Chemchemi
za
Kiswahili
Kidato
cha
2
K.W.
W
amitila
Gichohi
W
aihiga
Kimechapishwa na:
Longhorn Publishers (Kenya)
Ltd., Barabara ya Funzi,Eneo la
Viwandani, S.L.P.18033,
Nairobi.
Longhorn Publishers (Uganda) Ltd.,
Plot M220,Eneo laViwandani la
Ntinda, Barabara ya Jinja,
S.L.P.24745,
Kampala
Uganda.
Longhorn Publishers (Tanzania)
Ltd., Kitalu Na. 664, Eneo la
Msasani, Kitengo F, Jumba Na.
664,
Barabara ya zamani ya
Bagamoyo, S.L.P 1237,
Dar-es-
Salaam,
Tanzania.
© Haki ya kunakili ni ya K.W. Wamitila na G.Waihiga,2003
© Haki ya kunakili michoro ni ya Longhorn Publishers,2003
Haki za kimaadili za waandishi zimezingatiwa.
Haki zote zimehifadhiwa.Hairuhusiwi kuiga,kunakili,kupigisha chapa,kutafsiri au kukitoa kitabu hiki
kwa jinsi yoyote ile bila idhini,kwa maandishi,ya kampuni ya Longhorn Publishers Ltd.
Chapa ya kwanza,2003
Chapa ya nyingine,2004,2005,2007
Kimesahihishwa,2008, 2017
ISBN 978 9966
49
521
5
Kimeruwazwa na Noel Creative Media
Ltd. Jalada limesanifiwa na Noel
Lumbama.
Tunatoa shukrani kwa mashirika yafuatayo kwa kutupa idhini ya kunukuu makala kutoka kwenye
machapisho yao: Gazeti laTaifa Leo kwa makala –‘Kituo cha watoto chafungwa’ (uk.69),Longhorn
Publishers kwa shairi
‘Usafi ni Jambo Bora’ (uk.177) kutoka Kusoma na Kufahamu Mashairi 1 na S.Karama na K.Khan.
Taasisi ya
Kiswahili Zanzibar kwa shairi ‘Tuyazingatie Haya’ (uk.272) na MalengaWapya.
Kimepigwa chapa na ....................................................................
iiiiii
SURA YA
KWANZA
Ufahamu:
Ndugu Majuu na wakazi wa Kibabuu...................................... 1
Kusikiliza
na
Kuzungumza:
Isimu-Jamii
: M a ja d il i an o Mwanafunzi na mwalimu................... 4
Matamshi bora vitate s/sh……................................................................ 5
Saru
na
matumizi
ya
lugha:
Misingi ya maneno……… ...................................................................………..6
Kusoma:
Riwaya Utangulizi .... ........................................................... ..8
Kuandika:
Barua rasmi..………............................................................…..9
SURA YA PILI
Ufahamu:
Kumekucha.............................................................................. 14
Kusikiliza
na
kuzungumza:
Visasili ...........................................................................................................15
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Viambishi. ......................................... .17
Vivumishi…… ................................................................ .........…………….19
Kusoma:
Matumizi ya kamusi… ........................................................... ..20
Kuandika:
Insha ya maelezo…............................................................…..21
SURA YA TATU
Ufahamu:
Utamaduni……..................................................................……24
Kusikiliza
na
kuzungumza:
Isimu-Jamii:
M a z u n g u m z o Hotelini….............. ....... ......................26
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Nomino……............. ....…………………..28
Kuakisha……………… .................................................................... …………30
Kusoma:
Matumizi ya maktaba.. ........................................................... ..33
Kuandika:
Hadithi fupi…….... ........................................................... .....34
SURA YA NNE
Ufahamu:
Bwana Aisee na mradi kabambe…......……… ........……………37
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Methali…………………................ ……………40
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Nomino……………… ........... ………………42
Nyakati na ukanusho............… ...................................................................43
Kuandika:
Ratiba..……....…............................................................ ……. 45
SURA YA TANO
Ufahamu:
Mwanamke ana haki............................................................... 47
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Mjadala ..........................................................50
Yaliyomo
iv
v
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Nomino…........…............... ..………………52
Vielezi ……………….....…… ................................................................ ……53
Ngeli za nomino……........…….................................................................…54
Kusoma:
Mashairi huru…….......................................................................56
Kuandika:
Muhtasari……....… .............................................................. ...…57
SURA YA SITA
Ufahamu:
Chifu Somba na mbuzi wa serikali…….............. ..........…………60
Kusikiliza
na
kuzungumza
:
Isimu-Jamii:
Majadiliano—
Mwalimu na mzazi............ .................................................................. .......... 62
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Uundaji wa maneno……............ .………63
Kusoma:
Kusoma kwa mapana
magazeti…...... .......……………………68
Kuandika:
Mialiko……… .............................................................. ………….70
SURA YA SABA
Ufahamu:
Misitu na faida zake.............................................................…71
Kusikiliza
na
kuzungumza
:
Ufahamu wa kusikiliza………… ...................................................................73
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Vivumishi……............ ...........…....……73
Kuakisha…………..... .........................................................................…………74
Upatanisho wa kisarufi—
kivumishi ‘-enyewe’…… .........................…76
Upatanisho wa kisaru –– viambishi awali vya vitenzi ............................... 77
Kusoma:
Tamthilia —Utangulizi… .............................................................78
SURA YA NANE
Ufahamu:
Shairi Haki zetu
Kusikiliza
na
kuzungumza
:
Isimu-Jamii:
M a z u n g u m z o Hotelini……..... ....................................83
Matamshi bora - vitate d/nd...................................................................... ...85
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Vivumishi………… ............ …………………85
Kusoma:
Tamthilia………..… ............................................................. …….90
Kuandika:
Hotuba…………. ............................................................. …..….91
Zoezi
la
Marudio
1
………… ............................................................ ….….94
SURA YA TISA
Ufahamu:
Nchi za Afrika Mashariki na mustakabali wake............. ... .100
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Hekaya…………………… ............... ……102
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Vivumishi……......……… .......... ……….104
Upatanisho wa kisaru—
kivumishi ‘-ingine’….....…… ...................... …105
iv
v
Upatanisho wa kisaru —
kivumishi ‘-ote’…......… ......................………106
Kusoma:
Matumizi mengine ya kamusi………........…........... …............107
Kuandika:
Utungaji wa kiuamilifu - Matangazo…………….... …………108
SURA YA KUMI
Ufahamu:
Kibwana Jaku na nundu ya maisha…....…… ... ……………110
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Ushairi….....………………................ ………113
Matamshi bora - vitate b/mb…115
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Vivumishi…………............ ………………115
Upatanisho wa kisaru—
kivumishi ‘-ote’….................................………116
Nyakati—Ukanushaji wa wakati ujao kulingana na nafsi......................117
Kusoma:
Majarida......……..… ............................................................…118
Kuandika:
Tahadhari ilani/
onyo.................................. ............. ........119
SURA YA KUMI NA MOJA
Ufahamu:
Mraha na chupa za
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Hotuba……..................... .…………………124
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Usemi halisi na usemi wa
taarifa.……..............……… ..................................................................….126
Upatanisho wa kisaru —
kivumishi ‘-o-ote’…...........…..................... …129
Nyakati - hali ‘me–– kukanusha kulingana na nafsi….......... ......... ......131
Kusoma:
Vitabu vya ziada……............................................................…132
Kuandika:
Ushairi…………… ............................................................….132
SURA YA KUMI NA MBILI
Ufahamu:
Bwana Kaukata na soko la ulimwengu……..…….... ……….135
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Misemo….......…………… ............. ………138
Matamshi bora vitate g/ng… ....................................................................139
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Vinyume vya vitenzi…….......... ….…140
Upatanisho wa kisaru —
kivumishi ‘-o-ote-’…....… .................... ………141
Kukanusha wakati uliopita kulingana na nafsi……... .................. …….142
Kusoma:
Makala……….... ............................................................ ……….143
Kuandika:
Insha ya mdokezo..............................................................…143
SURA YA KUMI NA TATU
Ufahamu:
Uchafuzi wa mazingira........... ....................... ......................146
Kusikiliza
na
kuzungumza
:
Isimu-Jamii:
Mazungumzo—
posta.…......................... ....................148
Saru
na
matumizi
ya lugha: Hali za -nge-, -ngeli- na -ngali- .. ....….150
Upatanisho wa kisaru —
kivumishi ‘-ingineo’……….. ....................…..153
vi
vii
Kusoma:
Aina za kamusi……. ............................................................ ..…154
Kuandika:
Shajara………… ............................................................ ……156
SURA YA KUMI NA NNE
Ufahamu:
Runinga na ulimwengu wa leo…….........………..........………157
Kusikiliza
na
kuzungumza
:
Matamshi bora —vitate p/b… ................................................................... …160
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Kuakisha……............…… ..........……161
Upatanisho wa kisaru —
kivumishi ‘-ingineo’……… .................... ……163
Ukubwa na udogo katika nomino.. ......................................................................... .
164
Kusoma: Usomaji
wa kina Riwaya……...……........... ………………166
Kuandika:
Imla………………............................................................. ……167
SURA YA KUMI NA TANO
Ufahamu:
Mwabusara na siri kali......................................................…168
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Maigizo………………...................…………171
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Vitenzi…………………......... …………172
Mnyambuliko wa vitenzi…… ..................................................................…175
Kusoma:
Mashairi ya arudhi…............................................................…177
Kuandika:
Taarifa au ripoti fupi.................................. ......................…178
SURA YA KUMI NA SITA
Ufahamu:
Lumbwi na
Kindumbwendumbwe cha mageuzi.................................................................... .....181
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Vitendawili………………… .............….....184
Matamshi bora - vitate t/d…..........................................................................185
Saru
ya
matumizi
ya
lugha
: Sentensi za Kiswahili……...........……186
Kuakisha…............….…… ................................................................ 187
Kusoma:
Mashairi huru…….. ............................................................... .189
Kuandika:
Insha ya methali…............................................................…190
Mazoezi
ya
Marudio
II
……… ............................................................…192
SURA YA KUMI NA SABA
Ufahamu:
Ubabe wa Fumo
Liyongo............................... ....................…196
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Mighani…….. ............. .…………………199
Matamshi bora vitate ch/j… ..................................................................200
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Sentensi……… ........... ………....………201
Uundaji wa nomino kutokana na nomino………………........... ..…………203
Kusoma:
Matumizi ya maktaba…...................... ................................…204
Kuandika:
Utungaji wa kisanii
michezo ya kuigiza………....... ……205
vi
vii
SURA YA KUMI NA NANE
Ufahamu:
Mfumo wa jua na sayari.........................................................206
Kusikiliza
na
kuzungumza
:
Isimu-Jamii:Mazungumzo
Kituo cha polisi.................... ................................................................ .....208
Matamshi bora vitate f/v…................................................................ ..210
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Sentensi ambatano….....................…210
Vihusishi…………….....….….................................................................…212
Kusoma:
Makala………….… ........................................................... ……213
Kuandika:
Mahojiano……............................................................. ....……214
SURA YA KUMI NA TISA
Ufahamu:
Ndio zipi haki hizo…................................................................216
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Ufahamu wa kusikiliza…… ...................216
Matamshi bora - vitate ch/sh.......................... ............... .....................219
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Mnyambuliko wa vitenzi....... .............219
Kuakisha…………….......… .................................................................…221
Kusoma:
Usomaji wa kina Riwaya….........…… ..............……….……223
Kuandika:
Utungaji wa kiuamilifu Maagizo… ..……........…………223
SURA YA ISHIRINI
Ufahamu:
Vyombo vya habari na jamii ya leo…....……….......…………225
Kusikiliza
na
kuzungumza
:
Mafumbo….......………… ......................................................…227
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Viwakilishi..........................228
Kuakifisha……………….......................................................................…………229
Kusoma:
Mashairi huru…................................................. …..…231
Kuandika:
Dayalojia/ Mazungumzo........... .............. ................233
SURA YA ISHIRINI NA MOJA
Ufahamu:
Boramimi na njugu za ngwenje………………......... …………235
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Tanakali za sauti……… ............ …....…238
Matamshi bora vitate k/g.…................................................................ 240
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Viwakilishi……………… .......... .………241
Upatanisho
wa
kisarufi—
kivumishi enye’............... ............. ..........242
Kusoma:
Tamthilia -Fani
(mazungumzo)................ ..................... .........242
Kuandika:
Utungaji wa kiuamilifu— Risala……… .. ...................………243
SURA YA ISHIRINI NA MBILI
Ufahamu:
Pipo Jerevu na moto wa majini……......………..………… .....245
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Maigizo……………………....…… .............. 247
viii
PB
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Viwakilishi………………..……. ...........249
Vielezi…………...…………....… ................................................................ 250
Kusoma:
Riwaya Wahusika…. ........................................................... 251
Kuandika:
Utungaji wa kiuamilifu Orodha ya mambo……..... ....……252
SURA YA ISHIRINI NA TATU
Ufahamu:
Pimbi na hidaya ya kijiji…………............ ..............………………253
Kusikiliza
na
kuzungumza
: Mjadala………….......... ............ …………255
Saru
na
matumizi
ya
lugha
: Mnyambuliko wa vitenzi….... ....... ..256
Viwakilishi................................. ..................................................................................257
Kusoma:
Makala………........…............................................................…258
Kuandika:
Mahojiano……...…............................................................…259
SURA YA ISHIRINI NA NNE
Ufahamu:
Bwana Bafe na maradhi ya walalahoi……………… ... ..……261
Saru
na
matumizi
ya lugha: Hali
‘po’ …………..........………… ....….264
Kusoma:
Riwaya —Wahusika..... ............................................................267
Kuandika:
Resipe ……………… ........................................................... ..269
Sentensi zenye maana tatanishi............. .......................... ...................…270
Mazoezi
ya
Marudio
III
….............................................................. ……271
PB
1
Sura ya Kwanza
A. Ufahamu
Ndugu Majuu na wakazi wa Kibabuu
Hamna mtu hata mmoja aliyelijua jina la asili la Ndugu Majuu katika kijiji
kizima cha Kibabuu. Hata hivyo, sifa zake zilitangaa sehemu pana kama moto
wa porini. Nyumba yake iliyojengwa kwenye kilima cha pekee kijijini ilisika
ghaya kutokana na wajihi na wasifu wake wa nje. Jumba kuu la vyumba
kama vitano hivi lilikuwa fahari kwa yeyote aliyelitupia jicho. Lilijengwa kwa
mawe adimu katika eneo zima la kwao na kuezekwa kwa vigae vyekundu
vilivyoliongezea haiba na kulifanya lizungumziwe kwa kirefu na kila mkazi
wa eneo la Kibabuu.
Sifa moja iliyomtenganisha Ndugu Majuu na wanakijiji wengine ni
utajiri wake wa kupindukia. Alikuwa na biashara za kila aina kuanzia kijijini
hadi Jiji Kuu. Ilisemekana kuwa alikuwa na safu ya biashara huko jijini kiasi
cha watu kudai kuwa kuna mtaa mzima ambao ulikuwa mali yake binafsi.
Yamkini mengine yalikuwa yamepigwa chuku lakini ni kweli kuwa Ndugu
Majuu alikuwa mkwasi wa kutajika.
Hata hivyo, lazima utajiri huo ndio uliombadilisha kitabia. Ilidaiwa
kuwa hapo zamani alikuwa mcha Mungu sana lakini aliibwaga tabia
hiyo baada ya kutajirika. Utajiri uingiapo, ukari hujongea. Kutokana na
maendeleo hayo ya kiuchumi, kila alipozungumza, Ndugu Majuu alionyesha
kiburi kingi ajabu. Siku moja alipoulizwa na watu kwa nini hatangamani
nao katika miradi ya maendeleo pale kijijini alijibu, “Ndugu, haya mambo
ya akina baba kabwela siyawezi. Mimi ni mtu wa juu sio mtu wa chini kama
nyinyi.” Wengine wanasema kuwa huo ulikuwa mwanzo wake kuitwa ‘Ndugu
Majuu’. Hata hivyo, watu wengine walidai kuwa alibatizwa ‘Ndugu Majuu’
kutokana na mazoea yake ya kusari. Mara kwa mara alizuru nchi za ng’ambo
au ‘Majuu’ kama alivyoziita.
Kutokana na tabia yake ya kuzidi kuwapuuza watu, wanakijiji waliamua
kuendelea na maisha yao bila ya kumjali. Hata hivyo, hawakumwonyesha chuki
ya aina yoyote. Yeyote aliyebahatika kukutana naye hakumnyima salamu
ingawa Ndugu Majuu hakutilia maanani salamu hizo.
Siku moja Mzee Maarifa alimwendea Ndugu Majuu kumtaka msaada
wa usari wa gari. Asubuhi ile mjukuu wake wa pekee alishikwa na maradhi
ya ghaa na Mzee Maarifa hakujua la kufanya ila kumwendea Ndugu Majuu.
Hali ya usari katika sehemu hiyo ilikuwa mbaya sana. Tena hakuna mtu
mwingine yeyote pale kijijini aliyekuwa na gari ila Ndugu Majuu.
Mzee Maarifa alikuwa na bahati kama mtende kwa kuwa Ndugu Majuu
alikuwa nyumbani asubuhi hiyo. Alipoka alimsalimu na kumweleza haja
yake kwa maneno ya upole. Ndugu Majuu alimsikiliza kwa muda kabla ya
kumkatiza, “Ndugu Mzee...unaitwa nani vile?” Aliuliza Ndugu Majuu huku
akiibirua midomo yake kama mtu anayetazama kinyaa.
2
3
“Jina langu ni Maarifa. Nilikuwa kwenye kundi moja la tohara na
babako,” alisema Mzee Maarifa.
Ndugu Majuu aliangua kicheko kikubwa kisha akauliza kwa tadi, “Eti
ulikuwa katika kundi gani?”
“Moja la tohara na babako. Kwa kweli alikuwa raki yangu wa chanda
na pete,” alisema Maarifa.
Ndugu Majuu alimwangalia tena kwa muda, akaubirua mdomo wake
na kumwambia, “Sikiliza mzee, naona unajua sana kutoa kadhia. Nitamjuza
mwanangu akutembelee wakati wa utati wake wa somo la fasihi simulizi.
Hivi wanao walisoma lakini? Walisoma hadi darasa la ngapi? Ee? Niambie
mzee. Kwa ufupi ni hivi mzee, mimi nina safari muhimu sana leo kwenda
ng’ambo. Unasikia? Ng’ambo kwenyewe wanakoishi Wazungu hasa! Sina
muda wa kufanya hayo unayotaka. Haya sasa toka!”
Mzee Maarifa alishika
tariki kurudi zake nyumbani
huku huzuni na uchungu
mwingi ukimtafuna moyo.
Alimlaaani Ndugu Majuu
kimoyomoyo. “Mtu hana
hata huruma ya kibinadamu.
Muhimu kwake ni hizo safari
za biashara kwa Wazungu.
Hajui kuishi kwingi ni kuona
mengi? Siku moja bila shaka
huo Uzungu utamwonyesha
mizungu!”
Kwa vile Mzee Maarifa
hakufanikiwa kupata usafiri
haraka ilivyohitajika, mjukuu
huyo alipokishwa hospitalini
alikuwa anachungulia kaburini.
Juhudi za madaktari za kumwokoa hazikufanikiwa. Baada ya nusu saa hivi,
mjukuu wa Mzee Maarifa aliaga dunia. Kisa cha Ndugu Majuu na Mzee
Maarifa kilizungumzwa kijijini kwa siku nyingi.
Miezi kadha baadaye, serikali iliamua kuuboresha usari wa eneo
hilo na baadhi ya wanakijiji wakawahi kujinunulia magari ya kusarisha
bidhaa zao kupeleka sokoni. Mzee Maarifa alisikitika kuwa laiti maendeleo
hayo yangekuja kabla ya kifo cha mjukuu wake, maisha ya kijana huyo
yangeliokolewa. Lakini alishukuru kuwa sasa palikuwa na usari bora na
kwamba siku nyingine mwanakijiji mwingine hatakumbana na janga kama
lile lililomsibu.
Hata hivyo, licha ya hali ya usari kuimarika, wanakijiji hawakuweza
kusahau kamwe kitendo alichotenda Ndugu Majuu. Wote waliujua ukweli
kuwa kijengacho mtu ni utu na tabia. Lakini walishangaa kama Ndugu
Majuu alijua thamani ya msemo huo wa kale.
2
3
Siku moja ndugu Majuu alisari ng’ambo kama ilivyokuwa kawaida
yake. Lakini aliporudi akaanza kufanya mambo ya kushangaza. Aliwachukua
vijana wengi wa pale kijijini na kuwaajiri. Kazi yao kuu ilikuwa kusarisha
bidhaa zake za kibiashara kupeleka maeneo mbalimbali ya nchi. Wakati
mwingine aliposari ng’ambo alianza kuandamana na baadhi ya vijana
hao. Tendo hili lilizidi kuwashangaza wakazi wa Kibabuu. Bila shaka
Ndugu Majuu alikuwa amebadilika kweli. Wanakijiji walitoa maoni tofauti
kuhusu ukarimu huu mpya wa Ndugu Majuu. Baadhi yao waliamini kuwa
kilichomfanya abadilike hivyo ni kusumbuliwa na akili yake kutokana na
kitendo chake dhidi ya Mzee Maarifa. “Huyu analaumiwa na akili yake tu.
Ametambua kuwa mkataa wengi ni mchawi,” walisema. “Hapana, muwi
huwa mwema, Ndugu Majuu kabadilika kweli!” wengine wakadai. Hata
hivyo, Mzee Maarifa hakuwa na hakika kama Ndugu Majuu kabadilika kweli.
“Chui haachi madoa yake,” alisema. “Bwana Maarifa, Ndugu Majuu hayuko
juu tena keshashuka chini,” wanakijiji walimwambia. “Nyinyi hamjui kuwa
simba akienda mawindoni hucha makucha yake?” Aliwauliza wanakijiji.
Wote waliachama. Hawakujua wamjibu nini Mzee Maarifa.
Siku moja alipokuwa nyumbani akisikiliza habari za jioni katika
kijiredio chake, Mzee Maarifa alisikia tukio lililomshtua kidogo. Kilikuwa
kisa cha jamaa mmoja aliyebambwa na polisi kwenye uwanja wa ndege jijini
Nairobi akiwa na shehena ya dawa za kulevya. Ripoti hiyo ilisema kuwa
jamaa huyo alikuwa amemeza vidonge vya dawa ambavyo alivikopoa baada
ya kulazimishwa kwenda haja. Kilikuwa kisa cha kuchekesha na kusikitisha
wakati huo huo.
Siku iliyofuata ndipo kila kitu kilipodhihirika dhahiri shahiri. Jamaa
aliyeshikwa alikuwa kijana wa pale kijijini aliyekuwa miongoni mwa
wafanyakazi wa Ndugu Majuu. Kumbe kazi aliyokuwa amewaajiri vijana
ilikuwa kazi ya kusarisha dawa za kulevya. Watu wakapigwa na butwaa.
“Majuu Majuu kumbe huku juu hamnazo! Kumbe ni jambazi la dawa za
kulevya!” Walimaka. Baada ya kisa hicho Ndugu Majuu alitoweka kijijini
kama umande. Lakini mkono wa serikali ni mrefu kabisa. Mwezi mmoja
baadaye alitiwa mbaroni. Baada ya kesi iliyochukua muda wa miezi minne
na kufuatiliwa kwa makini na wakazi wa Kibabuu, Ndugu Majuu alielekezwa
gerezani kuanza kifungo cha miaka ishirini na kazi za sulubu. Nao vijana
aliowaajiri wakapata miaka kumi kila mmoja. Kweli ajidhaniaye amesimama
anafaa sana kuangalia asije akaanguka.
Maelezo ya msamiati
zilitangaa : zilienea
wajihi : umbo; sura
adimu : gumu kupatikana; nadra
haiba : kitu kinachovutia; chenye sura nzuri
akina baba kabwela : watu wa kawaida; akina yahe
kinyaa : uchafu; kinyesi
tadi : ujeuri; udhuli
4
5
Maswali
1. Ndugu Majuu alijulikana kutokana na sifa mbili kuu. Taja sifa hizo.
2. ‘Utajiri uingiapo ukari hujongea.’ Je, unakubaliana na usemi huo?
Fafanua.
3. Kulingana na wanakijiji, ni nini chanzo cha jina ‘Ndugu Majuu’?
4. Ndugu Majuu alisaidiana sana na wanakijiji wenzake katika kuendeleza
miradi ya maendeleo. Ni kweli au si kweli? Eleza ilivyokuwa.
5. Unadhani ni kwa nini Ndugu Majuu hakumsaidia Mzee Maarifa?
6. Toa maana ya methali zifuatazo kulingana na jinsi zilivyotumika katika
kifungu:
(a) Muwi huwa mwema.
(b) Mkataa wengi ni mchawi.
(c) Simba akienda mawindoni hucha makucha yake.
(d) Chui haachi madoa yake.
B. Kusikiliza na kuzungumza
IsimuJamii:
Majadiliano : Mwanafunzi na mwalimu
(Mwalimu anafanya kazi yake. Thuranira anaingia osini)
MwaliMu
: Karibu Thuranira. Hujambo?
Thuranira
: Sijambo sana mwalimu, shikamoo!
MwaliMu
: Marahaba (anatua kidogo). Je, umeuzingatia ushauri
wangu?
Thuranira
: Ndiyo mwalimu lakini…
MwaliMu
: Lakini nini?
Thuranira
: Bado lugha hii inanitatiza mwalimu!
MwaliMu
: Hapana sababu ya kutatizwa na lugha ya Kiswahili
(anaubadili mkao wake). Ni hivi Thuranira, lazima ujitahidi.
Waswahili wenyewe husema bandu bandu humaliza
gogo; ukijitahidi kidogo kidogo hatimaye utafanikiwa! Je,
umeanza kusomasoma vitabu vya hadithi vilivyoandikwa
kwa lugha ya Kiswahili?
Thuranira
: (Anasitasita) Mmn…
MwaliMu
: Umeanza kweli?
Thuranira
: Mm…bado mwalimu!
MwaliMu
: Unaona? Thuranira, hamna jema linalomjia mtu pasi na
juhudi. Lazima ujitahidi kuanza kusomasoma vitabu vya
hadithi; anza kwa vile vyepesi.
Thuranira
: Lakini mwalimu vitabu ni ghali mno!
4
5
MwaliMu
: Ni ghali ndiyo, lakini sikusema ununue. Anza kwa vichache
vilivyomo maktabani. (Anatua) Azima hata vya wenzako;
jitahidi kuichochea hamu mwenyewe; utamu huja kwa
kuonja! Kisha jitahidi kuongea na wenzako kwa Kiswahili;
nimeona kuwa unakichangamkia Kiingereza zaidi!
Thuranira
: Mwalimu, Kiingereza ni rahisi kuliko Kiswahili!
MwaliMu
: Thuranira! Kiingereza ni lugha ya kigeni sana; Kiswahili
ni lugha yetu wenyewe. Hii ni lugha ambayo tunatakiwa
kuikuza na kuionea fahari. Unasikia Thuranira!
Thuranira
: Ndiyo mwalimu.
MwaliMu
: Lugha ni muhimu; ni sehemu kubwa ya utamaduni na
utamaduni ni kitovu cha jamii. Tukiikosa tunakosa kiungo
muhimu cha uhai wetu, unasikia? (Thuranira anaitikia)
Lazima ujizoeze kuiongea lugha hii ili uukuze uwezo wako.
Thuranira
: Wenzangu wananicheka. Wanasema kuwa matamshi yangu
ni mabaya!
MwaliMu
: Ndivyo tunavyojifundisha sote Thuranira. Ukicha kusemwa
hutotenda jambo; hao wanaokucheka hawajui kuwa mtu
hazaliwi na lugha; hujifunza lugha hiyo! Usikubali hao
wakukatishe tamaa; unasikia? (Thuranira anaitikia) Mtaka
zuri sharti adhurike na kuteleza si kuanguka.
Thuranira
: Nimesikia mwalimu.
MwaliMu
: Basi hakikisha umeanza kutenda hayo leo wala si kesho.
Thuranira
: Nitafanya hivyo. Asante mwalimu.
MwaliMu
: Haya karibu. (Thuranira anaondoka. Mwalimu anaendelea
na kazi aliyokuwa nayo.)
Kazi ya kundi
1. Jaribuni kuigiza mazungumzo haya darasani.
2. Taja aina ya sajili iliyotumika katika mazungumzo.
3. Tambua sifa za sajili uliyoitaja katika swali la pili hapo juu.
Maswali
1) Je, Thuranira ana shida gani?
2) Unakiri Thuranira ni mwanafunzi wa aina gani? Kwa nini?
3) Je, mwalimu anampa Thuranira ushauri gani? Unakiri ni kwa nini
anamshauri hivyo?
(ii) Matamshi bora : Vitate s/sh
Soma maneno yafuatayo:
s sh
saba shaba
saka shaka
suka shuka
6
7
soga shoga
sababu shababu
Soma: Vitanza ndimi
1. Wale watu saba walipewa siku saba kutafuta shaba lakini siku saba
hazikutosha kupata shaba kwani shaba haiwezi kupatikana kwa siku
saba.
2. Bwana Mashaka na mashaka yake alikwenda kusaka chui lakini
akasahau kuwa kusaka chui kunahitaji mtu asiye na shaka kwani
mwenye mashaka akisaka chui hupatwa na mashaka zaidi.
3. Dada yangu mdogo alisema angetaka kushukwa nywele nikamwambia
nywele haishukwi bali husukwa.
4. Bi. Mwashengu alikwenda kupiga soga na mashoga zake akatwaliwa
na soga hadi kazi yake ikashindwa kusonga akicheka na mashoga zake
kwenye soga lao.
5. Kwa sababu alikuwa shababu, Shaaban alisahau kuwa maisha ya
shababu ni hatari sana kwa sababu shababu asipochunga huweza
kupotoshwa na mashababu wengine bila sababu maalum.
C. Saru na matumizi ya lugha
Misingi ya maneno
Momu
Momu ni kipashio kidogo zaidi katika lugha. Kipashio hiki huweza kuwa
neno zima au sehemu ya neno iliyo na maana. Hakiwezi kuvunjwavunjwa
zaidi bila ya kupoteza maana yake. Tazama maneno yafuatayo yalivyotengwa
katika momu zake mbalimbali:
(a) tunalima tu-na-lim-a
(b) alinijengea a-li-ni-jeng-e-a
(c) waliotuibia wa-li-o-tu-ib-i-a
(d) nitakusomea ni-ta-ku-som-e-a
(e) mmeondoka m-me-ondok-a
(f) mtoto m-toto
(g) kitu ki-tu
Momu katika vitenzi Kiswahili huwakilisha maana mbalimbali; kwa mfano:
(a) Nafsi
ni-ta-end-a tu-ta-end-a
u-ta-end-a m-ta-end-a
a-ta-end-a wa-ta-end-a
6
7
(b) Wakati (c) Hali
ni-li-end-a ni-nge-end-a
ni-na-end-a ni-ngeli-end-a
ni-ta-end-a ni-ngali-end-a
(d) Mzizi
ni-na-lim-a ni-na-som-a
ni-na-ruk-a ni-na-andik-a
ni-na-lal-a ni-na-pik-a
(e) Kauli (ya mnyambuliko)
Kutendwa Kutendea Kutendewa Kutendeka
pig-w-a pig-i-a pig-iw-a pig-ik-a
chez-w-a chez-e-a chez-ew-a chez-ek-a
lim-w-a lim-i-a lim-iw-a lim-ik-a
omb-w-a omb-e-a omb-ew-a omb-ek-a
som-w-a som-e-a som-ew-a som-ek-a
chor-w-a chor-e-a chor-ew-a chor-ek-a
chom-w-a chom-e-a chom-ew-a chom-ek-a
(f) Urejeshi
a-li-ye-anguk-a wa-li-o-anguk-a
li-li-lo-anguk-a ya-li-yo-anguk-a
u-li-o-anguk-a zi-li-zo-anguk-a
(g) Kitendwa/vitendwa
a-na-ki-be-ba a-na-vi-be-ba
a-na-ku-be-ba a-na-wa-be-ba
a-na-li-be-ba a-na-ya-be-ba
a-na-m-be-ba a-na-wa-be-ba
Aina za momu
Kuna aina mbili kuu za momu:
1. Momu huru.
2. Momu tegemezi.
1. Momu huru
Momu huru ni zile momu ambazo huweza kujisimamia na kuwa na maana
kamili bila kutegemea au kuongezewa momu nyingine. Yaani ni maneno
kamili. Kwa mfano:
(a) (i) kuku (ii) baba (iii) mama
(b) (i) labda (ii) lakini (iii) halafu
(c) (i) haraka (ii) sana (iii) jana
8
9
Mofimu huru pia hujulikana kama mofimu mwanana au mofimu za
kimsamiati.
2. Momu tegemezi
Momu tegemezi kwa upande mwingine, ni viungo vya maneno vyenye
maana fulani lakini haviwezi kujitegemea vikiwa peke yake. Inabidi
vifungamanishwe na momu nyingine ili maana yake yaweze kujitokeza
kikamilifu. Kwa mfano:
(i) a-na-kimbi-a (ii) tu-li-wa-pig-i-a
(iii) a-na-ye-ku-j-a (iv) ni-li-vyo-vi-chor-a
(v) li-li-lo-kunj-w-a
Momu hizi pia huitwa momu ambisho au momu andamizi.
Zoezi
1. Eleza tofauti kati ya momu huru na momu tegemezi. Toa mifano
mbalimbali ya kuthibitisha.
2. Tenganisha momu mbalimbali zinazounda maneno yafuatayo:
(a) nilikupigia (b) aliyeniletea
(c) wanaotusaidia (d) kilichoanguka
(e) tuliowapenda (f) lakini
D. Kusoma
Riwaya: Utangulizi
Riwaya ni hadithi ndefu ya kubuni (kutunga kwa kuwaza kisa) inayosimulia
tukio au matukio fulani. Hadithi hii hujishughulisha na maisha ya binadamu.
Riwaya inahusu sehemu au mwanda mpana, yaani inagusia sehemu kubwa,
inatumia lugha ya mfululizo au ya nathari, ina visa kadha na matukio yake
huundwa kwa ufundi.
Ni mambo gani yanayojenga riwaya?
1. Kuwepo kwa kisa kinachosimuliwa au hadithi.
2. Kuwepo kwa viumbe wanaotenda mambo mbalimbali au wahusika.
3. Kuwepo kwa mahali na wakati wa kutendeka kwa matukio, yaani
mandhari.
4. Kuwepo kwa lengo la mwandishi aliyeiandika riwaya hiyo au dhamira.
5. Kuwepo kwa lugha inayotumiwa kuwasilisha hadithi, kueleza matendo
au matukio na kueleza dhamira ya mwandishi.
Mambo ya kuchunguza tusomapo riwaya
Riwaya huundwa kwa sehemu mbili kuu: FANI na MAUDHUI.
8
9
MAUDHUI ni jumla ya mambo yanayozungumziwa katika riwaya.
Maudhui huhusisha mambo mengine kadha kama lengo la mwandishi au
dhamira, ujumbe anaotaka msomaji wake aupate baada ya kuisoma riwaya
hiyo na labda hata msimamo wa mwandishi kuhusu mambo mbalimbali. Kwa
mfano, riwaya inaweza kuzungumzia haki za mtoto, shida za wafanyakazi
watoto, dhiki za maisha ya mjini, umuhimu wa elimu n.k. Inawezekana
riwaya pia ikawa na maudhui ya uhalifu, kubadilika kitabia, mateso ya
wahalifu n.k. kama tunavyoona katika Mui huwa Mwema ya A. Jamaadar.
FANI ni jumla ya mbinu na sifa zote anazozitumia mwandishi
kuyawasilisha maudhui yake. Uhusiano wa maudhui na fani ni kama
wa kupika au kutayarisha ugali. Ugali wenyewe ni kama maudhui lakini
sufuria, unga, maji na mwiko ni kama fani; bila vitu hivi hatuwezi kuupata
ugali; vivyo hivyo bila fani hakuna maudhui. Fani inajumlisha vipengele
kadha kama: muundo au mpangilio wa riwaya (sura, mwanzo, kati, mwisho
n.k.), wahusika au watendaji wa mambo, matumizi ya lugha (methali,
misemo, msamiati, tamathali za usemi) na mandhari (mazingira ya hadithi
mashambani, mijini n.k.)
Maswali
1. Je, ni mambo gani ya kuzingatia kuihusu riwaya?
2. Kuna tofauti na uhusiano gani kati ya fani na maudhui?
3. Eleza maudhui manne ya riwaya ambayo umeisoma.
E. Kuandika
Barua rasmi
Barua ya aina hii inahusu shughuli za kikazi au kiasi kama vile kuomba
kazi, kutaka msaada, majibu ya barua nyingine rasmi, kutaka taarifa fulani,
kutoa maoni au maonyo magazetini na kadhalika.
Mambo muhimu kuhusu barua rasmi
1. Kwa kawaida huwa si ndefu.
2. Hoja muhimu zijitokeze bila ya kujirudiarudia. Umalizapo kuandika
pitia ili uondoe hoja zilizojirudia.
3. Tumia lugha nyepesi au inayoeleweka waziwazi na unayemwandikia.
4. Zingatia kanuni zifaazo za saru na maendelezo au tahajia za maneno.
5. Barua rasmi iliyoandikiwa mtu fulani inaweza kushughulikiwa na
mdogo wake baada ya kupewa mamlaka hayo. Kwa hivyo, katika majibu
yako asa anayeishughulikia huweza kuandika hivi:
Saul P. Mukasa
Kwa niaba ya Meneja Mkurugenzi
10
11
Muundo wa barua rasmi
Barua rasmi huwa na muundo ufuatao:
Anwani ya mwandishi
Hii huandikwa upande wa kulia juu kwenye karatasi. Kuna njia mbili za
kuandika anwani. Moja huitwa wima. Katika njia hii, maandishi huwa wima
wala hayalali au kuegemea upande wa kulia. Kwa mfano:
Shule ya Upili ya Mtoni,
S.L.P. 3112,
SIRIBE.
Njia nyingine huitwa mshazari. Katika njia hii maandishi hulala au huegemea
upande wa kulia. Kwa mfano:
Shule ya Upili ya Mtoni,
S.L.P. 3112 ,
SIRIBE.
Tarehe ya kuandika barua
Hii huandikwa upande wa kulia juu, chini ya anwani ya mwandishi. Kwa vile
tarehe si sehemu ya anwani, si lazima ilingane na anwani hii. Kwa mfano:
Shule ya Upili ya Mtoni,
S.L.P. 3112 ,
SIRIBE.
2/10/2003
Nambari ya kumbukumbu
Hii huandikwa upande wa kushoto juu, chini ya anwani na tarehe ya
mwandishi. Nambari hii ni muhimu hasa tunapowasiliana na kampuni
au mashirika makubwa yanayopokea barua nyingi kila siku. Husaidia
kuweka kumbukumbu na kuhifadhi barua au nakala ya barua yako katika
faili maalum inayohusu mada unayoiandikia. Kwa hivyo, inakuwa rahisi
kuirejelea na kuishughulikia hata katika siku za usoni.
Anwani ya mwandikiwa
Hii huandikwa upande wa kushoto chini ya anwani ya mwandishi, tarehe na
nambari ya kumbukumbu. Huandikwa kwa mtindo wa wima.
Mwanzo na kichwa cha barua
Katika kuanza barua, ni vyema kutumia maneno (nemsi) kama Bwana,
Bibi, Daktari, Mwalimu, Mkurugenzi n.k. Epuka maneno kama mazee,
buda, mathee, chali, braza, siste n.k Sababu ni kuwa uhusiano wako na
unayemwandikia ni wa kikazi wala si wa kiraki au kidugu.
10
11
Unapoandika kichwa cha barua rasmi ni bora kutaja kwa kifupi mada kuu ya
barua hiyo. Jambo hili husaidia asa anayeifungua kujua mara moja ni nani
anayepaswa kuishughulikia. Naye anayepewa wajibu huo wa kuishughulikia
huelewa mara moja inahusu jambo gani. Katika kuandika mada kuu, kwa
kawaida tunatumia maneno kama KUH: yaani ‘Kuhusu’, au MINT: yaani
‘Mintaarafu’ au YAH: yaani ‘Yahusu’ au MADA n.k.
Hitimisho la barua
Mwishoni mwa barua, ni vyema kumalizia kwa kutumia maneno
yanayoonyesha heshima na unyenyekevu, kwa mfano, ‘wako mwaminifu’,
‘wako mtiifu’, n.k. Usitumie maneno kama ‘wako wa maisha’, ‘wako wa
moyoni’ au mengine kama hayo kwa vile uhusiano wako na unayemwandikia
ni wa kikazi wala si wa kidugu au kiraki.
Mwisho kabisa usisahau kuandika jina na sahihi yako. Barua rasmi
isiyo na sahihi huenda isishughulikiwe hata ikapo unapoituma. Uandikapo
jina ni vizuri kujitambulisha kikamilifu kwa majina yako mawili au matatu.
Iwapo hati yako haisomeki kwa urahisi, unashauriwa kutumia heru kubwa,
kwa mfano;
Wako mwaminifu,
ISABELA M. MWAKAZI.
Mfano:
Isabela alikuwa mwenyekiti wa Chama cha Zaraa cha shule ya upili ya Mtoni.
Siku moja alimwandikia mkurugenzi wa kiwanda cha pamba cha Mumwe
barua ifuatayo:
Shule ya Upili ya Mtoni,
S. L. P. 3112,
SIRIBE.
2/10/2003.
NA. KUMB: MSS/216/F/1
Meneja Mkurugenzi,
Kiwanda cha Pamba cha Mumwe,
S. L. P. 2221,
KAMOKO.
Bwana/Bibi,
KUH: ZIARA KIWANDANI
Nashukuru kupata fursa hii ya kuwasiliana nawe ili kukujulisha kuhusu
azma yangu. Mimi ni mwenyekiti wa chama cha Zaraa hapa shuleni mwetu.
12
13
Wanachama wa chama hiki ni wanafunzi wanaopendelea masuala ya kilimo.
Wao wana vijishamba vyao huku shuleni wanapokuza mimea mbalimbali chini
ya uelekezi wa mwalimu wetu wa somo hili.
Tungependa kutembelea kiwanda cha Pamba cha Mumwe siku ya
Jumamosi tarehe 8/11/03. Tutashukuru sana ukitupa nafasi hii.
Tunataraji kupata majibu kutoka kwako. Asante.
Ni mimi wako mwaminifu,
ISABELA M. MWAKAZI
Majibu
Kiwanda cha Pamba cha Mumwe,
S.L.P. 2221,
KAMOKO.
11/10/03.
Na. KUMB: KPM/300/BR/17
Mwenyekiti Chama cha Zaraa,
Shule ya Upili ya Mtoni,
S.L.P. 3112,
SIRIBE.
Mwenyeketi,
KUH: ZIARA KIWANDANI
Nimeipokea barua yako NA. KUMB: MSS/216/F/1 ya tarehe 2/10/2003 kuhusu
mada iliyotajwa hapo juu. Ni furaha yetu kuwa mngependa kutembelea
kiwanda chetu. Hata hivyo, siku hiyo haitawezekana kufanya ziara hiyo kwa
vile itakuwa ni siku ya mkutano mkuu wa mwaka unaohusisha wafanyakazi
wote wa kiwanda hiki. Kutokana na sababu hii, ningependekeza mzuru
kiwanda chetu Jumamosi tarehe 15/11/03.
Iwapo itawezekana kufanya hivyo, tafadhali nijulishe haraka iwezekanavyo
ili nifanye mipango ya mapokezi na ratiba ya siku hiyo. Asante.
Ni mimi wako,
Isaya M. Njeremani,
Meneja Mkurugenzi.
12
13
Barua ya kufuatiliza
Shule ya Upili ya Mtoni,
S.L.P. 3112,
SIRIBE.
18/10/03.
KUMB: MSS/216/F/2
Meneja Mkurugenzi,
Kiwanda cha Pamba cha Mumwe,
S. L. P. 2221,
KAMOKO.
Bwana,
KUH: TAREHE MPYA YA ZIARA
Barua hii ni ya kufuatiliza yako NA. KUMB: KPM/300/BR/17 ya tarehe
11/10/2003. Ninakujulisha ya kwamba itakuwa ni furaha yetu kuzuru kiwanda
chenu Jumamosi tarehe 15/11/03 kama ulivyopendekeza.
Tutakuwa jumla ya wanafunzi 60 na tutaandamana na walimu wetu wawili.
Tunataraji kuwasili mwendo wa saa nne asubuhi. Asante.
Wako mwaminifu,
Isabela M. Mwakazi,
Mwenyekiti Chama cha Zaraa.
Zoezi
Wewe ni mwenyekiti wa Chama cha Kiswahili shuleni mwenu. Mwandikie
barua mwenyekiti wa Chama cha Kiswahili wa shule jirani ukiwaalika
wanachama wa chama chake kujiunga nanyi ili kushiriki katika mazungumzo
kuhusu kichwa ‘Jinsi ya kukuza lugha ya Kiswahili nchini Kenya’.
14
15
Sura ya Pili
A. Ufahamu
Kumekucha!
1. Kumekucha!
Jamani nisikizeni, masikio yategeni,
Nisemayo hadharani, muyatie akilini,
Msiyatie kapuni, mwambe hayana maani,
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
2. Kumekucha!
Kung’olewa masomoni, nirudishwe kijumbani,
Kisomo kiwe kapuni, ndipo niozwe mwishoni,
Hatima yangu gizani, nisijue hata wani,
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
3. Kumekucha!
Kupelekwa myomboni, kufanyiwa ukaini,
Nd’o nitoke utotoni, kwa kijembe cha mwilini,
Adhabu hino mwilini, ‘mefanya hatia gani?
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
4. Kumekucha!
Ajira ya majumbani, na malipo ya mapeni,
Kama jela kifungoni, na kuchunwa sikioni,
Na kupigwa mgongoni, kama mimi hayawani,
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
5. Kumekucha!
Ubakaji majiani, na majitu makaini,
Kisha iwe sheriani, wanakwepa hatimani,
Na fadhaa maishani, isin’ache mwafulani,
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
6. Kumekucha!
Kulala barabarani, na uchafu wa njiani,
Bila kivazi mwilini, au vyatu miguuni,
Wala mlo kitumboni, au kinywaji kinywani,
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
14
15
7. Kumekucha!
Gundi kuwa mdomoni, ‘subuhi hadi jioni,
Dharau za majiani, matusi vichochoroni,
Chakula cha mapipani, na maisha ya kinyani,
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
8. Kumekucha!
Sasa nenda darasani, nisome ya ubaoni,
Nibukue matabuni, ya dhahiri na batini,
Nd’o nitoke ujingani, nuru ing’ae njiani,
Nitolewe matopeni, penye mateso ya zani,
Kumekucha kulichele!
Maswali
1. Je, unakiri ni nani anayezungumza katika shairi hili na anazungumzia
nini?
2. Mzungumzaji anasema kuwa anatamani ‘kutolewa matopeni.’ Taja
matatizo kadha anayozungumzia katika shairi hili.
3. Kwa nini mzungumzaji anasema katika ubeti wa pili kuwa ‘hatima yangu
gizani?’
4. Kwenye ubeti wa mwisho wa shairi, mzungumzaji amekia uamuzi
fulani. Taja uamuzi huo na ueleze faida zake.
5. Eleza maana ya maneno haya kulingana na matumizi yake kwenye
shairi kisha uyatumie kutungia sentensi:
(a) ukaini (b) zani (c) hayawani (d) batini (e) ubakaji
6. Kifungu ‘msiyatie kapuni’ ni msemo wenye maana ‘msiyadharau’. Eleza
maana ya misemo ifuatayo:
(a) akina pangu pakavu (b) fumbua macho
(c) jambo la faragha (d) piga moyo konde (e) zamia lulu
B. Kusikiliza na kuzungumza
Visasili
Visasili ni hadithi za fasihi simulizi ambazo huelezea vyanzo au asili ya
matukio au mambo fulani katika jamii fulani. Kimsingi visasili huchunguza
na kutoa visa vya chimbuko la matukio au mambo yaliyomo katika jamii au
tabia ambayo imekuwako katika jamii kwa kipindi kirefu.
Visasili huwa na sifa zifuatazo:
1. Huweza kuwa ni matukio yanayofahamika au ya kawaida katika jamii
inayohusika. Kwa mfano, kwa nini watu hufa?
2. Hadithi hizi kama hadithi nyinginezo za fasihi simulizi huwatumia
wanyama kama wahusika wenye sifa sawa na binadamu.
16
17
3. Visasili ni msingi wa jamii mbalimbali wa kujielezea na kuyaeleza
mazingira yake na ni kielelezo kizuri cha historia ya jamii.
4. Visasili vina sifa inayokaribiana na masimulizi ya kihistoria.
Ni muhimu kutofautisha kati ya visasili na ngano za usuli/asili. Ngano
za usuli ni ngano ambazo zinaeleza chanzo cha hali au wasifu wa kimaumbile.
Kwa mfano, kwa nini si anachechemea? Kwa nini sungura ana mkia mfupi?
Kwa nini nyoka hana miguu? Kwa nini jua hutokeza mchana na mwezi usiku?
Ngano hizi hazihusiani na historia au imani za kihistoria kama ilivyo, kwa
mfano, asili ya kifo? Waswahili walitoka wapi? n.k.
Umuhimu wa visasili
1. Hutueleza chanzo au vyanzo vya matukio mbalimbali katika jamii zetu
na kwa hivyo kuonyesha imani za jamii fulani.
2. Huwa ni sehemu muhimu ya historia za jamii mbalimbali. Zamani jamii
zetu hazikuwa na mfumo wa maandishi, visasili vilitumiwa kama njia ya
kuhifadhi historia iliyopokezanwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
3. Visasili, kama ngano nyingine za fasihi simulizi, hutumbuiza na
kuwaburudisha wanaosimuliwa.
Mfano:
Asili ya kifo (jamii ya Wakamba)
Hapo zamani za kale Mulungu aliwaumba watu wa kwanza, mume na mke.
Baada ya kuwaumba aliwaonyesha pahali pa kuishi. Walikuwa na uhuru
wa kutumia vitu vilivyokuwako jinsi walivyotaka. Baada ya kuwaumba
Mulungu aliondoka na kwenda zake.
Huko alikokuwa alianza kuwaza kuhusu watu aliokuwa amewaumba.
Kama tujuavyo Mulungu ni Mungu mwenye huruma kubwa. Aliwaza na
kusema, “Sitaki mtu awe akifa na kuangamia. Badala yake atakuwa akifa na
kufufuka. Kwa njia hii ataweza kuishi maisha ya milele.” Kwa kuwa alikuwa
mbali na walikokuwa wakiishi, alilazimika kuuwasilisha uamuzi wake huo kwa
watu wenyewe. Basi alimwita kinyonga pamoja na ndege anayejulikana kama
mnanaa. Aliwaangalia wote wawili. Alijua kuwa kinyonga alikuwa na uwezo
wa kufanya mambo yake vyema. Mnanaa naye alikuwa ndege mwenye maneno
mengi sana. Mulungu alimtuma kinyonga kwa kumwambia, “Kawaambie watu
kuwa wataishi milele; wafapo watafufuka na kuishi tena!” Kinyonga aliondoka
kuelekea walikokuwa watu.
Alikwenda taratibu mpaka akafika. Huko nyuma yule mnanaa
alidanganya kuwa anatoka kidogo halafu arudi. Aliruka mpaka huko
alikokuwa ameenda kinyonga kuuwasilisha ujumbe wa Mulungu. Alipoka
huko alimkuta kinyonga akijaribu kuueleza ule ujumbe aliopewa. Alikuwa
akisema, “Niliambiwa… Niliambiwa… Niliambiwa!” Yule mnanaa aliingilia
kati na kusema, ‘Niliambiwa kuwa watu watakufa na kuangamia kama
mizizi ya mmea uitwao msubili.’ Kinyonga alibisha kwa kusema, ‘La.
Niliambiwa kuwa watu watakufa na kufufuka.’ Lakini yale maneno yalikuwa
16
17
yamechelewa; usemi wa kwanza ndio uliochukuliwa kama ukweli. Tangu
siku hizo watu hufa na hawafufuki.
Maswali
1. Je, kisasili hiki kina funzo gani?
2. Je, unakiri ni kwa nini mnanaa aliamua kudanganya kuwa anaondoka
na kurudi?
3. Je, mnanaa ana sifa zipi katika kisasili hiki. Je, unaweza kumfananisha
na mtu wa aina gani?
Kazi ya kundi
Toa mfano wa kisasili kutoka jamii yako na ulinganishe na kisasili cha
mwenzako darasani.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Viambishi
Kabla ya kuzungumzia maana ya neno kiambishi’ ingefaa kuelewa maana
ya neno mzizi’. Mzizi wa neno ni ile sehemu ya neno inayobeba maana yake
kuu na ambayo haiwezi kubadilika. Ikibadilika maana ya neno hilo ni lazima
yatabadilika (litakuwa neno tofauti). Kwa mfano:
(i) a-na-lim-a (ii) tu-me-lim-a
(iii) wa-li-lim-a (iv) ni-ta-lim-a
Navyo viambishi ni viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa
na mzizi wa neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali. Viambishi
huwakilisha maana mbalimali za kisaru kama vile nafsi, wakati, hali,
urejeshi, uyakinishi, ukanushi n.k. Tazama jedwali lifuatalo:
Kitenzi Nafsi Wakati Kirejeshi Kitendwa Mzizi Kiishio
aliyemleta a li ye m let a
kilichokileta ki li cho ki let a
ninavyovileta ni na vyo vi let a
lililolileta li li lo li let a
wanaolileta wa na o li let a
ninayewaleta ni na ye wa let a
tuliozileta tu li o zi let a
mlivyovileta m li vyo vi let a
ninayoyaleta ni na yo ya let a
niliyoileta ni li yo i let a
18
19
Aina za viambishi
Viambishi katika maneno ya Kiswahili ni vya aina mbili:
(a) Viambishi awali
(b) Viambishi tamati
Viambishi awali
Viambishi awali hutokea mwanzoni mwa neno kabla ya mzizi. Kwa mfano:
(i) a-na-ye-m-pig-a (ii) li-li-lo-wa-pig-a
(iii) wa-na-o-tu-pig-a (iv) ki-li-cho-ni-pig-a
Viambishi hivi huwakilisha maana mbalimbali kama vile:
(a) Nafsi katika umoja na wingi
(i) ninaleta tunaleta
(ii) unaleta mnaleta
(iii) analeta wanaleta
(b) Wakati na hali
(i) nilileta (ii) nitaleta
(iii) ninaleta (iv) ningeleta
(v) ningelileta (vi) ningalileta
(vii) nimeleta
(c) Urejeshi
(i) anayeleta (ii) kinacholeta
(iii) vilivyoleta (iv) iliyoleta
(d) Kitendwa/vitendwa/yambwa
(i) nilimleta (ii) nilivileta
(iii) niliyaleta (iv) nilikuleta
Viambishi tamati
Viambishi tamati hutokea mwishoni mwa neno baada ya mzizi. Kwa mfano:
(i) ni-li-m-pig-i-a (ii) ni-ta-m-chez-e-a
(iii) wa-na-m-lim-i-a (iv) a-ka-a-po
Huwakilisha maana mbalimbali. Kwa mfano:
(a) Wakati
(i) apikapo
(ii) aimbapo
(iii) akiripo
(iv) aendeshapo
(v) akamapo
(b) Mahali
(i) achezeako
18
19
(ii) aingiamo
(iii) aandikiapo
(c) Rai/himizo/kiishio:
(i) simameni (ii) niletee
(iii) njooni (iv) someni
(d) Kauli/hali ya kimnyambuliko
(i) nilimpigia (ii) kinapigika
(iii) nilimchezea
Zoezi
1. Tenganisha maneno yafuatayo kuonyesha mzizi na viambishi vyake.
(a) nilimchezea (b) atanisomesha
(c) wanalima (d) tutakulimia
(e) vinavyotakiwa (f) tuliwapikia
2. Tenganisha viambishi katika neno ‘nitamletea’ kisha ueleze maana ya
kila kiambishi.
3. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuandika viambishi mwafaka kulingana
na mfano uliopewa.
Kitenzi Nafsi Wakati Kirejeshi Mzizi Kauli Kiishio
(a) aliyepigiwa a– li– ye– pig– iw– a
(b) alivyopigiwa
(c) anayepigika
(d) wanaopigika
(e) tunaopigana
(f) mliopigwa
2. Vivumishi (V)
Vivumishi ni maneno yanayoeleza zaidi juu ya nomino. Kwa mfano: mrefu,
mfupi, zito, kibaya, wakubwa, tano n.k.
(a) Wanafunzi shupavu wamepewa zawadi.
(b) Msichana mtundu atapewa mawaidha.
(c) Majambazi kumi waliingia shuleni mwetu jana usiku.
(d) Nyumba ndefu itajengwa mjini Naivasha hivi karibuni.
(e) Wavulana wawili na wasichana watatu watatembelea kisiwa cha
Unguja mwakani.
Aina za vivumishi
Kuna vivumishi vya aina mbalimbali kama vifuatavyo:
(a) Vivumishi vya sifa
20
21
(b) Vivumishi vya kuonyesha (vionyeshi)
(c) Vivumishi vya kumiliki (vimilikishi)
(d) Vivumishi vya kuuliza (viulizi)
(e) Vivumishi vya idadi
(f) Vivumishi vya pekee
(g) Vivumishi vya majina
(h) Vivumishi vya A-unganifu
(i) Vivumishi vya kurejesha (virejeshi)
(j) Vivumishi vya kusisitiza (visisitizi)
(a) Vivumishi vya sifa
Hivi ni vivumishi vinavyotoa sifa za nomino. Sifa hizi zaweza kuwa nzuri,
mbaya au zozote zile. Kwa mfano:
(i) Mchezaji hodari alishinda mbio hizo.
(ii) Wanafunzi werevu wanasoma maktabani.
(iii) Kisu kikali kilimkata Mwikali.
(iv) Mtoto wangu atavaa nguo sa.
(v) Kijana maskini amesaidiwa na chifu.
(b) Vivumishi vya kuonyesha (vionyeshi/viashiria)
Hivi ni vivumishi vinavyotumika kuonyesha mahali kitu kilipo kwa njia ya
kuashiria. Ni maneno kama: yule, hicho, hivyo, wale n.k. Kwa mfano:
(i) Majambazi hawa wamewasumbua watu sana.
(ii) Kitabu hiki kina mafunzo mengi mno.
(iii) Matunda hayo ni machungu ajabu.
(iv) Mahali huku kuna giza totoro.
(v) Jiwe hilo linaweza kukuangukia.
Zoezi
1. Tunga sentensi ukitumia vivumishi vifuatavyo:
mvivu, mlevi, mrefu, shujaa, mfupi, kibaya, wadogo, vichache
2. Onyesha vivumishi vionyeshi katika sentensi zifuatazo:
(a) Wanawake wale wanawatafuta watoto hawa.
(b) Kioo kile ni kikubwa kuliko kioo hiki.
(c) Maduka haya ni ya mfanyabiashara yule.
(d) Mpira huu ni wa nani?
(e) Wanafunzi hawa na walimu wale watatembelea miji hiyo.
D. Kusoma
Matumizi ya kamusi
Kamusi ni kitabu cha marejeleo (cha kuangalia mara kwa mara)
ambacho hukusanya msamiati au maneno yanayopatikana katika lugha
20
21
inayozungumzwa na jamii fulani. Kitabu hiki huupanga msamiati huo kwa
utaratibu wa abjadi au alfabeti na kuuelezea kwa namna ambayo msomaji
anaweza kuelewa maana yake. Kamusi ni chombo muhimu na cha kimsingi
kwa yeyote anayejifundisha lugha fulani.
Kwa nini kamusi ni muhimu?
1. Huwasaidia watumiaji wake kujua jinsi ya kuliendeleza neno fulani kwa
njia ifaayo; yaani huonyesha tahajia sahihi za maneno mbalimbali.
2. Huonyesha maana au fasili mbalimbali za maneno yaliyoko katika lugha
inayohusika na kwa njia hii kumsaidia mtumiaji kuupanua ujuzi wake
wa lugha hiyo.
3. Hubainisha au huweka wazi aina za maneno. Kwa mfano, msomaji au
mtumiaji anajua ni neno lipi ambalo ni nomino, lipi ni kivumishi, lipi
ni kielezi, wingi wake ni nini n.k. Kwa mfano: Fundo ji ma- chuki,
hasira, kinyongo: ~ la moyo. Pia Mfundo. ‘Ji’ inayofuata neno lenyewe
ina maana kuwa neno ‘fundo’ ni jina au nomino, ‘ma’- inaonyesha kuwa
wingi wake ni ‘mafundo ilhali ~ la moyo inaonyesha ‘fundo la moyo’ ni
nahau au msemo.
4. Huonyesha misemo, nahau au semi na methali mbalimbali zinazopatikana
katika lugha fulani. Kwa kawaida, kuwepo kwa misemo, methali au
nahau huonyeshwa kwa matumizi ya vifupisho kama tutakavyoona hapa
chini.
5. Huweza kuonyesha asili za maneno mbalimbali, kwa mfano, neno fulani
linatokana na lugha fulani. Hata hivyo, sio kamusi zote ambazo huwa
na taarifa hizi.
6. Huonyesha vifupisho mbalimbali vinavyotumiwa katika lugha
inayohusika, kwa mfano: agh = aghalabu nom = nomino, kiel = kielezi,
kiv = kivumishi, n.k = na kadhalika, ki = kiingizi, k.m = kwa mfano,
kv = kivumishi, k.v. = kama vile, (ms) = msemo, (mt) = methali, m.y. =
maana yake, (nh) = nahau, taz. = tazama, kt = kitenzi, (ksh) = kishairi
na kadhalika.
Zoezi
1. Eleza maana ya kamusi.
2. Huku ukitoa mifano, taja faida nne kuu za kamusi.
E. Kuandika
Insha
Insha ni mtungo juu ya jambo fulani ambao huandikwa kwa lugha ya
mfululizo, hupangwa kwa njia nzuri, una mantiki, mtiririko na upatanifu au
mpatano. Madhumuni ya kuandika insha ni kumwezesha mtu kuyawasilisha
22
23
mawazo yake kwa njia inayoeleweka. Kabla ya kuiangalia insha ya maelezo,
inafaa kuangalia mambo muhimu katika uandishi wa insha kwa jumla:
1. Kuigawa insha katika aya mbalimbali na kila aya ibebe wazo moja na
lililokamilika kwa njia nzuri.
2. Pawepo na mpangilio mzuri wa maneno, kama inavyotarajiwa katika
Kiswahili Sanifu.
3. Kutumia lugha inayoeleweka na msomaji wala si maneno ambayo
hayakuzoeleka katika matumizi ya kawaida.
4. Kuigawa insha katika mwanzo, mwili au sehemu kuu na mwisho na
kuzifanya sehemu hizo zionekane wazi na msomaji wa insha hiyo.
5. Kuhakikisha kuwa insha imezingatia suala la nyakati mbalimbali-
wakati uliopita, uliopo na ujao; usichanganye nyakati.
6. Kujali na kuzingatia kwa makini matumizi ya alama za uakishi kama
koma, ritifaa, vituo, n.k.
7. Kuhakikisha kuwa insha haina makosa ya kisaru, maendelezo mabaya
tahajia n.k .
Insha ya maelezo
Maelezo ni maneno yanayofahamisha kitu au habari fulani, yaani ufafanuzi.
Basi insha ya maelezo inahusu kutoa maelezo au ufafanuzi kuhusu kitu,
mahali au jambo kwa jinsi inayomfanya msomaji akifahamu barabara. Kwa
mfano, uwanja wa michezo, jiji kuu nchini, jengo fulani n.k. Insha ya maelezo
huunda picha fulani ya kitu hicho kwa kutumia lugha.
Kituo cha Upimaji na Nasaha (VCT)
Yapata mita mia mbili upande wa kushoto wa barabara inayotoka mji wa
Kibwete, pana jengo kubwa la rangi ya hudhurungi, paa la vigae na madirisha
makubwa ya vioo yenye mapazia ya nili yaliyorembwa maua mazuri. Jengo hili
limepakana na kituo cha mafuta cha BP kwa upande wa kulia. Mkabala wa jengo
lenyewe pana ujia mwembamba unaotumiwa na watembeaji wanaomiminika
kama chungu kila uchao kuelekea mjini. Kwenye jengo hilo zuri na linalovutia
macho ndipo kilipo kituo cha Upimaji na Nasaha cha mji wa Kibwete.
Kwa nje jengo lenyewe linavutia kwa rangi na sura yake pamoja na
mandhari ya pale nje. Pana kitalu kizuri kilichopandwa maua ya kila aina kama
asumini. Kitalu hicho kimezungushiwa uzio ili kuyakinga maua hayo mazuri.
Ujia mdogo unaotoka barabarani kuelekea kituoni umesakiwa vyema; hauna
vumbi na daima huwa sa. Jengo lenyewe lina bango kubwa lenye maandishi
JISHINDE USHINDE VCT.
Kituo hicho kimegawika katika sehemu nne kuu. Kuna sehemu ya mapokezi
ambayo ina makochi mazuri yaliyopangwa kwa nidhamu. Katikati ya makochi
hayo yaliyofunikwa kwa bahameli ya buluu, pana kimeza kidogo cha duara.
Juu ya kimeza hicho pana majarida na vijitabu vya kila aina vinavyohusu afya,
22
23
magonjwa na hata burudani. Sehemu ya pili inahusiana na nasaha au ushauri.
Hapa ndipo wanaposhauriwa na kupewa nasaha walioka hapo kabla ya kupimwa
kama wana virusi vya Ukimwi au la. Wahudumu waliopo hapa ni wapole na wana
vipaji vya kuongea vizuri na watu wanaoka hapo.
Sehemu ya tatu ni chumba cha upimaji damu ambako ndiko shughuli ya
kuchukua damu na kuipima inapotokea. Hapa pia hufanyiwa ushauri kwa kiasi
fulani. Lengo kuu ni kuhakikisha kuwa anayetaka damu yake ipimwe amekata
kauli kabisa. Sehemu ya mwisho ya kituo chenyewe ni mahali pa kuhifadhia
vifaa mbalimbali vinavyotumiwa katika kituo kizima.
Wahudumu wa kituo hiki ni wapole na wana welewa mkubwa wa kazi yao.
Wana uwezo mkubwa wa kufahamisha na kuwaelekeza watu wote wanaoka
pale. Kwa kweli uzuri wa kituo hiki hauishii kwenye sura ya nje tu bali
unaonekana pale ndani. Kituo hiki kinaonyesha uzuri wa ndani na nje sio ule
wa mkakasi ndani kuwa kipande cha mti.
24
25
Sura ya Tatu
A. Ufahamu
Utamaduni
Siku moja babu yangu alinisimulia kisa cha mtu mmoja aliyeona fahari
ya kuzungumza Kiingereza kwa king’ong’o mpaka watu wa eneo la kwao
wakambatiza Ung’eng’e. Kwa sababu ya kusifiwa kutokana na lugha
yake hiyo, Bwana Ung’eng’e alianza kuisahau lugha yake asilia ambayo
hakuona faida yake. Watu walipomkumbusha kuwa ‘mwacha asili ni
mtumwa,’ aliangua kicheko kikubwa. “Nyie hamjui kuwa tunaishi katika
ulimwengu ambao unatawaliwa na Kiingereza?” alisema kwa kiburi. Jambo
la kustaajabisha ni kuwa, siku moja Mwingereza mmoja alipoka katika eneo
hilo kufanya utati fulani, alishindwa kumwelewa Bwana Ung’eng’e. Alisema
kuwa matamshi yake hayakuwa sahihi! Bwana Ung’eng’e alifedheheka sana.
Muda si muda, aligura sehemu ile na hakuna anayejua alikoyoyomea baada
ya kuadhirika vile.
Sijui kama kisa cha Ung’eng’e kilikuwa cha kweli au kilibuniwa na babu
lakini kila ninapokikumbuka hujiwa na suala la mabadiliko ya utamaduni.
Lugha ni chombo muhimu katika utamaduni wa jamii yoyote ile. Ung’eng’e
Baadhi ya vijana hupata utamaduni wa kwingineko kupitia kwenye mtandao.
alikuwa ametekwa na wimbi hilo la kubadilika kwa utamaduni. Lakini ni
nini hasa kinachosababisha kubadilika kwa utamaduni? Kuna sababu nyingi
24
25
zinazotolewa kuelezea mabadiliko ya utamaduni wa jamii fulani. Kwanza,
uvumbuzi mpya huweza kuzua mabadiliko makubwa sana ya kitamaduni.
Tunaishi katika kipindi cha kihistoria ambapo kuna mabadiliko makubwa
ya kisayansi na kiteknolojia. Mabadiliko haya yanaathiri matendo mengi
yaliyokuwako katika utamaduni wetu kwa sababu tunalazimika kuanza
kuyaigiza mambo mageni. Mathalan, mitindo ya mavazi na mienendo ya
watu, kuathiriwa na mawazo na kira za wengine kutokana na matumizi ya
tarakilishi, kuiga maadili na matendo ambayo hayakuwako katika utamaduni
n.k.
Pili, uhamaji na maingiliano ya watu kutoka sehemu mbalimbali
yanaathiri kwa kiasi kikubwa tamaduni za watu. Mathalan, wahamaji wa
nchi nyingine (kama wakimbizi) wanapoingia nchi yetu wanakuja na tabia
fulani maalumu za kitamaduni. Tabia hizi huweza kuenea na kusambaa
nchini na kuathiri tamaduni za jamii mbalimbali. Kwa upande ule mwingine,
watu wanaohamia mijini kutoka maeneo ya mashambani wanakumbana na
mawimbi tofauti ya kitamaduni ambayo yanaweza kuwateka kama Bwana
Ung’eng’e na kuwafanya wabadilishe matendo yao. Mabadiliko yao hayo
yanaweza kuishia kuwakia wenzao vijijini na kuwateka pia.
Tatu, sheria huweza kuchangia katika mabadiliko ya utamaduni
hususan pale ambapo sheria inapitishwa kuyadhibiti matendo fulani ya
kitamaduni. Mfano mzuri ni sheria iliyopitishwa kuhusu elimu ya msingi
ya lazima. Sheria hii inawalazimu wanajamii waliopuuza elimu kwa watoto
na labda hata kuwaoza watoto wakiwa wachanga kubadilisha matendo hayo
ya kitamaduni.
Nne, kuna matukio ya kimaumbile kama zilizala, ukame, gharika au
mafuriko ambayo huweza kusababisha mabadiliko ya kitamaduni. Kwa
nini? Inawezekana matukio haya yakawalazimisha watu kuzuka na mbinu
mpya za kuyazuia kama ujenzi mpya wa majengo, muungano wa pamoja wa
kuyakabili majanga kama hayo na hata kubadilisha imani zao. Kwa njia hii
utamaduni uliokuwako au vipengele fulani vya utamaduni huo vinaanza
kua na hatimaye kuzikwa katika kaburi la sahau. Chanzo kingine cha
mabadiliko ya utamaduni kinachohusiana na matukio haya ni kuwepo kwa
vita. Vita ni mojawapo wa vyanzo vya mabadiliko makubwa ya utamaduni
hususan katika kipindi kifupi sana. Vita huwalazimisha watu wa jamii
fulani kutoka maeneo yao na kuhamia sehemu au nchi nyingine ambayo ina
utamaduni tofauti. Matokeo ya hali hii ni kuchanganyika kwa tamaduni mbili
au zaidi tofauti. Mathalan, kuingia kwa Wamarekani nchini Ujapani baada
ya vita vikuu vya pili vya dunia kulisababisha kuwepo kwa vipengele vya
utamaduni wa Kimarekani kama uvaaji wa suti nchini humo. Kuwapo kwa
vita nchini Somalia, kulisababisha wimbi kubwa la Wasomali kuhamia nchini
Kenya. Asilimia kubwa ya Wasomali hao wameishia kutwaa sifa nyingi za
utamaduni wa nchi ya Kenya kama kuanza kuzungumza lugha ya Kiswahili.
Chanzo kingine na labda kikuu cha kubadilika kwa utamaduni ni
elimu na vyombo vya kisayansi. Mfumo wa elimu tulio nao unasababisha
kasi kubwa ya mabadiliko ya utamaduni. Kuwapo kwa maandishi au vitabu
26
27
kutoka kwa jamii mbalimbali kunaweza kuwafanya wanajamii kujifunza na
hata kuyachukua matendo ya kitamaduni kutokana na jamii mbalimbali
ulimwenguni. Wimbi hilo limeongezeka kwa kuwapo kwa vyombo vya
kisayansi hususan runinga na tarakilishi. Vyombo hivi vinarahisisha
mawasiliano kati ya wanajamii katika ulimwengu mzima katika kipindi
hiki kinachojulikana kama kipindi cha utandawazi. Kasi ya mabadiliko ya
kitamaduni imekia ngazi ya juu sana.
Licha ya hali hii tunayoishi, tunapaswa kukumbuka kuwa utamaduni
ni kitovu cha uhai wa jamii. Ndio, kuna mambo mengi ya tamaduni zetu
mbalimbali ambayo hayafai katika wakati tulio nao, lakini kuna mengine
ambayo bado ni muhimu sana. Ikiwa hatutatambua hili, tutaishia kuwa
kama Bwana Ung’eng’e aliyeipuuza lugha yake na kuishia kufedheheka.
Hatuwezi kuonea fahari utamaduni usiokuwa wetu kwa sababu nguo ya
kuazima haisitiri matako.
Maswali
1. Kwa nini Bwana Ung’eng’e alibatizwa jina hili?
2. Je, ni sababu gani iliyomfanya Bwana Ung’eng’e kuaibika? Je, unajifunza
nini kutokana na kisa hiki?
3. Taja sababu nne kuu zinazosababisha mabadiliko ya utamaduni.
4. Ni nini maana ya msemo “mwacha asili ni mtumwa”?
5. Eleza maana ya maneno yafuatayo kisha uyatumie kutungia sentensi:
(a) aligura (b) alikoyoyomea (c) kuadhirika (d) zilizala
(e) utandawazi
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimu Jamii: Mazungumzo hotelini
(Pana meza kadha. Wanaingia wateja wawili, Atieno na Kembo. Wanatafuta
mahali pa kukaa. Mhudumu wa hoteli anawaendea na kupangusapangusa
meza ile)
MhuduMu
: Karibuni (anatua). Mtapewa
nini?
aTieno
: Tutapewa nini? Je, hata
salamu hatupewi siku hizi
au nazo pia zinauzwa?
MhuduMu
: Ahh, samahani, habari
za leo?
keMbo
: Nzuri, wambaje?
MhuduMu
: Mzima.
aTieno
: Ehh, hivyo ndivyo
26
27
inavyotakiwa. Ndiyo jadi yetu Waafrika; licha ya umaskini
wetu bado tuna utu wetu au sio? (Mhudumu anaitikia)
MhuduMu
: Basi niwape nini?
keMbo
: (Kwa Atieno) Wewe kwanza. (Mhudumu anageuka nyuma na
kuchukua menu iliyoko juu ya meza ya pili na kumnyooshea
Atieno.)
aTieno
: Nipe chai, maandazi mawili na kimanda kimoja… (Anatulia)
Hivyo tu!
keMbo
: Mna kahawa?
MhuduMu
: Ipo ndiyo.
keMbo
: Basi kahawa kwangu, maandazi mawili na yai la kutokosa.
MhuduMu
: Kahawa ya maziwa au isiyo nayo?
keMbo
: Ya maziwa.
(Mhudumu anaondoka, baada ya muda anawaletea
walivyoagiza. Atieno na Kembo wanaanza kunywa chai
na kahawa, wakila vitafunio na kuongea mara moja
moja. Baada ya muda wanamaliza. Atieno anamwashiria
mhudumu)
aTieno
: Jumla ngapi?
MhuduMu
: Mia moja hamsini.
(Atieno anachukua mkoba wake mdogo na kutoa noti ya
shilingi mia mbili na kumkabidhi mhudumu ambaye
anaondoka)
keMbo
: (Akichekacheka) Nilitakiwa kulipa mimi!
aTieno
: Mbona wewe?
keMbo
: Si utamaduni! Mwanamume ndiye anayetakiwa kulipia bili!
aTieno
: Hizo ni kira za zamani! Sote tunafanya kazi mbona nisilipe
mimi.
keMbo
: Kweli ehh!
aTieno
: Ndiyo ehh, sisi sio watumwa wa utamaduni (Mhudumu
anarudi na kuwakabidhi bakaa yao. Wanasimama
kuondoka)
keMbo
: Kwaheri.
aTieno
: Na asante kwa huduma sa!
MhuduMu
: Kwaherini na karibuni tena!
Maswali
1. Je, kwa nini Atieno analalamika wanapoingia hotelini?
2. Eleza maana ya maneno haya:
28
29
(a) kimanda
(b) yai la kutokosa
(c) bakaa
3. Kwa nini Kembo anasema angelipa yeye? Je, una maoni gani kuhusu
suala hili? Jadiliana na wenzako darasani.
4. Kwa kurejelea kifugu cha mazungumzo hapo juu, taja sifa tano za sajili
ya hotelini.
C. Saru na matumizi ya lugha
Nomino
Nomino ni neno linalotaja kiumbe, hali, dhana, tendo, mahali au kitu chochote
kile; kwa mfano: nyumba, kengele, Maria, kisu, shamba, kulima n.k.
1. Wazee wa kanisa hili watakutana kesho alasiri.
2. Baba alinunua kondoo wawili, ngamia mmoja na mbuzi wanne.
3. Kenya, Uganda na Tanzania ni nchi zenye amani.
4. Nyumba hii ni ya nani?
5. Okoth na Aketch wamekwenda Ahero.
Zoezi
Onyesha nomino katika sentensi zifuatazo:
(a) Mto huu unaitwaje?
(b) Jambazi lile litashikwa na polisi.
(c) Niletee meza mbili na viti vitatu.
(d) Kalamu hii haiandiki hata kidogo.
(e) Ni nani meya wa Kakamega?
(f) Watieri ana watoto sita.
(g) Mwikali yuko wapi?
(h) Je, umemwona Salome au Chebet?
Aina za nomino
Nomino hugawika katika makundi yafuatayo:
1. Nomino za jumla (kawaida)
2. Nomino za pekee
3. Nomino dhahania
4. Nomino za jamii
5. Nomino za wingi
6. Nomino za vitenzi-jina
Nomino za jumla (kawaida)
Hizi ni nomino zinazotaja kitu bila kukitambulisha kwa jina lake halisi. Kwa
mfano, ikiwa ni mji hatuambiwi kama ni Nairobi, Mombasa au Kisumu.
28
29
Ikiwa ni mtu hatuambiwi kama ni Rosalia, Kiragu au Omwenga. Ikiwa ni
nchi hatuambiwi kama ni Kenya, Uganda, au Tanzania. Hutajwa tu kwa
jumla. Kwa mfano:
1. Watu wengi walika uwanjani jana alasiri.
2. Nchi hii ina wachezaji wengi shupavu.
3. Kitabu hiki ni cha nani?
4. Mto huu ni mrefu mno.
5. Mwalimu wao alika leo asubuhi.
Nomino za pekee
Tofauti na nomino za jumla, nomino za pekee hutaja kitu kwa kukitambulisha
waziwazi kwa jina au majina yake kamili. Kwa mfano, ikiwa ni mtu
tunaambiwa kama ni Kiseku, Mwajuma au Kariuki. Kama ni mto tunaambiwa
kama ni Tana, Nzoia au Miriu. Ikiwa ni ziwa tunaambiwa kama ni Viktoria,
Tanganyika au Bogoria. Ikiwa ni mwalimu, tunaambiwa kama ni Bi. Kamau,
Bi. Mwende au Bw. Makori. Kwa mfano:
(a) Mto wa Nile hupitia nchini Uganda, Sudan na Misri.
(b) Nkatha, Nteere na Mbogori wanasoma shuleni Nkubu.
(c) Ni ziwa lipi lililo na kina kirefu zaidi kati ya Viktoria, Naivasha na
Elementaita?
(d) Mama ameninunulia kitabu cha hadithi kiitwacho Mtu Mwenye
Miwani Myeusi.
Zoezi
Soma kifungu kifuatacho kwa makini.
Amina alikubali kuishi na Zawadi katika nyumba yake marehemu Rashid,
kule Kisauni. Dhiki iliyomkusa Zawadi ilikuwa kubwa mno. Bila shaka
alihitaji mtu wa kumhani na kumfariji. Nilishangaa kuona jinsi mabanati
hawa wawili walivyopatana na kuwa na itifaki njema baina yao. Walipendana
kama ndugu wa toka nitoke. Lao lilikuwa moja, la tamu na chungu. Baada
ya kitambo fulani cha kuomboleza, Zawadi akaanza kufundisha katika shule
ya msingi ya Mlaleo. Amina akawa yuauza matunda, viungo mbalimbali
na mboga pale pale Kisauni. Watu waliona vigumu kusadiki kuwa Amina
alimtupa jongoo na mti wake wala hakuwazia ukahaba tena. Ilikuwa
kama ajabu ya samaki kukataa maji na kwenda kuishi nchi kavu. Alikuwa
kajikwamua toka kwa tope la umalaya lililokuwa limemgandisha tangu hapo.
(Kifungu kimenukuliwa kutoka Siku Njema, na K. Walibora uk 86 ).
Kutokana na kifungu hicho kuna nomino kadha zilizoandikwa kwa heru
za mlazo. Orodhesha nomino hizo mahali pafaapo kwenye jedwali lifuatalo:
30
31
nomino za kawaida (jumla) nomino za pekee
K.m. shule Amina
Kuakisha
Kuakisha ni utumiaji wa alama mbalimbali katika maandishi ili kuweza
kuwasiliana vizuri na msomaji. Kunazo alama nyingi za kuakisha. Baadhi
ni kama zifuatazo:
1. Kitone/kikomo/nukta (.)
Hii ni alama inayotumika katika maandishi mbalimbali kama ifuatavyo:
(a) Mwishoni mwa sentensi. Kwa mfano:
(i) Baba yake amemnunulia mpira maridadi.
(ii) Watu walioka asubuhi ni wahubiri.
(iii) Kaikai ana watoto wawili.
(iv) Nguo zake zimeraruka.
(v) Nyumba hii inafaa kufagiliwa.
(b) Kuandika maneno kwa kifupi. Kwa mfano:
(i) Bw. Paul Mairongi (Bwana Paul Mairongi)
(ii) Bi. Rehema Mwanaisha (Bibi Rehema Mwanaisha)
(iii) S.L.P 451 Narok (Sanduku la Posta 451 Narok)
(iv) D.W. Musyoka (Daniel Williams Musyoka)
(c) Kutenganisha fedha shilingi na senti. Kwa mfano;
(i) 10.60 shilingi kumi na senti sitini
(ii) 3.40 shilingi tatu na senti arubaini
(iii) 99.90 shilingi tisini na tisa na senti tisini
2. Mkato/kipumuo/kituo/koma (,)
Alama hii hutumika katika mazingira yafuatayo:
(a) Wakati msomaji anapohitaji kutua. Kwa mfano:
(i) Baada ya wachezaji hao kusakata kabumbu kwa muda wa
dakika arubaini na tano, walikwenda mapumzikoni.
(ii) Ingawa wazazi wake walimlea Selemani Mapunda kwa tunu na
tamasha, aliwaaibisha kwa kujiunga na genge la majambazi.
(iii) Kwa vile wazazi wengi hapa nchini hawana uwezo wa
30
31
kuwapeleka watoto wao shuleni, walifurahi sana serikali
ilipotangaza masomo bila malipo katika shule zote za msingi.
(b) Kutenganisha maneno kwenye orodha. Kwa mfano:
(i) Siku ya mtihani nitahitaji kalamu, penseli, raba na madaftari
kadhaa.
(ii) Humo sokoni wanauza mbaazi, maharagwe, malimau, viazi na
mawele.
(iii) Nataka uninunulie kikombe, kijiko, sahani na uma.
(iv) Ng’ombe, punda, mbuzi, kondoo na ngamia ni wanyama wa
kufugwa.
(c) Kuandika anwani. Kwa mfano:
Hospitali kuu ya Jijibora,
S.L.P 11122,
JIJIBORA.
(d) Kabla ya kuandika (Kunukuu) maneno yaliyozungumzwa na msemaji
fulani. Kwa mfano:
(i) Askari aliponiona alisema, “Mikono juu mara moja.”
(ii) Mgeni alipoka mlangoni alibisha, “Hodi kwa wenyewe.”
(iii) Kabla ya kuondoka mama alitwambia, “Nitakaporudi nataka
nikute mmekamilisha kazi niliyowapa.”
(e) Baada ya maneno kama ndio, asante, n.k. Kwa mfano:
(i) La, hakuniambia atanikopesha pesa kamwe.
(ii) Ndio, nitafanya yale yote uliyoniambia.
(iii) Asante, nimefurahi sana kwa yote uliyonitendea.
(f) Baada ya kutaja jina la mtu anayepewa habari. Kwa mfano:
(i) Daktari, nimeka hapa ili unipe ushauri kuhusiana na ugonjwa
ulionisumbua kwa muda mrefu.
(ii) Mwalimu, mimi sikuelewa funzo la leo hata kidogo.
(iii) Mheshimiwa rais, watu wa eneo hili wanakuunga mkono kwa
dhati.
3. Heru kubwa
Heru kubwa hutumika mwanzoni mwa maandishi ya aina mbalimbali
kama yafuatayo:
(a) Mwanzoni mwa nomino za pekee:
Nomino za pekee ni zile zinazotaja jina la kitu, mtu, mahali na kadhalika
kwa majina yake kamili. Nazo ni kama zifuatazo:
(i) Za miezi: Oktoba, Novemba, Disemba na kadhalika.
(ii) Za watu: Kamau, Okoth, Oliech.
32
33
(iii) Za vitabu: Walenisi, Kiu, Kilio cha Haki.
(iv) Za siku za wiki: Alhamisi, Ijumaa, Jumamosi.
(v) Za sikukuu: Idd ul Fitr, Jamhuri, Krismasi
(vi) Za vyeo: Profesa Kimalat, Mfalme Suleimani, Malkia Viktoria.
(vii) Za mitaa: Dandora, Urumo, Zimmerman.
(viii) Za mahali: Nairobi, Kampala, Tanzania.
(ix) Za dini: Kikristo, Kihindu, Kiislamu.
(x) Za lugha: Kikikuyu, Kikamba, Kiyao.
(b) Mwanzoni mwa sentensi . Kwa Mfano:
(i) Wazee wamekatalia mbali ombi lako.
(ii) Mimi ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza.
(iii) Unakwenda wapi?
Zoezi
1. Andika heru kubwa, kikomo, au kipumuo mahali pafaapo kwenye
sentensi zifuatazo:
(a) kisumu, nairobi na mombasa ni miji mikuu ya kenya
(b) naftali temu, nyantika maiyoro, sarana antao, kipchoge keino na
julius sang’ ni wanamichezo wakongwe walioiletea nchi yetu sifa
nyingi
(c) ziwa tanganyika ziwa nyasa na ziwa turkana yako katika eneo la
mashariki mwa afrika
(d) mimi sipendi kitabu kiitwacho kikulacho ki nguoni mwako
(e) mwaka jana nilitembelea nchi za ufaransa ujerumani uingereza na
uhispania
2. Soma kifungu kifuatacho kisha ukisahihishe kwa kuandika heru kubwa
au kikomo mahali pafaapo:
Watu walishikilia kusema kuwa familia yetu ilikuwa na bahati ya
kikristo. baba alitamani familia hiyo iwe kielelezo cha kuigwa Yaelekea
watu walishaitambua dhamira yake hiyo au pengine yenyewe ilishaanza
kutekelezeka.
Sote tulikuwa wanne; watoto wanne, wote wasichana Mimi ndiye
niliyekuwa kifungua mimba. aliyenifuata ni roselyn, naye akafuatwa na
jacquiline. Kitinda mimba alikuwa redemta. Kati yangu na mnuna wangu
Roselyn palikuwa na tofauti ya miaka mitatu.
Kati ya Roselyn na Jacquiline palikuwepo na tofauti ya mwaka mmoja.
Siku moja nilimdadisi mama kuhusu tofauti hiyo ya miaka kati yangu na
roselyn. nilikuwa mtoto mdogo siku hizo. Mama alibabaisha tu; siyakumbuki
maelezo yake sawasawa ila alibabatiza kitu kama yalikuwa matokeo ya
mapenzi ya mungu lakini sikuacha kushangaa yalikokuwa mapenzi hayo
wakati wadogo zangu walipozaliwa. labda mapenzi ya mungu yalikuwa ya
32
33
aina mbalimbali. Nilishawishika kumuuliza baba lakini nilishindwa. alikuwa
mkali sana. Hakupenda maswali ambayo hayakuwa na maana Alisema
kuwa watoto wa familia ya kikristo hawakuwa na budi kuuliza maswali
yenye mwelekeo wa kikristo. siku hizo ilikuwa vigumu kujua ni maswali
yapi yaliyokuwa na mwelekeo huo Yaelekea mama naye hakuyajua maswali
hayo. haikosi tungeyajua siku moja. siku hiyo tungekuwa na uhuru zaidi.
(Imenukuliwa kutoka Nguvu ya Sala na K. W. Wamitila, uk 1).
D. Kusoma
Matumizi ya maktaba
Maktaba ni chumba ambako vitabu huhifadhiwa, kuazimwa na kusomwa.
Maktaba ni muhimu kwa kuwa inatusaidia kupata na kuyaendeleza maarifa
yetu mbalimbali katika masomo tofauti. Maktaba pia hutusaidia wakati
wa utati kwa kuwa huwepo vitabu vingi sana. Maktaba ni nyingi na za
aina mbalimbali kama vile: maktaba ya kibinafsi, maktaba ya taifa/umma,
maktaba ya darasa, maktaba ya shule, maktaba maalum ya kutunza nyaraka
muhimu yaani maakaba n.k.
Mambo ya kuzingatia uendapo maktabani
(a) Kutopiga kelele au kuwa na vifaa vitoavyo sauti kama, funguo n.k.
(b) Kutembea taratibu na kutowaghasi watumiaji wengine wa maktaba.
(c) Kutouvuruga utaratibu au mpangilio wa vitabu.
(d) Kuvitunza vitabu vya maktaba kwa njia ifaayo.
(e) Kuzingatia wakati ulioagizwa kuvirudisha vitabu vya maktaba.
(f) Kuwa na daftari ya kuandikia matokeo ya usomaji wako.
Vitabu vya marejeleo
Maktaba huwa na vitabu vingi na vya kila aina kuhusu masomo, mada na
masuala mbalimbali. Miongoni mwa vitabu hivi ni vile vinavyojulikana kama
vitabu vya rejea au marejeleo. Hivi ni vitabu ambavyo huwa na taarifa kuhusu
masuala mbalimbali au vinavyokuelekeza unakoweza kuipata taarifa hiyo.
Vitabu vya aina hii hutusaidia kupanua maarifa yetu. Vitabu hivi ni kama:
1. Ensaiklopedia: Hiki ni kitabu ambacho kina mkusanyiko wa makala
mbalimbali kuhusu mambo tofauti tofauti. Makala hizo huweza
kuambatanishwa na michoro, ramani n.k. Ikiwa unaandika ripoti fulani,
unaweza kufaidika sana kutokana na ensaiklopedia.
2. Vitabu vya ramani au atlasi: Hivi ni vitabu ambavyo huwa na ramani
zenye taarifa nyingi kuhusu nchi au miji fulani. Atlasi ni muhimu sio tu
katika somo kama jiograa bali pia kwa kutusaidia kuyapanua maarifa
yetu kuhusu nchi yetu, bara letu au ulimwengu wetu.
3. Kamusi: Maktaba huwa pia na kamusi za aina mbalimbali ambazo
hutusaidia tunapokumbana na maneno magumu katika kusoma kwetu.
34
35
Zoezi
(a) Taja aina nne tofauti za maktaba. Je, ni aina zipi zinazopatikana
karibu na unapoishi?
(b) Je, vitabu vya marejeleo ni nini na kwa nini ni muhimu kwetu?
E. Kuandika
Hadithi fupi
Hadithi fupi ni kisa ambacho huandikwa kwa maandishi ya nathari (ya
mfululizo au mjazo) ambacho husimulia tukio moja ambalo limekamilika na
ambalo huhusiana na hali au tendo la binadamu. Msingi mkubwa wa hadithi
fupi ni kuwa kisa kinachosimuliwa lazima kiweze kusimuliwa kwa ufupi.
Hadithi fupi nzuri humfanya msomaji aweze kugusika na avutiwe nayo.
Sifa za hadithi fupi
(i) Huhusu sehemu ambayo si pana sana kama riwaya; ambayo
inaweza kugusia matukio mengi yanayotokea sehemu
mbalimbali.
(ii) Huwa ni kazi ya kisanaa (yenye ufundi wa matumizi ya lugha)
ambayo ni fupi.
(iii) Hutumiwa kusimulia tukio moja kuu kwa sababu hakuna nafasi
ya kuzungumzia matukio mengi na wahusika wa utendaji wa
tukio hilo ni wachache.
(iv) Mhusika mmoja tu ndiye anayetawala tukio hilo kuu; hapana
nafasi ya wahusika wengi kama ilivyo katika riwaya.
(v) Mtindo wake ni mwepesi na unaweza kufuatika.
Muundo wa hadithi fupi
(a) Mwanzo: Hii ni sehemu muhimu ambapo unatakiwa kuhakikisha
kuwa umeivuta hamu ya msomaji pamoja na kuwatanguliza wahusika
au watendaji walioko hadithini na kuonyesha mwelekeo wa hadithi
hiyo. Hadithi fupi nzuri huanza kwa tatizo fulani na kukuzwa kwa
wahusika. Tatizo hilo linakuwa msingi wa kumfanya anayesoma awe
na hamu ya kusoma au taharuki.
(b) Mwili au sehemu kuu: Hapa lile suala kuu linaendelezwa; kwa
kuonyesha kuna mambo gani yanayotendeka, kuna misukosuko gani
na jinsi inavyoiendeleza hadithi hiyo.
(c) Mwisho: Sehemu hii inatuelekeza kwenye kilele cha hadithi na jinsi
tatizo fulani, linavyosuluhishwa, kama lipo. Mwisho huo lazima uwe
na mvuto mkubwa. Njia moja ya kufanya hivi ni kuwepo kwa mwisho
ambao haukutarajiwa na msomaji.
(d) Dhamira: Je, ni lengo gani kuu katika hadithi hiyo? Lazima kila hadithi
iwe na jambo ambalo unataka kuliandikia; kisa unachokisimulia,
mkasa fulani, tukio lililotokea n.k.
34
35
(e) Msuko: Lazima matukio yaliyopo yaonyeshe mpango mzuri wa
kuingiliana kwa matukio, tukio liwe na uhusiano na jingine yaani
lazima msomaji aweze kuona uhusiano huo na uwe umepangika
vizuri. Mpangilio huo ndio unaojulikana kama msuko.
Mambo ya kuzingatia unapoandika hadithi fupi:
(i) Iwe na mvuto wa kisanaa au matumizi ya lugha ambayo
yanampendeza msomaji wa hadithi hiyo; aweze kuikumbuka
baadaye.
(ii) Iweze kuiamsha hamu ya msomaji na imtie hamu ya kutaka
kuendelea kusoma na kutambua ni kitu gani kitakachotokea
baadaye.
(iii) Iwe hadithi iliyopangwa kwa mpango unaoonyesha mantiki na
unaoweza kufuatika na msomaji wa hadithi hiyo.
(iv) Ionyeshe matumizi fasaha ya lugha na kanuni nyingine za
uandishi kama alama za uakishi.
(v) Mwanzo na mwisho wake uwe wa kuvutia na uweze
kukumbukwa na msomaji wa hadithi hiyo.
Mfano wa hadithi fupi
Ndoto ya Chifu
Siku hiyo, Chifu Kibarasi aliamka akiwa na furaha nyingi ajabu. Kwa miezi
kadha iliyopita alikuwa akijiandalia siku hii kwa matumaini makubwa
sana. Tangu ilipotangazwa kuwa rais wa nchi atalitembelea eneo lao,
Kibarasi alianza kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha amepiga
hatua kubwa kimaendeleo. Hii ilikuwa nafasi ya pekee ya kumpendeza rais
wa jamhuri ambaye lazima angetambua juhudi zake na kumtunuku; labda
hata kumpandisha cheo.
Kwa muda mrefu eneo la kwao lilijulikana katika tarafa nzima kwa
ukosefu wa usalama. Visa vya wizi wa nguvu, ujambazi na maovu mengine
yalikuwa yamekithiri. Wananchi walilalamika lakini hamna lililofanyika
kwa kuwa Chifu Kibarasi alijitia hamnazo, hakujali kabisa. Watu walipiga
ripoti kwake mpaka wakakinai; wakaacha, naye akaendelea kufurahia maisha
yake kama zamani. Lakini habari za safari ya rais zilipotangazwa na redio
ya taifa, Chifu Kibarasi alivuvumka ghaa kama mlima wa volkeno. Sasa
alianza kufuatilia masuala hayo kwa nguvu mpya; hata magenge ya kuuzia
pombe ambayo yalikuwa yamechipua kama mmea wa uyoga yalikumbana
na Chifu Kibarasi mwingine.
Siku ya mkutano wa rais ilipowadia, Chifu Kibarasi aliamka mapema,
akavipiga viatu vyake rangi kwa mwangaza wa taa ya chemni. Hakutaka
kusubiri mpaka kucha kwa jua kwa kuhofu kuwa atachelewa na kuikosa
nafasi ya kupanda cheo. Asubuhi alipata chamshakinywa kwa wasiwasi;
hakuwa hata na subira ya kuimaliza chai yake, asije akamchelewesha
rais. Ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuka ulipofanyika mkutano huo
36
37
wa kiongozi wa nchi. Waliomwona Chifu Kibarasi walishangaa kwa jinsi
alivyokuwa amevaa kinadhifu. Wengine walimtania kwa kumwuliza, “Chifu,
waelekea arusini nini?” Naye aliwakumbusha , “Hivi ninyi hamjui kuwa hii ni
siku kubwa, siku ya ziara ya rais wa nchi?” aliwauliza. Hawakuelewa kuwa
alikuwa akitaraji kupandishwa cheo kutokana na juhudi zake za kufanya
kazi kwa nguvu.
Mkutano wa rais ulianza saa nne. Ingawa chifu Kibarasi alijitahidi
kuwa miongoni mwa watu waliomkaribisha rais, hakufanikiwa. Kazi
hiyo ilikuwa ya mkuu wa wilaya. Lakini Chifu Kibarasi hakukata tamaa,
aliamua kutumia mbinu nyingine ili kuhakikisha kuwa rais wa nchi
amemwona. Huko nyuma alikoketi alikuwa akipinda shingo huku na huku
kwa matumaini ya kuonekana na rais. Lakini hiyo haikufaa; baadaye
alisimama na kwenda sehemu ya mbele ambapo palikuwa na watu waliokuwa
wakisukumanasukumana kuelekea lilipokuwa jukwaa la rais. Alijua kuwa
akisimama huko na kuonyesha juhudi zake za kuwatuliza watu lazima rais
atamtambua na kupendezwa na utendakazi wake.
Rais aliposimama alizungumzia mambo mengi kuanzia umuhimu
wa elimu mpaka juhudi za serikali yake za kuwasaidia wananchi wake.
Aliwapongeza watu wa eneo hilo kwa juhudi zao za kulijenga taifa. Wakati
wote huu Chifu Kibarasi alikuwa ametega masikio yake kusikia kama atasikia
jina lake likitajwa na kupongezwa kwa mchango wake mkubwa. Alisikiliza
kwa makini na matumaini makubwa lakini rais hakulitaja jina lake wala
kumpandisha cheo alivyotarajia.
Rais alipoimaliza hotuba yake alisimama na kuelekea sehemu
walipokuwa watoto waliomtumbuiza kwa nyimbo nzuri. Sasa matumaini
ya Chifu Kibarasi yaliongezeka kwa sababu kundi hilo lilikuwa karibu na
alipokuwa amesimama. Alimwangalia kiongozi wa nchi kwa matumaini
makubwa. Rais aliwapongeza na kuondoka kuelekea lilipokuwa gari lake
la kifahari. Chifu Kibarasi aliamua kupiga hatua kuelekea huko labda
kumkumbusha rais kuwa alimsahau lakini walinzi wa rais hawakumruhusu.
Baada ya muda mfupi, msafara wa rais uliondoka na kutifua vumbi ukielekea
mjini.
Watu walifumukana kuelekea makwao na kumwacha Chifu Kibarasi
pale pale aliposimama akiangalia magari ya msafara wa rais yakipotelea
kwenye upeo wa macho. Viatu vyake vilivyokuwa viking’ara asubuhi vilikuwa
na vumbi jingi ajabu. Ndoto yake ya kupandishwa cheo haikutimia.
Zoezi
Baada ya kuusoma mfano huu, andika hadithi fupi kuhusu mojawapo wa
vichwa hivi.
(a) Jambazi sugu.
(b) Pigo la Maisha.
36
37
Sura ya Nne
A. Ufahamu
Bwana Aisee na Mradi Kabambe
Watu waliosoma na Bakuzi Baku walimjua kwa sababu moja tu. Alikuwa
mpenzi mkubwa wa lugha ya Kiingereza. Shuleni walimu walipenda kumteua
asome vitabu vya hadithi kwa sauti kwa kuwa walisema alijua kuyatamka
maneno ya Kiingereza kwa ufasaha mkubwa kama Waingereza wenyewe.
Ubingwa wake huu ulitokana na wepesi wake wa kuwasikiliza walimu
waliofundisha somo hilo kwa makini. Kutokana na tabia yake hii alipachikwa
majina ya kila aina: Bwana Aisee, Bwana Ung’eng’e, Bwana London na
mengine mengi.
Lakini jina la ‘Aisee’ ndilo lililoshika mizizi zaidi kutokana na tabia yake
ya kusema, “I say,” kila mara alipokuwa akizungumza. Tangu wakati huo,
jina lake la asili la Bakuzi Baku likapotea. Akawa ‘Aisee’. Watu waliokutana
naye baadaye hawakumjua kwa jina jingine isipokuwa ‘Bwana Aisee’.
Baada ya kumaliza masomo yake, Bwana Aisee aliyoyomea jijini Nairobi
kutafuta kazi. Alikuwa na bahati kama mtende kwani alipata kisimati cha
kazi katika kiwanda kimoja cha kusindika mafuta. Lakini hakukaa sana
hapo. Akafanya kazi kwa muda kisha akaondoka. “Aisee bwana, mtu lazima
utafute ustaarabu. Kukaa mahali pamoja sio ustaarabu, unaweza kuota
mizizi aisee!” aliwaambia waliomdadisi.
Baada ya kutoka kwenye kampuni hiyo ya mafuta, Bwana Aisee
akapata kazi nyingine katika shirika fulani la kimataifa. Bila shaka Bwana
Aisee alikuwa na nyota ya jaha. Kazi yake mpya ilimwezesha kupata fursa
ya kusari nchi nyingi ulimwenguni. “Aisee bwana, ni vyema ukatembea
uone dunia. Mtu hawezi kuishi pale pale kama jiwe,” alisema Bwana Aisee.
Aisee alitembelea nchi nyingi tangu Bukini, Ngazija, Omani, Ushelisheli
hadi Ufaransa na Ujerumani. Hali yake ya kiuchumi nayo ikapanda. Sasa
alikuwa na mali nyingi iliyomwezesha kuanzisha makampuni ya kila aina
jijini Nairobi na hata huko ng’ambo. Sasa hakuwa tena yule Aisee watu
waliomfahamu. La hasha. Alikuwa Bwana Aisee tofauti kabisa.
Hata hivyo, wakati Bwana Aisee alipanda ngazi ya kiuchumi, hali
ya wananchi wengi nchini iliendelea kuwa ya kuhuzunisha. Matatizo ya
kiuchumi yalifanya vijana wengi waliohitimu masomo kukosa nafasi za kazi.
Wengine waliokuwa na kazi hizo walifutwa kutokana na mipango mbalimbali
ya makampuni ya kuyabana matumizi yao. Watu wengi walijikuta mitaani
wakizunguka kutwa kuchwa bila ya kujua watakula nini wala watalala wapi.
Wengine walijikuta wakijutia pesa walizozihariji siku za nyuma walipodhani
watakuwa kazini milele wakiongozwa na ile imani ya ponda raha kufa kwaja.
Kwa wengi, jua la maisha yao mazuri lilikuwa linaelekea machweo. Lakini
kwa upande wa Bwana Aisee, jua la ufanisi lilikuwa bado mawio.
38
39
Siku moja Bwana Aisee alipokuwa katika safari zake katika nchi
za kigeni alikutana na maraki wawili mmoja kutoka nchi ya Nigeria na
mwingine kutoka huko Uarabuni. Wote walimchulia mpango waliokuwa
nao wa kuhakikisha wamekiongeza kipato chao maradufu tena bila ya
kusumbuka sana. Bwana Aisee alisisimka aliposikia mambo hayo na
kukubaliana nao mara moja, “Aisee bwana, huu ndio mradi kabambe hasa!
Kwa nini sikuuwazia kwa miaka hiyo yote! Hizo mbio mbio zote kila mahali
zingekuwa zimeishia kwenye ukingo wa pesa kochokocho! Aisee ni kweli
wajinga ndio waliwao!”
Bwana Aisee aliporudi jijini alifungua osi kubwa aliyoipamba kwa
samani za hali ya juu. Kisha, aliwasiliana na waandishi wa magazeti
mbalimbali. Alidai kuwa kulikuwako na mradi kabambe wa kuhakikisha
kuwa vijana waliokosa kazi wangeajiriwa kazi za maana kwenye mahoteli
ya kitalii huko Uarabuni na Ulaya na hata kwenye meli za kifahari. Viongozi
wengi walimshehenezea Bwana Aisee sifa kemkem. “Huyu ni mzalendo
kindakindaki! Anawakumbuka raia wenzake ambao hawana bahati kama
yeye!” Vijana waliokuwa na hamu na ghamu ya kwenda ugenini walifurika
ilipokuwa osi yake.
Walichohitajika kufanya tu ni kulipa ada ya shilingi elfu tano pamoja na
kiasi kingine kama hicho kugharamia vyeti vya usari. Licha ya kuwa wengi
wao hawakuwa na namna ya kuzipata pesa hizo, walikuwa radhi kukopa
wahakikishe kuwa wamepata nafasi hizo adimu. Vijana hao walitakiwa pia
kwenda hospitali fulani ya kibinafsi kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
“Aisee bwana, huo ndio ustaarabu wa wenzetu walioendelea. Ukitaka
kumwajiri mtu lazima uijue afya yake ikoje,” Bwana Aisee aliwakumbusha.
Hamna aliyejali. Kilichokuwa muhimu ni kuwa, baada ya miezi miwili
wangepata kazi ambazo zingewafanya waupige kumbo la milele umaskini
uliotishia kuwagubika kama mawingu.
Baada ya kuzikusanya hela hizo zilizolipwa na vijana zaidi ya elfu
thelathini, Bwana Aisee aliwaambia wangoje kwa muda wa miezi miwili.
Muda waliokuwa wamepewa wa kungojea mambo yaive ukapita. Tarehe ya
kusari kwenda kuanza kazi zao ikaahirishwa. Taarifa iliyotoka katika osi
kuu huko Ulaya ilidai kuwa kuahirishwa huko kulitokana na hali mbaya
ya usalama. Tarehe hizo zilipoahirishwa mara nyingine mbili, kila mmoja
alianza kutuhumu kuwa palikuwa na jambo. Malalamishi ya kila aina
yalianza kusikika kwenye vyombo vya habari. Wakaanza kumtafuta Bwana
Aisee. Lakini hawakujua kumbe bwana huyo alikuwa tayari ameingia mitini.
Uchunguzi wa historia ya Bwana Aisee ulianza kufanywa. Jamaa
waliosoma naye walitoa habari zake zote bila ya kusaza lolote. Walieleza jinsi
alivyokuwa fundi wa kuongea Kizungu. “Lakini huyu si fundi wa Kizungu
tu bali wa mizungu pia!” walisema wengine kwa hasira waliposikia habari
hizo. Serikali ilianza mipango kabambe ya kumsaka Bwana Aisee. Ilibidi
kuwashirikisha wachunguzi wa polisi wa kimataifa, INTERPOL, katika suala
zima. Haikuchukua muda kabla ya kugunduliwa kuwa mashirika yaliyodaiwa
kuhusika na suala la ajira hizo yalikuwa ya bandia.
38
39
Mambo yaliendelea kukanganya wakati osi ya Bwana Aisee iliyokuwa
jijini ilipochomeka siku moja wakati wa usiku na vyeti vyote kuteketea.
Nayo hospitali walikokuwa wameenda kufanyiwa uchunguzi wa kiafya wale
walioomba kazi ilifungwa ghaa na daktari aliyehusika kutoweka. Ilikuwa
wazi sasa kuwa watu walikuwa wametapeliwa.
“Kashfa ya Aisee” ilizungumziwa na wengi kote nchini si kwenye redio,
runinga lakini hata magazetini na kwingineko. Watu walilaani. Lakini njia
ya mwongo fupi. Bwana Aisee alibambwa na polisi wa kimataifa alipokuwa
kwenye uwanja wa ndege wa Frankfurt huko Ujerumani akijitayarisha
kupanda ndege kuelekea Afghanistan alikopanga kujicha kwa muda hadi
mambo yatulie.
Baada ya kutiwa mikononi, Bwana Aisee alisafirishwa chini ya
ulinzi mkali hadi jijini Nairobi alipokishwa mbele ya hakimu. Kesi yake
ilihudhuriwa na mamia ya vijana waliohasirika. Mwishowe, Bwana Aisee
alitumbukizwa gerezani kwa miaka minane ikiandamana na kazi za shokoa.
Mizungu yake ilikuwa imegota ukingoni. Kiingereza chake hakikumfaa tena.
Alibakia kugugumia, “…Ais....Aise..e. bwana, si makosa yangu ais…aise..!”
Ama kweli tamaa mbele mauti nyuma.
Maswali
1. Ni kwa nini jina la Bakuzi Baku lilibadilika na kuwa Bwana Aisee?
2. Kwa nini watu wengi waliofutwa kazi walijuta?
3. Bwana Aisee alitembea nchi mbalimbali za ulimwengu. Nchi zifuatazo
ziko katika mabara yapi? k.m Ngazija – Afrika
(a) Ushelisheli (c) Ufaransa (e) Msumbiji (g)Unguja
(b) Omani (d) Ujerumani (f) Uhispania
4. Wewe unadhani kulikuwa na kazi zozote za kuajiri vijana kama alivyodai
Bwana Aisee?
5. Je, unadhani kuwa Bwana Aisee alihusiana kwa njia yoyote na ile
hospitali walikofanyiwa uchunguzi wa kiafya wale vijana waliotaka kazi?
6. Ni nini wajibu wa INTERPOL?
7. Eleza maana ya maneno haya kulingana na matumizi yake katika
40
41
kifungu kisha uyatumie katika kutungia sentensi.
(a) kusindika (b) kuyabana (c) mawio
(d) kindakindaki (e) walimsheheneza (f) adimu
(g) kuwagubika (h) kusaza (i) wametapeliwa
(j) alibambwa
8. Eleza maana ya misemo na methali zifuatazo kulingana na matumizi
yake kwenye kifungu.
(a) kisimati cha kazi (b)ingia mitini (c) ponda raha kufa kwaja
(d) wajinga ndio waliwao
B. Kusikiliza na kuzungumza
Methali
Methali ni kijitanzu au kipera kimoja maarufu cha utanzu mpana wa semi.
Utanzu wa semi unahusisha vipera vingine kama: vitanza ndimi, misemo,
nahau, lakabu na mafumbo. Tazama mchoro ufuatao:
Lugha ya Kiswahili ina methali nyingi sana kama zilivyo lugha zetu
nyinginezo ambazo zina methali za kila aina. Aghalabu methali ni msemo
unaoeleza ukweli au hali fulani inayokubalika na jamii. Msemo huu huwa ni
wa kitamaduni na hurithishwa wanajamii kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Methali hutumiwa na wazungumzaji wa lugha kwa sababu kadha:
1. Kuonya. Methali kama ‘usipoziba ufa utajenga ukuta’ inamwonya
mtu kuwa ikiwa hatajitahidi kulikabili jambo likiwa dogo baadaye
atalazimika kupambana na jambo kubwa.
2. Kushauri na kutoa nasaha. Methali kama ‘baada ya dhiki ni faraja’
inamshauri mtu awe na subira katika maisha yake.
3. Kufundisha au kuelimisha wanajamii mbalimbali, kwa mfano, methali
kama ‘asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.’
Semi
misemo
nahau
methali
lakabu
mafumbo
vitanza
ndimi
mizungu
mafumbo
vitendawili
misimu
shirikina
40
41
4. Kutahadharisha. Methali huweza kutumiwa kumtahadharisha mtu
anayefanya jambo fulani kuwa asipofuata ushauri fulani atakwa na
madhara. Kwa mfano, ‘aonywaye, huonyeka.’
5. Kuirithisha jamii utamaduni wa jamii inayohusika. Kutokana na methali
za jamii zetu, tunajifunza thamani ya utamaduni wetu na kuuonea fahari
utamaduni huo.
6. Kuhimiza juhudi na moyo wa kutenda jambo kwa wanajamii fulani. Kwa
mfano’ ‘atafutaye hachoki na akichoka keshapata’ au ‘jembe halimtupi
mtu.’
7. Huhimiza ushirikiano miongoni mwa wanajamii mbalimbali. Kwa
mfano, ‘umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu’ inahimiza umoja na hali
ya kushirikiana.
Muundo wa methali
(a) Umbo
Kwa kawaida methali huwa na muundo wenye sehemu mbili. Sehemu ya
kwanza husema jambo linalokamilishwa au kujalizwa na sehemu ya pili.
Upande wa kwanza wa methali unaweza kuonyesha tabia, uzoefu wa tendo
fulani na wa pili matokeo yake. Tuangalie mifano hii:
1. Baada ya dhiki / faraja.
2. Usione kwenda mbele / kurudi nyuma si kazi.
3. Haba na haba / hujaza kibaba.
4. Siku za mwizi / ni arubaini.
5. Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
6. Mpanda ngazi / hushuka.
7. Mwenda kasi / mngojee achoke.
(b) Matumizi ya lugha
Methali huonyesha ufundi mkubwa katika matumizi yake ya lugha kwa
kuwa na mpangilio maalum wa maneno au matumizi ya tamathali za usemi
za ulinganishi kama tashbiha na sitiari. Hapa tutaangalia methali ambazo
zinaonyesha ulinganishi pamoja na nyingine zinazoonyesha mchezo fulani
wa sauti au maneno. Hebu tuangalie mifano ifuatayo:
a) Zinazoonyesha ulinganishi:
(i) Usilolijua ni kama usiku wa giza (usilolijua ni usiku wa giza)
tashbiha.
(ii) Kawaida ni kama sheria tashbiha.
(iii) Mgeni ni kuku mweupe sitiari.
b) Zinazoonyesha mchezo wa sauti/maneno:
(i) Haba na haba hujaza kibaba.
(ii) Pema usijapo pema ukipema si pema tena.
42
43
(iii) Ukiona neno usiseme neno, ukisema neno utapatwa na neno.
Zoezi
(a) Toa mifano mitano ya methali za Kiswahili zinazotumiwa kuonya.
(b) Andika methali tatu za Kiswahili zinazoonyesha matumizi ya
tashbiha au sitiari.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Nomino
(i) Nomino dhahania
Majina ya vitu vya kukirika tu wala haviwezi kugusika, kuonjeka au
kuonekana. Hujumuisha maneno kama usingizi, ula, wema, ubaya, uwongo,
imani, roho, wazo n.k. Ifuatayo ni mifano katika sentensi:
1. Uwongo wake ulimtia mashakani.
2. Ujambazi umerudisha maendeleo nyuma hapa tarafani.
3. Nina imani kuwa nitaishia kuwa tajiri mkubwa sana.
4. Amani haipatikani ila kwa ncha ya upanga.
5. Uchoyo una faida gani kwetu?
(ii) Nomino za kitenzi-jina
Hivi ni vitenzi vyenye kiambishi awali ‘ku’ au kw vinavyotumika kama
nomino. Kwa mfano, kucheka, kulia, kutembea, kulima n.k.
(a) Kusoma kuna faida nyingi.
(b) Kulala kuna hasara sana.
(c) Kuiba kwake kutamwongoza hadi gerezani.
(d) Kujivuna hakufai kamwe.
(e) Kuondoka kwake kulileta hasara kubwa.
42
43
2. Nyakati na ukanusho
Wakati uliopo
Umoja Wingi
nafsi ya kwanza
kuyakinisha kukanusha kuyakinisha kukanusha
ninalima silimi tunalima hatulimi
ninachimba sichimbi tunachimba hatuchimbi
ninakata sikati tunakata hatukati
ninajenga sijengi tunajenga hatujengi
nafsi ya pili
unalima hulimi mnalima hamlimi
unachimba huchimbi mnachimba hamchimbi
unakata hukati mnakata hamkati
unajenga hujengi mnajenga hamjengi
nafsi ya tatu
analima halimi wanalima hawalimi
anachimba hachimbi wanachimba hawachimbi
anakata hakati wanakata hawakati
anajenga hajengi wanajenga hawajengi
Zoezi
Sentensi zifuatazo ni za hali ya kukanusha. Ziandike katika hali ya
kuyakinisha. Kwa mfano:
Mjomba hajengi nyumba nzuri.
Mjomba anajenga nyumba nzuri.
1. Mama hapiki chakula kitamu.
2. Mimi siandiki barua ndefu.
3. Wandera havui samaki.
4. Golikipa hashiki mpira.
5. Rais haanzi kuhutubu.
6. Mwalimu haondoki sasa.
7. Nyanya hapakui chakula.
8. Ndovu havunji miamba.
9. Mchoraji hachori picha nzuri.
10. Dada hafagii nje ya nyumba.
44
45
D. Kusoma
Mashairi ya arudhi
Mashairi ya arudhi au mashairi mapokeo ni yale ambayo hutungwa kwa
kuzingatia kanuni fulani. Kanuni hizi (ambazo hujulikana kama arudhi) ni
vina, mizani, mishororo, beti n.k. Katika sehemu ifuatayo tutaangalia maana
ya maneno au istilahi za kimsingi kuhusiana na mashairi mapokeo.
Mshororo: Mstari wa shairi. Mshororo wa kwanza huitwa mwanzo,
wa pili mloto na wa tatu, mleo au mlea.
Mizani: Ni silabi katika maneno ya shairi. Kwa kawaida idadi ya
mizani katika kila mshororo huwa sawa katika shairi moja. Shairi huwa
na mizani 16 (lakini yapo mengine ambayo yana mizani mingi au michache
zaidi). Mifano:
I- sha-li-a ya m-ga-mbo (8), Wa-ke-nya ni-si-ki-ze-ni (8)
Na la-zi-ma pa-na ja-mbo (8), mu-hi-mu le-nye u-za-ni (8)…
Vina: Silabi za namna moja zinazotokea baada ya mizani kadha. Vina
hupatikana mahali ambapo pana mtuo fulani katika mshororo. Sehemu hiyo
huweza kuwa kati katikati au mwishoni mwa mshororo. Kwa mfano:
Ishalia ya mgambo, Wakenya nisikizeni,
Na lazima pana jambo, muhimu lenye uzani,
Kupuuza ni kigambo, na majuto hatimani,
Hino awamu nyingini, kitu kidogo haramu!
Ubeti: Ni kifungu cha mishororo kadha ya shairi. Idadi hii ni msingi
mkubwa wa kuelezea aina mbalimbali za mashairi. Kwa mfano:
(i) Shairi lenye mshororo mmoja katika kila ubeti huitwa
TAIHMINA au UMOJA.
(ii) Shairi la mishororo miwili katika kila ubeti huitwa TATHNIA
au UWILI.
(iii) Shairi la mishororo mitatu katika kila ubeti huitwa
TATHLITHA au UTATU.
(iv) Shairi la mishororo minne katika kila ubeti huitwa TARBIA au
UNNE.
(v) Shairi la mishororo mitano katika kila ubeti huitwa TAKHMISA
au UTANO.
(vi) Shairi la mishororo sita katika kila ubeti huitwa TASDISA au
USITA n.k.
Kipande: Sehemu mojawapo ya mshororo wa shairi. Shairi linaweza
kuwa na kipande kimoja au vipande kadha. Kipande cha kwanza ni UKWAPI,
cha pili UTAO, cha tatu MWANDAMIZI na cha nne UKINGO. Aghalabu
mashairi huwa na vipande viwili. Hata hivyo, yanaweza kuwa na vipande
zaidi.
Utoshelezi: Hii ni hali ya kukamilika kwa shairi la arudhi kiutunzi
(likawa limezingatia kanuni zote zifaazo) au hata kimaudhui (likawa
44
45
limezungumzia suala fulani kwa njia inayokamilika).
Mfano wa Shairi la Arudhi
Ya mgambo imelia, masikio yategeni,
Inalo lahadithia, muhimu lenye thamani,
Muhimu kwetu insia, latufaa maishani,
Usadi tutengeni, unaturudisha nyuma.
Papo hapo twakwamia, tuufanyapo mwandani,
Madawa kujiibia, huko hospitalini,
Kisha kwenda jiuzia, ndipo tupate mapeni,
Usadi tutengeni, unaturudisha nyuma.
Kazini wakikujia, watu watoe dhikini,
Rushwa ukajidaia, bila ya haya usoni,
Ndiposa kuhudumia, sasa haya mambo gani?
Usadi tutengeni, unaturudisha nyuma.
Faili kujichukulia, ukatia mvunguni,
Ndipo upate rupia, kuwadhili maskini,
Hwoni wajiharibia, kwa tamaa ya tumboni?
Usadi tutengeni, unaturudisha nyuma.
Maswali
1. Toa kichwa mwafaka cha shairi hili.
2. Je, hili ni shairi la aina gani? Toa sababu zako.
3. Je, mshairi anazungumzia nini? Je, kibwagizo cha shairi hili kina
umuhimu gani?
4. Taja sifa zozote nne za lugha ya kishairi.
E. Kuandika
Ratiba
Ratiba ni mfululizo wa mambo kama yanavyotarajiwa kutokea katika
kipindi fulani cha wakati kilichotengwa. Ratiba hutayarishwa kwa shughuli
mbalimbali. Kwa mfano, huweza kutayarishwa ili kutumiwa wakati wa
mashindano ya michezo baina ya shule mbalimbali, mkutano wa sherehe
na kadhalika.
Madhumuni ya ratiba
(i) Hupangilia matukio ili yatokee kwa mpango bila kuzusha
utatanishi wowote.
(ii) Husaidia katika matumizi ya wakati kwa vile huwezesha
mambo yaliyopangwa kutendeka kwa wakati unaofaa.
(iii) Husaidia kushughulikia mambo yote muhimu bila kusahaulika
mengine. Unapofanya mambo bila ratiba ni kama kufanya
mambo bila mpango, na tunajua kinachotokea hali ikiwa hivyo.
Mara nyingi utagundua kuwa mambo mengine yamesahaulika.
46
47
(iv) Husaidia kupangilia shughuli ili zitokee kwa utaratibu unaofaa.
Kwa mfano, husaidia kupanga mambo hivi kwamba mambo
fulani yanakuja mwanzo, mengine yanafuata na kuendelea
hivyo hadi shughuli zote kumalizika. Isipofanyika hivyo,
kuna uwezekano mkubwa kuwa mambo yanayofaa kufanyika
mwanzo yanafanyika mwisho na yale yanayofaa kuja mwisho
yanafanyika mwanzo na kwa hivyo kuvuruga shughuli yote.
(v) Husaidia kuwajulisha wanaohusika kuhusu wajibu wao.
Kwa mfano ikiwa ni mkutano wa harambee inajulisha yule
atakayemkaribisha mgeni na saa za kufanya hivyo, wale
watakaotoa hotuba, wale watakaotoa shukrani na saa za
kufanya hivyo n.k.
(vi) Husaidia wanaohusika kuzingatia muda waliopewa kufanya
shughuli fulani. Kwa mfano, ikiwa ni kutoa hotuba fupi ya
ufunguzi kuanzia saa nne hadi saa nne na robo, inabidi yule
anayehusika kuzingatia muda huo. Kwa njia hii shughuli
hukamilika kulingana na mpango.
Mfano
Ratiba ya ufunguzi wa maktaba ya Shule ya Upili ya Zama za Leo
tarehe 10/3/2004
Saa: 7:00 Wanafunzi kupata staftahi.
Saa: 8:00 Mkutano wa mwalimu mkuu na wanafunzi pamoja
na walimu.
Saa: 9:00 Kuwasili kwa wageni waalikwa.
Saa: 9:30 Kuwasili kwa mgeni rasmi Bi. Penina Nabutola.
Saa: 9:45 Hotuba ya mwenyekiti wa chama cha wazazi na walimu.
Saa: 10:00 Hotuba ya mwalimu anayehusika na maktaba shuleni.
Saa: 10:20 Hotuba ya mwalimu mkuu.
Saa: 10:45 Hotuba ya mgeni rasmi na ufunguzi wa maktaba.
Saa: 11:15 Wafadhili kupokeza mgeni rasmi misaada ya vitabu.
Saa: 11:30 Hotuba ya shukrani kutoka kwa kiranja anayesimamia
maktaba shuleni.
Saa: 11:45 *Asusa na vinywaji kuandaliwa.
Saa: 12:30 Mwisho wa shughuli za siku.
* Asusa - vyakula vyepesi kama vile vibanzi, kaukau n.k.
Zoezi
Andika ratiba ya siku ya mashindano ya michezo ya riadha kati ya shule
zote za tarafa yako yatakayofanyika shuleni mwenu.
46
47
Sura ya Tano
A. Ufahamu
Mwanamke ana haki
(Chumbani. Jedida ameketi huku amekiinamisha kichwa chake. Anainuka
kitini na kuanza kwenda huku na huku. Anaanza kuongea peke yake)
jedida
: (Kwa sauti iliyojaa huzuni)
Kwa nini lakini?
Hivi mimi sina uhuru kama kiumbe anayeishi katika dunia huru?
Sina? Sina? Sina?
Utamaduni, utamaduni!
Je, kwa nini utamaduni ututie sisi kongwa na kutuvuta kama
watumwa wake!
Ndiyo,
utamaduni ni kitovu cha uhai wa jamii. Lakini?
(Anasogea mbele)
Niambie, niambie, niambie niambilike!
Je, ni mambo yote yaliyoko katika utamaduni ambayo ni mema?
(Baada ya muda mlango unabishwa. Anaingia Ma´Jedida, mamake.
Uso wake unaonyesha wasiwasi fulani)
Ma´jedida
: Uko tayari?
jedida
: Tayari?
Ma´jedida
: Usijitie mwapuza! Unajua nina maana gani!
jedida
: Ma’ siwezi mimi!
Majedida
: Huwezi, huwezi nini? Hujasikia kuwa hili ni jambo la lazima.
Utamaduni huu, na mwacha mila ni mtumwa (Anapaaza
sauti) Hii ni ngazi muhimu ya utu uzima. Lazima uipitie.
Hata mimi mamako nimeipitia. Unasikia?
jedida
: Mama sitaki mimi! Huo utamaduni haufai, mama!
Majedida
: Hivi unanitania mwanangu! Katika jamii hii tohara ni
lazima. Unasikia (anamsogea). Hii ni njia ya pekee ya
kuonyesha kuwa umekuwa mtu mzima! Ni ngazi muhimu
hii!
jedida
: La! Nina haki ya kuamua lipi nishiriki na lipi nisishiriki.
Mama ...Hapana. Sitakubali!
Majedida
: (Kwa sauti ya chini) Kwa nini lakini?
jedida
: Ma’ hiyo ni mila ya zamani! Huu wakati mwingine. Utu
uzima hauwezi kuwa kwa tohara tu mama! Tena kijembe
ni kile kile. Kuna maradhi siku hizi mama!
Ma´ jedida
: Maradhi? Maradhi gani hayo ambayo hayakutupata sisi?
48
49
jedida
: Ukimwi!
Majedida
: (Akicheka na kutupa mikono) Huo! Huo mwanangu ni
ugonjwa wa asherati sio wa wanaopashwa tohara!
jedida
: Unaenezwa kwa damu, kijembe kile kile, sindano.
Majedida
: Maradhi yawepo yasiwepo hili ni lazima. Mimi sitakubali
mwanangu aniaibishe. Lazima tufanye hili. Watanicheka
kila mahali. Uso wangu nitauweka wapi? Wanaume
watakuambaa, utakosa wa kukuposa; mwanangu
utaadhirika.
jedida
: Huwezi kunilazimisha mama!
Majedida
: Siwezi? Naweza, tena sana!
jedida
: Mama nina haki...
Majedida
: Haki gani?
jedida
: Ya kuamua nikubali nini na nikatae nini?
Majedida
: (Kashangaa) Hiyo ndiyo elimu ya siku hizi? Ndiyo elimu
msomayo inayokuzuzua na kukufanya uuasi utamaduni?
jedida
: Si elimu tu mama. Hiyo ni dhuluma tupu.
Majedida
: Dhuluma unasema?
jedida
: Ndiyo. Ni dhuluma dhidi ya mwanamke! Huo mama ni
unyanyasaji wa wanawake!
Majedida
: Unyanyasaji? (Akicheka) Mwanangu usinichekeshe!
Mwanamke hana usemi katika utamaduni wetu. Tangu
zama za mababu, mwanamke hana maamuzi. Usipigane
na utamaduni mwanangu, ni kama kupiga mbizi nchi kavu,
utaupujua uso wako tu.
jedida
: Mama sisi sio watumwa wa utamaduni. Wakati umepita wa
kuyakubali mambo ambayo yanamdhalilisha mwanamke.
Majedida
: (Kwa huzuni) Mwanangu mwanamke hana uamuzi. Hii ni
dunia ya mwanamume.
jedida
: La! Mama. Wakati umebadilika. Mwanamke ana haki sawa
na mwanamume. Mwanamke ana uhuru wa kuamua lipi la
kukubali na lipi akatae.
Ma jedida
: Na ukilazimishwa?
jedida
: Mama kuna sheria! Huwezi kumlazimisha mtu kukubali
jambo kama hili kinyume na mapenzi yake.
Majedida
: (Kwa mshangao mkubwa) Jamani! Lo! Hivi mwanangu
unaweza kuwapeleka wazazi wako mahakamani...unaweza
kweli kuwashtaki wazazi wako? Ulimwengu gani huu
jamani! Haki!
(Anaingia babake Jedida Bw. Taasubi na mzee mwingine,
Mzekale)
48
49
bw. Taasubi
: (Kwa sauti ya juu) Mko tayari?
(Jedida na Ma’Jedida wanaangaliana)
Ma jedida
: M...baa...do!
bw. Taasubi
: (Kwa hasira) Ati nini?
jedida
: (Kwa sauti imara) Baba mimi siwezi kukubali! Huo ni
unyanyasaji wa watoto wa kike.
bw. Taasubi
: (Kwa mkewe) Unasikia ayasemayo bintiyo? Ndiwe
uliyemfundisha haya?
jedida
: La. Baba hiyo mila ya tohara ni ya zamani. Imepitwa na
wakati...
bw. Taasubi
: Huo wakati ulipita ukaenda wapi?
(Mlango unagongwa. Wote wanaangalia mlangoni. Mwalimu
anaingia)
Majedida
: Karibu mwalimu.
MwaliMu
: Shikamoo Ma’Jedida
Majedida
: Marahaba.
MwaliMu
: Shikamoo Bw. Taasubi!
bw. Taasubi
: Hamna cha kushika hapa!
MwaliMu
: Kuna nini?
bw. Taasubi
: Labda nikuulize wewe!
MwaliMu
: Nimeka kujua kwa nini Jedida hajaja shuleni. Hata jana
sikumwona.
Mzekale
: Huu msimu wa tohara mwalimu.
MwaliMu
: Eti tohara? Tohara kwa msichana?
bw. Taasubi
: Hasa! Ina nini kwani? Hii ni jadi yetu.
MwaliMu
: (Kwa mshangao) Tohara kwa wasichana! Huo ni ukeketaji.
Ni dhuluma kwa mtoto wa kike. (Anatua) Ni kinyume kabisa
cha haki ya mtoto wa kike. (Anatua) Isitoshe, inaweza
kumletea madhara makubwa...magonjwa, kifo kutokana na
uvujaji wa damu na hata matatizo ya kizazi hapo baadaye
(Kimya. Bw. Taasubi na Mzekale wanatazamana. Jedida
anasongea karibu na mwalimu). Sisemi utamaduni ni
mbaya lakini lazima uende na wakati. Hatupo kwa ajili ya
utamaduni bali utamaduni upo kwa ajili yetu. Tunaujenga
sisi, tunaubomoa sisi. Huu ni wakati mwingine na wakati
ni ukuta.
bw. Taasubi
: Nimeanza kuelewa sasa mwalimu. Kwa hakika singependa
kuhatarisha maisha ya mwanangu.
Ma jedida
: Asante mwalimu kwa kuokoa maisha ya mwanangu.
Tungekuuliza uhubiri habari hizi kwa jamii yetu ambayo
inashikilia sana utamaduni. Ukifanya hivyo utaokoa maisha
ya wasichana wengi.
50
51
MwaliMu
: Nitafanya hivyo. Nanyi nawauliza mjitoe mhanga kuwaeleza
wazee wengine hatari za tohara kwa wanawake. Pia,
waelezeni kuwa mwanamke ana haki sawa na mwanamume.
Mambo yote ya zamani yasiyofaa tunafaa kuyaacha kabisa
kwani yatarudisha nyuma maendeleo ya jamii yetu.
Ma jedida na
bw. Taasubi
: Tutafanya hivyo mwalimu.
MwaliMu
: Haya, kwaherini. (anaondoka)
Maswali
1. Mwanzoni mwa mazungumzo haya tunamwona Jedida akizungumza
pekee. Ni nini kinachomsumbua?
2. Ma’Jedida anatoa sababu gani kutetea utamaduni?
3. Jedida anajitetea vipi kuhusu kupashwa tohara?
4. Mwalimu anatoa sababu kadha dhidi ya tohara ya wanawake. Taja
sababu hizo.
5. Je, wewe una maoni yapi kuhusu tohara kwa wanawake?
6. Eleza maana ya maneno na misemo ifuatayo kama ilivyotumiwa katika
kifungu ulichosoma.
(a) usijitie mwapuza (c) watakuambaa
(b) inayokuzuzua (d) mpiga mbizi nchi kavu, huupujua uso wake
B. Kusikiliza na kuzungumza
(1) Mjadala
Mjadala ni mazungumzo yanayohusu suala fulani ambapo pana maoni
tofauti na mbalimbali. Lengo la mjadala ni kuukuza uwezo wa kuyawasilisha
mawazo au hoja kwa njia ya kushawishi na kusadikisha. Uwezo huo wa
kuongea, kutoa hoja, kushawishi, uko katika hata neno lenyewe ‘jadili’ ambalo
ndilo kitenzi cha nomino mjadala. Mjadala, ambao pia huitwa mdahalo,
unahusisha kuangalia pande zote mbili za suala linalohusika. Jambo hili
haliwezekani bila ya kufanya utati mzuri na kuhakikisha kuwa hoja zote
muhimu zinazohitajika zinashirikishwa.
Sifa za mjadala
(a) Kuwepo kwa pande mbili kuu: upande unaounga mkono na upande
unaopinga.
(b) Hoja muhimu kuhusu suala au mada ya mjadala kumezingatiwa.
(c) Kupanga hoja hizo kwa njia nzuri, yenye mantiki na inayoonyesha
mpangilio mzuri.
(d) Kuhakikisha kuwa umejiandaa kwa lugha fasaha, matumizi ya
misemo na nahau na msamiati unaohusiana na mada ya mjadala.
50
51
(e) Kutumia hoja kama msingi wa kuufanya upande wako uwe na uzito
fulani. Kumbuka mjadala hauwi na nguvu kutokana na hisia au sauti
ya juu bali nguvu ya hoja iliyotolewa.
(f) Kuwepo kwa matumizi ya lugha yanayozingatia kanuni zifaazo za
saru, mbeko na adabu katika matumizi ya lugha.
(g) Kutoa mifano inayoeleweka pale inapolazimu.
(h) Kuheshimu maoni ya wapinzani na kuyapinga kwa kuzingatia hoja
ya nidhamu.
Mfano wa mjadala
Mada: ‘Shule ni kama jamaa ya pili ya mwanafunzi.
Baadhi ya hoja muhimu za upande wa kuunga mkono:
(i) Wanafunzi wanatoka maeneo mbalimbali na kama watoto wana
sifa mbalimbali zinazowatambulisha kama kundi moja.
(ii) Wanafunzi wanaingiliana kwa udugu na mapenzi kama watoto
wa jamaa moja tu.
(iii) Wanafunzi wanasaidiana wawapo na shida za kila aina.
(iv) Wanashirikiana katika mambo mengi kama michezo, kusoma,
burudani n.k..
(v) Wanajaliana na kuthaminiana kama watoto wa jamaa moja.
(vi) Walimu walioko shuleni ni kama wazazi ambao huwaelekeza
wanafunzi na kuwafanya wayafurahie maisha yao.
(vii) Shule ni msingi mkubwa wa kufanikiwa maishani kwa
mwanafunzi kama ilivyo jamaa ambayo humwelekeza.
(viii) Shule ni muhimu kama nguzo ya kuhakikisha kuwa wanafunzi
wamejihisi kama watu wa taifa moja n.k.
Baadhi ya hoja za upande wa upinzani:
(i) Wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali huweza kufanya
maingiliano yao yawe magumu kwa sababu ya kira, mila na
desturi tofauti.
(ii) Si wanafunzi wote wanaotangamana kwa upendo; kuna wengine
wanaowakera wenzao kwa kuwa hakuna mchele usiokuwa na
ndume.
(iii) Baadhi ya wanafunzi wanakuwa na ubinafsi na huenda
wasiwasaidie wenzao kama ilivyo katika jamaa.
(iv) Wakati mwingine wanafunzi hushindwa kuingiliana vyema wao
kwa wao na kuishia hata kuwa na uadui n.k.
Zoezi
Kazi ya kundi: mjadala
Jitengeni katika makundi mawili, kisha mwanafunzi mmoja ateuliwe na
mwalimu kuwa mwelekezi wa mjadala. Wakati wa kujadiliana, zingatieni
wasifu wa kimsingi wa mjadala mzuri.
52
53
(2) Matamshi bora: Vitate j/nj
Tamka maneno haya:
j nj
jaa njaa
jema njema
jia njia
jozi njozi
jana njana
Soma: Vitanza ndimi
1. Nilipomwambia mama kuwa nina njaa alinipakulia chakula kikajaa bakuli
kwani anajua kuwa tumbo langu halijai chakula kisichojaa bakuli.
2. Tunasema jambo ‘jema’ wala si ‘njema’ na nyumba ‘njema’ wala si ‘jema’
kwani ‘jema’ na ‘njema’ hutumika katika ngeli tofauti.
3. Mgeni aliyetujia alitujia kwa njia tofauti wala sio njia tuliyodhania
ataitumia kutujia.
4. Nilipolala jana usiku niliota njozi ambapo mama alininunulia jozi kumi
za viatu, nikaamka haraka kuzipokea zile jozi lakini nikafadhaika
nilipogundua kumbe hakukuwa na jozi bali ni njozi tu.
5. Jana vijana walikwenda kuvua njana lakini njana walipowaona wale
vijana wakatoweka kwani wanajua vijana waonapo njana ni hatari.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Nomino
(i) Nomino za jamii
Hizi ni nomino za vitu vinavyotokea kwa makundi. Kila kundi hurejelewa
kwa kutumia jina au nomino maalum. Kwa mfano, genge, korija, shada, n.k.
Mifano katika sentensi:
(a) Wanyama ni mwenyekiti wa baraza la wazee hapa kijijini.
(b) Rais aliweka shada la maua kwenye kaburi la shujaa wa vita vya
ukombozi.
(c) Familia ya Mutuku imekwenda Kili.
(d) Bunge litafunguliwa kesho.
(e) Kamati kuu ya shule ya Suwerwa inakutana ukumbini.
(ii) Nomino za wingi
Nomino hizi hutokea tu kwa wingi. Haziwezi kugawika ili ziwe kitu
kimoja kimoja. Ni maneno kama maji, manukato, maziwa, maoni,
makazi, mazingira n.k.
(a) Ziwa Viktoria lina maji mengi sana.
(b) Manukato ya Maria yamemwagika.
(c) Si vizuri kutema mate ovyo ovyo.
(d) Msichana huyu amejipaka marashi mengi zaidi.
52
53
Zoezi
Onyesha aina za nomino zilizo kwenye jedwali lifuatalo:
Nomino Aina
k.m. uwongo dhahania
1. baraza ________
2. malaika ________
3. wizi ________
4. maziwa ________
5. jini ________
6. kulima ________
7. bunge ________
2. Vielezi
Vielezi ni maneno yanayotumika kufafanua kitenzi, kivumishi au kielezi
kingine. Hueleza kitenzi kilitendeka lini, wapi, jinsi gani n.k.
(i) Vinapotumika kufafanua vitenzi.
Kwa mfano:
(a) Mama ataondoka alfajiri na mapema.
(b) Ndege ilipoanguka ilivunjika vipande vipande.
(c) Nataka unipe pesa zangu sasa hivi.
(d) Mama yangu alilima shamba hili vizuri.
(e) Vitu hivi vimepangwa shaghalabaghala.
(ii) Vinapotumika kufafanua vivumishi.
Kwa mfano:
(a) Nyanya alininunulia baiskeli nzuri mno.
(b) Nyumba hiyo ni ndefu ajabu.
(c) Mwende ni msichana mrembo sana.
(d) Chakula ulichokipika ni kitamu kupindukia.
(e) Mpwa wetu ametupa peremende tatu tu.
(iii) Vinapotumika kufafanua vielezi vingine.
Kwa mfano:
(a) Mama alinizomea vikali mno.
(b) Wanafunzi hawa hufanya kazi yao vizuri sana.
(c) Mchezaji wa shule yetu ametupa mkuki mbali kabisa.
(d) Watu wale wanakimbia kasi ajabu.
Zoezi
Onyesha vielezi katika sentensi zifuatazo:
(a) Kariuki na Otieno ni wanafunzi watiifu sana.
(b) Kwa nini ulifanya kazi hiyo vibaya?
54
55
(c) Nyumba hii ina madirisha makubwa ajabu.
(d) Ndugu yangu atakwenda Nairobi kesho kutwa.
(e) Wezi walitushambulia jana jioni.
(f) Wakazi wa pwani hupenda kutembea ufuoni majira ya jioni.
(g) Mtu huyu huongea haraka haraka.
(h) Babu amelewa chakari.
(i) Wachezaji hao walifurahi kupindukia.
(j) Inafaa twende nyumbani sasa.
3. Ngeli za nomino: Upatanisho wa kisaru
Viambishi awali vya vitenzi vinavyotumika kubainisha
ngeli hutegemea ngeli mbalimbali. Makosa mengi ya kisaru
yanayotokea katika maongezi au maandishi ya Kiswahili hutokana
na kutozingatia utaratibu unaofaa wa viambishi hivi. Tazama
matumizi ya viambishi hivi.
Ngeli ya a/wa
Umoja Wingi
Siafu anauma. Siafu wanauma.
Konokono anateleza. Konokono wanateleza.
Mwizi ameshikwa. Wezi wameshikwa.
Ndege anataga yai. Ndege wanataga mayai.
Ngeli ya u/i
Mlango umefungwa. Milango imefungwa.
Mti umeanguka. Miti imeanguka.
Mpera umepandwa. Mipera imepandwa.
Mto utafurika. Mito itafurika.
Ngeli ya ki/vi
Cheti kitatolewa. Vyeti vitatolewa.
Chakula kimepikwa. Vyakula vimepikwa.
Chama kimevunjwa. Vyama vimevunjwa.
Kiti kitaanguka. Viti vitaanguka.
Ngeli ya u/ya
Ugonjwa ulitibiwa. Magonjwa yalitibiwa.
Ulezi umeanza. Malezi yameanza.
Upendo unafaa. Mapendo yanafaa.
Uovu ulizidi. Maovu yalizidi.
54
55
Ngeli ya li/ya
Yai limeanguliwa. Mayai yameanguliwa.
Limau limeliwa. Malimau yameliwa.
Jino litang’olewa. Meno yatang’olewa.
Jiko linawaka. Meko yanawaka
Ngeli ya ya/ya
Maziwa yameletwa. Maziwa yameletwa.
Maji yamenywewa. Maji yamenywewa.
Manukato yako wapi? Manukato yako wapi?
Marashi yamenunuliwa. Marashi yamenunuliwa.
Majira yana upepo. Majira yana upepo.
Ngeli ya ki/ki
Kiherehere kilimvaa. Kiherehere kiliwavaa.
Kiingereza kimeenea sana. Kiingereza kimeenea sana.
Ngeli ya vi
Vita vimezuka upya. Vita vimezuka upya.
Vijo vilisikika usiku. Vijo vilisikika usiku.
Zoezi
1. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuandika viambishi vifaavyo kisha
uonyeshe ngeli zake.
Umoja Wingi Ngeli
k.m. Mchezo umeanza. Michezo imeanza. u/i
a) Kitabu __ menunuliwa. Vitabu __ menunuliwa. _______
b) Ng’ombe __ tachinjwa Ng’ombe __tachinjwa. _______
c) Kiboko __ takuuma. Viboko __takuuma. _______
d) Tunda __meliwa. Matunda __meliwa. ––––––
e) Maji __ko wapi? Maji __ko wapi? ––––––
f) Kisa __lifurahisha. Visa __lifurahisha. _______
g) Mkate __meletwa. Mikate __meletwa. _______
h) Jibu __tatolewa. Majibu __tatolewa. _______
i) Ulezi __limfaa. Malezi __limfaa. _______
j) Mchezaji __mekuja. Wachezaji __mekuja. _______
k) Maziwa __ menywewa. Maziwa __menywewa. _______
l) Kikapu __na nini? Vikapu __na nini? _______
m) Mshipi __mekatika. Mishipi __mekatika. _______
n) Shangazi __meondoka. Shangazi __meondoka. _______
2. Chagua nomino mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo:
_________ (Kitabu, Mkate) kilinunuliwa na mwalimu.
Kitabu kilinunuliwa na mwalimu.
1. _________ (Maji, Mkuki) yatachotwa na nani?
56
57
2. _________ (Chakula, Kisu) kitapikwa leo jioni.
3. _________ (Chuo, Mlango) utafungwa.
4. _________ (Upendo, Manukato) yamekwisha.
5. _________ (Kuku, Shamba) litanunuliwa.
6. _________ (Kikombe, Ndege) ataruka.
7. _________ (Mlinzi, Kioo) kimevunjika.
8. _________ (Chama, Kiroboto) amekufa.
D. Kusoma
Mashairi huru
Mashairi huru hutofautiana na mashairi ya arudhi kwa kuwa haya
hayajifungi kwenye zile kanuni za utunzi wa mashairi ya arudhi kama vina,
mizani, idadi fulani ya mistari, kuwapo kwa vipande vya ushairi, kibwagizo
n.k. Yanaitwa ‘mashairi huru’ kwa sababu hayazingatii kanuni hizo. Hata
hivyo, mashairi haya yana sifa nyingine za ushairi au za kishairi. Nazo ni:
(i) Matumizi ya lugha ya mkato.
(ii) Kuwepo kwa mishororo au mistari yenye mpangilio fulani.
(iii) Matumizi ya mbinu za kuucha au kuusema ujumbe kwa njia ya
mkato na inayohitaji makini kutambua.
(iv) Matumizi ya mbinu za lugha kama urudiaji.
(v) Kuwepo kwa lugha yenye mvuto wa kisanaa.
Mambo muhimu katika mashairi huru
Mashairi yote huwa na MAUDHUI na FANI. Maudhui ni mambo au
masuala yanayozungumziwa katika shairi linalohusika. Maudhui yanaweza
kudokezwa na: kichwa cha shairi, mistari inayorudiwarudiwa n.k. Ili
kuyaelewa maudhui, baada ya kusoma jiulize: mshairi anasema nini na ni
kitu gani kinachozungumziwa, je, mshairi anataka nipate ujumbe gani, je
mtunzi alitaka tupate ujumbe gani? Hebu tuangalie mfano wa shairi huru
lifuatalo:
Hebu, tua katika hatua zako
Waza, ng’ariza macho
huko nyuma kwenye giza ulikotoka
Unakumbuka ulivyoteswa na mkoloni?
Unakumbuka ulivyodhalilishwa na mgeni?
Ukatumikishwa
Ukalimishwa
Ukatozwa kodi ya kuishi
Ukatokwa hata na jasho la damu
Lakini hatimaye,
‘lipochukia kunyanyaswa
‘lipambana na mateso
kukuru kakara, kukuru kakara, kukuru kakara’
56
57
hatimaye ukaubwaga ukoloni chini pwaa!
Ukasema shida zimeruka kama ndege
ikawa enzi mpya
Sasa jiangalie,
Kwa nini sasa
Kwa nini sema
unawatesa wenzako
unawanyonya watu wako
unawacheka wenye ngozi yako
Kwa kuwa leo, umekuwa kiongozi
Hujui
mkuki kwa nguruwe
kwa binadamu u chungu?
Maswali
1. Toa kichwa cha kufaa kwa shairi hili.
2. Baada ya kulisoma shairi hili kwa makini, unakiri linazungumzia nini?
Toa sababu zako.
Fani ya shairi huru
Fani ni jumla ya mbinu zinazotumiwa kuyawasilisha maudhui. Kama
msomaji unatakiwa kuangalia matumizi ya lugha, kwa mfano, msamiati
(maneno yasiyokuwa ya kawaida, maneno magumu, maneno yaliyoandikwa
kwa namna ambayo haikuzoeleka n.k.), tamathali za usemi kama tashbiha
na sitiari, mbinu nyingine kama urudiaji au takriri (ambazo hufanywa ili
kusisitiza jambo fulani), n.k.
Maswali
1. Katika shairi hili mshairi ametumia takriri au urudiaji kusisitiza ujumbe
wake, onyesha mifano ya takriri.
2. Taja tamathali mbili za usemi zilizotumiwa katika shairi hili.
3. Je, ni mbinu zipi nyingine ambazo mtunzi ametumia ili kuuwasilisha
ujumbe wake vizuri zaidi?
E. Kuandika
Muhtasari
Muhtasari ni maelezo yanayotolewa kwa kifupi. Hii huweza kutokea kwa
njia ya maandishi au ya kimazungumzo. Uwezo wa kuandika au kusema
maneno kwa kifupi ni stadi muhimu sana hata katika maisha ya kila siku.
Umuhimu wa muhtasari
1. Humsaidia mtu kusema mambo mengi kwa wakati mfupi bila kupoteza
maana yake kuu.
58
59
2. Licha ya kuokoa wakati, muhtasari huweza pia kusaidia kuokoa pesa.
Kwa mfano, katika siku hizi za simu tamba tunaweza kuwasiliana
kwa urahisi kwa kutuma ujumbe mfupi. Njia hii imeimarisha sana
mawasaliano kati ya watu kwa vile ujumbe huu humkia anayetumiwa
mara moja na kwa gharama ndogo sana.
3. Tunapoandika vitu kama simu au telegramu, matangazo mbalimbali
kama ya vifo, ya kibiashara; au ripoti, barua, kumbukumbu, makala
ya magazeti na kadhalika hutakiwa kuandika kwa kifupi. Matangazo,
kwa mfano ya kibiashara kwenye redio au runinga, ni ghali mno na
huhesabiwa kwa sekunde. Yasipoweza kuandikwa kwa kifupi itakuwa
hata haiwezekani kuyaweka hewani.
Hatua za uandishi wa muhtasari
Ujuzi wa kuandika muhtasari humpa mwanafunzi uwezo wa kusoma na
kutathmini maandishi. Ili kuandika muhtasari bora, lazima uzingatie hatua
zifuatazo:
1. Soma kifungu ulichopewa kwa makini na uangalifu.
2. Chagua mambo unayoyaona kuwa muhimu na kuacha yale yasiyo na
umuhimu sana. Unaweza kufanya hivi kwa kuziandika hoja hizo muhimu.
3. Pitia tena kuangalia kama kuna hoja zifaazo zilizoachwa nje.
4. Andika nakala ‘ya kwanza’ au ‘nakala chafu’. Huitwa ‘chafu’ kwa vile
hutumika kutathmini kama mambo yote yamezingatiwa. Pia, haitilii
maanani sana hati. Katika kuandika nakala hii, viunganishi vya aina
mbalimbali hutumika kama vile ‘yaani’, ‘na’, ‘ili’, ‘kwa vile’. Aidha, alama
za kuakisha kama mkato, koma, nukta mbili, nukta na mkato n.k.
hutumika ili kuunganisha mawazo makuu.
5. Pitia ili kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa. Hakikisha kuwa hakuna
hoja muhimu zilizoachwa na kuwa zimeunganishwa kwa mtiririko
unaofaa.
6. Chunguza kama maneno yamezidi au kupunguka kulingana na maagizo
uliyopewa. Ikiwa yamezidi tafuta njia ya kuondolea mbali maneno au
hoja zisizo na uzito mwingi. Unaweza pia kufupisha urefu wa muhtasari
kwa kuandika baadhi ya mawazo kwa maneno machache zaidi ili
usizidishe maneno yanayotakiwa.
7. Hakikisha kuwa hutumii maelezo mengi pale ambapo neno moja lingefaa
au kusibu. Kwa mfano, badala ya ‘sherehe ya waliohitimu kutuzwa vyeti
vyao’ (maneno 6) unaweza kutumia ‘mahafali.’
8. Iwapo maneno yamepungua, pitia nakala asilia ili kuona kama kuna
jambo muhimu lililoachwa kisha uliongeze. Mwisho, ukishahakikisha
kuwa kila kitu ni sawa unaweza kuandika nakala ‘sa’ kisha uipitie
kuhakikisha kuwa maneno yameendelezwa kwa njia sa na hakuna
makosa ya kisaru, kitahajia au ya uakishi. Kwa kawaida jumla ya
58
59
maneno katika ufupisho huweza kuzidi au kupungua lakini hayapaswi
kuzidi au kupungua kwa zaidi ya maneno matano.
9. Ni muhimu pia mwanafunzi aandike jumla ya maneno aliyoyatumia
katika ufupisho.
Zoezi
Soma makala haya kisha uyaandike kwa maneno yasiyozidi theluthi
moja.
Ilikuwa mwendo wa saa nne usiku.Nilikuwa ndio tu nimeingia kitandani kulala.Siku
iliyotangulia nilikuwa nimefanya kazi nyingi za kuchosha kwani nilishinda nikipalilia
bustani yangu kabla ya kutembea hadi soko kuu kununua miche ya kupanda kwa
vile msimu wa mvua ulikuwa umeka. Si ajabu basi kwamba nilipotulia kitandani
mwili ulikuwa mavunevune.
Nilipokuwa nikiwaza na kuwazua huku nikingoja kuchukuliwa na usingizi wa
pono,nilisikia sauti ya mchakato iliyofanywa na komeo ya mlango.Mara ya kwanza
nilidhani pengine ni paka au mbwa anapita, lakini niliposikia sauti hiyo mara ya pili
roho ikaanza kunienda mbio. Nilijua bila shaka maisha yangu yalikuwa hatarini.
Niliruka mara moja kuchukua upanga wangu ambao kwa kawaida nilikuwa
nikiuweka mvunguni mwa kitanda, lakini sikuwa na bahati. Mlango ulipigwa kikumbo
na nikajikuta natazamana na pandikizi la mtu mfano wa jitu. Nikasikia sauti ya kutisha
kama ya radi ikiniamrisha nilale mara moja na nijifunike gubigubi. Lakini nikaamua
kujitia ushujaa kidogo angalau nione kama nitalishtua lile jitu. Nikasema kwa
sauti ya kutetemeka, ‘Toka hapa mara moja au uone kioja!’ Lo! Kumbe nilikuwa
nimekoroga mzinga wa nyuki. Hata sikuwa nimemaliza kutamka neno la mwisho
niliposhtukia nimetandikwa inzirani kwenye bega langu la kushoto na kuanguka
kitandani kama kipande cha gogo. Nilipojaribu kunyanyuka nikapata nyingine ya
kifua, nikapoteza fahamu. Niliposhtukia nilijikuta nimelazwa kitandani hospitalini
mwili wangu ukiwa na maumivu makali sana.
60
61
Sura ya Sita
A. Ufahamu
Chifu Somba na mbuzi wa serikali
“Ah, ni kweli mambo kangaja huenda yakaja,” alimaka mzee Maarifa
akimwazia chifu wa eneo la kwao aliyejulikana kama Chifu Somba. Zamani,
Somba alikuwa jamaa mtulivu na asiyependa makuu aliyeingiliana na raia
wengine kwa njia nzuri. Hii ndiyo sababu iliyowafanya watu wafurahi sana
alipoteuliwa kama chifu wao. Kwa muda mrefu walikuwa na matatizo mengi
kuhusu usalama, wizi na hata kubughudhiwa kwa akina mama. Walitamani
kuona matatizo haya yamemalizika na maisha yao kuwa mazuri. Basi
alipoteuliwa kuwa chifu wa kata hiyo ya Tumaini kila mtu alijua kuwa
hatimaye dhiki iliyowakumba imekia hatima yake.
Chifu Somba naye alijitahidi kuitekeleza kazi yake kwa moyo wake
wote siku za mwanzo. Muda si muda, yale matatizo yaliyokuwa yakiwakalifu
mioyo wakazi wa kata hiyo ya Tumaini yakapeperuka peperu. Sasa tatizo
la wizi halikuwako tena, watu waliweza kwenda mashambani bila kuhofu
kuwa nguo walizokuwa wameanika uani zitaibiwa. Masoko ya sehemu hizo
yalibadilika ikawa hakuna hofu ya kupigwa kabari usiku na watu usiowajua.
Wanawake nao hawakubughudhiwa tena; maisha sasa yalikuwa shwari na
kila mmoja wao alikuwa tayari kuendelea na jukumu lake la kujenga taifa.
Kweli matumaini yalirudi katika kata ya Tumaini.
Chifu Somba naye alifurahi ghaya kuwa maisha ya wanakata yalikuwa
yamebadilika; yalibaidika na ya zamani kama ardhi na mbingu. Watu
walimpongeza kuwa alikuwa ametekeleza kazi kubwa. Chifu alitambua
kuwa asingefanikiwa katika kazi kubwa kama hii kama wanakata
wasingeshirikiana naye bega kwa bega. Wote waliifahamu vyema busara ya
kuwa kidole kimoja hakivunji chawa. Licha ya mafanikio haya makubwa,
Chifu Somba hakuwa na furaha kama wanakata wenzake. Moyoni alihisi
kuwa wanakijiji hawakuzithamini juhudi zake kama alivyotamani. Alihisi
kuwa aliwafanyia kazi kubwa na kwa misingi hiyo walipaswa kuonyesha
shukrani jazila kwake. Alijiona kama mkombozi wa aina fulani ambaye
aliikomboa kata nzima kutoka kwenye dhiki kubwa. “Shukrani zao zimekuwa
za punda kabisa!” Alijisemea.
Basi siku moja Chifu Somba alipokuwa osini akikuna kichwa chake,
alijiwa na wazo. Aliamua kuzuka na mbinu za kuhakikisha kuwa amepata
njia ya kujishukuru mwenyewe. Kwa kawaida palikuwa na mikutano kadha
ya kuyajadili masuala yaliyoihusu kata. Wanakata walitakiwa kuihudhuria
mikutano hiyo mara tu ilipoitishwa. Wote waliufahamu mchango wa chifu
katika kuibadilisha hali ya maisha yao. Kwa hiyo walifanya juu chini
kuhakikisha kuwa hawakuikosa mikutano hiyo na wale waliokosa fursa
na abra ya kuhudhuria baraza za chifu walihakikisha kuwa wameomba
udhuru. Chifu aliamua kuitumia nafasi hii. Alitangaza kuwa yeyote ambaye
60
61
alikosa kuihudhuria baraza ya chifu atatozwa faini ya mbuzi mmoja kwa kila
baraza tatu alizokosa. Wanakata waliposikia tangazo hilo walijitahidi sana
kuzihudhuria baraza.
Chifu Somba alitambua
kuwa mbinu hiyo haikumfaa
kama alivyodhani mwanzoni.
Sasa aliamua kufanya
marisedi mengine kwa
kuhakikisha kuwa taarifa za
baraza zake hazikutangazwa
vyema. Kwa njia hii ni
wachache walioweza
kuhudhuria baraza hizo.
Waliokosa walilazimika
kulipa fidia ya mbuzi.
Wakati mwingine chifu
aliwatuma askari wake na
vijana wengine waliohudumu
kwenye osi zake kwenda kusomba mbuzi wa wanakata. “Ah! Chifu Somba
sasa amekuwa somba kweli; anasomba kila kitu. Chifu aliyekuwa mtu mzuri
sasa ndio amelewa na uongozi nini?” alishangaa Bwana Maarifa.
Somba hakutulia kwenye matendo yake ambayo kwake ilikuwa njia
ya kujishukuru kwa mambo aliyowafanyia wanakata. Sifa alizopewa na
wanakata zilishamwingia kichwani na kumfanya azinze kichwa chake. Alianza
kuhisi kuwa alikuwa mtu muhimu sana na kwamba bila yeye wanakata
wangeshindwa kuishi. “Chifu Somba, mbuzi wote hawa utawafanyia nini?”
walimwuliza wanakata walipotambua jinsi Chifu Somba alivyowasomba
mbuzi wengi. “Hawa ni mbuzi wa serikali!” alisema kwa sauti ya kiburi huku
akiligusagusa tumbo lake kubwa. Wanakata nao walianza kulalamika, “Ni
serikali ya aina gani nayo hii isiyotosheka na mbuzi?”
Siku moja mwanakata mmoja aliamua kuwaunganisha wenzake
nao wakaamua kuandika barua kwa viongozi wa ngazi za juu serikalini.
Muda si muda, Chifu Somba aliachishwa madaraka yake ya uchifu na hata
kushtakiwa kwa kuitumia nafasi yake ya kazi kujitajirisha. “Bwana Hakimu
nimewafanyia wanakata kazi kubwa, waulize wenyewe watakwambia kuwa
nimekomesha wizi, nimeboresha usalama na kuzima bughudha kwa akina
mama,” alijitetea Chifu Somba. “Ndiyo sikatai, lakini serikali inakulipa
kuwahudumia wanakata hao. Huduma unayoitoa ni wajibu wako wa
kikazi wala sio fadhila unayowatendea wanakata, Bwana Somba,” alisema
hakimu. “Ili kutoa indhari kwa viongozi wa umma kama wewe unaamrishwa
kuregesha mbuzi wote uliowasomba lakini hutaepuka kifungo cha miaka
miwili gerezani!” alisema hakimu. Wanakata walipomsikia akilalamika
walisema kwa sauti, “Chifu Somba nasi tumeamka hatimaye sio bozi wa
serikali ulivyotudhani. Sheria ni msumeno hukata mbele na nyuma, Bwana
Somba.”
62
63
Maelezo ya msamiati
hatima : mwisho.
furahi ghaya : furahi sana; furahi upeo wa furaha.
yalibaidika : yalitengana; yalikuwa mbali kwa mbali.
abra : fursa; nafasi.
azinze kichwa : aringe; awe na kichwa kigumu.
indhari : onyo.
Maswali
1. Zamani, Somba aliingiliana vyema na watu. Ni kweli au la? Fafanua.
2. Baada ya kuchaguliwa chifu, Somba alileta mabadiliko mengi. Taja
mabadiliko hayo.
3. Unadhani Chifu Somba alitarajia shukrani za aina gani kutoka kwa
wanakata baada ya kuleta mabadiliko katika eneo lao?
4. Ni kwa nini Chifu Somba hakutaka taarifa za mikutano yake kutangazwa
vyema?
5. Toa maana ya methali zifuatazo kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu:
(a) Mambo kangaja huenda yakaja.
(b) Kidole kimoja hakivunji chawa.
(c) Sheria ni msumeno hukata mbele na nyuma.
6. Eleza maana ya maneno na vifungu hivi kulingana na muktadha wa
kifungu kisha uyatumie kutungia sentensi ili kuonyesha maana yake:
(a) kubughudhiwa (b) yakapeperuka (c) kupigwa kabari
(d) shukrani jazila (e) omba udhuru
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii
Majadiliano: Mwalimu na mzazi
(Ofisini. Mwalimu anashughulikashughulika pale akionekana kama
anayemsubiri mtu. Mzazi, mamake Bonaya, anaingia)
MaMake bonaya
: Habari za asubuhi mwalimu?
MwaliMu
: Nzuri, shikamoo!
MaMake bonaya
: Marahaba!
MwaliMu
: Umeka, ehh.
MaMake bonaya
: Ndiyo, mwalimu. (Mtuo) Sikutaka kuchelewa. Chelewa
chelewa si nzuri.
MwaliMu
: Ehh, wanasema utakuta mwana sio wako. (mtuo) Sasa
Mama Bonaya ni kama nilivyokudokezea.
62
63
MaMake bonaya
: Kwamba Bonaya haelekei kufanya vizuri darasani.
MwaliMu
: Ndiyo. (Mtuo) Na si yeye tu, kuna wenzake kadha.
Ndiyo maana nilitaka tukutane, tujadiliane la
kufanya.
MaMake bonaya
: Wewe ndiye unayekaa naye hapa shuleni, utaweza
kutambua jinsi ya kumsaidia.
MwaliMu
: Na wewe ndiye mamake!
MaMake bonaya
: Ni kweli! (Kimya) Itakuwa ni kusaidiana basi!
MwaliMu
: Hasa! Kinga na kinga ndipo moto uwakapo! Mimi
nitajitahidi upande wangu; nawe upande wako…
MaMake bonaya
: (Akiitikia) Ulezi ni kazi kubwa, mwalimu!
MwaliMu
: Ehh, na mwalimu peke yake hawezi kufanikiwa pasi
na msaada wa mzazi.
MaMake bonaya
: Mzazi naye ni vivyo; hawezi kufanikiwa bila ya msaada
wa mwalimu.
MwaliMu
: Ehh, kwa mfano una wajibu wa kumhimizahimiza
kuifanya kazi aliyopewa!
MaMake bonaya
: Mmm…lazima nikiri nimekuwa sifuatilii hilo sana.
MwaliMu
: Sisi pekee hatufanikiwi bila msaada wenu; nyumba
bila nguzo haisimami.
MaMake bonaya
: Ukweli huo!
Maswali
1. Kwa nini Mwalimu alitaka kuzungumza na mamake Bonaya?
2. Je, unadhani Bonaya alikuwa mwanafunzi wa aina gani? Toa sababu
zako.
3. Je, unajifunza nini kutokana na mazungumzo haya?
4. Eleza sifa za sajili ya shuleni kama zinavyodhihirika kwenye kifungu.
C. Saru na matumizi ya lugha
Uundaji wa maneno
Maneno ya Kiswahili huweza kuundwa kwa njia mbalimbali. Kwa mfano,
nomino huweza kuundwa kutokana na nomino nyingine au vivumishi. Hata
hivyo, nomino nyingi za Kiswahili huundwa kutokana na vitenzi.
Uundaji wa nomino kutokana na vitenzi
Katika kuunda nomino kutokana na vitenzi, viambishi mbalimbali hutumika.
Viambishi hivi hutokea mwanzoni na mwishoni mwa mzizi wa kitenzi.
Nomino zinazoundwa kwa njia hii huwa na maana mbalimbali. Katika
sehemu hii tutachunguza taratibu zinazotumika katika uundaji wa nomino
hizi kwa kuzingatia viishio mbalimbali.
64
65
(i) Kiishio “i”
Kitenzi Nomino
lea mlezi/walezi/malezi
okoa mwokozi/waokozi/uokozi
zika mzishi/wazishi/mazishi
penda mpenzi/wapenzi/mapenzi
pika mpishi/wapishi/upishi/mapishi
suka msusi/wasusi/ususi
fuata mfuasi/wafuasi/ufuasi
jenga mjenzi/wajenzi/ujenzi
tuma mtumishi/watumishi/utumishi
iba mwizi/wezi/wizi
panda mpanzi/wapanzi/upanzi
nyoa kinyozi/vinyozi
soma msomi/wasomi/usomi
zaa mzazi/wazazi/uzazi
Zoezi
Kutokana na vitenzi vilivyomo kwenye mabano, unda nomino yenye kiishio
‘i’ na uitumie kukamilisha sentensi zifuatazo. Kwa mfano:
Bara la Afrika lina ________ wengi wenye hekima. (ongoza)
Bara la Afrika lina viongozi wengi wenye hekima.
(a) Kakangu aliumia baada ya kutokea ________ huko uwanjani. (gomba)
(b) Mtaa huu una ________ wengi mno. (lewa)
(c) Mimi sikujua kuwa Karolina ni ________. (iba)
(d) Kesho tutahudhuria ________ ya raki yetu. (zika)
(e) Baada ya Marekani kuivamia Iraq kulitokea ________ makubwa.
(angamia)
(f) Rita alimsaidia Evelyn kwa ________ mengi ya nyumbani. (tumia)
(g) ________ ni kikohozi, hayawezi kuchika. (penda)
(h) Eneo hili halina maendeleo mengi kwa vile lina ________ wengi zaidi.
(roga)
(i) Huko Chuo Kikuu kuna ________ chungu nzima. (soma)
(j) Mimi sipendi mambo ya ________ kamwe. (zuka)
64
65
(ii) Kiishio ‘ji’
kitenzi nomino
omba mwombaji/waombaji/uombaji
soma msomaji/wasomaji/usomaji
okoa mwokoaji/waokoaji/uokoaji
ruka mrukaji/warukaji/urukaji
cheza mchezaji/wachezaji/uchezaji
winda mwindaji/wawindaji/uwindaji
tazama mtazamaji/watazamaji/utazamaji
imba mwimbaji/waimbaji/uimbaji
kunywa kinywaji/vinywaji/unywaji
kosa mkosaji/wakosaji/ukosaji
kimbia mkimbiaji/wakimbiaji/ukimbiaji
panda mpandaji/wapandaji/upandaji
chora mchoraji/wachoraji/uchoraji
Zoezi
1. Kutokana na vitenzi vilivyomo kwenye mabano, unda nomino yenye
kiishio ‘ji’ na uitumie kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) ________ umezidi mjini Nairobi. (omba)
(b) Kilelu ni ________ hodari sana. (cheza)
(c) Baada ya kuongea kwa muda mrefu______ wake walianza kuondoka.
(sikiliza)
(d) ________ haramu umepigwa marufuku hapa nchini. (winda)
(e) Jana ________ hawa walipoteza kondoo watano. (chunga)
2. Andika vitenzi vinavyozalisha nomino zilizoonyeshwa.
Kitenzi Nomino Kitenzi Nomino
k.m.okoa mwokoaji imba mwimbaji
1. _______ mchezaji 8. _______ mrukaji
2. _______ mtazamaji 9. _______ upandaji
3. _______ msomaji 10._______ msemaji
4. _______ uwindaji 11._______ mwekaji
5. _______ msikilizaji 12._______ uchoraji
6. _______ uombaji 13._______ mkimbiaji
7. _______ kinywaji
66
67
(iii) Kiishio ‘u’
Nomino nyingi zenye kiishio ‘u’ zinazoundwa kutokana na vitenzi huwa ni
nomino dhahania au matokeo ya vitendo fulani. Kwa mfano:
Kitenzi Nomino
tulia utulivu
vumilia uvumilivu
sikia usikivu
sahau usahaulivu
legea ulegevu
choka uchovu/machovu
haribu uharibifu
potea upotevu
tukuza utukufu
angalia uangalifu
sumbua usumbufu
okoa wokovu
kosa ukosefu
umia maumivu
onea maonevu
Zoezi
1. Tumia kitenzi kilichomo mabanoni kuunda nomino mwafaka inayoishia
kwa ‘u’ ili kukamilisha sentensi.
(a) ________ wake ulimsaidia sana. (elewa)
(b) Mgonjwa alipopelekwa hospitalini alikuwa na _______ mengi sana. (umia)
(c) Kuna ________ mengi sana hapa kwenye kiwanda hiki. (onea)
(d) ________ wa ajira ni tatizo sugu humu nchini mwetu. (kosa)
(e) Mtu ________ aliye na ________ hula mbivu. (stahimili)
2. Kutokana na kila kitenzi kilichoonyeshwa kwenye jedwali lifuatalo
andika nomino moja yenye kiishio ‘u’.
Kitenzi Nomino Kitenzi Nomino
k.m.vumilia mvumilivu legea mlegevu
1. tukuka ______ 9. kosa ______
2. tulia ______ 10. sikia ______
3. choka ______ 11. pumbaa ______
4. pungua ______ 12. sahau ______
5. onea ______ 13. okoa ______
6. umia ______ 14. haribu ______
7. angalia ______ 15. potea ______
8. sumbua ______
66
67
(iv) Kiishio ‘o’
Kiishio ‘o’ hutumika sana katika kuunda nomino kutokana na vitenzi. Tazama
mifano ifuatayo.
Kitenzi Nomino
fungua ufunguo/funguo
shona mshono/mishono
unda muundo/miundo/nyundo
sema msemo/misemo
lia mlio/milio/kilio/vilio
nena neno/maneno
simanga simango/masimango
imba wimbo/nyimbo
funika kifuniko/vifuniko
tua kituo/vituo/mtuo/mituo
ziba kizibo/vizibo
Zoezi
1. Tumia kitenzi kilichoko mabanoni kuundia nomino yenye kiishio ‘o’ ili
kujazia pengo lililo kwenye sentensi.
(a) ________ wa mama umepotea. (fagia)
(b) Yule simba mla watu ameingia kwenye________. (tega)
(c) Nguo za dadangu zina________ inayopendeza. (shona)
(d) ________ yangu yanauma. (sikia)
(e) Mwalimu amenunua gari lenye ________ wa kisasa. (unda)
(f) Waswahili husema kilicho na ________ hakikosi kuwa na ________.
(anza, isha)
(g) Tulitembea kwa ________ wa kasi ili tuke mjini kabla ya soko
kufungwa. (enda)
(h) Kesho ni siku ya ________ humu shuleni mwetu. (cheza)
(i) Baada ya kupotelea mwituni, nilisumbuliwa na ________ mengi kwa
muda mrefu. (waza)
(j) Mwalimu wetu ametupa________ mengi yenye manufaa. (funza)
68
69
2. Andika vitenzi vinavyotumika kuundia nomino zilizoonyeshwa kwenye
jedwali lifuatalo:
Kitenzi Nomino Kitenzi Nomino
k.m. shona mshono k.m. lia mlio
1. ________ kifuniko 10. ________ mwisho
2. ________ kituo 11. ________ pigo
3. ________ kizibo 12. ________ tendo
4. ________ upepeo 13. ________ maonjo
5. ________ ufagio 14. ________ mapatano
6. ________ mtego 15. ________ majibizano
7. ________ kipimo 16. ________ wimbo
8. ________ sikio 17. ________ ndoto
9. ________ ngurumo
(v) Kishio ‘e’
Nomino hizi huwa si nyingi sana. Ni kama zifuatazo:
Kitenzi Nomino
shinda ushinde/mshinde/washinde
umba kiumbe/viumbe
teua uteule/mteule/wateule
hama mahame
peta pete
Zoezi
1. Kutokana na kitenzi kilichomo mabanoni, unda nomino yenye kiishio ‘e’
na uitumie kukamilisha sentensi.
1. Dunia hii ina ________ wa aina nyingi. (umba)
2. Mimi nilisoma maandiko ya ________Paulo. (tuma)
3. ________ moja tu la damu yenye virusi huweza kusababisha Ukimwi.
(tona)
4. Kwa nini mama hakununua________? Tutakunywa chai bure? (kata)
5. ________ wangu alinifaa sana wakati wa harusi yangu. (pamba)
D. Kusoma
Kusoma kwa mapana: Magazeti
Magazeti ni machapisho yenye taarifa mbalimbali ambayo hutolewa au
huchapishwa kila siku na huuzwa. Magazeti huwa chanzo cha habari
mbalimbali na tuyasomapo hujua ni mambo gani yaliyotokea nchini,
ulimwenguni n.k. Magazeti yanahusu nchi na ulimwengu wetu, siasa zetu,
mazingira yetu n.k.
68
69
Umuhimu wa magazeti
1. Hutufahamisha habari muhimu zinazotuhusu maishani na kuuhusu
ulimwengu wetu.
2. Hutufahamisha mambo yanayowapata watu katika sehemu mbalimbali
na kwa njia hiyo kutujulisha umuhimu wa kuyaepuka, kwa mfano,
mapigano ya kikabila.
3. Hutuelimisha kupitia makala mbalimbali zinazohusu mambo tofauti
kama afya, elimu, siasa, uchumi, kilimo, biashara, magonjwa, teknolojia
n.k.
4. Hututangazia mambo mageni yaliyoko au yaliyovumbuliwa, kwa mfano,
bidhaa mpya.
5. Hutuwezesha kuupanua ujuzi wetu kuhusu lugha yetu, kwa mfano,
magazeti ya Kiswahili kama Taifa Leo huwa na makala ya lugha,
mafumbo, methali n.k.
6. Hutusaidia kuijenga hamu ya kusoma ambayo inaweza kutufaa hata
katika usomaji wetu mwingine.
7. Hutuburudisha kupitia habari za michezo, burudani, michoro ya vibonzo,
vichekesho n.k.
Sifa za lugha ya magazeti
a) Hutumia lugha yenye mvuto mkubwa.
b) Huwa na sifa ya kumtia hamu msomaji kutokana na ufupi wake.
Kwa mfano, anwani kama ‘Mhalifu kizimbani’, ‘Gor Mahia yainyukua
Tusker’ ‘Jambazi lakiona cha mtemakuni’ n.k.
c) Haitumii wakati uliopita katika anwani zake, kwa mfano
‘Watoto waandamana kudai kuandikishwa shuleni’ (badala ya
‘waliandamana…’) ‘Wabunge wajiongezea marupurupu’ n.k.
Mfano wa makala ya gazeti
hicho kinatumiwa kama njia ya kuwalaghai wafadhili.
Wasichana 16 walihamishiwa Makao ya Watoto ya Homa
Bay yanayodhiniwa na makanisa ya Full Gospel nchini.
Nao wavulana 40 walipelekwa katika kituo cha kurekebisha
tabia cha serikali mjini Kericho.
Hata hivyo, mkurugenzi wa Ogwedhi, Bw. Lawrence
Alosso aliishutumu serikali akisema ina nia mbaya
kuhusu kituo chake. “Kuna maelfu ya watoto wanoateseka
barabarani lakini serikali haijafanya lolote kuwasaidia. Hali
ya hapa kituoni ni bora kuliko barabarani,” akaongeza.
Na WILLIAM ORENDE
Kituo cha watoto mjini Homa Bay kimefungwa na watoto
59 kuhamishwa hadi vituo vingine kufuatia madai ya watoto
hao kuteswa.
Mkurugenzi msaidizi wa Huduma za Watoto, Bw. Ahmed
Hussein, akiandamana na Asa Mkuu wa Watoto mkoani
Nyanza, Bi. Josephine Konosi, waliwasili katika kituo hicho
jana asubuhi na kuamuru kifungwe.
Walisema makao hayo ya kufunza na kurekebisha
watoto ya Ogwedhi, ambayo yanadhaminiwa na Hazina ya
Mayatima ya Kenya, hayajasajiliwa na Serikali. Kadhalika,
maasa hao walisema wanachunguza madai kuwa kituo
Kituo cha watoto chafungwa
HOMABAY
70
71
E. Kuandika
Mialiko
Mwaliko (mialiko) ni barua ambayo hupeleka taarifa kwa mtu kumwomba
ahudhurie sherehe fulani kama harusi, kumbukumbu ya tukio fulani, ubatizo,
harambee au mchango n.k.
Kazi ya mwaliko
Mwaliko hutumiwa:
1. Kutujulisha kuwako kwa shughuli fulani.
2. Kuutaka msaada wetu katika shughuli fulani, kwa mfano, mchango wa
fedha.
3. Kutukumbusha kuwako kwa tukio fulani hasa kwa kuwako kwa hifadhi
ya kimaandishi tunayoweza kuisoma mara kwa mara.
4. Huwasaidia wanaoandaa shughuli fulani kupanga vizuri. Kutokana na
idadi ya mialiko wanaweza kujua wanahitaji chumba kikubwa kiasi
gani, watahitaji chakula kiasi gani n.k.
Mialiko kwa kawaida huwa mifupi; haina maelezo au taarifa ndefu.
Mialiko huzingatia:
(i) Jina la mwandishi/mwalikaji na anwani yake.
(ii) Jina la mwalikwa au mwandikiwa.
(iii) Kusudi la mwaliko/mwalikaji.
(iv) Tarehe ya sherehe na wakati itakapoanza.
(v) Mahali itakapofanyika/pa kukutania.
(vi) Anwani na nambari ya simu ya mwalikaji/jibu lipelekwe kwa
nani.
Mfano wa mwaliko
Bwana na Bi. Mwasimba Hemed wana furaha kukualika Bw/Bi Bashir
Mwamvuli kwenye sherehe/tafrija ya ndoa ya mwana wao Bwana Rashid
Mwasimba itakayofanyika katika shule ya upili ya Maji Mazuri tarehe 5:2:04
saa 2.00 kamili na baadaye kufuatiwa na karamu kwenye ukumbi wa Milimani.
Maswali
1. Je, mwaliko una umuhimu gani?
2. Kwa kuzingatia mfano uliopewa, toa mfano wa mwaliko.
70
71
Sura ya Saba
A. Ufahamu
Misitu na faida zake
Kati ya sehemu ambazo ni muhimu sana
katika mazingira ya binadamu ni misitu.
Wataalamu wa masuala ya mazingira
wanapendekeza angalau asilimia kumi
ya ardhi ya kila nchi kuwa na misitu.
Baadhi ya nchi zimekia kiwango hiki
na labda hata kukipiku ilhali nyingine
ziko chini ya kiwango hiki. Hali hii
hutokana na matumizi mabaya ya misitu
yenyewe, ufyekwaji wa miti ili kuchoma
makaa, unyakuzi wa misitu na ufyekaji
ili kuanzisha kilimo. Katika sehemu
nyinginezo kuruduka kwa idadi ya wakazi
kunawalazimisha watu kuyajongea maeneo
ya misitu kutafuta mahali pa kulima
na kuishi. Kuwepo kwa misitu ni jambo
linalopaswa kushikiliwa kwa udhati wa
moyo na kila mwananchi. Umuhimu wa
misitu unatokana na manufaa ya kila
nui yanayotokana na misitu hiyo kwa
wanaohusika.
Misitu husaidia kuhifadhi ardhi
isimomonyolewe na kuondolewa na maji ya
mvua kwa urahisi. Mmomonyoko wa ardhi
huishia kusababisha maafa na madhara
makubwa sana kwa watu. Aidha, misitu
husaidia kurekebisha mtiririko wa maji
ya mito; kwa sababu misitu huifanya mito
isifurike kupita kiasi. Sote tunaelewa
madhara yanayoweza kusababishwa na
gharika au mafuriko yanayotokana na
kunyesha kwa mvua za mzo. Kuwepo
kwa misitu pia huzuia kiwango cha
takataka kama mchanga, ardhi au majani
yanayochukuliwa na maji ya mito. Kwenye
mabonde ya baadhi ya mito huenda
kukawa na miradi kadha, mathalan
ya kutengeneza nguvu za umeme au
mashamba ya kumwagiliwa maji. Ikiwa
Ukataji wa miti misituni.
Msitu wa Mlima Kenya pamoja
na Mto Nyamindi unaopita
ndani yake.
72
73
takataka zote zibebwazo na maji hazikuchujwa uwezekano wa kuharibiwa
kwa miradi hii ni mkubwa.
Misitu hurekebisha kiasi cha maji yanayoingia ardhini pamoja na
akiba ya maji hayo ardhini. Kuwapo kwa misitu huzuia mvua kuipiga ardhi
moja kwa moja na pia huzuia kukaushwa kwa unyevu na jua. Mizizi ya miti
hufyonza maji kutoka ardhini na kutoa kiasi fulani kwenda angani kupitia
kwenye majani. Maji hayo hufanya hivi kwa kupitia kwenye unyevu ambao
unakuwa msingi wa mvua ya baadaye.
Misitu hutumiwa kama hifadhi na makao ya wanyama ambao sio
muhimu tu kama kivutio cha utalii bali ni muhimu pia katika kudumisha
mfumo ikolojia unaohitajika katika mazingira mazuri; yaani mpatano mzuri
kati ya watu, wanyama na mimea katika mazingira fulani. Fauka ya faida
hizi, kuna faida nyinginezo zinazotokana na misitu kama miti na mbao
za ujenzi. Misitu huwa na miti maarufu kama mininga, mifuu, mivule na
mipingo ambayo ni nyenzo muhimu wakati wa ujenzi. Baadhi ya miti hii
hutumiwa kuundia na kutengenezea bidhaa za kila aina kama samani na
vinyago ambavyo huweza kuuzwa na kuimarisha uchumi wa taifa.
Maendeleo ya utati wa kisayansi yameonyesha mchango mkubwa
unaotokana na miti hasa ya kienyeji kuhusiana na dawa zinazotumiwa
kuyatibia magonjwa sugu. Isitoshe, kuwapo kwa karatasi zinazotumiwa
kutengenezea vitabu huitegemea misitu. Sote tunapasa kuuelewa umuhimu
huu wa misitu na kuwajibika kuhakikisha kuwa misitu yetu haiharibiwi.
Ikiwa tutazembea katika wajibu wetu huu, basi kuna hatari ya maisha ya
kesho kuwa magumu kwa sababu ya matatizo ya ukosefu wa maji, kuwepo
kwa majangwa na kukosa maligha za kimsingi ambazo ni nguzo za uchumi
wetu wa leo.
Maelezo ya msamiati
kila nui : kila aina; sampuli mbalimbali.
mathalan : mfano; kwa mfano.
kivutio : kitu kipendezacho macho; kitu cha
kuvutia.
Maswali
1. Wataalamu wa masuala ya mazingira wanapendekeza kila nchi iwe na
kiasi kipi cha misitu?
2. Baadhi ya nchi zina misitu isiyokia kiwango kinachohitajika. Hali hii
husababishwa na nini?
3. Taja faida tano za misitu.
4. Wewe kama mwanafunzi unasaidiaje kuyatunza mazingira?
5. Taja aina kumi za miti unazozijua.
6. Tunga sentensi ukitumia maneno haya ili kuonyesha maana yake:
(a) kukipiku (b) kuruduka (c) mvua za mzo
(d) mfumo ikolojia (e) magonjwa sugu (f) maligha
72
73
B. Kusikiliza na kuzungumza
Ufahamu wa kusikiliza
Katika kidato cha kwanza, tuliona tofauti iliyoko kati ya ufahamu wa
kusikiliza na ule wa kusoma. Kimsingi katika ufahamu wa kusikiliza,
unapata taarifa iliyopo kwa kusikiliza au kwa kuyatumia masikio yako.
Unaweza kuipata habari hiyo kwa kusimuliwa (kwa mfano, hadithi katika
fasihi simulizi) au kwa kusomewa na mwalimu. Ili uweze kuipata habari
unayosikiliza au inayosomwa, lazima uzingatie mambo yafuatayo:
1. Kuwa makini kwa kile kinachosimuliwa au kinachosomwa.
2. Husisha mambo muhimu na habari inayosimuliwa.
3. Jua matamshi au zingatia matamshi ya asomaye.
4. Bainisha mawazo makuu katika kifungu unachosomewa.
5. Usijitahidi kuyakumbuka maneno bali mawazo na hoja kuu.
6. Iweke akili yako katika kuyasikiliza unayotakiwa kuyasikiliza
unayosomewa au kusimuliwa.
Zoezi la ufahamu wa kusikiliza
Sikiliza kwa makini kifungu atakachokisoma mwalimu halafu ujibu maswali
atakayokuuliza.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Vivumishi
(i) Vivumishi vya kumiliki (vimilikishi)
Hivi ni vivumishi vinavyoonyesha kuwa kitu fulani kinamilikiwa na mtu au
kitu fulani. Ni maneno kama yangu, chake, lake n.k. Kwa mfano:
a) Walimu wetu wamewasili.
b) Wazazi wao wamekwenda wapi?
c) Mimi nitamchungia ndama wake.
d) Kwa nini wamempiga mtoto wako?
e) Kuku wake na bata wangu wameliwa na mwewe.
(ii) Vivumishi vya kuuliza (viulizi)
Vivumishi vya aina hii hutumika katika kuuliza swali. Kwa mfano; ipi, zipi?
ngapi? gani? n.k. Tazama mifano:
a) Mama amesema atauza ng’ombe yupi?
b) Zawadi anasomea shule gani?
c) Baba amepika chakula kipi?
d) Ni wanafunzi wangapi wameondoka?
e) Ni methali ngapi zimetumika?
74
75
Zoezi
1. Soma aya ifuatayo kisha upigie mstari vivumishi vya kumiliki (vivumishi
vimilikishi) vilivyomo.
Ingawa Okelo hakupatikana na hatia, aliachishwa kazi kulingana na
ombi lake la kuacha kazi ambalo lilikuwa limekwishapokelewa. Okelo
alirejea nyumbani na kuwaambia wazazi wake kwamba angependa
kwenda Nairobi kujitafutia riziki mpya.
(Imenukuliwa kutoka Uhalifu Haulipi na Leo Odera Omolo.)
2. Chagua kivumishi mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo:
yapi, wepi, ipi, yupi, upi, kipi
1. Ni mfungwa _______ aliyetoroka?
2. Ni wanafunzi _______ waliohitimu?
3. Unataka kitabu _______?
4. Babu atavaa fulana _______?
5. Utatumia uzi _______?
6. Ni matunda _______ yamenunuliwa?
2. Kuakisha
(i) Nukta pacha/nukta mbili/koloni (:)
Nukta pacha, nukta mbili au koloni ni alama ya kuakisha itumikayo katika
mazingira ya kimaandishi kama yafuatayo:
Kutanguliza orodha; kwa mfano:
(a) Ingawa nilimwambia kakangu aniletee vifaa vya kuandikia,
alipokuja alikuwa amebeba vitu vitatu: upanga, jembe na uma.
(b) Katika kijiji kizima, hakuna mtu ambaye hakujua bidhaa zilizouzwa
katika duka la Bwana Jumakoshi: kamba, vikapu, miiko na mipini.
(c) Katika ligi kuu ya mchezo wa kandanda, kuna timu tatu maarufu
zaidi: AFC, Gor Mahia na Tusker.
Kutanguliza maelezo; kwa mfano:
(a) Tulipowasili mjini tulishangaa kuona duka la Bwana Jumakoshi
limefungwa: lazima kulikuwa na sababu maalum.
(b) Kakangu alipoka nyumbani jioni hiyo alikuwa na furaha ajabu: bila
shaka alikuwa amepita mtihani wake.
(c) Nilipoka hospitalini kumwona raki yangu aliyekuwa amelazwa
humo baada ya ajali ya barabarani, nilikuta kila mtu akilia: raki
yangu alikuwa ameaga dunia.
74
75
Kutanguliza wahusika katika michezo ya kuigiza; kwa mfano:
david
: (akikutana na Jane): Wikiendi kweli hii.
jane
: Kwa nini?
david
: Watu wajikwatua hata - salama lakini?
jane
: Salama tu. Bila shaka ni Flora unayemngojea.
david
: Hukosei Jane. Nipe ujumbe basi.
jane
: Mliagana siyo?
david
: La sivyo hungenikuta hapa nikionekana mjinga hivi,
peke yangu.
jane
: Basi mngojee bila shaka yuaja. Kwaheri ya kuonana.
david
: Haa haraka namna…
(Imenukuliwa kutoka Tazama Mbele na J. Kitsao, uk. 17)
(ii) Nukta mkato/semi koloni (;)
Nukta mkato au semi koloni ni alama inayotumika kutenganisha mafungu ya
maneno yenye maana sawa katika sentensi. Mafungu hayo huweza kusimama
peke yake na kuwa sentensi kamili, kwa mfano:
(a) Baada ya kushinda uchaguzi huo, wananchi hawakufurahi kama
ilivyotarajiwa; ahadi nyingi walizoahidiwa wakati wa kampeni za
uchaguzi hazikutimizwa.
(b) Siki hizi watu wengi wanapooa hawataki kupata watoto wengi;
gharama ya maisha imeenda juu zaidi.
(c) Kwa vile nimefanikiwa kujiunga na shule ya sekondari, nitajitahidi
kwa uwezo wangu wote; hii ndiyo njia ya pekee ya kuwashukuru
wazazi wangu.
(iii) Kiulizo/kiulizi (?)
Hii ni alama inayotumika katika kuulizia swali, kwa mfano:
(a) Sungura alitoroka vipi?
(b) Mchezo ulikwisha lini?
(c) Yule mtu anataka nini?
(d) Unakwenda wapi?
(e) Unamwandikia nani barua hiyo?
(iv) Alama ya hisi (!)
Hii ni alama inayotumika kuonyesha hisia za moyoni kama furaha, huzuni,
mshtuko, mshangao na kadhalika. Kwa mfano:
(a) Salala! Ni nani yule?
(b) Lo! Timu yetu imefungwa bao jingine.
(c) Naam! Nitakuandama mpaka ahera.
(d) Po! Wewe hujui unalofanya.
(e) Tutaonana inshallah!
(f) Baba amenunua baiskeli mpya!
76
77
3. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi -enyewe
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
-enyewe
a mchawi mwenyewe Mchawi mwenyewe amekufa.
wa wachawi wenyewe Wachawi wenyewe wamekufa.
u mkwaju wenyewe Mkwaju wenyewe umevunjika.
i mikwaju yenyewe Mikwaju yenyewe imevunjika.
u ulezi wenyewe Ulezi wenyewe unafaa.
ya malezi yenyewe Malezi yenyewe yanafaa.
ya maziwa yenyewe Maziwa yenyewe yamekwisha.
ya maziwa yenyewe Maziwa yenyewe yamekwisha.
li tunda lenyewe Tunda lenyewe limeiva.
ya matunda yenyewe Matunda yenyewe yameiva.
ki kiti chenyewe Kiti chenyewe kiko wapi?
vi viti vyenyewe Viti vyenyewe viko wapi?
vi visuguru vyenyewe Visuguru vyenyewe viko wapi?
ki kinaya chenyewe Kinaya chenyewe kinaudhi.
zi fedha zenyewe Fedha zenyewe hazitatosha.
Zoezi
1. Tumia kivumishi ‘-enyewe’ kukamilisha sentensi zifuatazo:
K.m. Mchezaji ________ameka.
Mchezaji mwenyewe ameka.
(a) Mtungi ________ umetumbukia kisimani.
Mitungi ________ imetumbukia visimani.
(b) Mzazi ________ alikasirika sana.
Wazazi ________ walikasirika sana.
(c) Ugonjwa ________ utakwisha.
Magonjwa ________ yatakwisha.
(d) Manukato ________ ni ya nani?
Manukato ________ ni ya nani?
(e) Mimi ninataka chakula ________.
Sisi tunataka vyakula ________.
2. Chagua nomino mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo.
(a) Jana jioni nilimwona ________ mwenyewe. (kikapu, mwizi)
(b) Wazalendo wa Msumbiji wameshinda ________ vyenyewe. (vita,
mchezo)
(c) Ni nani anayeeneza ________ wenyewe? (ugonjwa, magonjwa)
(d) ________ vya Maria vimeraruka vyenyewe. (rinda, viatu)
(e) ________ haya yenyewe ni ya nani? (embe, maembe)
(f) Wawindaji haramu wamewaua ________ wenyewe. (ndovu, kiroboto)
76
77
(g) Ni nani aliyekula ________ wenyewe? (chakula, mkate)
(h) ________ yenyewe yana chumvi. (chungwa, maji)
(i) Juzi tulitembelea ________ yenyewe. (makavazi, mji)
(j) ________ wenyewe ni wa hali ya juu. (ubora, shamba)
3. Andika sentensi zifuatazo katika umoja.
(a) Wakulima wenyewe wameka.
(b) Vijiko vyenyewe viko hapa.
(c) Magonjwa yenyewe yamekwisha.
(d) Mizinga yenyewe imejaa asali.
(e) Manukato yenyewe yananukia.
(f) Mende wenyewe wanaudhi.
(g) Mikate yenyewe inaliwa.
(h) Vyakula vyenyewe vina uchafu.
(i) Malezi yenyewe yalifaa sana.
(j) Kondoo wenyewe watachinjwa.
4. Upatanisho wa kisaru: Viambishi awali vya vitenzi
Ngeli ya i/zi
Umoja Wingi
Sahani imevunjika. Sahani zimevunjika.
Nyumba itajengwa. Nyumba zitajengwa.
Nchi imeendelea. Nchi zimeendelea.
Bandari ilifunguliwa. Bandari zilifunguliwa.
Koa imevuliwa. Koa zimevuliwa.
Ngeli ya u/zi
Umoja Wingi
Uzi umenunuliwa. Nyuzi zimenunuliwa.
Ufa utazibwa. Nyufa zitazibwa.
Uso unang’aa. Nyuso zinang’aa.
Ukuta utajengwa. Kuta zitajengwa.
Wimbo umekwisha. Nyimbo zimekwisha.
Ngeli ya u/u
Umoja Wingi
Ukulima unafaa. Ukulima unafaa.
Uasherati utamwua. Uasherati utawaua.
Usingizi ulizidi. Usingizi ulizidi.
Ulaghai utakwisha. Ulaghai utakwisha.
Ubora ulinipendeza. Ubora ulitupendeza.
78
79
Ngeli ya ku/ku
Umoja Wingi
Kutoroka kulimsaidia. Kutoroka kulimsaidia.
Kusoma kunafaa. Kusoma kunafaa.
Kulima kuna manufaa. Kulima kuna manufaa.
Kuiba kuna madhara. Kuiba kuna madhara.
Kuomba kunafaidi. Kuomba kunafaidi.
Ngeli ya pa/ku/mu
Umoja Wingi
Mahali panapendeza. Mahali panapendeza.
Mahali kunapendeza. Mahali kunapendeza.
Mahali mnapendeza. Mahali mnapendeza.
Zoezi
Soma kifungu kifuatacho huku ukijaza viambishi vya upatanisho
wa kisaru vilivyoachwa.
Nilipoka shuleni nilikuwa nimelimatia mno. Ukumbi wa mikutano katika
shule ya Suwerwa __likuwa __mefurika furifuri. Ulikuwa __meshiba mpaka
__katapika, kama wengine wasemavyo. Walimu __likuwa __meketi vitini kwa
safu, sehemu ya mbele zaidi ukumbini. Nilitengewa kiti __moja katika safu
hiyo ya walimu. Nilipokewa na Bi. Nambuye Pilipili kwa moyo __kunjufu.
__lipoingia ukumbini naye, umati __lizizima mzizimo wa kutisha. Moyo
wangu __karindima na kijasho chembamba kunichiriza. Mwalimu huyo wa
Kiswahili Bi. Nambuye Pilipili __kapanda jukwaani__likokuwa na kipaaza
sauti. “Hamjambo wanafunzi?” __kasema. “Hatujambo mwalimu,” __kajibu.
“Basi __nayo furaha tele kukuambieni kuwa mhadhiri wetu mgeni Kongowea
Mswahili__mewasili. Yeye ni malenga stadi na tena bingwa wa Kiswahili.
__takumbuka kuwa ni mwaka huu tu ndipo __lishinda katika shindano la
utunzi wa mashairi Kenya nzima. Kwamba __mekubali mwaliko wetu kuja
tumwone na __msikia ni heshima kubwa. Mada __takayoiongelea ni “Matatizo
__nayoikumba lugha ya Kiswahili.” Yeye ni kijana mdogo lakini karundikiwa
rundo la vipawa. Lakini sitaki kusema sana. Karibu Bwana Kongowea.
(Imenukuliwa kutoka Siku Njema na Ken Walibora, 1996 uk 126)
D. Kusoma
Tamthilia: Utangulizi
Katika kidato cha kwanza, tuliona kuwa tamthilia au mchezo wa kuigiza una
muundo tofauti na riwaya kwa kuwa hapa mazungumzo au dayolojia hutumiwa
sana. Sifa nyingine muhimu ni kuwa huandikwa kwa nia ya kuwasilishwa
jukwaani. Matendo ya wahusika ni muhimu na huwa fupi. Tunaweza kusema
78
79
kuwa tamthilia ni kama hadithi fupi inayoigizwa au kuwasilishwa jukwaani.
Tatu, riwaya inategemea usimulizi wa moja kwa moja wa mwandishi tofauti
na tamthilia ambayo hutegemea matendo na mazungumzo ya wahusika.
Ili tuweze kufaidika kutokana na usomaji wetu wa tamthilia, tunapaswa
kujiuliza maswali kadha:
(i) Je, ni mambo gani yanayozungumziwa?
(ii) Je, kuna mhusika anayetamani kupata kitu fulani maalum?
(iii) Je, yupo mhusika anayemzuia kukipata kitu hicho akitakacho?
(iv) Je, ni mambo gani makuu yanayozungumziwa katika tamthilia
hiyo?
(v) Je, kuna baadhi ya mambo ambayo hayachukui nafasi muhimu?
(vi) Je, wahusika waliopo ni wangapi na kila mmoja ana kazi gani?
(vii) Je, tamthilia hiyo ina muundo wa namna gani?
(viii) Je, lugha inayotumiwa na wahusika ina sifa gani? Je,
inatuonyesha nini kuwahusu wahusika wenyewe?
(ix) Je, wahusika hao wana sifa gani kama viumbe?
(x) Je, unaweza kutoa muhtasari wa hadithi ya tamthilia; yaani
mtu akikuuliza inahusu nini unaweza kumjibu?
Maswali haya ni muhimu sana katika kuisoma tamthilia. Maswali yenyewe
yanagusia sehemu mbili kuu za tamthilia (na pia kazi zote za kifasihi):
maudhui na fani.
Katika sura hii tutaangalia maudhui, kwa kujiuliza swali la kimsingi,
maudhui ni nini? Maudhui ni jumla ya mambo yanayozungumziwa katika
tamthilia au kitabu cha kifasihi. Maudhui hujumlisha dhamira ya mwandishi
wa tamthilia inayohusika. Pili, hujumlisha pia maadili au mafunzo; yaani
mambo ambayo mwandishi anataka sisi kama wasomaji tuyaelewe. Tatu,
hujumlisha pia msimamo wa mwandishi kuhusu mambo mbalimbali
anayoyazungumzia.
Jinsi ya kutambua maudhui
Ili kuweza kutambua maudhui ya tamthilia tunajiuliza:
(i) Je, anwani ya tamthilia hiyo ni ipi?
(ii) Je, wahusika wanazungumzia nini kwa mapana kuanzia
mwanzo hadi mwisho?
(iii) Je, ni mawazo gani yanayojitokeza mno katika mazungumzo?
(iv) Je, wahusika wanatamani kufanya nini na ni kitu gani
kinachotokea?
(v) Je, hadithi iliyopo inagusia mambo gani?
(vi) Je, ni matukio gani makuu yanayopatikana katika tamthilia?
Zoezi
(i) Je, kuna tofauti gani kuu kati ya tamthilia na riwaya?
(ii) Je, dhamira ni nini?
80
81
(iii) Je, ni mambo gani ya kuangalia unapotaka kujua maudhui ya
tamthilia.
D. Kuandika
Insha ya mazungumzo
Hii ni insha ambayo huwa na maongezi kati ya watu wawili au zaidi
kuhusu jambo fulani. Maongezi au mazungumzo hayo huwa na sifa kadha.
Sifa hizo ni:
a) Kiini au mada ya mazungumzo: Lazima mazungumzo yawe
yanazungumzia jambo fulani ambalo limekuzwa kuanzia mwanzo
hadi mwisho.
b) Hutumia usemi halisi kwa sababu mwandishi huandika maneno
kama yanavyotumiwa na wazungumzaji.
c) Lugha ya wazungumzaji hutegemea wanaohusika wana uhusiano
gani na wanazungumzia wapi na kuhusu nini?
d) Jina la mzungumzaji huandikwa kwanza na hufuatiwa na alama ya
koloni au nukta mbili (:) kabla ya maneno yenyewe.
e) Huwa na mchanganyiko wa majibu mafupi na marefu ili kubadilisha
mtindo.
f) Huwa na maelezo ya kando yanayofungiwa kwenye mabano ambayo
yanaonyesha maelezo ya wakati n. k.
Mfano wa insha ya mazungumzo
Chozi la jicho moja
(Makumba ameketi kitini huku ameshika tama. Anaonyesha huzuni
nyingi. Wakati huu anaingia raki yake Sululu)
sululu
: (Akishangaa) Umeamkaje mwenzangu?
MakuMba
: Nimeamka vyema, sijui nyinyi huko.
sululu
: Ahh hamna neno, tunashukuru.
MakuMba
: Haya karibu!
sululu
: Asante. (akimwangalia) Unaumwa au nini?
MakuMba
: Mimi?
sululu
: Ehh wewe raki yangu, Makumba!
MakuMba
: Nina huzuni!
sululu
: Huzuni?
MakuMba
: Ehh, tena kubwa (anapumua kidogo) Nina huzuni
inayoniliza chozi la jicho moja?
sululu
: (akicheka) Chozi la jicho moja? Ahh bwana we, mbona
unanichekesha…
MakuMba
: Hamna ucheshi hapa ni ukweli wenyewe!
80
81
sululu
: Lipi la mno?
MakuMba
: Si unamjua mwanangu aliyeyoyomea mjini?
sululu
: Si huyu huyu Kiparangoto?
MakuMba
: Huyo ehhh. (Anashusha pumzi) Basi mwenzio nimepata
taarifa jana kuwa amekamatwa kwa kuhusika na
ulanguzi wa dawa za kulevya…
sululu
: Ahh Mungu wee! (Akimsogea) Pole mwenzangu, pole
tena sana! (Kama anajisemea) Haya maovu ya siku hizi
jama, sijui tutaishia wapi?
Zoezi
Andika mazungumzo kati ya abiria na utingo.
82
83
Sura ya Nane
A. Ufahamu
Shairi
Haki zetu twazitaka
MToTo
: Usemi natanguliza, masikio yategeni,
Haya ninayoeleza, yaw’engie akilini,
Na mpate kuyawaza, msiyatie kapuni,
Hii awamu nyingini, haki zetu twazitaka.
Haki zetu twazitaka, tuishi kama wengini,
Na sote kujumuika, pia twende mashuleni,
Tusome ya kusomeka, yatufae maishani,
Hii awamu nyingini, haki zetu ni lazima.
Mwajiri
: Haki zenu ni lazima, hayo yameanza lini?
Hata hujui kusoma, hujatoka ujingani,
Burebure walalama, hali ni kama zamani,
Hiyo awamu nyingini, itabaki kuwa ndoto!
MToTo
: Itabaki kuwa ndoto, hii haiwezekani,
Japo tuwe tu watoto, twajua twataka nini,
Kutubebesha mazito, kama sisi hayawani,
Hii awamu nyingini, makazini hatutaki.
Makazini hatutaki, tunaumia milini,
Kufanya yasiyo haki, kazi isiyo mizani,
Na mkatutwisha dhiki, nyinyi kweli ni kaini,
Hii awamu nyingini, ‘tamalizika dhuluma.
Mwajiri
: ‘tamalizika dhuluma, ndiyo ipi hiyo kwani?
Nami ninakupa mema, chakula pia mapeni,
Au una lipi sema, nijue nifanye nini,
Kuwa awamu nyingini, naona umechochewa.
MToTo
: Kabisa sijachochewa, nimetoka ujingani,
Ja mnyama kutumiwa, yameka ukingoni,
Mambo mawi kufanyiwa, kama taka mapipani,
Hii awamu nyingini, haki zetu twazitaka.
Mwajiri
: Haki zenu mwazitaka, zipi hizo nambieni,
Ziseme zote haraka, nami niweze baini,
Ikiwa hazina shaka, mkono niwaungeni,
Hiyo awamu nyingini, huanza wapi jamani?
82
83
MToTo
: Huanza hivi jamani, kwa elimu darasani,
Elimu ni namba wani, inoangaza gizani,
Tusome kwayo makini, tuke hata chuoni,
Hii awamu nyingini, hilo la kwanza jueni.
Hilo la kwanza jueni, na pili sikilizeni,
Ajira itambueni, kututia makazini,
Dhuluma iso kifani, hutuathiri milini,
Hino awamu nyingini, yamepita ya zamani.
Yamepita ya zamani, ya kutengwa sheriani,
Na hata mahakamani, na mateso ya nyumbani,
Wala kero za njiani, matendo ya makaini,
Hino awamu nyingini, ikwingie akilini.
Mwajiri
: Kweli umeniangaza, nimeyajua yakini,
Kweli tumewachakaza, kuwap’uza maishani,
Nami leo natangaza, mikono nawashikeni,
Kweli awamu nyingini, kumekucha kulichele.
Maswali
1. Shairi hili linaongea kuhusu nini?
2. Taja haki zote anazotaka mtoto.
3. Mwajiri anajiteteaje katika ubeti wa tatu?
4. Mwishoni mwa shairi mwajiri anakubaliana na mtoto. Unadhani ni kwa
nini anafanya hivyo?
5. Tumia maneno haya kutungia sentensi kulingana na matumizi yake
kwenye kifungu:
(a) hayawani (b) kaini (c) mawi (d) baini
6. ‘Msiyatie kapuni’ ni mfano wa msemo. Eleza maana ya misemo ifuatayo
kisha uitumie kutungia sentensi:
a) fanyia kizungumkuti b) jifunga kibwebwe c) piga maji
d) patikana na mambo
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii:
Mazungumzo: Hotelini
(Kibwana Jaku anaingia hotelini. Anachagua meza ambayo iko pembeni si
mbali na ulipo mlango. Mhudumu wa hoteli anamjia)
MhuduMu
: Karibu, habari ya asubuhi?
kibwana jaku
: Poa tu. Vipi?
84
85
MhuduMu
: Hamna neno. (Anatua) Utakula nini?
kibwana jaku
: Mna nini kwani? (Kimya) Hamna
menu? (Mhudumu anageuka anakwenda
kumchukulia menu na kumkabidhi Kibwana Jaku). Asante.
Mna biriani?
MhuduMu
: Samahani imeisha hiyo!
kibwana jaku
: (Akiiangalia menu) Pilau nayo!
MhuduMu
: Imeisha pia!
kibwana jaku
: Nini ambacho hakijaisha basi?
MhuduMu
: Kuku na chapati, maini na ugali; karanga
na wali, bajia na pia chipsi.
kibwana jaku
: Nipe hiyo kuku na chapati.
MhuduMu
: Je, na kinywaji?
kibwana jaku
: Nipe soda tu. (Mhudumu anageuka) Aisee!
MhuduMu
: Naam!
kibwana jaku
: Na kuku usiniletee shingo, unasikia?
(Mhudumu anaitikia) Tafuta sehemu nzuri
kama kiga na rigisi. Kisha, usisahau na
kachumbari na pilipili kidogo ili utamu
wake unogee! (Baada ya muda anahudumiwa
na kuanza kula. Mhudumu anakwenda
kusimama kando. Baada ya muda) Aisee!
MhuduMu
: Nikusaidie nini?
kibwana jaku
: Njiti za kuchokonolea meno. Nyama zimesaki
kwenye meno na kuanza kunisumbua.
(Anaondoka na kurudi na njiti juu ya kisahani
kidogo. Kibwana Jaku anakichukua na kuanza
kuyachokonoa meno yake) Pesa ngapi?
MhuduMu
: Jumla mia mbili!
kibwana jaku
: Mia mbili kwa chakula hiki tu!
MhuduMu
: Ndiyo mzee!
kibwana jaku
: (Akitoa pesa. Kama anajisemea) Thamani ya
pesa imekwenda wapi? Chakula hata
hakijashuka kumi! Aah, jamani s huko ni
kutupunja tu! (Anatoa noti ya shilingi mia
tano na kumkabidhi. Baada ya muda mhudumu
anarudi na baki yake) Hata hamna
punguzo!
MhuduMu
: Mzee bei yenyewe si ya juu sana!
84
85
kibwana jaku
: Unaona? Hata wewe unajua ni ya juu, ni
kwamba tu si sana!
MhuduMu
: Ndiyo maisha! Kila kitu kimepanda bei siku
hizi; hata maisha yenyewe!
kibwana jaku
: Ndiyo lakini ni vizuri kutoa japo turuhani
ndogo kwa wateja wenu wa kila siku.
(Anainuka) Haya kwaheri!
MhuduMu
: Kwaheri na karibu tena!
Maswali
1. Je, kwa nini Kibwana Jaku anaelekea kushangaa mwanzoni? Unadhani
kwa nini mhudumu hasemi moja kwa moja kuwa hawana vyakula vingi?
2. Tunga sentensi kuonyesha kuwa unaelewa maana za maneno haya kama
yalivyotumiwa katika mazungumzo haya:
(a) biriani (b) bajia (c) viga (d) unogee (e) zimesaki
(f) turuhani
3. Taja sifa za lugha iliyotumiwa katika mazungumzo haya.
Matamshi bora: Vitate d/nd
Tamka maneno haya
d nd
dege ndege
doa ndoa
duni nduni
Soma: Vitanza ndimi
1. Bonaya alisema hatishwi na ndege lakini siku moja alipoliona dege kubwa
alishtuka na kuanza kutetemeka kama mtoto mwenye degedege.
2. Mhubiri alisema kuwa siku hizi ni vyema kuhakikisha kuwa mwenzako
hana doa kabla ya ndoa kwani akiwa na doa kabla ya ndoa huenda ndoa
yenu ikaporomoka kutokana na madoa.
3. Ingawa tulidhani yule mtu ni duni alitwonyesha nduni na ndipo
tukaamini kuwa unayemdhania kuwa duni huenda akakuonyesha
nduni.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Vivumishi
Vivumishi vya idadi
Hivi ni vivumishi vinavyoonyesha idadi ya nomino ambazo zinazungumziwa
au zinazorejelewa. Kwa mfano:
a) Ndovu watano walinaswa kijijini Kihome.
86
87
b) Wananchi wengi waliikaribisha serikali mpya.
c) Babu anafuga kondoo wachache.
d) Wachuuzi mia moja wametiwa mbaroni.
e) Watu milioni nyingi wanatumia lugha ya Kiswahili.
Jinsi tunavyoweza kuona katika mifano iliyopo hapo juu, baadhi ya vivumishi
hivi huwa ni vya idadi mahususi, kwa mfano: Ndovu watano, na baadhi ni
vya idadi ya jumla, kwa mfano: Wananchi wengi.
Vivumishi vya pekee
Hivi hutokana na mizizi ‘-ote, -o-ote, -ingine, -enye, na -enyewe’.
(i) Kivumishi ‘-ote’
Hiki huonyesha ujumla wa kitu au vitu bila kusaza. Kwa mfano:
(a) Waumini wote wamekwenda msikitini.
(b) Chakula chote kimeliwa na watoto.
(c) Shamba lote limelimwa.
(d) Nyumba yote imefagiliwa vizuri.
(e) Mahali pote pamechafuka.
(ii) Kivumishi ‘-o-ote’
Kivumishi hiki humaanisha ‘bila kubagua’. Kwa mfano:
(a) Kitabu chochote kinafaa.
(b) Mwalimu yeyote atatusaidia.
(c) Maembe yoyote yataliwa na wanafunzi.
(d) Mikeka yoyote itatandikwa huko ukumbini.
(e) Unaweza kununua bidhaa hizo kutoka duka lolote.
(iii) Kivumishi ‘-ingine’
Hutumika kuonyesha sehemu ya baadhi ya vitu. Hutumika pia kuonyesha
tofauti na/au zaidi ya kitu fulani. Kwa mfano:
1. Watu wengine wana tabia za kuchukiza.
2. Ameiba pesa zingine.
3. Kukopa kwingine kunaudhi.
4. Ubishi mwingine hauna maana.
5. Babu atachinja mbuzi wengine.
(iv) Kivumishi ‘-enye’
Kivumishi hiki huonyesha hali ya mtu au kitu ‘kuwa na’ au
kumiliki kitu fulani. Kwa mfano:
(a) Mtoto mwenye kitabu amekuja.
(b) Kiongozi mwenye bidii amechaguliwa tena.
86
87
(c) Kiatu chenye tundu kitashonwa.
(d) Wazee wenye busara watakata kesi hiyo.
(e) Mahali kwenye siafu hakukaliki.
(v) Kivumishi ‘-enyewe’
Hiki hutumika kusisitiza kuwa ni mtu au kitu halisi bila
kuwakilishwa. Pia humaanisha upekee au bila mwengine au kingine. Kwa
mfano:
(a) Nitajipakulia chakula mimi mwenyewe.
(b) Pesa zenyewe zilizokuwa zikitafutwa ndizo hizi.
(c) Magurudumu yenyewe tuliyoyanunua jana yameibwa.
(d) Mahali penyewe tunapoelekea pamefungwa.
(e) Jitu lenyewe limeuawa.
Upatanisho wa kisaru: Kivumishi ‘-ingine’ (Ngeli a/wa -
ki/vi)
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
‘-ingine’
a kondoo mwingine Kondoo mwingine amezaa.
wa kondoo wengine Kondoo wengine wamezaa.
u mshale mwingine Mshale mwingine umetupwa.
i mishale mingine Mishale mingine imetupwa.
u ugonjwa mwingine Ugonjwa mwingine umezuka.
ya magonjwa mengine Magonjwa mengine yamezuka.
ya maradhi mengine Maradhi mengine ni yapi?
ya maradhi mengine Maradhi mengine ni yapi?
li chungwa jingine Chungwa jingine litaliwa.
ya machungwa mengine Machungwa mengine yataliwa.
ki chama kingine Chama kingine kimeanzishwa.
vi vyama vingine Vyama vingine vimeanzishwa.
li joto lingine Joto jingine litatuchosha sana.
vi vitimbi vingine Vitimbi vingiine vimetokea wiki
jana.
ki kiko kingine Kiko kingine kimenunuliwa.
Zoezi
1. Andika sentensi zifuatazo katika wingi.
(a) Mtu mwingine amekamatwa na polisi.
(b) Mkoba mwingine umepotea.
(c) Matunda mengine yalinunuliwa.
(d) Maji mengine yamemwagika.
(e) Maziwa mengine yamekamuliwa.
(f) Kitanda kingine kinatengenezwa.
88
89
.
(g) Mlango mwingine umevunjwa.
(h) Chawa mwingine ameniuma.
(i) Kitabu kingine kitaandikwa.
(j) Ulezi mwingine utatolewa.
2. Tumia kivumishi -ingine kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) Watoto _______ wamepita mtihani.
(b) Viatu _______ vitapigwa rangi.
(c) Maziwa _______ yatamwagika.
(d) Kiti _______ kitaanguka.
(e) Vinanda _______ vitaibiwa.
(f) Jiwe _______ limemwangukia.
(g) Majira _______ yameanza.
(h) Kiko _______ kimewashwa.
(i) Ngamia _______ anakunywa maji.
(j) Miche _______ itapandwa.
Upatanisho wa kisaru: Kivumishi -enyewe
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
‘-enyewe’
i ndege yenyewe Ndege yenyewe inapaa.
zi ndege zenyewe Ndege zenyewe zinapaa.
u uchawi wenyewe Uchawi wenyewe unaua.
u uchawi wenyewe Uchawi wenyewe unaua.
u uzi wenyewe Uzi wenyewe uko hapa.
zi nyuzi zenyewe Nyuzi zenyewe ziko hapa.
ku kuishi kwenyewe Kuishi kwenyewe kunatatiza.
ku kuishi kwenyewe Kuishi kwenyewe kunatatiza.
pa pahali penyewe Pahali penyewe hapafai.
ku mahali kwenyewe Mahali kwenyewe hakufai.
mu mahali mwenyewe Mahali mwenyewe hamfai.
zi fedha zenyewe Fedha zenyewe hazifaidi.
li jua lenyewe Jua lenyewe halijachomoza.
vi vita vyenyewe Vita vyenyewe vinaudhi sana.
ki kimya chenyewe Kimya chenyewe kinatisha.
88
89
Zoezi
1. Tumia nomino iliyo mabanoni badala ya ile iliyopigiwa mstari.
Kwa mfano: Ndege yenyewe imeondoka. (mtoto)
Mtoto mwenyewe ameondoka.
(a) Nyumba yenyewe itabomoka. (jukwaa)
(b) Uzi wenyewe umepotea. (kalamu)
(c) Kucheza kwenyewe kunapendeza. (nguo)
(d) Ukuta wenyewe ni mrefu. (nyumba)
(e) Udaku wenyewe unaudhi. (kuchokoza )
(f) Mahali kwenyewe ni kupi? (uto)
(g) Njia yenyewe ni fupi. (ukuta)
Zoezi
Chagua kivumishi mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) Eropleni __________ imejaa. (yenyewe, zenyewe)
(b) Pahali __________ pamefunguliwa. (kwenyewe, penyewe)
(c) Kuchimbua __________ kumekwisha. (yenyewe, kwenyewe)
(d) Ulimi __________ unauma. (wenyewe, yenyewe)
(e) Nyimbo __________ zinaudhi. (zenyewe, yenyewe)
(f) Ukurasa __________ ni upi? (zenyewe, wenyewe)
(g) Ndoo __________ imejaa maji. (zenyewe, yenyewe)
(h) Wezi waliiba mbao__________. (zenyewe, chenyewe)
(i) Wembe __________ utamkata. (yenyewe, wenyewe)
Zoezi
Andika kifungu hiki na upigie mstari nomino za pekee.
Baada ya Koplo Maselle kukisogeza chombo cha kupigia simu karibu
yake, alikisasha kinywa chake kwa kwanguo moja la nguvu alilokohoa ili
apate kuzungumza barabara.
Koplo Maselle alizidi kubonyezabonyeza kengele ya simu mpaka
alipopata njia wazi hadi Musoma. Naye akaanza kuongea na Inspekta Willey
wa Musoma. Bila kuchelewa Koplo alimfahamisha jina la binti aliyepotea
na alama alizonazo.
Baada ya Inspekta Willey kupokea simu kutoka Morogoro kuhusu
Pili, Koplo Chacha aliingia ndani huku akitoa jasho jembamba na moyo
ukimwenda kasi. Naye alionyesha uchovu mwingi.
“Koplo Chacha, umefanikiwa kumpata yule jambazi aliyenyakua mali
ya yule Baniani aliyeleta taarifa juzi?” Inspekta Willey aliuliza. “Inspekta
Willey, sijui ni bahati gani tuliyoipata leo! Saa tatu barabara tuliingia ndani
ya jumba la anasa lililoenea mno huko mtaa wa Kivu. Tukiwa humo…
(Imedondolewa kutoka Doa la Mauti na P.C. Geranija/
A.S. Muwanga, uk. 15)
90
91
D. Kusoma
Tamthilia
Katika sura ya saba, tulieleza maudhui ni nini na jinsi ya kuyatambua
tunapoisoma tamthilia. Katika sura hii tutaangalia fani. Fani ni jumla ya
njia zinazotumiwa kuyawasilisha maudhui katika tamthilia unayoisoma
(au pia kazi yoyote ya fasihi). Maudhui hayawezi kuwako bila ya kuwako
kwa fani; na fani nayo haiwezi kuwako bila ya kuwako kwa maudhui. Fani
inajumlisha mambo kama vile:
Muundo: Tamthilia huwa na sura au umbo fulani. Ina maonyesho
(na wakati mwingine hata matendo), ina mwanzo, kati na mwisho.
Je, tamthilia hiyo inaanzia na kuishia wapi? Je, muundo wake ni
rahisi kueleweka, kwa mfano, kama wa tamthilia ya Ukame ya
A. S. Yahya na D. Mulwa?
Matumizi ya lugha: Lugha ni nguzo muhimu katika uandishi
wowote ule. Lugha ndiyo nyenzo kuu ya fasihi na jinsi anavyoitumia
mwandishi ni muhimu sana. Tuliona kuwa katika tamthilia,
mwandishi anatumia mazungumzo sana. Je, wahusika wanatumia
lugha ya aina gani? Je, ni rahisi au ni ngumu? wanachanganya lugha?
Je, msamiati anaoutumia mwandishi ni upi? Je, mwandishi anatumia
tamathali za usemi kama tashbiha na sitiari (na nyinginezo)?
Wahusika: Tamthilia inahusu matendo ambayo hutendwa na
binadamu ambao hujulikana kama wahusika. Je, kuna wahusika
wangapi katika tamthilia uliyoisoma? Je, unaweza kusema ni
mhusika yupi au ni wahusika wepi ambao wanachukua nafasi
muhimu sana na /au kwa nini? Je, wahusika hao wanatumiwa ili
kupitisha ujumbe wa aina gani? Je, wahusika hao wamepewa majina
ya aina gani na yana umuhimu wowote?
Mtindo: Kila mwandishi ana sifa zake tofauti za namna anavyotumia
lugha, anavyouteua msamiati wake, anavyowapa wahusika majina,
anavyotumia tamathali za usemi n.k. Huu ni mtindo wake.
Zoezi
(a) Eleza maana ya neno ‘fani’.
(b) Je, ni sehemu gani muhimu kuhusiana na fani?
90
91
E. Kuandika
Hotuba
Hotuba ni taarifa inayotolewa na mtu kwa nia ya kuwasiliana na hadhara
ya watu. Huweza kuandikwa ili isomwe mbele ya hadhara au itolewe moja
kwa moja bila kuhitaji kuandikwa popote kwani wasemaji stadi wana uwezo
wa kutoa hotuba bila ya kuzisoma kutoka popote. Hata hivyo, wasemaji wa
aina hii huhitajika kujua wanachotaka kukizungumzia na hupanga hoja zao
akilini mwao hivi kwamba wakapo kuongea hoja zao hutokea kwa mfululizo
unaofaa usiokanganya hadhira na bila kuacha hoja zozote muhimu.
Umuhimu wa hotuba
(a) Huweza kutolewa kwa nia ya kutoa taarifa fulani kwa hadhira, kwa
mfano, kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira, kujikinga na
magonjwa fulani ya kuambikiza, kufafanua mikakati kuhusu miradi
fulani, jinsi ya kupigana na kuenea kwa matumizi ya dawa za kulevya
n.k.
(b) Huweza kutolewa ili kuwashawishi watu kukubaliana na mawazo
fulani, kuwahimiza watende kazi fulani n.k.
Mambo muhimu kuhusu uandishi wa hotuba
1. Hotuba hugawika katika sehemu tatu kuu ambazo ni mwanzo, kati
na mwisho. Sehemu ya mwanzo ina salamu na utangulizi wa kiini
cha hotuba. Sehemu ya kati ndicho kiini ilhali ya mwisho ni kimalizio
au hitimisho. Sehemu hii hutoa muhtasari wa hotuba pamoja na
shukrani kwa walioisikiliza hotuba yenyewe.
2. Hotuba nzuri ni lazima itolewe kwa namna inayoridhisha.Vile vile,
ni lazima ipangiliwe kwa njia nzuri yenye mantiki.
3. Ili kuandika hotuba inayovutia ni vyema kujiweka katika nafasi ya
mtu atakayeiwasilisha hotuba yenyewe mbele ya hadhira.
4. Ijue hadhira yako ili uweze kujua ni lugha ya aina gani utakayoitumia.
Kwa mfano, ikiwa unawahutubia watoto, lugha yako itakuwa rahisi,
yenye sentensi fupi fupi, na iliyoshehenezwa tamathali wanazopenda
watoto kama vile tanakali za sauti n.k. Lakini unapowahutubia watu
wazima lugha huweza kuwa ya kiwango cha juu zaidi yenye methali,
misemo, tashbihi na tamathali nyingine.
5. Lugha ya hotuba hutakiwa kushawishi na kuhamasisha hadhira.
Pia ni lazima lugha izingatie muktadha unaohusika, mazingira
au utamaduni wa wanaohusika, umri wao n.k. Kwa mfano, lugha
inayotumika kutoa hotuba za mazishi ni tofauti na ile inayotumika
kutoa hotuba za michezoni au arusini.
6. Lugha ya hotuba inatakiwa pia iwe ya kusisimua. Iwapo ni ya
kuchosha huenda watu wakaondoka au ikiwa wanasikiliza hotuba
hii kwenye redio au runinga, huenda wakazima vyombo hivyo au
kuchagua stesheni tofauti.
92
93
7. Msemaji anafaa kutumia sauti ya juu inayosikika vyema na matamshi
mazuri. Halikadhalika, ni muhimu sana kujiepusha na lugha yenye
matusi au isiyozingatia kanuni zifaazo za adabu
8. Mzungumzaji anafaa kuwasilisha mawazo yake kwa nidhamu.
Mfano wa hotuba
Hotuba ya chifu
“Mkuu wa wilaya yetu ya Sebai, mkuu wa polisi wilayani, mkuu wa tarafa,
mabibi na mabwana. Mimi kama chifu wa kata hii, ninawakaribisha nyote
katika eneo hili kwa moyo mkunjufu. Pili, ninatoa shukrani jazila kwa mkuu
wa wilaya yetu kwa kupata nafasi ya kutembelea kata yetu siku ya leo.
Ninaelewa bila shaka ya kuwa amesikia kilio chetu na hii ndiyo sababu kuu
ya ziara yake hapa kwetu.
Mkuu wa wilaya, wananchi walio hapa wanaonyesha nyuso za uchangamfu,
si kwa vile wamekuwa wakiishi maisha mema, lakini ni kwa kutumaini kuwa
tatizo lao sugu litatatuliwa baada ya kungoja kwa muda mrefu. Ingawa
ninajua umeshaelezewa mengi kuhusu hali ya usalama katika eneo hili,
naona ni jambo bora nifafanue kidogo tu jinsi hali ilivyo kukia sasa.
Mkuu wa wilaya, kwa miaka mingi iliyopita, eneo letu halijawa na
tatizo la ukosefu wa usalama hata kidogo. Wananchi wamekuwa wakijiendea
kwenye shughuli zao wakati wowote bila kuhofu chochote. Lakini haya yote
yamebadilika sasa. Kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita, wakazi wa eneo
hili wamekabiliwa na tatizo la kuhosha. Kumezuka magenge ya majangili
ambayo azima yao kuu ni kuwavamia watu majumbani mwao nyakati za
usiku wa manane na kuwaibia mali yao. Vitendo hivi vimeacha mkururo wa
hasara na majonzi katika nyumba nyingi. Licha ya watu kupoteza mali yao,
wengine wamepata majeraha mabaya na hata wengine kupoteza maisha yao.
Isitoshe, siku hizi majangili hawa hawatosheki tu na mali wanazonyakua. La
hasha! Baada ya kusomba mali yenyewe na kuwakatakata watu wanaojaribu
kujitetea, wanawageukia kina mama na kina dada na kuwanajisi.
Kutokana na hali hii, watu wa eneo hili hawapati usingizi kwa
kuchelea kuvamiwa. Wengine wanalala vichakani ili kujinusuru. Vitendo
hivi vimezalisha matunda ya kuhuzunisha. Kutokana na vitendo vyao hivyo
vya unajisi, baadhi ya wanawake wamepata mimba na tayari wengine
wameshajifungua. Isitoshe, wengine wameambukizwa magonjwa ya zinaa
na hata Ukimwi. Majangili wenyewe hawachagui, bali huwanajisi wasichana
wadogo hata wenye umri usiozidi miaka saba.
Mkuu wa wilaya, kata yetu imetanda wingu la huzuni. Lakini jambo
linalokera zaidi ni kuwa, kwa muda huu wote, tumekuwa tukijaribu kusaka
usaidizi kutoka kwa polisi wa eneo hili lakini kukia sasa hatujaupata. Kila
siku mkuu wa polisi tarafani ametuahidi kuwa atatuma askari wa kutosha
ili kushika doria nyakati za usiku. Hata hivyo, hatujamwona askari yeyote.
Tunaozidi kuona ni majangili wanaoendeleza uhuni wao wapendavyo.
Mkuu wa wilaya, tunakuomba usikilize kilio chetu. Tungeomba serikali
ijenge kituo cha polisi katika eneo hili kama jambo la dharura. Lakini kabla
92
93
ya kutekeleza ujenzi huu ambao huenda ukachukua muda, tungeomba
utuletee askari wa kutosha na waliojihami vya kutosha ili kulinda usalama
nyakati za usiku. Majangili hawa hawabebi tu sime na marungu, lakini wana
silaha nyingine hatari zikiwepo bunduki za rasharasha. Iwapo jambo hili
halitafanyika, wakazi wengi wa eneo hili wako tayari kukusanya mali yao
iliyobaki na kuhamia sehemu nyingine za nchi zenye usalama.
Ninajua umekuja hapa leo kwa vile una nia ya kutusaidia. Wakazi wa
kata hii wana imani kuu kuwa utawatatulia tatizo hili lililowakumba kwa
muda wote huu. Asante kiongozi wa wilaya.”
Maswali
1. Hotuba ni nini?
2. Taja mambo manne makuu ya kuzingatia katika kuandika hotuba.
3. Watolee hotuba wenzako darasani kuhusu kichwa: ‘Tohara ya
wasichana’.
4. Umealikwa kwenye sherehe ya kuwahamasisha wanafunzi wa darasa
la nane kusoma kwa bidii, andika hotuba utakayoitoa.
94
95
Zoezi la marudio I
A. Ufahamu
Utalii ni tunu kwa uchumi
Mojawapo ya sekta muhimu na aali inayotoa mchango mkubwa katika
uchumi wa nchi zinazoendelea ni utalii. Utalii kwa jumla unakua duniani na
kuchangia pakubwa ukuaji wa uchumi wa dunia. Ikilinganishwa na miaka
50 iliyopita, idadi ya watalii imeongezeka kwa takriban mara 30. Kuwepo
kwa utalii kuna matokeo makubwa sana kwa kuwa nchi mbalimbali zinapata
kipato kinachoweza kutumiwa kuiendeleza nchi inayohusika. Fedha ambazo
zinatokana na utalii zinaweza kutumiwa kuhakikisha kuwa huduma za
kimsingi kama vituo vya afya zinasambazwa nchini. Aidha, utalii ni njia
mojawapo nzuri ya kuzipa nchi mbalimbali umaarufu ulimwenguni.
Utalii kama biashara unakua kwa kasi na watalii wamekuwa
wakimiminika kama kumbikumbi katika maeneo mengi yaliyo na vivutio.
watalii wakinunua bidhaa za kienyeji mjini Nairobi.
Vivutio hivi ni mbuga za wanyama, maumbile ya kuvutia kama milima, kanda
za pwani ambako watalii wanaweza kukoga na kufurahia jua, mandhari ya
kuvutia na hata utamaduni wa jamii mbalimbali. Mataifa mengi ya Afrika
yametunukiwa bahati ya kuwa na vivutio vingi ambavyo vinawavutia watalii
kutoka nchi zilizoendelea kuja barani. Pili, bara letu hili linajumlisha jamii
94
95
mbalimbali ambazo zina tamaduni mbalimbali zenye utajiri mkubwa ambao
unakuwa kivutio kikubwa. Ikiwa pato linalotokana na sekta hii ya utalii
litatumiwa vyema, upo uwezekano wa nchi zinazohusika kupiga maendeleo
makubwa ya kiuchumi.
Kiwango cha kukua kwa sekta ya utalii miongoni mwa nchi zinazoendelea
kinatazamiwa kukua kwa asilimia tano kwa mwaka hadi kukia mwaka wa
2020. Hali hii inaonyesha kuwa dalili za kuboreka kwa sekta hii siku za usoni
ni nzuri. Ili kuhakikisha kuwa sekta hii inaendelea kuwa kivutio kikubwa
cha pato la nchi, pana umuhimu wa mataifa yanayohusika kuhakikisha
kuwa yanaimarisha sekta hiyo. Uimarishaji huo ni kwa kupanua soko la
utalii kwa kuwahimiza wananchi wenyewe kutembelea sehemu mbalimbali,
yaani kuhimiza utalii wa ndani kwa ndani. Njia nyingine ni kuboresha
muundo msingi kama barabara, mahoteli na maeneo yanayopendwa na
watalii wenyewe ili kuwavuta wengine zaidi. Pana haja pia ya kuhakikisha
usalama umedumishwa katika maeneo yanayotembelewa na watalii. Sekta
hii haitafanikiwa vyema pasipokuwa na juhudi za kuitangaza nchi na vivutio
vyake vya utalii ili kuwavuta watalii wengi.
Fedha zinazotokana na sekta ya utalii zinaweza kutumiwa kwa
maarubu mbalimbali. Kwa mfano, fedha za kigeni zinazopatikana zinaweza
kusaidia kupunguza mzigo wa madeni ambao unazirudisha nyuma nchi
nyingi. Fedha hizi huweza pia kutumiwa kulipia bidhaa ambazo huagizwa
kutoka nje na ambazo kwa kawaida hulipiwa kwa fedha za kigeni. Tatu,
fedha hizi huweza kutumiwa kuimarisha muundo msingi wa ndani katika
nchi inayohusika ili kuhakikisha kuwa baadhi ya matatizo kama uhaba wa
barabara za kutegemewa yameondolewa. Aidha, hutumiwa kuboresha na
kuimarisha huduma za jamii katika nyanja mbalimbali kama elimu na afya
ambazo ni muhimu kama nguzo ya taifa lolote lile.
Kati ya nchi 49 zinazojulikana kama maskini sana, nyingi ziko barani
Afrika na utalii ni moja kati ya sekta muhimu zinazoziingizia fedha za kigeni.
Licha ya faida za utalii ambazo tumeziona hapo juu, kuna matatizo
kadha yanayoweza kuhusishwa na sekta hii ya utalii. Kwa mfano, miongoni
mwa nchi nyingi zinazoendelea, sehemu kubwa ya biashara ya utalii
imetawaliwa na makampuni na waendeshaji wa nje. Kwa mfano, hoteli nyingi
na mashirika yanayohusiana na utalii humilikiwa na wawekezaji wa nje, hali
ambayo inazinyima serikali na nchi zinazohusika kipato fulani. Pili, kutokana
na kutokuwepo kwa mipango mizuri, sekta hii ya utalii haiunganishwi vizuri
na sekta nyingine kama uvuvi, kilimo, viwanda, utamaduni na burudani hali
ambayo ingeweza kuipanua sekta yenyewe.
Isitoshe, kuibuka, siku hizi, kwa milolongo ya mahoteli ya kimataifa,
usarishaji wa watalii kwa njia za barabara na usari wa anga kunatishia
na kwa kiasi kikubwa hata kuondolea mbali uwezo wa hoteli ndogo na
makampuni ya wazalendo kushiriki katika biashara hii. Hoteli hizo ndogo,
kwa mfano, hazina uwezo wa kuumudu ushindani mkubwa kutoka kwa
hoteli hizo kubwa.
Katika sehemu iliyotangulia tumeona faida zinazotokana na utalii na
mchango wake katika kukua kwa uchumi. Je, kwa upande ule mwingine,
96
97
tunaweza kusema utalii una athari zozote hasi au mbaya? Kuwepo kwa utalii
kuna athari zake katika utamaduni wa jamii inayoyazunguka maeneo ya
utalii na kwa njia hiyo kuua thamani fulani muhimu za kitamaduni. Watu
wengine wanaishia kukengeushwa kiasi cha kuuacha utamaduni wao na
kuubabia utamaduni wa kigeni au utamaduni ajinabi. Ni kweli kuwa utalii
huo unaweza kukuza kuheshimika kwa makundi madogo ndani ya jamii,
kukuza lugha, dini na imani za asili na mitindo mingine ya maisha ambayo
ingeweza kufa iwapo si kwa biashara hiyo. Lakini katika maeneo mengine,
baadhi ya wazawa wameondolewa katika maeneo yao waliyokuwa wakiishi ili
kupanua utalii kama ilivyowahi kutokea nchini Kenya katika miaka ya 1950
na miaka ya karibuni katika jiji la Pagan nchini Burma. Utalii kwa njia hii
unasababisha kudhalilisha kwa wenyeji ili kuwakidhi watalii wanaotembelea
maeneo fulani.
Maeneo mengine yanaathiriwa pia, kwa mfano, yamekuwepo
malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Sakilla huko Arusha, nchini Tanzania
kuhusu mojawapo ya mabwawa yao ya asili, ambalo limeuzwa kwa ajili
ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa kibinafsi ili kuuendeleza utalii. Suala
muhimu ni kuwa lazima mataifa yanayohusika kuhakikisha kuwa jamii zao
zinafaidika kutokana na sekta hii sio tu kwa jinsi ya kipato chenyewe bali pia
uhusiano wa jamii mbalimbali na shughuli zenyewe za utalii. Lazima ziwepo
kanuni na njia za kufuatilia kuhakikisha kuwa matatizo yanayohusishwa na
utalii, kama kuhusishwa kwa watoto kwenye ukahaba (kama ilivyo nchini
Thailand), hayatuathiri. Tukumbuke kuwa utalii una tijara lakini tusiuuze
utu wetu kwa pupa ya pesa.
Maelezo ya msamiati
aali : zuri; bora.
maarubu : malengo; madhumuni.
uhaba : upungufu; ukosefu.
kukengeusha : kubaguliwa na kutengwa kwa
kushawishika kiakili.
kuubabia : kuupapia; kuukimbilia.
utamaduni ajinabi : utamaduni wa kigeni; utamaduni wa
mbali.
pupa : tamaa.
Maswali
1. Taja vivutio vitano vya watalii humu nchini mwetu.
2. Je, utalii unawezaje kuzifaidi nchi mbalimbali?
3. Kwa nini bara la Afrika linapokea idadi kubwa ya watalii?
4. Je, ni mambo gani yanayotakiwa kufanywa ili kuiendeleza sekta ya
utalii?
5. Eleza namna fedha zinazotokana na utalii zinavyoweza kutumiwa.
6. Huku ukitoa mifano, taja athari mbaya zinazotokana na biashara ya
utalii.
96
97
7. Mwandishi ana maana gani kwa kusema kuwa ‘tusiuuze utu wetu kwa
pupa ya pesa’
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Tegua vitendawili vifuatavyo:
(a) Mlima mmoja wapandwa kuanzia juu.
(b) Mfalme katikati lakini watumishi pembeni.
(c) Hana mizizi nimemkata mara nyingi lakini haachi kukua.
(d) Alinipa ngozi nikaipika; akanipa nyama nikaila; akanipa mchuzi
nikaunywa.
(e) Anakula lakini hashibi.
(f) Kitu changu asubuhi chatembea kwa miguu minne, saa sita kwa
miguu miwili na jioni kwa miguu mitatu.
(g) Kuku wangu aliangua mayai jana, lakini si kuku wala ndege.
(h) Likitoka halirudi.
(i) Mtoto asemea pangoni.
(j) Mdogo lakini humaliza gogo.
2. Je, visasili ni nini na vina jukumu gani?
3. Taja majukumu matano makuu ya methali katika jamii.
4. Tunga sentensi mbili kwa kila jozi ya maneno yafuatayo ili kutofautisha
maana yake:
(a) saa zaa
(b) suka zuka
(c) soga shoga
(d) saba shaba
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Ni nini maana ya neno ‘momu’?
2. Huku ukitoa mifano, tofautisha kati ya momu huru na momu tegemezi.
3. Tenganisha momu katika maneno yafuatayo:
a) aliyenipigia.
b) wanaosoma.
c) nilichomletea.
d) vinavyotumiwa.
4. Ni nini maana ya neno ‘kiambishi’? Toa mifano ya kuthibitisha.
5. Huku ukitumia mifano, tofautisha kati ya kiambishi awali na kiambishi
tamati.
98
99
6. Onyesha nomino katika sentensi zifuatazo:
(a) Kenya, Uganda na Tanzania ni nchi za Afrika Mashariki.
(b) Kwa nini hukuniletea kalamu na karatasi?
(c) Jungu kuu halikosi ukoko.
(d) Humu sokoni mnauzwa malimau, mafenesi, machungwa na matufaha.
(e) Yule tajiri ana majengo mengi kule mjini.
7. Soma kifungu kifuatacho huku ukiandika heru kubwa panapofaa.
Waziri wa kusadikika alikuwa mtu mwenye haiba kubwa na uhodari
mwingi, kwa hivi aliitwa majivuno. uwaziri wake ulianza zamani sana.
Alikuwa waziri wa wafalme watatu katika nyakati mbalimbali. babu
yake mfalme anayesimuliwa aliposhika ufalme, yeye alishika uwaziri;
baba yake alipokuwa nahodha wa chombo cha serikali, yeye alikuwa
rubani wake; akaendelea katika hadhi hiyo mpaka wakati wa enzi ya
mfalme mpya. umri wake mkubwa ulizifanya nywele zake kichwani kuwa
nyeupe kama fedha. kwa haiba hii aliweza kuyavuta macho ya watu;
na kwa ufasaha wa maneno aliweza kufanyiza fungu au mwamba wa
kuyavunja maisha ya mtu yeyote kama chombo. kipawa chochote cha
mtu kama hakikuongozwa vema huweza kuwa hatari au maangamizi
kwa wengine. mtu huyu alikuwa maarufu na mashuhuri lakini alijaa
tadi na inda kama hadithi hii inavyosimulia.
(Imenukuliwa na kuandikwa upya kutoka Kusadikika na S. Robert,
uk. 1)
8. Onyesha vielezi latika sentensi zifuatazo:
b) Nilika Nakuru saa saba adhuhuri.
c) Wazee wale watachinja kondoo wawili tu.
d) Nilifanya kazi hiyo kwa bidii nyingi ajabu.
e) Kesho tutakwenda msikitini.
f) Wezi waliingia chumbani mmoja mmoja.
9. Nomino hizi zimo katika ngeli zipi?
k.m. mlango - milango (Ngeli u-i)
(a) mwizi – wezi
(b) mtaro – mitaro
(c) ulezi – malezi
(d) maji – maji
(e) kikapu – vikapu
10. Tumia vivumishi vifuatavyo kutungia sentensi:
(a) mzuri
(b) kizuri
(c) vizuri
(d) zuri
98
99
11. Kutokana na vitenzi vilivyomo mabanoni, unda nomino mwafaka ili
kukamilisha sentensi zifuatazo. Kwa mfano:
________ wa mwanasiasa huyo wametiwa mbaroni. (fuata)
Wafuasi wa mwanasiasa huyo wametiwa mbaroni.
a) _________ yule hanyoi watu vizuri. (nyoa)
b) Jengo hili lilijengwa na __________ hodari. (jenga)
c) Hapa Kenya kuna _________ wengi kutoka nchi jirani. (kimbia)
d) Baada ya safari ndefu, tulipatwa na __________ mengi. (choka)
e) Ghasia zilipotokea huko uwanjani kulitokea __________ mwingi mno.
(haribu)
f) ________ hiki hutumiwa na watoto wa shule. (vuka)
g) Mimi sipendi _________ za kigeni. (imba)
h) Huyu ni _________ gani jamani! (umba)
i) __________ chako kimeniudhi. (tenda)
j) ___________ ilikuwa ya kuogofya mno. (ota)
12. Tumia kivumishi ‘-enyewe’ kukamilisha sentensi zifuatazo:
a) Wanawake __________ watakuja kesho.
b) Manukato ____________ yananukia.
c) Chakula ____________ hakina ladha.
d) Mimi nataka mikate ____________.
e) Jiko ____________ liko wapi?
D. Kusoma
a) Eleza maana ya fani na maudhui.
b) Je, ni sehemu zipi zinazounda fani?
E. Kuandika
a) Andika insha kuhusu shule yako.
b) Jichukulie kuwa wewe ni mwalimu mkuu wa shule yako. Andika
hotuba utakayoitoa wakati wa Siku ya Wazazi.
c) Soma tena kifungu kuhusu ‘Utalii ni tunu kwa uchumi’ kisha
ukiandike upya kwa urefu usiozidi nusu ya jumla ya maneno
yaliyomo.
100
101
Sura ya Tisa
A. Ufahamu
Nchi za Afrika Mashariki na mustakabali wake
Babu aliaga dunia mwaka wa 1978 miezi miwili baada ya kuvunjika kwa
Jumuiya ya Afrika Mashariki. Zamani babu alikuwa mfanyakazi wa Shirika
la Reli na aliishi mjini Arusha nchini Tanzania kwa kipindi kirefu. Kuvunjika
kwa jumuiya hiyo kulimwumiza moyo na kumtia katika simanzi isiyokadirika.
Nakumbuka alivyoizungumzia jumuiya hiyo kwa msisimko mkubwa.
“Mjukuu wangu, jumuiya hii ni juhudi nzuri. Kidole kimoja hakivunji chawa.
Tusipoungana tutaangamia na mustakabali wa nchi zetu utakuwa mbaya,”
alisema babu.
Kila ninapoziwazia nchi zetu za Afrika Mashariki, maneno hayo ya
babu huhuika akilini. Ushirikiano mpya kati ya nchi zetu hizi utakuwa na
manufaa makubwa sana. Msingi mkubwa wa maendeleo ya nchi yoyote ile ni
uchumi. Nchi yoyote hujiendeleza kiuchumi kwa njia kadha. Njia mojawapo
ni kwa biashara inayofanyika nchini na iliyopo kati ya nchi hiyo na nchi
nyingine. Maendeleo ya hali ya kiuchumi katika nchi moja yanawawezesha
raia wake kuwa na utajiri wa kutosha wa kuiendesha biashara ya maana.
Nchi zetu za Afrika Mashariki zinategemea kilimo kwa kiasi kikubwa.
Huu ndio msingi wa msemo kuwa kilimo ni uti wa mgongo wa mataifa
yetu. Maendeleo ya kilimo na biashara yake ni msingi muhimu wa ukuaji
wa uchumi wa mataifa yetu. Njia mojawapo ya kujenga na kuendeleza
ushirikiano ni kuacha biashara ya kawaida baina ya nchi zenyewe kuendelea
pasipo kizuizi chochote. Vizuizi vya biashara vinavyoweza kuwako kati
ya mataifa ni kama sheria na kanuni zinazokataza ununuzi wa bidhaa
kutoka nchi moja hadi nyingine. Pili, inawezekana pasiwepo na sheria za
aina hiyo bali pawepo na ushuru wa forodha ambao unaifanya biashara ya
aina hii kuwa ngumu. Bidhaa zinazotoka nchi moja zinatozwa ushuru wa
forodha wa juu unaofanya bei ya bidhaa zenyewe iwe ya juu. Ushuru kama
huo unapoondolewa biashara kati ya mataifa yanayohusika inaimarika na
kuchipua kama uyoga na kuwafaidi raia wa nchi zinazohusika.
Ushirikiano kati ya mataifa yetu ya Afrika Mashariki unaweza pia
kupatikana katika kiwango cha usari wa raia wenyewe. Nchi zetu zinaweza
kuruhusu usari wa raia zake kutoka nchi moja hadi nyingine kufanya
biashara, kufanya kazi au kuendesha biashara bila ya kizuizi chochote. Hii ni
dhamira moja kuu katika malengo ya Jumuiya hii mpya ambayo viongozi wa
nchi hizi wanajitahidi kuijenga upya. Shughuli hizi zitafanikiwa ikiwa raia
wanaohusika watakuwa na uhuru wa kutumia fedha zao huko wanakokwenda.
Huu ni msingi muhimu wa kuwako kwa soko moja.
Mataifa yetu yanaweza pia kushirikiana kwa kuwa na mikakati sawa
ya kuvuta misaada au uwekezaji wa mataifa ya nje. Mataifa hayo yanaweza
100
101
kuhakikisha kuwa mipango yao ya kiuchumi haihitilaani na inahimiza
maendeleo. Hali kama hii inaweza kukiwa ikiwa nchi hizo zitakuwa na
mshikamano mkubwa kama ndugu wa toka nitoke na kwamba siasa zao
hazina tofauti kubwa. Ikiwa mataifa mawili yatafuata siasa tofauti itakuwa
vigumu sana kushirikiana kiuchumi. Mathalani, nchi inayofuata siasa ya
ujamaa haiwezi kushirikiana vizuri na nyingine inayofuata mfumo usiokuwa
wa ujamaa. Hii ilikuwa sababu kuu ya kutofautiana katika miaka ya 1970
ambako kuliishia kuleta kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Ushirikiano wa kiuchumi hauwezi kufanyika shaghalabaghala. Lazima
yawepo mapatano fulani ya kiuchumi. Leo tunaishi katika kipindi ambapo
mazungumzo kuhusu utandawazi yameshika nguvu sana. Msingi mmojawapo
wa utandawazi ni kuondolewa kwa vikwazo vya kibiashara katika mataifa
mbalimbali ili kuimarisha biashara ulimwengu mzima. Lakini uondoaji
huu lazima pia uwe na misingi fulani. Bila ya misingi hiyo nchi ambazo
hazina uchumi imara zinaweza kuathiriwa vibaya na mfoko wa ghaa wa
bidhaa rahisi ambazo zinatishia viwanda na biashara changa. Kwa njia hii
biashara changa katika mataifa yenye uchumi usio imara zitatishiwa kwa
kiasi kikubwa na hata bidhaa zao kukosa soko.
Hatua moja muhimu ambayo imepigwa na mataifa ya Afrika Mashariki
ni kuunda Bunge la Afrika Mashariki ambalo lina makao makuu mjini
Arusha, Tanzania. Bunge ni chombo muhimu katika kujadili na kupitisha
makubaliano yanayoathiri utendakazi au jinsi shughuli mbalimbali
Marais Mwai Kibaki (Kenya), Museveni (Uganda), na Mkapa (Tanzania) wakiwasili
kwenye mkutano wa kujadili mustakabali wa Afrika Mashariki.
102
103
zinavyoendeshwa. Bunge la Afrika Mashariki linaweza kupitisha sheria
ambazo zitaudhibiti utendakazi na shughuli za wenyeji wa Afrika Mashariki.
Pia linaweza kupitisha sheria zinazosawazisha na zinazodhibiti biashara na
maingiliano ya wenyeji wa nchi zetu hizi. Zipo juhudi za kuhakikisha kuwa
pana mahakama inayoshughulikia masuala ya jumuiya hii mpya. Chombo
hiki kitakuwa msingi muhimu katika kulikabili suala la usalama katika
mataifa yetu haya. Kama tujuavyo, hamna taifa linaloweza kuendelea vizuri
ikiwa usalama wake hauna uhakika. Kila mfanyabiashara na mwekezaji
anapenda kufanya biashara au kuwekeza katika mazingira mazuri.
Hivi majuzi kumekuwapo na juhudi za kuhakikisha kuwa idara muhimu
za mataifa haya kama vile polisi, majeshi na idara ya uhamiaji zinashirikiana.
Huu utakuwa msingi mzuri wa ujenzi wa jumuiya mpya ya Afrika Mashariki.
Ni matarajio yetu kuwa karibuni ushirikiano huu utaonekana katika idara
nyinginezo na kuimarisha ushirikiano huo. Mataifa mengine ya ulimwenguni
yanashirikiana katika viwango mbalimbali, kwa nini sisi tupige zohali? Ni
vyema tuitambue ile busara ya babu kuwa kidole kimoja hakivunji chawa
na kuwa mustakabali wa mataifa yetu upo katika ushirikiano wetu.
Maswali
1. Ina maana gani kusema kilimo ndio uti wa mgongo wa mataifa yetu?
2. Ushuru wa forodha huathirije biashara kati ya nchi na nchi nyingine?
3. Usari kati ya nchi moja na nyingine unawezaje kusaidia kuimarisha
uchumi wa nchi hizo?
4. Tofauti kubwa za kisiasa kati ya nchi huweza kuathiri maendeleo ya
kiuchumi kati ya nchi hizo. Hii hutokeaje?
5. Utandawazi unawezaje kuathiri biashara changa?
6. Unadhani Bunge la Afrika Mashariki litasaidiaje kuleta ushirikiano kati
ya nchi hizi?
7. Eleza maana ya maneno haya kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu kisha uyatumie kutungia sentensi:
(a) mustakabali (b) ushuru wa forodha
(c) kuchipua (d) mikakati
(e) utandawazi (f) mfoko
(g) kupiga zohali
B. Kusikiliza na kuzungumza
Hekaya
Hiki ni kitanzu au kipera kimojawapo cha utanzu wa hadithi katika fasihi
simulizi. Hekaya ni hadithi ambazo huwatumia wanyama (hasa wanyama
102
103
wajanja) ili kuonyesha sifa fulani muhimu. Hekaya hujulikana pia kama
ngano za ayari. Wanyama hawa hutumiwa kama funzo kwa binadamu
dhidi ya kudanganyika kwa urahisi au kuonyesha madhara yanayoweza
kupatikana kutokana na kudanganyika huko.
Katika hekaya za jamii zetu nyingi, mnyama anayesawiriwa kama
mjanja ni sungura. Huyu huwa mnyama mjanja au ayari anayewadanganya
na kuwapumbaza wanyama wengine wakubwa. Funzo kuu katika hekaya au
ngano za ayari ni kuonyesha jinsi mtu mkubwa anavyoweza kushindwa kiakili
na mtu mdogo sana.
Umuhimu wa hekaya
1. Hekaya huwatahadharisha watu au wasikilizaji dhidi ya kudanganyika
haraka.
2. Huonyesha tabia ya udanganyifu na jinsi inavyoweza kuwaathiri watu.
3. Kuonyesha yanayoweza kuwapata wale ambao ni wadanganyifu.
4. Huwasilisha funzo fulani kuhusu jinsi ya kupambana na hali fulani
ngumu.
Mfano wa hekaya
Sungura alivyokwepa kuliwa na simba
Wanyama wa porini waliamua siku moja kumtuma mnyama mmoja kila
siku alikoishi simba kama chakula. Siku moja ilika zamu ya sungura
kwenda huko. Sungura alikuwa mjanja sana. Alipanga mpango mzuri wa
kumwangamiza simba.
Alienda alikoishi simba muda mrefu baada ya muda wa chakula cha
simba. Alimkuta simba na hasira kubwa sana. “Kwa nini umechelewa jinsi
hii?” aliuliza kwa hasira.
“Bwana wee!” alisema sungura kwa sauti ya upole, nilichelewa kwa
sababu simba mwingine alinikimbiza. Nilitaabika sana kabla ya kupata
upenyu wa kutoroka.”
“Simba mwingine? Je, katika pori hili?” aliuliza simba
“Ndiyo, Bwana Mkubwa. Najua anakoishi. Tuandamane nikakuonyeshe,”
alisema sungura.
Simba alijitayarisha kuandamana na sungura. Sungura aliongoza njia
hadi walipoka mahali palipokuwa na kisima kikubwa. Sungura alimgeukia
na kusema, “Anaishi hapa. Tafadhali njoo umwone!”
Simba alisogea ulipokuwa ukingo wa kile kisima. Aliyatupa macho huko
chini na kukiona kivuli chake. Alidhani kuwa huyo alikuwa simba mwingine.
Kwa hasira kubwa alifungua kinywa na kunguruma. Alimwona huyo simba
mwingine akimkenulia meno. Simba hakuweza kusubiri, alijitosa kisimani
apambane na simba huyo. Huo ulikuwa mwisho wake. Sungura aliondoka
akicheka akifurahi kuwa sasa wanyama hawataliwa tena na simba.
104
105
Zoezi
1. Hekaya ni nini? Je, zina umuhimu gani?
2. Je, kwa nini Simba alimkasirikia Sungura? Je, Simba alifanya nini
hatimaye?
3. Je, unajifunza nini kutokana na hekaya hii?
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Vivumishi
(i) Vivumishi vya majina
Hizi ni nomino ambazo hutumika kama vivumishi. Tazama sentensi
hizi:
(a) Mzee ameka.
(b) Maskini atapewa msaada.
(c) Shujaa atatunukiwa zawadi.
Maneno mzee, maskini na shujaa ni nomino. Lakini nomino hizi huweza
kugeuka na kuwa vivumishi ikiwa zitatumika kutoa sifa za nomino. Kwa
mfano:
(a) Mkulima mzee atasaidiwa na wanafunzi.
(b) Msichana maskini anasoma.
(c) Kijana shujaa amepongezwa na watu wote.
(ii) Vivumishi vya ‘-a’ unganifu
Hivi ni vivumishi vinavyoundwa kwa ‘-a’ unganifu na hutumika
kutoa sifa za nomino. Kwa mfano:
(a) Mke wa Hamisi amekwenda sokoni.
(b) Nyumba ya mwalimu imeharibiwa na upepo mkali.
(c) Nguo za mtoto zimechomeka.
(d) Matunda ya nyanya yamechukuliwa na nani?
(e) Duka la Alikiona hufunguliwa alfajiri.
Zoezi
1. Onyesha vivumishi vya majina katika sentensi zifuatazo:
(i) Msichana mrembo ameozwa kwa mvulana yule.
(ii) Mtoto bubu amelazwa hospitalini.
(iii) Mchezaji mzee ameshinda mchezo huo.
(iv) Mwindaji shujaa amewanasa wanyama wengi.
(v) Mwanamke tajiri atawatembelea watoto mayatima.
104
105
2. Onyesha vivumishi vya ‘-a’ unganifu katika sentensi zifuatazo:
(i) Mwanafunzi wa kwanza alipewa zawadi.
(ii) Duka la shangazi hufunguliwa asubuhi.
(iii) Majangili waliwavamia wakazi wa Nyamira.
(iv) Wanyama wa kufugwa wana faida nyingi.
(v) Wavulana wa kwetu huoa mapema.
2. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi -ingine (Ngeli i/zi–
pa/ku/mu)
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
-ingine
i sabuni nyingine Sabuni nyingine imenunuliwa.
zi sabuni nyingine Sabuni nyingine zimenunuliwa.
u uzembe mwingine Uzembe mwingine unaudhi.
u uzembe mwingine Uzembe mwingine unaudhi.
u uso mwingine Uso mwingine umepakwa mafuta.
zi nyuso nyingine Nyuso nyingine zimepakwa mafuta.
ku kulala kwingine Kulala kwingine kunaleta hasara.
ku kulala kwingine Kulala kwingine kunaleta hasara.
pa mahali pengine Mahali pengine pamechomwa.
ku mahali kwingine Mahali kwingine kumechomwa.
mu mahali mwingine Mahali mwingine mmechomwa.
zi fedha nyingine Fedha nyingine zimeibwa.
li jua lenyewe Joto jingine linaongezeka.
ki kiu kingine Kiu kingine kimezuka (kimeanza).
vi vijo vingine Vijo vingine vimesikika asubuhi.
Zoezi
Badala ya nomino iliyoandikwa kwa mkolezo tumia ile iliyomo mabanoni.
k.m. Kiatu kingine kimeraruka. (nguo)
Nguo nyingine imeraruka.
1. Vyakula vingine vimepikwa. (chakula)
2. Kisu kingine kitamkata. (wembe)
3. Mahali pengine patafagiliwa.(ukumbi)
4. Kutembea kwingine kumeanza. (uchoyo)
5. Mahali kwingine kunaudhi. (udaku)
6. Sahani nyingine imeletwa. (udongo)
7. Uzi mwingine utatumiwa. (mahali)
8. Fito zingine zimeletwa. (uto)
9. Nyumba nyingine imeuzwa. (uzi)
10. Ndoo nyingine imeanguka. (ukuta)
106
107
3. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi ‘-ote (Ngeli a/wa
ki/vi)
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
‘-ote’
a ngamia
wa ngamia wote Ngamia wote wamechunwa ngozi.
u mtaro wote Mtaro wote umejaa maji.
i mitaro yote Mitaro yote imejaa maji.
u upana wote Upana wote utafaa.
ya mapana yote Mapana yote yatafaa.
ya maziwa yote Maziwa yote yamenywewa.
ya maziwa yote Maziwa yote yamenywewa.
ki kisa chote Kisa chote kilisisimua.
vi visa vyote Visa vyote vilisisimua.
zi fedha zote Fedha zote zimefujwa.
ki kiharusi chote Kiharusi chote kilitibiwa.
li joto lote Joto lote limepungua.
Zoezi
1. Tumia kivumishi ‘-ote’ katika umoja na wingi kukamilisha sentensi
zifuatazo:
K.m. Chakula _______ kimeliwa.
Vyakula _______ vimeliwa.
Chakula chote kimeliwa.
Vyakula vyote vimeliwa
(a) Mkufu _______ unametameta.
Mikufu _______ inametameta.
(b) Ulezi _______ ulimfaa.
Malezi _______ yalimfaa.
(c) Nyoka _______ amebambuka ngozi.
Nyoka _______ wamebambuka ngozi.
(d) Kiatu _______ kinang’aa.
Viatu _______ vinang’aa.
(e) Msitu _______ umejaa kima.
Misitu _______ imejaa kima.
(f) Majira _______ yatakuwa baridi.
Majira _______ yatakuwa baridi.
(g) Mkate _______ una zabibu.
Mikate _______ ina zabibu.
(h) Maji _______ yatachemshwa.
Maji _______ yatachemshwa.
106
107
2. Andika sentensi zifuatazo katika umoja.
(a) Visima vyote vimejaa maji.
(b) Manukato yote yatauzwa.
(c) Vyakula vyote vimetayarishwa.
(d) Mifupa yote imevunjika.
(e) Mayai yote yatakaangwa.
(f) Matawi yote yananing’inia.
(g) Miaka yote ilikwisha.
(h) Miavuli yote imefunguliwa.
(i) Malezi yote yanapendeza.
(j) Matunda yote ni mabivu.
D. Kusoma
Matumizi mengine ya kamusi
Katika sura ya pili, tuliona baadhi ya matumizi na sifa za kamusi. Kamusi ni
muhimu sana kwa kila mwanafunzi anayejifundisha lugha. Kamusi inaweza
kumsaidia mwanafunzi kuupanua msamiati wake kwa kuyajua maneno
mengine ambayo yana maana sawa na neno analolichunguza. Maneno haya
hujulikana kama visawe. Sifa hii tunaiona katika kamusi ya kawaida, kwa
mfano, Kamusi ya Kiswahili Sanifu, na pia kamusi maalum kama, Kamusi
ya Visawe.
Pili, kamusi, hasa ya Kiswahili Sanifu, huonyesha mnyambuliko wa
vitenzi vya lugha ya Kiswahili na kumwezesha msomaji kuyafahamu maneno
mbalimbali. Lugha ya Kiswahili hutumia viambishi mbalimbali kuonyesha
hali (na maana) mbalimbali za vitenzi kama hali ya kufanyia, kufanyiwa
n.k. Tuangalie mifano ifuatayo:
a) pig.a : ~ ia = pigia (fanyia) ~ ika = pigika (fanyika) ~ isha
=pigisha (fanyisha) ~ wa = pigiwa (fanyiwa) ~ ana =
pigana(fanyana)
b) rush.a : ~ ia= rushia, ~ ika= rushika, ~ iwa =rushiwa, ~ ana=
rushana
c) bwag.a : ~ ia= bwagia, ~ ika=bwagika, ~ iza= bwagiza, ~wa=
bwagwa, ~ ana= bwagana.
Ukiangalia neno ‘piga’ katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu, utaona pana
kituo kati ya pig na a, hiyo ‘pig’ ndiyo sehemu ya neno ambayo haibadiliki na
inajitokeza katika maneno kama pigia, pigika, pigisha, pigiwa na pigiana.
Katika kamusi, alama ~ hutumiwa badala ya kurudiarudia mzizi wa kila
kitenzi.
Basi kwa kutumia kamusi, unaweza kujizoeza na kujifundisha
minyambuliko ya vitenzi vya Kiswahili. Kwa njia hii unauendeleza ujuzi
wako wa saru ya Kiswahili.
108
109
Maswali ya marudio
1) Je, visawe ni nini na vinahusianaje na kamusi?
2) Je, kamusi inatusaidia vipi kuhusu vitenzi vya lugha ya Kiswahili?
E. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Matangazo
Matangazo ni maneno yanayotolewa kwa maandishi au kwa sauti kwa lengo la
kuwasilisha ujumbe fulani kwa mkato na kwa njia inayoeleweka mara moja.
Aina za matangazo
Kuna aina mbalimbali za matangazo. Baadhi ni:
(a) Matangazo ya kibiashara ya kuwajulisha wateja kuhusu bidhaa fulani
inayopatikana sokoni, kwa mfano, sabuni mpya, kitabu kipya n.k.
(b) Matangazo ya kuwafahamisha watu hali iliyoko mahali fulani, kwa
mfano, kuhusu ujenzi unaoendelea, barabara iliyofungwa, mnada
unaofanyika n.k., kuelekeza, kwa mfano, jinsi ya kufanya jambo
fulani, kwa mfano, uendeshaji wa magari mahali au wakati fulani
n.k. nafasi za kazi, mikutano n.k.
(c) Matangazo ya tanzia au misiba.
(d) Matangazo ya kutahadharisha, kwa mfano, kuwa pana hatari fulani
n.k.
Sifa za Matangazo
Matangazo huwa na sifa kadha. Kwa mfano:
(a) Hutumia lugha kwa kifupi lakini inayovutia. Lugha hii hutegemea
aina ya tangazo na chombo kinachotumika kuwasilisha tangazo
linalohusika, iwapo ni redio, runinga, mabango, gazeti n.k.
(b) Matangazo mengi huongezwa picha au michoro ili kurahisisha
mawasiliano na kuibua msisimko.
(c) Katika runinga matangazo huambatanishwa na maigizo, michoro na
nyimbo za kuvutia.
(d) Huwa na lugha iliyotiwa chumvi ili inate na kuteka akili za walengwa.
Siku hizi kwa kutumia tarakilishi, matangazo huweza kuongezewa
madoido na kuyafanya yawe ya kupendeza na kuvutia sana.
(e) Matangazo mengi huandikwa kwa herufi kubwa, kwa rangi
zinazovutia macho au kwa heru nzito ili yaweze kuvuta makini ya
walengwa.
(f) Huweza pia kutumia maswali mafupi kama: lini? wapi? vipi? nani?
ili kumchagiza mlengwa.
108
109
Mifano:
KAA CHONJO!
VITA VYA TATU VYA DUNIA VIMEANZA!
DAWA MPYA YA ‘VITA VYA TATU’ IMEANZISHA VITA
VYA TATU VYA DUNIA DHIDI YA MENDE, KUNGUNI,
VIROBOTO, MBU NA MAADUI WENGINE WA
BINADAMU WANAOTAMBAA. ANGAMIZA MAADUI
ZAKO KWA ‘VITA VYA TATU’! KWAHERI KUNGUNI!
Zoezi
Kazi ya kundi
(a) Shirikiana na wenzio katika kundi kuandaa matangazo angalau mawili.
(b) Jitahidi kuzuka na tangazo lako mwenyewe.
Maswali
1. Kwa nini matangazo ni muhimu?
2. Je, ni sifa zipi zinazohusishwa na matangazo?
VITA
VYA
TATU
110
111
Sura ya Kumi
A. Ufahamu
Kibwana Jaku na nundu ya maisha
Maisha ya Kibwana Jaku yalibadilika alipoteuliwa kuwa mkurugenzi wa
shirika moja la umma. Kabla ya uteuzi huu, Kibwana Jaku alikuwa asa wa
masjala kuu ya shirika hilo lakini alipata uteuzi huo kutokana na uhusiano
wake na waziri aliyehusika. Ilidaiwa kuwa alikuwa na nasaba fulani na
waziri aliyependekeza apandishwe cheo kazini. Mkurugenzi aliyemtangulia
alitimuliwa na muda si muda akakishwa mahakamani kwa hatia ya
kughushi.
Kwa Kibwana Jaku, cheo hiki kilikuwa na maana moja tu: damu
nzito kuliko maji. Kwa muda mrefu alikuwa amemwomba jamaa yake huyo
amwazie wakati wa ugawaji wa vyeo. “Ndugu, unajua maisha katika nchi
hii ni vuta n’kuvute kati ya makabila mbalimbali,” waziri huyo alimwambia
siku moja. Kibwana Jaku aliitikia kwa kichwa kukubaliana na busara hiyo
kubwa. Baada ya muda waziri akaendelea, “Siku hizi ni kama tunawamba
ngoma. Na kila mwamba ngoma huvuta kwake,” aliongeza waziri kwa ujuzi
wa mtu anayejua alifanyalo. Miezi kadha baada ya maneno hayo, Kibwana
Jaku alipandishwa ngazi na kuwa mkurugenzi. Sasa hakuwa tena yule
‘kijana’ wa masjala bali ‘mzee’ hata kwa wafanyakazi waliompiku umri.
Kupanda kwa Kibwana Jaku kuliwatia wafanyakazi wa ngazi ya chini
moyo. Walidhani madhali mwenzao kapanda ngazi, sasa walikuwa na fursa
ya kutendewa haki. Alifanya kazi ya sulubu kama wao kwa hiyo aliweza
kutambua umuhimu wa kuwaauni wenzake. Kwa wakubwa, kuteuliwa kwa
Kibwana Jaku kulikuwa na maana moja tu: jamii haikuthamini tena uzoefu
wala maarifa ya kazi. Sasa aliwasimamia watu waliomzidi kwa uzoefu wa
kikazi pamoja na hitimu. Baadhi yao walikereka na kuamua kuiacha kazi
hiyo; heri kujiondokea kuliko fedheha ya kusimamiwa na jamaa kama
Kibwana Jaku.
Kibwana Jaku alifurahi upeo wa furaha kwa kuipata fursa ya kujipiga
msasa kimaisha. “Sasa nimekia nundu ya maisha!” alimwambia mfanya-
kazi mwenzake siku alipoyachukua madaraka yake mapya kwa mbwembwe
nyingi. Muda si muda, maisha yake yalianza kubadilika. Alitoka mtaa wa
Madongoporomoka na kuhamia mtaa wa Shahamu walikoishi watu wa kufu
yake. Baiskeli yake ya zamani kutoka Uchina ilipotea na wala hakuikumbuka.
Sasa alitembea kwenye magari mazito ya shirika yaliyokuwa na vioo vya rangi
ili kumzuia asikerwe na jua la mjini. Asubuhi hakula kiporo cha ugali tena
bali alitafuna vimanda vya mayai, soseji na kunywa maziwa. Kitumbo chake
kilichokuwa kimejizika kwenye mgongo wake kilifumuka na kuchungulia
mbele. Maisha yake ya sasa yalibaidika na ya zamani kama ardhi na mbingu.
Waziri naye hakusahau fadhila kubwa aliyomtendea mpwa wake.
Alimkumbusha maana ya methali kuwa viganja vya mikono huoshana na
110
111
kwamba alipaswa kuonyesha shukrani zake. Kibwana Jaku hakusahau
hilo. Aliamua kuonyesha shukrani zake kwa kuhakikisha kuwa shirika
sasa lilibadilisha benki yake. Akaunti iliyokuwako kwenye Benki ya Taifa
na Biashara ilihamishiwa kwenye benki iliyomilikiwa na waziri huyo. Pili,
alihakikisha kuwa amebadilisha kampuni ya bima ya shirika hadi kwenye
nyingine ya waziri huyo. Mkuu wa Masuala ya Fedha katika kampuni
alimshauri asifanye hivyo kwa kumwambia, “Bwana Mkurugenzi, kuna
hatari ya kuhamishia fedha za shirika kwenye benki ambazo hazina misingi
mizuri. Shirika linaweza kupata hasara kubwa sana.”
Aliposikia maneno hayo Mkurugenzi Jaku alipandwa na za kwao.
“Unadhani unajua sana ehh? Basi kwa nini hukupewa ukurugenzi wewe?
Mimi ndiye Mkurugenzi hapa; na nimekwisha kuamua. Ukitaka maamuzi
mengine itabidi usubiri mpaka zamu yako ike,” aligomba huku akikodoa
macho pima. Yule jamaa alipoona jinsi hali ilivyokuwa aliamua kujinyamazia
lakini akaamua kufanya uchunguzi wake chini kwa chini. Wenzake walikuwa
tayari kumsaidia kwa kuhofu kuona pesa za shirika lililojitegemea kama lile
zikifujwa ovyo ovyo. Naye Kibwana Jaku aliendelea kuifurahia nundu ya
maisha pamoja na mfadhili wake mkuu.
Hali ilibadilika mara tu ile benki ilipoanza kulisika. Haikuchukua
muda kabla ya benki yenyewe kufungwa. Muda mfupi baadaye, shirika la
bima nalo lilifungwa na waziri aliyehusika akahama nchini kisiri. Umma
ulikuja juu ukilalamika kwa uwezekano wa shirika lile kupoteza fedha
kiasi kile. Kibwana Jaku alishikwa na hofu kubwa mpaka kitambi chake
kikaanza kumtetemeka. Serikali iliiteua tume ya kuchunguza chanzo cha
hali iliyolikumba shirika lile pamoja na shughuli zote zilizokuwa zikitendeka.
112
113
Wale wafanyakazi waliokuwa wakifuatilia shughuli za pale walijitolea sabili
kuisaidia tume hiyo katika uchunguzi wao. Wakati huo huo Mkurugenzi
Jaku alisimamishwa kazi.
Matokeo ya uchunguzi yalibainisha maovu yote yaliyokuwa
yametendeka. Kibwana Jaku alipelekwa mahakamani kwa kosa la ufujaji wa
mali ya umma. Serikali iliomba msaada wa Shirika la Polisi la Ulimwengu,
INTERPOL, kusaidia kumsaka waziri aliyepotelea nchi za nje. Haikuchukua
muda kabla naye kutiwa mbaroni. Wakakishwa mahakamani na kushtakiwa
kwa wizi wa mali ya umma. Mfanyakazi mmoja aliyemwona Kibwana Jaku
akitoka mahakamani alipaaza sauti, “Ndugu Mkurugenzi, unafurahia nundu
ya maisha?” Kibwana Jaku aligeuza macho kumwangalia huku akijuta majuto
ya mjukuu. Wote waliishia kifungo cha miaka tisa gerezani.
Maelezo ya msamiati
masjala : idara inayoshughulika na upokezi na
kurekodi barua, faili n.k.
nasaba : jadi; uhusiano wa ukoo.
madhali : kwa sababu.
kughushi : kudanganya; kutumia mamlaka vibaya.
waliompiku : waliomzidi; waliompita.
kuwaauni : kuwasaidia; kuwanusuru.
hitimu : elimu au mafunzo muhimu kwa kazi
fulani.
kiporo : chakula kilicholala hadi asubuhi;
mwiku au uporo.
vimanda vya mayai : mkate wa mayai.
yalibaidika : yalijitenga; yalikuwa mbali na.
Maswali
1. Kabla ya kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa shirika la umma, Kibwana
Jaku alifanya kazi gani?
2. Ni kwa nini Kibwana Jaku aliamini kuwa cheo chake kipya kilimaanisha
kuwa damu ni nzito kuliko maji?
3. Yule waziri aliyemteua Kibwana Jaku kuwa mkurugenzi alifaidikaje
kutokana na uteuzi huo?
4. Ni kwa nini uteuzi huu uliwapa moyo wafanyakazi wa ngazi za chini?
5. Kibwana Jaku alimaanisha nini aliposema amekia nundu ya maisha?
6. Eleza jinsi maisha ya Kibwana Jaku yalivyobadilika baada ya kupata
cheo kipya.
7. Ni kwa nini Mkuu wa Masuala ya Fedha alifarakana na Kibwana Jaku?
Ni nini kilichotendeka baada ya Kibwana Jaku kukataa ushauri wa Mkuu
wa Masuala ya Fedha?
112
113
8. Eleza maana ya methali hizi kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu:
(a) Damu nzito kuliko maji.
(b) Kila mwamba ngoma huvutia kwake.
(c) Viganja vya mkono huoshana.
9. Eleza maana ya misemo ifuatayo kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu:
(a) kazi za sulubu.
(b) kupiga msasa.
(c) jitolea sabili.
(d) kodoa macho pima.
(e) watu wa kufu yake.
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Ushairi
Huu ni utanzu mmojawapo wa tanzu za fasihi simulizi; nyingine ni semi,
hadithi na maigizo. Tofauti kuu kati ya utanzu huu katika fasihi simulizi
na ulivyo katika fasihi andishi ni kuwa katika fasihi simulizi ushairi
unahusisha mapigo fulani ya kimuziki, mpangilio maalum wa maneno, na
utendaji, yaani kuwasilishwa mbele ya hadhira fulani; iwe jukwaani au la.
Tungo zinazohusishwa na ushairi wa fasihi simulizi huweza kubadilika kila
mara kwa kuwa mara nyingi hutegemea uwezo wa mtendaji wa kukumbuka.
Isitoshe, sifa moja kuu ya fasihi simulizi ni kuundwa upya kila mara tungo
zinapowasilishwa mbele ya hadhira. Ushairi una vipera vingine kama
mashairi, ngonjera, utenzi na nyimbo. Ushairi hutumiwa kuelezea tungo
nyingi ambazo hutumia mapigo maalum ya sauti.
nyimbo maghani ngonjera mashairi
ushairi
Sifa za ushairi wa fasihi simulizi
1. Huwa na mpangilio maalum wa maneno yake.
2. Huwa na mapigo ya kimuziki.
3. Huwa na uteuzi maalum wa msamiati au maneno.
4. Huwa na mwimbaji au waimbaji wanaoimba kwa sauti au wanaokariri
kwa sauti.
114
115
5. Huwa na watu wanaosikiliza uimbaji huo au kukaririwa huko, yaani
lazima pawepo na hadhira.
6. Huenda na shughuli au tukio fulani maalum na ambalo hujitokeza hata
katika uteuzi wake wa msamiati. Kwa mfano, kumbembeleza mtoto,
ushujaa, mazishi n.k.
Kipera cha nyimbo
Hizi ni tungo ambazo huwa na mahadhi ya kupanda na kushuka. Nyimbo
huundwa kwa lugha ya mkato, huwa na mapigo ya kisilabi na hutumia lugha
yenye uwezo wa kuleta picha akilini. Msingi mkubwa wa nyimbo ni kuwako
kwa sauti. Nyimbo hutumiwa kwa sababu mbalimbali:
1. Kutumbuiza.
2. Kuliwaza, kwa mfano, nyimbo za maafa.
3. Kumbembeleza mtoto alale.
4. Kuwahimiza watu wakiwa kazini, kwa mfano, nyimbo za kazi.
Katika jamii zetu, nyimbo huambatana na kila aina ya shughuli tunazofanya.
Nyimbo hutambulishwa na sifa kadha kama:
1. Watu wanaoimbiwa wimbo fulani; yaani hadhira.
2. Maneno au kifungu cha maneno yanayoimbwa.
3. Muziki wa vyombo au ala ikiwa zipo.
4. Sauti ya anayeimba wimbo fulani.
Nyimbo huambatana na shughuli nyingi za maisha yetu. Kutokana na sifa
hii tunapata aina nyingi za nyimbo kutokana na shughuli hizo mbalimbali.
Aina hizo ni kama:
(a) Bembelezi – yaani nyimbo zinazoimbwa kumbembeleza mtoto alale.
(b) Nyimbo za taifa nyimbo zinazoimbwa na watu wa taifa moja
kuonyesha mapenzi yao kwa nchi yao na uzalendo wao.
(c) Nyimbo za kazi Huandamana na kazi wanazofanya watu iwe kulima,
kupalilia, kuvuna au shughuli yoyote ile inayohusisha kutenda kazi.
(d) Nyimbo za tohara/nyiso Huandamana na shughuli za tohara katika
jamii ambazo zina sherehe hii ya kitamaduni. Huhusishwa na sherehe
za jando na unyago
(e) Nyimbo za siasa Nyimbo ambazo zinashughulika na masuala ya
kisiasa au zinazozungumzia mambo yanayohusiana na siasa.
(f) Tumbuizo Nyimbo ambazo huimbwa ili kuwafurahisha watu katika
matukio au sherehe mbalimbali na tofauti kama vile kwenye ngoma
au kwenye harusi.
(g) Mbolezi – Nyimbo za kilio na maombolezo
114
115
Zoezi
1) Je, ni sifa zipi kuu zinazohusishwa na utanzu wa ushairi katika fasihi
simulizi?
2) Toa mfano wa wimbo unaopatikana katika jamii yako na ueleze jukumu
lake.
2. Matamshi bora: vitate b/mb
Tamka maneno haya.
b mb
basi mbasi
buni mbuni
bali mbali
bega mbega
Soma: Vitanza ndimi
1. Nilipanda basi kuelekea Bassi anakoishi mbasi wangu, na basi lilipoka
Bassi nikamkuta mbasi wangu tayari ameka kunipokea.
2. Mbunda alibuni mbinu bora ya kumnasa mbuni kwani alijua mbuni ni
ndege mbunifu na asipobuni mbinu maalum hawezi kamwe kumnasa
mbuni.
3. Ukitaka kuwaona bata bukini wengi nenda mbali huko Bukini bali sio
hapa karibu ambako hakuna bata bukini wengi.
4. Nilipomshika mbega nilimfunga kwa kamba nikamweka begani.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Vivumishi
(i) Vivumishi vya kurejesha
Hivi ni vivumishi vinavyotumika kurejelea nomino. Hujengwa kwa kutumia
‘O-rejeshi’. Kwa mfano:
(a) Kondoo huyo alikuwa mnono sana.
(b) Kiti hicho kilipotea zamani.
(c) Shule hiyo itaanza kujengwa mwaka ujao.
(d) Duka hilo lilibomolewa na upepo wiki iliyopita.
(e) Mtu huyo alikufa zamani sana.
Zoezi
Onyesha kivumishi cha kurejesha katika sentensi zifuatazo:
1. Kichaka hicho kilikuwa kimejaa miti ya kiasili.
2. Nilikataa kabisa kutembelea nchi hiyo.
3. Kijiji hicho kilivamiwa na kundi la majangili.
116
117
4. Wazee hao wataka lini?
5. Kitanda hicho kilikuwa kimejaa kunguni.
(ii) Vivumishi vya kusisitiza
Hivi hutumiwa kusisitiza nomino iliyotajwa hapo awali. Kwa mfano:
(a) Kitabu kiki hiki ndicho kilichotumiwa na dadangu.
(b) Gari lili hili ndilo tutakalosaria.
(c) Sisi tutalala chumbani mumu humu.
(d) Wachezaji wawa hawa ndio watakaocheza mchezo huo.
(e) Kusoma kuku huku ndiko kunakosaidia.
Zoezi
Chagua kivumishi mwafaka cha kusisitiza ili kukamilisha sentensi zifuatazo:
kuku huku, lili hili, wawa hawa, kiki hiki, papa hapa, uu huu.
(a) Kiatu __________ ndicho kilichoshonwa wiki iliyopita.
(b) Pahali __________ ndipo palipofunguliwa asubuhi.
(a) Duka __________ ndilo lililovunjwa juzi usiku.
(b) Mjomba wangu hupenda kucheza mchezo __________.
(c) Wanyama __________ ndio waliokula maharagwe yangu.
(d) Kucheza __________ ndiko kulimpoteza Joseph Juma.
2. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi ‘-ote’
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
-ote
i safari yote Safari yote ilikuwa ya kupendeza.
zi safari zote Safari zote zilikuwa za kupendeza.
u ukulima wote Ukulima wote ulileta manufaa.
u ukulima wote Ukulima wote ulileta manufaa.
u utambi wote Utambi wote umekwisha.
zi tambi zote Tambi zote zimekwisha.
ku kuomba kote Kuomba kote kulisaidia.
ku kuomba kote Kuomba kote kulisaidia.
pa mahali pote Mahali pote pamejaa.
ku mahali kote Mahali kote kumejaa.
mu mahali mote Mahali mote mmejaa.
zi fedha zote Fedha zote zimepatikana.
ki kiherehere chote Kiherehere chote kimeisha.
li joto lote Joto lote limepungua.
vi visuguru vyote Visuguru vyote vimeuzwa.
116
117
1. Sahihisha kivumishi kilichoandikwa vibaya katika sentensi zifuatazo:
(a) Ngoma zote imepasuka.
Ngoma yote zimepasuka.
(b) Wema yote utasaidia.
Wema zote utasaidia.
(c) Pahali pote kulijaa maji.
Mahali mote palijaa maji.
(d) Njia zote inateleza.
Njia yote zinateleza.
(e) Uso yote umeparara.
Nyuso yote zimeparara.
2. Badala ya nomino iliyoandikwa kwa heru nzito, tumia ile iliyomo
mabanoni.
(a) Bandari yote imejaa. (ukumbi)
(b) Kukimbia kote kulisaidia. (wema)
(c) Umande wote umekwisha. (chakula)
(d) Mahali pote patafagiliwa. (nyumba)
(e) Wimbo wote ulipendeza. (nyimbo)
(f) Nyufa zote zitatengenezwa. (ukuta)
(g) Kulima kote kulifaa. (uto)
3. Nyakati
Ukanushaji wa wakati ujao kulingana na nafsi
Umoja Wingi
Nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nitatazama sitatazama tutatazama hatutatazama
nitacheka sitacheka tutacheka hatutacheka
nitaezeka sitaezeka tutaezeka hatutaezeka
nitavuna sitavuna tutavuna hatutavuna
Nafsi ya pili
utatazama hutatazama mtatazama hamtatazama
utacheka hutacheka mtacheka hamtacheka
utaezeka hutaezeka mtaezeka hamtaezeka
utavuna hutavuna mtavuna hamtavuna
Nafsi ya tatu
atatazama hatatazama watatazama hawatatazama
atacheka hatacheka watacheka hawatacheka
ataezeka hataezeka wataezeka hawataezeka
atavuna hatavuna watavuna hawatavuna
118
119
Zoezi
Kanusha sentensi zifuatazo.
(a) Mtoto atasimama wima.
(b) Mhunzi atakaa hapa.
(c) Mjomba atauza baiskeli yake.
(d) Baba yangu atasari kesho.
(e) Wachezaji watafurahi sana.
(f) Mwanafunzi huyu atavuta mkia.
(g) Dereva yule atasukuma gari hili.
(h) Mimi nitashuka kutoka kwenye basi.
(i) Waziri ataongea na wakulima.
(j) Anyango atakula wali.
D. Kusoma
Majarida
Katika kidato cha kwanza tuliona kuwa jarida ni chapisho ambalo hutolewa
baada ya kipindi fulani na huwa na sura ya kitabu. Jarida huwa na habari
mbalimbali ambazo huwasilishwa kwa makala mbalimbali kwenye jarida.
Kuna majarida ya aina mbalimbali kama: majarida ya lugha, majarida
ya habari, majarida ya burudani, majarida ya uchumi, majarida ya afya,
majarida ya biashara, majarida ya kidini, majarida ya magari n.k.
Umuhimu wa majarida
1. Hutusaidia kupata maarifa mbalimbali kuhusiana na mambo tofauti
tofauti.
2. Hutufahamisha mambo yanayohusiana na uwanja maalum; kwa mfano,
lugha, biashara n.k.
3. Huongeza maarifa yetu tunayoyapata kutoka usomaji wetu.
4. Hutuzoeza jinsi ya kuelezea mambo kwa ukamilifu fulani.
5. Hutuzoeza jinsi ya kuandika makala kuhusu masuala mbalimbali na
kwa njia ifaayo.
6. Hututanguliza kwenye njia na stadi za utati ambazo zinatusaidia katika
usomaji wetu.
7. Hutujulisha kwa kina mambo yanayotokea katika ulimwengu wetu
kuhusiana na siasa, utamaduni, uchumi, burudani n.k.
Maswali ya marudio
1) Toa mifano miwili ya majarida unayoyafahamu.
2) Je, kwa nini ni muhimu kusoma majarida?
118
119
E. Kuandika
Tahadhari: ilani/ Onyo
Tahadhari ni maneno yanayotoa hadhari au maonyo kwa msomaji, mtazamaji
au msikilizaji ili kumwepusha na majanga au hatari fulani. Tahadhari
hutumiwa wakati mwingine kwa maana sawa na onyo ingawa inawezekana
pia ikaeleza habari fulani tu za kumkumbusha au kumgutusha anayehusika.
Katika maisha yetu ya kila siku, tunakumbana na tahadhari za aina
mbalimbali. Hutokea katika mikebe, chupa au vijikaratasi vinavyofunga
dawa, mikebe na chupa za vyakula, maeneo ya shuleni au hospitalini,
barabarani n.k. Pia tahadhari huweza kupatikana katika vyumba mbalimbali
kutoa maonyo kuhusu uvutaji wa sigara, kutotumia simu ya mkono (hasa
kwenye benki) n.k.
Tahadhari huweza kutokea kwa maandishi au kwa sauti. Kwa
kawaida huwekwa mahali ambapo inaweza kusomeka na kueleweka haraka.
Tahadhari hutolewa kwa maneno machache lakini yenye mvuto na uwezo
mkubwa wa kuwahamasisha wanaohusika ili kuwasilisha mara moja ujumbe
uliodhamiriwa. Maandishi ya tahadhari huandikwa kwa heru zinazoweza
kuvutia macho na kusomeka kwa urahisi. Kwa hivyo, aghalabu huandikwa
kwa heru kubwa. Iwapo ni kwa heru ndogo, heru hizi mara nyingi huwa
nzito na za rangi zinazoonyesha hatari hasa nyekundu inayochukuliwa kuwa
rangi ya hatari. Siku hizi kutokana na maendeleo ya teknolojia hasa kupitia
tarakilishi, maandishi na hata michoro huweza kuongezewa madoido mengine
ili yawasilishe ujumbe vizuri zaidi. Pia, tahadhari huweza kutumia alama za
kuakisha zinazoibua hisia za moyoni hasa alama ya hisi (!), swali (?), mtajo
(“ ”), nukta mbili (:) na kupigia mstari (____). Tazama mifano ya tahadhari
ifuatayo na utaje umuhimu wake pamoja na pale inapoweza kupatikana.
(i)
TAHADHARI!
DARAJA HILI LINA KASORO.
TAFADHALI USILITUMIE!
120
121
(iii)
(ii)
(iv)
HATARI!
UA WA UMEME
ONYO
USISIMAME WALA KUEGESHA
GARI KWENYE ENEO HILI!
(v)
ILANI
BARABARA IMEFUNGWA
KWA MUDA
(vi)
CHUNGA!
WANYAMAPORI
Zoezi
Andika mifano yako mwenyewe miwili ya tahadhari/onyo na utaje umuhimu
wa kila moja.
HATARI!
TAFADHALI USITUMIE
SIMU YA MKONO
NDANI YA BENKI.
120
121
Sura ya Kumi na Moja
A. Ufahamu
Mraha na chupa za karaha
Mraha alikuwa mtu maarufu katika mtaa wa Buraha alikoishi kutokana
na hali yake nzuri ya maisha. Alikuwa mfanyabiashara maarufu. Biashara
yenyewe lazima ilimnyookea kwa kuwa alikuwa na kipato kizuri kweli.
Kipato hicho kilimwezesha kujenga nyumba kadha za kupangisha pale
mtaani pamoja na kununua gari dogo. Ingawa gari lenyewe lilikuwa mkweche
lakini lilimfaa sana kwenye hizo shughuli zake za kibiashara. Tabia ya
Mraha mwenyewe ilipatana vizuri sana na jina lake mwenyewe; alikuwa mtu
mchangamfu na alipenda sana mizaha. Kila alipoulizwa kuhusu biashara
yake, alijibu kwa bashasha, “Ni mradi fulani; unaweza kuuita mradi bubu
tu”. Basi kila wanamtaa walipomwona akiondoka kwenye mkweche wake
wa gari wakawa wanaambizana, “Mraha huyo, anapotelea kwenye mradi
wake bubu!”
Wanamtaa waliendelea na shughuli zao za maisha bighairi ya mradi
bubu wa Mraha hadi siku moja usiku yapata majira ya saa nne hivi.
Jamaa mmoja alishtuka alipomwona mtu ameliinamia gari la Mraha huku
amezungukwa na makatoni. Wazo lililomjia ni kuwa huyo alikuwa mwizi
122
123
wa magari. Katika siku za karibuni, wizi wa magari ulikuwa umetendesa
mjini na kuwatia wenye magari kihoro kikubwa. Basi jamaa yule aliamua
kumnyatia mwizi huyo polepole huku akihakikisha kuwa haonekani. Hata
hivyo, alipoka pale alishusha pumzi baada ya kutambua kuwa alikuwa
Mraha mwenyewe bali sio jambazi la magari. “Lakini makatoni ya nini haya
anayoyapakia garini saa hizi?” yule jamaa alijiuliza. Alijitahidi kuyakodoa
macho yake kujaribu kukitegua kitendawili kile lakini akashindwa na kujiwa
na wazo la kumwuliza Mraha mwenyewe. Alipiga hatua mbele kuelekea
alipokuwa Mraha lakini akaghairi, ‘Je, itakuwaje kama ni shughuli ambayo
hakutaka kuichua? Je, ikiwa ni ule mradi wake bubu atakubali kuuchua
vivi hivi tu?”
Yule jamaa aligeuka polepole na kuelekea ilipokuwa nyumba yake
huku mawazo mchafukoge yameitawala akili yake. Pashau kubwa ya kutaka
kujua ni biashara gani aliyokuwa akiifanya mzee huyo ilianza kumtawala
kabisa. Kuanzia siku hiyo aliamua kujitosa kwenye kazi ya ukachero mpaka
aikidhi kiu yake ya kujua ni makatoni ya aina gani aliyokuwa akiyapakia
Mraha siku ile usiku.
Hiyo haikuwa mara ya mwisho kwa jamaa huyo kumkuta Mraha
akiyapakia makatoni hayo. Mara moja ilitokea sadfa kuwa alipokuwa
akisogea upande ule, Mraha aligutuka na kugeuka nyuma. Alipomwona
alishtuka kidogo, “Mmm…ndugu, umenikuta… ehhh…nilikuwa nikijiandaa
kwa ajili ya shughuli fulani ya kibiashara na wajua tena mambo ya maisha
yetu ni kuwahi. Wanasema Waswahili kuwa msari ni aliye pwani, nami
nilitaka kujiweka sawa kabla ya asubuhi,” alijieleza. Jamaa huyo alitambua
kuwa Mraha alikuwa na wasiwasi fulani lakini hakutaka kumwonyesha hofu
wala tuhuma zake kuhusu matendo yake. Baada ya kusalimiana walitakiana
alamsiki kisha akashika njia akaelekea ilipokuwa nyumba yake huku
maswali mengi yakizidi kumzonga akilini.
Kwa muda wa miezi kadha iliyofuatia yule jamaa hakupata upenyu
wowote wa kuikidhi kiu yake kuhusu alichokuwa akifanya Mraha. Siku moja
alikuwa mjini akitafuta duka la kuuzia betri ndogo za saa za mkono. Kwa
kuwa alitaka kupata duka lenye bei nafuu, aliamua kwenda kwenye mtaa wa
Ulitima. Zaidi ya kupatikana bidhaa aina hii, mtaa huu pia ulijazana watu
wengi pamoja na watoto wengi wa mitaani. Alipokuwa akizungukazunguka
akitafuta duka alilotaka, alimwona mtu aliyesimama pembeni kidogo,
karibu na kizimba cha simu pamoja na watu kadha; wanaume na wanawake.
Ingawa alikuwa amevaa koa hakushindwa kumtambua: Mraha. “Hauchi
hauchi unakucha,” alijiambia moyoni. Aliamua kuacha shughuli ya kutafuta
betri ya saa kwa muda hadi akifumbue kitendawili alichokuwa akijaribu
kukifumbua kwa muda mrefu. Alisimama kwa muda hadi Mraha na rubaa
yake walipoanza kutembea kuelekea upande wa chini wa mtaa. Aliwafuata
kwa nyuma, nusu akitembea na nusu kukimbia ili wasimponyoke.
Hatimaye, walika mahali Mraha alipokuwa ameliegesha gari lake.
Akalifungua buti na kupakua makatoni kadha. Alifungua katoni moja na
kuanza kutoa chupa ndogo ndogo. Wale watu walifungua baadhi ya chupa
na kunusa kidogo kisha wakazifunga. Wakamtolea pesa naye akazihesabu
122
123
haraka haraka huku
akipepesapepesa huku na
kule kama mtu mwenye
woga. Kila mmoja
aliporidhika na shehena
yake wakaondoka. Mraha
alijitoma garini na
kuiwasha kisha
akayoyomea sehemu
nyingine ya mji. Yule jamaa
aliamua kumfuata mmoja
wa wateja wa
Mraha
hadi sehemu
palipokuwa
na kibanda kidogo cha
makatoni. Muda si muda, aliwaona vijana wa barabarani na ombaomba
wengine wakiingia mle huku wameshika vijichupa vyao vya gundi. Sasa
alijua kila kitu dhahiri shahiri: Mraha alikuwa akishiriki kwenye biashara
ya kuwauzia ombaomba gundi ya kunusa.
Alishika njia moja kwa moja hadi kituo cha polisi na kuwaeleza
waliohusika kila kitu kuanzia utandu mpaka ukoko. Polisi walika na alasiri
hiyo hiyo kuwatia jamaa hao mbaroni. Mraha aliwekewa mtego na alipokuwa
akizipanga chupa zake kwenye makatoni chumbani mwake akasikia hodi
mlangoni. Kwa kuwa hakuwa na wasiwasi wowote, aliacha kazi yake na
kwenda kuufungua mlango. “Ndugu niwasaidie nini, maji ya kunywa labda?”
aliwauliza kwa uchangamfu wake wa kawaida. Mmoja wa wale makachero
alimtolea kitambulisho chake na kumweleza, “sisi ni maasa wa polisi wa
kupambana na uhalifu.” Mwili wa Mraha ulipatwa na mzizimo mkubwa
akashindwa hata kuongea. Polisi mmoja alipiga hatua na kuelekea zilipokuwa
zile chupa na makatoni yake.
“Mraha hii ndiyo biashara yako ya kila siku?” aliuliza yule polisi huku
akiinua chupa mojawapo. Mraha hakuweza kumjibu; aliitikia tu kwa
kutikisa kichwa. Hakuweza kujibu kuwaeleza habari za mradi wake bubu.
Walimkamata na kuandamana naye kituoni pamoja na chupa zake za karaha.
Maelezo ya msamiati
mkweche : gari kuu kuu; gari zee.
tendesa : pita mpaka; zidi.
kihoro : hofu; huzuni.
akaghairi : akabadili nia.
mawazo mchafukoge : mawazo yaliyochafuka; yaliyovurugika;
yasiyo na utulivu.
kujitosa : kujiingiza.
pashau : hamu.
tuhuma : shaka.
rubaa yake : kikundi chake.
karaha : mambo ya kuudhi.
124
125
Maswali
1. Ni kitu gani kinachothibitisha kuwa Bwana Mraha alikuwa na kipato
kizuri?
2. Unadhani ni kwa nini Mraha aliita biashara yake ‘mradi bubu’?
3. Unadhani ni kwa nini Bwana Mraha alikuwa amevaa koa wakati
alipokuwa akiongea na wateja wake huko mtaani? Je, unakiri Mraha
ni mtu wa aina gani?
4. Toa mapendekezo matano unayokiria yanaweza kusaidia kutatua tatizo
la watoto wanaorandaranda mitaani.
5. Toa maana ya methali zifuatazo:
(a) Msari ni aliye pwani.
(b) Hauchi hauchi unakucha.
6. Simulia wenzako visa vinavyothibitisha ukweli wa methali hizo.
7. Linganisha sehemu A na B katika jedwali lifuatalo ili kukamilisha
methali zilizomo:
A B
1. Siku za mwizi huenda yakaja.
2. Mtaka nyingi nasaba hupata mwingi msiba.
3. Mbaazi ukikosa maua si maungwana.
4. Mambo ni kangaja si kuka.
5. Angepaa juu kipungu ni arobaini.
6. Kiburi huenda akauya hapo.
7. Kwenda mbio hakilii mbingu.
8. Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
9. Mchama ago hanyeli hapakosi moto
10. Penye moshi husingizia jua.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Hotuba
Hotuba ni maelezo au taarifa ambayo hutolewa mbele ya watu na kwa
madhumuni maalum. Taarifa hii huwa na umuhimu mkubwa kwa
mzungumzaji na anayezungumziwa. Kwa mfano, hotuba inaweza kutolewa
kwa madhumuni ya kuhimiza kazi, kufanya kampeni fulani, kutoa taarifa
fulani kwa watu n.k. Kuna hotuba za aina mbalimbali: hotuba za viongozi,
hotuba za kisiasa, hotuba za sherehe, hotuba za kidini, hotuba za masuala
ya kijamii, hotuba zihusuzo matatizo yanayowakabili watu n.k.
124
125
Sifa za hotuba
Hotuba nzuri haina budi kuwa na mambo yafuatayo:
1. Ukweli wa habari na taarifa inayozungumziwa.
2. Ufasaha wa lugha ili iweze kuvutia, kupendeza na kueleweka vizuri.
3. Iwe na nidhamu nzuri sio tu kwa mpangilio bali pia lugha ya msemaji
anayezungumza mbele ya watu.
4. Mfuatano mzuri kuanzia mwanzo penye maamkuzi hadi mwisho.
5. Sauti ya kusikika pamoja na ishara ambazo zinaeleweka.
Uwasilishaji mzuri wa hotuba huzingatia:
1. Hadhira au wanaozungumziwa na kuhakikisha kuwa lugha na
yanayozungumziwa yanawahusu na wanaweza kuyaelewa.
2. Matumizi ya lugha ambayo ina mvuto na inaweza kuwanasa wasikilizaji
waweze kuendelea kusikiliza.
3. Matumizi ya mbinu za usemaji kama ishara-uso, ishara za mikono na
mbinu nyingine za kutia utamu katika mazungumzo au hotuba.
4. Msemaji kuhakikisha kuwa hayazamishi macho tu kwenye hotuba (ikiwa
anaisoma) bali anawaangalia wasikilizaji wake.
5. Matumizi ya lugha inayoeleweka kwa urahisi na wanaolengwa.
6. Sifa za kuweza kuwachangamsha au hata kuwachekesha wasikilizaji.
Muundo wa hotuba
Mwanzo: Salamu; msemaji anatanguliza salamu ambazo huweza
kujibiwa na wanaomsikiliza, salamu huweza kufuatia
utambulisho kwa mfano, ‘Wananchi, mabibi na mabwana,
hamjambo?’
Mwili/Kati: Huwa kiini cha hotuba. Sehemu hii hutoa ujumbe kwa
wasikilizaji na ndiyo muhimu sana katika hotuba.
Mwisho: Hapa ni hitimisho na huweza kutoa muhtasari, hutoa
shukrani na maagizo.
Mfano wa hotuba
Hotuba ya mkuu wa wilaya
“Ndugu wananchi, mabibi na mabwana, hamjambo? Nina furaha kupata
fursa hii kuwazungumzia kuhusu suala la usalama na jinsi tunavyopasa
kufanya ili kuuboresha. Bila shaka nimepata ripoti nyingi kuhusu hali mbaya
ya usalama katika kata hii ya Ruthimitu.
Ni kweli kuwa katika miezi ya hivi karibuni, kumekuwapo na visa
vingi vya ujambazi, wizi na uvunjaji wa nyumba na hata unajisi kote katika
126
127
kata hii. Viongozi wenu wamekwisha kuwasilisha malalamiko yenu kwenye
makao makuu ya wilaya kuhusu suala hili na serikali nayo imekuwa ikifanya
uchunguzi wake. Nataka kuwahakikishia kuwa serikali imeamua kuanzisha
kituo cha polisi hapa kijijini ili kuimarisha hali ya usalama katika eneo
hili. Pili, katika makao makuu ya polisi wilayani, tumeanzisha osi ambayo
itashughulika na malalamiko ya wanakijiji sio tu kuhusu suala la usalama
bali pia masuala yote mengine yenye umuhimu katika maisha yenu. Ningetaka
mjue kuwa sisi kama viongozi hatuna nia ya kupiga ubwete tu bila ya kufanya
lolote.
Kwa upande mwingine, tunawahimiza ninyi muwe tayari kushirikiana
nasi kwa kuwa hatuwezi kufanikiwa bila msaada wenu. Waswahili husema
kuwa kinga na kinga ndipo moto uwakapo. Tunaomba ushirikiano wenu ili
tuwashe moto wa kuuzima kabisa uhalifu katika eneo hili. Ushauri wangu
basi ni kuwa msichelee kutoa taarifa mnazohisi kuwa zitatufaa. Pili, pasiwepo
mtu ambaye anampa hifadhi mhalifu yeyote. Mtu anayeshirikiana na waovu
ni mwovu pia. Wote tutawatia mbaroni.
Nina imani kuwa ikiwa tutashirikiana tutafanikiwa kulimaliza tatizo
hili na kuendelea kuishi kwa amani kama hapo mbeleni. Kwa hayo machache
nasema asanteni sana na kwaherini.”
Zoezi
1. Je, hotuba ni nini na ina muundo gani?
2. Umeteuliwa na mwalimu kuwazungumzia wanafunzi wenzako juu
ya umuhimu wa kujiepusha na maovu ya kijamii. Andika hotuba fupi
kuhusu suala hilo.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Usemi halisi na usemi wa taarifa
Usemi halisi
Usemi wa aina hii unahusu maneno halisi kama yanavyotamkwa na
msemaji. Maneno haya huandikwa bila kugeuza chochote. Huonyeshwa
kwa kunukuliwa kwa alama za mtajo/kunukuu. Alama hizi mara nyingi
huandikwa zikiwa mbilimbili lakini pia alama moja moja huweza kutumika.
Alama za kunukuu huwekwa mwanzoni na mwishoni mwa maneno
yanayohusika. Kwa mfano:
(a) “Wewe ni nani?” askari aliniuliza.
(b) “Mimi ni Kipchumba,” nilimjibu.
(c) Nilipoka nyumbani mama aliniuliza, “Wapi mboga nilizokutuma?”
(d) “Ingia chumbani mle uniniletee kikapu changu,” nilimwambia
mwanangu Auma.
(e) “Wiki ijayo tutahudhuria maonyesho ya kilimo ya Nairobi,” mwalimu
alitwambia.
126
127
Mambo muhimu kuhusu usemi halisi
Kila neno la kwanza katika usemi halisi huanza kwa heru kubwa hata
kama usemi huo umeanzia katikati mwa sentensi. Kwa mfano:
(i) Kakangu aliponiona alisema, “Lo! Nilidhani hutaka hapa
kamwe.”
(ii) Nilipomkuta raki yangu akifanya mambo maovu nilimkanya
vikali, “Sitaki siku nyingine kukuona ukifanya mambo kama
hayo!”
(iii) Wachezaji walipoka tulianza kuimba, “Leo ni leo. Asemaye
kesho ni mwongo!”
Iwapo sentensi mpya inaanza baada ya msemaji kutajwa, heru kubwa
hutumika mwanzoni mwa sentensi hiyo mpya. Kwa mfano:
(i) “Ni lazima kila mmoja wenu ajitahidi awezavyo kama mnataka
kufaulu maishani mwenu,” mwalimu wetu alitwambia. “Maisha
yenu ya baadaye yatategemea juhudi zenu za leo.”
(ii) “Tukika mjini Voi tutapumzika kwa muda wa saa moja,”
kiongozi wetu alisema. “Baadaye tutaondoka na kwenda moja
kwa moja hadi kisiwani Mombasa.”
(iii) “Nchi yetu inaweza kuendelea sana ikiwa tutapiga vita usadi,”
rais mpya alisema mara tu baada ya kuapishwa. “Tusipofanya
hivyo nchi yetu itazidi kudidimia katika lindi la umaskini.”
Ikiwa maneno yanayotumika yamo katika sentensi ya kawaida, kitone
hubadilika na kuwa kipumuo iwapo sentensi hiyo itageuka kuwa usemi
halisi. Kwa mfano:
(i) Daktari Rosalia alitwambia kuwa Ukimwi ni ugonjwa hatari mno.
Inakuwa
“Ukimwi ni ugonjwa hatari mno,” daktari Rosalia alitwambia.
(ii) Raki yangu aliniambia kuwa wiki iliyofuatia angekwenda
kujionea mechi kati ya Harambee Stars na Uganda Cranes.
Inakuwa
“Wiki ijayo nitakwenda kujionea mechi kati ya Harambee Stars
na Uganda Cranes”, raki yangu aliniambia.
Ikiwa msemaji anatajwa kabla ya usemi halisi wenyewe, tunaweka
kipumuo kabla ya kuweka alama za mtajo. Kwa mfano:
(i) Daktari Rosalia alitwambia, “Ukimwi ni ugonjwa hatari mno.”
(ii) Raki yangu aliniambia, “Wiki ijayo nitakwenda kujionea mechi
kati ya Harambee Stars na Uganda Cranes.”
Ikiwa usemi halisi una kiulizo au alama ya hisi, alama za mtajo huwekwa
mwanzoni mwa usemi huu na baada ya kiulizo au alama ya hisi. Kwa
mfano:
(i) “Mlifungwa mabao mangapi?” baba aliniuliza.
128
129
(ii) “Kesho tutaondoka saa ngapi?” Farida alisaili.
(iii) “Majangili wamevamia nyumba ya Mwinyi. Masalaale!” watu
walisema kwa mshangao.
(iv) “Toka hapa mara moja!” lile jitu liliniamuru.
Msemaji mpya anapoanza kusema, tunaanza aya mpya. Kwa mfano:
Rehema alifungua mdomo kwa mastaajabu, “Huendi kwa nini?”
“Sikupewa ruhusa,” alijibu Zahara, “tena nimeachiwa chakula cha
usiku nipike,” huku akipigana kuzuia machozi ya hamaki na maonevu
yasimdondoke mbele ya yule mwenziwe. Rehema alimwambia, “Na wewe
unakubali? Una wazimu; twende! Kwanza nani atajua?”
“Na chakula? Unakiri baba akija akakuta hakukupikwa…”
“Kwani mama yako yuko wapi?”
“Amekwisha toka zamani, amekwenda kuzungumza.”
“Basi kwaheri”, alimtupia…
(Imenukuliwa kutoka Mali ya Maskini na Z. Burhani, 1981 uk. 6)
Usemi wa taarifa
Usemi huu huwa ni ripoti kuhusu mambo yaliyosemwa. Katika usemi huu
si lazima maneno yatokee kama yalivyotamkwa na msemaji. Yanaweza
kubadilishwa lakini ni sharti ujumbe ubakie ule ule. Vile vile, alama za mtajo
au viulizi havitumiki katika kuandika usemi wa taarifa. Baadhi ya maneno
vile vile hubadilika; kwa mfano, ‘kwangu’ huwa ‘kwake’, ‘sasa’ huwa ‘wakati
huo’, ‘kwetu’ huwa ‘kwao’ n.k. Pia viambishi mbalimbali hubadilika. Mifano:
(i) “Kesho nitakwenda Kisumu,” Rehema alimwambia shangazi yake.
inakuwa
Rehema alimwambia shangazi yake kuwa keshoye angeenda
Kisumu.
(ii) “Chumbani mwangu mna nyoka!” Bahati alisema huku
akitetemeka.
inakuwa
Bahati alisema huku akitetemeka kuwa nyumbani mwake
mlikuwa na nyoka.
(iii) Ni lazima mwonyeshe heshima kwa watu wote ikiwa mnataka
kuendelea vyema maishani,’ kasisi alitwambia.
inakuwa
Kasisi alitwambia kuwa ikiwa tungependa kuendelea vyema
maishani, ingebidi tuonyeshe heshima kwa watu wote.
Zoezi
1. Geuza sentensi zifuatazo uziweke katika usemi wa taarifa.
(a) “Ukika shuleni mwambie mwalimu akupe ruhusa ili twende mjini
nikakununulie vitabu unavyotaka,” baba aliniambia.
(b) Binamu alipowasili alisema, “Samahani sana kwa kuchelewa. Gari
128
129
letu lilipata matatizo huko njiani.”
(c) Kilomia alipokishwa mbele ya baraza la wazee alijitetea, “Naomba
msamaha na naapa kuwa sitarudia kosa hilo tena.”
(d) “Wananchi wa Rwanda wameanza kupata utulivu baada ya vita vya
miaka mingi,” balozi wa Rwanda aliwaambia watu waliohudhuria
sherehe hiyo.
(e) “Uhuru huu tunaojivunia ulipatikana kwa umwagikaji mwingi wa
damu,” mwanasiasa alisema.
2. Andika sentensi zifuatazo katika usemi wa taarifa.
(a) “Ingawa nimemwonya Wekesa siku nyingi, amekataa kabisa kuacha
tabia ya kupiga kelele darasani,” kiranja alimwambia mwalimu.
(b) Askari alipomwona mwizi alimwambia, “Simama mara moja au
nikupige risasi.”
(c) Rais alipowasili kutoka Marekani aliwaambia waliomlaki, “Benki ya
dunia imekubali kuipa Kenya mkopo wa shilingi bilioni hamsini.”
(d) “Kwa nini huwasaidii maskini?” binamu yangu aliniuliza.
(e) “Baada ya kupika, ninataka uende sokoni ukanunue mboga na
nyanya,” mama aliniambia.
2. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi ‘-o-ote’
Kivumishi o-ote huchukua miundo tofauti, kutegemea ngeli ya nomino
inayohusika. Tazama mifano kwenye jedwali lifuatalo:
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
-o-ote
a panya yeyote Panya yeyote atanaswa.
wa panya wowote Panya wowote watanaswa.
u mchezo wowote Mchezo wowote unapendwa.
i michezo yoyote Michezo yoyote inapendwa.
u ulezi wowote Ulezi wowote unafaa.
ya malezi yoyote Malezi yoyote yanafaa.
ya maziwa yoyote Maziwa yoyote yatanywewa.
ya maziwa yoyote Maziwa yoyote yatanywewa.
li bunge lolote Bunge lolote hutunga sheria.
ya mabunge yoyote Mabunge yoyote hutunga sheria.
ki kisu chochote Kisu chochote kinakata.
vi visu vyovyote Visu vyovyote vinakata.
zi fedha zozote Fedha zozote zitasaidia.
ki kimya chochote Kimya chochote hakifai hata.
li joto lolote Joto lolote hufaa msimu huu.
vi vita vyovyote Vita vyovyote husababisha vifo.
130
131
Zoezi
Soma hadithi ifuatayo huku ukisahihisha matumizi mabaya ya kivumishi
-o-ote kilichoonyeshwa.
Hapo zamani za kale mbuzi na chui walikuwa maraki wa chanda na pete.
Waliishi katika nyumba moja na walipofanya jambo chochote walilifanya
pamoja. Walipokwenda mahali yoyote walikwenda pamoja, waliponunua
kitu zozote walitumia pamoja, walipopika chakula zozote walikula pamoja
na walipopata matatizo chochote waliyatatua pamoja. Mradi walitekeleza
shughuli yoyote zao kwa maelewano makubwa.
Muda si muda, kila mmoja wao akajaliwa kupata watoto. Waliwalea
vizuri kwa tunu na tamasha na kuwapa vyovyote walichohitaji. Siku moja chui
aliamua kwenda nyumbani kwao kuwaona wazazi wake. Alipoka alisikitika
sana. Nchi yao ilikuwa na ukame mkubwa. Hakukuwa na mahindi zozote,
maharagwe vyovyote, mihogo zozote, matunda lolote, viazi chochote au kitu
kingine yoyote cha kutiwa kinywani. Basi baada ya kujadiliana kwa muda
mrefu hawakupata suluhisho vyovyote. Mwishowe, wakakubaliana kuwa chui
atamdanganya mbuzi kuwa kuna karamu huko kwao kisha amlete pamoja
na wanawe ili wapate kitoweo angalau cha wiki moja. Chui alisikitika sana
kwa uamuzi huo lakini hakuwa na lingine chochote la kufanya kwa vile
hangetaka wazazi wake wafe njaa.
Aliporudi nyumbani alimwambia mbuzi kuwa huko kwao kuna sherehe
kubwa na angetaka waandamane naye keshoye ili amsaidie kubeba mizigo.
Mbuzi akakubali mara moja kisha akakimbia mtoni kuoga tayari kwa safari.
Alipokuwa mtoni chui akawashika watoto wote wa mbuzi bila kubakiza
chochote na kuwatumbukiza ndani ya gunia kisha akalifunga vizuri kwa
kamba. Wakang’oa nanga kuelekea nyumbani kwa kina chui. Chui alibeba
ule mzigo wenye watoto. Lakini walipokuwa njiani chui akataka kwenda
haja. Akamwambia mwenzake, “Tafadhali raki yangu, nishikie mzigo huu
ili nijisaidie.” Mbuzi akauchukua ule mzigo naye chui akaingia kichakani
kujisaidia. Hata hivyo, mbuzi alipoinua ule mzigo akaona ni mzito zaidi. Tena
vitu vilivyokuwa ndani vilikuwa vinatoa sauti fulani. Akasema, “Nitafungua
nione ni kitu gani kilicho ndani.” Alipofungua alishtuka sana alipowaona
wanawe ndani. Alitimua mbio akarudi nyumbani na kuwatoa watoto wake
bila kubakiza yoyote kisha akawashika wale wa chui na kuwatumbukiza ndani
ya gunia hilo. Akatimua mbio kurudi alikomuacha chui. Alipoka akakuta
ndio sasa amemaliza haja yake na anatoka kichakani. Wakaendelea na safari
hadi nyumbani kwa kina chui.
Walipowasili, mbuzi akawapa wazazi wa chui ule mzigo nao wakaupokea
kwa furaha kuu. Kisha mbuzi akajifanya anakwenda haja. Alipotoka nje
alipiga chenga hapa na pale kisha akatimua mbio hadi nyumbani kwake.
Haraka haraka akawachukua wanawe bila kumwacha lolote na kutorokea
nchi nyingine. Kule nyuma kwa kina chui kulikuwa na furaha ajabu.
Waliuchukua ule mzigo bila hata kuangalia ni nini kilichokuwa ndani
na kuutumbukiza kwenye chungu kilichokuwa kikichemka. Sasa wageni
wengi walikuwa wameanza kuwasili tayari kwa karamu wajomba zake
chui, binamu, shangazi, nyanya, babu na wengine wengi. Chakula kilipoiva
130
131
walikitoa kwenye chungu na kufungua. Walipigwa na butwaa wasijue la
kufanya walipowaona watoto wa chui wakiwa wafu. Chui alipiga usiahi wa
ajabu na kutimua mbio kuelekea nyumbani kwake ili akamrarue mbuzi.
Lakini alipoka akakuta ameshaondoka.
Tangu siku hiyo chui na mbuzi wamekuwa maadui wakubwa. Chui
bado anamtafuta mbuzi ili alipize kisasi.
3. Hali
Hali - me - na kukanusha kulingana na nafsi
Umoja Wingi
Nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nimekaza sijakaza tumekaza hatujakaza
nimekopa sijakopa tumekopa hatujakopa
nimebeba sijabeba tumebeba hatujabeba
nimelaani sijalaani tumelaani hatujalaani
Nafsi ya pili
umekaza hujakaza mmekaza hamjakaza
umekopa hujakopa mmekopa hamjakopa
umebeba hujabeba mmebeba hamjabeba
umelaani hujalaani mmelaani hamjalaani
Nafsi ya tatu
amekaza hajakaza wamekaza hawajakaza
amekopa hajakopa wamekopa hawajakopa
amebeba hajabeba wamebeba hawajabeba
amelaani hajalaani wamelaani hawajalaani
Zoezi
Kanusha sentensi zifuatazo:
1. Ndege amepaa angani. 6. Mtu yule amelemaa mkono wa kulia.
2. Wazee wamechoma nyama. 7. Yeye ameweza.
3. Sisi tumejadili suala hilo. 8. Wairimu amechanua nywele.
4. Watoto wameugua malaria. 9. Binamu amemwaga maji yangu.
5. Watu wote wamechanga pesa. 10. Sisi tumewasalimu.
132
133
D. Kusoma
Vitabu vya ziada
Wakati mwingine utalazimika kama mwanafunzi kusoma vitabu ambavyo
vitakusaidia kuyaongeza maarifa yako kuhusu mambo mbalimbali. Kwa
mfano, unaweza kwenda maktabani na kuchukua vitabu vya hadithi au
vitabu vinginevyo vitakavyoupanua ufahamu wako. Hivi ni vitabu vya ziada.
Ni vya ziada kwa kuwa vinaongeza maarifa yako.
Hatua muhimu katika usomaji wa vitabu vya ziada:
1. Ni vizuri kuwa na daftari la kuandikia.
2. Andika vidokezi wazi kuhusu ulichokisoma.
3. Andika kwa hati inayosomeka; yaani unayoweza kusoma siku nyingine.
4. Unapokumbana na maneno mapya hakikisha kwamba umeyaandika;
ni vizuri hata kuandika sentensi yalikotumiwa.
5. Chunguza maana za maneno mapya unayokumbana nayo.
6. Ikiwa unasoma mada fulani, andika hoja au mambo muhimu pamoja.
7. Andika pia anwani ya kitabu ulichosoma.
E. Kuandika
Ushairi
Ushairi ni sanaa ambayo imekuwako katika jamii zetu kwa kipindi kirefu.
Ushairi hutumiwa kuwasilisha mawazo, hisia, maoni na msimamo alionao
mtunzi kwa ufundi mkubwa. Ufundi huo unahusu upangaji maalum wa beti,
matumizi ya lugha nzito, uteuzi ufaao wa msamiati pamoja na matumizi ya
tamathali za usemi kama tashbiha, sitiari na nyinginezo. Mambo ya kimsingi
ya kuyajua kabla ya kuanza utunzi wa mashairi ni:
(i) Lengo la utunzi: Je, una dhamira gani katika utunzi wako?
Unataka kutunga shairi kuhusu jambo gani? Lazima shairi liwe
na dhamira au lengo wazi kwa atakayelisoma.
(ii) Walengwa: Je, shairi hilo unalotaka kutunga linawalenga
akina nani?
(iii) Utaratibu: Ikiwa unajua dhamira yako na walengwa wa shairi
unalotunga, utawezaje kuyapanga mawazo yako? Je, utatunga
shairi la aina gani? Je utatunga shairi la arudhi (linalofuata
mizani, vina n.k.) au utatunga shairi huru (lisilozingatia
arudhi)?
(iv) Lugha: Utunzi wowote unategemea lugha. Utunzi wa mashairi
132
133
una sifa kadha za matumizi ya lugha. Pili, lazima utumie lugha
ambayo ina uwezo wa kumvuta msomaji ili aweze kuathiriwa na
ujumbe wako.
(v) Mtiririko na utoshelezi: Lazima utungo unaoutunga uwe na
mtiririko kuanzia mwanzo hadi mwisho. Ikiwa umetunga shairi
la arudhi lazima uhakikishe pia kuwa kanuni zote zimefuatwa.
Mfano 1. Shairi la arudhi
Dhamira: Ajali za barabarani.
Walengwa: Wanafunzi wa kidato cha pili (na wasomaji wengine)
(a) Utaratibu: Unaweza kupanga hoja kwanza
Hoja kuu
(i) Ajali zimeongezeka
(ii) Huleta maafa makubwa
(iii) Huleta vifo, vilio n.k.
(iv) Umuhimu wa makini
(v) Usalama wa barabarani
(vi) Mchango wa abiria
(vii) Walevi wasiendeshe magari n.k
(b) Shairi lenyewe
Kuna jambo lanikera, liniumalo moyoni,
Leo nimepata ghera, kulisema hadharani,
Siposema nawa jura, siwafaidi wengini,
Ajali barabarani, jama zitatumaliza.
Jama zitatumaliza, kua barabarani,
Watu tunawapunguza, na wengine spitalini,
Hatwachi kuomboleza, kila afapo insani,
Ajali barabarani, jamani zinalemaza.
Jamani zinalemaza, tukaachwa taabani,
Madonda tukiunguza, na kilio cha moyoni,
Huku tukijiuliza, kwa nini jama kwa nini?
Ajali barabarani, jamani zaangamiza.
Jamani zaangamiza, sasa tuwe na makini,
Kutojitia mwapuza, wa sheria za njiani,
Tuwache mauzauza, tushikapo usukani,
Ajali barabarani, ni janga ninatangaza.
134
135
Ni janga ninatangaza, kujaza bia tumboni,
Halafu ‘kajitangaza, ‘ni dereva namba wani,
Ufuni wajisogeza, kwa kuwa vyema huoni,
Ajali barabarani, iweje tunanyamaza?
Iweje tunanyamaza, sisi tulio garini?
Midomo kutupooza, kwamba ‘haiwezekani!’
Dereva kutukimbiza, atuulie njiani!’
Ajali barabarani, jama zinatumaliza.
Zoezi
Tunga shairi jepesi la arudhi kuhusu mada yoyote utakayochagua.
134
135
Sura ya Kumi na Mbili
A. Ufahamu
Bwana Kaukata na Soko la Ulimwengu
Tarafa ya Hawinde ilikuwa maarufu kutokana na bidii za mchwa za wakazi
wake. Uchumi wa tarafa nzima ulitegemea kilimo licha ya kuwa wenyeji wa
eneo hili hawakuwa na mashamba makubwa bali vikataa vidogo vidogo tu.
Hata hivyo, wanatarafa hawa walijua jambo moja, kuwa ukilima pantosha,
utavuna pankwisha na kwa hiyo walitia juhudi kubwa katika kilimo chao.
Licha ya udogo wa vikataa hivyo, waliweza kupata mazao ya kazole kila
msimu wa kuvuna ulipowadia. Tatizo kuu walilopambana nalo kwa miaka
na mikaka lilikuwa usambazaji na uuzaji wa mazao yao. Lakini kwa bahati
nzuri pale tarafani palikuwa na mkulima mmoja wa miaka mingi. Yeye
alikuwa na migunda mikubwa sio vikataa kama wao. Alikuwa na uwezo wa
kiuchumi wa kununua mbolea na mbegu zilizopendekezwa na wataalamu wa
kilimo. Matokeo yake yakawa kuwa mapato yake yalikuwa mazuri na muda
si muda akawa ametajirika sana. Jina la mkulima huyo lilikuwa Kaukata.
Tatizo la uuzaji lilipowasonga, mwanatarafa mmoja alipendekeza kuwa
wamwendee Bwana Kaukata na kuomba msaada wake. “Huyu ana ujuzi
na anaijua mizungu yote ya uuzaji wa mazao huko mijini kwenye masoko
makubwa,” mmoja wao alisema. “Ahh, lakini yule bwana haaminiki, anaweza
akatukatalia pendekezo letu,” mwingine akasema. “Hapana, tujaribu tu
tuone atasema nini kwa kuwa ni mwanatarafa mwenzetu; ni mmoja wetu
na meno ya mbwa hayaumani bwana,” mzee mmoja akatoa pendekezo lake.
Basi wanatarafa wakaandamana hadi nyumbani kwa Bwana Kaukata na
kumweleza nia yao. Bwana Kaukata alitulia tuli huku akiyasikiliza maneno
ya wanatarafa. Hatimaye alisema, “Mimi niko tayari kuwasaidia wanatarafa
wenzangu kwa sababu sote tuna nia moja: kujiendeleza. Ikiwa tutafanikiwa
itakuwa bora kwa tarafa nzima na hata hali ilivyo katika ulimwengu mzima
ni kuwa watu wanashirikiana kwa kutambua busara ya kinga na kinga ndipo
moto uwakapo.”
Wanatarafa waliondoka pale kwa furaha ya kuwachania nguo. Njiani
walimfanyia stihizai mwenzao aliyekuwa akiwaambia kuwa Bwana Kaukata
haaminiki. “Unaona bwana, hofu ya bure, yule ni mtu anayejua utu ni nini.
Ni mwenzetu tunayeweza kumtegemea, hawezi kabisa kutudhuru; ni kama
wasemavyo watu meno ya mbwa hayaumani,” walisema. Yule jamaa alifyata
mkia tu lakini moyoni alikuwa na hofu fulani ambayo alishindwa kujua
ilikuwa inatoka wapi.
Msimu wa mavuno ulipoka, wanatarafa walivuna mazao yao na
kuyawasilisha kwa Bwana Kaukata. Bwana Kaukata, kwa nia sa wakati
huo, naye hakufanya taahira, aliyawasilisha mazao hayo sokoni huko mjini
na baada ya muda mfupi akawakabidhi wanatarafa fedha zilizotokana na
mazao yao. Furaha iliyotanda kama wingu kijijini siku ile haisemeki; kila
136
137
mmoja alitabasamu mpaka
gego la mwisho likaonekana.
Wote walikata kauli kuwa
watazidisha juhudi katika
kilimo ili kuhakikisha kuwa
mavuno yao
yameongezeka.
Walijua fika kuwa kwa
njia hii wataishia kuupa
kisogo umaskini uliokuwa
unabishia kwenye makazi
yao. Msimu wa pili mazao
yalikuwa mengi ajabu.
Walifanya kama mara ya
kwanza: wakamkabidhi
mwanatarafa mwenzao,
Bwana Kaukata mazao yao.
Wote walisubiri kwa hamu
kuyapata mapato yao na
kuyasuluhisha matatizo
chungu mbovu yaliyokuwa yakihitaji kushughulikiwa.
Lakini mara hii mapato hayakuwa kama mara ya kwanza. Licha ya
mazao kuwa mengi na hata bora, mapato yao yalishuka kwa kiasi fulani.
Walipomwuliza Bwana Kaukata aliwajibu haraka haraka, ‘Wenzangu, hizi
ndizo shida zetu sisi, bei za mazao hupangwa na mashirika ya kigeni na
mara kwa mara huenda chini au hata juu. Kuna Soko la Ulimwengu…eh
soko kubwa sio kama letu hili, ambako mazao hayo huuzwa na bei yake iko
chini mara hii,’ aliwaeleza. Wengi wao ambao hata kisomo kidogo hawana
waliridhika na maelezo hayo ya kitaalamu. Walikumbushana ile methali ya
kuwa meno ya mbwa hayaumani; kwa hiyo lazima Bwana Kaukata alikuwa
akiwaeleza hali halisi ya mambo ya uuzaji wa mazao. Waliamua kuendelea
kufanya kazi kwa bidii.
Wanatarafa waliendelea kulima kwa juhudi kubwa na hata kuhakikisha
wanajitahidi kupata mbegu zilizopendekezwa na wakuu wa kilimo. Wachache
waliokuwa na uwezo kidogo walijitahidi hata kupata mbolea za kutumia.
Lakini soko la ulimwengu liliendelea kuwapa mapato duni. Kwa upande
wake, Bwana Kaukata alizidi kunawiri. Wengi waliamini kuwa yeye alikuwa
na bahati ya mtoto aliyezaliwa na nyota ya jaha. Mashamba yake yalikuwa
makubwa, alikuwa na uwezo wa kiuchumi wa kutumia zana mpya na za
kisasa za kulimia na kuongeza tija ya mashamba yake makubwa. Wakati
wanatarafa wanaendelea kudidimia, Bwana Kaukata aliendelea kupanda
ngazi za kiuchumi na kuwa mfano wa kutajika sio tarafani tu bali wilaya
nzima.
Hali hii iliwapa wanatarafa msukumo mkubwa; wote walikuwa na hamu
ya kuwa kama yeye siku moja. “Tunachotakiwa kufanya ni bidii; ukitaka
miwaridi vumilia miba,” waliambiana wao kwa wao. Sasa walijifunga mkaja
136
137
na kuongeza juhudi maradufu. Lakini hali yao haikubadilika; bei ya mazao
yao iliendelea kubaki pale pale. Kila walipomwuliza mwenzao aliwajulisha,
“Ni njama za Soko la Ulimwengu; jamani tutafanya nini na huu ni ulimwengu
wa mwenye nguvu mpishe. Hata mazao yangu ni vivyo; labda tuongeze nguvu
tu na kuomba kuwa hali itabadilika msimu ujao,” alisema Bwana Kaukata
na kuwatia moyo. Waliyaamini maneno yake na kuongeza bidii, wakapanua
vikataa vyao, wakatumia samadi na kufanya kazi mchana kutwa. Lakini
ilikuwa mjango; hali yao ilibaki vilevile.
Basi siku moja mwanatarafa mmoja alianza kutuhumu kuwa labda
kulikuwa na jambo fulani. Aliwatajia wanatarafa wenzake ambao waliamua
kushirikiana naye kugundua kwa nini soko hili la ulimwengu lilikuwa
likiwapunja kila mara. Kwa bahati nzuri mwanatarafa huyo alikwisha fanya
kazi ya upelelezi zamani kabla ya kustaafu na kujiunga na wanatarafa
wenzake vijijini. Alianza kufanya utati wake polepole na kama wasemavyo
Waswahili papo kwa papo kamba hukata jiwe. Msimu uliofuatia wanatarafa
walimkabidhi Bwana Kaukata mazao yao kama kawaida. Mara hii yule
mwanakijiji alipanga safari ya kwenda mjini kufuatia malipo yake ya uzeeni
kama kawaida yake. Akiwa huko alifanya uchunguzi na kuishia kutambua
kuwa bei ya mazao ilikuwa imepanda sana. Aliwajulisha waliohusika
serikalini kuhusu hofu waliyokuwa nayo wanatarafa, nao wakajitosa kwenye
bahari ya uchunguzi kubainisha mbichi na mbivu.
Bwana Kaukata aliporudi kijijini alikuwa na wimbo wake wa kawaida,
“Soko la Ulimwengu bado linatudanganya!” Wanakijiji walipokea malipo yao
duni huku wakisikitika. Muda si muda, wachunguzi walimaliza uchunguzi
wao na kuka kijijini. Walimkuta Bwana Kaukata nyumbani akihesabu pesa
alizokuwa amepata kutokana na biashara zake nyingi. “Ama kweli mimi
sasa nimeukata umaskini kabisa!” walimsikia akisema kwa bashasha nyingi.
“Nasi tumeikata mirija yako ya kuwanyonya wanakijiji maskini!” mmoja wao
alisema kwa sauti ya juu. Bwana Kaukata alishtuka lakini hakuwa na la
kufanya; alitamani ardhi ipasuke immeze lakini hilo halikutokea. Alikamatwa
na kukishwa mahakamani kwa kosa la kuwadhulumu wakulima wadogo
haki zao. Alilazimishwa kuwalipa dia na malimbikizo ya fedha zao nyingi
alizowapunja. Aidha, alitiwa kifungoni kwa kipindi cha miaka mitano kwa
sababu ya kosa la ulanguzi. Bwana Kaukata aliyekuwa tajiri wa kupindukia
akaishia kuwa mkata mkuu. Laiti angejua kuwa siku za mwizi ni arobaini!
Maelezo ya msamiati
vikataa : mashamba madogo; vijishamba.
migunda : mashamba; makonde.
taahira : kuchelewa; kukawia.
kutuhumu : kushuku; kutilia shaka.
punja : kupa kidogo kuliko inavyostahiki.
dia : malipo kwa ajili ya hasara au maumivu.
138
PB
Maswali
1. Tarafa ya Hawinde ilitegemea nini kwa uchumi wake?
2. Hapo mwanzoni kabla ya kupewa jukumu la kutafutia wanatarafa soko,
Bwana Kaukata alitofautianaje na wanatarafa wengine kiuchumi?
3. Kwa nini wanatarafa walimwendea Bwana Kaukata kumwomba awauzie
mazao yao?
4. Unadhani ni kwa nini Bwana Kaukata hakuwapunja wanatarafa
alipowauzia mazao mara ya kwanza?
5. Je, Bwana Kaukata alikuwa na nia gani kwa kuwatajia wanatarafa
kuhusu Soko la Ulimwengu? Je, unadhani aliyosema ni kweli?
6. Toa maana ya methali zifuatazo kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu:
(a) Ukilima pantosha, utavuna pankwisha.
(b) Meno ya mbwa hayaumani.
(c) Kinga na kinga ndipo moto uwakapo.
(d) Ukitaka miwaridi lazima uvumilie miiba.
(e) Mwenye nguvu mpishe.
(f) Papo kwa papo kamba hukata jiwe.
(g) Siku za mwizi ni arubaini.
7. Eleza maana ya misemo ifuatayo kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu kisha uitumie kutungia sentensi:
(a) miaka na mikaka (b) alifyata mkia
(c) hakufanya taahira (d) walijifunga mkaja
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Misemo
Katika kidato cha kwanza, tuliona kuwa misemo ni kipera cha semi katika
fasihi simulizi. Kimsingi, neno msemo hutumiwa kuelezea fungu la maneno
ambalo huwa na maana maalum. Misemo huweza kujumlisha nahau na
misimu (au simo). Kabla ya kuangalia nahau na misimu tuangalie mifano
ifuatayo ya misemo:
(i) Akili ni mali.
(ii) Jembe ni uhai.
(iii) Ukulima ni uti wa mgongo wa taifa.
(iv) Misitu ni uhai.
(v) Kiumbe hachukuliki.
(vi) Elimu ni bahari.
PB
139
Hii yote ni misemo kwa kuwa inaeleza ukweli fulani tunaoufahamu sote.
Kwa mfano, ikiwa utatumia akili yako utaishia kupata mali au chanzo cha
kujikimu maishani (akili ni mali) na tunajua faida zinazotokana na misitu
(misitu ni uhai). Sasa tuangalie nahau na misimu.
(a) Nahau: Nahau kimsingi ni misemo lakini hii ina undani fulani wa
kimaana, yaani maana yake huwa yamechika. Nahau hutumiwa
sana katika kuipamba lugha na kuifanya iwe na mvuto wa kupendeza.
Hii ni mifano ya nahau: piga maji (lewa), piga chuku (danganya),
pata jiko (oa), liwa bangu (danganywa), agizia risasi (tupia risasi
kwa mbali) zamia lulu (enda mahali na kukawia), jitia za mtonga
(kujifanya hujui/ kujitia hamnazo), enda dalji (tembea kwa maringo)
n.k.
(b) Misimu: Hii ni misemo ambayo hutumiwa na kundi fulani la watu
kwa ajili ya mawasiliano yao. Kwa kawaida, misimu au simo huzuka
wakati fulani na huweza kupotea baada ya kipindi fulani. Misimu
huwa haikubaliki katika lugha sanifu ingawa baadhi huweza
kutumiwa kwa muda na kushika na hata kukubalika. Misimu
hutokana na nia ya kundi fulani kutaka kuwasiliana kwa siri au kwa
njia ambayo haifahamiki na kila mtu. Hii hapa ni mifano ya misimu:
leta munkari (leta fujo au ghasia), jisikia sukari (ringa au kujiona
bora), zua kasheshe (sababisha fujo au kisanga) n.k.
Maswali ya marudio
1. Eleza maana ya neno misemo pamoja na aina mbalimbali za misemo.
2. Eleza maana ya nahau na misimu ifuatayo:
(i) Jipalia makaa.
(ii) Piga vijembe.
(iii) Jikaza kisabuni.
(iv) Zunguka mbuyu.
(v) Kazi ya kijungu jiko.
(vi) Kula chumvi nyingi.
(vii) Tia madahiro.
(viii) Mwaga umombo (msimu).
(ix) Andika meza.
(x) Ringa ile mbaya (msimu).
(xi) Vaa mtumba (msimu).
2. Matamshi bora: vitate g/ng
Soma maneno haya:
g ng
gawa ngawa
guu nguu
goma ngoma
140
141
Soma: Vitanza ndimi
1. Baada ya Bwana Angawa kugawa ngawa akagawa chakula cha ngawa
ili kila ngawa apate chakula chake.
2. Jana nilitia guu kwenye maji nikaumwa na nguu kwa vile nguu wakiona
guu kwenye maji wanajua ni la mvuvi aliyekuja kuvua nguu.
3. Wanamuziki wa Ngomani wamegoma kucheza ngoma wakisema
wamegoma kwa kuwa kule Ngomani hakuna ngoma zinazofaa na hivyo
wameamua kugoma hadi chifu wa Ngomani anunue ngoma zinazofaa.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Vinyume vya vitenzi
Kinyume ni hali inayopingana moja kwa moja na hali iliyopo. Kwa mfano:
kitenzi kinyume kitenzi kinyume
funga fungua ingia toka
simama keti cheka lia
fumba fumbua tia toa
panga pangua choma chomoa
ziba zibua tega tegua
cha chua pakia pakua
umba umbua fuma fumua
kunja kunjua inama inuka
panda shuka funika funua
fukia fukua
Zoezi
Jaza kila pengo kwa kutumia kwa usahihi kinyume cha kitenzi kilichoandikwa
kwa heru za mlazo. Kwa mfano:
Kakangu alivaa sare ya shule asubuhi kisha _______ jioni alipotoka
shule.
Kakangu alivaa sare ya shule asubuhi kisha akaivua jioni alipotoka
shule.
(i) Utata uliozushwa na Hamisi _______ na mwalimu wetu.
(ii) Mimi hulala saa tatu usiku kisha hu _______ saa kumi na mbili
alfajiri.
(iii) Mimi _______yule kunguru aliyekuwa amenaswa na mtego.
(iv) Mimi nilijitwika mzigo huo kisha nikau _____ nilipoka nyumbani.
(v) Mtu akitenda mema hu_______ lakini akitenda maovu hulaaniwa.
(vi) _______ na kushuka ndiyo hali ya maisha.
(vii) Nilikasirishwa na raki yangu kwa _______ fulana niliyokuwa
nimefuma kwa ustadi mwingi.
140
141
(viii) Mwalimu aliingia darasani kisha _______ dakika chache baadaye.
(ix) Mtoto huyu hafanyi lolote siku nzima ila _______ na kufungua
milango.
2. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi ‘-o-ote’
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
-o-ote
i sahani yoyote Sahani yoyote itatumika.
zi sahani zozote Sahani zozote zitatumika.
u udaku wowote Udaku wowote unaaibisha.
u udaku wowote Udaku wowote unaaibisha..
u utepe wowote Utepe wowote utakatwa.
zi tepe zozote Tepe zozote zitakatwa.
ku kuchora kokote Kuchora kokote kunaliwaza.
ku kuchora kokote Kuchora kokote kunaliwaza.
pa mahali popote Mahali popote patanifaa.
ku mahali kokote Mahali kokote kutanifaa.
mu mahali momote Mahali momote mtanifaa.
Zoezi
1. Chagua kivumishi mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo:
(i) Mahali _______ patanifaa. (chochote, popote)
(ii) Ukora _______ haufai. (wowote, lolote)
(iii) Ubaya _______ unafaa nini? (wowote, lolote)
(iv) Mahali _______ kutatumika. (pokote, kokote)
(v) Kuliwaza _______ kunatuliza. (kokote, yoyote)
(vi) Senti _______ zitafaa kwa mahitaji yangu. (yoyote, zozote)
(vii) Ulaghai _______ hausaidii yeyote. (wowote, yoyote)
(viii) Wema _______ utawafaa watoto hawa. (yoyote, wowote)
2. Tunga sentensi ukitumia vivumishi vifuatavyo:
(i) kokote (ii) popote (iii) zozote
(iv) yoyote (v) wowote (vi) momote
142
143
3. Kukanusha wakati uliopita kulingana na nafsi
Umoja Wingi
Nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nilika sikuka tulika hatukuka
nilimaliza sikumaliza tulimaliza hatukumaliza
niliondoka sikuondoka tuliondoka hatukuondoka
nilijua sikujua tulijua hatukujua
Nafsi ya pili
ulika hukuka mlika hamkuka
ulimaliza hukumaliza mlimaliza hamkumaliza
uliondoka hukuondoka mliondoka hamkuondoka
ulifua hukufua mlifua hamkufua
Nafsi ya tatu
alika hakuka walika hawakuka
alimaliza hakumaliza walimaliza hawakumaliza
aliondoka hakuondoka waliondoka hawakuondoka
alifua hakufua walifua hawakufua
Zoezi
Sentensi zifuatazo zimeandikwa katika hali ya kukanusha. Ziandike katika
hali ya kuyakinisha. Kwa mfano:
Kaka hakusoma kitabu kizima.
Kaka alisoma kitabu kizima.
(a) Watoto hawakucheza mchezo huo.
(b) Mchezaji hakuanguka vibaya sana.
(c) Wewe hukunieleza ukweli.
(d) Jitu halikunitupia jiwe.
(e) Sikwenda mtoni kufua nguo.
(f) Wananchi hawakufanya kazi kwa nguvu.
(g) Wezi hawakuomba Mungu.
(h) Mimi sikukataa mwito.
(i) Naliaka hakununua kitabu.
(j) Nyanya hakutembea sana.
142
143
D. Kusoma
Makala
Soma makala ifuatayo kisha ujibu maswali uliyoulizwa.
Msingi wa mawasiliano kati ya binadamu ni neno. Neno laweza kutamkwa
kwa mdomo likasikika au kuandikwa likasomwa. Katika makala hii tutajadili
mabadiliko katika fasihi ya Kiswahili yatokanayo na neno lililoandikwa katika
nyakati mbalimbali za historia yake. Jambo lililo dhahiri mpaka sasa ni
kwamba neno la Kiswahili katika historia ya Afrika Mashariki limeleta umoja
ambao haupatikani katika sehemu zingine za bara hili. Historia ya fasihi
ya Kiswahili yaonyesha kwamba neno la Kiswahili limekuwa likijihusisha
na amani katika upwa wa Afrika ya Mashariki. Nchi za Afrika Mashariki
haziwezi kuingia katika hali ya uhasama wa muda mrefu kwa sababu watu
wake wanaendelea kuwasiliana katika lugha moja kuu inayoeleweka na wengi.
Daima kuna mawasiliano na kuna kujibizana. Mawasiliano yaliyopo kati ya
walio wengi ndiyo yanayoihakikishia Afrika Mashariki uwezekano wa amani
ya kudumu.
Mawasiliano yaliyopo hayawezi kukatishwa na mikondo ya kisiasa, hata
kama mikondo hiyo inaelekea njia tofauti. Kwa hivyo, lugha ya Kiswahili
ni lugha ya walio wengi na fasihi yake itaendelea kukua kufuatana na
mabadiliko ya kijamii na kihistoria ambayo husababishwa na watu wenyewe.
(E. Kezilahabi, ‘Siasa, tekinolojia na ukuaji wa Fasihi ya Kiswahili’
Katika Kioo cha Lugha Juzuu 1, 1995)
Maswali ya marudio
1. Je, makala haya yanahusu nini?
2. Mwandishi anamaanisha nini anaposema kuwa ‘Nchi za Afrika Mashariki
haziwezi kuingia katika hali ya uhasama.’ Je, kwa nini?
3. Je, unajifunza nini baada ya kuisoma makala hii?
E. Kuandika
Insha ya mdokezo
Hii ni aina ya insha ambapo umepewa mwelekezo wa kukuongoza jinsi ya
kuianzia au kuimalizia insha utakayoandika. Sababu ya kupewa mdokezo
huo ni kujaribu uwezo wako wa kuandika insha ambayo itaingiliana na
kifungu au sentensi uliyopewa. Maneno unayopewa huwa hayakumalizwa
bali yanaachwa kwa kuwepo kwa nukta tatu (. . .), ndiyo maana inaitwa
insha ya mdokezo; yaani umedokezewa tu.
Mambo ya kuzingatia wakati wa kuandika insha hii:
(i) Angalia mdokezo uliopewa na ujaribu kuwaza na kuona
utaingiliana na hadithi ya aina gani.
(ii) Kisa chako kifungamane na mdokezo huo kiasi kwamba msomaji
hatahisi kuwa umekilazimisha.
144
145
(iii) Tumia lugha fasaha ambayo inamvutia msomaji wa insha yako.
(iv) Zingatia kanuni zote za uandishi wa insha kama alama za
uakishi, saru bora, upangaji mzuri wa aya n.k.
(v) Insha utakayoandika iwe na mtiririko mzuri na iweze
kupendeza kusoma.
(vi) Tumia nahau, methali na msamiati ufaao ili kuukoleza utamu
wa insha yako.
Mfano wa insha ya mdokezo
‘Jua liliinuka kwa uzembe na kuisambaza mionzi yake kijijini…Endelea.
Kelele za asubuhi
Jua liliinuka kwa uzembe na kuisambaza mionzi yake kijijjini. Kadiri lilivyopanda
ndivyo lilivyouacha wekundu wake wa alfajiri na kuchukua sura nyingine.
Nilikuwa nimesimama kwenye ukuta ulioko mashariki, kama kawaida ya wakati
huu, kulifurahia joto tamu la jua la asubuhi. Ghaa, nilisikia sauti ikitokea
sehemu ya chini yapata kama mita mia nne hivi kutoka nilipokuwa nimesimama.
Sikuwa na wasaa wa kurudi na kuwajulisha waliokuwa jikoni: mama na
ndugu zangu wawili. Nilitimua mbio kuelekea upande ilikotokea sauti hiyo
ambayo sikuweza kujua kama ilitolewa na mtoto au mtu mzima. Baada ya muda
nilisimama tena ili kusikia kama nitaisikia sauti hiyo tena. Mara hii nilisikia
kelele nyingi, ‘Ondokeni njiani! Ondokeni njiani! Hatari! Hatari! Hatarii!” Ile
ilikuwa sauti ya mtu mzima sasa na lazima palikuwa na kitu cha kutisha.
Niligeuka kulia na kushoto na kuangalia mahali pa kujicha. Hapakuwa na
vichaka pale lakini kwa bahati nzuri palikuwa na mwembe uliokuwa mita kama
nne hivi, upande wa kushoto. Nilikimbilia huko na kuupanda mbio mbio; kwa kweli
sikuupanda bali niliuparaga kama nyani. Nilitafuta mahali pa kukaa na kujaribu
kuyaengua matawi ya mwembe huo ili nione upande wa chini kulikotokea ile
sauti. Niliweza kuwaona watu waliokuwa wakitimua mbio kuelekea upande wa
chini huko mbali. Hofu fulani ilinishika.
Niliangalia hapa na pale na kupanda juu mwembeni. Hatimaye, nilifanikiwa
kumwona ng’ombe aliyekuwa akikimbia kuelekea upande walikokuwa watu hao
ambao walipiga kelele nyingi ajabu. Labda zile kelele zilimfanya aibadili nia
yake na kuamua kushika njia iliyokuwa upande wa pili akaendelea kukimbia
mpaka akapotea kwenye upeo wa macho. Moyo wangu ulikuwa bado unarindima
kifuani; sikuthubutu kuteremka ingawa nilishangaa kwa nini watu walimkimbia
ng’ombe, labda fahali tu.
Niliteremka pale nilipomwona kakangu akitokea upande wa chini huku
ameshika mkongojo fulani. Hakuwa ameniona hadi niliposhuka chini naye
akanigeukia na kuniambia, “Una bahati kubwa sana wewe?”
“Ehh, nilisikia watu wakipiga kelele nami nikakwea mwembeni. Lakini
nilimwona yule ng’ombe!”
144
145
“Ng’ombe?” alisema kakangu kwa sauti ya juu iliyoonyesha mshangao
mkubwa.
“Ehh, si palikuwepo na ng’ombe mkubwa!”
Kakangu aliangua kicheko kwa muda. Nilishangaa kwa nini alicheka jinsi
hiyo. Hatimaye alisema kwa sauti imara, “Yule hakuwa ng’ombe kabisa bali
mbogo!” Moyo wangu ulipiga mara kadha. Kumbe niliponea chupuchupu hivyo?
Ilikuwa vyema kuwa niliamua kupanda mwembeni badala ya kuendelea kutembea
kuelekea walikokuwa watu. Nilikumbuka jinsi mama alivyotusimulia kumhusu
mnyama huyo mbaya. Hata hivyo, nilisikitika kuwa sikuweza kumkaribia na
kuiona sura yake vizuri.
Tulishika njia kuelekea nyumbani kusimulia kuhusu mbogo aliyepita
kijijini.
Zoezi
Andika insha inayoishia kwa maneno haya: tangu siku hiyo alikula yamini
kutoupuuza ushauri wa wazazi wake tena.
146
147
Sura ya Kumi na Tatu
A. Ufahamu
Uchafuzi wa mazingira
Uchafuzi ni hali ambapo vitu fulani au aina ya kawi hasi huongezwa kwenye
mazingira yetu kwa kasi ambayo inauzidi uwezo wa mazingira hayo wa
kupambana nayo. Uchafuzi ni tatizo la kijamii na matokeo yake huwahusisha
sio tu wanaoyatunza mazingira bali pia wananchi na raia wote wanaosakini
katika mazingira fulani. Ikiwa mazingira hayo yana uchafu fulani, lazima
uchafu huo utawaathiri wanaoishi pale. Kuna aina nyingi za uchafuzi wa
mazingira lakini katika kifungu hiki tunastahabu kuzungumzia aina mbili
tu: uchafuzi wa hewa na uchafuzi wa maji.
Je, ushawahi kutalii au kulizuru jiji fulani na kuona mawingu makubwa
yametanda juu ya jiji hilo kama mawingu ya mvua? Mawingu ya aina hii
hupatikana na kuonekana dhahiri shahiri wakati ambapo hamna upepo
unaopita unaoweza kuyasukumiza mbali. Siku kama hizo upepo huyapiga
mawingu hayo makubwa na kuyaeneza sehemu mbalimbali za jiji hilo.
Mawingu haya, ambayo ni tokeo la moshi wa viwandani pamoja na magari,
huwa ni kielelezo cha uchafuzi wa hewa. Wataalamu wanakisia kuwa
asilimia themanini ya vichafuzi vinavyopatikana hewani hutokana na moshi
unaotokana na kuchomwa kwa makaa, mafuta na fueli za kila aina. Vingine
hutokana na gesi za kila aina, majivu na vitu vingine vinavyosambazwa
na kuenea kwenye mazingira yetu. Asilimia kubwa ya vichafuzi hutokana
na moshi unaotokana na magari ambayo yamefurika furifuri katika majiji
makubwa.
Vichafuzi vingine
vya hewa ni vumbi ambalo
hutokana na
shughuli
na amali
mbalimbali
zinazotokea viwandani
au kwenye machimbo
ya madini.
Aidha,
unyunyiziaji
dawa za
mimea kama
viuawadudu
huweza
kusababisha
uchafuzi wa hewa kwa
sababu chembechembe
za dawa
hizo husambaa
na kupatana na
hewa
iliyopo. Nyingine
hupulizwa na upepo na kuenezwa sehemu pana. Ili tuweze kuielewa hatari
kuu ya uchafuzi wa hewa, inatubidi tujue jinsi unavyoweza kutuathiri sisi
tunaoishi katika mazingira hayo. Suala la kimsingi kutambua ni kuwa
Moshi kutoka kwenye magari makuukuu huchangia
uchafuzi wa hewa.
146
147
uchafuzi unafanya kazi na kuathiri polepole na kimyakimya. Uchafuzi
huathiri afya na upumuaji wa watu wengi; tunapopumua hewa ambayo
imejaa vichafuzi vya kila aina tunahatarisha afya zetu kwa kiasi kikubwa
mno. Uchafuzi pia husababisha kuwepo kwa kemikali inayojulikana kama
oksaidi; kemikali hii huathiri rangi za majengo, matofali ya kujengea na
hata mawe ya majengo. Hali hii husababisha kuharibika kwake haraka na
kuwalazimisha watu kufanya ukarabati wa mara kwa mara. Pili, uchafuzi
ulioko kwenye hewa huathiri mavazi au nguo zilizofuliwa na kuanikwa.
Tatu, uchafuzi wa aina hii huathiri mimea na wanyama katika mfumo wa
ikolojia. Aghalabu tunapochunguza mimea ikikua karibu na miji mikubwa,
tunaona kuwa huathiriwa na uchafuzi ulioko na kuishia hata kubadilika rangi
ikawa ya manjano. Nne, mchanganyiko wa uchafuzi pamoja na uharibifu wa
kimazingira unaishia kutishia uhai wa mimea, wanyama na ndege wengi
ulimwenguni. Uhai wa mimea, wanyama na ndege hao unaathiri mfumo
mzima wa ikolojia ambao binadamu wanautegemea. Mfano mmoja maarufu
wa madhara yanayotokana na uchafuzi wa mazingira ni kuzaliwa kwa watoto
wenye matatizo ya kiafya huko Hiroshima, nchini Japan na Chernobyl nchini
Urusi. Hali ya huko Hiroshima inatokana na bomu la atomiki lililoangushwa
huko wakati wa Vita Vikuu vya Pili na nchi ya Marekani. Janga la Chernobyl
linahusisha na uvujaji wa gesi mbaya uliotokea huko.
Je, na uchafuzi wa maji nao?
Hebu fikiria hali ambapo unaishi
karibu na mto unaopita karibu na
kiwanda kinachomwaga uchafu
wake
majini. Uchafu wa viwanda
unaotupwa kwenye mto huo
unaathiri mfumo ikolojia wa mto
huo. Aidha, uchafu huo unaweza
kuwa na madini kama risasi au zebaki
ambayo yana sumu ya kiwango cha
juu sana. Sumu hii inaendelea kukua
au kuongezeka kadiri uchafu huo
unavyoendelea kutupwa kwenye mto
huo. Aidha, kemikali zinazotokana
na dawa za kuulia wadudu au mbolea
za chumvichumvi huoshwa na maji
na kuishia kuchanganyika na maji
ya mto. Isitoshe, bidhaa za petroli
huweza pia kuishia kuyakia maji
ya mto au yaliyokusanyika karibu na
zinapochimbukia bidhaa hizo. Maji
hayo huishia kuka penye maziwa,
mabwawa au baharini ambako
maji yenyewe huishia kutumiwa na
binadamu. Asilimia kubwa ya dawa zinazotumiwa na binadamu zimeishia
Uchafu wa viwanda unaotupwa kwenye mto
unachangia uchafuzi wa maji.
148
149
kuzua uchafuzi wa maji ambayo huathiri mimea na viumbe wanaoishi mle
hususan samaki.
Uchafuzi wa baharini unaotokana na kuvuja kwa meli za mafuta
huathiri samaki na wanyama wengine wa baharini ambao huishia kufa.
Athari hizi huishia kutukia sisi binadamu. Suala la uchafuzi wa mazingira,
ni suala la kudararukiwa wala sio la kufanyiwa uzembe kwa kuwa linahusu
binadamu wote mahali popote walipo.
Maelezo ya msamiati
kawi : nguvu maalum au nishati.
wanaosakini : wanaoishi; wanaokaa; wanaofanya
maskani mahali fulani.
tunastahabu : tunapendelea.
husambaa : huenea.
ukarabati : utengenezaji wa kitu kilichoharibika ili
kukirudisha katika hali yake ya kawaida.
yamefurika furifuri : yamefurika kabisa.
mfumoikolojia : mahusiano na maingiliano ya viumbe
vyenye uhai katika mazingira vinamopatikana.
Maswali
1. Ni nini maana ya maneno ‘uchafuzi wa mazingira’?
2. Mawingu makubwa yanayotanda juu ya miji mikubwa husababishwa
na nini?
3. Asilimia kubwa ya vichafuzi vinavyopatikana hewani hutokana na nini?
4. Taja baadhi ya athari za uchafuzi wa hewa.
5. Wewe binafsi unaweza kuwashauri wenzako wafanyaje ili washiriki
katika uhifadhi wa mazingira?
6. Je, mtunzi ana maana gani asemapo kuwa ‘uchafuzi wa mazingira, ni
suala la kudararukiwa?’
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimu Jamii
Mazungumzo: Posta
(Posta. Njeru anaka akiwa na furushi mkononi. Mhudumu wa posta yuko
karibu na kidirisha cha kutolea huduma)
MhuduMu
: Habari za mchana?
njeru
: Hamna neno, vipi?
MhuduMu
: Salama. Nikusaidieje?
148
149
njeru
: Nina barua za kutuma hapa kisha nataka kutuma fedha
kwa hawala ya fedha.
MhuduMu
: Hebu nione hizo barua. (Njeru anatoa barua nne kwenye
lile furushi lake na kumkabidhi mhudumu. Anaziangalia.
Anachukua mbili na kuziweka juu ya mizani ya kupimia
uzito)
MhuduMu
: Hizi mbili zinahitaji shilingi sitini.
njeru
: Kwani stempu shilingi ngapi?
MhuduMu
: Thelathini kwa barua za nchini.
njeru
: Je, na hizo za nje?
MhuduMu
: Hizi ni shilingi mia kwa kila moja, jumla mia mbili.
njeru
: Lo! Naona tutashindwa kutuma barua.
MhuduMu
: Lakini nafuu barua; jaribu kuwapigia simu hawa walioko
Ulaya.
njeru
: Ehh, ngoma hiyo; hailipiki bei yake.
MhuduMu
: Unaona! Afadhali hizo barua. (Njeru anamkabidhi fedha
zinazohitajika. Anapewa stempu na barua zake pamoja
na fomu nyingine) Hiyo jaza kisha unikabidhi.
njeru
: Sawa. (Njeru anaelekea mahali pengine kujaza na
kuwapisha watu waliomfuata. Baada ya muda anarejea)
MhuduMu
: Tayari, ehh?
njeru
: Ndiyo nimejaza (anamkabidhi)
MhuduMu
: (akikagua) Sawa naona. Zi wapi hela zenyewe!
njeru
: (akimpa) Hizi hapa!
(Baada ya kumaliza mhudumu anamkabidhi Njeru hati
ya kuonyesha kuwa ametuma fedha)
njeru
: Fedha zitaka lakini?
MhuduMu
: Usiwe na hofu, zitaka tu.
njeru
: Haya kwaheri.
MhuduMu
: Kwaheri ndugu na karibu tena.
njeru
: Asante na siku njema.
Zoezi
1. Je, kwa nini Njeru alikwenda Posta?
2. Je, hawala ya fedha ni nini? Kwa nini hii ni njia nzuri ya kutuma pesa?
3. Je, ni nini kinachodhihirisha kwamba mazungumzo haya ni ya posta?
150
151
C Saru na matumizi ya lugha
1. Hali za -nge-, -ngeli-, na -ngali-
Viambishi -nge-, -ngeli- na -ngali- husimamia hali ambapo uwezekano wa
kitendo kimoja hutegemea kutendeka kwa kitendo kingine. Kwa mfano:
(a) Tungefanya mazoezi vizuri tungeshinda mchezo huo.
(b) Tungelifanya mazoezi vizuri tungelishinda mchezo huo.
(c) Tungalifanya mazoezi vizuri tungalishinda mchezo huo.
Sentensi hizi zinadhihirisha kuwa anayehusika hakufanya mazoezi vizuri
na kwa hivyo hakushinda. Kufanyika kwa kitendo cha pili kulitegemea
kufanyika kwa kitendo cha kwanza. Ni sharti kitendo cha kwanza
kingefanyika ili cha pili kifuate. Kwa vile hali haikuwa hivyo, basi kitendo cha
pili hakingetimilika. Viambishi hivi havibadilishani nafasi katika muktadha
fulani kwa vile ifanyikapo hivyo makosa ya kisaru hutokea. Kwa mfano:
(a) *Ningekuwa na pesa ningelinunua viatu.
(b) *Ningelikuwa na pesa ningalinunua viatu.
(c) *Ningalikuwa na pesa ningenunua viatu.
Viambishi hivi huweza kutokea katika wakati uliopo na uliopita.
Kukanusha hali za -nge-, -ngeli- na -ngali-
Kuna njia mbili za kukanusha vitenzi vya hali za -nge-, -ngeli- na -ngali-.
Katika njia ya kwanza, kiambishi -si- hutokea baada ya kiambishi awali cha
kitenzi. Haya hutegemea nafsi, umoja na wingi. Tazama jedwali lifuatalo:
Umoja Wingi
Nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
ningesoma nisingesoma tungesoma tusingesoma
ningeomba nisingeomba tungeomba tusingeomba
ningelihutubu nisingelihutubu tungelihutubu tusingelihutubu
ningalishiriki nisingalishiriki tungalishiriki tusingalishiriki
150
151
Umoja Wingi
Nafsi ya pili
ungesoma usingesoma mngesoma msingesoma
ungeomba usingeomba mngeomba msingeomba
ungelihutubu usingelihutubu mngelihutubu msingelihutubu
ungalishiriki usingalishiriki mngalishiriki msingalishiriki
Nafsi ya tatu
angesoma asingesoma wangesoma wasingesoma
angeomba asingeomba wangeomba wasingeomba
angelihutubu asingelihutubu wangelihutubu wasingelihutubu
angalishiriki asingalishiriki wangalishiriki wasingalishiriki
Zoezi
Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kukanusha vitenzi vilivyomo kwa njia
inayofaa.
Umoja Wingi
Nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
k.m. ningeingia nisingeingia tungeimba tusingeimba
ningeliruka tungeliruka
ningalicheza tungalicheza
Nafsi ya pili
ungeimba usingeimba mngeimba
ungeliruka mngeliruka
unaglicheza mngalicheza
Nafsi ya tatu
angeimba asingeimba wangeimba
angeliruka wangeliruka
angalicheza wangalicheza
152
153
Katika kuzingatia njia ya pili, viambishi si, hu, na ha hutumika kutegemea
nafsi, umoja au wingi. Tazama jedwali lifuatalo:
Umoja Wingi
Nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
ningesoma nisingesoma tungesoma tusingesoma
ningeomba nisingeomba tungeomba tusingeomba
ningelihutubu nisingelihutubu tungelihutubu tusingelihutubu
ningalishiriki nisingalishiriki tungalishiriki tusingalishiriki
Nafsi ya pili
ungesoma usingesoma mngesoma msingesoma
ungeomba usingeomba mngeomba msingeomba
ungelihutubu usingelihutubu mngelihutubu msingelihutubu
ungalishiriki usingalishiriki mngalishiriki msingalishiriki
Nafsi ya tatu
angesoma usingesoma wangesoma wasingesoma
angeomba usingeomba wangeomba wasingeomba
angelihutubu usingelihutubu wangelihutubu wasingelihutubu
angalishiriki usingalishiriki wangalishiriki wasingalishiriki
Zoezi
Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kukanusha vitenzi vilivyomo kwa njia
inayofaa:
Umoja Wingi
Nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
k.m. ningeruka singeruka tungeruka
ningelikimbia tungelikimbia
ningalilala tungalilala
Nafsi ya pili
ungeruka hungeruka mngeruka
ungelikimbia mngelikimbia
ungalilala mngalilala
Nafsi ya tatu
angeruka hangeruka wangeruka
angelikimbia wangelikimbia
angalikimbia wangalikimbia
152
153
2. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi ‘-ingineo’
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
-ingineo
a mwanafunzi mwingineo Mwanafunzi mwingineo atafanya
kazi hiyo.
wa wanafunzi wengineo Wanafunzi wengineo watafanya kazi
hiyo.
u mshipi mwingineo Mshipi mwingineo utanunuliwa.
i mishipi mingineyo Mishipi mingineyo itanunuliwa.
ya majira mengineyo Majira mengineyo yameanza.
ya majira mengineyo Majira mengineyo yameanza.
u ulezi mwingineo Ulezi mwingineo haufai.
ya malezi mengineyo Malezi mengineyo hayafai.
li kosa jinginelo Kosa jinginelo limetokea.
ya makosa mengineyo Makosa mengineyo yametokea.
ki kitanda kinginecho Kitanda kinginecho kitahitajika.
vi vitanda vinginevyo Vitanda vinginevyo vitahitajika.
zi fedha nyinginezo Fedha nyinginezo zitatumika kujenga
barabara.
ki kiu kinginecho Kiu kinginecho kimetokea.
li joto linginelo Jua linginelo litaharibu mahindi
yanayovunwa.
vi vitimbi vinginevyo Vitimbi vinginevyo havifurahishi.
Zoezi
1. Tumia nomino iliyomo mabanoni badala ya ile iliyoandikwa kwa heru
nzito.
k.m. Mbuzi mwingineo atanunuliwa. (kitabu)
Kitabu kinginecho kitanunuliwa.
(i) Mkate mwingineo umeletwa. (mikate)
(ii) Kikapu kinginecho kitatumika. (vioo)
(iii) Ugonjwa mwingineo umeanza. (michezo)
(iv) Virusi vinginevyo vitasababisha ugonjwa. (maji)
(v) Majira mengineyo yana shida. (ulezi)
(vi) Mwalimu mwingineo ataletwa. (manukato)
(vii) Wazee wengineo wataamua kesi hiyo. (mwalimu mkuu)
2. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuandika kiambishi cha kivumishi
‘-ingineo’ na kiambishi awali cha kitenzi.
154
155
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
pa mahali pengine Mahali pengine__ __mefunguliwa.
ku mahali kwingine Mahali kwingine__ __mefunguliwa.
mu mahali mwingine Mahali mwingine__ __mefunguliwa.
i ndoo nyingine Ndoo nyingine__ __natumika.
zi ndoo nyingine Ndoo nyingine__ __natumika.
ku kusoma kwingine Kusoma kwingine__ kunasaidia.
ku kusoma kwingine Kusoma kwingine__ kunasaidia.
u uchafu mwingine Uchafu mwingine__ __naudhi sana.
u uchafu mwingine Uchafu mwingineo__ __naudhi sana.
u ukurasa mwingine Ukurasa mwingine__ __mefunguliwa.
zi kurasa nyingine Kurasa nyinginezo __ __mefunguliwa.
D. Kusoma
Aina za kamusi
Huko nyuma tuliona matumizi ya kamusi na umuhimu wake. Katika sura hii
tutaangalia aina mbalimbali za kamusi ambazo hupatikana. Kuna kamusi
za aina mbalimbali. Aina hizi hutegemea idadi ya lugha ambazo zimetumiwa
katika kamusi moja, walengwa wa kamusi, mambo yanayoshughulikiwa
katika kamusi na ukubwa au upana wa kamusi inayohusika. Tuangalie
kamusi za aina mbalimbali:
(a) Kutegemea idadi ya lugha
i) Kamusi wahidiya: Hii ni kamusi yenye lugha moja. Maneno
yanayoingizwa kwenye kamusi (ambayo hujulikana kama vitomeo
au vidahizo) huwa ya lugha ile ile inayotumiwa kuyaelezea,
kwa mfano, kama ni lugha ya Kiswahili itakuwa hiyo hiyo
katika kamusi nzima. Kamusi ya aina hii humsaidia mtumiaji
kuukuza ujuzi wake katika lugha fulani moja. Mifano ni Kamusi
ya Kiswahili Sanifu (TUKI), Kamusi ya Kiswahili (F. Johnson),
Kamusi ya Maana na Matumizi ( S. Bakhressa) na kadhalika.
ii) Kamusi thaniya: Kamusi inayotumia lugha zaidi ya moja,
aghalabu mbili. Kwa mfano, maneno yanaweza yakawa ya
Kiswahili halafu yakaelezwa kwa Kiingereza au kupewa
visawe vyake kwa Kiingereza au kinyume chake. Hii ni kamusi
inayomsaidia mtumiaji kujua maneno katika lugha mbili tofauti.
Mifano ni Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza (TUKI), English-
Swahili Dictionary (TUKI), A Concise English-Swahili Dictionary-
R. A. Snoxall na H. B. Mshindo na kadhalika.
154
155
iii) Kamusi thulathiya: Hii ni kamusi ambayo inahusisha lugha
tatu. Maneno yanayopatikana yanapewa visawe vyake katika
lugha nyingine mbili.
(b) Kutegemea uwanja
i) Kamusi za istilahi: Hizi ni kamusi ambazo zinahusu uwanja
fulani maalum. Kwa mfano, kamusi zinazohusu somo fulani.
Hizi humsaidia mtumiaji kuongeza msamiati wake au kufahamu
maneno maalum ya uwanja huo maalum. Mifano ni Kamusi
Sanifu ya Isimu na Lugha (TUKI), Kamusi Sanifu ya Biolojia,
Fizikia na Kemia (TUKI), Kamusi ya Fasihi: Istilahi na Nadharia
(K. W. Wamitila).
ii) Kamusi za visawe au thesauri: Hizi ni kamusi ambazo huwa
na maneno pamoja na maneno yenye maana sawa na hayo au
yanayohusiana nayo. Kamusi za aina hii ni nzuri kwa kuupanua
msamiati wa mtumiaji wa kamusi. Mfano mzuri ni Kamusi ya
Visawe (S. A. Mohamed na M. Mohamed).
iii) Ensaiklopedia: Hizi ni aina za kamusi maalum zinazohusu
uwanja fulani maalum. Kwa kawaida kamusi hizi huwa na taarifa
nyingi sana kuhusu uwanja huo. Zipo ensaiklopedia za sayansi,
za lugha, za fasihi, za uchumi n.k. Kwa kawaida kamusi hizi
huwa na taarifa nyingi ambazo hazipatikani katika kamusi za
kawaida za lugha.
(c) Kutegemea walengwa
(i) Kamusi za wanafunzi: Hizi ni kamusi ambazo hulenga
wanafunzi wa kiwango fulani, wanaweza wakawa wa shule ya
msingi au wa sekondari au shule ya upili. Kamusi za aina hii
huwa na idadi ndogo ya maneno zikilinganishwa na kamusi za
kawaida ambazo hulengwa watumiaji wa kawaida wa lugha.
(ii) Kamusi za kawaida: Hizi ni kamusi za kawaida zinazopatikana
madukani na ambazo huwalenga watumiaji wa kawaida,
wanafunzi, wataalamu na wasiokuwa wataalamu. Kamusi ya
Kiswahili Sanifu ni mfano wa kamusi ya kawaida ya lugha.
Maswali ya marudio
1. Je, ukitaka kujua maana ya maneno haya, utaangalia katika kamusi
ya aina gani?
(a) kikwamizo, nazali , kipasuo, kimadende
(b) Tashbiha, sitiari, mhusika, hekaya
(c) biolojia, kimeng’enya, mbuti, utumbo
(d) chimney, circle, imitation
2. Je, ni kamusi za aina gani zinazopatikana shuleni?
156
157
E. Kuandika
Shajara
Shajara ni neno linalotumiwa kuelezea aina ya kitabu ambamo mtu huandika
matukio ya kila siku au mambo anayonuia kuyafanya. Kwa kawaida shajara
huwa na mpangilio wa tarehe, siku na hata mwaka. Kuna aina nyingine
ambazo huwa hata na sehemu ya saa mbalimbali kuanzia asubuhi (saa
moja hadi jioni). Kuna shajara ya kibinafsi, inayohifadhi matukio, maelezo
na mambo yanayomhusu mtu binafsi na shajara ya miadi ambayo aghalabu
hupatikana asini na huhifadhi miadi muhimu, saa, wakati na mahali pa
matukio. Shajara ya miadi huweza kupatikana hata shuleni.
Sifa na umuhimu wa shajara
(i) Huandikwa tarehe zenyewe, siku (Jumatatu, Jumanne, Jumatano)
n.k. ambazo huweza kutafsiriwa kwa lugha mbalimbali.
(ii) Huwa na sehemu ya kuandika matukio.
(iii) Aghalabu huandikwa mambo muhimu tu.
(iv) Huweza kuwa na orodha ya mambo ya maana ya kutekeleza siku
fulani, miadi ya kutimiza sehemu za kutembelea na kadhalika.
(v) Huweza kumsaidia mtumiaji kupanga matukio yake na kumkumbusha
ni mambo gani ya kufanya.
Mfano wa mpangilio wa shajara
Aprili, 1 2002
Jumatatu
Kwenda mjini (saa nne asubuhi)
Kununua mahitaji (Duka la Nguo)
Kupeleka barua posta
Kulipa bili ya umeme
Aprili 2, 2002
Jumanne
Mahojiano ya kazi (saa tatu asubuhi)
Kwenda marikiti na kadhalika.
Zoezi
Baada ya kuangalia mfano huu, andika shajara yako ya wiki moja ukiwa
shuleni.
156
157
Sura ya Kumi na Nne
A. Ufahamu
Runinga na ulimwengu wa leo
Siku moja tulikuwa hotelini kisiwani Lamu, au Amu kama wanavyokiita
wenyeji na rafiki yangu tukila wali kwa pweza. Aliingia mzee mmoja
aliyefahamika kisiwani kwa ugwiji wake wa masuala ya lugha ya Kiswahili.
Nilijiwa na hamu ya kumwuliza mzee huyo aliyetopea na kubobea katika
Kiswahili, jinsi neno ‘runinga’ lilivyozuka.
“Ahh, hilo?” alishangaa kwa sauti kabla ya kuendelea, ‘Kijana kaa
kitako nikweleze. Mswahili wa kwanza alipokiangalia kile chombo alishangaa.
Kilikuwa kinaeleza na kuweka wazi mbele ya macho yake habari za ajabu.
Hizi zilikuwa habari zilizotokea sehemu za mbali ambazo ni vigumu kujua
zilikotokea. Ni kitu kama uvumi hivi, huku kwetu tunasema ‘rununu’ basi ule
si wa kusikia bali ni wa kuona; yaani kwa macho ambayo zamani yaliiitwa
maninga. Basi ikawa rununu ya maninga; mwishowe runinga’ alieleza mzee
huyo kwa ufasaha mkubwa.
Kila ninapokiwazia chombo kinachojulikana kama runinga au
televisheni, kisa kile hufyatuka akilini na sura ya mzee huyo kunijia.
Tangu kuvumbuliwa kwake mwanzo mwanzo wa karne ya ishirini, runinga
imekuwa mojawapo wa vyanzo vikuu vya maarifa, taarifa, elimu na burudani
kwa watazamaji. Kutokana na chombo hiki tunapata picha za matendo
yanayotendeka kwenye maeneo yaliyoko mbali na tuishiko. Kinatuchulia
majanga yanayowafika wenzetu kutokana na mabaa ya vita au njaa;
huonyesha harakati za wanasayansi za kujaribu kuvumbua mambo mapya
kwenye anga zetu. Aidha, runinga hutusawiria matukio ya ulimwengu na
wakati huo huo yanapotokea yawe ni ya kusikitisha au ya kufurahisha.
Runinga ni nyenzo muhimu ya kutuelimisha na hata kutuburudisha kutokana
na vipindi vyake mbalimbali.
Vipindi vya runinga huwa ni ishara za elektroniki ambazo hutumwa
kama mawimbi ya redio na vyombo vinavyojulikana kama setilaiti au
kwa matumizi ya kebo ambazo hupitishwa ardhini. Setilaiti ina uwezo wa
kubadilisha ishara hizo na kuwa sauti na picha zinazoambatana na sauti hizo.
Je, ushawahi kuwazia ni mambo yepi yanatokea katika studio za
runinga hususan wakati wa kusomwa kwa taarifa ya habari? Aghalabu
wakati wa kusomwa kwa taarifa ya habari ni sehemu ndogo sana ya studio
inayoonekana. Asilimia kubwa huwa imechwa pamoja na mashine za kila
aina ambazo huhusika na uwasilishaji wa habari hizo. Aidha, wahudumu
wengine wanaohusika na majukumu mbalimbali kama udhibiti wa
mwangaza, uelekezaji wa wanaosoma kuhusu muda uliopo, mdhibiti wa
kamera zionyeshazo picha mbalimbali anayekuza picha kuhakikisha picha
zimeonekana vyema. Wapo wengine wanaoshughulika na majukumu anuwai
ambao hawaonyeshwi.
158
159
Mbele ya msomaji wa taarifa hizo huwa kuna televisheni ndogo ambayo
haionekani na ambayo humwonyesha picha zinazoonyeshwa. Aghalabu
hatuwaoni wasomaji wengi wa taarifa za habari wakisoma habari zao kutoka
maandishi wazi. Hali hii inatokana na kuwepo kwa kielekezi-runinga ambacho
anakitumia. Msomaji huyu husoma taarifa zake kutokana na maandishi
yanayoonekana kwenye mulishi au kiwambo cha kielekezi hicho. Maneno
hayo hukuzwa kwa njia mbili mbele ya lensi za kamera na kuweza kusomeka
vizuri. Yupo opareta ambaye kazi yake kuu ni kuhakikisha kuwa amedhibiti
kasi ya maneno yanayoonekana kwenye kielekezi-runinga hicho. Pia msomaji
anaweza kuongeza au kupunguza kasi ya maneno hayo kutegemea usomaji
wake akitumia kifaa maalum. Hata hivyo, msomaji huwa na nakala nyingine
ya habari iliyoandikwa anayoweza kuisoma iwapo pana hitilafu fulani ya
kielekezi-runinga.
Wataalamu wa chumba kikuu cha kuyadhibiti matangazo hutumia
vifaa maalumu vya sauti kuwakumbusha watangazaji kuhusu vipindi vya
kupumzika kwa ajili ya matangazo ya biashara au mabadiliko yoyote katika
mpangilio wa kipindi fulani. Huwapo pia wataalamu wanaohakikisha kuwa
picha zinazopatikana kwenye runinga ni sahihi na zinakubalika. Kutokana
na majukumu mbalimbali ya wanaohusika, watazamaji wanapata picha nzuri
na sauti zinazoaki picha hizo. Hii ni siri mojawapo ya siri nyingi ambazo
zimefumbatwa na uvumbuzi wa kisayansi.
Kama watazamaji wa runinga labda tunaishia kukubaliana na yule
mzee wa Lamu kuwa chombo hiki kina maajabu ya macho. Maajabu hayo
yanatuelimisha, kutujuza,
kutukumbusha na kutufanya
tushirikiane na wenzetu walio
mbali sana katika matukio
yetu. Masafa
yaliyoko kati
yao
yanafupishwa kwa kuwa
wanatujia kwenye vyumba
vyetu kama nasi tunavyofanya
huko kwao.
Maswali
1. Ni nini chanzo cha neno
‘runinga’?
2. Taja faida nne za runinga.
3. Tunaweza kutazama picha
za runinga kutoka kwenye vituo mbalimbali vya televisheni. Ni njia gani
inayotuwezesha kutazama vipindi vya runinga?
4. Wakati wa kusomwa kwa taarifa za habari kuna wataalamu mbalimbali
wanaohusika. Taja watatu.
5. Je, kwa nini mara nyingi msomaji wa habari haonekani kusoma habari
bali huongea akiangalia watazamaji tu?
158
159
6. Taja michezo miwili ya kimataifa iliyo maarufu zaidi inayotangazwa
moja kwa moja kupitia runinga kote ulimwenguni.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimu-jamii
Mazungumzo: Daktari na mgonjwa
(Chumbani mwa daktari. Daktari amevaa joho jeupe na amening’iniza
stetoskopu shingoni. Anaingia Mokaya)
dakTari
: Habari za asubuhi…Jina ni?
Mokaya
: Nzuri. Jina langu ni Mokaya.
dakTari
: Naam Mokaya, karibu ukae!
Mokaya
: Asante.
dakTari
: Haya, nieleze una shida gani?
Mokaya
: (Anashusha pumzi) Mmm…Nina maumivu ya kifua
halafu shida wakati wa kumeza chakula.
dakTari
: (Anachukua kifaa kidogo kinachofanana na tochi ndogo)
Hebu funua kinywa chako. (anafanya hivyo) Ehh tezi
zako zimevimba. (Anachukua kipimajoto kilichoko hapo
karibu) Hebu inua kwapa.
Mokaya
: (Kashangaa) Ni nini hii?
dakTari
: Nataka kujua joto lako tu. (Anakitia kile kipimajoto
kwapani. Baada ya muda anakitoa) Je, unakohoakohoa?
Mokaya
: Nilikohoakohoa majuzi lakini sasa sikohoi tena.
dakTari
: Je, chakula unakula vizuri?
Mokaya
: Nala vizuri tu.
dakTari
: Je, una shida nyingine yoyote?
Mokaya
: Sina.
(Daktari anarudi kitini na kuanza kuandikaandika)
Mokaya
: Nina nini daktari?
dakTari
: Shida ya kumeza inatokana na ugonjwa wa mandondo.
Huo hauna shida, unachohitaji ni dawa ya kiuavija na
tembe za kupunguza maumivu tu.
Mokaya
: Je, na kifua? Nina kichomi?
dakTari
: Siwezi kuwa na hakika kwa sasa. Kwanza, nataka
kukutuma kwenye maabara ya hospitali?
Mokaya
: Maabara?
dakTari
: Ehh, nataka wachunguze balaghamu au kohozi lako.
160
161
Mokaya
: Lina nini?
dakTari
: Kutokana na uchunguzi huo nitajua kuna shida gani.
Mokaya
: Nitadungwa sindano lakini?
dakTari
: Kwa nini unauliza?
Mokaya
: Kwa kuwa sipendi sindano; nastahabu tembe za kumeza.
dakTari
: (Akimkabidhi karatasi) Kwanza, peleka hii kwenye
maabara kisha ukirudi tutajua kama utahitaji kudungwa
sindano au la.
Mokaya
: Asante daktari.
dakTari
: Usiwe na hofu, utapona.
Maswali
1. Eleza maana ya maneno haya:
(a) Kipimajoto
(b) Mandondo
(c) Dawa ya kiuavija
(d) Kichomi
2. Taja sifa zinazodhihirisha kuwa mazungumzo haya ni sajili ya
hospitalini.
Matamshi bora : Vitate p/b
Soma maneno haya:
p b
pata bata
pango bango
pacha bacha
pania bania
pasi basi
papa baba
pana bana
punda bunda
panda banda
Zoezi
Chagua neno lifaalo kukamilisha sentensi zifuatazo:
1. Jana nilikwenda mtoni nikam_____ (bata, pata) yule ______ (bata, pata)
akiogelea.
2. Wanafunzi walipogoma walibeba ma_____ (bango, pango) kisha
wakatorokea kwenye ma________ (bango, pango) walipofukuzwa na
polisi.
3. Wale watoto ________ (pacha, bacha) wakiwa na watoto wengine
ma________ (bacha, pacha) walisoma vitabu vya hadithi kisha
wakaviweka kwenye ma________ (pacha, bacha).
160
161
4. Jana nili________ (pania, bania) kupata zile fedha lakini yule karani
bahili akazi________ (bania, pania) kabisa.
5. Siku ya Jumamosi nilipiga nguo zangu ________ (pasi, basi) kisha
nikakimbia kwenye kituo cha ma________ (pasi, basi) nikapanda ________
(basi, pasi) hadi mjini.
6. ________ (Baba, Papa) anapenda kuvua ________ (papa, baba) lakini
jana alipoenda baharini kuvua ________ (baba, papa) alimwona ________
(baba, papa) mkubwa kama ndovu akasema kamwe hatarudi tena kuvua
________ (baba, papa).
7. Mariamu alivaa blauzi inayom________ (pana, bana) sana lakini
nikamwambia si vyema kuvaa blauzi inayo________ (bana, pana) bali
ni vizuri kuvaa blauzi ________ (pana, bana) isiyo________ (bana, pana)
hata kidogo.
8. Abdul alibeba ________ (punda, bunda) la noti akanunue ________
(punda, bunda) lakini alipoka mjini akamwona yule ________ (bunda,
punda) akasema hawezi kununua ________ (bunda, punda) aliyekonda
hivyo na kwa hivyo akarudisha ________ (punda, bunda) lake mfukoni.
9. Watu wawili wali________ (banda, panda) ________ (banda, panda)
la Banda ili wakaibe ________ (panda, banda) lakini Bwana ________
(Banda, Panda) alipowaona akawaambia ________ (panda, banda) lake
hali________ (pandwi, bandwi) na watu wasiojua ku________ (panda,
banda) ma________ (panda, banda).
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Kuakisha
(i) Kistari kifupi (-)
Hutumika katika mazingira yafuatayo:
(a)kuonyesha kuwa neno linaendelea katika mstari wa pili. Kwa mfano:
(i) Jana tulikwenda uwanjani kuji-
onea mchezo wa kandanda.
(ii) Kiswahili ni lugha inayotumiwa na wana-
nchi wengi hapa Afrika ya Mashariki.
(iii) Shule zote za upili hapa wilayani zitanu-
faika kutokana na msaada wa kifedha utakaoto-
lewa na Jumuiya ya Madola.
Alama hii inapotumika hivyo, neno hukatwa mwishoni mwa silabi.
Lisipokatwa hivyo huwa ni makosa ya kisaru.
(b) Kuonyesha silabi za maneno; kwa mfano:
(i) ma-ne-no (ii) m-cha-ngo (iii) ki-to-we-o
(iv) cha-nga-ra-we (v) ki-zi-ngi-ti
162
163
(c) Kudokeza jambo kuhusu neno, kama vile mzizi. Kwa mfano:
(i) -eupe (ii) -eusi (iii) -enyewe (iv) -toto (v) -ingine
(d) Kutenganisha maneno ambatano. Kwa mfano:
(i) elimu-viumbe (ii) isimu-jamii
(e) Kudumisha sauti. Kwa mfano:
(i) masala-a-a-le!
(ii) Niliteleza mara moja chwa-a-a-a!
(f) Kuonyesha kipindi cha muda fulani. Kwa mfano:
(i) 1910-1920 (ii) 1949-1959 (iii) 1956-1960
(g) Kuonyesha aina za maneno yanayoandikwa kwa vitengo; kwa mfano:
(i) Shangazi anapika muhogo wa aina ya ‘binti-Athmani’.
(ii) Mpunga wa aina ya ‘tule-na-bwana’ unapendwa sana huko
kwetu.
(iii) Nyanya amepanda ndizi za aina ya ‘mkono-wa-tembo’.
(ii) Kistari kirefu (–)
Kistari kirefu hutumika katika mazingira yafuatayo:
(a) Kutanguliza usemi au maelezo. Kwa mfano:
(i) Wachezaji wa Kenya wa mpira wa kriketi – wale wote
waliochaguliwa hivi majuzi – wameondoka kuelekea Afrika
Kusini.
(ii) Nataka unirudishie vitu vyangu vyote – kiti, kabati, meza na
vingine vyote ulivyochukua jana.
(iii) Mali ya mwalimu wetu – yale yote yaliyoibiwa hivi majuzi
baada ya nyumba yake kuvamiwa na wezi – yamepatikana
huko mtaani Kariobangi.
Zoezi
Tumia kistari kirefu (–) au kifupi (-) mahali pafaapo kwenye sentensi
zifuatazo:
(a) Vita vya kwanza vya dunia vilitokea kati ya mwaka 1914 1918.
(b) Vita hivyo vilifuatiwa na vingine vilivyotokea kati ya mwaka 1939
1945.
(c) Mzee Jomo Kenyatta aliishi kati ya mwaka 1889 1978.
(d) Mimi niliamua kupaka nyumba yangu rangi ya aina ya damu- ya-
mzee.
(e) Watu wote waovu wezi, wauaji na wengine kama hao wanafaa
kutumbukizwa gerezani maisha.
(f) Rais amewafuta kazi mawaziri watatu Bw. Karanja, Bi. Akunda na
Bw. Adhola.
162
163
(iii) Kupigia mstari (_________)
Maneno hupigiwa mstari ili kuonyesha mambo kadhaa, kwa mfano:
(a) Kuonyesha anwani ya kitabu, gazeti, jarida n.k (pale ambapo
tunaandika kwa hati ya mkono).
(i) Ufahamu wa Lugha ya Kiswahili ni kitabu chenye mafunzo
mengi ya ufahamu kwa Kiswahili.
(ii) Jana nilinunua majarida ya Mulika, Times na Newsweek.
(iii) Kimbia dukani ukaniletee magazeti ya Daily Nation, E.A.
Standard na Daily News.” mama aliniambia.
(b) Kutilia mkazo neno au fungu la maneno; kwa mfano:
(i) Nimecha pesa mvunguni mwa kitanda.
(ii) Wezi walituvamia saa tisa usiku.
(iii) Waziri alichangisha kiasi cha shilingi milioni moja na laki sita.
2. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi -ingineo
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
-ingineo
i meza nyingineyo Meza nyingineyo itatumika.
zi meza nyinginezo Meza nyinginezo zitatumika.
u ukora mwingineo Ukora mwingineo umeanza.
u ukora mwingineo Ukora mwingineo umeanza.
u waraka mwingineo Waraka mwingineo umetumwa.
zi nyaraka nyinginezo Nyaraka nyinginezo zimetumwa.
ku kupigana kwingineko Kupigana kwingineko kunafaa nini?
ku kupigana kwingineko Kupigana kwingineko kunafaa nini?
pa mahali penginepo Mahali penginepo patafunguliwa.
ku mahali kwingineko Mahali kwingineko kutafunguliwa.
mu mahali mwinginemo Mahali mwinginemo mtafunguliwa.
Zoezi
Tumia kivumishi mwafaka badala ya kile kilichoandikwa kwa heru nzito.
1. Nyembe ingineyo itatumiwa.
2. Mbao nyingineyo zitapigiliwa misumari.
3. Mahali penginepo mmefagiliwa.
4. Ufagio mwinginemo uko wapi?
5. Nyakati nyingineyo zinafaa.
164
165
6. Dawa nyingineyo zitatumiwa.
7. Eropleni nyinginezo itaondoka.
8. Ufunguo mwingineyo umevunjika.
9. Mahali kwingineo kumefunguliwa.
10. Ugali mingineyo utapikwa.
3. Ukubwa na udogo katika nomino
Muundo wa nomino ya ukubwa hutegemea mzizi wa nomino inayohusika.
Ukubwa katika nomino
Mbali na hali ya wastani na ya udogo, nomino za Kiswahili huweza kutokea
katika hali ya ukubwa vile vile. Muundo wa nomino hizi hutegemea mzizi
wa nomino zenyewe.
Ikiwa mzizi wa nomino unaanza kwa irabu, kiambishi cha umoja huwa
ji (au j). Katika wingi, nomino huanza kwa kiambishi ma au mi kikitangulia
kiambishi ji (au j). Licha ya kuonyesha ukubwa, nomino hizi pia huweza
kuonyesha hali au tabia. Tazama jedwali lifuatalo:
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za ukubwa
Umoja Wingi Umoja Wingi
-ti mti miti jiti majiti/mijiti
-su kisu visu jisu majisu/mijisu
-ke mke wake jike majike/mijike
-bwa mbwa mbwa jibwa majibwa/mijibwa
Hata hivyo, baadhi ya nomino zenye mizizi ya zaidi ya silabi moja huweza
kutokea bila kiambishi ji cha umoja lakini huwa na kiambishi ma cha
wingi. Kwa mfano:
Mzizi wa nomino Nomino ya wastani Nomino ya ukubwa
Umoja Wingi Umoja Wingi
-buzi mbuzi mbuzi buzi mabuzi
-paka paka paka paka mapaka
-jia njia njia jia majia
-guo nguo nguo guo maguo
Udogo katika nomino
Ikiwa mzizi wa nomino umeundwa kwa silabi mbili au zaidi, viambishi
ki- (katika umoja) na vi-katika wingi hutokea mwanzoni mwa nomino.
Tazama jedwali lifuatalo:
164
165
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za udogo
Umoja Wingi Umoja Wingi
-fupa mfupa mifupa kifupa vifupa
-to uto to kito vito
-gari gari magari kigari vigari
-duka duka maduka kiduka viduka
-shamba shamba mashamba kishamba vishamba
-boga mboga miboga kiboga viboga
-dawa dawa dawa kidawa vidawa
Hata hivyo, kiambishi ji-huweza kutokea baada ya viambishi ki-na vi-
kuonyesha hali ya udogo, ya kudunisha au ya dharau. Tazama jedwali
lifuatalo:
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za udogo
Umoja Wingi Umoja Wingi
-fupa mfupa mifupa kijifupa vijifupa
-to uto to kijito vijito
-kuta ukuta kuta kijikuta vijikuta
-duka duka maduka kijiduka vijiduka
-shamba shamba mashamba kijishamba vijishamba
-boga mboga mboga kijiboga vijiboga
-dawa dawa dawa kijidawa vijidawa
Ikiwa mzizi wa nomino unaanza kwa irabu au umeundwa kwa silabi
moja, nomino ya udogo huanza kwa viambishi ki-na vi-vikifuatiwa na
ji- (au j). Tazama jedwali lifuatalo:
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za udogo
Umoja Wingi Umoja Wingi
-we jiwe mawe kijiwe vijiwe
-cho jicho macho kijicho vijicho
-ti mti miti kijiti vijiti
-su kisu visu kijisu vijisu
-ke mke wake kijike vijike
166
167
D. Kusoma
Usomaji wa kina: Riwaya
Huko nyuma tumeona kuwa kuna mambo mawili makuu ya kuchunguza
tunaposoma riwaya: MAUDHUI na FANI. Katika sura hii, tutaangalia
MAUDHUI kwa kina. Tuliona kuwa MAUDHUI ni jumla ya mambo au
masuala yanayozungumziwa katika kazi fulani ya kifasihi. Tuangalie mambo
yanayojenga maudhui:
1. Dhamira: Dhamira ni lengo la mwandishi wa riwaya, yaani ameandika
kazi hiyo kwa sababu gani? Ni jambo gani ambalo anataka msomaji
wake alielewe baada ya kusoma riwaya hiyo? Aghalabu dhamira hii
inajengwa kwa kuangalia ni jambo lipi linalokuzwa kuanzia mwanzo
mpaka mwisho. Wakati mwingine, tunatumia anwani ya kitabu kuijua
dhamira ya mwandishi, kwa mfano, riwaya ya Mui huwa Mwema
ina dhamira ya kuonyesha kuwa wema unashinda ubaya au mbaya
huweza kubadilika na kuwa mwema. Kwa upande ule mwingine,
dhamira ya Yatima ni kuonyesha dhiki zinazowakumba watoto wa
kike wanaolazimishwa kuajiriwa wakiwa wadogo.
2. Ujumbe: Riwaya zote huwa na ujumbe ambao wasomaji wanaupata
wanapozisoma. Ili dhamira ya mwandishi itimie, mwandishi hutoa
taarifa fulani kwa wasomaji wake. Taarifa hizo zinaweza kuwa wazi au
ziwe zimechika na ndizo zinazojulikana kama ujumbe. Kwa mfano,
ujumbe wa riwaya Mui huwa Mwema ni kuwa hakuna asiyeweza
kuigeuza tabia yake, tusikate tamaa kuihusu hali yoyote mbaya.
3. Falsafa: Neno hili hutumiwa kuelezea mawazo makuu aliyo nayo
mwandishi kuyahusu maisha. Tunaijua falsafa ya mwandishi kwa
kuisoma kwa makini riwaya au kazi ya fasihi aliyoiandika. Falsafa
huhusiana na MSIMAMO, yaani mwandishi ana maoni gani kuhusu
jambo fulani.
Maswali
1. Eleza maana ya dhamira. Je, kuna tofauti gani kati yake na maudhui?
2. Baada ya kuisoma riwaya yoyote ile, eleza maudhui makuu katika riwaya
hiyo.
E. Kuandika
Imla
Imla ni hali ambapo mtu anasikiliza maneno, sentensi au vifungu vya maneno
yanayosemwa au kusomwa na mtu mwingine kwa lengo la kuyaandika
166
167
kulingana na vile alivyoyasikia. Imla hutumika kuimarisha ujuzi wa
kusikiliza na kuandika.
Ili kuweza kuandika imla kwa njia mwafaka, mwandishi anafaa
kuzingatia mambo yafuatayo:
Awe msikivu. Ni lazima awe na makini sana katika kusikiliza
yanayosomwa ili ayaelewe vizuri.
Aandike aliyoyasikia bila kubadilisha chochote.
Azingatie alama za kuakisha kama vile nukta, kikomo, n.k.
Atumie hati sa ili kazi yake iweze kusomeka kwa urahisi.
Aandike maneno na mawazo kwa mfululizo kama alivyoyasikia.
Zoezi
Andika sentensi utakazosomewa na mwalimu katika daftari lako kwa usahihi
na kwa hati nadhifu.
168
169
Sura ya Kumi na Tano
A. Ufahamu
Mwabusara na siri kali
Mwabusara alijulikana kwenye kata nzima ya kwao kutokana na msimamo
wake mkali kuihusu serikali ya nchi yake. Watu wanasema kuwa hakuwa
hivi zamani hasa baada ya nchi yake kuupata uhuru kutoka kwa utawala
wa ki-istiimari. Siku hizo kama raia mwingine yeyote, Mwabusara alikuwa
na matumaini makubwa kwa serikali yake aliyoionea fahari na kuipenda
kama mboni yake ya jicho. Lakini wanasema kuwa hali ilibadilika wakati
wafanyakazi wa serikali ya Mwafrika yenyewe walipomshangaza Mwabusara
kwa vituko vyao vingi. Vilianza na jirani yake aliyekuwa na nafasi kubwa
serikalini. Huyu alimnyang’anya kipande chake cha ardhi alichorithi kutoka
kwa babu yake. Alipolalamika, jirani yake huyo alidai kuwa ilikuwa ardhi
yake. Mwabusara alipobisha sana, jirani huyo alikuja na kipande cha
karatasi. “Ni nini hiki?” aliuliza Mwabusara alipoonyeshwa kipande hicho.
‘‘Mzee, hiki ni cheti cha kuonyesha kuwa hii ardhi ni yangu…”alisema
jirani yake.
Mwabusara alipigwa na mughma, “Yamekuwaje ya kuwa hapa? Je,
kaandika marehemu babu nini?”aliuliza kwa mshangao mkubwa.
“La, Mzee hiki ni cheti cha serikali na kina siri kali; hamna wa kuweza
kuifuta,” alisema jirani huyo. Mwabusara alililia kipande chake cha ardhi
lakini ikawa hakuna aliyemsikiliza; alimpiga dua jirani yake lakini ikawa
ni dua ya kuku isiyompata mwewe.
Mwabusara aliendelea kulima kikataa chake kidogo huku akiungulika
ndani kwa ndani. Sasa serikali aliyoidhani kuwa itamfaidi yeye na watu wa
kufu yake haikufanya hivyo. “Kumbe inacha siri kali tu; siri ya kuwalinda
walio na mali tu?”alisema Mwabusara.
Tukio la pili lililomkuta Mwabusara linahusiana na ng’ombe wake
mmoja. Alikuwa mtamba mwenye afya nzuri aliyemshughulikia kama mtoto
wake. Inasemekana kuwa kulikuwa na mkutano ulioitishwa na chifu wa eneo
la kwao. Mwabusara hakuwa na uwezo wa kuuponda wa si mpaka ulikokuwa
mkutano wenyewe umbali wa kilomita tano hivi. Aliamua kujikalia zake
nyumbani lakini siku mbili baadaye yule mtamba wake alisombwa kwa amri
ya chifu. Mwabusara alipigwa na butwaa. Alipouliza alijulishwa, Ni amri
ya serikali ili kuwahimiza watu wahudhurie mikutano yake, na kumbuka
serikali ina siri kali.”
Uchungu aliokuwa nao Mwabusara uliongezeka na kuanza kupanda
kama zebaki kwenye kipimajoto. Siku aliposikia kuna uchaguzi unaojongea,
Mwabusara alishangaa na kuulizauliza umuhimu wake. Alielezwa kila kitu
na mjukuu wake aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule
ya upili ya Twajiweza. “Babu tunapiga kura kuichagua serikali nyingine,”
alisema mjukuu wake.
168
169
“Je, serikali hiyo itakuwa na siri kali?” aliuliza Mwabusara na kumfanya
mjukuu wake aachame kwa kukosa jibu. Lakini alikiri kwa muda kabla
ya kumwambia babu yake, “Babu, tutaamua wenyewe kama ina siri kali!”
Basi Mwabusara alikata kauli kushiriki kwenye maamuzi hayo pamoja na
wengine waliokuwa na machungu kama yake.
Uchaguzi ulikuja na kupita. Serikali mpya ilichaguliwa. Mwabusara
naye alikuwa tayari kusimama tisti mara hii. Ili kuuimarisha uwezo wake
wa kujitetea, aliamua kupata ushauri kutoka kwa mjukuu wake. Mjukuu
wake alipoka, Mwabusara alimwambia kwa sauti imara, “Mjukuu wangu
nataka uniambie hiyo serikali inapaswa kufanya nini. Mara hii sitaki inijie
na siri kali zake!” Mjukuu naye akatulia na kuanza kumwelimisha babu yake.
“Babu,” alianza mjukuu wake na kuendelea, “mwalimu alisema serikali
inapaswa kuhakikisha kuwa kuna sheria; yaani kanuni ambazo zinafuatwa
na kila mtu. Hufanya hivi kuhakikisha kuwa hakuna mtu anayeteswa wala
kupokonywa mali yake.”
“Kama yule mtamba wangu?” akauliza Mwabusara.
“Ndiyo, babu!” akamjibu mjukuu wake. Mwabusara aliangalia chini
kisha akauliza,
“Au kama kile kipande changu cha ardhi?”
“Ndiyo babu!” Baada ya jibu hilo akamwambia mjukuu wake aendelee
kumweleza mengi.
“Huhakikisha kuwa wanaokwenda kinyume na hayo wameadhibiwa kwa
sheria zinazokubalika na kila mtu nchini. Huweza kuadhibu kwa kifungo au
kulazimisha kurudisha alichochukua.” Mwabusara aliitikia na kumhimiza
mjukuu aendelee. “Serikali huwa na njia za kusuluhisha migogoro katika jamii;
migogoro hiyo inaweza kuwa ya mali, urithi, ndoa, madeni n.k. kwa kutumia
mahakama,” alieleza mjukuu. Mwabusara akaitikia tu. “Serikali huhakikisha
kuwa wananchi wanapata huduma za kila aina kama maji, vituo vya afya na
170
171
barabara za kutosha. Kwa ufupi babu, serikali inalinda raia wake wote kama
inavyostahili,” alimalizia mjukuu.
Mjarabu wa kumaliza maelezo yake, Mwabusara alichukua mkongojo
wake na kuelekea kwenye osi ya chifu. Njia nzima alitembea kwa hatua za
nia. Mjukuu wake alimfuata nyuma akijitahidi kumkia. Chifu alipomwona
ameandamana na mjukuu wake alishangaa. Mwabusara alijitoma osini kwa
chifu na baada ya salamu akasema, “Nimeijua!”
“Nini?” akauliza chifu kwa mshangao mkubwa. “Siri kali ya serikali!”
Chifu aliangalia huku na kule.
Mwabusara akauliza, “Si serikali inalinda raia wake?”
“Ndiyo inalinda!” akaitikia chifu.
“Si serikali inaadhibu wanaokosa?” akauliza Mwabusara.
“Ndiyo inawaadhibu!” akaitikia Chifu. Mwabusara alitabasamu na
kumwuliza mjukuu wake,
“Si serikali ina vitu vinavyojulikana kama mahakama?”
“Ndiyo babu,” mjukuu akahakikisha. Mwabusara akamgeukia chifu,
“Hiyo ndiyo siri kali nisemayo. Kipande changu cha ardhi nirudishiwe na
mtamba wangu naye nirudishiwe. Lau sivyo, nitachua siri kali kwa serikali!”
Chifu akapotewa na maneno.
Haikuchukua muda mrefu, Mwabusara akanunuliwa ng’ombe wa gredi
na chifu. Jirani yake naye akaanza harakati za kuandaa karatasi nyingine
yenye siri kali ili kurudisha kipande cha ardhi cha Mwabusara. Tangu siku
hiyo, wazee wa kata hiyo wakambatiza Mwabusara ‘mwalimu’ kutokana na
uzindushi na elimu aliyowapa kuhusu siri kali ya serikali. Wengi wa wale
waliokuwa wamenyang’anywa mali yao wakarudishiwa. Mjukuu wake naye
akawa chanzo cha mabadiliko makubwa katika eneo hilo.
Maelezo ya msamiati
kufu yake : aina yake.
alisombwa : alichukuliwa.
aachame : afungue kinywa kwa mshangao.
Maswali
1. Ni kwa nini Mwabusara alibadilika na kuwa na msimamo mkali dhidi
ya serikali?
2. Je, unadhani kwa nini Mwabusara hakuuona umuhimu wa uchaguzi?
3. Ni kwa nini Mwabusara alishika njia kuelekea kwa chifu baada ya
maelezo ya mjukuu wake?
4. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika kwenye kifungu
kisha uyatumie kutungia sentensi:
5. (a) ki-istiimari (b) mughma (c) akiungulika (d) mjarabu
(e) mtamba (f) kipimajoto (g) zebaki
6. Eleza maana ya misemo ifuatayo kulingana na matumizi yake kwenye
kamusi kisha uitumie kutungia sentensi:
170
171
(a) alimpiga dua (b) kuuponda wa si (c) alipigwa na butwaa
(d) alikata kauli (e) kusimama kidete
7. “Uchungu aliokuwa nao Mwabusara uliongezeka na kuanza kupanda
kama zebaki kwenye kipimajoto.” Maneno yaliyoandikwa kwa heru za
mlazo ni mfano wa tashbihi. Kamilishi tashbihi zifuatazo kwa kuchagua
vimalizio vifaavyo:
machozi ya ngamia, pamba, punda, uzi, maziwa ya kuku
(a) Laini kama _______________.
(b) Embamba kama _______________.
(c) Kaidi kama _______________.
(d) Adimika kama _______________.
(e) Tiririka kama machozi ya _______________.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Maigizo
Neno maigizo hutumiwa kuelezea utanzu mmojawapo wa fasihi simulizi.
Maigizo huelezea tungo zenye mpangilio wa maneno na ambazo huhusisha
watu wanaotenda, au kuigiza mbele ya watu wanaotazama yaani hadhira.
Msingi wa maigizo ni nia ya kuyaiga matendo mbalimbali ya kijamii kwa lengo
la kutumbuiza, kufunza, kuchekesha, kuelimisha n.k. Maigizo yanaweza
kuambatana na nyimbo au uimbaji au yasiambatane na uimbaji huo, yaani
yawe maneno tu yanayosemwa na wahusika. Utanzu huu una vitawi vingine,
yaani vipera kama ngonjera, vichekesho, michezo ya kuigiza na majigambo.
Je, ni mambo gani yanayozingatiwa kuhusiana na maigizo?
(i) Kuwapo kwa hadhira ambayo inayatazama maigizo hayo.
(ii) Kuwapo kwa watu au wahusika ambao wanayaigiza matendo
yenyewe.
(iii) Kuwapo kwa mahali ambapo maigizo hayo yanafanyika,
jukwaani au mahali wazi.
(iv) Kuwapo kwa mavazi yanayohusishwa na wahusika, yaani
wahusika wanavaa mavazi fulani ambayo yanawasaidia
kuuwasilisha ujumbe wao vizuri zaidi. Mavazi haya huitwa
maleba.
Mfano wa maigizo Ngonjera
Someni ngonjera hii na mjaribu kuiigiza darasani.
Mwajiriwa
: Limekucha sasa jua, nimetoka na gizani,
Haki zangu nazijua, ‘tasema nataka nini,
Mzigo huu najitua, ya jana yamo kapuni,
Vifaa naweka chini, kazi leo nagomea.
172
173
Mwajiri
: Hayo unayoyanena, hapa hayatakikani,
Ni hatia kubwa sana, kabisa iso kifani,
Mambo yaso na maana, kayasikia na nani,
Vifaa kuweka chini, wajitosa taabani.
Mwajiriwa
: Malipo ninayopata, si pesa ni mapeni,
Maisha yangu ni mwata, hayaniishi madeni,
Shida zinaniambata, kwa wangu umaskini,
Vifaa naweka chini, kazi leo nagomea.
Nitazame mwili wangu, sinayo siha mwilini,
Haitoshi kula yangu, kwa kuwa sina mapeni,
Ni mararu nguo zangu, nachekwa kiwa njiani,
Vifaa naweka chini, kazi leo nagomea.
Mwajiri
: Uchumi ’meharibika, kote kote duniani,
Hata huko Amerika, walia nifanye nini,
Kuache kulalamika, uchangamke kazini,
Vifaa kuweka chini, wajitosa taabani.
Maguo ya kujivika, sio lazima mwilini,
Mararu kujifunika, si fedheha mwafulani,
Mradi wanufaika, na malipo hatimani,
Vifaa kuweka chini, wajitosa taabani.
Mwajiriwa
: Kwa miaka na dahari, natumika kiwandani,
Silioni lenye heri, kwa nguvu za muilini,
Inaniandama shari, nyumbani hata kazini,
Vifaa naweka chini, sitaki tena utani.
Mwajiri
: Basi tuache hasira, isiongoze njiani,
Tuitumie busara, tuketi sisi thenini,
Bila hata ya papara, tupime kwenye mizani,
Vifaa siweke chini, sote tuwe taabani.
Maswali ya marudio
1. Je, maigizo ni nini?
2. Ni mambo gani ya kuzingatiwa katika maigizo?
3. Eleza dhamira ya ngonjera uliyoisoma.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Vitenzi
Vitenzi ni maneno yanayoarifu kuhusu jambo lionalotendwa au kutendewa
nomino. Kwa mfano kulima, kufagia, kukopa, kuogelea na kadhalika Kwa
mfano:
(a) Selemani analala.
172
173
(b) Binamu yangu atawasili kesho.
(c) Mpwa wake Makokha anaishi Bungoma.
(d) Mimi nitamwandikia dadangu barua.
(e) Jana tulicheza mpira wa vikapu.
Aina za vitenzi
Vitenzi huweza kugawika katika makundi mawili makuu:
(i) Vitenzi halisi (T)
(ii) Vitenzi vishirikishi (t)
(i) Vitenzi halisi (T)
Vitenzi halisi huarifu kuhusu jambo linalofanywa au kufanyiwa nomino.
Kwa mfano:
(a) Mama amekwenda kondeni.
(b) Panya ameshikwa na paka.
(c) Nyoka amemuuma ngamia yule.
(d) Kitabu chake kimeraruka.
(e) Wakulima wamevuna mahindi mengi.
Kitenzi halisi huweza kutokea katika mfululizo wa kitenzi sambamba
ambapo kimoja huwa ni kitenzi kikuu (T) na vingine ni vitenzi visaidizi (Ts).
Katika mfululizo huu, kitenzi kikuu hubeba maana kuu ya kitendo
nacho kitenzi kisaidizi huonyesha wakati wa kutendeka kwa kitendo, kama
kitendo ni yakinishi au kanushi, kauli ya kitenzi n.k. Kwa mfano:
(i) Jana asubuhi nilikuwa nikiandika barua.
Ts T
(ii) Kaloki alikuwa anataka kunishambulia.
Ts T
(iii) Mwanafunzi anapaswa kusoma kwa bidii.
Ts T
(iv) Sungura wangu angali anakula majani.
Ts T
(v) Sisi tumewahi kutembelea mji wa Dar es salaam.
Ts T
Maneno yanayoweza kutumika kama vitenzi visaidizi si mengi. Ni kama
yafuatayo: kwisha, pasa, taka, wahi, bidi, ngali, enda, kuja, weza, na kuwa.
(ii) Vitenzi vishirikishi (t)
Hivi ni vitenzi vinavyoshirikisha vitu kihali, kitabia au kimazingira. Kwa
mfano:
174
175
(a) Yeye ndiye mwalimu mkuu wa shule yetu.
(b) Mimi ni mwanafunzi wa kidato cha pili.
(c) Sisi tu wanafunzi wenye bidii na nidhamu.
(d) Yeye yu mwanamichezo mwenye ujuzi mwingi.
(e) Mariana si msichana mjinga!
Vitenzi vishirikishi ni vya aina mbili:
(a) Vitenzi vishirikishi vikamilifu
(b) Vitenzi vishirikishi vipungufu
(a) Vitenzi vishirikishi vikamilifu
Hivi vinaweza kuchukua viwakilishi nafsi au viambishi vya ngeli na pia
viambishi vya wakati. Ni maneno kama: weza, kuwa, kwisha, kuja, taka,
ngali, pasa, bidi, pata, na kwenda. Kwa mfano:
(a) Rais amekuwa ziarani Marekani.
(b) Polisi walikuwa wangali kwenye kituo hicho.
(c) Mtoto huyu anapaswa kuwa shuleni.
Vitenzi vishirikishi vikamilifu mara nyingine huweza kutokea kama
vitenzi visaidizi iwapo vinatokea sambamba na kitenzi kikuu. Tazama
sentensi zifuatazo:
(i) Baba alikuwa mkulima.
t
(ii) Baba alikuwa analima.
Ts T
(iii) Kakangu alikuwa angali anacheza.
Ts Ts T
(iv) Kakangu alikuwa angali mchezaji.
t t
(b) Vitenzi vishirikishi vipungufu
Vitenzi hivi haviwezi kuchukua viambishi vya wakati ingawa vinaweza
kuchukua viwakilishi nafsi viambata au viambishi ngeli. Navyo ni vifuatavyo:
ni, si, ndi, li na viwakilishi nafsi viambata visimamapo peke yake. Kwa mfano:
(a) Muthoni ni mwanafunzi hodari.
(b) Mimi ndimi kiongozi wa kijiji hiki.
(c) Wewe u mwananchi wa Tanzania.
(d) Ng’etich si mkulima shupavu.
(e) Kikombe ki mezani.
174
175
Zoezi
Ukitumia heru t, Ts au T bainisha aina za vitenzi vilivyoandikwa kwa
heru za mlazo kwenye sentensi zifuatazo:
Kwa mfano:
(i) Mama yu jikoni.
t
(ii) Mwalimu wetu alikuwa akifundisha.
Ts T
(a) Mimi ni daktari wa meno.
(b) Jana nilinunua maharagwe na sukumawiki.
(c) Mimi ndimi chifu wa kata hii.
(d) Yeye yu mgonjwa mahututi.
(e) Dadangu anapaswa kujitahidi sana.
(f) Kitabu chako ki mezani.
(g) Nilikuwa nikitaka kwenda msikitini.
(h) Mama yake anapika chakula.
(i) Kakangu amewahi kutembelea makavazi ya kitaifa.
(j) Wewe u mwizi.
2. Mnyambuliko wa vitenzi
Neno mnyambuliko linatokana na kitenzi ‘nyambua’ ambacho humaanisha
kukivuta au kukirefusha kitu (kama vile mpira). Katika saru, mnyambuliko
humaanisha hali ya kukipa kitenzi maana mbalimbali kwa kuongezea
viambishi tofauti tofauti. Katika kufanya hivyo, viambishi tamati ndivyo
vinavyotumika. Hivi ni viambishi vinavyotokea baada ya mzizi wa kitenzi.
Kauli ya kutendwa na kutendewa
Katika kunyambua vitenzi vya kauli za kutendwa na kutendewa, viambishi
tamati mbalimbali hutumika. Viambishi hivi hufungamanishwa na mzizi
wa kitenzi kama ifuatavyo:
Mzizi Kauli ya kutenda Kauli ya kutendwa Kauli ya kutendewa
pig- piga pig-w-a pig-iw-a
chez- cheza chez-w-a chez-ew-a
kop- kopa kop-w-a kop-ew-a
andik- andika andik-w-a andik-iw-a
lim- lima lim-w-a lim-iw-a
let- leta let-w-a let-ew-a
kat- kata kat-w-a kat-iw-a
kimbi- kimbia kimbi-w-a kimbi-liw-a
tup- tupa tup-w-a tup-iw-a
pik- pika pik-w-a pik-iw-a
176
177
Zoezi
1. Kamilisha jedwali lifuatalo:
Mzizi Kauli ya kutendwa Kauli ya kutendewa
k.m. shik- shik-w-a shik-iw-a
(a) pat- ____________ ____________
(b) tum- ____________ ____________
(c) fung- ____________ ____________
(d) anz- ____________ ____________
(e) tafut- ____________ ____________
(f) sem- ____________ ____________
(g) uliz- ____________ ____________
(h) kunj- ____________ ____________
2. Tumia kitenzi na kauli iliyomo mabanoni ili kukamilisha sentensi
zifuatazo:
Kwa mfano: Shamba lake lita______ kesho kutwa. (lima, tendwa)
Shamba lake litalimwa kesho kutwa.
(a) Mariamu ali______ barua. (andika, tendewa)
(b) Kaka ameka______ muwa na dada. (kata, tendewa)
(c) Jogoo yule ata______ kesho. (chinja, tendwa)
(d) Mwangi ame______ kuwa diwani wa eneo hili. (chagua, tendwa)
(e) Mti ume______ na radi. (piga, tendwa)
(f) Jana tuli______ zawadi na binamu zetu. (leta, tendewa)
(g) Waziri ata______ wimbo mtamu na watoto hawa. (imba, tendewa)
(h) Mchezo una______ sasa hivi. (cheza, tendwa)
(i) Wakazi wa Afrika wali______ kwa umwagikaji wa damu. (komboa,
tendewa)
(j) Wanyama wakali wali______ na askari msitu. (winda, tendwa)
3. Viunganishi (U)
Viunganishi ni maneno yanayotumika kuunganisha maneno, vifungu vya
maneno au sentensi mbalimbali. Kwa mfano:
(i) Mama na baba wamekwenda wapi?
(ii) Nilikwenda lakini sikuka.
(iii) Nipatie kikombe au sahani.
(iv) Wanafunzi walikwenda mjini bali si shambani.
(v) Itabidi uache kunywa pombe iwapo unataka kuishi maisha marefu.
(vi) Nitasoma kwa bidii sana ili nipite mtihani wangu.
(vii) Alifanya kazi hiyo kama kwamba atalipwa.
(viii) Nilimlipa mshahara wake wote ingawa hakufanya kazi mwezi
mzima.
176
177
Zoezi
1. Onyesha viunganishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Unataka kitabu au kalamu?
(b) Alikuja japo hakukubali niliyomwambia.
(c) Tutasari kwa miguu hadi Mtito Andei.
(d) Itabidi uamke mapema ikiwa unataka kuka shuleni mapema.
(e) Nilika shuleni mapema lakini sikumkuta mwalimu.
(f) Wakulima hawa watapata mazao mengi iwapo watatumia
mbolea.
2. Tumia viunganishi vifuatavyo kutungia sentensi:
(i) na (ii) lakini (iii) wala (iv) iwapo (v) ili (vi) kama
D. Kusoma
Mashairi ya arudhi
Soma shairi lifuatalo na ujibu maswali uliyoulizwa.
Naeleza sikashifu, wala sina masikhara,
Isipokuwa nasifu, na wachafu kuwakera,
Faida ya unadhifu, ya kuwa ni jambo bora,
Usa ni jambo bora, kiumbe uwe nadhifu.
Uchafu si kitu chema, tena waleta madhara,
Kisha wadhuru uzima, kwa mwili una hasara,
Na yako mja heshima, huwa ni kama tambara,
U s a n i j a m b o b o r a , k i u m b e u w e n a d h i f u .
Uchafu unasumbua, kwa harufu ya kuzira,
Mwilini hufanya chawa, wakajenga kwa imara,
Tena nguo hupasua, ukawa kama mkora,
Usa ni jambo bora, kiumbe uwe nadhifu.
Uchafu ninaolumba, si mmoja kwa ishara,
Ni wote ambao kwamba, hadi m’baya kwa sura,
Hata uchafu wa nyumba, pia watia hasara,
Usa ni jambo bora, kiumbe uwe nadhifu.
Tamati nikika, usa watia fora,
Tahadhari na kumbuka, mja ufanye kira,
Uchafu kuuwepuka, uwe mtu barabara,
Usa ni jambo bora, kiumbe uwe nadhifu.
(‘Usa ni Jambo bora,’ Karama na K. Khan, Kusoma na Kufahamu Mashairi
1, uk. 8)
178
179
Msamiati
nadhifu : sa.
kashifu : tukana.
kera : sumbua.
zira : chukiza.
mkora : mhuni; mtu ovyo.
lumba : sema, zungumzia.
tia fora : shinda, pendeza.
tamati : mwisho.
Maswali ya marudio
1. Je, shairi hili ni la aina gani? Kwa nini?
2. Taja aina mbalimbali za usa zinazozungumziwa.
E. Kuandika
Taarifa au ripoti fupi
Ripoti ni maelezo ya matukio, matendo au shughuli fulani. Uandishi wa
ripoti au taarifa ni muhimu sana; sio tu shuleni bali pia katika maisha ya
kawaida. Taarifa au ripoti ni maandishi ambayo yanatoa maelezo kuhusu hali
fulani ili kuonyesha jinsi ilivyo. Inawezekana ikawa ripoti kuhusu mkutano
uliofanyika, shughuli na matendo ya kundi fulani na kadhalika.
Mambo muhimu katika uandishi wa taarifa
1. Taaarifa iwe wazi, inapowezekana iwe na vichwa vidogo au mada ndogo
ndogo.
2. Iwe na mpangilio wazi na hoja zikuzwe katika aya mbalimbali.
3. Iwe fupi na inayosomeka kwa wepesi na rahisi.
4. Ijifunge kwenye mada inayohusika.
5. Lugha inayotumiwa iakiane na lugha rasmi.
6. Mwandishi atumie nafsi ya tatu ( a.. sio ni..)
Ripoti zinazopatikana kwa wingi katika mazingira ya shule ni zile
zinazohusiana na shughuli za makundi na vyama mbalimbali, michezo n.k.
Muundo wa Ripoti
Ripoti rasmi huwa na muundo maalum. Muundo huo unajumlisha:
(i) Anwani au kichwa: Anwani hii hutakiwa kuwa fupi na
inayomwelekeza msomaji kwenye mada ya ripoti au kinachohusika
katika ripoti hiyo. Sehemu hii huweza pia kuwa na tarehe na jina la
mwandishi. Ni bora sehemu hii ikaandikwa kwa heru kubwa.
(ii) Utangulizi: Sehemu hii hutaja ripoti inahusu nini na huwa na maelezo
178
179
ya kimsingi. Huweza pia kutoa maelezo ya kijumla kuihusu ripoti.
(iii) Mwili au ripoti yenyewe: Hii ni sehemu kuu na hutegemea kiini au
mada. Inawezekana (sio lazima) sehemu hii ikawa na vichwa vidogo
vidogo. Ni muhimu sana sehemu hii ionyeshe mtiririko mzuri wa
mawazo.
(iv) Hitimisho au mwisho: Sehemu hii hutoa muhtasari wa ripoti na
matokeo. Hii sio sehemu ya kutoa hoja au mawazo yanayoendeleza
ripoti bali ni kauli au maneno ya kumalizia tu.
Mfano wa ripoti
RIPOTI YA KUNDI LA WANAMAZINGIRA YA MWAKA 2002
Utangulizi
Mwaka huu umekuwa wa mafanikio makubwa katika shughuli za kundi la
Wanamazingira. Mwaka ulianza kwa uchaguzi wa viongozi wapya. Viongozi
hao wamekuwa nguzo kuu ya mafanikio yaliyokiwa na kundi hili. Viongozi
hao ni:
Seif Mwakalu Mwenyekiti
Redemta Mwiti Naibu Mwenyekiti
Zipporah Mirugi Katibu mkuu
Sauda Karisa Katibu mwenezi
Albert Likono Mweka hazina
Peter Poighisio Naibu mweka hazina
Kwa bahati mbaya mdhamini wa kundi hili aliondoka mwanzoni mwa
mwaka. Hata hivyo, tumekuwa na bahati ya kumpata mdhamini mwingine,
Bi. Rodah Oketch ambaye ametusaidia sana hasa kwa kutuchulia mbinu
zilizotuwezesha kukabiliana na tatizo kubwa la ukosefu wa wadhamini wa
miradi yetu mbalimbali.
Shughuli kuu za Mwaka 2002
Katika muhula wa kwanza, Kundi la Wanamazingira liliongoza shughuli
ya upanzi wa miche shuleni. Shughuli hii ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Asilimia tisini ya miche iliyopandwa wakati huu haikukauka na inakua
vyema. Shughuli hii ilifuatiwa na safari ya kuwahamasisha wanakijiji
kuhusu umuhimu wa upanzi wa miti pamoja na ule wa kuyatunza mazingira.
Kundi liliendeleza suala la uhamasishaji kwa kuandaa mikutano kadha na
watu wengi katika maeneo mbalimbali. Wakati wa shughuli hizi tulipiga
picha nyingi za kumbukumbu ambazo zimetundikwa kwenye ubao mkuu
wa ilani shuleni.
Katika muhula wa pili, wanakikundi walishirikiana na kamati ya wilaya
wakati wa maandalizi ya Maonyesho ya Ukulima. Wanamazingira waliitumia
fursa hii kuyasambaza maarifa mbalimbali kuhusu umuhimu wa kuyatunza
mazingira yetu. Kundi hili liliandaa mashindano ya uandishi wa insha
kuhusu ‘Mazingira niyapendayo.’ Mshindi wa insha hiyo alikuwa mwanafunzi
180
181
wa shule ya msingi; jambo linaloonyesha jinsi kundi lilivyofanikiwa katika
uhamasishaji wa watu wengi.
Muhula wa tatu haukuwa na shughuli nyingi hasa kwa kuwa baadhi
ya wanakamati na viongozi wa kundi walihusika na maandalizi ya mitihani.
Hata hivyo, wanakikundi walipata fursa ya kulitembelea jiji la Nairobi
kuhudhuria kongamano la kimazingira lililofanyika huko mwezi wa Oktoba.
Pili, wanakundi walipata nafasi ya kuongeza miche mingine kabla ya mvua
za vuli na kudia miche ambayo ilikauka mwanzoni.
Hitimisho
Viongozi wa Kundi la Wanamazingira linastahili pongezi kwa kazi kubwa
waliyoifanya. Aidha, wanachama wa kundi hili wamekuwa nguzo kuu ya
ufanisi wake. Kundi hili lina lengo kuu la kuhakikisha kuwa mazingira
yetu ni mazuri. Madhali kila mwanafunzi atapenda kuishi katika mazingira
mazuri, kundi hili linawakaribisha wanachama wengi kujiunga kwa kulipa
ada ya shilingi thelathini.
Ripoti imetayarishwa na Jina___________
Sahihi ___________
Tarehe_____________
Zoezi
Wewe ni katibu wa kikundi fulani shuleni au hata kijijini, andika ripoti
kuhusu shughuli za kikundi chenu za kipindi maalum.
180
181
Sura ya Kumi na Sita
A. Ufahamu
Lumbwi na kindumbwendumbwe cha mageuzi
Ingawa Lumbwi si mshirikina sana, ilika wakati alipoanza kuhisi kuwa
hakuwa na bahati na kwamba kisirani kilimwandama. Wakazi wa eneo
bunge la Kiumbi walishindwa kuelewa kwa nini Lumbwi aliishi maisha
aliyoyaishi. Maisha yake hayakuwa mabaya tangu hapo. Babake alikuwa
kiongozi maarufu katika wilaya nzima na aliwahi kuwa hata mbunge wa eneo
bunge hilo. Ilisadifu kuwa wakati huo serikali iliamua kuitia lami barabara
kuu kutoka mjini na hata kuanzisha kituo cha afya. Basi kwa wengi babake
Lumbwi alikuwa kiongozi wa kwanza kuleta maendeleo katika eneo bunge
la Kiumbi.
Wakati babake akiwa mbunge, Lumbwi alikuwa mwanafunzi katika
shule ya upili. Ingawa hakuwa mwanafunzi stadi darasani, alijitahidi na hata
kuhitimu kidato cha nne. Baadaye, alipata nafasi ya kujiendeleza kimasomo
kwenye taasisi moja iliyohusika na masomo ya kompyuta. Alipomaliza
masomo yake, aliajiriwa katika osi ya manispaa ya makao makuu ya wilaya.
Waliofanya kazi naye wanasema kuwa Lumbwi alikuwa na kiburi sana
siku hizo. Kiburi chake kilitokana na sababu kadha. Kwanza, akilinganishwa
na wenzake alikuwa na bahati kubwa ya kuanza kazi akiwa na umri mdogo
sana. Pili, kwa sababu ya kuchimbukia familia yenye misingi mizuri kiuchumi,
hakuwa na shida nyingi. Isitoshe, alikuwa mtaalamu wa tarakilishi wa pekee
katika manispaa nzima. Siku hizo ujuzi wa kompyuta ulikuwa adimu kama
barafu ya kukaanga.
Hata kompyuta zenyewe
zilikuwa adimu kama
ua la mkuyu. Lumbwi
alikuwa na osi yake ya
kipekee aliyotengewa.
Osi hiyo ilitiwa mapazia
yaliyoiziba ili watu
wasiweze kuiona ndani
kutoka nje. Ilisemwa
kuwa hii ilikuwa njia
ya kuhakikisha kuwa
kompyuta ya pekee
katika manispaa nzima
ilikuwa salama.
Lumbwi ndiye
aliyehusika na uandalizi
wa mishahara katika
manispaa nzima.
Haikumchukua muda
182
183
mrefu kutambua kuwa alikuwa mtu muhimu sana pale. Lumbwi aliingiwa
na kiburi cha utendakazi. Kila mwisho wa mwezi ulipokaribia, alijitia
maradhi ya kila aina ili asimalizie shughuli za uandalizi wa mishahara
ya wafanyakazi. Wengi wao walilazimika kuzunguka mbuyu ili akubali
kuimalizia shughuli ile.
Babake alipong’atuka kwenye uongozi wa kitaifa, Lumbwi alibadilika
ghaa kama kinyonga. Hakutaka kujimwagia unga kwa kuwa hakuwa na
mtu wa kumkimbilia au kumpa kichwa. Waliofanya kazi naye walishangaa
kuona jinsi alivyobadilika ghaa. Sasa hakulazimika kujitia ugonjwa ili
apewe chai ya kumhimiza. Lakini hawakujua kuwa alikuwa amepata upenyu
mwingine wa kujinufaisha. Kwao, Lumbwi alikuwa ametambua makosa yake
na kubadilika kabisa hadi akawa mfanyakazi mzuri ambaye alijitolea sabili
kuutekeleza wajibu wake.
Wakati wimbi la mageuzi lilipoka nchini ndipo cheche za siasa,
zilizokuwa kwenye moyo wa Lumbwi, zilipopata nguvu mpya. Mwana wa
mhunzi asiposana huvukuta. Lumbwi naye alikuwa na nia ya kuwahakikishia
watu wa eneo bunge la Kiumbi ukweli wa methali hii. Wakati wa kampeni za
uchaguzi, Lumbwi aliwakumbusha watu jinsi familia yao ilivyokuwa na jadi
ya uongozi. “Msisahau kuwa maendeleo ya pekee hapa yalipatikana zama za
babangu. Nia hasa sasa ni kuyaendeleza maendeleo hayo hadi yakie hatima
yake!” alisema Lumbwi kwa msisimko mkubwa. Mpinzani wake ambaye
alimjua tangu siku akijisingizia ugonjwa ili azungukwe mbuyu aliwaambia
watu, “Huyu ni kinyonga tu, anajua kwenda na majira. Msimwamini
kabisa huyu!” Lakini hakuna aliyemsikiliza. “Huyu anasumbuliwa na gere
tu. Mwangalieni! Amefanya kazi na huyu Lumbwi siku zote hizo mbona
hakujaribu angaa kujiendeleza!” walimpiga vijembe.
Uchaguzi ulipoka, Lumbwi alitifua kivumbi Kiumbi. Alichaguliwa
na kuwa mbunge mpya wa eneo bunge la Kiumbi. Wakazi wa eneo hili
walikuwa na matumaini makubwa ya kuona maendeleo katika kipindi
kichache chini ya uongozi wa Lumbwi. Walitamani kuona shida yao kuu ya
maji imeshughulikiwa. Walitamani kuona tatizo lao la njaa ya mara kwa
mara nalo limetadarukiwa kwa kuwa lilikuwa tatizo sugu. Walitamani kuona
maendeleo yasiyokuwa na chembe yoyote ya usadi. Wakati wa kampeni za
uchaguzi, Lumbwi alikuwa mstari wa mbele kupiga vita usadi. “Serikali
ijayo haina mchezo. Mtakiona kindumbwendumbwe cha mageuzi na usadi.
Hakuna kuhonga polisi tena! Hakuna unyangányi tena! Hakuna kuchukua
mali za watu! Hamna cha kutumia madaraka yako kujinufaisha tena!”
alisema Lumbwi kwa sauti kuu.
Lumbwi alifurahi upeo wa furaha baada ya kuchaguliwa na kuwa
Mheshimiwa. Alikuwa amepata abra adimu ya kuhakikisha kuwa familia yao
imeingia katika historia ya eneo hilo. Serikali mpya ilipoanza kazi ilijitahidi
kutimiza ahadi ilizotoa wakati wa kampeni. Kila raia nchini alitamani kuona
vita vya kupambana na usadi. Lumbwi alikuwa mmoja kati ya viongozi
waliopaaza sauti zao wakilaani matumizi mabaya ya mamlaka. Siku moja
aliwashutumu wabunge wenzake kadha waliokuwa wafanyakazi serikalini
kwa kujitajirisha kwa kutumia mamlaka yao. Nia yake hasa ilikuwa
182
183
kutambuliwa kama kiongozi aliyesimama tisti kupigania haki za wanyonge.
Lumbwi kawa Lumbwi kweli.
Babake aliyekuwa amepindwa mgongo na umri aliamua kumwita
mwanawe siku moja na kumshauri. “Mwanangu, usiwe nge ukajichoma kwa
mkia wako!” Lumbwi hakuwa na subira ya kuuelewa ujumbe wa babake.
“Baba, siasa ya siku hizi ni ya moto mmoja sio kama ya zama zenu!” Lumbwi
alisema kwa sauti ya ujuzi mkubwa.
Serikali ilipotoa ripoti ya uchunguzi wa usadi, Lumbwi alikuwa
mmoja wa viongozi walioorodheshwa kwa kuzitumia nafasi zao za kazi
kujinufaisha. Alijitahidi kujitetea lakini hakuweza. Alikishwa mahakamani
na kushtakiwa kwa hatia ya kuhusika katika matendo ya usadi. Alikuwa
ametwaa vipande kadha vya ardhi ya umma. Aidha, alikuwa ametwaa
nyumba kadha za manispaa ambazo alizibatilisha umilikaji wake alipokuwa
mtaalamu wa tarakilishi. Lumbwi akakumbwa na kindumbwendumbwe cha
mageuzi na kuiacha Kiumbi kwa kivumbi.
Maelezo ya msamiati
mshirikina : hali au tabia ya kuamini mambo ya
uchawi au mizimu.
alipong’atuka : alipoacha kazi; alipostaafu.
gere : wivu; kijicho; ngoa.
limetadarukiwa : limeshughulikiwa.
nge : mdudu mwenye miguu minane
anayechoma kwa mkia wake wenye sumu.
kindumbwendumbwe : ghasia; fujo; tukio lenye matokeo makubwa.
abra : nafasi; fursa.
alizibatilisha : alizigeuza; alizibadilisha.
Maswali
1. Je, ni kwa nini babake Lumbwi alidhaniwa kuwa kiongozi wa kwanza
kuleta maendeleo katika eneo la Kiumbi?
2. Ni kwa nini Lumbwi alikuwa na kiburi alipoanza kufanya kazi?
3. Je, ni kitendo gani alichofanya Lumbwi kila mwezi? Kwa nini?
4. Mtunzi ana maana gani kwa kusema ‘Lumbwi kawa lumbwi kweli?’
5. Ni kwa nini Lumbwi alibadilika baada ya babake kung’atuka?
6. Baada ya uchaguzi wakazi wa eneo la Kiumbi walitarajia kunufaika vipi
kutokana na ushindi wa Lumbwi?
7. Eleza jinsi Lumbwi alivyojichoma kama nge.
8. Eleza maana ya misemo hii kama ilivyotumiwa katika kifungu
ulichosoma:
(a) kumpa kichwa (b) alijitia maradhi (c) apewe chai
(d) alijitolea sabili (e) azungukwe mbuyu (f) aliyesimama tisti
184
185
B. Kusikiliza na kuzungumza
(a) Vitendawili
Kitendawili ni msemo wa kimafumbo ambao hufumba jambo fulani na
hutolewa kwa hadhira au wasikilizaji ili waufumbue. Kitendawili ni sehemu
ya mafumbo ambayo yanapatikana katika kundi pana la semi katika fasihi
simulizi. Vitendawili hukirisha na huingiliana na mazingira halisi ya jamii
inayohusika. Kitendawili kama fumbo au fungu la maneno hudai jibu na
huchochea udadisi na utati wa mambo kulingana na mazingira na wakati
maalum.
Kazi ya vitendawili katika jamii:
1. Kuielimisha jamii kuhusu mazingira yake.
2. Kuchochea utati wa watoto au wanajamii wanaolengwa na kitendawili
ili wachunguze mambo ya kimsingi na kuyahusisha na mazingira yao.
Kwa mfano, mtu anapoulizwa kitendawili kama ‘Nyumba yangu haina
mlango’ atalazimika kuihusisha na mazingira yake kabla ya kujibu kuwa
ni ‘yai.’
3. Huwawezesha wanajamii kuyaelewa mazingira yao na kuwa na jicho la
udadisi zaidi
4. Hutumiwa kuwasaidia wanaohusika pia kuuboresha uwezo wao wa
lugha, watoto wanaotegeana vitendawili hupata ujuzi wa kujieleza kwa
lugha fasaha kwa vitendawili.
5. Hutumiwa kufurahisha na kuburudisha jamii hasa wakati wa kutega na
kutegua vitendawili, jambo ambalo hufanywa aghalabu baada ya kazi.
6. Huweza pia kutumiwa kukejeli au kuonyesha dharau fulani. Kwa mfano,
‘Wazungu wawili wanachungulia dirishani’ - kamasi.
Muundo wa kitendawili
Kitendawili huwa na muundo maalum ambao unafuatwa katika jamii
mbalimbali. Muundo huo huwa na sehemu zifuatazo:
Kitangulizi: Hapa mtegaji husema, ‘Kitendawili’ na wanaotegewa
kujibu ‘Tega!’
Kitendawili chenyewe: Baada ya kutamka kitangulizi na kujibiwa,
mtegaji kitendawili hukisema kitendawili chenyewe. Kwa mfano,
‘Kuku wangu hutagia mibani’.
Swali la msaada: Baada ya kitendawili huweza kufuatia swali la
kumchochea anayetegewa kitendawili hicho. Huweza kuulizwa ‘Ni
yupi huyo” au ni ‘Ni nini hicho’. Swali hili sio la lazima, huenda
likaachwa.
Jibu lenyewe: Aliyetegewa kitendawili hicho huweza kujibu. Kwa
mfano, jibu la kitendawili kilichoko hapo juu ni ‘Nanasi.’ Ikiwa
ameshindwa jibu hutolewa na aliyekitega kitendawili hicho.
184
185
Zoezi
1. Toa mfano wa kitangulizi cha kitendawili kutoka jamii yako.
2. Toa mifano miwili ya vitendawili vinavyohusiana na mazingira ya jamii
yako.
3. Tegua vitendawili vifuatavyo:
(i) Kamba yangu ndefu haiwezi kufunga kuni.
(ii) Kipo lakini hukioni.
(iii) Kuku wangu katagia mibani.
(iv) Ninapompiga mwanangu watu hucheza.
(v) Nina saa ambayo haijasimama tangu kutiwa ufunguo.
(vi) Mzazi ana miguu bali mzaliwa hanayo.
(vii) Anataga huku akitambaa.
(viii) Nyumba yangu kubwa lakini ina mlango mdogo.
(ix) Nimeanika mpunga wangu juani lakini kulipopambazuka
sikuuona.
(x) Huku ng’o na kule ng’o.
(xi) Taa yangu yazagaa ulimwengu mzima.
(xii) Popote niendapo anifuata.
(xiii) Haukamatiki wala haushikiki.
(xiv) Nimemwona bikizee amejitwika machicha.
(xv) Niliona mkufu njiani lakini sikuweza kuunyanyua.
(b) Matamshi bora: vitate -t/d
Tamka maneno haya
t d
tamu damu
taka daka
tokeza dokeza
tai dai
Soma vitanza ndimi vifuatavyo:
1. Ingawa nilidhani kile kinywaji ni kitamu, nilipokimeza nilianza kutokwa
na damu.
2. Nilitaka kuudaka ule mpira lakini Bwana Kataka hakutaka niudake.
3. Jini lilipotokeza lilidokeza kuwa kama lingetokeza hapo awali lingedokeza
ni kwa nini lilitokeza.
4. Bwana Tai alidai kuwa tai huyo ni wake lakini madai ya Tai kuwa tai ni
wake hayakuwa na msingi kwa vile tai wote huishi huru huko kichakani.
186
187
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Sentensi za Kiswahili
Kirai
Kirai ni nini? Kirai ni kundi lolote la maneno lenye maana fulani ila maana
haya si kamilifu. Kwa mfano:
(i) mara kwa mara (ii) wakati wa likizo
(iii) katika mtaa huu (iv) kazi yoyote ile
(v) kitabu chochote
Mtu yeyote anayeelewa Kiswahili atafahamu kuwa vifungu hivyo vya maneno
si upuzi mtupu bali vina maana fulani ingawa maana yenyewe hayajitokezi
waziwazi. Maana ya virai hujitokeza tu vitumikapo katika muktadha wa
sentensi. Katika kufanya hivyo, inabidi kuongeza maneno zaidi kwenye virai
hivyo. Na kati ya maneno yanayoongezwa ni lazima pawe na kitenzi angalau
kimoja. Kwa mfano:
(a) Mimi huenda msikitini mara kwa mara.
(b) Sisi tutamtembelea shangazi yetu wakati wa likizo.
(c) Chifu amekataza unywaji wa pombe haramu katika mtaa huu.
(d) Wanjiru hufanya kazi yoyote ile.
(e) Mimi nitasoma kitabu chochote.
Kati ya maneno yaliyoongezwa kwenye virai hivyo ni vitenzi vifuatavyo:
(a) huenda (b) tutamtembelea (c) amekataza (d) hufanya
(e) nitasoma
Zoezi
1. Kati ya mafungu yafuatayo ya maneno, onyesha ni yapi sentensi na ni
yapi virai; kwa mfano:
(i) Aketch anakula wali. – sentensi
(ii) Kina mama wote – kirai
(a) Mimi nitakusaidia kesho.
(b) Kwa nini mama hakupika chakula?
(c) Ndani ya nyumba yetu
(d) Kwa bei ya shilingi mbili
(f) Aliwasili saa kumi na mbili jioni.
(g) Shuleni mwetu
(h) Mtoto mtundu sana
(h) Nimepokea barua kutoka Mombasa.
(i) Karibu na hospitali kuu
(j) Juu ya meza ile
186
187
2. Geuza virai vifuatavyo viwe sentensi kamilifu kwa kuviongezea maneno
yoyote mwafaka. Kwa mfano:
miezi michache iliyopita
Jumakoshi alianzisha biashara hii miezi michache iliyopita.
(a) kila Jumapili
(b) katika ukurasa wa mia moja
(c) ndani ya bahari
(d) juu ya sakafu hiyo
(e) katika kituo cha mabasi
(f) baada ya saa sita za mchana
(g) kwa kijiko
(h) jana usiku
(i) kando kando ya barabara
(j) pamoja na mama na baba
2. Kuakisha
(i) Ritifaa/Kibainishi (’)
(i) Hutumika katika mazingira mbalimbali ya kimaandishi kama yafuatayo:
(a) Kuonyesha tarakimu ambazo hazikuandikwa:
(i) Mwaka ’14-’18 (1914-1918)
(ii) Mwaka ’39 – ’45 (1939-1945)
(iii) Mwaka ’78-‘79 (1978-1979)
(b) Kuandika maneno kwa kifupi.
Hutumika zaidi kwenye ushairi: kwa mfano:
Haki ifukie chini, ipige na kuibuta,
’Tumbukize baharini, ’tazamia kuifwata,
Ukaiche jangwani, nitakwenda kuileta,
Itundike milimani, nitawana kuipata,
Haki yangu ’taidai, hata iwe ni kwa vita.
(Kutoka Kina cha Maisha na S.A. Mohamed, uk. 30)
(c) Kutofautisha sauti ng’ na ng; kwa mfano:
(i) Ali aliuza ng’ombe akanunua ngoma.
(ii) Kwa nini Ngumo hakung’oa magugu haya?
(iii) Ngome ilishambuliwa na majeshi yanayong’ang’ania uongozi.
(ii) Mabano/vifungo/parandesi ( )
Hutumika katika mazingira yafuatayo:
(a) Kuonyesha maneno yasiyokuwa ya lazima; kwa mfano:
(i) Mwalimu akiniita (bila shaka ataniita) mwambie nitakuja sasa
hivi.
188
189
(ii) Dadake Waithera (ni mtoto mvivu kweli) bado anaendelea
kulala.
(iii) Watu wanaorandaranda mitaani (na ni wengi mno) wanafaa
kusaidiwa ili wajikimu maishani.
(iv) Wanyama wote wa nyumbani (ng’ombe, kuku, mbuzi na
wengine) wanafaa kutunzwa vizuri.
(b) Kuzingira nambari au heru kwa mfano:
(a) (b) (c) (d) (e)
(1) (2) (3) (4) (5)
(i) (ii) (iii) (iv) (v)
(c) Kuonyesha maongezi au maandishi ya kitamthilia ili kutoa maelezo
kwa wasomaji na waigizaji. Kwa mfano:
Msichana
: (Anatokeza mbele. Anaubagaza mkoba wake wa shule
chini na kisha kuketi juu ya
kile kiti cha kukunja) Mamaaa!
MaMa
: (Anaitikia akiwa ndani kisha anatokeza) Mmetoka
shule tayari kumbe?
Msichana
: Mama ninasikia njaa kaliii! (Anajipweteka kitini na
kuitambaza miguu mbele)
Mvulana
: (Akitokeza nyuma huku akitembea kizembe na
kuuburura mkoba wake ambao umekatika ukanda
mmoja) Mama…
MaMa
: (Akiuangalia ule mkoba) Sasa ukiwa na njaa ndio
uuburure mfuko wa vitabu hivyo? Kalamu zenyewe
si utakuwa umezipoteza?
Msichana
: (Anakumbuka jambo fulani) Mama, baba yupo?
MaMa
: Amesha…
(iii) Heru nzito (H)
Hutumika kusisitiza au kutilia mkazo maandishi, kama ifuatavyo:
1. Kuonyesha aina mbalimbali za maneno; kwa mfano:
(a) Kuonyesha nomino:
(i) Nyumbani mwetu mna kuku na bata wengi.
(ii) Duka hili ni la Mzee Hamisi.
(iii) Watoto wawili na wazee watano wanalima shambani.
(iv) Juma na Wangui wako wapi?
(v) Msituni mna mikarafuu na miambako mingi.
(b) Kuonyesha vivumishi; kwa mfano:
(i) Watoto wazuri wanacheza nje ya nyumba.
(ii) Ndovu watano wamevamia nyumba zetu.
188
189
(iii) Umeniletea vitabu vingapi?
(iv) Chakula chako kimemwagika.
(v) Tunda hili limeiva.
(iv) Heru za mlazo/italiki (Hh)
Hutumika kama zinavyotumika heru nzito ili kutilia mkazo maandishi
mbalimbali; kwa mfano huweza kutumika:
(a) Kuonyesha aina za maneno, kwa mfano, vielezi kwenye sentensi:
(i) Mama alinizomea sana.
(ii) Wafungwa wale waliadhibiwa mno.
(iii) Nyadiega atafanya kazi hiyo vizuri sana.
(iv) Mwalimu atatueleza mambo hayo kinaganaga.
(b) Kuonyesha majina ya mito; kwa mfano:
(i) Maji ya Tana, Kagera na Ruvuma husaidia wakulima wengi.
(ii) Mto wa Nile una mamba wengi.
(iii) Mvua inaponyesha huko milimani husababisha mto wa Ruji
kufurika.
(c) Kuonyesha viambishi; kwa mfano, vya kurejesha:
(i) aliyeanguka walioanguka
(ii) lililoanguka yaliyoanguka
(iii) kilichoanguka vilivyoanguka
(iv) iliyoanguka zilizoanguka
D. Kusoma
Mashairi huru
Soma shairi lifuatalo na ujibu maswali uliyoulizwa.
Jama, jama jamani
mbona twabebeshwa mateso hivi
mizigo mikubwa ya dhiki kama
kwamba hatuna haki ya kusema
kukataa ndoa za lazima
kukataa kuozwa wazee
kukataa kukatishwa masomo
kukataa tohara ya lazima
Jama, jama jamani
iweje tuteswe mateso haya
na watu wasiokuwa hata na haya kama
kwamba hatuna haki ya kulalamika
kulalamikia kutumikishwa kama mayaya
190
191
kulalamikia kudhalilishwa kiunyama
kulalamikia kutolindwa na sheria
Jama, jama jamani
sasa hii ni awamu nyingine
na macho tumeyafungua kabisa
Tumekataa kudhalilishwa kabisa
Tumekataa kuteswa kama watumwa
Tumekataa tohara ya lazima
Tumekataa kuozwa…Tumekataa! Tumekataa
Hii awamu ya ‘Haki ya Mtoto wa Kike’
Zoezi
(a) Toa kichwa kifaacho kwa shairi hili.
(b) Je, msemaji analalamika kuhusu nini?
(c) Kwa nini anasema hii ni awamu nyingine?
(d) Taja sifa moja ya mtindo inayopatikana katika shairi hili. Je, ina
umuhimu gani?
E. Kuandika
Insha ya methali
Hii ni insha ambayo huandikwa kuonyesha ukweli wa methali fulani.
Aghalabu methali huwa na maana mbili kuu: maana ya juu na yale ya ndani
(maana batini). Maana ya juujuu ni yale ambayo huwa wazi kutokana na
maneno yaliyotumiwa. Maana ya ndani yanahusu kuchua ujumbe uliopo
na ndiyo yanayotuelekeza penye mafundisho ya methali hiyo. Ili kuweza
kuandika insha za methali, lazima ujitahidi kujifunza methali mbalimbali
na kuzijua vyema.
Sifa za insha ya methali
1. Kichwa chake huwa ni cha methali.
2. Huhusisha kueleza maana ya methali: maana ya juu juu na maana ya
ndani.
3. Huwapo na kisa kinachoingiliana na methali inayohusika.
4. Hutakiwa kuwa na sifa nyinginezo za uandishi wa insha kama:
uzingatiaji wa saru, alama za kuakisha, ugawaji wa aya, mtiririko
mzuri wa mawazo na mpango wa hoja wenye mantiki.
5. Huweza pia kuhusisha matumizi ya methali nyinginezo zinazoingiliana
na methali inayoshugulikiwa.
6. Kama insha nyinginezo lazima iwe nzuri na yenye mvuto.
190
191
Mfano
Mpanda ngazi hushuka
Maana ya juujuu ya methali hii ni kuwa mtu anayeikwea au kuipanda ngazi
huishia kuishuka au kuiteremka baada ya kukamilisha kazi aliyokuwa nayo.
Maana yake ya ndani ni kuwa mtu mwenye uwezo au mamlaka fulani huweza
kuishiwa nayo. Hii ni methali inayoweza kutumiwa kumpigia mfano mtu ambaye
anajitapa kutokana na uwezo alio nao.
Hamna anayedhihirisha ukweli wa methali hii kama Mzee Jitumbo
Kajiweza. Huyu alikuwa tajiri maarufu katika kijiji cha kwetu ambaye alijaliwa
bahati ya kupata mali nyingi ajabu. Mzee Jitumbo Kajiweza alikuwa na biashara
nyingi, maduka matatu ya kuuzia zana za ukulima, hoteli mbili na mtambo wa
kusagia mahindi. Alianzisha biashara zake hizi muda mfupi baada ya kustaafu
huko alikofanya kazi mjini kwa miaka kadha ingawa wakati wa kustaafu hakuwa
amekisha umri rasmi wa kustaafu.
Mzee Jitumbo Kajiweza aliingiwa na kiburi kingi kutokana na utajiri
wake mwingi. ‘Mimi ni tajiri kwa kuwa nina akili kuliko wanakijiji wote pamoja,’
alijitapa kila wakati. Aliwaruhusu watu kukopa vitu kwenye maduka yake
kisha wamlipe mwisho wa mwezi. Wengi walifurahi na kumwona mtu mzuri
lakini walilaani bahati yao hiyo walipokwenda kulipa na kutambua kuwa alikuwa
ameongeza kiasi cha pesa walichotakiwa kulipa. Aliwafanyia vitimbi vya kila
aina mpaka wengine wakatishia kumshtaki lakini aliposikia hayo aliyapuuza
kwa kusema, ‘Sasa mimi utanishtaki kwa nani?”
Wanakijiji walitaabika kutokana na hadaa kubwa walizokuwa wakifanyiwa
na Mzee Jitumbo Kajiweza. Hawakujua la kufanya ili kumkomesha tajiri huyo
aliyekuwa na uwezo mkubwa na aliyewasumbua wanakijiji sana. Walimlaani na
kumwapiza kila wakati lakini kwa kiburi chake akasema kuwa, “Dua la kuku
halimpati mwewe!’
Kumbe ni kama wasemavyo wahenga kuwa mbo ya mnyonge mli Mungu?
Hatimaye, mambo aliyoyafanya Mzee Jitumbo Kajiweza zamani yaliishia
kuchuliwa na kachero wa polisi. Iligunduliwa kuwa mali yake ilitokana na wizi
aliofanya alipokuwa Osa wa Masoko alikofanya kazi. Alishikwa na kupelekwa
mahakamani na kuishia kufungwa kifungo cha miaka sita na adhabu kali. Mali
aliyoiringia ilichukuliwa ili kudia fedha alizokuwa ameiba.
Mzee Jitumbo Kajiweza alipoachiliwa kutoka kifungoni hakuwa na
chochote; alikuwa maskini hohehahe. Watu aliowadharau hapo kabla walikuwa
wamepiga hatua kubwa maishani wakati yeye anadidimia. ‘Waama ni kweli
mpanda ngazi hushuka,’ walisema wanakijiji kila walipomwona Mzee Jitumbo
amejiinamia kwa unyonge.
Zoezi
Andika insha kuhusu mojawapo wa methali hizi:
(a) Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
(b) Mwenda tezi na omo marejeo ni ngamani.
(c) Usipoziba ufa utajenga ukuta.
192
193
Mazoezi ya Marudio II
A. Ufahamu
Je, tunaitaka jamii ya aina gani?
Toka binadamu aanze kuishi katika jamii, swali moja ambalo limemshughulisha
kwa mapana na marefu ni aina ipi ya jamii ambayo inafaa? Binadamu ameishi
ulimwenguni kwa karne nyingi na bado swali hili linabakia pale pale. Je, ni
jamii ipi ambayo inafaa? Kwa mfano, kwetu sisi kama Wakenya ni jamii ipi
ambayo ni nzuri kwetu? Hili ni suala ambalo linaweza kumfanya mtu ajikune
kichwa kwa muda mrefu na labda hata kukosa kupata jibu la moja kwa moja.
Lakini kimsingi kuna sifa kadha zinazotambulisha jamii ambayo wengi wetu
tutaipenda; tutaionea fahari na kutamani kuishi katika jamii hiyo.
Kila mtu anatamani kuwa na uhuru wa kufanya mambo yanayompendeza
na kumfurahisha. Huu ni mtazamo mzuri lakini sote tunajua kwamba
binadamu haishi peke yake bali anaishi na binadamu wenzake. Hii ina
maana kuwa uhuru wa mtu binafsi lazima uzingatie uhuru wa binadamu
hao wengine. Kwa mfano, uhuru wa mtu mmoja wa kusali na kuomba lazima
uzingatie kuwa jirani yake ana uhuru wa kulala bila ya kubughudhiwa usiku.
Kimsingi ni kuwa ikiwa uhuru wa mtu mmoja utaingilia uhuru wa mwenzake
basi pana tatizo. Hali hii inatukumbusha kuwa uhuru huenda na kiwango
na uwajibikaji; yaani kuujua wajibu wako kama mtu.
Ili jamii bora ipatikane ni lazima kuwepo na sheria na taratibu au
kanuni zinazokubalika na wanajamii wote. Haitoshi tu ziwepo sheria na
kanuni bali lazima sheria hizo zifuatwe na kuwaongoza wanajamii wote.
Ikiwa mwanajamii yeyote atakiuka sheria fulani anapaswa kuadhibiwa kwa
mujibu wa sheria zilizoko bila ya upendeleo. Upendeleo unapozuka unajenga
uadui kati ya wanajamii waliopo ambao huenda wahisi kuwa kuna watu
wanaopendelewa na sheria na wengine kudhulumiwa na sheria hizo. Huu
unakuwa msingi wa chuki kati ya makundi ya kijamii na ni moja kati ya
mambo yanayoishia kuleta mvutano wa makundi na hatimaye hata mapigano.
Mahitaji ya binadamu ulimwengu mzima yanawiana kwa kiasi kikubwa.
Sote tunahitaji maji sa, chakula bora, hewa sa, malazi mazuri na makazi
mema. Haya ni mahitaji ya kimsingi na kila mtu hutamani kuyapata. Sote
tutakuwa na furaha kuishi katika jamii ambapo mahitaji haya yanapatikana
bila ya kulazimika kuingilia uhalifu au kujitosa kwenye maovu mengine ya
kijamii. Jamii ifaayo ni ile ambayo inakidhi mahitaji haya kwa wote. Hii
haina maana kuwa lazima kila mwanajamii awe na uwezo wa kunywa maji
ya madini. La. Bali kila mwanajamii aweze kupata maji sa yasiyoweza
kuidhuru afya yake.
Jamii nzuri ni ile ambayo inahakikisha kuwa kila haki za kila
mwanajamii zimelindwa; pana usalama wa kila mwanajamii na kwamba kila
192
193
mwanajamii ana fursa ya kujiendeleza kadiri ya uwezo wake mradi havunji
sheria zilizopo. Jamii ya aina hiyo inahakikisha kuwa hakuna mapendeleo
kwa kundi fulani la wanajamii kwa misingi yoyote ile.
Hamna jamii yoyote inayoweza kuwa bora na nzuri ikiwa haizalishi kiasi
cha kuwatosha wanajamii. Lakini ni muhimu kujua kuwa jamii haizalishi tu
bali wanajamii wenyewe wanatoa mchango ufaao katika uzalishaji wa mali,
chakula na utajiri unaowafaidi wote. Matokeo ya uzalishaji huo yanapaswa
kuwafaidi wanajamii wote; wazima na walemavu; wanawake na wanaume;
wazee na watoto. Lazima pawepo na njia za kuhakikisha kuwa kipato cha
jamii hiyo kinaifaidi jamii nzima bali sio kigaro cha watu wachache ambao
wana nafasi za utawala au usimamizi.
Maswali
1. Ni kwa nini swali kuhusu ni jamii ipi inayofaa linaweza kumfanya mtu
ajikune kichwa?
2. Mtu haishi peke yake bali anaishi na binadamu wengine. Kutokana na
ukweli huu, mtu anafaa kuishije na wenzake?
3. Upendeleo katika kutekeleza sheria una hatari gani?
4. Binadamu wote wana mahitaji sawa ya kimsimgi. Taja mahitaji hayo.
5. Je, jamii nzuri ni ipi?
6. Mali inayozalishwa na jamii inafaa kutumiwaje?
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Eleza maana na sifa zinazohusishwa na maigizo.
2. Je, methali zina jukumu gani katika fasihi simulizi?
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Weka alama za mtajo mahali pafaapo kwenye sentensi zifuatazo:
(a) Wewe ni nani? Askari aliniuliza.
(b) Mimi ni Chebet, nilimjibu.
(c) Unatoka wapi saa hii? alizidi kuniuliza.
(d) Ninatoka dukani, nikamjibu.
(e) Basi kimbia nyumbani haraka, akaniambia.
(f) Mimi nimekuwa nikikuonya kila siku lakini hutaki kusikia; sasa
utajuta, mama aliniambia.
(g) Ugonjwa wa Ukimwi utawaua watu wote wasiokuwa waangalifu,
daktari alitushauri.
(h) Majambazi walipoingia walituamuru, mikono juu!
(i) Je, wewe umewahi kula ‘githeri’? raki yangu aliniuliza.
194
195
(j) La, sijala lakini nimewahi kula ‘muthokoi’ mara kadha, nikamjibu.
2. Sahihisha matumizi ya kivumishi ‘-ingine’ katika sentensi zifuatazo:
(a) Ndege mwingine zimeruka.
(b) Ukuta nyingine umebomoka.
(c) Kuchoka nyingine kunazidi.
(d) Mahali pengine kunachukiza.
(e) Wanyama mwingine ni hatari.
(f) Matunda zingine ni matamu sana.
(g) Vyama nyingine havina faida.
(h) Maradhi zingine zinaua.
(i) Ulezi nyingine unasaidia.
(j) Misitu nyingine ni hatari.
3. Tumia kivumishi ‘-ote’ kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) Mabasi _________ yameondoka.
(b) Vitabu _________ viko wapi?
(c) Wakulima _________ wanaandamana.
(d) Karani ametulipa pesa _________.
(e) Mahali _________ pamefagiliwa.
(f) Wizi _________ umekwisha.
(g) Mchezo _________ ulivutia sana.
(h) Manukato _________ yamemwagwa.
(i) Ugali _________ umeungua.
(j) Kucheza _________ kuliliwaza.
4. Andika sentensi zifuatazo katika usemi wa taarifa:
(a) “Sitaki kusikia kelele hizo tena,” mama alitwamuru.
(b) “Chukua pesa hizi uende dukani ukanunue mkate na maziwa,”
binamu aliniambia.
(c) Tulipoka nyumbani, mama alisema, “Karibuni wanangu.”
(d) “Jana mlikula nini?” nyanya alituuliza.
(e) “Ni nini tofauti kati ya vivumishi na viwakilishi?” mwalimu alituuliza.
5. Sahihisha matumizi ya kivumishi ‘-o-ote’ katika sentensi zifuatazo:
(a) Barabara zozote itanifaa.
(b) Utepe yoyote itakatwa.
(c) Mahali popote itafunguliwa.
(d) Njia zozote itafungwa.
(e) Kulala yoyote kunaudhi.
194
195
(f) Ukulima yoyote una manufaa mengi.
(g) Mahali kokote patanifaa.
(h) Ndoo zozote itatumika.
6. Ukitumia heru t, Ts na T bainisha maneno katika sentensi zifuatazo:
(a) Mimi nimewahi kutembea Mombasa.
(b) Yeye ni mchezaji shupavu.
(c) Kesho nitaandika barua.
(d) Waziri alikuwa anataka kuhutubu.
(e) Vikombe vi jikoni.
7. Andika sentensi zifuatazo katika kauli ya kutendewa:
(a) Mama anapika wali.
(b) Mwalimu amefuta ubao.
(c) Mkulima atalima shamba hili.
(d) Shabani ametupatia mpira.
(e) Shemeji aliandika barua.
8. Tumia virai vifuatavyo kutungia sentensi:
(a) saa moja na nusu
(b) kwa sababu ya pesa
(c) hadi saa tatu usiku
(d) jambo lolote lile
D. Kusoma
1. Taja aina tatu tofauti za kamusi unazozifahamu.
2. Je, Kamusi ya Kiswahili Sanifu itamsaidiaje mwanafunzi wa somo la
Kiswahili?
E. Kuandika
1. Andika hadithi fupi kuhusu tukio la kushangaza ulilowahi kushuhudia.
2. Mahali unapotoka kuna msitu ulio karibu. Hivi karibuni msitu huo
umekuwa makazi ya wahuni wanaojicha humo na kuwashambulia watu
wanaopita karibu au kuingia humo. Andika onyo ukiwatahadharisha
watu kuhusu hatari hiyo.
3. Andika hotuba kuhusu kichwa: “Mazingira ni maisha”.
4. Andika mahojiano yasiyozidi kurasa mbili za karatasi kati ya mfugaji
na daktari wa mifugo.
196
197
Sura ya Kumi na Saba
A. Ufahamu
Ubabe wa Fumo Liyongo
Kila jamii ulimwenguni ina historia yake ambayo inaitambulisha na huionea
fahari. Historia hii ni sehemu ya uhai wa jamii hiyo na hupokezanwa kutoka
kizazi hadi kingine ili kuwakumbusha watakaokuja baadaye kuwa wana
jadi na historia fulani. Historia ya jamii mbalimbali hupokezanwa kwa njia
ya masimulizi ya matukio na visa mbalimbali. Katika jamii zetu, kabla ya
majilio ya utamaduni wa maandishi, historia hii ilipokezanwa kwa njia ya
mdomo, yaani kwa fasihi simulizi.
Katika jamii ya Waswahili kuna kisa kimoja ambacho ni maarufu sana.
Hiki ni kisa cha Fumo Liyongo. Kisa hiki kimetapakaa miongoni mwa jamii
nyingi katika pwani ya Kenya kuanzia kisiwa cha Pate hadi maeneo ya Ozi
na Kipini. Hii ndiyo sababu majina ya mbabe huyu anayedaiwa aliishi maelfu
ya miaka iliyopita ni mengi sana. Kwa wengine ni Fumo Liyongo, wengine
kwao ni Liyongo Fumo au hata Fumo Aliongwe.
Masimulizi mengi yanayomhusu Fumo Liyongo hayadokezi lolote
kuhusu maisha yake ya utotoni. Lakini kuna madai kuwa alipozaliwa
alikunywa maziwa mengi ajabu na kula wali ulioweza kuulisha umati wa
watu. Kama barobaro, Liyongo alikuwa na nguvu za ajabu sana. Vijana
wenzake walimwogopa kutokana na misuli yáke na mwili wake uliotutumka
maungo makubwa. Alikuwa na urefu wa kushangaza. Inadaiwa kuwa Wagalla
ambao kwa kawaida ni warefu sana walimkia magotini tu.
Wasifu wa Fumo Liyongo ndio ulimchongea hatimaye. Ndugu yake
Daudi Mringwari aliyechukua mamlaka ya uongozi wa kisiwa cha Pate
baada ya kifo cha baba yao alimwogopa sana. Licha ya kuwa Fumo Liyongo
alikuwa mpole na maridhia, Mringwari alimchelea kuwa huenda aamue
kumnyang’anya uongozi wake. Basi kwa kuchelea kuipoteza hadhi yake hiyo,
Mringwari alifanya njama ya kumwangamiza Fumo Liyongo. Kwa bahati,
Fumo Liyongo alipata u wa njama hizo na kutoroka Pate akahamia bara
alikoenda kuishi na Wasanye walioishi huko.
Mfalme alikuwa bado na njama yake ya kumwangamiza Fumo Liyongo.
Basi aliwaita Wasanye akaenda mzengwe nao na kuahidi kuwatuza ikiwa
watafanikiwa kumwua Fumo Liyongo. Wale jamaa walimwendea Fumo
Liyongo. Alikuwa pandikizi la mtu; jitu la mataruma manne. Hawangeweza
kupambana naye na kumkamata kama alivyotaka mfalme wao. Basi
waliamua kumshawishi ajiunge nao kula kikoa. Kazi ya kila mwanakikoa
ilikuwa kutunda matunda ya mkoma. Walifanya kazi hiyo kwa zamu hadi
ilipoka zamu ya Fumo Liyongo.
Bwana Liyongo,” walimwambia.
Naaaam!” aliitikia kwa sauti yake nzito.
196
197
“ Imeka zamu yako ya kuyatunda makoma,” walimkumbusha.
“Utafuteni mkoma kisha mniite,” aliwaambia.
Basi waliondoka kwenda kuusaka mkoma uliokuwa na makoma.
Walipoupata walimwendea Fumo Liyongo na kumjulisha. Fumo Liyongo
alikwenda hapo na kuandika jicho ule mkoma. Alitambua kuwa ulikuwa
mrefu ajabu. Kumbe nia yao ilikuwa kwamba watasubiri mpaka Fumo
Liyongo aukwee na pindi awapo huko kileleni, wamfume kwa mishale na
kumwua. Lakini Fumo Liyongo alikuwa na akili nzuri sana, aliitambua njama
yao hiyo. Badala ya kuukwea ule mkoma aliitupa mishale yake akiwa chini
na kuangusha kitawi kilichokuwa na makoma wakala na kusaza.
Wale Wasanye walipigwa na butwaa. Walijua kuwa hawataweza
kumwua Fumo Liyongo. Basi walishika tariki hadi alipokuwa mfalme na
kumweleza kila kitu kuanzia utandu mpaka ukoko. Mfalme alisikiliza kwa
makini. Baadaye aliwaambia,
“Kamwambieni kuwa huku mjini hakuna tishio tena. Aje huku kwa
sababu kuna ngoma iitwayo gungu na mwao.” Kila mtu alijua kuwa Fumo
Liyongo alikuwa na faka kubwa ya ngoma hizo; asingeweza kuzikosa.
Walipomshauri Fumo Liyongo alikubali na kusari hadi mjini. Lakini
alipokuwa huko alivamiwa na askari wapatao mia moja, akakamatwa na
kutiwa ndani. Mlangoni paliwekwa askari waliomlinda usiku na mchana.
Mfalme aliruhusu Kijakazi Saada aliyetumwa na mamake Liyongo, Mbwasha,
ampelekee chakula huko gerezani. Kila mamake alipompa Kijakazi Saada
chakula kizuri wale askari walimpoka na kukila. Baada ya muda mfalme
aliamua kumwua Fumo Liyongo. Basi alitumwa mtu kwenda kumweleza
198
199
Fumo Liyongo. “Fumo Liyongo utauliwa baada ya siku tatu,” alimwambia
kisha akasema, “lakini mfalme anakupa ruhusa ya kuomba kitu chochote
ukitakacho kwa mara ya mwisho.”
Fumo Liyongo aliwaza kwa muda kabla ya kusema kuwa, “Naomba
iandaliwe ngoma ya mwao nje ya gereza langu.” Yule jamaa aliupeleka ujumbe
wa Fumo Liyongo kwa mfalme. Siku hiyo Kijakazi Saada alipoka, Fumo
Liyongo aliamua kumtuma kwa mamake. Alimpa ujumbe wa shairi. Wale
askari hawakuwa wakisikiliza wakati huo. Fumo Liyongo aliimba:
Kijakazi Saada nakutuma huyatumika
Kamwambie mama ni muinga siyalimka
Afanye mkate pale kati tupa kaweka
Nikereze pingu na minyoo ikinemuka
Baada ya mamake kuupata ule ujumbe alitengeneza mikate miwili
mmoja mzuri na mwingine wa wishwa, mbaya. Alitia tupa kwenye ule mkate
wa wishwa. Wale askari walipoiona ile mikate waliuchukua ule mzuri kisha
wakamwambia Kijakazi Saada,
“Huu wa wishwa wanakula watumwa, mpelekee!” Liyongo alipouona
mkate huo alichanua kama ua kwa furaha. Siku iliyofuata wakati wa mwao
watu walizunguka gereza la Fumo Liyongo. Huko ndani alikuwa akiyaghani
mashairi mazuri huku anazikereza pingu kwa ile tupa. Alipomaliza aliuvunja
ule mlango na kuwagonganisha wale askari vichwa vyao wakafa .
Watu walipoona hivyo walinunua ‘pijo’ aina ya mguu niponye naye Fumo
Liyongo akarudi zake bara. Mfalme hakuiacha nia yake ya kutaka kumwua
Fumo Liyongo. Mara hii alimzaini mwanake Liyongo akamshawishi ajue ni
kitu gani kinachoweza kumwua. Alimwahidi kuwa angemwoza binti yake
kama angefanikiwa kukigundua kinachoweza kumuua babake. Yule kijana
alifanikiwa kumshawishi babake ambaye alimweleza kuwa kilichoweza
kumwua ni sindano ya shaba ikidungwa kwenye kitovu chake.
Kijana aliposikia hayo alifyatuka kama mshale na kwenda kumtapikia
mfalme kila kitu. Mfalme alimpa sindano hiyo na kumwambia akamuue
babake.Yule kijana alirudi alikokuwa babake na siku moja alipokuwa
amelala usingizi wa pono, akamdunga ile sindano. Kwa uchungu mwingi
Liyongo alibumburuka huku ameshika uta na mishale yake na kukimbia
hadi kisimani. Alikufa huku amepiga magoti na mshale ukiwa upoteni. Watu
walishindwa kukikaribia kisima kwa kudhani kuwa alikuwa hai na alikuwa
amekasirika. Hatimaye, walimwendea mamake Liyongo ambaye alimsogea
huku akiimba tumbuizo nzuri kumliwaza.
Hatimaye, walitambua kuwa alikuwa mfu. Mawingu ya machozi
yalianguka siku hiyo. Watu walimchukua na kwenda kumzika sio mbali na
mji wa Kipini. Yule mtoto wa Fumo Liyongo hakupata tuzo aliyoahidiwa.
Alitorokea mbali na kwao ambako alipuuzwa na hatimaye kuishia kufa kwa
majuto na masikitiko makubwa.
198
199
Maelezo ya msamiati
barobaro : kijana wa kiume aliyekwisha baleghe.
akaenda mzengwe : akafanya mazungumzo ya siri.
kula kiapo : kushirikiana; kufanya kazi pamoja.
andika jicho : tazama; tupia jicho; angalia.
kusaza : kubakisha chakula.
faka : mapenzi ya kitu fulani; kupenda kitu sana.
walimpoka : walimnyang’anya.
akiyaghani : akiyaimba.
u : fununu; tetesi.
alimzaini : alimshawishi ili akatende jambo ovu.
Maswali
1. Fumo Liyongo alijulikana kwa majina mbalimbali. Yataje majina
hayo.
2. Alipokuwa kijana, Fumo Liyongo alikuwa na sifa zipi?
3. Kwa nini Mringwari alimwogopa sana Fumo Liyongo?
4. Ni kwa nini Fumo Liyongo alikataa kupanda mkoma?
5. Eleza jinsi Fumo Liyongo alivyojinusuru aliposhikwa na askari baada
ya kushawishiwa aende akahudhurie ngoma ya mwao.
6. Ukitumia maneno yako mwenyewe, eleza maana ya lile shairi ambalo
Fumo Liyongo alimwimbia Kijakazi Saada.
7. Ni nini maana ya misemo ifuatayo:
(a) jitu la mataruma manne (b) pandikizi la mtu (c) pigwa na butwaa
(d) shika tariki (e) kuanzia utandu mpaka ukoko (f) kula kikoa
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Mighani/ Migani
Mighani au migani (uchache: mugani) ni kisa kinachopatikana katika jamii
nyingi. Kimsingi, watu wanaokuwa msingi wa mighani huenda waliwahi
kuishi wakati fulani lakini maisha yao, matendo yao na mambo mengine
yanayowahusu huzungukwa na sifa zisizokuwa za kawaida. Mfano maarufu
wa mughani ni ‘Fumo Liyongo’ ambao unasimuliwa hapo juu. Kisome kifungu
hicho kwa mara nyingine na kuchunguza sifa za Fumo Liyongo. Mifano
mingine ya mighani ni Lwanda Magere (Wajaluo), Koomenjue (Wameru)
Wangu wa Makeri (Wakikuyu) n.k.
Sifa za migani
Mighani huwa na sifa kadha. Miongoni mwa sifa hizo ni:
1. Huwazungumzia watu ambao waliishi, (wanadhaniwa kuwa waliishi)
na walikuwa na ujasiri mkubwa sana katika matendo yao.
200
201
2. Kama visasili, mighani huchukuliwa na watu kama hadithi zenye
ukweli fulani.
3. Hurithishwa wanajamii kutoka kizazi kimoja hadi kingine na wanajamii
hupenda kujitambulisha na mighani hiyo.
4. Wanaosimuliwa katika mighani walikuwa na sifa zisizokuwa za kawaida:
kuzaliwa kwao ni kwa ajabu, wanaweza kuchelewa kukua, wanakuwa
na uwezo usiokuwa wa kawaida wa watoto wa umri wao, walifanyiwa
majaribio ya kuuliwa, wanalazimika kutoroka walikozaliwa, wanasaidia
kuikomboa jamii yao na kifo chao hutokana na kusalitiwa.
Zoezi
(a) Toa mfano wa mighani kutoka jamii yako. Linganisha sifa za mtu
anayezungumziwa katika mighani hiyo na zile za Fumo Liyongo.
2. Matamshi bora: Vitate ch/j
ch j
pacha paja
chini jini
chambo jambo
chema jema
choka joka
kucha kuja
chuma juma
chenga jenga
mchi mji
kichana kijana
Zoezi
Chagua jibu sahihi kukamilisha sentensi.
(a) Wale watoto ________ (pacha, paja) walienda kuota moto bila
uangalifu wakachomeka ma ________ (paja, pacha) vibaya sana.
(b) Haya ma ________ (chini, jini) yalilala ________ (jini, chini) yalipotuona
tukikaribia kwa vile yalijua hatuwezi kuona ma________ (jini, chini)
yaliyolala ________ (chini, jini).
(c) Ingawa nilikula yamini kuwa sitaeleza ________ (jambo, chambo)
hilo kwa yeyote, nilipoka mjini nilipewa pombe bila kujua ilikuwa
________ (jambo, chambo) cha kunifanya nieleze lile ________ (jambo,
chambo).
(d) Nilipoenda mjini nilinunua nanasi ________ (jema, chema) na kitabu
________ (chema, jema), limau ________ (jema, chema) na kiko
________ (jema, chema) kisha nikarudi nyumbani kwa furaha.
(e) Nilipo________ (joka, choka), niliamua kulala chini ya mti kisha
nikaumwa na ________ (joka, choka) nikasema laiti nisinge________
(joka, choka) nisingeumwa na ________ (choka, joka).
200
201
(f) Niliamua kukata ________ (kucha, kuja) zangu kabla hakuja ________
(kucha, kuja) kwa vile nilijua kukicha mama ata________ (kuja,
kucha) chumbani mwangu na kunikaripia kwa kutokata ________
(kucha, kuja) kabla ya yeye ________ (kuja, kucha).
(g) ________ (Juma, Chuma) hili nitanunua ________ (juma, chuma) ili
________ (chuma, juma) lijalo niende nyumbani nikajenge ua wa
________ (chuma, juma).
(h) Baada ya ku________ (jenga, chenga) lile jengo nilitahayari nilipoona
vile nilivyoli________ (chenga, jenga) na kwa hivyo nikaanza
kum________ (jenga, chenga) mwenyewe kwa vile ________ (jengo,
chengo) hilo halikuvutia kamwe.
(i) Katika ________ (mchi, mji) huu kuna________ (miji, michi) mingi
inayouzwa huko masokoni tofauti na ________ (michi, miji) mingi
ambapo hata ukitafuta siku nzima hutapata ________ (mji, mchi)
hata mmoja.
(j) Huyu ________ (kijana, kichana) alichukua ________ (kichana, kijana)
changu na baada ya kukitumia akampa ________ (kichana, kijana)
mwingine lakini nilipomuuliza ________ (kijana, kichana) huyo
akasema hana ________ (kijana, kichana) chochote.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Sentensi
Kikundi nomino (KN) na kikundi tenzi (KT)
Sentensi hugawika katika sehemu mbili kuu kikundi nomino (KN) na
kikundi tenzi (KT). Kikundi nomino ni neno au fungu la maneno ambalo
habari yake inatolewa katika sentensi. Nacho kikundi tenzi ni neno au fungu
la maneno ambalo linatoa habari zaidi kuhusu kikundi nomino. Tazama
jedwali lifuatalo:
Kikundi nomino (KN) Kikundi tenzi (KT)
Mama yangu amekwenda sokoni.
Wanafunzi waliokuja jana wataondoka kesho adhuhuri.
Nyumba nyingi zilichomeka jana usiku.
Mashamba makubwa yatanunuliwa mwaka ujao.
Washukiwa watano walikishwa mahakamani leo.
Kiatu chake kilishonwa vizuri.
Fahali wawili watachinjwa kesho alasiri.
Wazee wanakutana ukumbini.
Babu na nyanya watawasili leo alasiri.
Gari lake limeanguka mtoni.
202
203
Ukitazama sentensi hizi utaona kuwa kikundi tenzi kinatoa habari zaidi
kuhusu kikundi nomino. Kwa mfano, kikundi tenzi ‘amekwenda sokoni’
kinatoa habari kuhusu kikundi nomino ‘mama yangu’. Nacho kikundi
tenzi ‘wataondoka kesho adhuhuri’ kinatoa habari kuhusu kikundi nomino
‘wanafunzi waliokuja jana’ n.k.
Neno kuu katika kikundi nomino ni nomino au kiwakilishi chake, nalo
neno kuu katika ‘kikundi tenzi’ ni kitenzi.
Zoezi
1. Tenganisha kikundi nomino (KN) na kikundi tenzi (KT) katika
sentensi zifuatazo. Kwa mfano:
Kondoo huyu atachinjwa kesho alfajiri na mapema.
Kondoo huyu - KN
atachinjwa kesho alfajiri na mapema - KT
(a) Watoto watundu walimtusi mzee yule.
(b) Babu yetu alitutembelea wiki jana.
(c) Nyumba zote za mtaa huu zinavuja.
(d) Baiskeli ya Maimuna iko wapi?
(e) Mbwa na paka hawa watapigana.
(f) Mamangu ni mkulima shupavu.
(g) Watu wanane wametiwa mbaroni.
(h) Msitu wa Kaloleni una kima wengi mno.
(i) Ndege hii hubeba abiria wengi.
(j) Mwawasa ataondoka leo alasiri.
2. Ongeza vikundi nomino vyovyote vinavyofaa kwenye vikundi tenzi
vifuatavyo ili kukamilisha sentensi:
1. ……………… atashtakiwa mahakamani.
2. ……………… ni wakulima shupavu.
3. ……………… ni aina ya nafaka.
4. ……………… ameumia vibaya sana.
5. ……………… aliwasili leo.
6. ……………… tukashinda mchezo huo.
7. ………………wanachukiana sana.
8. ……………… ataka saa ngapi?
9. ……………… ameenda wapi?
10. ……………… atakusaidia.
3. Ongeza vikundi tenzi vyovyote vinavyofaa katika vikundi nomino
vifuatavyo ili kukamilisha sentensi.
(a) Dadangu mdogo ……………………………
(b) Kalamu yako ……………………………
(c) Shule yetu……………………………
202
203
(d) Nchi ya Tanzania ……………………………
(e) Watoto wachafu……………………………
(f) Duka la shangazi ……………………………
(g) Kunguni wengi……………………………
(h) Nyoka mkubwa ……………………………
(i) Soko hili……………………………
(j) Wazazi wake ……………………………
2. Uundaji wa nomino kutokana na nomino
Kutokana na nomino moja, twaweza kupata nomino nyingine. Pale ambapo
nomino moja yapatikana kutokana na nomino nyingine, nomino zote
zinazohusika huwa na mzizi mmoja. Mfano:
Nomino Mzizi wa nomino Nomino nyingine
(i) shujaa -shujaa ushujaa
(ii) mwalimu -alimu ualimu
(iii) mpambe -pambe upambe
(iv) watoto -toto utoto
(v) mnyama -nyama unyama
(vi) wazungu -zungu uzungu
(vii) mzalendo -zalendo uzalendo
(viii) mabingwa -bingwa ubingwa
(ix) mganga -ganga uganga
(x) mkalimani -kalimani ukalimani
Zoezi
Jaza mapengo kwenye jedwali lifuatalo:
Nomino Mzizi Nomino nyingine
1. mbabe -babe
2. gwiji ugwiji
3. utu
4. -pelelezi
5. ufalme
6. mtaalam taaluma
7. wazee -zee
204
205
D. Kusoma
Matumizi ya maktaba
Ukubwa wa maktaba unatofautiana; zipo maktaba kubwa na nyingine
ndogo. Mpangilio wa vitabu unaopatikana katika maktaba hufuata utaratibu
maalum. Katika maktaba huwa kuna sehemu ambayo ina orodha ya vitabu
vinavyopatikana maktabani, ambayo inaweza kuwa katika kitabu fulani
(ikiwa maktaba inayohusika ni ndogo sana) au kwa kadi. Ikiwa maktaba
ina kadi, kuna aina mbili kuu za kadi ambazo hupatikana. Hizo ni: kadi za
majina na kadi za mada au somo.
Kadi za majina, huwa na majina ya waandishi mbalimbali pamoja na
anwani za vitabu walivyoandika. Taarifa nyingine zinazokuwako ni mwaka
wa kuchapishwa kwa kitabu, jina la mchapishaji n.k. Majina haya hupangwa
kwa mtindo wa alfabeti; kuanzia A mpaka Z.
Kadi za somo au mada huwa na masomo mbalimbali. Hapa vitabu vya
somo moja hupangwa pamoja kuanzia kile cha kwanza (kuanzia heru A
hadi Z).
Mfano wa kadi ya jina
Nabhany, Ahmed Sheikh
Umbuji wa Mnazi, A. A. El- Maawy (Mhariri)
Nairobi East Africa Publishing House
Xvii, Kur. 168
Kadi za somo au mada huwa na masomo mbalimbali. Hapa vitabu vya
somo moja hupangwa pamoja kuanzia kile cha kwanza (kuanzia heru A
hadi Z).
Mfano wa kadi ya mada
USHAIRI
Nabhany, Ahmed Sheikh
Umbuji wa Mnazi, A. A. El- Maawy (Mhariri)
Nairobi East Africa Publishing House
Xvii, Kur. 168
204
205
E. Kuandika
Utungaji wa kisanii: Michezo ya kuigiza
Mchezo wa kuigiza hutofautiana na riwaya na hadithi fupi, kwa mambo kadha.
Kwanza, hapa mwandishi anategemea mazungumzo kwa kiasi kikubwa
kuliko kusimulia. Pili, mchezo wa kuigiza unalengwa kuwasilishwa jukwaani.
Unapotaka kuandika mchezo wa kuigiza lazima uwazie jinsi unavyoweza
kuigizwa au kuwasilishwa jukwaani. Njia nzuri ya kuhakikisha kuwa
umeimudu stadi hii ni kuitazama michezo inayoigizwa jukwaani. Kanuni
kubwa ya kuandika mchezo wa kuigiza ni KUONYESHA sio KUSIMULIA.
Sifa za mchezo wa kuigiza
1. Lazima pawepo na jambo linalotendeka, yaani tukio linalofanyika.
2. Lazima wawepo watu wa kulitenda jambo hilo au wahusika. Ni vyema
kuwa na idadi ndogo ya wahusika.
3. Lazima pawepo na jukwaa au wanakotendea jambo hilo. Ukiandika
lazima ujiulize je, tendo hili linatendewa wapi na lini?
4. Lazima wawepo watu wanaolitazama tendo hilo au hadhira na
unapoandika lazima utumie lugha inayoweza kuwavutia.
5. Lazima pawepo na lengo la kule kuandika mchezo huo wa kuigiza.
Kanuni moja kuu ya kuandika mchezo mzuri wa kuigiza ni kutumia
mazungumzo kati ya wahusika vizuri. Kumbuka tofauti na riwaya, katika
mchezo wa kuigiza hii ndiyo njia ya pekee ya kuwasilisha maudhui yako. Je,
mazungumzo hutumiwa kufanya nini?
1. Kujulisha kwa kuhusisha mtendaji na tukio fulani, kwa mfano, “Nitaenda
sokoni kununua mahitaji yangu’’.
2. Kuchua hisia na mwelekeo alio nao mhusika fulani, kwa mfano, ‘Yule
jamaa alinipuuza.’’
3. Kuonyesha majibu, ‘‘Usiseme hivyo.’’
4. Kutaka taarifa au maelezo fulani, ‘‘Kwa nini ulifanya hivyo lakini?”
Ukitaka kuandika mchezo mzuri wa kuigiza, jaribu kutumia lugha ya
mazungumzo inayokaribiana na hali ya kawaida ya maisha, hakikisha lugha
ya wahusika ina sifa za kawaida kama kuingiliana wakati wa kuongea n.k.
206
207
Sura ya Kumi na Nane
A. Ufahamu
Mfumo wa jua na sayari
Katika anga za juu, kuna vitu vingi vinavyoelea huko. Kati ya vitu hivyo
kuna baadhi ambavyo hutoa mwanga wake vyenyewe; mwanga ambao
unajulikana kama mwanga wa asili. Vitu hivyo vinavyotoa mwanga huo
wa asili hujulikana kama nyota na humeremeta. Hata hivyo, kuna vingine
ambavyo havina uwezo wa kuutoa mwanga huo vyenyewe bali huupokea
mwanga wa jua na kuuakisi. Mfano mmoja wa vitu hivi ni mwezi ambao
hauna mwanga wake wa asili bali huupokea mwanga wa jua na kuuakisi.
Mojawapo wa nyota zilizoko angani ni jua ambalo huwa karibu sana na
dunia yetu kuliko nyota nyingine. Licha ya kuwa jua huonekana kubwa kuliko
nyota nyinginezo, zipo nyota ambazo zina ukubwa unaoupiku ule wa jua. Kila
mara tuangaliapo angani hususan wakati wa usiku mwangavu, tunaweza
kuona mamia ya nyota ambazo ziko kwenye makundi au mikusanyiko mingi
ajabu. Mkusanyiko mkubwa sana wa nyota na sayari hujulikana kama galaksi
na kwa kawaida zipo galaksi nyingi na zenye majina mbalimbali. Jua ambalo
hutuangazia dunia yetu liko kwenye galaksi inayofahamika kama uwanda
wa maziwa. Uwanda huu unaweza kuonekana kutoka upande mmoja wa
anga hadi upande mwingine ulio mbali.
Jua pamoja na vitu vyote vinavyolizunguka huunda mfumo mmoja
unaojulikana kama mfumo wa jua. Mfumo huu ni sehemu ndogo tu katika
galaksi ya uwanda wa jua. Mfumo wa jua huelezea hasa uhusiano uliopo kati
ya jua, vimondo, asteroidi na sayari. Sayari ni neno linalotumiwa kuelezea
matufe makubwa yanayoelea kwenye anga za juu. Wataalamu wanaamini
kuwa sayari zilitokana na mabadiliko yaliyotokea kwenye jua. Inasemekana
kuwa zama za zama nyota moja kubwa ajabu ilipita karibu na jua kwa
mwendo wa kasi. Matokeo ya kupita huko yalikuwa ni kutibuliwa kwa ukanda
wa nje na baadhi ya maada ya jua hilo. Ni baada ya tukio hilo ambapo zile
maada zilikusanyika na kuunda sayari ambazo zilianza kulizunguka jua kwa
miduaradufu inayojulikana kama obiti.
Dunia yetu ni moja kati ya sayari hizo mbalimbali zilizoundwa
kutokana na kisa hiki kinachosimuliwa tangu zamani. Sayari nyingine ni
Zebaki, Zuhura, Mirihi, Mushtara, Sarateni, Zohali, Kauri na Utaridi. Hizi
ndizo sayari kuu ambazo zimegunduliwa na wanajimu mpaka leo. Licha
ya kuendelea kulizunguka jua, sayari hizi zinabaki kwenye mihimili yao
zenyewe. Dunia na Mirihi ni sayari ambazo zimeundwa kwa miamba, ilhali
Saratani, Mushtara, Zebaki, Zuhura na Utaridi zimeundwa kwa gesi kwa
kiasi kikubwa. Utaridi ni sayari ambayo ipo katika hali ya barafu na ndiyo
iliyo mbali sana kutoka lilipo jua.
Zebaki ndiyo sayari iliyo karibu sana na jua na ukubwa wake ni takriban
theluthi moja ya ukubwa wa Dunia. Sayari hii haina hewa wala mwezi
206
207
unaoizunguka kama ilivyo dunia. Zuhura ni sayari ya pili kutoka lilipo jua.
Hii ni sayari inayoonekana kwa urahisi sana kwa kuwa ndiyo inayofuatia
mwezi na jua kwa mng’ao angani. Sayari hii huweza kuonekana asubuhi
upande wa mashariki kabla ya kupambazuka kwa jua au mara tu baada ya
machweo ya jua. Kutokana na hali hii, sayari hii hujulikana kama nyota ya
asubuhi au nyota ya jioni. Sayari ya tatu kutoka lilipo jua ni Dunia.
Uhai uliopo katika Dunia ni tokeo la umbali wa wastani kutoka lilipo
jua. Kama sayari hii ingekuwa karibu na jua ingekuwa na joto jingi kiasi
cha kukosa uhai. Vivyo hivyo kama ingekuwa mbali sana na jua kama
ilivyo Utaridi pasingekuwa na uhai kwa sababu ya baridi nyingi mno. Kwa
kawaida Dunia hujizungusha kutoka Magharibi kuelekea Mashariki kwenye
mhimili wake na kufanya usiku na mchana. Ili kuweza kujizungusha mara
moja kwenye mhimili huo, Dunia huhitaji saa 24. Kutokana na umbo lake
la tufe au duara, kama sayari nyinginezo, upande mmoja uwapo na mwanga
mwingine huwa na giza.
Dunia hulizunguka jua mara moja kwa siku 365, saa 6 na dakika 9 na
sekunde 9 na kuunda kipindi ambacho hujulikana kama mwaka mmoja.
Dunia ina mwezi mmoja ambao huizunguka mara moja kwa siku 28. Mwezi
huo huakisi mwanga utokanao na jua na kusaidia kuiangaza Dunia wakati
wa usiku.
Sayari ya nne kutoka lilipo jua ni Mirihi. Sayari hii hujulikana kama
Sayari Nyekundu kwa kuwa ardhi yake huonekana kama jangwa jekundu
kutokana na picha ambazo zimewahi kupigwa kutoka huko. Sayari ya tano
kutoka lilipo Jua ni Mushtara au Sumbula na ndiyo sayari kubwa kuliko
sayari zote katika mfumo wa jua. Sayari hii imezungukwa na mawingu mengi
pamoja na gesi ya aina ya haidrojeni. Lipo wingu moja maarufu linaloizunguka
sayari hii ambalo hujulikana kama Doa Jekundu. Sayari inayoifuata kwa
umbali kutoka lilipo jua ni ile ya Sarateni ambayo imezungukwa na ringi
zinazoifanya ipendeze.
Sayari ya saba kutoka lilipo jua ni ile ya Zohali nayo inafuatiwa na
Kauri. Sayari hii ina miezi miwili inayoizunguka. Kauri ndiyo sayari ya
mwisho kabisa.
208
209
Maelezo ya msamiati
unaoupiku : unaoupita.
hususan : hasa.
tufe : kitu chenye umbo la mviringo.
tibuliwa : vurugiwa; haribiwa.
wanajimu : wataalamu wa anga za juu.
Maswali
1. Vitu vinavyotoa mwanga wa asili kwenye anga za juu huitwaje na vina
sifa gani?
2. Vitu ambavyo havina mwanga wa asili kwenye anga za juu hutoa mwanga
wake wapi? Toa mfano mmoja wa vitu hivyo.
3. Galaksi ni nini?
4. Ni nini maana ya ‘mfumo wa jua’?
5. Ni yepi mabadiliko yaliyosababisha kutokea kwa sayari?
6. Ni nini tofauti kati ya Dunia na Zebaki?
7. Kama dunia ingekuwa karibu sana na jua maisha yangelikuwa mazuri
mno. Je, ni kweli? Fafanua.
8. Dunia huhitaji siku ngapi kulizunguka jua?
9. Ni kwa ni Mirihi ikaitwa Sayari Nyekundu?
10. Taja sayari zinazowakilishwa na heru (a) – (i)
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimu Jamii
Mazungumzo : Kituo cha polisi
inspekTa njue
: Konstebo Mbarire!
Mbarire
: (Akipiga saluti): Ndiyo afande!
inspekTa njue
: Fanya chapchap kuwashughulikia watu hawa!
Mbarire
: Ndiyo afande! (Inspekta anaondoka. Mbarire
anawageukia waliopo) Nyie hapo! (Sota na
mkewe, Mueni, wanasogea karibu) Mna shida
nyie?
soTa
: Tunayo ehh!
Mbarire
: Ambayo ni?
Mueni
: Tunataka kupiga ripoti
Mbarire
: Kupiga ripoti?
soTa
: Ndiyo asa!
Mbarire
: (Anachukua kalamu na daftari) Kuhusu nini?
208
209
Mueni
: Kapotea; hatujui aliko!
Mbarire
: Jina lake ni nani?
sola
: Kim Mwau (Mbarire anaandika)
Mbarire
: Kapotea lini?
sola
: Hii siku ya tatu!
Mbarire
: Je, mmehakikisha kuwa hajaenda kwa maraki,
jamaa au popote pale!
Mueni
: Tumeulizia kote; hatukumpata.
Mbarire
: Je; ana tatizo la aina yoyote ile?
sola
: Tatizo?
Mbarire
: Ehhh, vipi akili yake!
Mueni
: Hana neno, mzima. (Mtuo) Tuseme hana shida
tunayoijua!
Mbarire
: Alipoteaje lakini?
sola
: Majuzi kenda kwenye sherehe ya mwenzake
lakini hajarudi tangu wakati huo!
Mbarire
: Mwenzake nani?
Mueni
: Mong’are; mwanafunzi mwenzake (Mbarire
anaandika jina hilo)
Mbarire
: Huyo Mong’are anasemaje?
sola
: Kwamba baada ya sherehe aliondoka; salama
salimini!
Mbarire
: (kama anakumbuka jambo) Mnasema sherehe
yenyewe ilikuwa lini?
sola
: Juzi jioni, kwenye mtaa wa Kizaizai!
Mbarire
: (Akimgeukia askari mwenzake aliyeko hapo
karibu) Aisee afande Magero, ile fujo ya Kizaizai
ilikuwa lini?
Magero
: Juzi Jumamosi.
Mbarire
: Je, kuna watu waliokamatwa huko?
Magero
: (Akiangalia kwenye kitabu alicho nacho) Wapo.
(Mtuo) Kuna vijana wawili…Sikumbuki idadi yao
hasa…walikamatwa na misokoto ya bangi.
Mbarire
: Unakumbuka majina yao?
Magero
: La….(anatua kidogo) Kim…sina hakika lakini
mmoja alikuwa anaitwa kitu kama M....
Mbarire
: Mwau?
Magero
: Jina ndilo hilo Kim Mwau! (Mbarire anawageukia
Sota na Mueni)
sola na Mueni
: (kwa pamoja) Mungu wangu!
210
211
Zoezi
1. Unakiri ni kwa nini kulikuwa na fujo Kizaizai?
2. Je, unajifunza nini kutokana na mazungumzo haya?
3. Taja mambo manne yanayoathiri na kuelekeza mazungumzo uliyoyasoma
hapo juu.
Matamshi bora: Vitate f/v
f v
afya avya
fito vito
fuja vuja
futa vuta
wafu wavu
Soma: Vitanza ndimi
(a) Nilimwambia rafiki yangu asiavye kwa sababu akiavya afya
itaharibika.
(b) Baba aliponiambia nimletee vito nilidhani ni to kwa hivyo nikaenda
msituni nikakata to nikamletea lakini aliponiona nimebeba to
badala ya vito akaniuliza ni tangu lini to zikawa vito.
(c) Jumba langu lilipoanza kuvuja nilianza kujuta kwa nini nilifuja pesa
zangu huku nikijua wazi kuwa mvua zikinyesha jumba langu litavuja.
(d) Mwalimu aliponiambia nifute ubao nilikiri ni kuvuta kwa hivyo
nikauvuta kwa nguvu zangu zote huku wanafunzi wenzangu
wakinicheka kwa kutojua tofauti ya kufuta na kuvuta!
(e) Kuna tofauti kubwa kati ya wafu na wavu kwa vile wafu ni watu
waliokufa na wavu ni kifaa cha kuvulia.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Sentensi ambatano
Ili kuweza kuelewa kinagaubaga muundo wa sentensi ambatano, inabidi
tujikumbushe kuhusu muundo wa sentensi sahili. Sentensi sahili ni sentensi
yenye kitenzi kimoja pekee. Kwa mfano:
(a) Onyango amekwenda sokoni.
(b) Siafu hawa watamuuma mwanangu.
(c) Wachezaji watawasili kesho.
(d) Wafungwa wametoroka.
(e) Vifaa vyote vitaletwa.
Nazo sentensi ambatano hujengwa kwa muungano wa sentensi mbili
zilizo sahili (ambazo pia hujulikana kama vishazi huru). Sentensi hizi
huunganishwa kwa matumizi ya viunganishi au kwa alama mbalimbali
za kuakisha. Tukitumia sentensi zilizotajwa hapo juu, tunaweza kuunda
210
211
sentensi ambatano kama zifuatazo:
(a) Onyango amekwenda mtoni na Oketch amekwenda shambani.
(b) Siafu hawa watamuuma mwanangu lakini mimi nitawaua wote.
(c) Wachezaji watawasili kesho kisha watasarishwa hadi hotelini mwao.
(d) Wafungwa wametoroka, hata hivyo watatiwa mbaroni wote.
(e) Vifaa vyote vitaletwa na vitauzwa kwa bei rahisi.
Tunaweza kufahamikiwa zaidi kuhusu sentensi ambatano kwa
kuzitazama katika mazingira ya jedwali lifuatalo:
Sentensi sahili Kiunganishi Sentensi sahili
Onyango amekwenda mtoni na Oketch analima
shambani.
Siafu hawa watakuuma lakini mimi nitawaua wote.
Wachezaji watawasili leo halafu rais atawahutubia
kesho.
Wafungwa watatoroka hata hivyo askari wetu
watawakamata wote.
Bidhaa nzuri zitaletwa kisha mchuuzi ataziuza kwa
bei nafuu.
Kutokana na jedwali hili, sentensi sahili zilizounda sentensi ambatano
zinaonekana wazi. Sentensi hizi sahili zinazoungana ili kuunda sentensi
ambatano huitwa vishazi huru. Lakini mengi zaidi kuhusu ‘vishazi’
tutayashughulikia katika kidato cha tatu.
Zoezi
Kutokana na sentensi sahili zifuatazo, unda sentensi ambatano ukitumia
viunganishi vya aina mbalimbali.
(a) Mama alika jana _____________.
(b) Watu walika uwanjani kwa wingi _______________.
(c) ________________ tutawapigia mako.
(d) ______________ tutaondoka.
(e) Wanafunzi wa kidato cha kwanza walifurahi ____________.
(f) _____________ nikalala usingizi wa pono.
(g) _____________ nitakaa hadi jioni.
(h) Nyoka aliuawa kwa ______________.
(i) _______________ hadi tukashiba.
(j) _______________ zitafunguliwa mwezi wa Januari.
Upambanuzi wa sentensi ambatano kwa kielelezo cha mstari
Kupambanua sentensi ni kuonyesha muundo wake au jinsi ilivyoundwa.
Katika kufanya haya, kitu cha kwanza ni kutambulisha sentensi sahili
212
213
zilizoijenga sentensi ambatano inayohusika pamoja na kiunganishi
kilichotumika kuziunganisha. Kisha tambulisha kikundi nomino na kikundi
tenzi katika kila sentensi sahili pamoja na aina mbalimbali za maneno
yanayojenga kila kikundi. Kwa kutumia sentensi ambatano tulizotaja hapo
awali tunaweza kuzipambanua kama ifuatavyo:
Zoezi
Pambanua sentensi ambatano zifuatazo ukitumia kielelezo cha mstari:
(a) Mama na baba wamekuja na wametuletea zawadi kemkem.
(b) Vitabu vitatu vilinunuliwa lakini vikaibiwa jana asubuhi.
(c) Chakula cha mtoto kimeiva hata hivyo kimeliwa na paka.
(d) Watoto wenye bidii walipongezwa sana kisha wakapewa zawadi.
(e) Wawindaji haramu wamekamatwa na watapelekwa kortini kesho.
2. Vihusishi (H)
Haya ni maneno yanayoonyesha uhusiano ulioko baina ya neno moja na
jingine au baina ya kikundi kimoja cha maneno na kingine. Kwa mfano:
(a) Punda analala kando ya barabara.
(b) Watoto wameweka vitabu juu ya meza.
(c) Mshtakiwa alihukumiwa kulingana na sheria.
(d) Niliweka sufuria chini ya meza.
(e) Nilikwenda mjini kwa basi.
Sentensi sahili Kiunganishi Sentensi sahili Muundo (kwa
kielelezo cha mstari)
Onyango na Oketch analima KN (N)+KT (T+E)+U+
amekwenda shambani. KN (N)+KT (T+E)
mtoni
Siafu hawa lakini mimi nitawaua KN (N+V)+KT (T)+U+
watakuuma wote. KN (W)+KT (T+W)
Wachezaji halafu rais atawahutubia KN (N)+KT (T+E)+U +
watawasili leo kesho. KN (N)+KT (T+E)
Wafungwa hata hivyo askari wetu KN (N)+KT (T)+U +
watatoroka watawakamata KN (N+V)+KT (T+W)
wote.
Bidhaa nzuri kisha mchuuzi ataziuza KN (N+V)+KT (T) + U +
zitaletwa kwa bei nafuu. KN (N)+KT (T+E)
212
213
(f) Sisi tulilipwa ridhaa na kampuni hiyo.
(g) Mama aliweka maziwa yangu katika kibuyu.
(h) Mimi sitakunywa chai bila sukari.
(i) Tulivumilia njaa hadi asubuhi.
(j) Nitatumia gari la raki yangu.
Zoezi
Tumia vihusishi vifuatavyo kutungia sentensi:
(a) kwa sababu ya (b) za (c) kuliko (d) zaidi ya (e) baada ya
D. Kusoma
Makala
Soma makala hii kisha ujibu maswali yafuatayo:
Methali zafaa sana katika malezi. Kwa maneno machache yaliyopangiliwa vito vya
hekima mtu huweza kupata kitabu kizima cha mafundisho. Maneno ndani ya methali
huvutia sana na kushawishi akili kuyakariri. Hivi, ili kupata maana sadifu ya methali ni
lazima mtu aweze kufafanua maneno yote yalivyotumiwa katika vipengee vyake vyote.
Kwa njia hii mwanafunzi anajiongezea msamiati wa Kiswahili na kuichambua lugha
vilivyo. Methali, mara kwa mara, hutumia tamathali za lugha katika kueleza mambo
ya dunia yanavyojiri. Hivi, methali huwa ni pambo kamili la lugha na vito vya hekima.
Mfano (a) Usiache mbachao kwa msala upitao.
Methali hii inazungumzia juu ya mbacha na msala (au mswala, kama wengine
walivyozoea kutamka). Methali hii inaonya. Inasema kuwa usiache mbacha wako kwa
tamaa ya msala upitao tu.
Mbacha na msala ni aina za mikeka. Hivyo, methali nzima inatoa fundisho kwa
kutumia mfano wa aina mbili za mikeka. Wale mabingwa wa sanaa na ufundi wa ususi
wataelewa vyema mfano huu. Mbacha ni namna ya mkeka mdogo mkuukuu. Watu
wengine hutumia neno hili wanapotaja mkeka wowote uliosukwa vibaya vibaya ambao
hauna mapambo, na pengine umechakaa. Hutumiwa kwa kutandikwa chini sakafuni,
au kwa kukalia, au kuanikia vitu. Msala ni namna ya mkeka mdogo vilevile, lakini
hutengenezwa maridadi kwa umbo pengine la mduara au mviringo. Ni mwepesi na
huchukulika kwa urahisi. Mara nyingi siku za Ijumaa au za sikukuu za Iddi, Waislamu
huenda nao misikitini. Hivi, msala hutumika sana kuswalia.
Methali hii inatuonya tusiwe na tabia mbaya ya kuacha vitu tulivyo
navyo, hata kama twaviona duni, kwa tamaa ya kupata vingine vizuri zaidi
ambavyo huenda tusivipate.
(Makala ya ‘Fasili ya Methali’, Peter A Msuya, Katika Mulika na 9, 1977)
214
215
Zoezi
1. Kwa nini tunasema kuwa kifungu hiki ni makala?
2. Toa mfano wa methali inayofanana kimaana na methali iliyofafanuliwa
katika makala hii.
E. Kuandika
Mahojiano
Mahojiano ni nomino inayotokana na kitenzi ‘hoji’ ambacho humaanisha
kudadisi au kuuliza maswali kwa nia ya kutaka kupata habari fulani. Kwa
kawaida mahojiano huhusisha watu wawili au zaidi: anayeuliza maswali
hayo (mhojaji) na anayeulizwa maswali yenyewe (mhojiwa). Mtu anayetaka
kufanya mahojiano huweza kuwa na maswali maalum ambayo ameyaandika
mahali fulani. Karatasi yenye maswali yanayotumiwa na mhojaji hujulikana
kama hojaji. Kuna mahojiano ya aina mbalimbali kama: mahojiano ya
kazi, mahojiano ya kujiunga na shule, mahojiano ya waandishi wa habari,
mahojiano ya mtati wakati wa utati n.k.
Sifa za mahojiano
1. Mhojaji huuliza maswali ambayo hujibiwa na mhojiwa.
2. Anayehoji huenda akafuata orodha ya maswali aliyo nayo au akahoji
pasi na orodha hiyo.
3. Mahojiano hufanyika kwa njia ya mazungumzo kati ya mhojaji na
mhojiwa
4. Mhojaji anaweza kuandika majibu ya maswali anayopewa kadiri
yanavyotolewa.
5. Mawazo yanayopatikana lazima yaonyeshe mtiririko mzuri na yawe
na mantiki.
Mahojiano kati ya Waziri wa Kilimo na mwandishi wa habari
Mwandishi wa habari
: Bwana Waziri, katika hotuba yako
umesema kuwa kuna matumaini
makubwa
ya mapato ya kilimo kuwa bora katika
miaka miwili ijayo?
waziri
: Ndiyo, naamini hivyo.
Mwandishi wa habari
: Ni sababu zipi zinazokufanya uamini hivyo?
waziri
: Kwanza, kwa bahati nzuri hali ya hewa
inaelekea kubadilika. Ukame ambao
umekuwako unatoweka na wataalam wa
hewa wanatabiri kuwa itakuwepo mvua
nzuri. Pili, siku hizi kuna njia nyingi na
214
215
bora zaidi zinazoweza kutumiwa katika
ukulima.
Mwandishi wa habari
: Ni kweli bwana Waziri lakini kuna tatizo
la umaskini pia. Wakulima wengi hawana
uwezo wa kununua vifaa muhimu au
kuitumia teknolojia hiyo mpya.
waziri
: Serikali inanuia kuwasaidia.
Mwandishi wa habari
: Kwa njia gani?
waziri
: Kwanza, tunadhamiria kuyasaidia
mashirika ya kilimo ambayo yamekuwa
yakiwapa mikopo wakulima kwa miaka
mingi. Pili, tunawahimiza wenye benki
za kibinafsi, wapunguze riba wanayotoza
mikopo wanayowapa wakulima ili
kuwahamasisha wakulima kuchukua
mikopo.
Mwandishi wa habari
: Je, wakulima wasiokuwa na uwezo wa
kuchukua mikopo wafanyeje?
waziri
: Tumepokea msaada kutoka kwa maraki
zetu ambao tunanuia kuutumia kuwasaidia
wakulima kama hao.
Mwandishi wa habari
: Kuwasaidia kwa njia ipi?
waziri
: Nyingi! Kwa mfano, kuwawezesha kupata
bidhaa fulani kwa bei nafuu zaidi.
Mwandishi wa habari
: Bwana waziri utasemaje kuhusu tatizo la
malipo ya wakulima kucheleweshwa?
waziri
: Hili ni tatizo kubwa sana. Wizara
yangu
inanuia kushirikiana na idara
zinazohusika kuhakikisha kuwa tatizo hilo
limepunguzwa…
Mwandishi wa habari
: Kupunguzwa tu?
waziri
: Sio kupunguzwa tu bali kuondolewa hasa!
Mwandishi wa habari
: Asante sana mheshimiwa Waziri.
Zoezi
Wewe ni mwandishi wa habari wa jarida la shuleni. Umetumwa kutafuta
maoni ya majirani zenu shuleni kuhusu wanafunzi wa shule yenu. Andika
mahojiano hayo.
216
217
Sura ya Kumi na Tisa
A Ufahamu
Ndizo zipi haki hizo?
MTu i
: Kuna jambo lanitinga, na kunipa dukuduku,
Sitaki niwe mjinga, wa kusemwa zumbukuku,
Nataka nipate mwanga, nitoke niliko huku,
Hizi haki za watoto, ndizo zipi haki hizo?
MTu ii
: Hata mimi kwa hakika, jambo hilo laniuma,
Watu wakijumuika, hayo hayo wanasema,
Yamenipata mashaka, sasa naomba kalima,
Hizi haki za watoto, ndizo zipi haki hizo?
Mjuzi
: Moja haki ya kuishi, aliyo nayo mtoto,
Asiuliwe bilashi, kuonekana kitoto,
Apumue na aishi, bila bughudha mtoto,
Hiyo haki ya mtoto, asiyejua ni nani?
MTu i
: Niambiye yenye mwanga, bila ya kutia chuku,
Hawa wetu vijulanga, ili wasije tushuku,
Kwamba tunawabananga, kwa maisha ya ki huku,
Hizo haki za watoto, nyingine nazo ni zipi?
MTu ii
: Sema bila ya wahaka, hata kama linauma,
Wala usiwe na shaka, mabaya tutakusema,
Penye giza tunatoka, akina baba na mama,
Hizo haki za watoto, nyingine nazo ni zipi?
Mjuzi
: Ni haki ya matibabu, nyingine yake mtoto,
Daktari kumtibu, impatapo vuguto,
Na wawepo matabibu, walipo wote watoto,
Hiyo haki ya mtoto, itieni akilini.
Halafu na lishe bora, na aipate mtoto,
Asile vya kuchakura, vilivyo na dhiki nzito,
Maji anywe yalo bora, wala si yale ya mto,
Hiyo haki ya mtoto, itieni akilini.
Tena awe na kivazi, pia makazi mtoto,
Asiyakose mavazi, muili wake ni kito,
Ukitunzewe mzazi, kinayo thamani nzito,
Hiyo haki ya mtoto, jamani ikumbukeni.
Anahitaji ulinzi, asikumbwe na mazito,
Hino kubwa yetu kanzi, athaminiwe mtoto,
216
217
Asichumishwe madanzi, kuajiriwa mtoto,
Hiyo haki ya mtoto, milele zingatieni.
Asiteswe asilani, ajevimba kama puto,
Asiwekwe gerezani, kufanyizwa kazi nzito,
Awe huru maishani, yasiwapate majuto,
Hiyo haki ya mtoto, daima ifumbateni.
MTu i
: Mambo umeshayapanga, hamna lililopiku,
Sasa ninaona mwanga, ushatoweka usiku,
Haki sitazibananga, na ni kweli sio chuku,
Zipo zilizobakiya, kama zipo zipi hizo?
Mjuzi
: Na apatiwe hifadhi, aishi vyema mtoto,
Bila shida na maudhi, kamwe asipigwe ngoto,
Yawe maisha ya hadhi, akue vyema mtoto,
Hiyo haki ya mtoto, kichwani izame ndani.
Kisha asipewe dawa, za kumlevya mtoto,
Akenda kilewalewa, hili kwanza fahamuto,
Kisha na kubughudhiwa, kingono huwa majuto,
Hiyo haki ya mtoto, moyoni isaki ndani.
Haramu kubaguliwa, ati kwamba ni kitoto,
Ujue haki ni sawa, na watu wote mtoto,
Na vita vikichipuwa, asipigane mtoto,
Hiyo haki ya mtoto, rohoni iche ndani.
Na awapo mlemavu, vyake viungo mtoto,
Asionyeshwe kibavu, leo ninatoa mwito,
Atunzwe kwa utulivu, pia mapenzi mtoto,
Hiyo haki ya mtoto, bongoni izike ndani.
Mwisho apate elimu, imfaayo mtoto,
Aupate utalamu, ajue zuri na zito,
Asibaki bahaimu, asijie mtoto,
Hiyo haki ya mtoto, kichwani izame ndani.
MTu ii
: Uliyosema muhibu, kinatosha chake kima,
Hiyo ya mwana taabu, ninaona itakoma,
Taweleza hata babu, na wote wasiosoma,
Hizi haki za watoto, watambue ndizo zipi!
218
219
Maelezo ya msamiati
zumbukuku : mjinga; mpumbavu; zuzu.
bilashi : bure.
bughudha : usumbufu.
tunawabananga : tunawaharibu.
wahaka : wasiwasi.
vuguto : hari; mwako; fukuto.
kuchakura : kupekuapekua.
kanzi : hazina.
kivazi : nguo; libasi.
kito : madini ya thamani.
ifumbateni : ishikeni vyema.
fahamuto : jua vizuri.
bahaimu : mjinga.
Maswali
1. Badala ya ‘Ndizo zipi haki hizo?’ unaweza kulipa shairi hili kichwa kipi?
Taja vichwa vitatu.
2. Je, shairi hili ni la aina gani? Kwa nini?
3. Ni vipi vina vya ukwapi na vya utao vya ubeti wa kwanza na wa pili?
4. Kila mshororo una mizani mingapi?
5. Taja haki tano za mtoto zilizozungumziwa katika shairi hili.
6. Kwa nini unadhani mtoto anafaa kulindwa?
7. Mtoto hapaswi kufanya kazi yoyote akiwa nyumbani isipokuwa kula,
kucheza na kulala. Hii ni mojawapo ya haki za mtoto. Je, unakubali?
Fafanua.
8. Taja njia tano unazojua ambazo hutumika kuwadhulumu watoto.
9. Eleza maana ya maneno haya kulingana na matumizi yake kwenye
shairi:
(a) muhibu (b) maudhi (c) isaki (d) puto
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Ufahamu wa kusikiliza
Sikiliza taarifa utakayosomewa na mwalimu yenye kichwa “Jembe halimtupi
mtu” kisha ujibu maswali yafuatayo:
1. Binadamu walijilisha vipi kabla ya majilio ya kilimo?
2. Ni mimea aina gani iliyokuzwa kwanza na binadamu?
3. Ni kwa vipi maisha ya kuhamahama yalipungua kutokana na maendeleo
ya kilimo?
4. Kutokana na mapinduzi ya karne ya kumi na nane kilimo kilibadilikaje?
218
219
5. Taja maendeleo mengine ya kilimo yaliyotokea katika karne ya kumi
na tisa na ishirini.
6. Ni nini maana ya methali ‘ukilima pantosha, utavuna pankwisha’?
2. Matamshi bora: Vitate ch/sh
Soma maneno haya:
ch sh
chati shati
chombo shombo
choka shoka
chokoa shokoa
Soma: Vitanza ndimi
1. Kakangu aliniletea chati lakini mimi nilitaka shati kwa vile nina chati
ila sina shati kwa hivyo nilimrudishia chati nikamwambia alete shati.
2. Yule mpishi alipoingia na chombo alianza kunuka shombo nikamwuliza
ni kwa nini ananuka shombo akasema si yeye ananuka shombo bali ni
chombo alichobeba kilichonuka shombo kwani chombo kilichopikiwa
samaki hakiachi kunuka shombo.
3. Achoka alichoka kwa kukata kuni kwa shoka butu.
C. Saru na matumizi ya lugha
Mnyambuliko wa vitenzi
Kauli ya kutendeka na kutendana
Kauli ya kutendeka huonyesha kuwa kitendo kinatokea tu bila kueleza ni
nani anayesababisha kufanyika kwake. Nayo kauli ya kutendana huashiria
kuwa watu (au viumbe vyovyote) wawili au zaidi wanafanya kitendo ambapo
mmoja anamfanya mwenzake naye mwenzake anamfanya kitendo kile kile.
Tazama jedwali lifuatalo:
mzizi kutenda kauli ya kutendeka kauli ya kutendana
pig- pig-a pig-ik-a pig-an-a
chor- chor-a chor-ek-a chor-an-a
ruk- ruk-a ruk-ik-a ruk-an-a
omb- omb-a omb-ek-a omb-an-a
fagi- fagi-a fagi-lik-a fagi-an-a
to- to-a to-lek-a to-an-a
chun- chun-a chun-ik-a chun-an-a
som- som-a som-ek-a som-an-a
anz- anz-a anz-ik-a anz-an-a
jeng- jeng-a jeng-ek-a jeng-an-a
220
221
Zoezi
1. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuandika vitenzi vilivyomo katika
kauli za kutendeka na kutendana.
Mzizi Kauli ya kutendeka Kauli ya kutendana
k.m. tum- tum-ik-a tum-an-a
kat- _______ _______
ruk- _______ _______
ongez- _______ _______
tend- _______ _______
tandik- _______ _______
fuat- _______ _______
pit- _______ _______
2. Geuza kitenzi kilichomo mabanoni kulingana na kauli uliyopewa.
Kwa mfano:
Nyumba hii ina________ rahisi. (jenga, tendeka)
Nyumba hii inajengeka rahisi.
(a) Chakula hiki kina________. (pika, tendeka)
(b) Mchezo huu una________ vizuri. (tendeka, cheza)
(c) Watu wale wana________ hadithi. (toa, tendana)
(d) Mama na baba wanafaa ku ________. (saidia, tendana)
(e) Wasichana hawa hupenda maisha ya ku________. (chimba, tendana)
Kauli ya kutendeana na kutendeshwa
Vitenzi hivi hujengwa kutokana na vitenzi vilivyonyambuliwa. Tazama
jedwali lifuatalo:
Mzizi Kauli ya Kauli ya Kauli ya
kutenda kutendeana kutendeshwa
pig- pig-a pig-i-an-a pig-ish-w-a
chez- chez-a chez-e-an-a chez-esh-w-a
som- som-a som-e-an-a som-esh-w-a
end- end-a end-e-an-a end-esh-w-a
kop- kop-a kop-e-an-a kop-esh-w-a
andik- andik-a andik-i-an-a andik-ish-w-a
lim- lim-a lim-i-an-a lim-ish-w-a
kat- kat-a kat-i-an-a kat-ish-w-a
Zoezi
Kamilisha jedwali lifuatalo:
220
221
Mzizi Kauli ya kutendeana Kauli ya kutendeshwa
pik- pik-i-an-a pik-ish-w-a
chom- _______ _______
imb- _______ _______
ka- _______ _______
twa- _______ _______
kop- _______ _______
kos- _______ _______
sem- _______ _______
o- _______ _______
tembe- _______ _______
to- _______ _______
2. Kuakisha
Alama za mtajo/kunukuu/usemi (“ ”)
Alama hizi hutumika ifuatavyo:
(a) Kuonyesha maneno halisi kama yalivyotajwa na msemaji bila
kubadilisha chochote; kwa mfano:
(i) Baada ya kumwona Kamau nilimwambia, “Wewe ni mtu mwongo
sana.”
(ii) “Sikiliza, tangu leo sitaki kukuona humu nyumbani mwangu,” Sarah
alinionya.
(iii) “Kila mwanafunzi anapaswa kulipa karo wiki ya kwanza baada ya
shule kufunguliwa,” mwalimu mkuu alisema.
Iwapo kuna dondoo ndogo katika dondoo kuu, dondoo kuu kwa kawaida
hunukuliwa kwa alama mbilimbili nayo dondoo ndogo kwa alama moja moja.
Kwa mfano:
(i) “Kwa nini hukusema ‘Jambo’ tulipokutana?” Kiprono aliniuliza.
(ii) “Nilipofungua mlango nilishtuliwa na maneno Wewe ni nani?’
yakitokea mvunguni mwa kitanda,” niliwaambia wazazi wangu.
(iii) “Mimi sikuweza kutazama sinema iitwayo Star Wars Episode
3 ingawa ilionyeshwa hapa mjini kwa miezi miwili,” Ojaamong’
alitwambia.
Zoezi
1. Akifisha sentensi zifuatazo kwa kuweka alama za mtajo mahali
panapofaa.
(a) Kwa nini hukunisalimia tulipokutana jana? raki yangu
aliniuliza.
(b) Sitaki Patrick alisema.
(c) Jana nilitazama sinema iitwayo The Ten Commandments
inayoonyeshwa huko mtaani Maringo nilimwambia Waithera.
222
223
(d) Wanafunzi hawa wana matatizo mengi hasa yanayohusiana na
matamshi ya maneno yenye sauti th na dh nilimwambia mkaguzi
wa shule.
(e) Nilisikia sauti ya Mwizi! Mwizi! kisha nikaona mtu aliyetimua
mbio huku akiandamwa na umati mkubwa wa watu nilimwambia
mwalimu.
2. Weka alama za mtajo mahali pafaapo kwenye kifungu kifuatacho:
Siku moja mwisho wa wiki Okelo, Kilonzo na watu wengi walika
kumwona mganga huyo mashuhuri. Kwa bahati mbaya hawakuweza kuonana
naye siku hiyo hadi siku ya pili. Okelo alipoenda kumwona, alimwambia jinsi
angependa sana kuwa mtu tajiri. Ninafanya kazi ya kila aina ili nijipatie
mali lakini umaskini wangu unazidi kuwa mbaya. Sasa nataka msaada wako
Mzee alisema Okelo. Babake Kilonzo kusikia hivyo aliangua kicheko kisha
alisema, Mwanangu, mimi naona kuwa ungali kijana ambaye ana nafasi
kubwa ya kujipatia mali, sioni kama unahitaji kugangwa ndipo upate mali
bali ningekushauri ufanye kazi kwa bidii. Okelo alisema Mzee, ni lazima
unipigie zile mburuga zako ndipo nipate kujua jinsi hali yangu ya siku
zijazo ilivyo ...
(Imenukuliwa kutoka Uhalifu Haulipi na Leo Odera Omolo, uk. 44)
Mstari wa mshazari (/)
Mstari wa mshazari hutumika katika mazingira yafuatayo:
(a) Kuonyesha kumbukumbu au tarehe; kwa mfano:
(i) Kumb. Na. A1/EMS/VU/2
(ii) Kumb. Na AC/KIA/SM/3
(iii) Kumb. Na. BN/KIMC/C2/100
(b) Kuonyesha kuwa maneno fulani yana maana sawa; kwa mfano:
(i) mkato/kipumuo/koma
(ii) kiulizo/kiulizi
(iii) alama za mtajo/kunukuu/usemi
(iv) mtu/binadamu
(v) duniani/ulimwenguni
(c) Kuonyesha ‘au’; kwa mfano:
(i) kondoo/mbuzi (kondoo au mbuzi)
(ii) wavulana/wasichana (wavulana au wasichana)
(iii) Kenya/Uganda/Tanzania (Kenya, Uganda au Tanzania)
(iv) watoto/watu wazima (watoto au watu wazima)
222
223
D. Kusoma
Usomaji wa kina: Riwaya
Katika sura ya kumi na tano, tulijadili maudhui ni nini na yanahusu nini
katika usomaji wa riwaya. Katika sura hii tutaangalia fani.
Fani, kama tulivyoona huko nyuma, ni jumla ya njia na mbinu
zinazotumiwa kuyawasilisha maudhui. Maudhui hayawezi kuwapo bila
ya kuwako kwa fani; fani nayo haiwezi kuwako bila ya kuwako kwa kitu
kinachozungumziwa. Maudhui na fani hutegemeana sana. Je, fani huhusisha
nini? Fani huhusisha vipengele kama muundo, matumizi ya lugha, wahusika,
mtindo na mandhari (wapi na lini). Hapa tutaangalia muundo na matumizi
ya lugha:
(a) Muundo: Riwaya huwa na mpangilio fulani. Kwa mfano, riwaya
yoyote huwa na sura mbalimbali na matukio yanayopatikana kwa
mpangilio au mfuatano maalum. Tukiangalia riwaya kama Mui
huwa Mwema ya A. Jamaadar, tunaona kuwa ina sura mbalimbali.
Matukio yanayopatikana humo yana mpangilio fulani. Kwa mfano,
tabia mbaya ya Kotini, nia ya kuiba, kucheza kamari, kukamatwa
na kutiwa gerezani n.k. Mpangilio huu unajulikana kama muundo.
(b) Matumizi ya lugha: Hatuwezi kuwa na riwaya au kazi ya kifasihi
bila ya kuwako kwa lugha. Fasihi inategemea lugha kwa kiasi
kikubwa, iwe fasihi simulizi au fasihi andishi. Hatuwezi kuyapata
maudhui au hadithi bila kuitumia lugha. Matumizi ya lugha
husimamia vitu kama:
(i) tamathali za usemi.
(ii) msamiati (na jinsi unavyotumiwa).
(iii) methali.
(iv) nahau..
(v) misemo.
(vi) miundo ya sentensi na kadhalika.
E. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Maagizo/maelekezo
Katika kidato cha kwanza, tuliona kuwa maagizo na maelekezo yana
nafasi muhimu katika shughuli nyingi tufanyazo. Kwa mfano, mwanafunzi
anayefanya mtihani hupewa maagizo ambayo yanamwongoza na kumwelekeza
jinsi ya kuufanya mtihani huo. Mgonjwa anayepewa dawa na daktari hupewa
maagizo ya jinsi ya kuitumia dawa hiyo. Isitoshe, mtu anayetumwa mahali
fulani hupewa maagizo fulani. Ikiwa watu hao wote watakosa kuyazingatia
maagizo hayo uwezekano wa kufaulu ni mdogo sana; au labda haupo.
224
225
Umuhimu wa maagizo/maelekezo
1. Huwa kielekezi cha kumwongoza mtu kuhusu jinsi ya kufanya jambo.
2. Huitia nidhamu katika shughuli yoyote inayofanywa na kuifanya iwe
na utaratibu fulani.
3. Huhakikisha kuwa mtu hapotezi wakati akiwaza lipi la kufanya na lipi
la kuepuka.
4. Hupunguza uwezekano wa mtu kufanya kosa kwa kufanya jambo lisilofaa
au hatari, kwa mfano, maagizo ya jinsi ya kuitumia dawa.
5. Humwongoza mtu, kwa mfano, maelekezo ya jinsi ya kwenda mahali
fulani au kutumia ramani.
Sifa za maagizo
1. Huwa na maelezo wazi na yasiyotatanisha, yaani yanaeleweka waziwazi.
2. Huweza pia kuambatanishwa na michoro au ramani, kwa mfano, maagizo
ya kwenda mahali fulani.
3. Huweza kuhusisha matumizi pia ya ishara au tarakimu fulani. Kwa
mfano, maagizo ya kutumia dawa 1 x 3 (tembe moja, mara tatu kwa
siku).
4. Huweza kuhusisha matumizi ya heru kubwa ili kutilia jambo fulani
mkazo, kwa mfano, ‘Jibu maswali MATATU pekee katika sehemu hii.’
Zoezi
Umeshuhudia janga fulani likitokea na unatamani kuwasaidia watu
wasikwe na janga kama hilo. Andika mfano wa maagizo kuhusu jinsi ya
kuepuka mkasa kama huo.
224
225
Sura ya Ishirini
A. Ufahamu
Vyombo vya habari na jamii ya leo
Mawasiliano kwa vyombo vya habari yamekia ngazi za juu sana katika
maisha yetu. Vyombo hivi vya habari ni kama magazeti, redio, simu, runinga
na mbinu nyingine ambazo zimevumbuliwa ili kusahilisha mawasiliano kati
ya binadamu. Kwa njia hii udhia wa kuwasilisha habari au taarifa kutoka
sehemu moja hadi nyingine umeondolewa. Siku hizi inawezekana kuwasiliana
na mtu yeyote popote pale alipo ulimwenguni kwa njia nyepesi na haraka
kupindukia.
Je, matumizi haya ya vyombo vya habari yana matokeo ya aina gani
katika jamii yetu? Je, vyombo hivi vinaacha athari na majukumu gani katika
jamii yetu? Kwanza, vyombo vya habari vina jukumu la kujuza au kufahamisha.
Kwa njia hii vyombo vya habari huchochea hamu na ghamu kutokana na kutoa
taarifa za kuwako kwa kitu fulani. Mathalan, tunapofahamishwa juu ya bidhaa
fulani, wasifu wake, tunajiwa na hamu ya kutaka kuinunua bidhaa hiyo ili
tuyakinishe ukweli wa wasifu huo.
Vyombo vya habari huweza pia kutumiwa kama vichocheo vya mabadiliko
au mageuzi katika jamii. Tunaishi katika jamii ambapo tunalalamika kila
uchao kuhusu jinsi wimbi la mabadiliko linavyoipiga jamii yetu. Mitindo ya
uvaaji wa nguo, hata miundo yenyewe ya mavazi hayo huathiriwa kwa kiasi
fulani na vyombo vya habari. Tunasoma magazeti, na hata kuangalia lamu
ambazo zinatuchochea kuiga mienendo fulani. Mienendo hiyo haiishii kwenye
wajihi wa nje. Baadhi yetu tunaathiriwa na jinsi tunavyowasikia wengine
wakiyatamka maneno kwa king’ong’o na kutaka kuwa kama wao labda bila
kutambua hatuwezi kujibagua na asili yetu wenyewe.
Vyombo vya habari huwa vyanzo vya mabadiliko makubwa katika
baadhi ya vipengele vya kiutamaduni hususan lugha. Unapofungua sahifa za
magazeti mbalimbali, utaona makala zinazohusu lugha. Yamkinika baadhi
yao yakawa na chemshabongo ambazo huwasaidia wasomaji wake kuukuza
uwezo wao katika lugha fulani. Katika redio nyingi kuna vipindi vya lugha
ambavyo huukiliwa kuwasaidia wasikilizaji kuupanua ujuzi wao kuhusu
lugha inayohusika. Fauka ya vipindi hivi vya lugha vipo vipindi vingine vingi
vinavyochangia katika kuyaeneza maarifa mbalimbali, kwa mfano, kuhusu
mazingira, utamaduni, siasa n.k.
Vyombo vya habari huweza kuwa vichochezi vya kusambaa na kuenea
kwa uvumi. Wakati mwingine, kutokana na mfumo wa uwasilishaji wa
taarifa mbalimbali katika vyombo vya habari, inawezekana mambo fulani
muhimu yakaachwa. Kuachwa kwa mambo hayo kunaweza kuwafanya watu
wajitose kwenye bahari ya uvumi. Kila mmoja atapiga mbizi katika bahari
hiyo kujaribu kuopoa habari zilizokosekana. Atajitahidi kuijaliza habari
iliyopungua adhaniavyo sawa. Kwa njia hii uvumi unaanza polepole na
226
227
kuishia kusambaa kama moto wa pori.
Isitoshe, vipo vyombo vya habari ambavyo huweza kusambaza habari
zinazochochea uvumi. Vyombo hivi huweza kufanya hivi kimakusudi. Katika
jamii ambapo pesa zimetawala vipengele vyote vya maisha ya binadamu,
si ajabu baadhi ya wanajamii wanaweza kutiwa shemere na tamaa ya pesa
kiasi cha kuamua kusambaza habari au taarifa zisizokuwa za kweli kwa nia
ya kujinufaisha kibinafsi.
Athari nyingine hasi ya vyombo vya habari ni kusambaza na kueneza
maadili mabaya. Kuna methali ya Kiswahili isemayo kuwa mcheza na
tope humrukia. Wanajamii waliojenga kitiba cha kusoma, kutazama au
kujihusisha na vyombo vya habari vinavyosambaza mawazo mabaya
wanaweza kuathirika kwa kiasi kikubwa. Kwa nini? Kwa sababu binadamu
ni kiumbe ambaye anapenda kuiga sana. Uigaji ni sehemu ya maumbile
yetu kama viumbe. Tunajifunza kula, kucheka, kulia, kutabasamu na hata
kutembea kwa kuwaangalia wazazi au wakubwa wetu; yaani tunaviiga au
kuvifuasa vitendo vyao. Uigaji huu ndio unaowafanya baadhi ya wanajamii
kuiga nyendo, mavazi na mitindo wanayoiona katika vyombo vya habari.
Uigaji mmoja mbaya sana ni ule wa vitendo vya kiuhalifu au vya
matumizi ya nguvu. Asilimia kubwa ya vijana wanaojitosa kwenye vitendo
vya matumizi ya nguvu hupata tabia hii kutokana na kuathiriwa na
vyombo vya habari. Vijana hao pia wanaweza kuwa wameiga matendo yao
ya kuonyeshana ubabe au kukomoana wao kwa wao kwenye vyombo hivyo
hasa runinga ambayo ina athari kubwa sana. Vipindi vingi vya runinga
vinaonyesha matumizi ya nguvu, kupigana masumbwi, kufyatuliana risasi
n.k. Si ajabu kwa baadhi ya watazamaji kuathiriwa na matendo hayo na
kupenda kuyaiga japo kwa mzaha. Lakini kama tujuavyo mzaha mzaha
hutumbuka usaha.
Vyombo vya habari huweza kuwa na mnato wa kipekee unaomfanya
anayehusika kuwa amezugwa. Mtu anapozugwa na kitu au jambo huwa
haoni wala kusikia. Akili yake hutekwa na jambo hilo; likamtia shemere na
kumkokota kama fahali asiyekuwa na hiari. Tabia hii ya kuzugwa inatokana
sana na vyombo vya habari kama lamu au video. Jinsi mtu anavyozugwa
na jambo fulani ndivyo ulivyo uwezekano wa mtu huyo kuathiriwa vibaya
na jambo hilo.
Maswali
1. Taja vyombo mbalimbali vya habari unavyovijua.
2. Je, vyombo vya habari vina umuhimu gani katika jamii?
3. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika kwenye kifungu
kisha uyatumie kutungia sentensi:
(a) kusahilisha (b) sahifa (c) huukiliwa (d) kuopoa
(e) shemere (f) hasi (g) kitiba (h) ubabe
4. ‘Kwa njia hii uvumi unaanza polepole na kuishia kusambaa kama
moto wa pori’. Maneno yaliyoandikwa kwa heru za mlazo ni mfano wa
tashbiha. Unganisha tashbiha katika jedwali lifuatalo:
226
227
A B
Bahatika kama pamba.
Ana miguu mirefu kama unyoya.
Ana maneno mengi kama mzazi aliyejifungua salama.
Tulikwenda mbio kama kidonda.
Yeye ananuka kama pilipili hoho.
Ana furaha kama korongo.
Kitabu hiki ni chepesi kama mwana aliyezaliwa Ijumaa.
Chakula hiki ni kikali kama umeme.
Nguo yake ni nyeupe kama chiriku.
5. ‘Lakini kama tujuavyo mzaha mzaha hutumbuka usaha’. Huu ni mfano
wa methali. Eleza maana ya methali zifuatazo:
(a) Abadi abadi kamba hukata jiwe.
(b) Abebwaye hujishika.
(c) Kunako matanga kumekufa mtu.
(d) Kupanda mchongoma kushuka ndio ngoma.
(e) Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Mafumbo/Chemshabongo
Mafumbo ni semi ambazo huwa na maana iliyofumbwa au kuchwa. Kauli
zinazoitwa mafumbo hutumia lugha iliyochwa na hukusudiwa kumkirisha
msikilizaji. Ikiwa anataka kuijua maana yake lazima akiri na kujaribu
kuivuta nadhari yake na labda hata kumbukumbu. Mafumbo ni sehemu ya
utanzu mpana unaojulikana kama semi au tanzu banifu. Ni tanzu banifu kwa
sababu ya ufupi wake. Mafumbo huhusisha vitendawili, mafumbo yenyewe
ni vitendawili. Ni sehemu ya chemshabongo, kwa kuwa inambidi msikilizaji
awaze na kukiri (kuichemsha bongo) kabla ya kutoa jibu lake.
Katika sura ya kumi na saba, tuliona maana ya vitendawili pamoja
na sifa zake. Fumbo ni usemi ambao huuliza swali ambalo linamlazimu
msikilizaji kuwaza au kukiri ili apate jibu. Lengo la mafumbo, kama vilivyo
vitendawili, ni kuuimarisha uwezo wa mtu kukiri haraka. Baada ya kuwaza
msikilizaji huweza kulifumbua fumbo lililoko.
Mifano ya mafumbo
1. Wapo jamaa zangu watatu. Kati ya jamaa hao watatu, wawili ni watoto
na wawili ni kina baba. Je, hao ni akina nani?- Hao ni babu, baba na
mtoto.
228
229
2. Kuna mtoto aliyepata ajali mbaya sana na kupelekwa hospitalini
na babake ambaye alikuwa daktari. Hata hivyo, babake hakuweza
kumfanyia upasuaji uliohitajika. Alipopelekwa kwenye chumba cha
upasuaji, daktari alisema kwa sauti kubwa, “La siwezi ni mwanangu!’
Ni nani huyo? – Mamake.
3. Ninataka kukaanga mayai. Nina mafuta, chumvi, moto, sufuria, kijiko
na hata pahala pa kupikia. Je, nimekosa nini?- Mayai.
4. Mimi ni bingwa katika nchi yangu. Nikipiga ngoma wote hutikisika.
Nikilala wote wanalala. Nikikwama wote wanakwama na nikiharakisha
wote huharakisha. Mimi ni nani?- Moyo.
Zoezi
(i) Kuna tofauti gani kati ya mafumbo na vitendawili?
(ii) Toa mifano minne ya mafumbo unayoyafahamu.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Viwakilishi
Viwakilishi ni maneno yanayosimamia nomino. Nomino husika huwa
haikutajwa katika maongezi au maandishi; kwa mfano:
(a) Yule anatakikana na mwalimu mkuu.
(b) Mimi ni dereva wa lori lile.
(c) Yeye atakuja kesho jioni.
(d) Nyinyi mlichelewa kwa nini?
(e) Hawa na wale wanahitaji msaada.
Viwakilishi hugawika katika makundi mbalimbali kama yafuatayo:
(i) Viwakilishi nafsi
(ii) Viwakilishi vya ngeli
(iii) Viwakilishi vya sifa
(iv) Viwakilishi vya idadi
(v) Viwakilishi vya kuuliza (viulizi)
(vi) Viwakilishi vya kumiliki (vimilikishi)
(vii) Viwakilishi vya A-unganifu
(viii) Viwakilishi vya pekee
(ix) Viwakilishi vya ‘o’ ‘rejeshi’
(x) Viwakilishi vya kusisitiza (visisitizi)
Viwakilishi nafsi
Hivi ni viwakilishi vinavyosimamia viumbe vyenye uhai. Kwa mfano:
(a) Mimi ni mwalimu wa Kiswahili.
(b) Yeye ataondoka leo jioni.
228
229
(c) Wao wamekwenda wapi?
(d) Sisi huwasaidia watu wenye shida.
Kuna aina mbili kuu ya viwakilishi vya nafsi:
1. Viwakilishi nafsi huru
2. Viwakilishi nafsi viambata (vitegemezi)
Viwakilishi nafsi huru
Hivi ni viwakilishi visivyohitaji kuongezewa viambishi vyovyote ili
kujikamilisha. Navyo ni sita:
mimi nafsi ya kwanza umoja
sisi nafsi ya kwanza wingi
wewe nafsi ya pili umoja
nyinyi nafsi ya pili wingi
yeye nafsi ya tatu umoja
wao nafsi ya tatu wingi
Matumizi
(a) Sisi na wao tutashindana kesho uwanjani.
(b) Mimi sikutaki kamwe.
(c) Kwa nini nyinyi mnanichezea?
(d) Yeye ni mfugaji.
Viwakilishi nafsi viambata/vitegemezi
Hivi ni viwakilishi vinavyotokea kama viambishi. Si maneno huru. Mifano:
1. Ninakwenda Nairobi leo.
2. Tunashirikiana na polisi.
3. Anawasumbua watu sana.
4. Mnataka nini?
2. Kuakisha
Nukta za dukuduku (…)
Hutumika katika mazingira mbalimbali kama yafuatayo:
(a) Kuonyesha kuwa maelezo yanaendelea ingawa maneno yenyewe
hayajaandikwa; kwa mfano:
(i) Babu aliniambia, “Kesho nataka umwambie mwalimu…”
(ii) Mzee Kenyatta alisema, “Tusahau ya…”
(b) Kuonyesha kuwa maneno yaliyoandikwa yametanguliwa na mengine
ambayo hayakutajwa au kuandikwa; kwa mfano:
(i) “…hata ikiwa mimi ni mwalimu wenu.”
(ii) “…kisha mwende nyumbani mkawapikie watoto.”
(iii) “…na siku hiyo sitaisahau hadi siku yangu ya mauti.”
(iv) “…hadi nilipokutana na raki yangu.”
230
231
(c) Kuonyesha kukatizwa usemi; kwa mfano
MwaliMu
: Jana nilikwambia umalize kazi hii, ulifanya nini?
Mwanafunzi
: Mwalimu jana sikuwa na…
MwaliMu
: Usiniambie hukuwa na nafasi na huku nilikuona
uwanjani ukicheza mpira.
Mwanafunzi
: Ndiyo, lakini…
MwaliMu
: Lakini nini?
Mwanafunzi
: Nilitaka…
Kinyota (*)
Alama hii hutumika kuonyesha jambo kuhusu maandishi. Kwa mfano:
(a) Kuonyesha kuwa neno fulani limeendelezwa kwa njia mbaya; kwa
mfano
1. *Mombassa (Mombasa)
2. *wanani (wanane)
3. *reo (leo)
(b) Kuonyesha kuwa sentensi fulani ina makosa ya kisaru, kwa mfano
1. *Ni nani yule kinachoniangalia?
2. *Ni ngapi wameka?
3. *Wazee hii inataka nini?
4. *Jawabu yako haikuniridhisha.
(c) Hutumika katika vitabu ili kutoa maelezo zaidi kuhusu maandishi
fulani. Maelezo hayo hutolewa pembeni upande wa chini wa karatasi.
Zoezi
Soma kifungu kifuatacho huku ukiweka alama ya kinyota mahali penye neno
lililoandikwa visivyo.
Siku ilipowadia, majjirani wote, tokea asubuhi, walikuwa katika
pirikapirika - wakiingia na kutoka kwa Bi Tatu, -wakipika na kusasha
na kpanga na kutengeneza kuonyesha furaha yaoo kwa kurejea kwa mtoto
wao. Saa za jioni, baba yake Monika, ambaye alivalia kansu nyeupe na
koa, akichukua koti lake mkononi, aliingia na kusema kuwa amekondi
magari matatu ili kuwachukua watu watakaopenda kwenda kumpokea
Monika kiwanjani. Magari hayo kwa kweli yasingelitosha hata kidogo kwa
wote, lakini ngari moja waliingia wazazi wake monika na ndugu zake, na
mawili yaliyobaki walijipakia majirani najamaa. Wengine walibaki pale pale
nyumbani wakimsubiri. salama alikuwa ni mmoja katika ya waliokweda
kiwanjani kumpokea.
(Imenukuliwa na kuandikwa upya kutoka riwaya ya Mwisho wa Kosa
na Z. Burhani, uk. 3).
230
231
3. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi ‘-enye’
Kivumishi ‘-enye’ huonyesha kitu au mtu anayemiliki kitu fulani. Tazama
jedwali lifuatalo:
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
‘-enye’
a mwizi mwenye Mwizi mwenye bunduki ametoroka.
wa wezi wenye Wezi wenye bunduki wametoroka.
u mnazi wenye Mnazi wenye matawi makubwa
umeanguka.
i minazi yenye Minazi yenye matawi makubwa
imeanguka.
u ulezi wenye Ulezi wenye kufaa utatolewa.
ya malezi yenye Malezi yenye kufaa yatatolewa.
ya mate yenye Mate yenye sumu yametemwa na nyoka.
ya mate yenye Mate yenye sumu yametemwa na nyoka.
li yai lenye Yai lenye utamu litaliwa.
ya mayai yenye Mayai yenye utamu yataliwa.
ki chama chenye Chama chenye manufaa kitaundwa.
vi vyama vyenye Vyama vyenye manufaa vitaundwa.
Zoezi
1. Badala ya nomino iliyoandikwa kwa heru nzito tumia ile iliyomo
mabanoni.
(a) Papai lenye utamu limeliwa (mayai).
(b) Visu vyenye makali vimenunuliwa (upanga).
(c) Manukato yenye kunukia ni yapi? (ua).
(d) Viatu vyenye bei ya juu vimeuzwa (manukato).
(e) Mwanafunzi mwenye kitabu amekuja (wanafunzi).
2. Rekebisha matumizi ya kivumishi ‘-enye’ katika sentensi zifuatazo:
(a) Mvulana yenye suruali nyekundu ndiye mwanangu.
(b) Ua yenye kupendwa ni hili.
(c) Kiatu zenye tundu ni kipi?
(d) Miji zenye watu wengi ina matatizo mengi.
(e) Mafuta wenye kunukia ni hayo.
D. Kusoma
Mashairi huru
Huko nyuma tuliona kuwa mashairi huru hutofautiana na mashairi ya arudhi
kwa kuwa hayana vina na mizani. Mashairi huru huonyesha matumizi ya
232
233
mistari ambayo haijakamilika kimaana na inabidi msomaji asome mstari
unaofuata ili aweze kuyapata maana kamili. Mistari ya aina hii hujulikana
kama mishata au mistari mishata. Hii hutumiwa kuujenga mwendo wa
shairi. Sifa nyingine inayopatikana sana katika mashairi huru ni urudiaji au
takriri. Inawezekana pakawa na maneno yaliyorudiwa, muundo uliorudiwa,
msamiati uliorudiwa n.k. Hii ni njia ya kuusisitiza ujumbe fulani. Hebu
tuangalie mfano huu:
Lini?
Naikumbuka
Siku nilipoka kijijini
Na kumkuta nyanya kaketi chini ya
Mgunga unaoelekeana na machweo
Akisaga ugoro wake
na
Kuyaangalia machweo
akiwasikiliza nyuni waliokuwa
Wakiimba kwa msisimko
Kuyaomboleza matanga ya
Magharibi
Naikumbuka kauli yake
‘Itakuwa lini nasi kuomboleza
Kifo cha dhiki?’
Naikumbuka sauti ya
Mama alipokuwa akiwinga
Bundi aliyekuwa akiimba
Mbolezi kuucheka umaskini
Kuudhihaki uwezo duni wa
Wanakijiji
Naikumbuka sauti ya mama
Na swali lake
‘Lini nasi tutawaimbia watutesao
mbolezi za bundi?...’
Msamiati
mbolezi : nyimbo za maafa.
Zoezi
1. Je, unakiri mshairi anazungumzia nini?
2. Onyesha mifano ya takriri au urudiaji katika shairi hili. Je, ni urudiaji
wa aina gani?
3. Toa mifano miwili ya mistari mishata katika shairi hili.
232
233
E. Kuandika
Dayalojia au mazungumzo
Dayalojia ni mazungumzo au majibizano ambayo hutumiwa kuelezea
mawasiliano yanayohusisha watu wawili au zaidi ambao huongea kwa
kujibizana. Ili kuweza kutunga dayolojia nzuri, ni vizuri kujifanya mhusika
wa mazungumzo au dayalojia hiyo. Pili, ni vizuri kuyapanga mawazo
yanayopatikana katika dayalojia kwa mantiki, yaonyeshe mtiririko mzuri,
na wahusika wanaopatikana waonyeshe sifa zinazohusiana na matendo
yao. Pia lugha yao lazima ionyeshe sifa zinazowatambulisha, kwa mfano,
mfanyabiashara awe na lugha inayoonyesha sifa hiyo.
Mambo ya kuzingatia katika mazungumzo
Ili kuandika dayalojia nzuri, lazima uzingatie mambo haya:
1. Lugha inayotumiwa na wahusika ifanane na lugha inayotumiwa katika
mazungumzo ya kawaida.
2. Majina ya wahusika yaandikwe kwanza na kufuatiwa na nukta mbili
au koloni.
3. Tumia alama za hisi (yaani vihisishi) na milio na mishangao mbalimbali
ili kuyafanya mahojiano yapendeze na kusisimua.
4. Wahusika wakatize maneno ya wahusika wengine ili mazungumzo
yafananane na hali ya kawaida.
5. Pawepo na utaratibu mzuri wa mawazo.
6. Pawepo na maelezo ya ufafanuzi katika mabano ili kuwafahamisha
wasomaji na wasikilizaji.
Katika kitabu hiki, kuna mifano mingi ya mazungumzo katika sehemu za
‘Kusikiliza na Kuzungumza’ Huu hapa ni mfano mwingine.
kipruTo
: (Kwa msisimko)Habari za leo Waliaula?
waliaula
: Nzuri ndugu yangu, hali?
kipruTo
: Hamna neno, tunashukuru.
waliaula
: Tumepoteana sana…
kipruTo
: Ndiyo maisha na shughuli zake.
waliaula
: Ehh, ambazo haziishi.
kipruTo
: Hasa! (Mtuo) Vipi sasa, nadhani sasa umekuwa
bingwa wa ukulima.
waliaula
: Wapi wee!
kipruTo
: Mbona?
waliaula
: Ahh, bwana wee. Bei yenyewe ndiyo hiyo tena,
imeshuka ukulima hautegemeki tena!
kipruTo
: Usiseme!
waliaula
: Kweli kabisa! Huu mwezi wa ngapi sijui bado
tunafuatilia malipo ya mwaka jana!
kipruTo
: Kumbe sio sisi tu tunaokumbana na shida hizo?
234
PB
waliaula
: (Akicheka) Nyie tu? Ni habari ya mwamba
ngoma…
kipruTo
: (akicheka pia) Ngozi kuvutia kwake!
waliuala
: Ehhh!
kipruTo
: Sasa tufanyeje?
waliaula
: Siku hizi naona wameanza kuchangamka.
kipruTo
: Afadhali hilo!
waliaula
: Bora hiyo! Hata sisi nasi tulikuwa tumeanza
kuchoka.
kipruTo
: Tunaomba iwe heri tu!
Zoezi
Andika mazungumzo yanayoweza kutokea katika hali mojawapo ya zifuatazo:
(i) Katika kituo cha mabasi kati ya abiria asiyekuwa na nauli ya kutosha
na mwenye matatu.
(ii) Mwanafunzi anayejiunga na kidato cha kwanza na mwanafunzi wa
kidato cha pili.
PB
235
Sura ya Ishirini na Moja
A. Ufahamu
Boramimi na njugu za Ngwenje
Babulao alifahamika na kila mtu katika eneobunge la Mipasho, kwanza
kutokana na mwendo wake wa kuguchia na pili kwa faka yake kubwa ya
kufuatilia masuala ya kisiasa. Tangu zamani alipokuwa mwanafunzi, Babulao
alikuwa na ndoto ya kuwa mwanasiasa mwenye kutajika. Baada ya hatima
ya masomo yake, ndoto yake haikutimia lakini hakukata tamaa kuwa siku
moja ataikata kiu yake ya uanasiasa.
Babulao alikuwa na kiredio chake kidogo alichokitumia kufuatilia
habari muhimu za nchi na matukio ya kutwa kucha. Kila wakati alizunguka
huku na huku amekibeba kiredio chake hicho. Alikuwa na tabia ya kujishaua
kwa kuwauliza wanakijiji maswali mbalimbali ya kisiasa, “Unajua waziri
amesema nini leo?” atamwuliza mmoja wao ambaye atajibu,
“sijui mimi!” Babulao ataangua kicheko na kusema,
“Ahh, bora mimi na kiredio changu! Nafahamu habari zote tangu
mwanzo mpaka aheri!” Atakutana na mwingine na kumwuliza, “Wajua
Bwana DC alikuwa wapi leo?”
“Sijui mimi,” atajibiwa.
Kisha atasema, “Aha, bora mimi na kiredio changu. Najua alipokuwa
Bwana DC leo!” Watu wa eneo hili wakambatiza ‘Boramimi’ na jina lake la
zamani likalia majinani.
Maisha ya Boramimi yalibadilika alipolipwa ridhaa kubwa kutoka
shirika la reli alikoumia mguu wake. Alizisarifu pesa zake vyema; akajenga
bahari ya nyumba kijijini na nyingine akaamua kuziweka akiba kwa nia ya
kujiingiza kwenye siasa. “Ninataka kuingia bungeni, nisikilizwe kwenye redio
mimi mwenyewe!” aliwaambia maraki zake. Muda si muda, habari zenyewe
zikatangaa kijiji kizima kama pepo za chamchela. “Babu wee, Boramimi
anataka kuwa mbunge!” Watu wakawa wanaambizana. Wengine walianza
kudhihaki kuwa hakuweza kumudu kampeni za uchaguzi ambazo zilikuwa
na kukuru kakara nyingi.
Harakati za uchaguzi zilipokaribia, Boramimi alifanya maandalizi yake
ya uchaguzi. Hata hivyo, watu walisema kuwa hakuwa na uwezo wowote kwa
sababu hakuwa na pesa za kutosha. Mpinzani wake, Mzee Ngwenje, alikuwa
ameahidi kufanya kampeni ya mwaka kuhakikisha kuwa ameuhifadhi
ubunge wake. Hata hivyo, licha ya kuwa alikuwa mbunge wa jimbo hilo kwa
takriban miaka kumi, Mzee Ngwenje hakuwa amefanya lolote. Kila mara
baada ya uchaguzi aliyoyomea mjini hadi uchaguzi mwingine ulipokaribia
tena. Hamna aliyemsikia kwa la heri wala kwa shari. “Hata mimi sikumsikia
kwenye kiredio changu! Boramimi aliwaambia watu.
236
237
Lakini Ngwenje naye alikuwa gwiji wa wajanja. Kila uchaguzi
ulipokaribia alinunua magunia ya mahindi na kuyasambaza haraka haraka
kwenye eneobunge lake. Ilitokea sadfa kuwa mara nyingi kulikuwa na njaa
kubwa wakati wa uchaguzi. Watu walipopata mahindi hayo walimpigia
Ngwenje kura naye akajisemea, “wajinga ndio waliwao!”
Lakini mara hii Mzee Ngwenje hakuwa na bahati kwa vile hakukuwa
na njaa hata kidogo. Mvua za masika zilinyesha vyema na watu wakavuna
mazao ya kazole. “Mara hii ataniona, ni mimi na yeye!” alisema Boramimi.
Ingawa watu hawakumpenda sana Boramimi, walimstahabu yeye kuliko
Bwana Ngwenje. Jinsi kampeni zilivyoendelea ndivyo ilivyozidi kuonekana
wazi kuwa huenda Boramimi akaibuka mshindi na Mzee Ngwenje kupoteza
kiti chake cha ubunge. Ngwenje alipotambua kuwa watu walikuwa
wakimshabikia Boramimi, alipigwa na butwaa. Sasa atafanya nini na watu
hawakuwa na njaa? Atatumia ujanja gani tena? Ilibidi atafute mbinu mpya.
Siku mbili kabla ya uchaguzi, Ngwenje alika kutoka jiji kuu na
magunia mawili yenye vifuko vilivyokuwa vimefungwa kama mchele au
sukari. Aliwachukua vijana kadha na kuwakabidhi mifuko hiyo ili kuwagawia
vijana wenzao walioshirikiana nao kumpigia kampeni. Ndani ya vijifuko
hivyo kulikuwa na njugu. Vijana wakashika safari na kutembelea kila kijiji
kusambaza zile njugu. Watu walipogundua mipango yao wakawaambia,
“Sisi si watoto wa kudanganywa kwa njugu; wapelekeeni watoto wa shule.”
“Hizi si njugu za huku mashenzini; hizi huipa miili nguvu mpya
ya kuweza kushiriki katika harakati za kampeni; ni uvumbuzi mpya wa
kisayansi. Ngwenje anataka tumfanyie kampeni kwa nguvu na msisimko ili
akamilishe miradi aliyoianzisha,” walisema. Vijana hawa wenyewe walikuwa
wakizitumia njugu hizo na kusisimkwa ajabu. Waliweza kuuponda wa si
wakiimba nyimbo za kumsifu Ngwenje na kuwahimiza watu wampigie kura.
Uvumi ulienezwa kuwa njugu hizo zilikuwa na uwezo wa kuituliza akili na
kulainisha viungo vya mwili ajabu. Baadhi ya watu waliingiwa na hamu ya
kujaribu njugu hizo za ajabu. “Ahh, si mbaya kama zinawatia watu hamasa
ya kutenda kazi,” wakasema kwa furaha. Hawa waliwashawishi wenzao
wengine na kuunda kundi sawa na la vijana waliompigia Ngwenje debe kwa
msisimko mkubwa.
Boramimi alifanya juu chini akajipatia kijifuko kimoja na kukihifadhi.
Kama kawaida yake hakusombwa na wimbi la kuzijaribu njugu hizo. Siku
ya uchaguzi ilipoka, Ngwenje akashinda kwa mara nyingine. Wakati
huo Boramimi alikuwa kaondoka kuelekea jiji kuu, wengine wakituhumu
kuwa alikwenda kufuatilia matokeo ya uchaguzi akishuku kuwa huenda
walimrubuni. Haukupita muda Boramimi akaka nyumbani akiandamana
na watu kadha aliowakabidhi kile kijifuko cha njugu. Baada ya kuzichunguza
wakathibitisha kuwa zilikuwa dawa za kulevya. Ngwenje akakamatwa mara
moja na kutiwa ndani akingojea mashtaka. Watu walipigwa na butwaa kubwa
kisha kimya kirefu kabla ya kusema, “Ahh Babu wee….Bora alaa!”
236
237
Tangu siku hiyo Babulao akawa shujaa wa eneo bunge zima. Na katika
uchaguzi wa marudio uliofanywa baada ya kisa hicho, Babulao akapata
ushindi mkubwa na kuwa mbunge mpya wa eneo bunge la Mipasho.
Maelezo ya msamiati
kuguchia : chechemea; chechea; tembea kwa njia
ambayo si ya kawaida hasa hatua za
mguu mmoja kutofuatana na za mguu
mwingine.
sarifu : hifadhi; tunza vizuri.
bahari ya nyumba : nyumba kubwa.
pepo za chamchela : kimbunga; pepo zinazozungukazunguka.
gwiji : mtaalamu; shujaa; mwenye ujuzi.
stahabu : pendelea jambo fulani kuliko jingine.
rubuni : changanya; hadaa.
Maswali
1. Kwa nini Babulao akaitwa Boramimi?
2. Alipolipwa ridhaa, Boramimi aliamua kuzitumiaje pesa zake?
3. Kwa nini watu walidhani Boramimi hangeshinda uchaguzi?
4. Bwana Ngwenje alileta maendeleo makubwa katika eneobunge la
Mipasho aliloliwakilisha. Unakubali? Fafanua.
5. Kwa nini Bwana Ngwenje alinunua magunia ya mahindi kila wakati wa
uchaguzi?
6. Kulikuwa na njaa kali wakati wa uchaguzi alioshiriki Babulao. Ni kweli?
Fafanua.
238
239
7. Je, unakiri ni kwa nini watu waliishia kumchagua Ngwenje?
8. Wewe binafsi unachukua hatua gani kuhakikisha kuwa huingii katika
mtego wa matumizi ya dawa za kulevya?
9. Fikiria kuwa raki yako mmoja amenaswa katika matumizi ya dawa za
kulevya. Utamsaidiaje ili kuokoa maisha yake?
10. Methali ‘wajinga ndio waliwao’ inahusianaje na wakazi wa eneo hili?
11. Eleza maana ya maneno na misemo hii kama ilivyotumiwa katika
kifungu ulichosoma:
(a) bahari ya nyumba (b) alizisarifu pesa (c) alikuwa gwiji
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Tanakali za sauti
Tanakali za sauti ni vipengele vya semi ambavyo hupatikana kwa wingi
katika lugha zetu mbalimbali. Tanakali za sauti hutumiwa kuelezea maneno
ambayo huiga sauti za jambo, tendo au tukio fulani. Sauti hiyo huwa inaiga
sauti inayotolewa na kitu fulani katika hali ya kawaida ya maisha.
Tanakali za sauti zinapotumiwa, msikilizaji anaweza kuiunda picha
fulani katika akili yake.
Tanakali huweza kuiga mlio wa mnyama, wa kitu kinachoanguka,
majani yanayokanyagwa n.k.
Tanakali za sauti huweza kutumiwa kuonyesha hisia fulani. Hizi ni
hisia za furaha, huzuni, kilio, majonzi n.k. Kwa njia hii tanakali za
sauti huifanya sanaa ivutie.
Tanakali husaidia kuufanya ujumbe uliopo katika maneno ya
mzungumzaji kuwa na uzito fulani.
Lugha ya Kiswahili inazo tanakali za sauti. Kwa mfano:
Anguka kacha! : Enda chini au anguka kama utanzu au tawi
la mti lililokatika.
Anguka pu! : Anguka mahali pagumu; anguka kutoka juu
kama maji mahali penye mteremko mkubwa.
Anguka pu pu pu! : Hutumiwa kuigizia mwanguko wa
kimfululizo kama wa nazi au maembe.
Anguka pukupuku!: Anguka kwa wingi kama vile mvua.
Anguka pwa! : Anguka mahali penye matope.
Anguka pwata! : Kuanguka kwa mtu au kitu kinene.
Anguka tang! : Anguka mahali pagumu kama sarafu sakafuni.
238
239
Anguka tapwi!: Anguka matopeni.
Anguka tifu!: Anguka mchangani.
Anguka tupwi!: Maana na matumizi yake ni sawa na ya anguka
chubwi!.
Bingirika bingiri bingiri!: Pinduka pinduka hasa katika mahali
penye mteremko.
Birua biru!:Angusha au hata kupindua; peleka huku na huku.
Boboka bo bo bo!: Payuka ovyo ovyo; sema maneno yasiyokuwa na
msingi.
Boboja bo bo bo!: Maana na matumizi yake ni sawa
na tanakali iliyoitangulia.
Bwakia bwaku: Tia kinywani upesi au akia.
Bwatika bwata: Enda chini kwa sauti au mshindo.
Bweka bwe bwe bwe!: Kulia kama mbwa; sema maneno yasiyo na
msingi au sema kwa kelele.
Bweka woo woo!: Bweka kama mbwa.
Chaga ngungundu: Kazania jambo fulani au shikilia jambo bila
kuachia.
Chakua nyaku nyaku: Tafuna au chakua chakula kwa kutoa sauti
ya kukirihi au hata kwa namna ya kuudhi.
Zoezi
Jaza tanakali za sauti zifaazo katika sentensi zinazofuata
1. Hata ukilia sikupi hata peni moja ________.
2. Yule mwanamke alijifunika __________ kwa buibui jeusi.
3. Kiti alichopewa kilikuwa kinalegalega ___________.
4. Alinyeshewa na mvua mpaka akaloa ____________.
5. Alipomsikia mbwa akibweka ______________ , Bosire alitimua mbio.
6. Mlezi alimwongoa mtoto mpaka akalala ___________.
7. Yule polisi alifyatua risasi zikalia _______________.
8. Lile gunia la sukari lilianguka mchangani __________.
9. Ule mti ulipopigwa na ile tufani ulikatika ____________.
10. Yule mpagazi alivishindilia vitu guniani ____________.
240
241
2. Matamshi bora: Vitate k/g
Soma maneno yafuatayo:
k g
koma goma
kamba gamba
konga gonga
koti goti
mfuko mfugo
mkuu mguu
oka oga
pika piga
tekua tegua
ukali ugali
Chagua neno mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo:
1. Tuli_______ (goma, koma) ku_______ (goma, koma) kwa vile tuligundua
kuwa tusipo_______ (koma, goma) ku_______ (koma, goma) tutafutwa
kazi mara moja.
2. Haya ma_______ (gamba, kamba) ya samaki hawa nitayaweka kwenye
gunia kisha nilifunge kwa _______ (kamba, gamba) nikayatupe jalalani.
3. Huyu ajuza ame_______ (gonga, konga) sana hivi kwamba hawezi
ku_______ (konga, gonga) nzi akamuua.
4. Musyoka alivaa _______ (goti, koti) lililomka kwenye_______ (koti, goti)
nikamwambia si vyema kuvaa _______ (koti, goti) kama hilo linaloka
ma_______ (kotini, gotini).
5. Nilitaka kununua ng’ombe, mbuzi, kondoo na mi_______ (fuko, fugo)
wengine, kwa hivyo nikabeba _______ (mfugo, mfuko) wangu uliojaa
ngwenje lakini nilipoka sokoni nikashtuka kugundua kwamba _______
(mfugo, mfuko) wangu umeshatoweka.
6. Tulipiga _______ (mkuu, mguu) hadi kwa _______ (mkuu, mguu) wa
wilaya lakini tulipoka akatuuliza ni kwa nini tumekuja kwa _______
(miguu, mikuu) tukasema ni kwa vile hatukuwa na nauli ikabidi tuje
kwa _______ (mikuu, miguu).
7. Baada ya ku_______ (oga, oka) mikate tuli_______ (oka, oga) mikono
tayari kwa karamu lakini wapishi wengine wakaambiwa waendelee
ku_______ (oga, oka) mikate zaidi.
8. Tulipokuwa tuki_______ (pika, piga) chakula cha jioni tulisikia watu
waki_______ (pika, piga) nduru tukaacha ku______ (piga, pika) kisha
nasi tukaanza ku_______ (piga, pika) nduru.
9. Tulipokuwa tukikimbia kuelekea nyumbani baada ya kuu_______ (tegua,
tekua) ule mtego, Ali alini_______ (tegua, tekua) nikaanguka chini pu!
240
241
10. Paulo alinizomea kwa _______ (ugali, ukali) kwa vile sikumpikia _______
(ukali, ugali) nikashangaa ni kwa nini alitaka nimpikie _______ (ukali,
ugali) hali anajua wazi kuwa kazi ya kupika _______ (ugali, ukali) si
yangu kamwe.
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Viwakilishi
(i) Viwakilishi vya idadi
Haya ni maneno ya idadi yanayotumika kama nomino. Kwa mfano:
(a) Watano wametiwa mbaroni.
(b) Serikali itawasaidia wengi.
(c) Maelfu na maelfu walipiga kura mwaka jana.
(d) Ni wachache tu walioka.
Zoezi
Onyesha viwakilishi vya idadi katika sentensi zifuatazo:
(a) Watatu wameka msikitini.
(b) Wengi waliumia vibaya sana.
(c) Mkurugenzi amewasaidia wengi.
(d) Elfu kumi na viwili vimeuzwa.
(e) Waziri atawaajiri kazi maelfu.
(ii) Viwakilishi vya kuuliza (viulizi)
Viwakilishi vya aina hii huwa ni viulizi vinavyotumika kama viwakilishi.
Kwa mfano:
(a) Wangapi wamepita mtihani?
(b) Unataka nini?
(c) Nyambura atanunua gani?
(d) Mwalimu alileta kipi?
(e) Ni nani anayeniita?
Zoezi
Onyesha viwakilishi vya kuuliza katika sentensi zifuatazo:
(a) Unataka nini?
(b) Wangapi wameka?
(c) Ni gani chako?
(d) Utachukua vipi?
(e) Unasema nini?
242
243
2. Upatanisho wa kisaru: Kivumishi cha pekee ‘-enye’
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
‘-enye’
i siku yenye Siku yenye baridi imepita.
zi siku zenye Siku zenye baridi zimepita.
i chumvi yenye Chumvi yenye bei ghali ni hii.
i chumvi yenye Chumvi yenye bei ghali ni hii.
u wavu wenye Wavu wenye tundu utashonwa.
zi nyavu zenye Nyavu zenye matundu zitashonwa.
u uzembe wenye Uzembe wenye kuudhi ni huu.
u uzembe wenye Uzembe wenye kuudhi ni huu.
ku kupika kwenye Kupika kwenye manufaa ni kupi?
ku kupika kwenye Kupika kwenye manufaa ni kupi?
pa mahali penye Mahali penye wezi hapafai.
ku mahali kwenye Mahali kwenye wezi hakufai.
mu mahali mwenye Mahali mwenye wezi hamfai.
zi fedha zenye Fedha zenye kuibwa zimepatikana.
ki kiwi chenye Kiwi chenye kumkosesha heshima
kimepungua.
Zoezi
1. Tumia vivumishi vya pekee vifuatavyo katika sentensi:
(a) mwenye (b) zenye (c) yenye (d) wenye (e) kwenye
2. Andika sentensi zifuatazo katika hali ya umoja.
(a) Nyumba zenye samani nzuri zimeuzwa.
(b) Sukari yenye bei ya juu ndiyo hii.
(c) Kusoma kwenye manufaa ni huko.
(d) Nyembe zenye makali zitatumiwa.
(e) Kulima kwenye manufaa kumeanza.
D. Kusoma
Tamthilia: Fani – kipengele cha mazungumzo
Katika sura ya nane, tuliona kuwa fani katika tamthilia hujengwa kwa
muundo, matumizi ya lugha, wahusika na mtindo. Kuhusu matumizi ya
lugha, tulitaja kuwa tamthilia hutumia mazungumzo kwa kiasi kikubwa
sana. Tofauti kuu kati ya riwaya na tamthilia ni kuwa tamthilia hutegemea
mazungumzo kuwasilisha maudhui kwa kiasi kikubwa sana. Riwaya kwa
242
243
upande mwingine hutumia usimulizi (hali ya kusimulia) wa mwandishi kwa
kiasi kikubwa. Katika sehemu hii, tutachunguza zaidi mazungumzo katika
tamthilia.
Mazungumzo ni yale majibizano yanayotokea kati ya wahusika walioko
jukwaani au katika tamthilia. Mazungumzo ya tamthilia sio majibizano tu
kwa ajili ya kujibizana bali hutumiwa kwa lengo la kuendeleza jambo kuu.
Mazungumzo huwa nguzo ya kukuza dhamira na maudhui.
Sifa za mazungumzo
Mazungumzo mazuri ya tamthilia huwa na sifa kadha nazo ni kama zifuatazo:
(a) Huwa yanakaribiana na hali halisi ya kimaisha; jinsi watu
wanavyotumia lugha maishani.
(b) Huendeleza tendo kuu linalotawala katika tamthilia; yaani
yanatusaidia kuona jinsi hadithi inavyoendelea.
(c) Huweza kuendelezwa kwa maneno machache tu au yakakuzwa kwa
vifungu virefu vya maneno.
(d) Huweza kuendeleza hadithi kwa kuwa mwandishi hana uhuru wa
kutumia usimulizi kama katika riwaya isipokuwa tu kwa maelekezo
ya jukwaa yaliyoko kwenye mabano.
(e) Huwaelekeza wasomaji au watazamaji kwenye tabia za wahusika na
masuala makuu katika tamthilia.
Zoezi
Kwa nini mazungumzo ni muhimu katika tamthilia?
E. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Risala
Risala hutumiwa kuelezea taarifa inayotoka kwa mtu au watu na ambayo
hueleza haja fulani. Aidha, hii ni hotuba fupi ambayo husomwa mbele ya
kiongozi au mkuu fulani kwa niaba ya kundi fulani kwa ajili ya kutoa maelezo
au kuuonyesha msimamo wa kikundi hicho kwa anayehusika. Risala huweza
pia kuwa taarifa fupi ya salamu au kutoa pole wakati wa majanga (kwa
mfano risala za rambirambi).
Muundo wa risala
Risala huwa na mwanzo, kati au mwili na mwisho. Mwanzo huwa na
utangulizi, salamu na lengo la risala hiyo. Sehemu ya kati au mwili ndiyo
sehemu kuu kwa kuwa hii ndiyo yenye kiini cha risala hiyo. Katika sehemu
hii risala hiyo huonyesha hali iliyoko, matatizo, mapendekezo na labda hata
maombi kwa wanaohusika. Sehemu ya mwisho huhusisha msisitizo wa hoja
zilizotolewa pamoja na hitimisho.
244
245
Mfano wa Risala
‘Suala la usalama kijijini’
Ndugu mkuu wa kituo cha polisi, kwa kipindi cha wiki nne zilizopita,
wanakijiji cha Beluwa, wamekumbwa na shida kubwa. Visa vya wizi
vimeongezeka na kututia sote katika hali ya wasiwasi na hofu kubwa.
Huko nyuma tulishawahi kuwa na tatizo hili miezi kadha iliyopita.
Siku hizo tulipopiga ripoti walitumwa polisi wa kushika doria. Tatizo hilo
lilipungua na hata kupotea na polisi nao wakaondoka hatimaye. Sasa hivi
limechipuka tena na hatuna usalama tena. Nguzo zetu zinaibiwa vivi hivi,
nyumba zinavunjwa, wasichana na wanawake wanabughudhiwa ovyo.
Tunapendekeza serikali ichukue hatua zifaazo kwa kuwatuma polisi sehemu
hiyo.
Sisi wanakijiji tuko tayari kushirikiana na polisi kuhakikisha kuwa
mara hii tatizo hili litapatiwa ufumbuzi wa kudumu. Kuwepo kwake
kunaathiri uhuru wetu kama wananchi wa kuweza kuchangia ipasavyo
katika maendeleo.
Zoezi
Umeteuliwa na wenzako kwenda kuyazungumzia matatizo ya darasa lenu
mbele ya mwalimu mkuu. Andika risala yako.
244
245
Sura ya Ishirini na Mbili
A. Ufahamu
Pipo Jerevu na moto wa majini
Pipo Jerevu alikuwa Asa Misitu wa msitu uliopakana na kijiji chetu na
uliotapakaa eneo kubwa kuelekea magharibi. Huu ndio msitu wa pekee nchi
nzima uliokuwa na miti ya kila aina; kuanzia ile ya asili hadi ile ya mbao
kama mininga, mifuu, mivule na mingine chungu nzima. Msitu wenyewe
ulivutia sana. Miti ilikuwa imeshikana ajabu kiasi kwamba hata kuingia
ndani ilikuwa shida kutokana na giza lililotokana na miti hiyo. Nyumba ya
Pipo Jerevu ilikuwa karibu sana na msitu wenyewe. Hata hivyo, hakuteuliwa
kuwa Asa Misitu kutokana na ujirani wake na msitu. Aliteuliwa kwa vile
aliaminiwa kuwa mtu mwadilifu na aliyeweza kuitunza rasilimali ya taifa.
Kutokana na hali ya msitu huo, watu wengi waliogopa kuingia kwenye
msitu wenyewe kwa kuchelea wanyama wa kila aina waliojaa pale msituni.
Wengine waliogopa kuingia msituni kutokana na hofu ya majini kwa sababu
ya imani yao ya ushirikina iliyowavaa kama lubega. Mle mna majini, ukienda
huko lazima yatakukaba koo,” waliambizana watu. Pipo Jerevu ndiye tu
aliyekuwa na ujasiri wa kuingia msituni huku akiwa amebeba bunduki, yake
ya rasharasha aliyopewa na waliohusika. Wengine waliishia kuamini kuwa
majini hayakuweza kumtisha mtu aliyekuwa na bunduki, hasa ya rasharasha.
Kijiji kizima kilipendezwa sana na juhudi kubwa za Pipo Jerevu.
Alikuwa na mazoea ya kuingia msituni na kuzunguka huko tangu asubuhi
hadi jioni akihakikisha kuwa hapakuwa na yeyote aliyeingia humo na kutishia
rasilimali ya taifa. Mara kwa mara hasa msimu wa upanzi, Pipo Jerevu
alitembelewa na jamaa waliotoka mjini. Wengi waliamini hao walikuwa
maasa misitu kama Pipo Jerevu. Yamkini walitaka kumsaidia mwenzao
kwenye shughuli kubwa ya kuulinda msitu wakati kama huu ambapo
mimea ya kila aina ilikua na kuvotana na kuifanya sehemu yenyewe kutisha
ajabu. Wakati mwingine walika jamaa waliokuwa na magari makubwa
hasa usiku usiku kumtembelea Pipo Jerevu. “Hawa ni washirika wangu wa
biashara huko mjini,” Pipo Jerevu aliwahi kuwaambia wanakijiji siku moja.
Ilivyokuwa, watu walimwamini Pipo kiasi kwamba hamna aliyeduhushi zaidi
ya hapo kujua ni biashara ya aina gani hiyo waliyofanya mjini.
Kila wakati watu hao walipoka kutoka mjini, hali ya Pipo Jerevu
ilizidi kubadilika. Alikuwa na furaha ya ajabu hadi ya kuwafanya wanakijiji
waamini kuwa wageni hao walikuwa wakimletea habari nzuri kila walipoka.
Wengine walichukulia ni uchangamfu wake wa kawaida au furaha ya mtu
aliyejua umuhimu wa kujituma kazini. Wageni wa Pipo Jerevu waliendelea
na ziara zao lakini hamna aliyejishughulisha nazo kwani watu waliamini
kuwa kila kitu kilikuwa shwari. Kwao kilichokuwa muhimu ni kuwa msitu
wao, ambao ni sehemu muhimu ya urithi wao ulitunzwa vizuri na bila shaka
wageni hao walikuwa wakija ili kusaidia Pipo katika wajibu huo muhimu.
246
247
Ilivyoelekea, Pipo Jerevu alifanya kazi yake hiyo kwa moyo wake wote na
walimwamini kabisa.
Siku moja mwanakijiji mmoja aliona kitu kilichofanana na moshi
kikitokea msituni. Alichana mbuga kuelekea ilipokuwa nyumba ya Asa
Misitu, Pipo Jerevu.
“Bwa..na… Pipo…” aliita huku akihemahema.
“Kuna nini…?” aliuliza Pipo.
“Moto…” alisema jamaa huyo.
“Wapi?” aliuliza Pipo.
“Msituni!” alisema yule jamaa. Pipo Jerevu aligutuka kidogo lakini
baada ya muda akatulizana. Aliingia ndani na kutoka na bunduki yake ya
rasharasha kisha akatimua mbio kuelekea msituni. Yule jamaa kwa kuogopa
alibaki pale pale hadi Pipo Jerevu alipotokeza tena akihemahema. “Hakuna
chochote kabisa! Hamna hata dalili ya moto!” alisema Pipo Jerevu akiangalia
huku na huku kwa wasiwasi; labda kutokana na mshtuko wa kusikia kuna
moto msituni.
Yule mzee kwa kuona haya alisema, “Labda ni moto wa majini tu!”
Pipo Jerevu alisema kwa msisimko, “Hakika! Lazima ni moto wa majini
ya msituni!” Hali hii ilitokea mara kadha. Kila mara watu waliambizana kwa
sauti ya juu, “Ni moto…ni ule moto wa majini tu!”
Siku moja wanakijiji wanne walipata ujasiri wa kuingia msituni. Wote
waliamua kuibeba mishale yao kwa kuogopa majini ya huko. Walitembea
nyatu nyatu hadi wakaka kwenye kiini cha msitu huo. Walitokeza sehemu
iliyokuwa na shamba kubwa lililokuwa na mimea iliyofanana na mitunguja.
Hapakuwa na miti hata kidogo. Upande wa kulia palikuwa na sehemu
iliyokuwa na magogo ya miti mingi. “Alaa! Hii nayo imekatwa na majini?
Je, moto wa majini ni wa kuchoma miti ili kupandwe mimea hii ya ajabu?”
waliulizana.
Walitoka pale mbio mbio na kwenda kupiga ripoti kwa waliohusika.
Hawakutaka
kumjulisha Pipo Jerevu.
Serikali ilipopata taarifa za
wanakijiji iliwatuma maasa
wa uchunguzi mahali hapo
mara moja. Muda si muda
kila kitu kiliwekwa wazi. Pipo
Jerevu akishirikiana na watu
wengine alikuwa na shughuli
kuu ya kuikata miti na
kuwauzia wafanyabiashara
matajiri, mingine aliichoma
makaa na sehemu hizo
kuchimbwa na kupandwa
bangi. Watu walikasirishwa
sana na vitendo vya mtu
waliyemwamini kiasi kile.
‘Kumbe huo ndio moto wa
246
247
majini?’ waliulizana. Pipo Jerevu alikishwa mahakamani na kufungwa
kifungo cha miaka kumi kwa kuuharibu msitu wa umma. Akawa pipi jerevu
kweli; ama kweli umdhaniaye siye ndiye.
Maswali
1. Ni kwa nini watu wengi walikuwa na imani kuu kwa Pipo Jerevu?
2. Toa sababu tatu zilizowafanya wanakijiji kuogopa kuingia msituni.
3. Unadhani wageni wa Pipo Jerevu walika kwa shughuli ipi?
4. “Kila wakati watu hao walipoka kutoka mjini hali ya Pipo Jerevu
ilibadilika sana.” Unadhani ni kwa nini?
5. Unadhani ule moshi uliotokea msituni ulitokana na nini?
6. Ni nini maana ya maneno haya kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu?
(a) ushirikina (b) kuvotana (c) bunduki ya rasharasha
(c) aliyeduhushi (d) alichana mbuga
7. Walitembea nyatu nyatu hadi wakaka kwenye kiini cha msitu huo.”
Maneno yaliyoandikwa kwa heru za mlazo ni mfano wa tanakali sauti.
Kamilisha tanakali zifuatazo kwa kuchagua majibu sahihi: puku puku,
pepepe, totoro, tititi, chapachapa
(a) Kule msituni kuna giza __________.
(b) Msitu wa kwetu ni mweusi __________.
(c) Alikata msitu hadi kote kukawa kweupe __________.
(d) Nilipoingia msituni nilinyeshewa na mvua nikaloa __________.
(e) Pipo Jerevu alipokamatwa kwa kuiba mali ya umma alikupukutika
machozi __________.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Maigizo
Katika sura ya kumi na sita, tuliona maigizo ni nini na vipera vyake
mbalimbali kwa kuanzia na ngonjera. Katika sura hii, tutaangalia vipera
vingine hasa vichekesho na michezo ya kuigiza. Msingi mkuu katika maigizo
ni kule kuwasilishwa mbele ya watu, hadhira au, watazamaji. Maigizo
hayategemei sauti ya anayeigiza bali pia na vitendo vyake.
A. Vichekesho
Hiki ni kipera cha maigizo ambacho huhusisha vifungu vya maneno, aghalabu
vifupi, ambavyo kimsingi hukusudiwa kuichekesha hadhira au walengwa.
Vichekesho hupatikana kwa wingi sana katika jamii zetu mbalimbali.
248
249
Jukumu la vichekesho
Vichekesho kama vipera vingine vya fasihi simulizi hutumiwa kwa lengo
maalum. Baadhi ya majukumu ya vichekesho ni kama ifuatavyo:
Kuchekesha: Hili ndilo lengo la kimsingi, yaani kuchekesha na
kuburudisha hadhira. Vichekesho huwa njia nzuri ya kuburudisha
baada ya kazi au jambo gumu.
Kuelimisha: Tunapoangalia vichekesho mbalimbali tunaweza kuhisi
kuwa pana lengo la kuelimisha hasa kwa kuonyesha jambo fulani
la kuchekesha au labda la kijinga alilolifanya mtu fulani.
Kuongeza utamu wa hadithi: Kuna baadhi ya watambaji wa hadithi
au ngano wanaotumia vichekesho kama njia ya kuifanya hadithi
ipendeze au ivutie.
Kukejeli: Inawezekana kichekesho kutumiwa kuonyesha ujinga
fulani au kukikejeli kitendo fulani alichokifanya mtu na ambacho
hakifai au hakistahili.
Mifano ya vichekesho
Jamaa mmoja ambaye kasikia kuwa nazi huliwa, alizichemsha
chunguni mpaka akamaliza kuni.
Mcheza kamari mmoja alipowaona askari wakimjia kumshika
alizichukua karata zenyewe akazibugia kinywani.
Mtu mmoja aliagizwa kwenda kuleta kima, ile nyama ya kusaga,
naye akatimua mbio kwenda porini kumtafuta nyani (kima ni nyani).
B. Michezo ya kuigiza au sanaa za maonyesho
Haya ni maigizo ambayo huwasilishwa mbele ya watu (jukwaani) na
watendaji. Michezo ya kuigiza huweza kuhusisha watoto. Katika jamii nyingi
kuna michezo ya kuigiza ambayo huchezwa na watoto.
Sifa za michezo ya kuigiza
Huwasilishwa mbele ya hadhira au watazamaji.
Huwa na watendaji ambao wanawasiliana kwa lugha ya
mazungumzo.
Huhusu jambo fulani, kwa mfano, michezo ya kuigiza ya baba na
mama, inayohusu matukio mbalimbali ya kitamaduni.
Huweza kuhusisha matumizi ya mavazi fulani au nguo fulani ili
kutia uhai katika maigizo hayo (mavazi haya hujulikana kama
maleba).
Zoezi
1. Je, michezo ya kuigiza huhusishwa na nini?
2. Toa mifano mitano ya vichekesho unavyovifahamu.
248
249
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Viwakilishi
(i) Viwakilishi vya pekee
Haya ni maneno yaliyoundwa kutokana na mizizi ‘-ingine’, ‘-ote’ ‘-o-ote’,
‘-enyewe’, na ‘-enye’ na kutumika kama viwakilishi. Kwa mfano:
(a) Wenyewe wamekubali lawama.
(b) Ameleta kingine.
(c) Chochote chaweza kutokea.
(d) Amepoteza vyote.
(e) Mwenye maradhi mabaya amepelekwa hospitalini.
(ii)Viwakilishi vya ‘o-rejeshi’ (virejeshi)
Hivi ni viwakilishi vinavyoundwa kutokana na kiambishi ‘o-rejeshi’.
Hutumika kuwakilisha nomino kwa njia ya kurejesha. Kwa mfano:
(a) Wanaokuja ni wezi.
(b) Mimi siwezi kuandamana na wasiofuata sheria.
(c) Wanaojitahidi hufaulu.
(d) Aliyeka jana yuko wapi?
(e) Kinachosomwa na mwanangu ni kizuri sana.
(iii) Viwakilishi vya kusisitiza (visisitizi)
Hivi ni viwakilishi vinavyotumika kusisitiza nomino ambayo yenyewe
haitajwi katika maandishi au maongezi. Kwa mfano:
(a) Mama anataka kiki hiki.
(b) Waziri atawasaidia wao hao.
(c) Mwalimu wetu atatununulia kile kile.
(d) Mchuuzi atatuuzia lilo hilo.
(e) Binamu yako atakwenda papo hapo.
Zoezi
Bainisha viwakilishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Yeye anawataka wao kuondoka sasa hivi.
(b) Nyinyi na sisi tutaka mapema.
(c) Ametuletea vingine.
(d) Waliovunja sheria wametiwa mbaroni.
(e) Kile ni cha nani?
(f) Vibaya vitachomwa.
(g) Wangapi walitibiwa?
(h) Cha Akoth kimeliwa na mbwa.
(i) Mimi ninataka kiki hiki.
(j) Wenyewe wamekataa katakata.
250
251
2. Vielezi
Aina za vielezi
Vielezi hugawika katika makundi manne makuu kama yafuatayo:
a) Vielezi vya namna/jinsi b) Vielezi vya mahali
c) Vielezi vya wakati d) Vielezi vya idadi
(a) Vielezi vya namna/jinsi
Hivi huonyesha namna kitendo kinavyotendeka. Kwa mfano:
(i) Mwizi huyo alinipiga vibaya.
(ii) Hoteli hii inapendwa sana.
(iii) Wakulima wa Kitale wana bidii mno.
(iv) Tulitembea haraka hadi mjini.
(v) Walioba hufanya kazi yake kijinga.
Zoezi
Onyesha kielezi cha namna/jinsi katika sentensi zifuatazo:
(i) Askari amesimama wima.
(ii) Dadangu anafanya kazi kivivu.
(iii) Dereva huyo huendesha gari barabara.
(iv) Fanya upesi.
(v) Maria hula chakula kisisi.
(b) Vielezi vya mahali
Hivi huonyesha mahali kitendo kinapotokea au kutendeka. Kwa mfano,
(i) Kesho nitakwenda shuleni.
(ii) Watoto hao wamekwenda kwao.
(iii) Weka mtungi huo chini.
(iv) Ndege imepaa angani.
(v) Nenda kwenu.
Zoezi
Tumia vielezi vya mahali vifuatavyo kutungia sentensi:
(a) kwako (b) Nairobi (c) juu (d) kondeni (e) humu
(c) Vielezi vya wakati
Hivi hueleza wakati wa kutendeka kwa kitendo. Kwa mfano:
(i) Alika jana.
(ii) Nitaondoka kesho kutwa.
(iii) Nakata uondoke sasa.
(iv) Leo nitalala mapema.
(v) Babu alikufa mwaka jana.
250
251
Zoezi
Tumia vielezi vya wakati vifuatavyo katika sentensi:
(a) Jumamosi (b) jana usiku (c) kesho alasiri (d) adhuhuri
(d) Vielezi vya idadi
Huonyesha kitendo kimetendeka mara ngapi. Kwa mfano:
(a) Wezi walitushambulia mara mbili.
(b) Alinipiga rungu mara kadha.
(c) Mungu atakuwepo milele.
(d) Nitakupenda daima.
Zoezi
Onyesha vielezi vya idadi kwenye sentensi zifuatazo:
1. Aghalabu ng’ombe wangu hunywa maji mtoni.
2. Sisi hupata likizo mara tatu kila mwaka.
3. Eneo la Budalang’i hukumbwa na mafuriko mara kwa mara.
4. Ugonjwa wa ukimwi huua mamilioni ya watu kila mwaka.
5. Mtu hufa mara moja tu maishani.
D. Kusoma
Riwaya: Wahusika
Huko nyuma tuliona kuwa wahusika ni kipengele muhimu katika usomaji
wa riwaya. Wahusika ni viumbe wa hadithini ambao huyatenda matendo
mbalimbali. Wahusika ni nguzo muhimu katika kuyawasilisha maudhui.
Hii ina maana kuwa lazima tuweze kuwaelewa na kuwaelezea wahusika
kwa njia ifaayo.
Mambo ya kuzingatia kuwahusu wahusika:
Tunapochunguza wahusika wa riwaya lazima tuyawazie mambo yafuatayo:
Majina ya wahusika: Je, wahusika waliopo wana majina gani? Je, majina
hayo yana maana yoyote? (yaani kama ni majina ya majazi). Je, majina hayo
yanahusiana vipi na mambo yanayozungumziwa?
Lugha ya wahusika: Je, wahusika hao wanaongea lugha ya aina gani? Je,
unajifunza nini kutokana na lugha hiyo? Je, wahusika wanatumia lugha
inayohusiana na ngazi zao za kielimu, kimaisha, kisiasa, kiuchumi n.k.?
Maelezo ya mwandishi kuwahusu: Je, mwandishi anatoa maelezo gani
kuwahusu wahusika hao? Je, unaweza kuwaelezea wahusika hao kwa
kutegemea maelezo ya mwandishi?
Matendo yao: Je, wahusika hao wanafanya mambo gani katika riwaya hiyo?
Je, matendo hayo wayafanyayo yana umuhimu gani? Unakiri kwa nini
wahusika hao wanayatenda matendo hayo?
252
253
Nafasi zao na umuhimu wao: Je, wahusika wanaopatikana katika riwaya
wana nafasi gani katika hadithi? Je, ni nani ambaye anachukua nafasi
muhimu hadithini? Je, ni mhusika yupi anayewakilisha msimamo mzuri na
yupi anayewakilisha ule mbaya? Je, unadhani mwandishi anataka ujifunze
nini kutokana na wahusika hao?
Zoezi
1. Je, ni maswali gani ya kimsingi tunayopaswa kujiuliza kuwahusu
wahusika wa riwaya?
E. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Orodha ya mambo
Orodha ni mlolongo wa mpango wa majina ya vitu vilivyoandikwa. Katika
maisha ya kila siku tunalazimika kuandika orodha mbalimbali. Kwa mfano,
orodha ya vitabu vya kusoma, orodha ya maneno, orodha ya mahitaji, kwa
mfano tuendapo sokoni, n.k.
Sifa muhimu za orodha:
Kutambua unachohitaji kwanza.
Kupanga ni kitu gani ambacho kinapaswa kupewa umuhimu wa kwanza
au kipaumbele halafu kukiweka hicho mwanzo.
Kitu ambacho hakina umuhimu mkubwa kinakuwa cha mwisho.
Ni vizuri kutumia nambari wakati wa kuandika orodha ili upate picha
kamili ya idadi ya mambo yanayohusika.
Kuandika mambo muhimu katika orodha kwa njia ya muhtasari,
njia unayoweza kuielewa au inayoweza kueleweka ikiwa orodha hiyo
inahitajika na mtu mwingine.
Mfano wa orodha
Vitu vya kuuzwa, mnada wa Tarehe 10- 12- 2002.
1. Meza ya duara
2. Viti:Jumla 10
3. Makochi: Seti 2
4. Mtungi wa gesi:Kilo 15
5. Jiko la gesi:Ariston (1)
6. Magodoro:Vono (6)
7. Vitanda vinne vya mbao
8. Taa za karabai:6
Zoezi
Andika mfano wa orodha ya mahitaji muhimu uendapo sokoni.
252
253
Sura ya Ishirini na Tatu
A. Ufahamu
Pimbi na hidaya ya kijiji
Kijiji cha Mwamana kilisika ghaya katika tarafa nzima ya Ngoa kutokana
na ushirikiano mkubwa kati ya watu. Walikuwa tayari kuchanga bia ili
kufanikiwa katika mambo yote waliyoyafanya. Hali hii iliwaletea baraka
nyingi na kijiji chenyewe kikawa kimepiga hatua nyingi kimaendeleo. Vijiji
vya karibu vilikililia ngoa kijiji kile kutokana na umoja wa wakazi wake. Wao
ulikuwa ushirikiano na utangamano wa kupigiwa mfano na uliwawezesha
kuonyesha ukweli wa methali isemayo, ‘Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu’.
Pale kijijini palikuwa na jamaa mmoja aliyejulikana na kila mtu.
Kiumbo hakuwa mnene wala mwembamba; alikuwa na mwili wastani.
Masikio yake yalikuwa madogo na nywele iliyodirwa vyema na ilimfanya awe
na wajihi wa kupendeza. Kila alipotembea hatua zake zilikuwa za haraka na
fupifupi na kumfanya aonekane kama anakimbia. Jamaa huyo alijulikana
kama Pimbi na alikuwa kapera aliyeishi peke yake ingawa alishirikiana
mara kwa mara na wanakijiji.
Pimbi alitambua jinsi wanakijiji wenzake walivyoshirikiana katika
mambo mengi. Basi siku moja alimwendea kiongozi wa kijiji na kumdokezea
haja aliyokuwa nayo. Alisema kuwa alikuwa na jambo lililohitaji pesa nyingi
na hakuwa na uwezo wa kifedha. Alitamani kupata msaada wa wanakijiji
ili kuhakikisha kuwa mipango yake haikupombojea. Kiongozi wa kijiji
alimwuliza, “Sasa ni shida gani hiyo uliyo nayo?” Pimbi alimwangalia, na
baada ya muda akasema,
“Nina nia ya kuoa kutoka kijiji cha mbali na huku kwetu. Wazee wa
mchumba wangu wanataka mahari nyingi takriban shilingi elfu themanini.”
“Ahh! Hilo tu. Ndoa ni heri mwanangu. Tutashirikiana kwa hali na mali
kuhakikisha kuwa umepata kiasi kinachohitajika. Kidole kimoja hakivunji
chawa mwanangu,” alisema kiongozi wa kijiji.
Baada ya muda mfupi, taarifa hiyo ilikuwa imesambazwa kijijini
na ikaenea kama wingu la masika. Kila mwanakijiji alitakiwa kutoa
alichoweza kuhakikisha kuwa wamemsaidia Pimbi. “Huyu ni mwanetu;
lazima tuwaonyeshe hao wanaotaka mahari kubwa hivyo kwamba tuna
uwezo,” waliambiwa wanakijiji. Kutokana na mazoea yao ya kushirikiana,
kila mwanakijiji alikuwa tayari kutoa mchango wake. Waliokuwa na mifugo
walijitolea kuipiga bei ili kumsaidia kijana wao aasi ukapera. Waliokuwa na
mazao waliyauza na kupata pesa za kutoa mchango.
Geza geza ndiyo mji. Hatimaye, kutokana na juhudi zao waliishia
kuchanga pesa nyingi. Kiasi kilichotakiwa kilipatikana pamoja hata na ziada
ya karibu elfu thelathini. Kwa kuwa hawakutaka maandalizi ya ndoa ya
Pimbi yaharibike, waliamua kumpa hata hiyo ziada. “Mwanetu, hii ni akiba
254
255
usije ukadharauliwa kuwa baada ya kupata mke huna chochote kingine,”
alisema kiongozi wa kijiji. Pimbi alichukua bunda kubwa la manoti na
kushukuru ghaya. Wanakijiji walifurahi kuwa walikuwa wameshirikiana
kwa mara nyingine. Wivu wa vijiji vya karibu uliongezeka baada ya kuona
mafanikio mengine makubwa ya kijijini Mwamana.
Siku moja asubuhi Pimbi alirauka mapema na kuchukua bunda lake la
pesa na kuondoka kijijini. Siku iliyotangulia alikuwa amemjulisha kiongozi
wa kijiji kuwa angeondoka siku hiyo. Wanakijiji walimtakia mafanikio
katika shughuli yake hiyo. Kila mmoja alisubiri arejee kijijini na mke wake
atakayekuwa mwanakijiji wao mpya kwa bashasha na matumaini makubwa.
Baada ya wiki moja Pimbi alirudi kijijini bila ya mke. Uso wake
ulikuwa umeiva kwa masikitiko
makubwa. Alipoulizwa kisa na
maana akasema kuwa pesa
walizochanga hazikutosha. “Watu
hawa bwana, wana tamaa ya fisi!
Wanawauza wasichana wao kama
dhahabu!” Alisema kwa masikitiko.
Wanakijiji waliungana tena na
kuamua kuwa kila mmoja wao
atajipigapiga ili angalau wapate pesa
zaidi zilizotakiwa. Waliokuwa na
akiba zao ndogo walizikung’uta zote
na kumkabidhi Pimbi. Sasa walikuwa
wamemchangia takriban shilingi laki
moja u nusu. Pimbi aliondoka huku
uso unachanua kwa furaha nyingi
ajabu.
Kila mtu kijijini alijua kuwa lazima mara hii Pimbi atafanikiwa
kumpata mke wake. Wanakijiji walibaki wakiwa na matumaini makubwa.
Wanawake walianza hata kutunga nyimbo za kumpongeza Pimbi. Wengine
walitunga nyimbo tamu za kumkaribisha mke huyo mpya ambaye angekuwa
kama hidaya ya kijiji. Vijana wenye nguvu walikuwa tayari kuyafyatua
matofali ya kumjengea Pimbi nyumba mpya. Ile alimoishi haikufaa. Kiongozi
wa kijiji alitoa fahali mmoja na mbuguma wa kuchinjwa wakati wa sherehe
hiyo.
Wanakijiji walisubiri kurudi kwa Pimbi. Lakini siku zilizidi kupita na
kuwa majuma na hatimaye hata miezi. Walianza kushikwa na wasiwasi huku
wakiomba kuwa hapakuwa na kizuizi kingine tena. Walisubiri wakijua kuwa
subira huvuta heri. Lakini Pimbi hakutokeza. Baada ya miezi minne, kijana
mmoja wa pale kijijini aliyefanya kazi mjini alirudi na habari za kushangaza.
Pimbi alikuwa amenunua kiwanja huko mjini na alikuwa akijitayarisha
kujenga nyumba ya kufanyia biashara. Aidha, alikuwa akizunguka huko mjini
akipiga raha zake kwa pesa walizochanga wanakijiji. “Huyu Pimbi ametupiga
mafamba kabisa. Atakiona kilichomtoa kanga manyoya, walilaani.” Bila
254
255
kusita mkuu wa kijiji akaita mkutano wa dharura.
Wanakijiji waliokuwa na hasira wakawachagua vijana kumi wa miraba
minne kwenda kumsaka Pimbi huko mjini walikomkuta amezama kwenye
raha na ureda. Keshoye wale vijana wakaondoka na jioni hiyo hiyo wakarejea
nyumbani na Pimbi. Pimbi alikabidhiwa polisi na akakishwa mbele ya
mahakama. Baada ya kesi, mali yake yote aliyokuwa amenunua huko mjini
yaliuzwa na pesa kurudishiwa wanakijiji. Hata hivyo, hakuepuka hukumu.
Alitiwa jela miaka sita.
Maelezo ya msamiati
hidaya : zawadi; tunu.
iliyodirwa : iliyokatwa ikawa ndogo.
wajihi : umbo; sura.
kapera : mwanamme asiye na mke.
haikupombojea : haikuharibika.
walizikung’uta : walizitoa.
Maswali
1. Ni kwa nini kijiji cha Mwamana kilisiwa?
2. Taja sifa za Pimbi kama zinavyoelezwa katika aya ya pili.
3. Je, unadhani ni kwa nini Pimbi aliamua kuwaeleza wanakijiji
aliyowaeleza?
4. Unadhani Pimbi alikuwa na nia ya kuoa akipata pesa? Eleza.
5. Fafanua maana ya methali hizi kulingana na matumizi yake kwenye
kifungu:
(a) Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.
(b) Kidole kimoja hakivunji chawa.
(c) Geza geza ndiyo mji.
(d) Subira huvuta heri.
6. Eleza maana ya misemo ifuatayo kama ilivyotumika kwenye kifungu.
(a) changa bia (b) piga hatua (c) lilia ngoa
(d) piga mafamba (e) asi ukapera
B. Kusikiliza na kuzungumza
Mjadala
“Maendeleo ya kisayansi yana manufaa makubwa kwa wananchi.”
256
257
C. Saru na matumizi ya lugha
Mnyambuliko wa vitenzi
1. Kauli ya kutendeshana na kutendeshea
Tazama jedwali lifuatalo:
mzizi kauli ya kauli ya kauli
kutenda kutendeshana kutendeshea
pig- pig-a pig-ish-an-a pig-ish-i-a
lim- lim-a lim-ish-an-a lim-ish-ia
ka- ka-a ka-lish-an-a ka-lish-i-a
end- end-a end-esh-an-a end-esh-e-a
kop- kop-a kop-esh-an-a kop-esh-e-a
sem- sem-a sem-esh-an-a sem-esh-e-a
som- som-a som-esh-an-a som-esh-e-a
fany- fany-a fany-iz-an-a fany-iz-i-a
va- va-a va-lish-an-a va-lish-i-a
Zoezi
Kamilisha jedwali lifuatalo:
mzizi kauli ya kutendeshana kauli ya kutendeshea
1. chez- ________________ ________________
2. beb- ________________ ________________
3. nyo- ________________ ________________
4. lim- ________________ ________________
5. pasu- ________________ ________________
6. ng’o- ________________ ________________
7. tambu- ________________ ________________
8. ju- ________________ ________________
9. sem- ________________ ________________
10. chang- ________________ ________________
11. kop- ________________ ________________
2. Viwakilishi
(i) Viwakilishi vya ngeli
Hivi ni viwakilishi vinavyoonyesha kuwa nomino inavyohusika imo katika
ngeli fulani. Kwa mfano:
1. Lililotengenezwa limeharibika tena.
256
257
2. Kinachopikwa ni changu.
3. Kutafunguliwa kesho asubuhi.
4. Alisema yatanunuliwa sokoni kesho.
5. Viko wapi?
Zoezi
Pigia mstari kiwakilishi cha ngeli katika sentensi zifuatazo:
(a) Lililokatwa limemea tena.
(b) Yaliyokatwa yamemea tena.
(c) Kilicholetwa jana ni changu.
(d) Vilivyoletwa jana ni vyangu.
(e) Hili linafaa kuliwa na mtoto.
(f) Haya yanafaa kuliwa na mtoto.
(g) Hii ilijengwa jana.
(h) Hizi zilijengwa jana.
(i) Ulionunuliwa leo ni upi?
(j) Zilizonunuliwa leo ni zipi?
(ii) Viwakilishi vya sifa
Haya ni maneno ya sifa yanayosimamia nomino. Kwa mfano:
1. Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.
2. Wakubwa na wadogo wote watasaidiwa.
3. Wanene na wakondefu watapewa nafasi sawa.
4. Hakuna tofauti yoyote kati ya warefu na wafupi.
Zoezi
Onyesha viwakilishi vya sifa katika sentensi zifuatazo:
(a) Wazuri na wabaya, wote ni viumbe vya Mungu.
(b) Chema hakikosi dosari.
(c) Virefu na vifupi ni sawa.
(d) Vyeusi havitakikani.
(e) Wazembe wamefutwa kazi.
(iii) Viwakilishi vya A-unganifu
Hivi hujengwa kwa kutumia A-unganifu. Kwa mfano,
1. Wa shamba hawiki mjini.
2. Ya kale hayanuki.
3. La kuvunda halina ubani.
4. Cha kuomba hakishibishi.
5. Ameniletea vya watoto.
258
259
Zoezi
Onyesha kiwakilishi cha A-unganifu katika sentensi zifuatazo:
a) Kwa nini umechukua la mama?
b) Ya mwalimu imeliwa na ng’ombe.
c) Cha mlevi huliwa na mgema.
d) Wa kwanza ameka.
e) La babu limefungwa.
(iv) Viwakilishi vimilikishi
Hivi ni viwakilishi vinavyosimamia nomino. Haviwezi kutumika pamoja na
nomino. Kwa mfano:
1. Wangu ameenda wapi?
2. Amepoteza vyake.
3. Chetu si changu.
4. Pangu pakavu tia mchuzi.
5. Yake imefunguliwa.
Zoezi
Tumia viwakilishi vimilikishi vifuatavyo kutungia sentensi.
(a) yangu (b) yako (c) vyake (d) petu (e) changu
D. Kusoma
Makala
Soma makala ifuatayo halafu ujibu maswali uliyoulizwa
Fasihi simulizi ni sanaa kama zilivyo sanaa nyingine kama vile ifuatayo:
unyanzi, usukaji, uchoraji na upigaji ala za muziki. Ni sanaa ambayo
yatokana na ubunifu na uwezo wa mwanadamu. Katika kubuni huko
hutumika vifaa mbalimbali. Kwa wanyanzi hutumiwa udongo, maji na
nyenzo nyingine. Wachoraji hutumia rangi na burashi. Wasukaji hutumia kili,
rangi, shazia na kadhalika. Hali kadhalika wachongaji wa vinyago hutumia
miti, patasi, msasa na kadhalika.
Msanii wa fasihi simulizi naye ana zana zake azitumiazo. Ni uhodari
wa maneno yaliyopangiliwa kwa utaratibu ambao huleta mguso na mnaso
kwa msikilizaji. Lugha iliyojaa usanifu, urazini na umahiri huwa ndicho
chombo maridhawa cha fasihi simulizi kitumikacho kutoa ujumbe wa fanani.
Fasihi simulizi ni chombo adhimu cha mawasiliano kufuatana na amali,
matakwa na itikadi ya jamii. Hivyo, huhifadhi, hubeba na kurithisha dhuriya
moja hadi nyingine kwa kutumia fanani wake. Fasihi simulizi haimo katika
ombwe, hivyo lazima yafuata mwelekeo wa jamii ikiwa ni sira ya maisha.
Fasihi simulizi hufunza, huadhibu, huonya na hutatua matatizo ya jamii
258
259
kadiri itakavyotumikishwa na jamii yenyewe. Fasihi simulizi ni ya aushi–
humpokea mwana anapozaliwa, ikamwengaenga, kumbebeja na kumkuza
hadi mauti.
Maswali
1. Je, makala haya yanazungumzia nini?
2. Je, nyenzo kuu ya fasihi simulizi ni nini? Je, na ya fasihi iliyoandikwa?
E. Kuandika
Mahojiano
Mahojiano ni mazungumzo kati ya watu wawili au zaidi ambapo mmoja
huwa mhojaji na ndiye anayeuliza maswali na mwingine ambaye ni mhojiwa
hujibu maswali anayoulizwa. Kwa kawaida katika mahojiano, anayeuliza
maswali huwa na jambo analotaka kujua kutoka kwa mhojiwa. Katika
kuandika mahojiano, ni muhimu anayeandika kufikiria kuhusu mada
anayoandikia ili aweze kuyapanga mawazo yake vyema. Ni muhimu pia kujua
jinsi atakavyoyapanga maneno ya wahusika ili mahojiano yenyewe yaweze
kufululika vyema na kuvutia anayesoma. Ufuatao ni mfano wa mahojiano kati
ya mkufunzi wa timu ya Harambee Stars na ripota wa gazeti la Msemakweli.
ripoTa
: Bwana kocha, timu ya Harambee Stars imezidi kuvutia
mashabiki wengi katika siku za hivi karibuni. Ni nini sababu
ya jambo hili?
Mkufunzi
: Sababu ni nyingi. Lakini sababu kuu ni kuwa timu yetu
inaendelea kufanya vyema katika mechi za kufuzu kwa
kinyang’anyiro cha Kombe la Dunia.
ripoTa
: Je, timu hii imecheza na timu zipi kukia sasa?
Mkufunzi
: Timu hii imecheza na timu ya Zimbabwe na ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo.
ripoTa
: Je, kukia sasa matokeo yamekuwa vipi?
Mkufunzi
: Kwanza, mechi tulizocheza kukia sasa tumezichezea katika
nchi hizo. Lakini licha ya upinzani mkali tuliopata kutoka
kwa timu hizo na hata kutoka kwa mashabiki, tuliweza
kupata ushindi wa bao moja kwa bila katika kila mechi.
Kwa hivyo, katika raundi ya pili tutachezea hapa nchini na
tunatarajia kupata ushindi mkubwa zaidi.
ripoTa
: Je, ni matayarisho yapi umefanya ili kukabiliana na timu
hizo katika raundi ya pili?
Mkufunzi
: Kwanza, vijana wote wamepiga kambi ya mazoezi katika
Uwanja wa Kimataifa wa Kasarani ambapo tunafanya mazoezi
makali kila siku kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na
mbili jioni. Pia tumecheza mechi kadha za kujipima nguvu na
260
261
timu zinazoshiriki katika ligi kuu ya taifa kama vile Tusker,
Gor Mahia na Nzoia. Isitoshe, tunatarajia kucheza mechi za
kiraki na timu za mataifa ya Misri, Ghana na Cameroon.
Hali kadhalika tunapanga kuzuru nchi kadha za ng’ambo
zikiwemo Uhispania, Ugiriki na Ujerumani ili kufanya
mazoezi zaidi na pia kucheza na timu kadha za huko.
ripoTa
: Je, unawashirikisha wachezaji wa kulipwa?
Mkufunzi
: Naam, ninawashirikisha. Wachezaji wa kulipwa wana ujuzi
mwingi na pia wamezoea kucheza mechi kalikali katika ligi
za huko Ulaya.
ripoTa
: Je, kuna wafadhili wowote waliojitolea kusaidia licha ya
udhamini unaotokana na wizara inayohusika na michezo?
Mkufunzi
: Bila shaka. Shughuli hii huhitaji pesa nyingi mno. Kwa
bahati nzuri kampuni kadha zimejitolea kutusaidia.
ripoTa
: Je, kampuni hizi zimetoa misaada ya aina gani?
Mkufunzi
: Zimetoa misaada mbalimbali. Zingine zimesimamia safari
zetu, zingine zimetoa pesa taslimu, zingine zimewanunulia
wachezaji sare za kuchezea na kufanyia mazoezi na kadhalika.
Tunashukuru sana kwa udhamini huu na tunauliza kampuni
zingine au watu binafsi kuzidi kutusaidia kwa njia yoyote ile
ili tuweze kufanikiwa katika jitihada zetu.
ripoTa
: Asante sana kwa kupata nafasi ya kuongea nami. Sisi
wanahabari pia tunaitakia timu yetu mafanikio katika
mechi zote zilizobaki.
Mkufunzi
: Asante.
Zoezi
Andika mahojiano yasiyozidi kurasa mbili kati ya mteja na mhudumu
hotelini.
260
261
Sura ya Ishirini na Nne
A. Ufahamu
Bwana Bafe na maradhi ya walalahoi
Bwana Kitumbo alitema kiburi kama bafe anavyoyarusha mate yake ya
sumu. Kutokana na hulka yake hii ya kukirihi, watu walioingiliana naye
walimpachika lakabu ya Bwana Bafe na jina lake la zamani likazikwa katika
kaburi la sahau; kilichobakia ni kitumbo chake kilichochongoka mbele.
Kiburi cha Bwana Bafe kilitokana na uwezo wake mkubwa wa kiuchumi.
Alikuwa na msururu mrefu wa biashara za kila aina kuanzia maduka ya
kuuzia vipodozi hadi karakana za kutengenezea vifaa vya zaraa. Kila uchao
alipanda ngazi ya kiuchumi na hali yake kuendelea kubaidika na ya wenzake
kama ardhi ya mbingu. Alikuwa na fedha chekwachekwa na uwezo mkubwa
wa kufanya lolote alilotaka.
Watu hawakuichukia tabia yake ya kuongea kwa kiburi tu bali pia
mienendo yake. Alikuwa mpenda raha sana na mlevi aliyekubuhu; akienda
baa hatoki mpaka imefungwa. Isitoshe, Bwana Bafe alikuwa na jicho la nje.
Kila maraki zake walipomkanya dhidi ya tabia hiyo aligomba sana. “Nyie
shida yenu ni ile ile; maradhi ya walalahoi, hamna pesa! Mimi ninazo; sharti
nitafute wa kunisaidia kuzitumia,” alibwata kama kawaida. Licha ya tamko
lake hili, maskini walipomwendea wakiwa na shida aligoma kuwasaidia.
“Acheni uzembe wenu! Hayo ndiyo maradhi ya walalahoi!” Alisema tena kwa
kujishasha kwingi. Bwana Bafe hakupigwa mshipa na maneno ya watu;
hakusikia la mwadhini wala la mteka maji msikitini.
Bwana Bafe aliendelea na raha zake za kila aina. Siku haikupita bila ya
Bwana Bafe kuonekana kwenye mabaa ya mjini aliposhinda akiimba nyimbo
za kilevi huku akisema kwa
sauti ya juu, “Ponda raha kufa
kwaja!”
Siku moja alika
mshauri wa afya pale
mjini. Serikali ilikuwa
imeamua kuwasambaza
washauri wa aina hii ili
kuwatahadharisha wananchi
dhidi ya magonjwa ya kila
aina mengine ambayo
yalikuwa hayaeleweki.
Mshauri huyo alikuwa na
vikao vyake kila siku ya
Ijumaa katika soko kuu
mjini. Siku hiyo watu
walitangamana hapo
262
263
kuusikiliza ushauri wa Bwana Afya kwa hamu na hamumu. Walihudhuria
watu wa kila umri na rika isipokuwa Bwana Bafe peke yake. Wenzake
walipomshauri ajiunge nao alikataa katakata na kuuliza kwa sauti, “Ati
nini”?
“Twende tukamsikilize Bwana Afya yahe; ushauri wake ni muhimu
sana,” walimwambia.
“Huyo ameletwa kuyatibu maradhi ya walalahoi; maradhi ya kutokula
chakula chenye lishe. Hamnioni mimi? Kiangalie kitambi changu; unaona
kimejaa lishe na siha? Nijali nini mimi? Nendeni nyinyi. Anawatafuta watu
kama nyinyi msiojiweza,” alijigamba.
Bwana Bafe aliendelea na maisha yake kama kawaida bila kujali wala
kubali maneno ya maraki zake wala ushauri wa Bwana Afya. Alipohisi kuwa
watu walianza kumbadilikia, Bwana Bafe alipotelea zake kwenye jiji jingine
lililokuwa mbali kidogo na hilo. Alirudi mara kwa mara kufuatilia maendeleo
ya biashara zake mbalimbali. Watu wa sehemu hiyo hawakushughulika
naye kwa sasa. Alishawaonyesha kuwa hakuwa mwenzao kwenye mambo
mengi, nao hawakutaka kujikalifu bure kumtaka ushirika. Hata hivyo, kila
alipotokeza walimsemesha kama kawaida; kwa kuwa hawakuwa na tabia
ya ubaguzi kama yeye.
Mwaka mmoja baada ya Bwana Bafe kuhamia jiji la Buraha alirudi
mjini alikotoka. Waliokumbana naye walimwuliza kwa sauti ya juu, “Bwa’
Bafe vipi; umetambua mwenda tezi na omo marejeo ni ngamani?” Aliangua
kicheko kisha akakohoakohoa kwa muda. Pumzi zilikuwa kama zinampalia.
“Pole Bwa’Bafe, ni vumbi la huku kwetu,wajua ni tofauti sana na huko jijini
ulikokuwa,” walimfariji.
Bwana Bafe aliitikia kwa kichwa kisha akaongeza kwa sauti imara,
“Ni haya maradhi…,” alisema lakini kabla hajamaliza mwanakijiji mmoja
akajaliza, “ya walalahoi!” Kwake hii ilikuwa njia ya kumfanyia stihizai
Bwana Bafe lakini Bafe mwenyewe hakulitambua hilo, aliitikia tu. Huo
ukawa mwisho wa kipindi kile.
Muda mfupi, Bwana Bafe alilazwa hospitalini akiwa na ugonjwa wa
kifua kikuu. Alipotoka hospitalini alikuwa amebadilika kwa kiasi kikubwa
sana. Ngozi ya mwili wake ilikuwa imeanza kupauka kama iliyomwagiwa
unga. Uso wenyewe ulikuwa umefumuka vipele vingi ajabu kama vya mgonjwa
wa upele. Baadhi ya watu waliomjua tangu utotoni walikuja juu, “Mnajua
Bwana Bafe hakuugua surua alipokuwa mtoto mdogo na huku tunaamini
kuwa lazima surua impate mtu hata utu uzimani wake!” Lakini wengine
walisema tu, “Ni maradhi ya walalahoi!” Ukimya mwingine ukafuatia baada
ya Bwana Bafe mwenyewe kupotea kwa muda mrefu.
Alipotokeza tena alikuwa kabadilika zaidi; sasa alikuwa amekondeana
ajabu. Kile kitumbo chake kilichokuwa ishara ya uwezo wake kilikuwa
kimeyeyuka kama umande jua liangazapo. Lakini kilichowashangaza watu
kabisa ni pale tu alipoanza kuzungumza. Kauli zake zilikuwa na utatanishi
mkubwa na ilikuwa vigumu kujua alichokuwa akimaanisha; alikuwa kama
anarogonya maneno tu yasiyoeleweka. Mkewe naye alikuwa ameanza
kuuguaugua. Mambo yalizidi kumharibikia Bwana Bafe na familia yake.
262
263
Ukweli ulibainika siku moja Bwana Bafe alipozimia na kulazimika
kupelekwa kwenye kituo cha afya akiwa hali mahututi. Ukweli ukidhihiri
uwongo hujitenga. Ilichuliwa kuwa Bwana Bafe hakuwa amefanyiwa sihiri
wala nini kama ilivyodhaniwa na wengine. Bwana Bafe alikuwa akiugua
Ukimwi. “Mungu wangu! Haya ndiyo maradhi ya walalahoi?” watu walimaka
kwa sauti ya juu. Hofu kubwa iliyowasambaa waliohusiana na Bwana Bafe
iliwafanya wachue siri walizokuwa wamefutika kwenye nyoyo zao. Muda
mfupi baadaye Bwana Bafe aliaga dunia na mkewe alifuatia baadaye pamoja
na watu wengine kadha waliohusiana nao. Lakini watu walijifunza umuhimu
wa kuuzungumzia ugonjwa huo pamoja na athari zake. “Huu ni ugonjwa wa
kila mtu; tajiri na mlalahoi; kijana na mzee; mwanamke na mwanamume;
haubagui wala hauheshimu umri wala staha,” walisema.
Maelezo ya msamiati
bafe : namna ya nyoka anayerusha mate yenye
sumu.
kukirihi : fanya mambo ya kuchukiza watu; fanya
karaha; udhi.
vipodozi : bidhaa za kujipamba kama vile manukato.
fedha chekwachekwa : fedha chungu nzima.
aliyekubuhu : aliyepita mipaka; aliyezidi.
kujishasha : kuringa; kujitapa.
kujikalifu : kujisumbua; kujitaabisha.
fanyia stihizai : ambia maneno ya dharau; kejeli.
kupauka : rangi kua; papara.
fumuka vipele : tokeza vipele.
anarogonya : anasema maneno yasiyotambulikana
kama mtu aliyepagawa.
sihiri : uganga; uchawi.
Maswali
1. Kwa nini Bwana Kitumbo akabatizwa ‘Bwana Bafe’?
2. Ni nini kilichokuwa chanzo cha kiburi cha Bwana Bafe?
3. Eleza tabia za Bwana Bafe zilizowakirihi watu.
4. Bwana Bafe alijibuje alipoambiwa aende akamsikilize Bwana Afya?
5. Ni kwa nini aliamua kuhamia jiji jingine?
6. Je, unadhani Bwana Bafe aliyapataje maradhi yake? Taja njia tatu
nyingine za kuweza kuyapata maradhi haya.
7. Je, watu walijifunza nini baada ya kifo cha Bwana Bafe?
8. Tumia misemo ifuatayo kwenye sentensi:
(a) haukumpiga mshipa
(b) hamu na hamumu
(c) aliangua kicheko
(d) jicho la nje
264
265
9. Kifungu ulichosoma kinazungumzia ugonjwa wa Ukimwi. Je, haya
yafuatayo ni magonjwa gani?
(a) degedege (b) kisukari (c) kimambe au mkamba
(d) rovu (e) kichomi (f) ukoma
(g) kifaduro
B. Saru na matumizi ya lugha
1. Hali ya ‘-po-’
Kiambishi ‘-po-’ huweza kutumiwa kuonyesha wakati au mahali. Tazama
mifano ifuatayo:
(i) Alalapo hukoroma (wakati).
(ii) Nitakuonyesha Saida aimbiapo (mahali).
(iii) Wakapo waambie waje wanione (wakati).
(iv) Mtu avutapo sigara hudhuru afya yake (wakati).
(v) Mhitajikapo kusimama ni hapa (mahali).
(vi Utakaposhikwa na malaria, ndipo utakapotambua umuhimu
wa kutumia chandarua (wakati).
(vii) Mtu hujikuna ajipatapo (mahali).
(viii) Samaki avuliwapo hufurukuta (wakati).
Kukanusha hali ya ‘-po-’
Tazama mifano kwenye jedwali:
Umoja Wingi
kuyakinisha kukanusha kuyakinisha kukanusha
(i) nilalapo nisipolala tulalapo tusipolala
(ii) niimbiapo nisipoimbia tuimbiapo tusipoimbia
(iii) ulalapo usipolala mlalapo msipolala
(iv) uimbiapo usipoimbia muimbiapo msipoimbia
(v) alalapo asipolala walalapo wasipolala
(vi) aimbiapo asipoimbia waimbiapo wasipoimbia
264
265
Zoezi
1. Taja kama hali ya ‘-po-’ katika sentensi zifuatazo ni ya wakati au mahali:
(i) Anapoongea Kiswahili hunivutia.
(ii) Mamangu anionapo hunikumbatia.
(iii) Nipikiapo sipo niliapo.
(iv) Kila niamkapo hujihisi mchangamfu.
(v) Wazalianapo mbu panasashwa.
2. Kanusha sentensi zifuatazo:
(i) Niishipo ninapafahamu.
(ii) Mtoto achezapo hujifunza mengi.
(iii) Wanafunzi wafanyapo bidii masomoni, hupita mitihani.
(iv) Angurumiapo huyu simba hutetemeka.
(v) Niendeshapo baiskeli hufurahi.
2. Vihisishi (I)
Vihisishi ni maneno yanayotoa hisia fulani za moyoni kama vile huzuni,
furaha, mshangao, masikitiko, kuudhika, na kadhalika. Kwa mfano:
(a) Lo! Lo! Ni nani yule?
(b) Salaala! Mtoto wako anampiga mwanangu.
(c) Ala! Kwani wewe husikii ninayoyasema?
(d) Aisee Juma, jana ulika nyumbani saa ngapi?
(e) Wanafunzi wetu wote wameanguka mtihani. Ajabu!
(f) Tutaonana Inshallah!
(g) Walahi nikikushika nitakumaliza!
(h) Hoyee! Timu yetu imeshinda.
(i) Laiti ningalijua yule kijana ni mtumizi wa dawa za kulevya!
(j) Nilifurahi sana kwa usaidizi wako. Asante.
Zoezi
1. Onyesha vihisishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Gor Mahia hoyee! Aberdare Stars ziii!
(b) Sawa! Siku nyingine sitakusaidia.
(c) Naam, nitafanya yote uliyoniagiza.
(d) Hodi kwa wenyewe!
(e) Ati Hosea amelazwa hospitalini?
2. Tunga sentensi ukitumia vihisishi vifuatavyo:
(i) enhe (ii) astagharuillah (iii) simile (iv) aha
(v) labeka (vi) taibu (vii) sasa (viii) afanalek
(ix) lahaula (x) hamadi
266
267
3. Upatanisho wa kisaru: Vivumishi vya sifa - Ngeli A/
WA - KI/VI
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
‘-zuri’ ‘-baya’
a mchezaji mzuri mbaya Mchezaji mzuri amepigiwa mako.
wa wachezaji wazuri wabaya Wachezaji wazuri wamepigiwa
mako.
u mlango mzuri mbaya Mlango mbaya umeng’olewa.
i milango mizuri mibaya Milango mibaya imeng’olewa.
u ulezi mzuri mbaya Ulezi mzuri ulisaidia.
ya malezi mazuri mabaya Malezi mazuri yalisaidia.
ya manukato mazuri mabaya Manukato mazuri yananukia.
ya manukato mazuri mabaya Manukato mazuri yananukia.
li shamba zuri baya Shamba baya limeuzwa.
ya mashamba mazuri mabaya Mashamba mabaya yameuzwa.
ki kinanda kizuri kibaya Kinanda kizuri kinacheza.
vi vinanda vizuri vibaya Vinanda vizuri vinacheza.
Zoezi
Rekebisha matumizi ya vivumishi vya sifa katika sentensi zifuatazo:
Kwa mfano:
Mfupa migumu umevunjika.
Mfupa mgumu umevunjika.
(a) Msichana warembo wanacheza ngoma.
(b) Kiatu mpya kilinunuliwa jana.
(c) Mshipi chembamba uko wapi?
(d) Malezi chema yanafaa sana.
(e) Kikapu nyekundu kiko kule.
(f) Matunda vyororo yanaliwa.
(g) Maji chungu hayanyweki.
(h) Malimau vibichi si mazuri.
(i) Fahali wanono amechinjwa.
(j) Kiti mfupi kimekaliwa.
266
267
Upatanisho wa kisaru: Vivumishi vya sifa
Ngeli I/ZI - PA-KU-MU
Ngeli Nomino Kivumishi Matumizi
‘-ema’ ‘-pya’
i nyumba njema mpya Nyumba mpya imejengwa.
zi nyumba njema mpya Nyumba mpya zimejengwa.
u uzi mwema mpya Uzi mwema utatumiwa.
zi nyuzi njema mpya Nyuzi njema zitatumiwa.
u usaidizi mwema mpya Usaidizi mpya utatolewa.
u usaidizi mwema mpya Usaidizi mpya utatolewa.
ku kulima kwema kupya Kulima kupya kumeanzishwa.
ku kulima kwema kupya Kulima kupya kumeanzishwa.
pa mahali pema papya Mahali pema ni papi?
ku mahali kwema kupya Mahali kwema ni kupi?
mu mahali mwema mpya Mahali pema ni wapi?
Zoezi
Chagua kivumishi mwafaka kukamilisha sentensi.
(a) Bahasha ____________ (jeupe, nyeupe) imenuliwa.
(b) Uto ________ (pana, mpana) utatumiwa.
(c) Nguo ________ (kuukuu, vikuukuu) imechomwa.
(d) Mimi sili wali ________ (kavu, mkavu).
(e) Mahali ________ (ndogo, padogo) pamefungwa.
(f) Mahali ________ (kutupu, tupu) kutawekwa mizigo.
(g) Kutembea ________ (mgeni, kugeni) kumeanza.
(h) Ndoo ________ (fupi, mfupi) imenunuliwa.
(i) Wembe ________ (nyepesi, mwepesi) uko wapi?
(j) Ukali ________ (mingi, mwingi) haufai.
D. Kusoma
1. Riwaya: Wahusika
Katika sura ya ishirini na mbili, tuliona kuwa kuna mambo kadha ya
kuangalia tunapowachunguza wahusika wa riwaya. Je, kuna wahusika
wa aina moja tu? Wahusika wanaopatikana katika riwaya huwa wa aina
mbalimbali. Tunaweza kuwaangalia wahusika kwa kujiuliza jukumu la
wahusika hao? Je, nafasi waliyo nayo wahusika hao ni ndogo au ni kubwa? Je,
maudhui ya riwaya na hadithi inayosimuliwa inawategemea wahusika hao?
Kwa msingi huu tunapata wahusika wakuu (wanaochukua nafasi kubwa) na
wahusika wadogo au wajenzi (wanaochukua nafasi ndogo au wanaowajenga
hao wakubwa).
268
269
Njia ya pili inayoweza kutumiwa kuelezea wahusika ni kuangalia sifa
zao za ndani na kujiuliza kama wanakua au la. Kuna baadhi ya wahusika
ambao hukua na kubadilika kama binadamu wa kawaida. Wahusika hawa
hufanana kwa kiasi kikubwa na sisi. Wahusika hawa hubadilika kiumbo,
kiakili, kimawazo, kimtazamo kadiri ploti ya riwaya inavyosonga. Wahusika
hawa hujulikana kama wahusika duara au wahusika wa miraba minne.
Wapo wengine ambao hawabadiliki bali wanabaki katika hali ile ile moja;
hawabadiliki kabisa. Hawa hujulikana kama wahusika bapa au wahusika
wa mraba mmoja.
Maswali
(a) Eleza njia mbili zinazoweza kutumiwa kuwaelezea wahusika
wanaopatikana katika riwaya.
(b) Je, kuna tofauti gani kati ya wahusika duara na wahusika bapa?
2. Sentensi zenye maana tatanishi
Katika lugha ya Kiswahili, huweza kutukia hali ambapo sentensi moja huweza
kuwa na maana zaidi ya moja. Inapokuwa hivi, sentensi hiyo husemwa kuwa
ina maana tatanishi au inatatanisha kimaana. Maana mbalimbali ya sentensi
yenye maana tatanishi aghalabu hubainishwa kupitia namna mbalimbali za
kuitamka, kuiandika au kuisoma sentensi hiyo. Tazama mifano:
1. Tumetengeneza barabara.
Sentensi hii inapotamkwa kwa kutilia mkazo/shadda kwenye silabi
ya pili kutoka mwisho (ilivyo kawaida katika lugha ya Kiswahili)
itamaanisha kuwa njia imetengenezwa. Lakini tukitia shadda kwenye
‘a’ ya tatu kutoka mwisho, yaani bar’abara, tunamaanisha kuwa kuna
kitu tulichokitengeneza vizuri.
2. Wanawake wengi wamewasili.
Kutegemea tunavyotamka sentensi hii, inaweza kumaanisha kuwa
watoto wengi wa mtu fulani wamewasili au kuwa watu wa kike wengi
wamewasili.
3. Ninataka damu hapa nyumbani.
Sentensi hii, kutegemea matamshi, yaweza kumaanisha kuwa
tunahitaji damu, yaani ngeu, kwenye maskani fulani au kuwa
tunaingia kwenye maskani kwa mara ya kwanza.
4. Sisi tunaondoka walakini wageni wanakuja.
Sentensi hii nayo inaweza kumaanisha kuwa sisi tunaondoka lakini
wageni wanakuja au kwamba sisi tunaondoka nanyi mnahitajika
kuwalaki wageni wanaokuja.
5. Baba, John ameka.
Tukisoma sentensi hii kwa kuzingatia kituo baada ya neno ‘baba’,
268
269
tunamaanisha kuwa tunamwarifu baba kuwa mtu aitwaye John
ameka. Tusipozingatia kituo hicho ifaavyo, itamaanisha kuwa baba
yake John, au mtu aitwaye ‘Baba John’ ndiye aliyeka.
Zoezi
Soma sentensi 1-5 hapo juu ukibainisha maana tofauti tofauti.
E. Kuandika
Resipe
Resipe ni neno linalotumiwa kuelezea mwongozo wa mapishi, yaani maelekezo
ya jinsi ya kutayarisha mapishi fulani; nini kinachohitajika, hatua za kuandaa
chakula hicho n.k. Resipe humsaidia mpishi au anayeandaa chakula awe
na mpangilio maalum katika kazi ya upishi; bila ya kuwa na mpangilio
huu hawezi kuandaa mapishi. Resipe huwa na sehemu tatu kuu: jina la
chakula (au mada) kinachoandaliwa, mahitaji ya kuandaa chakula hicho na
matayarisho au hatua zenyewe za mapishi.
Mfano wa 1
Mada: Upikaji wa uji (wa takriban watu wanne)
Unahitaji nini
1. Kikombe kimoja cha ulezi au unga wa kawaida.
2. Vikombe vitatu na nusu vya maji au maziwa au mchanganyiko wa
maziwa na maji.
3. Kijiko kimoja cha chumvi au viwili vya sukari.
Maandalizi
1. Chemsha maji au maziwa halafu uongezee unga taratibu huku ukikoroga.
2. Koroga ule mchanganyiko hadi uanze kushikamana na kuwa mzito.
3. Acha uchemke pole pole kwa dakika kumi hivi.
4. Andaa uji ukiwa bado u moto.
Mfano wa 2
Mada: Upikaji wa sambusa
Sambusa ni aina ya andazi dogo ambalo aghalabu huwa na nyama, viazi,
kitunguu na viungo vingine mbalimbali. Sambusa huwa tamu sana kama
zimetengenezwa inavyostahili. Ifuatayo ni resipe ya kuandaa sambusa.
Unahitaji nini
1. Nyama ya kusaga au kima ya nusu kilo.
2. Vitunguu mboga vinne ambavyo vimekatwakatwa vizuri.
3. Kijiko cha chai cha tangawizi iliyosagwa.
270
271
4. Nusu kijiko cha chai cha kitunguu saumu.
5. Chumvi ya kipimo cha robo moja ya kijiko cha chai.
6. Pilipili hoho moja, iliyokatwakatwa (si lazima).
7. Vijiko vitatu vya chai vya dania iliyosagwa.
8. Vijiko viwili vya chai vya maji ya ndimu.
9. Kikombe kimoja na nusu cha unga wa ngano.
10. Kikombe kimoja cha maji baridi.
11. Nusu kilo ya mafuta ya kukaangia/kupikia.
Maandalizi
1. Chukua sufuria au kikaangio kikubwa, changanya nyama, kitunguu
saumu, tangawizi, chumvi, maji ya ndimu na pilipili hoho (ikiwa
inahitajika).
2. Pika kwa joto la wastani huku ukitenganisha nyama kwa uma ili
isiungane na kuwa madonge.
3. Funika na upike kwa kati ya dakika 20 na 25 au hadi unyevunyevu uishe
na nyama kuiva.
4. Wakati nyama inaendelea kupikika, chungia unga na chumvi kwenye
bakuli. Ongeza ndimu na mafuta vijiko viwili vya chai pamoja kisha
uchanganye kwa maji hadi upate kinyunya kigumu. Changanya
kinyunya hicho vizuri mpaka kiwe laini na kiweze kuvutika.
5. Baadaye gawa kinyunya hicho katika vipira vyenye ukubwa wa kijiko
kikubwa.
6. Chukua kipira kimoja na ukikande hadi kichukue sura ya kisahani cha
kikombe cha chai. Paka mafuta upande wa ndani. Kata kisahani hicho
kiwe na sura ya pembetatu.
7. Chukua kijiko na uchote ule mchanganyiko wenye nyama na kutia
katikati.
8. Zichukue pembe za ile pembetatu na uzishikanishe. Unaweza kutumia
lahamu (ya kushikanisha) inayotokana na kuchanganya vijiko viwili vya
unga na maji baridi. Hakikisha kuwa pande zote zimeshikana vizuri ili
mafuta yasipenye ndani wakati wa kupika.
9. Rudia hatua hizi (kuanzia ya tano) hadi umalize kile kinyunya
ulichotayarisha.
10. Weka mafuta ya kutosha ndani ya kikaango na yape muda yachemke.
Kaanga sambusa chache kwa muda katika mafuta ya moto hadi ziwe
rangi ya hudhurungi isiyokolea sana. Kausha kwa kutumia karatasi
maalum.
11. Andaa zingali moto. (zaweza andaliwa na kinywaji moto au baridi)
Maswali
1. Je, kwa nini unakiri resipe ni muhimu?
2. Andika resipe ya upikaji wa chakula ambacho unakipenda.
270
271
Mazoezi ya marudio III
A. Ufahamu
Soma shairi lifuatalo halafu ujibu maswali uliyoulizwa
1. Wazalendo himahima, uchumi kuufufua,
Tena tusimame wima, hatua kuzichukua,
Jambo lililo lazima, mbinu bora kutumia,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
2. Uchumi kuufufua, si hotuba ndefu sana,
Moja litosaidia, ni kwa kuhamasishana,
Jengine lafuatia, sote kushirikiana,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
3. Malengo kuyakia, jamani si maongezi,
Hasa litotuinua, ni kuwa wachapa kazi,
Jukumu kutumikia, raia na viongozi,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
4. Kufanya kazi lazima, tuacheni utegezi,
Na jingine la kukoma, kuwepo kwa ubaguzi,
Kutupiana lawama, ni mambo ya kipuuzi,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
5. Uliyepewa dhamana, uache kupora mali,
Acha kutia tina, jungu si kitu amali,
Ni bora kukosoana, uonapo idhilali,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
6. Kile tunokipitisha, mumo mwetu vikaoni,
Isiwe kukikwamisha, tukawa hatukioni,
Au kukikadilisha, tusikione machoni,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
7. Ni lazima tuwe macho, kutekeleza sheria,
Tutumie tulonacho, uchumi kuufufua,
Tumtoe kwenye cho, kila ano mbaya nia,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
8. Tamaa ya utajiri, tuiacheni jamani,
Mbona hii hatari, inatutia shidani,
Mnaacha desturi, tunafata njia gani?
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
272
273
9. Jama zigo la makuti, katu tusijejitwika,
Sijeka katikati, mambo yakaja panguka,
Tukatafuta mauti, ahadi haijaka,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
10. Tuwekeni muongozo, tusijitie vikwazo,
Tupime wetu uwezo, tusibebe matatizo,
Yapokwepo mawazo, sijetokea mzozo,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
11. Ya kupanga yenye kheri, yalo na fanaka njema,
Tusitafute ya shari, ikajazuka zahama,
Mambo yanende vizuri, kama tulivyoyapima,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
(‘Tuyazingatie haya’ kutoka Malenga Wapya,
Taasisi ya Kiswahili Zanzibar, uk 27-28)
Maswali
1. Je, shairi hili ni la aina gani? Kwa nini?
2. Je, mshororo mmoja una mizani mingapi?
3. Katika ubeti wa kwanza mtunzi anasema kuwa kuna njia mbili muhimu
za kuufufua uchumi. Ni zipi hizo?
4. Je, ni mambo gani anayokataza mtunzi kuanzia ubeti wa pili hadi wa
sita?
5. Taja mambo sita anayoyasema mtunzi ambayo yatasaidia ili tusirudi
nyuma.
6. Je, ni ushauri gani anaoutoa mshairi kwa viongozi katika ubeti wa tano
na wa nane?
7. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa:
a) kuhamasishana b) utegezi c) jungu d) idhilali e) tunokipitisha
8. Taja methali moja inayoweza kueleza ujumbe wa shairi hili.
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Chagua jibu sahihi kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) _________ (avya, afya) ya mtoto huyu imezorota sana.
(b) Huko Somalia kumetokea _________ (vita, ta) vikali.
(c) Kamene ali_________ (futwa, vutwa) kazi jana.
(d) _________ (vaa, faa) nguo twende mjini.
(e) Mbarire ameenda mtoni _________ (kuvua, kufua) samaki.
272
273
2. Tunga sentensi ili kutofautisha maana ya maneno katika jozi zifuatazo:
(a) mkuu mguu
(b) ukali ugali
(c) mfuko mfugo
(d) koti goti
C. Saru na matumizi ya lugha
1. Tenganisha kikundi nomino (KN) na kikundi tenzi (KT) katika sentensi
zifuatazo:
Kwa mfano: Mama yangu ameenda sokoni.
mama yangu - KN
ameenda sokoni - KT
(a) Baba yake anaishi Cherangani.
(b) Ng’ombe wale watauzwa leo.
(c) Duka hili lilivunjwa usiku.
(d) Watoto wanataka chakula.
(e) Ndoo yangu inavuja.
(f) Gari hili lilianguka lini?
(g) Wanafunzi ishirini wamepita mtihani.
(h) Kitabu cha dadangu kimeibiwa.
(i) Kijiko cha mtoto kina uchafu.
2. Geuza kitenzi kilichomo mabanoni kulingana na kauli uliyopewa.
Kwa mfano: Nyumba hii hai_________. (jenga, tendeka)
Nyumba hii haijengeki.
(a) Kiatu hiki kime_________ . (rarua, tendeka)
(b) Watu wale wali_________ jana jioni. (piga, tendana)
(c) Wanafunzi wa shule hii hu________ kila wakati. (saidia, tendana)
(d) Mlango ule umeanza ku_________. (fungua, tendeka)
(e) Watoto wali_________. kimbia tendeshana)
3. Tambulisha viwakilishi nafsi huru katika sentensi zifuatazo:
(a) Wewe unaitwa nani?
(b) Mimi sitawasaidia wao.
(c) Nyinyi mlika lini?
(d) Sisi na wao tutaondoka kesho.
(e) Yeye alimuudhi mwalimu.
4. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kunyambua kitenzi katika kauli
uliyopewa:
274
PB
mzizi wa kitenzi kauli ya kutendeshana kauli ya kutendeshea
kwa mfano:
imba- imb-ish-an-a imb-ish-i-a
toa-
chek-
simam-
sari-
som-
5. Onyesha vihisishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Zii! Kwa nini unafanya mambo kama hayo?
(b) Pole! Sikutaka kukuudhi.
(c) Barabara! Tutaonana kesho panapo majaaliwa.
(d) Siwezi kukubali jambo kama hilo. La hasha!
(e) Hodi kwa wenyewe!
D. Kuandika
Muhtasari
Andika muhtasari wa kifungu kifuatacho kwa maneno yasiyozidi theluthi
moja:
Nchini Kenya, dhana ya mtoto inatofautiana kutoka jamii moja hadi nyingine.
Katika jamii nyingi, kuna mila na desturi ambazo huashiria kuvuka kutoka
utotoni kuingia utu uzima. Tutaziita mila hizi za upisho kwa sababu
humpitisha mtu kutoka kiwango kimoja hadi kingine. Mtu huwa mzima
punde anapopitia mila na desturi za upisho. Mila na desturi hizo za upisho
huwa muhimu kwa kuwa mtu akitambuliwa kama mtu mzima hupata uhuru
wa kutekeleza mambo fulani kama vile haki ya kuoa au kuolewa. Umri wa
kupitia mila na desturi za upisho hutofautiana kutegemea jamii. Mtu aliye
na umri wa miaka kumi na mitatu anaweza kuwa mtoto katika jamii moja,
na katika jamii nyingine akawa mtu mzima.
Serikali ya Kenya imepitisha sheria ya kusawazisha dhana ya mtoto.
Usawazishaji huo umeakiwa kwa kutumia umri. Kwa mujibu wa Sheria ya
Watoto ya Mwaka 2001, mtoto ni mtu aliye na umri wa chini ya miaka kumi
na minane. Hii ni kuambatana na Makubaliano Kuhuhsu Haki za Watoto
ya mwaka wa 1990.
Kwa kuzingatia kigezo cha umri, mtu anapotimiza umri wa miaka kumi na
minane huwa amepiga hatua muhimu katika ukuaji wa mwanadamu, na
hivyo huwa mzima anapotimiza miaka kumi na minane. Ijapokuwa haya ni
kweli katika ujumla wake, mazingira anamokulia mtu kama vile mazingira
ya kitamaduni, kijamii na kisiasa huchangia pakubwa katika kuamua ni
wakati gani mtu anapokuwa mzima.
(Imenukuliwa kutoka jarida la Watoto na Haki za Kibinadamu Nchini Kenya,
Legal Resources Foundation Trust 2002, uk. 1)