoka
katika mazungumzo ya adabu.
Habari za kimsingi
Somo hili linapaswa kuwaonyesha wanafunzi namna ya kushiriki katika mazungumzo
ya adabu na majibu yanayotarajiwa.
Nyenzo za kujifunzia
Chati
Picha
Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 6-7
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kuangalia picha ambazo zimo katika
Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 6. Waulize wakisie mazungumzo yanayoendelea
baina ya mwalimu na msichana.
10
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Ili kuendeleza stadi za mawasiliano na ushirikiano za wanafunzi, wakiwa katika
makundi madogo, wanafunzi wataje wanachoona katika kila picha.
2. Waelekeze kwenye picha huku ukipata makisio yao.
3. Waulize wanafunzi kuigiza mazungumzo baina ya Sara na mwalimu.
4. Waagize wanafunzi kujaza mapengo katika Zoezi la 2. Watoe majibu kwa zamu.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa 6
1. ingia
2. msamaha
3. chelewa
Zoezi la 3, ukurasa 7
1. Mwalimu atoe maagizo.
2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
3. Mwalimu atathmini uigizaji wa wanafunzi.
4. Mwalimu atathmini uigizaji wa wanafunzi.
5. Somo hili litachangia stadi za maisha za kujua na kuishi na wanafunzi wengine
kupitia mawasiliano fanikifu. Kwa hivyo, hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
ili kuendeleza mawasiliano, ushirikiano na umoja.
Hitimisho
Sisitiza kwa wanafunzi umuhimu wa kutumia lugha ya adabu. Hili litakuza thamani
kama umoja na heshima.
Tathmini
Andika baadhi ya maneno ya adabu ambayo yametumika katika taarifa yoyote ya
kurekodiwa kama namna ya kuendeleza ujuzi wa mifumo ya kidijitali.
Somo la 4: Mimi ni nani
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuandika maneno na sentensi ifaavyo.
11
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari ya kimsingi
Somo hili linapaswa kuwaonyesha wanafunzi namna mbalimbali za kuunda na kuandika
maneno na sentensi. Shirikisha wanafunzi katika mazoezi ya kujaza na kukamilisha
mapengo ili kuunda maneno na sentensi kamili. Hili lihusishe pia kauli za adabu
ambazo hutumiwa katika mawasiliano bora. Upange muda wa kutosha wanafunzi
wafanye mazoezi anuwai ya kuunda maneno mapya na kutunga sentensi sahihi.
Japo somo hili litazingatia stadi za kusilikiza zilizo katika Somo la 4.1 (Kuandika),
juhudi zifanywe kuhakikisha stadi nyingine kama kusikiliza, kuzungumza na kusoma
zimeshirikishwa katika somo.
Nyenzo za kujifunzia
Chati
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 7-8
Utangulizi
Tanguliza somo kwa mbinu ya maswali na majibu. Waombe wanafunzi mahsusi
kueleza wanayojua kuhusu maneno na sentensi. Eleza bayana ili wanafunzi waelewe
kuwa sauti huunda maneno na maneno huunda sentensi. Sentensi yaweza kuundwa
kwa neno moja au zaidi. Sentensi lazima iwe na kiima na kiarifu.
Shughuli za kujifunzia
1. Waongoze wanafunzi katika kuchunguza michoro uliyo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 7.
2. Ili kunoa stadi ya kimsingi ya utungaji na ubunifu, waulize wanfunzi mahsusi
kusema kile wanachoona katika kila picha.
3. Mwalimu aandike mifano ya orodha za maneno na sentensi zilizokitwa katika
picha zile.
4. Kwa zamu, wanafunzi wasome maneno/sentensi zilizoandikwa ili kuchangia stadi
ya kimsingi ya mawasiliano na ushirikiano.
5. Wanafunzi waimbe (wimbo katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 8 Zoezi la
2). Zoezi hili litachangia stadi za mawasiliano na pia kuendeleza thamani za
kushirikiana/muungano na umoja.
6. Waongoze wanafunzi kufanya mazoezi ya kujaza mapengo. Angalia, sahihisha
na kutoa majibu mara moja. Wapongeze kwa majibu sahihi ili kuwahamasisha
wanafunzi na uandike majibu vizuri ubaoni ili darasa zima lione majibu mwafaka.
12
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Majibu sahihi, zoezi la 3, ukurasa 9
1. a) Daktari
b) Mkulima
c) Dereva
d) Mwalimu
2. a. daktari
b. muuzaji duka
c. askari polisi
d. fundi wa nguo
Zoezi la kufanyia nyumbani, ukurasa 9
1. Katika makundi madogo, waongoze wanafunzi kutunga sentensi wakitumia
maneno yaliyotajwa hapo juu
Mifano ya sentensi
1. Mimi sipendi kwenda kumwona daktari.
2. Mimi hupenda kununua mkate kutoka kwa muuzaji duka.
3. Askari polisi wanapenda kuwasaka wezi.
4. Fundi wa nguo ameshona nguo maridadi.
2. Somo hili litachangia stadi za maisha, utungaji, uwazaji makinifu na kujiamini
katika utekelezaji wakati wanafunzi wanashiriki katika kuunda maneno na sentensi
kwa mawasiliano fanikifu. Kwa hivyo, hakikisha kila mwanafunzi anashiriki ili
kuendeleza mawasiliano, ushirikiano na umoja.
Hitimisho
Wanafunzi wataje maneno kutoka mazingira yaliyowazunguka. Waongoze katika
kutunga sentensi wakitumia maneno ambayo wamesomewa. Waeleze kwa kusisitiza
kuwa mtu anapaswa kuwa makini akitunga sentensi ili asikose kueleweka vilivyo.
Waonyeshe kuwa ni vizuri kila wakati kutunga sentensi fupi. Sentensi zinapaswa
kuanza kwa heru kubwa na kuisha kwa nukta.
Tathmini
Andika majina matano ya vitu vinavyopatikana nyumbani.
Somo la 5: Masomo ya kuchangamsha kama maagizo
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, wanafunzi waweze kufurahia masomo yao huku wakisikiliza
maagizo.
13
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Somo hili litawapa wanafunzi fursa ya kufurahia somo wakisikiliza na kufuata
maelezo yanayotolewa na mwalimu.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 9-10
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaomba wanafunzi kushiriki katika zoezi lililo hapa chini.
Wanafunzi wasikilize na kufuata maagizo.
Shughuli za kujifunzia
1. Waagize wanafunzi kushiriki katika zoezi hili. Wanapaswa kufuata maagizo
ipasavyo.
Zoezi
Maria akisema msimame, wasichana wote wanapaswa kusimama. Maria akisema
mketi, wasichana wote waketi chini.
Yohana akisema msimame, wavulana wote wasimame. Yohana akisema mketi, wavulana
wote waketi chini.
2. Mwalimu anapaswa kuongeza kasi anapotoa maagizo aone ni wanafunzi wepi
watatatizika.
3. Waruhusu wanafunzi kucheka na kufurahia somo.
Hitimisho
Wasisitizie wanafunzi umuhimu wa kusikiliza kwa makini maagizo yakitolewa.
Tathmini
1. Waulize wanafunzi kuandika maagizo ambayo wanapaswa kufuata wanapovuka
barabara.
2. Waagize wanafunzi kujaza majibu sahihi ya maswali yaliyo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 9-10.
Majibu, ukurasa 9-10
1. nitakuuma
2. nitakukimbiza
14
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
3. nitakumeza
4. nitakuna
5. nitakudunga
6. tutakuuma
7. nitakuumiza
8. mgonjwa
9. utavunjika
10. kivuko cha barabara
Zoezi la kufanyia nyumbani, ukurasa 11
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Wiki ya 2
Somo la 1: Kuonyesha kuelewa maswali na maagizo
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuuliza maswali kufatuta ubayana wa
maagizo
Habari za kimsingi
Katika somo hili, wanafunzi watadhihirisha ufahamu wa maswali yatakayoulizwa
na wajibu kwa njia mwafaka na kutafuta ubayana wanapokosa kuelewa maswali.
Washirikishe wanafunzi katika mazoezi mengi ya aina hii.
Nyenzo za kujifunzia
Chati ya maneno
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuinua chati za maneno zenye maneno yafuatayo: nini, nani, lini,
kwa nini. Maneno haya yanaweza kutumiwa kutafuta ubayana katika mazungumzo au
marudio na mnenaji iwapo mwanafunzi amepitwa na hoja fulani katika mazungumzo
ya mnenaji.
Njia za kufunzia
1. Soma mazungumzo yaliyo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11 ili
kuwapa mfuatano wa namna watakavyoyasoma.
2. Waweke wanafunzi katika jozi wakifanya zoezi hili ili kuchangia ushirikiano
15
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
kisha uwaagize kucheza mchezo huo. Mwambie mwanafunzi mmoja asome
sentensi ya kwanza na wa pili aulize swali la kutafuta ubayana.
3. Waambie wanafunzi wabadilishane nafasi na kufanya zoezi walilofanya
nambari 2.
4. Waambie wanafunzi watunge sentensi sahili wakitumia maneno kwenye
jedwali wakiwa katika jozi na kucheza mchezo wenyewe. Kwa mfano:
Ngamia ana nundu.
Ana nini?
Nundu
Nilibebwa na ngamia.
Na nini?
Ngamia
Hitimisho
Kamilisha somo kwa kuuliza jozi za wanafunzi kusoma sentensi walizotunga kutoka
kwa Zoezi 2 katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11 kuhakikisha walitunga
ilivyostahili.
Tathmini
Wape wanafunzi maswali yafuatayo na uwaambie waandike majibu katika madaftari
yao.
1. Bi. Kamau anaenda nyumbani.
Nani?
Bi. Kamau
Hatuwezi kwenda nje kucheza kwa sababu mvua inanyesha.
Kwa nini?
Kwa sababu mvua inanyesha.
Nipatie kikombe.
Nini?
Kikombe
Somo la 2: Kudhihirisha ufahamu wa maswali na maagizo
Lengo mahsusi ya somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kudhihirisha hamu ya kujibu maswali
na kufuata maagizo.
16
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Wanafunzi watadhihirisha kuwa wanaelewa maswali wanayoulizwa kwa kuyajibu
kwa nja mwafaka. Wanafunzi hivyo basi wataweza kufuata maagizo yaliyotolewa
kwa kutoa majibu yanayotarajiwa kama walivyoagizwa.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, rangi, penseli
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11-13
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuuliza wanafunzi kadhaa kusoma majibu yao kwa zoezi la Somo
la 1. Waambie wabadilishane vitabu na kuthibitishiana kazi zao unaposoma majibu.
Njia za kufunzia
1. Waambie wanafunzi wasome mazungumzo baina ya Kami na ngamia yaliyomo
katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 12-13 wakiwa katika jozi.
2. Mmoja asome nafasi ya Kami na mwingine asome ya ngamia.
3. Waambie wabadilishane zamu. Mwanafunzi aliyesoma nafasi ya Kami sasa
asome ya ngamia na kinyume chake. Zoezi hili litachangia umoja wa wanafunzi.
4. Waambie wanafunzi wajaze maneno ambayo yameachwa.
5. Waagize wanafunzi kuchora picha ya ngamia na kuipaka rangi.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi wabadilishane vitabu na kuangalia picha
za ngamia zilizochorwa na wenzao na kutoa maoni.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuchora mipira mitano ya kijani kibichi, vikombe vitatu vyekundu
na kiatu cha buluu.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 12-13
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 13
1. mirefu
2. nundu
3. shingo
Zoezi la 3, ukurasa 13
Mwalimu atathmini michoro ya wanafunzi
17
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 3: Kusoma
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo mwanafunzi aweze kuuliza maswali kuthibitisha na kupanua
ufahamu wake wa matini itakayosomwa.
Habari za msingi
Mwanafunzi atasoma, atauliza na kujibu maswali kutoka kwa hadithi au kifungu
kitakachosomwa.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 14-15
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi kubadilishana vitabu na kuangalia
zoezi la somo lililotangulia. Zunguka darasani ukihakikisha kuwa kila mwanafunzi
alikamilisha zoezi lile ipasavyo.
Njia za kufunzia
1. Waagize wanafunzi kusoma hadithi iliyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi
wakiwa katika jozi na wajibu kwa sauti maswali yanayofuatia. Hili litachangia
ushirikiano wa wanafunzi na umoja wanapotumia vifaa vya kusoma pamoja.
2. Waambie wachore picha ya bata na kutia rangi.
Majibu ya maswali katika zoezi la 2, ukurasa 15
1. Mama Bata
2. Wanane
3. Kaka Bata
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi kusoma majibu yao wakiwa katika jozi.
Waulize kama majibu yao yanafanana.
Tathmini
Waulize wanafunzi kusoma ukurasa mmoja wa kitabu cha hadithi watakachochagua
na kuzua maswali na kuyajibu.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa 15
Mwalimu atathmini michoro ya wanafunzi.
18
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 4: Kuzungumza kuhusu picha
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia vidokezi mwafaka visivyo vya
kiuneni kuonyesha ufahamu wa maswali na maagizo.
Habari za msingi
Wanafunzi wanatarajiwa kuweza kufuata maagizo ambayo si ya kiuneni kama vile
sheria au maagizo ambayo yameandikwa kwenye mabango au bodi za kutangazia.
Vifaa vilivyopendekezwa
Vitabu, makundi ya sentensi, chati za manila
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16-18
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kubadilishana vitabu na kuangalia kazi
za wenzao. Waagize waseme iwapo kuna mwenzao ambaye hakufanya zoezi. Hili
litawafunza kuwawajibikia wenzao.
Njia za kufunzia
1. Waonyeshe wanafunzi makundi ya sentensi zifuatazo
Usile chakula ukiwa ndani ya choo.
Usitembee nyasini.
Usipige kelele.
2. Waagize wanafunzi kusoma sentensi hizo kwa sauti.
3. Waonyeshe wanafunzi chati zifuatazo:
Chati ya mwanamume akitembea kwenye uwanja uliojaa nyasi badala ya
vichorochoro vya kutembelea.
Chati ya wanafunzi wakisoma vitabu vya hadithi maktabani.
Chati ya wanafunzi wakila chakula katika chumba cha maakuli shuleni.
4. Waagize wanafunzi kulinganisha chati na sentensi ulizowaonyesha. Fanya
zoezi hili katika darasa na uteue wanafunzi watakaojitolea kujibu.
5. Waambie wanafunzi wachunguze na kujadili picha zilizo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi ukurasa 16. Zoezi hili litachangia stadi za ushirikiano na
mawasiliano za wanafunzi wanapojadili picha na maagizo katika vitabu vyao
6. Waagize wanafunzi kubaini maagizo katika kila picha na wayaandike. Hili
litaboresha stadi za maisha za mwanafunzi za kujua na kuishi na wengine
kwa vile wanaweza kutambua maagizo ya kufuata kanuni.
7. Waagize wanafunzi kuandika matatizo yaliyomo kwenye kila picha. Zoezi
19
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
hili litachangia uwezo wa wanafunzi wa uwazaji makinifu na usuluhishaji
matatizo kwa vile watajua namna ya kujibu maagizo katika maisha yao ya
kila siku kwa vile wanaweza kutambua matatizo yaliyomo kwenye picha.
8. Tafuta mahadhi mwafaka ya kuimba wimbo ulio katika Zoezi la 2 katika
Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 17 na uwaambie warudie ukiimba. Kisha
uwaambie waimbe wakiwa peke yao.
9. Waulize kubaini maswali na majibu kwenye wimbo wakiwa katika makundi.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaeleza wanafunzi wawe wakisikiliza maagizo kwa sababu
itawasidia kuepuka matokeo ambayo yanaweza kuwadhuru wakati mwingine.
Waambie waulize maswali ikiwa wanahisi hawakuelewa baadhi ya maagizo.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika maagizo matano ambayo wameyaona katika mazingira
yao kwenye mikebe ya vyakula, maduka makuu na uwanja wa shule au hospitali.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 16
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 17
Mwalimu atathmini kukariri kwa wanafunzi.
Somo la 5: Kuandika kuhusu mnyama umpendaye
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia maneno na virai vya kawaida
kutunga sentensi sahili.
Habari za msingi
Wanafunzi watumie maneno ambayo wanajua tayari kutunga sentensi katika hati
nadhifu na inayosomeka na kuunda sentensi kwa njia sahihi wakitumia tahajia ifaayo,
viakishi mwafaka kama vile nukta na koma.
Vifaa vilivyopendekezwa
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 18
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi ikiwa wana wanyama wawapendao
nyumbani. Waulize wanafunzi wachache walio nao wanyama hawa ni wepi,
wanawapendea nini na wanakula chakula gani. Kwa wanafunzi ambao hawana,
20
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
waulize wangetaka kuwa na wanyama-pendwa gani, majina ambao wangewapa na
kwa nini.
Njia za kufunzia
1. Waagize wanafunzi kuandika sentensi sita kuhusu wanyama-pendwa wao au
wale ambao wangetaka kuwa nao.
2. Waambie wanafunzi wasome sentensi zao katika makundi na kusema ni kipi
kinawapendeza kuhusu wanyama-pendwa wa wenzao katika makundi.
3. Uliza kila kikundi kuteua mmoja wao ambaye atasoma sentensi zake kuhusu
mnyama-pendwa wake kwa darasa. Hakikisha kuwa wanafunzi wanazingatia
usawa wa jinsia na ushirikisho katika uteuzi wao. Kwa wanafunzi ambao
watakuwa wakisoma kwa lugha ya ishara, tafuta mkalimani wa kuwatafsiria
wenzao darasani.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wanawatendea haki wanyama.
Wahimize kuwatendea wema wanyama na kuwatunza vilivyo.
Tathmini
Waagize wanafunzi kutunga sentensi sita kuhusu chakula wakipendacho.
Wiki ya 3
Somo la 1: Kutamka maneno kwa usahihi
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutamka maneno kwa ufasaha.
Habari ya msingi
Somo litawawezesha wanafunzi kufanya mazoezi ya stadi za kusikiliza na kuzungumza
wanapotamka maneno waliyopewa na mwalimu kwa ufasaha.
Nyenzo za kujifunzia
Kadi
Maleba
Vifaa vya kuigizia
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 19
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwapa wanafunzi kadi zilizo na maneno ambayo ni magumu
kutamka. Waambie wasome maneno hayo katika makundi.
21
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Njia za kufunzia
1. Waagize wanafunzi kutamka maneno yaliyo kwenye kadi wakiwa katika
makundi. Waongoze wanapotatizika. Wanafunzi watapata thamani kama vile
heshima na umoja wanapofanya kazi pamoja. Stadi zao za ushirikiano pia
zitakuzwa.
2. Waagize wanafunzi kuigiza mazungumzo kati ya Lonyangapuo na Nemayian.
3. Waongoze katika kutamka maneno kwa ufasaha. Wanapotamka maneno yale,
stadi zao za mawasiliano zitaendelezwa.
Hitimisho
Waulize wanafunzi kusoma maneno kwa sauti na uwaongoze katika kufanya
marekebisho.
Tathmini
Waambie wanafunzi kuandika maana ya maneno magumu. Pia wayafahamu vilivyo
maneno hayo.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 19
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 19
Mwalimu atathmini maigizo ya wanafunzi.
Somo la 2: Kusoma katika jozi
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutoa maoni kuhusu kasi na ufasaha wa
usomaji wa mwanafunzi mwenza.
Habari za msingi
Wanafunzi watafanya mazoezi ya kusoma kwa ufasaha. Zingatia matamshi yao na
uwahimize kusoma kwa sauti inayosikika.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 20-21
Utangulizi
Waagize wanafunzi kubadilishana vitabu vyao na kusoma sentensi za wenzao za zoezi
lililotangulia. Wateue wanafunzi wawili wenye uwezo wa chini na mwingine mmoja
kusoma sentensi zao mbele ya darasa.
22
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Njia za kufunzia
1. Waagize wanafunzi kusoma hadithi katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa
20-21 wakiwa katika jozi. Mwagize kila mwanafunzi kuzingatia matamshi ya
mwenzake na kuyakosoa inapostahili. Hili litawafunza thamani ya kuwajibika
wanapojitolea kuboresha usomaji wa wenzao.
2. Wahimize wanafunzi kuuliza iwapo hawana hakika ya matamshi ya neno. Zoezi
hili litachangia usomaji na wenza wanafunzi wanaposhirikiana kukamilisha
zoezi kwa mawasiliano na ushirikiano.
3. Waagize wanafunzi kuigiza mazungumzo yale katika makundi. Stadi za
maisha za wanafunzi za kujua na kuishi na wengine kupitia mawasiliano
fanikifu zitachangiwa na zoezi hili wanafunzi wanapojaribu kuwasilisha kwa
uhalisi namna mazungumzo yalivyotokea. Wataweza kutumia ujuzi huu katika
nyanja nyingine maishani mwao.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi kutumia viakishi walivyopewa katika
usomaji na mazungumzo yao kwa mawasiliano fanikifu.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika mazungumzo baina yao na maraki zao wa dhati
na kubadilishana daftari zao na kusoma mazungumzo yale. Simamia zoezi hili
kuhakikisha kila mwanafunzi analifanya. Zunguka katika madawati mbalimbali na
kumsikiliza mwanafunzi akisoma.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa 21
1. Kanisani
2. Kwenye kivuko cha barabara
3. Ni hatari sana kucheza barabarani
4. Kuangalia kulia, kushoto kisha kulia tena.
Zoezi la 3, ukurasa 21
Mwalimu atathmini maigizo ya wanafunzi.
Somo la 3: Kutabiri hadithi inahusu nini
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kufanya utabiri kabla na wakati wa
kusoma.
23
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Wanafunzi watachunguza picha katika hadithi na kukisia hadithi inahusu nini. Kisha
watasoma hadithi ili kuthibitisha makisio yao.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 21-23
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kutaja kile wanachopenda kuhusu usomaji
wa hadithi. Washirikishe katika mjadala kuhusu hadithi wazipendazo na kwa nini
wanazipenda.
Njia za kufunzia
1. Waulize wanafunzi kuchunguza picha iliyo katika hadithi iliyo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi ukurasa 21.
2. Waagize wanafunzi kujadili wanachokisia kuwa ndani ya hadithi. Wape nafasi
wanafunzi kadhaa kueleza wenzao makisio yao.
3. Waagize wanafunzi kusoma hadithi katika jozi. Zoezi hili zitaendeleza uwezo
wa wanafunzi wa kujiamini katika utendaji wanapoendelea kujenga imani
katika uwezo wao wa kusoma.
4. Waulize wanafunzi kama makisio yao yalikuwa kweli. Waulize wale
wanafunzi ambao makisio yao yalikuwa sahihi walichokuwa wamekisia na pia
uwaulize hata wale ambao makisio yao hayakuwa sahihi. Zoezi hili litakuza
stadi za maisha za wanafunzi za kujua na kuishi pamoja na wengine kupitia
mawasiliano fanikifu.
5. Waagize wanafunzi kujibu maswali yale kwa sauti wakiwa katika jozi.
Hitimisho
Waambie wanafunzi kadhaa kutoa majibu yao ya maswali kwa wenzao darasani.
Waruhusu wakubaliane au kutokubaliana na jibu na kutoa sababu za kufanya vile.
Tathmini
Waambie wanafunzi wateue kitabu cha hadithi, wachunguze picha na kukisia hadithi,
kisha wasome hadithi na kuthibitisha makisio yao.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 22
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 23
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
24
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la 3, ukurasa 23
1. Sungura na Kobe
2. Uwanjani
3. Kobe alimshinda Sungura kwa mbio
4. Kobe
Somo la 4: Kuunda maneno na kutunga sentensi
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia maneno na virai vya kawaida
kutunga sentensi sahili.
Habari za kimsingi
Wanafunzi wataandika maneno na virai vya kawaida ambavyo wamesoma kukia
sasa.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, kadi za maelezo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 23-24
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi kutaja maneno wanayoyajua. Kila
mwanafunzi apate nafasi ya kutaja neno moja na kueleza maana yake.
Njia za kufunzia
1. Waagize wanafunzi kupanga heru kuunda maneno wakiwa katika jozi.
2. Uliza kila mwanafunzi kuwasomea wenzao maneno waliyounda.
3. Waagize wanafunzi kuandika upya sentensi zilizomo katika Kitabu cha
Wanafunzi ukurasa 24 kutunga sentensi sahihi wakiwa katika jozi. Zoezi
hili litaendeleza mawasiliano na ushirikiano wa wanafunzi wanapofanya
mazoezi ya kushirikiana kama hilo la kupanga upya maneno kuunda sentensi.
4. Waambie wanafunzi wasome sentensi zao kama darasa.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaonyesha wanafunzi kadi zilizoandikwa maneno yafuatayo
na kuwaagiza wayasome kwa sauti.
1. Furaha
2. Huzuni
3. Asubuhi
25
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
4. Gari
5. Ruka
6. Tabasamu
7. Kimbia
8. Raki
9. Wikendi
10. Jumatatu
Tathmini
Waambie wanafunzi wapange upya sentensi zifuatazo ziwe sahihi.
1. naona na yangu mimi mama alikuwa furaha.
2. paka panya alikula yule.
3. nyumbani naenda mimi.
4. dadangu na mtoto juu wa huruka chini.
5. nala mimi embe.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 23
1. baba
2. Kitabu
3. rula
4. mwalimu
5. shule
Zoezi la 2, ukurasa 24
1. Mvulana hucheza mpira kila siku.
2. Mimi hupenda kula maembe.
3. Mbwa alimuuma paka.
4. Mti uliangukia nyumba kubwa.
5. Njeri na Akinyi ni maraki wa karibu.
Somo la 5: Kutunga sentensi
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kukuza uwezo wa kusoma akiwa
darasani na kwingineko.
26
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatunga sentensi mbalimbali kuwahusu na watu wa karibu. Chunguza
matumizi yao ya maneno na viakishi vya kawaida. Katika usomaji wao, hakikisha
wanatamka maneno kwa ufasaha.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, sentensi zilizoandikwa
Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 24-26
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi kutunga sentensi kuhusu watu walio
karibu nao.
Njia za kufunzia
1. Waambie wanafunzi wasome mazungumzo katika Kitabu cha Mwanafunzi
ukurasa 24 wakiwa katika jozi.
2. Waagize wanafunzi waandike sentensi nne kujihusu katika madaftari yao.
3. Wanafunzi wabadilishane vitabu na kusoma kuhusu wenzao. Hili litachangia stadi
za ushirikiano na mawasiliano wanafunzi wanapokuja pamoja kutekeleza lengo
la somo.
4. Waambie wanafunzi wasome mazungumzo katika zoezi la 2 katika Kitabu cha
Mwanafunzi ukurasa 25. Mwagize mwanafunzi mmoja asome maneno ya Otieno
na mwingine ya Kambua.
5. Waangize wanafunzi kutunga sentensi nne kuhusu raki yao. Wanafunzi wabadilishane
vitabu na kusoma sentensi za wenzao. Kusoma kwa kushirikishwa katika makundi
kutachangia kujiamini katika utekelezaji kwa mwanafunzi.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi kadhaa wawasomee wenzao sentensi zao.
Rekebisha sentensi panapostahili.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika sentensi tano kuhusu mwanafamilia mmoja.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 24
Mwalimu atathmini matamshi na majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 25-26
Mwalimu atathmini matamshi na majibu ya wanafunzi.
27
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Wiki ya 4
Somo la 1: Kutunga sentensi kwa kutumia nomino
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutunga sentensi akitumia nomino.
Habari za kimsingi
Somo hili litawaonyesha wanafunzi namna mbalimbali za kutunga sentensi sahihi
wakitumia nomino. Somo hili litashughulikia stadi za uandishi zilizo katika Mada
ndogo 4.1 (Uandishi) lakini juhudi zifanywe kushirikisha stadi nyinginezo.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kadi za maneno
Kitabu cha Mwanafunzi, 26-27
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kutaja vitu ambavyo wanaona darasani.
Waeleze wanafunzi kuwa vitu walivyotaja vinaitwa nomino. Kwa mfano, dawati, kiti,
meza, vitabu, kalamu, n.k. Toa kadi zilizoandikwa nomino na uwaagize wanafunzi
kuyachunguza.
Njia za kufunzia
1. Wakiwa katika jozi, waambie wachunguze maneno yaliyoandikwa kwenye kadi.
Wajadili maana ya maneno yale. Wanapofanya kazi pamoja wanaendeleza stadi
zao za mawasiliano na ushirikiano.
2. Waagize wanafunzi kuandika maana ya maneno yale katika madaftari yao.
3. Waongoze wanafunzi katika kutunga sentensi wakitumia maneno waliyoandika.
4. Waambie wasome aya yenye anwani Shule yangu’. Wasaidie kubainisha nomino
kwenye aya.
5. Waulize wanafunzi binafsi kupigia mstari nomino kwenye sentensi zilizomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 26-27.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa 26
1. Mosii,jina
2. Kaunti,Maweni
3. Mito, maziwa, kaunti ndogo
4. chakula, maduka, sokoni
28
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
5. Ng’ombe na mbuzi
6. Mahindi, maharagwe na mtama
6. Waongoze wanafunzi kuhakikisha kuwa wameelewa dhana.
7. Hakikisha kuwa kila mwanafunzi ameshiriki.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi kadhaa kusoma sentensi zao darasani.
Rekebisha sentensi panapostahili.
Tathmini
Waagize wanafunzi kutunga sentensi wakitumia nomino zilizomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi.
Kubali sentensi mbalimbali ambazo ni sahihi.
Somo la 2: Kutunga sentensi kwa kutumia vitenzi
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutunga sentensi kwa kutumia vitenzi.
Habari za kimsingi
Somo hili linapaswa kuwaonyesha wanafunzi namna mbalimbali za kutunga sentensi
sahihi kwa kutumia vitenzi. Somo litashughulikia stadi za uandishi katika Mada
ndogo 4.1 (Kuandika), lakini juhudi zifanywe kushirikisha stadi nyinginezo.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kadi za maneno
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 27-28
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kufanya vitendo ambavyo utawaelekeza
k.v. simama, keti na imba. Waeleze wanafunzi kuwa vitenzi ni maneno ambayo
hutueleza kuhusu kitendo k.v. simama, keti, imba n.k. Toa kadi ambazo zimeandikwa
vitenzi na kuwauliza wanafunzi kuchunguza maneno yale na kuonyesha matendo
yanayonuiwa.
Njia za kufunzia
1. Wakiwa katika jozi, waagize wanafunzi kusoma sentensi zilizo katika Kitabu
cha Mwanafunzi ukurasa 27. Waambie wazingatie maneno yaliyopigiwa mstari.
Waeleze kuwa maneno yaliyopigiwa mstari huitwa vitenzi. Wanafunzi wanapofanya
kazi pamoja, wanaendeleza stadi zao za mawasiliano na ushirikiano.
29
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
2. Waagize kujaza mapengo katika sentensi zilizotolewa pale.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa 28
1. nunua
2. cheza
3. omba
4. penda
5. funza
6. cheka
3. Hakikisha kuwa wanafunzi wameelewa dhana.
4. Jadili zoezi na wanafunzi.
5. Hakikisha wanafunzi wote wameshiriki. Hili litahakikisha kuna kushirikishwa
kwa kila mwanafunzi.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia waandike vitenzi vitano.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika aya kuhusu matendo ambayo wanafanya tangu kuamka
hadi wanapoenda shuleni.
Somo la 3: Kutunga sentensi kwa kutumia vitenzi
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutunga sentensi kwa kutumia vitenzi.
Habari za kimsingi
Hili somo litawaonyesha wanafunzi namna mbalimbali za kutunga sentensi sahihi
kwa kutumia vitenzi. Litaendeleza msingi uliowekwa katika somo lililotangulia
kuhusu kubainisha vitenzi. Litashughulikia stadi za uandishi katika Mada ndogo 4.1
(Kuandika), lakini juhudi zifanywe kushirikisha stadi nyinginezo.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 28
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kutaja vitenzi ambavyo wanaweza
kukumbuka kutokana na somo lililotangulia.
30
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Njia za kufunzia
1. Wakiwa katika makundi waulize wanafunzi kutaja vitenzi ambavyo waliandika
katika zoezi lililotangulia.
2. Waulize wanafunzi kutunga binafsi sentensi kutokana na vitenzi walivyopewa.
3. Waambie wanafunzi kadhaa wasome sentensi kwa sauti. Wakati wanafunzi
wanaposoma kwa sauti, stadi zao za mawasiliano zinaendelezwa.
4. Rekebisha matamshipanapostahili.
5. Waagize wanafunzi kuandika sentensi wakitumia vitenzi vilivyo katika Kitabu
cha Mwanafunzi ukurasa 28. Kubali aina mbalimbali za sentensi sahihi.
6. Hakikisha wanafunzi wote wameshiriki. Hili litahakikisha kuna ushirikisho wa
wanafunzi wote.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi kutunga sentensi ambapo wametumia
vitenzi ipasavyo.
Tathmini
Agiza kila mwanafunzi kuandaa kadi zenye orodha ya vitenzi.
Somo la 4: Kuandika maneno na sentensi kwa njia ifaayo
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuandika maneno na sentensi kwa njia
sahihi.
Habari za kimsingi
Katika somo hili waruhusu wanafunzi kutunga sentensi ainati kujihusu, watu walio
karibu nao na vitu ambavyo wameviona katika mazingira. Thibiti matumizi yao
ya maneno na viakishi vya kawaida. Katika kusoma kwao, hakikisha wanatamka
maneno kwa ufasaha.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, maandishi ya sentensi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 29
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwapa wanafunzi orodha ya maneno na sentensi zilizochanganyika.
Wambie wachunguze maneno na sentensi zile.
31
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Njia za kufunzia
1. Katika makundi, waulize waandike upya maneno na sentensi zile kwa njia sahihi.
Hili litaendeleza stadi za ushirikiano na mawasiliano ya wanafunzi wanapokuja
pamoja kutimiza lengo la somo.
2. Waambie wawakilishi wachache wa makundi kusoma sentensi kwa sauti darasani.
Kusoma kwa ushirika wa kikundi kutaendekeza kujiamini katika utekelezaji
kwa wanafunzi.
3. Waagize wanafunzi kuandika maneno yaliyotolewa katika Kitabu cha Mwanafunzi
ukurasa 29 katika heru kubwa.
Zoezi la 2, ukurasa 29
1. CHUPA
2. PAKA
3. BABA
4. KITI
5. MFUKO
4. Waagize kuandika upya sentenzi zilizochanganyika zilizo katika Kitabu cha
Mwanafunzi ukurasa 29.
Majibu yanayotarajiwa
1. Ninaandikia kitabu changu.
2. Mamangu anaitwa Jane.
3. Natembea kuelekea shuleni.
4. Jana ilikuwa Jumatatu.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi wachache wasome sentensi darasani.
Rekebisha sentensi panapostahili.
Tathmini
Waagize wanafunzi kutunga sentensi kuhusu wanyama-pendwa wao.
Somo la 5: Kutunga sentensi
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kupata ari ya kuandika kwa starehe.
Habari za msingi
Somo hili linapaswa kuwahamasisha wanafunzi kuwa na ari ya kuandika kwa starehe.
Waagize wanafunzi kuandika sentensi sahihi nyingi inavyowezekana. Waongoze
32
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
wanafunzi katika kutunga sentensi nyingi iwezekanavyo. Waongoze pia kuandika aya
za mada zinazowavutia. Zingatia matumizi yao ya maneno na viakishi vya kawaida.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, sentensi zilizoandikwa
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 30
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi wapitie sentensi walizoandika katika
somo lililotangulia kuhusu wanyama wawapendao. Waambie wabadilishane vitabu
na kusoma sentensi za wenzao wanaoketi nao. Kusoma kwa kushirikishwa katika
makundi kutachangia kujiamini katika utekelezaji kwa mwanafunzi.
Njia za kufunzia
1. Waagize wanafunzi kuandika aya ya mada inayowavutia wao wenyewe. Kisha
wabadilishane vitabu na wasome aya za wenzao.
2. Waambie wanafunzi wachache wajitolee kusoma aya kadhaa kwa sauti. Kusoma
kwa kushirikishwa katika makundi kutachangia kujiamini katika utekelezaji
kwa mwanafunzi.
3. Waambie wanafunzi waandike sentensi nne kuhusu maraki zao daftarini.
4. Wanafunzi wabadilishane vitabu vyao na kusoma kazi za majirani zao. Hili
litachangia stadi za ushirikiano na mawasiliano za wanafunzi.
Hitimisho
Hitimisha kwa kuwauliza wanafunzi wachache kusoma sentensi zao kwa wengine
darasani. Rekebisha sentensi panapostahili.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika aya fupi kuhusu chakula wakipendacho.
33
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Mada ya 1.0
Kusikiliza
Mada ya 2.0
Kuzungumza
Mada ya 3.0
Kusoma
Mada ya 4.0
Kuandika
Somo la 1.2
Uundaji za
maneno na
sentensi
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kutambua idadi
ya silabi katika
neno.
b) Kutambua
maneno
yaliyo sauti
zinazofanana.
ch) Kuunganisha
silabi kuunda
neno.
d) Kuwaunganisha
maneno kuunda
sentensi
nyepesi.
e) Kuonea
fahari silabi
zinazounda
maneno.
Somo la 2.3
Utambuzi wa
sauti/fonimu
Kukia mwisho
wa somo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kutambua
na kutamka
maneno
ya sauti
mwambatano
kuunda silabi
na maneno.
b) Kuunganisha
na
kuvunjavunja
silabi kuunda
maneno
ifaavyo.
ch) Kutumia
maneno
mwafaka
kutunga
sentensi fupi
zenye maana.
d) Kuonea
fahari
jukumu la
kuunganisha
na
kuvunjavunja
maneno
katika
kuunda
sentensi.
Somo la 3.2
Usomaji
kimakundi
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kusoma
maandishi kwa
jumla kwa
ufasaha, usahihi
na kuelewa.
b) Kukuza stadi
za kujifunza
pamoja na
wenzake na
kujitathmini.
ch)Kuimarisha
ujasiri kutokana
na kufaana na
wenzake katika
kusoma katika
makundi.
d)Kujenga ari ya
kusoma kwa
jumla ndani na
nje ya darasa.
Somo la 4.2
Maagizo ya
kutahiji/
maendelezo
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kuongeza idadi
ya maneno ya
kuandika na
kuyaendeleza/
kuyatahiji vizuri
ifaavyo.
b) Kutahiji au
kutamka
maneno yaliyo
na konsonanti
mbili mfuatano
na makundi
mbalimbali ya
konsonanti.
ch) Kutumia ufahamu
wa sauti kutahiji
au kuendeleza na
kuandika maneno
yanayofahamika
na
yasiyofahamika.
d) Kutumia uhariri
wa kimsingi
kusahihisha hijai
katika sentensi
sahili.
e) Kuonea fahari
umuhimu wa
maendelezo
mazuri katika
kuandika.
Sehemu
2
Lenana na Kantai wapata maji
34
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
a) Ujasiri unaendelezwa katika wanafunzi wanapojieleza mbele ya wenzao.
b) Wanakuza ushirikiano na mawasiliano katika kushirikiana katika vikundi.
Aidha, wanakuza uwezo wao wa kujieleza ama kwa kuandika au kuzungumza.
ch) Uwezo wa kukiri na kutatua matatizo unakuzwa kutokana na kubuni na
kujieleza na vilevile kupanga mawazo vizuri kwa uwasilishaji.
d) Uwezo wa kidijitali unahimizwa wanapotumia vifaa vya kidijitali kusikiliza
mazungumzo.
e) Umilisi wa kujifunza ujifunzaji unakuzwa kutokana na wanafunzi hawa
kufanya mazungumzo na wazazi au walezi wao.
f) Wanajifunza umilisi wa kusoma kwa kasi na mawasiliano bora ili wasisitesite
wakati wa kusoma.
Uhusiano na masuala mtambuko
a) Ujuzi wa kujua jinsi ya kuishi na watu wengine katika jamii unakuzwa
kutokana na kushirikiana vyema na wenzao katika makundi.
b) Stadi ya maisha inakuzwa ya kuweza kuwa raia mwema wa kushirikiana na
wengine.
Uhusiano na desturi na maadili ya jamii
a) Heshima itaendelezwa wakifanya kazi pamoja na wanafunzi wenzao.
b) Umoja utahimizwa kutokana na ushirikiano na wenzao au katika vikundi.
ch) Wanajifunza kuwajibika wakitekeleza majukumu waliyopewa ya kusoma na
kutambua sentensi katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
a) Mathematical Activities wanapojigawa katika vikundi.
b) English Activities katika mada ya silabi katika maneno.
Shughuli za kijamii zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
a) Wanafunzi wanawahusisha wazazi/walezi wao kuwasaidia kuunda maneno na
sentensi kutokana na sauti walizojifunza.
b) Wanafunzi wanawasomea wazazi/walezi wao na wanajamii wengine hadithi
fupifupi.
ch) Wanafunzi wanashiriki katika mashindano ya kusoma.
d) Wanafunzi kusoma maktabani wakati wao wa ziada.
e) Wanafunzi wanaandika orodha ya vitu k.v. orodha ya bidhaa za kununua na
kuwapa wazazi.
f) Kutoa maombi mepesi katika muundo wa maandishi.
35
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli nyingine zisizo rasmi zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
a) Wanafunzi wanafanya mazoezi ya kuimba nyimbo, vitanzandimi, mashairi nje
na ndani ya darasa.
b) Wanafunzi wanafanya mazoezi ya kutamka heru na wenzao ndani na nje ya
darasa.
ch) Wanafunzi wanafanya mazoezi kutoa maombi mepesi katika njia ya maandishi.
d) Kusomea maktabani wakati wao wa ziada.
Tathmini zinazopendekezwa
a) Zoezi la kutenganisha silabi na sauti katika maneno.
b) Kuunda maneno na sentensi.
ch) Tathmini za wenzake, maswali/majibu, kusoma hadithi.
Nyenzo za ujifunzaji zinazopendekezwa
Rekodi za sauti, chati kwenye karatasi ngumu, nyenzo za kusikia na video, vitabu
vya hadithi, chati, picha, vitabu vya kusoma, magazeti, majarida, kanda za sauti, kadi
mulishi za maneno, vitabu n.k.
Kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalum
Usaidizi kwa wanafunzi wenye
uwezo mbalimbali
Usaidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji
maalum
Himiza wanafunzi wenye uelewa
wa polepole kushiriki katika
mazungumzo kama maigizo na
kusimulia hadithi.
Wape wanafunzi wenye uelewa
wa haraka kazi nyingi ili kuepuka
kuwachosha na kuzubaa darasani.
Wape wanafunzi wenye uelewa
wa polepole na haraka nafasi
za kutosha katika shughuli
za darasani. Una jukumu
la kuhakikisha kwamba
wanafurahiana na kufurahia
kukaa pamoja licha ya tofauti
zao.
Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa kuona,
wape breli, picha za kugusa na wale
wasioweza kuona vizuri wape maandishi
makubwa.
Kwa wanafunzi wasio sikia vizuri tumia
lugha ishara au kumleta mtaalamu wa lugha
ishara kufasiri.
Wanafunzi ambao hawawezi kuona mbali
wakae mbele darasani na wenye uwezo wa
kuona mbali wakae nyuma.
Wape wanafunzi wenye ulemavu majukumu
wanayoweza kutekeleza kama vile kuigiza
nafasi ya mwalimu mkuu au balozi wa kijiji.
Wape usaidizi wa kutosha na kuhakikisha
kwamba wanafunzi wengine wanafanya
hivyo, kwa mfano, kuwasaidia katika
kusukuma kitimaguru kwa mwanafunzi
mlemavu.
36
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Mpangilio wa vipindi
Somo la 1: Unganisha na utamke
Matokeo maalum ya ujifunzaji.
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutambua idadi ya silabi katika neno.
Habari za kimsingi
Kipindi hiki kitawasaidia wanafunzi kukuza stadi za kusikiliza na kuzungumza, hasa
zile zilizo chini ya (Somo la 1.2 uundaji wa maneno na sentensi). Mwalimu awape
wanafunzi maumbo mwafaka ya heru na sauti ili watamke katika makundi, wakiwa
wawili wawili au akiwa peke yake. Jitahidi kuunganisha kusoma na kuandika katika
kipindi kwa kutumia miktadha ya kufaa.
Nyenzo za ujifunzaji
Chati kwenye karatasi ngumu
Kitabu cha Mwanafunzi, uku 31-32.
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi kusikiliza kwa makini unapowasomea
silabi na maneno katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Andika maneno yanayofanana na hayo katika chati kwenye karatasi ngumu. Tambua
silabi katika kila neno.
Hakikisha kwamba unajumuisha maneno yenye konsonanti mwambatano na vokali
pekee kama silabi zake.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waelekeze wanafunzi kusoma kwa sauti maneno katika zoezi la kwanza kwenye
Kitabu cha mwanafunzi ukurasa 31.
2. Wakiwa wawili wawili, waulize wanafunzi kutambua silabi katika kila neno.
3. Waelekeze wanafunzi kusoma hadithi fupi ya Paka wa Pati.
4. Tambua nomino katika kisa na kukiandika ubaoni kila moja na silabi zake.
5. Waagize wanafunzi kupiga mako baada ya kusikia kila sauti ikitamkwa.
6. Tamka kila silabi kwa sauti.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 31
Mwalimu atathmini usomaji wa wanafunzi.
37
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la 2, ukurasa 31-32
1. a) neti b) koti c) paka d) pesa e) boti
2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
3. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
7. Angalia kazi za vikundi na kuwahimiza wanafunzi kuuliza maswali ikihitajika.
8. Hakikisha kwamba kila mwanafunzi anashiriki. Hili litaboresha mawasiliano na
ushirikiano miongoni mwa wanafunzi na kukuza maadili kama vile heshima na
umoja wakitangamana darasani.
Hitimisho
Waulize wanafunzi kukupa idadi ya silabi katika maneno waliyosoma.
Tathmini
Waulize wanafunzi kutambua silabi.
Somo la 2: Kutambua maneno yaliyo na sauti zinazofanana
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutambua maneno yaliyo na sauti
zinazofanana.
Habari za kimsingi
Kipindi hiki kiwawezeshe wanafunzi kujua maneno mbalimbali yaliyo na sauti
zinazofanana. Wape wanafunzi muda wa kutosha kufanya mazoezi ya kutahiji au
kutamka maneno. Kipindi hiki kinashughulikia stadi za kusikiliza na kuzungumza
chini ya Somo la 1.1. Hata hivyo, juhudi zifanyike kuunganisha stadi za kusoma na
kusikiliza katika kipindi kwa kutumia miktadha mwafaka.
Nyenzo za ujifunzaji
Chati, kadi mulishi za maneno
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 33-34
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kutandaza chati za maneno yaliyo na sauti zinazofanana. Soma
maneno hayo kwa sauti huku wanafunzi wakisikiliza.
38
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Waelekeze wanafunzi kutazama michoro katika Kitabu cha Mwanafunzi
ukurasa 33-34 na uwaagize kuyasoma maneno hayo wakiwa wawili wawili
na peke yao.
2. Sikiliza matamshi yao ya awali huku ukihakikisha ushiriki wa kila mwanafunzi.
3. Waelekeze wanafunzi kusoma shairi kaika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 34
na uwaulize kusoma shairi hilo wakiwa wawili wawili kisha wasome kibinafsi.
Wanafunzi wanapofanya kazi pamoja wakiwa wawiliwawili wanakuza stadi
za mawasiliano na ushirikiano. Aidha, maadili ya heshima na umoja
yanahimizwa.
4. Sikiliza matamshi ya maneno mbalimbali huku ukihakikisha kuwa kila
mwanafunzi anashiriki. Hili hukuza ujumuishwaji.
5. Waagize wanafunzi kupeana maagizo na maneno yenye sauti zinazofanana.
6. Wapongeze wanafunzi wanapotoa majibu sahihi ili kuwatia moyo na kisha
uwasomee majibu sahihi.
Zoezi la 1: Linganisha maneno yaliyo na sauti zinazofanana
pata goti
futa kiwiko
sima bata
koti vuta
kijiko zima
Majibu sahihi
Zoezi la 1, ukurasa 33
1. Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
2. Askari....................Bahari
Jua..........................Pua
Simu.......................Timu
Meza.......................Cheza
Nyani.....................Jani
39
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la 2, ukurasa 34
1. Mwalimu atathmini namna wanafunzi wanavyosema shairi.
2. Mtoto-Ndoto, Nanga-Mnapanga, Nazi-wazi
Hitimisho
1. Kipindi hiki kitakuza stadi ya maisha katika kujua jinsi ya kuishi na wanafunzi
wengine kutokana na mawasiliano bora. Hivyo basi, hakikisha kwamba kila
mwanafunzi anashiriki katika kazi hii ya darasa ili kuimarisha mawasiliano,
ushirikiano na umoja.
2. Wanafunzi wataje baadhi ya maneno yaliyo na sauti ambazo wamejifunza.
Tathmini
Katika vikundi, waagize wanafunzi kupanga kadi mulishi za maneno zilizo na
maneno yenye sauti zinazofanana.
Somo la 3: Kutambua silabi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kuunganisha silabi kuunda maneno
na kuunganisha maneno kuunda sentensi.
Habari za kimsingi
Kipindi hiki kiwawezeshe wanafunzi kujua kuunda maneno mepesi na sentensi sahili
wanazoweza kutumia kujieleza katika mazungumzo ya kila siku. Wape wanafunzi
muda wa kutosha kufanya mazoezi mbalimbali ya uundaji wa maneno kisha
uwasahihishe ifaavyo. Kipindi hiki kinashughulikia stadi za kusikiliza na kuzungumza
chini ya (Somo la 1). Hata hivyo, juhudi zifanyike kuunganisha stadi za kusoma na
kusikiliza katika kipindi kwa kutumia mikutadha mwafaka.
Nyenzo za ujifunzaji
Vitabu, kadi mulishi za maneno.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 34-36
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi kuimba wimbo mfupi huku wanafunzi
wakisikiliza. Wafanye hivi katika vikundi. Wape mfano kwa kuimba wimbo wa
Kiswahili. Kwa wanafunzi, mpe mmoja nafasi ya kuimba darasani huku wengine
wakisikiliza.
40
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Waelekeze wanafunzi kuimba wimbo ulio katika Kitabu cha Wanafunzi.
2. Tayarisha vipande vya maneno haya, na uweke kila sauti kivyake: pua, jua,
meza, simu, jani.
3. Katika vikundi, waelekeze wanafunzi kupanga sauti ili kuunda maneno.
4. Waelekeze wanafunzi kusoma kwa sauti mafungu ya maneno katika Kitabu
cha Mwanafunzi huku ukisikiliza matamshi yao. Wanapofanya hivi stadi za
mawasiliano zinakuzwa.
5. Waelekeze wanafunzi kutambua silabi katika maneno.
Hitimisho
Waelekeze wanafunzi kuelewa kwamba sehemu za mwili hujenga kitu kamili, na
hivyo silabi na maneno.
Tathmini
Wakiwa wawili wawili, waandike maneno matano yaliyo na silabi tatu kila mmoja.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 34
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi
Zoezi la 2, ukurasa 35
1. Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi
2. Kalamu kitabu darasa ubao sabuni
Kikombe sahani kijiko kijiko zawadi
Somo la 4: Kuunganisha silabi kuunda maneno
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutambua kwamba silabi huunda
maneno.
Nyenzo za ujifunzaji
Vitabu
Kadi mulishi za maneno
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 36-37
41
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kutandaza picha na michoro ifuatayo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma kwa sauti silabi katika Kitabu cha Mwanafunzi
ukurasa 36.
2. Hakikisha kwamba wanafunzi wanatamka silabi ipasavyo.
3. Waagize wanafunzi kutambua silabi katika maneno yaliyopeanwa.
4. Waagize wanafunzi kuandika maneno waliyounda kutokana na gurudumu la
maneno.
5. Waangalie wanafunzi ili wafanya kazi ya kuunganisha kwa makini.
6. Waagize wanafunzi kadhaa kutamka maneno ambayo wameyaandika. Kutokana
na wasilisho hili ujasiri na uwezo wa kujifaa utakaokuzwa.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi walichojifunza katika kipindi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kufanya zoezi la nyumbani katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa
37.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 36-37
1. Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
2. Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
3. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
4. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
ki
vuli
kombe
tabu
oo
42
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la 2, ukurasa 37
1. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
3. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
4. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
5. Kalamu Uwanja Masomo Chakula
Kabati Uwele Mapera Chpeo
Karoti Upele Mafuta Chiriku
Zoezi la kufanyia nyumbani, ukurasa 37
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 5: Kutenganisha silabi katika maneno
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kusikiliza kutambua na kutamka
silabi na maneno ya sauti mwambatano.
Habari za kimsingi
Kipindi hiki kitawasaidia wanafunzi kutamka maneno yaliyo na sauti mwambatano
wakiwa wawili wawili na katika vikundi. Kipindi hiki kinashughulikia stadi za kusikiliza na
kuzungumza chini ya Somo la 1. Hata hivyo, juhudi zifanyike kuunganisha stadi za
kusoma na kusikiliza katika kipindi kwa kutumia miktadha mwafaka.
Nyenzo zinazopendekezwa za ujifunzaji
Chati kwenye karatasi ngumu
Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 37-38
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza kutaja maneno ya silabi mbili waliyojifunza katika
kipindi kilichopita.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waelekeze wanafunzi kusoma maneno katika Kitabu cha Mwanafunzi.
43
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
2. Wakiwa wawili wawili, waagize wanafunzi kutambua silabi katika kila neno.
3. Tamka kila silabi kwa sauti.
4. Waelekeze wanafunzi kuimba wimbo wa uvunjaji.
5. Angalia kazi za makundi na uwahimize wanafunzi kujibu maswali ikihitajika.
6. Hakikisha kwamba kila mwanafunzi anashiriki. Hili litakuza stadi za mawasiliano
na ushirikiano miongoni mwa wanafunzi. Aidha, itakuza maadili kama heshima na
umoja wanapotangamana na kufanya kazi au shughuli darasani.
Hitimisho
Waagize wanafunzi kupeana idadi ya silabi katika maneno ambayo wamejifunza.
Tathmini
Waagize wanafunzi kutambua na kutenganisha silabi katika zoezi la 2 ukurasa 38.
Majibu sahihi kwa zoezi la 2, ukurasa 38
1. mtu m tu
2. tone to ne
3. mbawa mba wa
4. kichaka ki cha ka
5. rungu ru ngu
Wiki ya 6
Somo la 1: Kusoma ufahamu
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kujenga ari ya kusoma kwa pamoja
darasani na kuimarisha stadi za kujifunza kama vile kujitathmini.
Habari za kimsingi
Hakikisha kwamba kila mwanafunzi anakia Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 39-
40 ili kusoma hadithi katika vikundi na kisha wakiwa wawili wawili. Kipindi hiki
44
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
kinashughulikia stadi ya kusoma chini ya somo la 1. Hata hivyo, juhudi zifanyike
kuunganisha stadi za kusomana kusikiliza katika kipindi kwa kutumia miktadha
mwafaka.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 39-41
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi ikiwa wanajua hadithi yoyote, anwani ya
hadithi hiyo na wahusika wake.
Shughuli za ujifunzaji
a) Wagawe wanafunzi katika vikundi ili kufanikisha ujifunzaji na usaidizi.
b) Waagize wanafunzi kusoma hadithi ya Kantai na Lenana wapata maji’ katika
vikundi. Stadi za mawasiliano na ushirikiano zinakuzwa wanapofanya kazi
pamoja katika vikundi.
ch) Waagize wanafunzi kutambua maneno mapya na kuyaandika pamoja na maana
zake.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwashirikisha wanafunzi katika mjadala wa ufahamu katika
maswali.
Majibu
Zoezi la 2, ukurasa 40
1. Kantai na lenana kupata maji.
2. Mwalimu atathmini majibu.
3. Mwalimu atathmini majibu.
4. Mwalimu atathmini majibu.
5. Mwalimu atathmini majibu.
Zoezi la 3, ukurasa 41
a) Ulikuwa wakati wa kipindi.
b) Wanyama wanakufa kwa sababu ardhi imekauka na kuwa jangwa kwa
sababu ya kukosekana maji.
ch) Waliamua kutafuta maji.
45
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
d) Kantai na Lenana walibeba kibuyu kidogo cha maji.
e) Kantai ndiye aliyeona maji wa kwanza.
f) Wavulana hawa wawili walipiga mako na kucheza kwa furaha.
Tathmini
a) Waagize wanafunzi kuwasimulia wenzao upya kisa hicho darasani.
b) Mhitaji mwanafunzi wa kujitokeza kusimulia kisa hiki kwa wenzake darasani.
Somo la 2: Kusoma kifungu cha kuelekezwa
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kusoma maandishi kwa jumla kwa
ufasaha, usahihi na ufahamu.
Habari za kimsingi
Usomaji wa wanafunzi umeelekezwa kwa maswali. Kipindi hiki kinashughulikia
stadi za kusikiliza na kuzungumza chini ya Somo la 3. Hata hivyo, juhudi zifanyike
kuunganisha stadi za kusoma na kusikiliza katika kipindi kwa kutumia miktadha
mwafaka.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 41-42
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi ikiwa wanaweza kukumbuka hadithi
waliyosoma katika kipindi kilichopita, anwani ya hadithi hiyo, wahusika wake na
matukio makuu katika hadithi hiyo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Wanafunzi wachache wajitolee, kusema wanachokumbuka kuhusu kisa cha
Kantai and Lenana wapata maji’.
2. Waelekeze wanafunzi katika kusoma hadithi ya kuelekezwa na kisa, Tina
aenda dukani’.
3. Jadili na wanafunzi majibu kwa maswali ya kisa cha kuelekezwa. Kadiri
46
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
wanafunzi wanavyofanya kazi pamoja stadi za maisha kama vile heshima kwa
wenzao zinakuzwa na umoja kudumishwa.
4. Waagize wanafunzi kuandika maneno mapya waliyojifunza kutokana na
hadithi.
Baadhi ya majibu kwa zoezi la 1, ukurasa 41
1. Tina yuko katika duka la kuuza wanasesere.
2. Tina anataka kununua kifaa cha kuchezea kutoka dukani humo.
3. Kuna wanaserere wengi maridadi katika duka hilo.
4. Tina hawezi kuwa na mwanaserere mpya kwa sababu bei yake ni ghali.
Zoezi ukurasa 42-43
1. Tina
2. Anataka kununua mwanaserere
3. Kuna wanaserere wengi
4. Hawawezi kupata mwanaserere mpya
Zoezi la kufanyia nyumbani, ukurasa 43
Mwalimu atathmini usimulizi wa kila mwanafunzi.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwasomea wanafunzi hadithi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kujaribu kujibu maswali kutoka katika kifungu.
Somo la 3: Jinsi ya kuendeleza maneno
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutahiji au kuendeleza vizuri
maneno yaliyo na vokali moja na yale ya vokali mbili pamoja na yale ya konsonanti
mwambatano.
Habari za kimsingi
Kipindi hiki kitakuza stadi ya kuandika ya mwanafunzi. Hata hivyo, juhudi zifanywe
kujumuisha stadi nyingine katika kipindi kwa kurejelea miktadha mwafaka.
47
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Kipindi hiki kinahakikisha kwamba wanafunzi wanapata uwezo wa kujaza mapengo
kwa kutumia heru mwafaka kuunda neno.
Nyenzo za ujifunzaji
Chati kwenye karatasi ngumu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 43
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuandika maneno mapya waliyojifunza
katika kipindi kilichopita.
Shughuli za ujifunzaji
1. Tandaza chati ya karatasi ngumu iliyo na maneno mengi mepesi yaliyoendelezwa
ifaavyo.
2. Waagize wanafunzi kujibu zoezi la kwanza wakiwa wawili wawili.
3. Angalia ili kuhakikisha kwamba kuna utendakazi wa kushirikiana.
4. Waelekeze wanafunzi kufanya zoezi kibinafsi.
5. Waagize wanafunzi wachache kujitolea kutamka maneno. Hili linahakikisha
kwamba stadi ya mawasiliano imekuzwa na ujasiri wao umekuzwa vilevile.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 43
a e i o u
akili embe imla Oktoba maua
pata cheza ingia osha uzi
bata neno lima omba uma
pasi meza kijiko okota uza
Zoezi la 2, ukurasa 44
1. Jaza mapengo kwa kutumia silabi-heru m, ki, wa, cha, ye. Andika neno
linaloundwa.
48
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
m___ tu mtu
ki___ tu kitu
wa___ tu watu
cha___ tu chatu
ye __ tu yetu
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwaeleza wanafunzi umuhimu wa kuandika maendelezo
stahilifu kwa mawasiliano bora na ya wazi.
Tathmini
Buni ruwaza na maumbo mengine ya hijai ili kuwaelekeza wanafunzi kuhusu kuandika
maneno.
Somo la 4: Kuendeleza maneno vizuri
Matokeo maalumu ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia baadhi ya maneno na
kuyaendeleza vizuri.
Habari za kimsingi
Kipindi hiki kiwaelekeze wanafunzi kutambua makosa ya hijai au maendelezo katika
maandishi yao wenyewe au maandishi mengine. Kipindi hiki kinashughulikia stadi
ya kuandika Somo la 4. Hata hivyo, juhudi zifanyike kuunganisha stadi za kusikiliza,
kuzungumza na kusoma katika kipindi kwa kutumia miktadha mwafaka.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 44
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuandika ruwaza za maneno waliyojifunza
katika kipindi kilichopita.
49
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Waelekeze wanafunzi kufanya zoezi la kwanza.
2. Waagize wanafunzi kujitolea kufanya mazoezi ya tahajia ubaoni.
3. Waagize wanafunzi kufanya zoezi la 2 wakiwa wawiliwawili. Umoja wao
unakuzwa wanapofanya kazi pamoja.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 44
1. fukom ……………… mfuko
2. tigoma……………… magoti
3. ktadari……………….daktari
4. bukita ……………….kitabu
5. zame …………………meza
Zoezi la 2, ukurasa 45
1. Mama yangu ni mkulima.
2. Yeye ni mwalimu.
3. Sisi tunawapenda wageni sana.
4. Ubao wa darasa letu ni wa rangi nyeusi.
5. Amina ni dada yangu.
Hitimisho
1. Washirikishe wanafunzi katika mjadala mfupi kuhusu umuhimu wa maendelezo
sahihi ya maneno.
2. Waagize wanafunzi kutumia zoezi la kwanza kutunga sentensi zao sahili.
zoezi hili juu liwe la maongezi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuchora nomino zilizo katika zoezi la kwanza.
Somo la 5: Jenga msamiati wako
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia ujuzi wake wa sauti na
matamshi kutahiji au kuendeleza maneno anayoyajua na asiyoyajua.
50
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Hakikisha kwamba wanafunzi wameshika dhana ya kuandika maneno mapya na
umbo la mti wa maneno. Kipindi hiki kinashughulikia stadi ya kuandika Somo la 4.
Hata hivyo, juhudi zifanyike kuunganisha stadi za kusikiliza, kuzungumza na kusoma
katika kipindi kwa kutumia miktadha mwafaka.
Nyenzo za ujifunzaji
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 45-47
Nyenzo za kuchorea
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuandika majina yao. Kwanza waandike
katika heru kubwa kisha katika heru ndogo.
Shughuliza ujifunzaji
1. Teua wanafunzi wawili wa kujitolea kuandika majina yao ubaoni.
2. Waongoze kwa kuandika jina lako ubaoni. Tumia majina haya kujenga maneno
zaidi. Wanafunzi wanapobuni maneni ubunifu wao na uwezo wa kukiri
kwa kina unakuzwa.
3. Tumia maneno yaliyoundwa kuchora mti wa maneno.
4. Kujibu maswali darasani kutakuza na kuimarisha kujiamini kwa wanafunzi.
Hakikisha kwamba wanafunzi wanashiriki na kukuza kujitolea kwao kujibu
maswali.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi umuhimu wa mawasiliano bora
kwa kuandika ifaavyo.
Tathmini
Waelekeze wanafunzi kushughulikia zoezi la kwanza na la pili katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 45-46.
Waulize wanafunzi kuchora mti wa maneno kutokana na majina ya maraki zao.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 46
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
51
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la 2, ukurasa 46-47
1. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
3. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 3, ukurasa 47-48
1. Kivuli, Kikombe, Kioo, Kitabu
Zoezi la kufanyia nyumbani, ukurasa 45
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
52
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Sehemu
3
Adhuhuri ya mvua
Mada 1.0
Kusikiliza
Mada 2.0
Kuzungumza
Mada 3.0
Kusoma
Mada 4.0
Kuandika
Somo la 1.3
Kusimulia
hadithi
Kukia mwisho
wa somo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kupokea maadili
yanayofunzwa
kupitia hadithi
mbalimbali zenye
maudhui anuwai.
b) Kujenga
msamiati kwa
kusikiliza
hadithi.
ch)Kuwaonea imani
watu, mahali na
vitu.
d) Kumbuka
hoja muhimu
za hadithi na
kuisimulia upya.
Somo la 2.4
Kuzungumza
Kukia mwisho
wa somo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kueleza kwa
ukakamavu
wahusika na
matukio katika
hadithi au matini.
b) Husisha
wahusika na
matukio katika
hadithi na visa
vya maisha halisi.
ch)Kuonyesha hamu
ya kuwasiliana na
watu anaowajua
kwa kutumia
kauli za kiuneni
na zisizo za
kiuneni.
Somo la 3.3 Kusoma
kimya kimya
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kusoma matini
na vifungu kimya
kimya.
b) Kusoma kimya
kimya akionyesha
kuzingatia makini
kwa muda mrefu
zaidi (dakika 15-20).
ch)Kukisia maana ya
maneno mageni
d) Kujibu maswali ya
ufahamu kutoka kwa
matini zilizosomwa
e) Kuendeleza hamu ya
kusoma matini kwa
starehe.
Somo la 4.3
Hati
Kukia mwisho
wa somo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kutumia nafasi
zifaazo baina
ya maneno.
b) Kutumia
viakishi
kwa kawaida
ipasavyo.
ch)Kuunganisha
heru kuunda
maneno yenye
maana.
d) Kutumia
heru kubwa
ipasavyo.
e) Kuelewa
umuhimu wa
hati nadhifu
inayosomeka.
53
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Stadi za kimsingi zitakazokuzwa
1. Mawasiliano na ushirikiano.
2. Uwazaji makinifu na usuluhishaji wa matatizo.
3. Ujuzi wa kutumia mifumo ya kidijitali.
4. Kujifunza kusoma.
Uhusiano na masuala mtambuko
1. Stadi za maisha: stadi za kujua na kuishi na wengine – mawasiliano fanikifu
2. Uraia: muumano wa kijamii
3. Mifumo wa kusaidia usomaji: Ushauri na uandaaji-wanaposhiriki katika mazoezi
kama vile mashindano ya uandishi
Uhusiano na desturi na thamani za kijamii
1. Uwajibikaji
2. Uaminifu
3. Heshima
4. Umoja
Uhusiano na masomo mengine
Maeneo yote ya ufunzaji
Shughuli zingine zisizo rasmi zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
1. Wanafunzi wasimuliane hadithi.
2. Wanafunzi wasimulie wenzao mambo yaliyowapata.
3. Wanafunzi wasome vitabu vya hadithi.
4. Wanafunzi wafanye mazoezi ya hati wakiwa darasani na kwingineko.
Shughuli za kijamii zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
1. Wanafunzi wawatembelee wanajamii na kusikiliza hadithi zikisimuliwa.
2. Wanafunzi watembelee fanani na kuzungumzia suala fulani katika jamii.
3. Kusoma kimya kimya/kimoyomoyo nyumbani.
4. Wanafunzi kufanya mazoezi ya hati kwa kuwasilisha mahitaji kwa njia ya kuandika.
Nyenzo zinazopendekezwa
Mafanani, vitabu vya hadithi, magazeti, majarida, kanda za sauti na za sauti pamoja
na picha, vitabu vya hadithi vya darasani, vitabu, penseli, penseli za rangi, mafumbo
ya miraba ya maneno.
Tathmini iliyopendekezwa
1. Maswali/majibu, usimulizi, kujaza pengo
54
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
2. Mjadala wa makundi kuhusu suala linaloathiri jamii kama vile kuenea kwa funza,
malaria
3. Mwalimu kutoa matini inayoonyesha hati nzuri ambayo wanafunzi watanukuu
katika daftari zao
Kuzingatia wanafunzi wenye mahitaji ya kipekee katika elimu na ulemavu
Usaidizi kwa wanafunzi wenye
uwezo mbalimbali
Usaidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji
maalum
Himiza wanafunzi wenye uelewa
wa polepole kushiriki katika
mazungumzo kama maigizo na
kusimulia hadithi.
Wape wanafunzi wenye uelewa
wa haraka kazi nyingi ili kuepuka
kuwachosha na kuzubaa darasani.
Wape wanafunzi wenye uelewa
wa polepole na haraka nafasi
za kutosha katika shughuli
za darasani. Una jukumu
la kuhakikisha kwamba
wanafurahiana na kufurahia
kukaa pamoja licha ya tofauti
zao.
Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa kuona,
wape breli, picha za kugusa na wale
wasioweza kuona vizuri wape maandishi
makubwa.
Kwa wanafunzi wasio sikia vizuri tumia
lugha ishara au kumleta mtaalamu wa lugha
ishara kufasiri.
Wanafunzi ambao hawawezi kuona mbali
wakae mbele darasani na wenye uwezo wa
kuona mbali wakae nyuma.
Wape wanafunzi wenye ulemavu majukumu
wanayoweza kutekeleza kama vile kuigiza
nafasi ya mwalimu mkuu au balozi wa kijiji.
Wape usaidizi wa kutosha na kuhakikisha
kwamba wanafunzi wengine wanafanya
hivyo, kwa mfano, kuwasaidia katika
kusukuma kitimaguru kwa mwanafunzi
mlemavu.
Mpangilio wa masomo
Somo la 1: Moha ashinda shindano la mbio
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:
1. Kujenga msamiati kwa kusikiliza hadithi.
2. Kupokea maadili yanayofunzwa kupitia hadithi mbalimbali zenye maudhui
anuwai.
Habari za kimsingi
Somo hili litawasaidia wanafunzi kujenga stadi ya kusikiliza iliyo chini ya Somo la
55
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
1.3 (Kusimulia hadithi). Wanafunzi pia watajenga stadi ya kuzungumza kwa kujadili
hadithi, 2.4 (Kuzungumza). Mwalimu awahimize wanafunzi wote kushiriki katika
mjadala wa makundi na usimulizi wa hadithi. Waonyeshe namna ya kusimulia
hadithi.
Nyenzo za kujifunzia
Mafanani au waalikwa, vitabu vya hadithi, magazeti, majarida, kanda za sauti na
picha
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 49-51
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wamewahi kushiriki katika shindano
la mbio. Waambie waketi katika makundi ya waanafunzi watatu au wanne na kujadili
yaliyomo pichani. Hili litachangia stadi za uwazaji makinifu na usuluhishaji
matatizo za wanafunzi.
Shughuli za ujifunzaji
1. Mwombe mwanafunzi mmoja kusimulia kwa kifupi walichoona kwenye picha.
2. Waambie wanafunzi wakae wamekuelekea ili kusikiliza hadithi ambayo
utawasimulia.
3. Soma au usimulie hadithi iliyo hapa chini kwa kasi inayofaa wao kuelewa hadithi
inahusu nini. Hakikisha wanasikiliza usimulizi kwa makini. Unaposoma, onyesha
yalivyo maneno, viakishi na kiimbo.
4. Waulize maswali kwenye Kitabu cha Wanafunzi ili kuona kama walifuatilia.
Majibu
Zoezi la 3, ukurasa 50
1. Moha, Kalu, Javan na Wasike
2. Moha alishinda shindano la mbio.
3. Shule ya Malezi Bora
4. Darasa lake litashinda kombe muhula huu
1. Waambie wanafunzi wajadili waliyojifunza kutokana na hadithi. Wanapofanya
hivi, watakuwa wakiendeleza stadi za maisha za kujua na kuishi pamoja na
wengine – mawasiliano fanikifu.
Hitimisho
Waulize wanafunzi kutaja umuhimu wa kushiriki katika michezo.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike michezo mitano waijuayo.
56
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 2: Kusimulia hadithi upya
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:
1. Kumbuka hoja muhimu za hadithi na kuisimulia upya.
2. Kuonyesha imani kwa watu, mahali na vitu.
Habari za kimsingi
Somo hili linashughulikia kuzungumza, Somo la 2.4 (Kusimulia). Litawasaidia
wanafunzi kuendeleza mawasiliano na ushirikiano wanaposimulia upya hadithi
waliojifunza katika somo la 1. Litaendeleza pia stadi za kujua na kuishi na watu wengine
mawasiliano fanikifu.
Nyenzo za kujifunzia
Vifaa vya sauti na vya sauti pamoja na picha, mafanani/waalikwa.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 51
Utangulizi
Anza somo kwa kuwaagiza wanafunzi kutaja wavulana walioshiriki katika shindano
la mbio kwenye hadithi uliowasimulia. Jina la msichana lilikuwa lipi?
Shughuli za ujifunziaji
1. Wafahamishe wanafunzi kuwa wataisimulia upya hadithi kwa maneno yao.
2. Anza kwa kuwauliza maswali kuhusu hadithi.
3. Waulize wanafunzi kuketi katika jozi au makundi na kuisimulia upya hadithi kwa
wenzao kwa maneno yao. Warekodi hadithi zao wanapofanya hivi. Waongoze
wanaporekodi hadithi zao. Wanapofanya hivi wanakuza ujuzi wao wa kutumia
mifumo ya kidigitali. Zoezi hili pia litachangia mawasiliano, ushirikiano na
thamani za maisha kama vile heshima na umoja wanapotangamana.
4. Chagua wasimulizi wa hadithi walio bora zaidi ili wasimulie hadithi hiyo kwa
darasa zima.
5. Mkiwa na wanafunzi, sikilizeni rekodi kadhaa.
6. Waambie wanafunzi waigize hadithi ile.
Hitimisho
Uliza wanafunzi kubainisha baadhi ya maneno mapya ambayo wamesoma kutoka
kwenye hadithi. Yaandike ubaoni kisha ujadili maana yake. Agiza wanafunzi kadhaa
kuyatumia kutunga sentensi wakizitamka.
57
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Tathmini
1. Waambie wanafunzi watumie maneno yafuatayo kutunga sentensi:
muhula, kianzio cha mbio, kushangilia, kombe, limbi.
2. Waambie wanafunzi wasikilize au kusoma hadithi kutoka kwa asili nyingine
kama vitabu vya hadithi, televisheni au wanafamilia, ambazo watasimulia katika
somo litakalofuata la usimulizi wa hadithi. Hili litachangia ujuzi wa kutumia wa
mifumo ya kidijitali wanapojadili hadithi kutoka kwa vifaa vingine.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 50
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 3: Kuzungumzia siku ya michezo
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuongea kwa ukakamavu kuhusu
wahusika na matukio katika hadithi.
Habari za kimsingi
Somo hili linashughukia stadi ya kusikiliza na kuzungumza, Somo la 2.4 (Kuzungumza).
Linawapa wanafunzi nafasi ya kujieleza kwa uhuru. Mwalimu anapaswa kuhakikisha
wanafunzi wote wanashiriki katika zoezi hili.
Nyenzo za ujifunzaji
Vifaa vya sauti na sauti pamoja na picha, mafanani/waalikwa
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 52-53
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwakumbusha wanafunzi kuhusu hadithi ambayo walisoma.
Waulize kutaja walioshiriki katika shindano la mbio. Waulize wataje aliyeshinda
mbio na aliyekuwa wa mwisho.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waulize wanafunzi kutaja iwapo wamewahi kushiriki katika siku ya michezo
shuleni au kwingineko.
2. Wataje michezo ambayo wao hushiriki wakiwa shuleni na nyumbani.
3. Waambie waangalie picha na kujadili michezo iliyoonyeshwa katika kila picha.
4. Wakiwa wawiliwawili, washirikishe katika kueleza yale yanayofanyika katika
siku ya michezo shuleni. Waongoze kwa kutumia maswali yaliyo kitabuni. Zoezi
58
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
hili litachangia stadi za kujua na kuishi na wengine – mawasiliano fanikifu.
5. Wape baadhi yao nafasi ya kueleza wenzao darasani matukio katika siku ya
michezo.
Hitimisho
Waagize wanafunzi kueleza kwa nini wanapenda kushiriki katika mchezo
waupendao.
Tathmini
Andika michezo mitano ambayo wewe hucheza shuleni au nyumbani. Wasomee
wenzako darasani.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 52
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 52-53
1. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
3. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
4. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 4: Kusimulia hadithi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuhusisha wahusika na matukio katika
hadithi na visa halisi maishani.
Habari za kimsingi
Katika somo hili, wanafunzi wanapaswa kuigiza hadithi waliyosikiliza hapo awali.
Somo linashirikisha kusikiliza na kuzungumza, Somo la 2.4 (Kuzungumza).
Mwalimu awashirikishe wanafunzi wote katika kuigiza nafasi mbalimbali katika
hadithi. Kabla ya somo unaweza kufaragua baadhi ya vifaa vya uigizaji unavyohitaji
kama limbi na kombe.
Nyenzo za kujifunzia
Vifaa vya sauti na picha, kombe, limbi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 53
59
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Anza somo kwa kuwakumbusha hadithi ya ‘Moha ashinda shindano la mbio’.
Wataje kwa kifupi wahusika katika hadithi na matukio yaliyotukia.
Shughuli za ujifunziaji
1. Waeleze wanafunzi kuwa wataigiza hadithi ya ‘Moha ashinda shindano la mbio’.
2. Wachague wahusika wa kwanza na uwape nafasi watakazoigiza.
3. Wanafunzi waigize nafasi zao mbele ya darasa.
4. Badilisha nafasi na kushirikisha wahusika. Hakikisha kuwa wanafunzi wengi
kadiri inavyowezekana wanashirikishwa katika zoezi hili. Hili litachangia stadi za
kujua na kuishi na wengine mawasiliano fanikifu. Wanafunzi pia wataendeleza
thamani za maisha za uwajibikaji na heshima wanapoigiza pamoja.
5. Waongoze wanafunzi katika kujadili maswali yaliyo katika zoezi.
Hitimisho
Waagize wanafunzi kujadili kile walichojifunza kutokana na mchezo.
Tathmini
Andika sababu tatu kwa nini tunapaswa kushiriki katika uigizaji.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 53
1. Moha, Barri, Kalu, Wasike, Sara
2. Mwalimu atathmini majibu.
3. Mwalimu atathmini majibu.
4. Mwalimu atathmini majibu.
5. Mwalimu atathmini majibu.
Zoezi la 2, ukurasa 53-54
Mwalimu atathmini maigizo ya wanafunzi
Somo la 5: Kuunda upya hadithi
Matokeo maluum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:
1. Kuunda upya hadithi akitumia majina yao, ya shule yao, wanafunzi wenza na
michezo wanayopenda kushiriki.
2. Rekodi hadithi zao na kuziwasilisha darasani kwa wenzao.
60
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Somo hili linashughulikia kuzungumza, Somo la 2.4 (Kuzungumza). Litawasaidia
wanafunzi kuendeleza mawasiliano na ushirikiano wanapofanya kazi katika makundi
ili kuunda upya hadithi. Itaendeleza pia stadi za kujua na kuishi na wengine- mawasiliano
fanikifu.
Nyenzo zaa kujifunzia
Vifaa vya sauti na sauti pamoja na picha, mafanani/waalikwa
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 54
Utangulizi
Anzia somo kwa kuwaambia wanafunzi wasimulie tena hadithi ya Moha ashinda
shindano la mbio’.
Njia za kufunzia
1. Waambie wanafunzi wanapaswa kuunda upya hadithi kwa kutumia majina yao, ya
shule yao, wanafunzi wenzao na michezo ambayo wao hucheza shuleni.
2. Waagize wanafunzi kufanya kazi katika jozi au makundi.
3. Teua wasimulizi bora zaidi wasimulie hadithi ambazo wameunda upya darasani.
4. Waambie warekodi hadithi zao. Waongoze wanaporekodi hadithi zao.Wanapofanya
hivi wanakuza ujuzi wao wa kutumia mifumo ya kidigitali. Zoezi hili pia
litachangia mawasiliano, ushirikiano na thamani za maisha kama vile heshima na
umoja wanapotangamana.
5. Mkiwa na wanafunzi, sikilizeni rekodi kadhaa.
6. Waambie wanafunzi waigize hadithi ile.
Hitimisho
Waagize wanafunzi kuunda upya hadithi mbalimbali ambazo wamewahi kusoma
wakitumia sifa zao.
Tathmini
Waambie wanafunzi warekodi hadithi zao na kuziwasilisha kwa maraki na familia
zao.
Majibu
Mwalimu atathmini usimulizi na rekodi za wanafunzi.
61
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Wiki ya 8
Somo la 1: Kutoa kisa kwenye picha
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kusoma vifungu kimya kimya.
Habari za kimsingi
Somo hili linalenga kuwahimiza wanafunzi kusoma hadithi kimoyomoyo na kwa
kuelewa. Linashughulikia stadi ya kusoma, Somo la 3.3 (Kusoma kimya kimya).
Mwalimu hakikisha wanafunzi wote wanaweza kusoma peke yao kimoyomoyo
midomo yao ikiwa imetulia.
Nyenzo za ujifunziaji
Vitabu vya kusoma darasani, majarida, magazeti, vitabu vya hadithi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 54
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kupitia yaliyosomwa awali. Waulize wanafunzi kama
wamewahi kuchunga ng’ombe, mbuzi au kondoo. Baadhi yao wawaeleze wenzao
waliyofanya wakati wakichunga.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi waangalie picha kwenye kitabu chao.
2. Waambie waeleze kinachofanyika katika picha ya kwanza. Waruhusu wanafunzi
wengi kadri inavyowezekana kushiriki. Hili litawawezesha kuendeleza stadi za
kujua na kuishi na wengine – mawasiliano fanikifu.
3. Wakiwa wawiliwawili, waelezane yanayotendeka kwenye picha iliyosalia. Wanafunzi
watajifunza kuheshimu maoni ya watu wengine.
4. Wape baadhi yao nafasi ya kusimulia hadithi darasani kwa maneno yao.
5. Waagize waandike majibu ya maswali yaliyo katika kitabu chao.
Hitimisho
Waagize wajadili yale waliyojifunza kutoka na hadithi hiyo ya picha.
Tathmini
Andika aya moja kueleza yanayotendeka hadithini.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 54
Mwalimu atathmini masimulizi ya wanafunzi.
62
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 2: Kusoma kimya kimya
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kusoma kimya kimya akionyesha
kuzingatia makini kwa muda mrefu zaidi (dakika 15-20).
Habari za kimsingi
Somo hili linalenga kuwahamasisha wanafunzi kusoma matini peke yao na
kimoyomoyo kwa muda mrefu. Mwalimu ahakikishe kuwa wanafunzi wanasoma
bila kuzungumza na wenzao. Somo hili litawasaidia wanafunzi kufanya mazoezi
ya stadi ya kusoma, hasa yaliyo katika Somo la 3.3 (Kusoma kimya kimya).
Ikiwezekana, kila mwanafunzi awe na kitabu chake binafsi.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu vya hadithi, vitabu vya kusoma darasani, majarida, magazeti.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 55
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wamewahi kunyeshewa. Waeleze
ilifanyika lini na walifanya nini. Waeleze kuwa watasoma hadithi kuhusu alasiri
iliyojaa mvua.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie kuwa watasoma kimyakimya.
2. Wakumbushe sifa za usomaji bora. Kwa mfano, kusoma midomo ikiwa imetulia,
kusoma bila kufuata maneno kwa kidole n.k.
3. Wasome hadithi iliyo kwenye kitabu chao kimyakimya (dakika 10-15).
4. Waambie wabainishe maneno mapya kisha wajadili maana yake katika muktadha.
Hitimisho
Agiza mwanafunzi mmoja au wawili kusimulia hadithi ambayo wamesoma kwa
darasa zima.
Tathmini
Wanafunzi wajibu maswali katika Zoezi la 1 katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 55.
Zoezi la 1, ukurasa 55
1. Ijumaa alasiri
2. Radi (ngurumo)
63
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
3. Mawingu meusi
4. Nyumbani kwao
5. Mgonjwa
Somo la 3: Kusimulia visa vilivyopita
Matokeo maalum ya ujifuzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kujibu maswali ya ufahamu kuhusu
vifungu alivyosoma.
Habari za kimsingi
Somo hili linalenga kumpa mwanafunzi nafasi ya kuhusisha waliyosoma na visa halisi
maishani. Litamsaidia mwanafunzi kufanya mazoezi ya stadi zote nne za kusikiliza
na kuzungumza, kusoma na kuandika. Hata hivyo inajikita katika yaliyosomwa
katika usomaji, Somo la 3.3 (Kusoma kimya kimya). Wasaidie wanafunzi kuhusisha
waliyosoma vitabuni na yanayotendeka katika maisha yao ya kila siku.
Vifaa vya kufunzia
Vitabu vya hadithi, vitabu vya kusoma darasani, magazeti, chati.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 56
Utangulizi
Anza somo kwa kupitia yale ambayo wanafunzi walisoma katika somo lililotangulia.
Waulize wajadili kwa kifupi yaliyotendeka katika hadithi.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi waeleze wanachofanya mvua inaponyesha.
2. Waagize kuketi katika jozi na kujadili yanayotendeka katika picha. Lengo ni
kuwawezesha kujenga stadi za kujua na kuishi na wengine mawasiliano fanikifu.
3. Waruhusu mwanafunzi mmoja au wawili kusimulia yanayofanyika katika picha.
4. Waulize kama si sawa kuchezea mvuani kama wanavyofanya wavulana na
wasichana waliomo pichani. Wafafanue maoni yao. Zoezi hili litawawezesha
kuwajibika wanapocheza.
5. Waambie wanafunzi wafafanue kwa nini mvulana mdogo anatumia mwavuli.
Hitimisho
Wajadiliane kwa kifupi yepi yatafanyika wakicheza nje mvua inaponyesha.
64
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Tathmini
Waambie waandike sentensi tano zinazoanza na:
Wakati mvua inaponyesha, ninapenda
…………………………………………………
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 56
Mwalimu atathmini masimulizi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 56
Mwalimu atathmini maelezo ya wanafunzi.
Somo la 4: Kusoma mazungumzo
Lengo mahsusi la somo
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kukuza hamu ya kusoma matini kwa
starehe.
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Somo hili linashughulikia usomaji, Somo la 3.3 (Kusoma kimya kimya). Mwalimu
ahakikishe kuwa wanafunzi wanapata aina mbalimbali za vifaa vya kusoma na aina
tofauti za maandishi kama vile, masimulizi, mazungumzo (dayalojia), mashairi n.k.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu vya kusoma darasani, vitabu vya hadithi, majarida, magazeti.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 57-58.
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi kutaja virai na kauli ambazo wanatumia
katika mazungumzo rasmi na yasiyo rasmi ambavyo walisoma awali. Waruhusu
kutumia virai na kauli hizo kuwasiliana baina yao darasani.
Shughuli za ujifunzaji
1. Wafafanulie mazungumzo ni nini. Mazungumzo ni ubadilishanaji wa mawazo ya
binafsi kwa kuongea na watu wengine.
2. Waeleze kuwa watasoma mazungumzo baina ya maraki wawili.
3. Wanafunzi wasome mazungumzo yale peke yao kimya kimya. Hili litajenga
heshima kwa wengine na uwajibikaji kwa matendo yao.
4. Waulize wajadili katika makundi mazungumzo yanahusu nini.
65
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
5. Waambie waigize mazungumzo yale. Wabadilishane nafasi za uhusika. Uigizaji
huchangia mawasiliano na ushirikiano.
Hitimisho
Waulize wanafunzi kama mazungumzo haya ni rasmi au si rasmi. Wafafanulie
tofauti baina ya aina hizi mbili za mazungumzo.
Tathmini
Wajibu maswali katika Zoezi la 2 katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 57.
Majibu sahihi
1. Moha, Barri na Jevan
2. Mpira mkubwa uko na Moha
3. Mpira wa miguu
Somo la 5: Kusoma na kupata maana ya maneno
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kukisia maana ya maneno mapya.
Habari za kimsingi
Somo hili limekitwa katika usomaji, Somo la 3.3 (Kusoma kimoyomoyo). Mwanafunzi
anapaswa kusoma matini na kutafuta maana ya maneno katika muktadha. Waongoze
wanafunzi kukisia maana ya maneno mapya katika matini.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu vya hadithi, majarida, magazeti, vitabu vya kusoma darasani.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 58-59.
Utangulizi
Anza somo kwa kuwauliza wanafunzi kuchunguza picha zilizomo kwenye kitabu
chao. Waambie wataje kazi nyingine ambazo wanazijua.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wataje wangetaka kufanya kazi gani wakiwa watu wazima.
Pia waeleze ni kwa nini. Wanapofanya hivyo wataendeleza stadi za kujua na
kuishi na wengine mawasiliano fanikifu. Wanajifunza pia kuheshimu kazi za
watu wengine.
2. Waambie watasoma hadithi ile kimoyomoyo, kila mwanafunzi peke yake.
3. Hakikisha wanazingatia sifa za usomaji bora.
66
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
4. Waambie wabainishe maneno ambayo hawayaelewi katika matini ile.
5. Jadili maana ya maneno yale kisha watunge sentensi darasani wakiyatumia.
Hitimisho
Waeleze wanafunzi kuwa inawezekana wafanye kazi wanazotamani iwapo watasoma
kwa bidii shuleni na kuwa na nidhamu.
Tathmini
Waambie wanafunzi wanakili zoezi la fumbo la mraba lililo katika Kitabu cha
Mwanafunzi na watafute maneno yaliyomo katika mraba .
Baadhi ya maneno
(i) moja
(ii) bidii
(iii) mgonjwa
(iv) yeye
Wiki ya 9
Somo la 1: Kuandika mifumo ya heru
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia nafasi mwafaka kati ya
maneno tofauti.
Habari za kimsingi
Katika somo hili, mwanafunzi anatarajiwa kufanya mazoezi kuhusu kuacha nafasi
baina ya maneno. Somo limekitwa katika kuandika, Somo la 4.3 (Hati). Mwalimu
ahakikishe kuwa wanafunzi wanaweza kuacha nafasi zifaazo baina ya maneno.
Shirikisha stadi nyingine kwa kuwapa wanafunzi matini amabazo wanaweza kusoma
kwa sauti huku wakiona namna maneno yametenganishwa. Wafahamishe wanafunzi
kuja na picha za matunda zilizokatwa kutoka kwa matini mbalimbali na daftari la
maandishi anuwai kabla ya somo.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, penseli, penseli za rangi, mafumbo ya miraba, vitabu vya hadithi.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 59-60
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaonyesha wanafunzi vipande vya sentensi ambapo heru
67
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
zimekatwa vilivyo na nafasi mwafaka baina ya maneno kuzingatiwa. Waeleze kuwa
watafanya mazoezi ya kuacha nafasi mwafaka baina ya maneno.
Shughuli za ujifunzaji
1. Wape wanafunzi heru za alfabeti ambazo tayari zimekatwa wazitumie kuunda
maneno.
2. Waonyeshe namna ya kuunda majina ya vitu mbalimbali kwa kutumia heru
mbalimbali.
3. Waambie wakate na kuunganisha picha kwenye kitabu chao cha shughuli anuwai.
Zoezi hili litawasaidia wanafunzi kuwa na sifa ya uwajibikaji na heshima kwa
kazi za wengine.
4. Waambie waunde majina ya matunda kwa kuchukua heru zilizo chini ya kila
tunda.
5. Waagize kuwasilisha kazi zao kwa wenzao. Hili litachangia kujifunza kusoma.
6. Chagua kazi ambazo ni nzuri uziweke mahali ambapo darasa lote linaweza
kuziona.
Hitimisho
Watambue wanafunzi waliofanya vizuri na uwahimize kuunda maneno zaidi katika
jozi.
Tathmini
Waagize kufanya kazi iliyo katika zoezi la 2 katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
59. Wasisitizie kutumia nafasi mwafaka baina ya maneno.
Somo la 2: Kuandika alfabeti
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuandika alfabeti ipasavyo.
Habari za kimsingi
Katika somo hili, wanafunzi wanatarajiwa kuandika alfabeti ipasavyo. Hakikisha
kuwa wanafunzi wanaweza kukata heru kubwa na ndogo ipasavyo. Somo linazingatia
stadi ya kuandika, Somo la 4.3 (Hati).
Nyenzo za kujifunzia
Penseli, vitabu vya hadithi, vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 60
68
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaonyesha wanafunzi chati yenye heru za alfabeti.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kutaja heru zote za alfabeti.
2. Wape chati ambayo tayari imeandaliwa. Waambie wanakili alfabeti katika daftari
zao. Hakikisha wameandika heru kubwa na ndogo. Wasimamie na kuwaongoza
wanafunzi. Hili litachangia kuboresha hati zao na kuandika kazi nadhifu.
3. Waambie wanafunzi waandike sentensi tano za sifa za tunda walijualo. Hakikisha
wameakisha sentensi na kutumia heru kubwa ipasavyo.
Hitimisho
Wanafunzi wabadilishane vitabu na kusahihisha kazi za wenzao. Hili litachangia
ushirikiano na umoja wanapofanya kazi pamoja.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike aya kuhusu shule yao. Sisitiza matumizi sahihi za
heru kubwa na viakishi vingine.
Somo la 3: Kuandika mifumo ya maneno
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, wanafunzi waweze kuunganisha heru kuunda maneno
yenye maana.
Habari za kimsingi
Katika somo hili, mwanafunzi anapaswa kuweza kutumia heru kuunda maneno
yenye maana. Limekitwa katika stadi ya kuandika, Mada ndogo 4.3 (Hati). Mwalimu
anapaswa kuhakikisha wanafunzi wanafanya mazoezi mengi ya kuunda maneno.
Haya yanaweza kufanywa kwa kutumia kadi, mafumbo mepesi ya mraba au hata
kucheza skrabo.
Nyenzo za kujifunzia
Kadi, vitabu, mafumbo ya maneno, chati.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 61-62
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi maswali kuhusu walichosoma katika somo
lililotangulia. Utahakikisha wanafunzi wanakumbuka wanayosoma.
69
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunziaji
1. Onyesha chati iliyo na maneno mepesi na kuwauliza wasome maneno yaliyo
kwenye chati.
Kwa mfano: kitabu, nyumbani, kiti, mkoba, darasa, shamba, n.k.
2. Onyesha chati nyingi yenye maneno yaliyochanganyika heru na uwaambie
wanafunzi kuyaangalia na kujaribu kuyasoma.
Kwa mfano: mwmaenka, smiu, kapiuk, mteka, n.k. (mwanamke, simu, kikapu,
mkate)
3. Wakiwa wawiliwawili, wape heru zilizokatwa na kuwaambia waunde maneno
yaliyo kwenye chati. Hili litachangia kujifunza kusoma.
4. Waambie wakirie kuhusu maneno mengine na watumie heru kuyaunda.
Unaweza kulifanya kuwa shindano la jozi gani ambazo zitaunda maneno mengi
zaidi. Hili litachangia mawasiliano na ushirikiano.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaagiza wanafunzi kutumia baadhi ya maneno kuunda
sentensi darasani. Wasaidie inapobidi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kufanya kazi iliyo katika kitabu chao.
Somo la 4: Kuandika heru kubwa na ndogo
Matokeo maalum ya ujifunziaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia heru kubwa ipasavyo.
Habari za kimsingi
Mwanafunzi anapaswa kutumia heru kubwa anapoandika akiwa shuleni na
nyumbani. Mwalimu ahakikishe wanafunzi wanaweza kutambua na kutumia heru
kubwa ipasavyo. Wasichanganye heru kubwa na ndogo. Somo hili linazingatia stadi
ya kuandika, Somo la 4.3 (Hati).
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, vitabu vya hadithi, magazeti, majarida, mafumbo ya maneno
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 63-64
Utangulizi
Anza somo kwa kutathmini yaliyosomwa katika somo lililotangulia. Hakikisha kuwa
wanafunzi wote wanaweza kuunda maneno yenye maana kwa heru.
70
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kutaja viakishi ambavyo tayari wamesoma.
2. Rudia matumizi ya heru kubwa ambayo. Walikuwa wamesoma katika somo
lililotangulia.
3. Andika sentensi kadhaa ubaoni na kuwaambia wanafunzi kadhaa waziakishe kwa
heru kubwa. Waongoze panapostahili. Hili litakuza mifumo wa kusaidia usomaji:
Ushauri na uandaaji- wanaposhiriki katika mazoezi kama vile mashindano ya
uandishi.
4. Wakumbushe kuwa heru kubwa hutumika wakati mtu anaandika majina ya watu,
miji, taasisi kama vile shule na wakati wa kuanza sentensi.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi waandike majina matano ya watu walio
darasani.
Tathmini
1. Andika aya kwa kutumia heru kubwa ipasavyo.
2. Waagize wanafunzi kufanya Zoezi la 2.
Majibu sahihi, Zoezi la 2, ukurasa 63-64
1. Mama Nyambura huuza ndizi, machungwa, maembe na matikitimaji.
2. Anapenda kuwauzia majirani zake, wafanyakazi na wanafunzi.
3. Sara na Moha wanataka kumnunulia mama yao matunda.
4. Mama yao anapenda machungwa, maembe na matikitimaji na huyatumia
kutengeneza juisi.
Somo la 5: Kuandika sentensi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuelewa umuhimu wa hati nadhifu na
inayosomeka.
Habari za kimsingi
Somo hili linalenga kumwezesha mwanafunzi kuandika sentensi anazosomewa
akizingatia nafasi, uakishaji na hati inayosomeka. Endeleza somo hili la imla ili
kuwawezesha wanafunzi kuandika ipasavyo, na wakati uo huo waakishe ipasavyo.
Somo hili limekitwa katika stadi ya kuandika, Somo la 4.3 (Hati).
71
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Nyenzo za kujifunzia
Sentensi zilizoandikwa, chati, vitabu vya hadithi, mafumbo ya maneno.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 64-65
Utangulizi
Tathmini somo lililotangulia kuhusu matumizi ya heru kubwa, koma na nukta.
Waambie wanafunzi wataje matumizi ya viakishi hivi.
Shughuli za ujifunziaji
1. Waambie wanafunzi kuwa katika somo hili, wataandika sentensi ambazo
utawasomea.
2. Wakumbushe watumie heru kubwa, koma na nukta panapostahili.
3. Hakikisha tayari wana penseli na daftari zao kabla ya kuanza kuwasomea sentensi.
4. Soma sentensi zifuatazo polepole huku wakiandika. Unaweza kuongeza nyingine
kutegemea uwezo wa darasa lako. Zoezi la imla huchangia kujifunza kusoma
wakati wanafunzi wanalinganisha hati zao na za wenzao na kutambua njia
mbalimbali za kuboresha.
a. Kibet anacheza uwanjani.
b. Sisi tumeketi.
ch. Johari na Lulu walienda dukani.
d. Nairobi ni jiji kubwa.
e. Hidaya ana penseli, kitabu, rula na kifutio ndani ya mkoba wake.
f. Shule ya Elimu Bora ilipata kombe la uogeleaji.
5. Pitia kazi za wanafunzi.
Hitimisho
Andika sentensi sahihi ubaoni ili wale ambao walifanya kosa wazinakili.
Tathmini
Waagize waandike sentensi sita kuhusu shule yao.
Waagize wafanye zoezi la 1 na la 2.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 64
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 65
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
72
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Wiki ya 10
Mwendelezo wa Somo
Somo la 1: Angalia na uandike
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kujieleza ifaavyo akitumia msamiati
aliojifunza ili kuwasiliana kwa ufasaha.
Habari za kimsingi
Wanafunzi wanatarajiwa kushiriki katika mijadala na kuwasiliana kwa ufasaha kwa
kusoma na pia kuzungumza. Hakikisha kila mwanafunzi ameshiriki. Hivyo basi
watakuwa wakifanya mazoezi ya stadi za kusikiliza na kuzungumza.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 65-66
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wamewahi kuenda sokoni, kibandani,
dukani au katika duka kuu kununua bidhaa yoyote na namna walivyowasiliana na
muuzaji. Wape wamafunzi watakaojitolea fursa ya kueleza waliyowahi kukumbana
nayo katika shughuli kama hizo.
Shughuli za ujifunziaji
1. Waagize wanafunzi kuchunguza picha iliyomo katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 65 kwa makini na waseme vitu wanavyoona kwenye picha, wanadhani
mahali hapo ni wapi na ni yepi yanayotendeka pale. Wafanye hivyo katika
jozi. Hili litaendeleza uwezo wa mwanafunzi wa uwazaji makinifu na
mawasiliano.
2. Waagize wanafunzi kuandika sentensi tano kuhusu picha hiyo; wanayoyaona
na yanayoweza kuwa yakitendeka mle.
3. Waambie wanafunzi wajadili sentensi zao wakiwa katika jozi kisha wazisome
darasani. Hili litachangia kujiamini kwa wanafunzi na kuwashajiisha kushiriki
vilivyo katika shughuli za darasani.
4. Wahimize kutumia hati inayosomeka, kutumia miundo ifaayo ya sentensi na
kuakisha ipasavyo.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaagiza wanafunzi kuangalia kazi za wenzao na kuhakikisha
matumizi mwafaka ya maneno, uakishaji, nyakati na kusahihisha panapofaa
kurekebishwa.
Tathmini
Andika insha fupi kuhusu tukio lililokupata katika kibanda, duka, soko au duka kuu.
73
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 2: Kujaza mapengo
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia viunganishi mwafaka
kufuatanisha sentensi.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watahitajika kutumia viunganishi ifaavyo. Hakikisha wameelewa dhana
ya viunganishi na kuvitumia ipasavyo. Stadi za kuandika za wanafunzi zitaboreshwa
katika somo hili.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 66-67
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi kubadilishana vitabu na kusoma sentensi
za wenzao za tathmini ya somo la 1. Fuatilia na uhakikishe kila mwanafunzi amefanya
zoezi hilo.
Shughuli za ujifunziaji
1. Waagize wanafunzi kujaza maneno yaliyoachwa katika zoezi 1 kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi.
2. Wakiwa katika jozi, waambie walinganishe majibu yao na kuonyesha mahali
ambapo wanatatizika. Hili litaendeleza ushirikiano wa wanafunzi.
3. Waagize wanafunzi kujaza pengo katika zoezi wakitumia maneno waliyopewa
katika Kitabu cha Mwanafunzi. Angalia wanapofanya zoezi kuhakikisha kuwa
wanafunzi wameelewa dhana ya kutumia viunganishi katika sentensi.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwasomea majibu mwafaka na kuwaagiza kusahihisha ipasavyo.
Tathmini
Andika sentensi tano ukitumia vinganishi ‘kwa sababu’, ‘na’, ‘zaidi ya’ na ‘lakini’.
Majibu
Zoezi 1, ukurasa 66
1. Kibanda
2. Machungwa na ndizi
3. Nunua
Zoezi 2, ukurasa 66-67
Na, lakini, zaidi ya (hayo), au, kwa sababu, na.
74
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 3: Mchezo wa hadithi ya kuchangiana-kimnyororo
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kusikiliza na kuwasiliana ifaavyo
katika miktadha mbalimbali.
Habari za kimsingi
Katika somo hili, wanafunzi wanatarajiwa kuendeleza hoja zilizotolewa na wanafunzi
wengine kutunga hadithi kamili. Hili litaendeleza stadi zao za kusikiliza na
kuzungumza wanaposikiliza kwa makini ili kuendeleza hoja walizopewa na maraki
zao na pia kuwasiliana ifaavyo ili wanafunzi wenzao wawaelewe.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 67
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuagiza kila mwanafunzi kusoma sentensi walizoandika katika
tathmini ya somo la 2 darasani.
Shughuli za ujifunziaji
1. Wapange wanafunzi katika makundi ya watu, watano au makundi yanayodhibitika
na uwaagize kusimuliana hadithi..
2. Mwanafunzi mmoja aanze na wenzake waendeleze hadi wapatate hadithi
kamili. Hakikisha kila mwanafunzi ameshiriki. Hili litaendeleza ushirikiano,
mawasiliaono na uwazaji makinifu wa wanafunzi
3. Waagize wanafunzi kuandika hadithi hiyo.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuteua makundi mawili ambayo yatasoma hadithi zao darasani.
Tathmini
Waagize wanafunzi wacheze mchezo wa kusimuliana hadithi wakati wao wa
mapumziko.
Somo la 4: Soma na usambaze
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kujenga hamu ya kusoma kwa pamoja
darasani na kwingineko.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watahitajika kushiriki katika usomaji wa pamoja ili kuboresha hadithi
75
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
waliyotunga katika somo la 3. Wanafunzi wanatarajiwa kupiga chapa hadithi yao,
hivyo wapatie vifaa mwafaka vya kufanya hivi.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, kompyuta
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 68
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuuliza kundi jingine lisome darasani hadithi ambayo lilitunga
katika somo la 3. Waulize wanafunzi kutoa maoni kuhusu namna ya kuboresha hdithi
hiyo. Pata hoja kutoka kwa wanafunzi mbalimbali watakaojitolea.
Shughuli za ujifunziaji
1. Wakiwa katika makundi, waagize wasome hadithi walizotunga katika somo
la 3. Waambie wachunguze saru, nyakati, uakishaji na miundo ya sentensi.
Hili litaendeleza ushirikiano wa wanafunzi na thamani ya umoja.
2. Agiza kila kikundi kupiga chapa hadithi yao na utoe nakala za hadithi hizo.
3. Kila kikundi kiteue mwanafunzi atakayewasilisha hadithi darasani. Hili
litachangia kujiamini kwa mwanafunzi na pia kujienzi.
4. Waambie wanafunzi wapigie kura hadithi bora zaidi, kisha uiangike kwenye
bodi la matangazo darasani.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaagiza wanafunzi kubuni hadithi zao, wapige chapa na
kutoa nakala wakisaidiwa na walezi au wazazi na wawapatie maraki na wanafamilia
wasome.
Tathmini
Andika insha kuhusu mada yoyote utakayochagua. Piga chapa na utoe nakala.
Somo la 5: Imla
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia vifungu vya kawaida vya
maneno kutunga sentensi sahili.
Habari za kimsingi
Wanafunzi wanatarajiwa kusikiliza kwa makini na kuandika sentensi ambazo
utawasomea. Paza sauti ili wanafunzi wapate kusikia.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 68
76
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi; msichana mmoja na mvulana mmoja,
kusoma hadithi kutoka tathmini ya somo la 4 darasani.
Shughuli za ujifunziaji
1. Wasomee sentensi zifuatazo na uwaagize waziandike.
Sentensi
1. Mimi huamka mapema kila siku.
2. Wewe unapenda kusoma?
3. Hiki ni kitabu cha Anita.
4. Ndizi huwa tamu.
5. Kamau na Otieno ni maraki wa chanda na pete.
2. Rudia sentensi mara kadhaa kuhakikisha kila mwanafunzi ameandika.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kukagua sentensi za kila mwanafunzi kuhakikisha waetumia
alama za uakishaji ipasavyo. Kosoa panapostahili.
Tathmini
Someaneni sentensi wakati wenu wa mapumziko kisha mziandike.
77
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Sehemu
4
Mutulu amkasirisha mama yake
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Mada 1.0
Kusikiliza
Mada 2.0
Kuzungumza
Mada 3.0
Kusoma
Mada 4.0
Kuandika
Somo la 1.4
mawasiliano bora
Kukia mwisho wa
somo mwanafunzi
aweze:
a) Kusikiliza kwa
makini kubwa
urari, nyimbo,
mazungumzo na
hadithi.
b) Kusikiliza na
kuwasiliana
ifaavyo katika
hali tofauti.
ch) Kusikiliza visa
vya wengine na
kushawishika
ifaavyo kwa
mawazo
yanayojitokeza.
d) Kuvutiwa
na kusikiliza
vifungu
vya mada
mbalimbali.
Somo la 2.4
Kuzungumza
kujihusu
Kukia mwisho
wa somo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kueleza
kwa ujasiri
wahusika na
matukio katika
hadithi au
kifungu.
b) Kuona
uhusiano
uliopo baina
ya wahusika
na matukio
ya hadithi na
uhalisia wa
maisha.
ch) Kuwa na
hamu ya
kuzunngumza
na watu
amaowajua
akitumia
mawasiliano
ya kutamka na
kutotamka.
Somo la
3.4 Kujibu
maswali ya
ufahamu
Kukia mwisho
wa somo
mwanafunzi
aweze :
a) Kutambua
mambo
muhimu
kwenye
majibu ya
maswali
ya vifungu
ilivyosomwa
b) Kufupisha
vifungu kwa
kutambua
mambo
muhimu.
ch) Kutambua
maana ya
maneno
asiyoyajua
kimuktadha.
Somo la 4.4
Uandishi wa
kibunifu
Kukia mwisho wa
somo mwanafunzi
aweze:
a) Kutumia maarifa
ya hatua za
kuandika kwa
ubunifu kuandika
vifungu vyake?
b) Kundika vyema
sentensi kwa
kuzingatia tofauti
ya sntensi, urefu
na ruwaza.
ch) Kutumia
viunganishi
kuunda sentensi.
d) Kujieleza kisanii
kupitia uandishi
e) Kuamua
kuandika akiwa
pekee na muda
wake kibinafsi.
78
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
1. Mawasiliano na ushirikiano
2. Uwezo wa kukiri na kutatua matatizo
3. Ubunifu na uwezo wa kukiri
4. Ujuzi wa kidijitali
Uhusiano na masuala mtambuko
1. Ujuzi wa kujua jinsi ya kuishi na watu wengine katika jamii unakuzwa
kutokana na kushirikiana vyema na wenzao katika makundi na mawasiliano
bora.
2. Uraia unakuzwa kutokana na kuungana na utangamano wa kijamii.
3. Shughuli za kuwafaa wanafunzi kupitia ushauri na uelekezi.
Uhusiano na desturi na maadili ya jamii
a) Heshima
b) Uwajibikaji
ch) Umoja
d) Uadilifu
e) Kujithamini
Uhusiano na masomo mengine
Masomo mengine
Shughuli nyingine zisizo rasmi zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
a) Wanafunzi wanashiriki katika mazungumzo na wenzao na viongozi wafaao
kuhusu hali zao.
b) Wanafunzi wanahimizwa kujieleza hisia zao kwa wanafunzi wenzao.
ch) Wanafunzi wanafanya mazoezi ya kuwasomea wenzao maandishi mepesi.
d) Wanafunzi wahimizwe kuandika na kuwaonesha wenzao.
Shughuli za kijamii zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
a) Wanafunzi wakariri mashairi yanayohusu mada nyepesi.
b) Wanafunzi wanawashirikisha watu walio karibu nao katika mazungumzo.
ch) Wanafunzi wasome jumbe mbalimbali katika jamii kama vile vibandiko na
mabango.
d) Wanafunzi wanashiriki katika mashindano ya uandishi na kuandika kila wakati
kwa furaha na kujifurahisha.
Nyenzo za ujifunzaji zinazopendekezwa
Vifaa vya kurekodi sauti na video, vitabu vya kusoma,vifaa vya maigizo, kadi za
picha, mjuzi, magazeti, majarida, ramani, vifaa vya kuchapisha,vitabu, gundi, mkasi
na mikato ya sentensi.
Tathmini zinazopendekezwa
1. Mawasilisho ya kisimulizi.
2. Jopo la kujadili masuala yanayohusu jamii kama vile funza, Malaria, mafuriko
n.k.
79
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
3. Maswali na majibu na kujaza mapengo.
4. Wanafunzi waandike kisa kuhusu picha fulani.
Kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalum
Usaidizi kwa wanafunzi wenye
uwezo mbalimbali
Usaidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji
maalum
Himiza wanafunzi wenye uelewa
wa polepole kushiriki katika
mazungumzo kama maigizo na
kusimulia hadithi.
Wape wanafunzi wenye uelewa
wa haraka kazi nyingi ili kuepuka
kuwachosha na kuzubaa darasani.
Wape wanafunzi wenye uelewa
wa polepole na haraka nafasi
za kutosha katika shughuli
za darasani. Una jukumu
la kuhakikisha kwamba
wanafurahiana na kufurahia kukaa
pamoja licha ya tofauti zao.
Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona, wape breli, picha za kugusa na
wale wasioweza kuona vizuri wape
maandishi makubwa.
Kwa wanafunzi wasiosikia vizuri tumia
lugha ishara au kumleta mtaalamu wa
lugha ishara kufasiri.
Wanafunzi ambao hawawezi kuona
mbali wakae mbele darasani na wenye
uwezo wa kuona mbali wakae nyuma.
Wape wanafunzi wenye ulemavu
majukumu wanayoweza kutekeleza
kama vile kuigiza nafasi ya mwalimu
mkuu au balozi wa kijiji. Wape usaidizi
wa kutosha na kuhakikisha kwamba
wanafunzi wengine wanafanya hivyo,
kwa mfano, kuwasaidia katika kusukuma
kitimaguru kwa mwanafunzi mlemavu.
Wiki ya 11
Somo la 1: Tucheze mchezo
Mpangilio wa vipindi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a. Kusikiliza urari, nyimbo, mazungumzo na hadithi kwa kina.
b. Kusikiliza na kuwasiliana vyema katika hali tofauti.
Habari za kimsingi
Katika kipindi hiki, mwanafunzi ajihusishe katika shughuli zinazomhitaji kusikiliza
hadithi, mazungumzo na urari kwa makini ili wawaeleze maraki ma familia.Hii
itasaidia kuimarisha stadi ya kusikiliza.
80
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Nyenzo za ujifunzaji
Vitabu vya hadithi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 69-70
Hadithi
Hapo zamani za kale, wanyama wote walikuwa maraki wakubwa.Waliishi maisha
ya amani na furaha.Mfalme wao alikuwa simba.Wakati mmoja kulikuwa na kiangazi.
Visima na mito vilikauka. Mfalme simba akawaita wanyama wote kwenye mkutano.
Wanyama wote walipokutana, wakaongea kuhusu tatizo la maji na kuamua kuchimba
kisima. Sungura alikuwa mvivu sana, akadanganya kuwa mgonjwa. Wanyama
waliendelea kuchimba kisima.Kila asubuhi, walipoenda kuchimba kisima, walimwona
sungura akicheza nje ya nyumba yake.
Wanyama walifanya kazi kwa bidii.Walichimba kisima kikubwa. Siku moja waliyakia
maji.Maji yalijaa na kujaza kisima. Walifurahi sana.Walikunywa maji na kuyaoga.
Walifurahi na kucheza muziki. Sungura aliposikia muziki wao, alicheka na kwenda
kuungana nao.
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wacheze wimbo wa ‘Simon anasema.’Kwa
mfano, Simon aanasema, simama, Simon anasema keti. Mwanafunzi mmoja au wawili
waende mbele na kuwaongoza wenzao.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi kutazama picha kitabuni mwao na kuwaongoza kuongea
kuhusu picha.Tumia maswali ya kuelekeza kama:
a) Mwaona nini pichani?
b) Nini kinachoonekana pichani?
2. Waambie wanafunzi wabashiri na kuwaambia wenzao kinachotendeka katika
hadithi.
3. Sikiliza ubashiri kutoka kwa wanafunzi wawili na uwahimize wanafunzi
kutumia maswali kubashiri yatakayotendeka. Hakikisha kuwa kila
mwanafunzi anashiriki.
4. Waambie wanafunzi wafunge vitabu na kusikiliza rekodi au unapowasomea
hadithi(Soma hadithi mara mbili au tatu kwa sauti inayosikika.Tumia kasi
ambayo wanafunzi wote wataelewa).
5. Ongoza majadiliano ya wanafunzi kusaidia kujua ikiwa ubashiri waliofanya
ulikuwa sawa.
6. Wanafunzi kuwaambia wenzao hadithi mmoja baada ya mwingine
(Zunguka katika makundi wanapoelezana hadithi)
7. Toa majibu yafuatayo kutoka kwenye hadithi:
a) Wanyama wote. Wataje baadhi kama vile simba, si, jogoo, twiga
miongoni mwa wengine lakini wasisitiziwe kwamba wanyama walikuwa
wote isipokuwa sungura.
81
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
b) Walikuwa wakizungumzia tatizo la maji. Pia:
i) Kiangazi- ni jibu, lakini ndicho kisababishi cha ukosefu wa maji.
ii) Kuchimba kisima- ndio ulikuwa uamuzi.
8. Hakikisha kuwa wote wanahusika ili kuleta mawasiliano na ushirikiano
miongoni mwa wanafunzi na maadili kama heshima na umoja
wanaposhirikiana katika shughuli za darasa.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwauliza maswali mepesi kuhusu hadithi ya kujibiwa kwa
mazungumzo.Hili litasaidia kutathmini uelewa wa wanafunzi wako
Tathmini
Waongoze wanafunzi kujibu maswali vitabuni mwao kwenye makundi wakitumia
majibu yaliyotolewa.
Zoezi la kufanyia nyumbani
1. Waambie wanafunzi wako wawaeleze wazazi wao hadithi waliyosoma.
2. Waambie wanafunzi wawaambie wazazi wao wawahadithie kisa cha kusisimua.
Somo la 2: Sikiliza na uigize
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi,mwanafunzi aweze:
a) Kusikiliza hisia ya wengine na kuchangamkia vyema hisia na mawazo yao
b) Kusikiliza na kuwasiliana vyemakatika hali mbalimbali
Habari za kimsingi
Kupitia kipindi hiki, wanafunzi wafanye mazoezi ya mawasiliano kwenye makundi,
wawili wawili au darasa zima. Jambo la kusisistiza ni kusikiliza. Mwanafunzi
amsikilize msemaji na awe tayari kumsikiliza msemaji na kuchangamkia hisia na
mawazo yake. Hili litaimarisha stadi ya mawasiliano na umuhimu wa heshima kwa
kila mmoja.
Nyenzo za ujifunzaji
Vitabu, vifaa vya kutazama na kuona, na chati.
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 70-71
Swali la kuongoza
Je, tunawasiliana vipi?
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi waziseme hadithi walizoambiwa na
wazazi au walezi wao.
82
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wasikilize rekoda kwa makini (Ikiwa huna kifaa cha
kurekodi,wasomee wanafunzi hadithi)
Kisa cha 1
Siku moja, Barry alitaka kupiga meno mswaki. Alitafuta mswaki jikoni lakini
hakuupata. Akiutafuta bafuni lakini hakupata. Akatafuta kwenye chumba cha kulala
lakini hakupata.Alienda sebuleni ambapo mama alikuwa akifagia akamauuliza,”Mama,
mswaki wangu u wapi?” Mama akasema, Umo kabatini.” Barry alipanda kitini na
kutazama kabatini. Hapo ndipo alipouona mswaki. Aliuchukua na kuelekea bafuni
kupiga meno mswaki.
Kisa cha 2
Barry na Sara walikuwa wakitoka shuleni wakikimbia kuelekea nyumbani. Walikuwa
na furaha. Barry alijikwaa na kuanguka. Aliumiza mguu wake na kuanza kulia.Sara
alimsaidia kuinuka na kupangusa vumbi kwenye nguo. Akamwambia pole, wakaenda
nyumbani polepole.
2. Waambie wanafunzi wawaeleze wenzao kisa wakiwa wawili wawili.
3. Waambie waigize kisa katika makundi (Baadhi waigize wahusika wa kisa,
wengine wakiangalia polepole. Kisha wabadilishane).
4. Uliza maswali haya:
Kisa cha 1
i. Barry anatafuta nini?
ii. Alitafuta wapi mswaki?
iii. Nani alimwambia barry mahali mswaki ulikuwa
iv. Aliupata wapi mswaki?
Kisa cha 2
i. Taja majina ya mvulana na msichana kwenye kisa
ii. Barry na Sara walikuwa wakitoka wapi?
iii. Nani alianguka?
iv. Sara alimwambia nini mwenzake?
5. Waambie wanafunzi wajibu maswali ya kusikiliza kwa kuzungumza ili
utathmini uwezo wa kusikiliza na kuzungumza.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wajadili umuhimu wa kusikiliza wakati
wa mazungumzo.
Kipindi hiki kitaimarisha stadi ya maisha ya kutambua na kuishi na wengine kupitia
mawasiliano bora.Hakikisha kuwa kila mwanafunzi anahusika kikamilifu ili kukuza
mawasiliano, ushirikiano na umoja.
Tathmini
Waambie wanafunzi wajadiliane katika makundi mambo matatu au manne yaliyotangazwa
gwarideni na aliyetangaza.
83
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 3: Igiza na urekodi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuzungumzia kwa ujasiri wahusika na matukio katika kisa au kifungu.
b) Kuwahusisha wahusika na matukio ya kisa na hali halisi ya maisha.
Habari za kimsingi
Kupitia kipindi hiki, wanafunzi watapata ujasiri wa kusimama mbele ya wenzao na
kuigiza baada ya kusikiliza.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 71-72.
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kurejelea somo la awali
Shughuli za ujifunzaji
1. Wasomee kwa sauti mazungumzo yafuatayo:
Barry: Nilikuwa nikikimbia nikaanguka.
Pam: Pole, umeumia?
Barry: Kidogo tu.
Pam: Hatuchezi leo, nitawasomea kisa.
Barry: Asante Pam.
2. Wakiwa katika makundi, waigize maigizo kati ya Barry na Sara. Sisitiza kuwa
wanafunzi waoneshe hatua zifaazo wanapoigiza
3. Waeleze wanafunzi warekodi mazungumzo kwenye kifaa cha kurekodi
(Waelekeze wanafunzi kutumia kifaa cha kurekodi).
TANBIHI: Zunguka ukisikiliza majadaliano kwenye makundi, ukiwapa maelekezo
na masahihisho ifaapo
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi umuhimu wa kusikiliza kwa umakini
wanapozungumziwa.Waelekeze wanafunzi kuelewa kuwa mazungumzo pia yanahusu
mawasiliano ya kutotamka maneno.Hili humsaidia mzungumzaji kuelewa ujumbe
vyema.
Tathmini
Waelekeze wanafunzi kufanya kazi wawili wawili kupata majibu ya maswali kwenye
Kitabu cha mwanafunzi.
84
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waelekeze wanafunzi kuendelea kufanya mazoezi ya mazungumzo pamoja na
maraki zao wanapokuwa na nafasi.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 71
Mwalimu atathmini usomaji wa wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 72
Mwalimu atathmini maigizo ya wanafunzi.
Somo la 4: Kueleza hadithi upya
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuonesha uwezo wa kuzungumza na
watu anaowajua akitumia mbinu za mawasiliano na zisizo za mawasiliano.
Habari za kimsingi
Kipindi hiki ni cha kumwongoza mwanafunzi kuwazungumzia watu awajuao vyema.
Hili linakuza stadi za uwajibikaji, maadili na heshima. Hili litakuza stadi za kuwajua
na kuishi na wengine kwa kuwasiliana nao vyema. Jaribu kuchanganya na stadi ya
Kusikiliza kwani inahusu mbinu za maisha katika somo la 1.4.
Nyenzo za ujifunzaji
Vitabu, redio/simu ya rununu/kifaa cha kurekodi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 72
Utangulizi
Wahusishe wanafunzi katika uigizaji wa kuwasalimu watu tofauti wa vyeo tofauti.
(Hakikisha kuwa kuna usawa wa kijinsia na viwango vya wanafunzi ili wa viwango
tofauti wahusike.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waongoze wanafunzi kueleza hadithi walizoambiwa na walezi wao wakiwa
wawili wawili.
2. Waongoze wanafunzi watulie wakapo katikati ya visa vyao na kuwauliza
wenzao wanaowambia visa wajaribu kubashiri kisa kitakavyoendelea.
3. Zunguka katika kila kundi kuhakikisha kuwa wanahusika kikamilifu
4. Thibitisha kutoka kwa wale wanaosema visa ikiwa ubashiri wa maraki zao
uko sawa.
5. Thibitisha kuwa wanachama wanabadilishana majukumu na kujibu maswali
ya Kitabu cha Mwanafunzi.
6. Kila mwanafunzi ashiriki, ili kuwepo mawasiliano na ushirikiano miongoni
85
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
mwao na kukuza maadili ya heshima na umoja huku wanafunzi wakishirikiana
na wenzao katika shughuli za darasani.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi kurekodi hadithi watakayosimuliwa
nyumbani na mzazi au mlezi wako.
Tathmini
Waelekeze wanafunzi kutathmini masimulizi ya wenzao.
Majibu
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 5: Kubuni hadithi upya
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kuhusisha wahusika na matukio
kwenye hadithi na hali za maisha.
Habari za kimsingi
Ili kipindi kifanikiwe, mwanafunzi atahitajika kusikiliza kwa makini kisa kilichorekodiwa,
afahamu kisa na kukihusisha na maisha halisi katika shughuli za kila siku.Wajihusishe
katika shughuli za kutumia vifaa vya elektroniki kujifanyia rekodi zao.Hili litaimarisha
ubunifu na kukiria kwa kina, stadi za ushirikiano pamoja na stadi za masomo ya
kidijitali.
Nyenzo za ujifunzaji
Simu, rekoda
Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 73
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi waeleze visa vifupi wanavyojua.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wasikilize kifaa cha kurekodi kwa makini. (Hadithi
ya kurekodiwa iwe kuhusu utovu wa nidhamu na jinsi aliyekosa nidhamu
aliadhibiwa) Hadithi zinazopendekezwa:
a) Msichana ambaye hakujua kuweka siri.
b) Msichana aliyependa kusikiliza mazungumzo ya watu.
ch) Mvulana na mbwamwitu.
2. Jadiliana kisa hicho na wanafunzi. Waulize maswali ya kuwaongoza kuzua
mambo muhimu katika hadithi.
3. Waambie wafanye kazi katika makundi na kubuni mbinu za kukamilisha kisa
walichoanzishiwa. Kwa mfano,
Kulikuwa na msichana ambaye hakupenda kufuata maagizo…
86
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
4. Waongoze wanafunzi kurekodi na kusikiliza hadithi waliyorekodi kwenye
kifaa
5. Waruhusu wanafunzi waeleze hadithi iliyowapendeza kwa kunyosha mkono.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kukosoa baadhi ya makosa kama vile ya lugha au ya vifaa
vya kurekodi.
Tathmini
Waambie wanafunzi wabadilishane vifaa vya kurekodi na wale wa makundi mengine
na kusikiliza hadithi za wenzao.
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waambie wanafunzi wawaambie wazazi kuwasaidia kurekodi hadithi zaidi
wakitumia simu
Wiki ya 12
Somo la 1: Kusoma
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kuvutiwa na usomaji wa visa na
vifungu.
Habari za kimsingi
Ni kipindi cha kuvutia makini ya mwanafunzi katika kusoma visa kivyao, ili wawaeleze
wenzao kivyao au darasani.
Nyenzo za ujifunzaji
Vitabu, chati na magazeti
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 73-74
Utangulizi
Wanafunzi wasome na kusema vitanza ndimi kutoka kwenye chati. Kwa mfano:
a. Shirika la reli la Rwanda
b. Mbuzi hali nazi hapandi ngazi afanye kazi
Shughuli za ujifunzaji
1. Waongoze wanafunzi kutazama picha kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 73. Wapange katika makundi na kuwaruhusu kujadili maswali haya:
a) Unapenda chumba kipi?
b) Mbona unakipenda?
87
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Jawabu linalotarajiwa
Chumba cha kwanza
Waruhusu wanafunzi kutoa majibu tofauti ya sababu ya kupenda chumba cha
kwanza.
2. Waruhusu wajadili jinsi ya kufanya chumba kiwe nadhifu.’Kila mwanafunzi
achangie kwa kusema jambo moja linaloweza kunadhisha chumba.Wengine
wapige mako kila jawabu linapotolewa. Sahihisha kwa kupongeza juhudi za
kila mwanafunzi kisha utoe jawabu linalofaa.
3. Chagua makundi mawili kuwasilisha matokeo yao darasani, yaani, chumba
kipi wanakipenda na sababu ya kukipenda. Waruhusu wengine kuongezea
kutoka kundi lolote.
Hitimisho
Kamilisha kwa kuwaongoza kujadili picha.
Tathmini
Sikiliza majadiliano ya wanafunzi wote kuhusu vyumba hivyo.
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waambie wanafunzi wawasomee wazazi wao sentensi kuhusu chumba nadhifu wakapo
nyumbani.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 73
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi
Zoezi la 2, ukurasa 74
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi
Zoezi la 3, ukurasa 74
Mwalimu atathmini masimulizi ya wanafunzi
Somo la 2: Kusoma ufahamu
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kusoma na kuelewa hadithi na
kufuatilia masuala maalum akirejelea maswali ya kifungu alichosoma.
Habari za kimsingi
Katika kipindi hiki, wanafunzi wahusike katika shughuli za kuwaongoza kutambua
mambo maalum wanayohitaji ili kujibu maswali ya kifungu. Hili litasaidia kukuza
ubora wa kibinafsi.Wakifanya kazi katika makundi na wawili wawili, stadi zao za
mawasiliano na ushirikiano zitaimarishwa.
88
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Nyenzo za Kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 74-75
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kurejelea kipindi cha awali kwa kuuliza wanafunzi maswali
na kuwaruhusu kuyajibu.
Shughuli za ujifunzaji
1. Soma kisa kwa sauti(mara mbili)huku wanafunzi wakisikiliza na kufuatilia
kisa cha Mutulu amkasirisha mama yake kwa makini.(Kwenye kitabu cha
wanafunzi).
2. Waeleze wasomaji kusoma hadithi wakiwa wawili. Waruhusu wanafunzi
kusoma mmoja baada ya mwingine wakiwa wawili wawili.
3. Wapange wanafunzi katika kundi. Waruhusu kuwaambia wenzao visa vyao na
uhusiano wa hadithi.
4. Zunguka darasani kutazama maendeleo ya kila kundi.
5. Wanafunzi wajibu maswali katika kitabu cha wanafunzi.
Majibu
Zoezi la ukurasa 75
1. Jumamosi
2. Kazini
3. Mutheu na Mutulu
4. Chumba cha Mutulu ni kichafu.
5. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Waruhusu wawe wawili wawili na kujibu kuanzia swali la 5. Zunguka darasani na
kusikiliza kinachofanywa na kila kikundi. Sahihisha.
Hitimisho
Waulize maswali mepesi kuhusu hali zao binafsi. Mfano, nani husasha vyumba
vyao, wakati gani.Wanasaidia vipi nyumbani?
Tathmini
Teua wanafunzi wowote darasani wasome hadithi. Wenzao wasaidie walio na shida
ya kusoma.
Somo la 3: Kutafuta maana
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi atambue mambo muhimu yanayohusu maswali
ya kifungu.
89
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Shughuli zake zitahusu kujibu maswali ambayo majibu yake yanatoka kwenye hadithi.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 75
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi wasome hadithi ya Mutulu amkasirisha
mama yake.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waongoze wanafunzi kujibu maswali kwa kufuata hatua zifuatazo::
a. Soma maswali na kuelewa. Jaribu kutambua hoja muhimu zilizoulizwa.
Mfano, “Ni siku gani?” Jambo muhimu ni siku.
b. Waongoze wanafunzi kurejelea hadithi na kusoma kwa kuzingatia hoja
muhimu iliyoulizwa (Waeleze wasome na kutulia wanapoona jawabu.
Kwa mfano, Kila Jumamosi…)
ch. Msomaji anaotambua jibu, mruhusu kusoma swali tena na kutoa jibu.
d. Tumia njia hii kujibu maswali mengine.
e. Wape swali wajibu wakifuata hatua hizo katika makundi.
2. Shughuli hizi za kujibu maswali darasani zitasaidia kuleta kujitahamini kwa
mwanafunzi. Hakikisha wanafunzi wote wanashiriki na kukuza umuhimu wa
kujitolea kujibu maswali.
Hitimisho
Sisitizia mwanafunzi umuhimu wa kuelewa swali, kutambua hoja muhimu na kurejelea
hadithi kujibu.
Tathmini
Waambie wanafunzi wajadili na kufanya mazoezi yaliyotolewa vitabuni katika kundi.
Sisitiza kuwa wafuate utaratibu.
Zoezi la kufanyia nyumbani
Wape wanafunzi zoezi hili la kufanyia nyumbani:
Pamoja na wengine darasani na nje ya darasa, tafuteni hadithi zaidi.
Somo la 4: Kupata maana
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo mwanafunzi abaini maana ya maneno asiyojua kulingana
na muktadha.
90
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Kipindi kitamsaidia mwanafunzi kwa kumhimiza kukiria vyema na kwa undani ili
kuapata maana ya maneno magumu kimuktadha. Kufanya kazi pamoja katika makundi
kunaimarisha stadi za mawasiliano na ushirikiano. Pia, inaleta maadili ya kuwajibika
na heshima kwa wengine kwani wanafaa kuwaheshimu wenzao na maoni yao.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Vitabu, magazeti, chati
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 76
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kusoma kisa cha awali cha Mutulu
amkasirisha mama yake kimoyomoyo na kuandika maneno magumu katika hadithi.
Shughuli za ujifunzaji
1. Onesha chati ikiwa na maneno magumu yaliyoandikwa kitabuni. Waambie
wanafunzi wasome maneno kwa sauti.Kosoa matamshi inapobidi.
2. Waambie wanafunzi waongeze neno lolote kwenye hadithi linaloonekana
kuwa gumu.
3. Waambie wanafunzi wajadili maana ya maneno kwenye hadithi katika
makundi kisha waandike maana yake.
4. Waambie wanafunzi wafunge vitabu. Waongoze kupata maana ya maneno
kwa kuyaandika kwenye chati ifuatavyo:
a. Kiamsha kinywa - chakula cha kwanza cha siku kinacholiwa asubuhi.
b. Kitamu - ladha nzuri
ch. Kukagua - kuangalia vizuri
d. Kichafu - hakikupangwa
Msamiati mpya
a. Kiamsha kinywa
b. Kitamu
ch. Kukagua
d. Kichafu
Hitimisho
Waambie walinganishe majibu yao na yako kwenye chati. Waulize ikiwa yanafanana.
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waambie wanafunzi wawaambie wenzao nje ya darasa maana ya maneno mapya.
Somo la 5: Kusoma kwa kujifurahisha
Tokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi afupishe ujumbe kwa kutambua mambo
muhimu.
91
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Shughuli za kipindi hiki ziwaongoze wanafunzi kutambua hoja muhimu katika kifungu
ili wapate muhtasari.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Vitabu, magazeti, vifaa vya kusoma darasani
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 76-77
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuonesha chati na kuwaambia wanafunzi wasome maneno
kwenye chati. Waruhusu wasomaji kusoma kwa sauti. Maneno ni kama uraibu,
shindano, shiriki, tangaza.
Sahihisha matamshi ya mwanafunzi inapobidi.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waongoze wanafunzi kupata maana ya maneno kwa kuyajadili darasani.
Eleza maana ya maneno yasiyojulikana na wanafunzi wote na kusahihisha
wasipoelewa.
2. Waongoze wanafunzi kusoma hadithi ya ‘Ushindi wa Martin’Wasomee
wanafunzi kwa sauti kisha uwaruhusu wanafunzi kujisomea wakiwa wawili
wawili.
3. Waongoze wanafunzi kutambua hoja muhimu katika hadithi.Wafafanulie
wanafunzi kwamba wanafaa wakumbuke mambo hayo baada ya kusoma
hadithi. Wafafanulie kwamba, katika kufupisha, ni mambo muhimu pekee
yanayoandkwa. Waongoze kutambua hoja muhimu unapoziandika ubaoni.
Onesha hoja zifuatazo muhimu kutoka kwenye hadithi ya ‘ushindi wa
Martin’.
a. Martin ana miaka saba.
b. Uraibu wake ni kucheza kandanda na kusoma hadithi.
ch. Alishinda shindano la kuandika.
d. Anaenda katika shindano la kitaifa.
4. Waweke katika kikundi cha wanafunzi watatu.Waambie wajadili majibu ya
maswali ya shughuli ya pili katika kitabu cha mwanafunzi.
5. Wanafunzi wanaposhiriki katika shughuli hizi za kutambua hoja muhimu
kutoka kwenye hadithi iliyoskilizwa kutoka kwenye rekoda, wanakuza
ujuzi wa kidijitali. Wanapofanya kazi wakiwa wawili wawili au kimakundi,
wanakuza ujuzi wa mawasilaino na ushirikiano.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wasome kwa sauti muhtasari wa hoja
muhimu ubaoni.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike hoja za muhtasari zilizojadiliwa vitabuni mwao.
92
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waambie wanafunzi wachague kisa au gazeti wapendalo.waambie wachague aya
kisha wafupishe. Waambie wazazi au wakubwa wao kuwasahihishia palipo na kosa.
Wiki ya 13
Somo la 1: Shughuli baada ya kutoka shuleni
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kudhihirisha matendo ya kisanii kupitia
uandishi.
Habari za kimsingi
Ili kipindi kifaulu,waandae wanafunzi kabla ya kipindi na uwaambie watafute vifaa
vya kufanikisha somo kama vile picha za mambo wanayofanya baada ya shule.
Kipindi kinamfaa mwanafunzi kwani anapata stadi za ubunifu na kuwaza kwa kina
kupitia matumizi ya vifaa vya kisanii na kuvitumia kuunda kitu kinacholeta maana
(Cha kuleta hadithi). Wakifanya kazi katika kundi, wanaendelea kuboresha stadi za
mawasiliano na ushirikiano na maadili ya heshima na uwajibikaji.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Vipande vya magazeti,ramani, vifaa vya chapa na makasi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 77
Swali kuu
Tunapanga vipi mawazo kupata hadithi ya kuvutia?
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kurejelea kipindi kilichopita. Waambie wanafunzi wachache
wasome kwa sauti muhtasari wa kazi waliyoifanyia nyumbani.Wateue kwa
kuzingatia jinsia, uwezo na ulemavu wa mwili
Shughuli za ujifunzaji
1. Waongoze wanafunzi wawe wawili wawili na kuambiana shughuli wanazofanya
baada ya shule. Wakumbushe kutumia stadi za mazungumzo walizosoma awali
kama vile kusikiliza kwa makini, kumtazama msemaji kwa makini, kujibu tu
mzungumzaji anapomaliza kuzungumza, kuzumgumza na hisia zifaazo.
2. Waambie wanafunzi watafute picha za shughuli wanazofanya baada ya shule
kutokana na kazi walizoleta na zile uliziongeza.
93
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
3. Waambie wanafunzi waendelee kufanya kazi kimakundi na wapange picha
za kuleta kisa cha kufurahisha. Zunguka darasani ukitazama kazi yao na
kuwasaidia ifaapo.
Hitimisho
Waulize wanafunzi wote, ‘Nini hufanya kisa kipendeze?’ Waruhusu waeleze mawazo
yao na kuwatuza kwa mawazo mazuri na kwa kujaribu kutoa majibu.Wafafanulie
kuwa uchaguzi na mpangilio wa picha ndizo huleta kisa kizuri, hivyo wazingatie hayo
katika kazi yao.
Tathmini
Wanafunzi wanapoendelea kupanga na kupangua picha zao, zunguka ukiangalia kazi.
Zoezi la kufanyia nyumbani
Wambie wanafunzi watafute picha nzuri na kuandaa hadithi za kutumika katika kipindi
kijacho. Waambie kuwa wazazi, walezi na wenzao wanaweza kuwasaidia kutafuta.
Somo la 2: Kutengeneza kitabu cha picha
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipndi,mwanafunzi aandike vyema kwa sentensi tofauti kimuundo,
urefu na mipangilio.
Habari za kimsingi
Andaa kipindi mapemana kutoa vifaa vinavyohitajika au uwaambie wanafunzi walete
vifaa. Wanafunzi wanaweza kusaidiana vifaa ili kukuza ushirikiano na kuishi vyema
na wengine. Hili litazua maadili ya heshima, umoja na kujithamini
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Pichaa, mkasi, hundi na kitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 78
Swali kuu
Tunapanga vipi mawazo kuzua kisa cha kuvutia?
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi waoneshane zoezi lao la nyumbani. Waongoze
kutazama kazi za wenzao na kuchagua iliyo bora. Linganisha kazi ili waone iliyo bora.
Waambie wanafunzi wapigie mako waliofanya vyema.
94
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Waongoze katika hatua za kuunda kitabu cha picha (hakikisha kuwa wanafunzi
wote wanaona na kutazama kwa kina).
Hatua zinazopendekezwa
i) Panga picha kwenye dawati.
ii) Andika nambari ndogo chini kuanzia ya kwanza hadi mwisho zikifuatana.
iii) Andika nambari kwenye daftari, mahali ambapo utabandika picha ikiwa
na nambari hiyo.
iv) Kwa kutumia gundi, bandika picha zako kwa uangalifu zikifuatana ili
kazi isiwe chafu.
v) Ipe nafasi ya kuganda ili kazi isichafuke.
2. Waambie wanafunzi wafuate hatua hizo na kuunda vitabu vyao vya pichan
wakiwa katika makundi.
3. Waambie waandike sentensi zinazofaa kulingana na picha za kitabu.
Hitimisho
Hitimisha kwa kuambia kila kikundi kipeleke kazi kwenye meza ya mwalimu.
Tathmini
1. Waongoze wanafunzi kumchagua mwanfunzi mmoja kutoka kila kikundi kuwa
mwamuzi. Waambie wachague yule mwaminifu.
2. Zungumza na waamuzi waliochaguliwa na usisitize kuhusu uaminifu.Waongoze
katika hoja watakazozingatia wanapochagua picha bora. Mfano, inayovutia zaidi,
iliyopangwa vyema na sa, inayoleta kisa kizuri na sentensi zikiambatana na
picha.
3. Wape wanafunzi nafasi wafanye uamuzi.
4. Wapongeze washindi na kuwahimiza wengine
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waambie wanafunzi watumie picha za awali za zoezi la nyumbani kuunda kitabu
cha picha, kisha waandike sentensi zinazoambatana na picha hizo.
Somo la 3: Kutunga hadithi kutokana na picha
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutambua viunganishi mwafaka katika
sentensi.
Habari za kimsingi
Kipindi kinahitaji maandalizi (tafuta picha na sentensi zinazofanana kwa kila kikundi).
Wanafunzi waendelee kufanya kazi katika makundi.Wakumbushe wanafunzi sheria za
95
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
kimakundi kama vile kila mmoja kumakinikia kazi ya makundi. Wape wanakikundi
nafasi sawa na uwaruhusu wanafunzi kusaidiana panapofaa.
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Picha, hundi, sentensi zilizokatwa, kitabu, chati
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 79
Swali muhimu
Tunapanga vipi mawazo kufanya hadithi ivutie?
Utangulizi
Kwa kutumia chati yenye maelezo ya kuunda kitabu cha picha, tanguliza kipindi kwa
kuwaambia wanafunzi wasome kwa sauti yaliyo kwenye chati.
Shughuli za ujifunzaji
1. Kila kikundi kipewe picha kadhaa.
2. Waelekeze wanafunzi kupanga picha kuunda hadithi.
3. Bandika picha kwenye kitabu cha picha.
Hitimisho
Waambie wanafunzi wabadilishane kazi zao kimakundi na kulinganisha zao na za
wengine.
Tathmini
Angalia kazi na kutambua makosa waliyofanya kisha unakili.
Warudishie vitabu
Somo la 4: Kurekebisha makosa
Matokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia maarifa ya uandishi wa kibunifu
kuandika vifungu vyake na kurekebisha makosa katika vifungu walivyoandika.
Habari za kimsingi
Shughuli za kipindi hikizinamhitaji mwanafunzi atumie maarifa aliyopata katika
vipindi vya awali kurekebisha baadhi ya makosa katika uandishi.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu vya picha
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 79
96
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Swali muhimu
Tutapanga vipi mawazo kuunda sentensi ya kuvutia?
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwachemsha wanafunzi bongo kwa kutumia imla ya maneno
mepesi yaliyotumika katika somo kama vile kuosha, nguo, duka, viatu, na, sababu,
lakini, n.k.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wafanye kazi katika makundi. Wasahihishe makosa
waliyofanya kwenye kitabu cha picha katika somo lililopita.
2. Waambie wanafunzi kusoma kazi zilizosahihishwa kwenye makundi.
3. Waambie wanafunzi waweke mbali vitabu vilivyosahihishwa na wajaribu
kuandika upya kisa hicho katika vitabu vyao, kila mmoja kivyake.
Hitimisho
Kamilisha somo kwa kuwaambia wanafunzi wataje mambo muhimu katika hadithi.
Waambie wakusanye vitabu ili visahihishwe.
Tathmini
Sahihisha kazi iliyokusanywa
Wapangie wanafunzi wenye udhaifu somo la ziada
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waambie wanafunzi waandike mambo manne wanayosaidia wakiwa nyumbani.
Majibu, ukurasa 79
Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi
Somo la 5: Kutunga sentensi
Tokeo maalum la ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kupendelea kuandika akiwa na wakati.
Habari za kimsingi
Wakitumia ujuzi wa awali katika kipindi hiki, wanafunzi watahitajika kutunga kisa
kifupi kutoka kwa sentensi fupi. Mwalimu anafaa amsaidie kukua kutokana na makosa
na kumhimiza kuandika kila wakati.
97
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Nyenzo za ujifunzaji
Wanafunzi wenyewe
Vitabu na vifaa vya kuandikia
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 80-81
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kutaja baadhi ya viunganishi wanavyojua.
Wanapotaja, eleza matumizi yake katika sentensi. Waeleze matumizi ya viwakilishi ili
wasijirudierudie.
Shughuli za ujifunzaji
1. Uliza maswali mepesi na kuwaongoza wanafunzi jinsi ya kuanza majibu.
Mfano:
a. Mnawasaidia wazazi kufanya kazi zipi nyumbani?
Waambie waanze majibu yao kwa sentensi kama:
Ninawasaidia…
2. Wajibu maswali kwa kuzungumza katika darasa zima.
3. Waongoze kujibu maswali yaliyo kwenye kitabu cha kusoma. Kila mtu afanye
kazi kivyake.
4. Angalia kazi ya wanafunzi.
Hitimisho
Kamilisha kwa kuwambia wanafunzi kuwasilisha kazi yao darasani. Hakikisha usawa
wa jinsia na uwezo wa kundi wanafunzi yote yahusike. Watuze wawasilishaji.
Tathmini
Wanafunzi wanapowasilisha kazi, kosoa makosa darasani.
Zoezi la kufanyia nyumbani
Waambie wajikirie wakifanya kazi ya nyumbani wanayopenda.Waandike aya moja
kuhusu kazi hiyo.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 80
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 80-81
Mwalimu atathmini michoro ya wanafunzi.
98
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Sehemu
5
Fatuma aumia goti lake
Malengo mahsusi ya masomo
Mada 1.0
Kusikiliza
Mada 2.0
Kuzungumza
Mada 3.0
Kusoma
Mada 4.0
Kuandika
Somo la 1.5
Mazungumzo
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kusikiliza matini
zenye taarifa na
kudondoa hoja
muhimu
b) Kuuliza na kujibu
maswali yafaayo
katika matini ya
kusikiliza.
ch)Kuendeleza
mawazo na hoja
za wengine katika
mazungumzo kwa
kuunganisha hoja
zao na za wengine.
d) Kupanua ujuzi
wa msamiati
kwa kusoma kwa
makini na ufahamu
wa hoja za jumla
na zile mahsusi.
e) Kuonyesha
heshima kwa
wengine
anaposhiriki katika
mazungumzo.
f) Kufahamu
matumizi ya
lugha na mitindo
inayokubalika
katika jamii.
Somo la 2.5 Stadi
za kuwasilisha
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kujieleza
kikamilifu kwa
kutumia msamiati
aliojifunza
kuwasiliana kwa
ufanikifu
b) Kueleza shughuli
mbalimbali za
kijamii kwa
mfuatano ambao
zinatukia
ch)Kutumia
mabadiliko
mwafaka ya
kiimbo, matamshi
sahihi na mkazo
kujieleza kwa
ukakamavu
d) Kumbuka dhana
kuhusu maudhui
kwa kuzingatia
mantiki
e) Kubaini na
kutamka sauti
zenye heru
nyingi ili kujenga
silabi na maneno
Somo la 3.5
Kujibu maswali
ya ufahamu
Kukia mwisho
wa somo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kupata hoja
mahsusi katika
kujibu maswali
yanayohusu
matini
iliyosomwa
b) Kufupisha
matini
zilizosomwa
kwa kubaini
hoja muhimu
ch)Kupata maana
ya msamiati
mgeni
kutegemea
miktadha
Somo la 4.5
Uandishi wa
kiubunifu
Kukia mwisho
wa somo,
mwanafunzi
aweze:
a) Kutumia ujuzi
wa uandishi
wa kibunifu
kuandika matini
zake binafsi
b) Kuandika kwa
kueleweka
akitumia miundo
mbalimbali ya
sentensi, urefu
na ruwaza
anuwai
ch)Kutumia
viunganishi
mwafaka
kufuatanisha
sentensi
d) Kuonyesha kauli
za kisanii kupitia
maandishi
e) Kuamua
kuandika
kivyake katika
shughuli za
kujiamulia
99
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
1. Mawasiliano na ushirikiano unakuzwa kwa kufanya kazi katika vikundi.
2. Uwazaji makinifu na usuluhishaji wa matatizo unakuzwa katika kujibu
maswali na kusikiliza simulizi za wenzao.
3. Ubunifu na uwazaji kwa kina unaendelezwa na kuhimizwa katika kubuni visa
na kujibu maswali.
Uhusiano na masuala mtambuko
1. Stadi za maisha kujua na kuishi na wengine - mawasiliano fanikifu.
2. Stadi za kuelewa na kuishi yeye mwenyewe - kujiamini katika utekelezaji
wake.
3. Uraia unahimizwa katika muumano wa kijamii
Uhusiano wa thamani za maisha kitaifa
1. Uwajibikaji unahimizwa wanapofanya kazi wanazoagizwa.
2. Umoja unakuzwa kwa kufanya kazi katika vikundi.
3. Upendo unahimizwa wakishirikiana katka vikundi.
4. Heshima inahimizwa kwa kuheshimu wenzao katika vikundi.
5. Kujistahi kunakuzwa wanapojieleza na kusimulia visa vyao.
Uhusiano na masomo mengine
Maeneo yote ya ufunzaji
Shughuli nyingine zisizo rasmi zinazoweza kuchangia ujifunzaji
1. Wanafunzi kushirikiana katika mazungumzo yasiyo rasmi.
2. Wanafunzi washiriki katika mawasilisho ya kisimulizi yasiyo rasmi.
3. Wanafunzi kuwasilisha maarifa kutoka kwa matini walizosoma kwa wenzao
darasani na kwingineko.
4. Wanafunzi kuwasilisha maandishi yao kwa wenzao.
Mapendekezo ya huduma za kijamii katika ujifunzaji
1. Wanafunzi washiriki katika mazungumzo na wanajamii wazee katika jamii.
2. Wanafunzi kujieleza kwa wazazi/walezi.
3. Wanafunzi kusoma matini mbalimbali katika jamii kama vile matangazo na
mabango.
4. Wanafunzi kushiriki katika mashindano ya uandishi bunifu na kuandika kwa
starehe na burudani.
Nyenzo zinazopendekezwa
Rekoda za sauti na picha, vifungu vya kusimulia, vifaa vya sauti na picha, vielelezo,
picha za matukio mbalimbali, vitabu vya kusoma darasani, magazeti, majarida,
100
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
magazeti yaliyokatwa, ramani za hadithi, vifaa vya chapa, vitabu, gundi, makasi,
vipande vilivyoandikwa sentensi
Tathmini zinazopendekezwa
1. Wape mada ambazo watazingatia katika mazungumzo.
2. Kulinganisha picha na matukio, maswali/majibu.
3. Maswali/majibu, kujaza mapengo.
4. Wanafunzi kuandika hadithi iliyokitwa katika hadithi ya picha.
Kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalum
Usaidizi kwa usomaji wa wenye uwezo
wa viwango tofauti
Usaidizi kwa usomaji wa wenye
mahitaji ya kipekee
Himiza wanafunzi wenye uelewa wa
polepole kushiriki katika mazungumzo
kama vile uigizaji na usimulizi wa hadithi.
Wape wanafunzi wenye uelewa wa haraka
mazoezi ya ziada ili kuepuka kuwachosha
na kuzubaa darasani.
Wape wanafunzi wa viwango vyote viwili,
chini na juu, nafasi sawa za kushiriki
katika shughuli za darasani. Ni jukumu
lako kuhakikisha kwamba wanafurahiana
na kufurahia kukaa pamoja licha ya tofauti
zao.
Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
kabisa wape breli, picha za kugusa na
kwa wale wasioweza kuona vizuri, wape
mani zenye maandishi makubwa.
Kwa wanafunzi wenye matatizo ya
usikivu tumia lugha ya ishara au
ushirikishe mkalimani wa lugha ya ishara.
Waruhusu wanafunzi ambao hawaoni
mbali waketi mbele darasani na wale
wenye uwezo wa kuona mbali waketi
sehemu ya nyuma.
Wape wanafunzi wenye ulemavu wa
viungo nafasi ambazo wanaweza kuigiza
kama za mwalimu mkuu au mzee wa
kijiji. Wape msaada wa kutosha na
uhakikishe wanafunzi wenzao wamefanya
hivyo, kama kwa kusukuma kitimaguru
cha mwanafunzi mwenye ulemavu.
Wiki ya 14
Mpangilio wa vipindi
Somo la 1: Kufanya mazoezi ya mazungumzo
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuuliza na kujibu maswali mwafaka
katika matini ya kusikiliza.
101
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Wanafunzi wanatarajiwa kuuliza na kujibu maswali mwafaka katika miktadha fulani
na kuendeleza mazungumzo yaliyokitwa katika mada fulani kwa mtindo wa maswali
na majibu.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 82-83
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo huzungumza na maraki zao, aina za
mazungumzo ambazo huwa nazo na huzungumzia nini. Wanafunzi kadhaa wakueleze
nani raki yao darasani na wao huzungumzia nini wanapozungumza nao.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wachunguze picha iliyomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 82 na waeleze wanayoona katika picha.
2. Waagize wanafunzi wasome mazungumzo baina ya Nderitu na Chebet katika
jozi. Mwanafunzi mmoja asome ya Chebet na mwingine ya Nderitu. Hili
litaendeleza stadi za wanafunzi za mawasiliano na ushirikiano wanafunzi
wanaposhiriki katika mazungumzo.
3. Waambie wanafunzi wabadilishane nafasi na kusoma tena mazungumzo baina
ya Chebet na Nderitu.
4. Waambie wanafunzi wajifanye kuwa Nderitu na Chebet na watafute penseli
iliyopotea.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaeleza wanafunzi kanuni za mazungumzo. Waelekeze
wanafunzi namna wanapaswa kujibu maswali kutegemea umuhimu wa maswali
yaliyoulizwa bila kuyakwepa.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike mazungumzo baina yao na maraki zao wa dhati.
Waambie watumie mfumo wa:
Nderitu:
Chebet:
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 82-83
Mwalimu atathmini usomaji wa wanafunzi
Zoezi la 2, ukurasa 83
Mwalimu atathmini maigizo ya wanafunzi
102
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 2: Kariri na urekodi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kusikiliza matini zenye taarifa na
kudondoa hoja muhimu.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatarajiwa kuendeleza hoja walizopata kwenye mazungumzo na
wengine. Wanapaswa kuunganisha majibu na maswali ili kuendeleza mfululizo wa
mazungumzo. Hakikisha umeweka rekoda mahali mwafaka kurekodi shairi wakati
wanafunzi wanalikariri.
Vifaa vilivyopendekezwa
Wanafunzi wenyewe
Vitabu, rekoda za sauti na picha
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 83-84
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wanajua shairi au wimbo wowote
na unahusu nini. Waambie wanafunzi waimbe au kukariri mashairi hayo kwa
wenzao darasani.
Shughuli za ujifunzaji
1. Wakaririe wanafunzi shairi ambalo limo katika Kitabu cha Wanafunzi ukurasa
83.
2. Waambie wanafunzi wakariri shairi wakiwa wawili wawili, kisha kama darasa
zima.
3. Waambie wanafunzi wabainishe maswali katika shairi.
4. Wakiwa katika makundi, wanafunzi wajadili majibu yanayotarajiwa ya maswali
yaliyo kwenye shairi na waandike majibu yao. Zoezi hili litaendeleza suala
ibuka la uraia kupitia muumano wa kijamii wanafunzi wanaposhirikiana
kutafuta majibu na hivyo kuendeleza stadi za mawasiliano na ushirikiano.
5. Waambie wanafunzi wakariri shairi wakiwa darasa zima huku ukiwarekodi.
6. Wachezee rekodi hiyo na kuwaagiza waisikilize.
7. Waambie wanafunzi watunge sentensi wakitumia maneno: lini, kwa nini na
vipi katika muundo wa maswali na watoe majibu ya maswali yale.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaagiza wanafunzi kuulizana maswali kuhusu familia zao.
Kwa mfano: Una ndugu?
Jina la mama yako ni lipi?
Mu wangapi katika familia yenu?
103
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika maswali sita kuhusu shule zao na wawape wenzao
vitabu vyao wayajibu.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 83
Mwalimu atathmini ukariri wa wanafunzi
Zoezi la 2, ukurasa 84
Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi
Somo la 3: Kuzungumza kuhusu soko
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuendeleza dhana na mawazo ya
wengine katika mazungumzo kwa kuunganisha hoja zao na za wengine.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watazungumzia mambo waliyokumbana nayo sokoni. Watakita majibu
yao katika majibu yaliyotolewa na wanavikundi vyao hivyo kujenga mfuatano wa
mazungumzo uliojengwa kutokana na hoja ya kwanza iliyotolewa na mwanakikundi
wa kwanza aliyejibu maswali katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 84-85
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi kubadilishana vitabu na kusoma majibu
ya wenzao kutokana na zoezi la somo la 2. Waambie wanafunzi kadhaa kuelezea
majibu ambayo wenzao wametoa kuhusu shule yao.
Shughuli za ujifunzaji
1. Wapange wanafunzi katika makundi na uwaambie wajibu maswali kutoka
zoezi la 1 katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 84.
2. Waongoze wanafunzi uwaonyeshe namna ya kujibu swali bila kulirudia.
Baada ya mwanakikundi wa kwanza kujibu, wa pili anaongezea hoja kwa
yaliyosemwa na mwenzake.
3. Wanapojibu swali la tatu, waambie wanafunzi waeleze kuhusu wale watu
waliowaona.
4. Mazoezi katika somo hili yatawafaa wanafunzi kwa stadi za maisha kama vile
kujua na kuishi na wengine kupitia mawasiliano fanikifu. Wataweza kuuliza
na kujibu maswali yaliyokitwa katika hoja zilizomo kwenye mazungumzo
hivyo kujenga uwezo wa wanafunzi wa uwazaji makinifu na usuluhishaji
matatizo.
104
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
5. Waagize wanafunzi kuchunguza picha iliyo katika zoezi la 2 la Kitabu cha
Mwanafunzi ukurasa wa 84wakiwa katika makundi na waandike majibu yao.
Majibu yanayotarajiwa ya maswali
Zoezi la 2, ukurasa 85
1. Soko
2. mwanamke, mtoto (binti au mtoto wa kiume)
3. magari matatu
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaomba wanafunzi kadhaa kueleza darasani mambo waliyopata
sokoni.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika sentensi saba kuhusu yale wanayokumbuka zaidi kuhusu
masoko waliyozuru, wabadilishane vitabu na kusoma sentensi za wenzao.
Somo la 4: Kutamka na kusoma kwa sauti
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kufupisha matini alizosoma kwa kubaini
hoja muhimu.
Habari za kimsingi
Somo hili litawawezesha wanafunzi kujibu maswali ya ufahamu kutoka kwa matini
walizosoma. Waongoze wanafunzi katika kusoma na kufahamu hoja muhimu katika
hadithi.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 85-86
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi wataje maneno yoyote yenye urari wa
sauti.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wasome maneno yaliyo katika Kitabu cha Mwanafunzi
ukurasa 85 kwa sauti darasani.
2. Waagize wanafunzi kuchunguza na kulinganisha maneno yale. Wayajadili
wakiwa katika makundi. Hili litaendeleza stadi za maisha, hasa stadi na kujua
na kuishi na wengine kupitia mawasiliano fanikifu.
3. Waambie wanafunzi wasome hadithi ya Fatuma aumia goti lake katika
makundi.
105
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
4. Wanafunzi wajibu maswali yanayofuatia wakiwa katika jozi.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi wabadilishane vitabu na kulinganisha
majibu.
Tathmini
Waambie wanafunzi waadike maneno matano yenye ng isipokuwa yale yaliyotolewa
katika somo hili.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 85
Mwalimu atathmini usomaji wa wanafunzi
Zoezi la 2, ukurasa 86
1. Shonea
2. kisu
3. goti
4. anguka
5. jua
Somo la 5: Kusema, kusoma na kuandika sauti
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kubaini na kusema sauti zenye heru
nyingi ili kuunda silabi na maneno.
Habari za kimsingi
Wanafunzi wataonyeshwa kusoma maneno yenye sauti zinazotamkwa pamoja.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 86-87
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kutaja maneno wajuayo yenye sauti nyingi
zinazotamkwa pamoja. Waambie watoe mifano ya maneno kama haya.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma maneno katika zoezi la 1 katika Kitabu
cha Mwanafunzi ukurasa 86 wakiwa wawili wawili na kutambua sauti
zinazotamkwa pamoja.
2. Kila jozi ilieleze darasa sauti ambazo wamebaini. Hili litahakikisha kila
mwanafunzi anawajibikia zoezi na kulishiriki.
106
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
3. Waambie wanafunzi wasome maneno haya kwa sauti: mbwa, kubwa, bebwa,
bwana, bweni.
4. Waambie wanafunzi kuelezana darasani, sauti zinazotamkwa pamoja katika
maneno yale.
5. Waagize wanafunzi kusoma wakiwa wawili wawili sentensi ambazo zimo
katika Kitabu cha Wanafunzi ukurasa 86na wapigie mstari sauti zinazotamkwa
pamoja.
6. Waambie wanafunzi waandike maneno yaliyo katika zoezi la 2 ipasavyo na
walinganishe na ya wenzao kuona iwapo wameandika maneno yale yale.
7. Waagize wanafunzi kuchora picha ya mbwa na ya bweni.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi kusoma maneno yaliyo katika zoezi 2
kwa sauti.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika sentensi tatu wakitumia maneno yafuatayo:
Mbwa
Bweni
Bebwa
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 86
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi
Zoezi la 2, ukurasa 87
1. mbwa
2. bebwa
3. bwana
4. kubwa
5. bweni
2. Mwalimu atathmini michoro ya wanafunzi
Wiki ya 15
Mpangilio wa vipindi
Somo la 1: Kusoma na kujibu
Matokeao maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutambua hoja mahsusi katika kujibu
maswali yaliyo katika matini zilizosomwa.
107
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Wanafunzi wanatarajiwa kusoma kifungu na wadondoe majibu kutokana na kifungu
hicho.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 88-89
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wamesoma hadithi na hadithi
ambazo wanajua. Muombe mwanafunzi mmoja kusimulia wenzake darasani hadithi
na kuwauliza maswali kutokana na hadithi yake. Wanafunzi wajibu maswali yale.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wasome hadithi Kunguru mwenye kiu katika Kitabu cha
Mwanafunzi ukurasa 88.
2. Wanafunzi wajibu maswali yanayofuatia.
3. Waambie wanafunzi walinganishe majibu yao wakiwa katika jozi. Zoezi
hili litachangia stadi za maisha za wanafunzi za kujua na kuishi na wengine
kupitia mawasiliano fanikifu.
Hitimisho
Hitimisha kwa somo kwa kumwambia mwanafunzi mmoja asimulie tena kisa cha
Kunguru mwenye Kiu.
Tathmini
Waambie wanafunzi asimulie tena kisa cha Kunguru mwenye Kiu na kuulizana
maswali.
Majibu, ukurasa 89
1. Alikuwa akitafuta maji.
2. Aliona jagi la maji.
3. Mdomo wa jagi ulikuwa mwembamba.
4. Jagi lilikuwa zito.
5. Alitumbukiza jiwe moja moja kwenye jagi.
Somo la 2: Kusoma kimya kimya
Matokeao maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kupata maana ya maneno mapya katika
muktadha.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watasoma hadithi, wabaini hoja kuu katika hadithi na waandike majina
mageni watayopata kwenye hadithi.
108
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 89
Utangulizi
Tanguliza somo kwa wanafunzi kueleza baadhi ya maswali waliyopata kutokana na
hadithi ya Kunguru mwenye kiu waliyoisimulia upya.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wasome kimya kimya hadithi ya Kunguru mwenye kiu.
2. Wanafunzi waelezane hadithi inahusu nini.
3. Teua wanafunzi kadhaa wawaeleze wenzao darasani hadithi inahusu nini.
Zoezi hili litaendeleza mawasiliano na ushirikiano wanapoeleza wenzao
mambo yaliyomo katika hadithi.
4. Waambie wanafunzi waandike maneno mapya ambayo wamekumbana nayo
kwenye hadithi na wayawasilishe kwa wenzao.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi kutaja baadhi ya maneno mapya
ambayo wameandika.
Tathmini
Waambie wanafunzi wasome aya katika gazeti, kitabu cha hadithi au jarida na
waandike maneno mapya ambayo watapata mle.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 88
Mwalimu atathmini matamshi na majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 89
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 3: Kujenga msamiati
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kupata maana ya maneno mageni
katika muktadha fulani.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watakuwa wakisoma msamiati kutoka kwenye hadithi wanaposoma. Wataeleza
maana ya maneno yale kama yaliyotumiwa katika hadithi zile.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
109
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 90
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi wataje maneno mageni ambayo wamepata
kutokana na usomaji wao binafsi. Waambie wanafunzi wabadilishane daftari zao na
kusoma maneno mageni ambao wanafunzi wenzao wamepata.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kutafuta maana za maneno mapya kama yalivyotumiwa
katika hadithi.
2. Wahimize wanafunzi kusaidiana kutafuta maana za maneno wanapokumbana
na changamoto katika kupata maana za maneno mapya. Hili litachangia stadi
za mawasiliano na ushirikiano.
3. Wasaidie wanafunzi kupata maana za maneno mapya ambayo wamepata
changamoto katika kutafuta maana au wakaifasiri visivyo.
4. Waagize wanafunzi kutunga sentensi wakitumia maneno hayo mapya.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuangalia vitabu vya wanafunzi. Ikiwa wanafunzi wako ni
wengi kusanya vitabu ili kuona iwapo wanafunzi wanafanya inavyostahili. Wakosoe
na kuwashauri panapostahili.
Tathmini
Waagize wanafunzi kutunga sentensi wakitumia maneno waliyoandika katika
tathmini ya somo la 2.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 90
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 90
Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi.
Somo la 4: Kusimulia hadithi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kujieleza ipasavyo kwa kutumia
msamiati aliojifunza ili kuwasiliana.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watasimulia hadithi ambayo wanaijua na waihusishe na maisha halisi.
Wanafunzi wanapaswa kuhusisha hadithi waliyosoma na kile ambacho hadithi
inawakumbusha. Hakikisha kuwa kila mwanafunzi anashiriki.
110
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 90
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi kubadilishana vitabu na kusoma hadithi
ambazo wenzao wametunga kutokana na maneno mapya waliyosoma awali. Waongoze
wanafunzi katika kutumia maneno hayo ikiwezekana, katika hili somo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi waelezane hadithi ambazo wamesoma katika makundi.
Washauri wanafunzi kuhakikisha hadithi zao ni fupi ili kila mwanafunzi
apate nafasi ya kusimulia hadithi yake. Hili litaendeleza uwezo wa uwazaji
makinifu na usuluhishaji matatizo wa wanafunzi wanapopanga mawasilisho
yao.
2. Waambie wanafunzi waeleze walichokumbushwa na hadithi ambazo walisoma
kama mfano uliotolewa katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 89. Kusimuliana
mawazo hayo katika zoezi hili kunaendeleza thamani ya maisha ya mapenzi
kwa wanafunzi wanaposimulia kuhusu maraki zao au wanafamilia ambao
hadithi fulani huwakumbusha. Stadi za maisha za wanafunzi kama vile ile ya
kujua na kuishi wengine itaendelezwa kupitia mawasiliano fanikifu wakati
wanafunzi wanaposhiriki katika mijadala.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia baadhi ya wanafunzi kuwasilisha anwani za
hadithi ambazo wamesoma, maelezo mafupi kuhusu hadithi na kile ambacho hadithi
iliwakumbusha.
Tathmini
Waambie wanafunzi wawasilishe hisia zao kwa wazazi au walezi wao.
Somo la 5: Kuandika aya
Matokeo maaluma ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuandika vizuri na kwa aina mbalimbali
za sentensi kimuundo, urefu na ruwaza.
Habari za kimsingi
Mwanafunzi ataonyeshwa namna ya kuandika sentensi na kupanga upya sentensi
kuunda aya.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 90-91
111
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaomba wanafunzi kusimulia namna walivyowasilisha
hisia zao kwa wazazi au walezi wao. Wateue wanafunzi wachache watakaojitolea
kusimulia wenzao darasani.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma sentensi katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
90-91.
2. Waulize iwapo wanaona tatizo lolote kwenye sentensi zile.
3. Teua wanafunzi wachache watakaojitolea kutoa maoni yao.
4. Waagize wanafunzi kuziandika upya sentensi zile kwa njia sahihi. Hili
litaendeleza mawasiliano na ushirikiano wanafunzi wanapopanga na
kuandika mawazo yao wakiwa katika jozi au makundi.
5. Waambie wanafunzi wabadilishane vitabu na kusoma sentensi zilizosahihishwa
za wenzao na kuona iwapo zinalingana.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwauliza wanafunzi kusoma sentensi zao uangalie ikiwa
wameziandika ipasavyo.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 90-91
1. Kamau alipanda juu ya mti wa muembe
2. Alianguka kutoka mtini na akaumia mguu wake.
3. Daktari aliosha kidonda chake na akakifunga kwa bandeji.
4. Babake alimwambie asipande mti tena.
Zoezi la 2, ukurasa 91
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika sentensi sita kuhusu michezo ambayo hucheza nyumbani
baada ya masomo shuleni.
Wiki ya 16
Mpangilio wa vipindi
Somo la 1: Hadithi ya picha
Matokeo maaluma ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia ujuzi atakaopata wa mchakato
wa uandishi wa kiubunifu kuandika matini zake.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatumia hadithi za picha kubuni hadithi katika uandishi bunifu. Wanatarajiwa
112
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
kuandika miundo sahihi ya sentensi na hata kutumia maneno mapya ambayo
wamejifunza inapostahili. Chunguza kazi za wanafunzi na kuhakikisha kuwa hati yao
ni nadhifu na utungaji wao wa sentensi ni mzuri.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 91-92
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi ikiwa wao huandika maandishi ya ubunifu
wakiwa peke yao. Waulize kama wana shajara ambapo huandika matukio ya kila siku.
Muombe mwanafunzi ambaye ana shajara akueleze anayoyaandika mle.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kuchunguza picha zilizo katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 91-92 wakiwa wawili wawili na wajadili wanayoyaona kwenye
picha. Zoezi hili litaendeleza ubunifu na uwazaji makinifu wa wanafunzi
wanapoangalia, kuwaza na kuandika kutegemea vidokezo vya picha.
2. Waagize wanafunzi kuandika aya wakizingatia wanayoyaona yakitendeka
katika picha.
3. Waambie wanafunzi wabadilishane vitabu na kusoma aya zilizoandikwa na
wenzao.
4. Waambie wanafunzi waseme ni aya ya nani inayodhihirisha ubunifu wa hali
ya juu. Muombe huyo mwanafunzi kusoma aya yake darasani.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi wapige kura kubaini mwanafunzi
mwenye aya bora zaidi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika kuhusu maisha yao tangu kuzaliwa hadi wakati walipojiunga
ma shule kutegemea yale ambayo wameelezwa na wazazi au jamaa zao.
Somo la 2: Siku yangu ya kwanza shuleni
Matokeo maalum ya ujifunziaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuonyesha kauli za kisanii kupitia maandishi.
Habari za kimsingi
Wanafunzi wataandika kuhusu siku yao ya kwanza shuleni kutegemea kumbukumbu
zao. Wahimize kuwa wabunifu kadiri inavyowezekana.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 92
113
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi watatu wasome insha zao kutokana na
zoezi la somo la 1. Waambie wanafunzi wabadilishane vitabu vyao wakati wao wa
mapumziko na wasome aya za wenzao. Fuatilia kuhakikisha wamefanya hivyo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi wajadili kuhusu siku yao ya kwanza shuleni wakiwa katika
makundi. Hili litachangia stadi za wanafunzi za mawasiliano na ushirikiano.
2. Waagize wanafunzi waandike kuhusu siku yao ya kwanza shuleni.
3. Waambie wazingatie hoja zifuatazo na kuongezea nyingine:
Nani aliwapeleka shuleni?
Walihisi vipi?
Walikwenda shule gani?
Rangi ya sare zao ilikuwa ipi?
Mkoba wao wa vitabu wa kwanza ulikuwaje?
Jina la mwalimu wao lilikuwa lipi?
Raki yao wa kwanza shuleni alikuwa nani?
Uraki huo ulianzaje?
Walisoma nini?
4. Waambie wanafunzi waketi katika jozi na kubadilishana vitabu na kisha kazi
za wenzao.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi waeleze nani alikuwa ameandika hadithi
ya kuvutia zaidi kuhusu siku yake ya kwanza shuleni na kwa nini.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike insha kuhusu mwalimu wao wa kwanza.
Somo la 3: Kazi ninayoitamani
Matokeo maalum ya ujifunziaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia mabadiliko ya toni,
matamshi mwafaka na mkazo kujieleza kwa ukakamavu.
Habari za kimsingi
Wanafunzi waeleze kazi ambayo wangetaka kuifanya watakapokuwa watu wazima.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 92
114
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi watatu wasome kazi zao walizoandika
katika somo la 2 darasani. Wahimize wanafunzi kusoma hadithi za wenzao wakati wa
mapumziko na kuelezana kuhusu siku yao ya kwanza shuleni.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wajadili kazi ambayo wangetaka kufanya watakapokuwa
watu wazima na kwa nini, wakiwa katika makundi.
2. Waulize wanafunzi kazi ambazo zinawavutia na kwa nini.
3. Mpe kila mwanafunzi nafasi ya kusema kazi ambayo angetaka kufanya. Hili
hujenga kujistahi kwa mwanafunzi.
4. Waagize wanafunzi waandike kuhusu kazi ambayo wangetaka kufanya
watakapokuwa wazima.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwahamasisha wanafunzi kusoma kwa bidii shuleni ili wafanikiwe
kupata hizo kazi wanazozitamani.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike mambo matano ambayo watafanya ili kufanikiwa kupata
kazi ambayo wanatamani kufanya wakiwa wakubwa.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 92
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 4: Kuandika kwa kupanga upya maneno
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kutumia viunganishi mwafaka ili
kufuatanisha sentensi.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watapewa sentensi ambazo zitakuwa zimechanganyika ili waweze kuzipanga
upya.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 93
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwaambia wanafunzi watatu wasome sentensi walizoandika
katika zoezi la somo la 3 darasani.
115
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Shughuli za ujifunzaji
1. Onyesha vipande vya sentensi zifuatazo na kuwaambia wanafunzi wazipange
katika mfuatano ufaao.
i. Mimi huamka mapema sana kwenda shuleni.
ii. Kwa sababu sitaki kuadhibiwa kwa kuchelewa.
iii. Mimi huka shuleni kwa wakati ufaao.
iv. Kwa hivyo ninalala mapema kila siku.
2. Waambie wanafunzi watunge sentensi zao na kuwapa wenzao wazipange
ipasavyo. Hili litaendeleza stadi za wanafunzi za mawasiliano na ushirikiano.
3. Waagize wanafunzi kuandika upya sentensi zilizo katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 93 ipasavyo.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi walinganishe sentensi zao walizoandika
upya ili kuona kama zinalingana.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike upya sentensi zifuatazo:
1. Niliichukua na kumpelekea mamangu.
2. Alikuwa amemsikia Mama Joy akisema amepoteza noti ya shilingi mia tano.
3. Nilipoona noti ya shilingi mia tano.
4. Mama Joy alikuja na kunishukuru.
5. Mama alimpelekea Mama Joy.
6. Nilikuwa nikitoka shuleni siku moja.
Mpangilio ufaao ni
1. Nilikuwa nikitoka shuleni siku moja.
2. Nilipoona noti ya shilingi mia tano.
3. Niliichukua na kumpelekea mamangu.
4. Mama alimpelekea Mama Joy.
5. Alikuwa amemsikia Mama Joy akisema amepoteza noti ya shilingi mia tano.
6. Mama Joy alikuja na kunishukuru.
Majibu, Zoezi la ukurasa 93
Mwalimu atathmini namna wanafunzi wanafunzi wamepanga sentensi zao.
Somo la 5: Shajara yangu
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze kuamua kuandika kivyake wakati wa
shughuli zake binafsi.
116
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Wanafunzi wataonyeshwa namna ya kuandika matukio na kuhifadhi shajara. Waeleze
wanafunzi kuhusu mambo na mazoea ambayo yanahitajika katika kuandika na
kuhifadhi shajara.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 93
Utangulizi
Tanguliza somo kwa kuwauliza wanafunzi iwapo wanajua shajara, wanachoandika
kwenye shajara zao na mara ngapi wao huandika.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wajadili yaliyomo katika shajara wakiwa katika jozi.
Hili litaendeleza ubunifu na uwezo wa kuwaza kwa umakinifu wanafunzi
wanapojadili yale yanayopaswa kuwemo katika shajara.
2. Mwambie mwanafunzi mmoja mmoja kutoka jozi mbalimbali kueleza
waliyojadili katika jozi zao.
3. Waagize wanafunzi waandike shajara ya matukio ya siku hiyo. Wahimize
wanafunzi kutumia ubunifu na msamiati ambao wamesoma kukia sasa.
Hitimisho
Hitimisha somo kwa kuwaambia wanafunzi wawe na shajara.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike hadithi fupi kuhusu matukio ambayo yametukia
shuleni katika wiki hiyo.
117
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Sehemu
6
Treni mpya
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Mada 1.0
Kusikiliza
Mada 2.0
Kuzungumza
Mada 3.0
Kusoma
Mada 4.0
Kuandika
Somo la 1.6
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kutambua
maneno
yaliyo na sauti
zinazofanana.
b) Kujenga
msamiati kwa
kusikiliza
hadithi.
ch)Kukumbuka
matukio makuu
katika hadithi.
d) Kusikiliza na
kuwasiliana
ipasavyo katika
hali mbalimbali.
e) Kusikiliza
matini ya
kitaarifa na
kuteua ujumbe
mkuu.
Somo la 2.6
Kusoma wakiwa
wawili wawili
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kuzungumza
kwa ujasiri
kuhusu wahusika
na matukio
katika hadithi au
matini.
b) Kuhusisha
wahusika na
matukio katika
hadithi kwa yale
yanayofanyika
katika
ulimwengu
halisi.
ch)Kujieleza
ifaavyo kwa
kutumia
msamiati
mwafaka.
d) Kuuliza maswali
kuthibitisha na
kupanua uelewa
wa nyenzo
iliyosomwa.
e) Kutoa maoni
kuhusu usomaji
wa wenzake.
Somo la 3.6
Kusoma kwa ghibu
(kimoyomoyo) na
kusoma kimakundi
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kusoma matini
kwa ufasaha,
usahihi na
kuielewa.
b) Kuimarisha
ujasiri kutokana
na kusoma na
wenzake katika
makundi.
ch)Kujenga ari ya
kusoma kwa
jumla ndani na
nje ya darasa.
d) Kukisia maana
za maneno
asiyoyajua katika
hadithi.
e) Kusoma matini
na vifungu
kimoyomoyo.
f) Kujibu maswali
ya ufahamu
kutokana na
matini aliyosoma.
Somo la 4.6
Uundaji wa
maneno na
sentensi
Kukia mwisho wa
somo, mwanafunzi
aweze:
a) Kutumia
vifungu na
kauli wazozijua
katika kutunga
sentensi.
b) Kutumia
upatanisho
mzuri wa
kisaru kati
ya nomino na
kitenzi kutunga
sentensi
ch)Kujenga ari ya
kuandika.
d) Kutumia ujuzi
wa uandishi
wa kibunifu
kuandika matini
yao wenyewe.
e) Kutumia
viunganishi
mwafaka
katika kutunga
sentensi.
118
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
a) Wanakuza ushirikiano na mawasiliano katika kushirikiana katika vikundi. Aidha,
wanakuza uwezo wao wa kujieleza ama kwa kuandika au kuzungumza.
b) Uwezo wa kukiri na kutatua matatizo unakuzwa kutokana na kubuni na kujieleza
na vilevile kupanga mawazo vizuri kwa uwasilishaji.
Uhusiano na masuala mtambuko
a) Ujuzi wa kujua jinsi ya kuishi na watu wengine katika jamii unakuzwa kutokana
na kushirikiana vyema na wenzao katika makundi.
b) Stadi za maisha zinakuzwa katika kuwa raia mwema wa kuwasiliana na watu
vyema kutokana na mawasiliano bora.
ch) Uraia unahimizwa katika kufanya kazi kwa ushirikiano na wenzake katika
makundi.
Uhusiano na desturi na maadili ya jamii
a) Heshima itaendelezwa wakifanya kazi pamoja na wanafunzi wenzao.
b) Umoja utahimizwa kutokana na ushirikiano na wenzao au katika vikundi.
ch) Wanajifunza kuwajibika wakitekeleza majukumu wanayopewa.
Uhusiano na masomo mengine
a) Mathematical Activities wanapojigawa katika vikundi.
b) Masomo yote.
Shughuli za kijamii zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
a) Wanafunzi wanasimulia upya hadithi kutoka kwa jamii zao.
b) Wanafunzi wanashiriki katika mashindano ya kusoma.
ch) Wanafunzi wanasoma hadithi kama njia ya kujiingiza katika uandishi wa kibunifu.
Shughuli nyingine zisizo rasmi zinazopendekezwa kuchangia ujifunzaji
a) Wanafunzi wanazisimulia hadithi hizo upya kwa wenzao.
b) Wanafunzi wanawasomea wanawasomea wenzao visa katika muda wao wa
mapumziko.
ch) Wanafunzi wanaandika hadithi na kuwasomea wenzao.
Nyenzo zinazopendekezwa za ujifunzaji
Mjuzi mwalikwa, matini mbalimbali, magazeti, majarida, vitabu, penseli, vipande
vilivyokatwa vya magazeti, maleba ya uigizaji, vifaa vya uigizaji
Tathmini inayopendekezwa
1. Wanafunzi wanasimulia hadithi, maswali na majibu, maigizo
2. Kujaza mapengo
3. Kuwapa wanafunzi mada ya kuandika kama msingi wa kuandika hadithi fupi na
matini.
119
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalum
Usaidizi kwa wanafunzi wenye
uwezo mbalimbali
Usaidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji
maalum
Himiza wanafunzi wenye uelewa wa
polepole kushiriki katika mazungumzo,
maigizo na kusimulia hadithi.
Wape wanafunzi wenye uelewa wa
haraka kazi la ziada ili kuepuka
kuwachosha na kuzubaa darasani.
Wape wanafunzi wenye uelewa
wa polepole na haraka nafasi za
kutosha katika shughuli za darasani.
Una jukumu la kuhakikisha kwamba
wana kufurahia kukaa pamoja licha
ya tofauti zao.
Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona, wape breli, picha za kugusa na
wale wasioweza kuona vizuri wape
matini makubwa.
Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa
kusikia vizuri tumia lugha ishara au
mlete mtaalamu wa lugha ya ishara
kufasiri.
Wanafunzi ambao hawawezi kuona
mbali wakae mbele darasani na wenye
uwezo wa kuona mbali wakae nyuma.
Wape wanafunzi wenye ulemavu
majukumu wanayoweza kutekeleza.
Wape usaidizi wa kutosha na
kuhakikisha kwamba wanafunzi
wengine wanafanya hivyo, kwa mfano,
kuwasaidia katika kusukuma kitimaguru
kwa mwanafunzi mlemavu.
Wiki ya 17
Mpangilio wa masomo
Somo la 1: Kuzungumza kuhusu kwenda safarini
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kuhusisha wahusika na matukio
katika hadithi na ulimwengu halisi.
Habari za kimsingi
Wanafunzi waweze kuzungumzia matukio maishani mwao kwa ujasiri. Wanafunzi
watatarajiwa kuhusika katika mazungumzo mbalimbali kuhusu safari walizosari ili
kujiwezesha kuzungumzia mambo mengine nje ya kipindi. Utahitajika kuwachezea
sauti ya mtu anayezungumza kuhusu kitu fulani. Anaweza kuwa mwalimu mkuu
akizungumza kuhusu nidhamu shuleni, au mama akimshauri mwanawe. Iweke sauti
hiyo katika nafasi inayoweza kusikika na wanafunzi wote darasani.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 94-95
120
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuhusu maisha yao kwa jumla. Wahusishe
wanafunzi katika mazungumzo kuhusu kitu kizuri kabisa walichowahi kukipitia na hali
mbaya kabisa iliyowahi kuwafanyikia. Wape wanafunzi wengi kiasi cha haja nafasi
ya kujitokeza kuzungumza kuhusu tajiriba hizo zao maishani kwa wenzao darasani.
Wahimize wanafunzi wenye aibu na walemavu kushiriki katika mazungumzo hayo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusikiliza kwa makini sauti hiyo na kujaidiliana
anachokizungumzia mzungumzaji. Shughuli hii itawasaidia wanafunzi kukuza
ujuzi wa kidijitali kwa kuzungumzia hadithi iliyochezwa kwenye sauti.
2. Waagize wanafunzi kutazama picha katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 94
na kujadiliana kuhusu wanachokiona katika picha hizo. Shughuli hii inakuza
stadi za maisha katika kujua jinsi ya kuishi na wanafunzi wengine kutokana
na mawasiliano bora. Hivyo basi, hakikisha kwamba kila mwanafunzi
anashiriki katika kazi hii ya darasa ili kuimarisha mawasiliano, ushirikiano
na umoja.
3. Waagize wanafunzi kusoma mazungumzo kati ya Chacha na mamake wakiwa
katika makundi ya wanafunzi wawili wawili na uone ikiwa makisio ya yeyote
yalikuwa sahihi.
4. Waagize kujadiliana maswali kati Zoezi la 2 katika vikundi. Hakikisha kwamba
kila mwanafunzi yuko katika kikundi fulani na anaeleza kuhusu tajriba
zake. Hili litakuza stadi za mawasiliano na ushirikiano katika mwanafunzi
kutokana na kuhusiana na wenzake katika vikundi na kuelezeana kuhusu
tajiriba zao mbalimbali.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi sehemu ambazo wamewahi kusari,
waliyeenda naye, walichokiona na sehemu nyingine ambayo wangependa kutembelea.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuzungumza na wazazi wao kuhusu suala linalowasumbua au
jambo ambalo wangependa wazazi au walezi wao walibadili au kulishughulikia.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 94
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 95
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Somo la 2: Soma na utamke
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutambua maneno yaliyo na sauti au
heru zinazofanana.
121
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari za kimsingi
Wanafunzi watasoma sauti, kutazama picha na kueleza kinachotendeka katika picha.
Waweze kuzungumza kwa ujasiri kuhusu shughuli wanazoona zikifanyika katika
picha hizo na kuwaeleza wenzao darasani kuhusu mawazo yao.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 95-96
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi ikiwa walizungumza na wazazi au walezi
wao walivyoagizwa katika tathmini ya somo la 1. Waagize wanafunzi waliozungumza
na wazazi au walezi wao kuinua mikono na uwaulize wale ambao hawakuzungumza
na wazazi wao sababu ya kutofanya hivyo. Wale waliozungumza na wazazi wao
wawaeleze wenzao darasani kuhusu walichokizungumzia na jibu lilivyokuwa. Ikiwa
darasa lina wanafunzi wengi, teua wachache kutoa maelezo na mawazo yao na
uwaambie wale wengine kuzungumzia masuala yao katika muda wa ziada.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma sauti katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 95
na kutambua wanachokiona katika maneno hayo.
2. Waagize wanafunzi kutazama picha katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
95-96 wakiwa wawili wawili na kueleza wanachokiona. Hili litakuwa uraia
katika wanafunzi kutokana na mshikamano wa kijamii wanapojadiliana
kuhusu wanachokiona katika picha hizo.
3. Waagize wanafunzi kukamilisha zoezi katika zoezi la 3 kila mmoja peke yake
na kulinganisha majibu yao na yale ya wenzao wanaokaa kwenye dawati moja.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwateua wanafunzi wachache kuwasomea wenzao majibu ya
zoezi la 3.
Tathmini
Waagize wanafunzi kutunga sentensi tano kwa kutumia maneno katika zoezi la 1.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 95
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 95-96
Mwalimu atathmini maelezo ya wanafunzi.
Zoezi la 3, ukurasa 96
1. imba 2. mbawa 3. lia
4. fua 5. funge
122
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 3: Kuandika
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia kauli na maneno anayoyajua
kutunga sentensi sahili.
Habari za kimsingi
Wanafunzi wasome na kuandika maneno yanayoisha kwa silabi -ni. Maneno hayo
huashiria mahali. Wanafunzi watoe mifano ya maneno haya. Tumia kadi za maneno
haya kuonyesha mifano. Hakikisha kwamba kadi zinaonekana vizuri. Kwa wanafunzi
wenye matatizo ya kuona, wape breli.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 96-97
Kadi za maneno
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi kubadilishana na kusoma sentensi
zilizoandikwa katika somo la 2.
Shughuli za ujifunzaji
1. Tandaza kadi za maneno zilizo na maneno yafuatayo kwa wanafunzi:
a) Nyumbani
b) Sokoni
c) Bafuni
d) Shuleni
e) Darasani
2. Waagize wanafunzi kusoma kwa sauti maneno hayo na kuyaandika.
3. Waagize wanafunzi kusoma maneno katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa
97 wakiwa wawili wawili. Shughuli hii itakuza stadi za mawasiliano na
ushirikiano wanaposoma pamoja.
4. Wanafunzi wajadili kuhusu tofauti wanayoiona katika maneno hayo.
5. Waagize wanafunzi kuongeza -ni kwenye maneno yaliyo katika zoezi la 2
ukurasa 97.
6. Wanafunzi wayasome maneno hayo kwa sauti kwa pamoja darasani.
7. Waagize wanafunzi kutunga sentensi wakitumia maneno kufurahi, kulia,
kushinda, kugonga na kukoma.
8. Waagize wanafunzi kubadilishana vitabu na kusoma maneno waliyoyaandika
wenzao.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi wakiwa wawili wawili kuongeza -ni
kwenye maneno uliyokuwa umewaonyesha mwanzoni mwa kipindi.
123
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 96-97
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 97
1. Uwanjani 2. Garini 3. Majini
4. Dukani 5. Chupani
Zoezi la 3, ukurasa 97
1. Andika 2. Soma 3. Angalia
4. Chora 5. Toka
Somo la 4: Soma kwa sauti
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kusoma matini kwa jumla kwa
ufasaha, usahihi na kuelewa.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatathminiwa kuhusu ufasaha, usahihi na uelewa wa matini waliyosoma.
Sikiliza matamshi ya wanafunzi na kasi yao katika kusoma.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 98-99
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi kusoma sentensi walizotunga kutoka
katika somo la 3 wakiwa katika vikundi. Waagize wanafunzi kusoma sentensi hizo
kimoyomoyo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma kwa sauti maneno katika Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 98. Teua wanafunzi wachache bila utaratibu maalum kusoma kila
mojawapo ya maneno hayo. Hili litakuza kujiamini kwao kwa kuwajengea
ujasiri wa kusoma mbele ya darasa.
2. Waagize wanafunzi kusoma shairi wakiwa wawili wawili. Wahimize
wanafunzi kusaidiana kusoma kile kinachomtatiza mwenzake. Hili litakuza
stadi za mawasiliano na ushirikiano wanaposomea shairi.
3. Waambie wanafunzi waandike maneno yenye urari wakiwa wawili wawili na
kulinganisha maneno yao na ya wenzao.
4. Waagize wanafunzi kujaza maneno yanayokosekana kwa kutumia maneno
yenye urari kutoka kwenye shairi.
5. Waagize wanafunzi kuandika upya sentensi katika zoezi la 4 katika Kitabu cha
124
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Mwanafunzi, ukurasa 99 kila mmoja peke yake, kisha wabadilishane vitabu na
kusoma sentensi za wenzao.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi maana ya maneno yenye urari. Waagize
kusoma maneno yenye urari waliyoandikana kutokana na shairi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kusoma aya katika vikundi na kuandika sentensi tano kuhusu
ujumbe wa aya hiyo.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 98
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 98
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 3, ukurasa 98-99
1. kinasomeka 2. choreka
3. inaandikika 4. funguka
Somo la 5: Mchezo wa heru
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kujenga ari ya kuandika kwa starehe
na kujifurahia.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watacheza michezo kwa kutumia heru mbalimbali za alfabeti. Hili
litakuza stadi zao za utungaji wa sentensi na kujenga ari ya kuandika kwa starehe na
raha zao. Hakikisha kwamba wanafunzi wanashiriki katika shughuli hii na kutumia
heru nyingi za alfabeti kadiri ya uwezo wao kutunga sentensi.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 99
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kumwagiza kila mwanafunzi kuchukua heru moja ya abjadi/
alfabeti. Baada ya wote kuchukua heru, agiza kila mmoja kuunda neno kwa kutumia
heru aliyochagua, kisha atunge sentensi kwa kutumia neno hilo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi wakiwa wawili wawili kusoma shairi kutoka kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 99. Hili litakuza stadi za mawasiliano na
ushirikiano wanapobadilishana na kutumia vitu vyao pamoja.
125
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
2. Waagize wanafunzi kucheza mchezo wa maneno katika vikundi. Wahimize
wanafunzi wenye uelewa mwepesi kuwapa wenzao wasio na uelewa huo
mwepesi fursa ya kutunga sentensi zao. Waruhusu wanafunzi wenye ulemavu
wa kutosikia na kutoona vizuri kushiriki katika shughuli hizi. Zoezi hili
litakuwa stadi za maisha hasa stadi ya kujua jinsi ya kuishi na wengine
katika jamii kupitia kwa mawasiliano bora. Kupitia kwa zoezi hili, wanafunzi
watajifunza maadili ya heshima wakipeana nafasi sawa ya kushiriki katika
shughuli hizi.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kueleza darasani baadhi ya michezo ya
maneno waliyoicheza.
Tathmini
Waagize wanafunzi kubuni shairi la beti tatu kwa kutumia heru B, M, S za abjadi/
alfabeti.
Tanbihi
Tathmini tungo za wanafunzi. Soma baadhi ya mashairi yao darasani na kuwapongeza
waliojitahidi zaidi katika utunzi.
Wiki ya 18
Mpangilio wa masomo
Somo la 1: Kusoma pamoja
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kuuliza maswali ya kuthibitisha na
kupanua uelewa wake wa nyenzo aliyosoma.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watasoma kifungu cha ufahamu wakiwa wawili wawili na kutunga
maswali kutokana na kifungu hicho. Kisha wawaulize maraki zao maswali hayo.
Hili litapima uwezo wao wa kusoma kwa makini na kuelewa.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 100-101
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kueleza kuhusu hadithi walizosoma.
Waambie watoe maelezo mafupi kuhusu ujumbe wa hadithi, walichofurahia na
walichojifunza kutokana na hadithi hiyo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma kwa pamoja sentensi katika zoezi la 1 katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 100.
126
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
2. Waagize wanafunzi kutaja rangi za vitabu na penseli zao.
3. Waagize wanafunzi kusoma hadithi wakiwa wawili wawili. Hili litakuza stadi za
mawasiliano na ushirikiano wanafunzi wanaposhirikiana kufanikisha usomaji
wa pamoja na wenzao.
4. Waagize wanafunzi kila mmoja kutunga maswali kutokana na hadithi waliyoisoma
hivyo punde.
5. Waagize wanafunzi kubadilishana vitabu na kujibu maswali ya wenzao.
Hitimisho
Wahusishe wanafunzi katika mjadala mfupi kuhusu ujume wa hadithi hiyo waliyosoma.
Wape wanafunzi kadhaa nafasi ya kueleza kuhusu ujumbe wa hadithi hiyo mbele ya
wenzao darasani.
Tathmini
Waagize wanafunzi kusoma hadithi inayowaaki kiumri kutoka katika jarida au gazeti
na kutunga maswali kutokana na hadithi hiyo, kisha wajibu maswali hayo.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 100
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 100
Mwalimu atathmini matamshi na majibu ya wanafunzi.
Somo la 2: Kusoma na Raki
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutoa maoni kuhusu usomaji wa
mwenzake.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watasoma hadithi wakiwa wawili wawili na kutoa maoni kuhusu usomaji
wa wenzao. Wanafunzi watahitajika kuwasikiliza wenzao wakisoma na kutoa maoni
kuhusu utamkaji wao wa maneno, usahihi na kasi ya kusoma. Wahimize wanafunzi
kuwa makini na jasiri katika kutoa maoni yao kuhusu usomaji wa wenzao bila
mapendeleo na uchoyo. Hili litawafunza kuwawajibikia wenzao.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 101
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuzizungumzia hadithi walizosoma na
zilikotoka. Waambie wanafunzi wazungumze kuhusu hadithi walizosoma na maswali
waliyokutana nayo wakati wa mapumziko, wawasomee wenzao maswali waliyoyapata
127
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
pamoja na majibu waliyopata kwa maswali hayo. Hili litakuza kujiamini, ujasiri na
uwezo wa kuingiliana vizuri na ulimwengu wa nje.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma kwa sauti hadithi kutoka Kitabu cha Mwanafunzi,
ukurasa 101 wakiwa wawili wawili.
2. Kila mmoja wa wawili hao asome hadithi hiyo. Hili litakuza kujiamini kwao
na kujenga ujasiri wa wanafunzi hawa katika kusoma.
3. Waagize wanafunzi kibinafsi kuandika majibu kwa maswali kutoka kwenye
hadithi walioyoisoma.
4. Waagize wanafunzi kulinganisha majibu yao na kujaribu kuthibitisha majibu
sahihi kwa kusoma hadithi tena, pamoja na kupata majibu kutoka katika ufahamu.
Hili litakuza uwezo wa kukiri kwa kina na vilevile stadi za mawasiliano na
ushirikiano wanaposhirikiana kupata majibu kwa maswali hayo.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi ikiwa wamewahi kufanya sherehe au
ikiwa wamewahi kuhudhuria sherehe, kilichofanyika na ni nani mwingine aliyekuja.
Majibu ya maswali, ukurasa 101
1. Ilikuwa sherehe ya siku ya kuzaliwa ya Alina
2. Minane (8)
3. zawadi
4. Mwalimu wa darasa
5. furahi
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike aya moja kuhusu sherehe waliyohudhuria.
Somo la 3: Kujenga msamiati
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kukisia maana za maneno asiyoyajua.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatarajiwa kupata maana za maneno mapya kulingana na yalivyotumiwa
katika kifungu. Wahimize wanafunzi kutoa maoni yao na kuakiana kuhusu maana
mahususi kwa neno husika. Wasaidie wanafunzi kupata maana za maneno hayo pale
wanapotatizika.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102
128
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi kusoma upya hadithi katika somo la 2 na
kuandika maneno yoyote mapya wanayoyapata.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma maneno katika zoezi la 1 katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 102 na kulinganisha na maneno ambayo wameyaandika.
2. Waambie wanafunzi wabadilishane vitabu vyao na kulinganisha maneno
waliyo nayo na yale ya maraki zao. Maingiliano haya yatakuza uraia na
mshikamano wa kijamii.
3. Waagize wanafunzi kutunga sentensi wakitumia maneno katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 102.
4. Waagize wanafunzi kubadilishana na kusoma sentensi za wenzao. Hili litakuza
umoja wa wanafunzi wanapoingiliana katika kusoma sentensi za wenzao.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwahimiza wanafunzi kufanya mazoea ya kusoma na
kuimarisha msamiati. Wahimize kuweka kamusi yao na kuandika maneno mapya na
kutafuta maana za maneno kwa kusaidiwa na wazazi, walezi, walimu au wenzao.
Tathmini
Waagize wanafunzi kusoma aya fupi ya kitabu cha hadithi, uandike maneno mapya na
kutafuta maana za maneno hayo yaliyotumiwa katika hadithi.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 102
1. Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
2. Mwalimu atathmini sentensi ambazo wanafunzi watatunga.
Somo la 4: Kusoma peke yako
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
i. Kusoma matini na vifungu kimoyomoyo.
ii. Kujibu maswali ya ufahamu kutokana na matini aliyosoma.
Habari za kimsingi
Wanafunzi waweze kusoma vifungu kimoyomoyo na kujibu maswali ya ufahamu.
Hili litawasaidia katika kujisomea kibinafsi wakielewa hivyo, kuwahimiza kufanya
mazoea ya kusoma kwa kuwa watakuwa na uwezo wa kupokea na kufasiri ujumbe
katika vifungu hivyo na matini hizo.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102-103
129
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kueleza kwa kifupi ujumbe wa
hadithi waliyosoma mwisho. Wape wanafunzi wachache nafasi ya kueleza kuhusu
walichokisoma mwisho.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waelekeze wanafunzi kusoma kimoyomoyo kifungu Treni mpya katika Kitabu
cha Mwanafunzi ukurasa 102.
2. Waagize wanafunzi kujibu maswali kutoka kwenye kifungu.
3. Wanafunzi walinganishe majibu wakiwa wawili wawili na kurekebishana
inapohitajika kwa kuthibitisha majibu kutoka katika kifungu pamoja. Hili
litakuza maadili ya heshima katika wanafunzi kwa kuwa watarekebishana
kwa njia ya unyenyekevu na bila kuaibishana kwa kupata majibu yasiyo sahihi.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuhusu njia za usari wanazotumia
kusari na hisia zao kuzihusu.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika aya fupi kuhusu kuhusu safari waliyosari.
Majibu, ukurasa 102-103
1. Madaraka Express
2. Huenda Mombasa na kurudi Nairobi
3. Kapteni Judy
4. Bwana Tito
Somo la 5: Kujenga msamiati
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kukisia maana za maneno wasiyoyajua.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatarajiwa kupata maana za maneno mapya kulingana na yalivyotumiwa
katika kifungu. Wahimize wanafunzi kutoa maoni yao na kuakiana kuhusu maana ya
mahususi kwa neno husika. Wasaidie wanafunzi katika kupata maana za maneno hayo
pale wanapotatizika.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu, gazeti
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 103-104
130
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuhusu idadi ya maneno waliyo nayo
katika kamusi zao za kibinafsi. Kila mwanafunzi aseme idadi ya maneno aliyo nayo
katika kamusi yake ya kibinafsi na umpongeze aliye na maneno mengi.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma upya hadithi katika somo la 4 wakiwa katika
vikundi na kujibu maswali katika kipindi hiki kibinafsi.
2. Waambie wanafunzi walinganishe na kujadili majibu yao. Shughuli hii itakuza
stadi za mawasiliano na ushirikiano.
3. Waambie wanafunzi kutumia maneno yaliyopeanwa kutunga sentensi zao za
kibinafsi.
4. Wanafunzi wabadilishane madaftari yao na kusoma kazi za wenzao. Hili
litakuza stadi za kutunga sentensi walizojifunza awali.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwahimiza wanafunzi kusoma kwa mapana ili kujenga
msamiati wao, lugha na ubunifu.
Tathmini
Waagize wanafunzi kutunga sentensi sita kwa kutumia maneno kutoka katika kamusi
zao za kibinafsi.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 103
1. treni
2. abiria
3. kandawala
4. kusari
5. kabini
6. viti
Wiki ya 19
Mpangilio wa masomo
Somo la 1: Kuzungumza kuhusu jinsi tunavyosari
Habari za kimsingi
Wanafunzi watazungumza kuhusu njia mbalimbali za usari. Wanafunzi wazungumzie njia
mbalimbali, na anayeendesha au kusimamia njia hiyo ya usari. Wanafunzi wabadilishane
mawazo kuhusu njia mbalimbali ambazo wamewahi kuzitumia kusari.
131
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu, penseli za rangi
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 104-105
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kutaja njia mbalimbali za usari
wanazozijua.
Shughuli za ujifunzaji
1. Wahusishe wanafunzi katika mjadala kuhusu njia za usari ambazo wamewahi
kutumia na walivyoziona, walikoenda na waliyeenda naye.
2. Wanafunzi wataje mahali ambako wangependa kusari na njia za usari ambazo
wangependa kutumia kwenda huko. Hili, litakuza stadi za mawasiliano na
ushirikiano wakizungumza kuhusu njia za usari. Aidha, litakuza uraia
na mshikamano wa kijamii kwa kuwa wanafunzi wote watashiriki katika
mjadala.
3. Waagize wanafunzi kuchora njia mbalimbali za usari na kuzipaka rangi.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwaeleza wanafunzi kuzingatia kanuni za usalama barabarani.
Tathmini
Waagize wanafunzi kukusanya picha mbalimbali kuhusu njia za usari na kuzibandika
katika kitabu cha picha.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 104
Mwalimu atathmini michoro ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 104-105
Mwalimu atathmini kazi za wanafunzi.
Somo la 2: Kuunda maneno na kutunga sentensi
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kuunganisha maneno kuunda sentensi
rahisi.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatunga maneno na sentensi rahisi. Angalia tahajia na maendelezo ya
maneno na utungaji wa sentensi ili kuhakikisha kwamba wanafunzi walielewa mada
ya kipindi hiki. Warekebishe wanafunzi inapohitajika.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, kadi, vijikaratasi vya sentensi
132
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 105-106
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza kutaja neno lolote moja wanalojua.
Shughuli za ujifunzaji
1. Onyesha maneno yafuatayo kwenye kadi za maneno na uwaulize wanafunzi
kuyasoma kwa sauti
a) Nyumba
b) Mvua
ch) Msitu
d) Mto
e) Embe
2. Waagize wanafunzi kutunga sentensi wakitumia maneno hayo. Chukua wanafunzi
watakaojitolea katika shughuli hii.
3. Waonyeshe wanafunzi sentensi zifuatazo
a) Tuna nyumba sa.
b) Kuna mvua nyingi.
ch) Kuna msitu mkubwa karibu na nyumbani.
d) Nilikula embe jana.
4. Waagize wanafunzi kutumia maneno yafuatayo kutunga sentensi.
Msitu, nyumbani, mimi, kikombe, kijiko
5. Waagize wanafunzi kuandika upya maneno katika zoezi la 1 ifaavyo katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 105.
6. Wanafunzi walinganishe maneno yao na kuthibitisha ikiwa yako sawa. Shughuli
hii itakuza stadi za mawasiliano na ushirikiano pamoja na mshikamano wa
kijamii wanaposhiriki katika shughuli hizi kama kikundi. Itakuza suala la
umoja katika kufanya kazi katika vikundi.
Hitimisho
Hitimisha kwa kuangalia vitabu vya wanafunzi ili kuhakikisha kwamba sentensi na
maneno vimeundwa. Ikiwa kuna muda uliosalia, kusanya vitabu vya wanafunzi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika sentensi zilizo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa
105-106 ifaavyo.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 105
1. bauo…………………..ubao
2. mbekoki………………kikombe
3. zindi………………… ..ndizi
4. ngira…………………...rangi
5. kojiki………………….kijiko
133
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Zoezi la 2, ukurasa 105-106
1. Nilikula vibanzi kwa samaki.
2. Mwalimu alimpa Nekesa kazi ya nyumbani.
3. Ng’ombe anatupatia maziwa na nyama.
4. Jua linang’ara angani.
5. Ndani ya wiki kuna siku saba.
Somo la 3: Kuandika majina
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia kitenzi mwafaka na nomino
kutunga sentensi.
Habari za kimsingi
Wanafunzi wataandika majina picha zilizotolewa. Hili litawasaidia katika ujenzi
wa maneno na mwandiko. Angalia kazi ya kila mwanafunzi ili kuhakikisha kwamba
wanashiriki.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, penseli
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 106
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuteua wanafunzi bila kuzingatiaa utaratibu maalumu kusoma
sentensi kutoka katika zoezi.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi wakiwa wawili wawili kutazama picha katika Kitabu cha
Mwanafunzi, ukurasa 106 kwa makini na kusema wanachokiona.
2. Waagize wanafunzi kuandika majina ya vitu wanavyoviona katika picha hizo.
3. Waulize wanafunzi kutaja jina linalotumiwa kurejelea majina ya vifaa, wanyama,
mahali au watu.
4. Wataje nomino nyingine zaidi wanazojua. Hili litakuza kukiri kwa kina
katika wanafunzi. Wanafunzi watawazia mahali na wanyama wanaowajua na
hivyo kupata nomino.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kuandika baadhi ya nomino zilizotajwa
darasani. Angalia kazi ya wanafunzi.
Tathmini
Waagize wanafunzi kuandika majina ya sehemu tano na watu watano unaowajua.
134
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Majibu, Zoezi la ukurasa 106
a. Ngamia b. Penseli ch. Embe
d. Meza e. Treni
Somo la 4: Kuunda msamiati
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia maneno mapya aliyoyapata
katika kuongea na kuandika.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watatarajiwa kupata maana za maneno mapya yalivyotumiwa katika
kifungu. Wahimize wanafunzi kutoa maoni yao na hatimaye kuakiana kuhusu maana
za maneno mahususi. Wasaidie wanafunzi katika kupata maana za maneno mapya
pale wanapotatizika.
Nyenzo za kujifunzia
Vitabu, penseli
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 106-107
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi kusoma maneno machache na maana
zake kutoka katika kamusi ya kibinafsi.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi wakiwa wawili wawili kusoma maneno yaliyo katika
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 106-107. Shughuli hii inakuza stadi za
maisha hasa stadi ya kujua jinsi ya kuishi na watu wengine katika jamii kupitia
kwa mawasiliano bora.
2. Waagize wanafunzi kutunga sentensi ilivyooneshwa katika mfano.
3. Teua wanafunzi wachache kuwasomea wenzao darasani sentensi zao.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kutaja taaluma nyingine wanazojua na
wanachotaka kuwa wakiwa wakubwa.
Tathmini
Majibu, zoezi la ukurasa 106-107
1. a) mwalimu e) fundi wa nguo
b) nesi f) rubani
ch) mkulima
d) dereva
2. a) Mwalimu huwafundisha wanafunzi.
b) Daktari hutibu wagonjwa.
135
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
ch) Seremala hutengeneza viti vya mbao.
d) Rubani huendesha ndege.
e) Wakili hutetea watu mahakamani.
3. Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi
Somo la 5: Insha ya kuelekezwa
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia viunganishi mwafaka katika
kupanga na kuunganisha sentensi.
Habari za kimsingi
Wanafunzi watapewa vihasho watakavyohitajika kujaza. Wasaidie kwa uteuzi wa
maneno.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 107
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi kutaja maneno ya viunganishi wanayoyajua.
Watajie wanafunzi maneno kama vile kwanza, pili, hatimaye, hivi majuzi na kisha.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waagize wanafunzi kusoma insha ya vihasho katika Kitabu cha Mwanafunzi
ukurasa 107 na wajaze mapengo wakiwa wawili wawili. Hili litakuza ubunifu
na uwezo wa kuki kwa kina katika mwanafunzi.
2. Teua mmoja mmoja katika wawili wawili hao kusoma kifungu chao.
3. Fanyeni masahihisho pamoja darasani.
Hitimisho
Hitimisha kipindi kwa kuangalia kitabu cha mazoezi cha kila mwanafunzi na usahishe
kazi yake.
Tathmini
Angalia ufaafu wa majibu ya wanafunzi kulingana na zoezi katika Kitabu cha
Mwanafunzi.
Majibu
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi
136
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Wiki ya 20
Mpangilio wa masomo
Somo la 1: Kuzungumza kuhusu mji au kijiji chako
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kutumia kuhusisha wahusika na
matukio katika hadithi na maisha halisi.
Habari ya kimsingi
Wanafunzi watazungumza kuhusu kijiji au mji wao na kutazama picha katika Kitabu
cha Mwanafunzi ukurasa 108 ili kulinganisha. Hakikisha kuwa kila mwanafunzi
anahusika kwa kueleza kuhusu mki au kijiji chao.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 108-109
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi kueleza wanakotoka.
Shughuli za ujifunzaji
1. Wapange wanafunzi katika vikundi ili waambiane wanakotoka. Ni mji au
kijiji?
2. Waambie wanafunzi waeleze mijengo inayopatikana katika maeneo yao.Hili
litakuza uraia kupitia mshikamano wa kijamii. Wanafunzi watahusika katika
mjadala ambapo umoja utakuzwa.
3. Waambie wanafunzi watazame picha kwenye kitabu cha mwanafunzi wakiwa
wawili wawili. Waseme wanachoona kwenye picha.
4. Waambie wanafunzi wajadili kuhusu umuhimu wa mijengo.Hili litakuza stadi
ya mawasiliano na ushirikiano.
5. Waambie wajadili uhusiano baina ya picha na hali ya kwao. Waseme mijengo
inayopatikana kwao na kuandika ilivyo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wataje mijengo inayopatikana katika
maeneo yao.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike sentensi sita kufafanua maeneo yao.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 108
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 108-109
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
137
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Somo la 2: Chora na uonyeshe
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi,mwanafunzi aweze kutumia maneno na vifungu
anavyojua kuandika sentensi nyepesi.
Habari ya kimsingi
Wanafunzi watatumia picha kuunda maneno na sentensi kisha kuzifafanua. Angalia
wanavyotunga sentensi na uhimize matumizi ya msamiati.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 109
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi wabadilishane vitabu na kusoma
sentensi walizokuwa wameandika kuhusu maeneo yao.Teua wanafunzi watatu
kuwasomea wenzao sentensi zao.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wachore duka lolote kijijini au mjini na kuandika aya
fupi kulihusu.
2. Waambie waoneshane picha katika. Hili litakuza ushirikiano na mawasiliano.
Itakuza pia maadili ya heshima wanapotazama picha za wenzao na kutoa
maoni kuzihusu.
3. Waoneshe picha mmoja baada ya mwingine.
4. Wanafunzi wapige kura kuchagua picha bora.
5. Mwanafunzi ambaye picha yake imechaguliwa kuwa bora aichore upya kwenye
karatasi ya kuchora, na kuibandika ubaoni.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi waseme wanayopenda kuhusu maeneo
yao.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike aya fupi kuhusu wanachopenda katika maeneo yao
Somo la 3: Soma na uhadithie upya
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kukumbuka mambo muhimu kuhusu
visa na kuyaeleza.
138
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Habari ya kimsingi
Wanafunzi waweze kusikiliza hadithi kwa makini na kukumbuka mambo muhimu ya
hadithi hiyo.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu, magazeti
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 110
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwambia wanafunzi waseme hadithi walizosoma na kile
wanachokumbuka kuzihusu.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wasome hadithi kwenye kitabu cha mwanafunzi wakiwa
wawili wawili.
2. Waambie wanafunzi wakariri hadithi hiyo kwa maneno yao, mmoja baada ya
mwingine. Mmoja akariri mwenzake akisikiliza.
3. Waambie waambiane hadithi nyingine wanazojua. Hili litakuza uwezo wa
kukiria kwa kina wanapoambiana hadithi.
4. Mteue mwanafunzi mmoja wa kujitolea kuwaambia wenzake hadithi.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwahimiza wanafunzi kusoma hadithi na kuwaambia
wazazi au walezi wawaambie hadithi mara nyingi.
Tathmini
Waambie wanafunzi waseme hadithi wanazojua wakati wa muda wao wa mapumziko.
Somo la 4: Muulize raki yako
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa somo, mwanafunzi akuze msamiati kupitia kusikiliza visa au
vifungu.
Habari ya kimsingi
Wanafunzi wahusike katika mazungumzo na kujibu maswali yafaayo.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 110-111
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi ikiwa waliambiana hadithi kulingana
139
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
na tathmini ya somo la 3. Wanafunzi wawaambie wenzao mada za hadithi na funzo
walilopata kutoka kwa hadithi walizosoma.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wasikilize unaoposoma mazungumzo baina ya Maria na
mwalimu. Mwanafunzi mmoja awe Maria.
2. Waambie wanafunzi wasome mazungumzo wakiwa wawili wawili. Mmoja
awe Maria, mwingine mwalimu. Wabadilishane majukumu na kusoma tena.
3. Waambie wanafunzi waulizane maswali kuhusu maneneo yao, jinsi ilivyo
kwenye mazungumzo. Hili litakuza stadi ya kujua na kuishi na wengine kupitia
mawasiliano bora. Wataambiana kuhusu maeneo hayo, hivyo basi kukuza umoja.
4. Waambie waandike majibu yao
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwaambia wasomaji wabadilishane vitabu na kusoma sentensi
za wengine.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike sentensi tano kuhusu eneo la raki yake kwa kurejelea
waliyojadili.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 110-111
Mwalimu atathmini matamshi ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 111
Mwalimu atathmini maigizo ya wanafunzi.
Somo la 5: Kuandika majibu
Matokeo maalum ya ujifunzaji
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze kujieleza vyema kwa kutumia msamiati
kuawasiliana vyema.
Habari ya kimsingi
Wanafunzi watatumia maneno waliyozoea kutumia kueleza maeneo yao kuandika
majibu ya maswali ya kipindi hiki.Wanafunzi waweze kutumia msamiati kuandika
insha.
Nyenzo za kujifunzia
Wanafunzi wenyewe
Vitabu
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 111-112
140
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
Utangulizi
Tanguliza kipindi kwa kuwaambia wanafunzi watatu wasome sentensi walizoandika
ili kueleza maeneo ya raki yake. Muulize raki yake kuthibitisha maelezo hayo.
Shughuli za ujifunzaji
1. Waambie wanafunzi wajaze mapengo katika nafasi zilizoachwa kueleza wanakoishi.
2. Waambie wasome maneno ya zoezi la 2 katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa
112 ukurasakatika makundi.
3. Waambie watunge sentensi kwa maneno waliyopewa.
4. Waambie wabadilishane vitabu na kusoma sentensi za wenzao.
Hitimisho
Kamilisha kipindi kwa kuwaambia wanafunzi waseme walilojifunza kuhusu maeneo
ya maraki wao.
Tathmini
Waambie wanafunzi waandike insha kuhusu mazingira bora wanayotamani kuishi.
Majibu
Zoezi la 1, ukurasa 111-112
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Zoezi la 2, ukurasa 112
Mwalimu atathmini matamshi na majibu ya wanafunzi.