Kimeidhinishwa na KICD
Kimeidhinishwa na KICD
Longhorn
Mwanga
wa
Kiswahili
Mwongozo wa Mwalimu
Gredi ya 4
Ann Vaati
Sarah Kerubo
Mary Kikwanuu
Kenan Ngere
Hellen N. Kangai
Kimeidhinishwa na KICD
Kimechapishwa na:
Longhorn Publishers PLC,
Barabara ya Funzi, Eneo la Viwandani,
S.L.P. 18033 00500,
Nairobi, Kenya.
Simu: +254 02 6532579/81, +254 02 558551,
+254 708 282 260, +254 722 204 608
Baruapepe: enquiries@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Uganda) Ltd.,
Plot 4, Barabara ya Vubyabirenge,
Eneo la Ntinda,
S.L.P. 24745,
Kampala, Uganda.
Simu: +256 414 286 093
Baruapepe: ug@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Tanzania) Ltd.,
Barabara ya Bagamoyo/Barabara ya Garden,
Mikocheni B, Plot No. MKC/MCB/81,
S.L.P. 1237,
Dar es Salaam, Tanzania.
Simu: +255 714 184 465
Baruapepe: longhorntz@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
Longhorn Publishers (Rwanda) Ltd.,
Remera, mkabala wa Benki ya COGE,
S.L.P. 5910,
Kigali, Rwanda.
Simu: +250 784 398 098
Baruapepe: rwanda@longhornpublishers.com
Wavuti: www.longhornpublishers.com
© H. N. Kangai, A. Vaati, S. Kerubo, M. Kikwanuu, K. Ngere, 2019
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupigisha
chapa, kutafsiri au kukitoa kitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila idhini,
kwa maandishi, ya kampuni ya Longhorn Publishers PLC.
Chapa ya kwanza, 2019
Msanifu wa Jalada: Tu Mulokwa
ISBN 978-9966-64-291-2
Kimepigwa chapa na Modern Lithographic (K) Ltd
S.L.P. 52810-00200, Nairobi, Kenya
Kimeidhinishwa na KICD
iii
Kimeidhinishwa na KICD
Yaliyomo
NYUMBANI . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .1
Kusikiliza na Kuzungumza: Matamshi bora ...............................1
Kusoma: Kusoma kwa ufahamu .........................................11
Kuandika: Kuandika insha..............................................17
Saru: Aina za maneno ................................................22
NIDHAMU MEZANI . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 33
Kusikiliza na Kuzungumza: Maamkuzi na maagano .......................33
Kusoma: Kusoma kwa ufahamu .........................................38
Kuandika: Kuandika insha..............................................43
Saru: Aina za maneno.................................................47
MAVAZI . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 56
Kusikiliza na Kuzungumza: Matamshi Bora .............................56
Kusoma: Kusoma kwa ufahamu .........................................62
Kuandika: Kuandika kwa kutumia tarakilishi..............................67
Saru: Aina za maneno.................................................72
DIRA . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 84
Kusikiliza na Kuzungumza: Heshima, adabu na vyeo ......................84
Kusoma: Kusoma kwa mapana ..........................................88
Kuandika: Kuandika barua .............................................92
Saru: Ngeli za nomino ................................................96
USHAURI NASAHA . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 104
Kusikiliza na Kuzungumza: Methali ....................................104
Kusoma: Kusoma kwa ufahamu ........................................108
Kuandika: Kuandika Insha.............................................113
Saru: Umoja na wingi wa nomino .....................................118
BENDERA YA TAIFA . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 127
Kusikiliza na Kuzungumza............................................127
Kusoma kwa kina ....................................................131
iv
Kimeidhinishwa na KICD
Kuandika: Kuandika Insha.............................................135
Saru: Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya LI-YA ..................139
MATUNDA NA MIMEA . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 152
Kusikiliza na Kuzungumza............................................152
Kusoma: Kusoma kwa mapana .........................................156
Kuandika: Kuandika Insha.............................................161
Saru: Umoja na wingi wa sentensi .....................................165
WANYAMA WA PORINI . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 175
Kusikiliza na Kuzungumza: Visawe ....................................175
Kusoma: Kusoma kwa ufahamu ........................................179
Kuandika: Kuandika Insha.............................................185
Saru: Mnyambuliko wa vitenzi ........................................190
AFYA BORA . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 198
Kusikiliza na Kuzungumza: Mazungumzo ..............................198
Kusoma: Kusoma kwa mapana .........................................202
Kuandika: Kuandika insha.............................................208
Saru: Vinyume vya nomino...........................................212
KUKABILIANA NA UHALIFU . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 218
Kusikiliza na Kuzungumza: Tashbihi ...................................218
Kusoma: Kusoma kwa mapana .........................................222
Kuandika: Kuandika Insha.............................................227
Saru: Nyakati na hali.................................................231
MAPATO . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 239
Kusikiliza na Kuzungumza: Kuzungumza na kujieleza kwa ufasaha .........218
Kusoma: Kusoma kwa ufahamu ........................................243
Kuandika: Kuandika Barua ............................................248
Saru: Ukanushaji ....................................................252
Ukubwa na udogo wa nomino ...................................258
v
Kimeidhinishwa na KICD
UTANGULIZI
A. Taarifa kuhusu mtaala wa umilisi
Mabadiliko ya mtaala wa elimu ya msingi yalilenga kumwezesha kila Mkenya kuwa
raia aliyeshirikishwa, aliyewezeshwa na aliyeadilika. Haya yatatendeka kwa kumpa
kila mwanafunzi Mkenya kaida zinazofaa katika uwezo na ujuzi anaohitaji ili kufaulu
maishani.
Mwongozo huu wa mwalimu umeandaliwa ili kufanikisha jukumu la mwalimu wa
mtaala wa umilisi. Mwalimu katika mtaala wa kiumilisi ni mwezeshaji, kiongozi na
mwelekezi wa mwanafunzi katika shughuli mbalimbali za kiutendaji katika ujifunzaji
wa vipengele mbalimbali vya lugha ya Kiswahili. Mwongozo huu unampa mwalimu
mbinu za kutambua na kupalilia vipawa na mahitaji ya wanafunzi mapema kabisa
ili kuwaandaa kwa ulimwengu wa kazi, kujiendeleza kikazi na maendeleo endelevu.
Mtaala wa umilisi humfanya mwanafunzi kuwa kiini cha mchakato mzima wa kusoma.
Mwongozo huu wa mwalimu uliojengwa kwa mtaala uliokitwa katika umilisi unatoa
mbinu za kutathmini, kuendeleza maadili na mshikamano wa kitaifa.
Mwalimu anapaswa kupalilia uwezo wa mwanafunzi kupitia njia za usomaji ambazo
zimeangaziwa katika kitabu hiki. Nia ni kutambua uwezo wa mwanafunzi, vipaji na
vipawa ili pasiwe na mwanafunzi ambaye atadaiwa kuwa amefeli katika maisha au
katika masomo.
Kauli za Kimsingi za Lugha ya Kiswahili ya Masomo ya Shule ya Msingi, Gredi za Juu
Kiswahili ni lugha kuu ya mawasiliano, elimu, biashara, habari, diplomasia na
mahusiano ya kijamii. Ndiyo lugha ya mawasiliano mapana katika Afrika Mashariki
na Kati. Imeenea sana na hutumiwa katika maeneo mengine barani Afrika na sehemu
nyingine za ulimwengu na katika mitandao. Kiswahili ni lugha ya taifa na pia lugha
rasmi nchini Kenya. Hutumiwa kufunzia madarasa ya chini katika mfumo wa elimu.
Ni muhimu basi mwanafunzi awe na msingi thabiti katika lugha hii ili aweze kushiriki
ipasavyo katika shughuli za kitaifa, kikanda na kimataifa. Msingi huu pia utamfaa
mwanafunzi katika masomo ya awali ya shule ya upili.
Kwa hivyo, ustadi katika lugha ya Kiswahili ni muhimu katika kutimiza Malengo ya
Kitaifa ya Elimu na kutimiza wajibu wa kuwa kama chombo cha kuunganisha jamii ya
kimataifa na ufunguo wa mtandao wa habari wa kimataifa.
vi
Kimeidhinishwa na KICD
B. Malengo ya Kitaifa ya Elimu
Mfumo wa mtaala mpya utakitwa katika Malengo ya Kitaifa ya Elimu. Malengo haya
nchini Kenya ni:
1. Kukuza utaifa, uzalendo na kuendeleza umoja wa kitaifa
Kama tujuavyo, Wakenya ni wa asili, jamii na dini tofauti hivyo, wanapaswa kuishi na
kutangamana kama jamii moja. Elimu inapaswa kuwezesha mwanafunzi kuwa na hisia
za utaifa na uzalendo. Inapaswa kuhimiza utangamano na amani.
2. Kuendeleza ujenzi wa taifa kiuchumi, kiteknolojia na kijamii
Elimu inapaswa kumtayarisha mwanafunzi kushiriki inavyofaa kwa ukamilifu katika
taifa.
a) Mahitaji ya kijamii
Elimu inapaswa kuibua mbinu za kijamii kwa mwanafunzi ili aweze kushiriki kikamilifu
katika maendeleo ya familia, jamii, taifa, kanda na ulimwengu.
b) Mahitaji ya kiuchumi
Elimu inapaswa kumwandaa mwanafunzi na umilisi ambao unahitajika kuendeleza
uchumi ambao ni huru na wa kisasa na unaozidi kukua. Jambo hili litahakikisha kuwa
kila mtu anaishi maisha ya hadhi au kiwango cha juu.
ch) Mahitaji ya kiteknolojia na kiviwanda
Elimu inapaswa kumpa mwanafunzi umilisi mwafaka wa maendeleo ya kiteknolojia
na kiviwanda ya nchi, sawia na maendeleo ya mataifa mengine ulimwenguni.
3. Kujiendeleza na kujiajiri binafsi
Elimu inastahili kumwezesha mwanafunzi kujiendeleza hadi kukia upeo wa juu zaidi.
Hii ni pamoja na kuendeleza yamvutiayo, vipawa na mienendo ili kuchangia jamii
ifaavyo.
4. Kuendeleza uadilifu na amali za kidini
Elimu inafaa kukuza upataji wa maadili ya taifa kama ilivyowekwa wazi katika Katiba
ya Kenya. Inapaswa kulenga kukuza mwananchi mwenye nidhamu yake mwenyewe na
mwenye thamani za kimaadili na za kidini.
vii
Kimeidhinishwa na KICD
5. Kuhimiza usawa wa kijamii na uwajibikaji
Elimu inapaswa kuhimiza usawa wa kijamii na uwajibikaji. Inapaswa kuwawezesha
wananchi wote kupata elimu bora hata wale wanafunzi wenye mahitaji maalum ya
kiusomi na ulemavu.
6. Kukuza, kuhifadhi na kuthamini tamaduni za jamii mbalimbali nchini Kenya
Elimu inapaswa kumfanya mwanafunzi athamini turathi nyingi za aina mbalimbali
zilizomo nchini Kenya. Mwanafunzi anapaswa kuthamini na kuheshimu utamaduni
wake pamoja na wa wengine.
7. Kuendeleza uhusiano wa kimataifa na kudumisha mwelekeo ufaao kwa mataifa
mengine ulimwenguni
Elimu inapaswa kumwezesha mwanafunzi kuheshimu, kuthamini na kuhusika
katika nafasi zilizomo katika jamii ya kimataifa. Pia, elimu inapaswa kumwezesha
mwanafunzi kuishi katika jamii ya kimataifa akijua ka wajibu, majukumu, haki na
manufaa yanayotokana na uhusika huu.
8. Kuendeleza uhifadhi wa afya bora na mazingira
Elimu inafaa kumfunza mwanafunzi umuhimu wa afya ya kimwili na kiakili-kijamii;
yaani afya yake na ya wananchi wengine. Pia, inahimiza uhifadhi na utunzaji wa
mazingira na ustawi wa wanyama.
CH. Malengo ya Jumla ya Masomo ya Gredi za Kati
Kukia masomo ya gredi za kati, mwanafunzi anapaswa:
1. Kuwasiliana inavyostahili katika miktadha mbalimbali.
2. Kutumia elimu, stadi za kihisabati na uwazaji wenye mantiki katika kujieleza.
3. Kuwa na stadi za kijamii na thamani za kiimani na kimaadili ili kuishi pamoja
kwa amani.
4. Kutalii, kusimamia na kuhifadhi mazingira kwa ajili ya maendeleo endelevu.
5. Kuwa na usa wa binafsi, usa wa mazingira na lishe ili kuendeleza afya.
6. Kutumia ujuzi wa kidijitali unaofaa kwa ajili ya mawasiliano na elimu.
7. Kuadilika na kuonyesha uananchi unaofaa kama jukumu la kiraia.
8. Kuweza kuthamini turathi mbalimbali za nchi ili kuishi pamoja kwa amani.
9. Kudhibiti kwa ukamilifu masuala yaliyo muhimu na ya kisasa.
viii
Kimeidhinishwa na KICD
D. Malengo ya jumla ya masomo yanayohusu Kiswahili
Kufikia mwisho wa masomo ya gredi za juu katika shule ya msingi,
mwanafunzi anapaswa:
1.
Kusikiliza na kujibu inavyostahili anapopata ujumbe muhimu katika miktadha
tofauti tofauti.
2.
Kusoma matini mbalimbali kwa ufasaha, usahihi na kwa uchanganuzi kwa
ajili ya masomo endelevu.
3.
Kutumia maumbo ya kisarufi kuwasilisha hoja, maoni na hisia inavyofaa
katika miktadha mbalimbali.
4.
Kuandika matini kwa ajili ya malengo mbalimbali kwa hati inayosomeka,
usahihi, ubunifu, na ushikamano ili kujieleza.
5.
Kutumia ujuzi wa kidijitali kukuza umilisi wake wa lugha.
Utegemeano uliopo baina ya Malengo ya Kitaifa ya
Elimu, Malengo ya Jumla ya Masomo ya Gredi za
Kati, Malengo ya jumla ya mafunzo ya Kiswahili na
malengo mahususi ya mafunzo
E.
Mwalimu anapaswa kufahamu utegemeano uliopo baina ya Malengo ya Kitaifa ya
Elimu na Malengo ya Jumla ya Masomo ya Gredi za Kati. Ufahamu huu utamsaidia
kujenga mwingiliano baina ya malengo katika viwango mbalimbali na kuzihusisha na
utegemeano uliopo baina ya Malengo ya Kitaifa ya Elimu. Haya yatamsaidia mwalimu
kuwa na muumano wa utegemeano baina ya Malengo ya Kitaifa ya Elimu na malengo
katika viwango mbalimbali, atakuwa mbunifu na mvumbuzi katika mtazamo wa
mafunzo pamoja na kujua haki na majukumu ya wanafunzi.
Mfano:
Lengo la Kitaifa la Elimu
(Nambari 3)
Kujiendeleza na kujiajiri
kibinafsi.
Lengo la jumla la masomo ya Gredi za katikati
(Nambari 1)
Kuwasiliana vilivyo katika
miktadha mbalimbali.
Lengo la Jumla la Kujifunza Kiswahili (Nambari 1)
Kusikiliza na kujibu inavyopasa
anapopata taarifa muhimu katika
miktadha mbalimbali.
ix
Kimeidhinishwa na KICD
Lengo Mahususi la Somo (2)
Mada Kuu 2: Nidhamu Mezani
A. Kusikiliza na kuzungumza:
Mada ndogo: Maamkuzi na Maagano
Kutambua maamkuzi na maagano
ya nyakati mbalimbali ambayo
hutumiwa katika mawasiliano.
F. Muundo wa Mwongozo huu wa mwalimu
Mwongozo huu wa mwalimu umegawanywa katika sehemu mbili kuu:
Sehemu ya kwanza: inaangazia utangulizi wa jumla ambao unafafanua masuala
ya ufundishaji.
Sehemu ya pili: inaangazia maendelezo ya ufundishaji wa mada kuu ambazo
zimeshughulikiwa katika Kitabu cha Mwanafunzi.
1. Mada
Mada ni muktadha mpana unaotumiwa kufunzia lugha. Kwa mfano, katika Gredi
ya Nne tuna mada kama vile: Nyumbani, Nidhamu mezani, Kukabiliana na Uhalifu,
Mapato na mada nyinginezo. Kimsingi, zinahusiana na tajriba za wanafunzi na
shughuli ambazo wanafanya kila siku.
2. Matokeo tarajiwa maalumu
Haya ni matokeo ya ujifunzaji katika mada ndogo tofauti zilizomo katika mada kuu.
Huonyesha kwa kifupi, matokeo yote maalumu ambayo yatashughulikiwa katika mada
kuu nzima.
3. Maswali dadisi
Maswali dadisi ni mbinu ambapo mwalimu huuliza maswali ili kuhimiza fikra za
wanafunzi na kuwawezesha kuibua taarifa wakitumia maneno yao binafsi na uelewa
wao. Maswali dadisi husaidia:
Kuupa usomaji mwelekeo au mkondo wa kufuata;
Kuchunguza maana za ndani hivyo kuweka msingi wa uchunguzi wa baadaye;
Kujenga stadi za ukiriaji wa kina na utafutaji suluhu wa kiwango cha juu;
Kuwaruhusu wanafunzi kutalii hoja kwa njia iliyo wazi, isiyohukumu.
Kuhimiza ushirikiano baina ya wanafunzi, walimu na jamii na kushirikisha
teknolojia kuhimili mchakato wa masomo.
x
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya maswali dadisi yametolewa katika mwongozo huu. Mwalimu ana
uhuru wa kubuni na kuongeza yake katika kila somo. Anapobuni swali:
Azingatie lengo la matarajio yake ya somo na mada kama ilivyotolewa katika
mfumo wa mtaala;
Achunguze mada kuu au dhana katika mtaala ambayo yapaswa kuzingatiwa.
Azingatie maswali sita ya kawaida: Nani? Nini? Wapi? Lini? Kwa nini? Vipi?
4. Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mbinu iliyokitwa katika umilisi huwezesha mahusiano ndani ya somo na baina ya
masomo. Kuna aina saba za umilisi wa kimsingi ambazo kila mwanafunzi atapata:
a) Mawasiliano na ushirikiano b) Kujiamini
ch) Uwazaji kina na utatuzi wa matatizo d) Ubunifu
e) Uraia f) Ujuzi wa kidijitali
g) Hamu ya ujifunzaji
Aina hizi zitapatikana wakati wanafunzi watakuwa wametimiza malengo yote ya somo.
5. Uhusiano na masuala mtambuko
Watoto wanakumbana na changamoto chungu nzima kama ilivyo kwa watu wazima
kutokana na mabadiliko ya kisheria, kiteknolojia, kijamii, kitamaduni na kiuchumi
katika jamii. Changamoto ambazo watoto na watu wazima hukumbana nazo
zimeshughulikiwa katika mtaala mpya wa umilisi kama masuala mtambuko. Kuna
masuala sita ya mtambuko yaliyoangaziwa katika kitabu hiki:
a) Uraia wa kimataifa
b) Elimu ya afya
ch) Stadi za maisha na elimu ya maadili
d) Elimu ya maendeleo endelevu
e) Mipango ya kuwasaidia wanafunzi
f) Usomaji unaohusisha huduma kwa jamii na kushirikishwa kwa wazazi.
Masuala haya sita yameshirikishwa katika shughuli za ufunzaji za kila kipindi.
6. Uhusiano na maadili
Maadili ni vigezo ambavyo humwongoza mtu kwa namna ya kujibu au kutenda katika
muktadha fulani. Ufunzaji wa maadili utasaidia kukia malengo ya mabadiliko ya
mtaala wa kuibua wananchi waadilifu. Maadili ya kimsingi ambayo yamesisitizwa
xi
Kimeidhinishwa na KICD
katika mwongozo huu ni upendo, uwajibikaji, heshima, umoja, amani, uzalendo, haki
za kijamii na uadilifu.
7. Uhusiano na masomo mengine
Ni muhimu wanafunzi wakipata ufahamu wa uhusiano baina ya masomo tofauti ili
usomaji wa kila somo utiliwe mkazo katika mtaala mzima. Sehemu hii inamwandaa
mwalimu kuwafahamisha wanafunzi ili wajue kuhusu uhusiano huu.
8. Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Usomaji unaohusisha huduma kwa jamii ni mbinu ya usomaji kiutendaji ambao
hushirikisha usomaji darasani na usomaji kutokana na jamii ili kuwawezesha
wanafunzi kuwaza, kupitia na kujifunza kutokana na jamii. Shughuli za usomaji
unaohusisha huduma kwa jamii zimependekezwa ili wanafunzi watumie ujuzi na stadi
ambazo wamepata katika miktadha rasmi katika jamii zao wakati uo huo wakisoma
kutokana na jamii. Wanafunzi watapata stadi za kuwawezesha kuajiriwa na wakati uo
huo kuendeleza ukuaji wa binafsi kwa mahusiano thabiti na fanikifu katika jamii.
Shughuli nyingi za usomaji unaohusisha huduma kwa jamii zimejikita katika Uraia,
Ujasiriamali, Ujuzi wa Kiuchumi, Stadi za Maisha, Stadi za Mawasiliano na Utati.
9. Mbinu za tathmini zilizopendekezwa
Sehemu hii imeonyesha mbinu mbalimbali ambazo mwalimu anaweza kutumia
kutathmini maendeleo ya wanafunzi darasani.
10. Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Sehemu hii inaonyesha namna mwalimu anavyoweza kuwashughulikia wanafunzi
ambao wana mahitaji mbalimbali na maalumu katika ufundishaji. Mahitaji ya kila
kipindi yatiliwe maanani.
11. Maelezo ya jumla
Sehemu hii ina mapendekezo ya namna ambavyo mwalimu atatanguliza kipindi na
kuwashirikisha wanafunzi katika kipindi kizima. Pia, sehemu hii inamfahamisha
mwalimu namna ya kutumia nyenzo zinazopatikana kwa urahisi katika mazingira
yake kulingana na shughuli mbalimbali katika Kitabu cha Mwanafunzi.
12. Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
Nyenzo za kufundishia shughuli mbalimbali zimependekezwa kwa kila kipindi.
Mwalimu awe huru kubuni nyenzo zake kulingana na uwezo wake, mazingira yake na
muda alio nao.
xii
Kimeidhinishwa na KICD
13. Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Utaratibu wa kufundisha shughuli zote katika kitabu hiki umeangaziwa katika
kila kipindi. Hii ni kumwelekeza mwalimu kufuata mpangilio sahili kuanzia
kwa wanachokijua wanafunzi hadi kwa wasichokijua ambacho watajifunza kwa
kujigundulia.
G. Mchakato wa ufunzaji
Dhima ya mwalimu katika mtaala wa umilisi ni ile ya kuwa mwezeshaji. Yeye
huwezesha ugunduzi, upataji na usambazaji wa ujuzi, stadi, maadili na mielekeo
kupitia kwa shughuli za ujifunzaji. Mwalimu hupanga na kudhibiti shughuli hizi za
ujifunzaji darasani au nje ya darasa.
Matendo ya ujifunzaji ni jumla ya shughuli ambazo mwanafunzi anashiriki katika
kipindi. Shughuli hizi zinaweza kutekelezwa na mwanafunzi binafsi au kama kazi za
vikundi.
Matendo mbalimbali ya ujifunzaji humwezesha mwanafunzi:
Kupata ujuzi, ustadi na mielekeo.
Kupata umilisi uliolengwa.
Kujifunza kutoka kwa wenzao.
Kujitathmini na kuwatathmini wengine.
Kujishughulisha zaidi katika mada.
Kutafakari kuhusu mchakato wa ujifunzaji.
Kutangamana na wengine katika mchakato wa ujifunzaji.
Kuwaweka wanafunzi katika vikundi kwa matendo ya ujifunzaji
Mabadiliko kutoka kwa mtaala uliokitwa katika ujuzi hadi kwa mtaala wa umilisi
yatafanya upangaji wa wanafunzi katika vikundi kuwa jambo la kawaida katika
mchakato wa ufunzaji. Hizi ndizo njia mbalimbali za kuwaweka wanafunzi katika
vikundi:
a) Vikundi vya wenye uwezo uliolingana,
b) Vikundi vya wenye uwezo tofauti tofauti,
ch) Vikundi vya wanafunzi wenye kupenda vitu vinavyolingana,
d) Vikundi kwa sababu ya mahitaji mbalimbali,
e) Vikundi kwa misingi ya kijinsia.
xiii
Kimeidhinishwa na KICD
Kuwaweka wanafunzi katika vikundi kuna umuhimu kama vile:
a) Maendeleo na mahitaji ya mwanafunzi binafsi yanaweza kuonekana kwa
urahisi.
b) Uhusiano wa mwalimu na mwanafunzi unakuzwa.
ch) Mwalimu anaweza kushughulikia mahitaji na changamoto za kikundi kidogo.
d) Vifaa ambavyo havingetosha kumpa kila mwanafunzi vinaweza kutumiwa
katika vikundi.
e) Wanafunzi wanaweza kufundishana.
f) Wanafunzi wengi hupokea marekebisho kutoka kwa mwalimu kwa urahisi bila
kuhisi wameaibishwa wanapokuwa katika vikundi vidogo kuliko wakiwa peke
yao.
g) Ubunifu, uwajibikaji na stadi za uongozi za mwanafunzi zinaweza kukuzwa
kwa urahisi.
h) Wanafunzi hufanya kazi kutegemea uwezo wao.
Aina ya upangaji katika vikundi ambao mwalimu atateua utategemea:
a) Mada au shughuli ambayo inatekelezwa.
b) Vifaa vinavyopatikana.
ch) Uwezo wa wanafunzi darasani (juu, wastani, chini).
Hata hivyo, mwalimu anapaswa kuwa mfaraguzi kiasi kwamba anaweza kubadilisha
kidogo au kabisa mtindo wake wa kuwaweka wanafunzi katika vikundi ili kupambana
na hali tofauti katika mada fulani. Hakuna idadi halisi ya wanafunzi ambayo kikundi
kinaweza kuwa nayo. Idadi ya wanafunzi katika kikundi hutegemea shughuli
inatakayofanywa, vifaa vilivyopo, mienendo ya wanafunzi darasani na muda na nafasi
iliyopo. Wanafunzi wanaweza kufanya kazi katika vikundi wakiwa wawili wawili
au hata zaidi kutegemea atakavyowapanga mwalimu. Wanafunzi wanafaa kupangwa
katika vikundi kulingana na idadi yao na mahitaji yao.
Hakuna mbinu au mwelekeo mmoja wa ufunzaji ambao ni mwafaka kwa masomo
yote. Basi, mwalimu anapaswa kuchagua kwa busara mbinu au mchanganyiko wa
mbinu kutegemea mada kuu au mada ndogo inayoshughulikiwa.
xiv
Kimeidhinishwa na KICD
H. Stakabadhi za kikazi
Hizi ni stakabadhi zinazotumiwa na mwalimu katika kuandaa, kutekeleza na kutathmini
ufunzaji na ujifunzaji wa somo lake. Stakabadhi hizi ni muhimu kwa mwalimu. Sharti
awe nazo ili kujua namna ufundishaji wake unavyokwenda, kazi ya wanafunzi na pia
ili kufanya ufunzaji na ujifunzaji kufaulu zaidi.
Stakabadhi hizi ni:
1. Maazimio ya kazi
2. Mpangilio wa somo
3. Rekodi ya ufunzaji
4. Rekodi za maendeleo ya wanafunzi
1. Maazimio ya kazi
Maazimio ya kazi ni stakabadhi ambayo mwalimu hutayarisha kutokana na mfumo
wa mtaala husika. Maazimio ya kazi huonyesha namna yaliyomo katika mtaala
yatasambazwa kwa muda ambao umetengewa sehemu fulani ya vipindi.
Maazimio ya kazi humsaidia mwalimu:
Kupanga vifaa ambavyo vitahitajika.
Kuamua mbinu ambazo zitatumiwa kufundishia.
Kupanga kazi kwa ajili ya tathmini.
Kielelezo cha maazimio ya kazi
Jina la Shule Gredi Somo Muhula Mwaka Jina la Mwalimu
Shule ya
Msingi ya
Juhudi
4 Kiswahili 1 2020 Ahadi Petero
xv
Kimeidhinishwa na KICD
Wiki Kipindi Mada kuu Mada Mada
ndogo
Matokeo
tarajiwa
maalumu
Shughuli za
ujifunzaji
Maswali
dadisi
Nyenzo Tathmini Maoni
4 1
Nidhamu
Mezani
Kusikiliza na
kuzungumza:
Maamkuzi na
maagano
Maana ya
maamkuzi
Kukia mwisho
wa kipindi,
mwanafunzi
aweze:
a) Kutambua
aina mbalimbali
za maamkuzi
katika
mawasiliano.
b) Kueleza
maamkuzi
yanayotumika
katika miktadha
mbalimbali.
ch) Kutumia
aina mbalimbali
za maamkuzi
katika
mawasiliano.
Wanafunzi
wakiwa
wawili wawili
waongozwe
kujadiliana
kuhusu
maamkuzi
ambayo wao
hutumia
nyakati
mbalimbali.
Wanafunzi
wakiwa katika
vikundi wajadili
michoro iliyo
kitabuni mwao
inayoonyesha
maamkuzi
mbalimbali.
Wanafunzi
wakiwa katika
vikundi wataje
maamkuzi
ya asubuhi,
jioni na wakati
wowote.
1. Je, watu
husalimiana
vipi katika
jamii yako?
2. Asubuhi
utamsalimia
vipi mzazi
wako?
Kadi zenye
maamkuzi
mbalimbali.
Kitabu cha
Mwanafunzi,
ukurasa 21.
Breli.
Picha za
watu wa-
naoamkua-
na.
Maswali ya
moja kwa
moja:
Wanafunzi
watambue
maamkuzi
mbalimbali.
Matokeo:
Wanafunzi
waamkuane.
Tathmini ya
vikundi:
Wanafunzi
waigize
maamkuzi
waliyotambua.
xvi
Kimeidhinishwa na KICD
2. Mpangilio wa somo
Mpangilio wa somo ni stakabadhi muhimu katika kufunza na kujifunza. Mpangilio
bora wa somo humsaidia mwalimu:
Kupanga yaliyomo yatakayofunzwa awali kwa kuzingatia wazi yatakayofunzwa
na namna yatakavyofunzwa hivyo kuondoa uvulivuli na yasiyofaa.
Kupanga, kutayarisha na kukusanya vifaa vya ufunzaji/ujifunzaji.
Kuwasilisha dhana na stadi kwa utaratibu kwa kutumia mbinu mwafaka ili
kukia matokeo yanayotarajiwa yaliyotajwa.
Kutumia muda vizuri wakati wa somo.
Kuteua na kuandaa mbinu mwafaka za kupima ili kutathmini mchakato wa
ufunzaji na ujifunzaji.
Kujenga uhusiano baina ya vipengele.
Vipengele vya mpangilio wa kazi
a. Mpangilio wa ufunzaji: Sehemu hii huonyesha mahali ufunzaji utakapotokea.
Yaweza kuwa darasani au nje ya darasa ama ziara maktabani au shamba lililo karibu.
b. Utangulizi: Somo linapaswa kutangulizwa kwa namna ya kuvutia na kuchangamsha
ili kuamsha hamu ya ujifunzaji kwa wanafunzi. Shirikisha tajriba za awali za
wanafunzi iwezekanavyo, ukitumia ujuzi wao walio nao tayari ili kuwaandaa kwa
ujuzi mwingine ambao unataka kutanguliza.
ch. Maendelezo ya somo: Hapa ndipo ufunzaji wa yaliyomo hutokea. Mada
hugawanywa katika sehemu mbalimbali. Kila sehemu yapaswa kuwa na hoja au tukio
moja. Eleza kinaganaga utakavyowasilisha hoja za somo kwa wanafunzi na shughuli
ambazo zinapaswa kutekelezwa katika kila sehemu ili kukia matokeo yanayotarajiwa
ambayo tayari yamebainishwa.
Sehemu hii yapaswa kuonyesha wazi kinachofunzwa na namna kinavyofunzwa, pamoja
na shughuli za wanafunzi (shughuli za ujifunzaji). Mwalimu anapaswa kubadilisha
shughuli za ujifunzaji inapotokea haja.
d. Hitimisho: Hatua hii humalizia somo kwa kutilia mkazo hoja au dhana muhimu
ambazo zimezingatiwa. Katika sehemu hii, muhtasari wa somo hutolewa ili
kuwawezesha wanafunzi kupanga waliyofunzwa katika miktadha mwafaka kwenye
kra zao. Haya yaweza kufanywa kwa:
Kuuliza maswali ili kujua kama matokeo yaliyotarajiwa yameakiwa.
Kuwaruhusu wanafunzi kuuliza maswali ya kupata ubayana.
Kutoa muhtasari wa hoja muhimu katika somo.
Kuwapa shughuli za kufuatilia kama vile zoezi au kazi mradi.
xvii
Kimeidhinishwa na KICD
Ni muhimu kujua kuwa mpangilio wa somo huenda usiwe na taarifa zote kuhusu
yaliyomo, hivyo mwalimu anapaswa kuwa na matini za somo.
e. Kutafakari kuhusu somo: Huu ni uchanganuzi muhimu wa ujifunzaji. Mwalimu
anapaswa kutoa tathmini ya kweli kuhusu utendakazi wake na wa wanafunzi katika
somo na kutoa sababu za ufanisi au kutofanikiwa kwa somo. Mapendekezo ama
suluhisho linapaswa kuonyeshwa katika sehemu hii.
Upangaji wa somo utahitaji msisitizo katika kuingiza na kuchanganya masuala ya
mtaala wa umilisi kama vile: umilisi wa msingi, masuala mtambuko, maadili, shughuli
za ujifunzaji ambazo si rasmi, uhusiano na masomo mengine, nyenzo na tathmini.
Jitihada halisi zifanywe wakati wa upangaji ili kushirikisha aina za mbinu za kuuliza
maswali ambazo zitatumiwa katika somo.
Kielelezo cha mpangilio wa somo
Shule: Shule ya Msingi ya Juhudi
Jina la mwalimu: Ahadi Petero
Muhula Gredi Somo Tarehe Mada Kipindi Muda Idadi ya
Wanafunzi
Idadi ya
wanafunzi
wenye
mahitaji
maalumu
1 4 Kiswahili 14/02/2020
Kusikiliza na
kuzungumza
1
Dakika
35
40 2
Mada Kuu: Nidhamu Mezani
Mada Ndogo: Kusikiliza na kuzungumza: Maana ya maamkuzi
Matokeo maalumu yanayotarajiwa:
Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kutambua aina mbalimbali za maamkuzi katika mawasiliano.
2. Kueleza maamkuzi yanayotumika katika miktadha mbalimbali.
3. Kutumia aina mbalimbali za maamkuzi katika mawasiliano.
4. Kuchangamkia maamkuzi katika mahusiano.
xviii
Kimeidhinishwa na KICD
Nyenzo
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 21,
Kadi zenye maamkuzi mbalimbali,
Breli,
Picha za watu wanaoamkuana.
Utaratibu wa kipindi
Hatua Shughuli ya ujifunzaji Muda
Utangulizi
Hatua ya 1
Wanafunzi wataje maamkuzi yoyote wanayofahamu. Dakika 3
Uwasilishaji
Hatua ya 2
Wanafunzi wawili wawili wajadiliane kuhusu jinsi
wanavyowaamkua watu katika nyakati mbalimbali.
Dakika 5
Hatua ya 3 Wanafunzi wakiwa katika vikundi wajadili michoro
iliyo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 21.
Dakika 5
Hatua ya 4 Wanafunzi wacheze mchezo wa kutambua maamkuzi
mbalimbali kwa kutumia kadi zilizoandikwa
maamkuzi.
Dakika 7
Hatua ya 5 Wanafunzi waigize maamkuzi mbalimbali
waliyojifunza.
Dakika 10
Hitimisho
Hatua ya Mwisho
Wanafunzi wataje maamkuzi waliyojifunza. Dakika 5
Kazi ya ziada
Waambie wanafunzi wataje maamkuzi ya nyakati mbalimbali yaliyojadiliwa darasani.
Mwanafunzi apewe kazi ya ziada ambapo atashirikiana na mzazi au mlezi wake kutaja
maamkuzi katika lugha yao ya kwanza. Watafsiri maamkuzi hayo katika Kiswahili.
xix
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini ya kipindi
Tumia maswali haya kutathmini jinsi kipindi kilivyoeleweka:
1. Ni maamkuzi gani yalitatiza baadhi ya wanafunzi wakati wa kipindi?
2. Je, wanafunzi waliweza kushiriki katika maigizo ya maamkuzi katika vikundi?
3. Je, nyenzo nilizokuwa nimetayarisha zilifaulisha kipindi?
4. Je, ni wapi ninahitaji kuboresha ili kipindi kieleweke kwa wanafunzi ili
washiriki katika shughuli mbalimbali kikamilifu?
3. Rekodi ya ufunzaji
Rekodi ya ufunzaji ni stakabadhi inayohifadhiwa na mwalimu kuonyesha kazi ambayo
imefanywa mwishoni mwa kila kipindi, mada au mada ndogo. Mwalimu mahususi
hujaza aliyofanya kila siku. Husaidia katika:
Uwajibikaji na uwazi wa kazi iliyofanywa na mwalimu.
Mwendelezo wa ufunzaji wa darasa.
Ili mwalimu mgeni ajue wapi pa kuanza kufundisha darasa.
Kutathmini maazimio ya kazi baada ya kipindi fulani.
Kuleta usawa wa ufunzaji wa mada mahali ambapo kuna madarasa kadha.
Rekodi ya ufunzaji huonyesha kufanikiwa kwa matokeo yaliyotarajiwa na
umilisi alioupata mwanafunzi. Rekodi hii inaweza kumwonyesha mwalimu iwapo
ufunzaji wake umefanikiwa kushughulikia mahitaji ya ujifunzaji wa wanafunzi binafsi.
Hutumika basi kama mwongozo wa mwalimu ili aweze kuwapa muda wanafunzi
binafsi kuhakikisha matokeo yaliyotarajiwa kama ilivyotajwa katika mfumo wa mtaala
yanadhihirishwa na wanafunzi wote.
Sehemu za Rekodi ya ufunzaji
a. Muda: Huonyesha tarehe na juma ambalo kazi ilishughulikiwa.
b. Kazi iliyofanywa: Mada na mada ndogo kama zilivyotolewa kwenye matokeo
yanayotarajiwa.
ch. Mawazo: Hii ni sehemu ya maoni inayoonyesha ufanisi na changamoto za somo
lile na mapendekezo.
d. Maelezo kuhusu mwalimu: Haya ni pamoja na jina, sahihi au ufupisho wa majina
ya mwalimu aliyehusika ili kuonyesha uwajibikaji. Utawala wa shule unapaswa kutia
sahihi rekodi ya ufunzaji mara kwa mara.
xx
Kimeidhinishwa na KICD
Kielelezo cha Rekodi ya ufunzaji
Shule: Juhudi
Somo: Kiswahili
Mwalimu: Ahadi Petero
Gredi: 4
Tarehe Juma Kazi iliyofanywa Mawazo Sahihi
8/2/2019
4
Kuandika
maamkuzi
ya nyakati
mbalimbali.
Malengo
ya kipindi
yalitimia.
4. Rekodi za maendeleo ya wanafunzi
Hizi zinaweza kuandaliwa kwa taratibu-elekezi. Taratibu-elekezi ni namna ya
kutathmini maendeleo ya mwanafunzi kwa vigezo vilivyoelezwa kwa kina. Taratibu-
elekezi huonyesha sehemu kadha muhimu wakati wa kukadiria kazi ya binafsi. Humpa
mwalimu chombo ambacho kinahakikisha kuwa ukadiriaji ni wa haki na unafanana
kwa wanafunzi wote.
Matokeo ya ujifunzaji yanahitaji mbinu tofauti za kutathmini. Utaratibu-elekezi ni
chombo kilichoandaliwa na mwalimu ambacho huonyesha matokeo yanayotarajiwa
ambayo hudhihirisha utendaji, viwango vya ufanisi na uelewa wa matokeo. Taratibu-
elekezi zanuiwa kukusaidia katika kupima matokeo, mchakato na maendeleo ya
ujifunzaji. Isitoshe, utaratibu-elekezi utamhusisha mwanafunzi katika kuunda na
kuelewa vigezo vya tathmini ambavyo vinawaruhusu kushiriki vilivyo katika mchakato
unaotakikana ili kukia lengo.
Amua kuhusu viwango, kwa mfano: Vizuri sana, vizuri, anaendelea, anahitaji msaada.
Mfumo wa mtaala umetumia kuzidi matarajio, kukia matarajio, kukaribia matarajio
na mbali na matarajio. Huu ni mfano wa taratibu-elekezi.
xxi
Kimeidhinishwa na KICD
Kielelezo cha Rekodi ya maendeleo ya mwanafunzi
Jina: Shaniko Rehema
Gredi ya 4 Mwaka 2019 Muhula 1 Umri: Miaka 10
Mada
Zilizofunzwa
Mbinu Ishara za kufaulu
Maamkuzi
ya nyakati
mbalimbali
Kuandika
insha ya wasifu
Kutaja maamkuzi. Mwanafunzi anaweza kutaja
maamkuzi ya nyakati zote.
Kufuata maagizo rahisi. Anaweza kufuata maagizo rahisi.
Kutunga sentensi rahisi. Anaweza kutunga sentensi rahisi.
Kutumia maamkuzi katika
mawasiliano.
Anaweza kutumia maamkuzi katika
mawasiliano.
Kuandaa vidokezo vya
insha ya wasifu.
Anaweza kuandaa vidokezo sahihi
vya insha ya wasifu.
Uwezo wa kuandika insha
ya wasifu.
Anaweza kuandika insha ya wasifu.
Hitimisho
Mwongozo huu wa mwalimu umeandikwa ili kukusaidia kuwaelekeza wanafunzi
kujifunza Kiswahili kwa njia ambayo inavutia na kusisimua zaidi. Unakumbushwa
kuamsha hamu ya wanafunzi unapofunza. Mambo ambayo unaweza kufanya kabla ya
kwenda darasani kufunza ni kama vile:
Kupitia matokeo yanayotarajiwa haya yatakusaidia kuongoza namna ya kufunza.
Pitia somo kabla ili kupata taswira ya yaliyomo yatakayoshughulikiwa.
Ujenge taswira akilini ya shughuli za ufunzaji na namna ambavyo utawasilisha
somo hilo.
Tangamana na wanafunzi unapozingatia shughuli zilizopendekezwa.
Kusanya vifaa vitakavyohitajika katika somo kabla ya somo lenyewe.
Jaribu viungio vilivyopendekezwa awali ili kuhakikisha kuwa vinafanya kazi.
Kumbuka: Shughuli za ujifunzaji ambazo zimependekezwa humu ni kielelezo tu.
Si lazima uzifuate zote. Uko huru kushirikisha mbinu nyingine za kiuvumbuzi za
ufunzaji ambazo zitasaidia kuwasilisha yaliyomo yaliyokusudiwa kwa ufanisi zaidi.
xxii
Kimeidhinishwa na KICD
1
Kimeidhinishwa na KICD
NYUMBANI
1
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1)
A. Kusikiliza na Kuzungumza: Matamshi bora
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua silabi zinazotokana na sauti zinazokaribiana katika maneno.
b) Kutamka silabi zinazotokana na sauti zinazokaribiana kimatamshi.
ch) Kutamka vitanzandimi vinavyoundwa kwa silabi za sauti ambazo zinakaribiana
kimatamshi.
d) Kuunda vitanzandimi kutokana na sauti zinazokaribiana kimatamshi.
Maswali dadisi
1. Ni silabi zipi zinazorudiwa katika vitanzandimi ulivyokariri?
2. Ni silabi zipi zinazorudiwa katika vitanzandimi ulivyounda?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
katika kusikiliza na kusoma maneno yenye silabi za sauti zinazokaribiana.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi na
kutunga vitanzandimi.
Ubunifu - unakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika kuunda vitanzandimi,
kujibu maswali, kutunga na kusimulia kisa kinachohusu vifaa na shughuli za
nyumbani.
Uwazaji wa kina na utatuzi wa matatizo - unakuzwa mwanafunzi anapowaza
kuhusu maneno atakayotumia kuunda vitanzandimi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia - unakuzwa mwanafunzi anapotangamana na wenzake darasani.
Stadi za maisha - kutokana na maudhui katika vitanzandimi, mwanafunzi
ataweza kukiria jinsi ya kutatua changamoto zinazomkabili darasani na katika
jamii.
Kujiamini na kujithamini - kunakuzwa mwanafunzi anapowasiliana na wenzake
katika vikundi na anapotunga sentensi zenye vitanzandimi.
2
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika vikundi.
Uaminifu - mwanafunzi anapotunga vitanzandimi binafsi bila kunakili vya
wenzake.
Mapenzi - mwanafunzi anapokubali kuelekezwa na wenzake na kufanya shughuli
katika kikundi bila ugomvi.
Uhusiano na masomo mengine
Muziki, Kiingereza, Lugha za kiasili kama vile Kiarabu - masomo haya
yanafunza sauti zinazokaribiana kimatamshi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anatarajiwa kukabiliana na masuala mbalimbali yanayohitaji uwazaji wa
kina katika jamii. Hasa anapotunga sentensi zinazohusu masuala hayo akitumia silabi
za sauti zinazokaribiana kimatamshi.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua na
kutamka silabi
zinazotokana
na sauti
zinazokaribiana
kimatamshi
katika maneno.
Mwanafunzi
anatambua na
kutamka kwa
usahihi na
urahisi silabi
zinazotokana
na sauti
zinazokaribiana
kimatamshi
katika maneno.
Mwanafunzi
anatambua na
kutamka kwa
usahihi silabi
zinazotokana
na sauti
zinazokaribiana
kimatamshi
katika maneno.
Mwanafunzi
anatambua
na kutamka
baadhi ya silabi
zinazotokana
na sauti
zinazokaribiana
kimatamshi
katika maneno.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua na
kutamka silabi
zinazotokana
na sauti
zinazokaribiana
kimatamshi
katika maneno.
Kukariri kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anakariri jumla
ya vitanzandimi
vinavyoundwa
kutokana na
silabi za sauti
lengwa kwa
ufasaha na kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anakariri jumla
ya vitanzandimi
vinavyoundwa
kutokana na
silabi za sauti
lengwa kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anakariri
vitanzandimi
vinavyoundwa
kutokana na
silabi za sauti
lengwa kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anajaribu
kukariri baadhi
ya vitanzandimi
vinavyoundwa
kutokana na
silabi za sauti
lengwa.
3
Kimeidhinishwa na KICD
Kuunda
vitanzandimi
vya sauti lengwa
vyenye maana.
Mwanafunzi
anaunda
vitanzandimi
vyenye maana,
vinavyotokana
na silabi za sauti
lengwa kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anaunda
vitanzandimi
vyenye maana
vinavyotokana
na silabi za sauti
lengwa.
Mwanafunzi
anaunda baadhi
ya vitanzandimi
vyenye maana
vinavyotokana
na silabi za sauti
lengwa.
Mwanafunzi
anajaribu
kuunda
vitanzandimi
vinavyotokana
na silabi za sauti
lengwa.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wenye uwezo wa kungamua wanayojifunza kwa urahisi, baada ya
kushirikishwa katika shughuli za ujifunzaji, wapewe fursa ya kubuni maneno zaidi.
Maneno yenye silabi za sauti zinazokaribiana kimatamshi.
Kwa upande mwingine, wanafunzi wanaochukua muda zaidi kabla ya kufahamu
wanayojifunza washirikishwe katika shughuli zaidi na wapewe muda zaidi.
Baadhi ya wanafunzi wanaweza kuwa na mahitaji ya kisaikolojia kutokana na
matukio wanayokumbana nayo katika familia au jamii. Mwalimu ayafahamu
mahitaji hayo ili awasaidie kujiamini na kuchangamkia ujifunzaji. Mwalimu
anaweza kumhusisha mzazi au mlezi katika kutatua changamoto hizo.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuongea au kusikia watambue silabi zinazotokana
na sauti zinazokaribiana kimatamshi katika maneno kwa kuzipigia mistari kwenye
mraba. Pia, wanaweza kuzikoleza rangi kwa kutumia tarakilishi.
Wale ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli au kusikiliza silabi zinazotokana
na sauti zinazokaribiana zikisomwa na mwalimu, wanafunzi wenzao au kutoka
kwenye kanda iliyorekodiwa.
Maelezo ya jumla
Mada ya matamshi bora inamwezesha mwanafunzi kutambua silabi zinazotokana na
sauti zinazokaribiana kimatamshi. Inachangia uboreshaji wa matamshi ya mwanafunzi
katika mawasiliano.
Kipindi cha 1: Silabi na vitanzandimi vyenye sauti /p/ na /b/
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua silabi zinazotokana na sauti zinazokaribiana /p/ na /b/ katika
maneno.
b) Kutamka silabi zinazotokana na sauti zinazokaribiana kimatamshi /p/ na /b/.
ch) Kushirikiana na wenzake katika kuunda vitanzandimi vyenye silabi za sauti /p/
na /b/.
4
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Je, unajua kutamka silabi zinazotokana na sauti /p/ na /b/?
2. Ni silabi zipi zinazorudiwa katika vitanzandimi ulivyounda?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vitanzandimi ni sentensi zinazoundwa kutokana na maneno yenye silabi zinazotokana
na sauti zinazokaribiana kimatamshi. Maneno hayo huitwa vitate. Mwanafunzi
anapotambua, kutamka na kuunda maneno yenye vitate kwa usahihi, ataboresha
matamshi yake katika mawasiliano.
Ili kufanikisha ujifunzaji wa vitanzandimi, mwalimu ajiandae vyema kabla ya kipindi.
Awe na nyenzo zinazofaa kumshirikisha kila mwanafunzi kulingana na mahitaji yake.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1,
2. Breli,
3. Kanda iliyorekodiwa matamshi ya sauti /p/ na /b/,
4. Chati yenye sentensi mbalimbali zenye maneno yenye sauti /p/ na /b/,
5. Mraba wenye vitate vya sauti /p/ na /b/ kwenye tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi watamke alfabeti
za Kiswahili. Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa
kuwauliza watamke silabi za sauti /p/ baada yake. Iwapo mwalimu ana changamoto
ya kutamka sauti /p/, anaweza kumwalika mwalimu mwingine au hata mwanafunzi
azitamke au arekodi sauti hizo zikitamkwa kwa usahihi kabla ya kipindi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kutambua silabi za sauti /p/ katika maneno ambayo
wamepewa. Kwa mfano, neno pasi (silabi ni pa), neno pewa (silabi ni pe), neno pika
(silabi ni pi), neno ponda (silabi ni po) na neno punda (silabi ni pu).
Mwalimu awaulize wanafunzi watambue silabi za sauti /p/ katika maneno ya sentensi
atakazoandika kwenye ubao. Mwalimu abuni sentensi zenye silabi za sauti /p/,
aziandike ubaoni kisha wanafunzi watambue silabi za sauti /p/.
Mifano ya sentensi za kuandika ubaoni: 1. Mama amenunua pazia mbili. 2. Mimi
nilipewa pesa za kununua pipi. 3. Pipa letu limejaa maji ya mvua. 4. Dada yangu
amepona. 5. Mgonjwa anapumua haraka.
Katika shughuli ya pili, mwalimu aandike silabi za sauti /b/ ubaoni, azitamke kisha
awaulize wanafunzi wazitamke baada yake. Awaongoze kutambua silabi za sauti /b/
katika maneno yaliyo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 1. Maneno hayo ni: baba
5
Kimeidhinishwa na KICD
(silabi ni ba), mkebe (silabi ni be), bilauri (silabi ni bi), boma (silabi ni bo) na sebule
(silabi ni bu). Awaelekeze kutambua silabi za sauti /b/ katika maneno ya sentensi
zilizo kwenye chati. Mwalimu ahakikishe ameandaa chati hii mapema kabla ya kipindi
hiki. Pia, anaweza kutunga sentensi hizo kwenye tarakilishi na kuzionyesha kwenye
projekta.
Mifano ya sentensi za kuandika kwenye chati: 1. Baba na babu walimchinja bata jana.
2. Bibi ameka barabarani. 3. Globu hii ina mwangaza mwingi. 4. Birika lenye chai
limeanguka. 5. Babu amenunua baiskeli mbili.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya tatu kutambua
majina ya michoro iliyo katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 2. Majina ya michoro
hiyo ni: punda na bunda la noti, pasi na basi. Mwalimu anaweza kuwa na kadi zenye
majina haya. Awaeleze wanafunzi kuwa maneno waliyotambua katika michoro hiyo
yana sauti /p/ na /b/. Sauti hizi mbili zinakaribiana kimatamshi. Maneno yenye sauti
zinazokaribiana kimatamshi huitwa vitate. Umoja wake ni kitate
Mwalimu awaongoze wanafunzi kusikiliza maneno yenye sauti /p/ na /b/ yakitajwa
kutoka kwenye rununu na kuwauliza wanafunzi wayatamke na kuyaandika maneno
hayo. Mwalimu anaweza kutumia kinasasauti au rununu kurekodi maneno hayo kabla
ya kipindi. Iwapo mwalimu ana matatizo ya kimatamshi, anaweza kumhusisha mgeni
mwalikwa mwenye matamshi bora. Mgeni mwalikwa anaweza kuwa mwanafunzi wa
darasa jingine, mwalimu mwenzake au mtu yeyote mahiri katika utamkaji.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya nne kutambua vitate vya sauti /p/
na /b/ kutoka kwenye mraba waliopewa katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 2.
Wanafunzi washiriki katika shughuli hii wakiwa katika vikundi. Mwalimu awagawe
wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Vitate tarajiwa kutoka kwa mraba ni: punda/bunda (la noti), pasi/basi, pata/bata na
pipi/bibi. Mwalimu awaulize wanafunzi watumie vitate walivyotambua kutoka kwenye
mraba kutunga sentensi sahihi. Wanafunzi wasikilizane wakikariri kwa zamu na kwa
haraka sentensi walizotunga.
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa sentensi walizotunga huitwa vitanzandimi.
Wanafunzi wapewe kazi ya ziada. Waifanye kazi hiyo wakielekezwa na walezi au
wazazi wao kisha wajadiliane kuihusu katika kipindi kitakachofuata. Wajadiliane
kuhusu umuhimu wa vitanzandimi.
Majibu tarajiwa kuhusu umuhimu wa vitanzandimi:
1. Vitanzandimi husaidia katika uboreshaji wa matamshi na hatimaye huimarisha
mawasiliano.
2. Ujifunzaji wa vitanzandimi humfanya mwanafunzi achangamkie ujifunzaji ambapo
anajimudu katika kukariri vitanzandimi.
Mwalimu akubali jibu lolote sahihi ambalo linaeleza umuhimu wa vitanzandimi.
6
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu asikilize na kutathmini ikiwa mwanafunzi anaweza kutamka alfabeti
za Kiswahili kwa usahihi.
2. Asikilize na kutathmini ikiwa mwanafunzi anatamka silabi za sauti /p/ na /b/
kwa usahihi. Ikiwa anaweza kutambua silabi za sauti /p/ na /b/ katika maneno.
3. Asikilize mwanafunzi akisoma na kukariri vitanzandimi vya silabi za sauti /p/
na /b/ kwa sauti na kwa haraka.
Kipindi cha 2: Silabi na vitanzandimi vyenye sauti /t/ na /d/
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 3)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua silabi zinazotokana na sauti /t/ na /d/.
b) Kutamka silabi zinazotokana na sauti /t/ na /d/.
ch) Kutumia vitanzandimi vya sauti /t/ na /d/ kwa usahihi katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Je, unajua kutamka silabi zinazotokana na sauti /t/ na /d/?
2. Ni silabi zipi zilizorudiwa katika vitanzandimi ulivyokariri?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua, kutamka na kuunda maneno yenye silabi za sauti /t/ na /d/
ataboresha matamshi yake katika mawasiliano.
Mwalimu anaweza kubuni shughuli za ujifunzaji tofauti na zile za kipindi cha awali ili
kukuza hamu ya kujifunza zaidi kwa wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kanda ya vitanzandimi vyenye sauti /t/ na /d/ vilivyorekodiwa,
2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 3,
3. Breli,
4. Rununu au tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi waeleze
maana ya vitate au wataje vitanzandimi walivyojifunza katika kipindi kilichotangulia.
Wanafunzi wanapotaja vitanzandimi walivyojifunza awali, wanaweza kukumbuka
maelezo ya kipindi hicho na kuweza kutambua wanayojifunza katika kipindi hiki kwa
urahisi.
7
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kutamka silabi
za sauti /t/ kisha awaulize wanafunzi wazitamke baada yake. Awaelekeze wanafunzi
kutambua silabi za sauti /t/ katika maneno yaliyo kwenye kitabu chao. Maneno hayo
ni kitanda (silabi ni ta), uteo (silabi ni te), koti (silabi ni ti), tonge (silabi ni to) na
tunda (silabi ni tu). Mwalimu awaulize wanafunzi watambue silabi za sauti /t/ katika
maneno ya sentensi ambazo atawaonyesha kwenye tarakilishi yake. Mwalimu awe
ametunga sentensi hizi kabla ya kipindi hiki na kuziandika katika tarakilishi ambayo
atawaonyesha wanafunzi. Iwapo mwalimu hana uwezo wa kutumia tarakilishi, anaweza
kuziandika sentensi hizo ubaoni au kwenye chati.
Mifano ya sentensi: 1. Kiti cha nyanya kimevunjika. 2. Baba atanunua matunda mawili.
3. Taa ya jikoni imezimwa. 4. Mlinzi anatumia tochi kubwa.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kutamka silabi za sauti
/d/ kisha awaulize wanafunzi wazitamke baada yake.
Awaelekeze wanafunzi kutambua silabi za sauti /d/ katika maneno yaliyo kwenye
kitabu chao. Maneno hayo ni: seredani (silabi ni da), debe (silabi ni de), dirisha (silabi
ni di), donge (silabi ni do), mdudu (silabi ni du).
Mwalimu awaulize wanafunzi watambue silabi za sauti /d/ katika maneno ya sentensi
atakazoandika ubaoni.
Mifano ya sentensi: 1. Dada ametumwa dukani. 2. Babu anameza dawa ya homa. 3.
Dereva anaendesha gari polepole. 4. Rubani anatumia dira. 5. Dari yetu imepakwa
rangi nzuri.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya tatu. Awagawe katika vikundi
kulingana na idadi na mahitaji yao. Wanafunzi wasome kwa usahihi sentensi zilizo
katika Kitabu cha Mwanafunzi ukurasa 4. Mwalimu amwombe mwanafunzi mmoja
awarekodi wenzake wakisoma sentensi hizo. Anaweza kutumia tarakilishi au rununu
ya mwalimu.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kusikiliza na kutamka kwa haraka na kwa usahihi
sentensi zilizorekodiwa. Wanafunzi waunde vitanzandimi vyao wenyewe wakitumia
maneno yenye sauti /t/ na /d/. Wavikariri vitanzandimi hivyo kwa haraka.
Tathmini
1. Mwalimu asikilize iwapo mwanafunzi anaweza kutamka silabi za sauti /t/ na
/d/.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutambua silabi za sauti /t/ na
/d/ katika maneno na sentensi.
3. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutunga sentensi akitumia jozi
za vitate vya sauti /t/ na /d/.
4. Mwalimu atathmini matamshi ya mwanafunzi anapokariri kwa haraka
vitanzandimi vilivyorekodiwa kwenye rununu.
8
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 3: Silabi na vitanzandimi vyenye sauti /k/ na /g/
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 4)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua silabi zinazotokana na sauti /k/ na /g/.
b) Kutamka silabi zinazotokana na sauti /k/ na /g/.
ch) Kuunda vitanzandimi vya sauti /k/ na /g/.
Maswali dadisi
1. Je, unaweza kutamka sauti /k/ na /g/ kwa ufasaha?
2. Ni silabi zipi zilizorudiwa katika vitanzandimi ulivyokariri?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu amshauri mwanafunzi awafunze wenzake shuleni na hata nyumbani
vitanzandimi alivyojifunza ili kuimarisha matamshi yake katika mawasiliano katika
jamii.
Stadi za maisha kama vile uwezo wa kujieleza kwa ukakamavu na ufasaha hukuzwa
mwanafunzi anapozoea kujieleza katika vikundi darasani. Mwalimu awagawe
wanafunzi katika vikundi akizingatia idadi ya wanafunzi, jinsia na mahitaji yao
mbalimbali.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kanda iliyorekodiwa vitanzandimi vyenye sauti /k/ na /g/,
2. Chati yenye sentensi za maneno yenye sauti /k/ na /g/,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 4,
4. Mgeni mwalikwa, 5. Breli, 6. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wakariri
vitanzandimi walivyojifunza katika vipindi vilivyotangulia.
Mwalimu awapange wanafunzi katika vikundi na awahusishe katika shughuli ya
kwanza kwa kuwauliza watamke silabi ka, ke, ki, ko, ku.
Awaongoze wanafunzi kutambua silabi za sauti /k/ katika maneno yaliyo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 4. Maneno hayo ni kabati (silabi ni ka), keti (silabi ni
ke), kinu (silabi ni ki), kochi (silabi ni ko) na kufuli (silabi ni ku).
9
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua silabi za sauti /k/ katika maneno ya sentensi
atakazoandika kwenye ubao. Pia, mwalimu anaweza kuziandika sentensi hizo kwenye
chati kabla ya kipindi hiki.
Mifano ya sentensi: 1. Kanisa letu litajengwa. 2. Kelbu wenu anabweka kwa sauti.
3. Kikombe cha mtoto kimejaa maji. 4. Kunguni ni wadudu hatari.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kuwauliza watamke
silabi ga, ge, gi, go, gu. Awaulize watambue silabi za sauti /g/ katika maneno yaliyo
katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 4. Maneno hayo ni gawa (silabi ni ga), gesi
(silabi ni ge), ufagio (silabi ni gi), goti (silabi ni go) na gunia (silabi ni gu). Baadaye,
mwalimu awaongoze wanafunzi watambue silabi za sauti /g/ katika maneno ya sentensi
atakazoandika kwenye ubao. Mwalimu anaweza kutunga sentensi hizi kabla ya kipindi
hiki kisha akaziandika kwenye chati ambayo atawaonyesha wanafunzi darasani.
Mifano ya sentensi: 1. Nitarudi nyumbani kabla giza liingie. 2. Mchezaji yule anapiga
ngoma vizuri. 3. Unapenda kuvaa nguo gani? 4. Raki yangu aliumia kwenye goti.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya tatu kwa kutamka maneno yaliyo
kwenye jedwali kisha wakatamka baada yake. Ahakikishe kila mwanafunzi anatamka
kwa ufasaha na usahihi. Mwalimu amteue mwanafunzi mmoja ayarekodi matamshi
ya wanafunzi wengine kwa kutumia tarakilishi au rekoda. Wanafunzi washiriki katika
kuunda vitanzandimi vyenye sauti /k/ na /g/ kwa kutumia maneno yaliyorekodiwa.
Kila mwanafunzi ashiriki katika kukariri kwa zamu na kwa haraka vitanzandimi
vilivyoundwa.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi katika kufanya kazi ya ziada ambapo atahitajika
kumkariria mlezi au mzazi wake vitanzandimi vitano alivyojifunza shuleni. Pia,
amwombe mlezi au mzazi wake atumie rununu au tarakilishi kumrekodi akivikariri
vitanzandimi hivyo. Pia, mwanafunzi anaweza kutumia kinasasauti ama rekoda
kujirekodi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini ikiwa mwanafunzi anaweza kutamka silabi za sauti /k/ na
/g/ na kuzitambua katika maneno na sentensi.
2. Mwalimu asikilize mwanafunzi akikariri vitanzandimi kwa ufasaha na usahihi.
Kipindi cha 4: Silabi na vitanzandimi vyenye sauti /ch/ na /j/
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 5)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua silabi zinazotokana na sauti /ch/ na /j/.
b) Kukariri vitanzandimi vyenye silabi zinazotokana na sauti /ch/ na /j/.
ch) Kuunda vitanzandimi sahihi vinavyotokana na silabi za sauti /ch/ na /j/.
10
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Je, unaweza kutamka sauti /ch/ na /j/ kwa ufasaha?
2. Ni silabi zipi zinazorudiwa katika vitanzandimi ulivyounda?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu ajiandae kabla ya kipindi hiki ili aweze kuwa na nyenzo zitakazomwezesha
kuimarisha shughuli za ujifunzaji. Awaandalie wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
shughuli zinazowafaa ili waakie matarajio ya kipindi.
Mwanafunzi anapochangamkia kukariri vitanzandimi vinavyoundwa kwa silabi za
sauti lengwa huboresha matamshi yake katika mawasiliano.
Ikiwa mwalimu ana changamoto ya kutamka silabi hizo, amwalike mgeni ambaye
atazitamka sauti lengwa. Mgeni anaweza kuwa mwalimu mwingine au mtaalamu wa
lugha ya Kiswahili au hata mwanafunzi mahiri katika utamkaji. Mwalimu ahakikishe
kuwa mgeni anaweza kutamka silabi za sauti /ch na /j/ kwa ufasaha kabla ya kumwalika.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 5,
2. Chati yenye maneno ya silabi za sauti /ch/ na /j/,
3. Kanda iliyorekodiwa vitate vya sauti /ch/ na /j/,
4. Jedwali la maneno, 5. Breli, 6. Mgeni mwalikwa.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wakariri
vitanzandimi wanavyovijua.
Awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwauliza wasikilize
akizitamka silabi za sauti /ch/ kisha wazitamke. Awaongoze wanafunzi kutambua
silabi za sauti /ch/ katika maneno waliyopewa vitabuni mwao. Maneno hayo ni:
chakula (silabi ni cha), cherehani (silabi ni che), chiriku (silabi ni chi), choo (silabi ni
cho), chumba (silabi ni chu). Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua maneno yenye
silabi za sauti /ch/ katika sentensi atakazoziandika ubaoni.
Mifano ya sentensi: 1. Chungu cha nyanya kimejaa maharagwe. 2. Mimi ninachana
nywele zangu. 3. Mtoto amekula chakula chote. 4. Kuku atachinjwa leo jioni. 5. Baba
alijiunga katika chama cha wazee kijijini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kutamka silabi za sauti
/j/ na kuwaomba watamke baada yake. Awaongoze wanafunzi kutambua silabi za sauti
/j/ katika maneno yaliyo vitabuni mwao. Maneno hayo ni: jagi (silabi ni ja), jembe
(silabi ni je), jiko (silabi ni ji), jokofu (silabi ni jo), jua (silabi ni ju). Baadaye, mwalimu
11
Kimeidhinishwa na KICD
awashirikishe wanafunzi katika kutambua maneno yenye sauti /j/ katika sentensi
atakazotunga na kuziandika ubaoni. Mwalimu anaweza kutunga sentensi kabla ya
kipindi hiki na kuziandika kwenye chati atakayowaonyesha wanafunzi. Pia, mwalimu
anaweza kuwaomba wanafunzi watunge sentensi zenye sauti /j/ kisha akaziandika
ubaoni ili wanafunzi wengine wajifunze sauti lengwa.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaagize wanafunzi wasome vitate vilivyo kwenye
jedwali katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 6. Wanafunzi wasome vitate hivyo
wenzao wakiwasikiliza. Makosa ya kimatamshi yakosolewe. Mwanafunzi mmoja
ayarekodi matamshi ya wanafunzi wengine kwa kutumia rununu ya mwalimu. Wanafunzi
wakosoe makosa ya kimatamshi kutoka kwa rekodi hiyo.
Mwalimu awapange wanafunzi katika vikundi na kuwaelekeza kuunda vitanzandimi
ubaoni wakitumia maneno yaliyorekodiwa. Baadaye, wanafunzi washiriki katika
kusoma vitanzandimi walivyounda kwa sauti na kwa haraka. Baadhi ya vitanzandimi
tarajiwa ni: 1. Chungu ameingia kwenye jungu. 2. Chuma kilipatikana kwenye chumba
cha jumba hilo juma lililopita. 3. Mtoto mwenye kucha ndefu alikuja kwetu.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada ambapo watahitajika
kuwakariria walezi au wazazi wao vitanzandimi walivyojifunza. Wanafunzi wakariri
vitanzandimi hivyo pamoja na walezi au wazazi wao.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutamka silabi za sauti /ch/ na
/j/ na kuzitambua katika maneno na sentensi.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuunda vitanzandimi
akitumia silabi au maneno yenye sauti /ch/ na /j/.
B. Kusoma: Kusoma kwa ufahamu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 7
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa mada lengwa uliotumika katika kifungu cha hadithi ili
kuimarisha ufahamu.
b) Kutumia msamiati lengwa kwa usahihi katika sentensi.
ch) Kusoma kifungu cha hadithi kwa ufasaha.
d) Kuonyesha uelewa wa kifungu kwa kutoa muhtasari na kujibu maswali.
e) Kujenga mazoea ya usomaji bora katika maisha ya kila siku.
12
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Ni vifaa vipi vya nyumbani unavyovijua?
2. Je, unajua matumizi ya vifaa vipi vya nyumbani?
3. Vifungu vya kusoma vina umuhimu gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - huu unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
kusoma maneno.
Kujiamini na kujithamini - umilisi huu unakuzwa mwanafunzi anapowasiliana
na wenzake katika vikundi.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi akitumia msamiati
husika.
Uhusiano na masuala mtambuko
Kujitambua na kujitathmini anapotunga sentensi akitumia msamiati lengwa.
Uraia - unakuzwa mwanafunzi anapotangamana na wenzake darasani.
Stadi za maisha mwanafunzi ataweza kuzoea kuwaza ili kupata suluhisho la
changamoto baada ya kuzoea kujibu maswali dadisi katika ufahamu.
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika vikundi.
Uaminifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi mwenyewe kwa
kutumia msamiati lengwa bila kunakili za wenzake.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza, Kiarabu na Lugha za kiasili - masomo haya yana stadi ya kusoma.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wanafunzi wenzake shuleni na nyumbani katika kusoma
na kutambua msamiati wa nyumbani.
13
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
msamiati
lengwa katika
kifungu.
Mwanafunzi
anatambua
msamiati
lengwa kwenye
kifungu
alichosomewa
kwa urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
msamiati
lengwa katika
kifungu
alichosomewa.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
msamiati
lengwa kwenye
kifungu
alichosomewa.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
msamiati
lengwa kwenye
kifungu
alichosomewa.
Kueleza maana
na kutumia
msamiati
lengwa kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya msamiati
lengwa na
kuutumia kwa
ufasaha na
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya msamiati
lengwa na
kuutumia kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya baadhi
ya msamiati
lengwa na
kuutumia kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza maana
ya baadhi
ya msamiati
lengwa.
Kusoma kifungu
cha hadithi
kwa kuzingatia
ujumbe na kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anasoma kwa
ufasaha na
urahisi kwa
kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma kwa
ufasaha na
kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anajaribu
kusoma sehemu
za kifungu.
Kujibu maswali
ya ufahamu na
kutoa muhtasari
wa kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajibu maswali
ya ufahamu na
kutoa muhtasari
wa kifungu
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anajibu maswali
ya ufahamu na
kutoa muhtasari
wa kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajibu baadhi
ya maswali ya
ufahamu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kujibu baadhi
ya maswali ya
ufahamu.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuongea au kusikiliza, watambue maana ya msamiati
lengwa kwa kuandika na kuambatanisha neno na maana yake katika jedwali.
Wale ambao hawana uwezo wa kuona watumie breli au wasikilize maana ya
msamiati husika mwalimu na wenzao wanapoeleza.
Maelezo ya jumla
Mada ya kusoma ufahamu itamwezesha mwanafunzi kutambua maana ya msamiati
husika na kuweza kuutumia katika mawasiliano.
Kusoma ufahamu kutakuza hamu ya mwanafunzi ya kujifunza zaidi ili kuyafahamu
14
Kimeidhinishwa na KICD
maudhui mbalimbali katika vifungu mbalimbali vya fahamu.
Mwalimu ahimize kusoma kwa vifungu ndani na nje ya darasa ili kukuza stadi ya
usomaji ambayo humpa mwanafunzi maarifa zaidi.
Kipindi cha 1: Msamiati wa nyumbani
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 7)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa nyumbani.
b) Kutumia msamiati wa nyumbani kwa usahihi katika sentensi.
ch) Kutambua matumizi ya msamiati wa nyumbani.
Swali dadisi
Ni vifaa vipi vya nyumbani unavyovijua?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua msamiati wa nyumbani na kuutumia kwa usahihi katika
sentensi huboresha mawasiliano yake. Mwanafunzi pia huweza kufahamu mazingira
yake akiwa nyumbani.
Mwalimu aandae kadi zenye majina ya vifaa mbalimbali vya nyumbani kabla ya
kipindi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Tarakilishi, 3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 7,
4. Kadi zenye msamiati wa nyumbani.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wataje vifaa
mbalimbali ambavyo vinapatikana nyumbani.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na mahitaji yao kisha awaulize watazame michoro iliyo kitabuni mwao.
Wanafunzi wajadiliane kuhusu vifaa katika michoro hiyo na waeleze vinakopatikana
nyumbani. Majibu tarajiwa: Vitu hivi hupatikana jikoni, sebuleni na katika chumba
cha kulala. Mwalimu akubali majibu yoyote ambayo ni sahihi kwa kurejelea michoro
husika. Pia, wanafunzi wajadiliane kuhusu matumizi ya vifaa watakavyotaja. Wanafunzi
wawatajie wenzao vitu vinavyopatikana nyumbani kwao na namna wanavyovitumia
vitu hivyo.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kueleza kuhusu usalama wao wanapovitumia vifaa
vya nyumbani na jinsi wanavyofaa kuvitunza ili kuzuia gharama ya kununua vingine.
15
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awahusishe wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kuwaongoza kucheza
mchezo wa kadi zenye majina ya vifaa mbalimbali vya nyumbani. Amwulize
mwanafunzi mmoja achukue kadi kutoka kikapuni, asome jina la kifaa lililoandikwa
kwenye kadi hiyo kwa sauti kisha awaulize wenzake waeleze matumizi ya kifaa hicho.
Mwalimu ahakikishe wanafunzi wote wanashiriki katika kueleza matumizi ya kila
kifaa walichotaja.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi kutafuta michoro ya vifaa
ambavyo vimeorodheshwa katika Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 7 kwa kutumia
mtandao. Wavichore vifaa hivyo kwenye madaari yao na kueleza matumizi ya kila
kifaa walichochora. Pia, watunge sentensi sahihi wakitumia majina ya vifaa hivyo.
Iwapo mwanafunzi ana changamoto ya kutumia tarakilishi, mwalimu ampe mazoezi
zaidi ili aimarishe umilisi wa kidijitali na kuweza kufanya mazoezi yajayo kwa usahihi
na upesi. Pia, mwalimu anaweza kutumia wanafunzi wanaofahamu kutumia tarakilishi
bila changamoto kuwafunza au kuwakumbusha wenzao jinsi ya kutumia tarakilishi
kutekeleza shughuli hiyo.
Mwalimu amhimize kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kutaja vifaa vya jikoni
vinavyopatikana nyumbani kwao pamoja na matumizi ya kila kifaa. Kila mwanafunzi
atawasomea wanafunzi wenzake aliyoandika darasani katika kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua msamiati wa
nyumbani.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutumia msamiati wa
nyumbani katika sentensi kwa ufasaha na usahihi.
Kipindi cha 2: Kifungu cha hadithi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 8)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusoma kifungu cha hadithi kwa ufasaha.
b) Kutambua msamiati wa nyumbani uliotumika katika kifungu cha hadithi ili
kuimarisha ufahamu.
ch) Kuonyesha uelewa wa kifungu kwa kutoa muhtasari na kujibu maswali.
Swali dadisi
Vifungu vya kusoma vina umuhimu gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vifungu vya kusoma humsaidia mwanafunzi kukuza uelewa wa misamiati mbalimbali
ili kuitumia katika kuimarisha mawasiliano.
Vifungu vya hadithi pia humfahamisha mwanafunzi matukio yanayotokea katika
16
Kimeidhinishwa na KICD
mazingira mbalimbali na humwezesha kujitambua na kuthamini mazingira yake na
ya watu wengine.
Vifungu vya hadithi hukuza ubunifu wa mwanafunzi na humpa hamu ya kujifunza
zaidi hasa anaposoma visa vinavyosisimua.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 8, 2. Breli, 3. Tarakilishi,
4. Kadi zenye maagizo yanayohusiana na vitendo vya nyumbani,
5. Vikapu vya maneno.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi waeleze
waliyojifunza katika kipindi kilichotangulia.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi vya
wanafunzi wawili wawili. Watazame na kujadili mchoro ulio kitabuni mwao na kueleza
vitendo vinavyoendelea katika mchoro huo. Baadhi ya majibu tarajiwa: Bawabu
analinda nyumbani, mwanamume anampa ng’ombe chakula, msichana ananyunyizia
mimea maji. Mwalimu akubali majibu yoyote sahihi kulingana na mchoro husika.
Wanafunzi waelezane kuhusu kazi ambazo wao hufanya nyumbani ili kuwasaidia
wazazi au walezi wao.
Mwalimu amwulize mwanafunzi mmoja asome ufahamu kuhusu Nyumbani Kwetu
kwa sauti huku wanafunzi wengine wakimsikiliza kwa makini katika shughuli ya pili.
Wanafunzi wote darasani wasome tena ufahamu huo kwa sauti. Mwalimu ahakikishe
matumizi ya matamshi sahihi. Mwalimu awaelekeze wanafunzi wawili wawili kujibu
maswali waliyopewa baada ya kifungu hicho. Baadaye, wanafunzi waandike muhtasari
wa kifungu hicho.
Mifano ya majibu tarajiwa ya maswali ya kifungu kilichosomwa ni: (a) Watu huishi
kwenye nyumba ili kujisitiri kutokana na baridi au jua kali. (b) Sebule hutumika
kupumzikia au kuwakaribishia wageni. (ch) Baadhi ya vifaa vilivyotajwa katika kifungu
ni: seredani (hutumiwa kupikia), mchi (hutumiwa pamoja na kinu kutwangia nafaka),
ungo (kupepetea nafaka), makochi (kukalia) n.k. Mwalimu akubali majibu yoyote
sahihi. (d) Watu hutumia chumba hiki kuoga au kufua nguo ili kudumisha usa. (e)
Wanafunzi waeleze maana za maneno yaliyokolezwa rangi katika kifungu. Wanaweza
kutumia kamusi. (f) Wanafunzi waandike muhtasari wa kifungu walichosoma.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona wasikilize kifungu kutoka kwenye kanda
iliyorekodiwa au wasome kifungu kwa kutumia breli. Wanafunzi wasioweza kusikia,
wajibu maswali ya kisa kwa kuandika au kutumia lugha ishara ikiwa wenzake na
mwalimu wanaifahamu.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi wacheze mchezo wa kufumba na kufumbua katika
17
Kimeidhinishwa na KICD
shughuli ya tatu. Mwanafunzi mmoja mmoja afumbe macho kisha achukue kadi
moja kutoka kwenye kikapu. Afumbue macho na kuzingatia maelezo atakayosoma
kwenye kadi. Kadi hizo ziwe na vitendo mbalimbali vinavyotendwa nyumbani kama
vile: piga deki, pika, fagia, tandika kitanda, fyeka nyasi, okota takataka, oga, fua
nguo n.k. Mwalimu asahihishe majibu ya wanafunzi kulingana na maagizo ya kadi
atakayochukua. Mwalimu aandae kadi hizo kabla ya kipindi.
Mwalimu amwagize kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada kwa kutumia mtandao
kutafuta picha za vifaa alivyopewa katika kitabu chao. Mwanafunzi ahakikishe anaeleza
matumizi ya kila kifaa atakachotafuta mtandaoni. Awaeleze wanafunzi wenzake
matumizi hayo darasani katika kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua vitendo vinavyotendwa
nyumbani.
2. Mwalimu asikilize na atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kusoma kifungu na
kujibu maswali kwa ufasaha.
CH. Kuandika: Kuandika insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 10)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya wasifu kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya wasifu kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
ch) Kuchangamkia utunzi mzuri wa insha ya wasifu ili kujenga ubunifu wake.
d) Kutambua maana ya wasifu.
Maswali dadisi
1. Je, unajua maana ya wasifu?
2. Je, unazingatia mambo gani unapoandika insha ya wasifu?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - huu unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
kuandika na kusambaza insha zao mtandaoni na kurejelea kielelezo cha insha
ya wasifu.
Kujiamini na kujithamini - umilisi huu unakuzwa mwanafunzi anapowasiliana
na wenzake katika vikundi.
18
Kimeidhinishwa na KICD
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi
na anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi na vyombo vingine vya
kiteknolojia.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya wasifu.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia - unakuzwa mwanafunzi anapotangamana na wenzake darasani.
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika vikundi.
Uwajibikaji - mwanafunzi anapoandika insha mwenyewe.
Upendo - mwanafunzi anapowasiliana vyema na wenzake katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia stadi ya
kuandika.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi bora katika mawasiliano.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi matarajio Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kueleza maana
ya insha ya
wasifu na
kutaja mambo
anayozingatia
anapoiandika.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya insha ya wasifu
na kutaja mambo
anayozingatia
kuiandika kwa
ufasaha na urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya insha ya
wasifu na
kutaja mambo
anayozingatia
kuiandika kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anaeleza
maana ya insha
ya wasifu na
kutaja mambo
anayozingatia
kuiandika.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza maana
ya insha ya
wasifu na
kutaja mambo
anayozingatia
kuiandika.
Kuandika insha
ya wasifu kwa
kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio
mzuri wa
mawazo na
lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya wasifu kwa
kuzingatia kanuni
za lugha, mpangilio
mzuri wa mawazo
na kwa ubunifu wa
hali ya juu.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya wasifu
kwa kuzingatia
lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya wasifu
kwa kuzingatia
baadhi ya
kanuni za
lugha.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika insha
ya wasifu.
19
Kimeidhinishwa na KICD
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona watumie breli kusoma maana ya insha
ya wasifu na maelezo kuhusu mambo ya kuzingatia wanapoiandika. Pia, wanafunzi
wenzao wanaweza kuwasaidia kusoma maelezo hayo.
Wanafunzi wenye mahitaji ya kiafya yanayochangia kutozingatia kanuni bora za
uandishi wapewe mazoezi ya kutosha kabla ya kuandika insha. Mazoezi hayo ni
kama vile kupanga sentensi zilizotarakanywa katika aya ili kuboresha mtiririko wa
mawazo. Wasioweza kuandika heru za Kiswahili vizuri wahusishwe katika mazoezi
ya kunyanga heru hizo, kuzipaka rangi zikiwa kwenye chati na kuzifuma kwa
kutumia uzi. Wale wenye changamoto ya kutumia mkono kuandika wapewe muda
zaidi wa kuandika insha.
Maelezo ya jumla
Mada ya kuandika itamwezesha mwanafunzi kukuza ubunifu wake, kufahamu kanuni
za uandishi bora ili kuimarisha mawasiliano yake.
Kipindi cha 1: Maana ya wasifu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 10)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kufahamu maana ya wasifu.
b) Kueleza sifa za vitu na viumbe mbalimbali.
Swali dadisi
Je, wasifu ni nini?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapochangamkia utunzi wa insha ya wasifu hujenga ubunifu wake na
kuweza kuandika insha za kusisimua.
Mwalimu amhusishe mwanafunzi katika shughuli mbalimbali zitakazomwezesha
kuwa mwandishi bora. Ampongeze kwa kila hatua anayopiga katika uandishi ili
aendelee kujithamini.
Mwanafunzi awe na vifaa vyote anavyohitaji katika kujifunza kuandika insha.
Mwalimu ahakikishe ana nyenzo zote za ujifundishaji kabla ya kipindi. Avikague vifaa
vya kiteknolojia kabla ya kipindi ili kuhakikisha vitatumiwa bila changamoto.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa10, 2. Breli,
3. Chati za kuandika aya za wasifu, 4. Tarakilishi.
20
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwaongoza
kueleza sifa za raki zao katika vikundi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kujadili sifa za mchoro ulio
katika kitabu chao wakiwa katika vikundi. Mchoro ulio kitabuni mwao ni wa ngombe.
Mwalimu akubali majibu yoyote kumhusu ng’ombe aliye kwenye mchoro husika.
Mwalimu awahusishe wanafunzi katika shughuli ya tatu kwa kuwaongoza kutafuta
picha za meza, kitanda na jokofu mtandaoni na kueleza sifa za kila picha. Baadaye,
wanafunzi waelekezwe kuandika maelezo ya picha hizo katika madaari yao. Mwalimu
anaweza kuwapa wanafunzi majina ya viumbe na vifaa vingine ili waandike sifa zao
kulingana na mazingira yao.
Awaeleze wanafunzi kuwa kueleza sifa za mtu, kitu, mnyama au jambo ni sawa na
kueleza wasifu wake. Kuandika insha ya wasifu ni kuandika kifungu cha sifa. Ataje
kuwa mambo yanayozingatiwa mtu anapoandika insha ni: 1. Lazima kuwe na mada ya
insha. 2. Mpangilio wa sentensi ufuatane kwa usahihi. 3. Lazima lugha sahihi na sanifu
itumiwe 4. Mwandiko usomeke kwa urahisi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika vikundi kufanya kazi ya ziada kwa wakati wao.
Wanafunzi waandike aya moja kuhusu darasa lao kwenye chati kisha wazibandike
chati hizo ukutani darasani.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kueleza na kuandika sifa za kitu
au kiumbe kwa usahihi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuandika aya ya insha ya wasifu
kwa kuzingatia ujumbe, sentensi sahihi na usanifu.
Kipindi cha 2: Muundo wa insha ya wasifu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika insha ya wasifu kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
b) Kufahamu utunzi mzuri wa insha ya wasifu ili kujenga ubunifu wake.
Maswali dadisi
1. Je, unazingatia mambo yapi unapoandika insha ya wasifu?
2. Je, unafahamu muundo wa kuandika insha ya wasifu?
21
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awe amesoma Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11 kabla ya kipindi hiki ili
kujifahamisha yaliyomo.
Mwalimu arekodi maelezo kuhusu uandishi wa insha ya wasifu ili kuwafaa wanafunzi
wasioweza kuona maandishi ubaoni. Anaweza kumhusisha mwalimu mwingine kutoa
maelezo hayo ikiwa yeye ana changamoto ya matamshi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 11, 2. Breli,
3. Kielelezo cha insha ya wasifu.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje mambo
wanayofaa kuzingatia wanapoandika insha ya wasifu.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi kusoma insha ya wasifu
atakayowapa. Baada ya kusoma, wanafunzi wajadili muundo wa insha hiyo.
Mfano wa insha ambayo mwalimu atawapa wanafunzi.
Baba Yangu
Baba yangu anaitwa Bwana Baraka.Yeye ni mrefu na mwembamba. Nywele zake
ni fupi na nyeusi tititi. Anapenda kutabasamu sana.Yeye ni mtu mchangamfu mno.
Baba huvaa suti anapoenda kazini.Yeye ni mkurugenzi wa kampuni yake ambayo
hutengeneza fanicha mjini Tangaza. Kabla ya kuanzisha kampuni hiyo, baba
alikuwa ameajiriwa katika karakana mbalimbali kufanya kazi ya useremala.
Baba ni mtu mwenye bidii sana. Hapendi uvivu. Kila siku yeye huniambia kuwa
uvivu haufai. Ukija nyumbani kwetu utapata nyumba kubwa ambayo baba
alijenga. Pia, alitengeneza vifaa vya thamani kama vile makochi, meza na kabati
ambavyo hupatikana sebuleni mwetu.
Baba anapenda watoto watiifu.Yeye husema kuwa mtoto mtiifu hufanya vizuri
katika masomo yake. Yeye pia anapenda usa. Huwezi kukaa karibu na baba ukiwa
mchafu. Anaamini kuwa usa wa mwili na mazingira ni muhimu kwa afya ya
kila mwanadamu. Baba huosha matunda kabla ya kuyala. Anapotumia vyombo
vya jikoni kama vile sahani, bakuli, sufuria na vijiko, yeye huhakikisha ni sa ili
kujikinga dhidi ya magonjwa. Baba hupenda kumsaidia mama kufanya shughuli za
nyumbani kama vile kupika na kufua nguo.
Kila wikendi mimi,baba na kaka yangu hucheza kandanda katika uwanja ulio nje
ya nyumba yetu. Baba amenifundisha kushika mpira unapopigwa ukielekezwa
langoni. Amenisaidia kukuza ujuzi wa kuwa mlindalango hodari. Jioni, baba
hunisaidia kufanya kazi ya ziada ambayo huwa nimepewa na mwalimu.
22
Kimeidhinishwa na KICD
Ninampenda sana baba yangu. Ninamwomba Mungu aendelee kumlinda ili aishi
miaka mingi.
Mwalimu afahamu kuwa anaweza kubuni insha ya wasifu yenye mada tofauti na mfano
uliotolewa katika kitabu hiki na akawasomea wanafunzi darasani ili kuwapa mazoezi
zaidi.
Mwalimu amhusishe mwanafunzi katika shughuli ya pili kwa kumwagiza aendeleze
insha iliyo kwenye kitabu chao kwa maneno yake mwenyewe. Majibu tarajiwa: jina
la raki, mvulana/msichana/raki, mlingoti, pepepe, anapenda/anachukia, nyeusi/
fupi/ndefu, jina la raki, katika mtaa wa/mjini/mashambani/jina la nchi, kwanza/pili/
mwisho, kazi yoyote, kandanda/pete/raga/kikapu (ataje mchezo wowote), raki yangu/
jina la raki, majina ya vyakula vyovyote, yeye/jina la raki.
Mwalimu akubali majibu yoyote ambayo yataitiririsha insha na kuwa na maana
kulingana na ujumbe wa kifungu.
Hatimaye, mwalimu amhimize kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada. Mwanafunzi
aandike insha ya wasifu kumhusu mwalimu anayempenda. Ahakikishe anazingatia
muundo sahihi wa kuandika insha ya wasifu. Amsomee mzazi au mlezi wake insha
hiyo ili aitathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika insha ya wasifu kwa
kuzingatia muundo na mtindo, sentensi sahihi na sanifu, mtiririko wa mawazo
na ubunifu.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuendeleza kifungu cha insha
ya wasifu kwa kutumia maneno yanayofaa ili insha iwe na maana na mtitiriko.
D. Saru:Ainazamaneno
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 12)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya aina ya neno lengwa ili kutofautisha na aina nyingine za
maneno.
b) Kutambua aina ya neno lengwa katika kundi la maneno na sentensi.
ch) Kutumia aina ya neno lengwa kwa njia sahihi katika sentensi.
d) Kuonea fahari matumizi ya aina ya neno lengwa katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, ni vitu gani unavyoweza kupata nyumbani?
23
Kimeidhinishwa na KICD
2. Ni shughuli gani unazofanya kila siku?
3. Ni sifa zipi unazoweza kutambua katika nomino mbalimbali?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
kutambua aina za neno lengwa na kutunga sentensi mtandaoni.
Kujiamini na kujithamini - unakuzwa mwanafunzi anapofaulu kutambua neno
lengwa na kulitungia sentensi.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi akitumia aina ya neno
lengwa.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia - kutokana na kufanya kazi pamoja.
Utunzaji wa mazingira na wanyama, usalama, usadi na afya bora: wanafunzi
wanapotunga sentensi zinazoelekeza utoaji maelezo kuhusu masuala hayo.
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika vikundi.
Maadili mbalimbali yanaweza kulengwa katika utungaji wa sentensi kama vile
upendo, uwajibikaji, uaminifu, uzalendo, amani na umoja.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia mada ya saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu mawasiliano yenye
kuzingatia kanuni za kisaru.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
24
Kimeidhinishwa na KICD
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya aina
ya neno lengwa.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua aina
ya neno lengwa.
Kueleza maana
na kutoa mifano
ya aina ya neno
lengwa kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza na
kutoa mifano
ya aina ya neno
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
na kutoa mifano
ya aina ya neno
lengwa kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
na kujaribu
kutoa mifano
ya aina ya neno
lengwa.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza maana
ya aina ya neno
lengwa.
Kutumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatumia baadhi
ya aina ya neno
lengwa.
Mwanafunzi
anajaribu
kutumia aina ya
neno lengwa.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli kusoma maelezo
ya maana ya neno lengwa. Pia, mwalimu anaweza kuleta vitu halisi darasani ili
waviguse na kuvitambua.
Mwalimu arekodi video yenye mifano ya aina ya neno lengwa ili kuwafaa wanafunzi
wenye mahitaji ya kusikia.
Maelezo ya jumla
Mada ya saru humwezesha mwanafunzi kuimarisha matumizi ya aina mbalimbali za
maneno ili kuboresha mawasiliano yake.
Kipindi cha 1: Maana ya nomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 12)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya nomino ili kutofautisha na aina nyingine za maneno.
b) Kutambua nomino katika kundi la maneno na sentensi.
Maswali dadisi
1. Je, unajua nomino gani?
2. Je, ni vitu gani vinapatikana nyumbani?
25
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo kuhusu nomino kabla ya kipindi ili kufahamu zaidi kuhusu
shughuli za ujifunzaji atakazowahusisha wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Vifaa halisi kama vile simu, mpira n.k.,
2. Breli,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 12.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wataje vitu
vinavyopatikana nyumbani kwao.
Mwalimu amshirikishe mwanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kumwuliza ataje
vifaa vinavyopatikana shuleni na ambavyo pia hupatikana nyumbani kwao.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaambie wanafunzi wataje majina ya michoro
iliyo katika kitabu chao. Wanafunzi waelezane walichogundua kuhusu michoro hiyo
kisha wajadiliane kuhusu maana ya nomino.
Mwalimu awahusishe wanafunzi katika shughuli ya tatu kwa kuwaongoza kusoma
na kujaza mianya kwenye mazungumzo waliyopewa. Majibu ya mazungumzo haya
yatakuwa nomino. Baada ya kukamilisha mazungumzo, mwalimu awaongoze
wanafunzi kutambua kuwa nomino zinazotumiwa kutajia majina rasmi ya milima,
miezi, watu, wiki, siku na mahali huanza kwa heru kubwa.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kuandika nomino tatu za majina ya: miezi, watu, wiki
na mahali. Mwalimu akubali majina yoyote ambayo ni sahihi kwa kategoria husika.
Wanafunzi watathmini nomino walizoandika darasani.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutambua nomino katika
michoro.
2. Mwalimu atathmini maelezo ya mwanafunzi kuhusu maana ya nomino na
utambuzi wa nomino zinazotumiwa kutajia majina rasmi.
Kipindi cha 2: Nomino katika sentensi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 13)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia nomino kwa njia sahihi katika sentensi.
b) Kufahamu matumizi ya nomino katika mawasiliano.
26
Kimeidhinishwa na KICD
Swali dadisi
Je, ni nomino gani unazozijua?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua nomino huweza kuimarisha mawasiliano yake kwa
kuzitumia kutunga sentensi sahihi.
Hakikisha kila shughuli inafanywa ipasavyo kwa kutembelea kila kikundi darasani
wakati wa kila shughuli na kukielekeza.
Mwalimu awe makini katika ukuzaji wa maadili ya wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Kitabu cha mwanafunzi ukurasa 13,
3. Vifaa halisi, 4. Mti wa maneno.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje nomino wanazojua.
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi wawili wawili katika
shughuli ya kwanza. Mwalimu awaulize watambue nomino kutoka kwenye mti
wa maneno ulio kitabuni mwao. Pia, mwalimu anaweza kutengeneza gurudumu
linalozunguka lenye aina mbalimbali za maneno na kuwateua wanafunzi kulizungusha
na kutaja ikiwa neno lilipotulia pahali alipo mwanafunzi ni nomino au la. Wanafunzi
watunge sentensi kwa kutumia nomino walizotambua. Wabadilishane madaari ili
kusahihisha sentensi zao.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kucheza mchezo wa nomino.
Mwanafunzi mmoja aongoze mchezo huo kwa kutaja neno ambalo ni nomino na
wanafunzi wenzake waruke. Akitaja neno ambalo si nomino wanafunzi wasiruke.
Mchezo huu utawasaidia wanafunzi kufahamu nomino mbalimbali.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kuwaomba watunge
sentensi sahihi zenye majina ya vifaa vya chumba cha kulala. Mwanafunzi awasomee
wenzake darasani sentensi alizotunga ili wazitathmini na kuziboresha.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua nomino kutoka
kwa aina nyingine za maneno.
2. Mwalimu atathmini matumizi ya nomino katika kutunga sentensi sahihi.
27
Kimeidhinishwa na KICD
Aina za maneno
Kipindi cha 1: Vitenzi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 14)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya vitenzi ili kutofautisha na aina nyingine za maneno.
b) Kutambua vitenzi katika kundi la maneno na sentensi.
Swali dadisi
Ni shughuli gani unazofanya kila siku?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua vitenzi na matumizi yake huimarisha mawasiliano yake.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 14,
2. Breli,
3. Chati yenye maneno mbalimbali ya kuchagua.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje shughuli wanazofanya
kila siku.
Awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kutazama vitendo
anavyotenda mwalimu kisha waige vitendo hivyo. Wanafunzi wajadiliane na kueleza
vitendo hivyo.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili wajadiliane kuhusu vitendo
katika michoro iliyo kitabuni mwao. Majibu tarajiwa: Mwanamume anapika,
mwanamke anafagia, mwanamke anaendesha katapila, mvulana anacheza mpira.
Wanafunzi wajadiliane maana ya vitenzi.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya tatu kwa kuwaelekeza wasome
kifungu kilicho kitabuni mwao kinachomhusu Faiza. Baada ya kusoma, wanafunzi
watambue vitenzi vilivyotumika katika kifungu hicho. Mwalimu ahakikishe wanafunzi
wanasoma kifungu hicho kwa matamshi sahihi na wanatambua vitenzi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kujua kuwa maneno waliyotajia wanachofanya watu
katika michoro husika huitwa vitenzi. Umoja wa vitenzi ni kitenzi.
Katika kazi ya ziada, mwalimu awahimize wanafunzi kuchagua na kuandika vitenzi
kutoka kwa orodha ya maneno mbalimbali waliyopewa katika jedwali. Kila mwanafunzi
atunge sentensi akitumia vitenzi alivyochagua. Awasomee wanafunzi wenzake katika
28
Kimeidhinishwa na KICD
kipindi kijacho. Vitenzi kutoka kwa jedwali walilopewa ni: soma, ingia, wanacheza,
cheka, simama, keti, andika, nunua, anika na wanaimba.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini utambuzi wa vitenzi kutoka katika kundi la maneno na
sentensi.
2. Mwalimu asahihishe matumizi ya vitenzi katika sentensi zilizotungwa na
mwanafunzi. Atathmini umilisi unaokuzwa, uhusiano wa vitendo mbalimbali
na maadili, masomo mengine, masuala mtambuko na shughuli za kijamii
katika utunzi wa sentensi.
Kipindi cha 2: Vitenzi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia vitenzi ipasavyo katika sentensi.
b) Kufahamu matumizi ya vitenzi katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, umetambua vitenzi gani?
2. Je, unaweza kutunga sentensi sahihi kwa kutumia vitenzi mbalimbali?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu ahakikishe amesoma kuhusu vitenzi kabla ya kipindi hiki. Hii itamsaidia
kufahamu zaidi nyenzo atakazotumia na shughuli za kuwashirikisha wanafunzi
kulingana na mahitaji yao.
Mwalimu anaweza kubuni shughuli tofauti na zilizopendekezwa katika kitabu cha
mwanafunzi mradi ziweze kutimiza matokeo tarajiwa ya kipindi. Shughuli zaidi pia
zitawafaa wanafunzi ambao hung’amua wanayojifunza polepole.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 16,
2. Breli,
3. Chati iliyo na michoro kuonyesha vitendo mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje shughuli
wanazofanya shuleni na nyumbani.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwauliza
watazame michoro iliyo katika kitabu chao. Wanafunzi wajadiliane kuhusu vitendo
29
Kimeidhinishwa na KICD
vinavyofanyika katika michoro hiyo. Maelezo tarajiwa: Mtoto analisha mbwa, mtoto
anampa paka maziwa, mwanamume anampa ngombe nyasi, wanafunzi wanavuka
barabara, wanafunzi wanaagana, mwanamke amebeba mzigo kichwani, mzee
anatembea kwa mkongojo, mwanamume anavuka barabara n.k. Mwalimu akubali
maelezo yoyote ambayo ni sahihi kwa kurejelea kila mchoro. Wanafunzi waeleze
michoro hiyo kwa kutumia sentensi. Mwalimu ahakikishe wanafunzi wanatunga
sentensi sahihi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaulize wanafunzi wasimame ili kushiriki katika
mchezo wa kutambua vitenzi. Mwalimu ataje maneno mbalimbali. Akitaja kitenzi
wanafunzi waketi, akitaja neno ambalo si kitenzi wanafunzi wabaki wamesimama.
Mwanafunzi atakayekosa kuketi kitenzi kinapotajwa au atakayeketi neno ambalo si
kitenzi linapotajwa asimame mbele ya darasa. Mchezo huu utaboresha usikivu wa
wanafunzi na kuwachangamsha wakati wa kipindi na kukuza hamu ya kujifunza
zaidi. Ikiwa wanafunzi wataenda nyumbani na kuwafunza raki zao mchezo huu wa
kutambua vitenzi basi watakuwa wameihudumia jamii.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi atunge sentensi
tatu tatu sahihi akitumia vitendo mbalimbali vya darasani, nyumbani na uwanjani.
Aandike sentensi hizo katika daari lake kisha atawasomea wenzake darasani katika
kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua vitenzi katika
mchezo wa kutambua vitenzi darasani.
2. Mwalimu asahihishe sentensi ambazo mwanafunzi atatunga.
Aina za maneno
Kipindi cha 1: Vivumishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 17)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kivumishi ili kutofautisha na aina nyingine za maneno.
b) Kutambua vivumishi kutoka katika kundi la maneno na sentensi.
Maswali dadisi
1. Je, unajua maana ya kivumishi?
2. Ni sifa zipi unazoweza kutambua katika nomino?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua vivumishi na matumizi yake huimarisha mawasiliano.
Kivumishi ni neno linalotoa maelezo zaidi kuhusu nomino.
30
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awaongoze wanafunzi kutathmini kazi zao katika vikundi na wakiwa binafsi.
Wanafunzi wanapotunga sentensi, mwalimu atathmini umilisi mbalimbali unaokuzwa,
maadili na jinsi wanafunzi wanavyoweza kuhusisha mada ya vivumishi na masuala
mtambuko na masomo mengine kama vile lugha za kiasili.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 17,
2. Breli,
3. Vifaa halisi kama vile tunda bivu na bichi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi waeleze kuhusu vitu
mbalimbali darasani kwa kutumia urefu, rangi, unene, uzuri, ukubwa.
Mwalimu amhusishe mwanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kumwambia
amtazame mwenzake kisha ataje sifa za nywele zake, viatu vyake, kucha zake na sare
yake. Mwalimu ahakikishe wanafunzi wanataja sifa hizo.
Katika shughuli ya pili, mwalimu amwelekeze mwanafunzi kutambua michoro iliyo
katika kitabu chao. Atambue rangi, ukubwa, udogo, ubichi na ubivu wa vitu katika
michoro hiyo. Majibu tarajiwa: gari jekundu, gari la samawati, mwiko mdogo, mwiko
mkubwa, chungwa bivu na chungwa bichi. Wanafunzi wajadiliane kuhusu maana ya
vivumishi.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya tatu kwa kuwauliza watambue
vivumishi kutoka kwa kundi la maneno mbalimbali lililo kitabuni mwao.
Wanafunzi washiriki katika shughuli hii wakiwa wawili wawili. Majibu tarajiwa:
nyeupe, ndefu, wadogo, kizuri, mwema, wafupi. Kila mwanafunzi atunge sentensi
sahihi akitumia vivumishi walivyotambua. Mwalimu ahakikishe kuwa mwanafunzi
anatunga sentensi sahihi.
Kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada waliyopewa katika kitabu chao. Amshirikishe
mlezi au mzazi wake katika kueleza sifa za vitu mbalimbali vya sebuleni. Mwanafunzi
aandike sifa hizo katika daari lake kisha atawasomea wanafunzi wenzake darasani.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua sifa za vitu na
viumbe mbalimbali.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kueleza maana ya vivumishi
na kuvitambua kutoka kwa kundi la maneno mbalimbali.
Kipindi cha 2: Vivumishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 18)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia vivumishi ipasavyo katika sentensi na kifungu.
b) Kufahamu matumizi ya vivumishi katika sentensi.
31
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Ni sifa zipi unazoweza kutambua katika nomino?
2. Je, unaweza kutambua vivumishi katika kifungu?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapoweza kutumia vivumishi kwa usahihi katika sentensi na kifungu
ataimarisha mawasiliano yake.
Mwalimu amhusishe mwanafunzi katika shughuli kulingana na mahitaji yake. Aandae
funzo la vivumishi kabla ya kipindi ili kumwelekeza mwanafunzi ipasavyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 18, 2. Breli, 3. Vifaa halisi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje vivumishi
walivyojifunza katika kipindi kilichotangulia.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu amwongoze mwanafunzi kusoma kifungu
kilicho kitabuni mwao. Mwalimu ahakikishe kila mwanafunzi anasoma kifungu hicho
kwa matamshi sahihi na ujasiri. Baada ya kusoma, mwanafunzi ajibu maswali ya
kifungu katika kitabu cha mwanafunzi. Kila mwanafunzi atambue vivumishi vya sifa
katika kifungu hicho. Baadaye, atumie vivumishi alivyotambua kutunga kifungu cha
aya mbili. Wanafunzi wabadilishane madaari ili wavisahihishe vifungu vyao.
Majibu tarajiwa ya swali la kifungu: Vivumishi vya sifa ni zuri, nyeupe, kitamu,
kubwa, vichafu, sa.
Katika shughuli ya pili, mwalimu amwulize mwanafunzi atazame michoro iliyo
katika kitabu chao kisha aandike sifa za michoro hiyo. Majibu tarajiwa: mche mdogo,
mti mkubwa, shibli mdogo, simba mkubwa. Mwalimu akubali majibu yoyote ambayo
yanaambatana na michoro waliyopewa.
Mwalimu awaongoze wanafunzi wawili wawili kufanya shughuli ya tatu. Awaelekeze
wasahihishe sentensi zilizo katika kitabu chao. Mwalimu awasaidie wanafunzi
kusahihisha sentensi hizo ikiwa watakuwa na changamoto katika baadhi ya sentensi.
Pia, anaweza kuwahusisha wanafunzi zaidi kuwasaidia waliokosea kusahihisha
sentensi hizo. Majibu tarajiwa: 1. Vijiko vichafu vimesashwa. 2. Magari makubwa
yameuzwa. 3. Kifaranga mzuri amenyakuliwa na mwewe. 4. Miti mirefu inapendeza. 5.
Mazingira sa yanavutia.
Hatimaye, kila mwanafunzi ahimizwe kufanya kazi ya ziada. Mlezi au mzazi wake
amsaidie kutaja sifa za vifaa vya jikoni. Mwanafunzi aandike sifa hizo katika daari
lake kisha azitumie kutunga kifungu cha aya moja. Atawasomea wenzake kifungu
hicho darasani katika kipindi kijacho.
32
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua vivumishi katika
kifungu alichosoma.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutunga sentensi sahihi
pamoja na kifungu akitumia vivumishi vya sifa.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
Mwalimu atathmini sentensi zitakazotungwa na mwanafunzi. Sharti sentensi hizo
ziwe sahihi na zitumie vitate walivyopewa. Mifano ya sentensi hizo ni:
1. Mkulima huyu amekuza mimea ninayogusa.
2. Mgeni mwenye tai anadai malipo yake.
Mwalimu atathmini maelezo ya mwanafunzi kuhusu matumizi ya vifaa vya nyumbani
walivyotajiwa. Mifano ya matumizi hayo ni:
3. Jokofu huwa na ubaridi unaotumika kuhifadhi vinywaji na vyakula.
4. Maga ni mawe matatu ambayo hutumika kwenye moto kupikia.
5. Buli huhifadhi chai ikiwa moto.
6. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi amesoma kifungu chochote kuhusu vifaa
vya nyumbani. Asahihishe matumizi sahihi ya vifaa ambavyo mwanafunzi atataja.
7. Nomino ni: Nairobi, mji, Kenya
8. Baadhi ya mambo ya kuzingatia katika uandishi wa insha ya wasifu ni:
a) Mada lazima insha iwe na mada ya kuandikia.
b) Mtiririko wa mawazo matukio yaandikwe kwa mfuatano.
ch) Saru sahihi itumike. Saru inahusisha matumizi ya lugha sanifu, uakishaji
mwafaka na tahajia sahihi.
d) Hati au mwandiko unaosomeka kwa urahisi utumike.
9. Mwalimu atathmini insha ya wasifu ambayo mwanafunzi atabuni na kuandika.
Sharti insha hiyo izingatie muundo sahihi wa insha ya wasifu.
10. Aina tatu za maneno ambayo mwanafunzi amejifunza ni pamoja na: Nomino,
vitenzi na vivumishi.
a) Mifano ya nomino ni: bata, nyumba, kikombe, darasa, mama, Jumapili, Kenya.
b) Mifano ya vitenzi ni: keti, chora, ruka, simama, pika, fagia, soma.
ch) Mifano ya vivumishi ni: mkubwa, warefu, kidogo, sa, jeusi.
33
Kimeidhinishwa na KICD
NIDHAMU MEZANI
2
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 21)
A. Kusikiliza na Kuzungumza: Maamkuzi na maagano
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua aina mbalimbali za maamkuzi na maagano katika mawasiliano.
b) Kueleza maamkuzi na maagano yanayotumika katika miktadha mbalimbali.
ch) Kutumia aina mbalimbali za maamkuzi na maagano katika mawasiliano.
d) Kuchangamkia maamkuzi na maagano katika mahusiano.
Maswali dadisi
1. Je, watu husalimiana vipi katika jamii yako?
2. Je, watu huagana vipi katika jamii yako?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake kuigiza maamkuzi na maagano mbalimbali.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kidijitali
kujifunza.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anapotumia maamkuzi na maagano
ipasavyo.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya amani - kwa kuamkuana na kuagana.
Umoja wa kijamii - kupitia kuamkua na kujibu maamkuzi na maagano.
Uhusiano na maadili
Heshima - maamkuzi na maagano huimarisha heshima.
Upendo - maamkuzi na maagano huashiria upendo.
Umoja - maamkuzi na maagano huimarisha umoja na uhusiano mwema.
Uhusiano na masomo mengine
Somo la Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yana mada kuhusu
maamkuzi.
34
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake katika jamii kuhusu jinsi ya kuamkua, kuagana
na umuhimu wa maamkuzi na maagano.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
maamkuzi
na maagano
mbalimbali
na kuyatumia
katika miktadha
tofauti tofauti
kwa ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
maamkuzi
na maagano
mbalimbali
ya kutumia
katika miktadha
tofauti tofauti
kwa ufasaha na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
maamkuzi
na maagano
mbalimbali
na kuyatumia
katika miktadha
tofauti tofauti
kwa ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
maamkuzi na
maagano na
kuyatumia
katika miktadha
tofauti tofauti.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
maamkuzi na
maagano na
kuyatumia.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema na kusikia wajibu maamkuzi na maagano
kwa kuandika majibu sahihi. Pia, wanaweza kupigia mstari jibu sahihi la maamkuzi
na maagano. Wanafunzi walio na uwezo wa kusema wayatamke majibu. Vilevile,
video yaweza kutumika.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watumie breli au wasikilize maamkuzi na
maagano na majibu yao yakisomwa na mwalimu au wanafunzi wenzao.
Maelezo ya jumla
Mada ya maamkuzi na maagano ni muhimu kwa wanafunzi kwa kuwa itawawezesha
wanafunzi kuwa na uhusiano mwema na watu walio karibu nao na wote watangamanao
nao katika maisha yao ya kila siku.
Maamkuzi huwezesha amani na umoja kudumu katika jamii.
Kipindi cha 1: Maana ya maamkuzi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 21)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua aina mbalimbali za maamkuzi katika mawasiliano.
b) Kueleza maamkuzi yanayotumika katika miktadha mbalimbali.
ch) Kuchangamkia maamkuzi katika mahusiano.
35
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Je, watu husalimiana vipi katika jamii yako?
2. Asubuhi utamsalimia vipi mzazi wako?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kabla ya kipindi hiki, mwalimu afanye utati kuhusu maana ya maamkuzi. Afahamu
maamkuzi mbalimbali. Mwalimu aweze kutofautisha maamkuzi ya nyakati mbalimbali.
Maamkuzi ni maneno yanayotumika kumjulia mtu au watu hali. Pia huitwa salamu.
Mwalimu aweze kutofautisha maamkuzi na maagano. Maagano ni maneno ambayo
yanatumika wakati watu wanapoachana baada ya kuwa pamoja. Mwalimu arejelee
mafunzo ya maamkuzi ya gredi za awali. Mwalimu anaweza kuimba wimbo wa salamu
ikiwa anaufahamu wimbo wowote. Amwongoze mwanafunzi kutambua salamu
mbalimbali. Wakati wa kuigiza, mwalimu awape wanafunzi nyadhifa kulingana na
uwezo wao. Ikiwa kuna mavazi kama vile ya kimaasai, wanafunzi wanaweza kutumia
wakati wa kuigiza. Mwalimu atayarishe picha za watu wanaoamkuana kabla ya kipindi
hiki.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 21,
2. Picha za watu wanaoamkuana,
3. Video yenye maagano mbalimbali,
4. Kadi zenye maamkuzi mbalimbali,
5. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi wakiwa wawili wawili
kujadiliana namna wao huwaamkua walezi au wazazi wao asubuhi, namna mwalimu
wao huwaamkua darasani, namna wao huamkuana na maraki zao wakati wa jioni na
namna wao huwaamkua babu au nyanya zao.
Mwalimu akubali maamkuzi yoyote sahihi yanayotajwa na wanafunzi na ambayo
yanaendana na maswali waliyoulizwa. Mwalimu awaelekeze na kuwakosoa.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kujadili yale wanayoyaona
kwenye michoro waliyopewa kitabuni mwao. Waeleze watu walio katika michoro hiyo
wanatumia maneno gani kuamkuana. Mwalimu akubali majibu ya wanafunzi kwa
kurejelea michoro waliyopewa. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua maana ya
maamkuzi. Mwalimu awaongoze wanafunzi wakiwa wawili wawili waigize maamkuzi
ambayo watu katika michoro waliyotazama wanatumia. Mwalimu ahakikishe wanafunzi
wote wanahusika katika maigizo na kuelewa maamkuzi yanayorejelewa. Mwalimu
awahimize wanafunzi kuwa na ujasiri wa kuzungumza mbele ya watu.
36
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi wakiwa katika vikundi kutaja
maamkuzi mbalimbali ya asubuhi, jioni na wakati wowote. Pia, wanafunzi waelezane
wanavyoamkuana katika lugha zao za kwanza.
Mwalimu akubali maamkuzi yoyote sahihi kulingana na nyakati zilizotajwa. Kwa
kurejelea maamkuzi ya lugha za kwanza za wanafunzi, mwalimu awe na umilisi
wa kiujozi lugha ili kuwa katika nafasi nzuri ya kuelewa majibu sahihi. Anaweza
kuwatumia wanafunzi wengine kutathmini maamkuzi ya lugha zao za kwanza.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kucheza mchezo wa kadi katika shughuli ya nne.
Mwanafunzi mmoja achukue kadi iliyoandikwa maamkuzi kutoka kwa kikapu
na kuwasomea wanafunzi wenzake. Wanafunzi wenzake wajibu maamkuzi hayo.
Mwalimu ahakikishe wanafunzi wote wanashiriki kucheza mchezo huo. Wale walio
na mahitaji maalumu wahimizwe zaidi na kupewa majukumu ya kuwafanya wajiamini
na kujithamini.
Mwalimu ahitimishe kipindi hiki kwa kuwaelekeza wanafunzi namna ya kufanya kazi
ya ziada. Kila mwanafunzi amtajie mlezi au mzazi wake maamkuzi yanayotumika
nyakati mbalimbali. Mlezi au mzazi ajibu maamkuzi hayo. Mwanafunzi aandike
maamkuzi hayo na majibu yake katika daari lake. Mwalimu atathmini majibu hayo
katika kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anafahamu kuamkua vizuri.
2. Mwalimu asahihishe majibu ya mwanafunzi kuhusu maamkuzi mbalimbali.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anafahamu maamkuzi ya nyakati
mbalimbali.
Kipindi cha 2: Maamkuzi na maagano
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 23)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua aina mbalimbali za maagano katika mawasiliano.
b) Kueleza maagano yanayotumika katika miktadha mbalimbali.
ch) Kuchangamkia maamkuzi na maagano katika mahusiano.
Swali dadisi
Je, watu huagana vipi katika jamii yako?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Maagano ni maneno yanayotumika wakati watu wanapoachana. Kuna maagano ya
kawaida na yale ya wakati wa kulala. Mifano ya maagano ya kawaida ni kama vile:
37
Kimeidhinishwa na KICD
kwaheri, tuonane kesho na tuonane tena. Maagano ya wakati wa kulala ni kama vile:
alamsiki, usiku mwema, lala unono, lala salama. Mwalimu atafute mifano zaidi ya
maagano na majibu yao. Awaelekeze wanafunzi kuelewa tofauti kati ya maagano na
maamkuzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 23,
2. Breli,
3. Video ya maagano mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wajibu maswali katika
shughuli ya kwanza.
Majibu tarajiwa:
1. Kwaheri ya kuonana, tuonane kesho,
2. Lala unono, alamsiki, usiku mwema, lala salama,
3. Kwaheri, tuonane kesho,
4. Mwalimu awaelekeze wanafunzi wawili wawili waigize maagano waliyojadili.
Ahakikishe wanafunzi wanakuza ujasiri wao wa kuigiza na kuzungumza mbele
ya watu.
Katika shughuli ya pili, mwalimu aandae video ambayo atawaonyesha wanafunzi
darasani. Video hiyo ihusu watu wakiagana kwa kutumia maagano mbalimbali. Pia,
inaweza kuhusisha watu wakiamkuana kwa maamkuzi mbalimbali. Mwalimu aandae
video hii kabla ya kipindi hiki.
Wanafunzi waeleze watakayoyaona kwenye video watakayoonyeshwa. Mwalimu
akubali majibu yoyote yatakayohusu video husika. Mwalimu anaweza kutumia
tarakilishi, projekta, rununu au runinga kuwaonyesha wanafunzi video hiyo.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi wasome mazungumzo
kati ya Babu na Kemunto. Wanafunzi wasome wakiwa wawili wawili. Ahakikishe
wanafunzi wanasoma kwa usahihi.
Baada ya kusoma, wanafunzi wote waandike
maamkuzi yaliyotumiwa
katika mazungumzo hayo. Pia, wajadiliane kuhusu vitendo
vinavyoonyesha nidhamu ya mezani kama vilivyojitokeza katika mazungumzo
waliyosoma.
Majibu tarajiwa:
1. Mifano ya maamkuzi: shikamoo, habari n.k.
2. Mtu hafai kupitisha mkono juu ya vyakula kuchukua kitu, anaweza kumwaga
vyakula, mtu anafaa kula akiwa ameketi, mtu anafaa kula polepole ili
asisakamwe na chakula n.k.
38
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada ambapo atajadiliana
na mlezi au mzazi wake kuhusu vitendo katika mchoro waliopewa kitabuni mwao.
Wanafunzi waeleze maneno yanayotumiwa na watu katika mchoro husika. Pia,
mwanafunzi aandike baadhi ya vitendo wanavyotenda vinavyoonyesha nidhamu ya
mezani nyumbani kwao. Awaeleze wenzake darasani ili wajifunze.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini ikiwa mwanafunzi anaweza kutaja maagano mbalimbali.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutoa majibu ya maagano.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anafahamu vitendo mbalimbali vya
kuonyesha nidhamu ya mezani.
B. Kusoma: Kusoma kwa ufahamu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 25)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kamusi ili kuitofautisha na vitabu vingine.
b) Kutumia kamusi ipasavyo kutafuta maana za maneno asiyoyajua ili kukuza
msamiati wake.
ch) Kuchangamkia umuhimu wa kamusi katika kukuza msamiati wake.
Maswali dadisi
1. Unatafutaje maana za maneno kwenye kamusi?
2. Kamusi ina umuhimu gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake kutafuta maana za maneno.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia mtandao kutafuta
maana za maneno.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa wanafunzi wanapoanza kutumia kamusi
kutafuta maana za maneno.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha - uwezo wa kujitegemea katika kutumia kamusi.
Uhusiano na maadili
Uzalendo - hamu ya kukuza msamiati ili kuweza kutumia lugha ya Kiswahili
kama lugha ya taifa.
39
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya husisitiza matumizi mbalimbali
ya kamusi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi ataelekeza utumiaji sahihi wa maneno katika jamii.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutumia kamusi
kwa kuzingatia
mpangilio wa
maneno na
kujikita katika
maana za
maneno lengwa.
Mwanafunzi
anatumia
kamusi
kwa urahisi
akizingatia
mpangilio
wa maneno
na anajikita
katika maana za
maneno lengwa.
Mwanafunzi
anatumia
kamusi
akizingatia
mpangilio
wa maneno
na anajikita
katika maana za
maneno lengwa.
Mwanafunzi
anatumia
kamusi
akizingatia
mpangilio wa
maneno bila
kujikita katika
maana za
maneno lengwa.
Mwanafunzi
anajaribu
kutumia kamusi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watumie breli au kusikiliza maelezo kuhusu
matumizi ya kamusi kutoka kwenye tarakilishi au rekoda au kwa wanafunzi wenzao.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia wasome maelezo ya namna ya kutumia
kamusi kwenye kiwambo cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuongea wajibu maswali kwa kuandika madaarini
au kutumia lugha ishara ikiwa mwalimu anaifahamu.
Wanafunzi wanaoelewa kwa haraka wapewe mazoezi zaidi kuhusu matumizi ya
kamusi. Wanafunzi wanaochukua muda kuelewa wapewe muda zaidi ili wakamilishe
kazi zao.
Maelezo ya jumla
Kamusi ni kitabu cha maneno yaliyopangwa kwa utaratibu wa alfabeti. Hii hurahisisha
kutafuta maneno na kutolewa maana na maelezo mengine. Maelezo mengine ni kama
vile kutupa umoja au wingi wa neno. Pia, kamusi hutuwezesha kujua maneno mengine
yenye maana sawa na neno lengwa. Iwapo mtu hajui maendelezo sahihi, kamusi
itamwelekeza. Aina za maneno huonyeshwa kwenye kamusi.
40
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Matumizi ya kamusi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 25)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kamusi ili kuitofautisha na vitabu vingine.
b) Kutumia kamusi ipasavyo kutafuta maana za maneno asiyojua ili kukuza
msamiati wake.
ch) Kuchangamkia umuhimu wa kamusi katika kukuza msamiati wake.
Swali dadisi
Unatafutaje maneno kwenye kamusi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kamusi ni kitabu muhimu sana kwa kila mwanafunzi wa Kiswahili. Mwalimu
ahakikishe ametafuta vitabu halisi vilivyoonyeshwa katika kitabu cha mwanafunzi
kabla ya kipindi hiki ili awaonyeshe wanafunzi darasani.Vitabu hivyo ni kitabu cha
kiada cha Kiswahili, Kurani Tukufu, Kamusi na Biblia. Iwapo hatapata vitabu vyenyewe,
mwalimu atafute vitabu hivyo mtandaoni ili aweze kuwaonyesha wanafunzi picha
zao. Pia, anaweza kutumia picha za vitabu hivyo. Awaelekeze kutambua matumizi
ya vitabu hivyo na kuweza kutofautisha kamusi na vitabu hivyo. Biblia hutumiwa na
Wakristo, Kurani Tukufu hutumiwa na Waislamu, kitabu cha Kiswahili pamoja na
kamusi hutumiwa na wanafunzi wa Kiswahili.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 25, 2. Biblia, 3. Kurani Tukufu,
4. Kamusi, 5. Tarakilishi, 6. Rununu.
Mapendekezo ya shughuli za ufundishaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwapa wanafunzi fursa ya kutazama vitabu
mbalimbali alivyoleta darasani. Wanafunzi wavishike na kuvitambua. Katika shughuli
ya kwanza, wanafunzi watazame michoro ya vitabu mbalimbali iliyo katika kitabu
chao. Wanafunzi wajadiliane kuvihusu wakiwa katika vikundi. Mwalimu awagawe
wanafunzi katika vikundi akizingatia idadi na mahitaji yao. Wanafunzi wataje mahali
vitabu hivi hupatikana na umuhimu wake. Vilevile, wanafunzi wajadiliane kuhusu
maana ya kamusi.
Majibu tarajiwa: maktabani, darasani, kanisani, msikitini, kortini, garini, nyumbani
na pia mahali pengine ambapo panaweza kupatikana vitabu hivyo.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kujadiliana iwapo wamewahi
kutumia kamusi. Waulizwe waliitumia kutafuta maana ya maneno gani na matumizi
yao yalikuwa rahisi au magumu.
41
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu akubali majibu yoyote sahihi yanayolingana na maswali husika. Mwalimu
atarajie kuwa kuna wanafunzi ambao watakuwa wamewahi kutumia kamusi kwa hivyo
hao wanaweza kutaja maneno waliyoyatafuta. Kwa wale ambao hawajawahi kutumia
kamusi, mwalimu awaonyeshe na kuwaeleza zaidi kuhusu matumizi ya kamusi. Pia,
wanafunzi walioweza kutumia kamusi kwa urahisi wawaelekeze wenzao. Mwalimu
awasaidie wanafunzi kujua jinsi ya kutumia kamusi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya shughuli ya tatu katika vikundi. Wanafunzi
watumie kamusi yoyote ya Kiswahili kupanga maneno yaliyo katika kitabu chao
kwa utaratibu wa namna yalivyo kwenye kamusi. Ikiwa wanafunzi wana kamusi
zao, wazitumie kupanga maneno waliyopewa. Mwalimu anaweza kuwapa wanafunzi
kamusi kutoka kwa maktaba ya shule ili waweze kuzitumia katika vikundi vyao.
Majibu tarajiwa: beba, birika, meza, mpishi, nawa, sinia, tafuna, zabibu.
Wanafunzi watafute na kueleza maana za maneno waliyopanga kwa kutumia kamusi.
Mwalimu akubali maelezo au maana yoyote sahihi kutoka kwenye kamusi.
Mwalimu asahihishe kazi ya wanafunzi na awape majibu sahihi ili waweze kufanya
marudio.
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa usaidizi wa mlezi
au mzazi wake. Atumie kamusi iliyo mtandaoni kutafuta maana za maneno yaliyo
katika kitabu chake.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada: Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ameandika
maana au maelezo sahihi ya maneno aliyopewa kwa kutumia kamusi ya mtandaoni.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi ambao watakuwa na matatizo.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaelewa maana ya kamusi.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaelewa jinsi ya kutumia kamusi.
3. Mwalimu atathmini ikiwa mwanafunzi anajua kutumia kamusi ya mtandaoni
kupata maana za maneno.
Kipindi cha 2: Matumizi ya kamusi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 26)
Malengo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia kamusi ipasavyo kutafuta maana za maneno asiyoyajua ili kukuza
msamiati wake.
b) Kuchangamkia umuhimu wa kamusi katika kukuza msamiati wake.
42
Kimeidhinishwa na KICD
Swali dadisi
Kamusi ina umuhimu gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awapange wanafunzi kwenye vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Pia, azingatie vifaa au rasilimali zinazohitajika kama vile tarakilishi na vitabu vya
wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kamusi, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 26,
3. Tarakilishi, 4. Breli, 5. Rununu.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaongoze wanafunzi kusoma kifungu kuhusu
kamusi kilicho kwenye kitabu chao. Ahakikishe kila mwanafunzi anasoma kifungu
hicho na kukielewa. Mwalimu anaweza kuwauliza wanafunzi maswali yoyote kutokana
na kifungu hicho ili kutathmini uelewa wao. Awagawe wanafunzi katika vikundi
kisha wajibu maswali waliyopewa. Aelekeze kila kikundi kiteue mwakilishi ili aweze
kuwasilisha kazi yao mbele ya darasa. Wenzake wasikilize na kutathmini kazi yao.
Wanafunzi watakaokosea waelekezwe.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi na mahitaji yao. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutafuta maana ya maneno
yaliyo katika kitabu chao. Watumie tarakilishi au rununu ya mwalimu kutafuta
maana za maneno hayo. Wanafunzi wengine wasikilize maelezo kuhusu maneno hayo
yakisomwa na mmoja wao katika kikundi. Kila mwanafunzi aandike maelezo hayo
katika daari lake. Wanafunzi wajadiliane kuhusu maana za maneno waliyotafuta kwa
kurejelea nidhamu ya mezani.
Katika kazi ya ziada, mwalimu amwelekeze mwanafunzi kutumia mtandao kutafuta
picha za vifaa vyovyote vitano ambavyo hutumika mezani wakati wa kula chakula. Pia,
mwanafunzi atafute maana na matumizi ya vifaa alivyotaja na aandike katika daari
lake. Anaweza kutumia kamusi. Awasomee wenzake darasani aliyoandika ili wajifunze.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anajua kutafuta maana ya maneno kwa
kutumia kamusi.
2. Mwalimu atathmini ikiwa mwanafunzi anaelewa kutafuta matumizi ya vifaa
mbalimbali vya mezani kwa kutumia kamusi.
43
Kimeidhinishwa na KICD
CH. Kuandika: Kuandika insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 27)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi inayozingatia mada, ujumbe, mtindo na
muundo ufaao.
ch) Kuchangamkia utunzi mzuri wa insha ya masimulizi ili kukuza ubunifu.
Maswali dadisi
1. Insha ya masimulizi inahusu nini?
2. Je, unazingatia nini unapoandika insha ya masimulizi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinatumiwa
kuandika insha mtandaoni na kurejelea kielelezo cha insha ya masimulizi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya masimulizi.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yana mada kuhusu insha.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi bora katika mawasiliano.
44
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio
mzuri wa
mawazo na kwa
ubunifu wa hali
ya juu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha
na mpangilio
mzuri wa
mawazo.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika insha
ya masimulizi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watumie breli au kusikiliza maelezo kuhusu
insha ya masimulizi kutoka kwenye tarakilishi au rekoda.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia wasome maelezo ya insha ya masimulizi
kwenye kiwambo cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuongea wajibu maswali kwa kuandika madaarini
au kutumia lugha ishara ikiwa mwalimu anaifahamu.
Wanafunzi wanaoelewa kwa haraka wapewe mazoezi zaidi kuhusu insha ya
masimulizi. Wanafunzi wanaochukua muda kuelewa wapewe muda zaidi ili
wakamilishe kazi zao.
Maelezo ya jumla
Kuandika insha ya masimulizi kutamsaidia mwanafunzi kukuza stadi ya kuandika na
kuimarisha mawasiliano andishi shuleni na katika jamii.
Uandishi wa insha pia hukuza ubunifu wa mwanafunzi na kumwezesha kutatua
changamoto zinazomkabili shuleni na katika jamii.
Ikiwa mwanafunzi ataweza kuimarika katika stadi ya kusikiliza, kuzungumza na
kusoma ataweza kuimarisha stadi ya kuandika upesi. Kwa hivyo, mwalimu ahakikishe
mwanafunzi amejifunza vyema stadi hizo kabla ya kuandika insha ya masimulizi.
Kipindi cha 1: Maana ya masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 27)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi inayozingatia muundo.
45
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Insha ya masimulizi inahusu nini?
2. Je, unazingatia nini unapoandika insha ya masimulizi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome kitabu cha mwanafunzi ili kufahamu shughuli za kipindi hiki na
kuteua nyenzo zinazofaa na zinazopatikana kwa urahisi.
Mwalimu akubali na kutathmini maoni ya kila mwanafunzi kuhusu vidokezo vya
insha ili aweze kujithamini katika ubunifu na kuchangamkia uandishi wa insha.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 27, 2. Breli, 3. Gazeti.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awapange wanafunzi wawili wawili wasimuliane
kuhusu sherehe zozote ambazo wamewahi kuhudhuria. Shughuli hii itajenga uwezo
wao wa kujieleza.
Katika shughuli ya pili, wanafunzi wajadiliane katika vikundi kuhusu maswali
waliyopewa kitabuni mwao. Maswali hayo yanahusu kutembelewa na wageni nyumbani
kwao na nidhamu ya mezani iliyozingatiwa. Mwalimu awaelekeze wanafunzi wachague
kiongozi katika kila kikundi ambaye atawasilisha hoja zao. Mwalimu ayatathmini na
kuyakubali majibu ya wanafunzi katika vikundi tofauti tofauti kulingana na maswali
husika.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi kusoma insha ya masimulizi
iliyo katika kitabu chao. Baada ya kusoma na kujadili insha hiyo, wajibu maswali
waliyopewa. Kila mwanafunzi aandike muhtasari wa insha waliyosoma katika daari
lake. Vilevile wanafunzi wajadiliane kuhusu muundo wa insha ya wasifu waliyosoma.
Mwalimu atathmini kazi za wanafunzi.
Mwalimu awashauri wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Wanafunzi wasome kisa
chochote kutoka katika gazeti la Kiswahili. Baada ya kusoma, waandike muhtasari
wa kisa hicho. Mwanafunzi awasomee wenzake darasani pamoja na mwalimu ili
wautathmini muhtasari alioandika. Pia, mwanafunzi amsomee mzazi au mlezi wake
muhtasari alioandika ili autathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kusimulia mwenzake kuhusu
sherehe yoyote.
2. Mwalimu asikilize wanafunzi wakisoma mfano wa insha. Atathmini iwapo
wanatamka maneno kwa usahihi na urahisi, ikiwa wana ukakamavu
wanaposoma na kama wanazingatia alama za uakishaji wanaposoma.
46
Kimeidhinishwa na KICD
3. Mwalimu asahihishe insha ambayo mwanafunzi amebuni. Atathmini hati,
ubunifu, lugha sahihi na mfuatano wa mawazo kulingana na maswali
yaliyotumiwa kumwelekeza mwanafunzi.
Kipindi cha 2: Kuandika insha ya masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 30)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi inayozingatia mada ujumbe, mtindo na
muundo.
ch) Kuchangamkia utunzi mzuri wa insha ya masimulizi ili kukuza ubunifu wake.
Swali dadisi
Je, unazingatia nini unapoandika insha ya masimulizi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu anaweza kumhusisha mgeni mwalikwa katika kipindi hiki. Mwalimu
amtafute na kumwandaa kabla ya kipindi hiki. Ampe mada ya kuzungumzia ili aweze
kujiandaa kwa somo hili. Mada ihusu masimulizi kuhusu sherehe yoyote. Awajulishe
wanafunzi kuhusu mgeni mwalikwa na mada atakayozungumzia. Mwalimu ahakikishe
wanafunzi wanasikiliza kwa makini wakati mgeni mwalikwa atakuwa akisimulia na
waweze kunakili vidokezo muhimu kwa madhumuni ya kuandika muhtasari.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Mgeni mwalikwa, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 30, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi kusikiliza kwa makini
na kunakili hoja muhimu wakati mgeni mwalikwa atakuwa akisimulia. Wakiwa katika
vikundi watumie hoja walizonakili kujadili ujumbe wa masimulizi hayo. Mmoja wa
wanafunzi katika kila kikundi anaweza kuwasomea wenzake waliyojadili ili watathmini.
Kila mwanafunzi atumie hoja walizojadili kuandika muhtasari wa masimulizi
waliyosikiliza kutoka kwa mgeni mwalikwa.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kuzingatia waliyojadili
katika shughuli ya kwanza, kujadiliana kuhusu mada waliyopewa katika kitabu chao
kuhusu Harusi Niliyohudhuria. Wanafunzi waandae vidokezo muhimu kutokana na
majadiliano yao na wavitumie kuandika insha ya masimulizi.
Kila kikundi kimteue mwanafunzi atakayesoma insha waliyoandika mbele ya darasa.
47
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wengine pamoja na mwalimu wasikilize na kutathmini insha hiyo. Baada ya
kiongozi wa kikundi kusoma kazi yao, mwalimu atathmini kazi yao akitumia mambo
muhimu yanayozingatiwa wakati wa uandishi wa insha ya masimulizi
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Kila mwanafunzi amwambie
mlezi au mzazi wake amweleze kuhusu mambo ya kuzingatia ili kuwa na nidhamu
mezani. Mwanafunzi awaeleze wenzake darasani ili wajifunze. Mwalimu akubali
majibu yoyote sahihi yanayorejelea nidhamu ya mezani.
Tathmini
1. Mwalimu asikilize majibu ya wanafunzi kutokana na maswali ya insha
aliyowasomea darasani na kuyatathmini.
2. Mwalimu asahihishe insha waliyoandika wanafunzi. Atathmini hati, ubunifu,
usahihi wa lugha, uzingatiaji wa mada na ufafanuzi wa hoja za mada kwa
mfuatano.
D. Saru:Ainazamaneno
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 30)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya aina ya neno lengwa ili kulibainisha.
b) Kutambua aina ya neno lengwa katika kundi la maneno na sentensi.
ch) Kutumia viwakilishi ipasavyo katika sentensi.
d) Kuonea fahari matumizi ya aina ya neno lengwa katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Ni maneno gani ambayo hutumiwa badala ya nomino katika sentensi?
2. Ni maneno gani yanaweza kutumiwa kutoa habari zaidi kuhusu vitenzi
unavyojua?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
mijadala, kazi ya vikundi na mawasiliano mtandaoni.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
katika kutambua aina ya neno lengwa na kutunga sentensi mtandaoni.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi akitumia aina ya neno
lengwa.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anapofaulu kutambua aina ya neno lengwa
na kulitungia sentensi sahihi.
48
Kimeidhinishwa na KICD
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapotafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja.
Masuala mtambuko anuwai kutokana na sentensi zilizoelekeza utoaji wa maelezo
kuhusu masuala hayo kama vile utunzaji wa mazingira, afya bora na utunzaji wa
wanyama.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Maadili mbalimbali yaliyolengwa katika sentensi kama vile upendo, uaminifu,
uzalendo, amani na umoja.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo hayo yanafunza kanuni za lugha.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu mawasiliano yenye
kuzingatia kanuni za kisaru.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kueleza maana
na kutoa mifano
ya aina ya neno
lengwa kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
na kutoa mifano
ya aina ya
neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
na kutoa mifano
ya aina ya neno
lengwa kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
na kujaribu
kutoa mifano
ya aina ya neno
lengwa.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza maana
ya aina ya neno
lengwa.
Kutambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya aina
ya neno lengwa
kwa urahisi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
baadhi ya aina
ya neno lengwa.
Kutumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatumia
baadhi ya aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutumia aina ya
neno lengwa.
49
Kimeidhinishwa na KICD
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona mbali waketi karibu na ubao. Wale ambao
hawawezi kuona vitu vilivyo karibu nao waketi mbali na ubao ili waweze kuona
aina ya neno lengwa litakaloandikwa ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema watazame aina ya neno lengwa
likiigizwa darasani, wasome maelezo kuhusu aina hiyo ya neno kwenye ubao,
kiwambo cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi na kwenye chati.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kutambua aina ya neno lengwa kwa urahisi
wahusishwe katika shughuli zaidi za ujifunzaji. Pia, wapewe muda zaidi wa kujifunza
huku wakihimizwa kwa upendo ili wajithamini na kuchangamkia ujifunzaji. Hatua
yoyote wanayopiga katika ujifunzaji itambuliwe na mwalimu ili wawe na hamu ya
kujifunza zaidi.
Maelezo ya jumla
Mada hii inashughulikia viwakilishi na vielezi. Ujifunzaji wa viwakilishi na vielezi
hukuza utunzi wa sentensi sahihi na sanifu na huboresha mawasiliano.
Kiwakilishi ni neno ambalo linatumika badala ya nomino. Mwalimu atumie mifano
iliyo kwenye kitabu cha mwanafunzi kueleza maana ya neno kiwakilishi.
Vielezi hueleza vitendo. Mwalimu atumie mifano iliyo kwenye kitabu cha mwanafunzi
kueleza maana ya kielezi.
Kipindi cha 1: Viwakilishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 30)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kiwakilishi ili kukibainisha.
b) Kutambua viwakilishi katika kundi la maneno na sentensi.
Swali dadisi
Ni maneno gani ambayo hutumiwa badala ya nomino katika sentensi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kuelewa kuwa nomino na kiwakilishi haziwezi
kutumika katika sentensi moja. Kiwakilishi hutumika badala ya nomino.
Mapendekezo ya nyenzo za ufundishaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 30,
2. Breli,
3. Kikapu chenye kadi za maneno.
50
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu atumie michoro iliyo kwenye kitabu cha
mwanafunzi kuwaelekeza wanafunzi kuelewa maana ya neno kiwakilishi. Wanafunzi
watazame michoro hiyo wakiwa wawili wawili kisha wasome sentensi zilizo kando ya
kila mchoro. Mwalimu atathmini uelewa wao kwa kuwaelekeza wajadiliane kuhusu
maana ya viwakilishi. Mwalimu awaelekeze iwapo watakuwa na matatizo ya kueleza.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kusoma sentensi katika shughuli ya pili na wapigie
mistari viwakilishi. Shughuli hii itawasaidia wanafunzi kuweza kutambua viwakilishi
mbalimbali katika sentensi.
Majibu: yeye, wao, wangapi, hicho.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi jinsi ya kucheza mchezo wa
kuchagua viwakilishi kutoka kwenye kikapu cha maneno walichopewa katika kitabu
chao. Kila mwanafunzi aandike viwakilishi alivyochagua katika daari lake. Avitumie
viwakilishi hivyo kutunga sentensi sahihi.
Majibu: hiki, yeye, huyu, sisi
Mwalimu akubali sentensi zozote sahihi kutoka kwa wanafunzi. Sentensi hizo zitumie
viwakilishi vilivyo katika kikapu cha maneno kilicho kitabuni mwao.
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi atunge
sentensi tano sahihi zilizo na nomino. Aandike sentensi hizo upya bila kutumia
nomino. Badala yake atumie viwakilishi sahihi. Mwalimu akubali sentensi zozote
sahihi kisaru.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua viwakilishi kutoka
kwa maneno mengine.
2. Mwalimu asahihishe sentensi ambazo mwanafunzi ametunga kwa kutumia
viwakilishi walivyoonyeshwa na mwalimu.
Kipindi cha 2: Viwakilishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 32)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viwakilishi katika kundi la maneno na sentensi.
b) Kutumia viwakilishi ipasavyo katika sentensi.
ch) Kufahamu matumizi ya viwakilishi katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, kuna tofauti kati ya kiwakilishi na nomino?
51
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae chati yenye viwakilishi. Anaweza kutunga mifano ya sentensi
akitumia viwakilishi hivyo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Chati, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 32, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu amshirikishe mwanafunzi kumsomea mwanafunzi mwenzake sentensi
zilizo katika kitabu chao katika shughuli ya kwanza. Mwanafunzi atambue
viwakilishi katika sentensi hizo. Kila mwanafunzi atumie viwakilishi alivyotambua
kutunga sentensi sahihi. Wanafunzi wabadilishane madaari ili wazitathmini sentensi
walizotunga.
Mwalimu akubali sentensi zozote sahihi zitakazotolewa na wanafunzi. Sentensi hizo
zitumie viwakilishi walivyotambua.
Baada ya uelewa wa viwakilishi, mwanafunzi anaweza kuvipigia mistari viwakilishi
katika kifungu cha shughuli ya pili. Baada ya kuvipigia viwakilishi mistari, wanafunzi
katika vikundi watunge sentensi kwa kutumia viwakilishi walivyovipigia mistari.
Waandike sentensi hizo kwenye chati. Mmoja wao awasomee wanafunzi wengine
sentensi walizoandika kwenye chati ili wazisikilize na kuzitathmini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwalimu atathmini kazi ya
ziada ya kila mwanafunzi. Akubali sentensi zozote ambazo mwanafunzi atatunga kwa
kutumia viwakilishi mbalimbali.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua viwakilishi katika
sentensi na kifungu.
2. Mwalimu atathmini namna ambavyo mwanafunzi anatumia viwakilishi
kutunga sentensi.
Aina za maneno
Kipindi cha 1: Vielezi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 33)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kielezi ili kukibainisha.
b) Kutambua vielezi katika kundi la maneno na sentensi.
ch) Kutumia vielezi ipasavyo katika mawasiliano.
d) Kuonea fahari matumizi ya vielezi katika sentensi.
52
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Ni maneno gani yanaweza kutumiwa kutoa habari zaidi kuhusu vitenzi
unavyojua?
2. Unafanyaje shughuli zako za kila siku?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vielezi ni maneno ambayo hueleza zaidi kuhusu vitenzi. Michoro kwenye kitabu cha
mwanafunzi inaonyesha jinsi vitendo mbalimbali hufanywa, kwa mfano: mchoro wa
kobe anayetembea polepole na swara anayekimbia haraka/upesi, mchoro wa mtoto
anayekula vibaya, na mchoro wa mtoto anayekula vizuri. Maneno polepole, haraka/
upesi, vibaya na vizuri ni mifano ya vielezi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
1. Video za watu wanaoigiza wakitumia vielezi mbalimbali,
2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 3,
3. Breli, 4. Projekta, 5. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kuchunguza michoro iliyo katika shughuli ya kwanza
katika kitabu chao. Wanafunzi wajadili mwendo wa wanyama katika michoro hiyo.
Pia, wajadili jinsi watoto walio katika michoro hiyo wanavyokula. Watunge sentensi
sahihi kwa kila mchoro.
Majibu tarajiwa:
1. Kobe anatembea polepole. 2. Swara anakimbia haraka/upesi.
3. Mtoto anakula vibaya. 4. Mtoto anakula vizuri/kistaarabu.
Vielezi vinavyoendana na michoro hiyo vikubalike. Mwalimu awaelekeze wanafunzi
kujadiliana kuhusu maana ya vielezi. Wanafunzi waelezane kuhusu watu wa familia
zao wanaotembea polepole, upesi, wanaokula vizuri na wale wanaokula vibaya.
Mwalimu awapange wanafunzi kwenye vikundi kisha waigize vitendo mbalimbali
vilivyotajwa katika kitabu chao katika shughuli ya pili. Mwalimu atathmini utendaji
wa wanafunzi. Maigizo yatamsaidia mwanafunzi kukuza ujasiri wake wa kutenda
vitendo na kuzungumza mbele ya wanafunzi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaonyeshe wanafunzi video yenye vitendo
mbalimbali vinavyotendwa kwa njia mbalimbali. Video hii ni ya kuwasaidia wanafunzi
kufahamu zaidi matumizi ya vielezi. Baada ya kutazama video hiyo, watunge sentensi
sahihi kwa kutumia vielezi kuhusu vitendo walivyotazama.
Katika shughuli ya nne, mwalimu awaelekeze wanafunzi kupigia mistari vielezi katika
kifungu walichopewa kitabuni mwao kuhusu Anyango mrembo. Mwalimu ahakikishe
53
Kimeidhinishwa na KICD
kila mwanafunzi anashiriki katika shughuli hii ya kutambua vielezi katika kifungu.
Majibu tarajiwa ya shughuli ya nne: sana, kasi, polepole, upesi.
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kutunga sentensi
kumi sahihi akitumia vielezi mbalimbali akieleza kuhusu chakula anachokipenda.
Mwanafunzi amsomee mlezi au mzazi wake ili kutathmini sentensi zake. Mwanafunzi
azitumie sentensi alizotunga kubuni kifungu cha aya moja. Kifungu hicho kihusu
chakula anachopenda. Mwalimu atathmini kifungu kilichoandikwa na mwanafunzi.
Kifungu kilenge mada kuhusu chakula ambacho mwanafunzi anakipenda na atumie
vielezi mbalimbali.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini mwanafunzi alivyoigiza akitumia vielezi mbalimbali.
2. Mwalimu atathmini kifungu ambacho mwanafunzi alitunga akitumia vielezi.
3. Mwalimu achunguze jinsi ambavyo mwanafunzi anatumia vielezi katika
mawasiliano.
Kipindi cha 2: Vielezi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 35)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vielezi katika kundi la maneno na sentensi.
b) Kutumia vielezi ipasavyo katika mawasiliano.
ch) Kuonea fahari matumizi ya vielezi katika sentensi.
Swali dadisi
Je, vielezi hutumika vipi katika sentensi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu atayarishe kadi atakazotumia katika kipindi hiki. Kadi hizi ziwe za rangi
nyeupe na nyekundu au rangi nyingine mbili tofauti. Ikiwa hatapata kadi za rangi
hizo, anaweza kutumia vifaa vingine vyenye rangi mbili tofauti. Awaonyeshe wanafunzi
jinsi ya kucheza mchezo wa kadi wa kutambua vielezi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 35, 2. Breli, 3. Kikapu chenye kadi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua vielezi vilivyo
kwenye mviringo ulio na maneno. Wanafunzi watumie vielezi hivyo kutunga sentensi
54
Kimeidhinishwa na KICD
ubaoni. Mwalimu pamoja na wanafunzi wengine watathmini sentensi hizo.
Mwalimu awapange wanafunzi wawili wawili ili waigize vitendo mbalimbali ambavyo
vimetajwa kwenye shughuli ya pili. Mwanafunzi mmoja aigize vitendo hivyo na
mwenzake atunge sentensi sahihi kueleza vitendo hivyo kwa kutumia vielezi sahihi.
Katika vikundi, mwalimu awaelekeze wanafunzi kucheza mchezo wa kadi katika
shughuli ya tatu. Wanafunzi wote wahusishwe katika mchezo huu.
Wanafunzi katika vikundi vyao wapewe kadi mbili, nyeupe na nyekundu (au za
rangi nyingine au vifaa vingine). Mwalimu akitaja kielezi mwanafunzi mmoja (kwa
makubaliano na wengine) katika kila kikundi ainue kadi nyeupe. Mwalimu akitaja
neno lisilo kielezi mwanafunzi ainue kadi nyekundu. Kila kikudi kipewe alama za
majibu sahihi ubaoni.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi asaidiwe
na mlezi au mzazi wake kutunga sentensi sahihi kwa kutumia nomino pamoja
na vielezi alivyopewa katika kitabu chao. Baada ya kutunga sentensi, mwanafunzi
aziandike katika daari lake. Atawasomea wanafunzi wenzake sentensi alizotunga ili
wazisahihishe na kuziboresha. Mwalimu atathmini sentensi zilizotungwa na wanafunzi.
Ahakikishe wamezingatia matumizi sahihi ya nomino na vielezi walivyopewa katika
kitabu chao.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini namna mwanafunzi anavyojibu maswali.
2. Mwalimu atazame utendaji wa mwanafunzi katika maigizo.
3. Mwalimu atathmini utunzi wa sentensi wa mwanafunzi akitumia vielezi.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. a) Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Majibu yahusishe maamkuzi ya
asubuhi kama vile: Habari ya asubuhi?, Umeamka vipi?, Umelala vipi?
b) Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Majibu tarajiwa: majaliwa/
majaaliwa/inshallah.
2. a) Mwalimu akubali mpangilio sahihi wa maneno waliyopewa kwa mfuatano wa
kialfabeti. Mpangilio sahihi ni: bibi, kamusi, nidhamu, rununu, zawadi.
b) Mwalimu atathmini maana ambazo mwanafunzi ataeleza. Maana hizo ziwe
sahihi. Anaweza kutumia kamusi. Mifano ya majibu tarajiwa ni: bibi (mke
au nyanya), kamusi (kitabu maalumu chenye maana za maneno mbalimbali
yaliyopangwa kialfabeti), nidhamu (adabu, heshima), rununu (simu ya
55
Kimeidhinishwa na KICD
mkononi), zawadi (kitu anachopewa mtu kwa kutenda mema au kuwa mshindi).
3. Ninayo/Yashapita/Nishapoa
4. Mwalimu atathmini insha ambayo mwanafunzi ataandika. Sharti insha hiyo ihusu
sherehe ya mwaka mpya. Pia, lazima insha hiyo izingatie muundo sahihi wa insha
ya masimulizi.
5. Majibu yoyote sahihi kuhusu sababu za kunawa mikono yakubalike. Kwa mfano:
Watu hunawa mikono ili kuondoa uchafu unaoweza kusababisha maradhi ya tumbo.
6. Majibu yoyote sahihi kuhusu nidhamu ya mezani ya kutozungumza mtu akila
yakubalike. Kwa mfano: Mtu hafai kuongea akila kwa sababu anaweza kusakamwa
na chakula. Pia, anaweza kuwarushia wenzake vipande vipande vya chakula
anachotafuna hivyo kuwachafua au kuwaudhi.
7. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi atatunga. Sharti sentensi hizo
ziwe sahihi kisaru na zihusishe viwakilishi. Mifano ni kama vile:
a) Mimi ninakula wali.
b) Wale wanaenda shuleni.
ch) Hivi vimepikwa na kuiva vizuri.
8. Mwalimu akubali vielezi vyovyote sahihi ambavyo mwanafunzi atataja. Mifano
ni kama vile: andika vizuri, tembea haraka, cheka sana, kimbia upesi. Mwalimu
atathmini aya moja ya kifungu ambayo wanafunzi watatunga. Sharti aya hiyo
ihusishe vielezi alivyotaja. Sentensi katika aya hiyo ziwe sahihi kisaru na aya nzima
itiririke.
9. Mwalimu atathmini kifungu cha aya atakachotumiwa na mwanafunzi mtandaoni.
Mwalimu ahakikishe kuwa vielezi katika aya hiyo vimeandikwa kwa chapa koza.
10. Mwalimu akubali majina ya vifaa mbalimbali ambavyo hutumiwa wakati wa
maakuli. Mifano ni kama vile: kijiko, kisu, uma, sahani, bilauri, bakuli, sufuria,
gilasi, buli, sinia n.k.
56
MAVAZI
3
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 38)
A. Kusikiliza na Kuzungumza: Matamshi Bora
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vitendawili vyenye sauti radidi kwenye orodha.
b) Kutamka maneno yenye sauti radidi katika vitendawili lengwa.
ch) Kutega na kutegua vitendawili vyenye sauti radidi ili kujenga matamshi bora.
d) Kuchangamkia matumizi ya vitendawili vyenye sauti radidi kama njia ya
kujenga utamkaji bora wa maneno.
Swali dadisi
Je, unajua kutega na kutegua vitendawili gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
kutega na kutegua vitendawili kwenye vikundi.
Uwazaji kina na utatuzi wa matatizo - unakuzwa mwanafunzi anapokiria
kuhusu majibu ya vitendawili.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vyombo vya kidijitali
kusikiliza vitendawili vikitegwa na kuteguliwa.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anapotega na kutegua vitendawili.
Uhusiano na masuala mtambuko
Umoja wa kijamii kutokana na kushiriki katika vikundi.
Stadi za maisha kutokana na maudhui katika vitendawili.
Uhusiano na maadili
Heshima - mwanafunzi anapochangamkia maoni ya mwenzake.
Umoja - wanafunzi wanapofanya kazi katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Somo la Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili - masomo haya yana mada
kuhusu vitendawili.
57
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anatarajiwa kukabiliana na masuala mbalimbali yanayohitaji uwazaji wa
kina katika jamii.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua na
kutamka kwa
usahihi maneno
yenye sauti
radidi katika
vitendawili.
Mwanafunzi
anatambua na
kutamka kwa
usahihi na
urahisi maneno
yenye sauti
radidi katika
vitendawili.
Mwanafunzi
anatambua na
kutamka kwa
usahihi maneno
yenye sauti
radidi katika
vitendawili.
Mwanafunzi
anatambua
maneno
yenye sauti
radidi katika
vitendawili na
kutamka baadhi
ya maneno hayo.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
maneno
yenye sauti
radidi katika
vitendawili.
Kutega na
kutegua
vitendawili
vyenye sauti
radidi kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatega na
kutegua
vitendawili
vyenye sauti
radidi kwa
usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatega na
kutegua
vitendawili
vyenye sauti
radidi kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatega na
kutegua baadhi
ya vitendawili
vyenye sauti
radidi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutega na
kutegua
vitendawili
vyenye sauti
radidi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema au kusikia wategue vitendawili kwa kuandika
majibu sahihi au kulinganisha vitendawili na majibu yao au michoro sahihi. Pia,
wapigie mistari sauti radidi kwenye maneno husika huku walio na uwezo wa
kusema wakiyatamka.
Upande mwingine, wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli au kusikiliza
vitendawili na viteguzi vyao vikisomwa na mwalimu, wanafunzi wenzao au kutoka
kwenye kinasasauti.
Wanafunzi wenye uwezo wa kungamua wanayojifunza kwa urahisi baada ya
kushirikishwa katika shughuli za ujifunzaji wapewe fursa ya kubuni vitendawili
zaidi pamoja na kuwasaidia wenzao kupata viteguzi vya vitendawili hivyo.
Upande mwingine, wanafunzi wanaochukua muda zaidi kabla ya kufahamu
wanayojifunza washirikishwe katika shughuli zaidi na kupewa muda zaidi wa
kujifunza.
Iwapo baadhi ya wanafunzi wana mahitaji ya kisaikolojia kutokana na matukio
wanayokumbana nayo katika jamii, mwalimu ayafahamu mahitaji hayo ili awasaidie
kujiamini na kuchangamkia ujifunzaji.
58
Maelezo ya jumla
Mada hii inashughulikia vitendawili vyenye sauti radidi. Dhana ya vitendawili ni
muhimu kwa wanafunzi. Vitendawili vitawasaidia wanafunzi kuwaza kwa kina ili
kupata viteguzi sahihi vya vitendawili. Pia, vitendawili huweza kumsaidia mwanafunzi
kuyafahamu mazingira yake zaidi.
Matamshi sahihi ya maneno pia yanalengwa katika mada hii. Hivyo, ni vizuri
mwanafunzi aweze kutambua sauti radidi katika vitendawili alivyopewa na kuzitamka
kwa usahihi unaotakikana.
Kipindi cha 1: Vitendawili vya uradidi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 38)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vitendawili vyenye sauti radidi kutoka kwenye orodha.
b) Kutamka maneno yenye sauti radidi kwa usahihi.
ch) Kushirikiana na wenzake katika vikundi kutambua na kutamka sauti radidi
zilizotumika kwenye vitendawili.
Maswali dadisi
1. Je, unajua vitendawili vipi?
2. Unakiri ni kwa nini watu hutega na kutegua vitendawili?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vitendawili ni semi fupi ambazo huwa ni maswali yanayomhitaji mtu kukiria kwa
undani ili kupata majibu (viteguzi). Ili kupata jibu sahihi la kitendawili, mtu anahitaji
kufananisha hali, mambo au vitu halisi na swali la kitendawili.
Uradidi kwa upande mwingine ni hali ya dhana fulani kujirudiarudia. Vitendawili
vinaweza kuradidi sauti au maneno fulani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kanda yenye vitendawili vilivyorekodiwa, 2. Breli,
3. Rununu, 4. Kinasasauti au rekoda, 5. Tarakilishi,
6. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 38.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wataje
vitendawili ambavyo wanavijua. Ahakikishe kuwa majibu yanayotolewa na wanafunzi
ni vitendawili wala si methali au semi nyinginezo. Wanafunzi wataje vitendawili hivyo
huku wenzao wakitoa viteguzi sahihi. Wanafunzi wanapotaja vitendawili wanavyovijua,
59
wanajenga umilisi wao wa kujiamini na pia mawasiliano yao yanaimarika.
Katika vikundi, mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa
kujibu maswali yaliyo katika kitabu chao. Mwalimu awagawe wanafunzi kulingana na
idadi na mahitaji yao darasani. Wanafunzi wakiri na kujibu maswali waliyopewa.
Majibu tarajiwa: yai, mate, ngoma.
Katika shughuli ya pili, wanafunzi watumie majina ya michoro waliyopewa kutegua
orodha ya vitendawili walivyopewa. Uwazaji wa kina na utatuzi wa matatizo
utaimarishwa na shughuli hii. Mwalimu awaongoze wanafunzi ili waweze kutoa
majibu sahihi kwa vitendawili walivyopewa.
Majibu tarajiwa: 1. buibui 2. viatu 3. nguo/mavazi 4. bombo 5. mshipi 6. mwavuli
Mwalimu awaongoze wanafunzi waelewe maana ya uradidi, vitendawili na vitendawili
vya uradidi. Awaongoze wanafunzi kusoma maelezo yaliyotolewa kwenye kitabu chao
ili waelewe dhana hizo. Baada ya kusoma maelezo hayo, mwalimu awaulize maswali
mepesi kuhusu dhana hizo ili kutathmini uelewa wa walichosoma.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kuifanya shughuli ya tatu. Awaongoze wanafunzi
kusikiliza vitendawili vitakavyochezwa kutoka kwenye rekoda. Wanafunzi wasikilize
kwa makini vitendawili vilivyorekodiwa. Mwalimu anaweza kutumia rununu au
tarakilishi kuwachezea wanafunzi vitendawili mbalimbali vyenye sauti radidi. Ni
vyema mwalimu ahakikishe ameandaa rekodi ya vitendawili kabla ya kipindi. Pia,
anaweza kumpa kila mwanafunzi fursa ya kutumia kinasasauti huku akiwaongoza.
Kwa njia hii, ujuzi wao wa kutumia vyombo vya kidijitali utajengeka. Mwalimu arudie
vitendawili hivyo kisha awaulize wanafunzi watamke sauti au maneno radidi katika
vitendawili hivyo. Awaongoze wanafunzi ambao watapata matatizo katika kutambua
sauti au maneno hayo radidi. Mwanafunzi aandike katika daari lake vitendawili
alivyosikiliza.
Mifano ya vitendawili vya kurekodi
1. Kuku wangu anatagia mibani. - nanasi
2. Popoo mbili zavuka mto. - macho
3. Nipo hapa mpaka niondolewe. - gogo
4. Simwachi yaya wangu wakati wa masika. - mwavuli
5. Anayekigusa hakitumii, anayekitumia hakioni. sanda
6. Babu ana kabuti la chuma. mzee kobe
Mwisho, mwalimu amwelekeze mwanafunzi afanye kazi ya ziada akishirikiana na
mlezi au mzazi wake kutunga vitendawili vyenye sauti au maneno radidi. Mwanafunzi
aviandike vitendawili hivyo katika daari lake kisha awasomee wenzake pamoja na
mwalimu ili wavitathmini darasani.
60
Tathmini
1. Mwalimu atathmini utamkaji wa sauti radidi na maneno yenye uradidi katika
vitendawili.
2. Mwalimu atathmini uteguzi wa vitendawili kwa kutumia viteguzi sahihi.
Kipindi cha 2: Vitendawili vya uradidi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 40)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutega na kutegua vitendawili vyenye sauti radidi kama njia ya kujenga
matamshi bora.
b) Kuchangamkia matumizi ya vitendawili vyenye sauti radidi kama njia ya
kujenga matamshi bora.
ch) Kushirikiana na wenzake katika vikundi ili kutega na kutegua vitendawili vya
uradidi ili kukuza matamshi bora.
Swali dadisi
Unajua kutega na kutegua vitendawili gani vya uradidi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vitendawili vina kitangulizi maalumu ambacho hutumika mwanzoni mwa swali la
kitendawili. Mfano:
Mtegaji: Kitendawili?
Mteguzi: Tega!
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 40, 2. Breli, 3. Tarakilishi, 4. Rununu.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi yao na tarakilishi
zilizo darasani. Katika vikundi hivyo, wanafunzi watafute mtandaoni picha za
konokono na nanasi kama walivyoagizwa kitabuni katika shughuli ya kwanza.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watumie tarakilishi za breli. Wanafunzi wasio
na uwezo wa kusikia wapewe maagizo kwa kuandika. Wanafunzi wanaochukua muda
zaidi kuelewa wapewe muda zaidi. Mwalimu awaongoze wanafunzi wajadili sifa
mbalimbali za picha hizo. Shughuli hii itawasaidia wanafunzi kukuza ushirikiano na
ujuzi wa kidijitali utaimarika zaidi.
61
Mwalimu ahakikishe wanafunzi hawasakuri matini tofauti na zisizo salama
mtandaoni. Kwa kutumia kitangulizi walichopewa na mwalimu, wanafunzi watege na
kutegua vitendawili kwa kutumia majina ya picha hizo. Wazingatie sauti radidi husika.
Mifano ya vitendawili tarajiwa:
1. Achora lakini hajui achoracho. konokono
2. Kuku wangu atagia mibani. nanasi
Katika shughuli ya pili, wanafunzi watumie kitangulizi sahihi kutegeana vitendawili
vitano au zaidi na kuvitegua wakiwa wawili wawili. Mwalimu ahakikishe kwamba
vitendawili vinavyotegwa ni vya uradidi na majibu yanayotolewa ni sahihi. Mwalimu
anaweza kuwapa wanafunzi nafasi ya kutegeana na kutegua vitendawili mbele ya darasa
huku wengine wakisikiliza. Jambo hili litasaidia kuzua hamu ya kushindana na kuleta
mchangamko darasani. Pia, mwalimu ahakikishe kuwa matamshi bora yanazingatiwa
katika shughuli nzima ya utegaji na uteguzi huo. Mwalimu akubali vitendawili vyovyote
vyenye uradidi wa sauti au maneno ambavyo wanafunzi watatunga.
Kila mwanafunzi ashiriki katika shughuli ya tatu. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi
anachagua jibu sahihi kwa vitendawili alivyopewa kitabuni mwao.
Majibu: 1. kisogo 2. Mungu 3. sindano 4. kinywa 5. samaki
Mwalimu anaweza kuhitimisha kipindi hiki kwa kuwahimiza wanafunzi kujenga
tabia ya kutumia vitendawili ili kuchangamsha bongo. Pia, mwalimu awakumbushe
wanafunzi kuwashirikisha walezi, wazazi au raki kufanya kazi ya ziada. Wajadiliane
kuhusu umuhimu wa vitendawili. Pia, mlezi au mzazi amtajie mwanafunzi vitendawili
vitatu kwa lugha yake ya kwanza. Wavitafsiri vitendawili hivyo kwa Kiswahili.
Wanafunzi ambao lugha yao ya kwanza ni Kiswahili wategewe vitendawili kwa lugha
ya Kiingereza kisha wavitafsiri kwa Kiswahili.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini utegaji na uteguzi wa vitendawili vya uradidi.
2. Mwalimu atathmini utungaji wa vitendawili vya uradidi.
3. Mwalimu atathmini ushirikiano wa mwanafunzi na wenzake katika kutega na
kutegua vitendawili.
62
B. Kusoma: Kusoma kwa ufahamu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 41)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa mada lengwa uliotumika katika hadithi ili kuimarisha
ufahamu.
b) Kutumia msamiati lengwa kwa usahihi katika sentensi.
ch) Kusoma kifungu kwa ufasaha ili kupata ujumbe uliolengwa.
d) Kuonyesha ufahamu wa kifungu kwa kutoa muhtasari na kujibu maswali.
e) Kujenga mazoea ya usomaji bora katika maisha ya kila siku.
Maswali dadisi
1. Je, unapenda mavazi gani?
2. Ni mambo gani mtu huzingatia anapochagua mavazi yake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
katika kutazama vibonzo, mavazi na michoro kwenye video na tarakilishi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapochora mavazi mbalimbali.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anaposhiriki mijadala darasani na kujibu
maswali kwa usahihi.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake kwa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja.
Umoja wa kijamii kutokana na kushiriki katika vikundi.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili - masomo haya yanakuza stadi ya
kusoma.
63
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu mavazi yafaayo.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kueleza na
kutumia
msamiati
lengwa kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anaeleza msamiati
ulio katika kifungu
na kuutumia
kwa ufasaha na
wepesi.
Mwanafunzi
anaeleza
msamiati ulio
katika kifungu
na kuutumia
kwa ufasaha.
Mwanafunzi
anaeleza baadhi
ya msamiati ulio
katika kifungu
na kuutumia.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza
msamiati
ulio katika
kifungu.
Kusoma kwa
ufasaha na
kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma kwa
ufasaha na wepesi
kwa kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma kwa
ufasaha na
kwa kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma
sehemu ya
kifungu.
Mwanafunzi
anajaribu
kusoma
sehemu ya
kifungu.
Kuonyesha
ufahamu wa
ujumbe kwa
kujibu maswali
na kutoa
muhtasari kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaonyesha
ufahamu wa
kifungu kwa
kujibu maswali
yanayotokana
na kifungu na
kutoa muhtasari
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anaonyesha
ufahamu wa
kifungu kwa
kujibu maswali
yanayotokana
na kifungu na
kutoa muhtasari
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anajibu baadhi
ya maswali
yanayotokana
na kifungu.
Mwanafunzi
anajaribu
kujibu maswali
ya ufahamu.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema, wasikilize wengine wakisoma na kujibu
maswali ya ufahamu kwa kuandika.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli au wasikilize wengine
wakisoma kifungu na kujibu maswali ya kifungu kwa mdomo.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia, wamtazame mwalimu akitumia lugha ya
ishara na kujibu maswali ya ufahamu kwa ishara au wafuate maagizo kutoka ubaoni.
Wanafunzi wanaochukua muda mrefu kujifunza wapewe muda zaidi ili kukamilisha
shughuli zao. Hii inaweza kufanywa wakati wa mapumziko.
Wanafunzi walio na uwezo wa kuelewa kwa wepesi wapewe shughuli zaidi ili
wajishughulishe nazo.
64
Maelezo ya jumla
Mada hii inashughulikia usomaji ili kujenga na kukuza msamiati lengwa ambao ni wa
mavazi mbalimbali. Wanafunzi wasome kifungu kwa ufasaha ili kupata uelewa zaidi.
Ili kutathmini uelewa wa usomaji, mwalimu anaweza kumwuliza mwanafunzi atoe
muhtasari wa alichosoma.
Kipindi cha 1: Kifungu cha hadithi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 41)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusoma kifungu lengwa ili kupata msamiati lengwa.
b) Kutoa muhtasari wa kifungu kilichosomwa.
ch) Kujibu maswali ya kifungu kwa usahihi.
Maswali dadisi
1. Je, umevaa mavazi gani?
2. Je, unakiri ni kwa nini watu huvaa mavazi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vazi ni nguo yoyote inayovaliwa mwilini. Mavazi hutumika kusitiri uchi. Yapo
mavazi yanayovaliwa na wanawake na mengine yanayovaliwa na wanaume. Mavazi
yanayovaliwa na wanawake ni kama vile: rinda, sketi, kanchiri na mengineyo.
Mavazi yanayovaliwa na wanaume ni kama vile: suruali, shati na mengineyo. Kuna
mavazi ya majira ya joto na mavazi ya majira ya baridi. Wakati wa baridi tunavaa mavazi
mazito mazito kama vile sweta na koti ili kujikinga na baridi. Wakati wa joto tunavaa
mavazi mepesi kama vile shati, vesti, blauzi na mengineyo.
Mtu anapochagua mavazi ya kuvaa, sharti azingatie majira, mazingira, utamaduni na jinsia.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kupenda mavazi ya heshima yanayokubaliwa na jamii.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 41,
2. Michoro ya mavazi au picha,
3. Mavazi halisi,
4. Tarakilishi,
5. Kadi zenye majina ya mavazi mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwanafunzi na mwalimu washiriki katika shughuli ya kwanza. Mwanafunzi wa kike
na kiume au wote wawili wasimame mbele ya darasa. Wanafunzi wengine wataje mavazi
waliyovaa. Wanafunzi wataje mavazi wanayoona pekee. Majibu tarajiwa: kaptura,
65
rinda, sweta, blauzi, viatu, soksi, tai na mengineyo. Mwalimu anaweza kutumia mavazi
halisi yanayovaliwa na wanawake na wanaume au awaonyeshe wanafunzi picha au
michoro ya mavazi ya wanafunzi (sare).
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Awaongoze wanafunzi kushiriki katika shughuli ya pili. Wanafunzi wajadili michoro
waliyopewa kitabuni mwao na kuandika majina ya michoro hiyo. Wajadili mavazi
hayo huvaliwa na akina nani kisha watumie majina ya mavazi hayo kutunga sentensi
sahihi. Shughuli hii itasaidia kujenga na kukuza ushirikiano baina ya wanafunzi katika
vikundi.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona wanaweza kupewa mavazi halisi wakayatambua.
Majina ya michoro: surupwenye/bwelasuti, koa, kanzu, kizibao, kanchiri na tai.
Surupwenye ni vazi lenye suruali na shati zilizoshikana na huvaliwa na wanawake
na wanaume wakati wa kufanya kazi ili kuzuia mavazi mengine kuchafuka.
Koa ni aina ya vazi linalovaliwa kichwani na wanawake na wanaume.
Kanzu ni vazi refu kama gauni linalovaliwa na wanaume hasa wa kiislamu.
Kizibao ni vazi aina ya koti lililo fupi na lisilo na mikono.
Kanchiri ni vazi la kike linalovaliwa kifuani kushikilia maziwa.
Tai ni vazi ambalo ni jembamba na aghalabu refu linalovaliwa shingoni chini ya
ukosi wa shati au blauzi na kufungwa fundo shingoni.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi wasome kifungu kilicho katika shughuli ya tatu
ili kufahamu ujumbe wake. Mwalimu anaweza kumteua mwanafunzi mmoja asome
kifungu hicho kisha wengine wasome baada yake. Awasaidie wanafunzi kutamka
maneno ambayo yanawatatiza katika kifungu. Baadaye, mwalimu awaongoze
wanafunzi kujibu maswali ya ufahamu kwa usahihi pamoja na kila mwanafunzi
kuandika muhtasari wa kifungu husika.
Majibu tarajiwa ya ufahamu:
1. Ili asije akavalia kinyume na maadili na kujikosea heshima.
2. Kusitiri uchi, kujikinga dhidi ya baridi, kujikinga dhidi ya jua kali n.k.
3. Umri, mazingira, jinsia, majira, hali iliyoko.
4. Sweta/fulana, kabuti, chepeo, viatu, soksi, tai, kaptura, suruali n.k.
5. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi.
6. Mwalimu atathmini muhtasari wa kifungu atakaoandika mwanafunzi ili
kudhihirisha uelewa wake wa kifungu alichosoma.
Mwalimu ahitimishe somo kwa kumpa mwanafunzi kazi ya ziada itakayomshirikisha
mlezi au mzazi wake. Mlezi au mzazi amtajie mwanafunzi baadhi ya mavazi ambayo
wanawake na wanaume huvalia katika jamii yao. Pia, mwanafunzi anaweza kutumia
mtandao. Awaeleze wenzake darasani katika kipindi kijacho.
66
Tathmini
1. Mwalimu atathmini usomaji wa kifungu kwa ufasaha.
2. Mwalimu atathmini majibu ya maswali ya ufahamu.
3. Mwalimu atathmini uandishi wa muhtasari wa kifungu.
Kipindi cha 2: Kifungu cha hadithi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 43)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutunga sentensi kwa kutumia msamiati wa mavazi.
b) Kujenga mazoea ya usomaji katika maisha.
Swali dadisi
Je, wewe huzingatia mambo yapi unapochagua mavazi ya kuvaa?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awachangamshe wanafunzi wafahamu majina ya mavazi mbalimbali.
Anaweza kuwaonyesha picha, magazeti, tarakilishi, rununu, vitabu vilivyo na mavazi
mbalimbali. Pia, anaweza kuwaonyesha wanafunzi wafanyakazi shuleni waliovalia
mavazi mbalimbali.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Vipakatalishi/tarakilishi/rununu,
2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 43,
3. Kadi za maneno zenye majina ya mavazi mbalimbali,
4. Michoro au picha za mavazi mbalimbali,
5. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kucheza mchezo wa kadi katika shughuli ya kwanza.
Kwa maelekezo ya mwalimu, mwanafunzi mmoja achukue kadi kutoka kikapuni kisha
wengine wasome jina la vazi lililoandikwa kwenye kadi hiyo. Wanafunzi waeleze vazi
hilo huvaliwa na akina nani. Mchezo huu uendelee hadi kadi zote kikapuni zichukuliwe
na kusomwa. Mchezo huu utaimarisha ushirikiano wa wanafunzi darasani. Mwalimu
aandae kadi hizi kabla ya kipindi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kuchora mavazi yoyote matatu katika daari
lake kulingana na shughuli ya pili. Baadaye, mwanafunzi awaonyeshe wenzake na
mwalimu michoro yake ili waitathmini. Shughuli hii itakuza ubunifu wa mwanafunzi.
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kisha wajadiliane kuhusu umuhimu wa
mavazi mbalimbali waliyochora.
67
Majibu tarajiwa: 1. kujitambulisha 2. kuzuia uchafu 3. kuonyesha utamaduni
4. kuonyesha urembo 5. kusitiri uchi n.k.
Mwalimu akubali majibu yoyote sahihi kutoka kwa wanafunzi yanayohusu umuhimu
wa mavazi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi kuwasha tarakilishi na
kusakura picha za watu waliovaa mavazi tofauti tofauti mtandaoni. Mwalimu awasaidie
wanafunzi wanaotatizika. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutaja mavazi yaliyovaliwa
na watu hao.
Mwalimu akubali majibu yoyote ya wanafunzi yaliyo sahihi kulingana na picha
watakazotazama mtandaoni.
Mwalimu anaweza kuhitimisha somo kwa kuwaelekeza wanafunzi kufanya kazi ya
ziada. Kila mwanafunzi achore sare yake na aipake rangi sahihi. Anaweza kusaidiwa
na mlezi au mzazi wake. Baadaye, mwanafunzi aandike kifungu cha aya moja kuhusu
sare ya shule yake. Amsomee mlezi au mzazi wake kifungu hicho ili akitathmini.
Mwalimu atathmini kazi ya ziada ya mwanafunzi kwa kuzingatia alivyochora na rangi
alizopaka. Wanafunzi wanaweza kuonyeshana michoro yao ili waitathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini utambuaji wa mavazi mbalimbali na yanakovaliwa
mwilini.
2. Mwalimu atathmini utungaji sahihi wa sentensi kwa kutumia msamiati wa
mavazi.
3. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuchora na kupaka rangi sare
yake.
CH. Kuandika: Kuandika kwa kutumia tarakilishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 44)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sehemu mbalimbali za tarakilishi zinazotumika kupiga chapa.
b) Kufungua na kufunga tarakilishi ili kuandika kazi na kuhifadhi.
ch) Kuandika mada lengwa kwa kutumia tarakilishi.
d) Kuhariri kazi yake kwa kuzingatia uakisho ufaao.
e) Kuhifadhi kazi iliyoandikwa kwenye tarakilishi.
f) Kujenga mazoea ya kuandika kwa kutumia tarakilishi na kuhifadhi kazi yake ya
maandishi.
68
Swali dadisi
Je, ni sehemu zipi za tarakilishi unazotumia kuandika?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake katika vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia tarakilishi kuandika na
kuhifadhi kazi yake kwenye faili.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapotagusana na vyombo vya
kidijitali kama vile kutumia tarakilishi, kipakatalishi n.k.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya maendeleo endelevu - mwanafunzi anatumia ujuzi wa kiteknolojia
kufanikisha uandishi wake.
Uhusiano na maadili
Ushirikiano - unakuzwa kupitia kwa kazi za vikundi.
Uwajibikaji - mwanafunzi anaweza kuhifadhi au kutunza vyombo vya kidijitali.
Uhusiano na masomo mengine
Somo la Sayansi na Teknolojia na Kiingereza - masomo haya yanahimiza
matumizi ya tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
teknolojia na matumizi yake kurahisisha shughuli za kila siku.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua sehemu
mbalimbali za
kupigia chapa,
kutumia sehemu
hizo kupiga
chapa, kuhariri
na kuhifadhi kazi
kwenye tarakilishi.
Mwanafunzi
anatambua sehemu
mbalimbali za
tarakilishi za kupigia
chapa, anapiga
chapa, anahariri
na kuhifadhi kazi
kwenye tarakilishi
kwa urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
sehemu
mbalimbali
za tarakilishi,
anapiga chapa,
anahariri na
kuhifadhi
kazi kwenye
tarakilishi.
Mwanafunzi
anatambua
sehemu
mbalimbali
za tarakilishi
na anapiga
chapa.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
sehemu za
tarakilishi
na anajaribu
kupiga chapa.
69
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasioweza kuona wapige chapa kwa kutumia tarakilishi zenye breli.
Wanafunzi walio na uwezo wa kutumia tarakilishi kwa wepesi wapewe mazoezi zaidi
ili kuimarisha maarifa yao ya matumizi ya vifaa vya kidijitali. Wale wanaochukua
muda zaidi kuelewa matumizi ya tarakilishi wapewe muda zaidi ili kupata mazoea ya
matumizi ya vifaa vya kidijitali.
Maelezo ya jumla
Somo hili la kuandika kwa kutumia tarakilishi linalenga kumpa mwanafunzi stadi
za kuandika kwa kutumia tarakilishi. Uandishi huo uzingatie uakishaji bora na
maendelezo mwafaka ya maneno na sentensi.
Kipindi cha 1: Kutumia tarakilishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 44)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sehemu mbalimbali za tarakilishi zinazotumiwa kupigia chapa.
b) Kufunga na kufungua tarakilishi.
ch) Kuandika kwa kutumia tarakilishi.
d) Kuhifadhi kazi katika faili kwenye tarakilishi.
Maswali dadisi
1. Je, tarakilishi ni nini?
2. Je, tarakilishi hutumiwa kufanya nini?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Tarakilishi ni mtambo wa kielektroniki unaohifadhi na kuchanganua data, taarifa na
ujumbe. Mtambo huu una sehemu mbalimbali zinazotumika kupiga chapa. Sehemu
zenyewe ni:
Kiwambo (monitor) ni kioo kwenye tarakilishi ambapo picha na data
huonyeshwa. Pia, huitwa skrini.
Kipanya (mouse) ni kifaa cha kuonyeshea data kwenye kiwambo.
Kitufe (keyboard buttons) kifaa cha maelekezo kwenye bodidota.
Bodidota (keyboard) kifaa cha kuingizia data kwenye tarakilishi kinachotumika
kwa mkono. Pia, huitwa kiibodi.
Faili (le) - taarifa inayohifadhiwa kwenye tarakilishi kwa jina fulani maalumu.
Kitengo kikuu cha uchakataji (Central Processing Unit - CPU).
70
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Tarakilishi/vipakatalishi/rununu,
2. Picha ya mchoro unaoonyesha sehemu za tarakilishi,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 44,
4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu anaweza kubeba tarakilishi halisi darasani.
Iwapo hana, anaweza kumwazima mtu yeyote. Mwalimu awashirikishe wanafunzi
katika kujadiliana kuhusu kifaa alichokibeba (tarakilishi) kwa kuzingatia maswali
yaliyo kitabuni mwao. Akubali majibu ya wanafunzi yaliyo sahihi. Awape wanafunzi
uhuru wa kusema wanachojua kuhusu tarakilishi. Pia, anaweza kuwapa wanafunzi
kifaa hicho wakakigusa ila kwa tahadhari wasije wakakiharibu. Wanafunzi wafanye
mazoezi ya kuwasha na kuzima tarakilishi.
Wanafunzi watazame mchoro wa tarakilishi ulio kitabuni mwao katika shughuli ya
pili. Wajadiliane katika vikundi wanachoona katika mchoro huo. Wataje sehemu za
tarakilishi zilizoonyeshwa kwa nambari. Kwanza, wazitaje sehemu hizo kwa Kiingereza
kisha kwa Kiswahili. Mwalimu atathmini majibu yao. Pia, mwalimu awaonyeshe
sehemu hizo katika tarakilishi halisi aliyobeba darasani. Awaonyeshe sehemu hizo
kwenye vipakatalishi vyao na hata rununu yake.
Mwalimu awaeleze wanafunzi kwamba kitengo kikuu cha uchakataji cha kipakatalishi
kimeundwa kwa ndani hivyo basi hakionekani. Iwapo shule ina tarakilishi yoyote
ambayo sehemu hiyo imeundwa kwa nje (desktop), mwalimu awapeleke iliko ili
wanafunzi waione.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kujikumbusha kuwasha na kuzima tarakilishi. Awape
maelezo kamili ya kila sehemu ya kupigia chapa ya tarakilishi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi yao na idadi ya tarakilishi zinazopatikana. Wanafunzi waandike sentensi zilizo
kitabuni mwao kwenye tarakilishi. Maagizo waliyopewa kitabuni mwao yazingatiwe.
Sharti majina ya mavazi yaandikwe kwa rangi iliyokolezwa, italiki na yapigiwe
mstari.
Kazi hiyo ihifadhiwe kwenye faili kwa jina la kikundi chao watakalobuni.
Wanafunzi wanapoendelea kutumia tarakilishi, mwalimu atathmini kila mwanafunzi
kubaini iwapo anashiriki katika kutumia tarakilishi. Awasaidie wanafunzi walio na
matatizo ya kutumia tarakilishi.
Hatimaye, mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Kwa maelekezo na
ruhusa ya mlezi, walinganishe sehemu za rununu na zile za tarakilishi.
71
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua sehemu za
tarakilishi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuwasha na kuzima tarakilishi.
3. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuandika kwa kutumia
tarakilishi.
4. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuhifadhi kazi katika faili.
Kipindi cha 2: Kutumia tarakilishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 45)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuhariri kazi kwenye tarakilishi kwa kuzingatia uakishaji sahihi.
b) Kuhifadhi kazi kwenye faili.
ch) Kujenga mazoea ya kuandika kwa kutumia tarakilishi.
Swali dadisi
Unakiri ni kwa nini tunahifadhi kazi katika tarakilishi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kipindi hiki kinalenga kukamilisha kazi ambayo ilianzishwa katika kipindi ambacho
kilitangulia. Itachukuliwa kwamba tayari mwanafunzi ana ujuzi wa kupiga chapa na
kuhifadhi kazi kwenye faili.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Tarakilishi/vipakatalishi, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 45, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaongoze wanafunzi kushiriki katika shughuli ya kwanza ya kutaja baadhi
ya sehemu za tarakilishi walizojifunza katika kipindi kilichotangulia. Sehemu hizi ni:
kiwambo, kipanya, bodidota, kitengo kikuu cha uchakataji, kitufe n.k. Wanafunzi
wachore tarakilishi kwenye chati watakazopewa na mwalimu. Waonyeshe sehemu za
tarakilishi watakayochora. Mwalimu atathmini michoro ya kila kikundi. Wakimaliza
wazibandike chati hizo ukutani darasani.
Kwa kutumia tarakilishi, mwalimu amwongoze mwanafunzi kuandika kwenye
tarakilishi kifungu cha aya moja kuhusu mavazi yanayovaliwa katika jamii yake.
Akihariri na kukihifadhi kifungu hicho katika faili kwa jina lake kulingana na
shughuli ya pili. Mwalimu awasaidie wanafunzi wanaotatizika. Mwalimu amwelekeze
72
mwanafunzi kutuma kifungu cha aya alichoandika kwa wenzao na kwake pia kupitia
mtandaoni ili wakisahihishe. Iwapo mtandao haupo, mwanafunzi ampe mwenzake na
mwalimu kazi hiyo aitathmini kwenye tarakilishi yake.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa msaada wa mlezi au
mzazi wake. Mwanafunzi afanye mazoezi ya kuandika akitumia tarakilishi. Pia, atati
kuhusu umuhimu wa vifaa mbalimbali vya kidijitali. Mwanafunzi awaeleze wenzake
darasani umuhimu huo katika kipindi kijacho.
Mwalimu anaweza kutamatisha kipindi hiki kwa kuwahimiza wanafunzi wafanye
mazoezi ya kuandika kwenye tarakilishi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuandika kwa kutumia
tarakilishi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuhariri kazi kwenye tarakilishi.
3. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kushirikiana na wengine katika
vikundi.
D. Saru:Ainazamaneno
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 46)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya aina ya neno lengwa ili kulibainisha.
b) Kutambua aina ya neno lengwa katika kundi la maneno na sentensi.
ch) Kutumia aina ya neno lengwa kwa njia sahihi katika mawasiliano.
d) Kuonea fahari matumizi ya aina ya neno lengwa katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Je, unajua maana ya kiunganishi? Taja mifano.
2. Je, unajua maana ya kihusishi? Taja mifano.
3. Je, unajua maana ya kihisishi? Taja mifano.
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala, kazi za vikundi na mawasiliano mtandaoni.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
katika kutambua aina ya neno lengwa na kutunga sentensi mtandaoni.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi akitumia aina ya neno
lengwa.
73
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anapofaulu kutambua aina ya neno lengwa
na kulitungia sentensi sahihi.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapotafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja katika vikundi.
Masuala mtambuko anuwai kutokana na sentensi zinazoelekeza utoaji wa
maelezo kuhusu masuala hayo kama vile utunzaji wa mazingira, afya bora na
utunzaji wa wanyama.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Maadili mbalimbali yaliyolengwa katika sentensi kama vile upendo, uaminifu,
uzalendo, amani na umoja.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili - masomo haya yana mada kuhusu
kanuni za saru.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji za huduma kwa jamii
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu mawasiliano yenye
kuzingatia kanuni za kisaru.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kueleza maana
na kutoa mifano
ya aina ya neno
lengwa kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
na kutoa mifano
ya aina ya
neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatoa mifano
ya baadhi ya
aina ya neno
lengwa kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatoa mifano
ya baadhi ya
aina ya neno
lengwa kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu kutoa
mifano ya aina
ya neno lengwa.
Kutambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya aina
ya neno lengwa
kwa urahisi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua aina
ya neno lengwa.
74
Kutumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatumia aina
ya neno lengwa
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatumia baadhi
ya aina ya neno
lengwa.
Mwanafunzi
anajaribu
kutumia aina ya
neno lengwa.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watambue aina ya neno lengwa kwa kutumia
breli au wasikilize wanafunzi wengine wakisoma huku wao wakitambua maneno
hayo.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema watambue aina ya neno lengwa kwa kuandika
au kupigia mistari huku walio na uwezo wa kusema wakitamka kwa sauti. Wasio
na uwezo wa kusema pia wanaweza kushiriki kwa kuwapigia mako wanafunzi
wengine.
Wanafunzi walio na uelewa wa juu zaidi wapewe shughuli zaidi ili kuwakimu.
Wanafunzi ambao wanachukua muda kuelewa wapewe nafasi au muda zaidi
kukamilisha shughuli zao.
Maelezo ya jumla
Viunganishi hutumika kuunganisha maneno au sentensi. Mada hii itamsaidia
mwanafunzi kuchagua viunganishi kwa usahihi katika mawasiliano yake ya kila siku.
Vihusishi ni maneno yanayoonyesha uhusiano uliopo baina ya mtu, kitu au nomino
na mahali. Hueleza au kuonyesha kitu kilipo huku kikilinganishwa na kingine. Mada
hii itawapa wanafunzi uelewa utakaowasaidia katika mawasiliano yao maishani.
Kipindi cha 1: Viunganishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 46)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kiunganishi.
b) Kutambua viunganishi kutoka katika kundi la maneno na sentensi.
Swali dadisi
Je, unajua maana ya kiunganishi? Unajua mifano gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kiunganishi ni neno linalotumiwa kuunganisha sentensi. Kwa wingi ni viunganishi.
Mifano ya viunganishi ni: na, kwa sababu, lakini, kuliko, pia na vinginevyo.
75
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 46, 2. Breli, 3. Jedwali la maneno,
4. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu atangulize somo kwa kuwaelekeza wanafunzi
wawili wasimame mbele ya darasa na wataje majina yao. Wanafunzi wengine watunge
sentensi moja wakilinganisha majina yao. Mifano ya sentensi tarajiwa:
1. Birgen na wafula wamesimama mbele ya darasa.
2. Birgen na Wafula ni wanafunzi.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi kutambua kuwa na ni kiunganishi.
Wanafunzi wawili, mmoja mrefu na mwingine mfupi wasimame mbele ya darasa.
Wanafunzi wengine watunge sentensi moja wakilinganisha kimo chao.
Mifano ya sentensi tarajiwa
1. Amina ni mrefu kuliko Mutua.
2. Mutua ni mfupi lakini Amina ni mrefu.
Wanafunzi watambue kuwa kuliko na lakini ni viunganishi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kuunganisha sentensi mbilimbili zilizo katika
shughuli ya pili kitabuni mwao ili ziwe sentensi mojamoja. Mwanafunzi amwonyeshe
mwanafunzi mwenzake sentensi alizounganisha ili wazitathmini. Mwalimu awaeleze
wanafunzi kuwa maneno waliyotumia kuunganisha sentensi ni viunganishi. Wanafunzi
waeleze maana ya viunganishi.
Majibu tarajiwa:
1. Alilala kwa sababu alikuwa amechoka.
2. Msivute sigara wala kutumia dawa za kulevya.
3. Usile bila kunawa mikono.
4. Mama alienda sokoni lakini hakununua mboga.
Katika shughuli ya tatu, wanafunzi washirikiane katika vikundi kutambua viunganishi
kutoka kwenye jedwali lililo kitabuni mwao. Viunganishi hivyo ni: wala, bila, lakini,
ili, kisha, na, kwa sababu. Kila mwanafunzi atunge sentensi sahihi kwa kutumia
viunganishi walivyotambua kutoka kwa jedwali husika. Mwalimu atathmini sentensi
zitakazotungwa na mwanafunzi. Wanafunzi wanaweza kutathmini sentensi za wenzao
kwa maelekezo ya mwalimu.
Mwalimu atamatishe kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi kufanya kazi ya ziada.
76
Mwanafunzi amsimulie mlezi au mzazi wake kuhusu jinsi siku yake ilivyokuwa.
Ahakikishe anatumia viunganishi alivyojifunza darasani katika masimulizi yake.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kueleza maana ya kiunganishi.
2. Mwalimu atathmini utambuaji wa viunganishi kwa usahihi.
3. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutunga sentensi sahihi kwa
kutumia viunganishi.
Kipindi cha 2: Viunganishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 48)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viunganishi kutoka katika orodha.
b) Kutumia viunganishi kwa usahihi katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, unajua kazi ya viunganishi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anahitajika kumakinika katika utumiaji mzuri wa viunganishi katika
mawasiliano pamoja na utambuaji sahihi wa viunganishi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 48, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwaomba wanafunzi wataje baadhi ya viunganishi
walivyojifunza katika kipindi cha awali. Mwalimu pamoja na wanafunzi wengine
watathmini majibu yatakayotolewa.
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya kwanza, mwalimu
awaelekeze wanafunzi watambue viunganishi kutoka kwa orodha ya maneno iliyo
kitabuni mwao. Viunganishi wanavyofaa kutambua ni: lakini, pia, na, ili, bila, kwa
sababu, wala, kisha. Mwalimu awaongoze wanafunzi kushirikiana katika kutunga
sentensi sahihi kwa kutumia viunganishi walivyotambua. Mwalimu akubali sentensi
zozote zilizo sahihi zilizotumia viunganishi walivyotambua.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kutumia viunganishi
walivyotambua katika shughuli ya kwanza kutunga na kuandika kwenye tarakilishi
kifungu cha aya mbili. Wanafunzi watumie mtandao kuwatumia wanafunzi wenzao
pamoja na mwalimu vifungu vyao ili wavisome na kuvitathmini.
77
Hatimaye, mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kuzingatia
maagizo waliyopewa kitabuni mwao. Kila mwanafunzi atunge kifungu cha aya
mbili akilinganisha sare za shule yake na sare za shule iliyo karibu nao. Mwanafunzi
ahakikishe anatumia viunganishi katika kifungu chake. Mwanafunzi azingatie rangi na
aina ya sare atakazolinganisha. Mwanafunzi awasomee wanafunzi wenzake darasani
kifungu chake ili wakitathmini. Pia, mwalimu atathmini kazi za wanafunzi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini utambuaji wa viunganishi kutoka kwa orodha ya maneno.
2. Mwalimu atathmini utumiaji sahihi wa viunganishi katika sentensi.
Aina za maneno
Kipindi cha 1: Vihusishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 49)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kihusishi ili kukibainisha.
b) Kutambua vihusishi kutoka katika kundi la maneno na sentensi.
Swali dadisi
Je, unajua maana ya kihusishi? Unajua mifano gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vihusishi ni aina ya maneno yanayoonyesha uhusiano uliopo baina ya vitu, watu na
mahali. Mifano ya vihusishi ni: mbele ya, karibu na, kando ya, ndani ya, nyuma ya na
juu ya.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 49, 2. Jedwali la maneno,
3. Breli, 4. Mti wa maneno, 5. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize somo kwa kuwashirikisha wanafunzi katika shughuli ya kwanza.
Awaelekeze wanafunzi. Mwanafunzi mmoja asimame mbele ya darasa huku wanafunzi
wengine wakitunga sentensi kuonyesha kitendo chake na mahali alipo.
78
Mfano:
Aoko amesimama mbele ya darasa.
Mwalimu ateue wanafunzi wengine wanne, mmoja asimame nyuma ya darasa,
mwingine nje ya darasa, mwingine aketi juu ya dawati, mwingine asimame karibu
na mwalimu. Wanafunzi wengine watunge sentensi kuonyesha mahali wanafunzi hao
walipo.
Mifano: 1. Kendi amesimama nyuma ya darasa. 2.Tuzo amesimama nje ya darasa.
3. Zawadi amesimama karibu na mwalimu. 4. Baku ameketi juu ya dawati.
Mwalimu anaweza kutumia vifaa vingine kama vile kitabu juu ya meza, kalamu
chini ya dawati na kadhalika kuwafundishia wanafunzi kuhusu vihusishi. Mwalimu
awaelekeze wanafunzi kujadiliana kuhusu maana ya vihusishi.
Katika vikundi, wanafunzi wajadili michoro katika shughuli ya pili kisha watunge
sentensi sahihi kuhusu michoro hiyo. Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na mahitaji yao. Mwalimu ahakikishe kila mwanafunzi anahusishwa
katika shughuli hii.
Majibu tarajiwa: 1. Watu wawili wanapumzika chini ya mti. 2. Maziwa yamo ndani ya
gilasi. 3. Mwalimu amesimama mbele ya darasa./Tarakilishi iko juu ya meza.
4. Gari limeegeshwa nyuma ya nyumba.
Mwalimu akubali sentensi zozote sahihi zilizo na vihusishi na zinazolingana na
michoro husika.
Wanafunzi washirikiane katika vikundi kutambua vihusishi katika shughuli ya tatu
kutoka kwa maneno waliyopewa. Baada ya kutambua vihusishi hivyo, wavitumie
kutunga sentensi sahihi. Mwalimu ayakubali majibu yoyote sahihi.
Wanafunzi wafanye kazi ya ziada baadaye. Mwanafunzi aandike vitu vitano ambavyo
hupatikana nje ya darasa lao, nje ya nyumba yao, ndani ya darasa lao na ndani ya
nyumba yao. Awasomee wenzake darasani atakayoandika katika kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kueleza maana ya kihusishi.
2. Mwalimu atathmini utambuaji wa vihusishi kutoka katika orodha na sentensi.
Kipindi cha 2: Vihusishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 51)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia vihusishi katika sentensi kwa usahihi.
b) Kufahamu matumizi ya vihusishi katika mawasiliano.
79
Swali dadisi
Je, kazi ya vihusishi ni gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Katika kipindi hiki, inachukuliwa kwamba mwanafunzi ameshapata uwezo wa
kutambua vihusishi. Basi, mwanafunzi anatakiwa kufurahia matumizi ya vihusishi
katika mawasiliano. Jambo hili litaakiwa kwa kuhakikisha utunzi sahihi wa sentensi
kwa kutumia vihusishi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Tarakilishi, 2. Mti wa maneno, 3. Breli,
4. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 51.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika vikundi, mwalimu awape wanafunzi fursa ya kutambua vihusishi mbalimbali
kutoka kwenye mti wa maneno ulio katika shughuli ya kwanza. Mwalimu awagawe
wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao darasani.
Kila mwanafunzi atunge sentensi sahihi na kuziandika katika daari lake akitumia
vihusishi walivyotambua kutoka kwenye mti maneno. Baada ya utunzi wao, wanafunzi
wabadilishane madaari yao ili wazitathmini sentensi zao na kuziboresha.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi wakiwa katika vikundi
waandike aya moja kuhusu darasa lao kwenye tarakilishi huku wakitumia vihusishi
mbalimbali. Vihusishi watakavyotumia vionyeshwe kwa rangi iliyokolezwa.
Wanafunzi wahifadhi vifungu vyao kwenye faili kisha wavisambaze kwa wanafunzi
wenzao na mwalimu mtandaoni ili wavisome na kuvitathmini.
Mwalimu ahitimishe kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi kufanya kazi ya ziada
baadaye. Mwanafunzi amshirikishe mlezi au mzazi wake kuifanya kazi hiyo. Mlezi
au mzazi amtajie mwanafunzi vihusishi mbalimbali katika lugha yake ya kwanza.
Washirikiane kuvitafsiri vihusishi hivyo kwa Kiswahili. Iwapo lugha ya kwanza ya
mlezi au mzazi ni Kiswahili, basi amtajie mwanafunzi vihusishi kwa Kiswahili kisha
wavitafsiri kwa Kiingereza. Mwalimu ajitahidi kufahamu baadhi ya vihusishi katika
lugha tofauti tofauti za kwanza za wanafunzi ili kuwachangamsha wanafunzi darasani.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutumia vihusishi kwa usahihi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutumia tarakilishi kuandika
aya yenye vihusishi.
3. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kushirikiana na wanafunzi
wengine katika vikundi.
4. Mwalimu atathmini sentensi zitakazotungwa na mwanafunzi.
80
Aina za maneno
Kipindi cha 1: Vihisishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 52)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya vihisishi ili kuvibainisha.
b) Kutambua vihisishi katika orodha ya maneno na sentensi.
Swali dadisi
Je, unajua maana ya kihisishi? Unajua mifano gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vihisishi ni maneno yanayoonyesha hisia tofauti tofauti kama vile furaha, huzuni,
hasira, mshangao.
Maneno hayo huwekewa alama ya hisi (!).
Vihisishi vya furaha ni kama vile: Huree!, Oyee!.
Vihisishi vya huzuni ni kama vile: Jamani!, Mama ee!, Pole!.
Vihisishi vya mshangao ni kama vile: Kumbe!, Salaalee!, Lo!.
Vihisishi vya kukubali/kuitikia ni kama vile: Naam! Aha!.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi kutamka vihisishi mbalimbali kwa usahihi na kwa
kiimbo kinachofaa.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 52, 2. Tarakilishi,
3. Mchoro wenye vihisishi mbalimbali, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Awagawe wanafunzi
katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao. Wanafunzi wajadiliane kuhusu
maswali waliyopewa kitabuni mwao. Mwalimu akubali majibu ya wanafunzi kulingana
na maswali waliyoulizwa. Wanafunzi wanaweza kutaja hisia zao kwa lugha zao za
kwanza au Kiingereza. Mwalimu anaweza pia kubuni tukio la kufurahisha darasani
kama vile kuwazawidi wanafunzi au tukio la kushangaza kama vile kuwaambia
kwamba mwalimu mkali kabisa shuleni ndiye atakayekuwa akiwafunza Kiswahili.
Sikiliza maneno yao ya furaha na mshangao. Mwalimu anaweza kuwaeleza wanafunzi
maana ya hisia kutoka kwenye kamusi.
Katika vikundi vyao, wanafunzi wajadili hisia za watu walio katika michoro iliyo
kitabuni mwao katika shughuli ya pili. Michoro hiyo inaonyesha hisia za huzuni,
81
mshangao na furaha. Wanafunzi watunge sentensi sahihi kwa kila mchoro ili
kuonyesha hisia mbalimbali. Mwalimu ahakikishe wanafunzi wanatumia vihisishi
katika sentensi zao.
Mwalimu awape wanafunzi maelezo kamili kuhusu vihisishi huku akiwapa mifano.
Awaelekeze wanafunzi kujadiliana kuhusu maana ya vihisishi.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika mchezo wa kuchopoa kadi za maneno
kutoka kikapuni katika shughuli ya tatu. Mchezo huu ni wa kuwawezesha wanafunzi
watambue vihisishi kutoka kwa kundi la maneno mbalimbali. Mwanafunzi mmoja
achopoe kadi kutoka kikapuni huku wengine wakitambua na kusoma kihisishi
kilichoandikwa kwenye kadi hiyo. Wanafunzi watunge sentensi sahihi kwa kutumia
vihisishi mbalimbali watakavyotambua kutoka kwa kadi zilizo kikapuni.
Kwa kutumia tarakilishi, wanafunzi katika vikundi vyao waziandike sentensi
walizotunga huku wakionyesha vihisishi kwa italiki. Wanafunzi wapangwe katika
vikundi kulingana na idadi yao darasani na tarakilishi zilizopo. Wanafunzi watumie
mtandao kuzituma kazi zao kwa wanafunzi wenzao pamoja na mwalimu ili
wazitathmini na kuzisahihisha.
Mwalimu ahitimishe kipindi kwa kuwaagiza wanafunzi wafanye kazi ya ziada.
Mwanafunzi amwulize mzazi au mlezi wake iwapo amewahi kufurahi, kushangaa au
kukasirika. Mzazi au mlezi amweleze sababu ya kupatwa na hisia hizo.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kueleza maana ya vihisishi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua vihisishi katika
orodha na sentensi.
Kipindi cha 2: Vihisishi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 53)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia vihisishi kwa usahihi katika sentensi.
b) Kufahamu matumizi ya vihisishi katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, kazi ya vihisishi ni gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Utunzi wa sentensi kwa kutumia vihisishi sharti ufanywe kwa umakinifu zaidi ili hisia
zinazotolewa ziambatane na ujumbe uliomo.
82
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 53, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize somo kwa kuwapa wanafunzi wawili wawili nafasi washiriki
katika shughuli ya kwanza kwa kutaja vihisishi vya:
1. Furaha, kama vile: Huree!, 2. Mshangao, kama vile: Lo!, Salaale!
3. Huzuni, kama vile: Jamani!, Pole!
Kila mwanafunzi atunge sentensi sahihi kwa kutumia vihisishi walivyotaja. Aandike
sentensi atakazotunga katika daari lake.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi na mahitaji yao. Wanafunzi watambue vihisishi kutoka kwenye mstatili wenye
maneno ulio kitabuni mwao. Vihisishi wanavyofaa kutambua ni: Naam!, Kumbe!,
Salaale!, Jamani!, Aha!, Ala!, Oyee!, Pole!
Wanafunzi watunge sentensi sahihi kwa kutumia vihisishi walivyovitambua kutoka
kwenye mstatili waliopewa. Mwalimu atathmini na kukubali sentensi sahihi. Wanafunzi
katika vikundi vingine wanaweza kusahihisha sentensi za wanafunzi wa vikundi
vingine.
Mwalimu ahitimishe kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi kufanya kazi ya ziada.
Mwanafunzi amwombe mzazi au mlezi wake amtajie vihisishi katika lugha yake ya
kwanza. Wavitafsiri vihisishi hivyo kwa Kiswahili. Mwanafunzi anaweza kuwaeleza
wenzake darasani ili kuwachangamsha na wajifunze. Mwalimu afahamu vihisishi
katika lugha za kwanza mbalimbali ili kuwachangamsha wanafunzi darasani.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini matumizi sahihi ya vihisishi katika sentensi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kushirikiana na wengine katika
vikundi.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu atathmini vitendawili ambavyo mwanafunzi atatunga. Sharti vitendawili
hivyo viwe sahihi na vihusishe sauti zozote radidi. Urudiaji wa sauti uwepo. Mifano:
a) Pita huku nami nipite huko tukutane (jibu ni mshipi). Katika kitendawili hiki
sauti /p/, /t/ na /k/ zimerudiwa.
b) Anachora kitu asichokijua (jibu ni konokono). Katika kitendawili hiki sauti
/ch/ na /k/ zimerudiwa.
83
2. Mwalimu ahakikishe kuwa mwanafunzi anataja mavazi yanayovaliwa na Waislamu,
kwa mfano: buibui, kanzu, hijabu n.k.
3. Mwalimu atathmini aya atakayotunga mwanafunzi. Sharti aya hiyo ihusu umuhimu
wa mavazi kwa binadamu. Baadhi ya manufaa ya mavazi ni: kuzuia baridi, kusitiri
uchi, kuzuia kuchomwa na jua kali, kuzuia uchafu mwilini n.k.
4. Mwalimu atathmini aya atakayotumiwa na mwanafunzi mtandaoni. Aya hiyo ihusu
umuhimu wa mavazi kwa binadamu. Sharti sentensi katika aya hiyo ziwe sahihi
kisaru.
5. Mwalimu atathmini michoro itakayochorwa na mwanafunzi pamoja na rangi
atakazotumia. Michoro hiyo iwe ya mavazi yoyote.
6. Mwanafunzi ataje sehemu zozote nne za tarakilishi. Kisha aeleze matumizi ya
sehemu hizo. Mifano:
a) Kiwambo (kioo kwenye tarakilishi ambapo data na picha huonyeshwa),
b) Kipanya (hutumiwa kuonyeshea data kwenye kiwambo),
ch) Bodidota (kifaa cha kuingizia data kwenye tarakilishi),
d) Kitufe (kifaa cha maelekezo kwenye bodidota) n.k.
7. Mtoto amevalishwa sweta kwa sababu kuna baridi.
8. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi atatunga. Sharti sentensi hizo
ziwe sahihi kisaru. Pia, zihusishe vihusishi mbalimbali. Mifano:
a) Mwalimu amesimama mbele ya wanafunzi. ch) Mpira uko juu ya meza.
b) Ngombe anakula nyasi nyuma ya nyumba.
9. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anataja vihisishi vya mshangao kama vile Ala!,
Mama ee!, Lo! n.k. Mwalimu ahakikishe wanafunzi wanatunga sentensi sahihi kwa
kutumia vihisishi walivyotaja. Mifano:
a) Ala! Umeweza kuubeba mzigo huo peke yako.
b) Mama ee! Panya ametafuna pesa zangu.
ch) Lo! Mbwa wetu amekufa.
10. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi kuhusu aina ya mavazi yanayovaliwa
na watu wa jamii yake. Pia, mwanafunzi ataje rangi ya mavazi yanayopendelewa na
watu wa jamii yake.
84
DIRA
4
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 56)
A. KusikilizanaKuzungumza:Heshima,adabunavyeo
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua maneno ya upole yanayotumiwa katika mawasiliano.
b) Kutumia maneno ya upole katika mawasiliano.
ch) Kutathmini matumizi ya maneno ya upole katika mawasiliano.
Swali dadisi
Ni maneno gani yanayotumiwa kuonyesha upole katika mazungumzo?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanapojadiliana na kuigiza
katika vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vyombo vya kidijitali
katika ujifunzaji.
Uhusiano na masuala mtambuko
Umoja wa kijamii katika kujadiliana kwenye vikundi.
Stadi za maisha - anapotumia maneno ya upole.
Uhusiano na maadili
Heshima - mwanafunzi anapotumia maneno ya upole.
Upendo - mwanafunzi anapoonyesha upendo kwa kushirikiana na wenzake
katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza, Lugha za kiasili na Somo la Dini - lugha ya upole hufunzwa katika
masomo haya.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake kuhusu matumizi ya maneno ya upole katika
mahusiano yao.
85
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuyatambua
maneno ya
upole na
kuyatumia
ipasavyo.
Mwanafunzi
anayatambua
maneno ya
upole na
kuyatumia
ipasavyo kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anayatambua
maneno ya
upole na
kuyatumia
ipasavyo.
Mwanafunzi
anayatambua
baadhi ya
maneno ya
upole na
kuyatumia
ipasavyo.
Mwanafunzi
anajaribu
kuyatambua
maneno ya
upole.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia, wayasome maneno ya upole ubaoni kisha
watambue matumizi yake.
Wanafunzi walio na changamoto za kuona (wasioona kabisa) watumie breli kutambua
maneno ya upole. Wale wasioona mbali wakae karibu na ubao na wasioona karibu
wakae mbali na ubao. Wanafunzi wanaochukua muda zaidi kuelewa wapewe muda
zaidi. Wanafunzi wanaoelewa kwa wepesi wapewe mazoezi zaidi ili kuwaimarisha.
Maelezo ya jumla
Mada hii inashughulikia maneno ya heshima yanayofaa kutumiwa katika mawasiliano
ya kila siku. Maneno haya yatamwezesha mwanafunzi kuwasiliana na wanafunzi
wenzake pamoja na wakuu wake kwa upole ili kukuza upendo, heshima na ushirikiano.
Kipindi cha 1: Maneno ya upole
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 56)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua maneno ya upole yanayotumiwa katika mawasiliano.
b) Kutumia maneno ya upole katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, unayajua maneno yapi yanayotumiwa kuonyesha upole katika mazungumzo?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Maneno yenye upole hupunguza ukali wa hisia katika mawasiliano. Mwanafunzi
anapotambua na kuyatumia maneno haya huwa mwadilifu maishani. Ni vyema
mwalimu awatie moyo wanafunzi wazoee kutumia maneno ya upole maishani.
Mwalimu ajaribu pia kuwa na nyenzo zifaazo ili kufanikisha ufunzaji.
86
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 56, 2. Video ya mazungumzo,
3. Breli, 4. Mchoro wenye maneno ya vyeo mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa kuwaelekeza wanafunzi kufanya shughuli ya
kwanza kwa kujadili maswali waliyopewa kitabuni mwao. Wanafunzi wataje maneno
ya upole wanayotumia kuwaomba wenzao vitu, kubisha mlango, kuomba msamaha
na kuwashukuru watu wakiwarekebisha. Mwalimu awaongoze wanafunzi kutambua
maneno mbalimbali ya upole. Awashirikishe kujua maana na matumizi ya maneno ya
upole watakayotaja. Vilevile, awaongoze kuyatumia maneno hayo katika mazungumzo.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kujadili vitendo ambavyo
vinaendelea katika michoro waliyopewa kitabuni mwao. Awaongoze wanafunzi
kujadili maneno yanayotumiwa na watu katika michoro husika. Mwalimu awaeleze
umuhimu wa kuyatumia maneno ya upole katika mazungumzo.
Majibu tarajiwa ya michoro: a) Asante kwa matunda. b) Pole kwa kuumia. ch) Hodi
huku? Karibu. d) Tafadhali mwalimu naomba ruhusa ya kwenda msalani.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya tatu. Wanafunzi watumie maneno
ya upole badala ya maneno yaliyopigiwa mistari katika sentensi walizopewa kitabuni
mwao. Mwalimu awaongoze wanafunzi kusahihisha sentensi watakazoandika
darasani. Wanafunzi waliokosea wasahihishwe.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya nne kwa kuwaonyesha video
ya mazungumzo yaliyotumia maneno ya upole. Wanafunzi watazame na kusikiliza
video hiyo kwa makini. Baadaye, watambue na kujadiliana kuhusu maneno ya upole
yaliyotumiwa katika video hiyo. Mwalimu ahakikishe kuwa ameandaa video ya
mazungumzo yenye maneno ya upole na heshima kabla ya kipindi hiki.
Hatimaye, mwalimu awaelekeze wanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi
ajadiliane na mzazi au mlezi wake kuhusu umuhimu wa kutumia maneno ya upole
katika mazungumzo. Mwanafunzi awaeleze wenzake darasani kuhusu waliyojadili na
mzazi au mlezi wake.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada:
1. Kuonyesha heshima, 2. Kukuza maadili maishani,
3. Kuimarisha uhusiano, 4. Kuonyesha unyenyekevu.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua maneno ya upole.
2. Mwalimu atathmini uwezo wake wa kuyatumia maneno ya upole katika
mawasiliano.
87
3. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kujadiliana na wenzao katika
kikundi wakitumia maneno ya upole.
Kipindi cha 2: Maneno ya upole
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 58)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutathmini matumizi ya maneno ya upole katika mawasiliano.
b) Kutumia maneno ya upole katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, unaweza kutumia maneno ya upole kwa usahihi katika mawasiliano na wenzako?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awachochee wanafunzi kujikumbusha baadhi ya maneno ya upole
waliyosoma katika kipindi kilichopita. Awaeleze wanafunzi kuwa maneno ya upole
yana umuhimu katika mawasiliano. Pia, awakumbushe kuwa kuna watu wenye vyeo
tofauti shuleni mwao wanaofaa kuheshimiwa. Kwa mfano: mwalimu mkuu, kiranja wa
darasa, kinara wa chama cha Kiswahili n.k. Watu hawa wana mamlaka.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 58, 2. Sufuria yenye kadi za maneno,
3. Chati yenye maneno ya upole, 4. Breli, 5. Kamusi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu atangulize kipindi kwa kuwauliza wanafunzi
wataje mifano ya maneno ya upole waliyosoma katika kipindi kilichotangulia.
Mwalimu awaongoze kujadili maneno ya upole yaliyoandikwa kwenye chati
atakayowapa katika vikundi. Wanafunzi katika vikundi vyao wajadiliane kuhusu
maana na matumizi ya maneno yaliyo kwenye chati hiyo.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kuigiza mazungumzo yaliyo katika shughuli ya pili
wakiwa wawili wawili. Awaongoze wanafunzi kueleza maana ya maneno yaliyoandikwa
kwa rangi iliyokolezwa.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya tatu. Wajadili kuhusu kadi
za maneno zilizo kwenye mchoro wa sufuria vitabuni mwao. Wanafunzi wajadiliane
kuhusu watu walio na vyeo mbalimbali shuleni kwao. Wayataje majina halisi ya watu
hao katika shule yao wakianza na kiranja wa darasa lao. Mwanafunzi aliye na cheo
chochote shuleni awaeleze wenzake majukumu yake.
Mifano ya majibu tarajiwa:
1. Mwalimu mkuu - huongoza walimu na wanafunzi shuleni.
88
2. Mwalimu wa zamu - huhakikisha kuwa ratiba ya shuleni imefuatwa ipasavyo.
3. Kiranja wa darasa - hudumisha nidhamu darasani.
Mwalimu akubali majibu yoyote yaliyo sahihi na yanayoeleza majukumu ya watu
wenye vyeo mbalimbali shuleni. Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa watu wenye vyeo
mbalimbali wanafaa kuheshimiwa.
Mwisho, mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi
ajadiliane na mzazi au mlezi wake kuhusu umuhimu wa kutumia msala, umuhimu wa
kutumia maneno ya upole anapoomba kitu na umuhimu wa kula vyakula sa.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada: a) Kuzuia magonjwa/kutunza mazingira.
b) Kuboresha uhusiano/kuonyesha heshima. ch) Kuwa na afya njema/kujikinga dhidi
ya maradhi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuyatumia maneno ya upole
katika mawasiliano.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi ana ukakamavu wa kuigiza
mazungumzo yenye maneno ya upole.
3. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anafahamu majukumu ya watu wenye
vyeo mbalimbali shuleni mwao. Ayataje majina yao halisi.
B. Kusoma: Kusoma kwa mapana
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 60)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua na kufungua faili iliyo na kifungu cha kusoma.
b) Kutambua na kuzingatia hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya
kidijitali.
ch) Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata vifungu vya kusoma vyenye
mada lengwa.
d) Kutumia vyombo vya kidijitali kwa urahisi kupata matini yanayolengwa.
e) Kuchangamkia matumizi ya vifaa vya kidijitali katika kutafuta na kusoma
ujumbe ili kuimarisha maarifa yake.
Maswali dadisi
1. Je, ni hatua zipi za kiusalama unazofaa kuzingatia unapotumia mtandao?
2. Je, utafanya nini ili kupata matini ya kusoma mtandaoni?
89
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa vifaa vya kiteknolojia vinapotumika katika
kusakura na kusoma.
Hamu ya kujifunza - unakuzwa mwanafunzi anapotafuta matini ya kusoma
kwenye tarakilishi na mitandaoni.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha - ujuzi wa kidijitali na usalama mitandaoni.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - katika utunzaji wa vifaa vya kidijitali na kuzingatia mitandao
salama.
Uhusiano wa masomo na mengine
Masomo yote kwa vile yanatakiwa kuzingatia ujuzi wa kidijitali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awafahamishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu usalama
mitandaoni na manufaa ya ujuzi wa kidijitali. Maarifa haya yataimarisha usomaji na
kupata maarifa yanayohusu nyanja mbalimbali.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua na
kuzingatia hatua
za kiusalama
mtandaoni,
kutambua tovuti
salama zenye
habari lengwa,
kutafuta matini
kwenye kifaa
cha kidijitali
au mtandaoni
na kunakili
maneno na
habari muhimu
alizosoma.
Mwanafunzi
anatambua na
kuzingatia hatua
za kiusalama
mtandaoni,
anatambua
tovuti salama
zenye habari
lengwa,
anatafuta matini
kwenye kifaa
cha kidijitali
au mtandaoni
na ananakili
maneno na
habari muhimu
alizosoma kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua na
kuzingatia hatua
za kiusalama
mtandaoni,
anatambua
tovuti salama
zenye habari
lengwa,
anatafuta matini
kwenye kifaa
cha kidijitali
au mtandaoni
na ananakili
maneno na
habari muhimu
alizosoma.
Mwanafunzi
anatambua
na kuzingatia
baadhi ya hatua
za kiusalama
mtandaoni na
anatafuta matini
kwenye kifaa
cha kidijitali
au mtandaoni
na kunakili
aliyoyasoma.
Mwanafunzi
anatafuta baadhi
ya matini
kwenye kifaa
cha kidijitali
au mtandaoni
na kujaribu
kuyasoma bila
kuzingatia hatua
za kiusalama.
90
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wanaoelewa kwa haraka waongezwe mazoezi zaidi. Wanafunzi
wanaoelewa polepole wasaidiwe na wanafunzi wenzao wanaoelewa kwa wepesi.
Pia, wanafunzi hawa waongezwe muda zaidi. Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona
wanaweza kutumia tarakilishi za breli kusoma.
Maelezo ya jumla
Mada hii itamwezesha mwanafunzi kujua namna ya kujikinga na hatari za mtandaoni.
Atafahamu hatua za kiusalama anaposakura tovuti mbalimbali. Vilevile, atakuwa na
uwezo wa kutafuta maana ya maneno mtandaoni.
Kipindi cha 1: Matini ya kidijitali
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 60)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua na kufungua faili iliyo na kifungu cha kusoma.
b) Kutambua na kuzingatia hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya
kidijitali.
Maswali dadisi
1. Je, unafahamu kuwasha na kuzima tarakilishi?
2. Je, unafahamu kufungua faili ya kusoma kwenye tarakilishi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu ajiandae vyema kabla ya kipindi hiki kwa kuwa na vifaa halisi vya kidijitali.
Iwapo vifaa hivyo havitoshi, mwalimu anaweza kuwaomba walimu wenzake tarakilishi
zao au hata rununu zao. Mwalimu awape wanafunzi maelekezo wanapotumia vifaa
hivi kwa usalama wao na wa vifaa vyenyewe. Awaeleze namna ya kuvitunza vifaa
walivyopewa ili visiharibike. Hii itapunguza gharama ya kuvikarabati au kununua
vingine.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 60, 2. Rununu,
3. Tarakilishi, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wafanye shughuli ya kwanza.
Wanafunzi watazame michoro ya vifaa vya kidijitali vilivyo kitabuni mwao. Wanafunzi
wataje majina ya vifaa hivyo. Waeleze iwapo wamewahi kuviona na kuvitumia vifaa
hivyo. Waelezane walivitumia kusoma matini kuhusu nini. Pia, wanafunzi wajadili
vitendo katika mchoro d. Iwapo mwalimu atakuwa na vifaa hivyo halisi darasani,
91
wanafunzi wavitazame. Mwalimu awaruhusu waviguse ila kwa uangalifu.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi yao na tarakilishi zilizopo. Awaelekeze wanafunzi kuwasha na kuzima tarakilishi.
Awaongoze katika kutafuta mtandaoni matini kuhusu usalama wa watoto. Matini hiyo
iwe salama kwa kusoma na iwe ya kiwango chao. Awaongoze katika vikundi vyao
wasome matini hiyo kisha waandike muhtasari wa matini hiyo. Wahifadhi kazi zao
katika faili kwa jina la mmoja wao kisha wawatumie wenzao katika vikundi vingine
pamoja na mwalimu mtandaoni ili wazisome na kuzitathmini.
Hatimaye, mwalimu awaelekeze wanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi
amwombe mzazi au mlezi wake amweleze kuhusu matini zilizo salama kusoma
mtandaoni. Mwanafunzi anaweza kutumia tarakilishi au rununu.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua vifaa vya kidijitali.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kuwasha na kuzima tarakilishi.
3. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kufungua faili lengwa bila
tatizo kisha kutambua jina la faili hiyo.
Kipindi cha 2: Matini ya kidijitali
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 61)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata vifungu vya kusoma vyenye
mada lengwa.
b) Kutumia vyombo vya kidijitali kwa urahisi kupata matini yanayolengwa.
ch) Kuchangamkia matumizi ya vifaa vya kidijitali katika kutafuta na kusoma
ujumbe ili kuimarisha maarifa yake.
Maswali dadisi
1. Ni hatua zipi za kiusalama unazofaa kuzingatia unapotumia mtandao?
2. Utafanya nini ili kupata matini ya kusoma mtandaoni?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Vyombo vya kidijitali vinaweza kuwa na manufaa au madhara kwa watoto. Iwapo
mwanafunzi anasoma matini mtandaoni ni vyema mwalimu amhamasishe kusoma
matini zilizo salama.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 61, 2. Dira,
3. Tarakilishi, 4. Rununu, 5. Breli.
92
Mapendekezo ya shughuli za ufunzaji
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Wanafunzi wajadiliane
kuhusu visa vya utapeli kwa kujibu maswali waliyopewa kitabuni mwao. Mwalimu
awahimize wanafunzi kuwa waangalifu wanapokumbana na watu wasiowajua njiani,
kwenye rununu au hata mtandaoni.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili. Wanafunzi wajadiliane
kuhusu maswali waliyopewa kitabuni mwao. Wajadili umuhimu wa kutoa habari kwa
mwalimu, mlezi, mzazi au mtu yeyote mkuu kila wanapokumbana na hali isiyo salama.
Umuhimu huo ni kama vile: ili kupata usalama, kuwazuia wengine kupatwa na hatari
hiyo n.k. Pia, wanafunzi wajadiliane kuhusu upande jua linakotua. Waelezane katika
vikundi vyao kuhusu njia za kufuata kutoka nyumbani kwao hadi shuleni na kutoka
shuleni hadi kwenye hospitali iliyo karibu na shule yao.
Katika shughuli ya tatu, wanafunzi katika vikundi vyao wajadiliane kuhusu mchoro
wa dira ulio kitabuni mwao. Wataje pande za dira zilizoonyeshwa kwa nambari.
Mwalimu anaweza kubeba dira halisi darasani na wanafunzi wakaiona na hata
kuigusa.
Majibu tarajiwa ni: 1. Kaskazini 2. Kaskazini Mashariki 3. Mashariki 4. Kusini
Mashariki 5. Kusini 6. Kusini Magharibi 7. Magharibi 8. Kaskazini Magharibi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi amwandikie
shangazi yake maelekezo ya kutoka nyumbani kwake hadi nyumbani kwao. Mwanafunzi
ayatume maelekezo hayo kwa mwalimu wake ili ayatathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kusakura matini kwenye
tovuti salama na kupata vifungu salama vya kusoma vya kiwango chake.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutumia vyombo vya kidijitali
kupata matini salama.
3. Mwalimu atathmini uchoraji wa dira wa mwanafunzi na kuonyesha pande zake
nane.
CH. Kuandika:Kuandikabarua
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 63)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia muundo wake.
b) Kuandika barua ya kiraki inayozingatia mada kwa kufuata kanuni zifaazo.
ch) Kujadili umuhimu wa barua ya kiraki katika mawasiliano.
93
Maswali dadisi
1. Je, unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
2. Barua za kiraki zinashughulikia masuala gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
kuandika insha mtandaoni na kurejelea vielelezo vya barua za kiraki.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoandika barua za kiraki.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza, Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia uandishi wa barua.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Kuendeleza mawasiliano na wenzake pamoja na wazazi kwa kutumia barua za kiraki.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuandika barua ya
kiraki kwa
kuzingatia
muundo,
mtindo, ujumbe,
mpangilio mzuri
wa mawazo na
lugha ya kuvutia.
Mwanafunzi
anaandika
barua ya kiraki
kwa kuzingatia
muundo,
mtindo, ujumbe,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kuvutia.
Mwanafunzi
anaandika
barua ya kiraki
kwa kuzingatia
muundo, mtindo,
ujumbe na
mpangilio
mzuri wa
mawazo.
Mwanafunzi
anaandika
barua ya kiraki
kwa kuzingatia
muundo,
mtindo na
ujumbe.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika
barua ya
kiraki.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watumie breli kusoma. Wanafunzi wenye
ulemavu kama vile vikono watumie sehemu za mwili walizozoea kutumia kuandika
insha. Wanafunzi wanaochukua muda zaidi kuelewa wapewe mazoezi zaidi ili
94
wajifunze kutokana nayo. Kwa upande mwingine, wanafunzi wanaoelewa kwa
haraka wapewe kazi za ziada na waruhusiwe kuwasaidia wenzao.
Maelezo ya jumla
Mada hii itamwezesha mwanafunzi kutumia barua ya kiraki katika mawasiliano.
Atakapoandika atakuza ubunifu katika mawasiliano. Hivyo basi, mwalimu ahakikishe
kuwa kila mwanafunzi anapata uwezo wa kuandika.
Kipindi cha 1: Barua ya kiraki
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 63)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia mada kwa kufuata kanuni zifaazo.
b) Kuandika barua ya kiraki inayozingatia mada kwa kufuata kanuni zifaazo.
Maswali dadisi
1. Je, umewahi kuandika barua? Ilihusu nini?
2. Je, unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu anaweza kubeba bahasha zilizo na barua zozote. Awaeleze wanafunzi
kuwa watu walizoea kutumiana barua kabla vifaa vya kidijitali kugunduliwa. Barua
zilitumiwa kupasha ujumbe. Pia, mwalimu anaweza kutafuta picha ya chumba cha
posta na kuwaonyesha wanafunzi darasani pamoja na kuwaeleza umuhimu wake.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 63, 2. Picha ya posta,
3. Bahasha, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa shughuli ya kwanza. Wanafunzi wakiwa wawili
wawili wajadiliane maswali waliyopewa kitabuni mwao. Wataje maraki zao, shule
wanakosomea kisha waeleze namna wao huwasiliana. Mwalimu akubali majibu yoyote
sahihi yanayolingana na njia mbalimbali za mawasiliano.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili. Awagawe wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao. Wanafunzi wajadili kuhusu michoro iliyo
kitabuni mwao. Wanafunzi waeleze umuhimu wa bahasha kama vile kuweka barua ili
kuituma. Wanafunzi wafahamu kuwa watu huweza kutuma barua kupitia posta au njia
nyingine. Wanafunzi wafahamu kuwa ulemavu sio kutoweza.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi kusoma na kujadili kielelezo
95
cha barua ya kiraki kilicho kitabuni mwao. Awaeleze kuhusu muundo wa barua
ya kiraki. Sharti barua ya kiraki iwe na: anwani, utangulizi, kiwiliwili, mwisho na
maagano.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi amwombe
mzazi au mlezi wake iwapo ana barua yoyote aliyowahi kuandika au kuandikiwa
amwonyeshe. Mwanafunzi aichunguze barua hiyo ili kubaini iwapo iliandikwa kwa
kuzingatia muundo wa barua ya kiraki.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua barua ya kiraki.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi ana uwezo wa kueleza muundo wa
barua ya kiraki.
3. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi ana uwezo wa kusoma barua ya kiraki.
Kipindi cha 2: Barua ya kiraki
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 65)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kujadili umuhimu wa barua ya kiraki katika mawasiliano.
2. Kufahamu utunzi wa barua ya kiraki katika mawasiliano.
Swali dadisi
Barua za kiraki zinashughulikia masuala gani na zina umuhimu gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaongoze wanafunzi kukumbuka muundo wa barua ya kiraki kisha
katika vikundi wajadiliane. Awafahamishe kuwa katika uandishi, alama za uakishaji
huzingatiwa pamoja na lugha sahihi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 65, 2. Bahasha,
3. Tarakilishi, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwakumbusha wanafunzi kuhusu muundo wa
barua ya kiraki.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na mahitaji yao. Mwalimu awaongoze wanafunzi kuvitaja vidokezo vya
kuandikia barua ya kiraki kwa mlezi au mzazi wa mmoja wao kuhusu usalama
shuleni kwao. Wanafunzi waandike vidokezo hivyo katika madaari yao. Awaelekeze
wanafunzi jinsi ya kuvitumia vidokezo hivyo katika kuandika insha ya barua ya
96
kirafiki. Mmoja wao awasomee wenzake barua waliyoandika ili waitathmini.
Wanafunzi wajadiliane kuhusu umuhimu wa kuandika barua ya kiraki. Kwa mfano,
kupasha ujumbe, kujuliana hali na kukuza stadi za uandishi na ubunifu.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi katika shughuli ya pili aandike barua kwenye
tarakilishi kwa raki yake akimweleza kuhusu matumizi ya dira. Mwanafunzi atumie
mtandao kuituma barua hiyo kwa mwalimu na wanafunzi wenzake ili waisome na
kuisahihisha.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike barua
kwa raki yake akimwalika ahudhurie sherehe ya siku ya kuzaliwa kwake. Mwalimu
atathmini barua ambazo wanafunzi wataandika. Mwalimu akubali barua zote
watakazoandika wanafunzi kisha azisome na kubandika ukutani zilizo bora.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ana uwezo wa kuandika vidokezo vya
kumwongoza anapoandika insha ya barua ya kiraki.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kuandika barua ya kiraki
mtandaoni na kuisambaza kwa wenzake.
3. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kuushirikisha msamiati wa
mada lengwa (dira) katika uandishi wake.
D. Saru:Ngelizanomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 66)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya ngeli za nomino ili kuzibainisha.
b) Kutambua nomino katika ngeli ya A-WA.
ch) Kuandika nomino za ngeli ya A-WA.
d) Kuchangamkia kutumia nomino za ngeli ya A-WA katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Nomino zinazorejelea viumbe hai ni zipi?
2. Nomino zinazorejelea viumbe hai hutumiwa vipi katika sentensi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake katika vikundi.
97
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga mafungu ya maneno.
Kufikiri kwa kina - kunakuzwa mwanafunzi anapowaza kwa kina kuhusu
atakachoandika.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa tarakilishi inapotumika kutambua nomino na
mafungu ya maneno.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano - unakuzwa kupitia kazi za vikundi.
Stadi za maisha - zinakuzwa mwanafunzi apojifanyia kazi darasani.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - kutunza vipakatalishi anavyotumia.
Uzalendo - kufanya kazi na wengine kwenye vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hufundisha mada ya saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Kutumia lugha sanifu miongoni mwa wenzake shuleni na nyumbani kama kielelezo
cha kuzingatia Kiswahili sanifu.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya A-WA na
kuzitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi yenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya A-WA na
anazitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi yenye
maana kwa
usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya A-WA na
anazitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi yenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa baadhi
ya nomino
katika ngeli
ya A-WA na
kutumia baadhi
ya nomino
hizo kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
umoja na wingi
wa maneno na
sentensi katika
ngeli ya A-WA.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia washughulikiwe vilivyo. Mwalimu anaweza
98
kuwaandikia nomino ubaoni au kuandaa video ya kuonyesha nomino mbalimbali za
viumbe hai ili watazame. Wanafunzi wenye matatizo ya kuona wanaweza kutumia
tarakilishi za breli katika kusoma na kuandika. Wanafunzi wanaoelewa kwa haraka
wapewe mazoezi zaidi. Wanafunzi wasioona mbali waketi karibu na ubao. Wanafunzi
wanaochukua muda kuelewa wapewe muda zaidi na wasaidiwe.
Maelezo ya jumla
Mwalimu awafahamishe wanafunzi kuwa mada hii inahusu ngeli ya A-WA. Ngeli
hii inahusisha viumbe wote wenye uhai yaani: binadamu, wanyama, ndege, wadudu,
malaika, samaki, Mungu na hata shetani. Huitwa ngeli ya A-WA kwani kiambishi ngeli
katika umoja ni a- na katika wingi ni wa-. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutunga
sentensi sahihi kwa kutumia nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Kipindi cha 1: Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya A-WA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 66)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Aeleze maana ya ngeli za nomino.
b) Aweze kutambua nomino katika ngeli ya A-WA.
ch) Aweze kuandika nomino za ngeli za A-WA katika umoja na wingi.
Swali dadisi
Nomino zinazorejelea viumbe hai ni zipi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa ngeli ni kundi la maneno. Awaeleze kuwa viumbe
wote wenye uhai huwa katika ngeli ya A-WA. Anaweza kuwapeleka wanafunzi nje ya
darasa wakatazame viumbe hai wanaopatikana shuleni kwao au karibu na shule yao.
Mifano: watu mbalimbali, mifugo, ndege na wadudu.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 66,
2. Chati yenye picha za watu, wanyama na wadudu,
3. Tarakilishi, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu atangulize kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi
kutazama na kujadili michoro iliyo kitabuni mwao. Awaongoze kutaja nomino zilizo
katika ngeli ya A-WA za watu, wanyama, ndege na wadudu. Mwalimu awaelekeze
99
wanafunzi kujadiliana kuhusu maana ya ngeli. Mwalimu ahakikishe kila mwanafunzi
anashiriki katika shughuli hii.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kwenye shughuli ya pili. Waandike wingi wa majina
ya watu, wanyama, ndege na wadudu waliotaja katika shughuli ya kwanza. Kila
mwanafunzi amsomee mwenzake majina hayo ya wingi ili wayatathmini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
kwenye tarakilishi majina ya watu, wanyama na wadudu wanaopatikana nyumbani
kwao kisha awatumie wenzake na mwalimu mtandaoni ili wayatathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaelewa maana ya ngeli za nomino.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutambua nomino zilizo
kwenye ngeli ya A-WA.
3. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kuandika nomino za ngeli ya
A-WA katika umoja na wingi.
Kipindi cha 2: Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya A-WA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa wa 67)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya A-WA.
b) Kutumia nomino za ngeli ya A-WA katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, wavifahamu viambishi vya nomino katika ngeli ya A-WA katika umoja na wingi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa baadhi ya majina katika ngeli ya A-WA hubadilika
katika umoja na wingi. Mifano: mtu - watu, kiroboto - viroboto. Yapo majina mengine
ambayo huwa hayabadiliki. Mifano: mbuzi -mbuzi, kupe - kupe.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 67, 2. Chati yenye michoro, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaongoze wanafunzi katika kutazama michoro
waliyopewa kitabuni mwao kisha wajaze nafasi wazi katika sentensi zilizo chini ya
kila mchoro. Majibu tarajiwa: bata mmoja - mabata watatu, mvuvi mmoja - wavuvi
wawili, paka mmoja -paka wawili.
100
Mwalimu awaelekeze wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya pili. Wachague
nomino za ngeli ya A-WA kutoka kwa kundi la maneno walilopewa kitabuni mwao.
Kila mwanafunzi aandike mafungu ya nomino hizo katika umoja na wingi. Mfano:
Daktari mmoja -Madaktari wawili.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi asome kifungu
alichopewa kisha atambue nomino za ngeli ya A-WA. Aziandike nomino hizo katika
umoja na wingi.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada
1. mtoto - watoto 5. fahali - mafahali
2. kipepeo - vipepeo 6. mbuzi - mbuzi
3. panzi - panzi 7. kupe - kupe
4. kunguru - kunguru
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kusoma mafungu ya maneno
katika ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua viambishi vya
nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi.
Ngeli za nomino
Kipindi cha 1: Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya A-WA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 69)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya A-WA katika
umoja na wingi.
b) Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho sahihi wa kisaru.
Maswali dadisi
1. Je, unajua nomino gani za ngeli ya A-WA?
2. Nomino zinazorejelea viumbe hai hutumiwa vipi katika sentensi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu anaweza kutafuta nyenzo mbalimbali za kufunzia utunzi wa sentensi
katika ngeli ya A-WA. Anaweza pia kurekodi sentensi zilizotungwa na wanafunzi
wanaposoma sentensi hizo kisha awape wasikilize.
101
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 69, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa shughuli ya kwanza kwa kuwaelekeza wanafunzi
watambue nomino za ngeli ya A-WA kutoka kwa nomino kadhaa zilizoandikwa
ubaoni. Mwalimu ahakikishe anaandika ubaoni nomino kadhaa zilizochanganywa
ili kukuza uwezo wa mwanafunzi wa kutambua nomino za ngeli ya A-WA. Katika
vikundi, wanafunzi watunge sentensi sahihi kwa kutumia nomino walizotambua.
Mwalimu awagawe wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya pili. Mwanafunzi
mmoja asome sentensi zilizo kitabuni mwao katika umoja. Mwanafunzi mwingine
asome sentensi hizo katika wingi. Wanafunzi wajadiliane kuhusu viambishi vya ngeli
ya A-WA vilivyotumika katika sentensi walizosoma.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi akisaidiwa
na mzazi au mlezi wake ataje majina ya wanyama watano wanaofugwa kaskazini
mashariki mwa Kenya. Atunge sentensi katika umoja na wingi akitumia majina hayo.
Anaweza kutumia mtandao kufahamu wanyama wanaofugwa sehemu hiyo.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada
1. Ngamia anakunywa maji. - Ngamia wanakunywa maji.
2. Ng’o mbe anakula nyasi. - Ng’omb e wanakula nyasi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutaja nomino katika ngeli ya
A-WA katika umoja na wingi.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutambua sentensi
zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya A-WA.
Kipindi cha 2: Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya A-WA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 70)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya A-WA katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
b) Kufahamu matumizi ya nomino za ngeli ya A-WA katika mawasiliano.
102
Swali dadisi
Ni viambishi vipi vinavyotumiwa unapotunga sentensi za ngeli ya A-WA katika
umoja na wingi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaongoze wanafunzi kutaja nomino za ngeli ya A-WA walizojifunza.
Awaeleze kuwa wanapotunga sentensi katika ngeli ya A-WA, kiambishi ngeli huwa ni
a- katika umoja na wa- katika wingi. Anaweza kuandika sentensi sahihi walizotunga
kwenye chati ili watambue viambishi vya ngeli ya A-WA.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 70, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya kwanza watazame na kujadili
michoro iliyo kitabuni mwao. Wanafunzi wataje majina ya michoro hiyo. Watunge
sentensi sahihi katika umoja na wingi wakitumia majina ya michoro waliyotaja.
Wanafunzi wataje majina mengine ya viumbe wengine wa kategoria sawa na za walio
katika michoro waliyotazama. Watumie majina hayo kutunga sentensi sahihi katika
umoja na wingi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili. Waandike sentensi walizotunga
katika shughuli ya kwanza kwenye tarakilishi. Viambishi vya ngeli viandikwe kwa
kutumia chapa koza. Wanafunzi wawatumie wenzao pamoja na mwalimu sentensi
hizo ili wazisome na kuzitathmini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi akisaidiwa
na mlezi au mzazi wake ataje majina ya wanyama watatu wanaopatikana katika Ziwa
Victoria. Atumie majina hayo kutunga sentensi sahihi katika umoja na wingi.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada:
1. Baba alivua ngege wengi. 2. Kiboko huyu ni mkubwa sana.
Kimeidhinishwa na KICD
103
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza:
1. Kutambua nomino za ngeli ya A-WA.
2. Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya A-WA akizingatia
upatanisho sahihi wa kisaru.
3. Kutunga sentensi sahihi za ngeli ya A-WA kwenye tarakilishi katika umoja na
wingi na kuzituma kwa wenzake ili wazitathmini.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu akubali majibu yenye maneno ya heshima kwa kuzingatia muktadha wa
kuomba ruhusa ya kwenda msalani. Majibu tarajiwa ni: naomba, tafadhali.
2. Majibu yaonyeshe maneno ya upole yanayotumika kwa mtu aliyekosewa, kama vile
pole, niwie radhi, samahani.
3. Jua huchomoza kutoka upande wa mashariki.
4. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi amezingatia muundo wa kuandika barua
ya kiraki. Pia, mwalimu ahakikishe iwapo mwanafunzi amejikita katika muktadha
aliopewa (kumwelekeza mjomba wake).
5. Majibu yoyote ambayo yanahusu majukumu ya kiranja yakubalike, kwa mfano:
kuwakilisha wanafunzi wengine, kuhakikisha nidhamu inadumishwa darasani,
kuwasilisha changamoto za wanafunzi kwa walimu n.k.
6. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ameandika muhtasari wa matini kuhusu
usalama wa mtoto. Mwalimu atumiwe kazi hiyo kwenye mtandao.
7. Mwalimu akubali sentensi zozote sahihi zilizotumia majina ya ngeli ya A-WA katika
umoja na wingi. Mifano: Bata anacheza majini. - Mabata wanacheza majini.
8. Mwalimu atathmini sifa za pweza na mamba ambazo wataandika kutoka mtandaoni.
9. a) Kunguni ni wadudu hatari.
b) Mabata hawa wanapendeza.
10. Mwalimu atathmini mchoro wa dira pamoja na pande zake nne ambazo ni
Kaskazini, Mashariki, Kusini na Magharibi.
Kimeidhinishwa na KICD
104
Kimeidhinishwa na KICD
USHAURI NASAHA
5
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 72)
A. Kusikiliza na Kuzungumza: Methali
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua methali katika matini tofauti tofauti.
b) Kutaja methali zinazohusu malezi ili kuzitumia katika mawasiliano.
ch) Kueleza maana za methali kuhusu malezi.
d) Kutumia methali zinazohusu malezi katika mawasiliano.
e) Kuchangamkia matumizi ya methali katika miktadha mbalimbali.
Maswali dadisi
1. Ni methali gani zinazohusu malezi?
2. Methali hutumiwa kufanya nini?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kidijitali
katika kusikiliza na kusoma methali.
Kujiamini na kujithamini - kunakuzwa mwanafunzi anapowasiliana na
wenzake katika vikundi na anapotunga methali.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapotafakari kuhusu maana za
methali anazozitumia katika mawasiliano.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapowaza kuhusu maneno atakayotumia
kutunga sentensi zenye methali zinazohusu malezi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Ushauri nasaha - methali zinahusu malezi mema katika jamii kwa jumla.
Stadi za maisha - mwanafunzi anatumia methali kujieleza na kuwanasihi
wenzake.
105
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Heshima - mwanafunzi anajifunza kumheshimu na kumwajibikia mlezi wake
au mwenzake.
Uaminifu - mwanafunzi anapotunga methali binafsi bila kunakili za wenzake.
Mapenzi - mwanafunzi anapokubali kuelekezwa na mwenzake, mlezi au mzazi
wake na kufanya shughuli katika kikundi bila ugomvi.
Uhusiano na masomo mengine
Muziki, Kiingereza, Lugha za kiasili - masomo haya yanafunza mada kuhusu
methali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake shuleni na nyumbani kuhusu matumizi ya
methali ili kuimarisha mawasiliano.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
methali za
malezi, kueleza
maana za
methali hizo na
kutumia methali
hizo kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
methali
za malezi,
anazitolea
maelezo
mwafaka na
anazitumia
kwa ufasaha na
urahisi katika
mawasiliano.
Mwanafunzi
anatambua
methali
za malezi,
anazitolea
maelezo
mwafaka na
anazitumia
katika
mawasiliano.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
methali za
malezi na
anazitolea
maelezo
mwafaka.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
methali za
malezi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wenye uwezo wa kungamua wanayojifunza mara moja baada ya
kushirikishwa katika shughuli za ujifunzaji, wapewe fursa ya kutaja na kueleza
methali zaidi kuhusiana na malezi.
Wanafunzi wasio na uelewa wa haraka, wapewe muda zaidi kabla ya kufahamu
wanayojifunza. Washirikishwe katika shughuli zaidi na kupewa muda zaidi wa
kujifunza.
Wanafunzi wenye mahitaji ya kisaikolojia kutokana na matukio katika jamii
wasaidiwe na mwalimu kujiamini na kuchangamkia ujifunzaji. Mwalimu anaweza
kuwahusisha wazazi au walezi katika kutatua changamoto hizo.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema au kusikia, watambue methali kwa kuzipigia
mistari au kuzikoleza rangi kwa kutumia tarakilishi.
106
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli au wasikilize methali
zikisomwa na mwalimu, wanafunzi wenzao au kutoka kwenye kanda iliyorekodiwa.
Maelezo ya jumla
Mada ya methali itamwezesha mwanafunzi kutambua maneno na maana ya maneno
hayo kama yalivyotumiwa katika methali. Inachangia katika kuboresha uwazaji wa
kina wa mwanafunzi na kuboresha mawasiliano.
Kipindi cha 1: Methali zinazohusu malezi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 72)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua methali katika matini tofauti tofauti.
b) Kutaja methali zinazohusu malezi ili kuzitumia katika mawasiliano.
ch) Kueleza maana za methali zinazohusiana na malezi.
Swali dadisi
Je, unajua methali zozote zinazohusu malezi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Methali zinazohusu malezi husaidia kukuza tabia njema. Ili kufanikisha ujifunzaji wa
methali, mwalimu ajiandae vyema kabla ya kipindi. Awe ametati kuhusu methali
mbalimbali zinazohusu malezi. Pia, mwalimu awe na nyenzo zinazofaa kumshirikisha
kila mwanafunzi kulingana na mahitaji yake.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 72, 2. Breli,
3. Kadi zenye silabi za sauti, 4. Tarakilishi, 5. Rununu.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza kwa kuwaelekeza wanafunzi
wawili wawili wasome darasani mazungumzo kati ya Nyanya na Mjukuu. Mwalimu
ahakikishe mwanafunzi anatamka maneno kwa ufasaha. Wanafunzi wanaokosea
wasahihishwe. Baada ya kusoma, wanafunzi wajibu maswali waliyopewa kitabuni
mwao. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua maana ya methali pamoja na
mifano yake (iliyotumiwa katika mazungumzo waliyosoma).
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya shughuli ya pili. Awagawe wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao. Awaulize wanafunzi wataje methali zozote
za Kiswahili wanazojua. Wanafunzi wajadili maana za methali hizo kisha watambue
107
Kimeidhinishwa na KICD
methali zinazohusu malezi kutoka kwa zile walizojadili. Baadhi ya methali zisizohusu
malezi ni kama vile: a) Kuku mgeni hakosi kamba mguuni. b) Mwerevu hajinyoi.
ch) Ngoma ikilia sana hupasuka. d) Kukosa njia ndiko kujua njia, n.k.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi katika vikundi kujadili
vitendo katika kila mchoro waliopewa kitabuni mwao. Wanafunzi wajadiliane
maswali waliyopewa baada ya michoro. Waelezane kuhusu kazi ambazo wao huzifanya
nyumbani kuwasaidia walezi au wazazi wao. Mwalimu awahimize wanafunzi
kuwasaidia walezi au wazazi wao kufanya kazi mbalimbali nyumbani ambazo ni za
kiwango chao.
Katika kazi ya ziada, mwanafunzi amwombe mlezi au mzazi wake amtajie mafunzo
yoyote matano mazuri aliyopata kutoka kwa walezi wake. Mwanafunzi awaeleze
wenzake darasani katika kipindi kijacho ili wajifunze.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutaja methali za Kiswahili.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kueleza maana ya methali.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutumia methali hizo kwa
ufasaha na urahisi katika mawasiliano.
Kipindi cha 2: Methali zinazohusu malezi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 74)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana za methali kuhusu malezi.
b) Kutumia methali zinazohusu malezi katika mawasiliano.
ch) Kuchangamkia matumizi ya methali katika miktadha mbalimbali.
Swali dadisi
Methali hutumiwa kutekeleza shughuli gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua, kutamka na kutumia methali zinazohusu malezi anaboresha
matumizi yake ya lugha. Vilevile, anaboresha mienendo yake. Mwalimu anaweza kubuni
shughuli za ujifunzaji tofauti na zilizopendekezwa katika kipindi hiki ili kukuza hamu
ya kujifunza zaidi kwa wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kikapu chenye kadi zilizo na methali mbalimbali za malezi,
108
Kimeidhinishwa na KICD
2. Kamusi ya methali, 3. Tarakilishi,
4. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 74.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi waeleze
maana ya methali. Awaulize wataje methali mbalimbali walizojifunza katika kipindi
kilichotangulia.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi wasome kifungu kilicho
katika kitabu chao. Kila mwanafunzi asome kifungu hicho kwa matamshi sahihi.
Wanafunzi wawili wawili washirikiane kukamilisha methali zilizotumika katika
kifungu walichosoma kisha wajadili maana zao.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili. Mwanafunzi mmoja awe
akitoa kadi iliyoandikwa methali ya malezi kutoka kikapuni. Wanafunzi wengine
washirikiane kujadili maana ya methali hiyo. Mchezo huu uendelee hadi kadi zote
kikapuni zichukuliwe. Mwalimu ahakikishe kuwa darasa zima linashiriki katika
kujadili na kueleza maana za methali hizo. Mchezo huu unaweza kuwa shindano kati
ya vikundi viwili ambapo kikundi kitakachopata maana za methali nyingi kitapewa
alama nyingi. Kikundi kitakachokosa kupata jibu kitakosa alama. Shindano hili
litamchochea mwanafunzi kuwa na hamu ya kujifunza methali zaidi ili kuhakikisha
kikundi chake kimeibuka na ushindi katika vipindi vijavyo.
Katika vikundi, wanafunzi watunge vifungu vifupi wakitumia methali walizojadili
kutoka kwa kadi za kikapuni. Waandike vifungu hivyo kwenye tarakilishi kisha
wawatumie wenzao mtandaoni ili wavisome na kuvitathmini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kuhusu jinsi ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi
amwulize mlezi au mzazi wake amweleze umuhimu wa kuwapatia watoto malezi
mema. Mwanafunzi awaeleze wenzake darasani ili wajifunze.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua methali za malezi.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutumia methali za malezi
katika mawasiliano.
B. Kusoma: Kusoma kwa ufahamu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 75)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya shairi, ubeti na mshororo ili kuvibainisha.
109
Kimeidhinishwa na KICD
b) Kusoma shairi kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
ch) Kutambua beti na mishororo katika shairi.
d) Kutambua shairi kutokana na umbo lake.
e) Kufurahia kutumia lugha ya ushairi anapozungumzia ushairi.
Maswali dadisi
1. Unafahamu msamiati upi wa ushairi?
2. Mashairi yanaweza kuwasilisha ujumbe gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - huu unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
kusoma mashairi mbalimbali.
Kujiamini na kujithamini - umilisi huu unakuzwa mwanafunzi anapowasiliana
na wenzake katika vikundi.
Uwazaji kina - unakuzwa mwanafunzi anapong’amua ujumbe ulio katika shairi.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anapoimba au kukariri shairi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya maendeleo endelevu - mwanafunzi anapotafuta suluhu kwa masuala
mtambuko yanayojitokeza katika shairi.
Stadi za maisha - mwanafunzi atayatambua haya kutokana na ujumbe katika
mashairi ya ushauri nasaha.
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima - mashairi yanahusu ushauri nasaha na kuendeleza shughuli za
makundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza, Muziki, Somo la Dini na Lugha za kiasili - masomo haya
yanashughulikia nyimbo na mashairi.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
mashairi katika jamii.
110
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
shairi, ubeti,
mshororo na
ujumbe na
kulisoma au
kulikariri kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
shairi, ubeti,
mshororo na
ujumbe na
analisoma au
kulikariri kwa
ufasaha na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
shairi, ubeti,
mshororo na
ujumbe na
analisoma au
kulikariri kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
vipengele
vya shairi na
analisoma au
kulikariri.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
baadhi ya
vipengele
vya shairi na
pia anajaribu
kulisoma au
kulikariri.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema au kusikiliza watambue maana ya vipengele
vya mashairi lengwa kwa kuandika na kupigia mistari msamiati wa shairi.
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli au wasikilize maana ya
msamiati wa shairi husika ukielezwa na mwalimu au wenzao.
Wanafunzi wanaoelewa kwa haraka wapewe mazoezi zaidi huku wenzao
wanaochukua muda zaidi kuelewa wapewe muda zaidi ili wakamilishe shughuli
zao.
Maelezo ya jumla
Mada ya kusoma kwa ufahamu itamwezesha mwanafunzi kutambua maana ya
msamiati wa kishairi na kuweza kuutumia katika mawasiliano.
Kusoma ushairi kutakuza hamu ya mwanafunzi kujifunza zaidi ili kuyafahamu
maudhui mbalimbali katika mashairi.
Kipindi cha 1: Ujumbe na lugha katika ushairi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 75)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza tofauti za kimaana kati ya shairi, ubeti na mshororo ili kuvibainisha.
b) Kusoma shairi kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
ch) Kuandika beti za shairi anazosomewa na mwalimu.
d) Kutambua beti na mishororo katika shairi.
111
Kimeidhinishwa na KICD
Swali dadisi
Unaufahamu msamiati gani wa ushairi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua msamiati wa ushairi na kuutumia kwa usahihi katika
sentensi za ushairi huboresha mawasiliano yake.
Mwalimu asisitize mwanafunzi akariri au aimbe mashairi ambayo amewahi kusikia au
kufundishwa iwapo anakumbuka.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 4. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 75,
2. Tarakilishi, 5. Kanda iliyorekodi shairi kuhusu malezi.
3. Rununu,
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza ambapo atawauliza
wanafunzi maswali tangulizi kuhusu mashairi. Mwalimu awaulize wanafunzi
wajadiliane kuhusu maana ya shairi. Pia, awaulize wanafunzi iwapo wanakumbuka
shairi lolote ambalo waliwahi kufunzwa au kusikia. Iwapo wanafunzi wanakumbuka
basi wawaeleze wenzao darasani shairi hilo lilihusu nini. Wanafunzi wanaweza
kujitolea kukariri au kuimba shairi lolote wanalokumbuka.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awakaririe wanafunzi shairi lililo katika kitabu
chao. Mwalimu ahakikishe anakariri shairi hilo kwa matamshi bora na ikiwezekana
kwa mahadhi. Iwapo mwalimu ana matatizo ya matamshi, basi anaweza kumwomba
mwanafunzi mmoja akariri shairi hilo. Baada ya mwalimu kukariri, mwalimu awagawe
wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao. Katika vikundi hivyo,
wanafunzi wakariri shairi hilo baada ya mwalimu. Hatimaye, mwanafunzi mmoja
mmoja katika kila kikundi akariri shairi hilo peke yake huku wanafunzi wenzake
katika kikundi chao wakimsikiliza. Wanafunzi wajadiliane kuhusu ujumbe wa shairi
husika pamoja na maswali mengine yanayotokana na shairi hilo.
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa mkusanyiko wa beti huunda shairi. Wingi wa
shairi ni mashairi. Shairi linaweza kukaririwa, kusomwa au kuimbwa. Silabi za kati
na za mwisho katika kila kipande cha kila mstari huitwa vina. Umoja wa vina ni kina.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa ushirikiano na walezi
au wazazi wao. Mwanafunzi amwombe mlezi au mzazi wake amkaririe shairi lolote
analojua. Mwanafunzi aandike shairi hilo katika daari lake. Baada ya kuandika, kila
mwanafunzi awasomee wanafunzi wenzake shairi hilo darasani ili walitathmini na
kupata mafunzo.
112
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua msamiati wa mada
lengwa uliotumika katika shairi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kusoma au kukariri shairi
lengwa kwa ufasaha.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kueleza ujumbe wa shairi.
Kipindi cha 2: Ujumbe na lugha katika ushairi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 77)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua shairi kutokana na umbo lake.
b) Kutambua beti na mishororo katika shairi.
ch) Kufurahia kutumia lugha ya ushairi anapozungumzia ushairi.
Swali dadisi
Mashairi yanaweza kuwasilisha ujumbe gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kusoma au kukariri shairi humsaidia mwanafunzi kukuza uelewa wa misamiati
mbalimbali ya kishairi ili kuitumia katika kuimarisha mawasiliano katika miktadha
ya kishairi.
Beti na mishororo humfahamisha mwanafunzi matukio yanayotokea katika
mazingira mbalimbali. Pia, humwezesha kujitambua na kuthamini mazingira yake
na ya watu wengine. Mashairi hukuza ubunifu wa mwanafunzi na humpa hamu ya
kujifunza zaidi hasa anaposhiriki katika kukariri mashairi yanayosisimua.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 77, 2. Breli,
3. Tarakilishi, 4. Rununu,
5. Diwani au mkusanyiko wa mashairi, 6. Kanda iliyorekodiwa inayokariri
shairi linalohusu malezi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza kwa kuwauliza wanafunzi
wasikilize shairi litakalokaririwa kutoka kwa rekoda, rununu au tarakilishi ya mwalimu.
Mwalimu ahakikishe wanafunzi wanasikiliza shairi hilo kwa makini. Mwalimu aandae
113
Kimeidhinishwa na KICD
shairi hilo na kulirekodi kabla ya kipindi. Baada ya wanafunzi kusikiliza shairi hilo,
waliandike katika madaari yao. Baadaye, mwalimu awagawe wanafunzi katika
vikundi viwili ili wakariri shairi husika. Wajadiliane kuhusu ujumbe wa shairi husika.
Pia, wataje idadi ya mishororo katika shairi hilo.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaulize wanafunzi washirikiane katika vikundi
kutunga ubeti mmoja wa shairi kuhusu malezi mema. Kila mwanafunzi ashirikishwe
katika utunzi huu. Wanafunzi wanaotatizika wasaidiwe. Baada ya kutunga ubeti huo,
mmoja wao auandike ubaoni ili wanafunzi wenzao pamoja na mwalimu wausome na
kuutathmini. Makosa ya tahajia yasahihishwe.
Katika kufanya kazi ya ziada, mwalimu amwelekeze mwanafunzi atafute shairi lolote
mtandaoni, alisome na kuliandika katika daari lake. Aeleze ujumbe wa shairi hilo,
na ahesabu idadi ya mishororo yake. Hatimaye, amkaririe au amwimbie mlezi au
mzazi wake shairi hilo. Pia, anaweza kuwakariria wenzake darasani ili walitathmini
na kujifunza.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kusoma shairi kwa ufasaha.
2. Mwalimu atathmini uelewa wa mwanafunzi wa ujumbe wa shairi kwa ufasaha.
CH. Kuandika: Kuandika Insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 78)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua vifungu vya maelezo katika matini.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa kuzingatia mtindo na muundo ufaao.
ch) Kuchangamkia utunzi mzuri wa insha ya maelezo ili kujenga ubunifu wake.
Swali dadisi
Je, unazingatia mambo gani unapoandika insha ya maelezo?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - huu unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
kuandika na kusambaza insha zao mtandaoni.
Kujiamini na kujithamini - umilisi huu unakuzwa mwanafunzi anapowasiliana
na wenzake katika vikundi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya maelezo.
114
Kimeidhinishwa na KICD
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoulizia swali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia - unakuzwa mwanafunzi anapotangamana na wenzake darasani na katika
makundi.
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika vikundi.
Uwajibikaji - mwanafunzi anapoandika insha mwenyewe bila kunakili za
wengine.
Upendo - mwanafunzi anapowasiliana vyema na wenzake katika makundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia stadi ya
kuandika.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi bora katika mawasiliano.
Vigezo vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kueleza maana ya
insha ya maelezo
na kutaja mambo
anayozingatia
anapoiandika.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya insha ya
maelezo na
kutaja mambo
anayozingatia
kuiandika kwa
ufasaha na
urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya insha ya
maelezo na
kutaja mambo
anayozingatia
kuiandika kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anaeleza maana
ya insha ya
maelezo na
kutaja baadhi
ya mambo
anayozingatia
kuiandika.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza maana
ya insha ya
maelezo na
kutaja mambo
anayozingatia
kuiandika.
115
Kimeidhinishwa na KICD
Kuandika insha
ya maelezo
inayotumia
vivumishi na
vielezi kwa
ufasaha ili
kujenga picha
dhahiri kwa
kuzingatia kanuni
za lugha, na
mpangilio mzuri
wa mawazo.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio
mzuri wa
mawazo na kwa
ubunifu wa hali
ya juu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo
kwa kuzingatia
lugha,
mpangilio
mzuri wa
mawazo na
lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo
kwa kuzingatia
baadhi ya
kanuni za lugha.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika insha
ya maelezo.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli kusoma maana ya insha
ya maelezo na mambo ya kuzingatia wanapoiandika.
Wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali yanayochangia kutozingatia kanuni bora za
uandishi wapewe mazoezi ya kutosha kabla ya kuandika insha kama vile kupanga
sentensi zilizotarakanywa katika aya ili kuboresha mtiririko wa mawazo.
Wanafunzi wenye changamoto ya kutumia mkono kuandika wapewe muda zaidi
wa kuandika insha.
Maelezo ya jumla
Mada ya kuandika itamwezesha mwanafunzi kukuza ubunifu wake, kufahamu kanuni
za uandishi bora ili kuimarisha mawasiliano yake.
Hati sa na inayosomeka ni muhimu katika mawasiliano kwa kuwa itawezesha kazi ya
mwanafunzi kusomeka kwa urahisi. Mwalimu asisitize umuhimu wa mtiririko mzuri
wa mawazo.
Kipindi cha 1: Insha ya maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 78)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya maelezo kwa kuzingatia muundo.
b) Kusoma na kuandika muhtasari wa insha ya maelezo.
Swali dadisi
Je, unazingatia mambo yapi unapoandika insha ya maelezo?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapochangamkia utunzi wa insha ya maelezo hujenga ubunifu wake na
116
Kimeidhinishwa na KICD
kuweza kuandika insha za kusisimua. Mwalimu amhusishe mwanafunzi katika shughuli
mbalimbali zitakazomwezesha kuwa mwandishi bora. Ampongeze mwanafunzi kwa
kila hatua anayopiga katika uandishi ili aendelee kujithamini. Mwanafunzi awe na
vifaa vyote anavyohitaji katika kujifunza kuandika insha. Mwalimu ahakikishe kuwa
ana nyenzo zote za ujifundishaji kabla ya kipindi. Vifaa vya kiteknolojia vikaguliwe
kabla ya kipindi ili kuhakikisha vitatumiwa bila changamoto.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 78, 2. Breli, 3. Rekoda.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza. Amwelekeze mwanafunzi
mmoja asimame mbele ya darasa. Wanafunzi wenzake watoe maelezo yoyote kumhusu
mwanafunzi huyo. Mwalimu akubali majibu yoyote (chanya) ya wanafunzi kumhusu
mwanafunzi huyo. Baada ya wanafunzi kutoa maelezo hayo, wajigawe katika vikundi
viwili. Kikundi kimoja kitoe maelezo kuhusu darasa lao. Kikundi cha pili kitoe maelezo
kuhusu shule yao. Wajadiliane.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awasomee wanafunzi kifungu chochote cha maelezo
huku wakimsikiliza kwa makini. Mwalimu ahakikishe ameandaa kifungu hicho
mapema kabla ya kipindi hiki na akisome kwa matamshi sahihi. Iwapo mwalimu
ana matatizo ya matamshi, anaweza kumteua mwanafunzi mmoja akasoma kifungu
hicho. Baada ya kusoma kifungu hicho, mwalimu awapange wanafunzi katika vikundi
ili wajadili ujumbe unaojitokeza katika kifungu husika. Baadaye, kila mwanafunzi
aandike katika daari lake muhtasari wa kifungu alichosikiliza. Mwanafunzi ambaye
hakuelewa kifungu hicho anaweza kusomewa tena.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya shughuli ya tatu kwa kusoma mfano wa
insha ya maelezo ulio kitabuni mwao kwa sauti na kwa zamu wakiwa katika vikundi
viwili. Baada ya kusoma, wajadili mafunzo yaliyo katika mfano wa insha waliyosoma.
Wanafunzi waeleze maana ya maneno yaliyokolezwa rangi katika kielelezo cha insha
husika. Wanaweza kutumia kamusi.
Hatimaye, mwalimu awaeleze wanafunzi kuhusu muundo wa kuandika insha ufaao.
Awaeleze kuwa sharti insha hii iwe na mada, mtiririko wa mawazo, itumie saru
sahihi na ivutie msomaji. Kila mwanafunzi aandike insha ya maelezo kuhusu shule
yao. Awasomee wanafunzi wenzake darasani katika kipindi kijacho.
Katika kufanya kazi ya ziada, mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi ataje watu
ambao humpa ushauri mzuri kisha aeleze kuhusu ushauri ambao watu hao humpa.
Mwanafunzi awaeleze wenzake darasani kuhusu ushauri huo ili wajifunze.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada: Mwalimu akubali majibu yoyote yanayooana na
ushauri nasaha moja kwa moja. Watu waliotajwa wawe wana uwezo wa kutoa ushauri
mzuri.
117
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua insha ya maelezo
kwa kuzingatia muundo.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuandika muhtasari wa insha
ya maelezo kwa kuzingatia ujumbe, sentensi sahihi na sanifu.
Kipindi cha 2: Insha ya maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 80)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika insha ya maelezo kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
b) Kufahamu utunzi mzuri wa insha ya maelezo ili kujenga ubunifu wake.
Swali dadisi
Je, unazingatia mambo yapi unapoandika insha ya maelezo?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae maelezo kuhusu mambo ya kuzingatia katika uandishi wa insha ya
maelezo ili kuwafaa wanafunzi hasa wasioweza kuona michoro. Anaweza kumhusisha
mwalimu mwingine kutoa maelezo hayo ikiwa ana changamoto.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 80, 2. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwateua wanafunzi wachache wawasomee wenzao
darasani insha za maelezo walizoandika kuhusu shule yao. Mwalimu awasahihishe
panapostahili.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi wawili wawili
watazame na kujadili michoro iliyo kwenye kitabu chao. Wanafunzi waeleze vitendo
vinavyotendeka katika michoro hiyo. Pia, waeleze umuhimu wa watoto kuwasaidia
walezi au wazazi wao kufanya kazi mbalimbali nyumbani. Kila mwanafunzi aandae
vidokezo vya kuandika insha kulingana na michoro husika na avitumie kuandika
insha ya maelezo. Iwapo kuna muda, wanafunzi wachache wanaweza kuwasomea
wenzao maelezo waliyoandika ili wayatathmini.
Katika shughuli ya pili, mwalimu amteue mwanafunzi mmoja awasomee wenzake
kifungu kilicho kitabuni mwao. Kifungu hicho ni kielelezo cha insha ya maelezo.
Baada ya kusomewa kifungu hicho, wanafunzi wajadili kuhusu ushauri wa walimu
unaoangaziwa katika kielelezo walichosoma. Pia, wanafunzi wajadiliane kuhusu hatua
zinazochukuliwa kwa wanafunzi wasiofuata ushauri wa walimu katika shule yao.
118
Kimeidhinishwa na KICD
Katika kufanya kazi ya ziada, mwalimu amwagize kila mwanafunzi aandike insha fupi
ya maelezo kwa kutumia tarakilishi. Insha hiyo imhusu mtu yeyote mwenye nidhamu
ambaye angependa kumuiga maishani. Mwanafunzi ahifadhi insha yake kwenye faili
kwa jina la mtu huyo. Baadaye, awatumie wenzake pamoja na mwalimu insha hiyo
kwa kutumia mtandao ili waitathmini na kuisahihisha.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika insha ya maelezo
kwa kuzingatia muundo na mtindo sahihi, sentensi sahihi na sanifu, mtiririko
wa mawazo na ubunifu.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuendeleza insha ya maelezo
kwa kutumia maneno yanayofaa.
D. Saru:Umojanawingiwanomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 82)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino za ngeli ya U-I.
b) Kuandika nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
ch) Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya U-I.
d) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya U-I katika
umoja na wingi.
e) Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
Maswali dadisi
1. Je, nomino zinazorejelea mimea na vitu vya kimaumbile ni zipi?
2. Je, ni nomino gani za ngeli ya U-I unazozijua?
3. Je, katika sentensi, viambishi vya ngeli ya U-I ni vipi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika kazi
za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
kutambua aina za maneno lengwa na kutunga sentensi mtandaoni na katika
kusikiliza mafungu ya maneno kwenye kinasasauti.
119
Kimeidhinishwa na KICD
Kufikiria kwa kina - kunakuzwa mwanafunzi anapowaza na kudadisi
atakachoandika.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi akitumia aina ya neno
lengwa.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano - kutokana na kufanya kazi pamoja.
Stadi za maisha - kujifanyia kazi darasani.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - mwanafunzi anapotunza vifaa anavyotumia.
Maadili mbalimbali yanaweza kulengwa katika utungaji wa sentensi kama vile
upendo, uaminifu, uzalendo, amani na umoja.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia mada ya saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu mawasiliano yenye
kuzingatia kanuni za kisaru.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
umoja na wingi
wa nomino za
ngeli ya U-I
na kuzitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya U-I na
anazitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya U-I na
anazitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya U-I na
kutumia baadhi
ya nomino
hizo kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
umoja na wingi
wa nomino za
ngeli ya U-I.
120
Kimeidhinishwa na KICD
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli kusoma umoja na wingi wa
nomino za ngeli ya U-I. Pia, mwalimu anaweza kuleta darasani vitu halisi ili waviguse
na kuvitambua. Mwalimu arekodi video yenye mifano ya aina za nomino lengwa.
Pia, anaweza kurekodi sentensi zenye nomino za ngeli ya U-I zikisomwa ili kuwafaa
wanafunzi wenye mahitaji ya kusikia.
Maelezo ya jumla
Mada ya saru humwezesha mwanafunzi kuimarisha matumizi ya aina mbalimbali za
maneno ili kuboresha mawasiliano yake.
Kipindi cha 1: Ngeli ya U-I
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 82)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino zinazopatikana katika ngeli ya U-I.
b) Kutambua nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
Swali dadisi
Je, ni vifaa gani unavyoweza kupata nyumbani vinavyopatikana katika ngeli ya U-I?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo kuhusu nomino za ngeli ya U-I kabla ya kipindi ili kufahamu
zaidi kuhusu shughuli za ujifunzaji atakazowahusisha wanafunzi. Mwalimu awaeleze
wanafunzi kuwa majina ya mimea, miti, baadhi ya sehemu za mwili na rasilimali kama
vile milima, mito na misitu ni mifano ya nomino za ngeli ya U-I.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Vifaa halisi katika ngeli ya U-I,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 82.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa shughuli ya kwanza kwa kuwauliza wanafunzi katika
vikundi wajadiliane kuhusu maswali waliyopewa katika kitabu chao.
Majibu tarajiwa: 1. mpira 2. mkate 3. mti 4. mkoba/mfuko 5. mkono/mguu/mdomo.
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi katika shughuli hii kulingana na maswali
waliyoulizwa.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaulize wanafunzi wataje majina ya vitu
wanavyoona katika michoro waliyopewa kitabuni mwao. Wanafunzi watazame
michoro hiyo na waijadili.
121
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu: mto/mito, mti/miti.
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa majina waliyotaja katika shughuli ya kwanza na
ya pili ni ya ngeli ya U-I.
Mwalimu awaagize wanafunzi wakiwa wawili wawili katika shughuli ya tatu wasome
na kutamka maneno yaliyoorodheshwa kitabuni mwao katika umoja na wingi.
Mwanafunzi mmoja asome maneno hayo katika umoja na mwingine asome maneno
hayo katika wingi. Wanafunzi wajadiliane kuhusu maana za maneno waliyosoma.
Wanaweza kutumia kamusi au mtandao.
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
nomino za ngeli ya U-I za majina ya vitu vinavyopatikana nyumbani kwao katika
umoja na wingi. Mwalimu atathmini kazi ya mwanafunzi. Akubali nomino zozote
zinazotaja vitu vya nyumbani na ziwe za ngeli ya U-I.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutaja nomino za ngeli ya U-I
na kuzitambua zinazotumiwa kutajia majina ya vitu vinavyopatikana katika
mazingira yake.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa wanafunzi wa kutambua nomino za ngeli ya U-I
kutoka katika kundi la maneno.
Kipindi cha 2: Ngeli ya U-I
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 83)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia nomino za ngeli ya U-I kwa njia sahihi katika mawasiliano.
b) Kuonea fahari matumizi ya nomino na viambishi vya ngeli ya U-I katika
mawasiliano.
Swali dadisi
Je, ni nomino gani unazozijua za ngeli ya U-I?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua nomino huweza kuimarisha mawasiliano yake kwa
kuzitumia katika mawasiliano. Mwalimu ahakikishe kuwa kila shughuli inafanywa
ipasavyo kwa kuzuru kila kikundi darasani wakati wa kila shughuli za vikundi na
kuvielekeza.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Vifaa halisi vyenye majina ya ngeli ya U-I,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 83.
122
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wataje nomino za ngeli ya
U-I walizojifunza. Wazitaje katika umoja na wingi. Mwalimu akubali majibu yoyote
sahihi yanayorejelea ngeli ya U-I.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi wasome kifungu kilicho
kitabuni mwao. Kila mwanafunzi asome kifungu hicho kimya kimya. Mwalimu
anaweza kuwauliza wanafunzi maswali ili kubaini uelewa wao kwa kurejelea kifungu
husika. Mwanafunzi atambue nomino za ngeli ya U-I kutoka kwa kifungu alichosoma.
Aandike nomino hizo katika umoja na wingi.
Majibu tarajiwa: miche, miembe, mikebe, mkoba, mgongo, mikate, michungwa, mikono,
miguu, mpira. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi kwa kurejelea kifungu
walichosoma.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi wawili wawili wataje nomino
za ngeli ya U-I zinazohusu sehemu mbalimbali za mwili. Wanafunzi wanaweza
kuonyeshana sehemu hizo za mwili. Mwalimu ahakikishe wanafunzi wanaonyeshana
sehemu za mwili zinazoonekana pekee.
Majibu tarajiwa: mkono, mguu, mdomo, mgongo, muundi n.k.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya tatu. Watambue nomino za ngeli
ya U-I kutoka kwa kundi la maneno waliyopewa kitabuni mwao. Kila mwanafunzi
aweze kutambua nomino za ngeli ya U-I kutoka kwa kundi hilo.
Majibu tarajiwa: mguu, mkuki, mkeka, mwiko, mwavuli, mraba, mfereji mdomo,
muhogo. Kila mwanafunzi aandike nomino alizotambua katika wingi.
Mwalimu amhimize kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada. Kwa usaidizi wa mlezi
au mzazi, mwanafunzi azuru shamba lolote kisha aandike majina ya mimea katika
shamba hilo katika umoja na wingi. Mwanafunzi aandike matunda au mazao ya
mimea aliyotaja. Mfano: mgomba - ndizi. Mwanafunzi awe mwangalifu anapotembea
shambani huko ili asiiharibu mimea.
Pia, mwalimu anaweza kuwapeleka wanafunzi katika shamba la shule au kwenye
shamba lililo karibu na shule ili waandike majina ya mimea katika shamba hilo.
Mwalimu ahakikishe mimea imetunzwa.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutaja nomino za ngeli ya U-I.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anafahamu uhusiano wa viambishi vya
nomino za ngeli ya U-I hasa katika sentensi.
123
Kimeidhinishwa na KICD
Umoja na wingi wa sentensi
Kipindi cha 1: Ngeli ya U-I
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 85)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya U-I katika
umoja na wingi.
b) Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi
akizingatia upatanisho wa kisaru.
Swali dadisi
Ni nomino gani za ngeli ya U-I umewahi kutumia katika mawasiliano yako?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na rasilimali zilizo shuleni.
Mwanafunzi anapotambua viambishi vya ngeli ya U-I na upatanisho wake wa kisaru
huimarisha mawasiliano yake. Mwalimu asisitize upatanisho wa kisaru anapotathmini
sentensi zinazotungwa na wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 85, 2. Breli, 3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwateua wanafunzi watano ambao watasoma maneno
waliyopewa kitabuni mwao katika umoja na wingi katika shughuli ya kwanza. Wanafunzi
hao wasome maneno hayo kwa sauti na kwa zamu huku wenzao wakiwasikiliza kwa
makini. Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji
yao. Wanafunzi watunge sentensi katika vikundi vyao. Mmoja wao awasomee
wanafunzi wengine darasani sentensi walizotunga ili wazitathmini. Wanafunzi wajadili
walichogundua kuhusu sentensi hizo. Mwalimu awaelekeze kufahamu viambishi vya
ngeli ya U-I ambavyo ni u- katika umoja na i- katika wingi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awapange wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi yao na idadi ya tarakilishi zilizopo. Wanafunzi watumie sentensi walizotunga
katika shughuli ya kwanza kutunga kifungu cha aya mbili. Mmoja wao aandike kifungu
hicho kwenye tarakilishi. Ahifadhi kifungu chao kwenye faili kwa jina la mmoja wao
kisha wawatumie wenzao darasani kwa kutumia mtandao ili wakisome na kukiboresha
kifungu walichotunga. Wanafunzi wa vikundi vingine wafanye vivi hivi ili vifungu
vyao visomwe na kuboreshwa na wenzao pamoja na mwalimu.
124
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu amhimize kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada. Mwanafunzi kwa
kumshirikisha mlezi, mzazi wake au hata kwa kutumia mtandao aandike majina
ya milima minne ipatikanayo nchini Kenya kama vile Mlima Elgon, Mlima Kenya.
(Mwalimu akubali majina ya milima katika magatuzi mbalimbali). Mwanafunzi
aandike majina ya mito miwili iliyo katika kaunti yake pamoja na majina ya misitu
miwili iliyo nchini Kenya. Baada ya kuandika majina hayo, mwanafunzi atunge sentensi
sahihi akitumia majina hayo. Awasomee wenzake darasani sentensi atakazotunga
katika kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua viambishi vya ngeli
ya U-I katika sentensi.
2. Mwalimu asahihishe upatanisho wa kisaru katika sentensi zilizoandikwa na
mwanafunzi.
Kipindi cha 2: Ngeli ya U-I
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 86)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuunda sentensi akitumia nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi.
b) Kufurahia matumizi ya nomino za ngeli ya U-I katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, unaweza kutunga sentensi zenye nomino za ngeli ya U-I katika umoja na wingi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu ahakikishe ana nyenzo na shughuli kamilifu atakazotumia kuwashirikisha
wanafunzi darasani. Mwalimu azihifadhi kazi za wanafunzi vyema katika faili, vikapu,
kabati au kutundika kwenye kuta ili ziwe ithibati ya utekelezaji wa shughuli za usomaji.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 86, 2. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaulize wanafunzi wasimame ili washiriki
katika mchezo wa kutaja nomino mbalimbali za ngeli ya U-I pamoja na nomino
nyingine zisizo za ngeli ya U-I. Mwalimu akitaja nomino za ngeli ya U-I wanafunzi
wasimame, akitaja nomino ambayo si ya U-I waketi. Mwanafunzi atakayekosa kusimama
nomino za ngeli ya U-I zinapotajwa au atakayeketi nomino ambayo si ya ngeli hii
inapotajwa asimame mbele ya darasa. Wanafunzi watakaosimama mbele ya darasa
waelekezwe zaidi ili kuwa sahihi.
125
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awaulize wanafunzi watunge sentensi kumi sahihi katika shughuli
ya pili wakitumia nomino mbalimbali za ngeli ya U-I. Wanafunzi waziandike
sentensi hizo kwenye madaari yao. Wabadilishane madaari yao ili wazisahihishe
sentensi walizotunga.
Mwalimu katika shughuli ya tatu awaelekeze wanafunzi wawili wawili watunge
kifungu kifupi kuhusu Ukulima kwa kutumia nomino za ngeli ya U-I. Wanafunzi
watunge kifungu hicho na wakiandike kwenye madaari yao. Wapigie mistari nomino
za ngeli ya U-I katika kifungu hicho. Mwalimu akubali vifungu vitakavyoelezea
ukulima na viwe vimetumia majina ya mimea na sehemu za mwili zinazoshirikishwa
katika shughuli za ukulima. Pia, mwalimu ahakikishe kuwa vifungu hivyo vimezingatia
upatanisho wa kisaru wa ngeli ya U-I.
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi amshirikishe
mlezi au mzazi wake kueleza vyakula vilivyotajwa katika kitabu chao hutokana na
mimea gani.
Majibu tarajiwa: 1. wali - mpunga 2. ugali - mhindi 3. ndizi - mgomba
4. embe - mwembe 5. nazi - mnazi 6. chapati - ngano.
Tathmini
1. Mwalimu asikilize na kusahihisha mifano ya sentensi zitakazotungwa na
mwanafunzi.
2. Mwalimu atazame kila kikundi kikishiriki katika mchezo wa kusimama au
kukaa na kubaini kama vikundi hivyo vinatambua nomino za ngeli ya U-I
katika kifungu husika. Mwalimu awakosoe wanafunzi ambao watakosea.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu atathmini maana ya methali Samaki mkunje angali mbichi. Methali hii
inamaanisha kuwa ni heri kuzirekebisha tabia za mtoto angali mchanga badala ya
kusubiri awe mtu mzima ambaye huenda hataweza kurekebishika.
2. Mwanafunzi atafute shairi lolote zuri kutoka mtandaoni, kwenye kitabu chochote au
gazeti. Alinakili shairi hilo katika daari lake. Kisha awasomee wanafunzi wenzake
shairi hilo darasani. Mwalimu ahakikishe kuwa mwanafunzi ameandika shairi zuri
na kulikariri kwa usahihi. Mwanafunzi awaeleze wanafunzi wenzake ujumbe wa
shairi alilokariri.
3. Mwalimu atathmini insha ambayo mwanafunzi atatunga na kuandika. Sharti insha
hiyo ihusu athari za malezi mabaya. Mwalimu ahakikishe insha hiyo inazingatia
muundo wa insha ya maelezo. Pia, mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaandaa
vidokezo atakavyotumia, kwa mfano: Malezi mabaya ni nini? Nini husababisha
malezi mabaya? Mtu anaweza kufanya nini ili kuwa na malezi mazuri? n.k.
126
Kimeidhinishwa na KICD
4. Mwanafunzi ataje majina ya vitu vyovyote ambavyo amewahi kuvitumia ambavyo
majina yao ni ya ngeli ya U-I. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaandika majina
hayo katika umoja na wingi kwa usahihi. Sharti majina hayo yawe ya ngeli ya U-I.
Mifano: mpira mipira, mkeka mikeka, mto mito (ya kulalia), mkebe –mikebe
n.k.
5. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi amesoma kifungu chochote kinachohusu
‘Ukulima. Anaweza kumwuliza mwanafunzi kuhusu ujumbe wa kifungu hicho.
Pia, ahakikishe mwanafunzi ameandika muhtasari wa kifungu hicho na kupigia
mistari nomino za ngeli ua U-I.
6. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anatunga sentensi sahihi akitumia nomino za
ngeli ya U-I katika umoja pekee. Kwa mfano: Mpunga huu umekauka.
7. Mwalimu atathmini sentensi za wingi ambazo mwanafunzi ataandika. Sharti
sentensi hizo ziwe sahihi kisaru na zionyeshe wingi wa sentensi alizotunga katika
swali la 6. Kwa mfano: Mipunga hii imekauka.
8. Mwanafunzi atumie tarakilishi kuandika sentensi alizotunga katika umoja na wingi
(katika maswali ya 6 na 7). Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi amefahamu
kutumia tarakilishi pamoja na mtandao (kwa kuzituma sentensi hizo).
9. Mwanafunzi ahifadhi sentensi alizoandika katika faili kwa kutumia jina lake. Atumie
mtandao kutuma sentensi hizo. Mwalimu atathmini sentensi atakazotumiwa na
mwanafunzi. Pia, atathmini iwapo mwanafunzi ameelewa kutumia tarakilishi.
10. Mwalimu atathmini majina ya ngeli ya U-I ya sehemu za mwili ambayo mwanafunzi
ataandika katika umoja na wingi. Mifano: mguu miguu, mkono mikono,
mgongo migongo n.k.
127
Kimeidhinishwa na KICD
BENDERA YA TAIFA
6
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 88)
A. Kusikiliza na Kuzungumza
Kuzungumza na kujieleza kwa ufasaha
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kukariri na kuimba mashairi kwa matamshi na mahadhi mbalimbali.
b) Kueleza maana ya msamiati uliotumika katika shairi.
ch) Kutumia msamiati uliotumika katika shairi ili kuboresha mawasiliano.
d) Kueleza ujumbe wa shairi ili kudhihirisha ufahamu wake.
Swali dadisi
Ni kwa namna gani ushairi unaweza kuboresha mawasiliano yako?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanaposikiliza shairi lililorekodiwa
likikaririwa kupitia vifaa vya kidijitali.
Kujiamini na kujithamini - kunakuzwa mwanafunzi anapojenga umilisi huu
anapokariri shairi.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapotafakari swali dadisi na
kutunga mashairi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha kutokana na kukariri mashairi kwa mahadhi mbalimbali.
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima - mwanafunzi anapokariri na kujadiliana na wenzake katika
vikundi.
Uwajibikaji - majukumu katika vikundi na kufuata mafunzo katika shairi.
128
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza, Lugha za kiasili kama vile Kiarabu - masomo haya yana mada
kuhusu ushairi.
Muziki - somo hili hushughulikia nyimbo za mahadhi mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
mashairi katika kuboresha mazungumzo.
Mwanafunzi atawakariria watu mashairi katika haa mbalimbali.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kukariri au
kuimba shairi
kwa mahadhi
mbalimbali
kwa ufasaha.
Mwanafunzi
anakariri au
kuimba shairi
kwa mahadhi
mbalimbali
kwa ufasaha na
urahisi.
Mwanafunzi
anakariri au
kuimba shairi
kwa mahadhi
mbalimbali kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anakariri au
kuimba sehemu
za shairi kwa
kuzingatia baadhi
ya mahadhi.
Mwanafunzi
anajaribu
kukariri au
kuimba sehemu
za shairi.
Kueleza na
kutumia
msamiati
lengwa katika
tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza
msamiati
uliotumiwa
kwenye shairi
na kuutumia
katika tungo
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza
msamiati
uliotumiwa
kwenye shairi
na kuutumia
katika tungo
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza baadhi
ya msamiati
uliotumiwa kwenye
shairi na kuutumia
katika tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza baadhi
ya msamiati
uliotumiwa
kwenye shairi.
Kueleza
ujumbe,
matukio na
wahusika
katika shairi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza
ujumbe,
matukio na
wahusika
katika shairi
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
shairi kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatoa baadhi ya
maelezo kuhusu
ujumbe, matukio
na wahusika katika
shairi kwa usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutoa maelezo
kuhusu
ujumbe,
matukio na
wahusika
katika shairi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wenye uwezo wa kung’amua wanayojifunza mara moja baada ya
kushirikishwa katika shughuli za ujifunzaji wapewe fursa ya kuimba au kukariri
129
Kimeidhinishwa na KICD
mashairi zaidi. Kwa upande mwingine, wanafunzi wanaochukua muda zaidi kabla
ya kufahamu wanayojifunza washirikishwe katika shughuli zaidi na kupewa muda
zaidi wa kujifunza.
Baadhi ya wanafunzi walio na mahitaji ya kisaikolojia kutokana na matukio
wanayokumbana nayo katika jamii, wasaidiwe kujihusisha katika ujifunzaji.
Mwalimu anaweza kumhusisha mzazi au mlezi katika kutatua changamoto hiyo.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli au kusikiliza shairi likikaririwa
au kuimbwa na mwalimu, wanafunzi wenzao au kutoka kwenye kanda iliyorekodiwa.
Maelezo ya jumla
Mada ya kusikiliza na kuzungumza kuhusu mashairi itamwezesha mwanafunzi
kutambua msamiati unaotokana na shairi. Inachangia katika kuboresha matamshi ya
mwanafunzi katika mawasiliano.
Pia, itaboresha usahihi wa maneno katika stadi ya kuandika ambayo mwanafunzi
atashiriki baada ya kujua kukariri na kuimba mashairi kwa mahadhi mbalimbali.
Kipindi cha 1: Ushairi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 88)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kukariri na kuimba mashairi kwa matamshi na mahadhi mbalimbali.
b) Kueleza maana ya msamiati uliotumika katika shairi.
ch) Kutumia msamiati uliotumika katika shairi ili kuboresha mawasiliano.
Swali dadisi
Je, unajua namna shairi linaweza kuboresha mawasiliano?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Bendera ni kitambaa maalumu na cha kipekee kinachotumiwa na nchi kujitambulisha.
Ili kufanikisha shughuli za serikali na pia kuonyesha uzalendo katika nchi, lazima
bendera ya nchi hiyo ipeperushwe.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 88, 2. Rekoda, 3. Breli,
4. Mgeni mwalikwa, 5. Kanda iliyorekodiwa, 6. Rununu.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa kuwaelekeza wanafunzi kufanya shughuli ya
kwanza. Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji
yao. Wanafunzi watazame na kujadili mchoro ulio kitabuni mwao. Wajibu maswali
130
Kimeidhinishwa na KICD
yanayohusu mchoro huo katika vikundi. Mwalimu atathmini majibu yao.
Katika shughuli ya pili, wanafunzi wakariri shairi kwa pamoja wakizingatia msamiati
unaorejelea bendera ya taifa. Baada ya kukariri shairi, wanafunzi wajibu maswali
kulingana na shairi walilokariri. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Ili kushughulikia shughuli ya tatu, mwalimu ahakikishe kuwa wanafunzi katika vikundi
wameimba shairi lililo katika shughuli ya pili. Waimbe kwa mahadhi mbalimbali na
kwa zamu. Wanafunzi wa vikundi vingine wawasikilize wenzao wakiimba shairi hilo.
Mwalimu amhimize mwanafunzi kufanya kazi ya zaida. Mwanafunzi amwulize mlezi
au mzazi wake sababu za kusimama wima gwarideni, kitu kilicho katikati ya bendera
na sababu za kupandisha bendera shuleni kila wiki. Mwanafunzi awaeleze wenzake
darasani majibu ya maswali haya ili wayatathmini na kujifunza.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kukariri na kuimba mashairi
kwa mahadhi mbalimbali.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kueleza maana ya msamiati
uliotumika katika shairi.
Kipindi cha 2: Ushairi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 90)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia msamiati uliotumika katika shairi ili kuboresha mawasiliano.
b) Kueleza ujumbe wa shairi ili kudhihirisha ufahamu wake.
ch) Kuchangamkia ushairi kama njia ya kujieleza kwa ufasaha.
Swali dadisi
Ni shairi lipi lililokufurahisha na lilikaririwa ulivyokariri?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua, kutamka na kuunda sentensi zenye msamiati wa kishairi
ataboresha matamshi yake katika mawasiliano.
Mwalimu anaweza kubuni shughuli za ujifunzaji zilizo tofauti na zile za kipindi cha
awali ili kukuza hamu ya ujifunzaji zaidi kwa wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 90, 2. Rekoda, 3. Breli,
4. Mgeni mwalikwa, 5. Rununu.
131
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza kwa kuwauliza
wanafunzi wasome shairi lililo kitabuni mwao kimya kimya. Wakimaliza, wamsikilize
mgeni mwalikwa akikariri shairi walilosoma. Baada ya kumsikiliza mgeni mwalikwa,
wajibu maswali waliyopewa kitabuni mwao wakiwa katika vikundi. Mwalimu
ahakikishe amewagawa wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Majibu tarajiwa: a) Shairi linahusu umuhimu wa bendera. b) Wimbo wa taifa hutoa
ushauri nasaha kwa wananchi. ch) Mwalimu atumie kamusi. d) Mwanafunzi mmoja
atumie rekoda au rununu kurekodi mgeni mwalikwa akikariri shairi husika kisha
wenzake wasikilize rekodi hiyo na kukariri kwa sauti.
Katika shughuli ya pili, wanafunzi wawili wawili washirikiane kuandika beti tatu za
wimbo wa taifa la Kenya. Wajadili ujumbe katika beti hizo. Mwanafunzi mmoja aimbe
wimbo huo huku mwenzake akimsikiliza na kumsahihisha panapofaa.
Mwalimu amhimize mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi amwombe mlezi
au mzazi wake amrekodi akiimba beti tatu za wimbo wa taifa. Mlezi au mzazi anaweza
kutumia tarakilishi, rekoda au rununu.
Tathmini
1. Mwalimu amsikilize mwanafunzi akikariri shairi alilopewa kitabuni mwao ili
kumtathmini.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua msamiati wa
bendera kutoka kwa maneno yaliyotumiwa katika shairi.
3. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutambua ujumbe katika
shairi.
B. Kusoma kwa kina
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 91)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kusoma makala kwa kuzingatia vipengele mbalimbali vinavyoijenga.
b) Kusoma na kutambua umuhimu wa ujumbe wa makala husika.
ch) Kufurahia kusoma makala mbalimbali ili kukuza ufahamu.
Maswali dadisi
1. Kusoma hadithi kuna umuhimu gani?
2. Ni ujumbe upi ulipata katika makala uliyowahi kusoma?
132
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - huu unakuzwa wanafunzi wanaposoma makala kwenye
blogi.
Kujiamini na kujithamini - umilisi huu unakuzwa mwanafunzi anaposimulia
alichokisoma.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha mwanafunzi ataweza kuongoza na kuelekeza usomaji wake.
Uhusiano na maadili
Maadili mbalimbali hukuzwa kutegemea makala yaliyoteuliwa kama vile
heshima, upendo uzalendo n.k.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Masomo ya jamii masomo haya yanafundisha uraia mwema
na uzalendo.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atatumia mawazo na maadili aliyopata kutokana na hadithi kuwaelekeza
wenzake.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kusoma kwa
kuzingatia
ujumbe, vipengele
vya makala
na kueleza
alichokisoma.
Mwanafunzi
anasoma
akizingatia
ujumbe,
vipengele
vya makala
na kueleza
alichokisoma
kwa urahisi.
Mwanafunzi
anasoma
akizingatia
ujumbe,
vipengele
vya makala
na kueleza
alichokisoma.
Mwanafunzi
anasoma akizingatia
sehemu
za ujumbe,
anafahamu sehemu
za vipengele vya
makala
na kueleza baadhi ya
aliyoyasoma.
Mwanafunzi
anasoma
sehemu za
makala.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema au kusikia watambue makala lengwa kwa
kuandika.
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona watumie breli au kusikiliza makala
husika ikisomwa na kuelezewa na mwalimu au wanafunzi wenzao.
133
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya jumla
Mada ya kusoma kwa kina itamwezesha mwanafunzi kutambua ujumbe wa makala
mbalimbali husika na kuweza kuboresha mawasiliano yake.
Kusoma makala kutakuza hamu ya mwanafunzi ya kujifunza zaidi ili kuyafahamu
maudhui mbalimbali katika makala.
Mwalimu ahimize kusoma kwa kina ndani na nje ya darasa ili kukuza stadi ya usomaji
ambayo humpa mwanafunzi maarifa zaidi.
Kipindi cha 1: Makala
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 91)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusoma makala kwa kuzingatia vipengele mbalimbali vinavyoijenga.
b) Kusoma na kutambua umuhimu wa ujumbe wa makala husika.
Swali dadisi
Kusoma hadithi kuna umuhimu gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua msamiati wa makala na kuutumia kwa usahihi katika
sentensi huboresha mawasiliano yake.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 91, 3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza kwa kuwauliza wanafunzi
watazame mchoro ulio kitabuni mwao. Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na mahitaji yao kisha wajibu maswali waliyopewa kitabuni mwao.
Majibu tarajiwa:
1. Gwaride, wanafunzi, walimu, mlingoti, bendera n.k.
2. Gwarideni, shuleni n.k.
3. Wanapandisha bendera, wanaimba wimbo wa taifa, wamesimama wima n.k.
4. Ili kuonyesha uzalendo wao.
5. Wimbo wa taifa.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kusoma hadithi iliyo kitabuni
mwao. Kwanza, kila mwanafunzi aisome hadithi hiyo akiwa pekee kimya kimya
134
Kimeidhinishwa na KICD
kisha wanafunzi wasome wakiwa katika vikundi. Baada ya kusoma, wajibu maswali
waliyopewa kitabuni mwao. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi kubaini uelewa
wao wa kifungu walichosoma. Pia, mwalimu awaelekeze wanafunzi kujibu maswali
mengine waliyopewa wakirejelea shule yao. Wanafunzi ambao watakuwa na matatizo,
waelekezwe na mwalimu.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Kila mwanafunzi atafute
mtandaoni bendera ya Kenya, Uganda na Tanzania. Achore bendera hizo katika daari
lake kisha azipake rangi zao sahihi. Baada ya hapo, aeleze tofauti kati ya bendera hizo
kwa kuandika katika daari lake. Mwanafunzi awaeleze wenzake darasani tofauti hizo.
Mwalimu atathmini kazi ya mwanafunzi na kuwaelekeza wanafunzi wanaotatizika.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kueleza maana ya msamiati
wa bendera na gwaride.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuchora bendera ya taifa la
Kenya na kuipaka rangi zake nne.
3. Mwalimu atathmini ikiwa mwanafunzi anaweza kuibaini bendera ya Kenya
kutoka kwa bendera za nchi nyingine.
Kipindi cha 2: Makala
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 93)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusoma makala kwa kuzingatia vipengele mbalimbali vinavyoijenga.
b) Kusoma na kutambua umuhimu wa ujumbe wa makala husika.
Maswali dadisi
1. Kusoma hadithi kuna umuhimu gani?
2. Ni ujumbe upi ulipata kwenye makala uliyowahi kusoma?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu ahakikishe kuwa amewagawa wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi
na mahitaji yao. Wanafunzi walio na mahitaji mbalimbali wawe viongozi wa vikundi
ili waweze kujiamini na kujithamini.
Kipindi hiki kinahusu kusoma makala mbalimbali ili kukuza usomaji wa mwanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 93, 3. Gazeti.
135
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa kuwaelekeza wanafunzi wasome mazungumzo
yaliyo katika shughuli ya kwanza kitabuni mwao. Wanafunzi wakiwa wawili wawili
wasome mazungumzo hayo wakizingatia matamshi bora na sahihi. Baada ya kusoma,
wajibu maswali yanayotokana na mazungumzo hayo kwa kujadiliana. Mwalimu
atathmini majibu ya wanafunzi. Wanafunzi wanaweza kutumia kamusi au mtandao
kueleza maana ya maneno yaliyokolezwa rangi katika mazungumzo waliyosoma.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi waigize mbele ya darasa
mazungumzo yaliyo kitabuni mwao katika shughuli ya kwanza kati ya Rukia na Paulo.
Mwanafunzi mmoja achukue nafasi ya Paulo na mwingine achukue nafasi ya Rukia.
Baada ya maigizo hayo, wanafunzi wajadiliane kuhusu mambo waliyojifunza kutokana
na maigizo hayo, kama vile: kuwa jasiri unapozungumza mbele ya watu, kutamka
maneno kwa usahihi n.k.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi asome makala
kuhusu sherehe yoyote ya kitaifa kutoka kwenye gazeti la Kiswahili. Baada ya kusoma,
aandike muhtasari wa makala hiyo katika daari lake. Awasomee wanafunzi wenzake
muhtasari huo darasani ili wautathmini.
CH. Kuandika: Kuandika insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 95)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya wasifu kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya wasifu kwa kufuata kanuni zifaazo akizingatia vivumishi na
vielezi kujenga picha dhahiri ya anachokieleza.
ch) Kuchangamkia utunzi mzuri wa kuandika insha ya wasifu ili kukuza ubunifu.
Swali dadisi
Insha ya wasifu inahusu nini?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
kuandika insha mtandaoni na kurejelea vielelezo vya insha za wasifu.
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya wasifu.
Hamu ya ujifunzaji inakuzwa mwanafunzi anapotafakari swali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
136
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia unakuzwa kutokana na kufanya kazi pamoja.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika vikundi.
Insha ya wasifu yaweza kulenga watu ambao wanajulikana kwa uaminifu,
uwajibikaji, upendo na uzalendo.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia stadi ya
kuandika.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi bora katika mawasiliano.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuandika insha
ya wasifu kwa
kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya wasifu
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio
mzuri wa
mawazo na kwa
ubunifu wa hali
ya juu.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya wasifu
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya wasifu
kwa kuzingatia
baadhi ya
kanuni za lugha.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika insha
ya wasifu.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli kusoma maelezo kuhusu
insha ya wasifu pamoja na mambo ya kuzingatia wanapoiandika. Pia, wanafunzi
wenzao wanaweza kuwasaidia kusoma maelezo hayo huku wakisikiliza.
Wanafunzi wenye mahitaji ya kisaikolojia yanayochangia kutozingatia kanuni
bora za uandishi, wapewe mazoezi ya kutosha kabla ya kuandika insha. Wanaweza
kupanga sentensi zilizotarakanywa katika aya ili kuboresha mtiririko wa mawazo.
Pia, changamoto wanazopitia zinaweza kuangaziwa na wakuu shuleni na jamii.
Wasioweza kuandika heru za Kiswahili vizuri wahusishwe katika mazoezi ya
kunyanga heru hizo, kuzipaka rangi zikiwa kwenye chati na kuzifuma kwa
kutumia uzi. Wale wenye changamoto ya kutumia mkono kuandika wapewe muda
zaidi wa kuandika insha.
137
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya jumla
Mada ya kuandika itamwezesha mwanafunzi kukuza ubunifu wake, kufahamu kanuni
za uandishi bora ili kuimarisha mawasiliano yake.
Kipindi cha 1: Insha ya wasifu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 95)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya wasifu kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya wasifu kwa kufuata kanuni zifaazo akizingatia vivumishi na
vielezi ili kujenga picha dhahiri ya anachokielezea.
ch) Kuchangamkia utunzi mzuri wa kuandika insha ya wasifu ili kukuza ubunifu.
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapochangamkia utunzi wa insha ya wasifu hujenga ubunifu wake na
kuweza kuandika insha za kusisimua.
Mwalimu amhusishe kila mwanafunzi katika shughuli mbalimbali zitakazomwezesha
kuwa mwandishi bora. Ampongeze kila mwanafunzi kwa kila hatua anayopiga katika
uandishi ili aendelee kujithamini. Mwanafunzi awe na vifaa vyote anavyohitaji katika
kujifunza kuandika insha.
Mwalimu ahakikishe ana nyenzo zote za ujifundishaji kabla ya kipindi. Vifaa vya
kiteknolojia vikaguliwe kabla ya kipindi ili kuhakikisha vitatumiwa bila changamoto.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 95, 2. Breli, 3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa kuwaelekeza wanafunzi katika shughuli ya
kwanza. Awaulize wanafunzi watatu wasimame mbele ya darasa. Kila mwanafunzi
awaeleze wanafunzi wengine kuhusu sifa za raki yake akizingatia vidokezo alivyopewa
kitabuni mwao. Wanafunzi hao watatu waeleze sifa za maraki wao huku wengine
wakiwasikiliza kwa makini. Mwalimu atathmini maelezo ya kila mwanafunzi. Shughuli
hii itawasaidia wanafunzi kuelewa kuhusu sifa za watu mbalimbali. Pia, itakuza ujasiri
wa wanafunzi kuzungumza mbele ya wenzao.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya shughuli ya pili. Wanafunzi wawili wawili
wasome kifungu walichopewa kitabuni mwao. Washirikiane katika usomaji wao na
kukosoana panapowezekana. Mwalimu awasaidie wanafunzi wanaotatizika katika
usomaji wao. Wanafunzi wajibu maswali waliyopewa. Wataje sifa za Zawadi kutokana
na kifungu walichosoma. Pia, kila mwanafunzi aandike kifungu cha aya mbili kwa
kutumia sifa za Zawadi walizotaja. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua
138
Kimeidhinishwa na KICD
muundo wa kuandika insha ya wasifu: kuwepo kwa mada, mtiririko wa mawazo, saru
na tahajia sahihi izingatiwe pamoja na hati inayosomeka kwa urahisi.
Katika kazi ya ziada, kila mwanafunzi aandike insha ya wasifu kujihusu kwa kutumia
vidokezo vilivyo kitabuni mwao. Baada ya kuandika insha hiyo, awasomee wanafunzi
wenzake pamoja na mwalimu insha aliyoandika ili waitathmini na kuiboresha katika
kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kueleza maana ya wasifu.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua insha ya wasifu kwa
kuzingatia muundo.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika aya ya insha ya
wasifu kwa kuzingatia ujumbe, sentensi sahihi na sanifu.
Kipindi cha 2: Insha ya wasifu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 97)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika insha ya wasifu kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
b) Kuchangamkia utunzi mzuri wa insha ya wasifu ili kujenga ubunifu wake.
Maswali dadisi
1. Insha ya wasifu inahusu nini?
2. Je, unazingatia mambo yapi unapoandika insha ya wasifu?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo katika kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi ili
kujifahamisha yaliyomo. Mwalimu arekodi maelezo kuhusu uandishi wa insha ya
wasifu ili kuwafaa wanafunzi wasioweza kuona maandishi ubaoni.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 97, 2. Breli, 3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wajikumbushe
kuhusu mambo wanayofaa kuzingatia wanapoandika insha ya wasifu.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi kutazama na kuujadili
mchoro ulio kitabuni mwao. Baada ya kuujadili, wajibu maswali waliyopewa.
139
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi. Majibu tarajiwa: Mchoro huo ni wa mbuzi/
mwanambuzi. Mnyama hayo ana rangi ya hudhurungi na nyeupe. Wanyama wengine
wanaoishi na mbuzi ni kama vile ngombe, kondoo, paka, mbwa n.k.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kusoma kielelezo cha insha
ya wasifu walichopewa kitabuni mwao. Mwanafunzi mmoja asome insha hiyo huku
wanafunzi wengine wakisikiliza matamshi yake kwa makini kisha wajibu maswali
waliyopewa kitabuni mwao. Pia, wanafunzi wajadili muundo wa insha hiyo. Mwalimu
atathmini majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amwelekeze mwanafunzi kuandika insha ya wasifu
kuhusu mwalimu anayempenda kwenye tarakilishi. Shughuli hii itafanyika kulingana
na idadi ya tarakilishi zilizopo. Mwalimu awaelekeze wanafunzi ipasavyo. Mwanafunzi
aandike insha hiyo akizingatia vidokezo alivyopewa kitabuni mwake. Baada ya
kuandika, ahifadhi insha hiyo katika faili kwa kutumia jina la mwalimu huyo.
Awatumie wanafunzi wenzake insha hiyo mtandaoni ili waitathmini na kuiboresha.
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Kila mwanafunzi
aandike insha ya wasifu kumhusu mlezi au mzazi wake. Atumie vidokezo alivyopewa
katika kitabu chake.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika insha ya wasifu kwa
kuzingatia muundo na mtindo, sentensi sahihi na sanifu, mtiririko wa mawazo
na ubunifu.
2. Atathmini uchangamkiaji wa utunzi wa insha ya wasifu kwa mwanafunzi
kuuliza maswali au kuteua mada yake mwenyewe na kuandika insha na kumpa
mwalimu aitathmini.
D.Saru:Ngelizanomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 99)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya LI-YA.
b) Kuandika nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
ch) Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-YA.
d) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-YA katika
umoja na wingi.
e) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA, katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
140
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Nomino zinazorejelea matunda ni zipi?
2. Nomino zinazorejelea viungo vya mwili ni zipi?
3. Je, unaweza kuandika umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya LI-YA?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga mafungu ya maneno.
Kukiri kwa kina kunakuzwa mwanafunzi anapowaza kwa kina kuhusu
atakachoandika.
Ujuzi wa kidijitali unakuzwa tarakilishi inapotumiwa kutambua nomino na
ngeli ya LI-YA na katika kusikiliza mafungu kwenye rekoda.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano kufanya kazi katika vikundi.
Stadi za maisha kujifanyia kazi darasani bila kunakili za wengine.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - kutunza vipakatalishi anavyotumia.
Uzalendo kufanya kazi na wengine kwenye vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia
mada ya saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Kutumia lugha sanifu miongoni mwa wenzake shuleni na nyumbani kama kielelezo
cha kuzingatia Kiswahili sanifu.
141
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya LI-YA na
kuzitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya LI-YA na
anazitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
ufasaha na
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya LI-YA na
anazitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa baadhi ya
nomino katika
ngeli ya LI-YA
na kuzitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli ya
LI-YA.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi ambao hawana uwezo wa kuona, watumie breli kusoma maelezo ya
maana ya nomino za ngeli ya LI-YA. Pia, mwalimu anaweza kuleta vitu halisi
darasani ili waviguse na kutambua majina yao.
Mwalimu anaweza kurekodi video yenye mifano ya nomino za ngeli ya LI-YA.
Pia, anaweza kurekodi sentensi zenye nomino hizo ili kuwafaa wanafunzi wenye
mahitaji ya kusikia.
Maelezo ya jumla
Mada ya saru humwezesha mwanafunzi kuimarisha matumizi ya aina mbalimbali za
maneno ili kuboresha mawasiliano yake.
Kipindi cha 1: Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya LI-YA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 99)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutaja mifano ya majina katika ngeli ya LI-YA.
b) Kutambua na kuandika nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Maswali dadisi
1. Je, nomino za ngeli ya LI-YA ni zipi?
2. Je, nomino za ngeli ya LI-YA hubadilika vipi katika umoja na wingi?
142
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo kuhusu umoja na wingi wa nomino katika kitabu cha
mwanafunzi kabla ya kipindi ili kufahamu zaidi kuhusu shughuli za ujifunzaji
atakazowahusisha wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli,
2. Tarakilishi,
3. Vifaa halisi vya nomino za ngeli ya LI-YA,
4. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 99,
5. Kanda iliyorekodiwa inayoeleza kuhusu nomino za ngeli ya LI-YA.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza. Awagawe wanafunzi
katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao. Watazame na kujadili michoro iliyo
kitabuni mwao. Wanafunzi waandike majina ya michoro hiyo. Mwalimu atathmini
majibu ya wanafunzi. Majibu tarajiwa: nanasi, daari, dawati, gari.
Katika shughuli ya pili, mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi kusoma na kujadili
maneno yaliyo katika kitabu chao akiwa na mwanafunzi mwenzake. Wanafunzi
waelezane iwapo wamewahi kuviona vitu vyenye majina waliyosoma. Wanafunzi
waelezane walikoviona vitu hivyo. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amwongoze mwanafunzi kutambua majina ya
ngeli ya LI-YA kutoka kwa orodha ya maneno waliyopewa. Mwanafunzi achague
majina ya ngeli ya LI-YA pekee kutoka kwa orodha hiyo. Mwalimu atathmini majibu
ya mwanafunzi. Majibu tarajiwa: dirisha, duka, dawati, kanisa. Mwanafunzi aandike
majina aliyotambua katika wingi. Majibu tarajiwa: madirisha, maduka, madawati,
makanisa.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi namna ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi
aandike majina matano ya ngeli ya LI-YA ya vitu vinavyopatikana nyumbani kwao.
Mwanafunzi aandike majina hayo katika umoja na wingi. Mwalimu atathmini majibu
ya mwanafunzi kwa kurejelea majina ya vitu vinavyopatikana nyumbani katika ngeli
ya LI-YA.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua nomino za ngeli ya
LI-YA katika michoro.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kuandika majina ya ngeli ya
LI-YA katika umoja na wingi.
143
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2: Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya LI-YA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 100)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutaja mifano ya majina katika ngeli ya LI-YA.
b) Kutambua michoro ya vitu vya ngeli ya LI-YA.
ch) Kutambua na kuandika nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Swali dadisi
Je, unajua nomino gani za ngeli ya LI-YA?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua nomino huweza kuimarisha mawasiliano yake kwa
kuzitumia kutunga sentensi sahihi.
Mwalimu ahakikishe kuwa kila shughuli inafanywa ipasavyo kwa kutembelea kila
kikundi darasani wakati wa kila shughuli na kuwaelekeza wanafunzi. Awe makini
katika ukuzaji wa maadili ya wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli,
2. Vifaa halisi vyenye majina ya ngeli ya LI-YA,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 100,
4. Rekoda.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa shughuli ya kwanza. Wanafunzi wakiwa katika
vikundi wajishughulishe katika kutambua umoja na wingi wa nomino za ngeli ya
LI-YA. Watazame michoro iliyo kitabuni mwao kisha wajaze nafasi zilizo chini ya
kila mchoro. Wafanye hivi kwa kutaja majina ya michoro waliyotazama. Mwalimu
atathmini majibu ya kila kikundi.
Katika shughuli ya pili, wanafunzi wasikilize usomaji wa maneno ya ngeli ya LI-YA
kutoka kwa rekoda ya mwalimu. Wanafunzi wasikilize kwa makini kisha wayaandike
maneno hayo katika wingi. Mwalimu atathmini majibu yao. Mwalimu aandae rekoda,
ya nomino za ngeli ya LI-YA kabla ya kipindi hiki.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amwelekeze mwanafunzi kuchora michoro ya
vitu ambavyo majina yao yameandikwa kitabuni mwake. Mwanafunzi achore jembe,
chungwa na dawati. Anaweza kuipaka rangi michoro yake. Mwanafunzi ajadiliane na
mwanafunzi mwenzake kuhusu umuhimu wa vitu alivyochora kwa binadamu. Majibu
tarajiwa: Jembe hutumiwa kulima, chungwa huliwa na dawati hutumiwa na wanafunzi
kuketi na kuandikia.
144
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
majina ya ngeli ya LI-YA ya vitu vinavyopatikana shuleni kwao. Aandike majina hayo
katika umoja na wingi. Amsomee mlezi au mzazi wake majina hayo ili ayatathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua na kuandika umoja
na wingi wa nomino za ngeli ya LI-YA.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kuchora michoro ya nomino
za ngeli ya LI-YA.
Ngeli za nomino
Kipindi cha 1: Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya LI-YA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-YA katika
umoja na wingi.
b) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA, katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
ch) Kufurahia matumizi ya nomino za ngeli ya LI-YA katika umoja na wingi.
Maswali dadisi
1. Je, unaweza kuandika umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya LI-YA?
2. Ni nomino gani za ngeli ya LI-YA unaweza kutungia sentensi sahihi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo kuhusu upatanisho wa kisaru wa ngeli ya LI-YA katika
kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi ili kufahamu zaidi kuhusu shughuli za
ujifunzaji atakazowahusisha wanafunzi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Vifaa halisi vyenye majina ya ngeli ya LI-YA,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 102.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa maswali dadisi. Awaelekeze wanafunzi katika
shughuli ya kwanza wajigawe katika vikundi vya wanafunzi wawili wawili kisha
145
Kimeidhinishwa na KICD
watazame na kujadili michoro iliyo kitabuni mwao. Wanafunzi wakamilishe sentensi
iliyo kando ya kila mchoro kwa jina sahihi la kila mchoro. Mwalimu atathmini majibu
yao.
Katika shughuli ya pili, mwanafunzi atunge sentensi sahihi akitumia majina ya ngeli
ya LI-YA aliyopewa kitabuni mwake. Wanafunzi wawili wawili wajadiliane kuhusu
ugunduzi wao. Mwalimu atathmini majadiliano yao. Awaeleze wanafunzi kuwa
viambishi ngeli vya ngeli ya LI-YA ni li- katika umoja na ya- katika wingi.
Katika shughuli ya tatu, wanafunzi wapigie mistari viambishi vya ngeli ya LI-YA kwa
zamu kwenye sentensi zilizoandikwa ubaoni. Mwalimu atathmini majibu yao. Pia,
wanafunzi wawatathmini wenzao.
Katika kazi ya ziada, mwanafunzi atunge sentensi tano sahihi akitumia nomino za
ngeli ya LI-YA za vitu vinavyopatikana nyumbani kwao katika umoja. Mwalimu
asahihishe kazi hii. Mwanafunzi awasomee wanafunzi wenzake sentensi alizotunga.
Wanafunzi wazitathmini sentensi za wenzao.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kukamilisha na kutunga
sentensi za ngeli ya LI-YA.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutambua viambishi vya ngeli
ya LI-YA katika sentensi.
Kipindi cha 2: Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya LI-YA
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 103)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-YA katika
umoja na wingi.
b) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA, katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
Swali dadisi
Je, unaweza kutunga sentensi katika umoja na wingi katika ngeli ya LI-YA?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapotambua nomino, huweza kuimarisha mawasiliano yake kwa
kuzitumia kutunga sentensi sahihi.
Mwalimu ahakikishe kila shughuli inafanywa ipasavyo kwa kutembelea kila kikundi
darasani wakati wa kila shughuli na kuwaelekeza wanafunzi. Pia, mwalimu awe
makini katika ukuzaji wa maadili ya wanafunzi.
146
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Tarakilishi, 3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 103.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi swali dadisi. Katika
shughuli ya kwanza, wanafunzi wakiwa wawili wawili watazame na kujadili
michoro iliyo kitabuni mwao. Wanafunzi wakamilishe sentensi zilizo chini ya kila
mchoro. Mwalimu awaulize wanafunzi wajadili ugunduzi wao kwa kurejelea sentensi
walizotunga. Wanafunzi wabaini viambishi vya ngeli ya LI-YA katika sentensi ambavyo
ni li- katika umoja na ya- katika wingi. Majibu tarajiwa: 1. Gari hili lilinunuliwa jana.
- Magari haya yalinunuliwa jana. 2. Shoka hili litauzwa. - Mashoka haya yatauzwa.
Katika shughuli ya pili, mwanafunzi atunge sentensi sahihi katika umoja na wingi
kwa kutumia maneno ya ngeli ya LI-YA yaliyo kitabuni mwake. Mwalimu atathmini
majibu ya mwanafunzi. Shughuli hii itakuza ubunifu wa mwanafunzi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi katika shughuli ya tatu. Mwanafunzi aandike
sentensi alizotunga katika shughuli ya pili katika umoja na wingi kwenye tarakilishi.
Ahifadhi sentensi hizo kwenye faili kwa jina lake. Kwa kutumia mtandao, awatumie
wanafunzi wenzake pamoja na mwalimu ili wazisome na kuziboresha.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi atunge
sentensi zenye majina ya matunda matano katika ngeli ya LI-YA. Aandike sentensi hizo
katika umoja na wingi kisha atumie mtandao kutafuta picha za matunda aliyotungia
sentensi. Aandike rangi za matunda hayo. Awaeleze wenzake darasani katika kipindi
kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutunga sentensi katika
umoja na wingi akitumia nomino za ngeli ya LI-YA.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutumia tarakilishi kuandika
sentensi katika ngeli ya LI-YA na kuwatumia wenzake mtandaoni.
Saru: Ngeli za nomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 105)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya KI-VI.
b) Kutambua viambishi vipatanishi vya ngeli kwenye mafungu ya maneno.
ch) Kutumia nomino za ngeli ya KI-VI katika sentensi.
d) Kuchangamkia kutumia nomino za ngeli ya KI-VI katika mawasiliano.
147
Kimeidhinishwa na KICD
Swali dadisi
Ni nomino gani zilizo katika ngeli ya KI-VI?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi.
Uwazaji wa kina - unakuzwa mwanafunzi anapowaza kwa kina kuhusu
atakachoandika.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa tarakilishi inapotumiwa kutambua maneno na
katika kusikiliza sentensi kwenye rekoda.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano kufanya kazi katika kikundi.
Stadi za maisha kujifanyia kazi darasani bila kunakili za wengine.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji kutunza vipakatalishi.
Uzalendo kufanya kazi na wengine katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia mada ya
saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapojua saru sahihi atakuwa kielelezo kwa wenzake katika kutumia
Kiswahili ifaavyo.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi matarajio Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya KI-VI na
kuzitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua umoja
na wingi wa
nomino katika
ngeli ya KI-VI
na anazitumia
kwenye mafungu
ya maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi na urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
katika ngeli
ya KI-VI na
anazitumia
kwenye
mafungu ya
maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa baadhi ya
nomino za KI-
VI na kutumia
baadhi ya
nomino hizo
kwenye mafungu
ya maneno na
sentensi kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
umoja na
wingi wa
nomino katika
ngeli ya KI-VI.
148
Kimeidhinishwa na KICD
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, wasome maelezo ya umoja na wingi
wa nomino za KI-VI wakitumia breli. Pia, wanaweza kumsikiliza mwalimu au
wanafunzi wenzake wakisoma nomino na sentensi za ngeli ya KI-VI kwa sauti.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia, watazame nomino na sentensi za ngeli ya
KI-VI ubaoni au kwenye chati. Pia, mwalimu anaweza kuwaeleza jinsi ya kuandika
umoja na wingi katika ngeli ya KI-VI kwa lugha ishara iwapo anaijua.
Maelezo ya jumla
Majina ya ngeli ya KI-VI yana miundo miwili. Muundo wa kwanza ni wa majina
yanayoanza kwa ki- katika umoja na vi- katika wingi. Muundo wa pili ni wa majina
yanayoanza kwa ch- katika umoja na vy- katika wingi. Mwanafunzi anapojua umoja
na wingi wa maneno na sentensi katika ngeli ya KI-VI ataboresha mawasiliano yake.
Kipindi cha 1: Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya KI-VI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 105)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya KI-VI.
b) Kutambua viambishi vya umoja na wingi vya maneno katika ngeli ya KI-VI.
Maswali dadisi
1. Ni nomino gani zilizo katika ngeli ya KI-VI?
2. Nomino za ngeli ya KI-VI huchukua viambishi vipi vya umoja na wingi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo katika kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi ili afahamu
shughuli atakazowashirikisha wanafunzi wakati wa kipindi. Mwalimu aandae nyenzo
kulingana na mahitaji ya wanafunzi. Mwalimu anaweza kuwagawa wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 105, 2. Breli, 3. Rekoda,
4. Vifaa halisi vyenye majina ya ngeli ya KI-VI, 5. Boksi la maneno.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi hiki kwa maswali dadisi. Katika shughuli ya kwanza,
mwalimu awaelekeze wanafunzi kujadili michoro iliyo kitabuni mwao. Wanafunzi
washirikiane katika vikundi kujadili michoro hiyo na wakamilishe mafungu waliyopewa
149
Kimeidhinishwa na KICD
kisha wajibu swali walilopewa. Mwalimu atathmini majibu yao. Majibu tarajiwa:
Kikombe kimoja - vikombe viwili, choo kimoja - vyoo viwili.
Katika shughuli ya pili, wanafunzi wasome maneno yaliyo kwenye kitabu chao kwa
sauti wakiwa katika vikundi viwili. Baada ya kusoma, wanafunzi katika vikundi vyao
wajadili iwapo wamewahi kuviona vitu vyenye majina yaliyotajwa. Waelezane mahali
walikoviona pamoja na matumizi yao. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi
na kuwaelekeza panapofaa. Majibu tarajiwa: chakula - watu hula, kisu - hutumiwa
kukatia, kiti - cha kuketi, chumba - cha kuishi, kioo - cha kujitazama.
Katika shughuli ya tatu, wanafunzi wachague majina ya ngeli ya KI-VI kutoka kwenye
boksi la mseto wa maneno walilopewa kitabuni mwao. Mwalimu anaweza kuandaa
boksi halisi na akaandika maneno yaliyo kwenye boksi hiyo kwenye kadi mbalimbali
kisha wanafunzi wakachagua kadi hizo halisi. Waandike majina waliyochagua katika
wingi. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi. Awasahihishe wanapokosea.
Kwenye kazi ya ziada, wanafunzi waandike majina ya vitu vya darasani katika ngeli ya
KI-VI. Wayaandike majina hayo katika umoja na wingi. Mwanafunzi amsomee mlezi
au mzazi wake majina aliyoandika ili ayatathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuchagua nomino za ngeli ya
KI-VI kutoka kwa mseto wa maneno na kuziandika katika umoja na wingi.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutambua viambishi vya ngeli
vya nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
Kipindi cha 2: Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya KI-VI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 107)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika sentensi katika umoja na wingi akitumia nomino za ngeli ya KI-Vi.
b) Kutambua viambishi vya upatanisho vya nomino katika ngeli ya KI-VI katika
umoja na wingi.
Swali dadisi
Nomino za ngeli ya KI-VI huwa na viambishi gani vya upatanisho katika umoja na
wingi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo katika kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi ili afahamu
shughuli atakazotumia kuwashirikisha wanafunzi wakati wa kipindi.
Anapowagawa wanafunzi katika vikundi, mwalimu ahakikishe kila kikundi kina
150
Kimeidhinishwa na KICD
wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 107, 3. Rekoda,
2. Kanda iliyorekodiwa, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa swali dadisi. Katika shughuli ya
kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi wakiwa wawili wawili kujadili michoro iliyo
kitabuni mwao. Wakamilishe sentensi zilizo chini ya kila mchoro. Mwalimu atathmini
majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kutunga sentensi katika
umoja na wingi wakitumia maneno waliyopewa katika kitabu chao. Baada ya utunzi
wao, wanafunzi wabadilishane madaari ili wazitathmini sentensi zao. Mwalimu
atathmini sentensi za wanafunzi na kuwapa mwongozo panapofaa.
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa wanapoandika sentensi kwa kutumia majina ya
ngeli ya KI-VI, vitenzi vyote katika sentensi huanza kwa kiambishi ki- katika umoja
na vi- katika wingi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi kusikiliza kwa makini
sentensi zitakazosomwa kutoka kwenye rekoda ya mwalimu. Wakiwa katika vikundi,
wataje nomino za ngeli ya KI-VI zilizotumiwa katika sentensi hizo. Kisha, watumie
nomino walizotaja kutunga sentensi sahihi katika umoja na wingi. Kila kikundi
kitathmini sentensi za wengine. Mwalimu awape mwongozo panapofaa.
Mwisho, mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi
aandike majina ya vitu vya nyumbani yaliyo katika ngeli ya KI-VI katika umoja na
wingi. Awasomee wenzake darasani majina hayo.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kukamilisha sentensi za ngeli
ya KI-VI katika umoja na wingi.
2. Mwalimu atathmini kama mwanafunzi anaweza kutumia maneno ya ngeli ya
KI-VI kutunga sentensi katika umoja na wingi.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu atathmini mchoro wa bendera ambao wanafunzi watachora. Pia,
atathmini rangi ambazo watapaka mchoro huo. Sharti mwanafunzi atumie rangi
sahihi za bendera ya Kenya ambazo ni: nyekundu, kijani, nyeusi na nyeupe.
151
Kimeidhinishwa na KICD
2. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Rangi za bendera ni nne: nyeupe,
nyeusi, nyekundu na kijani. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaweza kueleza
maana ya kila rangi ya bendera ya Kenya. Rangi nyeupe huashiria amani. Rangi
nyeusi huashiria rangi ya ngozi ya Wakenya. Rangi ya kijani huashiria kilimo, rutuba
na misitu ya Kenya. Rangi nyekundu huashiria damu iliyomwagika ili tupate uhuru.
3. Mwalimu atathmini shairi ambalo mwanafunzi atatunga. Shairi hilo lihusu bendera
ya Kenya. Mwanafunzi ahesabu idadi ya mishororo na mizani katika ubeti wake.
Aandike idadi hiyo katika daari lake. Mwalimu atathmini idadi hiyo.
4. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi kwa kurejelea shule yake.
5. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaweza kuandika wimbo wa taifa katika daari
lake. Ikiwezekana, mwanafunzi aandike bila kunakili kutoka mahali popote bali
kutoka kichwani. Mwanafunzi aweze kuimba wimbo huo kwa ufasaha.
6. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi kuhusu tofauti kati ya bendera ya Kenya
na ya Rwanda. Bendera ya Rwanda ina rangi tatu (kijani, manjano na samawati)
ilhali bendera ya Kenya ina rangi nne (nyekundu, nyeupe, nyeusi na kijani). Bendera
ya Rwanda ina mchoro wa jua. Bendera ya Kenya ina ngao na mikuki miwili.
7. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaandaa vidokezo vya kuandikia insha kuhusu
mtu yeyote anayempenda. Kisha mwanafunzi aandike insha ya wasifu kumhusu
mtu huyo. Mwalimu atathmini kuwa mwanafunzi anazingatia muundo sahihi wa
insha ya wasifu.
8. Mwalimu ahakikishe kuwa mwanafunzi anaandika majina ya matunda
yanayopatikana katika ngeli ya LI-YA pekee. Mwanafunzi aandike majina hayo
katika umoja na wingi. Mifano: embe maembe, chungwa machungwa,
nanasi mananasi n.k.
9. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi atatunga. Sharti ziwe sahihi na
zitumie majina ya matunda aliyotaja katika swali la 8.
10. Mwalimu atathmini sentensi za mwanafunzi. Sentensi hizo zitumie nomino
alizopewa na ziwe katika umoja na wingi. Mifano:
a) Choo hiki kimesashwa. Vyoo hivi vimesashwa.
b) Chama cha Kiswahili kimeanza. Vyama vya Kiswahili vimeanza.
ch) Kioo kipya kimevunjika. Vioo vipya vimevunjika.
152
Kimeidhinishwa na KICD
MATUNDA NA MIMEA
7
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 109)
A. Kusikiliza na Kuzungumza: Nahau
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nahau za maadili na uraia katika matini mbalimbali.
b) Kutambua maana za nahau mbalimbali za maadili na uraia katika
mazungumzo.
ch) Kutumia nahau za maadili na uraia katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, ni nahau zipi zinazohusu maadili?
2. Je, ni nahau zipi zinazohusu uraia?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
shughuli za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kidijitali.
Hamu ya kuendelea kujifunza - inakuzwa mwanafunzi anapotafuta maana za
nahau na kuzitumia kwa ufasaha katika mawasiliano.
Uwazaji kina na utatuzi wa matatizo - unakuzwa mwanafunzi anapokiria
kuhusu maana za nahau na matumizi yake.
Uhusiano na masuala mtambuko
Umoja wa kijamii - unakuzwa kupitia kwa majadiliano katika vikundi.
Stadi za maisha (kujiamini) - mwanafunzi ataweza kutumia nahau kujieleza
kwa njia ya upole.
Uhusiano na maadili
Umoja na heshima hasa katika kufanya kazi kwa kikundi na wanafunzi
wanaposhirikiana katika majadiliano.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - nahau hufundishwa katika masomo haya.
153
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi kuwa kielelezo kwa wengine katika matumizi ya lugha kiubunifu.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
nahau za
maadili, kueleza
maana za
nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
nahau za
maadili,
anaeleza maana
za nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
nahau za
maadili,
anaeleza maana
za nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya nahau
za maadili,
anaeleza maana
za nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
nahau za
maadili.
Kutambua
nahau za uraia,
kueleza maana
za nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
nahau za uraia,
anaeleza maana
za nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha na kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
nahau za uraia,
anaeleza maana
za nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
nahau za uraia,
anaeleza maana
za nahau hizo
na kuzitumia
kujieleza kwa
ufasaha.
Mwanafunzi
anatambua
nahau za uraia.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wenye matatizo ya kuongea wanaweza kuandika majibu yao madaarini
au hata ubaoni. Wanafunzi wenye matatizo ya kuona wanaweza kutumia breli au
kuwasikiliza wenzao wakisoma nahau za uraia na maadili kwa sauti. Wale wenye
matatizo ya kisaikolojia wapewe ushauri nasaha na kuonyeshwa upendo zaidi.
Wanafunzi wenye matatizo ya kusikia wakae karibu na ubao (wasio viziwi). Mwalimu
anaweza kutumia lugha ishara iwapo anaifahamu. Wanafunzi wanaoelewa haraka
zaidi kuliko wengine wapewe mazoezi zaidi ya kufanya. Wanafunzi wanaochukua
muda kuelewa wapewe muda zaidi wa kukamilisha kazi zao.
Maelezo kwa jumla
Mada hii inashughulikia nahau za maadili na uraia ambazo mwanafunzi anaweza
kutumia katika mazungumzo yake. Nahau zitamwezesha mwanafunzi kukuza
msamiati anapowasiliana na wenzake darasani na hata nje ya darasa.
154
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Nahau za maadili
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 109)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nahau za maadili katika matini mbalimbali.
b) Kutambua maana za nahau mbalimbali za maadili katika mazungumzo.
ch) Kutumia nahau za maadili katika mawasiliano.
d) Kutathmini matumizi ya nahau za maadili katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, ni nahau zipi zinazohusu maadili?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa maadili ni mafunzo mema. Anaweza
kuwashirikisha katika kujadili baadhi ya matendo mema ambayo huonyesha
maadili. Wanafunzi wanaweza kuyaigiza matendo hayo darasani ili kufahamu zaidi.
Awaeleze kuwa matendo mema hukuza ushirikiano katika jamii. Mafungu ya maneno
yanayoonyesha matendo mema ndiyo nahau za maadili.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 109, 2. Tarakilishi,
3. Kadi zenye nahau za uraia na maadili, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje maneno ya upole
wanayoyajua au waliyosoma hapo awali. Mwalimu akubali majibu ya wanafunzi
yanayorejelea maneno ya upole.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Wanafunzi wakiwa
wawili wawili wajadiliane kuhusu maswali waliyopewa kitabuni mwao. Baada ya
majadiliano yao, wanafunzi wanaweza kushirikishwa kuyaigiza matendo waliyojadili
kwa kutumia maneno ya upole. Mwalimu atathmini maigizo ya wanafunzi. Maigizo
humfanya mwanafunzi kujiamini na kujithamini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili. Mwanafunzi mmoja asome
nahau za maadili zilizo kitabuni mwao kisha wanafunzi wengine wasome maelezo ya
nahau hizo. Wanafunzi wakiwa katika vikundi, wajadiliane kuhusu nahau hizo, maana
zake pamoja na matumizi yake. Wanafunzi watumie nahau za maadili walizojadiliana
kutunga sentensi sahihi. Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya tatu. Awaelekeze wanafunzi
kusoma mazungumzo yaliyo kitabuni mwao kisha watambue nahau zilizotumiwa
155
Kimeidhinishwa na KICD
katika mazungumzo hayo kwa kuzipigia mistari. Wanafunzi watumie nahau walizopigia
mistari kutunga sentensi sahihi. Mwalimu awaelekeze wanafunzi watambue majina
ya mimea na matunda yaliyotumiwa katika mazungumzo hayo. Wanafunzi watumie
mtandao kutafuta picha za mimea na matunda waliyotambua.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada daftarini mwake kwa
kuandika maana za nahau zilizo kitabuni mwake. Mwanafunzi atunge sentensi
kwa kutumia nahau za maadili alizopewa. Amsomee mlezi au mzazi wake sentensi
alizotunga.
Majibu tarajiwa ya kazi ya ziada:
1. a) kujikaza kisabuni - kujitahidi/kufanya bidii b) omba kibali - pata ruhusa
ch) kumpa mtu mkono wa tahania - kumpongeza d) shika sikio - fuata maagizo.
e) anguka miguuni - nyenyekea f) piga dua - omba
2. Mwalimu akubali sentensi zozote sahihi zilizotumia nahau husika.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza:
1. Kutambua nahau za maadili kwenye matini mbalimbali.
2. Kutambua maana ya nahau za maadili.
3. Kutumia nahau za maadili katika mawasiliano.
Kipindi cha 2: Nahau za uraia
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 111)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nahau za uraia katika matini mbalimbali.
b) Kutambua maana za nahau mbalimbali za uraia katika mazungumzo.
ch) Kutumia nahau za uraia katika mawasiliano.
d) Kutathmini matumizi ya nahau za uraia katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, ni nahau zipi zinahusu uraia?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuhusu maana ya nahau za uraia. Uraia hukuza
uzalendo miongoni mwa wanafunzi. Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa uzalendo
hujikita katika mwananchi kuipenda na kuitunza nchi yake.
156
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 111, 2. Breli, 3. Kadi,
4. Kadi zenye nahau za uraia na maadili.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Wanafunzi wajadili
michoro iliyo kitabuni mwao na wajibu maswali waliyopewa. Michoro hiyo ni ya
gwaride na bunge. Mwalimu atathmini usahihi wa majibu ya wanafunzi wote. Majibu
yalingane na michoro husika. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutaja majina ya
viongozi mbalimbali hasa wa eneo la shule yao ambao hupatikana bungeni. Shughuli
hii itakuza uraia miongoni mwa wanafunzi.
Mwalimu amwongoze mwanafunzi kutambua nahau za uraia zilizotumiwa kwenye
kifungu kilicho katika shughuli ya pili. Mwanafunzi aandike maana ya nahau hizo
kisha azitumie kutunga sentensi sahihi. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi kucheza mchezo wa kadi za
nahau. Mwalimu awape kikapu chenye kadi zilizoandikwa nahau mbalimbali kisha
wachague nahau za uraia na maadili pekee. Mwanafunzi mmoja asome nahau hizo
kisha wengine waeleze maana zao.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi atunge sentensi
sahihi kwa kutumia nahau za uraia na maadili walizotambua katika shughuli ya tatu.
Awasomee wenzake nahau hizo darasani ili wazisikilize na kuzitathmini.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza:
1. Kutambua nahau za uraia katika matini mbalimbali.
2. Kutambua maana za nahau za uraia katika mazungumzo.
3. Kutumia nahau za uraia katika mawasiliano.
B. Kusoma: Kusoma kwa mapana
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 113
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini ya aina mbalimbali ya kusoma na kuchagua yanayomvutia.
b) Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
Maswali dadisi
1. Kwa nini unapenda kusoma?
157
Kimeidhinishwa na KICD
2. Ni nini kinachokufanya uchague kitabu au makala ya kusoma?
3. Ni nini kinachokuvutia unaposoma hadithi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposimulia na
kujadiliana na wenzake katika vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia tarakilishi na mtandao
kupata matini ya kusoma.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapojichagulia matini na kuisoma.
Uhusiano na masuala mtambuko
Matini anayochagua mwanafunzi itakuwa na masuala mtambuko mbalimbali
kama vile mazingira, utoshelevu wa chakula n.k.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - mwanafunzi anapotunza tarakilishi anayotumia.
Heshima - mwanafunzi anapojadiliana na wenzake kuhusu alichosoma.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanajumuisha mada ya kusoma
kama mojawapo ya stadi za lugha.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Kuwa kielelezo cha utamaduni wa kusoma shuleni na nyumbani. Maarifa anayopata
mwanafunzi kutokana na usomaji wake ayatumie shuleni na nyumbani kuifaidi jamii.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Utamaduni
mzuri wa
kusoma
matini za aina
mbalimbali
shuleni na
nje ya shule
na kusimulia
kwa ufasaha
alichokisoma.
Mwanafunzi
ana utamaduni
mzuri wa
kusoma
matini za aina
mbalimbali
shuleni na
nje ya shule
na kusimulia
kwa ufasaha
na usahihi
alichokisoma.
Mwanafunzi
ana utamaduni
mzuri wa
kusoma
matini ya aina
mbalimbali
shuleni na nje
ya shule na
anasimulia
kwa ufasaha
alichokisoma.
Mwanafunzi
ana utamaduni
wa kusoma
baadhi za
sampuli za
matini shuleni
na kusimulia.
Mwanafunzi
anajaribu
kusoma baadhi
ya matini
shuleni.
158
Kimeidhinishwa na KICD
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wenye matatizo ya kuona, watumie breli wanaposoma. Ni vyema
wanafunzi wenye matatizo ya kusikia vizuri waketi karibu na ubao. Kwa upande
mwingine, wanafunzi ambao huelewa haraka kuliko wenzao wapewe mazoezi
zaidi huku wenzao wanaochukua muda zaidi kuelewa wakipewa muda zaidi.
Maelezo kwa jumla
Mada hii inashughulikia usomaji wa matini mbalimbali. Kusoma humwezesha
mwanafunzi kukuza ubunifu wake katika uandishi na mawasiliano. Pia, mwanafunzi
anaweza kujua misamiati mbalimbali ili kuboresha lugha na hata uandishi wake. Hivyo
basi ni vyema mwalimu amtie moyo mwanafunzi asome matini mbalimbali.
Kipindi cha 1: Matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 113)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini za aina mbalimbali ya kusoma na kuchagua inayomvutia.
b) Kusoma matini alizochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
Swali dadisi
Kwa nini unapenda kusoma?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asisitize kuwa usomaji wa matini ni muhimu. Mwalimu awe na nyenzo
halisi kama vile vitabu vya hadithi, michoro ya maktaba, magazeti mbalimbali pamoja
na majarida mbalimbali. Awaeleze wanafunzi kuwa wanaposoma matini mbalimbali
ubunifu wao utakuzwa. Hivyo, ni vyema kusoma matini mbalimbali zilizo bora na za
kiwango chao.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 113, 4. Vitabu vya hadithi,
2. Breli, 5. Gazeti.
3. Tarakilishi,
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Wanafunzi wawili
wawili watazame mchoro ulio kitabuni mwao kisha waujadili. Baada ya kuujadili,
wajibu maswali waliyopewa kuhusu mchoro huo. Mwalimu atathmini majibu yao.
159
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kujadiliana wakiwa wawili
wawili kuhusu maswali waliyopewa kitabuni mwao. Kila mwanafunzi aandike
muhtasari wa matini yoyote aliyowahi kusoma maktabani. Watathmini kazi zao katika
vikundi vyao.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya tatu kutumia tarakilishi kutafuta
matini yoyote mtandaoni kuhusu mimea au matunda. Awaongoze katika kuzisoma
matini walizopata. Baada ya kusoma na kuelewa, wanafunzi waandike muhtasari wa
matini hiyo. Hatimaye, wawatumie wenzao mtandaoni ili wazitathmini kazi zao.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
majina ya mimea inayopatikana katika shamba lao au hata la jirani yao. Pia, aandike
majina ya matunda ambayo wao hula nyumbani na awaeleze wenzake darasani
wanakoyatoa matunda hayo. Mwalimu akubali majibu yaliyo sahihi yanayohusu
matunda na mimea.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi:
1. Anaweza kutambua matini za aina mbalimbali za kusoma.
2. Anaweza kuchagua matini ya kusoma na ya kuvutia mtandaoni, vitabuni au
gazetini.
3. Anaweza kutambua majina ya mimea na matunda mbalimbali.
Kipindi cha 2: Matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 114)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
b) Kusoma matini mbalimbali za kiwango chake.
Maswali dadisi
1. Ni nini kinachokufanya uchague kitabu na makala ya kusoma?
2. Unafaidi vipi unaposoma matini mbalimbali?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa kusoma matini mbalimbali humwezesha kufaidi
ujumbe na pia lugha iliyotumiwa. Ni vyema pia kuhakikisha wanafunzi wamechagua
matini salama za kiwango chao.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 114, 4. Nakala za gazeti,
2. Tarakilishi, 5. Vitabu vya hadithi.
3. Kamusi,
160
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaongoze wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya kwanza wajadili
wanachokiona kwenye michoro iliyo kitabuni mwao. Michoro hiyo ni ya gazeti na
kitabu cha hadithi. Mwalimu awaongoze wanafunzi katika kutaja vitabu vya hadithi
walivyowahi kusoma. Vilevile, wataje magazeti yanayopatikana nchini Kenya hasa ya
Kiswahili. Wanafunzi watambue faida za kusoma matini mbalimbali.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kusoma hadithi iliyo
kitabuni mwao. Wajadiliane kuhusu ujumbe na lugha ya hadithi hiyo kisha wajibu
maswali waliyopewa. Wanafunzi wajibu maswali yanayotokana na hadithi hiyo.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
jina la zao linalotokana na mmea unaoitwa mhindi. Pia, mwanafunzi aeleze umuhimu
wa zaa hilo kwa binadamu. Anaweza kusaidiwa na mlezi au mzazi wake. Pia, anaweza
kutumia tarakilishi kutafuta umuhimu huo mtandaoni.
Majibu tarajiwa: 1. Mahindi 2. Mahindi ni chakula kwa binadamu na wanyama.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi:
1. Anaweza kuchagua matini salama za kusoma zenye ujumbe faafu.
2. Anaweza kueleza umuhimu wa kusoma matini mbalimbali.
3. Amefaidi kutokana na ujumbe na lugha iliyotumiwa kwenye matini aliyosoma.
Kipindi cha 3: Matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 116)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
1. Kufurahia usomaji wa aina mbalimbali za matini.
2. Kupata mafunzo kutoka kwa matini mbalimbali.
Swali dadisi
Ni nini kinachokuvutia unaposoma hadithi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa kusoma matini mbalimbali hutokana na mvuto
uliopo. Unaweza kuwa mvuto wa picha kwenye matini hiyo au lugha iliyotumiwa.
Awaeleze kuwa ni muhimu kusoma zaidi na zaidi ili kujifurahisha na kujielimisha.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 116, 2. Mgeni mwalikwa, 3. Breli.
161
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaongoze wanafunzi kutazama mchoro
ulio kitabuni mwao wakiwa katika vikundi. Wanafunzi wajibu maswali yanayotokana
na mchoro huo.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili wasikilize masimulizi kutoka
kwa mgeni mwalikwa kuhusu ukulima. Mwalimu anaweza kumwalika mkulima
yeyote akawasimulia wanafunzi kuhusu shughuli za ukulima. Pia, anaweza kumwalika
mwanamazingira yeyote akawasimulia kuhusu utunzaji wa mazingira. Wanafunzi
wasikilize masimulizi hayo kwa makini kisha waandike muhtasari wake. Mwanafunzi
aandike majina ya mimea iliyotajwa katika masimulizi hayo.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kusoma kitabu
chochote cha hadithi maktabani kisha aandike maneno mapya aliyojifunza katika
daari lake. Mwanafunzi amsimulie mlezi au mzazi wake hadithi aliyosoma.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi:
1. Anaweza kusikiliza kisa kutoka kwa mgeni mwalikwa na kukisimulia kwa
wenzake.
2. Anaweza kuandika daarini kisa alichosimuliwa.
CH. Kuandika: Kuandika Insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 117)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya maelezo katika matini.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
Swali dadisi
Je, ni vitu gani vinavyoweza kuandikiwa insha ya maelezo?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
kuandika insha mtandaoni na kurejelea kielelezo cha insha ya maelezo.
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya maelezo.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapotafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
162
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja katika vikundi.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia uandishi wa insha.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi mzuri katika mawasiliano.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuandika insha
ya maelezo
inayotumia
vivumishi na
vielezi kwa
ufasaha kujenga
picha dhahiri
yenye kuzingatia
kanuni za lugha
na mpangilio
mzuri wa
mawazo.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo
akitumia
vivumishi na
vielezi kwa
ufasaha kujenga
picha dhahiri
akizingatia
kanuni za lugha
na mpangilio
mzuri wa
mawazo kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo
akitumia
vivumishi na
vielezi kwa
ufasaha kujenga
picha dhahiri
akizingatia
kanuni za lugha
na mpangilio
mzuri wa
mawazo.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo
akitumia
vivumishi
na vielezi
kwa uchache
akizingatia
baadhi ya
kanuni za lugha.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika insha
ya maelezo.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, wasome maelezo ya insha ya maelezo kwa
kutumia breli.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuzungumza, wajibu maswali kwa kuandika daarini
au kwenye tarakilishi.
Wanafunzi wasioweza kusema au kusikia, watumie lugha ishara kueleza kuhusu
insha ya maelezo. Pia, wajibu swali dadisi kwa kuandika daarini au kwenye
vipakatalishi. Mwalimu aandike maelezo ya insha ya maelezo ubaoni au kwenye
chati ili waweze kuyasoma.
163
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuandika kwa kutumia mikono wahimizwe kutumia
viungo vingine kama vile miguu ama midomo kushika kalamu na kuandika. Wapewe
muda zaidi. Mwalimu awahamasishe wanafunzi wengine kuhusu umuhimu wa
kumkubali mtu bila kujali mahitaji yake. Kufanya hivyo, kutazuia unyanyapaa kwa
wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali.
Maelezo ya jumla
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuhusu insha ya maelezo. Awaeleze kuwa mifano ya
insha hii inaweza kupatikana kwenye matini mtandaoni. Wafahamu kuwa sharti insha
hii iwe na mada ya kuandikia. Pia, awaeleze kuhusu kanuni za kufuata wanapoandika
insha hii. Uandishi hukuza ubunifu wa mwanafunzi.
Kipindi cha 1: Insha ya maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 117)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya maelezo katika matini.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
Maswali dadisi
1. Je, ni vitu gani vinavyoweza kuandikiwa insha ya maelezo?
2. Ni vivumishi vipi vya sifa unavyovifahamu?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa insha ya maelezo ina muundo wake maalumu.
Huandikwa kwa kutumia vivumishi na vielezi ili kufafanua mada husika. Maelezo
haya yanafaa kutiririsha hoja moja baada ya nyingine.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 117, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa maswali dadisi. Awashirikishe wanafunzi katika
shughuli ya kwanza. Awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na
mahitaji yao kisha awaelekeze watazame michoro iliyo kitabuni mwao. Wanafunzi
wajadili vitendo katika michoro waliyopewa na wajibu maswali yaliyomo. Baadaye,
kila mwanafunzi aandike aya mbili za maelezo kuhusu vitendo katika michoro husika.
Majibu tarajiwa: 1. Hutupa chakula/matunda, hutuletea pesa yanapouzwa n.k.
2. mwembe - embe, mchungwa - chungwa, mzabibu - zabibu n.k. 3. Mwalimu atathmini
insha ya maelezo ya wanafunzi.
164
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili wasome kielelezo cha insha
ya maelezo walichopewa kitabuni mwao. Wanafunzi wajibu maswali ya insha hiyo.
Mwalimu atathmini majibu yao.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya tatu watafute mtandaoni picha
za matunda na mimea iliyotajwa katika shughuli ya pili. Wanafunzi waandike rangi za
matunda hayo.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya ziada kwa kuchora na kupaka
rangi matunda waliyotajiwa katika kitabu chao. Wanafunzi waonyeshane michoro yao
darasani. Majibu tarajiwa: mwalimu asahihishe michoro halisi ilivyo na rangi ifaayo
kwa kila mchoro.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo:
1. Mwanafunzi anatambua vifungu vya maelezo kwenye matini mbalimbali.
2. Mwanafunzi anauelewa muundo wa kuandika insha ya maelezo.
3. Mwanafunzi anaelewa matumizi ya vivumishi, vielezi na vidokezo katika
uandishi wa insha ya maelezo.
Kipindi cha 2: Insha ya maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 119)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
b) Kuelewa utunzi mzuri wa insha ya maelezo ili kukuza ubunifu.
Maswali dadisi
1. Je, ni vitu gani vinavyoweza kuandikiwa insha ya maelezo?
2. Je, wazifahamu nahau na methali zipi zinazofaa kutumiwa tunapoandika insha
ya maelezo?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa insha ya maelezo ina kanuni za kuzingatia.
Awafahamishe kuwa ili kuboresha insha ya maelezo wanapoiandika wanaweza
kutumia nahau na hata methali. Ni vyema pia kuzingatia mada lengwa ili wasipotoke.
Anaweza kuwakumbusha baadhi ya nahau walizosoma katika kipindi cha hapo awali.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifuzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 119, 2. Breli,
3. Ziara ya kuzuru shamba la shule.
165
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifuzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na mahitaji yao. Wanafunzi wajadili vitendo katika michoro iliyo kitabuni
mwao kisha wajibu maswali waliyopewa. Mwalimu atathmini majibu yao. Majibu
tarajiwa: Umuhimu wa kupanda miti (kupata matunda, kupata mbao, kuleta mvua,
kuleta hewa sa, kupata kivuli, kupata vyakula vya wanyama n.k.), madhara ya kukata
miti (kukosa umuhimu wote wa miti).
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kufanya ziara nje ya
darasa. Mwalimu anaweza kupanga ziara hii wakati wa wikendi, likizo au siku moja
jioni ili wapate muda wa kutosha huko shambani. Mwalimu awapeleke wanafunzi
katika shamba la shule ili watazame mimea shambani humo na waandike majina
yao. Pia, mwalimu awapeleke wanafunzi katika shamba lililo jirani na shule yao ili
watazame mimea iliyo huko na waandike majina yao.
Katika kazi ya ziada, mwalimu amwelekeze mwanafunzi kuandika insha ya maelezo
katika daari lake. Azingatie mada lengwa ambayo ni namna ya kutunza mimea
shambani kuanzia upanzi hadi uvunaji. Mwanafunzi akumbuke kutumia kanuni
zifaazo na muundo sahihi wa insha ya maelezo. Mwalimu asahihishe insha za
wanafunzi. Awasomee wanafunzi insha bora zaidi ili wajifunze.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi:
1. Anaweza kutazama na kujadili michoro ipasavyo.
2. Anaweza kuandika majina ya mimea na matunda mbalimbali.
3. Anaweza kuandika insha ya maelezo kwa kuzingatia muundo sahihi.
D. Saru:Umojanawingiwasentensi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 120)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya KI-VI katika
umoja na wingi.
b) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
Swali dadisi
Ni nomino gani za ngeli ya KI-VI unazozijua?
166
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika kazi
za vikundi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika kutunga sentensi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia tarakilishi na mtandao.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu endelevu - wanafunzi wanapotoa mifano ya nomino zinazohusu masuala
mtambuko kama vile upanzi wa mimea, mazingira, ugaidi n.k.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - unakuzwa mwanafunzi anapotunza tarakilishi.
Heshima - inakuzwa mwanafunzi anapofanya kazi na wenzake katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu mawasiliano yenye
kuzingatia kanuni za kisaru.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutunga
sentensi sahihi
zinazozingatia
upatanisho wa
kisaru wa ngeli
ya KI-VI katika
umoja na wingi.
Mwanafunzi
anatunga
sentensi sahihi
zinazozingatia
upatanisho wa
kisaru wa ngeli
ya KI-VI katika
umoja na wingi
kwa urahisi.
Mwanafunzi
anatunga
sentensi sahihi
zinazozingatia
upatanisho wa
kisaru wa ngeli
ya KI-VI katika
umoja na wingi.
Mwanafunzi
anatunga baadhi
ya sentensi
zinazozingatia
upatanisho wa
kisaru wa ngeli
ya KI-VI katika
umoja na wingi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutunga
sentensi
zinazozingatia
upatanisho wa
kisaru wa ngeli
ya KI-VI.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona mbali waketi karibu na ubao. Wasioweza
kuona vitu vilivyo karibu nao waketi mbali na ubao ili waweze kuona vizuri ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema watazame kwenye ubao, kiwambo
cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au kwenye chati.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kutambua nomino za ngeli ya KI-VI kwa urahisi
wahusishwe katika shughuli zaidi za ujifunzaji. Wapewe muda zaidi wa kujifunza
huku wakihimizwa kwa upendo ili wajithamini na kuchangamkia ujifunzaji. Hatua
167
Kimeidhinishwa na KICD
yoyote wanayopiga katika ujifunzaji itambuliwe na mwalimu ili wawe na hamu ya
kujifunza zaidi.
Maelezo ya jumla
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kuhusu ngeli ya KI-VI. Wanafunzi waelewe kuwa
nomino katika ngeli hii huanza kwa silabi ki- au ch- katika umoja na vi- au vy- katika
wingi. Katika kuunda sentensi, kiambishi ngeli katika umoja ni ki- na katika wingi ni
vi-. Hii ndiyo sababu ikaitwa ngeli ya KI-VI.
Kipindi cha 1: Sentensi katika ngeli ya KI-VI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 120)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya KI-VI katika
umoja na wingi.
b) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
Swali dadisi
Ni nomino gani za ngeli ya KI-VI unazozijua?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa ngeli ya KI-VI inahusu nomino zinazoanza kwa
silabi ki- au ch- katika umoja na vi- au vy- katika wingi. Mwalimu awatahadharishe
wanafunzi dhidi ya maneno ya viumbe wenye uhai ambao majina yao huanza kwa
silabi ki- au ch- katika umoja na vi- au vy- katika wingi. Kwa mfano: kipofu - vipofu,
chura - vyura.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 120, 2. Breli,
3. Mchoro wa mche wenye sentensi za ngeli ya KI-VI.
Mapendekezo ya shughuli za ujifuzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa shughuli ya kwanza kwa kuwauliza wanafunzi
wataje nomino mbalimbali zinazoanza kwa silabi ki- au ch- katika umoja. Awaongoze
wanafunzi waandike wingi wa nomino walizotaja. Vilevile, awaongoze wanafunzi
kujadili kuhusu waliyogundua katika umoja na wingi wa nomino walizotaja.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awashirikishe wanafunzi watambue baadhi ya
nomino za vyakula, sehemu za mwili, vifaa vya darasani na nyumbani zilizo katika
168
Kimeidhinishwa na KICD
ngeli ya KI-VI. Wanafunzi watumie nomino hizo kutunga sentensi sahihi. Mwalimu
atathmini majibu yao.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya tatu. Wapigie mistari nomino za
ngeli ya KI-VI katika sentensi zilizo kwenye mchoro wa mche ulio kitabuni mwao.
Vilevile, watunge sentensi sahihi kwa kutumia nomino walizopigia mistari. Mwalimu
atathmini sentensi watakazotunga.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kuandika kifungu cha
aya mbili akitumia nomino zozote za ngeli ya KI-VI. Wazipigie mistari nomino hizo.
Mwalimu asahihishe vifungu vya wanafunzi darasani. Anaweza kuwasomea wanafunzi
kifungu bora zaidi ili wajifunze.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo:
1. Mwanafunzi anaweza kutaja nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na wingi.
2. Anaweza kutunga sentensi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI.
Kipindi cha 2: Sentensi katika ngeli ya KI-VI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 121)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino za ngeli ya KI-VI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
b) Kufahamu matumizi ya nomino za ngeli ya KI-VI katika mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Je, ni nomino gani za ngeli ya KI-VI unazozijua?
2. Ni viambishi ngeli vipi tunavyotumia tunapounda sentensi kwa umoja na wingi
katika ngeli ya KI-VI?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awakumbushe wanafunzi wataje nomino katika ngeli ya KI-VI. Awaeleze
kuwa wanapotunga sentensi, viambishi ngeli ki- na vi- hutumika katika umoja na wingi
mtawalia. Haya yatamwezesha mwanafunzi katika kuwasiliana akizingatia upatanisho
sahihi wa kisaru.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 121, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
169
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifuzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwaongoza wanafunzi kutazama michoro iliyo
kitabuni mwao katika shughuli ya kwanza. Awaongoze kujaza nafasi katika sentensi
zilizo chini ya kila mchoro. Awaelekeze watunge sentensi sahihi katika ngeli ya KI-VI
kwa kutumia nomino za michoro waliyotazama.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili. Wasome sentensi zilizo
kitabuni mwao wakiwa katika vikundi viwili. Kikundi kimoja kisome sentensi za
umoja na kingine kisome sentensi za wingi. Kila mwanafunzi aandike sentensi hizo
katika daari lake kisha apigie mistari viambishi vya ngeli ya KI-VI.
Mwalimu amwongoze mwanafunzi katika shughuli ya tatu. Aandike sentensi kumi za
ngeli ya KI-VI kwenye tarakilishi katika umoja na wingi akizingatia upatanisho sahihi
wa kisaru. Amwongoze mwanafunzi katika kuzisambaza kwa wenzake mtandaoni ili
wazisome na kuziboresha.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada iliyo kitabuni mwao.
Mwanafunzi atunge shairi la beti mbili akitumia nomino za ngeli ya KI-VI. Mwalimu
atathmini shairi la kila mwanafunzi. Mwalimu awateue wanafunzi wachache wawasomee
wenzao mashairi yao darasani.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi:
1. Anaweza kuandika sentensi, kuandika kifungu au kutunga shairi akitumia
nomino katika ngeli ya KI-VI kwa kuzingatia upatanisho wa kisaru.
2. Anaweza kutunga sentensi sahihi kwenye tarakilishi katika umoja na wingi
kisha kuzisambaza kwa wenzake mtandaoni.
Umoja na wingi wa nomino
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya LI-LI.
b) Kutambua nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na wingi.
ch) Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-LI.
d) Kutumia nomino za lugha za ngeli ya LI-LI katika mawasiliano.
e) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-LI katika
umoja na wingi.
f) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino katika ngeli ya LI-LI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
Maswali dadisi
1. Ni nomino gani za LI-LI unazozijua?
170
Kimeidhinishwa na KICD
2. Ni viambishi vipi vya ngeli vinavyotumiwa katika kuunda sentensi katika ngeli
ya LI-LI katika umoja na wingi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga mafungu ya maneno ya ngeli ya
LI-LI.
Kukiria kwa kina - kunakuzwa mwanafunzi anapowaza kwa kina kuhusu
atakachoandika.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia tarakilishi kutambua
nomino na katika kusikiliza mafungu ya maneno yakisomwa.
Uhusiano na masuala mtambuko
Utangamano - unakuzwa kwa kufanya kazi katika vikundi.
Stadi za maisha - zinakuzwa kwa kujifanyia kazi darasani bila kunakili za
wengine.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - kutunza vipakatalishi anavyotumia.
Uzalendo - kufanya kazi na wengine kwenye vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - nomino hufundishwa katika masomo haya.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Kutumia lugha sanifu miongoni mwa wenzake shuleni na nyumbani kama kielelezo
cha kuzingatia Kiswahili sanifu.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi matarajio Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua umoja
na wingi wa
nomino katika
ngeli ya LI-LI
na kuzitumia
kwenye mafungu
ya maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua umoja
na wingi wa
nomino katika
ngeli ya LI-LI
na anazitumia
kwenye mafungu
ya maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi na urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli
ya LI-LI na
anazitumia
kwenye mafungu
ya maneno na
sentensi zenye
maana kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
umoja na wingi
wa baadhi ya
nomino katika
ngeli ya LI-LI na
kutumia baadhi
ya nomino
hizo kwenye
mafungu ya
maneno kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
umoja na wingi
wa nomino
katika ngeli ya
LI-LI.
171
Kimeidhinishwa na KICD
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona mbali waketi karibu na ubao. Wasioweza
kuona vitu vilivyo karibu nao waketi mbali na ubao ili waweze kuona vizuri ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema watazame kwenye ubao, kiwambo
cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au kwenye chati.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kutambua nomino za ngeli ya LI-LI kwa urahisi
wahusishwe katika shughuli zaidi za ujifunzaji. Wapewe muda zaidi wa kujifunza
huku wakihimizwa kwa upendo ili wajithamini na kuchangamkia ujifunzaji. Hatua
yoyote wanayopiga katika ujifunzaji itambuliwe na mwalimu ili wawe na hamu ya
kujifunza zaidi.
Maelezo kwa jumla
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa nomino katika ngeli ya LI-LI huwa hazibadiliki
katika umoja na wingi. Awape mifano.
Kipindi cha 1: Nomino katika ngeli ya LI-LI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 123)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua nomino katika ngeli ya LI-LI.
b) Kuandika nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na wingi.
ch) Kuandika umoja na wingi wa mafungu ya maneno katika ngeli ya LI-LI.
Swali dadisi
Ni nomino zipi zilizo katika ngeli ya LI-LI?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuhusu ngeli ya LI-LI. Awaeleze kwamba ngeli hii
inahusisha nomino zisizobadilika katika wingi na ambazo kiambishi ngeli katika
umoja ni li- na katika wingi ni li-. Nomino za ngeli ya LI-LI hazina wingi. Hubaki
vilevile. Anaweza kuwatoa nje wanafunzi wakatazama jua. Aandae rekoda iliyo na
nomino za ngeli ya LI-LI.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 123, 4. Tarakilishi,
2. Rekoda, 5. Mti wa nomino za ngeli ya LI-LI,
3. Breli, 6. Kadi za nomino za ngeli ya LI-LI.
172
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa shughuli ya kwanza akiwaruhusu wanafunzi
kuulizana na kujibu maswali waliyopewa kitabuni mwao huku wakielezana wenyewe
kwa wenyewe. Mwalimu atathmini majibu yao.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaandalie wanafunzi rekodi ya nomino za ngeli
ya LI-LI na awachezee rekodi hiyo huku wakisikiliza usomaji wa nomino lengwa.
Wanafunzi watamke maneno waliyosikiliza kwa kuzingatia matamshi bora. Baadaye,
waandike katika madaari yao maneno hayo katika umoja na wingi. Mwalimu
atathmini majibu yao.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya tatu kusoma kifungu na kupigia
mistari nomino za ngeli ya LI-LI pamoja na majina ya matunda. Mwalimu atathmini
majibu yao.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi ashirikiane na
mlezi au mzazi wake katika kujibu maswali aliyopewa kitabuni mwake. Mwalimu
atathmini majibu ya kila mwanafunzi kulingana na maswali yaliyoulizwa.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi:
1. Anaweza kutaja nomino zilizo katika ngeli ya LI-LI.
2. Anaweza kutambua na kuandika nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na
wingi.
Kipindi cha 2: Ngeli ya LI-LI
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 124)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua sentensi zilizoundwa kutokana na nomino za ngeli ya LI-LI katika
umoja na wingi.
b) Kuunda sentensi sahihi akitumia nomino katika ngeli ya LI-LI katika umoja na
wingi akizingatia upatanisho wa kisaru.
Maswali dadisi
1. Ni nomino gani za ngeli ya LI-LI unazozijua?
2. Ni viambishi vipi vya ngeli vinavyotumiwa katika kuunda sentensi katika ngeli
ya Li-Li kwa umoja na wingi?
173
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awakumbushe wanafunzi nomino za ngeli ya LI-LI katika umoja na wingi.
Sentensi zilizotungwa katika ngeli hii huchukua kiambishi li- katika umoja na li- katika
wingi. Mwalimu akumbuke kuwa nomino hizi hazibadiliki katika umoja na wingi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 124, 2. Tarakilishi,
3. Mti wa nomino za ngeli ya LI-LI, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa shughuli ya kwanza kwa kuwaongoza wanafunzi
kutazama mti wa maneno ulio kitabuni mwao. Wanafunzi wataje nomino za ngeli ya
LI-LI kwenye mti huo. Awaongoze wanafunzi kutumia nomino walizochagua kutoka
kwa mti wa maneno kutunga sentensi sahihi katika umoja na wingi. Mwalimu
atathmini sentensi za wanafunzi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili wajadiliane kuhusu
wanachoona katika michoro iliyo kitabuni mwao. Awaongoze wanafunzi waeleze
sababu inayochangia mtu kuwa katika hali ya mchoro wa kwanza ya mtu aliyetokwa
na jasho. Majibu tarajiwa: kukimbia, kuwa mgonjwa, kutembea haraka, kuchomwa na
jua n.k. Vilevile, wanafunzi waeleze mchoro wa pili (b) wa jua una umuhimu gani kwa
watu na mimea. Majibu tarajiwa: kukausha nguo, kukausha nafaka, kusaidia mimea
kukua, kumpa binadamu vitamini D n.k.
Mwalimu awahusishe wanafunzi katika shughuli ya tatu ya kuchopoa kadi
zilizoandikwa nomino za ngeli ya LI-LI kutoka kwenye boksi. Wazisome nomino
hizo kwa sauti katika umoja na wingi. Mwalimu amwongoze mwanafunzi kutunga
kifungu cha aya mbili katika daari lake kwa kutumia nomino walizosoma. Mwalimu
atathmini vifungu vya wanafunzi. Vifungu bora zaidi visomwe darasani ili wengine
wajifunze.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike kifungu
alichotunga katika shughuli ya tatu kwenye tarakilishi. Ahifadhi kifungu hicho
kwenye faili kwa jina lake kisha awasambazie wenzake mtandaoni ili wakisome na
kukitathmini.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo:
1. Mwanafunzi anaweza kutaja nomino katika ngeli ya LI-LI.
2. Mwanafunzi anaweza kutunga sentensi na kifungu akitumia nomino katika
ngeli ya LI-LI ipasavyo kwa umoja na wingi.
174
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu atathmini maana za nahau ambazo mwanafunzi ataeleza. Maana hizo
ziwe sahihi. Maana ya nahau shika hatamu’ ni kuchukua uongozi. Maana ya nahau
‘vulia koa ni kumheshimu mtu au kuonyesha kuwa mtu amekupiku kwa jambo
fulani. Mwanafunzi atunge sentensi sahihi kwa kutumia nahau hizo mbili. Mifano:
Rais mwingine ameshika hatamu. Nilimvulia koa mgeni mheshimiwa.
2. Mwalimu atathmini shughuli za maktabani ambazo mwanafunzi ataeleza. Sharti
shughuli hizo zihusu maktaba. Mifano ya shughuli za maktabani ni: kusoma vitabu
vya hadithi, kusoma magazeti, kufanya mazoezi ya darasani kwa kutumia vitabu vya
kiada, kudurusu karatasi za mitihani, kuchora n.k.
3. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaandika insha ya maelezo kuhusu tunda
lolote ambalo analipenda. Mwalimu atathmini muundo atakaotumia mwanafunzi
ili kuhakikisha ndio muundo sahihi wa insha ya maelezo. Mwalimu ahakikishe
mwanafunzi anaandaa vidokezo vya kutumia.
4. Mwanafunzi atathmini majibu ya mwanafunzi kwa kurejelea mazingira ya ndani na
nje ya shule yao. Mifano ya mimea ni: mihindi, mwembe, mparachichi, nyasi, maua
mbalimbali n.k.
5. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi.
a) Vitabu vimeraruliwa.
b) Vijiko vimechafuliwa.
6. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi.
a) Jasho linaonekana.
b) Joto linakera.
7. Mwalimu atathmini maelezo ya mwanafunzi kuhusu jinsi ya kuitunza mimea
shambani. Kwa mfano: kuipalilia, kuinyunyizia maji (katika sehemu kame),
kuinyunyizia dawa, kuiwekea mbolea, kuipogoa n.k.
8. Mwalimu akubali majibu yote yanayotaja majina ya vifaa vya nyumbani yaliyo
katika ngeli ya KI-VI. Mifano: kijiko, kisu, kikombe, chungu, kiberiti, kiti, kitanda,
kioo n.k.
9. Neno lisilofaa kati ya aliyopewa mwanafunzi ni kiota. Mwalimu atathmini sentensi
atakayotunga mwanafunzi akitumia neno kiota. Sharti sentensi hiyo iwe sahihi
kisaru. Mfano: Kiota cha ndege kimeharibika.
10. Mwalimu atathmini aya moja ya kifungu atakayotumiwa na mwanafunzi katika
mtandao. Ahakikishe aya hiyo inahusisha nomino za ngeli ya LI-LI. Nomino za
ngeli ya LI-LI ziandikwe kwa kutumia chapa koza.
175
Kimeidhinishwa na KICD
WANYAMA WA PORINI
8
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 127)
A. KusikilizanaKuzungumza:Visawe
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kisawe ili kukibainisha.
b) Kutambua visawe vya maneno mawili katika kundi la maneno.
ch) Kutumia visawe vya kiwango chake ifaavyo katika mawasiliano.
d) Kuthamini matumizi ya visawe katika mawasiliano.
Swali dadisi
Unajua maneno gani ya Kiswahili yaliyo na maana sawa?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Uwazaji wa kina na utatuzi wa matatizo - unakuzwa mwanafunzi anapokiria
kuhusu visawe mwafaka vya maneno.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali kama
nyenzo za kufaulisha mada.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anapoweza kutunga sentensi zenye visawe.
Hamu ya kuendelea kujikuza - umilisi huu unakuzwa mwanafunzi anapokuwa
na shauku ya kuendelea kutati ili kujifunza mengi zaidi kuhusu wanyama wa
porini na visawe vya maneno.
Uhusiano na masuala mtambuko
Umoja wa kijamii - unakuzwa wanafunzi wanapofanya kazi katika vikundi.
Stadi za maisha - zinakuzwa katika kujieleza kwa kutumia visawe mbalimbali.
Elimu ya maendeleo endelevu - wanafunzi wanapoendeleza masuala ya ustawi
wa wanyama wa porini wakiwa shuleni na katika maisha yao ya usoni.
Uhusiano na maadili
Umoja, uzalendo na upendo - unakuzwa mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake katika vikundi.
176
Kimeidhinishwa na KICD
Uwajibikaji - unakuzwa mwanafunzi anapotekeleza majukumu yake katika
kikundi vilevile kutunza vifaa anavyotumia katika somo.
Heshima - inakuzwa mwanafunzi anapoweza kuwa na maoni chanya kwake
mwenyewe na wanafunzi wengine bila kujali mahitaji yao tofauti darasani.
Uzalendo - unakuzwa mwanafunzi anapojitolea kuwaheshimu wanafunzi na
walimu ambao ni raia wenzake darasani na anapowatunza wanyama wa porini
kama rasilimali ya nchi yake.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza - somo hili hushirikisha mada ya visawe.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awe kielelezo katika jamii katika kutumia lugha mwafaka na maneno
tofauti kujieleza.
Mwanafunzi pia atakuwa kielelezo kwa jamii anaposhiriki katika vilabu vya kuwatunza
wanyama wa porini.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
visawe vya
maneno mawili
na kubadilisha
kisawe kimoja
na kingine
ifaavyo katika
sentensi.
Mwanafunzi
anatambua
visawe vya
maneno mawili,
anabadilisha
kisawe kimoja
na kingine
ifaavyo katika
sentensi kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
visawe vya
maneno mawili,
anabadilisha
kisawe kimoja
na kingine
ifaavyo katika
sentensi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
visawe vya
maneno mawili,
anabadilisha
kisawe kimoja
na kingine
ifaavyo katika
sentensi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
visawe vya
maneno mawili.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema au kusikia, watambue visawe vya maneno
mawili kwa kukoleza maneno hayo rangi kwenye tarakilishi.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watumie breli au kusikiliza maelezo ya
visawe vya maneno mawili vikisomwa na mwalimu, wanafunzi wenzao au kanda
iliyorekodiwa.
Wanafunzi wanaoelewa kwa haraka wapewe mazoezi zaidi ili kujiimarisha kabisa.
Wale wanaochukua muda kuelewa wapewe muda zaidi pamoja na mwalimu
kuwaelekeza.
177
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya jumla
Mada ndogo ya visawe vya maneno mawili inamwezesha mwanafunzi kutambua neno
la kutumia badala ya jingine na kuboresha mawasiliano yake katika jamii anapotumia
maneno tofauti ifaavyo kujieleza.
Mwalimu anaweza kuwaandalia wanafunzi ziara ya kuzuru mbuga ya wanyama wa
porini ili watazame wanyama wenye majina zaidi ya moja. Pia, ili kujifunza zaidi
kuhusu wanyama wa porini ili kufaulisha mada hii.
Mwalimu awe na vifaa halisi au picha za vitu atakavyotumia kuwaongoza wanafunzi
kupata visawe vyake ili kuwawezesha kuwa na kumbukumbu ya wanayojifunza.
Kipindi cha 1: Visawe vya maneno mawili
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 127)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kisawe ili kukibainisha.
b) Kutambua visawe vya maneno mawili katika kundi la maneno.
Swali dadisi
Unajua maneno gani ya Kiswahili yaliyo na maana sawa?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Visawe ni maneno mawili au zaidi yanayotumiwa kutajia kitu kimoja. Mwanafunzi
anapotambua visawe vya maneno ataweza kujieleza kwa kutumia maneno tofauti
ifaavyo. Pia, ataboresha mawasiliano katika jamii.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 127,
2. Video yenye vitu na wanyama wenye majina zaidi ya moja,
3. Chati yenye vitu na wanyama wenye majina zaidi ya moja,
4. Tarakilishi na projekta, 5. Breli, 6. Kamusi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwagawa katika
vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao. Wanafunzi watazame michoro iliyo katika
kitabu chao na wataje majina ya michoro hiyo. Mwalimu awaulize wanafunzi waeleze
iwapo wanajua jina jingine la kila mchoro waliotazama.
Majibu tarajiwa: runinga/televisheni, ndovu/tembo, kinyonga/lumbwi, mbogo/nyati.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili ambapo watatazama video
178
Kimeidhinishwa na KICD
atakayowaonyesha darasani. Awaulize wataje wanyama au vitu walivyotazama vyenye
majina zaidi ya moja. Ikiwa mwalimu hataweza kuandaa video, anaweza kutumia chati
yenye michoro au picha za vitu vyenye majina zaidi ya moja zilizopigwa kwa kutumia
kamera.
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa majina mawili au zaidi yanayotumiwa kutajia kitu
kimoja huitwa visawe. Umoja wake ni kisawe.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi kutafuta visawe vya maneno
yaliyo kitabuni mwao kwa kutumia kamusi au mtandao.
Majibu tarajiwa: a) tumbili/ngedere b) bendera/beramu ch) asali/uki d) ngiri/nguruwe-
mwitu e) baba/abu f) mama/nina g) mke/bibi h) sare/yunifomu i) kilimo/zaraa.
Mwalimu awaulize wanafunzi watunge sentensi sahihi wakitumia visawe walivyotafuta.
Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi.
Mwalimu amwelekeze kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada kwa kutunga kifungu cha
aya moja akitumia majina ya wanyamapori mbalimbali. Baadaye, mwanafunzi aandike
upya kifungu hicho akitumia visawe vya majina ya wanyamapori aliotaja katika swali
la 1.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo:
1. Mwanafunzi anaweza kutaja visawe mbalimbali.
2. Mwanafunzi anaweza kutumia visawe kutunga sentensi na kifungu kwa
usahihi.
Kipindi cha 2: Visawe vya maneno mawili
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 128)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia visawe vya kiwango chake katika mawasiliano.
b) Kufahamu matumizi ya visawe katika mawasiliano.
Swali dadisi
Unajua maneno gani ya Kiswahili yaliyo na maana sawa?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapoweza kutumia visawe vya kiwango chake katika sentensi ataboresha
mawasiliano. Mwalimu asome kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi ili kufahamu
zaidi mambo yaliyoshughulikiwa na atakavyowashirikisha wanafunzi wake.
179
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Tarakilishi, 3. Kamusi,
4. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 128.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwashirikisha wanafunzi katika shughuli ya
kwanza. Awagawe wanafunzi katika vikundi viwili kisha awaongoze kucheza mchezo
wa kutambua visawe. Azingatie maelezo ya mchezo huo katika kitabu cha mwanafunzi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu amwelekeze mwanafunzi asome maneno yaliyo
kitabuni mwao. Amwagize atafute visawe vya maneno hayo katika mraba waliopewa.
Mwanafunzi aandike visawe hivyo katika daari lake.
Visawe tarajiwa: 1. mbogo 2. tembo 3. lumbwi 4. panda 5. runinga 6. kompyuta 7. bibi
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya tatu kwa kuwaongoza kutafuta
picha za nomino zozote kumi mtandaoni zilizo na visawe. Wanafunzi wafanye shughuli
hii wakiwa katika vikundi. Kila mwanafunzi aandike majina hayo pamoja na visawe
vyake katika daari lake. Wanafunzi watambue visawe vya maneno mawili pekee.
Katika zoezi la ziada, mwalimu amwelekeze mwanafunzi aandike sifa za wanyama
watano wa porini. Mwanafunzi anaweza kutumia mtandao. Mwalimu anaweza kubuni
shughuli tofauti ya ziada na kumwuliza mwanafunzi amhusishe mlezi au mzazi wake.
Tathmini
Mwalimu atathmini iwapo:
1. Mwanafunzi anaweza kutambua na kutaja visawe mbalimbali.
2. Mwanafunzi anaweza kutafuta picha za nomino zilizo na visawe mtandaoni.
B. Kusoma: Kusoma kwa ufahamu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 129)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya mchezo wa kuigiza, mhusika na maelekezo.
b) Kutambua mchezo wa kuigiza katika matini.
ch) Kutambua wahusika na maelekezo katika mchezo mfupi wa kuigiza.
d) Kusoma mchezo mfupi wa kuigiza kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
e) Kuigiza mchezo mfupi kwa kutumia maelekezo.
180
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Je, mhusika katika mchezo wa kuigiza ni nani?
2. Je, maelekezo katika mchezo wa kuigiza ni nini?
3. Je, unapata vipi ujumbe katika mchezo wa kuigiza?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika kazi
za vikundi.
Uwazaji wa kina - unakuzwa mwanafunzi anapongamua ujumbe ulio kwenye
mchezo wa kuigiza.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika kusoma na kuigiza
mchezo.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali kama
nyenzo za kufanikisha mada.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya maendeleo endelevu - mwanafunzi anapopata maarifa kuhusu utunzaji
wa wanyama wa porini.
Uhusiano na maadili
Umoja, uzalendo na upendo - unakuzwa mwanafunzi anaposhirikiana na
wenzake katika vikundi.
Uwajibikaji - unakuzwa mwanafunzi anapotekeleza majukumu yake katika
kikundi na kutunza vifaa anavyotumia katika ujifunzaji.
Heshima - heshima kwa wanyamapori na kuendeleza shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia michezo ya
kuigiza.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake kuhusu umuhimu wa kutunza wanyamapori
na ujenzi wa vipawa hasa katika uigizaji.
181
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kueleza na
kutumia
msamiati
lengwa katika
tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza
msamiati
lengwa na
kuutumia
katika tungo
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza
msamiati
lengwa na
kuutumia katika
tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza baadhi
ya msamiati
lengwa na
kuutumia katika
tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu kueleza
msamiati lengwa.
Kusoma kifungu
kwa ufasaha na
kwa kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma
kifungu kwa
ufasaha na
wepesi kwa
kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma
kifungu kwa
ufasaha na
kwa kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anasoma
kifungu kwa
kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anajaribu
kusoma kifungu.
Kujibu maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajibu maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anajibu maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajibu baadhi
ya maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kujibu maswali
yanayolenga
ujumbe, matukio
na wahusika
katika kifungu.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia, wasome maelezo ya mchezo wa kuigiza
kwenye kiwambo cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli au wasikilize maelezo ya
mchezo wa kuigiza, wahusika na maelekezo yakisomwa na mwalimu, wanafunzi
wenzao au kanda iliyorekodiwa.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuzungumza, wajibu maswali kwa kuandika
madaarini au kwa kutumia lugha ishara ikiwa mwalimu anaifahamu.
Maelezo ya jumla
Mada hii itamwezesha mwanafunzi kukuza umilisi wa kutunza mazingira hasa misitu
anapotambua wanyamapori hutegemea misitu. Pia, itakuza mtazamo chanya kuhusu
utunzaji wa wanyamapori. Mwanafunzi anaposoma kifungu cha mchezo wa kuigiza
182
Kimeidhinishwa na KICD
ataboresha usomaji wake. Mwalimu asisitize uzingatiaji wa mbinu bora za usomaji
wanafunzi wanaposoma kifungu. Ikiwa kuna mwanafunzi anayejitenga na wenzake
hasa katika vikundi, mwalimu awasiliane naye ili kujua sababu kwa madhumuni ya
kumpa ushauri unaomfaa ili ajithamini na kuchangamkia masomo.
Kipindi cha 1: Mchezo mfupi wa kuigiza
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa, 129)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya mchezo wa kuigiza, mhusika na maelekezo.
b) Kutambua mchezo wa kuigiza katika matini.
Maswali dadisi
1. Je, mhusika katika mchezo wa kuigiza ni nani?
2. Je, maelekezo katika mchezo wa kuigiza ni nini?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mada ndogo ya mchezo wa kuigiza inakuza kipawa cha mwanafunzi katika uigizaji.
Mwanafunzi anapojua kuandika mchezo wa kuigiza au kuigiza yeye mwenyewe
atakuwa amekuza maendeleo yake binafsi na kumwezesha kukimu maslahi yake
maishani. Mwalimu awatayarishe wanafunzi ambao wataigiza mchezo mfupi darasani
kabla ya kipindi ili wafahamu jinsi ya kushiriki. Mwalimu aandae video ambazo
atatumia darasani kabla ya kipindi ili kufaulisha kipindi.
Mwalimu ampe kila mwanafunzi nafasi ya kujieleza akiwa binafsi na katika vikundi ili
kukuza usawa wa kijamii na uwajibikaji.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kanda yenye video ya mchezo wa kuigiza, 3. Tarakilishi na projekta,
2. Breli, 4. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 129.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwaagiza
wanafunzi wawili waigize mazungumzo kuhusu wanyama wowote wa porini darasani.
Wanafunzi wengine watazame na wasikilize mazungumzo hayo kwa makini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua maana ya wahusika (mhusika) na
maelekezo katika mchezo wa kuigiza. Majibu tarajiwa: watu wanaoshiriki katika
mazungumzo huitwa wahusika. Kando na kuzungumza, wahusika hutenda vitendo
vingine kwa ishara ambavyo huitwa maelekezo.
183
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi watazame video ambazo
atawaonyesha kwenye runinga au tarakilishi. Wanafunzi wajadili matendo katika
video hiyo. Mwalimu ahakikishe anaandaa video yoyote nzuri ya mchezo wa kuigiza
ili wanafunzi wajifunze kuhusu wahusika na maelekezo. Baadaye, mwalimu awaagize
wanafunzi waigize vitendo walivyotazama kwenye video husika.
Mwalimu amwongoze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kubuni mazungumzo
kati yake na rafiki yake kuhusu faida za wanyamapori. Mwanafunzi ayaandike
mazungumzo hayo kwenye tarakilishi kisha awatumie wanafunzi wenzake pamoja na
mwalimu mtandaoni ili wayatathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi amefahamu maana ya mchezo wa
kuigiza, wahusika na maelekezo.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kubuni mazungumzo yaliyo
mfano wa mchezo wa kuigiza.
Kipindi cha 2: Mchezo mfupi wa kuigiza
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 131)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua wahusika na maelekezo katika mchezo mfupi wa kuigiza.
b) Kusoma mchezo mfupi wa kuigiza kwa ufasaha kwa kuzingatia ujumbe.
Swali dadisi
Je, maelekezo katika mchezo wa kuigiza ni nini?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu ahakikishe anawagawa wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi
na mahitaji yao. Wanafunzi wenye mahitaji spesheli kama wale wasio na uwezo
wa kusimama wanaweza kuteuliwa kuwa viongozi wa vikundi ili wanapotekeleza
majukumu yao wajiamini na kujithamini zaidi.
Mwalimu ateue nyenzo za ujifunzaji akizingatia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
ili kufaulisha matokeo tarajiwa katika kipindi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 131, 3. Kamusi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza wakiwa katika vikundi.
184
Kimeidhinishwa na KICD
Awaongoze kutazama na kujadili mchoro ulio kitabuni mwao. Awaulize wanafunzi
wataje majina ya wanyama wanaowaona kwenye mchoro husika. Waelezane iwapo
wamewahi kuwaona wanyama hao na walikowaona.
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi viwili. Awahusishe katika shughuli ya
pili kwa kukipa kila kikundi nafasi ya mhusika katika mchezo wa kuigiza ulio kitabuni
mwao. Wanafunzi wasome mchezo huo wa kuigiza. Baadaye, mwalimu awaongoze
wanafunzi kujibu maswali waliyopewa baada ya mchoro huo.
Majibu tarajiwa: 1. Wahusika katika mchezo huu ni: Mwalimu, Mwanaisha, Rukia,
Pendo, Tamara, Wanjala, Mohammed, Yona, Amani, Baraka.
2. Ujumbe uliojitokeza katika mchezo wa kuigiza ni maelezo kuhusu majina, tabia
na sura za wanyama mbalimbali wa porini.
3. Wanyama waliotajwa ni: chui, mbogo/nyati, kifaru, nguruwe-mwitu/ngiri.
4. Alirekodi wanyama hao kwa kutumia kamera alipozuru mbuga ya wanyama
akiwa na wazazi wake.
5. Baadhi ya mambo ya kuzingatia: kutunza misitu ili wapate chakula, kutowaua,
kutunza vianzo vya maji, kuwatibu n.k.
Katika kazi ya ziada, mwalimu amwulize kila mwanafunzi arejelee mchezo wowote
wa kuigiza ambao amewahi kuutazama kwenye runinga kisha ataje wahusika katika
mchezo huo. Pia, awaeleze wenzake darasani mafunzo aliyopata kutokana na mchezo
huo. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuchambua mchezo wa
kuigiza.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kubuni mchezo wa kuigiza.
Kipindi cha 3: Mchezo mfupi wa kuigiza
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 133)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuigiza mchezo mfupi kwa kutumia maelekezo.
b) Kusoma michezo ya kuigiza.
Swali dadisi
Je, unapata vipi ujumbe katika mchezo wa kuigiza?
185
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi na kila kikundi kiwe na wanafunzi
wenye mahitaji mbalimbali na jinsia tofauti ikiwa shule ina wanafunzi wa jinsia ya
kike na kiume. Wanafunzi wenyewe wachague kiongozi wao katika kila kikundi.
Mwalimu asome kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi hiki ili kuyafahamu mambo
yatakayoshughulikiwa.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 133, 2. Breli,
3. Kanda iliyorekodiwa yenye mchezo mfupi wa kuigiza.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwagawa katika
vikundi kisha awasomee maelekezo ya mchezo wa kuigiza. Kila kikundi kiigize mchezo
mfupi kikizingatia maelekezo ya mwalimu. Mwalimu awaeleze wanafunzi wabuni
maneno yao wenyewe yatakayotumiwa na kila mhusika. Awaeleze kuwa sharti mchezo
wao wa kuigiza uwe na ujumbe, mtiririko mwema wa mawazo na lugha sahihi. Kila
kikundi kiigize mchezo wao kwa zamu wenzao wakiwatazama na kuwasikiliza.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kujadili ujumbe uliojitokeza
katika mchezo wa kuigiza ambao waliigiza katika vikundi katika shughuli ya kwanza.
Awaulize wanafunzi katika vikundi vyao wataje wahusika wa mchezo wao kisha
wajadili tabia za wahusika hao.
Mwalimu amwagize kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada kwa kutumia mtandao
kutafuta picha za wanyama wowote watatu wa porini. Awachore wanyama hao katika
daari lake kisha awapake rangi. Hatimaye, aandike majina ya watoto wa wanyama hao
na kueleza vyakula vyao. Mwanafunzi awaonyeshe wenzake michoro yake darasani
katika kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo wanafunzi wanaweza kuigiza mchezo mfupi kwa
ukakamavu kulingana na maelekezo aliyowasomea.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuwachora wanyamapori na
kutaja majina ya watoto wao.
CH. Kuandika: Kuandika Insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 133)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
186
Kimeidhinishwa na KICD
b) Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
Maswali dadisi
1. Insha ya masimulizi inahusu nini?
2. Je, unazingatia nini ili kuandika insha nzuri ya masimulizi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika kazi
za vikundi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya masimulizi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali kama
nyenzo za kufanikisha ujifunzaji.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi anapotunza vifaa vya ujifunzaji.
Kujiamini na kujithamini kunakuzwa mwanafunzi anapoweza kubuni na
kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja.
Utunzaji wa wanyamapori.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu mwanafunzi anapotumia lugha ya heshima kujadiliana na
wenzake katika vikundi.
Umoja, uzalendo na upendo - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi na kuthamini maoni yao hata yanapokuwa tofauti na yake.
Uwajibikaji - mwanafunzi anapotekeleza majukumu yake katika kikundi na
kutunza vifaa anavyotumia.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia uandishi kama
mojawapo ya stadi za lugha.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atawahamasisha wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi bora katika mawasiliano pamoja na umuhimu wa kuwatunza wanyamapori.
187
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo na
ubunifu wa hali
ya juu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
baadhi ya
kanuni za lugha.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika insha
ya masimulizi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, wasome maelezo ya insha ya masimulizi kwa
kutumia breli.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuzungumza, wajibu maswali kwa kuandika daarini
au kwenye tarakilishi.
Wanafunzi wasioweza kusema au kusikia, watumie lugha ishara kueleza kuhusu
insha ya masimulizi. Pia, wajibu maswali dadisi kwa kuandika madaarini au
kwenye tarakilishi. Mwalimu aandike maelezo ya insha ya masimulizi ubaoni au
kwenye chati ili waweze kuyasoma.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuandika kwa kutumia mikono wahimizwe kutumia
kiungo kingine kama vile mguu ama midomo kushika kalamu na kuandika. Wapewe
muda zaidi. Mwalimu awahamasishe wanafunzi wengine kuhusu umuhimu wa
kumkubali mtu bila kujali mahitaji yake. Kufanya hivyo, kutazuia unyanyapaa kwa
wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali.
Maelezo ya jumla
Kuandika insha ya masimulizi kutamsaidia mwanafunzi kukuza stadi ya kuandika na
kuimarisha mawasiliano andishi shuleni na katika jamii. Pia, kutakuza ubunifu wake
na kumwezesha kutatua changamoto zinazomkabili shuleni na katika jamii.
Ikiwa mwanafunzi ataweza kuimarika katika stadi ya kusikiliza, kuzungumza na
kusoma ataweza kuimarisha stadi ya kuandika upesi.
Kipindi cha 1: Insha ya masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 133)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
188
Kimeidhinishwa na KICD
Swali dadisi
Insha ya masimulizi inahusu nini?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome kitabu cha mwanafunzi ili kufahamu shughuli za kipindi hiki na
kuweza kuteua nyenzo zinazofaa. Wanafunzi wawe na vifaa vya kuandikia kabla ya
kuanza kujifunza. Mwalimu apongeze maoni ya kila mwanafunzi kuhusu vidokezo
vya insha ili aweze kujithamini katika ubunifu na kuchangamkia uandishi wa insha.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Tarakilishi/tabuleti,
3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 133, 4. Vinyago vya wanyama wa porini.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu amshirikishe mwanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kumwuliza
amsimulie mwanafunzi mwenzake kuhusu likizo ya Disemba kwa kujibu maswali 1-5
yaliyo kitabuni mwao.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kutazama na kujadili
matukio yanayoendelea katika michoro iliyo kitabuni mwao wakiwa katika vikundi.
Mwanafunzi aeleze iwapo amewahi kuwaona wanyama walio katika michoro hiyo na
alikowaona. Ataje majina ya wanyama hao. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua
muundo wa kuandika insha ya masimulizi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi kusoma mfano wa insha
ya masimulizi ulio kitabuni mwao kisha wajibu maswali waliyopewa wakiwa katika
vikundi.
Majibu tarajiwa: 1. Wanafunzi walibeba kamera ili kurekodi mambo ambayo
wangejifunza. 2. Pundamilia, twiga, sungura, nyati, swara. 3. Wanyamapori huletea
nchi pesa za kigeni. 4. Wanyama watatoroka. 5. Mwalimu atathmini majibu.
Mwalimu amhimize kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada. Amwombe mlezi au
mzazi wake amsimulie kisa chochote kinachohusu wanyamapori. Awasimulie wenzake
darasani kuhusu kisa hicho katika kipindi kijacho.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kusimulia.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaelewa muundo wa insha ya
masimulizi.
189
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2: Insha ya masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 136)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
b) Kufahamu utunzi mzuri wa insha ya masimulizi ili kujenga ubunifu wake.
Swali dadisi
Je, unazingatia nini ili kuandika insha nzuri ya masimulizi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Uandishi wa insha ya masimulizi utaliwezesha taifa la Kenya kuafikia mojawapo
ya malengo ya taifa ya elimu ya kukuza maendeleo ya mtu binafsi na kujitegemea.
Mwanafunzi ataweza kuandika insha bora na mwishowe kuandika makala mbalimbali
yatakayompamapatomaishani. Maoni ya mwalimu yataje ubora wa insha iliyoandikwa
na mwanafunzi na kumshauri jinsi ya kuiboresha. Kufanya hivyo kutachochea
mwanafunzi kujithamini na kuwa na hamu ya kuandika insha za masimulizi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 2. Tarakilishi, 3. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 136.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwauliza
wasikilize insha atakayowasomea. Asome insha ifuatayo. Pia, anaweza kutunga insha
yake na akawasomea darasani.
Wanyama wa Porini
Sadiki ni mwanafunzi wa gredi ya nne. Siku moja, mwalimu aliwapatia zoezi la
ziada. Alimwagiza kila mwanafunzi kumwomba mzazi au mlezi wake amsimulie kisa
kinachohusu wanyama wa porini. Sadiki alifurahi sana. Alipenda kusikiliza masimulizi.
Alipoka nyumbani jioni hiyo, alimwomba baba yake amsimulie kisa alichoagizwa na
mwalimu wake. Baba alikubali ombi la mwanawe. Waliketi kwenye kochi jekundu
lililokuwa sebuleni akaanza kumsimulia.“Hapo zamani za kale wanyama wa porini
waliishi bila kutunzwa na binadamu. Watu waliwawinda na kuwaua wanyama wa
porini ili kupata ngozi, nyama na pembe. Upande mwingine, wanyama wa porini
waliwashambulia watu na kuwaumiza hadi kuwaua. Mimea ya wakulima iliharibiwa
na hayawani hao.
Siku hizi mambo yamebadilika. Binadamu ni rafiki wa wanyama wa porini. Ni
hatia kuwatesa au kuwaua wanyama wa porini. Wao pia wana haki ya kuishi. Watu
wanawatunza kwa kuwazingira kwa nyua za umeme katika mbuga za wanyama. Askari
hulinda mbuga hizo usiku na mchana ili kuhakikisha wanyama wako salama salimini.
190
Kimeidhinishwa na KICD
Wanyama wa porini wana faida nyingi. Wanyama kama vile ndovu, simba, nyati, chui
na kifaru huwavutia watalii wa humu nchini na ng’ambo.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kujibu maswali ambayo wamepewa kitabuni mwao
kuhusu insha ambayo amewasomea. Mwalimu akubali majibu yoyote sahihi ili
kuwawezesha wanafunzi kuwa wabunifu kutokana na uwazaji wa kina.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi na awaelekeze
watumie mtandao kutafuta mbuga zozote mbili za wanyamapori nchini Kenya.
Awaongoze kujadili kuhusu mahali mbuga hizo zinapatikana na wataje majina ya
baadhi ya wanyama wanaopatikana katika mbuga hizo. Wanafunzi wajadiliane iwapo
wamewahi kuzuru mbuga hizo.
Shughuli ya tatu inahusu kufanya ziara ya mbugani. Mwalimu anashauriwa apange
ziara ya wanafunzi kuzuru mbuga yoyote ya wanyama iliyo karibu na shule yao.
Ziara hii inaweza kufanywa wakati wa wikendi au likizo yoyote. Mwalimu atafiti
kuhusu mbuga hiyo, umbali wake kutoka shuleni mwao, wanyama walioko huko,
usalama wa eneo hilo, usari utakaotumika pamoja na vifaa na pesa zitakazohitajika.
Wakati na baada ya ziara, wanafunzi waelekezwe kuandika majina ya wanyamapori
wanaopatikana katika mbuga hiyo. Pia, wanafunzi waandike insha ya masimulizi
kuhusu ziara hiyo.
Mwalimu amhimize mwanafunzi kufanya kazi ya ziada ambapo ataandika maelezo
kuhusu madhara ya wanyama wa porini kwa watu, mimea na wanyama wenzao.
Aeleze jinsi wanyama wa porini wanavyotunzwa kisha awasomee wenzake maelezo
aliyoandika darasani.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutumia mtandao kujifunza
zaidi kuhusu wanyamapori.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika insha ya masimulizi
akirejelea ziara ya mbugani.
D. Saru:Mnyambulikowavitenzi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 137)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya mnyambuliko wa vitenzi ili kuubainisha.
b) Kueleza maana ya kauli za kutenda, kutendea na kutendwa ili kuzitofautisha.
ch) Kutambua vitenzi katika kauli za kutenda, kutendea na kutendwa katika matini.
d) Kutumia vitenzi katika kauli za kutenda, kutendea na kutendwa ipasavyo
anapowasiliana.
191
Kimeidhinishwa na KICD
Swali dadisi
Je, vitenzi vinaweza kubadilika vipi mwishoni ili kuleta maana mbalimbali?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanapofanya kazi wakiwa
wawili wawili na katika vikundi.
Uwazaji wa kina na utatuzi wa matatizo - unakuzwa wakati ambapo wanafunzi
wananyambua vitenzi katika kauli mbalimbali.
Kujiamini - kunakuzwa wanafunzi wanapotoa majibu na kushiriki katika
shughuli mbalimbali.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wanafunzi wanapotumia vifaa vya kidijitali
kujifunza kuhusu mnyambuliko wa vitenzi mbalimbali.
Uhusiano na masuala mtambuko
Umoja wa jamii wanapofanya kazi pamoja.
Utunzaji wa wanyamapori na mazingira wanapotumia vitenzi vya mnyambuliko
mbalimbali kutunga sentensi.
Uhusiano na maadili
Upendo, umoja, ushirikiano, heshima na uzalendo vinavyojitokeza wanafunzi
wanaposhirikiana katika somo na vilevile katika sentensi zitakazotungwa.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia vitenzi kama
mada muhimu.
Muziki - wanafunzi wanapotunga na kuimba nyimbo kuhusu mnyambuliko wa
vitenzi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji na huduma za jamii
Mwanafunzi awe kielelezo kifaacho cha matumizi ya lugha ifaayo katika kuwasilisha
ujumbe.
192
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua vitenzi
katika kauli za
kutenda, kutendea
na kutendwa,
kuvibadilisha
katika kauli hizi
na kuvitumia
katika sentensi
ifaavyo.
Mwanafunzi
anatambua
vitenzi
katika kauli
za kutenda,
kutendea na
kutendwa,
anavibadilisha
katika kauli hizi
na kuvitumia
katika sentensi
ifaavyo kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
vitenzi
katika kauli
za kutenda,
kutendea na
kutendwa,
anavibadilisha
katika kauli hizi
na kuvitumia
katika sentensi
ifaavyo.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi
ya vitenzi
katika kauli
za kutenda,
kutendea na
kutendwa,
anavibadilisha
katika kauli hizi
na kuvitumia
katika sentensi
ifaavyo.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
vitenzi
katika kauli
za kutenda,
kutendea na
kutendwa.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona mbali, waketi karibu na ubao. Wasioweza
kuona vitu vilivyo karibu nao waketi mbali na ubao ili waweze kuona vitenzi
vitakavyoandikwa na kunyambuliwa ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema watazame vitenzi vya
kutenda, kutendea na kutendwa vikiigizwa darasani, wasome maelezo kuhusu
mnyambuliko wa vitenzi hivyo kwenye ubao, kiwambo cha tarakilishi, kitabu
cha mwanafunzi na kwenye chati.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusimama wahusishwe katika uigizaji wa vitenzi
ambavyo havitawahitaji kusimama.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kutambua vitenzi kwa urahisi wahusishwe katika
shughuli zaidi za ujifunzaji na wapewe muda zaidi wa kujifunza. Wahimizwe kwa
upendo ili wajithamini na kuchangamkia ujifunzaji. Hatua yoyote wanayopiga
katika ujifunzaji itambuliwe na mwalimu ili wawe na hamu ya kujifunza zaidi.
Maelezo ya jumla
Ujifunzaji wa mnyambuliko wa vitenzi hukuza utunzi wa sentensi sahihi na sanifu na
huboresha mawasiliano. Mwanafunzi anapotambua vitenzi katika kauli ya kutenda,
kutendea na kutendwa na kuvitumia ipasavyo katika sentensi itakuwa rahisi kwake
kujifunza mnyambuliko wa vitenzi katika kauli nyingine.
193
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Kauli ya kutenda
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 137)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya mnyambuliko wa vitenzi ili kuubainisha.
b) Kueleza maana ya kauli ya kutenda.
ch) Kutambua na kutumia vitenzi katika kauli ya kutenda anapowasiliana.
Maswali dadisi
1. Je, vitenzi vinaweza kubadilika vipi mwishoni ili kuleta maana mbalimbali?
2. Unafahamu jinsi vitenzi hunyambuliwa katika kauli ya kutenda?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kitendo ni jambo linalofanywa au kutendwa. Mtu anapotaja vitendo katika kauli
mbalimbali huwa anavinyambua. Kutenda ni kufanya jambo. Katika kauli ya kutenda,
mtu hufanya jambo au hutenda kitendo mwenyewe.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 137,
2. Chati yenye vitenzi katika kauli ya kutenda,
3. Kikapu chenye kadi zenye vitenzi katika kauli ya kutenda,
4. Breli, 5. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kuwauliza wacheze
mchezo ulio kitabuni mwao. Afuate maagizo yaliyo katika kitabu hicho kuwaelekeza
wanafunzi. Wanafunzi waandike sentensi katika madaari yao kwa kutumia kila
kitenzi walichoigiza.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaagize wanafunzi watazame michoro iliyo
kitabuni mwao kisha waeleze vitendo vya wanyama katika michoro hiyo. Mwanafunzi
aandike sentensi moja kuhusu kila kitendo kinachotendwa na wanyama hao.
Majibu tarajiwa: Nyati anakula nyasi, nyani amesimama, simba amelala.
Mwalimu amwongoze kila mwanafunzi kutunga sentensi sahihi kwa kila mchoro
kueleza kitendo kinachotendeka katika kauli ya kutenda.
Mwalimu awahusishe wanafunzi wakiwa katika vikundi katika shughuli ya tatu
kwa kuwaonyesha kadi kumi zilizoandikwa vitenzi vya kauli ya kutenda. Awaambie
waandike sentensi sahihi kwa kila kitenzi na kuwasomea wenzao ili wazisikilize na
kuziboresha.
194
Kimeidhinishwa na KICD
Katika kazi ya ziada, mwalimu amwulize mwanafunzi amwombe mlezi au mzazi wake
atende vitendo kumi mbalimbali. Mwanafunzi atunge sentensi akitumia kila kitendo
ambacho mlezi au mzazi atatenda. Mwanafunzi aandike sentensi hizo katika daari
lake na apigie mstari vitenzi vya kauli ya kutenda.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua vitenzi katika kauli
ya kutenda.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutunga sentensi sahihi
katika kauli ya kutenda.
Kipindi cha 2: Kauli ya kutendea
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 139)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kauli ya kutendea ili kuibainisha.
b) Kutambua vitenzi katika kauli ya kutendea.
ch) Kutumia vitenzi katika kauli ya kutendea ipasavyo kuwasiliana.
Maswali dadisi
1. Ni nini maana ya kauli ya kutendea?
2. Je, unaweza kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendea?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kutendea ni kauli ya kufanyia. Katika kauli hii, mtu mwingine hupokea kitendo
kilichofanywa na mtu wa kwanza. Mwanafunzi anapoweza kutambua vitenzi katika
kauli ya kutendea, kuvibainisha na kuvitumia kutunga sentensi sahihi huboresha
mawasiliano yake.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 3. Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 139,
2. Chati yenye vitenzi katika kauli ya kutendea, 4. Kamusi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi waeleze
walichojifunza katika kipindi kilichotangulia.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaulize wanafunzi wawili wawili wasome
sentensi zilizo vitabuni mwao na wajadili jibu sahihi kwa kila sentensi.
195
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu tarajiwa:
1. Nilimsomea mwenzangu sentensi. 2. Kaka alimpikia mpishi. 3. Nitamfulia dada
nguo. 4. Nitamwandikia nyanya barua.
Mwalimu amshirikishe mwanafunzi katika shughuli ya pili kwa kumwuliza
mwenzake vitendo ambavyo angependa amfanyie. Mwanafunzi huyo amtendee vitendo
atakavyoambiwa. Mwenzake atunge sentensi akitumia kila kitendo alichotendewa.
Mwalimu awaulize wanafunzi wawasomee wenzao sentensi ambazo wametunga
ili wazitathmini.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi kusoma kifungu kilicho
kitabuni mwao kwa sauti. Watambue na kuandika katika madaari yao vitenzi vilivyo
katika kauli ya kutendea kutoka kwenye kifungu hicho.
Majibu tarajiwa: nilimpikia, alimfulia, alimpigia, alimhurumia, walimwandikia,
alimpigia, aliyompatia.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi watunge sentensi sahihi kwa kutumia vitenzi vya
kauli ya kutendea walivyotambua kwenye kifungu walichosoma.
Mwalimu amwulize kila mwanafunzi afanye kazi ya ziada ambapo atapigia mistari
vitenzi vya kauli ya kutendea katika sentensi alizopewa kitabuni mwao. Amwagize
aandike vitenzi alivyopigia mstari katika kauli ya kutenda. Awaonyeshe wenzake
darasani. Majibu tarajiwa: a) alimwimbia b) ulimtembelea ch) atanifungia
d) alinisimulia e) watawakariria. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi kuhusu
namna walivyoandika vitenzi vya kauli ya kutendea katika kauli ya kutenda.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua vitenzi vya kauli ya
kutendea katika sentensi au kifungu.
2. Mwalimu atathmini ikiwa mwanafunzi anaweza kubadilisha vitenzi vya kauli
ya kutendea kuwa katika kauli ya kutenda.
Kipindi cha 3: Kauli ya kutendwa
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 140)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kauli ya kutendwa ili kuibainisha.
b) Kutambua vitenzi katika kauli ya kutendwa.
ch) Kutumia vitenzi katika kauli ya kutendwa ipasavyo kuwasiliana.
Maswali dadisi
1. Ni nini maana ya kauli ya kutendwa?
2. Je, unaweza kunyambua vitenzi katika kauli ya kutendwa?
196
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Kutendwa ni kauli ambayo huonyesha mtu au kitu kimefanywa kitendo fulani.
Mwanafunzi akiweza kutambua vitenzi katika kauli ya kutendwa na kuvitumia kwa
usahihi katika sentensi ataimarisha mawasiliano yake.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Breli, 3. Chati yenye vitenzi katika kauli ya kutendwa,
2. Tarakilishi, 4. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 140.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu amshirikishe mwanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kumwuliza
avitende vitu vitendo kisha amwulize mwenzake aseme vitu hivyo vimetendwa nini.
Atumie mifano 1-4 iliyo kitabuni mwao. Awaelekeze wanafunzi kutambua kuwa
kutendwa ni kauli inayoonyesha mtu au kitu kimefanywa kitendo fulani.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kusoma sentensi zenye
vitenzi vya kauli ya kutendwa wakiwa katika vikundi. Wapigie mistari vitenzi katika
kauli ya kutendwa kisha wavibadilishe vitenzi walivyopigia mstari viwe katika kauli ya
kutenda na kutendea.
Mwalimu amwongoze mwanafunzi kufanya shughuli ya tatu ambapo ataandika
sentensi tano zenye vitenzi vya kauli ya kutendwa. Mwanafunzi aandike sentensi hizo
kwenye tarakilishi. Awatumie wenzake sentensi hizo mtandaoni ili wazibadilishe ziwe
katika kauli ya kutenda. Wanafunzi wasome sentensi hizo darasani ili wazitathmini.
Mwalimu amhimize mwanafunzi afanye kazi ya ziada kwa kujaza nafasi zilizo kwenye
jedwali walilopewa kwa mnyambuliko sahihi wa kila kitenzi. Mwalimu atathmini
sentensi ambazo wanafunzi wametunga kwa kutumia vitenzi walivyojaza katika
jedwali.
Majibu tarajiwa:
Tenda Tende a Tendwa
1. lima limia limwa
2. tunza tunzia tunzwa
3. beba bebea bebwa
4. imba imbia imbwa
5. shona shonea shonwa
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua vitenzi katika kauli
ya kutenda, kutendea na kutendwa.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutunga sentensi sahihi
akitumia vitenzi katika kauli ya kutenda, kutendea na kutendwa.
197
Kimeidhinishwa na KICD
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaandika kisawe sahihi cha barua ambacho ni
waraka. Pia, aandike kisawe sahihi cha neno mama ambacho ni nina.
2. Mwanafunzi aandike kisawe sahihi cha neno tembo ambacho katika muktadha huu
ni ndovu.
3. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Ahakikishe mwanafunzi anaeleza
kuhusu maana ya wahusika katika muktadha wa mchezo wa kuigiza. Wahusika ni
viumbe ambao hushiriki katika mazungumzo katika mchezo wa kuigiza.
4. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaandika insha ya maelezo kwa kuzingatia
muundo unaofaa. Insha hiyo ihusu mnyama yeyote wa porini ambaye mwanafunzi
anapenda. Mwalimu ahakikishe kuwa mwanafunzi anaandaa vidokezo ambavyo
atatumia kuandika insha hiyo.
5. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Ahakikishe mwanafunzi ameeleza sifa
za wanyamapori watano wakubwa. Mwanafunzi atumie mtandao kutazama picha
za wanyama hao. Iwapo mwanafunzi hana uwezo wa kupata mtandao, anaweza
kupewa picha za wanyama hao akazitazama kisha akaandika sifa zao.
6. Mwalimu atathmini jibu litakalotolewa na mwanafunzi. Jibu sahihi lionyeshe
kitenzi kilichonyambuliwa katika kauli ya kutendwa. Jibu ni: Wanyama wa porini
wanalindwa na wananchi.
7. Mwalimu atathmini jibu litakalotolewa na mwanafunzi. Jibu sahihi lionyeshe kitenzi
kilichonyambuliwa katika kauli ya kutendwa. Jibu ni: Vyombo vyote vilioshwa na
mama.
8. Mwalimu atathmini sentensi ambayo mwanafunzi atatunga akitumia jina la mnyama
alilopewa. Sentensi atakayotunga iwe katika kauli ya kutenda. Mfano: Swara
anakimbia mbio.
9. Mwalimu atathmini sentensi ambayo mwanafunzi atatunga akitumia jina la
mnyama alilopewa. Sentensi atakayotunga iwe katika kauli ya kutenda. Mfano:
Chui anakula nyama.
10. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi atatunga. Ahakikishe sentensi
hizo ziko katika kauli ya kutendwa. Mifano:
a) Wanyamapori hawa hulindwa usiku.
b) Simba yule anatunzwa vizuri.
198
Kimeidhinishwa na KICD
AFYA BORA
9
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 143)
A. Kusikiliza na Kuzungumza: Mazungumzo
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua miktadha ya mawasiliano isiyo rasmi.
b) Kutumia lugha ipasavyo katika miktadha isiyo rasmi.
Swali dadisi
Ni lini tunatumia lugha isiyo rasmi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa kupitia kwa kushiriki katika kazi ya
vikundi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika mazungumzo.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kidijitali
kusikiliza na kutazama mazungumzo.
Uhusiano na masuala mtambuko
Mazungumzo yahusishe masuala mtambuko kama vile lishe bora na mazingira.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji katika kutunza vifaa vya kidijitali.
Heshima na ushirikiano katika uigizaji na kushiriki katika mazungumzo.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia
matumizi ya lugha katika miktadha mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awe kielelezo cha wengine katika kutumia lugha kwa heshima na ufasaha
katika miktadha isiyo rasmi.
199
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua lugha
isiyo rasmi na
kuitumia kuleta
utangamano,
kuheshimu
maoni ya
wengine na
kushiriki
mazungumzo
na wenzake.
Mwanafunzi
anatambua
lugha isiyo
rasmi na
kuitumia kwa
urahisi kuleta
utangamano,
anaheshimu
maoni ya
wengine na
kushiriki
mazungumzo
na mwenzake.
Mwanafunzi
anatambua
lugha isiyo
rasmi na
kuitumia kuleta
utangamano,
anaheshimu
maoni ya
wengine na
kushiriki
mazungumzo
na wenzake.
Mwanafunzi
anatambua kwa
kiasi, lugha
isiyo rasmi na
kuitumia katika
mazungumzo
na wenzake.
Mwanafunzi
anatumia
lugha katika
mazungumzo.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli kusoma mazungumzo
mbalimbali ya miktadha isiyo rasmi. Pia, wanafunziwengine wanaweza kuwasaidia
kusoma mazungumzo hayo wakisikiliza.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia, wasome mazungumzo yaliyoandikwa
kwenye kiwambo cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi, chati au ubaoni.
Wanafunzi wenye mahitaji ya kisaikolojia yanayochangia kutozingatia kanuni
bora za kuzungumza, wapewe mazoezi ya kutosha ili kuboresha uwezo wao wa
kuzungumza. Pia, changamoto wanazopitia zinaweza kushughulikiwa na wakuu
shuleni na katika jamii.
Maelezo ya jumla
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuwa mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi
hutokea katika mazingira mbalimbali. Mifano ya mazungumzo katika miktadha isiyo
rasmi inaweza kupatikana kwenye matini mtandaoni.
Kipindi cha 1: Mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 143)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua miktadha ya mawasiliano isiyo rasmi.
b) Kutumia lugha ipasavyo katika miktadha isiyo rasmi.
200
Kimeidhinishwa na KICD
Swali dadisi
Ni lini na wapi tunatumia lugha isiyo rasmi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mazungumzo huwa ya aina mbili. Kuna mazungumzo rasmi na mazungumzo yasiyo
rasmi. Mazungumzo hutegemea wanaozungumza. Mazungumzo rasmi ni kama vile:
mazungumzo kati ya mwalimu na mwanafunzi, mwalimu mkuu na mzazi, mwajiri na
mwajiriwa n.k. Mazungumzo yasiyo rasmi ni kama vile: kati ya mtoto na wenzake,
mtoto na wazazi, ndugu na ndugu, nyanya na babu na wajukuu nyumbani. Mwalimu
awaeleze wanafunzi umuhimu wa nidhamu ya lugha wakati wa mazungumzo kwa
mfano lugha ya upole, heshima na kumpa mwenzake nafasi ya kuzungumza na
kusikiliza kwa makini.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kanda ya video, 3. Breli,
2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 143, 4. Tarakilishi/runinga.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa swali dadisi. Katika shughuli ya
kwanza, mwalimu awateue wanafunzi wawili waigize mbele ya darasa mazungumzo
yao wakiwa uwanjani. Wengine wasikilize kisha mwalimu awaongoze kujadiliana
kuhusu lugha iliyotumika. Mwalimu awateue wanafunzi wengine wawili waigize
mazungumzo yao wakiwa nyumbani. Kikundi cha tatu kiigize mazungumzo kati ya
mwalimu na mwanafunzi. Wanafunzi wajadiliane kuhusu lugha yao.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaonyeshe wanafunzi video mbili. Video ya
kwanza ihusu mazungumzo rasmi na video ya pili ihusu mazungumzo yasiyo rasmi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kujadili tofauti za lugha zilizotumika katika video
hizo. Wanafunzi wataje baadhi ya maneno ambayo yametumika. Mwalimu awaelekeze
wanafunzi kutambua umuhimu wa kutumia lugha ya nidhamu katika mazungumzo
yao katika miktadha isiyo rasmi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Wanafunzi waandike mifano
ya mahali ambapo mazungumzo yasiyo rasmi hutokea. Mwanafunzi abuni na kuandika
katika daari lake mazungumzo kati yake na raki yake aliyekutana naye barabarani.
Mwanafunzi amsomee mlezi au mzazi wake mazungumzo hayo ili ayatathmini. Pia,
awasomee wenzake darasani ili wayasikilize na kuyatathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuigiza mazungumzo katika
muktadha usio rasmi.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutofautisha lugha
inayotumiwa katika mazungumzo katika muktadha rasmi na muktadha usio
rasmi.
201
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2: Mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 144)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia lugha ipasavyo katika miktadha isiyo rasmi.
b) Kufahamu matumizi ya lugha katika miktadha isiyo rasmi.
Swali dadisi
Ni maneno gani hutumika wakati wa mazungumzo yasiyo rasmi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awasaidie wanafunzi kuelewa kwamba lugha inayotumika wakati
wa mazungumzo katika miktadha isiyo rasmi ni tofauti na inayotumika wakati wa
mazungumzo rasmi.
Pia, mwalimu afanye utafiti wa vyakula mbalimbali kama vile vyakula vya protini,
vyakula vya wanga na vyakula vya vitamini. Mwisho, mwalimu afanye utati kuhusu
magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na ukosefu wa vyakula mbalimbali.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 144, 2. Breli, 3. Vyakula halisi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaelekeze wanafunzi wasome mazungumzo yaliyo katika shughuli ya
kwanza kitabuni mwao. Matamshi sahihi yazingatiwe. Wanafunzi wajibu maswali
yaliyo kitabuni mwao. Pia, watathmini iwapo mazungumzo hayo ni rasmi au si rasmi.
Mwalimu atathmini majibu yao.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaelekeze wanafunzi kujadiliana wakiwa wawili
wawili kuhusu vyakula mbalimbali vya asubuhi, mchana na jioni. Wanafunzi waelezane
wao hula vyakula vipi wakati wa asubuhi, mchana na jioni. Mwalimu atathmini majibu
yao.
Mwalimu amhimize mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Wanafunzi wajibu maswali
kuhusu magonjwa mbalimbali yaliyotajwa kitabuni mwao. Mwalimu atathmini majibu
ya wanafunzi na kuyakubali kulingana na mahitaji ya maswali.
Majibu tarajiwa: 1. Maini, mboga, mayai, nyama, maharagwe, njugu n.k. 2. Karoti,
viazi vitamu, mboga, maini n.k. 3. Kwashakoo 4. Ili kuzuia maradhi mwilini, kupata
nguvu za kufanya kazi, kusaidia mwili kukua n.k.
202
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutofautisha mazungumzo
rasmi na mazungumzo ambayo si rasmi.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anajua umuhimu wa vyakula
mbalimbali mwilini.
3. Mwalimu atathmini iwapo wanafunzi wanafahamu magonjwa mbalimbali
ambayo husababishwa na ukosefu wa vyakula mbalimbali.
B. Kusoma: Kusoma kwa mapana
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 146)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini ya kusoma ya aina mbalimbali na kuchagua zinazomvutia.
b) Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
Maswali dadisi
1. Kwa nini unapenda kusoma?
2. Ni nini kinachokufanya uchague kitabu au makala ya kusoma?
3. Ni nini kinachokuvutia unaposoma hadithi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposimulia na
kujadiliana na wenzake.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia tarakilishi na mtandao
kupata matini ya kusoma.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapojichagulia matini na
kuyasoma kwa mapana.
Uhusiano na masuala mtambuko
Matini anazochagua mwanafunzi zitakuwa na masuala mtambuko mbalimbali
kwa mfano chanjo ya watoto, utapiamlo na mihadarati.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji unakuzwa mwanafunzi anapotunza matini anazosoma.
Heshima inakuzwa mwanafunzi anapojadiliana na wenzake kuhusu
alichokisoma.
203
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia mada za kusikiliza
na kuzungumza.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awe kielelezo cha utamaduni wa kusoma shuleni na nyumbani. Maarifa
anayopata kutokana na usomaji wake ayatumie shuleni na nyumbani kuifaidi jamii.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Utamaduni
mzuri wa
kusoma
matini za aina
mbalimbali
shuleni na
nje ya shule
na kusimulia
kwa ufasaha
alichokisoma.
Mwanafunzi ana
utamaduni mzuri
wa kusoma matini
za aina mbalimbali
shuleni na nje ya
shule na anapenda
kusimulia kwa
ufasaha na
kwa urahisi
alichokisoma.
Mwanafunzi
ana utamaduni
mzuri wa
kusoma
matini za aina
mbalimbali
shuleni na
nje ya shule
na kusimulia
alichokisoma.
Mwanafunzi
ana utamaduni
wa kusoma
baadhi ya
sampuli za
matini shuleni
na kuzisimulia.
Mwanafunzi
anajaribu
kusoma
baadhi ya
matini shuleni.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli au wawasikilize wenzao au
mwalimu akisoma matini kwa sauti.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuzungumza, wajibu maswali kwa kuandika
daarini, kwenye tarakilishi au kwenye chati. Pia, wanaweza kutumia lugha ishara
kueleza majibu yao iwapo mwalimu anaifahamu.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuandika kwa kutumia mikono wahimizwe kutumia
kiungo kingine kama vile mguu ama midomo kushika kalamu na kuandika. Wapewe
muda zaidi. Mwalimu awahamasishe wanafunzi wengine kuhusu umuhimu wa
kumkubali mtu bila kujali mahitaji yake. Kufanya hivyo kutazuia unyanyapaa kwa
wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali.
Maelezo ya jumla
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuhusu umuhimu wa kusoma matini mbalimbali.
Usomaji huo utaboresha matamshi yake na kukuza msamiati wake. Pia, awaeleze kuwa
matini mbalimbali zinaweza kupatikana mtandaoni.
204
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 146)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini za kusoma za aina mbalimbali na kuchagua zinazomvutia.
b) Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
Maswali dadisi
1. Kwa nini unapenda kusoma?
2. Ni nini kinachokufanya uchague kitabu au makala ya kusoma?
3. Ni nini kinachokuvutia unaposoma hadithi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu anaweza kutumia vyanzo mbalimbali halisi vya matini kama vile magazeti,
vitabu vya hadithi, tarakilishi, rununu, majarida, vitabu vya kiada n.k. katika
ufundishaji wa mada hii.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 146, 2. Breli, 3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa maswali dadisi. Katika shughuli ya kwanza,
mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Katika vikundi hivyo, wanafunzi watazame na kujadili mchoro ulio kitabuni mwao.
Wanafunzi washirikiane kujibu maswali waliyopewa. Mwalimu atathmini majibu ya
wanafunzi.
Majibu tarajiwa: 1. Watoto walio na magonjwa ya kwashakoo, utapiamlo na matege
2. Kwashakoo husababishwa na ukosefu wa vyakula vya protini mwilini, utapiamlo
husababishwa na ukosefu wa viinilishe mwilini, matege husababishwa na ukosefu wa
vitamini D. 3. Kitabu cha kiada 4. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu amwelekeze mwanafunzi asome kifungu kilicho
kitabuni mwao kisha ajibu maswali yanayofuata kuhusu kifungu hicho. Mwalimu
atathmini majibu ya wanafunzi. Wanafunzi wanaweza kujadiliana kuhusu maswali
hayo. Mwalimu awaeleze wanafunzi kuhusu magonjwa ambayo husababishwa na
ukosefu wa lishe bora. Pia, awaeleze kuwa lishe bora ni ulaji wa vyakula vya wanga,
protini na vitamini kwa viwango vinavyohitajika mwilini.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi atumie mtandao
kusoma kuhusu magonjwa yoyote mawili yanayosababishwa na ukosefu wa lishe bora.
205
Kimeidhinishwa na KICD
Aandike maelezo hayo katika daari lake. Mwalimu atathmini maelezo ya wanafunzi.
Mwanafunzi anaweza kuwasomea wenzake maelezo hayo darasani.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua umuhimu wa kula
vyakula mbalimbali mwilini.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua magonjwa
mbalimbali yanayosababishwa na ukosefu wa lishe bora mwilini.
Kipindi cha 2: Matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 148)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini za kusoma za aina mbalimbali na kuchagua zinazomvutia.
b) Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
Swali dadisi
Ni nini kinachokufanya uchague kitabu au makala ya kusoma?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae chati au jedwali lenye michoro ya vyakula mbalimbali pamoja
na umuhimu wake mwilini kabla ya kipindi hiki. Atumie nyenzo hizo kuwaeleza
wanafunzi kuhusu umuhimu wa vyakula mbalimbali mwilini. Pia, atunge kifungu
kuhusu afya bora atakachowasomea wanafunzi darasani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 148, 3. Breli, 5. Tarakilishi,
2. Kifungu cha matini, 4. Chati ya michoro ya vyakula mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa maswali dadisi kisha, awapange
wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao. Wanafunzi washirikishwe
kutaja majina ya vyakula vilivyo katika mchoro wa shughuli ya kwanza. Majibu
tarajiwa: nanasi, tikitimaji, zabibu, boga, karoti, ndizi, tufaha n.k. Mwalimu awaongoze
wanafunzi katika kujadiliana kuhusu umuhimu wa vyakula hivyo mwilini na mahali
vinapatikana. Wanafunzi wajadiliane katika vikundi vyao. Mwalimu awafahamishe
wanafunzi kuwa wanaweza kupata matini kuhusu afya bora mtandaoni na wakasoma.
Katikashughuli ya pili, mwalimu awasomee wanafunzi kifungu atakachotunga kuhusu
afya bora. Wanafunzi wasikilize kwa makini. Mwalimu ahakikishe anasoma kifungu
hicho kwa matamshi sahihi. Ufuatao ni mfano wa kifungu anachoweza kuwasomea:
206
Kimeidhinishwa na KICD
Wakio
Wakio ni mwanafunzi wa shule ya msingi ya Kineni. Kineni ni shule ya bweni
inayopatikana katika mtaa wa Sengera. Ni shule iliyoanzishwa kwa nia ya kuwasaidia
mayatima wa eneo hilo.
Wanafunzi wa shule ya Kineni hupata chakula chao cha mchana shuleni. Hii ni kwa
sababu wengi wao hutoka katika familia ambazo zina mapato madogo. Mwalimu mkuu
wa shule ya Kineni huhakikisha kuwa wanafunzi wote wamepewa lishe bora.
Wakio na wenzake hupewa vyakula vya protini kama vile maziwa, nyama, maharagwe
na mayai. Vyakula hivi huwasaidia kujenga mwili na kukua. Pili, wao hupewa vyakula
vya wanga kama vile ugali, wali, viazi na pure. Hivi huwasaidia kupata nguvu za
kusoma na kucheza michezo mbalimbali. Vilevile wanafunzi hawa hupewa vyakula vya
vitamini kama vile matunda na mboga ambavyo huwakinga dhidi ya magonjwa.
Wakio na wenzake ni wanafunzi wenye afya njema. Nyuso zao huwa zenye furaha kila
wakati.
Baada ya kusikiliza kifungu hiki, wanafunzi waelekezwe kujibu maswali waliyopewa
kitabuni mwao.
Majibu tarajiwa: 1. Shule ya Msingi ya Kineni 2. Vyakula vya protini, vya wanga na
vya vitamini 3. Kumpa nguvu, kumkinga dhidi ya magonjwa na kumsaidia kukua.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi na mahitaji yao. Awaelekeze wanafunzi kujadiliana maswali yaliyo kitabuni
mwao katika vikundi vyao. Wanafunzi wataje umuhimu wa maji, waeleze kiasi cha
maji ambacho mtu anafaa kunywa kwa siku na wataje baadhi ya vitu vinavyoweza
kuchafua maji. Pia, wajadiliane kuhusu madhara ya kunywa maji machafu. Majibu
tarajiwa: 1. Maji husaidia viungo vya mwili kufanya kazi vizuri. 2. Gilasi nane za maji
3. Husababisha magonjwa hasa ya tumbo kama vile kuendesha, kichocho n.k.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aeleze
mambo mengine yanayochangia afya bora isipokuwa lishe bora. Anaweza kumwuliza
mlezi au mzazi. Pia, anaweza kutumia mtandao. Mwanafunzi awasomee wenzake
aliyoyaandika darasani ili wajifunze.
Majibu tarajiwa: Kunywa maji ya kutosha, kufanya mazoezi ya mwili, kulala kwa saa
za kutosha, kupunguza mawazo mengi n.k.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kujadili umuhimu wa vyakula
mbalimbali.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ametambua mambo mengine
yanayochangia afya bora isipokuwa lishe bora.
207
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 3: Matini
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 150)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua matini za kusoma za aina mbalimbali na kuchagua zinazomvutia.
b) Kusoma matini aliyochagua ili kufaidi ujumbe na lugha iliyotumiwa.
Swali dadisi
Ni nini kinachokuvutia unaposoma hadithi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu atayarishe matini atakazotumia wakati wa kipindi hiki. Atafute matini
kutoka kwenye gazeti, vitabu vya hadithi au mtandao. Anaweza kuzipiga chapa au
wanafunzi watumie vifaa vya kidijitali kuzisoma. Matini atakazotafuta zilenge afya
bora. Pia, mwalimu atayarishe video atakayotumia. Video atakayoandaa ihusu watu
wanaotumia dawa za kulevya kama vile kuvuta sigara na kunywa pombe. Mwalimu
awaeleze wanafunzi kuwa dawa za kulevya zina madhara makubwa mwilini. Dawa za
kulevya huathiri mapafu, maini, ubongo na husababisha ugonjwa wa saratani. Vilevile,
dawa za kulevya zinaweza kusababisha vifo na uraibu kwa watumiaji.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 150, 2. Tarakilishi, 3. Breli,
4. Kanda ya video, 5. Magazeti.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi na
awaelekeze watazame na kujadili mchoro ulio kitabuni mwao. Mwalimu anaweza
kuwaonyesha wanafunzi gazeti halisi darasani linalozungumzia madhara ya dawa za
kulevya. Wanafunzi wajibu maswali yanayohusu mchoro huo kwa kujadiliana katika
vikundi vyao. Mwalimu atathmini majibu yao.
Majibu tarajiwa: 1. Dawa za kulevya huathiri mapafu, ubongo, maini na viungo vingine
vya mwili, huweza kusababisha maafa n.k. 2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
3. Ajiunge na taasisi za kurekebisha uraibu, aache kutumia dawa za kulevya, n.k.
Mwalimu katika shughuli ya pili awaonyeshe wanafunzi video kuhusu matumizi
na madhara ya mihadarati. Wanafunzi wajadili video waliyoonyeshwa kisha wajibu
maswali yanayohusu video hiyo. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
mazungumzo kati yake na raki yake akimshauri aache kutumia dawa za kulevya.
Mwalimu ahakikishe ushauri utakaotolewa na mwanafunzi ni chanya ili kuwasaidia
kuepukana na matumizi ya dawa za kulevya.
208
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anajua madhara ya mihadarati.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kumshauri mtu yeyote
kuhusiana na matumizi ya dawa za kulevya.
CH. Kuandika: Kuandika insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 151)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya maelezo katika matini.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
Maswali dadisi
1. Je, ni vitu gani vinaweza kutungiwa insha ya maelezo?
2. Ni mambo gani unastahili kuzingatia unapoandika insha ya maelezo?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
kuandika insha mtandaoni na kurejelea kielelezo cha insha ya maelezo.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya maelezo.
Hamu ya ujifunzaji - inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia uandishi wa insha
ya maelezo.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi mzuri katika mawasiliano.
209
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuandika insha
ya maelezo fasaha
inayozingatia
lugha ya
kiubunifu ili
kujenga picha
dhahiri yenye
kuzingatia kanuni
za lugha na
mpangilio mzuri
wa mawazo.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo fasaha
akizingatia lugha
ya kiubunifu
ili kujenga
picha dhahiri
akizingatia
kanuni za lugha
na mpangilio
mzuri wa mawazo
kwa urahisi.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya maelezo fasaha
inayozingatia
lugha ya kiubunifu
ili kujenga picha
dhahiri akizingatia
kanuni za lugha na
mpangilio mzuri
wa mawazo.
Mwanafunzi
anaandika
insha ya
maelezo
akizingatia
lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika
insha ya
maelezo.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, wasome maelezo ya insha ya maelezo kwa
kutumia breli au wawasikilize wenzao au mwalimu akizisoma.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuzungumza au kusikia, wajibu maswali kwa
kuandika madaarini au kwenye tarakilishi. Pia, wanaweza kutumia lugha ishara
kueleza kuhusu insha ya maelezo iwapo wanaifahamu. Mwalimu aandike maelezo
ya insha ya masimulizi ubaoni au kwenye chati ili waweze kuyasoma.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuandika kwa kutumia mikono wahimizwe kutumia
kiungo kingine kama vile mguu ama midomo kushika kalamu na kuandika. Wapewe
muda zaidi. Mwalimu awahamasishe wanafunzi wengine kuhusu umuhimu wa
kumkubali mtu bila kujali mahitaji yake. Kufanya hivyo kutazuia unyanyapaa kwa
wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali.
Maelezo ya jumla
Mwalimu awaeleze wanafunzi kuhusu insha ya maelezo. Awaeleze kuwa insha hii
hutoa maelezo au ufafanuzi kuhusu kitu, kiumbe au jambo lolote. Insha hii huandikwa
kwa kuzingatia mada husika. Awaeleze kanuni za kufuata insha hii inapoandikwa.
Kipindi cha 1: Insha ya maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 151)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya maelezo katika matini.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
210
Kimeidhinishwa na KICD
Maswali dadisi
1. Je, ni vitu gani vinaweza kutungiwa insha ya maelezo?
2. Ni mambo gani unayostahili kuzingatia unapoandika insha ya maelezo?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Insha ya maelezo ni insha ambayo hutoa taswira kamili ya jambo, kiumbe au kitu
fulani. Mambo yanayostahili kuzingatiwa wakati wa kuandika insha ya maelezo ni
kama vile: kuwepo kwa mada, mtiririko wa mawazo, saru sahihi, tahajia sahihi, hati
inayosomeka kwa urahisi, lugha ya kuvutia na bunifu n.k. Mwalimu aandae kielelezo
cha insha ya maelezo atakachowasomea wanafunzi darasani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 151,
2. Breli,
3. Kielelezo cha insha ya maelezo.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa maswali dadisi. Mwalimu awaongoze
wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Wajadiliane kuhusu mambo ya kuzingatiwa
katika uandishi wa insha ya maelezo waliyofundishwa hapo awali. Wanafunzi wataje
vipengele muhimu vya insha ya maelezo kama vile mada, mwili na hitimisho. Mwalimu
atathmini hoja za wanafunzi katika majadiliano ya vikundi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awasomee wanafunzi kifungu cha maelezo
ambacho atakuwa amebuni kabla ya kipindi hiki. Kifungu hicho kihusu utoaji wa
maelezo yoyote. Wanafunzi wasikilize kwa makini kifungu hicho kisha wajibu maswali
waliyopewa kitabuni mwao wakiwa wawili wawili. Mwalimu amwelekeze mwanafunzi
kuandika muhtasari wa kifungu walichosomewa katika daftari lake. Mwalimu
atathmini kazi ya mwanafunzi. Wanafunzi wanaweza kubadilishana madaftari na
wakazitathmini kazi za wenzao darasani. Muhtasari bora zaidi usomwe darasani ili
wengine wajifunze.
Katika shughuli ya tatu, wanafunzi wakiwa katika vikundi waelekezwe kutazama na
kujadili vitendo katika michoro iliyo kitabuni mwao. Baada ya majadiliano, waandike
insha ya maelezo wakirejelea vitendo vya michoro hiyo. Wanafunzi watathmini kazi
zao katika vikundi vyao. Mwalimu atathmini kazi za vikundi vyote. Insha bora zaidi
zisomwe darasani ili wanafunzi wajifunze.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi ajadiliane na
mlezi au mzazi wake kuhusu nyakati zifaazo za kunawa mikono. Pia, wajadiliane
kuhusu umuhimu wa watu kunawa mikono. Aandike umuhimu huo katika daari
lake. Awaeleze wenzake umuhimu huo darasani ili wajifunze. Majibu tarajiwa: Watu
wanafaa kunawa mikono kabla ya kula, baada ya kutoka msalani, baada ya kugusa
uchafu n.k. Umuhimu wa kunawa mikono ni ili kuzuia magonjwa hasa ya tumbo.
211
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua vipengele vya kuzingatia
katika kuandika insha ya maelezo.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anafahamu umuhimu wa kunawa
mikono.
Kipindi cha 2: Insha ya maelezo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 152)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya maelezo katika matini.
b) Kuandika insha ya maelezo kwa kufuata kanuni zifaazo.
Swali dadisi
Ni mambo gani unayostahili kuzingatia unapoandika insha ya maelezo?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awakumbushe wanafunzi kuhusu vipengele na mambo ya kuzingatia katika
uandishi wa insha ya maelezo na katika tathmini ya insha hizo. Mambo hayo ni kama
vile: anwani, mpangilio wa mawazo, hati sa, tahajia, kanuni za saru, uakishaji na
matumizi ya misemo na nahau.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 152,
2. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi maswali
dadisi. Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi na
kuwaelekeza wajadili kuhusu njia mbalimbali za kudumisha afya bora. Wanafunzi
waandike vidokezo watakavyojadili katika madaari yao. Kila mwanafunzi atumie
vidokezo alivyoandika kuandika insha ya maelezo kuhusu afya bora. Mwalimu
atathmini insha za maelezo zitakazoandikwa na wanafunzi iwapo zimezingatia
vipengele vyote. Insha bora zaidi zisomwe darasani ili wanafunzi wajifunze.
Katika shughuli ya pili, mwanafunzi ajadiliane na mwenzake kuhusu maswali
waliyopewa kitabuni mwao. Mwalimu atathmini majibu hayo.
Katika kazi ya ziada, mwalimu amwelekeze mwanafunzi kuandika insha ya maelezo
kuhusu madhara ya kutodumisha usa. Mwanafunzi amsomee mlezi au mzazi wake
insha hiyo ili aitathmini. Pia, anaweza kuwasomea wenzake darasani insha hiyo ili
waitathmini na kujifunza.
212
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika insha ya maelezo
kwa kuzingatia vipengele muhimu vya uandishi wake.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kujadiliana na wenzake
kuhusu umuhimu wa kudumisha usa na madhara ya kutodumisha usa.
D. Saru:Vinyumevyanomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 153)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kinyume cha nomino ili kukibainisha.
b) Kutambua vinyume vya nomino katika matini.
ch) Kuunda sentensi kwa kutumia vinyume vya nomino ipasavyo.
Swali dadisi
Je, ni nomino gani unaweza kutambua vinyume vyake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika kazi
za vikundi.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika kutunga sentensi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia tarakilishi au mtandao.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu endelevu - mwanafunzi anapanua mawazo kuhusu mazingira yake
anapotambua vinyume vya nomino kutoka kwa mazingira hayo.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - unakuzwa mwanafunzi anapotunza vifaa vya kidijitali.
Heshima na ushirikiano - unakuzwa mwanafunzi anapofanya kazi na wenzake
katika vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya hushughulikia saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awe kielelezo cha wengine katika kutumia lugha kwa ufasaha.
213
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
vinyume
vya nomino
mbalimbali
na kuvitumia
katika sentensi
ipasavyo.
Mwanafunzi
anatambua
vinyume
vya nomino
mbalimbali
na kuvitumia
katika sentensi
ipasavyo kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
vinyume
vya nomino
mbalimbali
na kuvitumia
katika sentensi
ipasavyo.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
vinyume vya
nomino na
kuvitumia
katika sentensi
ipasavyo.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
vinyume vya
nomino.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona mbali waketi karibu na ubao. Wasioweza
kuona vitu vilivyo karibu nao waketi mbali na ubao ili waweze kuona vizuri ubaoni.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema watazame kwenye ubao, kiwambo
cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au kwenye chati.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kutambua vinyume vya nomino kwa urahisi
wahusishwe katika shughuli zaidi za ujifunzaji na wapewe muda zaidi wa kujifunza.
Wahimizwe kwa upendo ili wajithamini na kuchangamkia ujifunzaji. Hatua yoyote
wanayopiga katika ujifunzaji itambuliwe na mwalimu ili wawe na hamu ya kujifunza
zaidi.
Maelezo ya jumla
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua vinyume mbalimbali vya nomino.
Wanafunzi waelewe kuwa kinyume ni hali ya kuwa tofauti na kitu kingine au mtu
mwingine.
Kipindi cha 1: Vinyume vya nomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 153)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kinyume cha nomino ili kukibainisha.
b) Kutambua vinyume vya nomino katika matini.
ch) Kuunda sentensi kwa kutumia vinyume vya nomino ipasavyo.
Swali dadisi
Je, ni nomino gani unaweza kutambua vinyume vyake?
214
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi maana ya neno nomino. Awaeleze kuwa nomino ni aina
ya neno la kutajia viumbe, vitu au mahali. Mifano ni kama vile: paka, meza, Maria,
Kenya, choo, sahani na Aprili. Kinyume ni hali ya kuwa tofauti na kingine. Kinyume
huweza kufanyika katika neno, kitendo au jambo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 153,
2. Breli,
3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awahusishe wanafunzi wawili wawili wajadili
na kutaja majina ya michoro iliyo kitabu mwao. Wanafunzi waeleze uhusiano wa
watu katika michoro waliyojadili. Mwalimu atathmini maelezo ya wanafunzi kisha
awaelekeze kutambua kuwa majina ya watu waliotaja kwa kila mchoro ni ya kinyume.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaulize wanafunzi katika vikundi wataje nomino
mbalimbali ambazo wanaweza kutambua vinyume vyao. Wanafunzi wachangamkie
shughuli hii. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya shughuli ya tatu. Wanafunzi watumie
kamusi au tarakilishi kujibu maswali waliyopewa kitabuni mwao. Wanafunzi watafute
vinyume vya nomino walizopewa kitabuni mwao. Watunge sentensi kwa kutumia
vinyume walivyoandika. Hatimaye, waandike sentensi walizotunga kwenye tarakilishi
kisha wawatumie wenzao sentensi hizo mtandaoni ili wazisome na kuzisahihisha.
Mwalimu amhimize mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi atafute vinyume
vya nomino alizopewa kitabuni mwake. Anaweza kutumia mtandao au kamusi. Pia,
anaweza kumwuliza mlezi au mzazi wake. Atumie nomino alizopewa pamoja na
vinyume vyao kutunga sentensi sahihi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutafuta vinyume vya nomino
na kutumia nomino hizo pamoja na vinyume hivyo kutunga sentensi sahihi.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutunga sentensi akitumia
nomino na vinyume vyao kwenye tarakilishi.
215
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2: Vinyume vya nomino
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 155)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya kinyume cha nomino ili kukibainisha.
b) Kutambua vinyume vya nomino katika matini.
Swali dadisi
Je, ni nomino zote zina vinyume?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awakumbushe wanafunzi maana ya nomino. Awaeleze kuwa nomino ni aina
ya neno la kutajia viumbe, vitu au mahali. Kinyume ni hali ya kuwa tofauti na kingine
au mwingine. Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika vikundi na wakiwa peke yao
kutunga sentensi sahihi kwa kutumia nomino na vinyume vyao. Mwalimu awasaidie
wanafunzi wanaotatizika.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Mti wa vinyume, 2. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 155, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa swali dadisi. Awaelekeze wanafunzi
wakiwa wawili wawili wafanye shughuli ya kwanza. Wachunguze nomino za vinyume
zilizo katika mti wa maneno kitabuni mwao. Walinganishe nomino zilizopo na
vinyume vyao kwa usahihi. Wanafunzi waandike nomino hizo na vinyume vyao katika
madaari yao. Mwalimu atathmini kazi za wanafunzi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaagize wanafunzi watumie nomino pamoja
na vinyume vyao kutoka katika shughuli ya kwanza kutunga sentensi sahihi. Kila
mwanafunzi atunge na aandike sentensi hizo katika daftari lake kisha awasomee
wenzake darasani. Mwalimu na wanafunzi wenzake wasahihishe sentensi hizo.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na
idadi na mahitaji yao. Wanafunzi watumie nomino mbalimbali pamoja na vinyume
vyao kubuni kifungu kifupi. Mwanafunzi mmoja kutoka katika kila kikundi awasomee
wengine kifungu walichobuni ili wakisikilize na kukitathmini. Pia, mwalimu ashiriki
katika tathmini hii.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi asaidiwe na mlezi
au mzazi wake kutaja majina ya watu katika familia yao. Wajadiliane kuhusu vinyume
vya majina hayo kisha atumie majina hayo na vinyume vyao kutunga sentensi sahihi.
Sentensi hizi zitathminiwe katika kipindi kijacho.
216
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika vinyume vya
nomino mbalimbali.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutumia vinyume vya nomino
kutunga sentensi sahihi na kifungu kifupi.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Mwanafunzi ataje mahali mbalimbali
ambapo mazungumzo yasiyo rasmi hutokea. Kwa mfano: sokoni, dukani, hotelini,
nyumbani, njiani, barabarani, kinyozi, saluni n.k.
2. Mwalimu atathmini mazungumzo ambayo mwanafunzi atabuni. Mazungumzo
hayo yawe kati ya mwanafunzi na raki yake katika mazingira yasiyo rasmi ambayo
ni njiani.
3. Mwalimu atathmini majina ya vyakula ambavyo mwanafunzi atataja kwa kila
kategoria aliyopewa. Mwanafunzi atumie mtandao kutafuta picha za vyakula hivyo.
Iwapo mwanafunzi hataweza kupata mtandao, anaweza kupewa picha za vyakula
hivyo akataja majina yao.
a) Mifano ya vyakula vya protini ni: nyama, maziwa, mayai, maharagwe, samaki
n.k.
b) Mifano ya vyakula vya wanga ni: mahindi, ugali, wali, chapati, mihogo n.k.
ch) Mifano ya vyakula vya vitamini ni: matunda na mboga mbalimbali.
4. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi kuhusu umuhimu wa vyakula vya kila
kategoria aliyopewa katika swali la 3. Vyakula vya protini husaidia kuujenga mwili.
Vyakula vya wanga husaidia kuupatia mwili nguvu za kufanya kazi. Vyakula vya
vitamini huukinga mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali.
5. Mwalimu atathmini jibu la mwanafunzi. Mwanafunzi aandike kinyume cha nomino
‘daktari ambacho ni mgonjwa. Kisha mwanafunzi atunge sentensi sahihi akitumia
nomino mgonjwa. Mfano: Mgonjwa amepona.
6. Mwalimu atathmini jibu la mwanafunzi. Mwanafunzi aandike kinyume cha nomino
mama ambacho ni ‘baba. Kisha mwanafunzi atunge sentensi sahihi akitumia
nomino ‘baba. Mfano: Baba anasoma gazeti.
7. Mwalimu atathmini jibu la mwanafunzi. Mwanafunzi atambue vinyume vya
nomino katika sentensi aliyopewa kisha aandike sentensi hiyo upya kwa kutumia
vinyume hivyo. Jibu ni: Mwanafunzi alimtembelea kaka yangu.
217
Kimeidhinishwa na KICD
8. Mwanafunzi aeleze umuhimu wa maji katika mwili wa binadamu. Mwalimu
akubali majibu yoyote sahihi yanayohusu umuhimu wa maji mwilini. Mifano ni:
maji huvifanya viungo mbalimbali kufanya kazi vizuri hasa go, maji hupunguza
joto mwilini, maji huboresha mwonekano wa ngozi n.k.
9. Mwalimu atathmini magonjwa ambayo mwanafunzi atataja. Magonjwa hayo yawe
yanayosababishwa na ukosefu wa lishe bora pekee. Mifano: kwashakoo, utapiamlo,
matege n.k.
10. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anaandika insha ya maelezo kuhusu njia
mbalimbali za kudumisha afya bora kwa binadamu. Mwalimu atathmini muundo
atakaotumia mwanafunzi kuandika insha yake. Sharti muundo huo uwe sahihi na
unaofaa katika uandishi wa insha ya maelezo.
218
Kimeidhinishwa na KICD
KUKABILIANA NA UHALIFU
10
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 157)
A. Kusikiliza na Kuzungumza: Tashbihi
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya tashbihi ili kuibainisha.
b) Kutambua tashbihi za kimo na umbo katika matini.
ch) Kutumia tashbihi za kimo na umbo kwa usahihi katika sentensi.
Maswali dadisi
1. Ni tashbihi zipi hutumiwa kueleza kimo cha kitu?
2. Ni tashbihi zipi hutumiwa kueleza umbo la kitu?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika kazi
ya vikundi.
Hamu ya kujifunza inakuzwa kutokana na kazi ya ziada anayopewa
mwanafunzi kuhusu tashbihi za kimo na umbo.
Ujuzi wa kidijitali unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kidijitali
katika kujifunza tashbihi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Elimu ya mazingira mwanafunzi anarejelea mifano ya vitu na viumbe katika
mazingira yake.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu kupitia kazi ya vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili masomo haya hushughulikia mada
ya tashbihi.
219
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anatarajiwa kuwa kielelezo cha kutumia lugha kwa ufasaha shuleni na
nyumbani.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
tashbihi za kimo
na umbo na
kuzitumia kwa
usahihi katika
sentensi.
Mwanafunzi
anatambua
tashbihi za
kimo na umbo
na kuzitumia
kwa usahihi na
urahisi katika
sentensi.
Mwanafunzi
anatambua
tashbihi za kimo
na umbo na
kuzitumia kwa
usahihi katika
sentensi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
tashbihi za kimo
na umbo na
kuzitumia kwa
usahihi katika
sentensi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
baadhi ya
tashbihi za kimo
na umbo.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli kutambua tashbihi za kimo
na umbo. Pia, wanaweza kuwasikiliza wanafunzi wenzao na mwalimu wakisoma
tashbihi za kimo na umbo kwa sauti.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema, watumie ishara kutambua
tashbihi za kimo na umbo huku wanafunzi wengine wakizitamka na kuwapigia
mako. Wanafunzi hawa wanaweza kuandika majibu madaarini mwao.
Maelezo ya jumla
Mada hii inalenga kukuza stadi ya kusikiliza na kuzungumza. Mwanafunzi anaweza
kusikiliza tashbihi za kimo na umbo kutoka kwa mwalimu au rekoda. Mwanafunzi
akiweza kutaja na kuunda sentensi atakuwa akikuza uwezo wake wa kuzungumza na
kuwa mbunifu.
Kipindi cha 1: Tashbihi za kimo na umbo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 157)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya tashbihi.
b) Kutambua tashbihi za kimo na umbo.
Maswali dadisi
1. Ni mnyama yupi mwenye shingo ndefu kabisa?
2. Je, ni mnyama yupi aliye mnono zaidi?
220
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Tashbihi ni fani ya lugha inayolinganisha hali au tabia za vitu au viumbe. Kimo ni
urefu au ufupi wa kitu au mtu. Ili kupima kimo, unahitaji utepe, rula au uzi. Umbo ni
mkao wa kitu. Unene na wembamba ni sifa za umbo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 157, 2. Utepe/uzi/rula,
3. Breli, 4. Mizani, 5. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize somo kwa kuuliza maswali dadisi. Majibu tarajiwa: twiga,
nguruwe. Mwalimu akubali majibu yoyote sahihi kutoka kwa wanafunzi.
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaelekeze wanafunzi kujigawa katika vikundi
mbalimbali kulingana na kimo chao. Mwanafunzi mmoja awahesabu wanafunzi
warefu zaidi na kutaja idadi yao. Vilevile, awahesabu wanafunzi wafupi zaidi na kutaja
idadi yao. Kwa kutumia utepe, uzi au rula, mwalimu awasaidie wanafunzi kupima
urefu wa mwanafunzi mrefu zaidi na pia yule mfupi zaidi. Mwanafunzi ajitambulishe
na kikundi kulingana na kimo chake. Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua kuwa
kimo ni urefu au ufupi wa kitu au mtu.
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na unene au wembamba wao
katika shughuli ya pili. Mwanafunzi mmoja awahesabu wanafunzi wanene zaidi na
kutaja idadi yao. Vilevile, awahesabu wanafunzi wembamba zaidi na kutaja idadi yao.
Kwa kutumia mizani wanafunzi wapime uzito wa mwanafunzi mnene zaidi na yule
mwembamba zaidi. Mwalimu awahusishe wanafunzi wote huku akiwatathmini ili
kujua uelewa wao.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi watazame na kujadili
michoro waliyopewa kitabuni mwao. Wajibu maswali waliyopewa baada ya michoro
hiyo.
Majibu tarajiwa: 1. twiga, nguruwe 2. Mwanafunzi ni mrefu kama twiga. 3. Mzee ni
mnene kama kiboko. 4. Mwalimu atathmini sentensi za mwanafunzi.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie breli kujibu maswali husika.
Mwalimu ahitimishe kipindi kwa kuwaelekeza wanafunzi jinsi ya kufanya kazi ya
ziada. Mwanafunzi ataje vitu ambavyo vinafanana kwa umbo na kimo na aviandike
katika daari lake. Atumie mtandao kutazama picha za vitu alivyoandika. Awaeleze
wenzake darasani kuhusu vitu hivyo na ufananisho wake. Mwalimu atathmini majibu
ya wanafunzi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kueleza maana ya tashbihi.
221
Kimeidhinishwa na KICD
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua tashbihi za umbo na
kimo.
Kipindi cha 2: Tashbihi za kimo na umbo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 159)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia tashbihi za umbo na kimo katika matini.
b) Kufahamu matumizi ya tashbihi za kimo na umbo katika mawasiliano.
Swali dadisi
Unakiri tofauti ya kimo na umbo ni nini?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutumia tashbihi kwa usahihi katika mawasiliano.
Ahakikishe wanafunzi wanatambua vitu kadhaa vilivyo na sifa sawa zinazorejelea
kimo na umbo.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 159, 2. Tarakilishi,
3. Kamusi, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwashirikisha wanafunzi wawili wawili katika
shughuli ya kwanza. Kila mwanafunzi ataje tashbihi zozote kumi anazojua. Wajadili
tashbihi hizo kisha watambue tashbihi za kimo na umbo kati ya walizotaja. Waziandike
tashbihi hizo katika madaari yao. Majibu tarajiwa: 1. Mnene kama nguruwe. 2.
Mfupi kama nyundo. 3. Mwembamba kama sindano. 4. Tamu kama asali. Mwalimu
atathmini majibu ya wanafunzi na akubali yaliyo sahihi.
Mwalimu amteue mwanafunzi mmoja asome kifungu katika shughuli ya pili.
Wanafunzi wengine wamsikilize kwa makini kisha wasome kifungu hicho pia.
Mwalimu awasaidie kutamka maneno yanayowatatanisha. Mwalimu awaongoze
wanafunzi kujibu maswali waliyopewa kitabuni mwao.
Majibu tarajiwa: 1. Mfupi kama nyundo - ufupi unalinganishwa na nyundo. 2.
Mnene kama nguruwe - unene unalinganishwa na nguruwe. 3. Mrefu kama mlingoti -
urefu unalinganishwa na mlingoti. 4. Mwembamba kama sindano - wembamba
unalinganishwa na sindano. Mwalimu akubali majibu ya wanafunzi yaliyo sahihi kwa
kurejelea kifungu walichosoma. Wanafunzi watumie tashbihi walizotambua kutunga
sentensi sahihi. Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi.
222
Kimeidhinishwa na KICD
Kila mwanafunzi ashiriki katika shughuli ya tatu kwa kutumia majina ya michoro
waliyopewa kitabuni mwao kukamilisha tashbihi walizopewa.
Majibu tarajiwa: ana nguvu kama tembo, mfupi kama nyundo, ana miguu mirefu
kama korongo, mrefu kama mlingoti, miembamba kama sindano.
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi kwa kurejelea michoro iliyopo.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi atumie mtandao
kutafuta picha za vitu na viumbe waliotajwa kitabuni mwao. Watumie picha hizo
kuunda tashbihi. Majibu tarajiwa: macho makubwa kama gololi, mweusi kama
makaa, mwenye maringo kama tausi, mfupi kama mbilikimo. Mwanafunzi amsomee
mlezi au mzazi wake tashbihi alizounda. Pia, anaweza kuwasomea wenzake darasani
ili wasikilize na kuzitathmini tashbihi hizo.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutumia tashbihi kwa usahihi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuunda tashbihi sahihi.
B. Kusoma: Kusoma kwa mapana
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 161)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua na kuzingatia hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya
kidijitali.
b) Kutambua na kufungua faili iliyo na kifungu cha kusoma ili kuimarisha umilisi
wake wa kutumia tarakilishi.
ch) Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata vifungu vya kusoma vyenye
mada lengwa.
d) Kusoma matini lengwa ili kupata ujumbe.
Maswali dadisi
1. Ni masuala gani ambayo umewahi kusoma mtandaoni?
2. Ukitaka kupata matini ya kusoma mtandaoni utafanya nini?
3. Utafanya nini mtu usiyemjua akikutumia ujumbe mtandaoni?
223
Kimeidhinishwa na KICD
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa kutafuta,
kusakura na kusoma matini mtandaoni.
Hamu ya kujifunza - inakuzwa mwanafunzi anapopata hamu ya kutafuta matini
ya kusoma mitandaoni.
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha ujuzi wa kidijitali na usalama mitandaoni.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji katika utunzaji wa vifaa vya kidijitali na kuzingatia mitandao
salama.
Uhusiano na masomo mengine
Masomo yote kwa vile yanatakiwa kuzingatia ujuzi wa kidijitali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu usalama kwenye
mitandao na manufaa ya ujuzi wa kidijitali. Haya yatamsaidia kuimarisha usomaji
wake na kupata maarifa yanayohusu nyanja mbalimbali.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua na
kuzingatia hatua
za kiusalama
mtandaoni,
kutambua tovuti
salama zenye habari
lengwa, kutafuta
matini kwenye
kifaa cha kidijitali
au mtandaoni na
kunakili maneno
na habari muhimu
alizosoma.
Mwanafunzi
anatambua na
kuzingatia hatua
za kiusalama
mtandaoni,
anatambua tovuti
salama zenye
habari lengwa,
anatafuta matini
kwenye kifaa
cha kidijitali
au mtandaoni
na ananakili
maneno na
habari muhimu
alizosoma kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
na kuzingatia
hatua za
kiusalama
mtandaoni,
anatambua
tovuti salama
zenye habari
lengwa,
anatafuta
matini kwenye
kifaa cha
kidijitali au
mtandaoni na
kuyasoma.
Mwanafunzi
anatafuta
matini
mtandaoni na
kwenye kifaa
cha kidijitali na
kuzisoma.
Mwanafunzi
anajaribu
kutafuta
matini
mtandaoni au
kwenye kifaa
cha kidijitali.
224
Kimeidhinishwa na KICD
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, watumie tarakilishi za breli. Wasio na uwezo
wa kusikia waandikiwe maagizo ubaoni au kitabuni. Walio na ulemavu wa mkono
au mikono watumie kiungo chochote ambacho wamezoea kukitumia kuandika.
Walio na uwezo wa kujifunza kwa haraka, wapewe mazoezi zaidi. Wanafunzi
wanaochukua muda kuelewa wapewe muda zaidi ili kukamilisha shughuli zao.
Maelezo ya jumla
Mada hii ya kusoma inalenga kumpa msomaji ujuzi zaidi wa kidijitali pamoja na
uelewa mkuu wa mambo tofauti maishani kupitia matini mtandaoni. Mwanafunzi
aweze kutambua matini salama ambazo anaweza kusoma ili kupata ujumbe atakao.
Pia, mwanafunzi aelewe kwamba mtandao una hatari zake endapo hatua za kiusalama
hazizingatiwi.
Kipindi cha 1: Matini ya kidijitali
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 161)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua na kuzingatia hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya
kidijitali.
b) Kutambua na kufungua faili iliyo na kifungu cha kusoma ili kuimarisha umilisi
wake wa kutumia tarakilishi.
Maswali dadisi
1. Je, ni makala gani ambayo wewe umewahi kusoma mtandaoni?
2. Ili kupata matini mtandaoni, ulitumia kifaa gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Ili kufanikisha kipindi hiki, sharti mwalimu awe na ujuzi na uelewa mzuri wa
kidijitali. Katika kujiandaa kufundisha kipindi hiki, mwalimu ayasakure matini lengwa
ili kuhakikisha kuwa anayafahamu na kuelewa yaliyomo. Pia, aandae tarakilishi za
kutosha kulifanikisha somo hili. Iwapo tarakilishi hazitoshi, anaweza kutumia rununu
au kuazima tarakilishi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 161, 2. Rununu,
3. Tarakilishi, 4. Breli.
225
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize somo kwa kuwashirikisha wanafunzi katika shughuli ya kwanza.
Wanafunzi wakiwa wawili wawili wajibu maswali yaliyo vitabuni mwao.
Majibu tarajiwa: 1. Kuandika/kusoma/kutazama picha/kutuma ujumbe/kucheza
muziki n.k. 2. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi. 3. Simu, televisheni/runinga,
redio, rekoda n.k. 4. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Katika vikundi, wanafunzi watazame michoro iliyo katika shughuli ya pili na kujadili
matumizi ya kila kifaa katika michoro hiyo. Majibu tarajiwa: Rununu/simu tamba
kupiga na kupigiwa simu, kutuma na kupokea ujumbe, kupigia picha n.k. Televisheni/
runinga kupasha habari, kutazama matukio tofauti n.k. Kipakatalishi kuandikia
ujumbe, kuhifadhi kazi, kusakura matini n.k. Mwalimu akubali majibu yoyote sahihi
kutoka kwa wanafunzi.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awape wanafunzi tarakilishi katika vikundi kisha
awape maelekezo. Wawashe tarakilishi hizo na wasakure matini kuhusu utekaji nyara
wa watoto mtandaoni. Wasome matini hiyo na kujadili ujumbe uliomo. Mwalimu
awaelekeze wanafunzi kuandika muhtasari wa matini hiyo na kuhifadhi kazi zao katika
faili kwa jina la mmoja wao. Wanafunzi waitume kazi hiyo kwa wanafunzi wenzao na
mwalimu mtandaoni ili waisome na kuiboresha. Pia, mmoja wao awasomee wengine
muhtasari huo ili wasikilize na kuusahihisha.
Mwalimu amhimize mwanafunzi amshirikishe mlezi au mzazi wake katika kujadili
kazi ya ziada. Wajadiliane kuhusu umuhimu na madhara ya mtandao. Mwanafunzi
aandike hoja zake katika daari lake. Majibu tarajiwa: Umuhimu wa mtandao -
tunapata ujumbe, tunatoa maoni, tunaungana na walio mbali n.k. Hasara za mtandao
- una hatari nyingi, una matini yasiyo na maadili n.k.
Pia, mwanafunzi ajadiliane na mlezi au mzazi wake kuhusu umuhimu wa polisi katika
jamii. Anaweza kutumia mtandao kupata umuhimu wa polisi. Awaeleze wenzake
umuhimu huo darasani. Majibu tarajiwa: kudumisha amani, kukabiliana na uhalifu,
kulinda usalama n.k. Mwanafunzi awasomee wenzake umuhimu huo darasani ili
wajifunze.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua na kuzingatia hatua
za kiusalama anapotumia vifaa vya kidijitali.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua na kufungua faili
iliyo na matini salama ya kusoma mtandaoni.
226
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2: Matini ya kidijitali
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 163)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusakura matini kwenye tovuti salama ili kupata vifungu vya kusoma vyenye
mada lengwa.
b) Kusoma matini lengwa ili kupata ujumbe.
Maswali dadisi
1. Ukitaka kukia matini ya kusoma mtandaoni utafanya nini?
2. Utafanya nini mtu usiyemjua akikutumia ujumbe mtandaoni?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaeleze wanafunzi kwamba mtandao una umuhimu wake vilevile madhara
yake. Ni vizuri mwanafunzi atumie mtandao kwa tahadhari kuu. Mwalimu awaonye
wanafunzi dhidi ya kuwasiliana mtandaoni na watu asiowajua au kukubali zawadi
mtandaoni kutoka kwa watu asiowajua. Visa vya utekaji nyara, mauaji, utapeli, wizi
na vinginevyo vimeripotiwa kutokana na matumizi mabaya ya mtandao. Wanafunzi
watahadharishwe kufuata hatua za kiusalama ili kufaidika na mtandao.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 163, 2. Breli, 3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwashirikisha wanafunzi katika shughuli ya
kwanza. Awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Wanafunzi wajadili maswali yaliyo kitabuni mwao. Mwalimu atathmini majibu ya
wanafunzi kulingana na maswali waliyoulizwa. Majibu tarajiwa: 1.Ulihusu wizi,
ubakaji, ulaghai/utapeli, mauaji n.k. 2. Ulihusisha watoto, akina mama, wazee, vijana
n.k. 3. Suluhisho lilikuwa kupiga ripoti kwa polisi, wazazi, mwalimu n.k.
Wanafunzi wakiwa wawili wawili wajadiliane kuhusu maswali yaliyo kitabuni mwao
katika shughuli ya pili. Wanafunzi waelezane umuhimu wa kutoa habari kuhusu hatari
zozote zinazowakumba. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi. Majibu tarajiwa:
Ili kuokoa maisha yako na ya wengine, kukomesha uhalifu, ili kuadhibu wavunja sheria
n.k. Mwalimu akubali majibu sahihi ya wanafunzi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kusoma matini iliyo kwenye shughuli ya tatu.
Mwanafunzi asome matini hiyo kwa matamshi sahihi. Ajibu maswali yaliyo kitabuni
mwao kwa kurejelea matini aliyosoma. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Majibu tarajiwa: 1. Kuzuia matukio mbalimbali ya uhalifu. 2. Madereva wa pikipiki,
teksi na magari ya usari wa umma. 3. Mitaa ya mabanda, misikiti na makanisa.
227
Kimeidhinishwa na KICD
4. Mwanafunzi atumie kamusi kueleza maana ya maneno. 5. Mwalimu atathmini
muhtasari wa mwanafunzi.
Mwalimu ahitimishe kipindi kwa kumwelekeza mwanafunzi afanye kazi ya ziada.
Mwanafunzi ajadiliane na mlezi au mzazi wake kuhusu kisa chochote cha wizi
kilichowahi kufanyika wanakoishi. Mwanafunzi aandike mafunzo anayopata kutokana
na kisa hicho. Mwanafunzi na mlezi au mzazi wake wajadili aina nyingine za uhalifu.
Wanaweza kutumia mtandao. Mwanafunzi awaeleze wenzake darasani aliyojifunza.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kusakura matini salama kwenye
tovuti na kupata ujumbe lengwa.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutumia vifaa vya kidijitali.
CH. Kuandika: Kuandika Insha
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 165)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
Swali dadisi
Je, unazingatia nini ili kuandika insha nzuri ya masimulizi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano vinakuzwa wanafunzi wanaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali unakuzwa wakati vifaa vya kiteknolojia vinapotumiwa
kuandika insha mtandaoni na kurejelea kielelezo cha insha ya masimulizi.
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi anapoandika insha ya masimulizi.
Hamu ya ujifunzaji inakuzwa mwanafunzi anapoyatafakari maswali dadisi na
anapoimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia kutokana na kufanya kazi pamoja.
Jinsi ya kukabiliana na uhalifu kulingana na mada.
228
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu hasa katika shughuli za vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili masomo haya huishughulikia
mada ya kuandika.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu umuhimu wa
uandishi bora katika mawasiliano.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajo
Mbali na
matarajio
Kuandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio
mzuri wa
mawazo na kwa
ubunifu wa hali
ya juu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
kanuni za lugha,
mpangilio mzuri
wa mawazo
na lugha ya
kiubunifu.
Mwanafunzi
anaandika insha
ya masimulizi
kwa kuzingatia
baadhi ya
kanuni za lugha.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika insha
ya masimulizi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, waandike kwa kutumia breli au wawasikilize
wenzao na mwalimu wakisoma maelezo kuhusu insha za masimulizi. Walio na
ulemavu wa mkono au mikono, watumie kiungo chochote cha mwili ambacho
wamezoea kuandika nacho. Wale walio na uwezo wa kuelewa kwa haraka wapewe
mazoezi zaidi. Wanafunzi wanaochukua muda kuelewa wapewe muda zaidi
kukamilisha shughuli zao.
Maelezo ya jumla
Mada hii inakusudiwa kumsaidia mwanafunzi kujenga na kuboresha ubunifu wake
katika uandishi kama njia mojawapo ya mawasiliano. Hivyo, mwalimu ana jukumu
la kumwelekeza mwanafunzi kukia viwango vya juu vya ubunifu. Pia, mwalimu
ahakikishe kuwa anajenga hamu ya uandishi kwa wanafunzi wasiopenda kuandika.
Uandishi huu utahusu kuandika madaarini na pia kuandika kwa kutumia tarakilishi.
229
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Insha ya masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 165)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua insha ya masimulizi kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo.
b) Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
Swali dadisi
Je, unazingatia nini ili kuandika insha nzuri ya masimulizi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Insha ya masimulizi inahusu kutoa maelezo kuhusu mtu, mahali au kitu fulani. Ujumbe,
mtindo na muundo sharti vizingatiwe unapoandika insha ya masimulizi. Mwalimu
amshauri mwanafunzi kubuni au kutunga kisa chake mwenyewe badala ya kunakili
kisa kilichobuniwa na mtu mwingine. Mwalimu aandae mgeni mwalikwa ambaye
anakusudiwa kutoa masimulizi kwa wanafunzi kuhusu uhalifu wowote. Mgeni huyo
anaweza kuwa mwalimu, mwanafunzi au asa wa kiusalama. Sharti awe na matamshi
sahihi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 165, 2. Breli, 3. Mgeni mwalikwa.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwashirikisha wanafunzi katika shughuli ya kwanza.
Wanafunzi wakiwa wawili wawili wajadili muundo pamoja na mambo ya kuzingatia
katika uandishi wa insha ya masimulizi. Wanafunzi wajikumbushe kuhusu mambo
haya ambayo tayari walishafundishwa katika vipindi vya awali. Mwalimu atathmini
majibu ya wanafunzi. Majibu tarajiwa: Mambo ya kuzingatia katika uandishi wa insha
ya masimulizi ni ujumbe, mtindo, saru sahihi, hati nzuri na muundo.
Wanafunzi wakiwa katika vikundi wajadiliane kwa kujibu maswali yaliyo kitabuni
mwao katika shughuli ya pili. Wanafunzi wasimuliane kuhusu yaliyowatendekea
siku zao za kwanza shuleni. Kila mwanafunzi aandike masimulizi mafupi kutokana
na majadiliano yao kwenye daari lake. Wanafunzi watathmini masimulizi yao katika
vikundi vyao. Mwalimu awasaidie wanaotatizika.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amkaribishe na kumtambulisha mgeni mwalikwa
darasani ambaye atawasimulia wanafunzi kuhusu uhalifu wowote. Mgeni mwalikwa
ahakikishe anatamka maneno kwa usahihi na kwa sauti ya kusikika na wanafunzi wote.
Wanafunzi wamsikilize mgeni huyo kwa makini. Baada ya masimulizi, wanafunzi
wakiwa katika vikundi, wajibu maswali waliyopewa kitabuni mwao. Mwalimu
atathmini majibu ya wanafunzi kulingana na masimulizi waliyosimuliwa.
230
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi abuni na
aandike insha ya masimulizi kuhusu kisa chochote cha mwanafunzi aliyeiba shuleni.
Mwalimu asahihishe insha hiyo na awaelekeze wanafunzi wanaotatizika. Insha
bora zaidi zisomwe darasani ili wanafunzi wajifunze. Wanafunzi wajadili mafunzo
wanayopata kutokana na insha walizoandika.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua insha ya masimulizi.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuandika insha ya masimilizi
kwa kuzingatia kanuni zifaazo.
Kipindi cha 2: Insha ya masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 166)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika insha ya masimulizi kwa kufuata kanuni zifaazo.
b) Kufahamu utunzi mzuri wa insha ya masimulizi ili kujenga ubunifu wake.
Swali dadisi
Je, mwanafunzi anahitaji kufanya nini ili kujenga ubunifu?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaandae wanafunzi kwa kipindi cha kuandika ili wawe na nyenzo muhimu
zinazohitajika katika uandishi.
Mapendekazo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 166, 2. Breli, 3. Tarakilishi.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwahusisha wanafunzi katika shughuli ya kwanza
ya kutazama michoro wakiwa wawili wawili. Wanafunzi wajadili michoro hiyo kisha
waandike insha ya masimulizi kuhusu matukio katika michoro hiyo. Majibu tarajiwa:
Mwanafunzi asimulie kuhusu mwizi aliyeiba kisha akakamatwa. Mwalimu atathmini
masimulizi ya mwanafunzi kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo na michoro
husika.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya pili inayohusu kujadili insha
kuhusu njia mbalimbali za kukabiliana na uhalifu. Kazi hii ifanywe katika vikundi.
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Wanafunzi waandike vidokezo kisha wavitumie kuandika insha yenyewe kwenye
tarakilishi. Wawatumie wenzao insha hiyo mtandaoni ili waisome na kuiboresha.
231
Kimeidhinishwa na KICD
Katika vikundi vivyo hivyo, wanafunzi wajadiliane kuhusu jinsi serikali inavyoweza
kusaidia katika kukabiliana na uhalifu nchini katika shughuli ya tatu. Wanafunzi
waandike hoja zao kwenye madaari yao. Wabadilishane madaari na vikundi vingine
ili watathmini hoja zao. Majibu tarajiwa: Kuwachukulia hatua kali wanaopatikana
wakivunja sheria, kuwahamasisha wananchi kuhusu uhalifu, kuongeza maasa wa
usalama n.k. Mwalimu atathmini hoja za wanafunzi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kufanya kazi ya ziada kwenye madaftari yao.
Wanafunzi wabuni kisa chochote kuhusu utapeli wa pesa ambacho wamewahi kusikia
au kusoma. Wanaweza kutumia kamusi au mtandao. Mwanafunzi awasomee wenzake
insha aliyoandika darasani. Mwalimu atathmini insha ya mwanafunzi kwa kuhakikisha
imefuata vigezo vya insha ya masimulizi na mada lengwa.
Tathmini
1. Mwanafunzi atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kubuni insha ya masimulizi
akizingatia kanuni zifaazo.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kuchangamkia utunzi mzuri wa
insha ya masimulizi.
D. Saru:Nyakatinahali
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 167)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vya nyakati kwenye vitenzi.
b) Kutambua vitenzi katika nyakati tofauti hali ya kuendelea kwenye matini.
ch) Kutunga sentensi akitumia vitenzi katika nyakati mbalimbali hali ya kuendelea.
Swali dadisi
Ni viambishi vipi hutumika kuwakilisha nyakati mbalimbali katika vitenzi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
shughuli za vikundi darasani na mtandaoni.
Ubunifu unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi.
Hamu ya ujifunzaji inakuzwa mwanafunzi anapofaulu kutunga sentensi
sahihi katika nyakati mbalimbali hali ya kuendelea.
Ujuzi wa kidijitali unakuzwa mwanafunzi anapotumia kipakatalishi au
tarakilishi kutunga sentensi na vilevile kuzisambaza mtandaoni.
232
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha - kujitambua na kujithamini anapotunga sentensi na kuzitumia
kujieleza.
Uhusiano na maadili
Heshima anapojifunza kuthamini maoni ya wengine.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili masomo haya yanashughulikia
mada za nyakati na hali.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anakuwa kielelezo kwa wenzake shuleni na nyumbani katika kutumia
Kiswahili kwa kuzingatia kanuni za kisaru.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
maratajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
viambishi
vya wakati
uliopita hali
ya kuendelea
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi
vya wakati
uliopita hali
ya kuendelea
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi
vya wakati
uliopita hali
ya kuendelea
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi
vya wakati
uliopita hali
ya kuendelea
katika baadhi ya
vitenzi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
viambishi
vya wakati
uliopita hali
ya kuendelea
katika vitenzi.
Kutambua
viambishi vya
wakati uliopo
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
wakati uliopo
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
wakati uliopo
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
wakati uliopo
katika baadhi ya
vitenzi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
viambishi vya
wakati uliopo
katika vitenzi.
233
Kimeidhinishwa na KICD
Kutambua
viambishi vya
wakati ujao hali
ya kuendelea
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
wakati ujao hali
ya kuendelea
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
wakati ujao hali
ya kuendelea
na kuvitumia
katika sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
wakati ujao hali
ya kuendelea
katika baadhi ya
vitenzi.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
viambishi vya
wakati ujao hali
ya kuendelea
katika vitenzi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona, mbali waketi karibu na ubao. Wasioweza
kuona vitu vilivyo karibu nao waketi mbali na ubao ili waweze kuona vitenzi
vitakavyoandikwa ubaoni vya nyakati mbalimbali hali ya kuendelea.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema, watazame vitenzi vya nyakati
mbalimbali hali ya kuendelea, wasome maelezo kuvihusu ubaoni, kwenye kiwambo
cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au kwenye chati.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kutambua vitenzi kwa urahisi wahusishwe katika
shughuli zaidi za ujifunzaji na wapewe muda zaidi wa kujifunza. Wahimizwe kwa
upendo ili wajithamini na kuchangamkia ujifunzaji. Hatua yoyote wanayopiga
katika ujifunzaji itambuliwe na mwalimu ili wawe na hamu ya kujifunza zaidi.
Maelezo ya jumla
Mada hii ya saru inalenga kumwezesha mwanafunzi kutumia lugha kwa usanifu
hasa akizingatia nyakati na hali tofauti. Nyakati na hali zinapotumiwa kwa usahihi
huimarisha mawasiliano na ujumbe unaowasilishwa hueleweka vyema zaidi.
Kipindi cha 1: Wakati uliopita hali ya kuendelea
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 167)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua kiambishi cha wakati uliopita hali ya kuendelea katika sentensi.
b) Kutunga sentensi sahihi katika wakati uliopita hali ya kuendelea.
ch) Kuandika upya sentensi kutoka katika wakati wowote hadi katika wakati uliopita
hali ya kuendelea.
Swali dadisi
Ni viambishi vipi hutumika kuwakilisha wakati uliopita hali ya kuendelea?
234
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Matendo ambayo tayari yameshafanyika huwa katika wakati uliopita na kiambishi
kinachotumika ni -li-. Mfano: Wafanyakazi walitozwa ushuru. Vitendo vinapoendelea
kutendwa katika wakati uliopita huwa katika wakati uliopita hali ya kuendelea na
viambishi vyake ni likuwa- na ki-.
Mfano: Mtoto alikuwa akinywa maziwa mama alipoingia.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 167, 2. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwashirikisha wanafunzi wawili wawili katika
shughuli ya kwanza ya kujadiliana. Wanafunzi wajadiliane kuhusu maswali yaliyo
kitabuni mwao. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi kulingana na maswali
husika. Wanafunzi watakaopata changamoto waelekezwe.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na mahitaji yao. Waandike aya moja kuhusu likizo ya Disemba iliyopita.
Mwanafunzi mmoja kutoka katika kila kikundi awasomee wanafunzi wengine aya
waliyoandika ili waisikilize na kuchunguza wakati uliotumika. Mwalimu atathmini
vifungu vya wanafunzi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kushiriki katika shughuli ya tatu katika vikundi
vya wanafunzi wawili wawili. Mwalimu akubali majibu ya wanafunzi yaliyo sahihi.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua kuwa hali ya kitendo kuendelea katika
wakati uliopita huwa wakati uliopita hali ya kuendelea.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya nne. Wanafunzi
wapigie mstari viambishi -likuwa- na -ki- katika kila sentensi waliyopewa. Wanafunzi
watunge sentensi tano kuonyesha wakati uliopita hali ya kuendelea. Watathmini
sentensi zao. Mwalimu awasaidie wanafunzi wanaotatizika.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi abadilishe
vitenzi vilivyo mabanoni viwe katika wakati uliopita hali ya kuendelea. Awasomee
wenzake darasani ili wazisahihishe sentensi zake.
Majibu tarajiwa:1.Wakulima walikuwa wakipalilia mimea mvua ilipoanza. 2. Mpishi
alikuwa akioka mikate tulipowasili. 3. Wasari walikuwa wakikata tiketi gari lilipowasili.
4. Meza ilikuwa ikipakwa rangi na seremala. 5. Rununu ilikuwa ikitengenezwa na fundi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua viambishi vya wakati
uliopita pamoja na viambishi vya wakati uliopita hali ya kuendelea.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutunga sentensi katika wakati
uliopita hali ya kuendelea na kuzibadilisha sentensi kutoka wakati wowote hadi
kwa wakati uliopita hali ya kuendelea.
235
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2: Wakati uliopo
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 169)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vya wakati uliopo.
b) Kutunga sentensi katika wakati uliopo.
ch) Kuandika upya sentensi kutoka katika wakati wowote hadi katika wakati uliopo.
Swali dadisi
Ni viambishi vipi ambavyo hutumika katika wakati uliopo?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Wakati uliopo ni wakati wa sasa. Huonyesha kuwa kitendo kinaendelea sasa hivi.
Kiambishi cha wakati uliopo kwenye kitenzi ni -na-.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 169, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize kipindi kwa kuwashirikisha wanafunzi katika shughuli ya
kwanza. Wanafunzi wawili wawili wajadiliane kuhusu maswali yaliyo kitabuni mwao.
Waelezane kuhusu vitendo vinavyofanyika sasa hivi wakirejelea maswali waliyopewa.
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya shughuli ya pili. Mwanafunzi asome
sentensi zilizo kitabuni mwao kisha apigie mistari viambishi vya wakati uliopo. Majibu
tarajiwa: Mwanafunzi apigie mstari kiambishi -ni- katika kila sentensi. Mwanafunzi
akiwa na mwenzake waandike upya sentensi walizosoma ziwe katika wakati uliopita.
Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi.
Katika vikundi, mwalimu awaelekeze wanafunzi kutumia tarakilishi kufanya shughuli
ya tatu. Wanafunzi watunge sentensi sahihi wakitumia vitenzi walivyopewa kitabuni
mwao katika wakati uliopo. Wazitume sentensi hizo kwa wenzao mtandaoni
ili waziandike upya katika wakati uliopita. Wanafunzi watathmini sentensi zao.
Mwalimu awasaidie wanafunzi wanaotatizika.
Ili kuhitimisha kipindi, mwalimu ampe mwanafunzi maelekezo ya kuifanya kazi ya
ziada. Mwanafunzi abadilishe sentensi alizopewa kitabuni mwao ziwe katika wakati
uliopo. Awasomee wenzake sentensi hizo darasani ili wazitathmini na kuziboresha.
Majibu tarajiwa: 1. Ninaripoti hatari zozote. 2. Ninawaona askari wakishika doria.
3. Unasaidia polisi kukamata wezi. 4. Unazisoma matini za kidijitali. 5. Mwalimu
anaitathmini kazi yangu.
236
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua viambishi vya wakati
uliopo na kutunga sentensi katika wakati uliopo.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kubadilisha sentensi kutoka
kwa wakati wowote hadi kwa wakati uliopo.
Kipindi cha 3: Wakati ujao hali ya kuendelea
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 171)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua viambishi vya wakati ujao hali ya kuendelea.
b) Kutunga sentensi sahihi katika wakati ujao hali ya kuendelea.
ch) Kubadilisha sentensi kutoka katika wakati wowote hadi katika wakati ujao hali
ya kuendelea.
Swali dadisi
Ni viambishi vipi hutumika kuwakilisha wakati ujao hali ya kuendelea?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutambua kuwa: kiambishi cha wakati ujao ni -ta-.
Viambishi vya wakati ujao hali ya kuendelea ni -takuwa- na –ki-.
Mfano: Mtoto atakuwa akinywa maziwa kila siku.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 171, 2. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu atangulize somo kwa kuwaelekeza wanafunzi wajibu maswali yaliyo kitabuni
mwao katika shughuli ya kwanza. Kazi hii ifanywe katika vikundi kulingana na idadi
na mahitaji ya wanafunzi. Majibu ya wanafunzi yawe na kiambishi -ta-. Wanafunzi
wayaandike majibu yao kwa kutunga sentensi katika madaari yao. Mwalimu atathmini
majibu yao na kuwakosoa kwa mujibu wa majibu yao.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya pili. Wajadiliane
kuhusu maswali yaliyo kitabuni mwao na wayaandike majibu yao katika madaari yao.
Majibu yawe na viambishi -takuwa- na -ki-. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Wanafunzi wawili wawili washiriki katika shughuli ya tatu kwa kupigia mstari
viambishi vya wakati ujao hali ya kuendelea kwenye sentensi zilizo kitabuni mwao.
Wanafunzi watunge sentensi tano sahihi katika wakati ujao hali ya kuendelea. Baadaye,
237
Kimeidhinishwa na KICD
wazibadilishe sentensi walizotunga ziwe katika wakati uliopita hali ya kuendelea.
Wanafunzi watathmini sentensi zao. Mwalimu atathmini sentensi za wanafunzi pia.
Mwalimu ahitimishe kipindi kwa kumpa mwanafunzi maelekezo ya kufanya kazi
ya ziada. Mwanafunzi aandike upya sentensi alizopewa kitabuni mwao kulingana
na wakati ulio katika mabano. Majibu tarajiwa: 1. Kazana alikuwa na kipawa cha
uchoraji. 2. Ulimwengu utakuwa ukifaidika kutokana na teknolojia. 3. Watoto wa kike
na wa kiume wanakuwa na haki sawa. Watoto wa kike na wa kiume wana haki sawa.
4. Chuki na ukabila vinakomeshwa nchini Kenya. 5. Mtaala mpya wa elimu utakuwa
ukiwafaidi Wakenya.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutambua viambishi vya wakati
ujao pamoja na vya wakati ujao hali ya kuendelea.
2. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kutunga sentensi katika wakati
ujao hali ya kuendelea.
3. Mwalimu atathmini uwezo wa mwanafunzi wa kubadilisha sentensi kutoka
kwa wakati wowote hadi kwa wakati ujao hali ya kuendelea.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu atathmini maana ambazo mwanafunzi ataeleza. Mwanafunzi anaweza
kutumia kamusi yoyote ya Kiswahili au hata mtandao. Majibu ni kama vile:
a) Tembo ni ndovu (mnyama mkubwa wa porini mwenye nguvu nyingi zaidi na
masikio makubwa),
b) Mbilikimo ni mtu mfupi ajabu,
ch) Korongo ni ndege mwenye shingo na miguu mirefu.
2. Mwalimu atathmini tashbihi ambazo mwanafunzi atatunga. Sharti tashbihi hizo
zitumie maneno aliyoelezea maana katika swali la 1. Mifano ni kama vile:
a) Mwenye nguvu kama tembo.
b) Mfupi kama mbilikimo.
ch) Ana miguu mirefu kama korongo.
2. Mwanafunzi atumie tashbihi alizobuni katika swali la 2 kubuni kisa chochote cha
aya moja. Mwalimu ahakikishe kuwa kisa hicho kinahusisha tashbihi alizotunga.
Mwanafunzi ana uhuru wa kuongeza tashbihi nyingine katika kisa atakachotunga.
Kisa hicho kiwe na mtiririko unaoeleweka.
3. Mwanafunzi asome matini yoyote inayohusu usalama kutoka mtandaoni kwa
kutumia rununu au tarakilishi. Kisha, aandike muhtasari wa kifungu hicho.
Mwalimu atathmini muhtasari ambao mwanafunzi ataandika. Ahakikishe
238
Kimeidhinishwa na KICD
muhtasari huo unahusu usalama na unatiririka. Mwalimu atathmini mafunzo
ambayo mwanafunzi alipata kutokana na muhtasari alioandika.
4. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi atatunga. Mwanafunzi atunge
sentensi sahihi kwa kutumia maneno aliyopewa. Sentensi hizo ziwe katika wakati
uliopo. Mifano:
a) Mwizi anamvamia jirani yetu.
b) Mama anaandika ripoti kuhusu kesi ile.
5. Mwalimu atathmini sentensi za mwanafunzi. Sharti mwanafunzi abadilishe sentensi
alizotunga katika swali la 5 ziwe katika wakati uliopita. Mifano:
a) Mwizi alimvamia jirani yetu.
b) Mama aliandika ripoti kuhusu kesi ile.
7. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi ataandika. Sharti sentensi hizo
ziwe zile alizoandika katika swali la 6 na ziwe katika wakati ujao hali ya kuendelea.
Mifano:
a) Mwizi atakuwa akimvamia jirani yetu.
b) Mama atakuwa akiandika ripoti kuhusu kesi ile.
8. Mwalimu atathmini insha ambayo mwanafunzi ataandika. Insha hiyo iwe ya
masimulizi na ihusu kisa chochote cha uhalifu ambacho mwanafunzi amewahi
kushuhudia au kusikia kilitendeka. Mwalimu ahakikishe insha hiyo imeandikwa
kwa kuzingatia muundo sahihi wa insha ya masimulizi. Insha hiyo itiririke vizuri
kimatukio.
9. Mwanafunzi aandike majukumu mbalimbali ya polisi. Mwalimu atathmini majibu
ya mwanafunzi. Mifano ya majukumu ya polisi ni: kulinda usalama wa wananchi,
kuwakamata wezi, kuelekeza magari barabarani n.k.
10. Mwalimu atathmini jibu la mwanafunzi. Mwalimu ahakikishe mwanafunzi anataja
mtu ambaye anaweza kuwajibika wakati wa hatari. Mwanafunzi aeleze umuhimu
wa kuripoti anapokumbana na hatari. Kwa mfano: ili kupata msaada, ili kuzuia
watu wengine kupatwa na madhara n.k.
239
Kimeidhinishwa na KICD
MAPATO
11
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 174)
A. Kusikiliza na Kuzungumza
Kuzungumza na kujieleza kwa ufasaha
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kusimulia tungo kwa kuzingatia mada, ubunifu na usanifu mbele ya wenzake.
b) Kutumia ishara zifaazo ili kuimarisha masimulizi yake.
Swali dadisi
Je, ni nini unachozingatia unapotoa masimulizi?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga na kusimulia visa mbalimbali.
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki mijadala
katika vikundi.
Kujiamini - kunakuzwa mwanafunzi anaposimulia visa mbele ya wenzake.
Hamu ya kuendelea kujifunza - inakuzwa mwanafunzi anapochangamkia
masimulizi na kuendelea kusoma matini yenye visa vya mazingira mbalimbali.
Elimu kwa maendeleo endelevu - inakuzwa mwanafunzi anapopata uelewa wa
fedha na masuala ya uchumi katika mada ya mapato.
Uhusiano na masuala mtambuko
Ujuzi na matumizi ya fedha anaposimulia kuhusu mapato.
Ushirikishwaji wa wazazi au walezi na ujifunzaji wa huduma za jamii -
mwanafunzi anapaswa kuwashirikisha walezi wake pamoja na jamii katika
mambo anayojifunza shuleni kupitia kwa kazi za ziada.
Programu za kusaidia wanafunzi - kupitia mada ya mapato, mwanafunzi
ataweza kufahamu programu ambazo anaweza kushiriki ili kujipatia riziki na
kujitegemea maishani hasa baada ya kuhitimu masomo ya shuleni.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - mwanafunzi anapokamilisha shughuli mbalimbali za ujifunzaji.
Haki za kijamii mwanafunzi anapoweza kuimarisha uhusiano kati yake na
240
Kimeidhinishwa na KICD
jamii na kupata nafasi ya kujiendeleza maishani na kudumisha usawa katika
jamii.
Amani - mwanafunzi anapojitambua na kubaki mtulivu na mnyenyekevu licha
ya mazingira yanayomzunguka hasa anapojifunza na katika maisha ya baadaye.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na masomo ya Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia
ufasaha wa kusema kwa ubunifu.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi asimulie kuhusu mapato kwa wenzake katika miktadha mbalimbali.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kubuni na
kusimulia
tungo kwa
kuzingatia
ujumbe, ufasaha
wa lugha na
ishara zifaazo.
Mwanafunzi
anabuni na
kusimulia tungo
kwa kuzingatia
ujumbe, ufasaha
na lugha ishara
zifaazo kwa
urahisi.
Mwanafunzi
anabuni na
kusimulia tungo
kwa kuzingatia
ujumbe, ufasaha
wa lugha na
ishara zifaazo.
Mwanafunzi
anabuni na
kusimulia tungo
kwa kuzingatia
ujumbe.
Mwanafunzi
anajaribu
kubuni na
kusimulia
tungo.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasioweza kungamua wanayojifunza kwa urahisi, wapatiwe muda zaidi
wa kujifunza. Mwalimu aepuke kuwakosoa kwa mtazamo hasi ili kuwawezesha
kujithamini na kuwa na hamu ya kujifunza zaidi. Wapongezwe kwa hatua yoyote
wanayopiga katika kujifunza.
Wanafunzi wanaoweza kung’amua wanayojifunza upesi, wapewe shughuli zaidi
za ujifunzaji au majukumu mengine darasani. Hii ni kuhakikisha wanaendelea
kujifunza baada ya kukamilisha shughuli zao za ujifunzaji kabla ya wengine.
Wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali ya afya washughulikiwe na kupewa shughuli
za ujifunzaji kulingana na mahitaji yao.
Maelezo ya jumla
Mada ya mapato itamwezesha mwanafunzi kujifunza njia mbalimbali za kujipatia
riziki maishani kupitia simulizi atakazosikiliza na kusoma. Ni mada inayomtayarisha
mwanafunzi kukabiliana na changamoto za kiuchumi hasa baada ya kuhitimu masomo.
Baada ya kushiriki katika miradi ya kujipatia mapato shuleni na nyumbani, mwanafunzi
ataweza kuthamini shughuli za kibiashara na baadaye kushiriki katika maendeleo ya
taifa na ulimwengu kwa jumla.
241
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 174)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusimulia tungo kwa kuzingatia mada, ubunifu na usanifu wa lugha mbele ya
wenzake.
b) Kutumia ishara zifaazo ili kuimarisha masimulizi yake.
Swali dadisi
Je, ni nini unachozingatia unapotoa masimulizi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapoweza kusimulia visa mbalimbali ataimarisha mawasiliano
yake katika jamii. Ataweza kujithamini na kuwa huru kukiri kwa kina ili kutatua
changamoto zinazoikumba jamii.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 174, 2. Kanda iliyorekodiwa,
3. Mgeni mwalikwa, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje masimulizi
ambayo wamewahi kusikiliza. Mwalimu awahusishe wanafunzi katika shughuli ya
kwanza. Ateue vikundi vinne vya wanafunzi wawili wawili na kuwaongoza kuigiza
mazungumzo yaliyo kitabuni mwao. Mwalimu awaulize wanafunzi wajibu maswali
yaliyo kitabuni mwao.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kuwauliza wasikilize
masimulizi yatakayosimuliwa na mgeni mwalikwa. Wanafunzi wajibu maswali
waliyopewa kitabuni mwao kutokana na masimulizi waliyosikiliza. Masimulizi
ya mgeni mwalikwa yalenge njia mbalimbali za watu kujipatia mapato. Mwalimu
amchague mgeni mwalikwa mwenye matamshi na lugha sahihi. Pia, mwalimu anaweza
kutunga kisa na kuwasimulia wanafunzi darasani.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi katika vikundi watazame
michoro iliyo kitabuni mwao. Wajadili shughuli zinazoendelea katika michoro hiyo.
Waelezane iwapo wanawajua watu wanaofanya kazi zilizo katika michoro hiyo. Majibu
tarajiwa: Mhasibu anawahudumia wateja katika benki, mwanamke anaendesha
baiskeli akiwa na mteja wake, watu wanasasha magari, polisi anawaelekeza madereva
barabarani.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
kuhusu kazi ambayo mlezi wake hufanya ili kujipatia riziki. Amhusishe mlezi wake
kufanya kazi hiyo.
242
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua maana ya masimulizi.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua njia mbalimbali za
kujipatia riziki.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kusimulia tungo kwa
kuzingatia mada, ubunifu na usanifu wa lugha mbele ya wenzake.
Kipindi cha 2: Kutoa masimulizi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 175)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kusimulia tungo kwa kuzingatia mada, ubunifu na usanifu wa lugha mbele ya
wenzake.
b) Kutumia ishara zifaazo ili kuimarisha masimulizi yake.
Swali dadisi
Je, ni nini unachozingatia unapotoa masimulizi?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae video ambayo atawaonyesha wanafunzi wakati wa kipindi. Ahakikishe
ina watu wanaofanya shughuli mbalimbali za kujipatia riziki. Mwalimu ana uhuru wa
kubuni nyenzo na shughuli nyingine za ujifunzaji kando na zilizopendekezwa katika
kipindi hiki mradi ziweze kuakia matokeo tarajiwa ya kipindi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 175,
2. Noti na sarafu mpya za pesa za Kenya,
3. Tarakilishi na projekta,
4. Breli,
5. Mti wenye msamiati wa mapato,
6. Kanda iliyorekodiwa watu wanaofanya kazi mbalimbali.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi hiki kwa kuwauliza wanafunzi wataje
walichojifunza katika kipindi kilichopita. Katika shughuli ya kwanza, mwalimu
awaonyeshe wanafunzi video kuhusu njia mbalimbali za watu kujipatia mapato. Baada
ya kutazama video, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kisha wajadiliane
jinsi watu wanavyojipatia riziki kutokana na video waliyotazama.
243
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya pili katika vikundi. Wajadiliane
kuhusu umuhimu wa watu kujitafutia riziki. Awaongoze wanafunzi kubuni masimulizi
kuhusu waliyojadili na kuyaandika katika madaftari yao. Mmoja wao awasomee
wenzake masimulizi hayo ili wayasikilize na kuyaboresha.
Katika shughuli ya tatu mwalimu awaulize wanafunzi katika vikundi wajadiliane
kuhusu umuhimu wa kazi ya mhubiri/padri/shehe, mpishi hotelini na mwimbaji
wa nyimbo zozote. Pia, mwalimu awaelekeze wanafunzi katika vikundi vyao wajibu
maswali 2a)- d) yaliyo kitabuni mwao. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
kujibu maswali
Mwalimu amwulize mwanafunzi atumie mtandao kuzitafuta pesa mpya zinazotumiwa
nchini Kenya katika kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike rangi za pesa hizo pamoja na
vitu, watu au wanyama wanaoonekana kwenye pesa hizo. Mwalimu atathmini majibu
ya mwanafunzi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini hoja za majadiliano ya wanafunzi kuhusu jinsi ya kujipatia
riziki.
2. Mwalimu atathmini ujasiri wa mwanafunzi, ubunifu na ufasaha anapowasiliana
na wenzake.
B. Kusoma: Kusoma kwa ufahamu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 177)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa mapato uliotumiwa katika hadithi ili kuimarisha
ufahamu.
b) Kutumia msamiati lengwa kwa usahihi katika sentensi.
ch) Kusoma kifungu kwa ufasaha ili kuimarisha ufahamu.
d) Kuonyesha ufahamu wa kifungu kwa kutoa muhtasari na kujibu maswali.
Maswali dadisi
1. Unajua shughuli gani za mapato?
2. Je, kwa nini mapato ni muhimu?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoigiza matukio yanayohusu shughuli za
mapato.
244
Kimeidhinishwa na KICD
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kiteknolojia
kutazama vibonzo na michoro kwenye video na tarakilishi.
Hamu ya ujifunzaji inakuzwa mwanafunzi anapotafakari maswali dadisi na
anapoendelea kuimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Uhusiano na masuala mtambuko
Ujuzi na matumizi ya fedha mwanafunzi anapotumia msamiati wa mapato.
Ushirikishwaji wa wazazi au walezi na ujifunzaji wa huduma za jamii -
mwanafunzi anapomshirikisha mzazi na jamii katika mradi wa kujipatia
mapato.
Uraia - kutokana na kufanya kazi pamoja.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu - mwanafunzi anapotumia lugha ya heshima katika kazi za
makundi.
Uwajibikaji - mwanafunzi anapokamilisha shughuli mbalimbali za ujifunzaji.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza somo hili linashughulikia shughuli za ufahamu.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi awahamasishe wenzake shuleni na nyumbani kuhusu mapato.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kueleza na
kutumia
msamiati
lengwa katika
tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza
msamiati
lengwa na
kuutumia
katika tungo
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anaeleza
msamiati
lengwa na
kuutumia katika
tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anaeleza baadhi
ya msamiati
lengwa na
kuutumia katika
tungo kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kueleza
msamiati
lengwa.
245
Kimeidhinishwa na KICD
Kujibu maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajibu maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anajibu maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajibu baadhi
ya maswali
yanayolenga
ujumbe,
matukio na
wahusika katika
kifungu kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kujibu maswali
yanayolenga
ujumbe na
wahusika katika
kifungu.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona wasome kifungu kwa kutumia breli. Pia,
wasikilize maana ya msamiati wa mapato kutoka kwa wenzao, mwalimu au rekoda.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusimama washirikishwe katika shughuli
kwa kupatiwa majukumu yasiyowahitaji kusimama.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusema, waandike majibu ya maswali ya ufahamu
kwenye madaari, tabuleti au watumie lugha ishara ikiwa mwalimu anaifahamu.
Maelezo ya jumla
Kusoma msamiati na tungo mbalimbali zinazohusu mapato kutaboresha mawasiliano
ya mwanafunzi katika jamii.
Kipindi cha 1: Kifungu cha ufahamu
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 177)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua msamiati wa mapato uliotumiwa katika hadithi ili kuimarisha
ufahamu.
b) Kutumia msamiati lengwa kwa usahihi katika sentensi.
ch) Kusoma kifungu kwa ufasaha ili kuimarisha ufahamu.
Maswali dadisi
1. Unajua shughuli gani za mapato?
2. Je, kwa nini mapato ni muhimu?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae nyenzo muhimu atakazohitaji kulingana na mahitaji ya wanafunzi
kabla ya kipindi.
246
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 177,
2. Breli,
3. Mti wenye msamiati wa mapato.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje mambo
waliyojifunza katika kipindi kilichotangulia.
Mwalimu awahusishe wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Awagawe wanafunzi
katika vikundi kisha wajadili shughuli zinazoendelea katika michoro iliyo kitabuni
mwao. Majibu tarajiwa: Mtoto anawalisha ndege, mtoto na mlezi wake wanauza mayai
sokoni, mtoto anafundishwa kuvua samaki, mtoto anafundishwa kushona. Mwalimu
atathmini majibu ya wanafunzi kulingana na michoro iliyopo. Wanafunzi wajadiliane
kuhusu maswali yaliyo kitabuni mwao.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kuwaelekeza wasome
kifungu kilicho kitabuni mwao. Wajibu maswali ya kifungu. Majibu tarajiwa: 1. Bahati
na Raha waliuza magazeti makuukuu. 2. Bahati na Raha walinunua sungura wawili na
vitabu vya hadithi. 3. Baada ya kuhitimu masomo na kuwa na biashara zilizosajiliwa.
4. Mwalimu akubali majibu yanayohusiana na umuhimu wa mapato. 5. Wanafunzi
watumie kamusi. 6. Mwanafunzi aandike muhtasari wa kifungu walichosoma.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amwelekeze mwanafunzi atazame mti wa maneno
ulio kitabuni mwao kisha atambue misamiati inayohusu mapato. Aeleze maana za
misamiati hiyo. Anaweza kutumia kamusi au mtandao kisha atunge sentensi sahihi
akitumia misamiati hiyo.
Mwalimu amhimize mwanafunzi afanye kazi ya ziada kwa kuandika umuhimu wa
kulipa ushuru. Mwanafunzi anaweza kumhusisha mlezi, mzazi au atumie mtandao.
Mwanafunzi atati kuhusu kinachoweza kumtendekea mwananchi asiyelipa ushuru.
Pia, afahamu malipo mengine ambayo wananchi hulipa serikali isipokuwa ushuru.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua shughuli mbalimbali za
kujipatia mapato.
2. Mwalimu asikilize mwanafunzi akitoa maelezo kuhusu maana ya misamiati ya
mapato na kutathmini.
3. Mwalimu asahihishe sentensi ambazo mwanafunzi ameandika kuhusu
umuhimu wa kulipa ushuru.
247
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 2: Kifungu cha hadithi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 180)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia msamiati wa mapato kwa usahihi katika sentensi.
b) Kuonyesha ufahamu wa kifungu kwa kutoa muhtasari na kujibu maswali.
Maswali dadisi
1. Watu hujipatia mapato vipi?
2. Je, kwa nini mapato ni muhimu?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu atembelee soko ambalo anatarajia kuwapeleka wanafunzi kufanya ziara
kabla ya siku ya ziara na aombe idhini ya kuwapeleka wanafunzi huko. Pia, awaarifu
viongozi wa shule kama vile mwalimu mkuu kuhusu ziara hiyo.
Mwalimu awahusishe walimu wa masomo mengine katika ziara hiyo ili wanafunzi
waweze kuhusisha shughuli za kipindi hicho na masomo mengine. Walimu hao pia
watasaidia kulinda usalama wa wanafunzi sokoni.
Awafahamishe wanafunzi kuhusu usalama wao watakapokuwa sokoni kama vile
kutochukua vitu ambavyo hawajanunua au kupewa vitu na watu wasiowajua.
Mwalimu abebe vifaa vya kurekodi shughuli za ujifunzaji kama vile kamera. Awaeleze
wanafunzi kuhusu matokeo maalumu anayotarajia kutoka kwa ujifunzaji wao pale
sokoni.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 180, 2. Kamera,
3. Kitabu cha kuandika mambo ya ziara ya sokoni.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje walichojifunza
katika kipindi kilichopita. Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaongoze wanafunzi
katika ziara ya sokoni. Awaulize wajibu maswali 1- 6 yaliyoorodheshwa katika kitabu
chao. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi kwa kurejelea soko walilozuru. Baada
ya ziara, wanafunzi waigize darasani shughuli walizoona sokoni. Mwalimu atathmini
maigizo hayo.
248
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu amshirikishe mwanafunzi katika shughuli ya pili kwa kumwagiza ajadiliane
na wenzake katika vikundi kuhusu serikali inakotoa pesa za matumizi yake. Pia,
wajadili kuhusu serikali inavyotumia pesa zake.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaulize wanafunzi katika vikundi wajadiliane
kuhusu shughuli wanazoweza kufanya wakati wa likizo ili kupata mapato. Pia, kila
mwanafunzi aandae bajeti ya jinsi anavyoweza kutumia shilingi elfu kumi. Awaonyeshe
wenzake katika kikundi chake.
Katika kazi ya ziada, mwanafunzi ajadiliane na mlezi au mzazi wake kuhusu madhara
ya ukosefu wa mapato. Aandike hoja hizo katika daari lake kisha atawaeleza wenzake
darasani ili wajifunze.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini uchunguzi wa wanafunzi kuhusu soko walilozuru.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ametambua jinsi serikali hupata pesa
za matumizi yake
3. Mwalimu akague bajeti ya mwanafunzi kulingana na mahitaji muhimu zaidi.
CH. Kuandika: Kuandika Barua
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 181)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika barua ya kiraki kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
Maswali dadisi
1. Je, unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
2. Barua za kiraki zina umuhimu gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapoandika barua ya kiraki.
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki katika
mijadala na kazi za vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kiteknolojia
kuandika insha mtandaoni na kurejelea vielelezo vya barua ya kiraki.
Hamu ya ujifunzaji inakuzwa mwanafunzi anapotafakari maswali dadisi na
anapoendelea kuimarisha ujuzi wake wa kutumia tarakilishi.
Kujiamini na kujithamini - kunakuzwa mwanafunzi anapotambua barua ya
kiraki na kuweza kuiandika akitumia muundo na mtindo ufaao.
249
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Ujuzi na matumizi ya fedha unajitokeza katika kushughulikia mapato
yanayotokana na shughuli mbalimbali.
Uraia - kutokana na kufanya kazi pamoja.
Uhusiano na maadili
Heshima na adabu - mwanafunzi anapotumia lugha ya heshima katika kazi za
vikundi.
Uwajibikaji - mwanafunzi anapokamilisha shughuli mbalimbali za ujifunzaji.
Uaminifu - mwanafunzi anapobuni na kuandika barua yake mwenyewe bila
kunakili maandishi ya wenzake.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili masomo haya hushughulikia uandishi kama
mojawapo ya stadi za lugha.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi ataendeleza mawasiliano na wenzake pamoja na wazazi na maraki kwa
kutumia barua ya kiraki.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kuandika barua
ya kiraki kwa
kuzingatia
ujumbe, muundo,
mpangilio mzuri
wa mawazo na
lugha yenye
ubunifu.
Mwanafunzi
anaandika
barua ya kiraki
kwa kuzingatia
ujumbe,
muundo,
mpangilio mzuri
wa mawazo na
lugha yenye
ubunifu wa hali
ya juu.
Mwanafunzi
anaandika
barua ya kiraki
kwa kuzingatia
ujumbe,
muundo,
mpangilio mzuri
wa mawazo na
lugha yenye
ubunifu.
Mwanafunzi
anaandika
barua ya kiraki
kwa kuzingatia
baadhi ya
vipengele vya
insha husika.
Mwanafunzi
anajaribu
kuandika
barua ya
kiraki.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona watambue barua ya kiraki kwa kurejelea
vielelezo vya barua za kiraki zilizoandikwa kwa kutumia breli.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuandika kwa kutumia mkono wapewe muda zaidi
ili waweze kuakia matarajio ya kipindi hiki.
250
Kimeidhinishwa na KICD
Wanafunzi wasioweza kusema watumie lugha ishara kujadili kuhusu barua ya
kiraki na pia watazame muundo wake katika matini, ubaoni au kwenye chati.
Maelezo ya jumla
Kuandika barua ya kiraki kutamwezesha mwanafunzi kuimarisha mawasiliano yake
katika jamii.
Kipindi cha 1: Barua ya kiraki
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 181)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua barua ya kiraki kwa kuzingatia muundo.
b) Kuandika barua ya kiraki kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
Maswali dadisi
1. Je, unazingatia nini ili kuandika barua nzuri ya kiraki?
2. Barua za kiraki zina umuhimu gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae nyenzo kulingana na mahitaji ya wanafunzi kabla ya kipindi.
Asisitize uandishi bora wa kila heru ili mwandiko wa mwanafunzi uweze kusomeka
kwa urahisi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 181, 2. Tarakilishi,
3. Chati yenye muundo wa barua ya kiraki, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kumwuliza mwanafunzi ataje chochote
anachokumbuka kuhusu uandishi wa barua ya kirafiki. Mwalimu amhusishe
mwanafunzi katika shughuli ya kwanza kwa kumwuliza ajadiliane na mwenzake
iwapo amewahi kuandika barua ya kirafiki. Wajadiliane kuhusu barua walizowahi
kuandika, kuandikiwa na zilihusu nini.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi wawili wawili wasome
kielelezo cha barua ya kiraki kilicho kitabuni mwao. Wajibu maswali waliyopewa.
Majibu tarajiwa: 1. Ahadi Petero, Jitahidi. 2. Barua ina anwani moja, mtajo, mwili
na hitimisho/mwisho. 3. Lugha iliyotumika si rasmi/inavutia. 4. Barua ilihusu miradi
ambayo Petero na wazazi wake wanaendesha ili kujipatia mapato. Mwalimu akubali
majibu sahihi kulingana na barua husika.
251
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu awashirikishe wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya tatu. Awaongoze
waandike vidokezo watakavyotumia kuandika barua ya kiraki kwa mlezi au mzazi
akimshukuru kwa kumlipia karo na kumtimizia mahitaji mengine.
Katika kazi ya ziada, mwanafunzi atumie vidokezo alivyoandika katika shughuli ya
tatu kuandika barua yenyewe kwa mlezi au mzazi wake kwenye tarakilishi. Awatumie
wenzake insha hiyo mtandaoni ili waisome na kuiboresha.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua muundo wa kuandika
barua ya kiraki.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuandika barua ya kiraki
kwenye tarakilishi na kuwatumia wenzake mtandaoni.
Kipindi cha 2: Barua ya kiraki
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 183)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kuandika barua ya kiraki kwa kuzingatia ujumbe, mtindo na muundo ufaao.
b) Kufahamu umuhimu wa barua katika mawasiliano.
Swali dadisi
Je, barua ya kiraki ina umuhimu gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae nyenzo za ujifunzaji kabla ya kipindi hiki. Ahakikishe vifaa vya
kiteknolojia vinafanya kazi ili kufaulisha shughuli za kipindi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 183, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana
na idadi na mahitaji yao kisha awaulize wajadili kuhusu muundo wa barua ya kiraki.
Pia, wajadiliane kuhusu mambo yanayozingatiwa katika uandishi wa barua ya kiraki.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika vikundi katika shughuli ya pili. Katika
vikundi hivyo, wanafunzi waandike vidokezo vya barua ya kiraki kwa ndugu ya
mmoja wao. Vidokezo hivyo vihusu umuhimu wa kuweka akiba. Watumie tarakilishi
kuandika barua yenyewe. Waihifadhi barua hiyo katika faili kwa jina la ndugu
huyo kisha wawatumie wenzao na mwalimu barua hiyo mtandaoni ili waisome na
kuitathmini.
252
Kimeidhinishwa na KICD
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaongoze wanafunzi kujadili umuhimu wa barua
ya kiraki katika mawasiliano wakiwa katika vikundi.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kubuni na kuandika
barua ya kiraki kwa nyanya au babu yake. Barua hiyo ihusu kutaka kujua maendeleo
ya biashara yake ya ufugaji wa kuku. Pia, aombe kuelezwa faida zinatokana na biashara
hiyo. Mwanafunzi awasomee wenzake barua hiyo darasani ili wasikilize na kuitathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua muundo wa barua ya
kiraki.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua umuhimu wa akiba.
D. Saru:Ukanushaji
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 184)
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya ukanushaji ili kuubainisha.
b) Kutambua maneno yaliyokanushwa katika kundi la maneno.
ch) Kutambua viambishi vya nafsi na wakati katika maneno.
d) Kukanusha maneno na sentensi kwa kuzingatia nafsi na wakati katika
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unajua nafsi gani?
2. Unajua viambishi gani vya nafsi?
3. Unajua viambishi gani vya wakati?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki mijadala
katika vikundi.
Uwazaji wa kina na utatuzi wa matatizo - unakuzwa mwanafunzi anapojaribu
kukanusha maneno na sentensi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia vifaa vya kiteknolojia
kujifunza.
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga na kukanusha sentensi katika
nafsi na nyakati mbalimbali.
253
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na masuala mtambuko
Stadi za maisha mwanafunzi anakuza uwezo wa kukubali na kukabili au
kukataa mambo mbalimbali maishani.
Uhusiano na maadili
Uwajibikaji - mwanafunzi anapokamilisha shughuli mbalimbali za ujifunzaji.
Heshima na ushirikiano - mwanafunzi anaposhirikiana na wenzake katika
vikundi.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia mada ya saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi anapojua saru sahihi atakuwa kielelezo kwa wenzake katika kutumia
Kiswahili ifaavyo.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
viambishi vya
nafsi na wakati
katika maneno
na kukanusha
maneno na
sentensi kwa
kuzingatia
wakati na nafsi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
nafsi na wakati
katika maneno
na kukanusha
maneno na
sentensi kwa
kuzingatia
wakati na nafsi
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
viambishi vya
nafsi na wakati
katika maneno
na kukanusha
maneno na
sentensi kwa
kuzingatia
wakati na nafsi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
viambishi vya
nafsi na wakati
katika maneno
na kukanusha
maneno na
sentensi kwa
kuzingatia
wakati na nafsi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anajaribu
kukanusha
maneno na
sentensi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona wasome maelezo ya ukanusho kwa kutumia
breli. Pia, wasikilize mwalimu anapowaongoza kukanusha sentensi kwa sauti.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia, watazame maneno na sentensi zilizokanushwa
ubaoni au kwenye chati. Pia, mwalimu anaweza kuwaeleza jinsi ya kukanusha
maneno na sentensi kwa lugha ishara iwapo anaifahamu.
Maelezo ya jumla
Mwalimu afahamu kuwa kukanusha ni kukataa. Mwanafunzi anapojua kukanusha
maneno na sentensi ataboresha mawasiliano yake.
254
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Ukanushaji wa maneno na sentensi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 184)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya ukanushaji ili kuubainisha.
b) Kutambua maneno yaliyokanushwa katika kundi la maneno.
Maswali dadisi
1. Unajua nafsi gani?
2. Unajua viambishi gani vya nafsi?
3. Kukanusha ni kufanya nini?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome maelezo yaliyo katika kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi ili
afahamu shughuli atakazowashirikisha wanafunzi. Mwalimu aandae nyenzo kulingana
na mahitaji ya wanafunzi. Mwalimu anaweza kuwagawa wanafunzi katika vikundi
kulingana na idadi na mahitaji yao.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha mwanafunzi, ukurasa 184,
2. Mti wenye vitenzi vilivyokanushwa,
3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaulize wanafunzi wawili wawili waelezane
iwapo wamewahi kuulizwa wafanye vitendo fulani wakakataa. Waeleze vitendo
hivyo vilihusu nini na sababu za kukataa kuvitenda. Mwalimu awaongoze wanafunzi
kutambua kuwa kukataa kutenda kitendo au kukana jambo ni kukanusha.
Mwalimu awashirikishe wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kuwaelekeza watunge
sentensi wakiwa katika vikundi. Waziandike sentensi hizo kwenye madaftari yao
kisha wazikanushe. Katika vikundi vyao, waigize vitendo vya sentensi walizotunga na
walizokanusha. Mwalimu atathmini maigizo yao.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amwulize mwanafunzi atambue maneno
yaliyokanushwa kutoka kwa mti wa maneno ulio kitabuni mwao. Majibu tarajiwa:
usile, msinywe, usioge, msiwapige, msije, usimwambie, usinunue, msiende.
Mwalimu awaagize wanafunzi watumie maneno waliyotambua kwenye mti wa maneno
kutunga sentensi sahihi. Wanafunzi wabadilishane madaari ili wazitathmini sentensi
zao. Wataje nafsi iliyotumika katika kila sentensi.
255
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu amwongoze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada kwa kukanusha sentensi
zilizo kitabuni mwao. Majibu tarajiwa: a) Sitengenezi kitanda. b) Sijauza ng’ombe.
ch) Hatutafagia madarasa yote. d) Sisi hatununui matunda sokoni. e) Hatukuimba
gwarideni. f) Hatufyeki nyasi. Mwalimu amwongoze mwanafunzi kuandika sentensi
alizokanusha katika umoja na wingi. Awasomee wenzake sentensi alizokanusha ili
azitathmini.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ameelewa maana ya kukanusha.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kukanusha sentensi.
3. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ameweza kutambua viambishi vya
nafsi na wakati katika sentensi.
Kipindi cha 2: Ukanushaji wa maneno na sentensi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 186)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua maneno yaliyokanushwa katika kundi la maneno.
b) Kutambua viambishi vya nafsi na wakati katika maneno.
ch) Kukanusha maneno na sentensi kwa kuzingatia nafsi na wakati katika
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unajua viambishi gani vya nafsi?
2. Unajua viambishi gani vya wakati?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asome kitabu cha mwanafunzi kabla ya kipindi ili afahamu shughuli
atakazowashirikisha wanafunzi wakati wa kipindi.
Mwalimu anapowagawa wanafunzi katika vikundi ahakikishe anazingatia idadi na
mahitaji yao.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 186, 2. Breli,
3. Kadi zenye sentensi za kukanushwa.
256
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaelekeze wanafunzi katika shughuli ya kwanza. Awagawe katika vikundi
viwili kisha awaelekeze wacheze mchezo wa kadi zenye sentensi za kukanushwa.
Wazingatie maelekezo ya mchezo yaliyo kitabuni mwao.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya shughuli ya pili. Awaulize wanafunzi wawili
wawili watambue na kupigia mistari viambishi vya nafsi na wakati katika sentensi
walizopewa vitabuni mwao. Wakanushe sentensi walizopewa. Wataje nafsi iliyotumika
katika sentensi hizo.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada ya kukanusha sentensi
alizopewa kitabuni mwake. Apigie mistari viambishi vya nafsi na wakati. Awaonyeshe
wenzake viambishi hivyo darasani. Majibu tarajiwa: a) Hukuteka maji kisimani. b)
Husomi sentensi vizuri. ch) Huji kwangu. d) Hamuuzi bidhaa sokoni. e) Hamjapika
chakula kitamu. f) Hujakaanga nyama.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anatambua maneno yaliyokanushwa.
2. Mwalimu asahihishe utambuaji wa viambishi vya wakati na nafsi katika
sentensi.
Kipindi cha 3: Ukanushaji wa maneno na sentensi
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 186)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutambua maneno yaliyokanushwa katika kundi la maneno.
b) Kutambua viambishi vya nafsi na wakati katika maneno.
ch) Kukanusha maneno na sentensi kwa kuzingatia nafsi na wakati katika
mawasiliano.
Maswali dadisi
1. Unajua viambishi gani vya nafsi?
2. Unajua viambishi gani vya wakati?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwanafunzi anapoweza kukanusha sentensi ataimarisha mawasiliano yake. Mwalimu
aandae nyenzo kulingana na mahitaji ya wanafunzi kabla ya kipindi.
257
Kimeidhinishwa na KICD
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 186, 2. Tarakilishi, 3. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu anaweza kutanguliza kipindi kwa kuwauliza wanafunzi wataje mambo
waliyojifunza katika kipindi kilichotangulia. Mwalimu awahusishe wanafunzi katika
vikundi katika shughuli ya kwanza. Awaulize wasome sentensi zilizo kitabuni mwao na
watambue viambishi vya nafsi na wakati. Wakanushe sentensi hizo. Majibu tarajiwa:
Wao hawakupanda miti mabondeni. b) Hasashi soko lote. ch) Hawatawekeza mapato
yao. d) Hajapata faida baada ya kuuza bidhaa. e) Hakupata hasara baada ya duka lake
kuteketea.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya shughuli ya pili kwa kuwauliza watunge
kifungu cha aya moja wakitumia nafsi ya tatu. Wanafunzi waandike upya aya hiyo kwa
kukanusha vitenzi walivyotumia. Wanafunzi wajadiliane kuhusu walichojifunza.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amwelekeze mwanafunzi atunge na kuandika
sentensi tano kwenye tarakilishi akitumia nafsi yoyote. Azikanushe sentensi hizo.
Mwanafunzi ahifadhi kazi yake katika faili kwa jina lake. Baadaye, awatumie wenzake
na mwalimu sentensi hizo mtandaoni ili wazisome na kuzisahihisha.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Akanushe sentensi zilizo
kitabuni mwake. Majibu tarajiwa:
a) Mkulima hakati mti.
b) Sijatuzwa na mwalimu mkuu.
ch) Hakuenda sokoni na mtoto wake.
d) Yeye hatanyunyizia mmea maji.
e) Mgeni wa heshima hatawasili mapema.
Mwalimu aitathmini kazi hiyo.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kutambua viambishi nafsi na
wakati katika sentensi.
2. Mwalimu atathmini jinsi mwanafunzi anavyotunga na kukanusha sentensi
mtandaoni.
258
Kimeidhinishwa na KICD
Ukubwa na udogo wa nomino
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya ukubwa wa nomino ili kuubainisha.
b) Kutambua nomino zinazoanza kwa heru m- na zenye mzizi wa silabi moja.
ch) Kutambua nomino katika hali ya ukubwa.
d) Kubadilisha nomino katika hali ya wastani kuwa katika hali ya ukubwa.
e) Kutumia nomino katika hali ya ukubwa kwenye sentensi.
Swali dadisi
Ni nomino gani unazoweza kutaja ukubwa wake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi katika hali ya udogo.
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki mijadala
katika vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa wakati mwanafunzi anapotumia tarakilishi
kuambatanisha nomino katika hali ya wastani na ukubwa.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi zenye uraia mwema.
Uhusiano na maadili
Ushirikiano - wanafunzi wanapofanya kazi pamoja.
Uwajibikaji - mwanafunzi anapokamilisha shughuli mbalimbali za ujifunzaji.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakuwa kielelezo cha kutumia lugha kwa ufasaha shuleni na nyumbani.
259
Kimeidhinishwa na KICD
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
nomino
zinazoanza na
heru m- za
mzizi wa silabi
moja kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino
zinazoanza
kwa heru
m- za mzizi
wa silabi moja
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino
zinazoanza
kwa heru
m- za mzizi wa
silabi moja kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
nomino
zinazoanza kwa
heru m- za
mzizi wa silabi
moja.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
nomino
zinazoanza na
heru m- na
mzizi wa silabi
moja.
Kutambua
nomino katika
hali ya ukubwa
na kuzitumia
kwenye sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino katika
hali ya ukubwa
na anazitumia
kwenye sentensi
kwa urahisi na
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino katika
hali ya ukubwa
na anazitumia
kwenye sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
nomino katika
hali ya ukubwa
na vilevile
kuzitumia
kwenye sentensi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino katika
hali ya ukubwa
na anajaribu
kuzitumia
katika sentensi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali ya afya washughulikiwe kulingana na
mahitaji maalumu ya kila mwanafunzi. Mwalimu awe na rekodi ya wanafunzi
hao ili aweze kuwapa huduma ya kwanza kabla ya kutafuta usaidizi zaidi ikiwa
watakumbwa na changamoto wanapojifunza.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona mbali waketi karibu na ubao. Wasioweza
kuona vitu vilivyo karibu nao waketi mbali na ubao ili waweze kuona nomino za
silabi moja zitakazoandikwa ubaoni katika hali ya wastani na ukubwa.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia na kusema watazame nomino za silabi moja
katika wastani na ukubwa, au wasome maelezo kuzihusu ubaoni, kwenye kiwambo
cha tarakilishi, kitabu cha mwanafunzi au kwenye chati.
Maelezo ya jumla
Mada kuhusu ukubwa na udogo wa nomino zenye mzizi wa m- itamwezesha
mwanafunzi kuimarisha mawasiliano yake katika jamii.
260
Kimeidhinishwa na KICD
Kipindi cha 1: Ukubwa wa nomino zinazoanza kwa m- na zenye
mzizi wa silabi moja
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 188)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya ukubwa wa nomino ili kuubainisha.
b) Kutambua nomino zinazoanza kwa heru m- na zenye mzizi wa silabi moja.
ch) Kutambua nomino katika hali ya ukubwa.
Swali dadisi
Ni nomino gani unazoweza kutaja ukubwa wake?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu asiwatumie wanafunzi wenye mwili mkubwa kupita kiasi kufunzia ukubwa
na udogo kwa sababu wanaweza kuwa na mtazamo hasi kujihusu. Mwalimu aandae
nyenzo kulingana na mahitaji ya wanafunzi kabla ya kipindi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 188,
2. Breli,
3. Jedwali lenye michoro ya wastani na kubwa.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awahusishe wanafunzi wawili wawili katika shughuli ya kwanza kwa
kuwauliza watazame na kutaja majina ya michoro iliyo kitabuni mwao. Awaelekeze
watumie majina ya michoro hiyo kutunga sentensi sahihi.
Mwalimu awagawe wanafunzi katika vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao.
Awashirikishe katika shughuli ya pili kwa kuwaelekeza wajadili muundo wa majina
ya michoro waliyotazama katika shughuli ya kwanza. Awaulize waandike majina
mengine yanayoanza na heru m- yaliyo na muundo sawa na majina ya michoro.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu awaelekeze wanafunzi kutazama na kujadili
michoro wakiwa wawili wawili. Baada ya kutazama, watunge sentensi kwa kila mchoro.
Mwalimu awaongoze wanafunzi kujadili walichotambua kuhusu ukubwa na udogo wa
michoro hiyo.
Katika shughuli ya nne, mwalimu awaulize wanafunzi katika vikundi wajaze nafasi
wazi kwenye jedwali walilopewa kitabuni mwao wakitumia ukubwa na udogo kwa
usahihi. Wanafunzi wajadili kuhusu walichogundua.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi aandike
umuhimu wa nomino alizopewa kitabuni mwao. Majibu tarajiwa: a) Mchi hutumiwa
261
Kimeidhinishwa na KICD
kutwangia nafaka. b) Mti hutupatia kivuli, matunda n.k. ch) Mji ni makao ya watu.
d) Mto hutupa maji ya matumizi mbalimbali. e) Mke huwalea watoto.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ametambua majina yanayoanza na
heru m- yenye mzizi wa silabi moja.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ametambua viambishi vya nomino
katika udogo na ukubwa.
Kipindi cha 2: Ukubwa wa nomino zinazoanza kwa m- na zenye
mzizi wa silabi moja
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 190)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kutumia nomino katika hali ya ukubwa kwenye sentensi.
b) Kufahamu kutumia nomino katika hali ya ukubwa kwa usahihi ili kuimarisha
mawasiliano.
Swali dadisi
Unaweza kutaja ukubwa wa nomino gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awe na michoro ya kufunzia ukubwa wa nomino. Awagawe wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao darasani.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 190, 2. Tarakilishi,
3. Jedwali lenye nomino za ukubwa, 4. Breli.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Katika shughuli ya kwanza, mwalimu awaongoze wanafunzi kuambatanisha kwa
usahihi nomino za wastani na za ukubwa zilizo katika jedwali walilopewa kitabuni
mwao. Majibu tarajiwa: mtu - jitu, mji - jiji, mto - jito, mke - jike, mti - jiti.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili. Wanafunzi watumie nomino
walizoambatanisha katika shughuli ya kwanza kutunga sentensi sahihi wakiwa katika
vikundi. Waandike sentensi hizo kwenye tarakilishi. Wawatumie wenzao sentensi hizo
mtandaoni ili wazisome na kuzitathmini.
262
Kimeidhinishwa na KICD
Mwalimu amwongoze mwanafunzi katika shughuli ya tatu atambue nomino zilizo
katika hali ya ukubwa kwenye mraba ulio kitabuni mwao. Majibu tarajiwa: jike, jiji,
jito, jiti, jitu. Mwalimu amwelekeze mwanafunzi atumie nomino alizotambua kutunga
sentensi sahihi. Wanafunzi wasahihishe sentensi zao wakiwa katika vikundi.
Mwalimu amhimize mwanafunzi kufanya kazi ya ziada. Atumie mtandao kutaja
majina ya mito mitano na miji mitatu inayopatikana nchini Kenya. Pia, atafute picha
ya mchi na aichore daarini mwake. Awaeleze wenzake darasani kuhusu aliyoandika.
Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi.
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kuambatanisha nomino za
wastani na za ukubwa kwa usahihi katika jedwali.
2. Mwalimu atathmini sentensi zilizotungwa na mwanafunzi baada ya kutambua
majina ya nomino za ukubwa na wastani.
Ukubwa na udogo wa nomino
Matokeo tarajiwa: Kukia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya udogo wa nomino ili kuubainisha.
b) Kutambua nomino zinazoanza kwa heru m- na zenye mzizi wa silabi moja.
ch) Kutambua nomino katika hali ya udogo.
d) Kubadilisha nomino katika hali ya wastani kuwa katika hali ya udogo.
e) Kutumia nomino katika hali ya udogo kwenye sentensi.
Swali dadisi
Ni nomino gani unazoweza kutaja udogo wake?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa
Ubunifu - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi katika hali ya udogo.
Mawasiliano na ushirikiano - vinakuzwa mwanafunzi anaposhiriki mijadala
katika vikundi.
Ujuzi wa kidijitali - unakuzwa mwanafunzi anapotumia tarakilishi
kuambatanisha nomino katika hali ya wastani na udogo.
Uhusiano na masuala mtambuko
Uraia - unakuzwa mwanafunzi anapotunga sentensi zenye uraia mwema.
263
Kimeidhinishwa na KICD
Uhusiano na maadili
Ushirikiano - wanafunzi wanapofanya kazi pamoja.
Uwajibikaji - mwanafunzi anapokamilisha shughuli mbalimbali za ujifunzaji.
Uhusiano na masomo mengine
Kiingereza na Lugha za kiasili - masomo haya yanashughulikia saru.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji
Mwanafunzi atakuwa kielelezo cha kutumia lugha kwa ufasaha shuleni na nyumbani.
Viwango vya kuzingatia katika kutathmini
Vigezo Kuzidi
matarajio
Kukia
matarajio
Kukaribia
matarajio
Mbali na
matarajio
Kutambua
nomino
zinazoanza na
heru m- za
mzizi wa silabi
moja kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino
zinazoanza
kwa heru
m- za mzizi
wa silabi moja
kwa usahihi na
urahisi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino
zinazoanza
kwa heru
m- za mzizi wa
silabi moja kwa
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
nomino
zinazoanza kwa
heru m- za
mzizi wa silabi
moja.
Mwanafunzi
anajaribu
kutambua
nomino
zinazoanza na
heru m- za
mzizi wa silabi
moja.
Kutambua
nomino katika
hali ya udogo
na kuzitumia
kwenye sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino katika
hali ya udogo
na anazitumia
kwenye sentensi
kwa urahisi na
usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino
katika hali
ya udogo na
anazitumia
kwenye sentensi
kwa usahihi.
Mwanafunzi
anatambua
baadhi ya
nomino katika
hali ya udogo
na vilevile
kuzitumia
kwenye sentensi.
Mwanafunzi
anatambua
nomino katika
hali ya udogo
na anajaribu
kuzitumia
katika sentensi.
Namna ya kuwashughulikia wanafunzi wenye mahitaji mbalimbali
Wanafunzi wasioweza kuona watumie breli kujifunza. Wasio na uwezo wa
kuzungumza watumie lugha ishara.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kuona wasome maelezo ya nomino za wastani na
udogo wakitumia breli. Pia, wanaweza kumsikiliza mwalimu au wanafunzi wenzake
wakisoma nomino na sentensi za wastani na udogo kwa sauti.
Wanafunzi wasio na uwezo wa kusikia watazame nomino na sentensi za wastani
na ukubwa ubaoni au kwenye chati. Pia, mwalimu anaweza kuwaeleza jinsi ya
kuandika udogo wa nomino kwa lugha ishara iwapo anaijua.
264
Kimeidhinishwa na KICD
Maelezo ya jumla
Mada ya udogo wa nomino zenye mzizi wa m- itamwezesha mwanafunzi kuimarisha
mawasiliano yake katika jamii.
Kipindi cha 1: Udogo wa nomino zinazoanza kwa m- na zenye
mzizi wa silabi moja
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 191)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kueleza maana ya ukubwa wa nomino ili kuubainisha.
b) Kutambua nomino zinazoanza kwa heru m- na zenye mzizi wa silabi moja.
ch) Kutambua nomino katika hali ya udogo.
Swali dadisi
Ni nomino gani unazoweza kutaja udogo wake?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu aandae nyenzo atakazohitaji kulingana na mahitaji ya wanafunzi kabla ya
kipindi.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 191, 2. Tarakilishi, 3. Kamusi,
4. Breli, 5. Jedwali lenye nomino za wastani na udogo.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awahusishe wanafunzi katika vikundi katika shughuli ya kwanza. Awaulize
watazame na kujadili kuhusu udogo na ukubwa wa michoro iliyo kitabuni mwao.
Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Mwalimu awaongoze wanafunzi katika shughuli ya pili kwa kuwauliza wajaze nafasi
wazi zilizo katika jedwali walilopewa kitabuni mwao. Watumie majina ya wastani,
ukubwa na udogo. Wanafunzi waelezane walichogundua. Mwalimu atathmini maelezo
yao.
Katika shughuli ya tatu, mwalimu amwongoze mwanafunzi kueleza maana ya nomino
zinazoanza kwa heru m- alizopewa kitabuni mwao. Anaweza kutumia kamusi au
mtandao kupata maana hizo.
Mwalimu amwelekeze mwanafunzi kubuni kifungu cha aya moja kisha akiandike
katika daftari lake akitumia maneno aliyopewa katika kazi ya ziada. Mwalimu
atathmini kifungu cha wanafunzi.
265
Kimeidhinishwa na KICD
Tathmini
1. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi ametambua viambishi vya nomino
katika udogo na ukubwa.
2. Mwalimu atathmini iwapo mwanafunzi anaweza kubadilisha nomino zilizo
katika hali ya wastani na kuwa katika udogo.
Kipindi cha 2: Udogo wa nomino zinazoanza kwa m- na zenye
mzizi wa silabi moja
(Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 193)
Matokeo tarajiwa maalumu: Kukia mwisho wa kipindi, mwanafunzi aweze:
a) Kubadilisha nomino katika hali ya wastani kuwa katika hali ya udogo.
b) Kutumia nomino katika hali ya udogo kwenye sentensi.
ch) Kufurahia kutumia nomino katika hali ya udogo kwa usahihi ili kuimarisha
mawasiliano.
Swali dadisi
Unaweza kutaja udogo wa nomino gani?
Maelezo ya ziada kwa mwalimu
Mwalimu awe na nyenzo za kufunzia udogo wa nomino. Awagawe wanafunzi katika
vikundi kulingana na idadi na mahitaji yao darasani. Ajiandae kabla ya kipindi ili
kufanikisha shughuli za ujifunzaji.
Mapendekezo ya nyenzo za ujifunzaji
1. Kitabu cha Mwanafunzi, ukurasa 193,
2. Breli,
3. Chati yenye nomino za wastani na udogo.
Mapendekezo ya shughuli za ujifunzaji
Mwalimu awaongoze wanafunzi kufanya shughuli ya kwanza. Awaulize wanafunzi
waambatanishe nomino za wastani na za udogo kwa usahihi katika jedwali walilopewa
kitabuni mwao. Mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi.
Katika shughuli ya pili, mwalimu awaongoze wanafunzi kucheza mchezo wa
kubadilisha nomino kutoka kwa wastani hadi udogo wakiwa katika vikundi viwili.
Mwalimu awaelekeze wanafunzi kwa kuzingatia maelezo yaliyo kitabuni mwao.
Wanafunzi wajadiliane kuhusu sentensi walizotunga.
266
Kimeidhinishwa na KICD
Baadaye katika shughuli ya tatu, mwalimu awaulize wanafunzi wawili wawili watunge
sentensi sahihi wakitumia nomino walizopewa kitabuni mwao. Mwalimu akubali
sentensi zozote sahihi zinazohusu maneno husika.
Mwalimu amwongoze mwanafunzi katika kufanya kazi ya ziada. Mwanafunzi
abadilishe sentensi alizopewa kitabuni mwake ziwe katika hali zilizoandikwa
kwenye mabano. Mwanafunzi awasomee wenzake darasani sentensi alizobadilisha ili
wazisikilize na kuzisahihisha.
Tathmini
1. Mwalimu asahihishe jinsi mwanafunzi alivyoambatanisha nomino za wastani
na udogo katika jedwali.
2. Mwalimu atathmini sentensi zilizotungwa na mwanafunzi kwa kutumia majina
ya nomino za udogo.
Majibu ya zoezi la mwisho wa mada
1. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi kuhusu njia zozote ambazo anaweza
kutumia ili kujipatia riziki. Sharti njia hizo ziwe halali na za kiwango cha
mwanafunzi. Mwalimu awahimize wanafunzi kutumia muda wao hasa wa likizo
kujipatia riziki halali.
2. Mwalimu atathmini bajeti atakayounda mwanafunzi ya jinsi ya kutumia shilingi
elfu moja. Mwalimu ahakikishe bajeti hiyo inaonyesha matumizi mazuri ya pesa
hizo. Mwanafunzi afahamu umuhimu wa kuwa na bajeti kila mara anapopata pesa
zozote. Bajeti humsaidia mtu kuzitumia pesa zake vizuri.
3. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi atatunga. Sharti sentensi hizo
ziwe sahihi kisaru na zihusishe maneno waliyopewa. Mifano:
a) Mimi hulipa ushuru. b) Baba alipata faida katika biashara yake.
4. Mwanafunzi aandike barua ya kirafiki kwa rafiki yake akimwalika ahudhurie
harusi ya mwalimu wao. Mwalimu ahakikishe barua hiyo inafuata muundo sahihi
wa kuandika barua ya kiraki. Pia, lugha itakayotumika iwe ya kiraki na sahihi
kisaru.
5. Mwanafunzi aeleze kazi ambazo hufanywa na watu waliotajwa ili kujipatia riziki.
Mifano:
a) Taniboi hukusanya nauli kutoka kwa abiria. Yeye hulipwa mshahara.
b) Mkulima hupanda mimea na kuvuna mazao ambayo huyauza ili kupata pesa.
ch) Kinyozi huwanyoa watu nywele na watu hao humlipa pesa.
267
Kimeidhinishwa na KICD
6. Mwalimu atathmini sentensi ambazo mwanafunzi atakanusha. Sharti ukanusho
ufanyike kwa usahihi. Mifano:
a) Wauzaji hawafagii soko. b) Kibanda hicho hakina matunda.
7. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi kwa kurejelea mazingira yake.
Mwanafunzi ataje wafanyakazi mbalimbali katika shule yao, kwa mfano: walimu,
wapishi, mlinda lango, mhazili n.k.
8. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Majibu ni:
a) kijito b) kijiji
9. Mwanafunzi atunge sentensi sahihi kwa kutumia maneno ya udogo aliyoandika
katika swali la 8. Sentensi ambazo mwanafunzi atatunga zifuate mtindo wa ngeli ya
KI-VI. Mifano:
a) Kijito kile kina maji machache. b) Kijiji chetu kimesashwa.
10. Mwalimu atathmini majibu ya mwanafunzi. Mwanafunzi ataje njia mbalimbali
ambazo watu hutumia pesa vibaya. Kwa mfano: kununua vitu wasivyohitaji, kununua
dawa za kulevya n.k.