
3
3
Bakari na mkewe, Bahati, waliishi kwenye
nyumba ya wastani iliyoezekwa paa la makuti. Ilijikita
masafa mafupi kutoka kwenye Ufuo wa Watamu.
Bakari aliinukia katika kizazi cha wavuvi. Uvuvi
kwake ulikuwa kazi tunu sana. Aliyapenda maisha ya
bahari, na vilevile, alikuwa mpiga mbizi stadi. Moja
kati ya vipenzi vyake vya kuburudika ilikuwa kupiga
picha samaki mbalimbali wa baharini. Pia alikusanya
sanaa ambazo ziliundwa kwa kutumia viumbe hao
waliokaushwa. Haikushangaza kwamba nyumba ya
familia yake ilikabiliana na bahari.
Mandhari ya bahari ya Ufuo wa Watamu
yalionekana mtu alipochungulia dirishani. Mtu aliweza
pia kuona majabali matatu ambayo yalichomoza
kutoka baharini.
Jabali moja kubwa na bapa, lilijitandaza kuliani. La
pili kwa ukubwa, lilichongoka juu kidogo kushotoni.
La tatu, ambalo lilikuwa dogo kabisa, lilijipachika
katikati. Sura za majabali hayo zilikuwa kitambulisho
maarufu cha Ufuo wa Watamu.
Mara kwa mara, wakati wowote Bakari angetaka
kujivinjari na wanawe, ungemwona pwani akitembea.
Pembeni mwake watoto wake wangeruka wakifurahia
mandhari ya ufuoni. Vinyama mbalimbali vya baharini
vingekimbilia machoni vikihoa usalama wao.
Bakari na Bahati walibarikiwa kupata watoto
watatu. Kijana Adili alikuwa mkubwa kabisa,