
71
Kimeidhinishwa na KICD-Toleo la 2018
d) Wanafunzi wanachangia makala kwa jarida la shule.
Tathmini zinazopendekezwa
a) Kusimulia hadithi (zingatia matumizi ya mianzo ya masimulizi)
b) Maswali na majibu, maigizo, usikilizaji wa kuigiza
c) Kusoma maneno na kauli fupi fupi
d) Wanafunzi wanajipanga kutoa hadithi mmoja na mwingine kusimulia hadithi
na kuandika maneno ya kufafanua picha.
Nyenzo za ujifunzaji zinazopendekezwa
Penseli, kadi za kusoma, picha, vipande vilivyokatwa vya magazeti, vitabu vya hadithi,
kanda za sauti, kanda za video kuhusu mazungumzo yanayohusiana na mada hii,
simu, nyenzo za kusoma, kadi za picha, chati, maktaba, rialia, mipangilio ya hadithi,
maneno funguzi katika hadithi nk.
Kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalum
Usaidizi kwa wanafunzi wenye uwezo
mbalimbali
Usaidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji
maalum
· Himiza wanafunzi wenye uelewa wa
polepole kushiriki katika mazungumzo
kama maigizo na kusimulia hadithi.
· Wape wanafunzi wenye uelewa
wa haraka kazi nyingi ili kuepuka
kuwachosha na kuzubaa darasani.
· Wape wanafunzi wenye uelewa wa
polepole na haraka nafasi za kutosha
katika shughuli za darasani. Una jukumu
la kuhakikisha kwamba wanafurahiana
na kufurahia kukaa pamoja licha ya
tofauti zao.
· Kwa wanafunzi wasio na uwezo wa
kuona, wape breli, picha za kugusa
na wale wasioweza kuona vizuri wape
maandishi makubwa.
· Kwa wanafunzi walio na shida ya
kusikia vizuri tumia lugha ishara au
kumleta mtaalamu wa lugha ishara
kufasiri.
· Wanafunzi ambao hawawezi kuona
mbali wakae mbele darasani na wenye
uwezo wa kuona mbali wakae nyuma.
· Wape wanafunzi wenye ulemavu
majukumu wanayoweza kutekeleza
kama vile kuigiza nafasi ya mwalimu
mkuu au balozi wa kijiji. Wape usaidizi
wa kutosha na kuhakikisha kwamba
wanafunzi wengine wanafanya
hivyo, kwa mfano, kuwasaidia katika
kusukuma kitimagurudumu cha kwa
mwanafunzi mlemavu.