Chemchemi za Kiswahili
Kidato cha Kwanza
(Toleo Jipya)
K. W. Wamitila
Gichohi Waihiga
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 1 12/11/2019 09:44
Kimechapishwa na:
Longhorn Publishers (Kenya) Ltd.,
Barabara ya Funzi, Eneo la Viwandani,
S.L.P. 18033-00500,
Nairobi,
Kenya.
Longhorn Publishers (Uganda) Ltd.,
Kitalu Na. M220, Eneo la Viwandani la Ntinda,
Barabara ya Jinja,
S.L.P. 24745,
Kampala,
Uganda.
Longhorn Publishers (Tanzania) Ltd.,
Kitalu Na. 664, Eneo la Msasani,
Kitengo F, Jumba Na. 664,
Barabara ya zamani ya Bagamoyo,
S.L.P 1237,
Dar-es-Salaam,
Tanzania.
© K. W. Wamitila, G. Waihiga, 2003
© Michoro: Longhorn Publishers
Haki za kimaadili za waandishi zimezingatiwa.
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupiga chapa, kutafsiri au
kukitoa kitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila idhini, kwa maandishi, ya Longhorn
Publishers Limited.
Chapa ya kwanza 2003
Chapa nyingine 2003 (mara mbili), 2004 (mara tatu), 2005, 2006, 2007
Kimefanyiwa masahihisho mara ya kwanza 2008, 2017
Toleo hili, 2019.
ISBN 978 9966 49 519 3
Kurasa zimeruwazwa na Steve Nganyi
Michoro imechorwa na Tu Mulokwa
Kimepigwa chapa na ............................................................
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 2 12/11/2019 09:44
iii
Yaliyomo
Sura ya Kwanza.............................................................................................................. 1
Ufahamu
Karibuni wanafunzi..................................................................................................................... 1
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora.............................................................................................................................3
Aina za sauti ................................................................................................................................5
Saru na matumizi ya lugha
Dhima ya lugha ...........................................................................................................................9
Vipashio vya lugha ....................................................................................................................10
Sauti za Kiswahili....................................................................................................................... 10
Viambishi ................................................................................................................................... 11
Kusoma
Ufahamu ....................................................................................................................................13
Kuandika
Insha ..........................................................................................................................................14
Sura ya Pili................................................................................................................... 18
Ufahamu
Ielewe lugha yako ......................................................................................................................18
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi: Kiimbo.................................................................................................................... 20
Shadda/Mkazo ...........................................................................................................................20
Saru na matumizi ya lugha
Kuakisha ..................................................................................................................................21
Kusoma
Kusoma kwa kina: Mashairi ya arudhi ...................................................................................23
Kuandika
Aina za insha..............................................................................................................................24
Sura ya Tatu ................................................................................................................. 28
Ufahamu
Fadhila za punda .......................................................................................................................28
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi: Utangulizi....................................................................................................................... 30
Saru na matumizi ya lugha
Mpangilio wa sauti katika silabi na maneno.......................................................................... 31
Kusoma
Kusoma kwa kina: Mashairi huru ...........................................................................................34
Kuandika
Maana na dhima ya utungaji....................................................................................................35
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 3 12/11/2019 09:44
iv
Sura ya Nne.................................................................................................................. 38
Ufahamu
Hoteli ya vizito...........................................................................................................................38
Kusikiliza na Kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - p/b....................................................................................................40
Isimujamii................................................................................................................................... 40
Saru na matumizi ya lugha
Kuakisha/uakishaji ...............................................................................................................41
Vivumishi (V) ............................................................................................................................43
Kusoma
Kusoma kwa mapana: Magazeti ..............................................................................................44
Kuandika
Insha za mdokezo......................................................................................................................45
Sura ya Tano ................................................................................................................ 49
Ufahamu
Chifu Mbuguma na mali ya umma......................................................................................... 49
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - t/d .....................................................................................................51
Fasihi ..........................................................................................................................................52
Saru na matumizi ya lugha
Viwakilishi (W) .........................................................................................................................54
Wakati uliopo NA ..................................................................................................................55
Kukanusha wakati uliopo kulingana na nafsi........................................................................55
Kusoma
Matumizi ya maktaba ...............................................................................................................56
Sura ya Sita .................................................................................................................. 59
Ufahamu
Kamusi ni kurunzi ya lugha.....................................................................................................59
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - k/g .....................................................................................................60
Isimujamii................................................................................................................................... 60
Saru na matumizi ya lugha
Vitenzi (T) ..................................................................................................................................62
Kusoma
Mambo muhimu ya kujua kuhusiana na maktaba ...............................................................64
Kuandika
Utungaji wa kisanii: Utangulizi ...............................................................................................65
Sura ya Saba................................................................................................................. 67
Ufahamu
Dawa za kulevya na jamii.........................................................................................................67
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 4 12/11/2019 09:44
v
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - ch/j ...................................................................................................69
Ufahamu wa kusikiliza..............................................................................................................69
Saru na matumizi ya lugha
Vielezi (E) ...................................................................................................................................70
Wakati ujao - TA........................................................................................................................ 71
Kukanusha wakati ujao kulingana na nafsi............................................................................71
Kusoma
Kusoma kwa kina: Majarida.....................................................................................................72
Kuandika
Utungaji wa kisanii.................................................................................................................... 73
Sura ya Nane................................................................................................................ 76
Ufahamu
Katiba ya Msenangu..................................................................................................................76
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate f/v.....................................................................................................79
Fasihi simulizi: Hurafa..............................................................................................................79
Saru na matumizi ya lugha
Vihisishi (I)................................................................................................................................. 80
Uakishaji...................................................................................................................................81
Mnyambuliko wa vitenzi..........................................................................................................82
Kusoma
Kusoma kwa kina: Utangulizi..................................................................................................84
Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Barua................................................................................................. 85
Zoezi la Marudio I....................................................................................................... 88
Ufahamu .....................................................................................................................................88
Kusikiliza na kuzungumza .......................................................................................................89
Saru na matumizi ya lugha ....................................................................................................89
Kusoma ......................................................................................................................................92
Kuandika .................................................................................................................................... 92
Isimujamii................................................................................................................................... 92
Sura ya Tisa.................................................................................................................. 93
Ufahamu
Si maradhi ni kumbakumba.....................................................................................................93
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora-Vitate: ch/sh ...................................................................................................96
Soma: Vitanza ndimi................................................................................................................ 96
Sajili ya dukani...........................................................................................................................96
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 5 12/11/2019 09:44
vi
Saru na matumizi ya lugha
Hali ya me .................................................................................................................................97
Viunganishi (U).........................................................................................................................99
Kusoma
Kusoma kwa kina: Ushairi kwa jumla ....................................................................................99
Kuandika
Barua rasmi ..............................................................................................................................100
Sura ya Kumi ............................................................................................................. 105
Ufahamu
Tangu lini nikawa kiatu?.........................................................................................................105
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora ........................................................................................................................107
Hekaya ..................................................................................................................................107
Saru na matumizi ya lugha
Vihusishi (H)............................................................................................................................108
Uakishaji.................................................................................................................................109
Mnyambuliko wa vitenzi: Kauli ya kutenda, kutendwa na kutendeka.............................110
Kusoma
Usomaji wa kina: Ushairi.......................................................................................................111
Kuandika
Hadithi fupi..............................................................................................................................113
Sura ya Kumi na Moja ............................................................................................... 116
Ufahamu
Jumakoshi alikiona..................................................................................................................116
Kusikiliza na kuzungumza
Semi ..........................................................................................................................................119
Methali......................................................................................................................................119
Saru na matumizi ya lugha
Hali ya mazoea (HU) ..............................................................................................................120
Tashbiha/Tashbihi ...................................................................................................................122
Kubainisha maneno katika sentensi......................................................................................122
Kusoma
Fasihi Andishi: Riwaya ...........................................................................................................123
Kuandika
Insha ya maelezo......................................................................................................................124
Sura ya Kumi na Mbili............................................................................................... 127
Ufahamu
Peremende za Bwana Pipi ......................................................................................................127
Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii: Sajili ya sokoni ....................................................................................................129
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 6 12/11/2019 09:44
vii
Saru na matumizi ya lugha
Ngeli za nomino.......................................................................................................................131
Kusoma
Fasihi andishi: Tamthiliya ......................................................................................................133
Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Ratiba..............................................................................................133
Sura ya Kumi na Tatu ................................................................................................ 136
Ufahamu
Methali ni johari......................................................................................................................136
Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii: Sajili: Lugha ya shuleni ......................................................................................137
Saru na matumizi ya lugha
Ukubwa na udogo wa nomino...............................................................................................139
Kusoma
Matumizi ya kamusi................................................................................................................141
Umuhimu wa kamusi..............................................................................................................142
Muundo na mpangilio wa kamusi ........................................................................................142
Kuandika
Uandishi wa insha ya masimulizi..........................................................................................143
Sura ya Kumi na Nne................................................................................................. 145
Ufahamu
Fungua Sesame .......................................................................................................................145
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi simulizi: Vitendawili na Mafumbo ............................................................................147
Saru na matumizi ya lugha
Ngeli za nomino ......................................................................................................................148
Kuakisha.................................................................................................................................150
Kusoma
Kusoma kwa mapana: Makala na vitabu vya ziada.............................................................151
Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Tahadhari .......................................................................................151
Sura ya Kumi na Tano ............................................................................................... 154
Ufahamu
Ulimwengu wa kompyuta .....................................................................................................154
Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii: Sajili ya shuleni II ...............................................................................................156
Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -angu’, -ako’, -ake ..................................................157
Kuakisha.................................................................................................................................159
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 7 12/11/2019 09:44
viii
Kuandika
Utungaji wa kisanii: Vitendawili na mafumbo/chemshabongo......................................160
Sura ya Kumi na Sita ................................................................................................. 163
Ufahamu
Bado ningali kijana .................................................................................................................163
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi..........................................................................................................................165
Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -angu, -ako’, -ake ..................................................166
Kuakisha.................................................................................................................................167
Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Matangazo......................................................................................168
Zoezi la Marudio II ................................................................................................... 171
Ufahamu ..................................................................................................................................171
Kusikiliza na kuzungumza .....................................................................................................172
Saru na matumizi ya lugha ..................................................................................................174
Kusoma .....................................................................................................................................177
Kuandika ..................................................................................................................................178
Sura ya Kumi na Saba................................................................................................ 179
Ufahamu
Teknolojia na maisha ya sasa ................................................................................................180
Kusikiliza na kuzungumza
Mjadala .....................................................................................................................................181
Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Kirejeshi amba- ..........................................................................181
Mnyambuliko wa vitenzi: Kauli ya kutendana na kutendesha..........................................182
Kuandika
Imla ...........................................................................................................................................184
Utungaji wa kiuamilifu: Kujaza fomu...................................................................................184
Jaza fomu ifuatayo kwa usahihi .............................................................................................185
Sura ya Kumi na Nane............................................................................................... 187
Ufahamu
Runinga ya Mizengwe.............................................................................................................187
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi simulizi ..........................................................................................................................189
Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Kirejeshi amba-............................................................................190
Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Hotuba............................................................................................191
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 8 12/11/2019 09:44
ix
Sura ya Kumi na Tisa................................................................................................. 194
Ufahamu
Polisi na dhima yao .................................................................................................................194
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi simulizi ..........................................................................................................................196
Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -etu, -enu na -ao ..................................................197
Kuakisha.................................................................................................................................198
Sentensi ya Kiswahili ..............................................................................................................199
Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Maagizo/maelekezo ......................................................................200
Utungaji wa kiuamilifu: Mahojiano na dayalojia................................................................201
Vidokezi muhimu....................................................................................................................202
Sura ya Ishirini .......................................................................................................... 204
Ufahamu
Siri ya jirani ..............................................................................................................................204
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi..........................................................................................................................206
Saru na matumizi ya lugha
Muundo wa sentensi: Kirai ....................................................................................................207
Kikundi nomino na kikundi tenzi.........................................................................................208
Kusoma
Matumizi ya aina mbalimbali za kamusi..............................................................................210
Kuandika
Utungaji wa kisanii: Vitanza ndimi.......................................................................................211
Sura ya Ishiri na Moja ............................................................................................... 213
Ufahamu
Simu na mawasiliano ya binadamu.......................................................................................213
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi: Maigizo .........................................................................................................214
Utangulizi .................................................................................................................................214
Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -etu’, -enu’, -ao.......................................................215
Kuakisha.................................................................................................................................216
Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Taarifa............................................................................................217
Sura ya Ishirini na Mbili ........................................................................................... 219
Ufahamu
Uchafuzi wa Mazingira...........................................................................................................219
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 9 12/11/2019 09:44
x
Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi..........................................................................................................................220
Saru na matumizi ya lugha
Sentensi sahili ..........................................................................................................................222
Kuandika
Muhtasari: Utangulizi .............................................................................................................224
Sura ya Ishirini na Tatu ............................................................................................. 226
Ufahamu
Si urogi, ni ugonjwa ................................................................................................................226
Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii: Sajili ya mtaani....................................................................................................228
Matamshi bora: vitate a/h.......................................................................................................229
Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vionyeshi ......................................................................................230
Kuandika
Muhtasari/ufupisho.................................................................................................................231
Sura ya Ishirini na Nne.............................................................................................. 233
Ufahamu
Kisa cha Edipode.....................................................................................................................233
Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - l/r....................................................................................................235
Saru na matumizi ya lugha
Kuakisha.................................................................................................................................235
Upatanisho wa kisaru: Vionyeshi.......................................................................................236
Kuandika
Barua za magazetini ................................................................................................................238
Zoezi la Marudio III.................................................................................................. 241
Ufahamu ..................................................................................................................................241
Kusikiliza na kuzungumza .....................................................................................................242
Saru na matumizi ya lugha ..................................................................................................242
Kusoma .....................................................................................................................................245
Kuandika ..................................................................................................................................246
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 10 12/11/2019 09:44
1
A. Ufahamu
Karibuni wanafunzi
Wanafunzi walikuwa wakiterema kwa furaha katika ukumbi wa shule. Hii ilikuwa siku yao ya
kwanza katika shule ya upili. Waliyasubiri kwa hamu kuu makaribisho rasmi ya mwalimu mkuu
wa shule hii yenye sifa kem kem. Muda si muda mlango ulifunguliwa. Sauti zilizokuwa juu
zilinywea. Wanafunzi wote waliyaelekeza macho mlangoni. Mwalimu mkuu aliingia. Alikohoa
kidogo kulisasha koo kisha akasema, “Wanafunzi wa kidato cha kwanza hamjambo?”
“Hatujambo mwalimu!” tulijibu kwa pamoja.
“Ni furaha yangu kuu kuwakaribisha katika shule hii ya kitaifa ya Fanaka. Madhumuni ya
kuwataka mtangamane hapa, fauka ya kuwakaribisha rasmi, ni kuwajulisha na kuwafahamisha
mambo kadha. Maisha yenu ya baadaye ni kama jengo, na jengo likikosa msingi imara na madhubuti
hutetereka na hatimaye kuanguka.
Lengo la kimsingi la shule ni kuwakuza wanafunzi ambao, zaidi ya kufuzu vizuri katika masomo
yao, watakuwa vielelezo kwa taifa zima. Ninajua mna furaha kubwa baada ya kuhitimu mtihani wa
darasa la nane. Ni kweli kuwa kila mtu ana haki ya kuufurahia ufanisi wake, lakini tujue pia kuwa
tamu ikizidi tamu huwa si tamu tena. Ninachomaanisha ni kuwa inatujuzu kukumbuka kuwa,
baada ya sherehe kuna kazi pia. Ili muweze kuwa na furaha kama hii tena baada ya matokeo ya
mtihani wa kidato cha nne, lazima muwe na bidii kuanzia mwanzo. Elimu ni kama safari na ni
muhimu kuwa tayari mapema. Waswahili husema kuwa msari ni aliye pwani.
Ni matumaini yangu kuwa haitawachukua muda mrefu kutulia na kuyazoea maisha yenu
mapya. Kutulia huko ni muhimu ili kuwawezesha kukabiliana na majukumu mazito na adhimu
yatakayowakabili. Ili kuwasaidia katika kutulia na kujizoeza vyema kwenye mazingira haya mapya,
kila mmoja atapewa mwelekezi wa kumwongoza na kumshauri kuhusu kanuni za shule pamoja na
kumjuza sehemu mbalimbali ambako shughuli fulani maalum huendeshewa. Baadhi ya sehemu
muhimu mnazotakiwa kuzijua ni maabara. Mathalani, maabara ya Kemia, Elimu-Viumbe na
Sura ya Kwanza
Karibuni wanafunzi
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 1 12/11/2019 09:44
2
Fizikia. Aidha kuna chumba cha mafunzo ya tarakilishi. Kama mnavyojua, tunaishi katika karne
ambapo maendeleo ya kisayansi ni nguzo kuu ya ufanisi wa maisha ya binadamu.
Ni muhimu kukumbuka siku zote kuwa shule yetu hii imejengwa kwenye misingi ya nidhamu
kwa kutambua kuwa kijengacho mtu ni utu na tabia. Kila mwanafunzi anatarajiwa kuonyesha
nidhamu ya hali ya juu kwa walimu, wafanyikazi wengine wa shule, viranja na kwa wanafunzi
wenzake. Ni lazima kila mwanafunzi ahakikishe kuwa amezingatia adabu na mbeko katika
matumizi ya lugha, kuzifuata kanuni zote za shule na kujiweka katika hali nadhifu.
Yamkini wengi mmeyazoea maisha ya nyumbani, lakini hivi sasa mtalazimika kukaa mbali na
ndugu, raki na aila zenu. Hali hii mpya haipaswi kuwa sababu ya kuwatosa katika biwi la simanzi.
Badala ya kuhuzunika, mnapaswa kufurahia kuipata fursa na abra hii ya kujipatia maraki
wapya wa rika lenu. Aidha, hii ni nafasi nzuri ya kukumbana na hali nyingine ya maisha ambayo
itawawezesha kuupanua ufahamu pamoja na uzoefu wenu wa kimaisha. Maraki utakaokutana
nao hapa wanatoka sehemu mbalimbali za nchi yetu na kwa kushirikiana nao na kufanya usuhuba
nao utajenga nguzo imara ya ushirikiano katika miaka ya usoni. Huu ni msingi muhimu wa
ushirikiano katika kiwango cha taifa, na kiini cha utangamano mkubwa wa utaifa. Hata hivyo,
sio maraki wote ambao ni wazuri kwa sababu hakuna mchele ukosao ndume. Lazima muwe na
uangalifu katika kuwachagua maraki zenu. Ukishirikiana na raki mbaya lazima atakuathiri.
Nadhani sote tunajua kuwa mcheza na tope humrukia.
Ikiwa utakumbana na matatizo yoyote usisite kumwuliza mwelekezi wako. Aidha, ni muhimu
kuwauliza wanafunzi wengine ambao wana tajiriba ya mambo hayo hapa shuleni au hata
walimu wenu. Usilifutike jambo linalokusumbua au kukukalifu moyoni kwa sababu mwishowe
litakuletea madhara makubwa. Ni muhimu kukumbuka niliyotangulia kusema kuwa, nia yetu
siyo kuwaandaa wanafunzi wanaomudu masomo pekee, bali kuwakuza watu waliokamilika
kiakili na kiutu. Hali hii haiwezi kukiwa ikiwa kila mmoja atajitenga kivyake. Sote tunaelewa
umuhimu wa methali isemayo umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.
Ningependa kumalizia kwa kutoa mfano huu. Mimi binafsi huiona shule kama kuku
anayeatamia mayai. Akiyaatamia vizuri na katika mazingira mema, yale mayai yatatotoa vifaranga
wengi na wenye matumaini. Vifaranga hawa nao wataiendeleza jamii ya kesho. Lazima sote
tushirikiane kuhakikisha kuwa hakuna mayai viza katika shule hii yetu.
Katika kipindi kijacho cha siku tatu, mtapata fursa ya kujulishwa sehemu mbalimbali za shule
yetu na kuwajua walimu wenu. Ni matumaini yangu kuwa baada ya kipindi hicho, kila mmoja
wenu atakuwa tayari kuyaanza masomo yake kwa msukumo mpya na bidii kubwa. Kwa miaka
minne ijayo tutakutana mara nyingi na kuyazungumza mengi. Kwa mara nyingine nawapongeza
kwa matokeo bora katika mtihani wenu wa darasa la nane. La kuwakumbusha tu ni kuwa ukilima
pantosha, utavuna pankwisha.
Sasa mnaweza kurejea madarasani mwenu kuwasubiri walimu ambao watawapa maelekezo
na maagizo zaidi. Asanteni.
Maelezo ya msamiati
aila : watu wanaohusiana kwa njia fulani kama vile kifamilia, kidugu, n.k.
kukukalifu : kukusumbua; kukutaabisha; kukuhangaisha.
abra : nafasi; wasaa.
adhimu : yenye sifa; zuri; tukufu.
vielelezo : mfano bora; mfano wa kuigwa.
mbeko : adabu; heshima.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 2 12/11/2019 09:44
3
wakiterema : wakiwa na furaha na uchangamfu.
inatujuzu : inatupasa.
zilinywea : zilia.
madhubuti : yenye nguvu; imara; thabiti.
Maswali
1. Ni kwa nini wanafunzi walikuwa na furaha kiasi hiki?
2. Shule ya kitaifa ni shule ya aina gani?
3. Mwalimu mkuu alikuwa na maana gani aliposema tamu ikizidi tamu huwa si tamu tena?”
4. Taja mawaidha matatu ambayo mwalimu mkuu aliwapa wanafunzi.
5. Ni kwa njia ipi shule inaweza kulinganishwa na kuku anayeatamia mayai?
6. Maraki ambao wanafunzi watakutana nao shuleni watakuwa na umuhimu gani katika
maisha yao ya siku za usoni?
7. Mwalimu mkuu aliwatahadharisha wanafunzi kuhusu maraki wabaya. Kwa nini?
8. Ni nini umuhimu wa nidhamu kwa mwanafunzi na binadamu yeyote kwa jumla?
9. Eleza maana ya misemo ifuatayo kama ilivyotumika kwenye kifungu:
(a) furaha ya kuchania nguo (b) subiri kwa hamu na ghamu
(ch) biwi la simanzi (d) miaka ya usoni
10. Eleza maana ya methali zifuatazo kama zilivyotumika katika kifungu:
(a) Msari ni aliye pwani.
(b) Hakuna mchele ukosao ndume.
(ch) Mcheza na tope humrukia.
(d) Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu.
11. Methali ukilima pantosha utavuna pankwisha inahusiana vipi na maisha ya binadamu
kwa jumla?
12. Eleza maana ya maneno yafuatayo kulingana na vile yalivyotumika kwenye kifungu:
(a) tarakilishi (b) maabara
(ch) viranja (d) mayai viza
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora
Hatua ya kwanza ya kuongea lugha ni kutamka sauti. Utamkaji wa sauti za lugha huhusisha hewa
inayotoka mapafuni. Mapafu husukuma hewa katika mkondo wa hewa na kuielekeza kooni.
Katika sehemu ya koo, hewa hupitia katika kiungo muhimu sana kinachotetemeka na kutoa
sauti, kinachoitwa nyuzi za sauti. Nyuzi za sauti ndicho chanzo cha sauti zote zinazotamkwa
na binadamu. Baada ya kupitia nyuzi za sauti, hewa huendelea kuelekea kinywani. Tazama
mchoro ufuatao:
Ala za kutamkia
Katika eneo la kinywani, hewa hukumbana na viungo mbalimbali ambavyo ndivyo msingi wa
utamkaji wa sauti. Viungo hivi hujulikana kama ala za kutamkia au ala za sauti. Tazama mchoro
ufuatao unaohusu ala hizi:
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 3 12/11/2019 09:44
4
Mkondo wa hewa
Chemba cha pua
Chemba cha kinywa
Koromeo
Umio wa hewa
Mkondo wa hewa
Mapafu
Ala za kutamkia
Katika eneo la kinywani, hewa hukumbana na viungo mbalimbali ambavyo ndivyo msingi wa
utamkaji wa sauti. Viungo hivi hujulikana kama ala za kutamkia au ala za sauti. Tazama mchoro
ufuatao unaohusu ala hizi:
(a) midomo (g) kaakaa laini
(b) me no (h) kidakatonge
(ch) uzi (i) chemba cha pua
(d) ulimi (j) nyuzi za sauti
(e) chemba cha kinywa (k) umio wa hewa/koo
(f) kaakaa gumu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 4 12/11/2019 09:44
5
Aina za sauti
Kunazo aina mbili kuu za sauti: irabu na konsonanti. Mifano ya irabu ni a, e, i, n.k. Konsonanti
nazo ni kama vile b, ch, d, f, g, h, n.k. Tofauti kuu kati ya irabu na konsonanti ni kwamba wakati
wa kuzitamka irabu, hewa haizuiwi mahali popote, ilhali wakati wa kuzitamka konsonanti hewa
huzuiwa kwenye ala mbalimbali za kutamkia.
Irabu
Irabu za Kiswahili ni tano, nazo ni: a, e, i, o, na u. Katika kuzifafanua na kuzigawa irabu za
Kiswahili katika vikundi au aina mbalimbali, tunazingatia viungo viwili vikuu: ulimi na midomo.
(a) Ulimi
(i) Irabu za mbele: Hizi ni irabu i na e. Hutamkwa kwa kuitumia hasa sehemu ya mbele
ya ulimi, ndiyo sababu zikaitwa irabu za mbele.
(ii) Irabu ya kati: Hii ni irabu a. Hutamkwa kwa kuitumia sehemu ya kati ya ulimi.
(iii) Irabu za nyuma: Hizi ni irabu u na o. Irabu hizi hutamkiwa hasa sehemu ya nyuma
ya ulimi.
(b) Midomo
(i) Midomo ikiwa imetandazwa: Irabu a, e na i hutamkwa midomo ikiwa imetandazwa.
(ii) Midomo ikiwa imeviringwa: Irabu o na u hutamkwa midomo ikiwa imeviringwa.
Hebu itazame midomo ya mwenzio anapozitamka sauti za irabu a, e na i, na kisha
anapozitamka sauti za irabu o na u. Utaona tofauti ya hali ya midomo katika kutamka
vikundi hivyo viwili vya sauti za irabu.
i
e
u
juu
chini
mbele nyuma
o
a
Aina za konsonanti na jinsi ya kuzitamka
Katika utamkaji wa konsonanti, hewa inapopitia kinywani kutoka mapafuni huzuiliwa na viungo
mbalimbali vya kutamkia. Viungo hivyo ni meno, uzi, midomo n.k. Ili kuzielewa aina mbalimbali
za konsonanti za Kiswahili, ni lazima tuzingatie jinsi konsonanti hizi zinavyotamkwa kinywani
mwa binadamu. Katika kufanya haya, tunachunguza sifa zifuatazo:
(a) Mahali hewa inapozuiliwa.
(b) Jinsi hewa inavyozuiliwa.
(ch) Hali ya mtetemeko katika nyuzi za sauti.
(a) Mahali hewa inapozuiliwa
Mahali hewa inapozuiliwa wakati wa kuitamka sauti fulani ya konsonanti, ndipo hasa
mahali sauti hiyo inapotamkiwa. Kwa kuzingatia sifa hii ya mahali hewa inapozuiliwa,
tunaweza kupata vikundi saba vya konsonanti za Kiswahili kama ifuatavyo:
(i) za midomo: m, p, w, b
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 5 12/11/2019 09:44
6
(ii) za meno: th, dh
(iii) za mdomo na meno: f, v
(iv) za uzi: t, d, n, s, z, l, r
(v) za kaakaa gumu: j, ch, ny, sh, y
(vi) za kaakaa laini: k, g, ng’, gh
(vii) ya koromeo: h
(b) Jinsi hewa inavyozuiliwa
Katika kutamka konsonanti mbalimbali, ala za kutamkia hukutanishwa au kukaribiana
halafu hutenganishwa kwa namna mbalimbali. Konsonanti fulani zinapotamkwa, ala za
kutamkia hukutanishwa, ilhali zipo konsonanti ambazo zinapotamkwa ala za kutamkia
hukaribiana tu bali hazikutani. Ala hizi huweza kutenganishwa kwa ghaa na kutokeza
sauti p, b, t, n.k. au kwa mkwaruzano na kutokeza sauti s, f, v, n.k.
(ch) Hali ya mtetemeko katika nyuzi za sauti
Sifa ya tatu ya kuelezea konsonanti inahusu mtetemeko unaotokea katika nyuzi za sauti.
Kwa mfano tunapotamka sauti p, s au t, hakuna mtetemeko wowote unaotokea kwenye
nyuzi za sauti. Lakini tunapotamka b, z, au d, kunatokea mtetemeko fulani kooni. Ili
kuweza kuthibitisha jambo hili unaweza kuziba masikio kwa viganja vya mikono yako au
kufunika utosi kwa kiganja kisha ujaribu kusema s-s-s-s-s-s halafu z-z-z-z-z-z. Utagundua
kuwa katika matamshi ya kwanza (s), sauti inayotokea ni hafu (hakuna mtetemeko).
Na katika matamshi ya pili (z), sauti inayotokea ni nzito (kuna mtetemeko). Konsonanti
zinazotokeza mtetemeko zinapotamkwa hujulikana kama konsonanti ghuna GH. Nazo
zile ambazo hazitokezi mtetemeko wowote huitwa konsonanti hafu (H) au sighuna.
Kutokana na sifa hizo za kimatamshi (yaani: mahali hewa inapozuiliwa, jinsi hewa
inavyozuiliwa, na hali ya mtetemeko katika nyuzi za sauti), konsonanti za Kiswahili
hugawika katika vikundi saba vifuatavyo:
1. Vipasuo 5. Kimadende
2. Kipasuo - kwamizo 6. Nusu irabu
3. Vikwamizo 7. Kitambaza
4. Nazali
1. Vipasuo
Vipasuo ni konsonanti ambazo zinapotamkwa, ala za kutamkia hukutanishwa halafu
hutenganishwa ghaa. Hivyo panatokea sauti ndogo ya mpasuko. Ndiyo sababu sauti hizi zikaitwa
‘vipasuo. Nazo ni p, b, t, d, j, k na g.
Matamshi
papa tata kuku tini
baba dada gugu jini
2. Vikwamizo
Vikwamizo ni konsonanti ambazo wakati wa kuzitamka, ala za kutamkia hukaribiana, kisha hewa
hupitishwa katikati ya ala hizo hivi kwamba kunatokea sauti ya kukwamizwa. Hii ndiyo sababu
konsonanti hizi zikaitwa vikwamizo. Hizi ndizo konsonanti nyingi zaidi za Kiswahili. Nazo ni
f, v, th, dh, s, z, sh, gh na h.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 6 12/11/2019 09:44
7
Matamshi
mfu thamini sisi shati ___
mvi dhamini zizi habari ghali
3. Kipasuo-kwamizo
Hii ni konsonanti moja pekee ambayo ni ch. Inapotamkwa, bapa la ulimi na kaakaa gumu
hukutanishwa halafu hewa hupitishwa katikati hivi kwamba panatokea sauti ndogo ya mpasuko
ikichanganyika na mkwamizo (hali ya kukwama).
Matamshi
cheza chaza chechemea
4. Nazali/Ving’ong’o
Nazali ni konsonanti ambazo zinapotamkwa, ala za kutamkia hukutanishwa halafu kaakaa laini
pamoja na kidakatonge huziba njia ya kuingilia kwenye chemba cha kinywa (tazama mchoro wa
ala za kutamkia) hivi kwamba hewa nyingi hutokea puani. Nazo ni m, n, ny, na ng’.
Ili kuweza kuthibitisha kuwa hewa hupitia puani katika kuzitamka nazali, unaweza kuziba mianzi
ya pua yako, halafu uzitamke sauti hizo. Utaona kuwa hazitamkiki ipasavyo.
Matamshi
mama nane nyanya ng’ang’ana
5. Kitambaza
Kitambaza ni konsonanti moja ambayo ni (l) na inapotamkwa, ncha ya ulimi hukutanishwa na
uzi, halafu hewa huachiliwa kutokea pembeni mwa ulimi, upande wa kulia na kushoto.
Matamshi l
lalia mlima lalamika kula leta
6. Kimadende
Kimadende ni konsonanti moja ambayo ni (r) na inapotamkwa, ncha ya ulimi hukutanishwa na
uzi, halafu hewa hupitishwa katikati hivi kwamba ncha hii hupigapiga uzi mfululizo.
Matamshi
kura zaraa raha rula reli
7. Nusu irabu/Viyeyusho
Nusu irabu au viyeyusho ni konsonanti mbili pekee ambazo zinapotamkwa, hewa hutoka kwa njia
laini kama kwamba inayeyuka au kama irabu. Ndiyo sababu zikaitwa nusu irabu. Zinapotamkwa,
ala za kutamkia hukaribiana, halafu hewa hupitishwa katikati ya ala hizo kwa utaratibu. Nazo
ni w na y.
Matamshi
wewe yeye yowe wavu wivu
Kwa muhtasari, konsonanti zote za Kiswahili zaweza kuwasilishwa katika jedwali lifuatalo. Jedwali
hili linaonyesha mahali pa kutamkia konsonanti mbalimbali, aina tofauti tofauti za konsonanti
na kama konsonanti hizo ni hafu (H) au ni ghuna (GH).
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 7 12/11/2019 09:44
8
Konsonanti za Kiswahili
Mahali
aina
Midomo
meno
Mdomo Meno Uzi Kaakaa
gumu
Kaakaa
Laini
Koromeo
Vipasuo (H) (Gh) p b t d j k g
Kipasuo - (H) Kwamizo ch
Nazali m n ny ng’
Vikwamizo (H)
(Gh)
f
v
th
dh
s
z
sh
gh
h
Kitambaza l
Kimadende r
Nusu Irabu/Viyeyusho w y
Zoezi
1. Sahihisha maneno yaliyoandikwa vibaya katika kifungu kifuatacho.
Rengo kuu la lugha ni kuwasiliana. Mawaziliano haya yanabaswa kuereweka mocha kwa
mocha bila kuzusha utatanishi wowote.
Mawasiliano huwesa kudokea kwa jia mbili - kwa mazungumso au kwa maandisi. Katika
njia hisi mbiri, kuna mbinu zinazotumika ili kufanikisha mawasiliano. Mbinu senyewe
zinatofautiana. Mbinu zinazotumika katika masungumso ni tofauti na sile zinazotumika
katika maandishi. Tukianza na masungumso, tunawesa kuona binu kadhaa ambaso
hazitumiki katika maandisi.
Imeandikwa upya kutoka Saru Fafanuzi ya Kiswahili, Longhorn, 1999 uk. 199.
2. (a) Taja aina mbili kuu za sauti za Kiswahili.
(b) Eleza kwa ufupi tofauti kuu hasa baina ya aina hizo mbili kuu za sauti.
3. (a) Ni nini tofauti kati ya irabu za mbele na irabu za nyuma?
(b) Taja irabu mbili ambazo hutamkwa midomo ikiwa imeviringwa.
4. Taja vikundi vyovyote vitano vya konsonanti za Kiswahili.
5. Taja sauti mbili za konsonanti za Kiswahili za aina ya vipasuo.
Sauti mwambatano
Sauti mwambatano au vichangamano huundwa kwa kuweka pamoja konsonanti mbili au zaidi, kila
heru huweza kutambulika. Kwa mfano ng, nj, nd, mw, n.k. Baadhi ya wasemaji wana matatizo
ya kutamka konsonanti hizi. Kwa mfano, wengine watasema:
* Ameingia dani ya nyuba.
badala ya
Ameingia ndani ya nyumba.
* Tulienda bali sana.
badala ya
Tulienda mbali sana.
* Tutapitia jia hii.
badala ya
Tutapitia njia hii.
Mifano zaidi
vy - vyakula
sw - swala, swali, swaga
bw - bwaga, bwia
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 8 12/11/2019 09:44
9
Matamshi (kwa kulinganisha na sauti zinazoleta utata)
(a) Ndui ni ugonjwa mbaya.
Adui alitushambulia jana usiku.
(b) Alienda mbali ili asifanye kazi.
Alienda bali hakufanya kazi.
(a) Njozi hiyo iliogofya sana.
Jozi hiyo ya viatu ni yangu.
(b) Mambo yote yalikuwa shwari.
Mambo yote yalikuwa swali.
CH.Saru na matumizi ya lugha
Dhima ya lugha
Katika maisha yetu ya kila siku, tunatumia lugha kwa njia moja au nyingine tangu tuamkapo
hadi tulalapo. Hata hivyo, si wengi wetu tunaojishughulisha na kuchunguza kwa undani maana
na wajibu wa lugha katika maisha yetu. Tunaichukulia kuwa ni kitu cha kimaumbile tu kama
ilivyo milima, mito, misitu na kadhalika. Lakini tukitua kidogo na kujiuliza maisha yangelikuwa
namna gani kama tusingekuwa na lugha, ndipo tunapoweza kuelewa dhima au umuhimu wa
lugha katika maisha yetu.
Lugha hutekeleza wajibu muhimu sana katika jamii. Kwa hakika ni vigumu kukiria jinsi
maisha yanavyoweza kuwa kama binadamu asingekuwa na lugha. Tukijaribu kuwazia shughuli
zote tunazotenda kila siku tukitumia lugha, basi tunaweza kupata mwangaza tosha kuhusu
umuhimu wa lugha katika maisha yetu.
Iwapo binadamu asingekuwa na lugha, bila shaka maisha yake yangekuwa yamejaa mashaka
matupu. Yangekuwa yamezungukwa na migogoro, migongano, kutoelewana, dhiki, mafarakano
na mengine mengi yasiyokuwa na faida kwake hata chembe. Ni kwa kupitia lugha tunapoweza
kushirikiana na kuwasiliana kwa mema au mabaya. Shughuli zote katika ulimwengu huu
tunamoishi - mazuri na mabaya, migogoro na hata vita hutatuliwa kwa kutumia lugha.
Vile vile, binadamu hawezi kuyaelewa mazingira yake asipokuwa na lugha. Ni muhimu
kwa binadamu kuyaelewa mazingira yake ili aweze kuyapanga kwa utaratibu unaofaa na
kuyapambanua vilivyo. Kwa mfano, katika mazingira yetu kunayo miti na mimea mingine
mbalimbali. Tunahitaji kuipa miti na mimea hii majina, iwe ni miembe, mipera, mikarafuu,
mihogo na mingineyo. Kunao pia wanyama ambao tunahitaji kuwabainisha kwa maneno, wawe
ni ngombe, nguruwe, nyati, nyoka, nyangumi na wengine. Miongoni mwa wadudu tuna sisimizi,
viroboto, viwavi, panzi, vipepeo na wengine wengi. Je, kama tusingekuwa na lugha tungewaitaje?
Zaidi ya vitu hivyo, kuna vingine chungu nzima ambavyo vinahitaji kubuniwa majina kama
vile samaki, vyombo mbalimbali vya ukulima, upishi, au jikoni; rangi mbalimbali, nyakati za siku,
sehemu za mwili, vifaa vya dukani, ndege, mavazi, vyakula, afya na usa, magonjwa, maumbo,
matunda, mapambo, siku na miezi, dawa, vyombo vya sayansi na teknolojia na vingine vingi.
Tunahitaji lugha ili kuvibainisha vitu hivyo vyote.
Aidha, maendeleo ya nchi zetu yangeathirika mno. Maendeleo hutokana na mawasiliano
ambayo huwapa watu uwezo wa kubadilishana mawazo. Kwa njia hii watu huanzisha miradi
aina mbalimbali na kuinua uchumi wao binafsi na wa jamii na nchi zao kwa jumla. Bila lugha
ushirikiano kama huu usingewezekana kati ya watu binafsi au hata kati ya nchi na nyingine kwani
unategemea mawasiliano ya kimazungumzo ya moja kwa moja au kwa maandishi. Isitoshe, lugha
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 9 12/11/2019 09:44
10
ndicho chombo cha kimsingi katika kuendeleza taaluma za aina nyingi kama vile elimu, sheria,
ukulima, teknolojia, michezo, utawala, siasa, sayansi na nyinginezo. Hivi ni kusema kuwa lugha
ni kama uhai wa binadamu kimaendeleo. Iwapo haipo, basi maendeleo vilevile hayawezi kuwapo.
Zoezi
Taja na ueleze shughuli tatu zinazotekelezwa na binadamu kwa kutumia lugha.
Vipashio vya lugha
Vipashio vya lugha ni vipengele ambavyo hushirikiana ili kujenga lugha. Katika utaratibu huu,
vipashio vidogo vya lugha huungana na kujenga vipashio vikubwa zaidi. Vipashio hivi ndivyo
nguzo ya lugha na vinapoungana ndipo lugha hujengeka. Katika kiwango cha chini zaidi kuna
sauti. Sauti huungana na kujenga silabi, nazo silabi huungana kujenga neno. Maneno huungana
kujenga sentensi. Tazama mchoro ufuatao:
sentensi
neno
silabi
sauti
Sauti za Kiswahili
Sauti zinazojenga maneno ya Kiswahili hugawika katika makundi mawili: irabu na konsonanti.
Irabu ni jumla ya sauti tano ambazo ni a, e, i, o, na u. Nazo konsonanti ni jumla ya sauti ishirini
na tano ambazo ni b, ch, d, dh, f, g, gh, h, j, k, l, m, n, ny, ng, p, r, s, sh, t, th, v, w, y, z. Kiswahili
hakina sauti q wala x. Tazama jedwali lifuatalo lenye sauti hizi zote pamoja na matamshi na
matumizi yake.
Sauti Matamshi Matumizi Sauti Matamshi Matumizi
a
b
ch
d
dh
e
f
g
gh
h
i
j
k
l
m
aa
be
che
de
dhe
ee
fe
ge
ghe
he
ii
je
ke
le
me
amani
beberu
cheche
deni
dhehebu
eleza
fedha
gereza
ghera
hepa
ingiza
jeraha
kelele
lelewa
meza
n
ng’
ny
o
p
r
s
sh
t
th
u
v
w
y
z
ne
n g ’e
nye
oo
pe
re
se
she
te
the
uu
ve
we
ye
ze
nenepa
kerengende
nyenyekea
okoa
pepea
refa
sema
shehena
tetea
thelathini
ugua
vema
wewe
yeye
zeze
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 10 12/11/2019 09:44
11
Viambishi
Neno ‘kiambishi linatokana na kitenzi ambisha yaani fungamanisha. Kwa hivyo, viambishi ni
viungo vyenye maana ya kisaru ambavyo huambatishwa au hufungamanishwa kwenye mzizi
wa neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali. Mzizi wa neno ni ile sehemu ya neno inayobeba
maana kuu na ambayo haibadiliki bila kupoteza maana ya neno hilo. Tazama maneno haya:
pig-a som-a
ku-pig-a ana-som-a
pig-an-a som-e-a
pig-an-i-a som-esh-a
pig-i-an-a som-e-an-a
Viungo vya maneno vilivyoonyeshwa kwa heru nzito ndivyo mizizi ya maneno hayo. Sehemu
nyingine ni viambishi vinavyotumika kulipa neno maana mbalimbali ya kisaru. Baadhi ya
maana ya kisaru yanayowakilishwa na viambishi katika maneno ya Kiswahili ni kama yafuatayo:
1. Nafsi
Nafsi ni kiambishi au neno linalowakilisha kiumbe mwenye uhai.
Kwa mfano: a-lipika (nafsi ya tatu–umoja) wa-takuja (nafsi ya tatu–wingi)
ni-naomba (nafsi ya kwanza–umoja) tu-meka (nafsi ya kwanza–wingi)
2. Wakati au hali
Kwa mfano: a-me-ondoka (hali timilifu) wa-ta-lima (wakati ujao)
ni-na-soma (wakati uliopo) u-li-shinda (wakati uliopita)
3. Kirejeshi
Kirejeshi ni kiambishi kinachorejelea nomino.
Kwa mfano: ali-ye-kopa kili-cho-potea
lili-lo-ulizwa ina-yo-jengwa
4. Kitendwa/vitendwa
Hiki ni kiambishi kinachowakilisha nomino inayotendwa au kutendewa kitendo.
ana-m-piga nita-vi-leta
anao-u-panda anaye-ya-lima
Tazama jedwali hili la viambishi:
Kitenzi Nafsi Wa k ati Kirejeshi Kitendwa Mzizi Kiishio
aliyempiga a li ye m pig a
tuliowapiga tu li o wa pig a
wanaowapiga wa na o wa pig a
nilivyovipiga ni li vyo vi pig a
unachokipiga u na cho ki pig a
alilolipiga a li lo li pig a
wanaoipiga wa na o i pig a
mlivyovipiga m li vyo vi pig a
ninazozipiga ni na zo zi pig a
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 11 12/11/2019 09:44
12
Aina za viambishi
Maneno ya Kiswahili huweza kuchukua aina mbili za viambishi:
(a) Viambishi awali (b) Viambishi tamati
(i) Viambishi awali
Viambishi awali hutokea mwanzoni mwa neno kabla ya mzizi. Kwa mfano, kutokana na jedwali
lililo hapo juu, viambishi vyote vinavyotokea kabla ya mzizi ni viambishi awali. Mathalan:
a-li-ye-m-pig-a tu-li-o-wa-let-a
wa-na-o-wa-beb-a ni-li-vyo-vi-tup-a
Viambishi awali huweza kutumika kuwakilisha dhana zifuatazo:
1. Nafsi ya umoja na wingi
Kwa mfano:
umoja wingi
ni-nalala tu-nalala
u-nalala m-nalala
a-nalala wa-nalala
2. Nyakati
(i) Wakati uliopo
ni-na-lia u-na-andika
a-na-anguka ni-na-soma
(ii) Wakati uliopita
a-li-lima tu-li-cheza
wa-li-imba ni-li-tulia
(iii) Wakati ujao
a-ta-ondoka tu-ta-lala
ni-ta-kuita u-ta-kimbia
3. Urejeshi
ali-ye-kuja uli-lo-leta
ana-ye-ondoka vitaka-vyo-potea
4. Kitendwa/vitendwa
nita-ku-saidia wali-wa-ongoza
tuta-ku-pita ana-ki-chukua
5. Mahali/wakati
ali-mo-ingia ana-ko-enda
(ii) Viambishi tamati
Viambishi tamati hutokea mwishoni mwa neno baada ya mzizi. Viambishi hivi hutumiwa
kuonyesha:
1. Mahali/wakati
aingia-mo alala-po achezea-ko
2. Rai/himizo/kiishio
nilete-e omb-e-ni som-a
3. Kauli
pig-i-a chez-e-a
twa-li-a pik-ik-a
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 12 12/11/2019 09:44
13
Zoezi
1. Tenganisha maneno yafuatayo katika viambishi vyake mbalimbali: Bainisha viambishi
mbalimbali katika maneno yafuatayo:
(i) nitakuletea (ii) anayelima
(iii) tutaondoka (iv) kimepikika
(v) anasomesha (vi) alitusumbua
(vii) anavyoandika (viii) nitamchagulia
2. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuandika viambishi mwafaka kulingana na kitenzi
ulichopewa.
Kitenzi Nafsi Wa k ati Kirejeshi Kitendwa Mzizi Kiishio
K.m. anaye-
waleta
a na ye wa let a
ninachokileta
unachokileta
waliomleta
anayekuleta
walilolileta
uliyoileta
tulichokileta
aliouleta
D. Kusoma
Ufahamu
Kufahamu ni kulijua jambo na kuweza hata kulieleza vizuri inapokupasa kufanya hivyo. Ufahamu
ni sehemu mojawapo na muhimu katika kujifundisha lugha. Sehemu hii humtayarisha msomaji
kuweza kuelewa na kukizingatia alichokisoma au kukisikia. Kuna aina mbili kuu za ufahamu:
ufahamu wa kusoma na ufahamu wa kusikiliza.
Ufahamu wa aina ya kwanza ni ule ambao umeandikwa, na mwanafunzi hutakiwa kuusoma
kwa makini kabla ya kuyajibu maswali fulani kuuhusu. Ufahamu wa kusikiliza kwa upande
mwingine, ni ule unaosomwa wakati mwanafunzi anasikiliza halafu anaulizwa maswali kuuhusu.
Umuhimu wa ufahamu
(a) Unamwelimisha mwanafunzi kwa kuukuza uwezo wake wa kuelewa na kutafakari au
kukikiria kifungu alichokisoma.
(b) Unasaidia kuukuza na kuuendeleza msamiati na lugha ya mwanafunzi. Kwa kusoma
vifungu vya ufahamu, mwanafunzi anaupanua uwezo wake wa lugha na msamiati.
(ch) Humwongezea msomaji maarifa kuhusu mambo mbalimbali. Kwa mfano, vifungu vya
ufahamu vinavyopatikana katika kitabu hiki vinahusu mambo mbalimbali kama vile
uchafuzi wa mazingira, sayansi na teknolojia, haki za watoto, maadili, n.k.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 13 12/11/2019 09:44
14
(d) Huukuza uwezo wa msomaji wa kuweza kubainisha mambo muhimu na yasiyokuwa
muhimu.
(e) Hutoa taarifa mbalimbali kwa muhtasari na kwa njia yenye msisitizo.
Ufahamu wa kusoma
(a) Ufahamu wa aina hii huzingatia neno, maneno, sentensi, aya na habari nzima inayohusika
katika kifungu unachokisoma.
(b) Ni muhimu kuyaelewa masuala makuu yanayozungumziwa katika kifungu unachokisoma.
(ch) Uelewaji wa lugha na msamiati kama ulivyotumiwa katika kifungu unachokisoma ni
muhimu sana.
Vidokezo muhimu kwa mwanafunzi
1. Soma kifungu ulichopewa kwa mara ya kwanza ili kuzipata hoja muhimu au kuipata
hadithi yenyewe.
2. Soma mara nyingine kuyapata maelezo muhimu katika kifungu hicho.
3. Chunguza maswali uliyopewa. Angalia sehemu za ufahamu zinazohusika kuyajibu.
4. Yasome tena maswali na ujitahidi kuandika majibu yake kwa kutumia lugha yako; usitumie
lugha ile ile ya kifungu cha ufahamu.
5. Hakikisha umeandika majibu yako kwa hati sa inayoweza kusomeka vizuri.
6. Andika majibu yako kwa kutumia sentensi zilizokamilika isipokuwa pale tu unapoeleza
msamiati.
7. Ukiulizwa maana ya maneno kulingana na matumizi kwenye kifungu, hakikisha umejibu
kisahihi na kwa maneno yako mwenyewe ukizingatia mahali na jinsi neno lilivyotumiwa,
wala sio unavyolielewa wewe kikawaida.
Maswali
(a) Taja aina mbili za ufahamu.
(b) Je, kwa nini tunasoma ufahamu?
(ch) Taja hatua za kusoma na kuyajibu maswali ya ufahamu
E. Kuandika
Insha
Insha ni mtungo ambao huundwa kwa mfululizo wa sentensi zilizoandikwa na zinazozungumzia
jambo, tukio au kitu fulani. Insha hupangwa katika mafungu ya sentensi kadhaa zilizowekwa
pamoja. Mafungu haya hujulikana kama aya. Kila aya hubeba wazo fulani ambalo linasaidia
kuijenga insha nzima. Aya mbalimbali zina mchango wa kuukuza mtungo huo hadi ukakamilika.
Insha huwa na muundo ufuatao:
(a) Kichwa au anwani ya insha: Hii inazingatia wazo kuu la insha. Kwa kawaida huandikwa
mwanzoni mwa insha yenyewe. Ni vizuri ikiwa kichwa hiki hakizidi maneno sita kwa
kuzingatia aina ya insha. Kwa mfano kumbukumbu huzidi maneno sita.
(b) Utangulizi au mwanzo: Hii ni sehemu inayotanguliza kwenye jambo linalozungumziwa.
Utangulizi huu huwa aya moja tu na isiyokuwa ndefu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 14 12/11/2019 09:44
15
(ch) Mwili au kiini cha insha: Hii ndiyo sehemu kuu ya insha. Ni katika sehemu hii ambapo
wazo kuu huendelezwa. Mawazo yanapaswa kuunganishwa kwa lugha ya mfululizo na
yenye ufasaha. Sehemu hii huwa na aya kadhaa.
(d) Hitimisho: Hii ndiyo sehemu ya mwisho. Inatoa muhtasari na msisitizo wa jambo
lililozungumziwa. Ikiwa ni insha ya kusimulia kisa au tukio, sehemu hii huonyesha jinsi
kisa au tukio hilo lilivyoisha.
Sifa za insha nzuri
Ina urefu ufaao.
Ina utangulizi unaomvutia msomaji.
Inazingatia kichwa cha habari inayotakiwa.
Imeandikwa kwa utaratibu ufaao.
Imetumia alama za kuakisha kama vituo, ritifaa, viulizo n.k. ifaavyo.
Inatiririka vizuri na kuonyesha mawazo yanavyofuatana.
Ina mpangilio mzuri wa mawazo. Kila wazo limekuzwa katika aya yake na aya zote
zinahusiana.
Yenye lugha fasaha isiyokuwa na makosa ya kisaru, hijai au tahajia.
Yenye mwisho mzuri wa kumteka msomaji.
Mfano















Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 15 12/11/2019 09:44
16




















Zoezi
Andika insha kuhusu kisa au tukio lolote ulilowahi kushuhudia.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 16 12/11/2019 09:44
17
Chemshabongo
Tazama jedwali lifuatalo kisha ujibu swali lililo chini ya jedwali lenyewe.
U B K I P A S U O S P F F Y M I U W V V J M D C M
L Y N B L F P G O I N S H A M T N A Z A L I A A A
I J S X G A R I G C A Z W V S A R C E G A N X R T
M I G I N G H A E W K I M A D E N D E H U Y W L A
I T K U R S K Z D X Y I V R A J P R G H S Y U O M
I D H O I K V N B T O B S M T B H U G Z I T K B S
O G M I A A E A N G H O T U B A L O L L I G A W H
W M K I F T A U I M O S U P M R S L H W D C N B I
U X A J I O L T A M A T I Z C I V Y C C B K U U U
U N Y K O K O N S O N A N T I W S A G B E X S H D
W R D M C I Q F P E Y X E X J O X Z Y O E G H O V
U Z F I O T K J S E O G M Z I Z I U G I F Y I Q P
W U Z Q C E P L N U F I Z I C K I K W A M I Z O J
M R W N F N F K K I R E J E S H I R D Z P W V V A
I W I T D M E U H F H F M F M N A F S I W A Z V Q
O B Q R K L Q K I A M B I S H I D C Z L W Y I Y P
X R I E V I M I R H Q B K Y N D K J W N V R G G T
Tafuta maneno yafuatayo kutoka kwenye jedwali:
HOTUBA MATAMSHI ULIMI KONSONANTI UFIZI GHUNA ISOGHUNA
KIAMBISHI KITENDWA KIREJESHI INSHA UKANUSHI TAMATI MZIZI
KIISHIO NAFSI LUGHA KIPASUO KIMADENDE NAZALI KIKWAMIZO
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 17 12/11/2019 09:44
18
A. Ufahamu
Ielewe lugha yako
Wanafunzi wa Darasa la Nane wa shule ya msingi ya Karuthi walihitaji to za kuumalizia mradi
waliopewa na mwalimu wao wa somo la Zaraa. Wakapewa ruhusa kwenda kuzitafuta. Kisha
wakaelekea katika kichaka kilichokuwa kama kilomita mbili u nusu kutoka shuleni mwao. Kabla
ya kuingia kichakani wakakutana na mtu aliyetimua mbio akitokea huko kichakani. Akawaambia
kwa sauti ya juu huku akihemahema, “Nidiru …rakaha, naku masib…kuho lebem!” Wanafunzi
waliposikia maneno hayo wakashangaa na kuulizana, Ala! Ana nini huyu mzee? Labda kichwa
kimemruka, twendeni zetu!”
Ndipo walipoendelea na safari yao na kuingia kichakani kutafuta to. Lakini mara hiyo
wakasikia mngurumo mkali ukitokea kichakani. Kutupa macho mbele wakaona simba wawili,
jike na dume, pamoja na shibli wao. Vijana wakaduwaa. Wakajaribu kutoroka lakini wapi! Simba
kuona kitoweo chao kinatoweka na huku wana njaa kali, wakawafuata mbio mbio. Mara moja
akili zikawaambia wanafunzi kuwa simba hawezi kupanda mti. Ndipo walipoamua kuiparaga
miti iliyokuwa karibu kwa ustadi wa nyani kuyaokoa maisha yao. Wakiwa juu mitini waliendelea
kupiga kamsa hadi watu waliokuwa makondeni wakawasikia. Wakachukua silaha na kuwafukuza
wale simba.
Kumbe yule mtu alikuwa akiwaonya wanafunzi kuwa kuna simba huko wanakoenda! Laiti
angelizipanga sauti za maneno yake vizuri, wangelielewa kuwa alikuwa akiwaambia, “Rudini
haraka, kuna simba huko mbele!”
Je, lugha ni nini? Lugha ni mpangilio wa sauti za kusemwa zenye kubeba maana. Mpangilio huu
ni lazima uwe umekubaliwa na jamii ya watu inayotumia lugha inayohusika. Hebu tuyafafanue
maelezo hayo vizuri ili tuweze kuelewa kinagaubaga maana ya neno hili ‘lugha.
Tunaposema kuwa lugha ni mpangilio wa sauti, ina maana kuwa lugha hutokana na vipande-
sauti vilivyopangwa kwa njia maalum ili kujenga maneno. Vipande-sauti hivi huitwa vitamkwa.
Katika maandishi, vitamkwa huwakilishwa na heru za alfabeti kama a, e, i, k, m, n.k. Yaani,
Sura ya Pili
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 18 12/11/2019 09:44
19
sauti za lugha hazitokei kishaghalabaghala tu. Hutokea kwa mpango. Zikitokea bila mpango,
kama kwenye kisa tulichosimuliwa hapo juu, basi hapatakuwako na mawasiliano yafaayo.
Ni kutokana na mpangilio huu mahususi wa vitamkwa tunapoweza kuunda maneno
mbalimbali ya lugha. Kwa mfano: kutokana na vitamkwa i, a, na t, tunaweza kuunda maneno ya
Kiswahili kama vile ati, tia, tai, na ita. Kutokana na a, o, na t, tunaweza kuunda maneno toa, ota
na tao. Lakini mpangilio wa vitamkwa hivi usipozingatiwa kwa makini maneno yatakayoundwa
huenda yasiwe na maana yoyote katika lugha ya Kiswahili. Kwa mfano, kutokana na vitamkwa
a, i, na t, hatuwezi kuunda maneno ya Kiswahili kama *iat au *ait. Vile vile, hatuwezi kuunda
maneno *oat au *aot kwa sababu msamiati kama huu hauko kabisa katika lugha ya Kiswahili.
Sababu mojawapo ni kwamba, maneno ya Kiswahili, hasa yale yenye asili ya Kibantu hayaishii
kwa konsonanti. Hata hivyo, katika lugha nyingine, mipangilio kama hii ya sauti hukubalika.
Kwa mfano, lugha kama vile Kiingereza ina maneno mengi yanayoishia kwa konsonanti. Kwa
hivyo, kutokana na vitamkwa vilivyotajwa hapo juu, yaani o, a, na t tunaweza kuunda neno *oat
(yaani shayiri). Neno hili lina maana kamili katika lugha ya Kiingereza ingawa neno lili hili halina
maana yoyote katika Kiswahili ingawa sauti zilizotumika kuliunda ni zile zile.
Tunaposema kuwa lugha ni sauti za kusemwa ina maana kuwa sauti za lugha hutokana na
kutamkwa. Ni mali ya binadamu kwa vile ndiye aliye na uwezo wa kutumia sauti na maneno.
Mawasiliano baina ya wanyama, ndege au wadudu siyo lugha kwa vile viumbe hawa hawana
uwezo wa kuongea kwa kutumia sauti na maneno.
Mtu anapotamka sauti za lugha hutumia viungo mbalimbali vya kutamkia kama vile midomo,
meno, uzi, ulimi na vinginevyo. Viungo hivi huitwa ala za sauti au viungo/ala za kutamkia. Hivi
ni kumaanisha kuwa sauti nyingine zinazotolewa na binadamu kama vile kukohoa, kukoroma,
kupiga chafya, kupiga mbinja, kulia, kucheka na nyingine sio lugha ingawa huweza kuwa na maana
fulani. Ishara pia kama vile kupungia mkono, kukonyeza jicho na nyingine sio lugha kwa vile
ishara hizo hazitumii sauti au maneno.
Maswali
1. Ni kwa nini wanafunzi wa shule ya Karuthi hawakuelewa alichosema yule mtu aliyetokea
kichakani?
2. Unda sentensi tano zenye maneno yenye sauti zilizopangiliwa vibaya kisha uziandike vizuri
ili ziweze kueleweka. Kwa mfano:
Amam akiaa koshe hibusua - Mama ataka kesho asubuhi.
3. Ina maana gani kusema kuwa lugha ni sauti za “kusemwa?
4. Maneno ya lugha hutokana na sauti/vitamkwa vilivyopangwa kwa utaratibu maalum.
Kutokana na sauti a, u, t, ch, i, a, o, p, m, b, z, unda maneno matano ya Kiswahili. k.m.
zao, chui.
5. Tenganisha vitamkwa vya maneno haya: Kwa mfano: cherehani ch-e-r-e-h-a-n-i
(i) kalamu (ii) waziri (iii) gari
(iv) n g ’o m b e (v) shaghalabaghala
6. Eleza maana ya maneno na misemo ifuatayo kulingana na matumizi yake kwenye kifungu:
(i) kuiparaga (ii) ala za sauti (iii) kupiga chafya
(iv) wakaduwaa (v) piga kamsa
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 19 12/11/2019 09:44
20
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi: Kiimbo
Neno ‘kiimbo limetokana na kitenzi ‘imba au ‘kuimba. Kiimbo ni mawimbi ya sauti, yaani jinsi
sauti inavyopanda na kushuka mtu anapoongea. Kwa njia hii hutokeza mikazo fulani kwenye
maongezi ambayo huibua maana halisi ya maneno yanayosemwa.
Kiimbo ni kipengele muhimu katika maongezi. Ni kutokana na kiimbo ambapo maana halisi
ya maneno yanayosemwa huweza kujitokeza vizuri. Kwa mfano: kutokana na mabadiliko ya
kiimbo tunaweza kutofautisha kati ya usemi wa taarifa, usemi halisi, swali, ombi, amri, mshangao,
msisitizo, kejeli, shaka, dharau na mengine. Tazama sentensi zifuatazo:
(a) Sentensi za taarifa:
Ni sentensi ambazo huarifu au hujuza.
(i) Mtoto anaandika barua. (iii) Uvutaji sigara ni hatari kwa afya.
(ii) Mama alipika uji jana. (iv) Wewe utakwenda shambani.
(b) Sentensi za maswali:
Ni sentensi ambazo huhoji au huuliza swali.
(i) Mtoto anaandika nini?
(ii) Mama alipika nini jana?
(iii) Walimu walinunua vitabu vingapi?
(iv) Mbona unamtesa mtoto?
(ch) Sentensi za rai au ombi:
Ni sentensi ambazo hutumika kuombea. Hutoa dhana ya kutaka kusaidiwa katika jambo
fulani.
(i) Nifungulie mlango. (iii) Naomba uwaite wanafunzi.
(ii) Hebu nipikie chakula hiki. (iv) Niongezee tafadhali.
(d) Sentensi za amri:
Ni sentensi ambazo huleta dhana ya lazima au masharti kwa anayeambiwa.
(i) Fungua mlango! (ii) Pika chakula hiki!
(iii) Waite wanafunzi! (iv) Niongezee!
(e) Sentensi za mshangao au kustaajabu:
(i) Lo! Kemunto ameanguka vibaya!
(ii) Masalaale! Nyanya anapika nini sasa!
(iii) Aka! Kwani wewe hula chakula kingi jinsi gani!
(iv) Gari alilonunua jana limeibiwa!
Vikundi hivyo vyote vya sentensi vina viimbo tofauti. Ndiyo sababu maana zake zinatofautiana.
Shadda/Mkazo
Shadda ni mkazo unaowekwa kwenye silabi fulani ya neno ili neno hilo liweze kutokeza maana
yake halisi. Aghalabu, shadda katika lugha ya Kiswahili huwekwa kwenye silabi ya pili kutoka
mwisho wa neno.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 20 12/11/2019 09:44
21
Kwa mfano: linganisha
maneno
ka’lamu
‘meza
Alama ya ritifaa (’) inayotambulisha shadda katika maneno haya, imewekwa mbele ya silabi
yenye mkazo. Hali kadhalika, shadda husaidia kutofautisha maneno yanayofanana kimuundo
lakini yenye maana tofauti. Tazama mifano ifuatayo:
barabara - njia kuu
ba’rabara - sawasawa; shwari; sawa
walakini - lakini; hata hivyo; ingawaje
walakini - dosari; kasoro; ila
Maana ya kila mojawapo ya maneno hayo imetofautishwa tu na mahali shadda inapowekwa.
Katika maneno yenye silabi moja, neno huwekewa shadda iwapo tu neno hilo limetamkwa kwa
msisitizo. Kwa mfano:
1. Mtoto ‘yu mgonjwa. 3. Tunda ‘li sakafuni.
2. Sisi tu wachafu. 4. Chakula ‘ki jikoni.
Zoezi
Onyesha silabi inayowekewa shadda kwenye maneno yafuatayo:
(a) baba (f) shairi
(b) marudio (g) mapenzi
(ch) sentensi (h) kibuyu
(d) karatasi (i) mto
(e) mahindi (j) samahani
CH. Saru na matumizi ya lugha
Kuakisha
Neno kuakisha (au uakishaji) linamaanisha utumiaji wa alama mbalimbali maalum katika
maandishi ili kuweza kuwasiliana na msomaji ifaavyo. Kunazo alama mbalimbali za uakishaji.
Baadhi ya alama hizo ni kama zifuatavyo:
Heru kubwa na ndogo
Heru kubwa hutumika mwanzoni mwa maandishi mbalimbali kama yafuatayo:
1. Nomino za pekee; kwa mfano:
(a) Majina ya watu na vyeo k.m. Peter, Malkia Elizabeth, Dkt. Adhiambo, Mfalme Jeta,
Profesa Kibwana.
(b) Za mahali k.m. Kenya, Kabete, Uganda, Kapenguria, Machakos.
(ch) Za miezi k.m. Januari, Februari, Machi, Aprili.
(d) Za sikukuu k.m. Krismasi, Madaraka, Jamhuri.
(e) Za lugha k.m. Kiswahili, Luganda, Kifaransa.
(f) Za dini k.m. Kikristo, Kiislamu, Kihindu.
(g) Za vitabu k.m. Siku Njema, Adili na Nduguze, Hekaya za Abunuwasi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 21 12/11/2019 09:44
22
(h) Za mitaa k.m. Kariobangi, Jericho, Umoja, Majengo.
(i) Za siku za juma k.m. Jumatatu, Alhamisi, Ijumaa.
(j) Za masomo k.m. Historia, Hisabati, Kiswahili.
2. Mwanzoni mwa sentensi; kwa mfano:
(a) Jana nilikwenda sokoni kununua samaki.
(b) Wezi wawili wamefungwa gerezani.
(ch) Hakuna chakula hata kidogo.
3. Hutumika baada ya alama ya kishangao, na kiulizi.
(a) Mama wee! “Unataka kuniua?”
(b) Unasema nini Mwehu we? Usilete mchezo hapa.
Heru ndogo
Heru ndogo hutumika mwanzoni mwa maandishi yote mengine ambayo si ya pekee, kama vile
mwanzoni mwa maneno yanayotokea katikati ya sentensi. Kwa mfano:
(a) Mimi nitakwenda sokoni.
(b) Jogoo na sungura walipendana.
(ch) Haba na haba hujaza kibaba.
Pia, heru ndogo hutumika mwanzoni mwa nomino zisizo za pekee isipokuwa kama nomino
hizi zimetokea mwanzoni mwa sentensi. K.m. shamba, kikombe, sufuria, kitabu, kalamu, kondoo,
mji, mvulana n.k.
Heru nzito
Heru nzito ni zile zinazoandikwa kwa rangi iliyokolea sana ili kuyafanya maandishi kuonekana
tofauti na mengine yaliyoandikwa kwa njia ya kawaida. Heru nzito hutumika kwa madhumuni
mbalimbali. Wajibu wake mkuu ni kusisitiza au kuyapa umuhimu maandishi fulani. Kwa mfano:
(a) Wakati
a-na-lima a-me-lima a-ta-lima a-nge-lima n.k.
(b) Umoja na wingi
mtoto watoto
mkulima wakulima
mshale mishale
kikapu vikapu
kiatu viatu
(ch) Aina ya neno, kama vile nomino kwenye sentensi; kwa mfano:
(i) Nairobi, na Mombasa ni miji mikubwa mno.
(ii) Kwa nini umenipa chakula kidogo namna hiyo?
(iii) Kiroboto na chawa ni wadudu wa kuchukiza.
(iv) Wazee wale wanahitaji uji.
(v) Jana tulijenga kizimba cha kuku.
Zoezi
1. Andika nomino zifuatazo kwa njia inayofaa:
hassan nairobi kitale isiolo jane
wafula musyoka malkia uganda afrika
ujerumani italia thika eldoret
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 22 12/11/2019 09:44
23
2. Katika kila kimojawapo cha vikundi vifuatavyo vya maneno, ni nomino mbili pekee
zinazofaa kuanzia kwa heru kubwa. Ni zipi hizo?
(a) nguruwe
elizabeth
achieng
nyumba
maradhi
(b) uingereza
maziwa
mti
kisumu
redio
(ch) jana
juzi
jumatatu
asubuhi
ijumaa
3. Akisha tungo zifuatazo:
(a) je, mariamu ameandika barua niliyomwambia?
(b) mimi nilimwona mfalme haile sellasie wa ethiopia.
(ch) mwaka ujao walioba na nafula watatembelea ujerumani, marekani na uingereza.
(d) anwani kwenye barua hiyo ilikuwa:
bw p.s. muthoka
s.l.p. 30001
kisumu
kenya
(e) nelson mandela, aliyekuwa rais wa afrika kusini, alifanya mashauri na mobutu ses-
eseko wa zaire.
(f) katika falaki kuna sayari kadha kama vile zeibaki, sartani, dunia, mirihi na nyingine.
(g) jana tulifundishwa historia na mwalimu kemunto, lakini leo tutafundishwa na mwal-
imu kerubo kwa vile mwalimu kemunto amekwenda keroka kumwona nyakerario.
D. Kusoma
Kusoma kwa kina: Mashairi ya arudhi
Mashairi yalianza kutungwa zamani sana. Mashairi ya mwanzo yalifuata muundo na mpangilio
maalum wa sauti na maneno. Haya yanaitwa mashairi mapokeo au mashairi ya arudhi. Usomaji
wa mashairi ya aina hii hauna budi kuchunguza sifa kadha zinazohusishwa na utungaji wake. Ili
tuweze kuzielewa sifa hizi, hebu tuangalie mfano ufuatao kwanza:
Ukimwi vielelezo, vyake vinoendeleza,
Mtu hasa ni wa mwanzo, yule asojituliza,
Hupata maambukizo, wengine kuwarukiza,
Hiyo njia moja wapo, inosambaza ukimwi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 23 12/11/2019 09:44
24
Damu nayo huchangiya, pasi na kuichunguza,
Yenye vidudu vibaya, mwengine kumuongeza,
Kuona wasaidiya, kumbe wamuangamiza,
Na hilo ni moja wapo, lisambazalo ukimwi.
Shindano kutochemsha, hata na hilo laweza,
Ukimwi kusababisha, kwengine kuukiza,
Kuona wasalimisha, na huku wadidimiza,
Hiyo ni njia ya tatu, kutapakaza ukimwi.
Tuwe nayo tahadhari, hayana kujikimbiza,
Ni ugonjwa wa hatari, waganga wanaeleza,
Tuufate ushauri, ule wa kujituliza,
Hii ndiyo njia bora, kujikinga na ukimwi.
(Haji Gora Haji, Vielezeo, Kimbunga, uk 3-4).
Tukiliangalia shairi hili tunaona lina sifa kadha. Kwanza limepangwa katika mafungu ya
sentensi ambayo huitwa beti (uchache: ubeti). Kila ubeti una mistari minne (mstari mmoja
huitwa mshororo: wingi mishororo). Shairi lenye mistari minne huitwa shairi la unne au tarbia.
Kila mshororo una idadi maalum ya maneno yenye mpigo au silabi. Silabi hizi hujulikana kama
mizani. Kila mshororo katika shairi hili una mizani kumi na sita:
u-ki-mwi vi-e-le-le-zo, vya-ke vi-no-e-nde-le-za = 16.
Kila mshororo umegawika kwenye vipande viwili, cha kwanza huitwa ukwapi na cha pili
huitwa utao. Mwisho wa kila kipande kuna sauti zinazofanana katika mishororo yote mitatu.
Kwenye shairi sauti hizi zimeandikwa kwa heru nzito na hujulikana kama kina (wingi: vina).
Katika shairi la arudhi, mshororo wa kwanza huitwa mwanzo, wa pili mloto, wa tatu mleo, wa
nne kimalizio au kiitikio.
Unaposoma shairi la arudhi, lazima uchunguze muundo huu. Hii ni sehemu ya kile tulichokiita
fani. Ni muhimu pia kujiuliza shairi lina maudhui ya aina gani. Kwa mfano: katika shairi hili
mshairi anazungumzia jinsi ukimwi unavyosambazwa na jinsi ya kujiepusha na ukimwi. Dhamira
ya mwandishi ni kutufahamisha njia za kusambaza ukimwi na jinsi za kujikinga. Ujumbe
wake ni kuwa ukimwi unaweza kusambazwa kwa kutojituliza, kwa kuongezewa damu ambayo
haikuchunguzwa, kutochemsha sindano n.k. Maadili ya shairi hili ni kuwa kufuata ushauri na
kujituliza ndiyo njia bora ya kuepuka ukimwi.
E. Kuandika
Aina za insha
Kuna aina tofauti za insha ambazo hutegemea mtindo na jinsi insha inavyoandikwa. Baadhi
yake ni zifuatazo:
(i) Insha za picha
(ii) Insha za maelezo
(iii) Insha za methali
(iv) Insha za masimulizi
(v) Insha za mdokezo
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 24 12/11/2019 09:44
25
Insha ya picha
Hii ni insha ambapo mwanafunzi anaonyeshwa picha kadha. Picha hizo huonyesha matendo,
mahali au matukio fulani. Inawezekana pakawa na maneno machache hapa na pale. Mwanafunzi
anatakiwa kutunga kisa na kueleza yote yanayotokea kwenye picha alizopewa. Zingatia mambo
haya:
(a) Zichunguze picha kwa makini ili uelewe kinachotendeka katika kila picha.
(b) Jaribu kuwazia anwani ya kisa ambacho kinahusika.
(ch) Unaweza kupanga kila picha kuwa na aya moja.
(d) Unapoandika insha hakikisha kuwa ina mtiririko mzuri kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
(e) Insha iwe inaeleweka na kufungamana na picha na imvutie msomaji.
Sifa za insha nzuri ya picha
(i) Ina kichwa kinachoakiana na picha ulizopewa.
(ii) Ina utaratibu mzuri na imepangwa vizuri; mawazo yanayotiririka kwa namna nzuri.
(iii) Inasomeka na kuunda kisa kinachomvutia msomaji.
(iv) Inaonyesha matumizi mazuri ya lugha, msamiati, methali na misemo.
(v) Inakubalika kwa kuwa imeeleza mambo yote yanayohusiana na picha zilizopo na kwa
namna nzuri.
Zoezi
Andika insha yenye kichwa, ‘Siku yangu ya kwanza katika shule ya upili kutokana na picha
zifuatazo:
(a)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 25 12/11/2019 09:44
26
(b)
(ch)
(d)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 26 12/11/2019 09:44
27
Chemshabongo
Tazama jedwali hili kisha ujibu swali lililo chini yalo.
M K O F Y Y X V M X Q I N N J V T K K R V W G C K
O N F C M U O A H Y Q V C P P Y H F B G M J V W V
Y L A M V T H L F Y A A U N N T A U W P M G L U W
X K D M O S O U I S Y I T Z N Q N R X S Q B L J P
W S W L I D H J A D K I I M B O D R I P A U E Q J
K D M F B M H V K Z F W K T Z E E H N T U G U L N
Q Q I R A J S P V W U E S X J E J D M J I O X C W
N K T Y X A Q H S E N T E N S I M O N L A F Z Z S
A K V C I L Q Z O N S M T Y S G E I K H L O A A K
F V B B L J T G C R E D I Q E L M U C L Q N W A M
K W N A I B M D P Q O B W T M K D U H L Z K L O W
A H H Z Z P N I P E R R W R D W G R O N M F Z C R
X E T S D A R U D H I S O A G W N M J A R A P M W
O U B T X I U B E T I N E V L J V G T Y K N Q R F
P Q P U M J O W R C E Z V J I A X I J M E A M Q E
L F K S B B B G Q H Q B L H S W V O M Q F C U M M
M W U H A M J O L A O X T K K S H A D D A A Z K R
Tafuta maneno yafuatayo kutoka kwenye jedwali:
MLEO KIIMBO RITIFAA ARUDHI
AKIFISHA SENTENSI VITAMKWA MSHORORO
MLOTO SHADDA UBETI MKAZO
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 27 12/11/2019 09:44
28
A. Ufahamu
Fadhila za punda
Rita na Evelyn walikuwa maraki wa chanda na pete kwa muda mrefu. Waliishi katika mtaa
wa Kibokoni jijini Mombasa. Evelyn alikuwa mwanafunzi wa masomo ya uhazili katika chuo
kimoja pale mjini. Naye Rita alifanya kazi ya ukarani papo hapo mjini. Waliishi kidugu katika
chumba kimoja walichopanga pale mtaani.
Ingawa maraki hawa walishirikiana kwa kila njia katika shughuli za upishi, kupiga deki,
kufagia, kufua na kazi nyinginezo za nyumbani, aliyekuwa akitoa msaada mkubwa zaidi ni
Rita. Rita alikuwa na mazoea ya kutunza pesa zake vyema. Aidha alijua maana ya haba na haba
hujaza kibaba. Alijua kuwa Evelyn, kama mwanafunzi, hakuwa na uwezo wa kuyakidhi baadhi
ya mahitaji yake. Alijitolea sabili hata kumnunulia Evelyn nguo, viatu na vitu vingine alivyohitaji.
Mara nyingine ilibidi Rita kulipa kodi ya nyumba peke yake kwa vile mwenzake hangeweza kupata
pesa kwa wakati. Hakuwahi hata siku moja kumkera wala kumtesa Evelyn kwa jinsi yoyote ile.
Fauka ya hayo, hakuwahi kumsemesha vibaya wala kuonyesha dharau kwake. Aliamini kama
wanavyosema watu kuwa dunia rangi rangile, huenda siku moja atahitaji kusaidiwa yeye pia.
Siku kama hiyo atamtegemea Evelyn, mwandani wake.
Evelyn alipomaliza masomo yake alikuwa na bahati ya mtende. Alipata kazi nzuri mara moja
katika kampuni moja ya mafuta hapo hapo jijini. Lakini muda si muda, mambo ya ajabu yalianza
kutokea. Baada ya kupata kazi yenye kipato kizuri, kichwa cha Evelyn kilianza kufura mfano
wa kaimati. Badala ya kumsaidia mwenzake katika kazi za pale nyumbani pamoja na gharama
za maisha, alifuatilia raha za jijini kwa kuamini ule msemo wa ponda raha kufa kwaja. Rita
alipomwuliza alimjibu kwa ukali, Nikusaidie nini? Sasa si kama wakati nilipokuwa mwanafunzi.
Kila mtu ana pesa zake. Ala!”
Rita hakumwelewa tena Evelyn. Isitoshe, alianza kumwibia Rita vitu vyake wakati alipokuwa
hayupo nyumbani. Mara kwa mara Rita aligundua kuwa pesa alizokuwa amecha sehemu fulani
nyumbani zimedokolewa. Alipomwuliza Evelyn alikuja juu, “Unakiri mimi sina pesa? Unadhani
ni wewe tu uliyeajiriwa?” Rita alizidi kushangaa. Muda wote alioishi na kumfadhili raki yake
aliamini kuwa atamlipa mema. “Kumbe fadhila za punda ni mateke?” alijiuliza Rita. Baada ya
muda, uraki wao ulivunjika na Evelyn akahamia mtaa wa Furaha alikoendelea na maisha yake
ya starehe na ureda.
Hata hivyo, mambo yalianza kumwendea mrama Evelyn. Wakubwa wake kazini
hawakupendezwa na jinsi alivyoendesha shughuli zake pale osini. Mara nyingi alika kazini
akiwa amechelewa na kila wakati alitoa vijisababu mbalimbali ambavyo havikumridhisha
yeyote. Aidha, alipokuwa osini hakufanya mengi isipokuwa kutembea kutoka osi hii hadi
nyingine akiwasumbua watu kazini mwao. Mara kwa mara alionekana akisinzia wakati wenzake
walipokuwa wakichapa kazi. Lakini lililowakera zaidi wakuu wa kampuni hiyo ya mafuta ni jambo
fulani lililoanza kutendeka pale. Vitu vya watu vilianza kupoteapotea. Mara mfanyikazi huyu
anapoteza saa yake, mara mwingine anapoteza pesa, mara hiki mara kile. Wakuu walipoyatupa
mawazo yao nyuma wakagundua kuwa mambo haya yalianza kutendeka mara tu alipowasili
Evelyn. Wakaamua kumwekea mtego. Evelyn alishikwa kimasomaso akidokoa mkoba wa
msichana mwenzake. Mkoba huo ulikuwa umeachwa juu ya dawati kimakusudi ili kumvutia
Sura ya Tatu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 28 12/11/2019 09:44
29
Evelyn. Evelyn alifutwa kazi papo hapo. Fauka ya hayo, alitiwa mikononi na kukabidhiwa polisi
waliomtupa korokoroni. Kesho yake Evelyn alikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa kosa
la wizi. Alitozwa faini ya shilingi elfu tano au kifungo cha miezi sita. Hakuwa na pesa zozote
za kulipia faini hii. Akawekwa rumande. Hata raki mmoja hakuwa naye wa kumuauni katika
wakati huo wa majaribu.
Kwa bahati, Rita alisikia kuhusu kadhia hiyo. Hakupoteza muda. Akashika njia moja kwa moja
hadi kituo cha polisi. Mpango ukafanywa na akamlipia Evelyn ile faini. Evelyn alipoachiliwa huru
akashangaa. Yaani nimesamehewa ama nini?” aliuliza. “La. Hujasamehewa. Faini uliyotozwa
imelipwa na msichana yule. Evelyn akageuka na kumwona Rita. Alimtazama kwa muda bila
kujua la kusema. Mwishowe alimsogea kisha wakakaribiana polepole na kukumbatiana. Machozi
yakaanza kumdondoka Evelyn nde! nde! nde! Akalia kilio cha uchungu na soni. Akamwomba
Rita msamaha, Nisamehe, sikujua nililokuwa nikifanya. Nilidhani kuwa baada ya kupata kazi
sitahitaji tena uraki wako. Haya yaliyonipata yamenifunza, alisema kwa masikitiko. “Evelyn,
kijengacho mtu ni utu na tabia, alisema Rita. “Ni kweli raki yangu, alitamka Evelyn, Sasa
nimejitia kwenye shida. Hata kazi yangu nzuri nimeipoteza. Sina mahali pa kuishi. Itabidi
nirudi kijijini kwa baba na mama. Kwaheri raki yangu na asante kwa yote uliyonifanyia. “La!
Hutaondoka. Rita alimwambia kwa dhati, “Tutakwenda nawe nyumbani mwangu tukaishi pamoja
kama zamani. Nitayagharamia mahitaji yako yote hadi utakapopata kazi.
Basi Rita na Evelyn wakaungana tena na kuishi vizuri katika nyumba ile ile mtaani Kibokoni.
Kweli akufaaye kwa dhiki ndiye raki.
Maswali
1. Maisha ya Evelyn na Rita yalikuwaje kabla ya Evelyn kupata kazi?
2. Kutokana na jinsi Rita alivyomtunza Evelyn, unakiri yeye alikuwa ni mtu wa aina gani?
3. Eleza baadhi ya mambo ambayo Rita alimtendea mwenzake.
4. Baada ya kupata kazi Evelyn alikuwa mtu mkarimu. Je, unakubali? Eleza ilivyokuwa.
5. Unakiri ni kwa nini Evelyn alibadilika?
6. Evelyn alipokuwa mwanafunzi hakuwa na tabia ya udokozi. Unakiri ni kwa nini alianza
tabia hiyo baada ya kuajiriwa?
7. Asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu. Methali hii inahusianaje na Evelyn?
8. Akufaaye kwa dhiki ndiye raki. Methali hii inahusianaje na Rita?
9. Kisa hiki kina mafunzo gani kwetu?
10. Eleza maana ya misemo ifuatayo kama ilivyotumika kwenye kifungu:
(a) maraki wa chanda na pete (e) toza faini
(b) enda mrama (f) jitolea sabili
(ch) tia mikononi (g) chapa kazi
(d) weka rumande (h) shika njia
11. Eleza maana ya methali zifuatazo kulingana na matumizi yake kwenye kifungu:
(a) Haba na haba hujaza kibaba. (d) Fadhila za punda ni mateke.
(b) Ponda raha kufa kwaja. (e) Akufaaye kwa dhiki ndiye raki.
(ch) Dunia rangi rangile.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 29 12/11/2019 09:44
30
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi: Utangulizi
Fasihi ni sanaa inayotumia lugha kuwasilisha ujumbe unaomhusu binadamu. Sanaa ni ufundi wa
kuwasilisha mawazo yanayotokana na kira za binadamu. Ufundi huu unaweza kuwasilishwa kwa
michoro, uchongaji, unyanzi n.k. Katika fasihi, ufundi huo huwasilishwa kwa kutumia lugha.
Fasihi hujitokeza kwa masimulizi ya mdomo au kwa maandishi. Fasihi inayowasilishwa kwa njia
ya mdomo hujulikana kama fasihi simulizi. Fasihi inayotegemea maandishi hujulikana kama
fasihi andishi.
Fasihi ina majukumu mbalimbali:
1. Kuelimisha: Kwa kusikiliza masimulizi au kusoma maandishi tunajifunza mambo mengi. Fasihi
huwa na mafunzo mengi au maadili ya tabia nzuri, mwenendo ufaao n.k.
2. Kuburudisha: Tunaweza pia kuitumia fasihi ili kujiburudisha. Tunaweza kusikiliza hadithi
tunazosimuliwa ili kujiburudisha, kuupitisha wakati na kujituliza n.k.
3. Kuelekeza: Kutokana na fasihi wasomaji huelekezwa jinsi ya kuikabili hali fulani.
4. Kuonya na kushauri: Visa vinavyopatikana katika matini za fasihi huweza kutumiwa kuwa
msingi wa kutoa mashauri au kuwaonya binadamu.
5. Kututazamisha mazingira yetu: Fasihi inamhusu binadamu. Inazungumzia mambo
yanayompata na kumzunguka. Kwa njia hii inamfanya binadamu ayatazame mazingira
yake upya na kuona yanayotendeka.
6. Kuukuza uwezo wa kukiri: Fasihi humsaidia msomaji kuukuza uwezo wake wa kuwaza
na kufahamu mambo. Si mambo yote yanayokuwa wazi; wakati mwingine huhitaji akili
kuielewa fasihi.
7. Kuendeleza utamaduni: Tanzu nyingi za fasihi ni ghala ya utamaduni wa jamii.
Fasihi simulizi Fasihi andishi
1. Huwasilishwa kwa njia ya mdomo kutoka
kizazi hadi kingine.
1. Njia yake kuu ya kuwasilishiwa ni kwa
maandishi yaliyomo kitabuni.
2. Huhifadhiwa akilini au katika kumbukumbu
za wanajamii ingawa siku hizi kuna njia
nyingine kama kutumia kanda, video n.k.
2. Njia kuu ya kuhifadhi ni kwa maandishi.
3. Huweza kubadilishwa papo kwa hapo
wakati msimulizi anapowasilisha jukwaani.
3. Maandishi yaliyoandikwa hayabadiliki
isipokuwapale mwandishianapoandikaupya.
4. Hii ni mali ya jamii; hakuna anayeweza
kudai kuwa ni mali yake binafsi.
4. Kitabu cha kifasihi ni mali ya mwandishi
aliyekiandika.
5. Muundo wake aghalabu huwa rahisi na
hufuatika kwa urahisi.
5. Huenda muundo wake ukawa mgumu na
usio rahisi kufuatika.
6. Uzuri wake unategemea ubingwa wa
anayewasilisha jukwaani.
6. Uzuri wake unategemea usanii wa
mwandishi anayehusika.
7. Ni rahisi sifa zake fulani za zamani kupotea
hadithi inapopokezanwa.
7. Hadithi iliyoandikwa inaweza kukaa katika
hali hiyo kwa miaka mingi.
8. Hadhira au wasikilizaji wanaweza kuathiri
jinsi msimulizi anavyoisimulia hadithi yake au
kuwasilisha tanzu fulani.
8. Hadhira au wasomaji hawana mchango wa
moja kwa moja katika fasihi andishi.
9. Mwanzo wake ni kipawa cha usimulizi. 9. Mwanzo wake ni kipawa cha uandishi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 30 12/11/2019 09:44
31
Kwa muhtasari tunaweza kueleza sifa za fasihi simulizi na fasihi andishi kama ifuatavyo:
CH. Saru na matumizi ya lugha
Mpangilio wa sauti katika silabi na maneno
Sauti za irabu huweza kutokea mahali popote katika neno - mwanzoni, katikati au mwishoni.
Huweza kutangulia au kufuatwa na konsonanti yoyote. Mathalan:
anza tilia mbali nyanya ng’oa cheza
Maneno ya Kiswahili huishia kwa irabu. Yale yanayotokana na lugha za kigeni yanayoishia kwa
konsonanti katika lugha zao za kiasili huongezewa irabu mwishoni ili yaambatane na utaratibu
wa maneno ya Kiswahili.
Kwa mfano:
bint (Kiarabu) - binti
kiosk (Kingereza) - kioski
hundir (Kihindi) - hundi
lakh (Kihindi) - laki
shukran (Kiarabu) - shukurani
shirt (Kiingereza) - shati
rushn (Kiajemi) - roshani
kod (Kiajemi) - kodi
du vin (Kifaransa) - divai
Baadhi ya maneno ya asili ya kigeni huweza kuishia kwa konsonanti. Kwa mfano: takriban
maalumabad a n mathalan
Hata hivyo baadhi ya maneno haya huweza pia kuongezewa irabu mwishoni. Mathalan:
maalumu takribani abadanimathalani
Irabu mbili au zaidi za Kiswahili huweza kutokea zikifuatana. Kwa mfano:
aliyeiokoa waliifuta salaala wanaoieua nuia
Konsonanti huweza kutokea katikati ya irabu zozote. Kwa mfano:
mazao tema thelathini udhi
Konsonanti m na n huweza kuambatana na b, d, g, na j na kuunda sauti mwambatano kama vile
mb, nd, nj, na ng. Kwa mfano:
mbali ndani njia nguo
Kwa kawaida konsonanti zinazofanana haziwezi kutokea katika silabi moja isipokuwa kama neno
linalohusika ni la asili ya kigeni. Kwa mfano:
umma shadda
Hata hivyo baadhi ya maneno ya asili ya kigeni yenye heru mbili zinazofanana katika silabi
moja hupoteza heru moja yanapoingia katika lugha ya Kiswahili. Kwa mfano:
hakk (Kiarabu) - haki
oce (Kiingereza) - osi
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 31 12/11/2019 09:44
32
\Maneno ya asili ya kigeni hufuata utaratibu tofauti katika kujenga maneno yake. Kwa mfano:
mpangilio ufuatao unahusu hasa maneno ya asili ya kigeni:
bd - labda kt - nukta sk - deski - daari
rt - masharti
Muundo wa silabi
Silabi ya Kiswahili huweza kuundwa kwa irabu moja pekee, konsonanti moja pekee, au kwa
mwambatano wa konsonanti na irabu. Ifuatayo ni baadhi ya mipangilio ya sauti zinazounda
silabi za maneno ya Kiswahili.
1. Silabi za irabu moja: (I)
oa - o-a ua - u-a (I)+(I)
2. Silabi za konsonanti moja: (K)
labda - la-b-da (K+I) + (K) + (K+I)
thumni - thu-m-ni (K+K+I) + (K) + (K+I)
blanketi - b-la-n-ke-ti (K)+(K+I) + (K) + (K+I)+ (K+I)
3. Silabi za mwambatano wa konsonanti na irabu: (KI)
kamata - ka-ma-ta (K+I)+ (K+I) + (K+I)
wakulima - wa-ku-li-ma (K+I) + (K+I) + (K+I) + (K+I)
karatasi - ka-ra-ta-si (K+I) + (K+I) + (K+I) + (K+I)
4. Silabi za konsonanti mwambatano za heru tatu pamoja na irabu: (KKI)
mbali - mba-li (K+K+I) + (K+I)
ndani - nda-ni (K+K+I) + (K+I)
kunja - ku-nja (K+I) + (K+K+I)
5. Silabi za konsonanti tatu mwambatano pamoja na irabu: (KKKI)
mchwa - m-chwa (K) + (K+ K+ K + I)
chanjwa - cha-njwa (K+I) + (K+ K+ K + I)
mbweha - mbwe-ha (K+K+K+I) + (K+ I)
jangwa - ja-ngwa (K+I) + (K+K+K+ I)
Zoezi
1. (a) Nini tofauti ya maneno ya asili ya kigeni na yale ya asili ya Kiswahili?
(b) Toa mifano minne ya maneno ya asili ya kigeni na ya asili ya Kiswahili.
2. (a) Taja miundo mitano ya silabi ya Kiswahili.
(b) Toa mifano mitatu kwa kila aina ya silabi ya Kiswahili.
(ch) Andika maneno yenye miundo ya silabi zifuatazo:
(i) (K+I) + (K+K+I).
(ii) (K) + (K+I).
(iii) (I) + (I) + (I).
(iv) (K+ I) + (K+ I) + (K+ I)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 32 12/11/2019 09:44
33
Nomino (N)
Nomino ni neno linalotaja mtu, kitu, hali au mahali. Nomino ni neno maarufu sana katika
mawasiliano. Hii ni kwa sababu kila sentensi ni lazima iwe na nomino au kiwakilishi chake. Na
kwa kuwa tunapoongea tunatumia sentensi, basi ni wazi kwamba hatuwezi kuwasiliana vizuri
bila kutumia nomino. Tazama nomino zilivyotumika katika sentensi zifuatazo:
(a) Walioba amekwenda shambani.
(b) Mama na baba wataninunulia kitabu na kalamu.
(ch) Nyumba ya babu imejengwa karibu na mto.
(d) Juzi tulikwenda Kakamega kuwatembelea wanafunzi wa shule ya Mukumu.
(e) Paka na mbwa ni maraki wa binadamu.
Zoezi
1. Andika nomino kumi kumi kwa kila kitu kifuatacho:
(i) watu k.m. Abdillahi
(ii) wanyama k.m. ndovu
(iii) wadudu k.m. kiroboto
(iv) ndege k. m. kasuku
(v) nchi k.m. Kenya
2. Onyesha nomino katika sentensi zifuatazo:
(a) Mbwa anabweka.
(b) Baba anataka kuuza redio anunue runinga.
(ch) Kenneth Kaunda alikuwa rais wa nchi ya Zambia.
(d) Wakulima wamepeleka mazao kiwandani.
(e) Ni makosa kuwatesa wanyama.
(f) Je, umemwona Mwihaki?
(g) Dukani humu mna mkate, maziwa na sukari.
(h) Kwa nini hutaki kununua nyanya na vitunguu?
(i) Batamzinga na batabukini ni ndege wenye nyama tamu.
(j) Brian ataondoka leo usiku.
3. Jaza pengo kwa nomino yoyote mwafaka.
(a) __________ anaendesha lori lakini ___________________ anaendesha basi.
(b) _________ alicheza na wembe ukamkata ___________.
(ch) Hapa porini pana aina tatu za ndege, _______, ______________, na _______.
(d) ___________ alikwea mti ule na akaturushia _________________.
(e) Mwalimu alikwenda dukani akanunua ________________.
(f) Yule ____________ aliimba _____________ mtamu sana.
(g) Haraka haraka haina _____________.
(h) Tafadhali nenda dukani ukaninunulie ______________.
(i) __________, ___________ na ______________ ni wanyama wa kufugwa.
(j) Wezi walipovunja nyumba yetu waliiba __________, ________ na ________.
Kuakisha: Heru za mlazo/italiki
Heru za mlazo au italiki ni zile zinazochapwa kwa namna ambavyo zinaegemea kulia. Hufanya
kazi karibu sawa na heru nzito. Wajibu wake mkuu ni kuzipa uzito au kusisitiza heru, nambari,
neno, kifungu cha maneno au sentensi katika maandishi. Huweza kutumika kwa nia mbalimbali.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 33 12/11/2019 09:44
34
Kwa mfano:
1. Kuonyesha kiambishi; Kwa mfano: cha kurejesha:
ana-ye-kuja
kili-cho-anguka
vitaka-vyo-tupwa
lina-lo-liwa
2. Kuonyesha jina la kitabu:
(a) Hadithi katika Hekaya za Abunuwasi zinavutia sana.
(b) Kitabu kiitwacho Adili na Nduguze kiko wapi?
(ch) Ni nani amewahi kusoma riwaya iitwayo Nyota ya Rehema.
3. Kuonyesha maneno ya kigeni:
(a) Nenda dukani ukaninunulie gazeti la Daily Nation.
(b) Mara nyingi tunahitaji kutumia tu common sense.
(ch) Jana nilimletea baba jarida la Newsweek.
4. Hutumiwa katika maelezo yanayotoa maelekezo. K.m. Usiandike kwenye mistari ya
pambizoni.
5. Kuonyesha maneno yaliyonukuliwa moja kwa moja. K.m. Usivute sigara.
Zoezi
Pigia mstari maneno yanayofaa kuandikwa kwa heru za mlazo katika sentensi zifuatazo:
(a) Mama ameninunulia Kamusi ya Kiswahili Sanifu.
(b) Kwa nini hukusoma Taifa Leo jana?
(ch) Mimi sipendi kula kuon.
(d) Ukitaka anwani ya kampuni hiyo itabidi utazame kwenye Yellow Pages.
D. Kusoma
Kusoma kwa kina: Mashairi huru
Mashairi huru ni mashairi ambayo hayafuati kanuni za utunzi wa mashairi kama vina, mizani
n.k. Pia huitwa mashairi vue. Shairi la aina hii huweza kuwa na idadi tofauti tofauti ya mishororo
katika beti zake. Mashairi haya huwa na beti zenye idadi tofauti ya mishororo. Tunapoyasoma
mashairi huru tunachunguza mpangilio wa mishororo, matumizi ya lugha kama tamathali za
usemi, msamiati, matumizi ya maelezo yanayojenga picha au kutufanya tuikirie hali fulani n.k.
Sifa nyingine ni matumizi ya urudiaji, yaani maneno fulani kurudiwarudiwa n.k. Tuangalie
mfano ufuatao:
Kwa nini?
Ewe
Ndiyo, ewe upitaye majiani,
kwa maringo na kwingi kujishasha.
Unayenitazama kwa chuki kwa sababu,
ya mavazi yangu,
mavazi yaliyochakaa,
mavazi yaliyofukaa,
mavazi ya kifukara.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 34 12/11/2019 09:44
35
Ewe
Ndiyo, ewe unayeniogopa kama tauni,
unionaye na kutimua mbio kwa hofu,
unayeniona na kupiga mkubwa usiahi.
kwa ajili ya sura yangu,
sura yangu iliyoharibika,
sura yangu iliyobadilika,
sura ya kimaskini.
Ewe
Ndiyo, ewe uniashiriaye kwa mbali,
kunionyesha kama mnyama mbuai,
unayeniogopa kunikaribia,
ukayaona jinsi ninavyoishi,
jinsi ninavyoishi maisha yangu,
maisha yangu ya kusikitisha,
maisha yangu yanayotisha,
maisha ya kifakiri.
Umefanya nini?
Umesema nini?
niache maisha duni.
uniitaye mtoto wa mitaani.
Maswali
(a) Je, ni nani anayeongea katika shairi hili?
(b) Ni shida zipi anazopambana nazo mzungumzaji?
(ch) Je, mzungumzaji anauliza nini? Kwa nini?
(d) Onyesha kuwa hili ni shairi huru.
E. Kuandika
Maana na dhima ya utungaji
Kutunga ni kuunda hoja au mawazo fulani kwa kutumia kira na kuyapanga mawazo hayo kwa
utaratibu mzuri na kwa lugha ifaayo. Sababu kuu ya kutunga huwa ni kuwasiliana na mtu au
watu fulani wanaokusudiwa. Utungaji unaweza kuwa na lengo la kuarifu, kujulisha, kufahamisha,
kuelekeza, kuburudisha n.k.
Kuna aina mbili kuu za utungaji: utungaji unaodhamiriwa kutenda au kutekeleza kazi fulani
kama vile kuonya, kuarifu, kufahamisha, kujuza na kutahadharisha; na utungaji unaodhamiriwa
kuelezea kisa cha kubuni tukio, au hali fulani kwa lugha yenye mvuto mkubwa bila ya kuwa na
lengo jingine la ziada. Aina ya kwanza huitwa utungaji wa kiuamilifu ilhali aina ya pili ni utungaji
wa kisanii. Kuna utungaji wa kawaida unaohusu, kwa mfano: uandishi wa insha ambao unaweza
kuwa na sifa fulani za uandishi wa kisanii.
Katika sura hii, hatutaangalia aina hizi mbili za utungaji kwa undani, bali tutaangalia sifa za
utungaji kwa jumla. Je, ni mambo yapi anayotakiwa mwanafunzi kuyazingatia anapojihusisha
na shughuli ya utungaji?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 35 12/11/2019 09:44
36
Lazima kama mtunzi ukifahamu kitu unachotaka kukitunga na kujua kina sifa za aina
gani.
Pana umuhimu wa kuyapanga mawazo yako vizuri kuhakikisha kuwa unachodhamiria
kukitunga au kukieleza kimeelezeka kwa njia ifaayo na kamilifu.
Ikiwa unatoa taarifa fulani, ni muhimu kuhakikisha kuwa maelezo yote muhimu
yanayohitajika yapo.
Lazima lugha unayoitumia iwe na uwezo wa kuuwasilisha ujumbe unaotaka na kwa namna
ifaayo.
Ili uweze kueleweka vizuri, pana umuhimu wa kutumia alama za uakishi vizuri kwa njia
iliyo wazi; lugha sanifu na mpangilio mwafaka wa mawazo. Tazama:
1. Juma aliondoka. Jana alasiri. Hapa pana matatizo ya uakishi, badala yake inapaswa
kuwa: Juma aliondoka jana alasiri.
2. Nilichukua mkuki sime upanga na mshale wangu nikaondoka. Sentensi hii ina makosa
ya kutoweka vituo mahali panapofaa. Inapaswa kuwa: Nilichukua mkuki, sime, upanga
na mshale wangu nikaondoka.
Ikiwa unatunga kisa cha kubuni ni vizuri ukakifungamanisha na mambo
unayoyafahamu. Tunaweza kuelezea mambo tuyajuayo vyema kuliko mambo
tusiyoyajua.
Tumia lugha ambayo msomaji hatatatizika kuielewa au kuupata ujumbe wako.
Kumbuka unapotunga hujitungii, bali unataka kuwasiliana na msomaji mwingine.
Tunga kwa namna inayomwezesha huyo msomaji mwingine kukuelewa bila ya
kujiuliza, ‘Huyu alitaka kusema nini hapa?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 36 12/11/2019 09:44
37
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
S
3
4
A U
5 6
S
7
8
O
9
D
10
N
11
12 13 14
15
I
16
17
I
18
19
A
KULIA
2. Sehemu ya nyumba iliyo nje aghalabu watu hupumuzikia
4. Maskini hana miko
5. Mojawapo ya masomo ya Kiswahili
8. Utamaduni wa kurithishwa kutoka kizazi hadi kizazi
9. Moja kati ya alama za uakishi pia namna ya kulaza
10. Namna ya kuweka mawazo pamoja kwa mtiririko mzuri
13. Moja ya aina za fasihi
15. Ushuru au malipo ya kukodi nyumba au kitu
17. Hawala
18. Duka dogo la kuuza bidhaa mbalimbali
19. Namna ya kushukuru
CHINI
1. Hutumiwa katika maongezi au mawasiliano
3. Saidia
6. Sehemu ya utanzu wa fasihi
8. Insha ya uelekezaji
11. Fanya kuwa na maarifa
12. Aina ya kinywaji
14. Isiyokuwa na kanuni au sheria mahsusi
16. Jukumu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 37 12/11/2019 09:44
38
A. Ufahamu
Hoteli ya vizito
BwaTakuro alifahamika katika idara ya Mauzo na Usambazaji alikofanya kazi. Alikuwa Meneja
wa Mauzo katika kampuni iliyokuwa maarufu sana jijini. Lakini hakujulikana kutokana na nafasi
yake ya kazini bali kutokana na wasifu wake. Alikuwa jamaa aliyependa kujisifusifu sana. Daima
BwaTakuro alipenda kuvaa suti na kufunga tai zilizochukuana vyema na suti zenyewe. Lakini
hakuwa na tabia hii zamani. Wanaomjua kwa karibu wanasema kuwa alianza kuvaa suti mara
tu aliporudi kutoka Uingereza alikoenda kufanya kozi ya kujiendeleza kimaarifa, wenyewe wakiita
kozi ya kujipiga msasa.
BwaTakuro alirudi kutoka Uingereza kajipiga msasa kwelikweli. Aliibwaga chini tabia yake ya
hapo kabla ya kuvaa vitenge na suruali zilizopauka rangi. Viatu vyake vilikuwa tofauti kabisa. Mara
hii alivaa viatu vilivyopigwa rangi na sulu kiasi cha kuwa aina ya vioo. Viatu hivyo vilipatana vyema
na suti zake nzuri zilizokuwa na vifungo vya ajabu. Kazini nako alipandishwa madaraka. Kabla ya
kwenda Uingereza kujipiga msasa alikuwa Naibu Meneja Mauzo. Sasa alipandishwa madaraka na
kuwa Meneja Mauzo mwenyewe.
Pia alipewa gari zuri kazini. Sasa
hakuwa akijiunga na wenzake
tena kung’angaania usafiri wa
matatu saa za asubuhi.
Wakati wa chakula cha
mchana, wafanyikazi wa idara ya
Mauzo na Usambazajiwalikwenda
kula kwenye kioski cha Mzee
Turungi iliyokuwa mkabala na
mahali pao pa kazi. Chakula
kilichoandaliwa hapo kilikuwa
kizuri na bei yake iliwafaa
wote. Hapo zamani BwaTakuro
aliandamana na wenzake kwenda
kwenye kioski hicho kupata
chakula cha mchana. Lakini
alipotoka Uingereza alikuwa mtu mwingine kabisa. Alikuwa kama nyoka aliyejibambua gamba
lake la zamani; sasa hakuwa BwaTakuro yule watu waliyemzoea. La hasha! Alikuwa BwaTakuro
mwingine.
Siku moja mwenzake kazini alimwendea na kumwambia, “BwaTakuro, si leo twende pahali
petu pa kawaida. Bwa’Takuro alimwangalia kupitia juu ya miwani yake. Akamwuliza, “Wapi
huko?” Yule mfanyikazi alikiri labda BwaTakuro alikuwa amesahau mahali walikozoea kula
chakula cha mchana baada ya kuishi Uingereza kwa miezi sita. Si pale tu kwenye kioski chetu
cha kawaida; kwa Mzee Turungi. Pale pale tulipokwenda kila siku. Umesahau mara moja hii
bwana?” alisema mwenzake.
Sura ya Nne
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 38 12/11/2019 09:44
39
BwaTakuro alimpiga jicho tena halafu akaangua kicheko kikubwa. Alicheka mpaka machozi
yakamtoka. Kwa nini unacheka hivyo?” aliuliza mwenzake. “Bwana wee, mimi huko siendi tena.
Siku hizi nimepanda ngazi bwana. Wewe huoni hivyo? Mimi sasa huenda kwenye hoteli ya vizito
kama mimi mwenyewe, alisema BwaTakuro. Yule mwenzake alijiondokea kwenda kujiunga na
wenzake. Alimwacha BwaTakuro aende kwenye hoteli yake ya vizito.
Lakini angepanda juu kipungu hakilii mbinguni. Baada ya miezi kadha, mambo yalianza
kubadilika. Ingawa BwaTakuro alidhani amesoma sana, lakini alisahau kuwa kulikuwa na vijana
wengi waliokuwa wakiyaendeleza masomo ya juu huko ngambo na hata hapa nchini. Walipopata
maarifa ya kutosha walirejea na kushikilia nyadhifa mbalimbali kwenye osi za serikali na
kampuni. Ujuzi wao uliuzidi ule wa BwaTakuro mara kadha. Haikuchukua muda kabla cheo
cha BwaTakuro kunyakuliwa. Sasa akawa Naibu wa Meneja Mauzo. Lakini kabla ya miezi mitatu
kupita mambo yakazidi kumwendea kombo BwaTakuro. Kazi yake ya Naibu wa Meneja Mauzo
nayo ikanyakuliwa na kijana aliyekuwa amepelekwa ngambo kwa masomo na idara hiyo hiyo
ya Mauzo na Usambazaji. Ikabidi BwaTakuro kurejea kwenye kazi yake ya zamani ya ukarani.
Alijaribu juu chini kuishi kama vizito wenzake aliokutana nao katika hoteli zake za kifahari
akashindwa. Alishindwa hata kununua suti nyingine na kubakia na zile zile alizotoka nazo Ulaya.
Zamani alikuwa na mazoea ya kupita kwa wapiga rangi kumpigia viatu rangi na kuvingarisha.
Lakini aliiacha tabia hiyo vilevile.
Hali ilipomharibikia kabisa, BwaTakuro aliacha kwenda hotelini saa saba. Hatua ya kwanza
ilikuwa kuanza kuagiza aletewe chakula osini. Alidai kuwa alikuwa na kazi nyingi. Aliwapa
pesa kidogo za chai waliokubali kumletea. Lakini baada ya muda hakuweza kuendelea na tabia
yake hiyo. Aliwaza la kufanya. ‘Je, nijibebee vyakula vyepesi asubuhi nije kulia osini?’ alijiuliza.
Lakini aliona kuwa watu watamcheka. Alisumbuka mpaka hatimaye akaamua kurudi pale pale
walipokuwa wakienda zamani, yaani kioski ya Mzee Turungi.
Siku ya kwanza aliamua kutumia njia iliyokuwa upande wa nyuma. Alihakikisha kuwa
ametangulia kabla ya wenzake kuka hapo ndipo abugie chakula chake na atokomee kabla wenzake
hawajaingia. Lakini kwa bahati mbaya, wenzake walimkuta hapo hapo. Yule jamaa aliyekuwa
amemuuliza waende kula huko alikuwa wa kwanza kumwona. Alipaaza sauti na kumwambia,
“BwaTakuro karibu tena bwana. Hii ndiyo hoteli ya vizito yenyewe!” Wenzake walicheka kwa
sauti ya juu. BwaTakuro alitahayari. Ni kweli mpanda ngazi hushuka.
Maelezo ya msamiati
bambua : ondoa ngozi ya juu; funua.
piga jicho : tazama; angalia.
panda ngazi : pata maendeleo; pata ukuu; tajirika.
nyadhifa : nafasi za kazi au madaraka.
vizito : wenye mali; matajiri.
tahayari : ona aibu.
Maswali
1. Ina maana gani kusema kuwa BwaTakuro alikuwa amekwenda ngambo ‘kujipiga
msasa?
2. Baada ya kutoka ngambo BwaTakuro alikuwa amebadilisha vipi tabia zake?
3. Eleza alivyovalia BwaTakuro baada ya kutoka ng’ambo.
4. Ni manufaa yapi Bwa’Takuro aliyoyapata kazini baada ya kutoka Uingereza?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 39 12/11/2019 09:44
40
5. Kwa nini unakiri Bwa’Takuro hakutaka kuandamana na wenzake kula chakula kwa Mzee
Turungi?
6. BwaTakuro alipomwambia mwenzake kuwa amepanda ngazi alimaanisha nini?
7. Unakiria ni kwa nini hoteli aliyopenda BwaTakuro ikaitwa ‘vizito’?
8. Eleza jinsi madaraka ya BwaTakuro yalivyoanza kuporomoka.
9. Je hadithi ya BwaTakuro ina mafunzo gani kwetu?
10. Eleza maana ya misemo ifuatayo kama ilivyotumika kwenye kifungu kisha uitumie
katika sentensi:
(a) piga msasa (b) bwaga chini (ch) enda kombo (d) piga sulu
(b) andaa chakula (f) angua kicheko (g) bugia chakula
11. Methali mpanda ngazi hushuka inahusianaje na kisa hiki?
B. Kusikiliza na Kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - p/b
Vitate ni maneno ambayo yanatatiza wakati wa kuyatamka.
Tamka maneno haya:
p b
papa baba
pana bana
pima bima
punda bunda
panda banda
Soma: Vitanza ndimi
Vitanzi ndimi ni maneno au vifungu vya maneno yenye sauti ambazo zinatatiza kutamka (yaani
vitate) hasa kutokana na jinsi sauti zake zinavyokaribiana kimatamshi.
(a) Baba alimbana Mukabana apanue upana wa banda la babu kwani upana wa banda la babu
ulifaa kuwa mpana kama bandari pana iliyopanuliwa hapo Mpanda.
(b) Bunda Mshirikina alichukua bunda la noti akaenda Mabunda kununua punda lakini akiwa
njiani akasikia bundi akahofu bunda lake la noti huenda likambanduka.
(ch) Nilipopanda Mpanda niliona kibanda cha Banda na banda la Panda nikajua nimeka
Mpanda waishipo Banda na Panda.
Isimujamii
Maamkizi na mazungumzo: Utangulizi
Katika maisha yake ya kila siku, binadamu huhusiana na kuingiliana katika shughuli zao. Hatua
ya kwanza ya maingiliano hayo ni maamkizi, yaani kusalimiana na kujuliana hali. Mazungumzo
ni maongezi kati ya mtu mmoja na mwingine au watu wengine. Hii ndiyo njia ya kawaida ya
binadamu kuingiliana na wenzake. Maamkizi na mazungumzo haya yana sifa kadha:
Umri wa wanaohusika: watu wa umri wa chini hutumia aina fulani ya maamkizi
wanapowaamkia watu wazima shikamoo halafu hujibiwa marahaba.
Wakati: Maamkizi ya asubuhi ni tofauti na wakati mwingine. Kwa mfano: asubuhi
tutatumia maamkizi kama: habari za asubuhi, mmeamkaje, sabalkheri n.k.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 40 12/11/2019 09:44
41
Mahusiano: Uhusiano uliopo kati ya watu wanaozungumza unaweza kuwa msingi wa
lugha ya maamkizi pamoja na mazungumzo. Kwa mfano: utawasikia vijana maraki
wakiamkuana, Sasa!” au Sema!” n.k.
Utambulishaji: Maamkizi pia huhusisha kujitambulisha kwa wanaohusika. Kwa
mfano: ikiwa umekutana na mgeni, kujitambulisha ni sifa muhimu katika maamkizi
yoyote yawayo. Mimi ni. . ., Kwa jina naitwa...
Mazungumzo huwa na utaratibu fulani. Kwa mfano: haitakuwa vyema swali la kuji-
tambulisha (jina lako ni nani?) kutangulia salamu (hujambo/ habari yako/ wambaje
n.k.)
Mfano: Maamkizi kati ya majirani
: (M) H  , K
: (K) N, S
: M (A) H K…
: N
: U    (K ) L K  

: J 
: E,     N   .
: K  , . J     
  . N  ;   
 .
: Y  . N       
 . H  
: B
: N, 
: Y, .
: H       .
: S . N. (K . M   
 )
Zoezi
(a) Kwa kurejelea kifungu hiki, taja na ueleze mambo matano yanayoathiri uteuzi wa lugha
inayotumika katika mazungumzo
(b) Eleza umuhimu wa somo la isimujamii
CH. Saru na matumizi ya lugha
Kuakisha/uakishaji
(A) Kitone/kikomo/nukta (.)
Kitone hutumiwa katika maandishi ya aina mbalimbali kama yafuatayo:-
1. Mwishoni mwa sentensi; kwa mfano:
(i) Nitakwenda chuoni kujipiga msasa.
(ii) Juzi tulimtembelea shangazi yetu.
(iii) BwaTakuro alipenda hoteli ya vizito.
(iv) Bi. Mairongi anawafundisha wanafunzi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 41 12/11/2019 09:44
42
(v) Nilipiga viatu vyangu sulu.
(vi) Kesho tutakwenda uwanjani kucheza mpira wa magongo.
(vii) Hassan ameka msikitini.
(viii) Ni vyema kumwamini raki yako.
(ix) Mzee Turungi hupika chai tamu.
(x) Meneja wa Mauzo amekwenda Uingereza.
2. Kuandika maneno kwa kifupi; kwa mfano:
Dkt. Lekarsia (Daktari Lekarsia)
S.L.P. (Sanduku la Posta)
Bi. Karanja (Bibi Karanja)/Binti Karanja).
P.M.L. Kimeto (Peter Martins Lumumba Kimeto)
3. Kutenga fedha - shilingi na senti; kwa mfano:
6.50 - shilingi sita na senti hamsini
12.90 - shilingi kumi na mbili na senti tisini
Baadhi ya watu hutumia mshazari (/) badala ya nukta ili kutenga fedha.
Kwa mfano: 6/50 au 12/90. Hata hivyo njia zote mbili ni sahihi.
4. Hutumiwa kutenga vipimo, saa na dakika na tarehe k.m. mita 2. 55, saa 1.40, tarehe
05.03.2015
(B) Mkato/kipumuo/kituo/koma (,)
Hii ni alama ya kuakisha inayotumika katika mazingira mbalimbali ya kimaandishi kama
yafuatayo:
1. Msomaji anapohitaji kutua; kama ifuatavyo:
(i) Baada ya safari ndefu ya kupanda na kushuka iliyotuchukua saa nane, tulianza kuona
mlima Kilimanjaro.
(ii) Ingawa nilitaka kumsaidia BwaTakuro, hakusikiliza mawaidha yangu.
(iii) Jonathan Murimi, mchezaji aliyeshinda nishani ya dhahabu katika michezo ya Ju-
muiya ya Madola mwaka uliopita, ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu.
2. Kutenganisha maneno kwenye orodha:
(i) Mbuzi, kondoo, ng’ombe, farasi na nguruwe ni wanyama wa kufuga.
(ii) Malaria, malale, kipindupindu, surua na ukambi ni baadhi ya magonjwa mabaya zaidi.
(iii) Maganga alipokwenda sokoni alinunua viazi, sukumawiki, kabeji na ndizi.
3. Kuandika anwani:
Shule ya Mawazo,
S.L.P 3091,
IMANI.
4. Kuonyesha mwanzo au mwisho wa usemi halisi:
(i) Mama akasema, “Hebu nenda sokoni ukanunue samaki.
(ii) Niliporejea kutoka sokoni, baba aliniuliza, Kwa nini umekawia hivyo?”
(iii) Mimi nimechoka, Nafula aliniambia.
5. Baada ya maneno kama ndio, la, asante n.k.
(i) Ndio, nitakuja kesho jioni.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 42 12/11/2019 09:44
43
(ii) La, sitakwenda Mombasa wiki ijayo.
(iii) Asante, sitasahau uliyonitendea.
6. Baada ya kutaja jina la mtu anayepewa habari:
(i) Mheshimiwa, nilimuona mtu huyu mwovu akimpiga mkewe vibaya sana.
(ii) Daktari, mgonjwa wangu amepata nafuu?
(iii) Aisee Cheupe, jana ulimwona Bahati huko sokoni?
7. Baada ya vina vya kati na vya mwisho katika mashairi. Kwa mfano:
(i) Mtu ni kuwa na utu, ndipo akaitwa mtu,
(ii) Ikiwa amekosa utu, huwa kapunguwa kitu,
(iii) Kuheshimiwa ni katu, wanamdharau watu,
(iv) Mwanadamu aso utu, siyo binadamu kitu.
Zoezi
Andika sentensi hizi upya ukitumia heru kubwa, kikomo au mkato panapofaa.
(a) baada ya kutembea kwa mwendo mrefu waigwa aliwasili mjini kakamega
(b) ikiwa utamwona kilonzo siku ya jumapili mwambie nataka anifulie shati tai fulana na
suruali
(ch) nchi za kenya uganda na tanzania zina uelewano mwema uliowekewa msingi na marais
nyerere, kenyatta na obote
(d) wanyama wote ni sawa lakini baadhi yao ni sawa kuliko wengine
(e) kiminza wambua mutuku na nduta ni wanafunzi wa shule ya kaloleni
(f) adolf hitler aliyekuwa mtawala mbaya huko ujerumani aliogopwa sana
(g) nchi za japani ujerumani ufaransa na uingereza zina utajiri mwingi wa viwanda
(h) nyumbani kwa cherono mna makochi meza viti vitanda na mazulia
(i) baada ya lori moja kuanguka huko kibkabus magunia ya mahindi mtama mawele na
maharagwe yalitapakaa kote barabarani
Vivumishi (V)
Vivumishi ni maneno yanayotoa habari zaidi kuhusu nomino au kiwakilishi cha nomino. Kwa
njia hii huzifafanua au kuzivumisha nomino. Tazama sentensi zifuatazo:
(a) Nyumba mpya imejengwa mtaani Kariobangi.
(b) Watoto watundu wamempiga mwanangu.
(ch) Jiwe kubwa limemwangukia ngamia mfupi.
(d) Mkulima shupavu amepewa zawadi.
(e) Kiti kifupi kilinunuliwa jana.
(f) Shule maridadi imejengwa na mwashi hodari.
(g) Kitabu kizuri kinauzwa kwenye duka jipya.
(h) Hapa sebuleni pana meza moja na viti vitano.
(i) Magari meupe yatatumia barabara pana.
(j) Redio hii na runinga ile ni za mwalimu wetu.
Onyesha kivumishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Baba alijenga chumba kidogo.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 43 12/11/2019 09:44
44
(b) Peter ni mwanafunzi mwerevu sana.
(ch) Mti huu una maua mekundu.
(d) Bwana Takaungu ni mtu mkarimu.
(e) Farasi huyu ana mbio sana.
(f) Maria amenunua viatu vyeusi.
(g) Chui ni mnyama mkali ajabu.
(h) Nairobi ni mji mkubwa mno.
(i) Michungwa mirefu imezaa machungwa machungu.
(j) Mto mrefu una maji mengi.
Andika kivumishi mwafaka ili kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) Mwalimu ___________ alitufundisha hisabati.
(b) Ngombe ____________ ametoa maziwa _________.
(ch) Chakula _____________ kililiwa jana kwenye harusi.
(d) Wasichana __________ wanafua nguo ___________.
(e) Daktari ___________ amenipa dawa ____________.
(f) Mbwa _____________ amemuuma kijana ___________.
(g) Matunda ____________ yameletwa na kijana _____________.
(h) Kondoo ______________ atachungwa kesho na wavulana _______.
(i) Viazi _____________ vilipikwa jana.
(j) Kitabu __________ kilisomwa na watoto _________.
D. Kusoma
Kusoma kwa mapana: Magazeti
Magazeti ni machapisho yanayochapishwa ili kueneza na kusambaza habari au taarifa fulani kila
siku nchini. Magazeti huundwa kwa karatasi kubwa na pana zinazowekwa pamoja. Yanatumiwa
kueneza habari muhimu kwa wasomaji, zinazohusiana na maisha yao, mazingira yao, nchi yao,
utamaduni wao, siasa zao, habari za kwingineko (za kimataifa) n.k.
Kwa nini tunayasoma magazeti?
Kujifahamisha mambo mbalimbali: Unaposoma gazeti unajua mambo yanayoendelea
sehemu mbalimbali za ulimwengu.
Kujielimisha: Magazeti huwa na maarifa ambayo humwelimisha msomaji. Kwa mfano: gazeti
huweza kuwa na makala fulani ambayo yanahusu elimu, teknolojia, ajira, maendeleo ya
sayansi, katiba, uvumbuzi, kilimo, biashara n.k. Unapoyasoma makala hayo unajielimisha.
Kujiburudisha: Magazeti huweza pia kuwaburudisha wasomaji. Inawezekana gazeti likawa
na visa vya kufurahisha, michoro ya vibonzo, vichekesho n.k.
Kuupanua ujuzi wetu wa lugha. Kuna magazeti ambayo huwa na makala yanayozungumzia
lugha au msamiati wa lugha. Kwa kuyasoma makala haya, wasomaji wanaupanua uwezo
na upeo wao wa lugha. Pia huwa na fumbo la chemshabongo ambalo huupima uwezo wa
msomaji wa lugha.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 44 12/11/2019 09:44
45
Mfano wa makala kutoka gazetini
Lugha na elimu
Hakuna taifa ulimwenguni ambalo limepiga hatua kiufundi, kisayansi na kiuchumi kwa kutegemea
lugha na utamaduni wa lugha nyingine za kigeni. Hili limethibitika kwa nchi kama vile Japan,
Korea, India na Uchina.
Japan leo imepiga hatua kubwa viwandani na katika sayansi na ufundi kwa kutumia lugha
yao wenyewe. Ujuzi wanaofunzwa watokana na lugha yao wenyewe, ndiposa wamejimudu kutenda
yanayotendwa na mataifa yaliyowatangulia. Korea na Uchina hali kadhalika.
Ni sisi Waafrika tu ndio tumelazimika kupoteza wakati wetu mwingi kwa kujifunza lugha za
kigeni kwanza ndipo tuweze kuelimishwa. Madola makubwa yalitunyanyasa na kutugandamiza
kwa kufaharisha, kutukuza na kuzitia thamani lugha zao na kuzidunisha zetu.
Unapokwenda Ujerumani katika taasisi za elimu kusoma, ni lazima uende ukajifunze
Kijerumani kwa muda wa miezi sita ndipo uruhusiwe kuendelea na masomo yako. Unapokwenda
Ufaransa hali kadhalika. Hili linatupotezea muda wetu mwingi wakati mtu angemaliza masomo
yake haraka.
Kwa mfano, Serikali ya Majimbo ya bara Hindi imezidi kunawiri kitaalamu kwa sababu ya
lugha zinazotumika shuleni. Kila moja kati ya majimbo 25 nchini humo lina lugha inayotumika
rasmi katika asi na hata madarasani. Kwa mfano: Maharashtra -jimbo la Marathi, Gujarati -
jimbo la New Delhi. Hizi ni kati ya lugha ambazo zimedumishwa sana na kuchangia maendeleo
makubwa katika majimbo hayo. La ajabu ni kwamba wanafunzi hutarajiwa kuifahamu lugha yao ya
mama vizuri na baadaye kufundishwa yale yote ambayo ni mageni kwao. Hili limeimarisha ustawi
wa nchi hii kwa kuwa wanafunzi hujivunia ujuzi waliojifunza katika lugha waliyoielewa vizuri.
(Lugha na elimu, makala ya A. H. Njama, Taifa Leo, Septemba, 9, 2002.)
E. Kuandika
Insha za mdokezo
Hii ni aina ya insha ambapo mwandishi hupewa mdokezo fulani. ‘Kudokeza ni kutoa ishara au
dalili ya jambo au kielekezi cha kumwongoza mtu. Katika insha ya aina hii, mwanafunzi hupewa
kielekezi anachotakiwa kukifuata katika kuiandika insha yake. Inawezekana mwanafunzi akapewa
maneno fulani ya kuianzia au kuimalizia hadithi. Kimsingi, hii ni insha ambayo inataka uwezo
mzuri wa kubuni au kutunga kisa kitakachoingiliana na maneno aliyopewa.
Mambo ya kuzingatia:
(a) Chunguza mdokezo ujue unaweza kufungamana na hadithi ya aina gani.
(b) Wazia kisa ambacho kitaingiliana vizuri na mdokezo uliopewa bila ya kuonekana kama
umekilazimisha kisa hicho.
(ch) Hakikisha insha yako itaingiliana vizuri na mdokezo uliopewa kwa upande wa
unayoyazungumzia na hata lugha uitumiayo.
(d) Lazima insha ionyeshe mtiririko mzuri, itumie Kiswahili fasaha na iliyojaa vikolezo vya
utamu wa lugha kama nahau, methali na msamiati.
(e) Unaweza kupanga vidokezo fulani ambavyo utavitumia kama vielekezi vyako wakati wa
kuiandika ile insha.
(f) Chunguza insha uliyoiandika kuhakikisha kuwa pana mpatano mzuri, mtiririko unaofaa
na matumizi ya lugha yanayovutia na kuingiliana vyema na insha yako.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 45 12/11/2019 09:44
46
Mfano



Endelea.






















Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 46 12/11/2019 09:44
47

















Zoezi
Andika insha inayoishia maneno haya . . . aligeuka na kuangalia nyuma alikotoka. Ndimi za moto
zilikuwa bado zikionekana na kumkumbusha janga lililomka.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 47 12/11/2019 09:44
48
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2 3 4
5
A
6
V
7
8
U
9 10
K
11
A
12
13
A
14
15 16
A
17
A
18
A
19
KULIA
3. Hutumiwa mwishoni mwa sentensi
5. Mji mkuu wake ni Beljing.
6. Maneno yenye utata kimatamshi
10. Ufupisho wake ni (V); aina ya neno
11. Ona soni
13. Samaki mkubwa na hatari
15. Mamlaka au cheo
16. Wingi wa taifa
17. Maswali yanayohitaji majibu ili kuchangamsha akili
18. Bila uoga au kutetereka
19. Neno jipya
CHINI
1. Wanaosoma
2. Kwa kufuata utaratibu mwanzo mpaka mwisho
4. Kueneza kote/utapakazaji
7. Tawi la lugha linalochunguza lugha na matumizi yake
8. Kuweka alama za uakisho katika sentensi
9. Hutupasha habari kila siku
10. Tajiri
12. Mzazi wa kiume
14. Mnyama ambaye hutumika katika mashindano ya mbio
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 48 12/11/2019 09:44
49
A. Ufahamu
Chifu Mbuguma na mali ya umma
Mbuguma alikuwa maarufu huko sehemu za kwao kutokana na kiburi chake. Lakini Waswahili
husema mgalla muue na haki umpe. Licha ya kiburi chake hicho, Mbuguma alisika kutokana
na bidii zake za kujiendeleza kimaisha.
Mbuguma alikuwa mfanya biashara katika soko la kwao, kazi aliyoianza baada ya kuuza
maziwa kwa miaka mingi. Siku hizo alikuwa na mazoea ya kwenda kununua maziwa kwenye
shamba la ushirika na kuzunguka kijijini akiyauza kwa baiskeli yake bila kuyajali maneno ya watu.
Watu walipoisikia kengele ya baiskeli walisema kwa sauti, Haya, Mbuguma huyo na maziwa
yake!” Hata hivyo wapo waliolalamika kuwa aliyatohoa maziwa yake kwa maji ili azidishe kipato
chake. Lakini Mbuguma aliendelea na biashara yake. Biashara hii ilikuwa msingi mzuri wa kuishia
kuanzisha kiduka chake cha kwanza. Muda si muda Mbuguma alipanda ngazi na kuwa na duka
kubwa na kipato chake kubadilika sana. Hakuwa tena yule Mbuguma anayeipiga malapa baiskeli
yake kila siku kuchuuza maziwa, bali mtu mwenye kiburi kingi. Isitoshe, alianza tabia nyingine
ya kuwanyanganya washitiri waliokwenda dukani mwake hasa wale wazee na wasiokuwa na
uwezo wa kujitetea kama wanawake na watoto. Watu walichukia sana tabia hii na hata kupiga
ripoti kwa chifu wa eneo hilo lakini hakuna lililofanyika. Mbuguma alikuwa na pesa za kutosha
kumlainisha chifu huyo ili asichukue hatua yoyote au kumsema vibaya katika mikutano yake.
Mbuguma akawa anajigamba kila wakati, “Nani alisema kuna kitu chenye uwezo mkubwa kuliko
pesa ulimwengu huu?”
Watu waliomjua tangu zamani waliifufua historia yake na kusema kuwa Mbuguma alifukuzwa
shuleni akiwa kidato cha pili kutokana na wizi. Huo ndio uliokuwa mwisho wa elimu yake na
Sura ya Tano
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 49 12/11/2019 09:44
50
mwanzo wa biashara yake ya maziwa. Wanakijiji waliendelea kuvilaani vitendo vya Mbuguma
huku naye akiyaendeleza matendo yake pamoja na unyang’anyi mkubwa.
Tabia ya Mbuguma ilikia kilele wakati chifu wa eneo la kwao alipostaafu na Mbuguma
mwenyewe kuteuliwa kuichukua nafasi yake. Zilikuwako tetesi kuwa alikuwa na jamaa fulani
mwenye madaraka makubwa serikalini aliyehakikisha kuwa ameteuliwa kuitwaa nafasi hiyo.
Mbuguma hakubadilika kamwe baada ya kukitwaa cheo cha uchifu; badala yake alikitumia cheo
hicho kujitajirisha zaidi. Alihakikisha kuwa kila alipotaka kuweko na baraza, taarifa za baraza
hizo hazikuenezwa vizuri. Hii ilikuwa mbinu yake ya kuhakikisha mahudhurio yenyewe yalikuwa
mabaya na kwa hivyo kumpa sababu ya kuwatuma askari wake kwenda kuyasomba mali ya watu
kudia ‘kutohudhuria mabaraza ya chifu.
Watu wa kwao waliendelea kulalamika lakini hayo hayakumpiga mshipa Mbuguma. Kila mara
watu walipomwuliza, “Chifu Mbuguma, mbona unawanyanyasa watu na kuchukua mali zao?”
yeye alijibu, “Hii sio mali ya watu, hii ni mali ya umma!” Wakati ukame ulipolivamia eneo hilo
na serikali kutuma msaada wa chakula, Mbuguma aliyachukua magunia yote na kuyatia kwenye
maduka yake. Sasa tayari alikuwa na maduka mawili. Watu walilazimika kukinunua chakula hicho
kutoka humo madukani mwake kwa bei ya juu. Kila alipoulizwa kisa na maana ya unyama huo,
Mbuguma alisema tu, “Hiki si chakula cha mtu; hii ni mali ya umma!”
Hali iliendelea hivi hadi siku moja taarifa ya matendo ya Mbuguma ilipowakia wakuu wake
wa kazi. Wakati huo yule jamaa aliyemtegemea alikuwa amestaafu lakini Mbuguma aliamini
hakumhitaji tena. Alikuwa ameshazoea unyanganyi wake na hadi kudai hadharani kuwa ndege
mkubwa hakamatwi kwa makapi. Wakuu wake kazini walifanya uchunguzi wao baada ya
kukipokea kilio cha watu wa eneo hilo. Siku moja walika askari kanzu kwenye duka lake na
kushuhudia Mbuguma akiwapunja wateja wake.
Mbuguma alitiwa pingu na kuchukuliwa na askari kanzu hao. Wanakijiji walipomwona
akiingizwa kwenye gari la polisi, walipaaza sauti, Chifu Mbuguma, je sasa umekwenda kula
mali ya umma zaidi?” Kijana mmoja alisema kwa sauti, “Jela kuna maharagwe na mahindi;
hiyo Mbuguma ndiyo mali ya umma halisi. Nenda ukaifurahie kabisa! Watu waliokuwa pale
waliangua kicheko kikubwa licha ya uchungu waliokuwa nao kutokana na vitendo vya chifu wao.
Baadaye Mbuguma alikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa kosa la usadi na akafungwa
jela kwa kipindi cha miaka mitano. Kijijini kisa chake kiligeuka wimbo wa kuwakumbusha watu
matokeo ya usadi na kutumia madaraka yao vibaya.
Baada ya Mbuguma kupata makao mapya huko gerezani, maendeleo mengi yalianza
kupatikana pale kijijini na kuifanya sehemu hii kuwa miongoni mwa baadhi ya maeneo
yaliyoendelea zaidi kote wilayani.
Maelezo ya msamiati
aliyatohoa : aliyafanya dhaifu kwa kuongeza maji.
anayeipiga malapa : anayeiendesha baiskeli kwa maringo.
tetesi : uvumi.
hayakumpiga mshipa : hayakumshughulisha; hayakumjalisha.
jigamba : jivuna.
kutwaa : kuchukua; kunyakua.
washitiri : wanunuzi; wateja
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 50 12/11/2019 09:44
51
Maswali
1. Mgalla muue na haki umpe. Methali hii inahusianaje na maisha ya hapo awali ya mzee
Mbuguma?
2. Baada ya kuanza kupata utajiri, tabia za Mbuguma zilibadilika. Eleza maovu aliyoanza
kuwatendea watu.
3. Kwa nini Mbuguma hakuchukuliwa hatua na chifu?
4. Eleza jinsi Mbuguma alivyozidisha unyonyaji wake baada ya kutwaa cheo cha uchifu.
5. Mali ya umma ni mali ya aina gani?
6. Eleza ilivyokuwa hadi Mbuguma akaishia kifungoni.
7. Taarifa hii ina mafunzo gani kwetu?
8. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika kwenye kifungu kisha uyatumie kutungia
sentensi:
(i) muda si muda (ii) kumlainisha
(iii) kuyasomba (iv) amestaafu
(v) akiwapunja (vi) askari kanzu
(vii) tiwa pingu (viii) waliangua kicheko
(x) usadi
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - t/d.
Tamka maneno haya:
t d
tata dada
tua dua
toa doa
tundu dundu
tuma duma
Soma vitanza ndimi vifuatavyo ili kujizoeza matamshi mwafaka ya sauti hizo.
(a) Matata yenye utata ya dadake Tata yalitatuliwa na dadake Tatu.
(b) Tai alitaka kuvaa tai aliyoletewa na dada lakini alipoichukua ile tai akaona dudu kwenye
tai akaitupa hiyo tai akisema hawezi kuvaa tai yenye dudu.
(ch) Siku ya ndoa nilifungua sanduku nikatoa tai isiyo na doa ili nisiyatie madoa kwenye ndoa.
(d) Mtoto mtundu alimchukua dundu akamtupa tunduni kisha akachukua dundu la kubebea
maji akamwingiza dundu mwingine na kulitupa dundu tunduni.
(e) Bwana Tumwa alitumwa dume akakutana na duma aliyedumaa akadhani duma aliyedumaa
si duma kumbe ni duma mkali.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 51 12/11/2019 09:44
52
Fasihi
Vipera vya fasihi simulizi
Fasihi simulizi hugawika katika tanzu au vipera mbalimbali. Ili kuvigawa na kuvipanga vipera
hivyo, inabidi tutegemee sifa mbalimbali. Kwanza, inabidi tuchunguze lugha inayotumiwa kama
ni ya kishairi au inafululiza moja kwa moja kama lugha ya insha, yaani lugha ya nathari. Pili,
tunaangalia kama lugha hiyo inawasilishwa kwetu kama hadithi au kwa njia ya mazungumzo.
Tatu, tunaangalia ule muundo unaohusika na kujiuliza una sifa gani. Kutokana na sifa hizo
mbalimbali tunapata tanzu nne kuu:
Fasihi simulizi
A
hadithi
B
maigizo
C
ushairi
D
semi
hurafa
mazungumzo
michezo ya
kuigiza
ngonjera
mashairi
methali
misemo
vitendawili
nyimbo nahau
hekaya
visasili
mighani
mitanziko
(a) Hadithi
Hutumiwa kuelezea masimulizi ambayo yanatumia lugha inayofanana na ile ya insha,
yaani ya mfululizo. Urefu wa hadithi hutofautiana; kuna baadhi ya hadithi ambazo ni fupi
na nyingine ambazo ni ndefu. Hadithi hizi ni za aina mbalimbali. Hii ina maana kuwa
utanzu wa hadithi huweza kugawika katika vikundi mbalimbali kama vile hurafa, hekaya
n.k. Katika lugha ya Kiswahili, msimulizi aghalabu huianza hadithi kwa maneno yafuatayo:
Huitwa kitangulizi.
Msimulizi: Paukwa au
Msikilizaji: Pakawa Msimulizi: Paukwa!
Msimulizi: Sahani Msikilizaji: Pakawa!
Msikilizaji: Ya mchele... Msimulizi: Kaondokea chanjagaa,
au kajenga nyumba kakaa,
Msimulizi: Hadithi hadithi! mwanangu mwanasiti,
Msikilizaji: Hadithi njoo! kijino kama chikichi,
Msimulizi: Hadithi hadithi! cha kujengea kikuta
Msikilizaji: Hadithi njoo na vilango vya kupita.
Msimulizi: Kaondokea... Hapo zamani za kale ...
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 52 12/11/2019 09:44
53
Mfano wa hadithi
Kuna watu wawili waliogombana sana. Basi wakaamua kwenda mahali palipokuwa na shimo
wakasema maneno yao wakinena: Sisi hatugombani tena, na maneno yetu tunayatia shimoni
ili tupate kuelewana. Siku iliyofuata wakaona mche mdogo umeota pale shimoni walipokuwa.
Mmoja wao akauliza: Mche huu ni wa mti gani? Mwenzake akasema: Mimi pia siujui ni mche
gani. Ule mche ukakaa mpaka ukakua na kuwa mkubwa na kuzaa, wakasema: Ule mche umezaa
sasa. Mmoja akasema: ule si mche, ule ni mti; na mti ule jina lake mgomba, ni ule ugomvi wetu na
matunda yake ndizi ni kule kuelewana kwetu. Mwenzake akasema: naam, sahihi. Ndipo ukawa
mgomba na ndizi.
(b) Maigizo
Neno hili hutumiwa kuelezea chochote kinachowasilishwa kwa njia ya kuigiza. Kuigiza
ni kuiga vitendo fulani anavyofanya mtu. Maigizo huhusisha watu kadha. Maigizo huweza
kuhusisha michezo ya jukwaani, mazungumzo, ngonjera au mashairi ya kujibizana n.k
Maigizo hujumlisha pia mazungumzo. Mazungumzo hapa hutumiwa kuelezea maongezi
baina ya watu wawili au zaidi ambayo yana usanii au ubunifu. Mazungumzo hayo yanaeleza
mambo yanayoihusu jamii katika miktadha tofauti. Mazungumzo yanahusisha vipera
kadha au vingine kama ulumbi (maongezi yanayoonyesha ubingwa, umahiri au ufarisi
fulani), malumbano au majibizano ya utani (yanayosheheni au kujaza mizaha), mawaidha
(ushauri au nasaha kuhusu masuala mbalimbali maishani) n.k.
Mfano wa maigizo:
: Hivi usemavyo ni kweli?
: Kabisa!
: Acha we!
: Ni kweli kabisa. Zile alizodai ni peremende hazikuwa peremende bali dawa za
kulevya.
: Kumbe vile?
: Nikwambie nini tena! Kazitumia akili zikamduru akapita majiani anawasalimu
wanyama na mimea.
: (akichekacheka) Ehh, unachekesha!
: Nachekesha lakini mwenyewe alisikitisha!
(ch) Ushairi
Neno hili hutumiwa kuelezea tungo ambazo hazitumii lugha ya mjazo au ya mfululizo
kama ya insha. Tungo hizi hutumia lugha fupi, ya mkato na iliyopangwa kwa utaratibu
fulani. Utanzu huu unajumlisha vipera vinginevyo kama nyimbo na mashairi.
Mfano:
: Binti yangu nisogeya, nipate kukuambiya,
Umri ulokiya, sasa umeshatimiya,
Tohara umeikiya, nasi ni kufurahiya,
Huu ni utamaduni.
: Hayo unayonambiya, nyuma tumeyaachiya,
Si faida ni hatiya, baba haya nakwambiya,
Hii janga kwa aya, ukeketaji sikiya,
Huu ni umaluuni.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 53 12/11/2019 09:44
54
(d) Semi
Hili ni neno linalotumiwa kuelezea kauli au sentensi fupi zenye maana fulani. Semi ni neno
linalojumlisha vipera vya fasihi simulizi kama vitendawili, methali, misemo na nahau n.k.
Mfano:
(a) Methali: Mpanda ngazi hushuka.
Haraka haraka haina baraka.
(b) Vitendawili: Popoo mbili zavuka mto (macho).
(ch) Nahau: Agizia risasi, piga maji, piga konde, piga mafamba.
Maswali
1. Taja na ueleze vipera vikuu vya fasihi simulizi.
2. Je, tunategemea nini kuvipanga vipera hivyo?
CH. Saru na matumizi ya lugha
Viwakilishi (W)
Kiwakilishi ni neno au kiambishi ambacho huchukua nafasi ya nomino. Kwa njia hii huwakilisha
nomino ambayo yenyewe haikutajwa katika maongezi au maandishi yanayohusika. Tazama
sentensi zifuatazo:
(a) Wale wanataka kulima shamba hili. (f) Niliwapatia.
(b) Wao na sisi tunasaidiana sana. (g) Amechoka.
(ch) Unataka nini wewe? (h) Tulishuhudia.
(d) Hivi na vile vinaweza kutupwa jalalani.
(e) Wangapi wameka?
Zoezi
1. Onyesha viwakilishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Huyu na huyu wamepita mtihani.
(b) Ni nani amechukua kitabu changu?
(ch) Wale wanatakiwa na mwalimu.
(d) Sisi tutaondoka leo jioni.
(e) Nieleze tofauti kati ya hiki na kile.
(f) Mbugoma anataka gani?
(g) Chake kimeliwa na mtoto mla.
(h) Hii ni nini?
(i) Yeye anataka sisi tuandamane na babu hadi mtoni.
(j) Chenyewe kilipikwa jana.
2. Tumia kiwakilishi badala ya nomino iliyoandikwa kwa heru za mlazo.
(a) Jina langu ni Juma. Juma ni furaha yangu kukutana na Kamau, Kipruto na Salome.
Je, Kamau, Kipruto na Salome mna furaha kukutana na Juma?
(b) Naam, Kamau, Kipruto na Salome tuna furaha kuu kukutana na Juma.
(ch) Jana nilikutana na Mariamu. Mariamu alikuwa akinunua matunda.
(d) Watoto wanaozurura mitaani wanahitaji kusaidiwa. Watoto wanapata shida nyingi
huko mitaani.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 54 12/11/2019 09:44
55
Wakati uliopo NA
Wakati uliopo huonyesha kitendo kinachoendelea kutendeka. Kwa mfano:
(a) Mama anapika uji.
(b) Mwalimu anafundisha watoto.
(ch) Ngombe wanakwenda mtoni.
(d) Paka na panya wanachukiana.
(e) Kuku na mwewe wanapigana.
Zoezi
Andika sentensi zifuatazo katika wakati uliopo.
(a) Mimi niliandika barua.
(b) Yeye atakwenda ng’ambo.
(ch) Bi. Mwikali alikwenda Mwingi.
(d) Mama amelala.
(e) Gari litatengenezwa kesho.
(f) Mahindi yalisarishwa kwa lori.
(g) Jogoo wa shamba aliwika mjini.
(h) Waruguru atamsaidia mwanawe.
(i) Wazee hukumbuka.
(j) Kizuri kilijiuza kibaya kilijitembeza.
Kukanusha wakati uliopo kulingana na nafsi
Tazama jedwali lifuatalo:
Umoja Wingi
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nafsi ya kwanza
ninaimba siimbi tunaimba hatuimbi
ninacheza sichezi tunacheza hatuchezi
ninaandika siandiki tunaandika hatuandiki
ninasoma sisomi tunasoma hatusomi
ninahutubu sihutubu tunahutubu hatuhutubu
nafsi ya pili
unaimba huimbi mnaimba hamuimbi
unacheza huchezi mnacheza hamchezi
unaandika huandiki mnaandika hamuandiki
unasoma husomi mnasoma hamsomi
unahutubu huhutubu mnahutubu hamhutubu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 55 12/11/2019 09:44
56
Umoja Wingi
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nafsi ya tatu
anaimba haimbi wanaimba hawaimbi
anacheza hachezi wanacheza hawachezi
anaandika haandiki wanaandika hawaandiki
anasoma hasomi wanasoma hawasomi
anahutubu hahutubu wanahutubu hawahutubu
Zoezi
Kanusha sentensi zifuatazo:
(a) Mama anapika chakula.
(b) Sisi tunaogopa simba.
(ch) Wao wanafagia nyumba.
(d) Nyinyi mtarudi nyumbani.
(e) Ninafundisha wanafunzi wazuri.
(f) Anakwenda kuogelea.
(g) Tunasari leo usiku.
(h) Wananunua mboga na sukumawiki.
(i) Wao wanacheza kandanda.
(j) Sisi tunachora picha.
D. Kusoma
Matumizi ya maktaba
Maktaba ni chumba au jumba lenye mkusanyiko wa vitabu vya kusoma na kuazimwa. Vitabu hivi
huhitajika kwa ajili ya masomo ya kawaida au nyongeza ya usomaji. Kwa mfano unaweza kupata
vitabu vya kila aina kwa ajili ya kusoma kwa ziada. Hivi ni kama vitabu vya kujiburudisha kama
hadithi, vya kuupanua uwezo au ufahamu wako, vya kuuongeza msamiati wako n.k. Maktaba ni
hazina muhimu ya maarifa yanayoikuza na kuiendeleza akili ya binadamu.
Aina za maktaba
Kuna aina kadha za maktaba kutegemea lengo lake, ukubwa wake au mahali zinapopatikana, na
wajibu wake. Aina hizi ni zifuatazo:
1. Maktaba ya darasa
Hii ni maktaba ndogo ya darasa moja na huwa na vitabu vinavyotumiwa na wanafunzi
wa darasa hilo.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 56 12/11/2019 09:44
57
2. Maktaba ya shule
Hii ni kubwa na huwa na vitabu vinavyotumiwa na wanafunzi wa shule nzima. Huwa pia
na sehemu ya kusomea.
3. Maktaba ya taifa
Hii ni maktaba ambayo inatumiwa na watu wote. Maktaba za aina hii hupatikana mijini
na huwafaidi watu wengi. Kwa kawaida huwa na vitabu vingi pamoja na sehemu kubwa
ya kusomea.
4. Maktaba ya kibinafsi
Mtu mmoja huweza kuwa na maktaba ndogo ya vitabu vyake. Kwa kawaida maktaba ya
aina hii huwa ya mtu mmoja tu.
Umuhimu wa maktaba
(i) Ni njia nzuri ya kuyaongeza maarifa yako. Unapata fursa nzuri ya kuupanua ujuzi wako
na ufahamu wako.
(ii) Maktaba inakuwezesha kufaidika kutokana na hazina kubwa ya vitabu na maarifa yaliyomo
vitabuni.
(iii) Ni njia nzuri ya kuhakikisha kuwa umeboresha ufahamu wako wa mambo na masuala
mbalimbali.
(iv) Hukuwezesha kuongeza maarifa au kuuendeleza ufahamu unaotokana na mafunzo
uliyoyapata darasani.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 57 12/11/2019 09:44
58
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2 3
G
4 5
9
U
7
8
A
9
V
10 11
S
12
H
13
14
15 16
I
17
18
S
19
A
20
KULIA
2. Mikogo
6. Kuchukua kwa nguvu kisicho chako
7. Fumba
9. Visa vinavyoeleza asili ya kitu
10. Maovu kama vile kutoa hongo
12. Moja kati ya tanzu za fasihi simulizi
15. Methali, vitendawili, mafumbo n.k
18. Neno linalosimama badala ya nomino
19. Utungo unaotumia maneno machache mateule kuwasilisha ujumbe
20. Kufanya au kutenda kama kitu au mtu afanyavyo
CHINI
1. Hadithi za wanyama 16. Mahali pa kuhifadhi vitabu ili kuvisoma
2. Mahali wafungwa hukaa 14. Kila mwananchi
4. Watu wanaonunua bidhaa au huduma 17. Kipera cha ushairi simulizi
5. Hali ya kuwa chifu
8. Moja kati ya hadithi za kihistoria
11. Kuwacha kazi kwa sababu ya umri au uzee
13. Sawa na fununu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 58 12/11/2019 09:44
59
A. Ufahamu
Kamusi ni kurunzi ya lugha
Kila msomaji wa lugha yoyote huhitaji kuwa na kamusi. Kamusi ni kitabu kinachokusanya
maneno yaliyomo katika lugha fulani na kuyaelezea ili watumiaji waelewe maana zake na
waweze kuyatumia ipasavyo. Bila ya kamusi ni vigumu sana kwa mwanafunzi anayejifundisha
lugha kuimudu lugha hiyo. Mwanafunzi asiyekuwa na kamusi anafanana na mtu anayetapatapa
kwenye giza bila mwangaza wa kummulikia. Anahitaji kurunzi ya kumwelekeza ili apate njia ya
kujinusuru. Kurunzi hiyo ni kamusi. Kwa jumla kamusi yoyote inayolenga watu fulani lazima
iweze kuyatosheleza mahitaji yao.
Zipo kamusi za aina nyingi. Ili kugawa kamusi katika makundi mbalimbali, tunazingatia sifa
fulani. Kwanza tunaangalia walengwa wa kamusi hiyo. Tunajiuliza je, ile kamusi inalenga akina
nani? Je, imeandikwa ili iwafaidi watu wa ngazi gani?
Kwa kuzingatia sifa hii, tunazo aina mbili kuu za kamusi. Aina ya kwanza ni kamusi ya kawaida.
Hii ni kamusi ambayo inawalenga watumiaji wa lugha fulani kwa jumla. Watumiaji hao wanaweza
kuwa wanafunzi, wasomaji wa kawaida, watu wenye ujuzi mpana wa lugha, wasiokuwa na ujuzi
mpana n.k. Mfano wa kamusi za kawaida ni Kamusi ya karne ya 21 (Longhorn), Kamusi ya
Kiswahili Sanifu (TATAKI) au Kamusi Pevu ya Kiswahili (Vide-Muwa). Hizi ni kamusi zinazoweza
kumsaidia mtumiaji yeyote wa lugha ya Kiswahili. Aina ya pili ya kamusi ya kawaida ni kamusi
ya shule. Kwa nini ikaitwa kamusi ya shule? Huitwa hivi kwa sababu huandaliwa mahususi
kuwafaidi wanafunzi katika viwango mbalimbali vya elimu. Kwa mfano: tunaweza kuwa na
kamusi ya shule inayolenga wanafunzi wa shule za msingi, nyingine inayolenga wanafunzi wa
shule za upili na nyingine wanafunzi wa ngazi za juu zaidi kama vile vyuo vya walimu au vyuo
vikuu. Sifa moja ya kamusi za shule ni kuwa zina idadi ndogo ya maneno. Maneno yanayopatikana
katika kamusi hizi huelezwa kwa lugha nyepesi isiyokuwa na ugumu. Huweza pia kuonyesha
mifano ya matumizi ya msamiati unaohusika katika sentensi na labda hata michoro au vibonzo
vya kusaidia kueleweka kwa neno.
Sifa ya pili ya kugawa kamusi ni kwa kuzingatia ukubwa wake. Kwa mfano: zipo kamusi ndogo
ambazo huweza kutiwa mfukoni kwa urahisi. Hizi huitwa kamusi za mfukoni. Licha ya udogo
wake, kamusi hizi huweza kuwa na maneno mengi mno. Lakini maneno hayo huelezwa kwa
ufupi na mara nyingi kwa heru ndogo zilizobana. Kamusi za aina hii huwafaa sana watumiaji
wanaotaka kuangalia maana ya neno haraka haraka na popote walipo au kuangalia jinsi neno
fulani linavyoendelezwa.
Njia ya tatu ya kugawa aina za kamusi ni kwa kuzingatia idadi ya lugha zilizotumika. Zipo
kamusi ambazo hutumia lugha moja tu. Maneno yanayopatikana katika kamusi hizi pamoja
na maelezo yake, huwa katika lugha moja. Hizi huitwa kamusi wahidiya. Kamusi za aina hii
hulenga watumiaji wa lugha hiyo moja. Watumiaji wa kamusi za aina hii huwa na ufahamu wa
lugha hiyo wa kuwawezesha kuyafuata na kuyaelewa maelezo yaliyomo. Aidha, kuna kamusi
zinazochanganya lugha mbili. Hizi hujulikana kama kamusi thaniya. Kamusi za aina hii huwalenga
watumiaji wanaoifahamu lugha moja vizuri kati ya lugha mbili zilizotumiwa kwenye kamusi. Vile
vile huwalenga watu wanaozielewa lugha zote mbili vizuri lakini mara kwa mara wanazihitaji
kamusi thaniya ili kupata tafsiri ya maneno mbalimbali.
Sura ya Sita
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 59 12/11/2019 09:44
60
Maswali
1. Je, kamusi ni nini?
2. Taja sifa tatu zilizotajwa katika kifungu hiki ambazo zinatumika kugawa kamusi katika
makundi mbalimbali.
3. Kamusi ya kawaida ina sifa gani? Toa mifano miwili ya kamusi ya kawaida.
4. Chukua kamusi yoyote ya shule na uichunguze vizuri, kisha utaje mambo mbalimbali
yaliyoonyeshwa kwenye kamusi hii ili kumfaidi mtumiaji.
5. Nikitaka kujua tafsiri ya neno kutoka lugha moja hadi nyingine nitatumia aina gani ya
kamusi?
6. Eleza maana za maneno haya kama yalivyotumika kwenye taarifa kisha uyatungie sentensi:
(i) anayetapatapa (ii) kurunzi
(iii) kuyatosheleza (iv) kamusi ya kawaida
(v) kamusi ya shule (vi) kamusi ya mfukoni
(vii) walengwa (viii) kamusi wahidiya
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - k/g
Tamka maneno haya.
k g
kuku gugu
kuni guni
kuna guna
kenge genge
kesi gesi
Soma vitanza ndimi vifuatavyo ili kujizoeza matamshi sahihi ya sauti hizo.
(a) Kuku wa Magugu alipelekwa gulio akaona gugu la Makuku akaguna akidhani gugu la
Makuku ni kuku na si gugu akasahau kuwa gugu haliwezi kamwe kuwa kuku kwani gugu
na kuku ni vitu tofauti.
(b) Nilipoanza kukuna nazi Muguna aliguna akaniuliza ni kwa nini ninakuna nazi nami
nikaguna na kumwambia kuwa nazi hukunwa.
(ch) Katika kesi kati ya Mwakesi na Mwagesi iliyohusu gesi, Mwakesi alisema kesi ya gesi ni
kesi mbaya kwani kesi zote za gesi hutokana na gesi ya Mwakesi kulipuka na hivyo gesi
hii kusababisha kesi.
Isimujamii
Katika sura ya nne, tulifafanua maana ya isimujamii. Aidha, tulieleza kaida au kanuni zinazotawala
matumizi ya lugha katika miktadha mbalimbali. Kaida hizi huzua au husababisha kuwepo kwa
mitindo mbalimbali ya lugha katika miktadha tofauti. Huu ndio msingi wa tulichokieleza kama
sajili. Sajili au rejista ni matumizi ya lugha kutegemea muktadha. Kuna sajili mbalimbali kama
sajili ya mazungumzo, sajili ya biashara, sajili ya nyumbani, sajili ya osini, sajili ya michezoni,
sajili ya bungeni, sajili ya sokoni, sajili ya hospitalini n.k.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 60 12/11/2019 09:44
61
Lugha ya nyumbani au sajili ya nyumbani
Lugha ya nyumbani itategemea wanaohusika ni nani. Kwa mfano, mazungumzo au maongezi
yanaweza kuwepo baina ya mzazi na mwanawe, mtu na ndugu yake n.k. Lugha inayotumiwa
itategemea wanaohusika ni nani. Kwa mfano, mzazi na mwanawe hawazungumzi kwa namna
sawa na dada na dada au dada na kaka n.k. Hata hivyo, kuna sifa za jumla zinazotambulisha sajili
au lugha ya nyumbani. Miongoni mwa hizi ni:
(a) msamiati mwepesi: Lugha inayotumiwa katika muktadha huu huwa haina msamiati mgumu
kwa kuwa lengo kuu ni kuwasiliana
(b) matumizi ya lakabu au majina ambayo si rasmi. Ni sifa ya kawaida kwa mzazi au ndugu
kuitana kwa kutumia lakabu au majina yasiyokuwa rasmi kutokana na kuwa na uhusiano
wa karibu sana
(ch) matumizi ya maneno ya mkato na lugha isiyokuwa na maelezo marefu. Wazungumzaji
hujuana na aghalabu huongea katika muktadha unaoeleweka na kila mmoja wao. Hali hii
inaweza kusababisha kuwepo kwa matumizi ya lugha ya mkato na maelezo mafupi tu
(d) kukatizana usemi. Mzungumzaji anayeongea anaweza kukatizwa au kukatwa kauli na
mwenzake ili kujibu au kujaliza hoja au neno fulani. Kukatizana huwepo katika lugha hii
kwa sababu hii si lugha rasmi
(e) matumizi ya vihisishi. Si ajabu kuona matumizi ya maneno yanayoonyesha hisia kali kama
vile Ahaaa!, ‘La!’ ‘Hapana’! ‘Ehhh!’ Kabisa!’ Si ndiyo hayo!’ Shabash!’ n.k.
(f) matumizi ya viziada lugha. Viziadalugha ni mbinu ambazo si za lugha ambazo hutumiwa
kurahisisha mazungumzo. Mbinu hizi ni kama ishara za mikono, ishara za uso, miondoko
ya mwili, kukonyeza kwa jicho, kuashiria kwa vidole au mdomo, kushika sehemu
Soma kifungu kifuatacho na ujibu maswali uliyoulizwa
(Nyumbani. Mama anaonekana chumbani akishughulika hapa na pale. Mwiro anatokeza upande
mmoja akikicha macho yake)
: H  
: N. M     
: M… (A tumbo lake) N  .
: U 
: N .
: S    
: L    …
: N    .
: M…J,  
: K  S        
   . U    .
: M….
: K   . (M   .
M  )
Zoezi
(a) Kwa kurejelea kifungu ulichosoma, eleza sifa za sajili hii.
(b) Eleza sifa zinazoongoza matumizi ya lugha katika muktadha huu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 61 12/11/2019 09:44
62
CH. Saru na matumizi ya lugha
Vitenzi (T)
Vitenzi ni maneno yanayoeleza kuhusu jambo linalotendwa. Jambo hilo linahusisha nomino au
kiwakilishi chake. Kwa mfano:
(a) Mlama anakwenda sokoni.
(b) Mzee atatembea kwa mkongojo.
(ch) Otieno amechukua mpira.
(d) Kawewa atawaongoza wafanyakazi.
(e) Wavuvi walinasa samaki wengi.
(f) Wachezaji walikwenda uwanjani.
(g) Kuku atataga mayai.
(h) Chama kizuri kimeundwa.
(i) Kalimbi anachora picha.
(j) Kamau alinunua ngamia wawili.
Onyesha vitenzi katika sentensi zifuatazo.
(a) Kimanzi anatumia tarakilishi.
(b) Muthee alipita mtihani.
(ch) Wadudu watamuuma mtoto.
(d) Mti umeanguka.
(e) Rosalia anaigiza mchezo jukwaani.
(f) Mwalimu mkuu alituhutubia.
(g) Kuku ametaga mayai.
(h) Tausi ameruka angani.
(i) Viatu vyangu vimepotea.
Wakati uliopita - LI
Huonyesha kuwa kitendo kilitendeka. Huwakilishwa kwa kiambishi LI. Kwa mfano:
(a) Ngiri alimuuma mwindaji.
(b) Kioko alikwenda Taveta.
(ch) Auma alichimba mtaro.
(d) Mimi nilimsaidia Mwongera.
(e) Shule ilifungwa jana jioni.
Zoezi
Geuza sentensi zifuatazo ili ziwe katika wakati uliopita.
(a) Wewe unatakiwa na mwalimu mkuu.
(b) Nyinyi mtatumwa dukani.
(ch) Jogoo anawika.
(d) Daktari amempa Mwikali dawa.
(e) Maimu atawapa kuku chakula.
(f) Wanafunzi husoma kwa bidii.
(g) Nitakula matunda.
(h) Nyanya na shangazi wamesari kwenda Kapenguria.
(i) Mutuku anakataa kwenda shuleni.
(j) Yeye amechoka.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 62 12/11/2019 09:44
63
Kukanusha wakati uliopita kulingana na nafsi
Tazama jedwali lifuatalo:
Umoja Wingi
nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nilivuka sikuvuka tulivuka hatukuvuka
niliimba sikuimba
tuliimba hatukuimba
nilisoma sikusoma
tulisoma hatukusoma
nilitubu sikutubu tulitubu hatukutubu
nilikana sikukana
tulikana hatukukana
nafsi ya pili
ulivuka hukuvuka mlivuka hamkuvuka
uliimba hukuimba
mliimba hamkuimba
ulisoma hukusoma
mlisoma hamkusoma
ulitubu hukutubu mlitubu hamkutubu
ulikana hukukana
mlikana hamkukana
nafsi ya tatu
alivuka hakuvuka walivuka hawakuvuka
aliimba hakuimba
waliimba hawakuimba
alisoma hakusoma
walisoma hawakusoma
alitubu hakutubu walitubu hawakutubu
alikana hakukana
walikana hawakukana
Zoezi
Kanusha sentensi zifuatazo:
(a) Niliandika.
(b) Watoto walisimuliana hadithi.
(ch) Jeremia alichunga ng’ombe.
(d) Wazazi wangu waliniletea zawadi.
(e) Karatasi zilichomeka.
(f) Kitabu kiliandikwa mwaka jana.
(g) Kuku alitaga yai.
(h) Farasi alikimbia.
(i) Shangazi Naomi alifuga batabukini.
(j) Mizengwe alipoteza runinga yake.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 63 12/11/2019 09:44
64
D. Kusoma
Mambo muhimu ya kujua kuhusiana na maktaba
Haiwezekani kufaidika kutokana na maktaba bila ya kuzijua kanuni zake. Maktaba huwa na
vitabu vingi na vizuri, lakini haviwezi kumfaidi mtu asiyejua jinsi maktaba yenyewe ilivyo au
jinsi vitabu hivyo vilivyopangiliwa. Mtumiaji mzuri wa maktaba ni yule anayezifahamu kanuni
na sifa kadha kuihusu maktaba.
(i) Maktaba nyingi huwa na vitabu vinavyoweza kuazimwa na vingine visivyoweza kuazimwa.
Hivi visivyoweza kuazimwa hujulikana kama vitabu vya rejea/marejeleo. Hivi ni kama
kamusi na vitabu vya ramani. Vitabu vya aina hii huhitajika kwa muda mfupi na mtumiaji
huweza kuvitumia akiwa maktabani tu. Vitabu vinavyoazimwa huwekwa kwenye makundi
mapana: vya hadithi na visivyokuwa vya hadithi.
(ii) Vitabu visivyokuwa vya hadithi hupangwa maktabani kwa kutegemea somo linalohusika.
(iii) Vitabu vilivyoko maktabani hupewa nambari za kuvitambulisha. Kwa kawaida nambari
hizi hutegemea mfumo maalum. Huu unajulikana kama mfumo wa kidesimali wa Dewey.
Huu ni mfumo unaotumiwa katika nchi nyingi ikiwemo Kenya. Mfumo huu hutumia
makundi kumi yanayotumia tarakimu kuanzia 0 mpaka 9. Kila kundi huwa na idadi mia
moja. Makundi hayo ni:
000 Vitabu visivyokuwa maalum (000- 099)
100 Falsafa (100- 199)
200 Dini (200-299)
300 Sayansi ya kijamii (300-399)
400 Lugha (400- 499)
500 Sayansi (menyu) (500- 599)
600 Teknolojia (600- 699)
700 Sanaa (700- 799)
800 Fasihi (800- 899)
900 Historia, Jiograa, Wasifu (900- 999)
Kamusi zinapatikana chini ya kundi la 400 kwa sababu zinahusiana na lugha. Hata hivyo,
kamusi maalum kama zile za ensaiklopidia, hupatikana chini ya 000. Vitabu vya hisabati
vitakuwa chini ya 500 (kwa sababu ni Sayansi Menyu). Mfumo huu wa upangaji vitabu
unawezesha kuwapo na utaratibu mzuri. Ikiwa kuna aina ndogo ndogo zinazopatikana
chini ya kundi fulani huwepo matumizi ya nukta. Kwa mfano:
796. Riadha, michezo ya ndani na nje
796. 3 Michezo ya mipira ya nje
796. 3.2 Mpira wa vikapu, netiboli, mpira wa mikono
796. 3.3 Kandanda
(iv) Maktaba huwa na vielekezi vya kumsaidia mtumiaji kujua kilipo kitabu anachotaka.
Hapo awali maktaba zilitumia utaratibu wa kadi kama njia ya kumwelekeza mtumiaji
kupata kitabu fulani. Ingawa utaratibu huu unaweza bado kupatikana katika baadhi ya
maktaba, siku hizi pana mwelekeo mkubwa wa kutumia tarakilishi. Hili linatokana na
maendeleo ya kiteknolojia. Matumizi ya tarakilishi yanarahisisha utafutaji wa vitabu.
Tarakilishi hiyo huhifadhi data au maelezo muhimu kuhusu vitabu vilivyo kwenye maktaba
inayohusika. Anayetafuka kitabu kwa njia hii, anaweza kutumia vigezo kama vile jina la
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 64 12/11/2019 09:44
65
mtunzi au mwandishi, mada za kitabu, anwani za vitabu. Akishapata habari kuhusu kitabu
anachotafuta ambapo ni pamoja na nambari ya usajili ya kitabu chenyewe anaweza kwenda
kwenye sehemu mahsusi ya maktaba kukitafuta. Katika maktaba nyingine za kisasa huenda
pakawa na chumba mahsusi ambapo mtumiaji anaruhusiwa kukaa na kukisoma kitabu
fulani kwa njia ya tarakilishi ikiwa kitabu chenyewe hakikuchapishwa kama kitabu cha
kuazima. Hili hutokea pale ambapo pana vitabu-elektroniki, yaani vitabu vinavyoweza tu
kusomwa kwa njia ya kielektroniki. Siku hizi kuna vifaa maalum vinavyotumiwa kusomea
vitabu vya aina hiyo.
Zoezi
Eleza utaratibu wa kupanga vitabu maktabani.
E. Kuandika
Utungaji wa kisanii: Utangulizi
Huu ni utungaji au uandishi ambao ni wa kisanaa. Sanaa ni ufundi na urembo unaotokana na jinsi
kitu fulani kinavyowasilishwa. Urembo na ufundi huo ni jinsi lugha inavyotumiwa. Hapa lugha
inatumiwa kutungia kisa, hadithi au shairi lenye ujumbe fulani na lenye mvuto kwa msomaji.
Msomaji anapata hamu kutokana na lugha iliyotumika.
Sifa za utungaji wa kisanii
Uandishi huu una sifa kadha muhimu; yaani unapotaka kuandika kisa fulani lazima uzingatie
mambo muhimu yafuatayo:
1. Kiwazie vizuri kisa unachokiandika.
2. Hakikisha kuwa mawazo yako yamepangika vizuri.
3. Hakikisha kuwa kisa unachotunga kina mtiririko mzuri na kinaweza kumvutia msomaji
kuanzia mwanzo hadi mwisho.
4. Hati yako inapaswa kusomeka kwa urahisi; hakikisha umeandika vyema.
5. Tumia alama zifaazo za uakishi ili maana iweze kutokea kwa njia nzuri.
6. Zingatia matumizi yafaayo ya Kiswahili sanifu pamoja na mpangilio fasaha wa mawazo
yenyewe.
7. Hakikisha kuwa kisa unachotunga kinaweza kumvutia msomaji. Kipange kwa namna
inayomfanya msomaji apende kuendelea kusoma.
8. Ni muhimu kutumia misemo, nahau na methali ili kuongeza utamu wa kisa unachokitunga.
Zoezi
Tunga kisa chochote kinachohusu wizi ukitilia maanani sifa za utungaji mzuri wa kisanii.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 65 12/11/2019 09:44
66
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3
4 5
6 8
9 10
7
11 12 13 14
15
16
17 18
19 20
KULIA
3. Tohoa supermarket
8. Hama
9. Fanya jambo au kitu kifuate kanuni kwa kuondoa kasoro
10. Kusisimua au kuwa kizuri cha kupendeza
13. Mazingara
16. Chelewa- kutoka kwa wakati
17. Lugha ya taifa
18. Neno linaloarifu au tutaarifu
19. Nyimbo za kubembeleza
20. Kulingana na
CHINI
1. Kuuza na kununua bidhaa au huduma
2. Matwana
4. Jina jingine la kiima
5. Wanaoenda kununua bidhaa na huduma
6. Kuleta msisimko
7. Sehemu katika sentensi ambayo huwa na mtenda
11. Kutokuwa na uwezo wa kujikimu kimaisha
12. Binadamu wa kiume
14. Kipashio cha kimuundo kiundwacho kwa neno moja au zaidi
15. Bila haraka na kwa mpango
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 66 12/11/2019 09:44
67
A. Ufahamu
Dawa za kulevya na jamii
Tatizo la dawa za kulevya ni moja kati ya matatizo makuu katika jamii zetu. Pombe, ambayo
inaweza kujumlishwa katika kundi pana la dawa za kulevya, imetumiwa kama burudani katika
jamii kwa kipindi kirefu sana. Katika jamii za zama za leo, kuna shinikizo za kijamii na kitamaduni
ambazo zinawafanya watu wengi kuishia kuitumia pombe au bia na kuvuta sigara. Ikiwa utumiaji
wake unaathiri anayehusika pamoja na jamii yake, basi pana sababu kubwa ya kulishughulikia
suala hili.
Sote tunafahamu kuwa dawa huwa na mchango mkubwa wa kimatibabu. Lakini ikiwa dawa
zimetumiwa kwa sababu ambayo haihusiani na matibabu au kwa njia mbaya, huwa na matokeo
mabaya. Chanzo kikuu cha kutumia dawa vibaya ni kuzipata athari fulani zinazohusishwa na
dawa zinazohusika. Matumizi ya aina hii huweza kusababisha utegemeaji wa dawa kiasi kwamba
mtu hawezi kutenda kazi fulani pasi na kuzitumia dawa zinazohusika. Utegemeaji huu wa dawa
unaathiri mwili wa anayehusika na jinsi unavyofanya kazi. Kisaikolojia au kiakili anayehusika
huweza kuzitegemea dawa kiasi kwamba hawezi kufanya lolote pasi na kuzitumia dawa fulani.
Miongoni mwa watu wanaoathirika kwa kiasi kikubwa na tatizo la dawa za kulevya ni vijana.
Kwa nini vijana wanaathirika kiasi hiki? Utumiaji wa dawa za kulevya unawavuta vijana ambao
wamo katika harakati za kuwa huru na kuusaka ujitambuaji. Baadhi yao wanaelekea kuamini
kuwa dawa hizi zitawapa sifa muhimu za kujitambua kama ujasiri, kujiamini, hisia za kuwa huru
n.k. Asilimia kubwa ya vijana katika nchi nyingi zinazoendelea na zilizoendelea wamezongwa
na tatizo hili. Ikiwa asilimia kubwa ya vijana itaathirika, basi pana hatari kubwa ya jamii za
ulimwengu kuvipoteza vizazi vya kesho. Suala la dawa za kulevya sio tatizo la nchi zilizoendelea
tu wala tatizo la maeneo ya mijini tu. Hili ni tatizo ambalo linasambaa kila sehemu kwa kasi ya
ajabu sana.
Nchi zinazoendelea zinaathirika zaidi kwa kuwa maendeleo yao yanakitegemea kizazi cha
vijana. Ni katika hali hii ambapo elimu ifaayo ni muhimu ili kusaidia kuwaelimisha wanaohusika
pamoja na jamii nzima.
Moja kati ya sababu kuu zinazochangia kuweko kwa tatizo la utumiaji mbaya wa dawa ni
kuvunjika kwa muundo na mshikamano wa kijamii ambao ni msingi muhimu sana. Ikiwa
msingi huu uliotegemewa na wanajamii umevunjika, kuna uwezekano kuwa baadhi ya wanajamii
watashindwa kukabiliana na hali yao mpya. Hawa watajaribu kusaka kimbilio fulani kwenye
dawa za kulevya. Hii kwao inakuwa kama njia ya kujipumbaza na kujihakikishia kuwa wanaweza
kuikabili hali hii mpya. Katika mataifa mengi, kuna uhamaji mkubwa wa watu kutoka maeneo
ya mashambani hadi mijini. Asilimia kubwa ya watu hawa wanakabiliana na matatizo mengi
wanapoingia mijini. Matatizo haya ni kama ukosefu wa ajira, malazi, chakula na mahitaji
ya kimsingi. Pili, wanakumbana na tatizo la ukiwa na upweke wa kutengana na jamaa zao
waliowasaidia kupambana na hali za maisha. Tatu, wanakumbana na hali ambazo hawakuzizoea
katika utamaduni walimokulia. Matatizo yanayohusiana na ulimbukeni huo wa maisha ya mjini
yanaweza kumtosa mtu kwenye dawa za kulevya.
Je, matumizi ya dawa za kulevya yanaiathiri vipi jamii? Jambo la kwanza ni kutambua kuwa
suala la dawa za kulevya ni tanzia ya kijamii. Hili sio tatizo ambalo limetengewa sehemu nyu
Sura ya Saba
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 67 12/11/2019 09:44
68
za jamii; linaiathiri jamii nzima. Hili sio tatizo la mitaani tu bali limeziathiri jamaa, maeneo ya
kazi, shule na taasisi nyingine zozote. Ni tatizo ambalo linawaathiri watu wa kila umri, kuanzia
vijana wa shule hadi watu wazima.
Katika kiwango cha jamaa, matumizi ya dawa za kulevya yanauathiri ushikamano na umoja
wao. Watumiaji wa dawa za kulevya wanazugwa na kurengwa na tabia yao kiasi kwamba haja
za watu wengine sio muhimu kwao. Anayehusika anaathirika kiafya na kisaikolojia. Jamaa yake
nayo inateseka kumwona mwenzao akiangamia kutokana na kuzitegemea dawa za kulevya. Ikiwa
wanaotumia dawa za kulevya ni watu wazima, pana uwezekano watoto wakaishia kuamini kuwa
kutumia dawa hizo ni jambo la kawaida na linalofaa. Utumiaji wa dawa za kulevya unaweza
pia kuiingiza jamaa inayohusika kwenye matatizo ya uhalifu. Mtumiaji aliyerengwa na dawa za
kulevya huwa tayari kufanya lolote lile ili apate pesa za kununulia dawa hizo.
Katika kiwango cha shule, dawa za kulevya huwaathiri vijana vibaya sana. Kwanza, huathiri
ukuaji wa kijana anayehusika. Dawa hizi huua seli za ubongo na kuathiri uwezo wa mwanafunzi
wa kuweza kuyafuatilia masomo yake vizuri. Pili, kutegemea dawa za kulevya huweza kuathiri
ukuaji wa kawaida wa mwili. Tatu, ukuaji wa kimaadili wa mwanafunzi unahiribika. Dawa za
kulevya zinaathiri tabia za wanaohusika na kuwapa hisia ambazo haziwezi kuifaidi jamii. Nne,
matumizi ya dawa za kulevya huathiri uwezo wa mwanafunzi kimasomo. Tano, matumizi ya
dawa za kulevya shuleni yanachochea kuwapo kwa matendo yanayohusishwa nayo. Matendo
haya ni kama wizi, uhalifu, ukahaba, unyang’anyi, utovu wa nidhamu na uuzaji wa dawa zenyewe.
Jamii yoyote inayotaka kuendelea haina budi kuzipiga vita dawa za kulevya.
Maelezo ya msamiati
shinikizo za kijamii : nguvu inayotokana na jamii.
burudani : -enye kuburudisha; -enye kuleta raha au kufurahisha.
kuusaka ujitambuaji : kuutafuta ukweli wa nafsi zao; kutaka kujijua vizuri .
wanazugwa na kurengwa : wanapumbazwa na kushawishiwa kabisa.
wamezongwa : wamezidiwa/wamezungukwa na matatizo.
linasambaa : linaenea kila mahali; linatapakaa; linazagaa.
kujipumbaza : kujidanganya.
ukosefu wa ajira : ukosefu wa kazi.
ulimbukeni : hali ya kutofahamu mambo vizuri.
sehemu nyu ya jamii : sehemu moja tu ya jamii; sehemu ndogo tu ya jamii.
Maswali
1. Mwandishi anasema pombe huweza kuwa dawa ya kulevya. Hii hutokeaje?
2. Dawa ya kawaida inawezaje kugeuka kuwa dawa ya kulevya?
3. Ni sababu zipi zinazowavuta vijana kutumia dawa za kulevya?
4. Kuvunjika kwa muundo wa kijamii kunachangiaje matumizi ya dawa za kulevya? Taja
sababu zinazowaelekeza watu wanaohamia mijini kujiingiza katika matumizi ya dawa za
kulevya.
5. Eleza jinsi jamii inavyoathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya.
6. Wewe binafsi utachukua hatua gani kuhakikisha kuwa hutaingia katika tabia ya kutumia
dawa za kulevya?
7. Tumia maneno haya kwenye sentensi kuonyesha maana yake kulingana na yalivyotumika
kwenye kifungu.
(i) linasambaa (ii) zama za leo (iii) ukiwa (iv) pasi (v) dawa za kulevya
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 68 12/11/2019 09:44
69
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - ch/j
Tamka maneno haya
ch j
changa janga
chema jema
chini jini
choka joka
chungu jungu
Soma vitanza ndimi vifuatavyo ili kujizoeza matamshi yafaayo ya sauti hizo.
(a) Watoto wa Muchanga wangekwa na majanga baada ya Muchanga kuchimba shimo apate
mchanga akisahau mashimo yasiyo na mchanga huleta majanga.
(b) Nilipohitaji majembe nilienda kwa Majembe lakini sikumkuta Majembe bali Kajembe
aliyeniita chemba kumpiga Majembe vijembe.
(ch) Nilipoliona jini la majini niliamua kulala chini kwani nikilala chini sitaonekana na jini la
majini kwa vile majini ya majini hayaoni mtu akilala chini.
Ufahamu wa kusikiliza
Ufahamu wa kusikiliza unahusu kuyazingatia au kuyatilia maanani yasemwayo na mtu mwingine.
Huyo mtu mwingine anasoma kifungu fulani huku wewe ukisikiliza. Inawezekana ukatakiwa
kulisikiliza jambo, taarifa au habari ili uweze kumweleza mtu baadaye. Kwa mfano, baba au
mama anaweza kukuomba usikilize taarifa ya habari inayosomwa redioni halafu umweleze
yaliyosemwa baadaye.
Mambo ya kuzingatia kuhusu ufahamu wa kusikiliza
1. Lazima uwe msikivu; usikilize yanayosemwa kwa makini na uzingatifu mkubwa.
2. Ni muhimu kuwa na utulivu. Huwezi kusikiliza vyema bila ya kutulia.
3. Jitahidi kuyashika mambo muhimu. Kila taarifa au habari inayosomwa huwa na mambo
muhimu yanayotawala; jaribu kuyashika mambo haya vizuri.
4. Hakikisha kuwa umeyaelewa mambo hayo muhimu. Haitoshi tu kuyashika mambo
yanayohusika, lazima pia uyaelewe vizuri.
5. Lazima uweze kuyaeleza upya mambo uliyoyasikiliza. Unatakiwa kuyaeleza mambo hayo
kwa kuitumia lugha yako mwenyewe. Ikiwa umelielewa jambo fulani utaweza kulieleza
kwa lugha yako vizuri.
6. Hakikisha kuwa maelezo yako yanahusisha mambo yote muhimu na makuu yaliyokuwako
katika taarifa uliyosikiliza.
Zoezi
Sikiliza kwa makini kifungu cha ufahamu atakachokisoma mwalimu halafu uyajibu maswali
yafuatayo:
1. Ni shida zipi ambazo watoto wanakabiliana nazo?
2. Kuna maana gani kusema kuwa kila mtoto ana haki ya kuishi?
3. Ni nini maana ya kulinda mtoto kutokana na ajira ya watoto?
4. Ni nani wanaopaswa kuwalinda watoto?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 69 12/11/2019 09:44
70
5. Ajira hii ya watoto ina athari gani kwao?
6. Mtoto anawezaje kupata habari muhimu zinazomhusu?
CH. Saru na matumizi ya lugha
Vielezi (E)
Vielezi ni maneno yanayofafanua vitenzi, vivumishi au vielezi vingine. Hueleza kitendo
kinatendeka wapi, vipi, saa ngapi, mara ngapi n.k. Kwa mfano:
(a) Dawa za kulevya ni hatari sana.
(b) Mukhobero aliwapa watoto peremende tamu ajabu.
(ch) Mwashigadi atajenga nyumba kubwa mno.
(d) Mwalimu alitueleza kinaganaga kuhusu madhara ya dawa za kulevya.
(e) Mimi nimetembelea Mombasa mara mbili.
Zoezi
Onyesha vielezi katika sentensi zifuatazo:
1. Ndege waliruka mbali sana.
2. Nyanya anatembea polepole.
3. Watoto walicheza kwa furaha.
4. Ni nani anaongea vibaya hivyo?
5. Askari yule alipigana kishujaa.
6. Wakaba anatembea kingwana.
7. Mbwa alibweka bwe!
8. Katana amelewa chakari.
9. Fisi hula chakula haraka haraka.
10. Nitakuja jioni.
Tumia mzizi wa neno lililo kwenye mabano ili kuunda kielezi kinachofaa kukamilisha sentensi.
Kwa mfano:
Wachezaji wa timu hiyo hucheza mpira_____________ . (-baya)
Wachezaji wa timu hiyo hucheza mpira vibaya.
1. Alipokunywa dawa ya kulevya alianza kuhisi_____________ . (-baya)
2. Shangazi hupika pilau _____________. (-ema) sana.
3. Mwangangi anakula chakula _________________. (-si)
4. Kwa nini Makokha hutembea ______________? (-ile)
5. Yule mwizi alishambuliwa _______________. (-kali)
6. Prisca amerudi ______________. (-ao)
7. Sina raha _____________. (moyo-)
8. Yule mtoto amefanya kazi hii _________________. (-zuri)
9. Acha kunisemesha ______________. (-koloni)
10. Unahitaji kufanya kazi ____________. (-ume)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 70 12/11/2019 09:44
71
Wakati ujao - TA
Wakati huu huonyesha kitendo ambacho hakijatendeka lakini kinatarajiwa kutendeka baadaye
pengine kesho, kesho kutwa, mwaka ujao n.k. Huwakilishwa na kiambishi TA kwa mfano:
1. Mwalimu wetu atakuja kesho.
2. Nyumba itajengwa na Njenga.
3. Binamu atamwosha mtoto wake.
4. Ng ’o m b e a takamuliwa leo jioni.
5. Vikombe vitaletwa na Lamayian.
Zoezi
Andika sentensi zifuatazo katika wakati ujao:
1. Khapus alinunua pikipiki maridadi.
2. Mama anamkama ngombe wetu.
3. Wezi hutembea usiku.
4. Kazi hii ilikwisha.
5. Kioko anasoma kitabu.
6. Batabukini wanaogelea.
7. Chema kilijiuza, kibaya kilijitembeza.
8. Nteere anachoma takataka.
9. Mjomba hufanya kazi ya kufagia.
10. Farasi alikimbia.
11. Haraka haraka haina baraka.
12. Halima alinipikia chai.
13. Mbogori hufanya kazi kwa bidii.
14. Kaimuri alikwenda Muthetheni.
15. Wazee hawa wanashauriana.
Kukanusha wakati ujao kulingana na nafsi
Kukanusha kitenzi ni kukiweka katika hali ya kukataa au kupinga.
Tazama jedwali lifuatalo:
Umoja Wingi
nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nitaimba sitaimba tutaimba hatutaimba
nitagundua sitagundua tutagundua hatutagundua
nitarudi sitarudi tutarudi hatutarudi
nitapita sitapita tutapita hatutapita
nafsi ya pili
utaimba hutaimba mtaimba hamtaimba
utagundua hutagundua mtagundua hamtagundua
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 71 12/11/2019 09:44
72
utarudi hutarudi mtarudi hamtarudi
utapita hutapita mtapita hamtapita
nafsi ya tatu
ataimba hataimba wataimba hawataimba
atagundua hatagundua watagundua hawatagundua
atarudi hatarudi watarudi hawatarudi
atapita hatapita watapita hawatapita
Zoezi
Kanusha sentensi zifuatazo:
1. Mwalimu atatufundisha jioni.
2. Yeye ataniletea maharagwe.
3. Waziri atafungua maonyesho.
4. Wazee wataamua kesi hiyo.
5. Mpwa wangu ataniletea zawadi.
6. Sisi tutapiga vita utumiaji wa dawa za kulevya.
7. Kina Wairimu watanunua vitabu.
8. Wewe utaondoka kesho.
9. Nyinyi mnatakiwa na polisi.
10. Mimi nitamruhusu.
D. Kusoma
Kusoma kwa kina: Majarida
Jarida ni chapisho linalofanana na kitabu linalokusanya maandishi mbalimbali ya waandishi
tofauti kuhusu jambo fulani. Maandishi hayo mbalimbali hujulikana kama makala. Kwa kawaida
jarida, tofauti na gazeti, halichapishwi kila siku bali huchapishwa baada ya kipindi maalum. Yapo
majarida ya aina mbalimbali. Kuna majarida yanayowahusu watu wa makundi mbalimbali k.m.
majarida ya wanawake, ya vijana, na ya wasomi au wataalamu. Majarida yanaweza kuhusu elimu,
ufundishaji, matibabu, maendeleo ya kisayansi n.k.
Kwa nini tunasoma majarida?
Kuupanua ujuzi na maarifa yetu kuhusu jambo fulani.
Kujifahamisha mambo yanayoendelea ulimwenguni au katika uwanja fulani maalum.
Kujifundisha jinsi ya kuweza kuandika na kuyakuza mawazo yetu kuhusu jambo fulani.
Kupata maarifa ya ziada baada ya kusoma kwetu darasani na kwingineko.
Kujikuza kama wanafunzi kwa kujua mawazo ya watu wengine kuhusu mambo na masuala
tofauti.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 72 12/11/2019 09:44
73
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata.
Riwaya yoyote ile haikosi mhusika na mara nyingi sana huwepo wahusika kadhaa. Tuzungumziapo
mhusika tunasisitiza kwenye mhusika mkuu. Wahusika ni watu ambao msanii mwenyewe
huwabuni kutokana na maisha ya jamii yake kulingana na kile anachotaka kukifafanua. Uchunguzi
wa wahusika wake ndio hasa unaomwezesha kuijenga hadithi yake. Hadithi yoyote ile itakuwa
inahusu watu wa jamii fulani, ikiwa na malengo tofauti kama vile kutatua migogoro, kukosoa
au kufunza. Hali hizi zitakuwa zimejitokeza kwa msanii na yeye akawa na maoni yake ambayo
huyaona muhimu kujadili kwa manufaa ya jamii nzima. Hivyo, mjadala huo anaukuza na
kuupanua kwa kuwatumia watu anaowatoa huko kwenye jamii yake. Hii ina maana kuwa wahusika
ni watu tunaoishi nao ambao wamechujwa, wamechunguzwa na kusomwa tabia zao, matendo
na sifa zao, halafu wakachukuliwa kama mifano bora ya kuweza kuitoa picha halisi. Picha hiyo
inaweza kuwa ya tabia za binadamu na desturi zao, matendo na kira. Iwapo msanii amefanikiwa
kumchora mhusika wake haiwi taabu kumpata mtu wa aina hiyo katika jamii. Si bure waandishi
huanza kwa kutoa tahadhari. “Watu wote na majina yote yaliyomo katika hadithi hii ni ya kubuni
wala hakuna uhusiano wowote na watu waliowahi kuishi duniani (Mwana wa Yungi hulewa).
(Makala ya S. A. Mlacha Wahusika katika riwaya za Kiswahili, Tanzania
(1970- 1982). Katika Mulika, 17, 1985, uk 29- 45.)
Maswali
(a) Je, mhusika ni nani?
(b) Je, msanii au mwandishi anawajenga wahusika kwa kutegemea nini?
(ch) Kwa nini waandishi wengine wanatoa tahadhari?
E. Kuandika
Utungaji wa kisanii
Mashairi mepesi
Mashairi ni aina ya tungo ambazo huwa na muundo na mdundo (mapigo) fulani maalum. Tungo
hizi hutumia lugha ya mkato inayoweza kukumbukika haraka. Mashairi huwa na ujumbe fulani,
yaani anayetunga shairi anataka kusema jambo fulani. Kuna aina mbili kuu za mashairi: mashairi
mapokeo (ya arudhi) na mashairi huru. Mashairi mapokeo yana mpangilio maalum wa sentensi,
sauti fulani zinazofanana katika sehemu sawa, idadi maalum ya sentensi (mishororo) n.k. Mashairi
huru hayana mpangilio huo maalum na siyo lazima sauti fulani zifanane.
Mambo ya kuzingatia katika kutunga shairi:
1. Kwanza lazima uwe na jambo unalotaka kulisema.
2. Ni muhimu uyapange mawazo yako, ujue ni lipi la kutangulia na litakalofuata.
3. Lazima ujumbe wa shairi lako utokeze wazi wazi.
4. Ujumbe unaweza kuwa na matokeo mazuri ikiwa umewasilishwa kwa lugha yenye mvuto.
5. Kumbuka, katika ushairi, kuna matumizi mengi ya lugha ya mkato. Kwa mfano: nenda
badala ya ninaenda, aso’kula badala ya asiyekula, usache badala ya usiache, asejua badala
ya asiyejua n.k.
6. Jitahidi kutumia ulinganishi ili kuongezea nguvu yale unayotaka kusema.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 73 12/11/2019 09:44
74
Mfano 1: Shairi mapokeo
Soma mwanafunzi
Mwanafunzi hizi zama, hizi tuishizo zama,
Huna budi ya kusoma, bila kamwe kulalama,
Usome baba na mama, kuandika na kusoma,
Uweze pia kusema, na Kiswahili sanifu.
Soma pia ukulima, mbinu zote kuandama,
Sayansi pia soma, ni somo la taadhima,
Fasihi usache nyuma, ya vitabu na kalima,
Uweze pia kusema, na Kiswahili sanifu.
Elimu-viumbe soma, uifahamu kwa kima,
Ina maarifa mema, ya usa na lukuma
Historia pia soma, jua utokako nyuma,
Uweze pia kusema, na Kiswahili sanifu.
Maelezo ya msamiati
taadhima : heshima.
us’ache : usiache.
kalima : usemi; kauli.
lukuma : chakula.
Maswali
1. Je, kwa nini mtunzi ametunga shairi hili?
2. Je, ni masomo yapi anayoshauriwa asome mwanafunzi? Atafaidikaje?
3. Je, mstari (mshororo) wa mwisho unasisitiza nini?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 74 12/11/2019 09:44
75
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3 4
5
6 7
8
9 10
11
12
13 14
15
16 17
18
19
20
KULIA
3. Magonjwa
5. Ugonjwa wa kifua unaofanya magonjwa kukohoa sana na kupumua kwa tabu; hupata watoto
wadogo
6. Umoja wa vyombo
9. Ujumbe mkuu katika hadithi
11. Anayetibu
12. Pahali pa matibabu
13. -enye kufuata sheria za kiutendaji zilizowekwa
14. Kastoma
16. Waba
18. Chunguza mtu au jambo kwa kusaili au kuuliza maswali
19. Tetemaji
20. Pamoja na kuwa
CHINI
1. Kiunganishi 15. Upungufu wa kinga mwilini
2. Maneno yanayotatiza ulimi kimatamshi 17. Jedhamu
4. Mdudu asababishaye maradhi
7. Anayenunua
8. Wanaotaka au wanaoenda kutibiwa
10. Maneno ya kuunganisha
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 75 12/11/2019 09:44
76
Sura ya Nane
A. Ufahamu
Katiba ya Msenangu
Msenangu alifahamika katika kijiji cha kwao na takriban kila mtu. Watoto walimfahamu kutokana
na mtindo wake wa kutembea. Alitembea wima kama askari jeshi na kila alipokwenda malevini
na kupiga chupa zake, alikuwa na mazoea ya kupiga kwata kama mwanajeshi chuoni. Sababu
nyingine iliyomfanya Msenangu afahamike ni ucheshi wake. Aliwasimulia vijana hadithi za kila
aina na kuwavunja mbavu kwa umahiri wake wa kuzitamba hadithi zenyewe.
Ingawa Msenangu alikuwa na umri mpevu sana, alikuwa mmoja kati ya wazee wachache wa
kwao waliojua kusoma. Idadi ya waliojua kusoma ilikuwa akali sana na mzee huyo aliona fahari
ya kuwa miongoni mwa hao wachache.
Siku habari za kuandikwa kwa katiba mpya ya nchi zilipoka kijijini, Msenangu alifurahi na
kuchanua uso. “Hii ni nafasi ya kuhakikisha kuwa nimewaeleza yote yanayohitajika kufanywa,
alijitapa Msenangu. Wanakijiji walitaka kuwateua vijana wawawakilishe siku ambapo tume ya
kuandika katiba mpya itaka pale kijijini. Hata hivyo, Msenangu alikazania kuwa ni lazima
atakuwa mmoja wao. Licha ya uwezo wake wa kusoma, wanakijiji wengi hawakuamini kuwa
alijua lolote kuhusiana na katiba. Mzee, mambo haya yanahitaji vijana waliosoma juzi juzi,
sio kabwela wasiojua lolote, walimwambia. “Jambo usilolijua ni usiku wa kiza. Ngojeni mpaka
wataalamu wenyewe wake huku ndipo niwaelimishe, alijibu Msenangu. Watu waliangua kicheko.
Siku ya siku ilika. Ukumbi ulijaa furifuri hadi ukatapika watu nje. Wote walikuwa na hamu
siyo tu ya kujua mambo hayo ya katiba mpya bali kuyasikiliza mawazo na mapendekezo ya vijana
wao wenye elimu na hasa kushuhudia vituko vya Mzee Msenangu.
Umati ulipotulizana, mwenyekiti wa kamati alisimama, kisha akasema, “Ndugu wananchi,
tumefurahi kuka hapa kijijini siku ya leo. Nia yetu ni kuyapata maoni yenu kuhusu katiba mpya.
Katiba ni kielekezi cha jinsi ya kuiendesha nchi na masuala ya utawala. Ni chombo cha kulinda
haki za kila mwananchi bila ya kuzingatia tabaka, maumbile wala jinsia. Karibuni mtupe maoni
yenu, alimaliza na kuketi.
Wale vijana walioteuliwa walisimama na kutoa maoni kwa niaba ya wanakijiji. Vijana hao
walitumia lugha ya kisheria ambayo ni dhahiri wanakijiji wengi hawakuielewa. Baadhi yao
walianza kulalamika kwa sauti za chini, “hii katiba ni ngumu sana. Ni mambo mengi yasiyotuhusu
sisi, walisema watu waliokuwa wameanza kuchoka. Muda si muda watu walianza kutoka
ukumbini mmoja mmoja. Ndipo, bila kungojea aalikwe, Mzee Msenangu alisimama. Watu
waliokuwa nje ya ukumbi waliambizana, “Haya, Msenangu huyo!” Alianza kuongea.
“Ndugu wanakamati, nimeisubiri fursa hii kwa hamu kubwa. Maneno yangu mimi si mengi
kwani sikusoma mambo hayo ya ‘yesi yesi. Lakini ningetaka kusema machache niliyo nayo
moyoni. Nataka iandikwe katiba itakayoiendesha nchi yetu kwa njia nzuri kwa miaka mingi ijayo.
Katiba hiyo ni lazima iwalinde raia wote, walemavu na wasio walemavu, waonao na wasioona,
waumini na walevi, alianza Msenangu. Watu walitazamana kwa mshangao mkubwa. Alaa! Huyo
ni Msenangu jamani? Mbona leo ana mawazo mazito sana!” waliambizana kwa sauti. Waliokuwa
nje ya ukumbi walitafuta mianya na kuchungulia ndani kuhakikisha kuwa kweli maneno hayo
yalitoka kinywani mwa Msenangu. Waliokuwa wamejiandaa kucheka walibakia kuachama;
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 76 12/11/2019 09:44
77
midomo wazi. “Tulieni tumsikilize!” wengine walisema. Wale waliokuwa wakiondoka ukumbini
walirudi haraka na kuketi.
Msenangu aliendelea, Katiba inayoifaa nchi ni ile isiyozingatia matakwa ya kundi moja
la jamii tu. Lazima ziwepo njia za kuwadhibiti hawa viongozi kuhakikisha kuwa wanapotwaa
madaraka hawatugeuzi sisi wanyonge wanasesere wao wa kuchezea, alisema Msenangu na kutua.
Ukumbi mzima sasa ulikuwa umemtegea masikio yote ndi huku wakijiuliza ni wapi mzee huyo
alikoyaibua mawazo mazito kama hayo. Lakini mambo yalikuwa bado.
Wanakamati walikuwa wanashughulika kuandika huku wakiitikia kwa vichwa vyao. Msenangu,
aliyekuwa fundi wa kuongea, alitua kidogo na kuzungusha kichwa chake huku na huko ukumbini.
Aliona sasa umati wote ulikuwa umemkazia macho wakitarajia mengi zaidi. “Leo watamtambua
Msenangu mwenyewe ni nani, alijiambia moyoni. Alijikohoza tena na kuendelea. Sisi wanyonge
tunaoishi huku mashambani tuna shida. Wahenga husema sheria ni msumeno, hukata nyuma
na mbele. Lakini kwetu huku haikati mbele, inakata nyuma tu. Wenye vyeo wanapotamani
vikataa vyetu wanavitwaa tu kwa njia rahisi wakitumia vyeo vyao. Tunaposhindwa kulipa pesa
za michango ambazo hatuna, machifu wanaamuru mifugo wetu wasombwe. Pawepo na sheria
za kuwadhibiti watu kama hao; wadhibitiwe ili wajue wenzao wana haki bali sio magombe
ya kukokotwa bila ya hiari. Kwa kifupi, pawepo na sheria inayokata mbele na nyuma; sheria
inayotetea tajiri na maskini, mnyonge na mwenye nguvu, aliyenacho na asiyenacho.
“Wanakamati wapendwa, usalama umeadimika kama mito jangwani. Sisi wenyewe ndio
tumegeuka walinda usalama. Lakini jambo la kushangaza ni kwamba, tuwatiapo wahuni hao
mikononi, kesho yake tunakutana nao kijijini - wameshaachiliwa huru baada ya kutoa chai.
Mambo hayo lazima yakome.
“Katika nchi inayothamini raia wake, bei za bidhaa haziongezeki kishaghalabaghala tu bila
mpango. Kila wiki bei za bidhaa zinabadilika; ni nani anayetujali sisi raia wa kawaida? “Ningetaka
katiba mpya iangalie jambo hili. Hiyo wazee wangu ndiyo katiba yangu!” alimaliza Msenangu.
Baada ya kuyasema haya, Msenangu akachukua mkongojo wake na polepole akatoka ukumbini
na kuuacha umati umeduwaa. Kisha ukumbi ukalipuka pu kwa mako na vigelegele ukimshangilia
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 77 12/11/2019 09:44
78
Mzee Msenangu ambaye tayari alikuwa ameshaondoka. Jamaa waliokuwa wameka kumwona
akifedheheka walikuwa bado wameachama.
Kikao kilipofumukana siku hiyo jioni, jua lilikuwa limeikalia milima ya magharibi. Ingawa
watu zaidi walipewa fursa ya kutoa maoni yao mbele ya wanakamati, wanakijiji walipokuwa
wakielekea makwao walikuwa wakiyacheua maneno na kuitafakari tu katiba ya Msenangu.
Maelezo ya msamiati
takriban kila mtu : karibu kila mtu.
umahiri : uhodari.
umri mpevu : uzee.
jitapa : jigamba; ringa/jivuna.
akali : chache; kidogo.
kabwela : raia; mwananchi wa kawaida.
kielekezi : mwongozo.
alikoyaibua : alikoyatoa; alikoyapata.
vikataa : mashamba madogo; vishamba.
umeduwaa : umeshangaa; umepigwa na butwaa.
akifedheheka : akiaibika; akipata soni.
magombe : ngombe wakubwa (hali ya ukubwa).
kishaghalabaghala : bila mpango maalum; ovyo ovyo.
kilipofumukana : kilipotawanyika.
Maswali
1. Msenangu alijulikana kama mzee wa mizaha tu. Taja tabia zake mbili zinazothibitisha
haya.
2. Ni kwa nini wanakijiji walishangaa Msenangu alipojitolea kutoa maoni yake kuhusu katiba
kwa wataalamu?
3. Ni kwa nini unakiri watu walianza kuchoshwa na wale vijana wawili waliowachagua
kuongea mambo ya katiba siku hiyo?
4. Andika mapendekezo yote yaliyotolewa na mzee Msenangu.
5. Ni dhahiri kuwa wanakamati walipendezwa na mawazo ya Msenangu. Ni nini kinachoweza
kuthibitisha hayo?
6. Kifungu hiki kinatufundisha nini kuhusu raia na katiba yao?
7. Eleza maana ya misemo ifuatayo kama ilivyotumiwa kwenye kifungu:
(a) piga chupa (b) kazia macho (i) jaa furifuri
(ch) piga kwata (d) tega masikio
(e) vunja mbavu (f) toa chai
(g) chanua uso (h) ona fahari
8. Soma vifungu hivi vya maneno:
(a) tembea kama askari jeshi
(b) badilika kama hali ya hewa
(ch) adimika kama mito jangwani
Vifungu kama hivi vinavyotumia maneno ya mlinganisho kama vile: kama, mithili ya, mfano
wa, n.k. huitwa tashbiha au tashbihi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 78 12/11/2019 09:44
79
Chagua jibu sahihi kukamilisha tashbihi zifuatazo:
ng’onda, mchuzi wa ugali, mwana aliyezaliwa Ijumaa, mtu anayekata roho, kigaga
(a) Bahatika kama _________________.
(b) Dahadari kama ________________.
(ch) Ganda kama _________________.
(d) Jitia katikati kama ______________.
(e) Konda kama ________________.
9. Tumia maneno haya katika sentensi ili kuonyesha maana yake kama yanavyojitokeza
kwenye kifungu:
(a) katiba
(b) wasombwe
(ch) wakiyacheua
(d) kuitafakari
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate f/v
Tamka maneno haya
f v
faa vaa
fua vua
fika vika
fuka vuka
fuma vuma
Soma vitanza ndimi vifuatavyo:
(a) Ulipoka msimu wa vuli, mwalimu Mvita alimwambia Fum avae vazi linalofaa.
(b) Nilipoka nyumbani nilivua nguo nikakimbia mtoni kuzifua nikamkuta Mwamvua akivua,
nikashangaa kwa nini Mwamvua anavua badala ya kufua.
(ch) Bwana Mka alika avikwe taji na walioka.
Fasihi simulizi: Hurafa
Hurafa ni hadithi ya fasihi simulizi ambayo inahusisha wanyama. Hurafa ni kipera cha utanzu wa
hadithi. Wanyama huwa wahusika wakuu katika hadithi ya aina hii na hupewa uwezo sawa na
binadamu. Wao hula, huongea, hucheka, hulia, husikitika na hufanya matendo yote anayoyafanya
binadamu. Wanyama katika hurafa huwakilisha binadamu wa kawaida. Kwa mfano: mnyama
ambaye ni katili huwakilisha binadamu mwenye sifa kama hiyo. Mafunzo yanayotokana na
hurafa, kwa hivyo, humhusu binadamu. Hulenga kuadilisha au kuonya wanajamii wenye tabia
kama hizo ili kuchochea mabadiliko.
Mfano
Simba na Panya
Hapo zamani za kale paliondokea simba ambaye alijitosa katika safari zake za kila siku za
kuwatafuta wanyama ili apate chakula. Alizunguka huku na huku lakini akashindwa kumpata
mnyama yeyote, wanyama walijicha walipomwona. Basi alianza kutembea polepole akirudi
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 79 12/11/2019 09:44
80
yalipokuwa makao yake makuu huku amejiinamia kwa huzuni na unyonge wa kukosa chakula.
Kwa bahati nzuri alikutana na panya aliyekuwa akijiendea zake. Simba aliamua kumkamata
panya na kumla ili kuikidhi njaa yake kubwa. Mimi nimekosa chakula, kwa hiyo nitakukamata
wewe panya nikumeze, alisema simba kwa sauti nzito. Panya alimwangalia simba na kusema kwa
sauti ya unyonge, “Sasa simba ukinila utafaidi nini na mwili wangu ni mdogo siwezi hata kutoshea
hata kwenye magego yako. Naomba uniachilie niende zangu labda siku moja nitaweza kukulipa
kwa fadhila yako hii, alisema panya. Simba aliangua kicheko kikubwa na kusema, sasa mnyama
mdogo kama wewe utanifaa kwa nini? Lakini haidhuru nitakuachilia uende zako, alisema simba
na kushika njia akaenda zake. Panya naye alitimua mbio kuelekea nyumbani akiwa na furaha
kubwa baada ya kunusurika.
Basi siku moja simba alipokuwa akizungukazunguka huko mwituni akitafuta chakula,
alinaswa na kimia au wavu mkubwa akawa hawezi kujinasua. Alijaribu kujirusharusha huku na
kule lakini akashindwa kabisa kujitoa kwenye mtego ule. Alinguruma kwa sauti yake ya kutisha
lakini haikufaa kitu; ule wavu uliendelea kumnasa simba kabisa. Kwa bahati nzuri alitokeza
panya aliyekuwa akienda kwenye safari zake za kutafuta chakula kama kawaida. Alipomwona
simba alimsogelea na kumwuliza, Je simba raki yangu kwa nini unalia jinsi hii?
“Nimezongwa
na huu wavu nisiweze kutoka kabisa, sijui hata nitafanya nini?”alijibu simba. Mimi nitakusaidia
raki yangu, alisema panya. Simba aliangua kicheko kikubwa na kuuliza, Nimeshindwa mimi
mwenye nguvu nyingi utawezaje wewe mnyama dhaifu? “Simba mimi nina meno makali kama
kijembe, nitaukata wavu haraka utaona tu, alisema panya halafu akaanza kuutafuna ule wavu.
Muda si muda panya alimaliza kuukata ule wavu na simba akatoka nje na kumshukuru sana.
Tangu siku hiyo wakaendelea kuishi kwa masikilizano na uraki mwema.
Maswali
1. Kwa nini simba alitaka kumla panya?
2. Je, ni sababu gani iliyomfanya simba amwachilie panya?
3. Eleza jinsi panya alivyorudisha fadhila za simba?
4. Je, unajifunza nini kutokana na hurafa hii?
CH. Saru na matumizi ya lugha
Vihisishi (I)
Vihisishi ni maneno yanayoonyesha hisi za moyoni. Hisia hizi ni kama kushangaa, kuhuzunika,
kufurahi, kuajabia au kustaajabia, kukata tamaa, kushangilia, kuhongera, kukemea n.k. Hisi
huonyeshwa kwa kuwepo kwa alama ya mshangao (!). Baadhi ya vihisishi ni: Lo!, aka! Labeka!,
Salaala! La! Mungu wangu! Barabara!
Kwa mfano:
(a) Lo! Lo! Fisi anamshambulia kondoo wetu.
(b) Salaala! Kwa nini unawatukana watu hivyo?
(ch) Hoyee! Timu yetu imeshinda.
(d) Aisee unakwenda wapi?
(e) La hasha! Siwezi kuiba vitu vya watu.
(f) Salaala! Unywaji pombe umemharibu afya namna ile?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 80 12/11/2019 09:44
81
Zoezi
1. Onyesha vihisishi kwenye sentensi zifuatazo:
(a) Lo! Lo! Lo! Yule ni nani?
(b) Hewaa! Sasa nitaweza kusari Mombasa.
(ch) Simile! Rais anapita.
(d) Kusema kweli mimi sikumpiga mtoto huyo.
(e) Sawa sawa, tutakutana kesho.
(f) Kamwenja hoyee! Kericho zii!
(g) Haki ya Mungu wewe utanitambua.
(h) Barabara! Sasa tumeelewana.
(i) Masalaale! Gari limeanguka mtoni.
(j) Eti! Mimi siwezi kuamini mambo kama hayo.
2. Tunga sentensi ukitumia vihisishi vifuatavyo:
(a) Aka! (b) Abe! (ch) Labeka!
(d) Mungu wangu! (e) Ewe! (f) Mama yangu!
Uakishaji
Nukta mkato/semi koloni/Nusu koloni (;)
Hii ni alama ya kuakisha inayoweza kutumika kwa njia mbalimbali kama zifuatazo:
1. Kutenganisha sehemu kuu za sentensi. Kwa mfano:
(a) Nilipoka arusini hakukuwa na dalili za sherehe hata kidogo; ilibidi kusubiri hadi
saa tisa.
(b) Mapenzi ni kama surua; kila mtu ni lazima apite njia hiyo.
(ch) Nitaondoka mapema sana; chelewa chelewa utakuta mwana si wako.
(d) Kila binadamu hutaka kuishi maisha marefu; lakini hakuna binadamu anayetaka
kuzeeka.
2. Kwenye sentensi iliyo na vituo vingi ili kutenganisha sehemu zake kuu kwa mfano:
(a) Tulipoka hospitalini, mahali tulipokuwa tukipanga kuja tangu Jumatatu, tulimkuta
raki yetu ashafariki; laiti tungalijua.
(b) Kivuva, iwapo unataka twende pamoja, ingawa najua unataka, itabidi uamke mapema
sana; nataka kuka huko kabla ya sherehe hizo kuanza.
Nukta pacha/nukta mbili/koloni (:)
Hii ni alama ya kuakisha ambayo hutumika katika mazingira mbalimbali kama yafuatayo:
1. Kutanguliza orodha ya maneno. Kwa mfano:
(a) Tulipoka uwanjani tulikuta timu tatu zimewasili: AFC, Gor Mahia na Reunion.
(b) Kuna njia mbili tu za kufaulu maishani: bidii na nidhamu.
(ch) Mama amenunua matunda aina tatu: malimau, mapapai na machungwa.
2. Kutanguliza maelezo fulani. Kwa mfano:
(a) Mbwa walianza kubweka: lazima walikuwa na sababu.
(b) Nilipowasili nyumbani nilishtuka kweli: dadangu anayeishi Marekani alikuwa ame-
wasili.
(ch) Baada ya kufungua barua hiyo niliduwaa nisijue la kufanya: nilikuwa nimefutwa
kazi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 81 12/11/2019 09:44
82
3. Huweza pia kutumika hutanguliza usemi halisi. Kwa mfano:
(a) Mama alianza: Mimi sitaki kuwa ninarudia jambo moja kila siku na hakuna yule
anayetaka kunisikiliza.
(b) Kisha Rais akamaliza: “Yule asiyetaka kufuata sheria za nchi hii ajue serikali mkono
wake ni mrefu.
Mnyambuliko wa vitenzi
Neno mnyambuliko linatokana na kitenzi nyambua au nyumbua. Maana yake ni kuvuta au
kutanua kitu chororo ili kukirefusha. Kunyambua maneno ni kuyarefusha kwa kuyaongezea
viambishi. Kwa njia hii neno hupata maana mbalimbali. Kwa mfano: vya tukitaka kuunda maneno
ya kauli ya kutenda, kutendea au kutendewa, itabidi tuongeze viambishi aina mbalimbali katika
mizizi ya vitenzi vinavyohusika:
1. Kauli ya kutenda: Hii huwakilisha vitenzi katika hali ya kawaida. Kitenzi cha kauli hii huwa
mzizi na kiishio au kiambishi tamati bila ya kuongezewa viambishi vyovyote vingine.
Mifano:
acha, andama, apa, amua, cheza, beba, ona, soma, piga, pika, andika, koga n.k.
2. Kauli ya kutendea: Kiambishi kinachoonyesha hali ya kutendea au kufanyia huwa tofauti
kutegemea irabu iliyoko kwenye mzizi wa neno. Kwa mfano, ikiwa mzizi una irabu ya:{
a}, {i }na {u} na wenyewe unaishia na konsonanti, kiambishi cha kauli ya kutendea huwa
{i}. Mifano
piga................pig..................pigia
pika................pik..................pikia.
unda...............und................undia
kumba............kumb..............kumbia
aga..................ag..................agia
Ikiwa mzizi wa irabu una irabu {e} au {u} na unaishia na unaishia kwa konsonanti, kiambishi
{e} hutumiwa. Mifano:
choma.........chom..............chomea
gonga...........gong.................gongea
soma.............som...................somea
enda............end.......................endea
tema...........tem......................temea
Hali hii hubadilika ikiwa kiambishi cha mwisho cha mzizi ni irabu kama {e} au {o}. Hapo
kiambishi {le} hutumiwa. Mifano:
ondoa..............ondo.............ondolea
oa....................o...................olea
ongoa...............ongo.............ongolea
Hata hivyo, ikiwa mzizi unaisha kwa irabu {a}, {i} au {u} kiambishi hicho huwa {li}
kaa................ka................kalia
ania...............ani...............anilia (ania ni kusudia au dhamiria)
angua............angu............angulia
babadua........babadu.........babadulia (babadua ni tenganisha)
gua................gu................gulia (gua ni ondoa ganda la juu la tunda)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 82 12/11/2019 09:44
83
Kauli ya kutenda huwa na maana kadha:
(a) Kuonyesha kuwa kitendo kimefanyiwa mtu au watu.
(i) Juma alimpikia Maria chakula (Chakula kimepikwa kwa ajili ya Maria).
(ii) Mafamba aliniandikia barua. (Mafamba ameandika barua kwangu).
(b) Kuonyesha nia ya kuelekea kwenye mtu au watu, kitu au vitu.
(i) Watoto walimkimbilia mama yao.
(ii) Wezi walitorokea porini.
(ch) Kuonyesha kilichotumika kufanyia kitendo.
(i) Yeye alisaria basi. (alitumia basi kusari)
(ii) Tuliabiria ndege. (Tulitumia ndege kuabiri)
(d) Kitendo kimefanywa kwa niaba ya mtu.
(i) Mwalimu mwenza alimfundishia darasa hilo. (Yaani alifundisha darasa kwa niaba
yake).
(ii) Alinitolea udhuru kwenye mkutano. (Alitoa udhuru kwa niaba yangu).
3. Kauli ya kutendewa: Hii hutumiwa kuonyesha mtu au kitu kinachopokea kitendo kama
vile kitendo kimeelekezewa mtu au watu. Viambishi vinavyotumiwa hapa ni {iw}, {ew},
{liw} na {lew}. Kama tulivyoona hapo, hutegemea irabi zilizopo kwenye mzizi au jinsi
mzizi wenyewe unavyoisha (kama una irabu au la)
(i) Wanafunzi walitambiwa ngano na mwalimu. (Mzizi ni tamb’)
(ii) Meno yake yote yameng’olewa. (mzizi ni ngoa’)
(iii) Amepikiwa chakula. (mzizi ni pik’)
(iv) Chumba kimeandaliwa. ( mzizi ni anda’)
Mzizi Kauli ya kutenda Kauli ya kutendea Kauli ya kutendewa
-pig- pig-a pig-i-a pig-iw-a
-pik- pik-a pik-i-a pik-iw-a
-omb- omb-a omb-e-a omb-ew-a
-chor- chor-a chor-e-a chor-ew-a
-imb- imb-a imb-i-a imb-iw-a
-ruk- ruk-a ruk-i-a ruk-iw-a
-jeng- jeng-a jeng-e-a jeng-ew-a
-fag- fagi-a fagi-li-a fagi-liw-a
-andik- andik-a andik-i-a andik-iw-a
Zoezi
Andika vitenzi vifuatavyo vilivyo katika kauli ya kutenda ili viwe katika kauli ya kutendea na
kutendewa.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 83 12/11/2019 09:44
84
Kauli ya kutenda Kauli ya kutendea Kauli ya kutendewa
k.m. som-a
to-a
chinj-a
sugu-a
lim-a
kop-a
kat-a
chimb-a
chagu-a
chez-a
chom-a
som-e-a
som-ew-a
Geuza kitenzi kilichomo mabanoni kulingana na kauli uliyopewa.
(a) Mwalimu alitu _____________ (soma, tendea) hadithi.
(b) Wanafunzi wali ____________ (jenga, tendewa) maktaba na waziri.
(ch) Odhiambo alini ____________ (tupa, tendea) mpira.
(d) Mwanaisha ata ____________ (leta, tendewa) nguo nzuri na dadake.
(e) Mkaza mjomba atani _________ (pika, tendea) pilau.
(f) Ng’ombe wali _______________(kama, tendewa) maziwa na mtoto yule.
(g) Nyanya ana ________________ (fagia, tendewa) nyumba na Ethuro.
(h) Cheupe ana _______________ (andika, tendea) Boke barua.
(i) Mama ame __________________ (pata, tendewa) pesa na baba.
D. Kusoma
Kusoma kwa kina: Utangulizi
Usomaji wa kina ni usomaji wa ndani au wa kuchunguza mambo yaliyochwa na ya ndani. Kila
tunaposoma kitabu cha hadithi au mchezo wa kuigiza au shairi hufurahia kuijua hadithi hiyo.
Lakini ili tuweze kufaidi vizuri, tunalazimika kuchunguza mambo ya ndani. Mambo haya ni
kujiuliza hadithi hiyo inahusu nini hasa? Je, imeundwa namna gani? Je, ina ujumbe gani? Je,
ina mafunzo gani?
Hadithi yoyote au shairi lolote huwa na umbo la nje na umbo la ndani. Umbo la nje ni jinsi
linavyoonekana, na umbo la ndani ni yanayozungumziwa. Kitabu cha hadithi huwa na mambo
mawili makuu ambayo tunaposoma tutayazingatia: fani na maudhui.
Fani ni neno linalotumiwa kuelezea njia au nyenzo inayotumiwa kuwasilisha jumla ya mambo
yanayozungumziwa, yaani maudhui. Ni kama mtu anayetaka kutayarisha wali, atahitaji sufuria,
mchele, maga n.k. Wali wake ni maudhui na sufuria, maji na maga ni fani. Bila fani maudhui
hayapatikani; yaani vinategemeana; kila kimoja ni muhimu. Fani hujumlisha:
(a) Matumizi ya lugha
Mpangilio wa maneno, tamathali za usemi kama tashibiha au ujenzi wa picha. Uteuzi wa
tamathali unategemea na unahusiana na maudhui.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 84 12/11/2019 09:44
85
(b) Muundo
Je, kitabu unachosoma kina muundo wa aina gani? Je, hadithi yenyewe inakwenda moja
kwa moja au ni tofauti. Je, hadithi fulani ina sifa gani za lugha?
(ch) Wahusika
Hawa ni wale watendaji wanaopatikana katika hadithi, yaani viumbe wanaotenda matendo
mbalimbali ambao wanaweza kuwa binadamu au wanyama.
E. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Barua
Barua ni ujumbe unaopelekwa kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine kwa maandishi yenye
muundo fulani maalum. Barua huandikwa kwa ajili ya kujulisha, kufahamisha, kueleza, kuomba
msaada fulani, kuomba kazi n.k. Huu ndio unaojulikana kama uamilifu wake au utenda kazi
wa barua. Tunaweza kuandika barua kwa watu tunaojuana nao kama ndugu, maraki au jamaa.
Barua za aina hii hujulikana kama barua za kiraki au kidugu. Inawezekana tukaandika barua
kwa watu wasiokuwa jamaa, maraki au ndugu, kwa mfano:, kuomba kazi, kutoa malalamiko
fulani kutafuta usaidizi n.k. Hizi hujulikana kama barua rasmi au za kiosi.
Sifa za barua za kiraki
Huandikiwa maraki, wazazi, ndugu na jamaa.
Mwandishi ana uhuru mkubwa katika matumizi ya lugha.
Lugha inayotumiwa hutegemea uhusiano uliopo kati ya mwandishi wa barua na
anayeandikiwa barua hiyo.
Mwandishi ana uhuru wa kuandika barua yenye urefu anaoutaka.
Muundo wa barua ya kiraki
Barua ya kiraki huwa na:
1. Anwani ya mwandishi.
2. Tarehe ya kuandikwa kwa barua- iandikwe pale juu pembeni, upande wa kulia.
3. Mwanzo wa barua- aghalabu huwa/huitwa mtajo.
4. Kiini cha barua.
5. Hitimisho la barua.
6. Jina la mwandishi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 85 12/11/2019 09:44
86
Muundo kimchoro
Anwani ya mwandishi
Tarehe ya kuandikwa
Mwanzo wa barua/Mtajo
Kiini/ujumbe wa barua
Mwisho/uhitimisho wa barua
Jina la mwandishi
Mfano wa barua ya kiraki
Shule ya Upili ya Kijembe,
S. L. P 45591,
Maji Mazuri.
13- 6-2018
Raki mpendwa,
Pokea salamu nyingi kutoka kwangu huku nikitumai kuwa u mzima na buheri wa afya.
Huku mjini hatuna neno, shughuli za kikazi pamoja na harakati za huku unazozifahamu tu. Hivi
sasa baridi ya mwezi wa saba, yaani kipupwe, imeanza kusogea na kutulazimisha kujivika maguo
mazito mazito.
Nia hasa ya kukuandikia barua hii ni kukujulisha kuwa mwezi wa nane nitapata likizo fupi
ya wiki mbili. Ninadhamiria kuandamana na jamaa yangu hadi nyumbani. Watoto wamekazania
kumwona nyanya yao na nadhani hii ni fursa nzuri. Ninakusudia kukitumia kipindi hicho
kumalizia ule ununuzi wa ile ploti huko nyumbani ili ikapo Disemba, tukijaliwa, nianze shughuli
za ujenzi. Nakuomba basi uwasiliane na mwenye ploti kwa niaba yangu na kisha unipe taarifa
kamili.
Nitaisubiri barua yako kwa hamu kuu. Nisalimie jamaa huko nyumbani.
Ni mimi wako,
Jumakoshi.
Zoezi
1. Andika barua kwa mzazi au mlezi wako ukimjulisha jinsi unavyoyaona masomo ya kidato
cha kwanza.
2. Andika barua kwa raki yako ukimjulisha maendeleo yako shuleni.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 86 12/11/2019 09:44
87
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3 4 5 6 7
8
9
10
11 12 13
14 15 16
17
18
19
20
KULIA
3. Rada
5. Kupimana uwezo, nguvu au uhodari
8. Wivu
9. Ujanja unaofanywa katika utendaji wa kitu au jambo ili kucha ukweli
12. Kuwa karibu na
14. Mtu anayetoa hotuba
16. Shughuli za kiuchumi, kisiasa na kijamii za kunufaisha watu
17. Kitu cha kuonyesha ukweli
18. Enda na isionekane
19. Kinyume cha uongo
20. Hutolewa na hatibu
CHINI
1. Mahali wafungwa hukaa
2. Wanaosikiliza
4. Huzalishwa kulingana na mvuke, maji au upepo
6. Ukemi
7. Shairi la majibizano baina ya watu wawili au zaidi
10. Wanaolinda usalama
11. Tunaweza
13. Tamka
15. Mahali jua huchomozea
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 87 12/11/2019 09:44
88
Zoezi la Marudio I
A. Ufahamu
Uzuiaji wa uhalifu ni bora kuliko tiba
Asilimia kubwa ya mataifa ya ulimwengu yamekia ngazi za juu katika maendeleo ya afya ya
umma katika miaka thelathini iliyopita. Kuna sababu nyingi ambazo zimesababisha hali hii.
Moja kati ya sababu hizi ni kuwako kwa ufahamu wa kina kuhusiana na magonjwa na vyanzo
vyake. Pili, kuwako kwa njia wazi za utambuzi wa makundi yanayoathirika na magonjwa fulani.
Tatu, utekelezaji na usambazaji wa maarifa pamoja na uhamasishaji wa makundi yanayohusika
kubadili tabia zao au kuchukua hatua bora za kiafya. Msemo wa kuwa ni heri kuzuia kuliko
kutibu umekuwa nguzo kuu ya matendo hayo.
Hata hivyo hali kama hii haionekani kuhusiana na suala la usalama wa umma. Katika miji
mingi ulimwenguni, hususan ile mikubwa, viwango vya uhalifu vimepanda. Ghasia zinazohusiana
na vijana, ukosefu wa usalama kwa watoto na wanawake, wizi wa magari, uvunjaji wa nyumba,
utumiaji wa nguvu, wizi wa mabavu na ukosefu wa usalama kwa jumla, yamekuwa matatizo
sugu. Je, ni kwa nini hali ikawa mbaya kiasi hiki?
Hali hii inatokana na mambo mengi. Mojawapo ni upungufu wa njia asilia za kuukabili
uhalifu kama polisi, mahakama na magereza. Pili, ni kutochunguza na kujaribu kusuluhisha
matatizo ya kimsingi yanayochangia kuwako kwa uhalifu.
Usalama wa umma ni moja kati ya vigezo vya kimsingi vya maisha bora pamoja na maendeleo
ya kijamii na kiuchumi. Usalama huu unapaswa kuzingatiwa kama msingi muhimu na kila
mwanajamii ana jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa umepatikana. Suala la uhalifu sio suala la
polisi na mfumo wa utendaji haki tu. Ili kufanikiwa katika uzuiaji wa uhalifu, lazima washika
dau wote wahusike katika suala hili. Je, ni mambo gani tunayopaswa kufanya ili tuzuie uhalifu?
Kwanza, pana haja kubwa ya kuchunguza na kuielewa barabara misingi ya uhalifu na ghasia
za mijini. Baada ya kuchunguza pana haja ya kuchukua hatua zitakazosaidia kupunguza idadi
ya waathiriwa na jamii ya wahalifu mijini. Hatua hizi ni kama kuwako kwa muundo mzuri na
salama wa miji, kusaidia watoto na jamaa zisizokuwa na uwezo, kuhimiza uwajibikaji wa jamii,
kuzalisha kazi za kuwaajiri vijana, kuhakikisha baadhi ya huduma kama za polisi na utekelezaji
wa haki zimetegemezwa kwenye jamii, kuwawezesha wahalifu kuyarudia maisha ya kawaida na
kuwasaidia waathiriwa wa uhalifu.
Pili, njia za kuzuia uhalifu lazima zihusishe sehemu zote za jamii kama polisi, mfumo wa
utendaji haki, huduma za kiafya na kijamii, huduma za makazi, sekta ya kibinafsi na mashirika
ya umma.
Uzuiaji wa uhalifu unachangia kuleta umoja, ushirika wa raia na utawala ufaao. Unachangia kwa
kiasi kikubwa katika ukuzaji na uendelezaji wa taasisi za kidemokrasia, uwajibikaji wa huduma
za umma kama polisi na mfumo wa utendaji haki. Kama ilivyo kuhusiana na ugonjwa ni heri
kuzuia kuliko kutibu. Vivyo hivyo, uzuiaji wa uhalifu ni bora kuliko kuukabili na kuutibu uhalifu
wenyewe.
Maswali
1. Ni kwa nini maendeleo ya afya ya umma yameimarika? Toa sababu tatu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 88 12/11/2019 09:44
89
2. Kulingana na kifungu taja uhalifu aina tatu unaothibitisha kwamba hali ya usalama ni
mbaya.
3. Jamii inafaa kufanya nini íli kushiriki katika kulinda usalama wao?
4. Onyesha maana ya maneno haya kwa kuyatumia katika sentensi.
(a) umma (b) hususan (ch) matatizo sugu
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Eleza maana ya:
(a) kiimbo
(b) shadda
2. Onyesha shadda katika maneno yafuatayo. Kwa mfano: limau, chere’hani
(a) kitabu (b) mama
(ch) maharagwe (d) mashairi
3. Andika konsonanti mbili zinazotamkwa katika viungo vifuatavyo vya kutamkia:
Kwa mfano: uzi - n, t
(i) midomo (ii) uzi
(iii) kaakaa laini (v) kaakaa gumu
CH. Saru na matumizi ya lugha
1. Tenganisha viambishi katika maneno yafuatayo:
Kwa mfano: anayeleta - a-na-ye-let-a
(a) atakupiga (ch) nilimsaidia (e) tunaimba
(b) uliyemleta (d) kilichoanguka
2. Tenganisha maneno yafuatayo ili kuonyesha viambishi awali, mzizi na viambishi tamati.
Neno Viambishi awali Mzizi Viambishi tamati
k.m. anamsomesha
tulilolipenda
alinitilia
umefungika
nitamfagilia
wanaopendana
a-na-m
som
e-sh-a
3. Tumia heru kubwa panapofaa.
(a) bwana khamisi amekwenda kwale kumtembelea mogaka.
(b) kwa nini miji ya nakuru, mombasa na kisumu ina watu wengi hivyo?
(ch) sikukuu ya madaraka nilikwenda meru kumwona nteere naye akasema atakuja
kuniona pamoja na mkewe maria sikukuu ya jamhuri.
(d) mimi ninapenda somo la hisabati lakini dadangu rehema anapenda somo la kiswahili.
(e) shule zilifunguliwa mwezi wa januari kisha zikafungwa mwezi wa machi na kufun-
guliwa tena mwezi wa mei.
4. Andika maneno mengine matatu yanayoweza kujengwa kwa kubadilisha sauti moja tu
katika kila neno lifuatalo: k.m. pua - paa, dua, pia
(i) taa (ii) tai (iii) baba (iv) kuta
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 89 12/11/2019 09:44
90
5. Ni nini wajibu mkuu wa lugha katika jamii?
6. Mwanafunzi mmoja alipoambiwa aorodheshe heru za alfabeti ya Kiswahili aliandika
hivi: a, b, c, d, e, f, g, h, i, j, k, l, m, n, o, p, q, r, s, t, u, v, w, x, y, z. Je alifanya makosa gani?
7. Kivumishi ni nini?
8. Onyesha kivumishi katika sentensi zifuatazo.
Kwa mfano: Watoto wazuri wanasoma darasani.
(a) Mtu mrefu ameshinda mbio hizo.
(b) Wachezaji hodari wameka.
(ch) Wazee watano watakata kesi hii.
(d) Mji mkubwa utajengwa wilayani mwetu.
(e) Mashamba mengi yatalimwa mwaka ujao.
(f) Mama ameninunulia viatu vyekundu.
(g) Matunda matano yameliwa na wanafunzi.
(h) Ni mwalimu yupi aliyekuja?
(i) Mpira mpya umepotea.
(j) Meza hii ni ya babu.
9. Weka alama ya kikomo au koma panapofaa katika maandishi yafuatayo.
(a) SLP 189 NAKURU
(b) Dkt Mumbo
(ch) Bw Koskei
(d) Shangazi amekwenda mjini
(e) Jana tulifanya mtihani wa Kiswahili
10. Weka alama ya kituo/koma mahali pafaapo katika sentensi zifuatazo.
(a) Nyanya amenunua kabeji kitunguu saumu mchicha na sukumawiki.
(b) Mwalimu wetu wa zaraa alitwambia tuje na jembe panga reki na uma.
(ch) Paul Kimanzi mwanafunzi shupavu aliyeshinda mtihani wa kidato cha nne wa mwaka
jana amejiunga na Chuo Kikuu.
(d) Mama sahani na sufuria ziko wapi?
(e) La hakusema atakuja kesho.
11. Onyesha viwakilishi katika sentensi zifuatazo.
(a) Huyu analia.
(b) Yule na huyo wamemaliza kazi yao.
(ch) Unataka gani?
(d) Alitaka vingapi?
(e) Umemlipia yupi?
12. Geuza sentensi zifuatazo ili ziwe katika wakati uliopo.
(a) Mbuzi na kondoo wengi waliuzwa.
(b) Nyumba hiyo itafagiliwa.
(ch) Mwalimu wetu atatupatia kazi ya kufanya.
(d) Lumumba atavuna mazao mengi.
(e) Mwasimba aliimba wimbo mtamu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 90 12/11/2019 09:44
91
13. Kanusha sentensi zifuatazo.
K.m. Mimi ninacheza mpira. - Mimi sichezi mpira.
(a) Kioko anatangaza habari.
(b) Nyinyi mnaandika barua.
(ch) Yeye anachunga mbuzi wao.
(d) Sisi tunatembea.
(e) Mama anatuchemshia maji ya kunywa.
(f) Wao wanapiga kelele.
(g) Wanasiasa wanahutubu uwanjani.
(h) Mimi ninataka kulala.
14. Onyesha kitenzi katika sentensi zifuatazo.
K.m. Mimi ninaandika insha.
(a) Dereva anaendesha lori kubwa.
(b) Shangazi anapika pilau.
(ch) Wazazi watakutana shuleni.
(d) Muindi anafanya nini?
(e) Kakangu amechora picha nzuri.
(f) Nyumba hii itaanguka.
(g) Wakulima wamepanda mahindi mengi.
(h) Gari hili lilinunuliwa jana.
15. Andika sentensi hizi katika wakati uliopita.
(a) Dadangu anasoma.
(b) Mlinzi atakukataza kuingia.
(ch) Mwajuma analima kondeni.
(d) Mtoto analala.
(e) Koti hili litafuliwa na kakangu.
(f) Shati hili linahitaji kupigwa pasi.
(g) Rehema anakwenda wapi?
(h) Nyumba hii itafagiliwa.
16. Kanusha sentensi zifuatazo.
(a) Nyinyi mlihitajika na mwalimu.
(b) Karauri aliwaongoza wanafunzi.
(ch) Wewe ulimwadhibu mwanangu.
(d) Wazee walikopa pesa nyingi.
(e) Binamu yangu alisari ngambo.
(f) Mtoto alilia sana.
17. Onyesha vielezi katika sentensi zifuatazo.
K.m. Jua limewaka sana.
(a) Mama amepika chai tamu sana.
(b) Shule yetu ina wanafunzi wengi mno.
(ch) Alibeba mzigo huo vipi?
(d) Alinichapa ko mara mbili.
(e) Nitakutembelea kesho jioni.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 91 12/11/2019 09:44
92
18. Andika sentensi zifuatazo katika wakati ujao.
(a) Mpwa wangu anafua nguo zake.
(b) Mjukuu wake aliondoka.
(ch) Brian alinunua pikipiki.
(d) Kitabu hiki kinapendeza.
(e) Jua linawaka sana.
(f) Mto ulifurika.
(g) Wanafunzi wanaimba.
19. Kanusha sentensi zifuatazo:
K.m Mjomba ataondoka kesho.
Mjomba hataondoka kesho.
(a) Mureithi atasoma kitabu.
(b) Waziri atawasaidia wanafunzi.
(ch) Aoko atafaulu mtihani.
(d) Fahali atachinjwa kesho.
(e) Dadangu atakuja.
D. Kusoma
1. Taja aina nne kuu za maktaba.
2. Maktaba ni muhimu sana kwa mwanafunzi. Toa sababu tatu kuu kueleza umuhimu wa
maktaba kwa mwanafunzi.
E. Kuandika
1. Andika barua kwa mwalimu wako wa zamani ukimweleza jinsi unavyoendelea na masomo
katika shule ya upili.
F. Isimujamii
Fafanua mambo mbalimbali yanayoongoza matumizi ya lugha katika miktadha mbalimbali
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 92 12/11/2019 09:44
93
A. Ufahamu
Si maradhi ni kumbakumba
Kwa kipindi kirefu katika kijiji cha Limbukeni, ugonjwa wa pekee uliowatisha watu ni ukoma.
Ulikitawala kijiji hicho kwa miaka mingi kabla ya maendeleo ya sayansi kuuwahi. Miaka na dahari
imepita tangu mgonjwa wa mwisho kuugua ugonjwa huo. Sifa za ugonjwa wenyewe ziliendelea
kuwako. Lakini haya yote yalibadilika siku moja baada ya kifo cha Mkota.
Mkota alisiwa sana kijijini kwa kuwa mwanakijiji wa kwanza kusoma mpaka akaenda
ngambo. Aliporudi alipata kazi jijini Nairobi. Lakini hakusahau kijiji chao cha Limbukeni. Watu
wa Limbukeni walidai kuwa wale wote walioelimika wakienda jijini Nairobi walizamia huko zii.
Yaani, walikwenda kukaa bwete. Kwa sababu hiyo walilibadilisha jina la Nairobi; likawa Kibwete.
Mkota basi hakutaka kuzamia Kibwete.
Mkota alirudi kijijini akajenga nyumba nzuri na ya kusiwa. Isitoshe, aliwasaidia wanakijiji
kujenga shule nzuri ya msingi na kuanzisha jengo la kituo cha afya au zahanati. Baadaye alioa na
kumwacha mkewe akifanya kazi ya kuliendeleza shamba lao la ekari kumi na mbili alilonunua
hapo karibu na jengo jipya la shule. Mara kwa mara alirudi kumjulia hali mkewe na watoto na
pia kukagua hali ya shamba lake na jengo la zahanati. Mambo yalikwenda sawa hadi habari za
kuugua kwa Mkota zilipoka kijijini. Ilisemekana kuwa alikuwa na maradhi ya homa ya mbu.
“Unajua kuwa anazungukazunguka jioni kupunga hewa kama wafanyavyo huko ng’ambo, lazima
ameumwa na mbu, walisema waliosikia. Hali ya Mkota iliendelea kuwa mbaya. Waliokwenda
kumtembelea walirudi na habari nyingine. “Mkota anakohoakohoa sana, walisema. “Basi lazima
ni vumbi la huku. Mwenzetu kazoea kuishi ng’ambo kusikokuwa na hata vumbi!” alisema mmoja.
“Hapana ni kifaduro!” alibisha mwingine.
“La. Kifaduro ni ugonjwa wa watoto!” alisema mwingine.
“Labda ni mkamba au kimambe, maana nasikia kupumua kunamtatiza, akasema kijana
mmoja.
Wanakijiji waliendelea kumwombea Mkota apone haraka awasaidie kumalizia lile jengo la
kituo cha afya. Lakini badala ya kupata habari njema za kupona kwa Mkota, habari nyingine
zikaka kijijini kuwa Mkota alikuwa akisumbuliwa na vidonda na majipu mengi. Unajua hata
babu yake alikuwa na ugonjwa huo, alisema mzee mmoja aliposikia habari hizo. Baadaye zikaja
habari nyingine. “Mkota amebebwa kwa machela, sasa yuko hospitalini, kinywa kimejaa vidonda
na nywele zinamnyonyoka, waliambiwa watu. Amerogwa na watu wanaomwonea wivu, alisema
mzee mwingine. Baada ya mwezi mmoja, Mkota yuko chumba cha wagonjwa mahututi.”
Hali iliendelea hivyo hadi Mkota akaaga dunia na kuzikwa pale kijijini. Kifo cha Mkota
kiliwashtua watu wote kijijini Limbukeni. Huo ulikuwa msiba mkubwa mno kwao. Jengo la
zahanati lilikuwa bado pale pale, halijakamilika.
Miezi michache baada ya Mkota kuaga dunia, mke wake naye alianza kuugua. Hatua za
ugonjwa wake zilikuwa zile zile tu. “Ni kihoro baada ya kifo cha mumewe, walisema watu.
Muda mfupi baadaye mke wa Mkota naye akaaga dunia. Huyo alifuatiwa na wanakijiji wengine
wanne. Mmoja alikuwa mwanamke wa makamo aliyesemekana kuwa raki yake marehemu
Mkota. Huyu alikufa akifuatiwa na mumewe. Mwingine alisemekana kuwa raki yake marehemu
mkewe Mkota. Naye alifuatana na mkewe. Haya si maradhi ni kumbakumba, alisema Domeniko
Sura ya Tisa
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 93 12/11/2019 09:44
94
Mhenga, mzee aliyeheshimiwa sana kijijini Limbukeni.
Sasa wanakijiji walikuwa wameduwaa. Je, ukoma umerudi tena nini?” waliulizana.
Ulikuwa wakati huu serikali ilipojitolea kulimaliza lile jengo la zahanati. Muda mfupi baadaye
aliletwa daktari wa kwanza kijijini, kijana mcheshi aliyejulikana kama Mvita Mjuzi. Siku alipoka
kijijini kila mtu alifurahi. Watu kijijini walikuwa bado wanakufa kutokana na ugonjwa huo wa
ajabu. Sasa hivi kila mtu alikuwa akisema kama mzee Mhenga: Si maradhi ni kumbakumba!”
Siku ya pili baada ya daktari kuwasili, wanakijiji waliamua kuongozana hadi kwa Daktari Mvita
Mjuzi kumweleza kila kitu kuanzia utandu mpaka ukoko. Daktari aliwasikiliza kwa makini.
Walipomaliza alisimama na kusema, Kwa mujibu wa maelezo yenu, dalili za ugonjwa huu
ni ukosefu wa hamu ya chakula. Ukikosa hamu ya chakula, mwili wako unaathirika kwa sababu
ya kukosa lishe muhimu. Si ajabu basi kuwa mgonjwa anaishia kukonda sana. Dalili nyingine
ni kuendesha kwa kipindi kirefu, alisema daktari na kutulia akiangalia karatasi yake. Baada ya
muda aliendelea, “kisha mgonjwa anakuwa na uvimbe shingoni.
“Ehh kama mgonjwa wa rovu, alisema kijana mmoja. Daktari aliitikia halafu akaendelea,
mgonjwa pia anasumbuliwa na kikohozi kikavu tu. Anakuwa na udhaifu wa mwili, anatokwa
na jasho jingi hasa usiku, na hutapika mara kwa mara. Mwisho ni kuwepo kwa vidonda kwenye
sehemu za siri na kinywani, alisema Mvita Mjuzi.
“Kumbe hata wewe unajua? Mbona hukuletwa mapema kututatulia janga hili?” aliuliza mzee
mwingine.
“Ugonjwa huu jamani ni Ukimwi, alisema daktari.
“Ukimwi? alishangaa kijana mmoja.
“Ehh unaitwa Ukimwi na ni ugonjwa mbaya unaoweza kuambukizwa kwa njia mbalimbali
hasa kwa kuhusiana kimwili au kwa kupokea damu yenye virusi, alieleza daktari.
“Je, ni mbaya kama ukoma?” aliuliza mzee mmoja aliyekula chumvi nyingi.
“Huu ni ugonjwa mbaya zaidi na hauna tiba, alisema daktari Mvita Mjuzi. Ukimya mkubwa
ulifuatia. Kisha daktari akaendelea kuwapa wanakijiji mashauri mengi kuhusu adui huyu Ukimwi.
Aliwanasihi jinsi ya kujikinga wasiambukizwe virusi vya ukimwi. Aidha aliwarai kuwa
wanapoambukizwa, wasichelee kutembea kutembelea vituo vya afya kwa nasaha na ushauri.
“Kupata ukimwi si huku ya kifo!” alishauri. Aliwakumbusha kuwa kuna dawa za kupunguza
makali ya ugonjwa wenyewe. Isitoshe, wapo wengi walioathirika na ambao bado wanaishi kwa
sababu ya kutumia dawa, kuzingatia lishe inayofaa na kujitunza. Vilevile aliwatahadharisha dhidi
ya kuwanyanyapaa walioambukizwa ukimwi. Aliwakumbusha methali ya Kiswahili isemayo,
hujafa hujaumbika.
Tangu siku hiyo, wanakijiji waliamua kushirikiana na daktari wao mpya kuyasambaza
maarifa kuhusu ugonjwa huu kila mahali: shuleni, michezoni, mabarazani na majumbani.
Walikumbushana si maradhi ni kumbakumba.
Maelezo ya msamiati
kukaa bwete : kukaa bila kazi.
siwa ghaya : siwa sana.
duwaa : shangaa; pumbaa.
kumbakumba : hali ya kukusanya bila kubakisha.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 94 12/11/2019 09:44
95
Maswali
1. Ni kwa nini wana kijiji cha Limbukeni waliliita jiji la Nairobi ‘Kibwete’?
2. Mkota hakutaka kupotelea Kibwete. Alifanyaje ili kuinua hali ya maisha yake binafsi na
ya wanakijiji wenzake?
3. Mkota alipoanza kuugua, watu wengi hawakufahamu anaugua ugonjwa gani. Ni mambo
gani yanayodhihirisha hayo?
4. Unakiri watu waliokufa baada ya Mkota waliupataje ugonjwa huu?
5. Panga matukio yafuatayo kwa utaratibu ufaao tangu mwanzo hadi mwisho.
(a) Mkota aaga dunia.
(b) Mkota ajenga jumba la aushi.
(ch) Mkota aenda ng’ambo kwa masomo.
(d) Mkewe Mkota aaga dunia.
(e) Daktari Mvita Mjuzi aletwa kijijini.
(f) Mkota abebwa kwa machela.
(g) Rakiye mkewe Mkota aaga dunia.
(h) Serikali yamaliza kujenga zahanati.
(i) Daktari awaeleza watu kuhusu ugonjwa uliowasumbua.
(j) Mkota aoa.
6. Tumia maneno haya kwenye sentensi ili kuonyesha maana yake.
(i) kuanzia utandu mpaka ukoko (ii) maarifa
(iii) kihoro (iv) miaka na dahari
(v) kuuwahi (vi) zahanati
(vi) majipu (vii) wagonjwa mahututi
7. Wana-Limbukeni waliamini kuwa watu waliosoma walizamia Nairobi zii. ‘Kuzama zii
ni mfano wa tanakali sauti. Chagua jibu mwafaka kukamilisha tanakali za sauti zifuatazo:
zii, twaa, gubigubi, tumbwi, chiriri, fofofo, chepechepe, ndi, ndindindi, tititi
(a) Watetu ni msichana mweusi ________.
(b) Fisi alipigwa hadi akafa ________.
(ch) Nilipomwona mama nilijifunika ___________.
(d) Babu alinyeshewa akalowa ___________.
(e) Nilipowaona wezi nilifunga mlango __________.
(f) Jiwe lilitumbukia mtoni __________.
(g) Daktari Mvita alipoongea tulitega masikio __________.
(h) Baada ya kunyimwa pesa machozi yalimtiririka ________.
(i) Barabara ya kwenda Kisumu imenyooka __________.
(j) Meli ilizama baharini _________.
8. Haya ni magonjwa gani?
(i) ukoma (ii) kipindupindu (iii) tauni
(iv) surua/ukambi (v) ukimwi (vi) kifaduro
(vii) kimambe (viii) rovu (ix) tetewanga
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 95 12/11/2019 09:44
96
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora-Vitate: ch/sh
Tamka maneno haya:
ch sh
chaka shaka
chali shali
chati shati
choka shoka
chombo shombo
Soma: Vitanza ndimi
(a) Bwana Mashaka wa Chakani alikuwa na mashaka kwa kuishi kwenye chaka lenye mashaka
kutokana na baridi.
(b) Baada ya kuifua shati ya Chalo, Mwachali alilala chali.
(ch) Yule Chalo chali hangeweza kwenda Chale anapoishi Mwashali ili wakavue chale.
(d) Mchati alichachama kisha akachechemea kwa kuwekewa masharti anunue chati ingawa
alitaka shati peke yake tu.
(e) Ingawa Achoka alikuwa amechoka alikwenda Chuka kuomba shoka kwa Machoka na
alipoka Chuka akamkuta Machoka lakini Machoka hakumpa shoka.
(f) Nilimuuliza Bwana Chembe kwa nini ananuka shombo akasema yeye hunuka shombo
kwa vile hutumia chombo kupikia samaki na chombo kikipikiwa samaki hakiachi kunuka
shombo.
Sajili ya dukani
Sajili ya dukani ni matumizi ya lugha katika muktadha wa madukani. Hii inaweza kuangaliwa
kama sehemu ya sajili pana ya biashara. Neno biashara ni pana na huwa na miktadha tofauti
tofauti. Kwa msingi huu basi kuna sajili nyingi na tofauti. Sajili hii ina sifa maalum
(a) Pana matumizi ya msamiati maalum. Msamiati huo unarejelea shughuli inayoendeshwa
dukani. Msamiati huu unaweza kuhusu bidhaa zenyewe k.v. sukari, chumvi, n.k.
Wanaohusika katika shughuli yenyewe kama vile mnunuzi/muuzaji, mwenye duka n.k.
(b) Matumizi ya sentensi fupi fupi. Mteja atasema anachohitaji na muuzaji kujibu bila ya
kuhangaika.
(ch) Muundo wa maswali na majibu. Mnunuzi au mshitiri anauliza anachokitaka, bei au hata
punguzo la bei na muuzaji naye anajibu swali analoulizwa
(d) Huweza kuwepo na matumizi ya lugha ya kushawishi. Kwa mfano, ikiwa muuzaji hana
bidhaa fulani na anataka kumshawishi mnunuzi kununua bidhaa mbadala au iliyoko.
(e) Matumizi ya viziada lugha. Si ajabu kuona matumizi ya ishara mbalimbali kama njia ya
kuwasiliana k.v. kuashiria ilipo bidhaa, kuitikia kwa kichwa au kukataa kwa ishara ya
kichwa n.k.
(f) Kuwepo kwa utohozi au msamiati unaotokana na lugha nyingine k.v. kastoma badala ya
mteja n.k.
(g) Matumizi ya vihisishi au maneno ya kuonyesha mshangao aghalabu kuhusu bei ya bidhaa
au gharama ya maisha n.k.
(h) Maongezi yanayogusia hali ya maisha au mazingira katika jamii au muktadha fulani.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 96 12/11/2019 09:44
97
Soma kifungu kifuatacho halafu ujibu maswali yanayofuatia
M (): H 
M: S.
M: N  
M: N   ,      .
M: N 
M: H.... () N    .
M: S
M: P  
M: (A) S     .
M: L M   H    . V
,  ,      . T
  (A )
M: H   . N     ..
W    . (A )
H    ...
M: (A ) M ....A 
M: A .
Maswali
1. Bainisha sajili ya mazungumzo haya.
2. Eleza sifa za sajili hii kwa kutumia mifano kutoka kwenye kifungu ulichokisoma.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Hali ya me
Kiambishi me huonyesha kuwa kitendo kimetimilika kabla ya kutolewa kwa taarifa na matokeo
yake yangali yanadumu; kwa mfano:
(a) Mama amepika pilau.
(b) Baba ameniletea zawadi.
(ch) Mti umeanguka barabarani.
(d) Karauri amefagia nyumba ya nyanyake.
(e) Waziri mkuu amewasili nchini.
Zoezi A
Geuza sentensi hizi ziwe katika hali ya ‘me.
(a) Shemeji yangu anapika viazi.
(b) Waithaka alikwenda Nakuru.
(ch) Mtangazaji atasoma habari hii.
(d) Siafu walimuuma mwanangu.
(e) Redio hii ilinunuliwa Meru.
(f) Karisa atatangaza msimamo.
(g) Koome anasoma kitabu cha Historia.
(h) Karani aliniandikia barua.
(i) Batamzinga anataga yai.
(j) Abdi alifungwa gerezani.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 97 12/11/2019 09:44
98
Kukanusha hali ya ‘me kulingana na nafsi
Tazama jedwali lifuatalo:
Umoja Wingi
nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
nimeruka sijaruka
nimekopa sijakopa
nimepewa sijapewa
nimefaidi sijafaidi
tumeruka hatujaruka
tumekopa hatujakopa
tumepewa hatujapewa
tumefaidi hatujafaidi
nafsi ya pili
umeruka hujaruka
kopa hujakopa
hujapewa mmepewa
mmefaidi hamjafaidi
mmeruka hamjaruka
mmekopa hamjakopa
mmepewa hamjapewa
mmefaidi hamjafaidi
nafsi ya tatu
ameruka hajaruka
amekopa hajakopa
amepewa hajapewa
amefaidi hajafaidi
wameruka hawajaruka
wamekopa hawajakopa
wamepewa hawajapewa
wamefaidi hawajafaidi
Zoezi B
Kanusha sentensi zifuatazo.
(a) Amoit ameruka mbali.
(b) Ndege ametua mtini.
(ch) Kakangu ameimba wimbo mtamu.
(d) Mwalimu amemwokoa Mwakio.
(e) Nyinyi mmetumwa sokoni.
(f) Sisi tumefurahi kwa kupita mtihani.
(g) Wale watu wamelima shamba vizuri.
(h) Mimi nimelala.
(i) Lodup amejenga kibanda.
(j) Karweti amenunua chumvi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 98 12/11/2019 09:44
99
Viunganishi (U)
Viunganishi ni maneno yanayounga maneno, vifungu vya maneno au sentensi. Kwa mfano:
(a) Mkota na mkewe wamekufa.
(b) Nitakusaidia ingawa wewe ni mtu mwovu sana.
(ch) Hakunipa chakula wala chai.
(d) Nipatie kikombe, pia sahani.
(e) Alikufa kwa ukoma au kwa Ukimwi?
Zoezi
1. Onyesha viunganishi katika sentensi hizi.
(a) Mimi ninampenda mamangu, tena sana.
(b) Sijui babu atakuja lini, labda kesho.
(ch) Nataka kukutuma mjini lakini singetaka ukawie.
(d) Jiwe lilibingirika hadi mtoni.
(e) Tutakuja kwako pamoja na mwalimu.
(f) Hatukujenga zahanati kwa vile hatukuwa na pesa za kutosha.
(g) Yule jambazi ataadhibiwa kulingana na sheria.
(h) Daktari Mvita Mjuzi ana maarifa kuliko mganga Kalumanzila.
(i) Sikutaka ununue ngombe bali nilitaka mbuzi.
(j) Mwalimu alisema kwamba hatakuja leo.
2. Tumia viunganishi vifuatavyo kukamilisha sentensi.
afadhali, tena, bila, kama, kushinda, kuliko, au, na
1. Niletee mboga __________ samaki.
2. Wewe nitakuadhibu________ nitakuadhibu sana.
3. Shule yetu ni kubwa __________________ yenu.
4. Ameenda shambani __________________ jembe.
5. Kaari ana shida nyingi _________________ wewe.
6. Unataka nikupe kalamu ____________________ unataka nini?
7. Badala ya kunipa wali _____________________ unipe pure.
8. Nipatie shilingi mia moja ________________ unataka nikuletee matunda.
D. Kusoma
Kusoma kwa kina: Ushairi kwa jumla
Usomaji wa ushairi unaweza kuwa mzuri ikiwa utachunguza mambo mawili makuu kama
tulivyoona katika sura zilizotangulia. Mambo haya ni yale yanayozungumziwa katika shairi
fulani na jinsi yanavyozungumziwa. Hayo yanayozungumziwa, kama tulivyoona katika sura ya
nane, ni maudhui na jinsi yanavyozungumziwa ni fani. Ili tuweze kufaidikia na usomaji wetu,
lazima tujiulize maswali kadha kuhusiana na sehemu zote mbili.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 99 12/11/2019 09:44
100
Maudhui
Je, mshairi anazungumzia nini?
Je, kichwa cha shairi ni kipi na kinahusiana vipi na yanayozungumziwa?
Je, mshairi anataka msomaji apate ujumbe gani?
Je, baada ya kusoma shairi fulani unajiwa na wazo gani?
Je, unakiri mtunzi alitunga shairi hilo ili apitishe ujumbe wa aina gani?
Fani
Je, mtunzi anatumia tamathali za aina gani? (tashbiha/sitiari n.k)
Je, shairi hilo lina muundo wa aina gani?
Je, ni shairi la arudhi au ni shairi huru?
Ikiwa ni shairi la arudhi lina sifa gani? Lina mishororo mingapi? Lina beti ngapi ? Vina
vyake ni vipi?
Je, kuna matumizi gani ya lugha ambayo ni ya kipekee?
Je, ni maneno gani yanayorudiwarudiwa?
Je, msamiati wa shairi ni mgumu au ni mwepesi?
E. Kuandika
Barua rasmi
Barua rasmi huandikwa:
Ili kutumwa osi mbalimbali kwa makusudi ya kuomba kazi au kuomba msaada fulani,
kutaka taarifa fulani, n.k.
Kwa minajili ya shughuli fulani rasmi kwa mfano: shughuli za kibiashara.
Kutoa maoni magazetini, n.k.
Mambo ya kuzingatia:
1. Anwani mbili: ya mwandishi na ya mwandikiwa.
2. Tarehe ya kuandika.
3. Nambari ya kumbukumbu (hasa kwa barua zinazotokana na mashirika, kampuni n.k.)
4. Kichwa cha barua.
5. Kiini cha barua.
6. Hitimisho la barua.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 100 12/11/2019 09:44
101
Meneja Mkurugenzi,
Benki ya Barclays,
S.L.P. 200545-00100,
Kitale.
15-15-2006.
Mkurugenzi,
Mzima Boys Centre,
S.L.P. 1409-05601,
Voi.
Bw./Bi. Mkurugenzi,
KUH: KUKARABATI MAKTABA
Tulipata ombi lako. Tungependa kukueleza kuwa tutakarabati maktaba kama ulivyoomba.
Ukarabati huu utaanza baada ya miezi mitatu.
Ninakuomba unijulishe mapema iwezekanavyo iwapo kuna tashwishi yoyote, ili tuweze
kuandaa mipango yote kwa wakati ufaao.
Wako mwaminifu,
Dkt. M.R. Mbalukula.
MENEJA MKURUGENZI
Mfano 1
BW.Mbalukula
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 101 12/11/2019 09:44
102
Mfano 2
Anwani ziandikwe kwa mtindo wa wima.
Shule ya Upili ya Mnazi Mmoja,
S. L. P. 4588,
Kurasini.
15-1-2003
Meneja wa Uchapishaji,
Kampuni ya Vitabu ya Mkuki,
S. L. P. 500,
Jijibora.
Bwana Meneja,
Kuh: Kuwasilisha mswada wa hadithi
Mimi ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule iliyotajwa hapo juu. Nimeandika
hadithi inayoitwa Sanda ya Jambazi. Ningependa kuuwasilisha mswada wa hadithi hiyo
kwenu ili uchunguzwe kama unaweza kuchapishwa.
Nitafurahi kupokea majibu yenu kuuhusu mswada huu.
Wako mwaminifu,
Deogratias Mkota.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 102 12/11/2019 09:44
103
Anwani ziandikwe kwa mtindo wa wima.
Kampuni ya Vitabu ya Mkuki,
S. L. P. 500,
Jijibora.
2/2/2003
MSK/ 143/ 2
Deogratias Mkota,
Shule ya Upili ya Mnazi Mmoja,
S. L. P. 4588,
Kurasini.
Bwana Mkota,
Kuh: Sanda ya Jambazi
Nitapenda kukufahamisha kuwa tumeupokea mswada wako uliotutumia hivi majuzi.
Tunahitaji kipindi cha miezi mitatu kuupitia na kuchunguza uwezekano wa kuuchapisha.
Baada ya kipindi hicho tutakujulisha uamuzi wetu. Tunakushukuru kwa kuamua kutupa
nafasi hii ya kuutathmini msaada huu.
Wako mwaminifu,
Ahmed Babukubwa.
MENEJA WA UCHAPISHAJI
Zoezi
Andika barua kwa mwalimu mkuu ukimweleza kwa nini ulichelewa kurudi shuleni
baada ya kupewa likizo fupi.
Majibu kwa (barua ya Mfano 3)
AB
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 103 12/11/2019 09:44
104
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3 4
5
6 7
8 9 10
11
12
13
14
15
16 17 18
19
KULIA
1. Ugunduzi
3. La maana
5. Mambo ya kisasa
7. Kipindi cha muda fulani
9. Amba- umoja ngeli ya A-WA
11. Sawa na kompyuta
12. Unanitenda nakutenda
15. Kupashana habari na kuelewana
16. Vijana katika shule; sekondari au chuo
17. Iliyozeeka sana
18. Somo ambapo wanafunzi hupimwa uwezo wa kusikiliza na kuandika kwa usahihi
19. Pahali pa kuzalisha bidhaa mbalimbali
CHINI
2. Sehemu inayobeba chavua katika mmea wa mahindi au mtama
3. Kuandikisha
4. Namna ya kufanya shughuli
6. Mahuluki
8. Injinia
10. Majadiliano kuhusu jambo fulani
13. Eksirei
14. Uwanja wa taaluma fulani
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 104 12/11/2019 09:44
105
A. Ufahamu
Tangu lini nikawa kiatu?
Mwanamke:
Usemi ninabtadi, kukuuliza mwenzangu,
Ipo shida ya fuadi, inayonipa machungu,
Nimeihifadhi hadi, ukanipata uchungu,
Tangu lini niambiya, mimi nikawa kiatu?
Kazi kutwa nifanyiza, huku nahisi uchungu,
Kelele kunipigiza, kunipikia majungu,
Kwamba nimekuwa boza, nichapuke wanguwangu,
Tangu lini niambiya, mimi nikawa kiatu?
M:
Tatizo lako sikiya, umekuwa ja kasuku,
Kila siku unaliya, na wako mwingi udaku,
Mumeo kunitishiya, kwa usemi wenye paku,
Tangu zama za zamani, ni utamaduni wetu!
Ni wajibu fahamiya, ni maisha ya ki huku,
Mke kumhudumiya, mumewe liyempiku,
Mabaya kumwepuliya, mchana pia usiku,
Tangu zama za zamani, ni utamaduni wetu!
Sura ya Kumi
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 105 12/11/2019 09:44
106
M:
Mbona ndani kunifuga, nisiwe kamwe natoka,
Nisiwe nao mashoga, pamoja kujumuika,
‘Wachi matusi kubwaga, majina kunipachika,
Tangu lini niambiya, mimi nikawa kiatu?
Hata nijapo kutoka, hata iwe ni sokoni,
Maelezo unataka, niliyofanya njiani,
Hata kama nimecheka, lazima niseme kwani,
Tangu lini niambiya, mimi nikawa kiatu?
M:
Nina kazi nisikiya, kukutunza mke wangu,
U kama kinda sikiya, wa kuepushwa kipungu,
Lau sivyo tajutiya, yakupate na machungu,
Ndivyo alivyonambiya, babu zama za zamani.
M:
Zimepita na dahari, twashikilia ukale,
Pasi kamwe kukiri, kuhusu haya na yale,
Mema na yenye uthori, tuchambue ja mchele,
Tangu lini niambiya, mimi nikawa kiatu?
M:
Mwacha asili sikiya, huwa ni kama mnyama,
Hana cha kujishikiya, daima anumanuma,
Hata ‘kienda Ulaya, hana thamani ja duma,
Ndivyo alivyonambiya, babu zama za zamani.
M:
Mambo yamebadilika, sasa si kama zamani,
Wake wanajumuika, na waume osini,
Wote wanashughulika, usibaki wa zamani,
Tangu lini niambiya, mimi nikawa kiatu?
Maelezo ya msamiati
nabtadi : naanza.
boza : mzembe.
ja : kama.
wachi : huachi.
dahari : wakati.
fuadi : moyo.
niambiya : niambie.
wanguwangu : harakaharaka; upesi upesi.
udaku : hali ya kutaka sana kufuatilia habari za watu; umbeya.
mumewe ‘liyempiku : mumewe aliye na nguvu na uwezo zaidi kuliko mwanamke.
uthori : ubaya; uovu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 106 12/11/2019 09:44
107
Maswali
1. Katika shairi hili mwanamke analalamika. Taja mambo yanayomfanya alalamike.
2. Kila ubeti wa shairi hili una mishororo minne. Shairi lenye beti za mishororo minne
laitwaje?
3. Mwanamume anajitetea vipi?
4. Katika shairi hili, mwanamke na mwanamume wanajibizana. Shairi la majibizano huitwaje?
5. Taja vina vya kati na vya mwisho vya ubeti wa tatu na wa tano.
6. Shairi hili lina mafunzo gani kwa wanaume?
7. Eleza maana ya msamiati huu kama ulivyotumiwa kwenye kifungu:
(a) wanguwangu (b) liyempiku (ch) kinda (d) mashoga
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora
Vitate: th/dh
th dh
thamini dhamini
thibiti dhibiti
Soma vitanza ndimi vifuatavyo kujizoeza matamshi sahihi ya sauti hizo.
(a) Kwa vile Dhahabu ni mchezaji dhabiti alitaka nimdhamini ili anipe dhahabu na
nilipoithamini dhahabu nikaona ina thamani nikasema nimdhamini kwani nikimdhamini
atanipa dhahabu yenye thamani.
(b) Ingawa Madhubuti ni dhabiti, udhabiti wake hauwezi kuthibitika kwa vile ni dhahiri
alithubutu kuwadhibiti wafanyi kazi wenye uthabiti thabiti na kwa hivyo hata ikiwa
Madhubuti ni dhabiti anahitaji udhabiti ili asithubutu kwadhibiti wafanya kazi thabiti.
Hekaya
Hizi ni hadithi ambazo huweza kuchanganya wahusika wanyama na binadamu. Mara nyingi
katika hekaya kuna mhusika mmoja anayewafanyia wengine ujanja fulani. Katika jamii zetu
mbalimbali, mhusika wa aina hiyo aghalabu ni sungura. Kuna masimulizi ya zamani ya aina
hii ambapo mhusika aliyekuwa akiwadanganya wale wengine alijulikana kama Abunuwasi.
Masimulizi hayo yalijulikana kama Hekaya za Abunuwasi.
Hekaya huweza kuwa na matukio ambayo si ya kawaida, yaani huenda yasitokee katika maisha
ya kawaida. Huwa na mafunzo pia. Baada ya kukisoma kile kisa tunapata mafunzo fulani ambayo
yanajulikana kama maadili.
Mfano wa hekaya
Sungura na Panya buku
Siku moja aliondoka Sungura kwenda kutafuta chakula msituni na akaona mbuyu mkubwa sana.
Alipoyatupa macho yake juu aliuona mzinga mkubwa wa asali ya nyuki. Aliamua kurudi zake
nyumbani ili akawaite wenzake waje naye wapate kuila asali hiyo.
Alipita alikoishi panya buku ambaye alimkaribisha wakakaa kitako. Baada ya mazungumzo,
Sungura alimwambia, “Baba ameaga dunia na kuniachia mzinga wa asali, twende tukaile asali
hiyo. Basi baada ya kusema hivyo, wote wakaondoka kuelekea mwituni. Walipoka huko,
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 107 12/11/2019 09:44
108
Sungura akamwambia mwenzake, Basi panda juu. Panya buku akafanya hivyo na Sungura naye
akamfuatia. Walikuwa na mienge ya moto waliyoitumia kuwachomea nyuki waliojazana mzingani.
Baada ya kufanya hivyo wakaanza kuila asali iliyokuwako.
Mara akatokea Simba chini ya ule mbuyu uliokuwa na mzinga wa nyuki. Yule Simba aliyatupa
macho yake juu na kuona watu wanakula, akawauliza, “Ninyi ni nani? Sungura akamwambia
buku, “Nyamaza, ana wazimu mzee yule!” Simba akauliza tena, “Nani ninyi, hamsemi?” Panya
buku akaogopa baada ya kuisikia ile sauti ya mngurumo wa Simba akajibu, “Sisi hapa!” Sungura
akamwambia buku, Nitwae mimi, unitie ndani ya mwenge, umwambie mzee Simba, jitenge
niutupe mwenge, nami ninakuja. Buku akafanya kama alivyoshauriwa na Sungura. Alipomtajia
Simba akajitenga na buku akautupa mwenge chini. Ulipoanguka chini, Sungura akafyatuka kama
mshale, huyoo akakimbia akaenda zake.
Baada ya muda Simba akamwambia buku, shuka basi”. Buku akashuka kwa hofu na wasiwasi
mkubwa. Alipoka chini tu, Simba akamkamata. Akamwuliza, “Ulikuwa wewe na nani huko
juu?” Alimwambia, mimi na Sungura. Je, hukumwona hapa nilipomtupa?’ Simba akamwambia,
sikumwona. Akamshika buku na kumla papo hapo. Baadaye akatoka kwenda kumtafuta Sungura
asimwone. Akaapa kuwa atamtafuta kote hadi ampate.
Kila aliyekutana naye anamwuliza, nyumba ya Sungura i wapi?” Aliowauliza wakamwambia,
“hatuijui. Kumbe Sungura amekwisha kumwambia mkewe, tuhame nyumba hii. Wakahama.
Simba akaenda kuuliza, wakamwambia watu, nyumba yake ile pale juu ya mlima. Akaenda
Simba, hata akaka lakini hakuwako Sungura. Simba akasema, nitajicha ndani ya nyumba,
hata Sungura akija na mkewe, nitawala wote wawili.
Sungura akaja, yeye na mkewe, hana habari lakini njiani akaona nyayo za Simba, akamwambia
mkewe, rudi wewe, Simba amepita hapa ananitafuta mimi. Akamwambia, Sirudi, nitakufuata
mume wangu. Sungura akamwambia, “Wewe mtoto wa watu, rudi. Akarudi. Sungura akaenda,
akafuata nyayo za miguu, akaona zimeingia ndani ya nyumba yake. Akasema, “Loo! Simba yumo
ndani. Basi akarudi taratibu, akaenda akasimama mbali, akatoa salamu, akasema, “Salaam
nyumba! Salaamu nyumba! Salaam nyumba!” Akasikia kimya. Akanena Sungura, “Jinsi gani
kila siku nikipita hapa, nikitoa salaamu, nyumba hunijibu, labda leo mna mtu humo ndani. Yule
Simba akadanganyika, akaitikia Salaamu!”
Akamwambia, Loo! Simba umo ndani, wataka kunila mimi, ukasikia wapi nyumba kusema?”
Simba akamwambia, “Uningoje basi. Sungura akatimua mbio, wakafukuzana hata Simba
akachoka. Akawaambia watu, “Sungura amenishinda basi, simtaki
tena. Akarudi zake.
Maswali
1. Je, sungura alitumia ujanja gani?
2. Kwa nini simba alitaka kumshika sungura?
3. Je, hekaya hii ina mafunzo gani?
CH. Saru na matumizi ya lugha
Vihusishi (H)
Vihusishi ni maneno yanayoonyesha uhusiano kati ya maneno. Kwa mfano:
(a) Sungura analala kando ya mti.
(b) Salma anatembea karibu na barabara.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 108 12/11/2019 09:44
109
(ch) Simba anangoja ndani ya nyumba.
(d) Mama anaweka mkate ndani ya kabati.
(e) Mwizi amejicha nyuma ya nyumba.
(f) Kuna mechi kali baina ya Gor Mahia na AFC.
(g) Rais ameelekea upande wa magharibi.
(h) Panya buku amepanda juu ya mti ule.
(i) Aliingia osini kabla ya kupewa ruhusa.
(j) Watu wote waliondoka baada ya kuisikiliza hotuba ya katibu mkuu.
Zoezi
1. Onyesha vihusishi katika sentensi zifuatazo.
(a) Watoto walicheza nje ya nyumba.
(b) Watu kadiri ya elfu kumi walika uwanjani.
(ch) Nyanyangu hutusaidia wakati wa shida.
(d) Nitaenda mjini kwa miguu.
(e) Mtoto ameketi kati ya babake na mamake.
2. Tunga sentensi ukitumia vihusishi vifuatavyo: kando ya, baina ya, upande wa, karibu na,
ndani ya, chini ya, kati ya.
Uakishaji
Kiulizi
Hii ni alama ya kuakisha inayotumika kuulizia swali. Kwa mfano:
(a) Babu amekwenda wapi?
(b) Sasa ni saa ngapi?
(ch) Tutakwenda sokoni siku gani?
(d) Ng’ombe watafunguliwa lini?
(e) Ulizaliwa mwaka gani?
Alama ya hisi (!)
Alama hisi huonyesha hisi za moyoni kama vile furaha, huzuni, majuto, mshangao n.k.
Kwa mfano:
(a) Lo! Lo! Simba anawashambulia kondoo wetu.
(b) Nenda pale mara moja!
(ch) Kumbe yule mtu alikuwa mwizi!
(d) Hoyee! Timu yetu imefunga bao.
(e) Sitaki! Unasikia? Sitaki na sitaki!
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 109 12/11/2019 09:44
110
Mnyambuliko wa vitenzi: Kauli ya kutenda, kutendwa na kutendeka
Kauli ya kutendwa: Humaanisha kuwa jambo limefanywa na mtu au kitu. Yaani huonyesha kuwa
mtu fulani (au watu fulani), kitu au vitu vimepokea tendo fulani. Kiambishi cha kauli hii ni {w}
(ingawa inaweza pia kutokeza kama {liw} au {lew} kutegemea sifa ya irabu katika mzizi au jinsi
mzizi unavyoisha. Mifano ni:
kata................katwa
pika...............pikwa
choma...........chomwa
chukua...........chukuliwa
ondoa...............ondolewa
Kauli ya kutendekaa: Kauli hii huwakilisha uwezekano wa jambo kufanyika bila ya kuonyesha
moja kwa moja anayehusika ni nani (au jambo hili linasababishwa na nani au nini). Viambishi
vya kauli hii ni {ik}, {ek}, {k} {lik} na {lek}. Mifano:
lima.............limika
ngoa..........ng’oka
soma........someka
vua...........vulika
vaa..........valika
lea............leleka
Tazama jedwali lifuatalo.
Mzizi Kauli ya kutenda Kauli ya kutendwa Kauli ya kutendeka
-chez-
-som-
-andik-
-lim-
-pik-
-kat-
-chom-
-fagi-
-pig-
-fung-
chez-a
som-a
andik-a
lim-a
pik-a
kat-a
chom-a
fagi-a
pig-a
fung-a
chez-w-a
som-w-a
andik-w-a
lim-w-a
pik-w-a
kat-w-a
chom-w-a
fagili-w-a
pig-w-a
fung-w-a
chez-ek-a
som-ek-a
andik-ik-a
lim-ik-a
pik-ik-a
kat-ik-a
chom-ek-a
fagi-lik-a
pig-ik-a
fung-ik-a
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 110 12/11/2019 09:44
111
Zoezi
1. Kamilisha jedwali lifuatalo:
Kauli ya kutenda Kauli ya kutendwa Kauli ya kutendeka
lim-a
pang-a
let-a
fum-a
uliz-a
und-a
fany-a
pig-a
geuz-a
tawal-a
lim-w-a
lim-ik-a
2. Geuza kitenzi kilichoko kwenye mabano ili kiwe cha kauli ya kutenda, kutendwa au
kutendeka kulingana na maelekezo.
Kwa mfano: Kitabu changu kime_________. (leta, tendwa)
Kitabu changu kimeletwa.
(a) Mlango ume_____ wenyewe. (funga, tendeka)
(b) Shamba lita_____ na wanafunzi wale. (lima, tendwa)
(ch) Mchezo uta_____ keshokutwa. (cheza, tendwa)
(d) Punda ata_____ mzigo. (beba, tenda)
(e) Mchezo huu hauwezi ku_____. (cheza, tendeka)
(f) Kwa nini ulim_____ mwanangu? (piga, tenda)
(g) Nilijaribu kujenga lakini nikagundua kuwa nyumba hiyo haiwezi ku_____. (jenga,
tendeka)
(h) Kijiti hiki hakiwezi ku_____. (kata, tendeka)
(i) Kitabu kita_____ kesho. (nunua, tendwa)
(j) Kwa nini hatuwezi kum_____ bata yule? (chinja, tenda)
D. Kusoma
Usomaji wa kina: Ushairi
Katika sura iliyopita, tuliangalia mambo ya kuchunguza tunapoyasoma mashairi. Sasa soma
mashairi yafuatayo halafu ujibu maswali.
(A) Usinibague
Sikiza kilio changu, kisha ukizingatie,
Huku si kupenda kwangu, mjini nikimbilie,
Yalinikuta machungu, sikiza nihadithie,
Nionyesha penzi mie, kamwe usinibague.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 111 12/11/2019 09:44
112
Kibaya kisomo changu, shida ziniandamie,
Hawapo wazazi wangu, kwa ukimwi walie,
Nikawa sina uvungu, popote nishikilie,
Nionyesha penzi mie, kamwe usinibague.
Tazama na afya yangu, na huruma unonee,
Useme ni kama wangu, mwana nisimbague,
Nipeke penye kidungu, penye jaa unepue,
Nionyesha penzi mie, kamwe nisibague.
Kiona kivuli changu, mbio kubwa sitimue,
Mimi mtu sio changu, huruma jama nonee,
Lakereta tumbo langu, sasa nifanyeni mie,
Nionyesha penzi mie, kamwe usinibague.
Maswali
(a) Je, shairi hili ni la aina gani? Onyesha vina vya kati na vya mwisho.
(b) Je, maudhui ya shairi hili ni nini?
(ch) Msemaji anamaanisha nini anaposema, ‘Nionyesha penzi mie, kamwe usinibague?
(B) Mambo gani haya?
Tazameni magari
yanayoendeshwa kwa kasi
yajazayo abiria pasi kiasi
yavunjayo sheria bila kukisi
kisha
yakazua majanga
yakaua abiria
na kutuachia wingu la kilio kiso na mfano.
Madereva haya ni mambo gani?
Kwa nini hamtulizani barabarani?
Mkaendesha magari kwa makini.
Kwa nini ? Kwa nini? Kwani?
Maswali
(a) Je, shairi hili linahusu nini?
(b) Je, mshairi anapendekeza nini?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 112 12/11/2019 09:44
113
E. Kuandika
Hadithi fupi
Hadithi fupi ni kisa kinachogusia jambo fulani na ambacho sio kirefu na kinaweza kusomwa kwa
kipindi kifupi sana. Uandishi mzuri wa hadithi ni ule uliopangwa vizuri. Ikiwa utakosa kupanga
unapoandika, pana uwezekano wa kuacha mambo muhimu katika hadithi yako. Pili, inawezekana
ukayachanganya maelezo na kumfanya msomaji ashindwe kuifuata hadithi.
Mpango wa hadithi fupi uhusishe:
1. Wakati: Tukio au tendo lolote hufanyika wakati fulani.
2. Mahali: Tendo lolote hutendeka mahali fulani maalumu.
3. Wahusi ka: Tukio haliwezi kukamilika bila ya kuwa na watu wanaolitenda au wanaohusika
na utendaji wa tendo hilo.
4. Tukio: Hiki ni kiini kilichotendeka. Ikiwa pana wahusika waliopo mahali na wakati
fulani lazima wanatenda jambo fulani. Jambo hilo ni tukio.
5. Hisia zako: Mtu anayeshuhudia jambo fulani ana hisia fulani. Je, unapoona watu wakitenda
jambo fulani unajiwa na nini akilini? Je, unachukia, kupenda, kukasirika au
kuvutiwa? Hizi ni hisia zako.
Mfano wa hadithi
Pwagu hupata pwaguzi
Yalikuwa majira ya jioni siku ya Jumatatu wakati wa msimu wa baridi. Ingawa haikuwa saa moja
tayari, giza la jioni lilikuwa limeshika huku na huku. Giza hilo liliongezwa na mawingu yaliyotanda
angani mchana kutwa. Siku nzima ilifanana na mtu aliyekuwa amenuna; haikuonyesha furaha
ya aina yoyote na jua nalo halikuonekana.
Hali ya hewa iliyokuwako ilimvutia sana Kanda aliyeisubiri jioni hiyo kwa hamu kubwa.
Tangu alipoyaacha masomo yake yapata miaka minne iliyopita, Kanda aliifurahia kazi yake mpya.
Mwanangu, mambo unayoyafanya sio mazuri, alimkanya babake. Lakini Kanda hakuusikiliza
wala kuuzingatia ushauri aliopewa na babake mzazi. “Mwanangu, dunia hii ina matatizo makubwa
na ukipanda mabaya utavuna majuto, alimshauri mamake mzazi. Lakini Kanda hakusikia la
mwadhini wala la mteka maji msikitini kwa kuamini kuwa aliweza kuamua la kufanya.
Siku iliyotangulia alifanya uchunguzi wake na kutambua kuwa jirani yao, Bwana Kanzi,
alikuwa na hazina kubwa ya pete za dhahabu za mkewe Nassra. Nia yake leo ilikuwa kutafuta
njia ya kuingia katika nyumba yake kubwa na kuzitwaa pete hizo kwenda kuuza. Basi baada ya
kujiandaa alitoka nyumbani kuelekea kwa Mzee Kanzi. Aliufunika uso wake kizuizui ili asiweze
kutambuliwa na yeyote wakati huo.
Alipoka ulipokuwa mji wa Mzee Kanzi alitafuta mwanya wa kupenyezea. Sehemu aliyokuwa
ameiona mchana ilikuwa imezibwa kwa matawi ya miba. “Sasa ni nani aliyefanya hivi? alijiuliza
Kanda akienda huko na huko kutafuta mahali pengine. Kwa bahati nzuri, aliweza kupata mahali pa
kupitia na kuingia uwanjani. Alipotokeza uwanjani tu, alikumbana na jambo ambalo hakulitarajia.
Alisikia mbwa aliyebweka kwa sauti ya juu sana. Mbona mbwa wa Kanzi nilimtilia sumu wiki
iliyopita akafa jana, sasa huyu ametoka wapi? alijiuliza akirudi kinyumenyume.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 113 12/11/2019 09:44
114
Alijigonga kwa kisiki kilichokuwa nyuma yake na kuanguka chini. Wakati huu yule mbwa
alikuwa amkimbilia na kubweka kwa sauti ya juu kabisa. Kanda hakuwa na wakati wa kusimama
na kuweza kununua pujo aina mguu niponye. Mzee Kanzi na wanawe walitokeza wakati huo
na tochi kubwa iliyokuwa na mwanga mkali kama wa mbalamwezi. Walimshika Kanda na
kumfunga kwa kamba halafu Mzee Kanzi akaliwasha gari lake wakampeleka kwenye kituo cha
polisi kilichokuwa karibu.
Kanda hakujua maana ya asiyefunzwa na mamake hufunzwa na ulimwengu hadi siku hiyo.
Zoezi
Andika kisa chochote kinachoonyesha ukweli wa methali Mpanda ngazi hushuka au Asiyesikia
la mkuu huvunjika guu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 114 12/11/2019 09:44
115
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3
4
5
6 7
8
9 10
11 12
13
14
15 16 17
18
19
KULIA
3. Aina ya konsonanti
4. /b/ na /p/ ni mfano wa _______
6. Hutumika katika mawasiliano
7. Kinachotendewa au kufanywa
8. Sauti ambazo hukuna mtetemeko zinapotamkwa
11. Jinsi ya utamkaji wa sauti katika lugha
12. Sehemu ya neno isiyobadilika
14. Sauti ambazo hutetemesha koo zinapotamkwa
15. Huwekwa kwenye mzizi wa neno ili kuleta maana
17. Ni za aina tatu; kwanza, pili na tatu
18. Masine
19. Kinyume cha uyakinishi
CHINI
1. /m/, /n/, /ny/ na /ng’/
2. Kiambishi cha mwisho katika neno
3. Neno linalotumiwa kurelejea nomino au kusisitiza
5. Mwisho
7. Zinapotamkwa hewa hubanwa au kuzuiliwa
9. Hatibu hutoa
10. /r/
13. Kiungo kisichokuwa na mfupa- kiungo muhimu cha matamshi
16. Maelezo ya mawazo kuhusu jambo fulani
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 115 12/11/2019 09:44
116
A. Ufahamu
Jumakoshi alikiona
Duka la Alikiona lilikuwa maarufu katika soko la kwetu. Hili lilikuwa duka la pekee kwenye soko
hilo lililouza bidhaa zilizotengenezwa kwa mikono. Katika duka hili paliuzwa bidhaa za kila aina
kuanzia viatu, mishipi, makasha na nyingine nyingi. Mtu akika sokoni aliweza kutambua mara
moja kuwa lilikuwa wazi kutokana na baiskeli ya mwenyewe. Baiskeli hii iliegemezwa kwenye ukuta
wa jengo la duka. Mwenye duka hilo alikuwa mtu wa kwanza kuka sokoni. Aliamini kwamba
aendaye kisimani kwanza hunywa maji maenge. Alikuwa mchapa kazi aliyesiwa hadi ya sifa
katika soko zima. Na hakuna mtu ambaye hakujua jina la mwenye duka hilo: Jumakoshi. Lakini
mwenyewe alijibatiza Alikiona. Na kusema kweli, Jumakoshi alikiona.
Jumakoshi alikuwa mwenyeji wa kwanza wa kwetu kuhamia jijini baada ya masomo yake
kugonga mwamba. Wazazi wake walifanya kila juhudi kumshawishi asiyaache masomo, lakini
Jumakoshi akatia pamba masikioni; hakusikia la mwadhini wala la mteka maji msikitini. Wazazi
waliposhindwa wakasema, Asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Lakini Jumakoshi hakujali. Yeye
alikuwa na hamu kubwa ya kukimbilia jijini alikodhani kumejaa maisha ya raha na starehe.
Hata hivyo maisha ya jijini hayakuondokea kuwa ya burudani kama alivyodhani Jumakoshi.
Tatizo la kwanza lilikuwa kutokuwa na mahali pa kulala. Yeye na vijana wengine waliishia kujilaza
kwenye majalala ya takataka au kwenye penu za majengo makubwa ya jijini. Chakula kilikuwa cha
shida kweli. Walilazimika kuzunguka huku na huko kukomba chakula au kungangania makombo
na majibwa ya jiji. Mambo yalizidi kumwendea kombo Jumakoshi na wenzake. Nguo alizokuwa
nazo zilibadilika kabisa na kuwa nyeusi kama lami. Mwili wake ulichakaa na kutisha kutokana na
kuchafuka kwa kutooga kwa siku nyingi. Nywele zake zilitimka na kumfanya atishe kama chakari.
Chakula kilipokosekana kabisa waliunda vikundi au vigenge fulani vya kuvamia mahoteli na
maduka ya jijini na kuwanyanganya watu mali zao. Na kwa kweli, Jumakoshi aliyafurahia sana
maisha hayo.
Angeendelea kufurahia maisha yake ya mitaani na unyanganyi hadi siku moja. Siku hiyo
aliteuliwa kuwa kiongozi wa kigenge kilichopanga kwenda kuvamia duka moja la kuuzia chakula.
Walishafanya uchunguzi na kujua kuwa duka lenyewe hufunguliwa saa ngapi kila asubuhi.
Walikuwa na hakika kuwa saa hizo hapakuwako hatari ya kushikwa na polisi wa doria.
Asubuhi ya ‘kazi, Jumakoshi na kigenge chake waliondoka na kujibanza sehemu fulani karibu
na lile duka ili kumtegea mwenye duka hilo. Sehemu walikojicha ilikuwa na jalala kubwa. Muda
si muda yule mwenye duka alika, akaliegesha gari lake na kutoka. Alianza kutembea kuelekea
kwenye duka lake. Kwenye mkono wake wa kulia alishika kibweta. “Haya, jiandaeni. Tutatimua
mbio na kumpiga dafrao ghaa. Mimi ndiye nitakayekibwakura kile kibweta, alitoa maelekezo
Jumakoshi. “La. Ni mimi. Ninaweza kutimua mbio kuliko mtu mwingine yeyote hapa, alisema
kijana mwingine aliyejulikana kama Isaka. “Haya. Moja! Mbili! Tatu…! Walifyatuka kama mishale
kuelekea alipokuwa yule bwana. Ghaa bin vuu alishtukia amepigwa kikumbo na kibweta chake
kunyakuliwa mfano wa mwewe anyakuavyo kifaranga. Mwenye duka alipiga kamsa ya Mwizi!
Mwizi! Saidia! Naye Jumakoshi na wenzake wakatimua mbio za umeme. Lakini hawakujua kuwa
palikuwa na polisi waliokuwa wameshika doria karibu na mahali hapo.
Sura ya Kumi na Moja
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 116 12/11/2019 09:44
117
Kumbe ni kweli siku za mwizi ni arobaini! Polisi mmoja alifyatua risasi iliyompata Isaka
mguuni na kumwangusha. Yeye ndiye aliyekuwa amebeba kile kibweta. “Wooi! Wooi!” alipiga
usiahi mkali wa maumivu. Risasi ziliendelea kulia. Kijana mwingine aliyeitwa Kibao akapata moja
ya paja, akalamba mchanga. Jumakoshi sasa alijua kuwa maisha yake yalikuwa hatarini. Mara
moja aliamua kununua gari aina mguu niponye, akatimua mbio za upepo na kupiga chenga hapa
na pale mpaka akapotea. Alipotokezea mahali salama akajicha huku akihemahema kama chura
hadi kulipotulizana. Wenzake wote walitiwa mbaroni wakiwa na maumivu mabaya. Hapana,
siwezi kuishi maisha ya aina hii! Nimeponea tundu ya sindano!” alijiambia.
Tangu siku hiyo, Jumakoshi alianza kuishi maisha yaliyojaa wasiwasi. Kwa bahati nzuri palikuwa
na kikundi kilichojulikana kama ‘Jibadilishe Ujifae. Hiki kilikuwa kikundi kilichowasaidia vijana
wa mitaani kuanza maisha mapya. Alipokutana na viongozi wa kikundi hicho, walimpokea kwa
mikono miwili. Alihamia kwenye makao yao. Huko ndiko alikojifundishia maarifa ya kutengeneza
bidhaa kwa mikono. Alijifunza mambo mengi kwa kiu na hamu kubwa.
Baadaye Jumakoshi aliamua kurudi nyumbani. Wazazi wake walifurahi ghaya walipomwona.
Ingawa alikuwa ametoroka nyumbani, hawakumkataa. Walijua kuwa mwenda tezi na omo
marejeo ni ngamani. Walikuwa tayari kumsaidia kuanzisha biashara ya kujikimu. Hivi ndivyo
alivyolianzisha duka akaliita Alikiona.
Kila alipokutana na wanafunzi aliwaambia, “Funzo la mjinga tabu. Msifanye nilivyofanya
kwa kutoroka shule. Jueni kwamba mimi Jumakoshi nilikiona. Wazazi wa Jumakoshi walifurahi
kuwa alikuwa amebadilika na kuwa mtu mwingine kabisa ambaye hata aliwapa mawaidha vijana
wengine na pengine kuokoa maisha yao. Walisema, “Ni kweli mui huwa mwema!” Wazazi mle
kijijini mwetu walifurahi sana kuona Jumakoshi akiwashauri wanafunzi wasome. Duka lake
halikuwa duka la kuuzia bidhaa mbalimbali tu, bali pia duka la kutolea mashauri na mawaidha
bora.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 117 12/11/2019 09:44
118
Maelezo ya msamiati
kasha : sanduku.
maji maenge : maji sa; maji yasiyokuwa na uchafu.
kigenge : kikundi.
makombo : mabaki ya chakula.
kukomba chakula : kuombaomba chakula; kula makombo au masalio ya chakula.
penu za majengo : nafasi chini ya mapaa katika viambaza vya kando ya majengo
ulichakaa : uliharibika; ulidhooka.
polisi wa doria : polisi wanaozunguka mahali fulani ili kulinda usalama.
kujibanza : kujicha.
akaliegesha : akaliweka pembeni au mahali maalumu.
nitakayekibwakura : nitakayekinyakua; nitakayempokonya.
kujikimu : kupata mahitaji ya maisha.
kibweta : kisanduku/kikasha
Maswali
1. Ni kwa nini Jumakoshi alijibatiza Alikiona?’
2. Unadhani ni kwa nini watu wengi walimfahamu Jumakoshi?
3. Ina maana gani kusema kuwa masomo ya Jumakoshi ‘yaligonga mwamba?’
4. Jumakoshi alifurahia sana maisha yake huko jijini. Ni kweli? Elezea.
5. Eleza jinsi Jumakoshi alivyoendesha maisha yake huko mjini kabla ya ile siku ya kulivamia
duka.
6. Ni kwa nini Jumakoshi alibadilika na kuamua kurudi nyumbani?
7. Methali asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu inahusianaje na kisa hiki?
8. Eleza maana ya methali hizi kulingana na kifungu:
(a) Aendaye kisimani kwanza hunywa maji maenge.
(b) Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
(ch) Siku za mwizi ni arobaini.
(d) Mwenda tezi na omo marejeo ni ngamani.
(e) Mui huwa mwema.
(f) Kuishi kwingi ni kuona mengi.
(g) Funzo la mjinga tabu.
9. Mguu niponye ni gari la aina gani?
10. Tunga sentensi ili kuonyesha maana za misemo ifuatayo:
(a) chapa kazi (d) piga dafrao (h) piga kamsa
(b) piga kikumbo (e) piga usiahi (g) piga chenga
(ch) ponea tundu ya sindano (f) pokea kwa mikono miwili
11. Toa maana za maneno haya kama yalivyotumiwa kwenye kifungu kisha uyatungie sentensi:
(i) burudani
(ii) majalala
(iii) jikimu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 118 12/11/2019 09:44
119
B. Kusikiliza na kuzungumza
Semi
Neno hili hutumiwa kuelezea utanzu wa fasihi simulizi ambao ni mfupi au uundwao kwa maneno
machache au sentensi kadha. Huu ni utanzu muhimu katika fasihi simulizi na una vipera au
vijitawi kadha wa kadha kama vile methali, vitendawili, misemo, misimu, mafumbo n.k. Semi
ni muhimu katika lugha ya kila siku kwa sababu:
Husaidia kuifanya lugha iwe na mvuto mkubwa.
Huitia lugha ya mazungumzo ladha na kuifanya ipendeze kwa watakaosoma au
wanaosikiliza.
Methali humwezesha mtu kusema mambo muhimu kwa njia ya mkato bila ya
kuyatumia maelezo mengi na marefu.
Huongeza uzito wa yale yasemwayo.
Katika sura hii, tutaangalia aina au kipera kimoja cha utanzu wa semi: misemo. Misemo hutumiwa
kuelezea maneno au vifungu vya maneno ambavyo hutumiwa kwa maana maalum. Maneno au
vifungu hivyo huwa na maana tofauti na ile ya juu. Kwa mfano katika maneno askari kanzu,
neno askari lina maana ya polisi, na kanzu ni aina ya vazi. Lakini haimaanishi kuwa huyu ni
polisi aliyevalia kanzu. Huu ni msemo au nahau yenye maana ya ‘kachero au askari asiyevaa
mavazi rasmi.
Lugha ya Kiswahili ina mifano mingi ya misemo na nahau. Mathalani, soma kifungu
kifuatacho:
Sote tulikuwa tumekwisha inawa mikono baada ya wenyeji wetu kuandika meza mlango
ulipogongwa kwa kishindo. Tulitulizana na kukaa tutwe huku tukiuangalia mlango. Baada ya muda
yule mgongaji alikirudia kitendo chake tena; mara hii aligonga kwa nguvu za ajabu. Ule ukali wa
sauti ulitutia kihoro; mtoto mdogo aliyekuwa hapo chini alipiga unyende akikimbilia alipokuwa
mamake. Mwenyeji wetu aliamua kusogea karibu na dirisha na kulivuta kidogo na kuyatupa macho
nje. Alirudi polepole tulipokuwa na kusema ni majambazi watatu, sasa pigeni kelele ili wadhani
tuko wengi waogope. Tulifanya kama alivyosema, tukaiga sauti za kila aina. Aliporudi dirishani
hakuwaona; alisogea mlangoni na kuufungua polepole na kuwaona wakipotelea huko chini. Kumbe
kwa bahati nzuri askari kanzu aliyeishi hapo karibu alisikia sauti zetu na kutokeza. Alimwagizia
risasi jambazi mmoja lakini akaponea chupuchupu na kutokomea kwenye giza mbwi la usiku huo.
Zoezi
(a) Taja na ueleze maana ya misemo iliyotumiwa katika kifungu hiki.
(b) Eleza kwa kifupi maana ya neno semi.
(ch) Toa mifano sita ya misemo na sita ya methali katika lugha ya Kiswahili.
Methali
Methali ni msemo wa kimapokeo (yaani unaopokezanwa kutoka kizazi hadi kingine) wenye
muundo fulani mfupi na wa kukumbukika. Msemo huu unaeleza ukweli fulani unaokubalika
katika jamii. Kwa mfano tuangalie mfano wa methali: Mpanda ngazi hushuka.
Methali hii inakumbukika kwa urahisi sana. Pili, inaeleza ukweli fulani kuwa mtu anayepanda
ngazi lazima ashuke au ateremke. Kwa kutumia ukweli huu unaojulikana, methali hii inakuwa na
maana nyingine; yaani mtu anayekuwa na cheo au mali huweza kuishiwa nayo na kuwa maskini.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 119 12/11/2019 09:44
120
Basi mtu kama huyo anaonywa asiwe na kiburi au maringo kwa kuwa na mali hiyo.
Muundo wa methali
Methali huundwa kwa maneno machache ambayo yanakumbukika rahisi. Kwa kawaida methali
huwa na mpangilio wa maneno ambao unaonyesha pande mbili za kira. Pande hizi huweza kuwa:
(i) kutuonyesha tendo, hali au masharti.
(ii) matokeo ya tendo, hali au masharti yanayohusika. Tuangalie mifano:
(a) Mpanda ngazi (kitendo cha kwenda juu) hushuka (tokeo lake)
(b) Asiyesikia la mkuu (kitendo cha kupuuuza ushauri) huvunjika guu (matokeo yake)
(ch) Subira (hali ya kuwa na uvumilivu) huvuta heri (matokeo ya kuwa mvumilivu)
Umuhimu wa methali
Methali hutumiwa kwa sababu mbalimbali:
Kuonya au kuelekeza. Kwa mfano: kiongozi anayewatesa watu anapowaongoza anapoambiwa
mpanda ngazi hushuka anaonywa.
Kuongeza utamu katika mazungumzo. Lugha inayotumia methali huwa na utamu.
Kuipamba lugha: Methali hutumiwa kuipamba lugha na kuifanya iwe na mvuto.
Kuelimisha: Methali hutumiwa kama njia ya kumwelimisha mtu ajue ni jambo lipi la kutilia
maanani na lipi sio muhimu.
Zoezi
Andika methali tano za Kiswahili zinazotumiwa kuonya au kunasihi watu wasiwadharau wengine.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Hali ya mazoea (HU)
Hali hii huwakilishwa na kiambishi HU na huonyesha kuwa kitendo hufanywa mara kwa mara
hadi kikawa mazoea. Kwa mfano:
1. Mwalimu husahihisha kazi yetu.
2. Gari langu huharibika mara kwa mara.
3. Mjomba hutuletea zawadi wakati wa Krismasi.
4. Mama hunilipia karo kila muhula.
5. Mimi huishi mashambani.
Zoezi
Andika sentensi zifuatazo katika hali ya mazoea hu.
(a) Janet anasoma kitabu cha Kiswahili kila mara.
(b) Mchoraji yule anachora picha nzuri.
(ch) Mkulima anatayarisha shamba lake mapema.
(d) Kiongozi yule anawaongoza waandamanaji.
(e) Paka atamshambulia panya kila ampatapo.
(f) Mbunge wetu anawahutubia wananchi.
(g) Mpishi atapika chakula kitamu.
(h) Kuku wetu alitaga mayai mengi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 120 12/11/2019 09:44
121
(i) Yohana anafanya biashara mjini.
(j) Asa wa elimu atakagua shule yetu.
Kukanusha hali ya mazoea
Tazama jedwali lifuatalo:
Umoja
Wingi
nafsi ya kwanza
Kuyakinisha Kukanusha Kuyakinisha Kukanusha
hucheza sichezi
huimba siimbi
huandika siandiki
hutembea sitembei
hucheza hatuchezi
huimba hatuimbi
huandika hatuandiki
hutembea hatutembei
nafsi ya pili
hucheza huchezi
huimba huimbi
huandika huandiki
hutembea hutembei
hucheza hamchezi
huimba hamuimbi
huandika hamuandiki
hutembea hamtembei
nafsi ya tatu
hucheza hachezi
huimba haimbi
huandika haandiki
hutembea hatembei
hucheza hawachezi
huimba hawaimbi
huandika hawaandiki
hutembea hawatembei
Zoezi
Kanusha sentensi zifuatazo.
(a) Ochieng huenda sokoni siku ya Jumanne.
(b) Wachezaji wa mpira wa magongo hufanya mazoezi yao alasiri.
(ch) Waruinge hucheza ndondi za kulipwa.
(d) Mpishi wetu hupika uji kila asubuhi.
(e) Nekesa hurudi shuleni saa nane.
(f) Mogeni husari kila wiki.
(g) Mimi hutia bidii masomoni.
(h) Wewe huwasaidia wazazi wako.
(i) Daktari huwatibu wagonjwa.
(j) Nyinyi huchota maji katika mto huu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 121 12/11/2019 09:44
122
Tashbiha/Tashbihi
Soma sentensi zifuatazo:
(a) Nguo za Alikiona zilibadilika na kuwa nyeusi kama lami.
(b) Nywele zake zilimtimka na kumfanya atishe kama chakari.
Hiyo ni mifano ya tashbiha au tashbihi. Tashbiha ni mafungu ya maneno ya kulin-
ganisha. Hutumia maneno ya mlinganisho kama vile: kama, mfano wa, mithili ya, ja
(katika mashairi) n.k. Chagua maneno yafaayo kukamilisha tashbiha zifuatazo: kiriba,
komanzi, pamba, nanga, ruhani, mauti, mpingo, sungura, nyundo, jongoo.
(a) Laini kama ______
(b) Mjanja kama _____
(ch) Hakika kama ______
(d) Fupi kama ______
(e) Zito kama ______
(f) Pofu kama ______
(g) Mrefu kama _______
(h) Mweusi kama ______
(i) Nukia kama _______
(j) Mwenye tumbo kama _______
Kubainisha maneno katika sentensi
Kubainisha au kuainisha maneno ni kuonyesha aina ya neno katika tungo, sentensi au fungu
lolote lile la maneno. Kila aina ya neno huwakilishwa na heru fulani kama ifuatavyo:
Nomino - N
Vivumishi - V
Vielezi - E
Viwakilishi - W
Vitenzi - T
Viunganishi - U
Vihusishi - H
Vihisishi - I
Kwa mfano:
1. Mama amekwenda sokoni.
N T E
2. Watieri atakuja kwetu.
N T E
3. Shule hii huwasaidia watoto mia tatu.
N V T N V
4. Wazee wanashauriana uwanjani.
N T E
5. Mwalimu amenunua gari jekundu.
N T N V
6. Mtoto mdogo ameimba wimbo mtamu sana.
N V T N V E
7. Masalaale! Nani yule?
I W V
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 122 12/11/2019 09:44
123
8. Nilikwenda shuleni lakini sikumkuta mwalimu wetu.
T E U T N V
9. La hasha! Sitakubali kamwe.
I T E
10. Hawa na wale watakwenda mtoni.
W U W T E
11. Paka amelala chini ya mti.
N T E
12. Yusufu na Danieli wamekwenda wapi jamani?
N U N T E I
13. Watu watatu watakishwa mahakamani leo asubuhi.
N V T E E
14. Kusema kweli mimi sikumpiga.
I W T
15. Haki ya Mungu utanitambua.
I T
Zoezi
Bainisha maneno katika sentensi zifuatazo.
(a) Mimi nitakwenda Kakamega kesho.
(b) Yeye anaogopa kuvuka mto huo.
(ch) Mji huo unaongozwa vizuri.
(d) Watoto hawa wanacheza.
(e) Watu wote wameangamia.
(f) Wale watafungwa.
(g) Mtoto anatembea polepole.
(h) Salaala! Kawewa amemwaga maziwa yangu?
(i) Jamani! Majangili wamewaua ndovu kumi leo asubuhi.
(j) Mlima mrefu utapandwa na watalii ishirini.
D. Kusoma
FASIHI ANDISHI: Riwaya
Riwaya ni kisa cha kubuni kinachosimulia matukio fulani, na chenye mafunzo fulani. Kiini cha
kisa hiki ni matendo, maisha, na matukio yanayomhusu binadamu. Kila mara tunasoma riwaya
za aina mbalimbali na zinazohusu mambo tofauti tofauti. Mfano mmoja wa riwaya fupi ni
Yatima ya K. W. Wamitila. Hii ni riwaya inayogusia suala la mtoto wa kike na hasa yatima na
changamoto anazokumbana nazo.
Vidokezi vya usomaji
1. Soma mara ya kwanza ili uweze kukipata kisa kikuu kwanza na jinsi kinavyofu- luliza,
yaani ile hadithi yake kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
2. Soma mara ya pili ili uyajue mambo muhimu yanayozungumziwa katika riwaya hiyo(yaani
maudhui). Hapa utaweza kuwajua wanaotenda mambo mbalimbali katika kisa hicho ambao
wanajulikana kama wahusika. Hawa ni binadamu wa hadithini.
3. Usomaji wa pili unakuwezesha pia kujua jambo kuu linalozungumziwa katika riwaya
uliyosoma (yaani dhamira).
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 123 12/11/2019 09:44
124
4. Chunguza jinsi wazo hilo kuu na mambo mengine yanavyowasilishwa (hii ni fani)
katika riwaya uliyosoma. Kama tulivyoona katika sura iliyotangulia, utaangalia: (i)hadithi
na ilivyosimuliwa, matumizi ya lugha (kama mbinu mbalimbali kama tashbihi, sitiari n.k.,
msamiati, mpangilio wa matukio mbalimbali,au muundo, wahusika n.k..
5. Ni muhimu pia kuangalia matumizi mbalimbali ya misemo na nahau, methali na hata
msamiati. Unapokumbana na neno usilolijua maana jaribu kwanza kuan- galia kama
unaweza kulielewa jinsi lilivyotumiwa. Ukishindwa kulielewa angalia katika kamusi yako.
Kamusi huweza kuwa na maana mbalimbali, chunguza ni maana ipi inayolingana na
matumizi ya neno hilo kwenye hadithi.
6. Waangalie wahusika wanaopatikana katika hadithi na kujiuliza unajifunza nini kutokana
na matendo yao. Je, matendo yao yanachochewa na nini? Je, mwanadishi anataka tujifunze
nini kutokana na wahusika hao? Je, wanasaidia vipi kuendeleza maudhui?
7. Chunguza dhamira ya riwaya ambayo imefumbatwa na anwani ya kitabu. Jiulize maadili
(mafunzo) ya riwaya ni nini.
Zoezi
1. Je, riwaya ni nini? 2. Wahusika ni nini?
E. Kuandika
Insha ya maelezo
Hii ni aina ya insha ambapo mtu anatoa maelezo juu ya kitu, jambo, mtu au pahali fulani. Katika
insha hii, maelezo hayo yanapaswa kutolewa hatua kwa hatua na kwa njia wazi ili kinachoelezwa
kiwe bayana kwa msomaji. Ili kuandika insha ya aina hii, mwanafunzi anahitaji msamiati wa
kutosha, methali na hata misemo au nahau ili kutoa maelezo yanayokidhi.
Je, ni mambo gani ya kuzingatia katika uandishi wa insha za aina hii?
(a) Hakikisha kuwa una mpango mzuri wa mambo muhimu katika insha yako.
(b) Hakikisha una maelezo yote muhimu.
(ch) Yapange maelezo kwa utaratibu mzuri.
(d) Tumia msamiati unaofaa kuelezea unachotaka kuelezea.
(e) Hakikisha umetumia lugha yenye mvuto na kamilifu.
Mfano:
Shule yetu





Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 124 12/11/2019 09:44
125























Zoezi
1. Andika insha kuhusu maabara yenu ya shule.
2. Andika insha kuhusu kaunti yako.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 125 12/11/2019 09:44
126
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1
2
3
4 5
6 7
8
9 10 11
12 13
14 15
16 17
18
19
KULIA
2. Aina aina
4. Wanaotazama
7. Mkuzaji mimea mbalimbali
10. Onyo
11. Tohoa satellite
12. Anayetumia
14. Simu ya mkononi
16. Kutoa maelezo kuhusu jambo au kisa
17. Hali ya kuwa sa
18. Utaratibu wa kufanya mambo
19. Waliohudhuria
CHINI
1. Upashanaji habari au taarifa kwa njia mbalimbali
3. Habari inayotumwa kwa mtu ili kumfahamisha jambo
5. Uwezo
6. Kwenye jukwaa
7. Kutenda kama kitu au mtu afanyavyo
8. Mafanikio/ustawi
9. Wanaosoma shuleni
13. Uasisi/uchuaji
15. Ni alama ya uakishi pia huonekana usiku (udogo)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 126 12/11/2019 09:44
127
A. Ufahamu
Peremende za Bwana Pipi
Bwana Marisedi alifahamika ka pale kijijini Mairo. Alikuwa akifanya kazi jijini. Alipotelea huko
mara tu baada ya kuyamaliza masomo yake ya shule ya upili ambamo hakufua dafu kamwe.
Wazazi wake hawakuwa watu wenye uwezo. Babake alikuwa mfuga nyuki maarufu ambaye
hakuwanyima wanakijiji asali kila alipoirina. Lakini sasa biashara hiyo ilikuwa imeenda chini
sana. Mamake naye alikuwa mkulima wa mboga alizozichuuza katika soko la kijiji. Alitumia
maji ya chemchemi ndogo katikati ya shamba lake kunyunyizia maji mboga zake hizo.
Hata hivyo, hali ya wazazi wa Marisedi ilibadilika alipokwenda mjini. Baada ya kuishi mjini
kwa muda wa miezi sita, alituma ripoti nyumbani kuwa ameshapata kazi ya maana. Miezi kadhaa
baadaye alirejea nyumbani na mabunda ya noti. Kwanza aliwajengea wazazi wake nyumba nzuri
sana. Aliwalipia karo ndugu zake waliokuwa washafukuzwa shuleni kutokana na kutolipa karo.
Alijijengea jumba la fahari huko huko kijijini. Maisha ya familia nzima yalibadilika kabisa kwa
muda mfupi sana. Amepata wapi pesa za aina hii kwa kipindi kifupi hivi? watu waliulizana.
Baada ya kuikamilisha miradi yake pale kijijini, Marisedi alirudi jijini. “Likizo yangu sasa
imekwisha. Itabidi nirejee kazini kule jijini, aliwaambia watu. Sasa alizoea kuka kijijini kila
mwishoni mwa wiki. Lakini wakati huu alikuja na vijifuko vya peremende. Mara nyingi mwishoni
mwa wiki kulikuwa na mchezo wa kandanda kwenye uwanja wa kijiji uliokuwa karibu na soko
kuu. Bwana Marisedi alikuwa akiliegesha gari lake la kifahari pale. Baada ya mchezo kumalizika,
alichukua mfuko wa peremende na kuwapa vijana huku akiwapongeza, Mmecheza vyema sana
leo. Hii zawadi yenu ya pipi!” Walizichukua na kuzimung’unya kwa furaha huku wakimshukuru
Bwana Marisedi kwa ukarimu wake huo. Vijana wengi walizidi kuvutiwa sana na zawadi za
Bwana Marisedi. Hata jina lake sasa wakalibadilisha. Wakamwita Bwana Pipi.
Siku zilipozidi kupita, peremende za Bwana Pipi zikazidi kuwavutia vijana wengi zaidi.
Ilisemekana kwamba wale waliozitumia hawakuburudika tu bali walicheza kwa nguvu zaidi
wakiwa na msisimko mkubwa. Bwana Pipi akazidi kuwa mtu maarufu kweli kweli pale kijijini
Mairo. Lakini siku moja alipoka kijijini hakuwa na pipi zake. Alipoulizwa kisa na maana akasema,
Siku hizi imekuwa vigumu kuzipata. Nilikuwa nikipewa bure na jamaa mmoja raki yangu,
lakini sasa amefunga duka na kuhamia kwao Bara Hindi. Sasa nikizitaka itabidi nizinunue. Na
zenyewe ni ghali mno. Naona afadhali tukae tu. Tutazoea. Lakini vijana hawakutaka kusikia
hayo. “Si utanunua tu. Kwani ni pesa ngapi? Twambie tukutume ukatununulie.
Basi ikakubaliwa vijana wachange pesa ili wamtume Bwana Pipi akawaletee peremende. Wiki
iliyofuatia, Bwana Pipi alirejea na mifuko mingi ya pipi. Kulikuwa na furaha ya ajabu. Siku hiyo
vijana walicheza kwa furaha nyingi. Baada ya mchezo, badala ya kushangilia timu iliyoshinda,
Bwana Pipi ndiye aliyepata shangwe. “Bwana Pipi hoyee!” wengine walisema. Hoyeee!” wenzao
waliitikia.
Kila Jumamosi Bwana Pipi alirejea kijijini akiwa na mifuko chungu nzima ya pipi alizokuwa
ametumwa na vijana awanunulie huko jijini.
Sura ya Kumi na Mbili
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 127 12/11/2019 09:44
128
Lakini siku moja jambo la ajabu sana lilitokea. Siku hiyo kulikuwa na mashindano ya kuwania
ubingwa wa soka tarafani. Kwa hivyo ilibidi kila timu ijibwage uwanjani mara kadha. Kwa mara
ya kwanza michezo hiyo mwaka huo ilifanyika pale kijijini Mairo. Timu nyingi zilika kutoka
kila pembe tarafani. Kila baada ya mechi kumalizika, Bwana Pipi aliwapa wachezaji wa timu ya
Mairo pipi zao. Nao wakazifurahia kweli kweli. Siku hiyo wachezaji wa Mairo walibugia pipi
mara tatu zaidi ya vile walivyozoea. Walikuwa na hamu kuu ya kuwa mabingwa wa soka tarafani
kwa mara ya kwanza. Ndipo mambo ya kushangaza yalipoanza kutokea. Katika mechi ya nusu
fainali kati ya timu ya Mairo na ile ya Ichagaki mwendo wa saa tisa alasiri, mchezaji wa timu
ya Mairo akaanza kuona kizunguzungu. Baada ya muda akaanguka na kuzimia. Akakimbizwa
haraka katika zahanati iliyokuwa karibu na soko kuu. Mchezo ukaendelea. Lakini mambo yakazidi
kuharibika. Wachezaji watano zaidi wa timu ya Mairo walianguka mmoja baada ya mwingine na
kuzimia. Walibebwa hangahanga hadi kwenye zahanati kupewa huduma ya kwanza. Baadhi ya
watu wakaamua kumuuliza Bwana Pipi kama kulikuwa na uwezekano kuwa zile peremende zake
zilikuwa na kasoro siku hiyo. Wakamtafuta kila mahali uwanjani. Hakuweko. Bwana Pipi alikuwa
ametoweka. Watu wakazidi kushangaa. Na jambo la ajabu ni kuwa miongoni mwa wachezaji wa
timu ya Ichagaki waliokuwa wakicheza na Mairo hakuna aliyekuwa na shida. Ilibidi mchezo
usimamishwe. Wazazi waliokuwa wamekuja kutazama mchezo siku hiyo walizingira lango la
kuingilia zahanati huku wakilengwalengwa na machozi. Hali ya vijana hao ilizidi kuharibika.
Ilibidi wakimbizwe haraka hadi hospitali kuu ya wilaya ambako walilazwa wakiwa hali mahututi.
Siku mbili baadaye, taarifa ya kushangaza ilika kijijini kutoka hospitali kuu wilayani.
Ilitambuliwa kuwa wale vijana walikuwa wamemeza dawa za kulevya. Peremende za Bwana
Pipi hazikuwa peremende za kweli, bali zilikuwa zimechanganywa na dawa za kulevya. Oh!
Jamani! Kumbe umdhaniaye siye ndiye na umdhaniaye ndiye siye?” waliulizana wanakijiji kwa
mshangao mkubwa. Tangu siku hiyo, Bwana Pipi alitoweka kijijini kama umande. Lakini duru
za kuaminika zilisema kuwa mkono mrefu wa serikali ulikuwa ukimsaka Bwana Pipi usiku na
mchana na kulikuwa na matumaini kuwa siku yake ya arobaini ilikuwa ikikaribia.
Kutokana na kisa hicho cha kuhuzunisha, wanakijiji wa Mairo walianza harakati za
kuwaelimisha vijana na jamii nzima kuhusu hatari za dawa za kulevya.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 128 12/11/2019 09:44
129
Maelezo ya msamiati
fahamu ka : fahamu vizuri au kabisa.
kabumbu : kandanda.
bugia : kula kwa wingi; jaza kinywani; kula haraka.
Maswali
1. Eleza jinsi wazazi wa Bwana Pipi walivyokuwa kabla ya yeye kuhamia jijini.
2. Je, unakiri Bwana Pipi alipotuma taarifa kuwa amepata kazi ya maana alikuwa akisema
ukweli? Fafanua.
3. Unakiria Bwana Pipi alipata wapi pesa za kufanya yote aliyofanya pale kijijini?
4. Panga sentensi hizi kulingana na jinsi mambo yalivyotokea pale kijijini Mairo:
(a) Bwana Pipi atoweka.
(b) Bwana Pipi awaambia vijana kuwa hawezi kupata tena pipi.
(ch) Bwana Pipi awajengea wazazi wake nyumba.
(d) Bwana Pipi aenda kutafuta kazi jijini.
(e) Bwana Pipi awapa vijana pipi kupita kiasi siku ya michezo.
5. Unakiri ni kwa nini Bwana Pipi alitoweka?
6. Je, hadithi hii ina mafunzo gani kuhusu dawa za kulevya?
7. Onyesha maana za maneno na misemo hii kulingana na vile ilivyotumika kwenye kifungu:
(i) zahanati (ii) kuzichuuza (iii) chemchemi
(iv) umande (v) ametoweka (vi) pipi
(vii) kuona kizunguzungu (viii) beba hangahanga (ix) huduma ya kwanza
(x) dawa za kulevya
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii
Sajili ya sokoni
Sura ya Tisa ilizungumzia sajili ya dukani. Sajili ya sokoni, sawa na sajili ya dukani, hujumlishwa
kwenye sajili pana ya biashara. Hivyo basi baadhi ya sifa hufanana.
Sifa za sajili ya sokoni ni:
(a) kuwepo kwa msamiati maalum ambao unarejelea shughuli zinazoendelea sokoni k.v.
bidhaa tofauti tofauti, harakati za sokoni n.k.
(b) matumizi ya chuku au tabia ya kuongeza chumvi katika maongezi au mazungumzo. Muuzaji
hujaribu kusifu bidhaa zake kupita kiasi ili kumshawishi mnunuzi
(ch) lugha ya kushawishi: Lengo kubwa ni kuhakikisha kuwa mnunuzi amenunua bidhaa. Ili
kufanikiwa katika lengo hili muuzaji hutumia lugha ya kushawishi
(d) kuchanganya au kubadilisha ndimi au msimbo: Msimbo ni mfumo maalum wa kuwasiliana
ambao unaweza kuwa lugha au matumizi ya ishara. Katika muktadha wa sokoni, uwezekano
wa kuchanganya lugha, k.v. sheng, Kiingereza, Kiswahili au hata lugha nyingine za kikabila
ni mkubwa
(e) matumizi ya kauli fupi fupi: Lengo la kuuza na kununua ni kutimiza shughuli hiyo kwa
ufupi. Hapana sababu ya kuwepo kwa maelezo marefu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 129 12/11/2019 09:44
130
(f) Mvutano katika mazungumzo: Hali hii hutokana kwa sababu muuzaji anataka kunufaika
na mnunuzi kwa upande wake anataka kupata anachohitaji kwa bei nzuri
(g) Kutozingatia lugha sanifu au kanuni za lugha kama sarufi. Si ajabu kuona lugha
inayotumiwa inavunja kanuni za lugha kwa sababu lengo ni kuhakikisha kuwa wanaohusika
wamewasiliana.
(h) Matumizi ya misimu au maneno yasiyokuwa rasmi. Huu ni muktadha usiokuwa rasmi kwa
hivyo si ajabu kuona matumizi ya maneno ambayo hupatikana katika lugha ya mitaani.
Soma kifungu kifuatacho
(Mteja anakwenda. Anasogelea mahali ambako kuna mfanyi biashara)
: H  
: N, 
: S.
: H,   
: N    ,   ,  
    .
: U    .
: H 
: I (). T    (M 
  ) V  
: J,     
: J    .
: L V      
: N   
: J K    
: L H      . L   
  .
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 130 12/11/2019 09:44
131
: N       . ( ) S 
    
: L      . (  )
: () H    
: H     
: H  , .
: K 
Zoezi
1. Eleza kwa kifupi sifa za lugha ya sokoni
2. Je, ni mambo yepi yanayoongoza uteuzi wa lugha katika muktadha wa sokoni
CH. Saru na matumizi ya lugha
Ngeli za nomino
Upatanisho wa kisaru: Viambishi awali vya vitenzi
Viambishi vya upatanisho wa kisaru ni vile ambavyo hutumika kulingana na ngeli. Kwa hivyo
ngeli inapobadilika navyo viambishi hivi hubadilika. Mara nyingi makosa ya kisaru hutokana
na matumizi mabaya ya viambishi hivi vya upatanisho wa kisaru.
Ngeli ya a-wa
umoja wingi
Ng ’o m b e analala. Ng’ombe wanalala.
Punda atachoka. Punda watachoka.
Mtoto alisoma. Watoto walisoma.
Panya ametoroka. Panya wametoroka.
Mkulima amevuna. Wakulima wamevuna.
Ngeli ya u-i
umoja wingi
Mti umeanguka. Miti imeanguka.
Mfupa utavunjika. Mifupa itavunjika.
Mwiba ulikuchoma. Miiba ilikuchoma.
Mkate umeliwa. Mikate imeliwa.
Msumari uko wapi? Misumari iko wapi?
Ngeli ya u-ya
umoja wingi
Ugonjwa umekwisha. Magonjwa yamekwisha.
Upana utatosha. Mapana yatatosha.
Uasi umeanza. Maasi yameanza.
Uchungu ulizidi. Machungu yalizidi.
Ulezi ulifaa. Malezi yalifaa.
Ngeli ya li-ya
umoja wingi
Tunda linaliwa. Matunda yanaliwa.
Yai liko wapi? Mayai yako wapi?
Tawi litakatwa. Matawi yatakatwa.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 131 12/11/2019 09:44
132
Ua limechanua. Maua yamechanua.
Nanasi limeliwa. Mananasi yameliwa.
Ngeli ya ya
umoja wingi
Maji yamekwisha. Maji yamekwisha.
Manukato yananukia. Manukato yananukia.
Maziwa yamechemka. Maziwa yamechemka.
Majira yana baridi. Majira yana baridi.
Marashi yamenunuliwa. Marashi yamenunuliwa.
Ngeli ya ki-vi
umoja wingi
Kiatu kitapotea. Viatu vitapotea.
Kisu kiko pale. Visu viko pale.
Cheti kimetolewa. Vyeti vimetolewa.
Chakula kimekwisha. Vyakula vimekwisha.
Kitabu kiko ndani. Vitabu viko ndani.
Zoezi
Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kujaza pengo kwa viambishi mwafaka vya upatanisho wa kisaru
kisha uonyeshe ni vya ngeli gani.
Umoja Wingi
Ngeli
K.m. Mtoto analia.
Kisu mepotea.
Mlima tapandwa.
Ugonjwa likwisha.
Kuku mechinjwa.
Duka na vitabu.
Shamba lilimwa.
Kiti lianguka.
Ulezi nafaa.
Mkufu mepotea.
Chuo tafungwa.
Nzi naruka.
Kioo mevunjwa.
Mwizi metoroka.
Upendo lizidi.
Maji memwagwa.
Mtaro lichimbwa.
Kiroboto mekufa.
Manukato nanukia.
Shamba talimwa.
Mjomba takuja.
Watoto wanalia.
Visu
mepotea.
Milima
tapandwa.
Magonjwa
likwisha.
Kuku
mechinjwa.
Maduka
na vitabu.
Mashamba
lilimwa.
Viti
lianguka.
Malezi nafaa.
Mikufu mepotea.
Vyuo tafungwa.
Nzi naruka.
Vioo mevunjwa.
Wezi metoroka.
Mapendo lizidi.
Maji memwagwa.
Mitaro lichimbwa.
Viroboto mekufa.
Manukato nanukia.
Mashamba talimwa.
Wajomba takuja.
a wa
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 132 12/11/2019 09:44
133
D. Kusoma
Fasihi andishi: Tamthiliya
Tamthilia ni mchezo (wa kuigiza) ulioandikwa kwa mtindo wa mazungumzo baina ya watu
mbalimbali. Usomaji wa tamthilia unapaswa kuzingatia mambo kadha. Tamthilia hutumia lugha
ya mazungumzo sio lugha ya insha kama riwaya. Pili, huandikwa ili kuigizwa jukwaani. Tatu,
haina sura bali ina maonyesho au matendo. Nne, kwa kawaida huwa fupi kuliko riwaya.
Mambo ya kuchunguza
Baada ya kuisoma tamthilia, tunapasa kujiuliza inazungumzia nini, yaani ina maudhui gani?
Ili kulijibu swali hili kikamilifu tunaangalia mambo wanayoyazungumzia wahusika kuanzia
mwanzo mpaka mwisho. Tunaangalia:
(a) Dhamira: Je, lengo la mwandishi ni nini? Kwa kawaida tunaelekezwa kwenye dhamira na
kichwa cha tamthilia.
(b) Maadili/mafunzo: Je, mwandishi anawasilisha mafunzo ya aina gani? Je, anataka tujifunze
mambo ya aina gani kutokana na wahusika wake au maudhui?
Baada ya kujua tamthilia inazungumzia nini, tunapaswa sasa kuangalia jinsi mambo hayo
yanavyozungumziwa, yaani fani. Hapa tunaangalia:
(i) Matumizi ya lugha: Tofauti na riwaya, katika tamthilia wahusika wanaongea
kwa kujibizana au kwa mazungumzo au dayalojia. Tunapaswa kuangalia jinsi
wanavyotumia lugha yao n.k.
(ii) Muundo na mtindo: Je, tamthlia imepangwa namna gani? Je, ina maonyesho au
matendo mangapi? Je, inaanzia wapi na kuishia wapi? Je, kuna sifa zipi za matumizi
ya lugha?
(iii) Wahusika: Matendo ya tamthilia yanatendwa na viumbe ambao ni wahusika. Je,
kuna wahusika wangapi? Je, wahusika hao wanafanya nini? Je, wahusika hao wana
sifa gani?
E. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Ratiba
Ratiba ni mpango wa mfululizo wa mambo yanayofanyika au yatakayofanyika katika uendeshaji
wa shughuli fulani kulingana na wakati uliotengwa. Ratiba hutayarishwa kwa shughuli mbalimbali.
Kwa mfano: huweza kutayarishwa ili kutumiwa wakati wa mashindano ya michezo baina ya shule
mbalimbali au mabweni katika shule moja, wakati wa mkutano fulani, sherehe mbalimbali, n.k.
Mambo muhimu katika uandishi wa ratiba:
Kutambua, kwanza, ni shughuli zipi zitakazohusika wakati fulani maalum.
Kupanga kila shughuli kuanzia ya kwanza hadi ya mwisho.
Kuhakikisha kuwa kila shughuli inapangiwa wakati maalumu.
Kuhakikisha kuwa kichwa cha shughuli inayohusika kimeandikwa juu pamoja na tarehe
na mahali pa shughuli inayohusika.
Kila tukio liambatanishwe na wakati wa kutendeka kwake.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 133 12/11/2019 09:44
134
Aghalabu tukio la kwanza huwa ni ufunguzi na maamkizi, hotuba fupi na uzinduzi wa
sherehe.
Tukio la mwisho huweza kuwa hotuba fupi, kutoa shukrani na kufunga.
Utaratibu wa ratiba hufungamana na suala linalohusika.
Mfano
Ratiba ya Mkutano wa Harambee ya Ujenzi wa Bweni
Shule ya Upili ya Twaweza, Tarehe 4 - 4 - 2018
Saa 7.30 asubuhi: Mkutano wa wanafunzi na mwalimu mkuu.
Saa 8.00 asubuhi: Kupangwa kwa uwanja wa mkutano.
Saa 9.00 asubuhi: Wanafunzi, walimu na wageni waalikwa kuketi.
Saa 9.30 asubuhi: Kuwasili kwa mgeni mheshimiwa, Prof. Kiwilo Massamba,
Waziri wa Elimu.
Saa 9.45 asubuhi: Kukaribishwa kwa mwalimu mkuu na Mwenyekiti wa PTA
Saa 10.00 asubuhi: Burudani ya muziki na vikundi mbalimbali vya shule.
Saa: 10.30 asubuhi: Hotuba fupi ya mwalimu mkuu, Bwana Mjawema Kibao.
Maelezo mafupi kuhusu malengo ya harambee.
Saa 10.40 asubuhi: Harambee kuanza
Saa 1.00-2.00 asubuhi: Kumalizika kwa harambee. Maakuli kwa wageni walioteuliwa
na wanafunzi.
Zoezi
Andika ratiba ya sherehe za kuzaliwa kwa dada yako mdogo itakayofanyika Jumamosi ijayo.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 134 12/11/2019 09:44
135
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2 3 4
5
6 7 8
9 10
11
12 13
14
15
16
17
18
19
KULIA
2. KT
10. Bila kucha
12. Mambo yanayotuzunguka
14. KN
16. Vinavyokaa bila mpango na havifai kwa matumizi
17. Ufupisho
18. Pahali pa kusindikia bidhaa
19. Wingi wa kichekesho
CHINI
1. Hali ya kufanya mazingira kutokua sa
3. Aina ya shairi
4. Kumi mara tatu
5. Aina ya sentensi
6. Saratani
7. Wingu jeupe au jeusi litokanalo na kuunguzwa kwa kitu
8. Vinavyosababisha kuchafuka
9. Hali ya kuwa sa
11. Simba, chui, swara, ndovu n.k
13. Yenye maana
15. Ndani ya bahari
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 135 12/11/2019 09:44
136
A. Ufahamu
Methali ni johari
Methali ni fungu fupi la maneno lenye asili ya maarifa mengi. Methali ni tokeo la hekima ya
jamii. Tumekuwa tukipokezana methali toka zamani za kale. Kweli halisi au neno lenye maana
kubwa hupita mara kwa mara kutoka mtu hadi mtu likawa methali. Methali ni kiini cha hekima
na utaalamu. Haijadiliani wala haielezi; husema kweli tupu waziwazi kwa ufupi wenye maana.
Licha ya kuwa methali husema kweli fulani kwa ufupi, maisha si mepesi sana ya kuelezwa
kwa fungu moja la maneno au methali. Hivyo methali hueleza sehemu moja tu ya kweli nayo si
ukweli wote. Kweli huwezekanaje kuelezwa kwa fungu moja la maneno? Mtaalamu huona kweli
katika pembe fulani akaeleza kwa namna ya methali. Wataalamu mbalimbali wana maarifa tofauti.
Huona maisha katika pembe mbalimbali. Pengine maoni yao huakiana na pengine hayaakiani.
Pana methali inenayo, “Mwenda pole haumii mguu. Methali hii yafanana na nyingine isemayo
“Haraka haraka haina baraka. Juu ya hili, pana methali zisizopatana kama Bahati ya mwenzio
usiilalie nje na Kila jasiri salama. Methali moja yasema, Nyama ya usiku hainoni” wakati
methali nyingine isemapo, “Usiku ni libasi bora. Methali kama hizi hueleza namna mbili za
maarifa au pande mbili za ukweli.
Hapana methali ambayo kinyume chake hakipatikani. Lakini hili halimaanishi kwamba
methali zina dosari au hazifai. Hii ni sifa ya methali zote zinazopatikana katika jamii mbalimbali.
Kila jamii ina methali zake. Licha ya haya, tunaona mara nyingi kwamba methali nyingi za
jamii moja hufanana na zile za jamii nyingine. Hali hii huonyesha maarifa mamoja kila mahali
na kwamba kweli hudumu bila ya kubadilika katika nchi mbalimbali na watu mbalimbali.
Methali hutumiwa na jamii zote za watu. Pengine wakubwa wetu wanapotushauri hudondoa
methali. Hata methali za maneno makali hutumiwa. Watu wazima hutumia sana methali kwa
kuwafaidi na kuwafurahisha. Inasemekana kwamba washairi bora, wataalamu weledi, wanachuoni
arifu na waandishi mahiri wamezifurahia methali sana. Wamezitumia sana tena mara kwa mara.
Methali hutufaa kwa kutukumbusha yatupasayo kutenda. Ni raki, mwalimu na mwongozi
kwa mtu wa desturi. Tukizitia maanani sana twaweza kuzitumia kama walimu katika maisha yetu.
Ukurasa wa maandiko au mashauri haufai sana kuliko nusu ya mstari wa methali. Huwezekana
kukumbukwa upesi. Baadaye methali nyingi huwa sehemu ya maisha yetu. Tukizifuata kwa
uangalifu, tutapata faida chungu nzima. “Ukila cha mwenzio na chako huliwa, ina onyo jema,
ambalo likifuatwa, huepusha matata mengi.
Methali zisichekwe wala zisidharauliwe kwa sababu ni nyepesi na nyingi. Kwa mfano methali
inayojulikana na watu wote, Haraka haraka haina baraka, labda twaikariri kama kasuku bila
kukiri, lakini hatuzingatii ubora wake mpaka tunapoharibu kazi yetu kwa haraka. Wazia methali
nyingine “Ukitaka kuruka agana na nyonga. Je, tunaikumbuka methali hii wakati tutendapo
mambo muhimu?
Methali ni hekima ya vizazi vya wanadamu iliyofupishwa kwa maneno machache mazuri. Ni
urithi wetu bora kabisa. Yatupasa kuzihifadhi na kuzitumia kwa uangalifu.
(Kifungu hiki kimehaririwa upya kutoka S. Robert ‘Methali na Matumizi yake, Kielezo cha Insha,
uk. 37- 8)
Sura ya Kumi na Tatu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 136 12/11/2019 09:44
137
Maelezo ya msamiati
weledi : bora; wazuri.
arifu : wenye ujuzi; wenye maarifa.
mahiri : stadi; bora.
Maswali
1. Ni nini asili ya methali?
2. Andika methali nne zilizotajwa kwenye kifungu hiki na ueleze maana zake.
3. Ina maana gani kusema, maisha hayawezi kuelezwa kwa fungu moja la maneno?’
4. Andika jozi tano za methali zenye maana zinazofanana na uonyeshe jinsi maana zake
zinavyofanana.
5. Methali zina manufaa yapi katika maisha yetu?
6. Kamilisha methali zifuatazo na ueleze maana zake:
(a) Aambiwaye akakataa _______________.
(b) Abakiaye mekoni ______________.
(ch) __________ hujishika.
(d) Acha koko __________.
(e) Achanikaye kwenye mpini __________.
(f) Achekaye kilema ______________.
(g) Achezeaye tope ____________.
(h) Ada ya mja hunena: ______________.
(i) ________________, faida yake huonekana mtoto akuapo.
(j) ____________ aijuaye maiti.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii: Sajili: Lugha ya shuleni
Isimujamii: Sajili ya shuleni
Lugha inayotumiwa shuleni ina sifa mbili kuu. Kwanza, huwa rasmi pale ambapo wanaohusika
wanaingiliana katika muktadha rasmi kama mwalimu na mwanafunzi. Wanafunzi wanapokuwa
peke yao huweza kutumia lugha ambayo si rasmi na ambayo inafungamana na mada zao wenyewe
kwa wenyewe. Katika muktadha huu basi, sajili hii huongozwa na kuelekezwa na uhusiano baina
ya wanaohusika. Sajili ya shuleni ina sifa zifuatazo:
(a) Lugha sanifu: Hali hii hutokea hasa katika muktadha rasmi kama darasani au osini
(b) Matumizi ya sentensi ndefu au maelezo ya kina hasa katika muktadha wa darasani. Kwa
mfano, panapofafanuliwa hoja au wazo fulani k.v. mwalimu anapofundishwa
(ch) Lugha inayoonyesha tofauti za cheo au ngazi: Mwanafunzi anayeongea na mwalimu hawezi
kutumia lugha kama anavyokuwa na mwanafunzi mwenzake. Msamiati atakaoutumia
unaonyesha tofauti hizi. Kwa mfano, matumizi ya maneno ya heshima au adaabu, lugha
ya unyenyekevu n.k. Mwalimu anaweza kutumia lugha ya kuhoji zaidi
(d) Kuchanganya ndimi huweza kutokea katika miktadha fulani
(e) Mwelekeo wa kuwepo na mzungumzaji anayeyaongoza mazungumzo. Kwa mfano,
mwalimu anapotaka kutambua jambo fulani, atauliza maswali ambayo yanaonyesha kuwa
ndiye anayeyaongoza na kuyaelekeza mazungumzo.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 137 12/11/2019 09:44
138
(f) Kuwepo kwa lugha ya ushauri na nasaha hasa pale ambapo mwalimu anawaelekeza
wanafunzi.
(g) Huweza kuwepo na msamiati unaoeleweka tu katika muktadha wa shule inayohusika
k.v. wazungumzaji wanapozungumzia mada zinazohusu mazingira ya shule yenyewe k.v.
mabweni, maeneo mahsusi ambayo yana majina fulani
Soma kifungu kifuatacho
(Mwalimu mkuu yuko osini. Mlango unagongwa na mwanafunzi anaingia ndani.)
’: S 
 : M, E’ 
’: S. (K) M   
: N  . H   (E’  ) K
. (A) S E’. . .
’: N 
: N      .
’: N 
: N   ;   .
’: N 
: U     . U
        
  . W    
. N      
 . J,     (K) J, 
   
’: L
: J, 
’: (A ) M. . .
: N   
’: M… ()
: U E’;    .
’: N 
: (A   ) B  
’: S . . . (   )
: (  ) U E’ H    
E’
’: H   () A . H  …
  .
: (A ) P… () J,   
  K
’: L. A  
: M…N,      . E’,
      . L …
    . (  ) J, 
     J   S
W
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 138 12/11/2019 09:44
139
’: (A  ) N 
: N . L      
,  (  ) K   
,       
 . () K     .
’: A  ()
Maswali
1. Je, ni sifa zipi za sajili ya shuleni zinazodhihirika kwenye kifungu hiki?
2. Eleza kaida zinazoongoza matumizi ya lugha katika muktadha wa shuleni.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Ukubwa na udogo wa nomino
Nomino huweza kuwa katika hali ya wastani, hali ya udogo au hali ya ukubwa. Kiungo muhimu
katika kuunda nomino za hali ya ukubwa au udogo ni mzizi wa nomino. Ikiwa mzizi wa nomino
umeundwa kwa silabi mbili au zaidi, kiambishi cha nomino ya hali ya udogo huwa ki katika
umoja na vi katika wingi. Licha ya udogo, viambishi hivi huweza kutumika kwa nia ya kudunisha
au kudharau.Tazama jedwali lifuatalo:
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za udogo
umoja wingi umoja wingi
-toto
-lima
-buzi
-pete
-fupa
-zee
-guu
-lango
-goma
-dege
-meza
-twana
mtoto watoto
mlima milima
mbuzi mbuzi
pete pete
mfupa mifupa
mzee wazee
mguu miguu
mlango milango
ngoma ngoma
ndege ndege
meza meza
mtwana watwana
kitoto vitoto
kilima vilima
kibuzi vibuzi
kipete vipete
kifupa vifupa
kizee vizee
kiguu viguu
kilango vilango
kigoma vigoma
kidege videge
kimeza vimeza
kitwana vitwana
Hata hivyo, kiambishi ji huweza kutokea baada ya ki hata ikiwa mzizi wa nomino umeundwa
kwa zaidi ya silabi moja. Jambo hili huonyesha hasa dhana ya dharau au kudunisha.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 139 12/11/2019 09:44
140
Tazama jedwali lifuatalo:
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za udogo
umoja wingi umoja wingi
-toto
-lima
-buzi
-pete
-fupa
-zee
-guu
-lango
-goma
-dege
-meza
-twana
mtoto watoto
mlima milima
mbuzi mbuzi
pete pete
mfupa mifupa
mzee wazee
mguu miguu
mlango milango
ngoma ngoma
ndege ndege
meza meza
mtwana watwana
kijitoto vijitoto
kijilima vijilima
kijibuzi vijibuzi
kijipesa vijipesa
kijifupa vijifupa
kijiduka vijiduka
kijiguu vijiguu
kijilango vijilango
kijigoma vijigoma
kijidege vijidege
kijimeza vijimeza
kijitwana vijitwana
Iwapo mzizi wa nomino umeundwa kwa silabi moja au unaanza kwa irabu, nomino ya udogo
huchukua kiambishi ki katika umoja na vi katika wingi vikifuatwa na ji (au j).
Tazama jedwali lifuatalo:
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za udogo
umoja wingi umoja wingi
-tu
-ji
-ana
-to
-oka
-izi
-umba
-su
-chwa
-we
-iko
mtu watu
mji mji
mwana wana
mto mito
nyoka nyoka
mwizi wezi
nyumba nyumba
kisu visu
kichwa vichwa
jiwe mawe
mwiko miko
kijitu vijitu
kijiji vijiji
kijana vijana
kijito vijito
kijoka vijoka
kijizi vijizi
kijumba vijumba
kijisu vijisu
kijichwa vijichwa
kijiwe vijiwe
kijiko vijiko
Katika hali ya ukubwa, iwapo mzizi wa nomino umeundwa kwa silabi moja au umeanza kwa
irabu, kiambishi cha hali ya umoja ni ji au j. Katika wingi, nomino huanza kwa kiambishi ma
(au mi) kikifuatwa na kiambishi ji (au j). Zaidi ya kuonyesha ukubwa, viambishi hivi pia huweza
kuonyesha hali/tabia.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 140 12/11/2019 09:44
141
Tazama jedwali lifuatalo:
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za ukubwa
umoja wingi umoja wingi
-tu
-to
-oka
-ti
-ana
-umba
-ungu
-izi
-su
-ke
-bwa
mtu watu
mto mito
nyoka nyoka
mti miti
mwana wana
nyumba nyumba
nyungu nyungu
mwizi wezi
kisu visu
mke wake
mbwa mbwa
jitu majitu/mijitu
jito majito/mijito joka
majoka/mijoka
jiti majiti/mijiti
jana majana/mijana
jumba majumba/mijumba
jungu majungu/mijungu
jizi majizi/mijizi
jisu majisu/mijisu
jike majike/mijike
jibwa majibwa/mijibwa
Nomino nyingi zilizoundwa kwa mizizi ya zaidi ya silabi moja hazina kiambishi ji cha umoja
lakini huchukua kiambishi ma cha wingi. Tazama:
Mzizi Nomino ya wastani Nomino ya ukubwa
umoja wingi umoja wingi
-toto
-dude
-paka
-buzi
-goma
-dege
mtoto watoto
kidude vidude
paka paka
mbuzi mbuzi
ngoma ngoma
ndege ndege
toto matoto
dude madude
paka mapaka
buzi mabuzi
goma magoma
dege madege
Zoezi
Andika udogo na ukubwa wa nomino hizi:
(a) kitabu (b) mbuzi (ch) ugonjwa (d) simu
(d) n g ’o m b e (e) tunda (f) mwenge (g) kioo
(h) jicho (i) kiti
D. Kusoma
Matumizi ya kamusi
Kamusi ni kitabu kinachohifadhi maneno yanayopatikana katika lugha fulani katika wakati fulani.
Hueleza maana ya maneno hayo kwa njia inayoeleweka na watumiaji wa lugha hiyo pamoja na
wanaojifundisha lugha inayohusika.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 141 12/11/2019 09:44
142
Umuhimu wa kamusi
Kujua maana za maneno mbalimbali tunayokumbana nayo katika kusoma kwetu.
Kujua jinsi maneno mbalimbali yanavyoendelezwa au kuandikwa; yaani kuzijua tahajia
zake.
Hutoa maelezo au taarifa kuhusiana na ngeli za nomino zinazopatikana katika lugha
inayohusika.
Kupata maelezo kuhusu umoja na wingi. Kuna maneno ambayo yanabadilika kiumbo
katika wingi na mengine ambayo hayabadiliki. Taarifa hizi hupatikana katika kamusi.
Kutuelekeza jinsi ya kutumia neno fulani. Kuna kamusi ambazo hutoa mifano ya jinsi ya
kuyatumia maneno mbalimbali kwa kutumia sentensi fulani. Msomaji anafaidika kwa
kujua jinsi ya kulitumia neno ipasavyo.
Kuonyesha jinsi ya kuyatamka maneno. Kamusi zenye maelezo ya jinsi ya kutamka
huwasaidia watumiaji wa kamusi kujua jinsi ya kulitamka neno ipasavyo. Kamusi nyingi
zilizoandikwa kwa lugha ya Kiswahili hazina taarifa hizi lakini za Kiingereza zinazo. Hii
ni kwa sababu maneno mengi ya Kiswahili hutamkwa jinsi yanavyoandikwa.
Kamusi humwezesha mtumiaji kujua ni maneno yapi yenye maana sawa (visawe) na ni
maneno yapi yenye maana ya kinyume (vitawe). Sifa hizi hupatikana katika kamusi maalum
kama kamusi ya visawe.
Muundo na mpangilio wa kamusi
Maneno yanayopatikana katika kamusi hupangwa kwa utaratibu wa kialfabeti au kiabjadi
kuanzia A mpaka Z.
Upande wa juu pembeni mwa kamusi huwa na maneno ya kumwongoza mtumiaji. Maneno
haya hujulikana kama maneno elekezi. Kwa kawaida ukurasa wa kamusi huwa na vipande
viwili. Neno elekezi la kwanza huwa ni lile la kwanza katika kipande cha kwanza upande
wa kushoto. Neno elekezi la pili huwa ni neno la mwisho kwenye kipande cha pili kulia.
Kwa kuangalia maneno hayo, mtumiaji anaweza kutambua kama neno analotafuta linaingia
pale kiabjadi. Tuangalie mfano huu:
baka bananga
baka: doa, baku, paku.
Baada ya kupoa jeraha alikuwa na baka
kubwa mkononi.
bananga: haribu kazi. Haijui kazi hii
anaibananga tu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 142 12/11/2019 09:44
143
Kwa kuangalia mfano huu wa ukurasa, mtumiaji anayetafuta maana ya neno ‘banda
anatambua kuwa halipatikani katika ukurasa huo kwa sababu kulingana na alfabeti neno
hilo linakuja baada ya ‘bananga.
Maneno elekezi yanamwezesha mtumiaji wa kamusi kuweza kulitafuta neno haraka bila
ya kupoteza wakati mwingi katika ukurasa fulani.
Kutambua neno lipi linakuja lini kunamaanisha kuwa lazima msomaji au mtumiaji wa
kamusi azijue alfabeti au abjadi zake vizuri. Kujua huku sio kwa kuangalia heru za kwanza
bali pia heru zinazofuata ili kuweza kutambua neno lipi linatangulia na lipi linafuatia.
Kwa mfano: kuku/kalamu/koa yote yanaanza kwa ‘k lakini yanafuatana hivi: kalamu/koa/
kuku.
Maneno huingizwa katika kamusi kama neno moja. Ikiwa ni kitenzi neno hilo huingizwa
bila ya kiambishi ‘ku cha kitenzi, yaani huwa: punga, piga, bana n.k. Neno linaloingizwa
katika kamusi hujulikana kitaalamu kama kidahizo (wingi: vidahizo)
Maswali
1. Taja manufaa manne ya kamusi.
2. Ukitaka kuangalia maana ya maneno yafuatayo kwenye kamusi utatazama maneno gani?
(a) ulinisumbua
(b) tutakusaidia
(ch) ninasoma
(d) alimchukulia
(e) wanalia
E. Kuandika
Uandishi wa insha ya masimulizi
Insha ya masimulizi ni insha inayohusu kusimulia kisa au tukio fulani lililotokea (uliloshuhudia).
Tukio hilo au kisa hicho kinaweza kuwa kisa ulichokishuhudia au kinginecho chochote; yaani
kinaweza kuwa kisa cha kubuni au cha kweli.
Mambo ya kuzingatia
Hakikisha umeteua insha itakayomsisimua msomaji.
Utangulizi wako uwe wa kuvutia au kumteka msomaji kiasi kwamba ana hamu ya
kuendelea.
Tumia lugha inayomnasa msomaji kwa utamu wake. Hakikisha umetumia nahau, methali
na misemo ya kila aina.
Hakikisha kuwa mawazo yako na lugha yako inaonyesha mfululizo na mtiririko mzuri
kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
Zoezi
Andika insha yenye kichwa Arusi niliyoishuhudia.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 143 12/11/2019 09:44
144
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3 4
5
6 7
8 9
10
11 12
13
14
15 16
17 18
KULIA
3. Sehemu ya mwili inayounga paja na gimba
4. Kupashana habari au taarifa
6. Ujuzi
8. Fanya kitu kiharibike haribu kitu
10. Maneno yanayotumiwa kutaja mtu au kitu
11. Pahali watu hupewa elimu au maarifa
13. Elimu aipatayo mtu kutokana na kusoma au kutenda
14 Viambishi vinavyokuja mwanzoni mwa kitenzi
15. Maana/ukuu
16. Kujali au kuwa macho
17. Hucha uchi
18. Werevu wa kuweza kuchagua linalofaa
CHINI
1. Ukubwa wa ngombe
2. Kueleza kuhusu tukio au kisa
4. Kitu kigumu cheupe ambacho hushikilia nyama ya mwili
5. Neno kuu katika kamusi
7. Toa msaada/saidia
9. Maneno yenye maana sawa
12. Mila
13. Mjuzi katika jambo fulani
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 144 12/11/2019 09:44
145
A. Ufahamu
Fungua Sesame
Jina la Nimrod lilipotea mara tu alipoanza kufanya kazi jijini Nairobi. Maraki na jamaa zake
waliamini kuwa alikuwa ameajiriwa huko mjini ingawa hakuna aliyeijua kazi yenyewe vizuri.
Hata hivyo waliamini kuwa lazima alikuwa na kibonge cha kazi kwa sababu alivalia kinadhifu
na kuishi maisha ya starehe. Tena yeye mwenyewe alikazania kusema kuwa alikuwa ameajiriwa
kazi ya maana. Maraki zake walimfahamu kama Bwana Sesame. Mtu wa kwanza aliyempa jina
hilo alisema alipendezwa na ujuzi na maarifa yake. “Huyu hakosi ufumbuzi wa tatizo lolote. Ni
kama ule mlango wa kisa cha Ali Baba na Wezi Arobaini. Ukisema fungua sesame unafunguka
tu, alisema mtu huyo.
Jamaa walioishi naye katika mtaa wa Urumo walishangazwa na utaratibu wake wa kazi. Mchana
kutwa alishinda chumbani mwake. Mara nyingi utamkuta ametulia tuli akitazama runinga yake
ndogo. Wakati mwingine atakuwa akifanya kazi zake ndogo ndogo huku akipiga mluzi bubu,
ambao haukusikika vizuri. Wakati mwingine atakuwa akiusikiliza muziki kwenye chombo chake
cha muziki kilichotingisha jengo zima kutokana na sauti yake nene.
Kwa kawaida alitoka chumbani jioni. Waliomjua walimchangamkia kutokana na uchangamfu
wake. Alipenda sana mizaha. Waliopenda kupiga soga walivutiwa na maongezi yake hasa kuhusiana
na magari. Aliyajua magari mengi. “Mimi naweza kuijua aina ya gari kwa kuusikiliza mlio wake
tu, alisema kila wakati. Wacha kutuvungavunga bwana wee, haiwezekani! atasema mwingine.
“Nini? Unajua mimi ndiye Bwana Sesame mwenyewe!” atasema, halafu wote wataangua kicheko.
Ilika wakati kampuni kadha zilipoamua kuwapunguza wafanyikazi wake kutokana na hali
mbaya ya kiuchumi. Lakini Bwana Sesame hakuwa mmoja wa hao. Hali yake ilibakia vile vile.
Aliendelea kuvalia kinadhifu na kuishi maisha yake ya fawaishi. Wakati wenzake wanalalamikia
hali ngumu ya maisha, Bwana Sesame hakuwa na lolote la kumsumbua. Aliendelea kukaa bila
ya kazi wala bazi. Lakini watu walitambua kuwa alikuwa na mazoea ya kutoka chumbani majira
ya jioni. Hakuna aliyejua alirejea lini.
Siku moja Bwana Sesame alitoka jioni kama kawaida na kuelekea kwenye shughuli zake za
kawaida. Siku hiyo jamaa mmoja wa mtaani alikumbana naye kwenye lango kuu. “Bwana Sesame,
leo wapi yahe?” alimwuliza. Bwana Sesame alimwangalia na kusema, Natoka nje kidogo yahe.
Jiji hili lataka ustaarabu, alijibu. Yule jamaa alimwangalia na kumwambia, Nina shida kidogo,
sijui kama utanifaa mwenzangu. Wajua tena hali zenyewe siku hizi, alisema. “Nini tena?” aliuliza
Bwana Sesame. Nina gari langu ambalo halina redio. Natafuta moja ya bei nafuu... kitu kama
Sony hivi, alisema. Bwana Sesame alimwangalia na kusema, Hiyo kazi nyepesi kwangu yahe,
papai kwa kijiko!” alisema Bwana Sesame akicheka. Jamaa yule alishukuru na wakaagana.
Bwana Sesame alishika njia kuelekea sehemu zake za kawaida majira kama haya. Naye yule
jamaa akapinda kama anaingia mtaani, lakini baada ya muda akageuka na kuamua kumfuata
Bwana Sesame.
Bwana Sesame alishika tariki mpaka sehemu yake ya mazoea. Yule jamaa alimfuata kwa
mbali na kwa mwendo wa paka. Alimwona Bwana Sesame akiingia mahali palipokuwa na banda
kuukuu. Muda si muda alitoka na jamaa wengine wakiwa wamevalia maguo ya ajabu ajabu. Yule
jamaa aliwafuata hadi mahali palipokuwa na ujia mwembamba ulioachana na barabara kuu.
Sura ya Kumi na Nne
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 145 12/11/2019 09:44
146
Alijicha mahali, na kutokana na hali ya sehemu ile akawa haonekani.
Muda si muda palitokeza gari dogo lililokuwa likiendeshwa na mwanamke mmoja. Bwana
Sesame na wenzake walitokeza na kutupa gogo lililomzuia yule mwanamke. Ghaa bin vuu
walimvamia; wakaifungua milango ya gari mbio na kujivurumisha ndani. Gari lilitimuliwa kama
risasi kuelekea upande wa pili. Wakati huo yule jamaa ashaliangalia gari lenyewe na kuzihifadhi
nambari zake. Alishika njia kurudi zake chumbani.
Siku iliyofuata huyo jamaa hakuwa kazini. Alipokuwa akifungua kinywa alisikia sauti ya
kugongwa kwa mlango. Aliinuka na kwenda kuufungua. Bwana Sesame aliingia ndani. Vipi yahe?
Hujenda kazini leo? Au umelala sana bwana?” alisema Bwana Sesame kwa uchangamfu wake.
Muda si muda alimwonyesha redio ya gari aliyokuwa nayo. “Umeipata mara moja hii kumbe?”
aliuliza yule jamaa. Si nilikwambia yahe! Mimi ndiye Bwana Sesame mwenyewe. Hii kwangu
si kazi. Ninafahamiana na jamaa wengi wanaoifanya kazi hii, alisema Bwana Sesame. Naona
kweli. Ehh bwana we! Ndipo Waswahili wakasema, ukitaka kuvua vua na wavuvi! alisema yule
jamaa. Ni kweli kabisa!” alijibu Bwana Sesame huku akicheka kwa furaha.
Yule jamaa alisimama kuelekea chumbani. Bwana Sesame alitulia akisubiri kupokea ujira
wake. Muda mfupi ulipita, kisha mlango wa nyumba ukagongwa. “Yahe Bwana, kunagongwa
huku!” Bwana Sesame akasema. Yule jamaa alitoka chumbani na kuelekea mlangoni. Mlango
ulipofunguliwa waliingia askari polisi wawili. Bwana Sesame hakuwa na upenyu wa kutokea.
Alitiwa mikononi. Hakujua kumbe yule jamaa alikuwa kachero. Hapakuwa na ujanja tena. Siku
hiyo pwagu alipata pwaguzi. Fungua Sesame haikufaa tena.
Maelezo ya msamiati
kibonge cha kazi : kazi nzuri.
runinga : televisheni.
vunga : danganya; fanyia ujanja.
fawaishi : raha; maisha ya fawaishi ni maisha ya raha.
upenyu : nafasi ndogo.
Maswali
1. Kwa nini Nimrod alibatizwa Bwana Sesame’?
2. Kwa nini watu walioishi mtaani Urumo walishangazwa na utaratibu wa kazi wa Bwana
Sesame?
3. Unakiri ni kwa nini Bwana Sesame alifahamu sana juu ya magari?
4. Je, unakiri yule jamaa aliyeagiza aletewe redio alikuwa na haja sana na kifaa hicho kama
alivyosema?
5. Bwana Sesame alikuwa kachero. Unakubali? Toa maelezo?
6. Yule jamaa alipoingia chumbani na kumwacha Bwana Sesame sebuleni unakiri alikwenda
kufanya nini?
7. Je, hadithi hii ina mafunzo gani kwako?
8. Eleza maana ya misemo ifuatayo kisha uitumie katika sentensi.
(a) piga mluzi
(b) piga soga
(ch) shika tariki
(d) tia mkononi
(e) angua kicheko
(f) shika njia
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 146 12/11/2019 09:44
147
9. Toa maana ya methali zifuatazo kisha uzitumie katika sentensi ili kuonyesha maana zake:
(a) Ukitaka kuvua vua na wavuvi.
(b) Pwagu hupata pwaguzi.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi simulizi: Vitendawili na Mafumbo
I. Vitendawili
Hiki ni kipera cha utanzu wa semi.Vitendawili ni semi ambazo huwa zimefumbwa na hutolewa
kwa mtu ili azifumbue, kwa muundo wa swali. Vitendawili hupatikana katika jamii nyingi na
ni maarufu miongoni mwa watoto.
Umuhimu wa vitendawili
Vitendawili hutumiwa kwa sababu kadhaa:
(i) Kuupanua ujuzi wa watoto wa mazingira yao.
(ii) Kuelimisha: hutumiwa kuwaelimisha watoto kuhusu mazingira yao.
(iii) Kuukuza uwezo wa watoto wa kukiri. Mtoto hulazimika kukiri na kuhusisha mambo
yaliyoko kwenye mazingira yake ili aweze kukifumbua kitendawili fulani.
(iv) Kuchangamsha na kufurahisha wanaotegeana.
Vitendawili ni sehemu ya mafumbo yanayopatikana katika jamii. Mafumbo haya ni sehemu ya
utanzu unaojulikana kama semi. Kitendawili huweza kuwa sentensi fupi au maelezo marefu.
Sifa za vitendawili
(i) Hutanguliwa na maneno fulani. Anayekitega kitendawili husema: Kitendawili! na kujibiwa
na anaowategea: tega!
(ii) Vitendawili huwa na ujumbe wa kimafumbo. Maana yake huwa imechwa na huhitaji
akili kuifumbua.
(iii) Vitendawili huwa na ufupi wa kimaelezo.
(iv) Kitendawili hujengwa kwa kutegemea ulinganishi au sitiari, ambapo kitu fulani kinapewa
sifa ya kingine.
(v) Kuna vitendawili vinavyoundwa kwa neno moja, kwa mfano: Hauonekani (upepo) n.k.
(vi) Vitendawili huweza kuwa na urudiaji wa maneno: Mama kazaa mtoto na mtoto kazaa
mtoto na mtoto kazaa mtoto. (kuku na yai)
Mafumbo/Chemshabongo
Hiki vile vile ni kipera cha utanzu wa semi. Mafumbo ni semi ambazo huwa zimecha
jambo fulani ambalo msikilizaji wake anapaswa kulifumbua. Kwa kawaida mafumbo hubuniwa
na msemaji kwa ajili ya hadhira maalum. Sio semi za kimapokeo au zinazopokezanwa kutoka
kizazi kimoja hadi kingine kama methali na vitendawili. Nia ya mafumbo ni kuujaribu uwezo
wa msikilizaji wa kuweza kufumbua jambo fulani. Sifa hii inayafanya mafumbo kufanana na
vitendawili.
Kwa msingi huu, mafumbo huweza kuwa ya aina mbili kuu:
1. Vitendawili ambavyo husema jambo ambalo msikilizaji anaelewa jibu lake ikiwaanatoka
kwenye utamaduni wake.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 147 12/11/2019 09:44
148
2. Maelezo marefu yanayofumba kitu au jambo bila ya kuwa na muundo wa
kitendawili.
Mifano ya mafumbo
1. Palikuwa na ndege kumi mtini, nami nikampiga mmoja jiwe kwa manati, je ni ndege
wangapi waliobaki mtini? - Hakuna ndege aliyebaki kwa sababu wale wengine walirufai
au kuruka na kuondoka.
2. Baharia mia moja waliharibikiwa na chombo chao baharini na ikabidi waruke majini kabla
hakijazama. Basi wote walijitumbukiza majini. Walilowa kila mahali isipokuwa nywele.
Kwa nini? Kwa sababu walikuwa na vipara.
3. Fahali watatu wanaweza kutoa maziwa painti sitini. Je, fahali mmoja atatoa maziwa painti
ngapi?- Fahali hatoi maziwa.
4. Jumapili moja Juma alisonga sima kwa kitoweo cha nyama. Punde tu, kabla ya kula akasikia
mwizi na kutoka nje kuchungulia. Aliporudi alipata nyama yote imeliwa na mbwa. Je,
alikula ugali kwa nini? Mdomo.
Zoezi
(i) Toa mifano minne ya mafumbo unayoyafahamu.
(ii) Toa mifano mitano ya vitendawili kutoka jamii yako kujadiliana na wenzako darasani.
(iii) Tegua vitendawili vifuatavyo:
(a) Samaki wangu anaelea kimgongomgongo.
(b) Kuku mweupe hufanya harusi.
(ch) Kamba yangu ndefu lakini haiwezi kufunga kuni.
(d) Nyumba yangu ina mlango mdogo.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Ngeli za nomino
Upatanisho wa kisaru: Viambishi awali vya vitenzi
Ngeli ya i
/-zi
umoja wingi
Nyumba imejengwa. Nyumba zimejengwa.
Ndoo imejaa. Ndoo zimejaa.
Shule itafungwa. Shule zitafungwa.
Kamati itaundwa. Kamati zitaundwa.
Baiskeli imepotea. Baiskeli zimepotea.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 148 12/11/2019 09:44
149
Ngeli ya i
umoja wingi
Mvua imekwisha. Mvua imekwisha.
Chumvi iko wapi? Chumvi iko wapi?
Sukari imemwagika. Sukari imemwagika.
Subira ilisaidia. Subira ilisaidia.
Ngeli ya u-zi
umoja wingi
Uzi umekatika. Nyuzi zimekatika
Ubao umevunjika. Mbao zimevunjika
Uto uko hapa. Fito ziko hapa.
Ukoo ulimsaidia. Koo zilimsaidia.
Waraka umetumwa. Nyaraka zimetumwa.
Ngeli ya u-u
umoja wingi
Uchoyo unaudhi. Uchoyo unaudhi.
Ukora ulikwisha. Ukora ulikwisha.
Ulaji unadhuru. Ulaji unadhuru.
Ulanguzi umeanza. Ulanguzi umeanza.
Ukweli unafaa. Ukweli unafaa.
Ngeli ya ku
umoja wingi
Kusoma kunafaa. Kusoma kunafaa.
Kucheka kunaliwaza. Kucheka kunaliwaza.
Kuandika kulikwisha. Kuandika kulikwisha.
Kufagia kulisaidia. Kufagia kulisaidia.
Kucheza kulimpoteza. Kucheza kulimpoteza.
Ngeli ya pa-ku-wmu
umoja wingi
Mahali panafaa. Mahali panafaa.
Mahali kunafaa. Mahali kunafaa.
Mahali mnafaa. Mahali mnafaa.
Tanbihi: Matumizi ya ngeli ya pa/ku/mu hutegemea, wakati fulani, muktadha wa mazugumzo.
Wakati fulani, mtu anayeishi Kenya anaweza kusema, Hapa Marekani, badala ya Kule Marekani.
Kusema hivyo ni kwa muktadha kwamba Marekani ni karibu.
Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kujaza pengo kwa viambishi vifaavyo kisha uonyeshe vinawakilisha
ngeli gani.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 149 12/11/2019 09:44
150
Umoja Wingi Ngeli
K.m Dakika imepita.
Meza__metengenezwa.
Mahali pamefagiliwa.
Chai __mepikwa.
Kuongoza __naleta shida.
Uso __na harara.
Ukuta __mebomoka.
Utoto __liudhi.
Udongo __lisombwa.
Mahali __lifungwa.
Kusoma __nasaidia.
Ndege__meka.
Utepe __takatwa.
Wimbo __liimbwa.
Mahali kulifunguliwa.
Wavu __takatika.
Nchi __meendelea.
Kuiba __nadhuru.
Nyundo __ko wapi?
Utambi __likwisha.
Mahali__litosha.
Dakika zimepita.
Meza metengenezwa.
Mahali __mefagiliwa.
Chai __mepikwa.
Kuongoza __naleta shida.
Nyuso __na harara.
Kuta __mebomoka.
Utoto __liudhi.
Udongo __lisombwa.
Mahali __lifungwa.
Kusoma __nasaidia.
Ndege __meka.
Tepe__takatwa.
Nyimbo __liimbwa.
Mahali __lifunguliwa.
Nyavu __takatika.
Nchi __meendelea.
Kuiba __nadhuru.
Nyundo ___ko wapi?
Tambi __likwisha.
Mahali __litosha.
i-zi
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
_____
Kuakisha
Alama ya mabano/vifungo/parandesi ( )
Alama hizi hutumika katika mazingira mbalimbali ya maandishi kama yafuatayo:
(a) Kuonyesha maneno ambayo si ya lazima katika usemi; kwa mfano:
(i) Tukishinda mchezo huu (ingawa sina matumaini) tutapewa zawadi nono.
(ii) Mgonjwa akipata nafuu (nina matumaini makubwa) wazazi wake watafurahi sana.
(iii) Tukitia bidii masomoni (jambo ambalo ni la lazima) tutaishi maisha yenye furaha
na mafanikio.
(iv) Peter Tino (ni mchezaji hatari kweli kweli) anatarajiwa kuwasili leo alasiri.
(b) Kuonyesha jambo la ziada; kwa mfano:
(i) Vita vya Kwanza vya Dunia (1914 1918) viliangamiza watu wengi.
(ii) Shule ya Malani (ina wanafunzi elfu moja) ni kati ya shule kubwa zaidi hapa wilayani.
(iii) Wanafunzi wote watiifu (kina Peter, Makokha na wengine) watatunukiwa zawadi
na mkuu wa wilaya.
(iv) Mji wa Johannesburg (una wakora wengi kweli) ni mmoja kati ya miji mikubwa
barani Afrika.
(ch) Kuzingira nambari, hasa katika orodha. Kwa mfano:
(i) (ii) (iii)
(1) (2) (3)
(d) Katika maandishi ya kitamthilia kutoa maelekezo kwa waigizaji na wasomaji;
kwa mfano:
Mama: (anaita) Belinda, hebu niletee hiyo sufuria huko jikoni. Umenisikia?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 150 12/11/2019 09:44
151
Belinda: (hajasikia) Eti wasemaje mama?
Mama: (amekasirika. Anajisemea mwenyewe) Watoto wa siku hizi sijui wana nini.
(anapaaza sauti) Naam, huwezi kusikia. Utasikiaje na huku redio waweka sauti
ya juu sijui mpaka wapi…
Zoezi
Weka mabano katika sehemu zifaazo kwenye sentensi zifuatazo.
(i) Wanjiku ni mwanawe Macharia atajiunga na Chuo Kikuu cha Egerton.
(ii) Bwana Kanamai ni meneja shupavu kwelikweli ameteuliwa kusimamia kampuni mpya ya
mafuta.
(iii) Vifaa vya jikoni sufuria, vikombe, vijiko na vingine vinahitajika kesho kwenye arusi ya
Ali.
(iv) Nikifanikiwa kusari ngambo nina hakika nitasari nitakuletea vitu unavyohitaji.
D. Kusoma
Kusoma kwa mapana: Makala na vitabu vya ziada
Sio wakati wote ambapo mwanafunzi hutegemea vitabu vya darasani; wakati mwingine
mwanafunzi hulazimika kusoma vitabu vingine zaidi ya vile vya kiada anavyovitumia darasani.
Hivi hujulikana kama vitabu vya ziada, yaani vya nyongeza. Hivi vinaweza kuwa vya hadithi
au vya kitaalamu na aghalabu huvisoma kwa sababu maalum. Usomaji huu unaweza kuhusisha
kusoma makala au maandishi yanayopatikana katika majarida kuhusu masuala fulani. Usomaji
huu ni muhimu kwa sababu kadha:
Kuupanua ufahamu wako kuhusu masuala kadha.
Kuuendeleza ujuzi wako hasa pale ambapo hukuelewa vyema jambo fulani.
Kujifahamisha mambo muhimu kuhusiana na taaluma mbalimbali.
Hatua za usomaji wa aina hii
Hakikisha kuwa una daari ya kuandikia.
Kila unaposoma jambo geni andika vidokezi katika daari lako.
Andika maelezo ya dhana au maneno mapya unayokumbana nayo.
Chunguza maana za maneno mapya katika kamusi yako au kamusi zinazopatikana
maktabani.
Panga hoja/mawazo kwa njia inayoeleweka usomapo baadaye.
E. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Tahadhari
Tahadhari au hadhari ni uangalifu. Kuna maandishi ambayo hutungwa ili kuwatahadharisha
watu au kuwafanya wawe waangalifu. Haya huweza kuwatahadharisha dhidi ya kufanya jambo
fulani, kuvuka barabara, kupita sehemu fulani, kucheza na vitu fulani n.k.
Sifa za tahadhari
Huandikwa kwa heru kubwa na nzito.
Huweza kuambatanishwa na michoro au ishara.
Huweza kutumia rangi fulani aghalabu nyekundu kupitisha ujumbe huo.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 151 12/11/2019 09:44
152
Huwa na maneno machache.
Huwekwa mahali inaposomeka waziwazi.
Huwa ni maneno rahisi, yanayoeleweka haraka.
Mara nyingi huambatanishwa na alama ya mshangao au kihisishi (!).
Baadhi huwa ni ishara fulani tu bila maandishi.
Mifano ya tahadhari:
SAKAFU
INATELEZA
Tahadhari hii huwekwa kwenye
majengo, magari, maeneo yenye hospitali au
viwanda n.k.
ambako uvutaji sigara hauruhusiwi.
Tahadhari hii yaweza kupatikana
kwenye eneo ambako ulishaji
mifugo hauruhusiwi.
USIVUTE SIGARA!
NI HATIA KULISHA
MIFUGO KATIKA
ENEO HILI
TAHADHARI!
Weka Mbali Na
Watoto
Tahadhari hii hupatikana kwenye chupa
za dawa, kemikali fulani, vyombo fulani
n.k. ambavyo vyaweza kuwadhuru watoto
kutokana na kutoelewa kwao.
Zoezi
Tunga mifano miwili ya tahadhari.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 152 12/11/2019 09:44
153
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2 3
4
5
6
7
8 9
10
11 12 13 14
15
16 17
18 19
CHINI
1. Mstari katika shairi au wimbo
6. Ni chombo cha kusarishia abiria
7. Moja kati ya vipera vya semi
9. Pululu au nyika
5. Hutumika kama dawa ya kienyeji, huwa kali
2. Kisa cha nchi ya Uyunani cha zamani
4. Ndoto isiyo nzuri (ya kutisha)
3. Mtu aliyelaaniwa/aliyesemewa maneno mabaya yakamfuata
13. K i n g ’o n g ’o
14. Sononeko/huzuni
KULIA
8. Mtu ambaye huwaelekeza au kusimamia wengine
5. Vitu vinavyotuzunguka
10. Kusema yatakayotokea usoni
12. Wasiwasi
15. Mja
17. Kisichotakikana mahali fulani
19. Huchapishwa kila siku kutupasha habari
16. Wanaosoma
18. Namna ya kufanyia
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 153 12/11/2019 09:44
154
Sura ya Kumi na Tano
A. Ufahamu
Ulimwengu wa kompyuta
Kompyuta au tarakilishi ni mojawapo wa vyombo muhimu katika maisha ya binadamu katika
karne hii ambapo maendeleo ya sayansi yamekia ngazi za juu sana. Utabiri sahihi wa hali
ya hewa, usari wa ndege na teknolojia ya kutegemewa ya kimatibabu ni baadhi ya mambo
yanayotegemea kuwako kwa chombo hiki. Ikiwa kitakosekana, shughuli hizi zitashindikana au
kulegalega kwa kiasi kikubwa.
Kompyuta ni chombo cha kipekee. Licha ya kuwa haina uwezo wa kukiri yenyewe kama
binadamu, inafanya kazi kama aina ya akili inayotegemea nguvu za umeme. Chombo hiki kina
uwezo mkubwa wa kutekeleza majukumu mengi pamoja na kuchunguza, kufasiri na kuchambua
ujumbe wa aina mbalimbali kwa usahihi wa kushangaza.
Uendeshaji wa ndege siku hizi unategemea kompyuta. Aidha, kompyuta kuu zinazopatikana
katika kituo kikuu cha kuzielekeza ndege kwenye viwanja vya ndege, zina uwezo wa kuchunguza
mamia kwa mamia ya ndege, kufuatilia safari zao na kuzielekeza zinakotakiwa kwenda ili
kuepusha uwezekano wa ajali. Usalama wa abiria unakitegemea chombo hiki.
Lakini je, kompyuta huwezaje kuifanya miujiza hii yote? Kompyuta inajumlisha mamia ya
saketi za umeme. Ili iweze kufanya kazi vizuri, inahitaji kupewa maagizo fulani. Maagizo hayo
hujulikana kama programu na huielekeza kompyuta jinsi ya kuifanya kazi. Kila programu hiyo
inapofanya kazi, kompyuta inaweza kuyatekeleza majukumu yake. Inafanya hivi kwa kuchunguza,
kupitia na kutathmini maarifa au maelezo fulani kwa utaratibu ambao unajulikana kama
uchakataji.
Uchakataji wa kompyuta unafanywa na sehemu inayojulikana kama KIU, yaani Kitengo Kikuu
cha Uchakataji. Hii ndiyo sehemu yenye mfumo mzima wa kuiendesha kompyuta yenyewe.
Sehemu hii huwa na sehemu zinazotumiwa kuwekea programu kwenye kompyuta. Programu za
kompyuta huweza kufanya kazi kutokana na nguzo iliyopo katika kompyuta hiyo. Nguzo hiyo
hujulikana kama maunzi. Ikiwa kompyuta haina maunzi inayohitajika, programu inayohusika
haiwezi kufanya kazi.
KIU huwa na sehemu inayoweza kuhifadhi maarifa fulani. Kwa mfano, mtu anapochapa
maandishi fulani kwa kuitumia kompyuta, anaweza kuyahifadhi katika kompyuta hiyo. Sehemu
anayohifadhi maandishi hayo hujulikana kama diski ngumu au dhiba. Wakati mwingine
inawezekana kuhifadhi taarifa kwenye vyombo mbalimbali. Teknolojia hubadilika kila uchao na
mabadiliko hayo huziathiri njia za kuhifadhia taarifa au data. Taarifa huweza kuhifadhiwa kwenye
chombo kidogo kinachounganishwa na KIU au diski mweko, huwezekana pia kuhifadhiwa kwenye
chombo kinachofanana na santuri, yaani sidii au dividii. Siku za karibu kuna njia za kuhifadhi
data ambazo humwezesha aliyezihifadhi kuzifanyia kazi bila ya kuwa na tarakilishi yake alipo
mradi ana huduma za intaneti
Kazi yoyote ya kompyuta haiwezi kufanyika bila ya kuwako na chombo cha kuchapia. Hiki ni
chombo ambacho kina heru na tarakimu mbalimbali. Chombo hiki hujulikana kama bodi ya
dota. Bodi ya dota hufanana sana na mashine ya kupigia chapa.Chombo hiki kimeunganishwa na
KIU na husaidiana na kifaa kingine kinachobonyezwa na kutoa sauti ya kualika. Hiki kinajulikana
kama kipanya. Maandishi au shughuli zinazoendelea kwenye kompyuta hujitokeza kwenye kioo
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 154 12/11/2019 09:44
155
kinachoshabihiana na kile cha runinga. Hiki hujulikana kama kiwambo au mulishi. Kila kipanya
kinaposogezwa, kuna kishale kinachosogea kwenye mulishi na ambacho humwelekeza mtumiaji
wa kompyuta. Hii huwa njia nyepesi ya kuipa kompyuta maagizo fulani.
Hakuna kompyuta inayoweza kufanya kazi bila ya kuwepo kwa sehemu zote hizo. Kompyuta
inatuwezesha kufanya mambo mengi sana. Ni moja kati ya vyombo muhimu kuwahi kuvumbuliwa
katika historia ya binadamu. Kuwepo kwake kumesaidia siyo tu katika utati na uchunguzi
hata kuhusiana na magonjwa bali pia katika mawasiliano kati ya watu walioko kwenye pembe
mbalimbali za ulimwengu. Na siku hizi, kila yeyote aliye na nia ya kupiga hatua kimaendeleo
katika maisha yake, hana budi kukaa chonjo na kompyuta. La sivyo atajikuta yu pweke katika
ulimwengu mpya wa tarakilishi.
Maelezo ya msamiati
zitashindikana : hazitafaulu; hazitawezekana.
kulegalega : kutokuwa thabiti au imara.
programu : maagizo yanayoelekeza kompyuta jinsi ya kufanya kazi fulani.
uchakataji : utaratibu wa kompyuta wa kuchunguza na kutathmini
maelezo fulani ili kuweza kutekeleza majukumu yake.
maunzi : nguzo ya kompyuta inayowezesha programu kufanya kazi.
dhiba : sehemu ya kompyuta inayohifadhi maandishi
yanayoandikwa kwenye kompyuta. Diski ngumu pia
huweza kufanya kazi hiyo.
kipanya : kifaa kinachobonyezwa ili kuwezesha mtu kutumia
kompyuta.
kiwambo (mulishi) : kifaa cha kompyuta kinachofanana na runinga
kinachowezesha mtumiaji kuona kazi anayofanya kwenye
kompyuta.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 155 12/11/2019 09:44
156
Maswali
1. Kulingana na kifungu hiki, ni mambo gani yanayoweza kutekelezwa na kompyuta?
2. Kwa nini kompyuta inalinganishwa na akili ya binadamu?
3. Ni nini kazi ya programu katika kompyuta?
4. Ni sehemu gani kuu kati ya sehemu zote zilizotajwa?
5. Ni nini kazi ya ‘bodi ya dota’?
6. Taja kazi nyingine tatu unazojua zinazotekelezwa na kompyuta.
7. Tumia maneno haya kutungia sentensi ili kuonyesha maana zake:
(a) programu
(b) kipanya
(ch) mulishi
(d) KIU
(e) dhiba
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii: Sajili ya shuleni II
Sifa za sajili ya shuleni zimeangaziwa katika katika sura ya 13. Hapa pana aina nyingine ya sajili
hiyo kwa njia ya mahojiano. Mahojiano hushirikisha sifa za ziada. Sifa hizo ni:
(a) Muundo bayana au wazi wa maswali na majibu: Lengo kuu ni kupata taarifa fulani na
maswali yanayoulizwa huwa yanadhamiria kupata taarifa hizo.
(b) Huweza kutokea mahali popote pale shuleni k.v. osini, uwanjani, darasani
(ch) Mpangilio wa maswali na majibu yake hubainisha mwelekeo fulani. Maswali huweza
kuambatana na kauli za tathmini au hata za kumtaka anayeulizwa au kuhojiwa kufafanua
hoja fulani
(d) Maswali yenyewe huwa mafupi sawa na majibu yake isipokuwa tu pale ambapo pana haja
ya ufafanuzi zaidi.
Soma kifungu kisha ujibu maswali
(Mwalimu anaingia darasani na kuwasalimu wanafunzi)
 : H 
 : H .
 : (A    ) K   
 : N, 
 : (A) U 
 : () K 
 : U    
 : N 
 : U    
 : N   U.
 : H  
 : H    
 : K     
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 156 12/11/2019 09:44
157
 : M      . I
  .
 : H . N       .
 : N
 : E,  B    K   
    ( ) W
    ,  .
(  )
Maswali
1. Je, ni sifa zipi za sajili ya shuleni zinazojitokeza kwenye kifungu hiki?
2. Je, mahojiano baina ya mwalimu na mwanafunzi huongozwa na kaida zipi?
CH. Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -angu’, -ako’, -ake
Kumiliki ni ‘kuwa na Vivumishi vimilikishi ni vivumishi ambavyo huonyesha kuwa vitu au hali
zinazomilikiwa na nomino. Mizizi ya vivumishi hivi huwa sita kutegemea nafsi ya mlengwa
(umoja na wingi). Mizizi hiyo ni: -angu, -ako, ake (umoja) na -etu, -enu, -ao (wingi)
Tazama jedwali hili:
ngeli nomino vimilikishi matumizi
-angu -ako -ake
a
wa
mtoto
watoto
wangu
wangu
wako
wako
wake
wake
Watoto wako wameka.
Watoto wako wameka.
u
i
mshipi
mishipi
wangu
yangu
wako
yako
wake
yake
Mshipi wake umepotea.
Mishipi yake imepotea.
u
ya
ugonjwa
magonjwa
wangu
yangu
wako
yako
wake
yake
Ugonjwa wangu utakwisha.
Magonjwa yangu yatakwisha.
ya
ya
maji
maji
yangu
yangu
yako
yako
yake
yake
Maji yangu yako wapi?
Maji yangu yako wapi?
li
ya
limau
malimau
langu
yangu
lako
yako
lake
yake
Limau lako limeoza.
Malimau yako yameoza.
ki
vi
chama
vyama
changu
vyangu
chako
vyako
chake
vyake
Chama chake kimenawiri.
Vyama vyake vimenawiri.
zi fedha zangu zako zake Fedha zake zimepotea.
li jua langu lako lake Jua lake limechomoza.
vi vita vyangu vyako vyake Vita vya Iraq vimezidi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 157 12/11/2019 09:44
158
Zoezi
1. Tumia vimilikishi mwafaka katika sentensi zifuatazo kulingana na mzizi wa kimilikishi
ulichopewa kwenye mabano.
(a) Mwalimu ____ amekuja. (-ako)
Walimu ____ wamekuja. (-ake)
(b) Tunda ____ limeoza. (-angu)
Matunda ____ yameoza. (-ako)
(ch) Kisu ____ kimenikata. (-angu)
Visu ____vimenikata. (-ako)
(d) Manukato ____ yananukia. (-angu)
Manukato ____ yananukia. (-ake)
(e) Ulezi ____ unafaa sana. (-ake)
Malezi ____ yanafaa sana. (-ako)
(f) Mtambo ____umeharibika. (-ake)
Mitambo ____ imeharibika. (-angu)
(g) Punda _____ amekufa. (-ako)
Punda _____wamekufa. (-angu)
(h) Yai ________ liko wapi? (-ako)
Mayai ________ wapi? (-ake)
(i) Upana _____ulitosha. (-ake)
Mapana ______ yalitosha. (-angu)
(j) Kiatu ___________ kimeraruka. (-ake)
Viatu ___________ vimeraruka. (-ako)
2. Andika sentensi zifuatazo kwa wingi:
Kwa mfano: Kitabu chake kimepotea. - Vitabu vyao vimepotea.
(a) Mwalimu wake ameondoka.
(b) Kondoo wangu amekufa.
(ch) Chakula chake kiko wapi?
(d) Ugonjwa wangu umekwisha.
(e) Maziwa yako yako hapa.
(f) Cheti chako kitachomeka.
(g) Punda wako atabeba mzigo mzito.
(h) Pera lako liko wapi?
(i) Mpira wangu umeibiwa.
(j) Maji yake yatamwagika.
Kuakisha
Kistari kifupi (-)
Kistari kifupi hutumika katika mazingira mbalimbali kama ifuatavyo:
(a) Kutenganisha silabi ili kuonyesha kuwa neno linaendelea katika mstari wa pili wa
karatasi; kwa mfano:
(i) Jana nilimwona mwalimu wetu huko so-
koni.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 158 12/11/2019 09:44
159
(ii) Juma hili watu watano wameambukizwa kipindu-
pindu.
(iii) Waziri anawahutubia watu huko katika uwanja wa kima-
taifa.
Kumbuka, neno hukatwa mwishoni mwa silabi.
(b) Kutenganisha silabi za neno; kwa mfano:
ni - na - so- ma
a - ta - kwe - nda
u - li - ki - mbi- a
m - me - fa - u - lu
(ch) Kudokeza jambo muhimu kuhusu neno, kama vile mzizi; kwa mfano:
-eusi
-toto
-eupe
-ingine
(d) Kutenganisha maneno yanayoandikwa kwa kuambatana; kwa mfano:
(i) isimu-jamii
(ii) elimu-viumbe
(iii) mwana-harakati
(e) Kudumisha sauti wakati neno linapotamkwa kwa kuvutwa; kwa mfano:
(i) Lo! Masala-a-a-a-le!
(ii) Hoye-e-e-e!
(iii) Niliteleza mara moja chwa-a-a-a!
(f) Katika tarakimu kuonyesha mwanzo hadi mwisho; kwa mfano:
mwaka 1914-1918
1939-1945
1922-1996
(g) Kuonyesha maneno yanayoandikwa kwa vitengo; kwa mfano:
(i) Nitakapojenga nyumba yangu nitaipaka rangi aina ya damu-ya-mzee.
(ii) Shangazi amepanda mpunga aina ya tule-na-bwana.
(iii) Babu hupenda sana ndizi aina ya mkono-wa-tembo.
Kistari kirefu (___ )
Hutumika katika mazingira yafuatayo ya maandishi:
1. Kutoa maelezo ya ziada; kwa mfano:
(a) Nchi zote za Afrika mashariki Kenya, Uganda na Tanzania zinawavutia watalii
wengi kila mwaka.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 159 12/11/2019 09:44
160
(b) Wachezaji wa timu ya mchezo wa kandanda ya Ushelisheli wale waliowasili jana
kutoka Ufaransa walilakiwa kwa shangwe na wapenzi wa soka nchini.
(ch) Watu wanaojigamba kuwa wanajua mengi kuanzia alfa hadi omega mara nyingi
hujikuta wameshindwa na mambo madogo madogo tu.
2. Kuonyesha mabadiliko ya ghaa; kwa mfano:
(a) Siwataki hapa watu wasiojua wanafanya nini samahani sikunuia kuwatusi.
(b) Otieno ameleta kuku, batamaji, batabukini sijui kwa nini akafanya hivyo pamoja
na batamzinga.
3. Kuonyesha ni nani aliyesema maneno fulani; kwa mfano:
(a) Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu Peter Anyanzwa.
(b) Tuijenge nchi yetu kufuatana na mwito wa umoja, amani na upendo Mbunge wa
Kilome.
Zoezi
1. Tunga sentensi tano kuonyesha matumizi mbalimbali ya kistari kifupi
2. Tumia sentensi kuonyesha matumizi mwafaka ya kistari kirefu katika uakishaji
D. Kuandika
Utungaji wa kisanii: Vitendawili na mafumbo/chemshabongo
Vitendawili hutofautiana na methali kwa kuwa hivi hukua sana. Katika jamii zetu kuna
vitendawili ambavyo tunavijua kutokana na mapokeo ya jamii zetu; yaani kutokana na kutegewa
vitendawili hivyo tulipokuwa watoto. Vitendawili hutokana na mazingira ya jamii fulani. Mambo
yanayoizunguka jamii hiyo au yanayotokea katika jamii hiyo ni msingi wa kutungwa kwa
vitendawili hivyo. Haya ndiyo mazingira yake.
Mazingira hayo yanaweza kuwa ya kihistoria, kijiograa, kiuchumi, kisayansi na kisiasa.
Vitendawili vitakavyotungwa kuhusiana na mazingira ya kisayansi vitajaribu kuuliza swali
linalohusiana na mambo au matukio ya kisayansi yaliyopo katika jamii. Haya ni yale yanayoweza
kutambuliwa na wanajamii wote. Mafumbo nayo, ambayo ni semi zinazofumba swali fulani,
hutungwa namna hiyo.
Mifano ya vitendawili
Ifuatayo ni mifano ya vitendawili vilivyotungwa kutokana na mazingira mapya ya kisayansi:
1. Nakupikia kila siku lakini hunioni, unachokiona ni miale yangu tu. - Gesi.
2. Kila nituapo na nirukapo hulia kwa sauti ya ajabu sana. - Ndege.
3. Nijazapo tumbo langu huelea lakini sizami. - Meli.
4. Ninalia huku nikiunganisha nguo. - Cherehani.
5. Ng’ombe wangu akinywa maji halafu atembee, utajua tu pahali alipopita. - Kalamu.
6. Nikiongea unajua kila kitu. - Redio.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 160 12/11/2019 09:44
161
Mafumbo
1. Kuna mchungwa wenye machungwa mengi. Nina hamu ya kuyala lakini kuna tumbili
aliyeko huko juu, na mimi ninamwogopa tumbili sana. Nifanyeje ili niweze kuyapata
machungwa hayo? -Mtupie tumbili jiwe ili naye akurushie chungwa.
2. Mama mmoja alienda sokoni na mwavuli wenye tundu kubwa sana. Lakini alipokuwa
akitoka sokoni hakunyeshewa. Kwa nini?- Kwa sababu hapakuwa na mvua yoyote.
3. Kulikuwa na ajali kwenye barabara kuu itokayo mjini. Palikuwa na watu wanne waliokufa
na kuzikwa hapo na manusura wanne. Je, manusura walizikwa wapi?- Manusura hawazikwi.
Zoezi
1. Tunga vitendawili viwili kuhusiana na mazingira ya shule.
2. Toa mfano wa fumbo linalohusiana na maendeleo ya kisayansi au ya kijamii.
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1
2
3
4 5
6
7 8
9 10 11 12
13 14
15
16 17
18 19
20
CHINI
3. Hadithi ambayo si ndefu
1. Baa
7. Maneno yanayoeleza uhusiano wa kitu na kingine au mtu na kitu
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 161 12/11/2019 09:44
162
2. Mwizi mkubwa
4. Shamba kutayarishwa kwa ajili ya upanzi
10. Pahali pa kupitia watu au magari
13. Mambo ya kitambo
14. Watu wanaoendesha magari
KULIA
6. Husukuma damu mwilini
5. Tabia au hulka zinazokubalika katika jamii
8. Utanzu wa fasihi simulizi
9. Tangulia
11. Upelelezi
15. Bila kukawia au kusita
16. Hadithi za wanyama kama wahusika
17. Mnyama mjanja sana
18. Bila kuwa na mwisho
19. Kuteua au kuchukua kwa misingi ya kabila au rangi ya mtu
20. Alama inayotumika katika kutaka kujua
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 162 12/11/2019 09:44
163
Sura ya Kumi na Sita
A. Ufahamu
Bado ningali kijana
:
Kwa nini huruma huna, nieleze waziwazi;
Mbona kunitesa sana, kwayo nyingi hino kazi?
Sasa nimekondeana, macho hayeshi machozi;
Ni unyama sio kazi, nami ningali kijana.
:
Japo ungalia sana, kikombe kujaza chozi;
Usiku au mchana, sijali wako ulizi;
Ulitaka kazi sana, sasa huna uchaguzi;
Utafanya yangu kazi, hata ukiwa kijana.
:
Nilipunjwa hiyo jana, kwao mwingi ubazazi;
Kwambiwa kazi hakuna, naja kula maandazi;
Halafu tasoma sana, pasi kamwe simbulizi;
Kumbe naja fanya kazi, nami ningali kijana.
:
Sasa hayo unonena, kwangu mimi ni upuzi;
Kamwe hayana maana, muhimu kuchapa kazi;
Pesa zangu zinanena, nilizompa shangazi;
Utafanya yangu kazi, hata ukiwa kijana.
:
Masikio kunikuna, kuniita mchopozi;
Chakula wanyima tena, eti ni rada ya mwizi;
Mwili kubaki rabana, kwa kukikosa kivazi;
Huna huruma mzazi, nami ningali kijana.
:
Sikia ninayonena, ewe mkubwa kilizi;
Ninao wangu waana, tena hawa sio wezi;
Ninawathamini sana, mimi kwao ni mzazi;
Wewe kwangu kijakazi, hata ukiwa kijana.
:
Hunayo huruma tena, japo wewe u mzazi;
Umri wangu ‘kiona, mdogo kwa yako kazi;
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 163 12/11/2019 09:44
164
Hata kumi myaka sina, wanifanya mchukuzi;
Hata hunayo mbawazi, nami ningali kijana.
:
Sikia wewe Sichana, mekuwa kidomo wazi;
Wewe mtu duni sana, jua hili waziwazi;
amani kamwe hauna, hata ulie machozi;
Utafanya yangu kazi, hata uwe u kijana.
:
Japo pesa nyingi sina, nakweleza waziwazi;
Nina haki kubwa sana, mimi kamwe sio bozi;
Liso na mwisho hakuna, hata liwe ujakazi;
Ya madhila hino kazi, nami ningali kijana.
M:
Sasa kweli nimeona, kunishukuru huwezi;
Ni huruma niliona, kukufanya kijakazi;
Sasa kwamba umenona, waniletea upuzi;
Umejazwa uchochezi, japo ungali kijana.
M:
Ajira hino wanena, wale wenye na mbawazi;
Kuwaajiri waana, kuwafanyiza na kazi;
Ni hatia kubwa sana, hata kuuliko wizi;
Sizitaki shida hizi, mimi ningali kijana.
Nimepevuka nanena, hutoweza nibazazi;
Kunita mjalaana, fakiri na mkwepuzi;
Sasa mwanga nimeona, nimekutambua wazi;
Tena nakwambia wazi, mimi ningali kijana.
Nataka kusoma sana, kila kitu nimaizi;
Mawi nipate yanena, wote wapate maizi;
Kwamba wajakazi wana, wala si punda wa kazi;
Watambue wazi wazi, mimi ningali kijana.
Maelezo ya msamiati
hayeshi : hayaishi.
ubazazi : udanganyifu; hila.
simbulizi : kusumbuliwa.
mchopozi : mwizi.
rada ya mwizi : malipo ya mwizi.
rabana : uchi.
kivazi : mavazi.
kijakazi : mtumishi mwanamke.
mbawazi : huruma.
bozi : mpumbavu.
madhila : mateso, taabu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 164 12/11/2019 09:44
165
mjalaana : aliyelaaniwa.
mkwepuzi : mwizi.
nimaizi : nielewe; nifahamu.
Maswali
1. Hili ni shairi la majibizano kati ya mwajiri na mwajiriwa. Shairi la aina hii huitwaje?
2. Msichana analalamika kuwa anatendewa maovu na mwajiri wake. Yataje maovu hayo.
3. Mwajiri anajitetea vipi?
4. Mwishoni mwa shairi msichana anakia uamuzi. Ni uamuzi gani anaokia?
5. Vina vya kati na vya mwisho katika kila ubeti wa shairi hili ni vipi?
6. (a) Kila ubeti una mishororo mingapi?
(b) Ubeti wa aina hii huitwaje?
7. Shairi hili lina mafunzo gani kwa waajiri?
8. Tunga sentensi ukitumia maneno haya:
(a) nilipunjwa (b) ubabazi (ch)mchopozi
(d) rada ya mwizi (e) kijakazi (f) mbawazi
(g) ajira (h) mjalaana (i) mkwepuzi
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi
Misemo
Misemo ni neno au fungu la maneno lenye maana fulani maalum. Lugha zetu mbalimbali huwa
na misemo mingi ambayo hutumiwa kuifanya lugha yenyewe iwe na mvuto mkubwa. Misemo
huweza kujumlisha tungo maalum au nahau ambazo hupatikana kwa wingi sana au maneno
yanayotumika kwa kipindi maalum na kisha kutoweka yaani misimu.
Lugha ya Kiswahili kwa mfano ina nahau nyingi ambazo hutumiwa kuifanya lugha iwe na
mvuto mkubwa. Hii ni baadhi ya mifano:
Angua kicheko. (nahau) Jipodoa. (msemo)
Agizia risasi.(nahau) Piga mafamba. (nahau)
Domo kaya. (msemo) Paka mafuta kwa mgongo wa chupa. (msemo)
Akina pangu pakavu tia mchuzi. (msemo)
Chapa maji.(nahau) Tia wasiwasi (nahau) n.k.
Tanbihi: Nahau huwa na muundo wa kitenzi na nomino ilhali misemo haina muundo huo na
huweza kuwa neno moja (kitenzi) au kishazi au sentensi.
Misimu au semi ni maneno yanayozuka na kutumika kwa kipindi fulani na labda kutoweka
baadaye. Baadhi ya misimu hushika na kuendelea kutumiwa katika lugha fulani. Hii ni misimu
inayotumiwa katika lugha ya Kiswahili:
Jisikia sukari (kujiona/kuringa).
Achwa kwenye mataa (achwa mahali ukiwa umezubaa au kupuuzwa).
Kula kuku kwa mrija (kuendelea vizuri kiuchumi n.k.)
Kaa ngumu (kutotishika/kuvumilia)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 165 12/11/2019 09:44
166
Zoezi
Andika misemo au nahau sita zenye neno piga halafu ueleze maana zake.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -angu’, -ako’, -ake
Tazama jedwali hili:
Ngeli Nomino
Vimilikishi
Msatumizi
-angu -ako -ake
i
zi
kalamu
kalamu
yangu
zangu
yako
zako
yake
zake
Kalamu yako imepotea.
Kalamu zako zimepotea.
i
i
chai chai yangu
yangu
yako
yako
yake
yake
Chai yake imekwisha. Chai
yake imekwisha.
u
zi
uzi nyuzi wangu
zangu
wako
zako
wake
zake
Uzi wangu umeibiwa. Nyuzi
zangu zimeibiwa.
u
u
ugali ugali wangu
wangu
wako
wako
wake
wake
Ugali wangu uko wapi? Ugali
wangu uko wapi?
ku ku kukopa
kukopa
kwangu
kwangu
kwako
kwako
kwake
kwake
Kukopa kwake kunaudhi.
Kukopa kwake kunaudhi.
pa
ku mu
mahali
mahali
mahali
pangu
kwangu
mwangu
pako
kwako
mwako
pake
kwake
mwake
Mahali pake panatosha.
Mahali kwake kunatosha.
Mahali mwake mnatosha.
zi fedha z angu zako zake Fedha zake zimepatikana.
Zoezi
1. Chagua nomino mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo.
Kwa mfano: _______ wake umeliwa (Ugali, Nyumba).
Ugali wake umeliwa.
(a) _________ pake pamenyakuliwa. (mahali, kucheza)
(b) _________ kwako hakufai kitu. (mahali, uzi)
(ch) ________ yangu imetoboka. (uji, ndoo).
(d) ________ zako zitajengwa lini? (chakula, kuta).
(e) ________ zangu zimetua. (ndege, mvua)
(f) _________ kwako hakufai kitu. (kulima, chai).
(g) _______ wangu umepikwa. (uji, chai).
(h) _________ zangu zimeoshwa na mfanyakazi. (ufa, baiskeli).
(i) __________ yako imekwisha. (ulemavu, sukari)
(j) __________ mwangu mnapendeza. (kuishi, mahali).
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 166 12/11/2019 09:44
167
2. Andika sentensi zifuatazo kwa umoja.
Kwa mfano: Baiskeli zake zimepotea.
Baiskeli yake imepotea.
(a) Nyumba zao zimejengwa vizuri.
(b) Mahali pangu panapendeza sana.
(ch) Ukweli wako utakufaa.
(d) Chumvi yake itatumika.
(e) Baiskeli zangu ziko wapi?
(f) Ndoo zangu zimejaa maji.
(g) Mahali mwangu mmefungwa.
(h) Kucheza kwako hakufai.
(i) Kutembea kwake kulimsaidia.
(j) Nyimbo zangu ziliwapendeza.
Kuakisha
Alama za mtajo/kunukuu/usemi (“ ”)
Alama hizi hutumiwa:
1. Kuonyesha maneno halisi kama yalivyoandikwa au kutajwa na msemaji bila kugeuza
chochote; kwa mfano:
(a) Mama aliniambia, Maria, amka ukimbie shuleni.
(b) Waziri aliwaambia waandamanaji, “Sioni kwa nini msirejee kazini mara moja madhali
nimewaeleza kuwa matakwa yenu yanachunguzwa.
(ch) “Fungua mlango mara moja, wezi waliniamuru.
Iwapo kuna dondoo dogo ndani ya dondoo kuu, dondoo dogo hunukuliwa kwa alama
moja moja (‘ ’) na dondoo kuu kwa alama mbili mbili (“ ”). Kwa mfano:
(a) “Kwa nini hukusema ‘kwaheri’ ulipoondoka?” Mwanaisha aliniuliza.
(b) “Nilisikia sauti ya ‘Toka! Toka! Toka!’ kabla ya mlio wa risasi, nilimwambia baba
yangu.
(ch) “Ukika mjini tafadhali niletee jarida la ‘Mwanasiasa wa kesho liuzwalo kwenye
duka la Bwana Jumakoshi, babu aliniambia.
2. Kuonyesha majina ya vitu kama lamu, makala n.k. Kwa mfano:
(a) Kipindi cha “Zilizovuma kinapendwa na wasikilizaji wengi sana wa redio.
(b) Makala ya “Ukumbi wa lugha yanawasisimua wasomaji wengi wa gazeti la Taifa
l e o”.
(ch) Je, umewahi kutazama lamu iitwayo Saikati”?
3. Kuonyesha lugha ngeni; kwa mfano:
(a) Rais alipowasili tulimchezea “isikuti.
(b) Nikika Kitui nitaingia hotelini ili nijipatie muthokoi.
(ch) Mara nyingi binadamu huhitajika tu kutumia common sense.
(d) Jana tulisari kwa matatu hadi Mombasa.
4. Kuonyesha neno ambalo pengine halijulikani sana au lile ambalo halijakubaliwa rasmi;
kwa mfano:
(a) Kimeu alipokisha umri wa miaka 50 aliamua “kungatuka.
(b) Tulipoka nchi ya Wamasai, tulikaribishwa kwa maziwa kwenye manyatta.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 167 12/11/2019 09:44
168
Zoezi
Weka alama za kuakisha mahali pafaapo kwenye sentensi hizi:
(a) niletee .gazeti la daily nation mwalimu aliniambia
(b) siwezi kumsaidia mhuni kama wewe aoko aliniambia
(ch) kipindi cha redio kiitwacho usalama barabarani kina manufaa mengi
(d) kimbia haraka ukanunue kitunguu sokoni nyanya aliniamuru
Alama ya mshazari (/)
Alama hii yaweza kutumika katika mazingira kama yafuatayo.
1. Kuonyesha kumbukumbu au tarehe; kwa mfano:
(a) KUMB. EML/VU/J1
(b) KUMB. AD/159/SW/2
(ch) tarehe 3/8/2002
2. Kuonyesha kuwa maneno fulani yako na maana sawa; kwa mfano:
(a) nukta mkato/semi koloni
(b) heru mlazo/italiki
(ch) watu/binadamu
(d) mbogo/nyati
(e) shule/skuli
3. Kuonyesha au”; kwa mfano:
(a) wanawake/wanaume (wanawake au wanaume).
(b) mbuzi/sungura (mbuzi au sungura).
(ch) wazee/vijana (wazee au vijana)
D. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Matangazo
Matangazo ni maandishi yanayotolewa ili kuuwasilisha ujumbe fulani kwa njia ya mkato na
inayoeleweka vizuri. Matangazo ya aina mbalimbali yana malengo mbalimbali. Lakini sababu
kuu ya kuwako kwa matangazo ni kutoa taarifa fulani hasa kwa watu wengi.
Matangazo mengi huweza kuambatanishwa na picha au michoro ili ujumbe wake uweze kueleweka
kwa urahisi, uwe na mnato na usisimue. Ni muhimu yule anayelengwa aweze kuupata ujumbe
ule kwa maneno machache na auelewe ipasavyo. Ikiwa anayelengwa hatauelewa ujumbe ule,
ujumbe huo utakuwa umeshindwa kulikia lengo lake la kimsingi la kuwasiliana.
Lengo la matangazo
Kutoa tahadhari kwa watu wasifanye jambo fulani. Kwa mfano mchoro wa fuvu la kichwa
na mifupa nyuma iliyofanya alama ya X na maneno HATARI hutumiwa kuwaonya watu
wasikaribie au kugusa kitu fulani kwa mfano nyaya za umeme.
Kutoa maelekezo. Kwa mfano, kwenye barabara zetu kuna matangazo mengi
yanayowaelekeza waendeshaji wa magari jinsi ya kuyaendesha ili waepuke ajali.
Matangazo hutumiwa pia kwa nia ya kufahamisha; kwa mfano: kumjulisha mtu kuwa
kuna bidhaa fulani mpya.
Kutoa taarifa za kibiashara. Kila siku tunakumbana na matangazo ya biashara magazetini
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 168 12/11/2019 09:44
169
au hata kwenye runinga. Matangazo haya hutumia lugha ya kushawishi ili wanunuzi
wainunue bidhaa fulani.
Bei imepunguzwa !
Jinunulie Redio
ya
Jihadhari na
UKIMWI
Ukimwi hauna
tiba na wala
haubagui !
Sote tunauthamini usa
wa jiji letu.
TUSITUPE TAKA
OVYO OVYO!
SUPERSOUND
leo
Sifa nyingine za matangazo
Matangazo mengi huandikwa kwa heru kubwa na kwa wino mzito au kwa heru nzito
au hata kwa rangi za kupendeza ili yaweze kuyavuta makini ya wasomaji.
Ujumbe wenyewe hutolewa kwa maneno machache yanayoeleweka waziwazi.
Matangazo yanaweza kuwa maswali mepesi kama: Lini, Wapi, Vipi, Nani n.k.
Siku hizi kwa kutumia tarakilishi, matangazo huweza kuandikwa kwa kuongezea madoido
na kuyafanya ya kupendeza na kuvutia sana.
Tazama mfano ufuatao wa tangazo:
HATIMAYE!
USOMAJI WA KISWAHILI SASA
NI PAPAI KWA KIJIKO !
VITABU MAALUM VYA
SASA VIMEWASILI MADUKANI.
JINUNULIE NAKALA YAKO LEO!
NGOMA YA LUGHA
NGOMA YA LUGHA
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 169 12/11/2019 09:44
170
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1
2
3 4 5
6 7
8 9
10 11 12
13 14
15 16
17
18
19
KULIA
1. Momu zinazoambishwa kwenye mzizi wa neno
3. RITASKI
4. Fahari
6. Mpelelezi
10. Kioo cha tarakilishi au runinga
12. Misemo iliyocha maana
13. Moja kati ya sehumu kuu na maalum ya tarakilishi
15. Rununu ya maninga
16. Kuongea
17. Tungo ambazo hutoa taarifa kamili
18. Kutokuwa na uwezo mkubwa wa kujikumu
19 Mtiririko wa hatua kwa hatua hasa katika kompyuta
CHINI
1. Wingi wa chake
2. Kipashio cha lugha
5. Ameaga dunia
7. Maneno yanayoonyesha kuwa na kitu au hali
8. MURAGPRO
9. Mtindo wa kufuata katika utekelezaji wa jambo fulani
11. Vitu au mambo yanayotuzunguka
14 Ninachomiliki
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 170 12/11/2019 09:44
171
A. Ufahamu
Magazeti na Umuhimu wake
Ni asilimia ndogo sana ya watu ambao hawajawahi kuliona gazeti. Labda wengi wetu huwaona
wachuuzi wa magazeti wakizunguka hapa na pale wakiyauza magazeti asubuhi au wakati wowote
ule. Wengine wetu hukumbana na wasomaji wa magazeti ambao wamezama kwenye habari
zilizomo gazetini. Baadhi yetu huipata fursa ya kulisoma gazeti ili kufuatilia visa mbalimbali.
Lakini je, tumewahi kuwazia hali ingekuwa namna gani kama kusingekuwako na magazeti?
Historia ya magazeti ilianza katika karne ya kumi na saba nchini Ujerumani wakati ambapo
gazeti la kwanza lilichapishwa. Kabla ya hapo habari ziliandikwa kwenye karatasi moja moja na
kusomwa hivyo.
Magazeti humsaidia na kuhakikisha kuwa msomaji anaelewa ni mambo gani yanayoendelea
sio tu pale anapoishi bali pia kwingineko. Msomaji anapata fursa ya kujua mambo mengi na
kwa undani kwa gharama ndogo. Magazeti yanamwezesha msomaji kuipata taarifa fulani kwa
kina na mapana yasiyowezekana kwa kutumia vyombo kama redio au runinga. Aidha hadithi
na taarifa zinazopatikana katika magazeti hugusia masuala mbalimbali. Fauka ya kuwako kwa
taarifa muhimu, magazeti huwa na habari kochokocho kuhusu siasa, sanaa, michezo, mitindo
ya mavazi na matendo, biashara, teknolojia, sayansi na mazingira. Magazeti huwa pia na maoni
na mitazamo mbalimbali ya watu wengine. Kwa njia hii huchangia na kuhimiza kubadilishana
kwa mawazo pamoja na kuelimishana.
Magazeti yanaweza kuwa ya kieneo yanayopatikana katika sehemu fulani ndogo tu, au ya kitaifa
ambayo hupatikana katika taifa zima. Magazeti ya kieneo huzungumzia masuala yanayolihusu
eneo fulani, mji fulani mahsusi au sehemu fulani ndogo. Usambazaji wa magazeti ya aina hii ni
mdogo na yanapatikana katika sehemu ndogo tu. Magazeti ya kitaifa kwa upande wake husambaa
sana na huzungumzia masuala yanayolihusu taifa fulani na ya ulimwengu mzima pia. Kila nchi
huwa na magazeti yake ambayo huchapishwa kila siku na mengine ambayo huweza kuchapishwa
mara moja kwa wingi. Nchini Kenya tuna magazeti ya kitaifa kama e Daily Nation, Taifa Leo,
e Standard, e People na Kenya Times.
Uuzaji wa magazeti hutofautiana. Kuna magazeti ambayo huuza nakala nyingi kwa siku
moja. Sababu kuu zinazoathiri uuzaji wa magazeti ni mapendeleo ya wasomaji, uzuri au ubora
wa uwasilishaji wa habari zenyewe (uwasilishaji wake wa habari bila kubagua wala kupendelea),
usambazaji wake, bei yake pamoja na hisia mbalimbali za wasomaji wenyewe. Kimuundo gazeti
huwa na muundo fulani maalum. Kila gazeti lina mpangilio wake maalum. Licha ya tofauti hizi,
magazeti yote huwa na jina lake lililoandikwa kwa heru kubwa kwenye ukurasa wa kwanza.
Huu ndio ukurasa unaokuwa na kichwa cha habari kuu ambacho aghalabu huandikwa kwa
heru kubwa nzito. Itokeapo kwamba kuna matukio makubwa na muhimu nchini siku hiyo
hiyo moja, inawezekana magazeti kutolewa tena yakiwa na vichwa vingine tofauti. Haya huwa
matoleo maalum ya magazeti na hukusudiwa kuhakikisha kuwa wasomaji wamepata habari hizo
mpya haraka na kwa ukamilifu.
Magazeti hayawezi kuwako bila ya kuwapo kwa chumba cha habari. Chumba cha habari
kinaweza kuchukuliwa kama kiini cha habari au chumba cha uhariri. Katika chumba hiki, habari
za kila aina hupokelewa kutoka maeneo mbalimbali nchini na nje za nchi. Habari hizi hupokelewa
Zoezi la Marudio II
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 171 12/11/2019 09:44
172
kwa njia mbalimbali kama simu, mashine za kutumia vipepesi au faksi, kompyuta, setilaiti n.k.
Habari hizo hutokana na mashirika mengine ya habari au waandishi wa habari walioko sehemu
fulani. Ni katika chumba cha habari pia ambapo waandishi wa habari huandika hadithi zao au
visa mbalimbali kutokana na taarifa walizozipata. Baada ya kuandikwa huko wahariri wasaidizi
huzipitia na kuzitathmini kabla ya kupitishwa kwa wahariri wanaozichuja na kutathmini kuujua
uzito wake ili kujua ni hadithi na habari zipi za kuchapishwa na zipi sio za kuchapishwa, zipi za
kupewa uzito na zipi sio za kupewa uzito.
Baada ya uamuzi huo kufanywa, maandalizi ya uchapaji hufanywa ili kuhakikisha kuwa
habari hizo zimewakia waliolengwa. Uchapaji wa magazeti hufanywa kwa mashine kubwa
ambazo hupatikana katika matbaa ya kampuni inayohusika. Mashine zinazotumiwa huwa na
uwezo mkubwa wa kuchapa habari hizo kwenye mitandao mikubwa ya karatasi ambayo huweza
kukia hata kilomita kadha. Zipo mashine nyingine ambazo huhusika na uchapaji, nyingine
ukataji, ukunjaji na nyingine usombaji wa magazeti yaliyochapishwa kwenye matita kadha katika
kipindi kifupi sana.
Magazeti yaliyochapishwa husambazwa kwa magari sehemu mbalimbali ili kuwakia wasomaji
walengwa wakati ufaao. Aghalabu usambazaji wa magazeti hufanywa usiku ili kuhakikisha
kuwa wasomaji wanayapata magazeti hayo alfajiri. Siku hizi taarifa zilizochapishwa magazetini
husambazwa kwa njia ya mtandao wa intaneti na kuhakikisha kuwa wasomaji walio mbali
wanaweza kufuatilia habari za nyumbani kwa njia ya tarakilishi. Kuwapo kwa magazeti ni njia
mojawapo muhimu ya kuelimisha, kufahamisha na kuhakikisha maendeleo ya taifa na ulimwengu
mzima.
Maswali
1. Kabla ya kuvumbuliwa kwa magazeti, habari ziliandikwaje?
2. Taja manufaa yanayotokana na usomaji wa magazeti.
3. Eleza tofauti kati ya magazeti ya kieneo na magazeti ya kitaifa.
4. Habari zinazochapishwa magazetini hupokelewa kwa njia zipi?
5. Panga shughuli zifuatazo kuhusu uchapaji wa magazeti kwa mpangilio ufaao:
(a) usambazaji wa magazeti
(b) kupokelewa kwa habari
(ch) kuhaririwa kwa habari
(d) uchapaji
(e) uandalizi wa uchapaji
6. Eleza maana za maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu hiki:
(a) huipata fursa (b) habari kochokocho (ch) husambaa (d) tarakilishi
B. Kusikiliza na kuzungumza
(1) Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali.
Hapo zamani za kale mamba na mbuni walikuwa maraki wakubwa sana. Hakuna siku ambayo
ilipita bila ya maraki hawa wawili kutembeleana na kujuliana hali. Kama kawaida, mamba aliishi
mtoni lakini raki yake mbuni aliishi kwenye pori lililokuwa hapo karibu. Kila siku wakati jua
lilipotokeza na kupanda juu, mamba alitoka majini na kumsubiri raki yake hapo nje. Alijitandaza
kwenye mchanga kulifurahia jua la wakati ule. Mtu akiwa mbali alishindwa kumtambua.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 172 12/11/2019 09:44
173
Mamba alipokuwa na njaa alirudi majini na kujicha ndani hadi mnyama mmoja kama paa
alipotokeza. Mamba alijicha na kusogea karibu na ukingo kwa ujanja na kumkamata mnyama
huyo. Mbuni hakuwa na sababu ya kuwa na wasiwasi hata kidogo. Alijua kuwa mamba alikuwa
raki yake wa miaka mingi. Hakuweza kumdhuru yeye raki yake mkubwa kiasi hicho.
Lakini siku moja hali ilimbadilikia mamba. Siku hiyo aliwasubiri wanyama waje majini kama
kawaida lakini hawakuja. Alishikwa na njaa kubwa sana. “Sasa nifanyeje leo? Hali ikiendelea
jinsi hii huenda nikafa kwa njaa, alijiambia. Alitupa macho huku na kule kuangalia kama kuna
mnyama aliyekuwa akisogea lakini hakuwa na bahati. Hatimaye alimwona raki yake mbuni
akitokeza kwa mbali.
Mbuni alipoka ukingoni alimkuta raki yake mamba. Lakini alipomsalimu hakumjibu kwa
bashasha kama kawaida yake. Alikuwa na huzuni nyingi. Mamba alijiambia moyoni, Hii ndiyo
nafasi niliyoisubiri Mbuni alimuuliza, Raki yangu mpendwa, ni kitu gani kinachokusumbua?”
Mamba aliuinua uso wake kwa huzuni. Alisema kwa sauti ya masikitiko, nina jino langu
linalonisumbua sana, alisema. Jino tu?” alishangaa mbuni. Ndiyo, tena lile la mwisho,
limenisumbua mno, alijibu mamba. Hebu fungua kinywa, niangalie, alisema mbuni.
Mamba alifungua kinywa naye mbuni akaiingiza shingo yake ndani. Mara tu baada ya
kuiingiza shingo ndani, mamba alifumba kinywa na kuanza kujivuta kurudi majini. Mbuni alijivuta
kwa nguvu zake. Walivutana, wakavutana, wakavutana weee. Hatimaye mbuni alifanikiwa kutoka
kinywani mwa mamba. Shingo yake ilikuwa imerefuka ajabu. Alitimua mbio kuelekea porini huku
akilaani. “Huyu ni raki wa aina gani jamani?” Uraki wao uliisha siku hiyo.
Maswali
1. (a) Hadithi hii huitwaje?
(b) Je, kwa nini mamba alikuwa na huzuni nyingi?
(ch) Je, unadhani mamba ni raki wa aina gani?
(d) Je, unajifunza nini baada ya kusoma hadithi hii?
(e) Taja sifa za hurafa katika hadithi uliyoisoma.
2. Tegua vitendawili vifuatavyo.
(a) Kipo lakini hukioni.
(b) Ninapompiga mwanangu watu hucheza.
(ch) Nina saa ambayo haijasimama tangu kutiwa ufunguo.
(d) Mzazi ana miguu bali mzaliwa hana.
(e) Anataga huku akitambaa.
(f) Nyumba yangu kuu lakini ina mlango mdogo.
(g) Nimeanika mpunga wangu usiku kulipopambazuka sikuuona.
(h) Taa yangu yazagaa ulimwengu mzima.
(i) Popote niendapo anifuata.
(j) Haukamatiki wala haushikiki.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 173 12/11/2019 09:44
174
CH. Saru na matumizi ya lugha
1. Onyesha vihisishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Lo! Lo! Yule ni nani?
(b) Salaala! Mbwa mkali amemuuma Maimuna.
(ch) Kumbe! Mimi sitakusaidia tena.
(d) La hasha! Siwezi kukopesha pesa nyingine.
(e) Zii! Kwani wewe huna aibu?
2. Andika vitenzi hivi katika kauli ya kutendea na kutendewa.
Kauli ya kutenda Kauli ya kutendea Kauli ya kutendewa
k.m. piga
lima
andika
koroga
chora
chapa
pigia
pigiwa
3. Kamilisha tashbiha zifuatazo kwa kuchagua jibu sahihi: tausi, maji ya mtungi, mfungwa,
fuka, barafu
(a) Yule mlevi amekuwa mchafu kama ____ siku hizi.
(b) Siku hizi nimepoa kama _______; maneno mengi sipendelei.
(ch) Tangu aingie kidato cha kwanza, Kanana anaringa kama______.
(d) Nimeshindwa kuinywa hii soda kwa sababu ni baridi kama ______.
(e) Huyu mtoto hachezi na wenzake, kwani anachungwa kama _____.
4. Andika sentensi zifuatazo katika hali ya ‘me.
Kwa mfano: Baba analala.
Baba amelala.
(a) Mabati yananunuliwa.
(b) Baba atakwenda dukani.
(ch) Punda anakunywa maji.
(d) Nyanya alimtuma nani sokoni?
(e) Wasukuma wanachonga vinyago.
(f) Paka atamkamata panya.
(g) Chifu aliwahutubia wanakijiji.
(h) Watoto watacheza mpira.
5. Kanusha sentensi zifuatazo.
Kwa mfano: Baba amenipa chungwa tamu.
Baba hajanipa chungwa tamu.
(a) Kondoo amekula majani.
(b) Sisi tumefurahi.
(ch) Nyinyi mmepewa ruhusa.
(d) Baba ameandika barua ndefu.
(e) Mbu amemuuma mtoto.
(f) Galgalo amechimba mtaro.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 174 12/11/2019 09:44
175
6. Chagua kiunganishi mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo: tena, kisha, wala, mpaka,
lakini
(a) Sikwenda sokoni ________ dukani.
(b) Nilikwenda ________ sikupata nilichotaka.
(ch) Mimi nimekasirika, _______ nimekasirika sana.
(d) Tutajitahidi ________ tupite mitihani yote.
(e) Niliosha vyombo ________ nikaenda kulala.
7. Onyesha vihusishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Abeid amejicha ndani ya nyumba.
(b) Kuna uhasama mwingi kati ya Kemunto na Keraro.
(ch) Kakangu anatembea kando ya barabara.
(d) Weka mtungi huu nje ya kibanda kile.
(e) Wafungwa kadiri ya mia moja wameachiliwa huru.
8. Andika maneno yafuatayo katika kauli ya kutendwa na kutendeka.
Kauli ya kutenda Kauli ya kutendwa Kauli ya kutendeka
k.m. piga
chora
lima
pita
funga
chota
kata
ruka
kopa
panda
tenda
pigwa
pigika
9. Chagua majibu mwafaka kukamilisha tashbihi zifuatazo: kiriba, twiga, nyundo, sungura,
sindano, makaa
(a) Mwanaisha ni mjanja kama __________.
(b) Munavu hahitaji uto kuangua matunda kwani ni mrefu kama ________.
(ch) Oprong amekonda kama ________ kwa sababu ya maradhi.
(d) Paka mweusi kama __________ amemkamata panya.
(e) Chifu Mbuguma alikuwa na tumbo kubwa kama ________ kabla ya kupelekwa jela.
(f) Ndunge ameshindwa kuikia kamba ya kuingilia kwenye lori kwa sababu ni mfupi
kama __________.
10. Kanusha sentensi zifuatazo:
(a) Nyanya hunipikia uji wa wimbi.
(b) Mbithi hufanya kazi kwa bidii.
(ch) Wao hutembea usiku.
(d) Sisi huwafundisha wanafunzi wale.
(e) Nyinyi hulima kondeni.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 175 12/11/2019 09:44
176
11. Bainisha maneno katika sentensi zifuatazo.
Kwa mfano: Mama amekwenda shambani.
N T E
(a) Mvua kubwa ilinyesha jana.
(b) La hasha! Sitakwenda sokoni leo.
(ch) Mama na baba wameka.
(d) Watoto watatu wameingia darasani.
(e) Mbwa na paka wanachukiana sana.
12. Sahihisha viambishi vilivyotumiwa vibaya kwenye sentensi zifuatazo:
Kwa mfano: Mtoto limeanguka.
Mtoto alianguka.
(a) Kiatu ameraruka.
(b) Matunda imenunuliwa sokoni.
(ch) Maji umekwisha.
(d) Ugali iko wapi?
(e) Chakula yuko hapa.
(f) Mshumaa anawaka.
(g) Paka imeshika panya.
(h) Ugonjwa vimekwisha.
14. Kamilisha jedwali lifuatalo ili kuonyesha udogo wa nomino ulizopewa katika umoja na
wingi.
Mzizi wa nomino Nomino za wastani Nomino za udogo
umoja wingi umoja wingi
k.m. –ti
–su
–tu
mti miti
kisu visu
mtu watu
kijiti vijiti
–ana
–jia
–toto
–duka
–iko
mwana wana
njia njia
mtoto watoto
duka maduka
mwiko miko
15. Andika sentensi zifuatazo upya kwa kugeuza nomino iliyopigiwa mstari kuwa ya ukubwa.
K.m. Mto huu utafurika leo usiku ______
Jito hili litafurika leo usiku.
(a) Mtu huyu anatakaje?
(b) Wachezaji shupavu walipiga ngoma kwa ustadi.
(ch) Huyu ndege huenda akakuumiza.
(d) Paka na mbwa hawa wanangang’ania chakula.
(e) Mwizi huyu atashikwa siku moja.
16. Weka mabano mahali panapofaa kwenye sentensi hizi.
K.m. Mwinyimkuu (ni mzee mcheshi kwelikweli) amepewa zawadi nono.
(a) Tukienda Mombasa mwakani ingawa sina matumaini makubwa nitakununulia nazi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 176 12/11/2019 09:44
177
(b) Wale wote waliotaka kufaulu kina Matovu na wenzake itabidi watie bidii sana.
(ch) Vita vya kwanza vya dunia 1914-1918 viliathiri sana uchumi wa ulimwengu.
17. Chagua kimilikishi mwafaka kukamilisha sentensi.
K.m. Mtoto ______________ (chako, wako, lako) anaugua malaria.
Mtoto wako anaugua malaria.
(a) Kikapu ___________ (yako, vyako, chako) kimejaa matunda.
(b) Machungwa ____________ (yako, wako, vyako) yameliwa.
(ch) Mshipi ___________ (wangu, yangu, langu) uko wapi?
(d) Mafuta ________ (chako, wako, yako) yamemwagika.
(e) Chungwa ___________ (yangu, langu, changu) limeanguka.
D. Kusoma
Isimujamii
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali uliyoulizwa
A: Vipi mtu wangu?
B: Poa. Habari za masiku?
A: Kusota na kubangaiza tu. Sijui hela zimehamia wapi?
B: Wewe hapo ulipo unajifungia nyumbani kama mboch. Unadhani zitakufuata huko?
A: Nilihustle hadi nikachoka tik. Nikaamua kutulia nyumbani kwa muda.
B: Sasa sikiza mshikaji; gava ina mipango ya mayuts kupata mikopo wakuze bizna.
A: Sema, nakusikiliza.
B: Mbona tusiunde kikundu chetu tutafute kamradi kisha tuendee hizo pesa za gava? Mtu
ni kujipanga bwana.
A: Una hakika tutaweza kupata hizo fedha za gava?
B: Wee wacha woga. Tutachora plan poa ya bizna. Najua mtu anayeweza kutufaa kuichora
hiyo. Ana experience kibao.
A: Haya! Tukutane kesho jioni tupange.
B: Sawa! Wewe tafuta mayuts wengine wawili-watatu ambao ni trustworthy. Na mimi nitafute
wangu. Group ya wasee sita ni poa.
A: Nitawasaka majamaa niwajuao kesho mtu wangu.
B: Perfect!
Maswali
(i) Hii ni sajili gani
(ii) Je, ni masharti yepi ya lugha yaliyoongoza mazungumzo haya?
(iii) Eleza sifa za sajili hii.
Fasihi simulizi:
Soma makala haya kisha ujibu maswali yanayofuata.
Fasihi simulizi ni sanaa ambayo inatofautiana sana na fasihi andishi katika vipengele vyake.
Fasihi simulizi ni fasihi ya masimulizi ingawa hivi leo baadhi ya tanzu zake tunazihifadhi katika
maandishi. Tofauti kubwa iliyoko yahusu masimulizi ambayo humtegemea msimulizi ambaye
naye sharti awe mbele ya msikilizaji ambaye aghalabu ni msimulizi pia. Hali hii ya ana kwa ana
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 177 12/11/2019 09:44
178
hurahisisha kuona na kusikia vitendo na masimulizi yatolewayo waziwazi. Utoaji wa masimulizi
hayo hutegemea mazingira, wakati na hali ya wasikilizaji na aghalabu hutawaliwa na mambo
haya kwani iko kwa sababu hiyo.
Fasihi simulizi ni sanaa inayokua, hubadilika na hufa kutegemea matumizi na heshima
inayopewa na jamii. Ujenzi wa sanaa hii hutegemea sana fanani (mwanasanaa) ambaye hupewa
msukumo na jamii yake kuitumia sanaa hiyo kwa manufaa ya jamii hiyo. Kila jamii inapobadilika,
fanani wa fasihi simulizi nao hubadilika kulingana na mazingira, wakati huo na matakwa ya watu
wa wakati huo.
Hivi leo, maendeleo ya kisayansi yameleta nyenzo mpya ambazo zina nafasi katika kusaidia
kuleta mabadiliko ya utoaji wa masimulizi. Ni juu yetu kutafuta njia bora za kuunganishia usasa
na ukale wa masimulizi kwa manufaa ya fasihi simulizi.
Lengo la kufundisha fasihi simulizi shuleni ni kuuondoa na kuzika kabisa mawazo na kira
duni ambazo tumerithi kutokana na utaalamu wa kigeni, aghalabu kutoka Ulaya na Marekani
kwamba sanaa ya zamani ya fasihi simulizi ni ya kishenzi. Sisi tunaamini vingine. Tunaamini
kuwa fasihi hii katika ukuaji na maendeleo yake, imethibitika kuwa njia au nyenzo bora sana ya
mawasiliano na ufundishaji wa jamii zetu leo na kesho. Kwa imani hii, fasihi simulizi inaletwa
shuleni kwa lengo la “kuifufua kutokana na hali ya kushwa kwake kwa miaka mingi iliyopita;
pia kuihifadhi, kuikuza na kuiendeleza kwa kuwafanya watoto wetu waithamini, waipende na
waitumie katika maisha yao ya kila siku kama ilivyokuwa ikitumika tangu hapo.
(Makala ya “Fasihi Simulizi: Mwongozo wa walimu wa Fasihi Simulizi, Mulika, 1977, uk. 22- 27)
Maswali
1. Je, kifungu hiki kinazungumzia nini?
2. Taja tofauti kuu kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi kwa mujibu wa kifungu hiki.
3. Kwa nini ni muhimu kufundisha fasihi simulizi?
4. Mwandishi ana maana gani anaposema “waipende na waitumie katika maisha yao ya kila
siku kama ilivyokuwa ikitumiwa tangu hapo.
E. Kuandika
Umepewa jukumu la kushiriki katika maandalizi ya siku ya michezo shuleni. Andika ratiba
itakayofuatwa siku hiyo.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 178 12/11/2019 09:44
179
A. Ufahamu
Teknolojia na maisha ya sasa
Teknolojia ni maarifa ya kuyatumia mawazo ya kisayansi kuunda vyombo au mashine ambazo
hurahisisha kazi au maisha. Teknolojia ilianza zama kongwe kiasi cha miaka milioni mbili iliyopita
wakati binadamu alipotengeneza ala kwa mawe. Kwa mara ya kwanza binadamu alitambua kuwa
aliweza kufanya kazi kama kukatakata kwa kutumia ala hizo.
Licha ya kwamba teknolojia ilianza zama kongwe za mawe, haikuendelea haraka hadi baada ya
Mapinduzi ya Viwanda katika karne ya kumi na nane. Tangu wakati huo, teknolojia imekuwa na
athari kubwa katika maisha yetu sisi binadamu. Maendeleo yake yamekuwa na matokeo makubwa
na yameathiri pakubwa mkondo wa maisha tunayoishi. Imetuletea njia za usari nyepesi na
salama zaidi, imetuletea bidhaa za kila aina kama za plastiki, imeturahisishia mawasiliano kwa
kuvumbuliwa kwa vyombo kama simu, runinga na katika miaka ya hivi karibuni, tarakilishi au
kompyuta pamoja na vyombo vingine muhimu.
Moja kati ya matokeo makubwa yanayohusishwa na maendeleo ya teknolojia ni katika
dawa na matibabu. Kutokana na teknolojia, binadamu ameweza kuyavumbua mambo
mengi na dawa
nyingi ambazo
zimemwezesha
kuyadhibiti
magonjwa sugu
na kwa njia hii
kuyarefusha maisha
yake. Katika miaka
ya huko nyuma,
baadhi ya magonjwa
yaliwaangamiza
watu kwa wingi,
lakini kutokana
na maendeleo
ya teknolojia,
binadamu amepata
njia za kuyakabili. Baadhi ya magonjwa hayo ni kama ukoma, ukambi au surua. Pili,
kuvumbuliwa kwa mashine kama uyoka au eksirei kunawawezesha madaktari kuutambua
ugonjwa mapema na kukabiliana nao kabla ya athari zake kutokeza.
Biashara ya siku hizi inawezekana kutokana na maendeleo ya teknolojia. Ni rahisi kama
kula papai kwa kijiko kusarisha bidhaa kutoka sehemu moja ya ulimwengu hadi nyingine.
Wavumbuzi wamevumbua mashine zinazoendesha magari, meli, ndege na vyombo vingine kwa
kasi sana. Wahandisi nao wamejenga madaraja, barabara, reli, bandari na viwanja vya ndege
kurahisisha mawasiliano baina ya watu.
Maendeleo upande wa mawasiliano yanahakikisha kuwa watu wanaoishi mbali wanawasiliana
haraka sana na kuondoa tatizo la ukiwa. Wanaweza kufanya hivi kwa kutegemea simu, kutumia
Sura ya Kumi na Saba
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 179 12/11/2019 09:44
180
runinga au hata tarakilishi hasa katika awamu tuliyo nayo sasa.
Licha ya faida zake nyingi, maendeleo ya teknolojia yana madhara yake pia. Maendeleo haya
yamesababisha pia kuwako kwa zana hatari za kivita ambazo huweza kumwangamiza binadamu.
Mfano mzuri ni silaha za kinyuklia ambazo zina uwezo wa kuangamiza mamilioni ya watu. Suala
muhimu analopasa kukumbuka binadamu ni kuwa ana wajibu wa kuitawala teknolojia lakini siyo
kuiacha teknolojia yenyewe imtawale. Lazima mahusiano yake na binadamu wengine yatawaliwe
na utu. Kwa njia hii maendeleo ya teknolojia yatatumika kwa faida ya binadamu.
Maswali
1. Teknolojia ilianza lini?
2. Taja matokeo matano ya maendeleo ya teknolojia.
3. Eleza jinsi maendeleo ya teknolojoa yameathiri uwanja wa dawa na matibabu.
4. Ni madhara yapi yanayotokana na maendeleo ya teknolojia?
5. Taja vifaa kumi katika shule yako ambavyo ni matokeo ya maendeleo ya teknolojia.
6. Je, unaweza kukisia maendeleo ya teknolojia yatakayokuweko katika mwongo mmoja
ujao?
7. Wewe binafsi unawezaje kuchangia katika maendeleo ya teknolojia.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Mjadala
Mjadala ni mazungumzo ya kimvutano kuhusu jambo fulani. Katika mjadala huwa kuna pande
mbili zinazojadiliana. Kila upande huwa na msimamo tofauti na upande wa pili. Upande huo
unakuwa na mawazo au hoja za kueleza kwa nini unapendelea msimamo huo mmoja au kwa
nini unaunga mkono upande huo. Huu huitwa upande wa kuunga mkono. Upande wa pili nao
huwa na msimamo wake tofauti. Upande huu huitwa upande wa kupinga mjadala. Upande huo
utakuwa pia na hoja za kuonyesha kwa nini wanachukua msimamo huo walio nao. Suala kuu
linalozungumziwa au kujadiliwa hujulikana kama mada.
Mambo muhimu kuhusiana na mjadala
Kuwako kwa vikundi viwili vinavyopingana au vyenye misimamo tofauti.
Kupanga hoja au mawazo kwa utaratibu.
Kuwasilisha mawazo au hoja kwa lugha inayosisitiza ujumbe ulio nao.
Kutumia lugha yenye uwezo wa kuwasadikisha wapinzani wako. Siri kuu ya mjadala ni
uwezo wa kuwafanya wapinzani wako kukubaliana na mawazo yako.
Kuhakikisha kuwa una hoja muhimu za kuutilia nguvu upande wako.
Katika sehemu hii, mtajadiliana kuhusu mada Umoja na utangamano wa jamaa ni muhimu
sana katika maisha ya siku hizi Mwalimu atawagawa wanafunzi katika makundi mawili kwa
ajili ya mjadala wa mada iliyotajwa.
Upande wa kuunga mkono
1. Jamaa huweza kusaidiana wakati wa shida.
2. Damu ni nzito kuliko maji.
3. Umoja na utangamano wa jamaa ni msingi wa ufanisi.
4. Nchi haiwezi kuwa na maendeleo bila ya kuwa na msingi huu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 180 12/11/2019 09:44
181
5. Msingi wa amani ya nchi hutegemea umoja wa raia. Lazima umoja na utangamano huo
kuanzia kiwango cha jamaa.
6. Utangamano huu unarahisisha mambo mengi.
7. Jamaa husaidiana kupambana na dhiki na shida za maisha.
Upande wa kupinga
1. Gharama ya maisha imepanda kiasi cha kuathiri mahusiano.
2. Maingiliano ya kutangamana kwingi kusababisha wivu na chuki.
3. Maisha yamebadilika sio kama zamani watu walipotegemea utendakazi wa pamoja.
4. Watu wengi huweza kufanya utenda kazi wao kuwa mgumu n.k.
5. Jamaa wanaweza kukukimbia kama huna pesa.
6. Wakati wa shida unalazimika kupambana na shida peke yako.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Kirejeshi amba-
Kirejeshi ni aina ya kivumishi ambayo hurejesha au husisitiza zaidi kuhusu nomino.
Tazama jedwali lifuatalo:
Ngeli Nomino Kirejeshi Matumizi
a
wa
kuku
kuku
ambaye
ambao
Kuku ambaye anataga ni wangu.
u
i
mlango
milango
ambao
ambayo
Mlango ambao utafungwa ni huu.
Milango ambayo itafungwa ni hii.
u
ya
ulezi
malezi
ambao
ambayo
Ulezi ambao alipata ni upi?
Malezi ambayo alipata ni yapi?
ya
ya
majira
majira
ambayo
ambayo
Majira ambayo yameanza yana baridi.
Majira ambayo yameanza yana baridi.
li
ya
embe
maembe
ambalo
ambayo
Embe ambalo unakula ni langu.
Maembe ambayo unakula ni yangu.
ki
vi
kikombe
vikombe
ambacho
ambavyo
Kikombe ambacho kimeanguka ni cha nani?
Vikombe ambavyo vimeanguka ni vya nani?
Sifa: (a) Huchukua viambishi tamati katika kuleta upatanisho wa kisaru.
(b) Huwa huru. Hakiambatishwi na kitenzi.
Zoezi
1. Tumia kirejeshi amba-” kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) Kipepeo __________ anaruka ni maridadi.
Vipepeo __________ wanaruka ni maridadi.
(b) Ulezi __________ alipewa ulimsaidia.
Malezi __________ walipewa yaliwasaidia.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 181 12/11/2019 09:44
182
(ch) Kiboko __________ kilitumika ni hatari.
Viboko __________ vilitumika ni hatari.
(d) Jicho _____________ linauma ni lipi?
Macho __________ yanauma ni yapi?
(e) Marashi _____________ yatatumiwa ni yapi?
Marashi __________ yatatumika ni yapi?
(f) Mshipi _____________ ulipotea ni wa baba.
Mishipi __________ ilipotea ni ya baba.
(g) Kiroboto ____________ anaruka atakuuma.
Viroboto wanaruka watakuuma.
(h) Maji _____________ yanamwagika ni sa.
Maji __________ yanamwagika ni sa.
(i) Neno _____________ linasomwa ni muhimu.
Maneno yanaosomwa ni muhimu.
(j) Kijitu _____________ kinakuja kitakushambulia.
Vijitu _____________ vinakuja vitakushambulia.
2. Badala ya nomino iliyopigiwa mstari, tumia ile iliyomo mabanoni.
Kwa mfano: Mtoto ambaye ameanguka ni wa nani? (kijitu)
Kijitu ambacho kimeanguka ni cha nani?
(a) Tunda ambalo limeanguka ni langu. (kiti)
(b) Mwanamke ambaye alipotea amepatikana. (maembe)
(ch) Kitabu ambacho kimekamilika ni kizuri mno. (upana)
(d) Ugonjwa ambao umekwisha ni upi? (maji)
(e) Kisu ambacho kilimkata kilinolewa zaidi. (jembe)
(f) Mawazo ambayo yalitolewa yalifaa. (kondoo)
(g) Manukato ambayo yalinunuliwa ni ya nani? (mshipi)
(h) Viatu ambavyo unataka si vizuri. (matunda).
(i) Maziwa ambayo yamenywewa ni matamu. (maji)
(j) Mchango ambao umetolewa ni upi? (jino)
Mnyambuliko wa vitenzi: Kauli ya kutendana na kutendesha
1. Kauli ya kutendana: Kitendo kile kile hufanywa na watu wawili. Mmoja naamfanyia
mwenzake kitendo fulani, naye huyo aliyefanyiwa na anamwendea mwenzake kitendo
hicho hicho. Kimsingi, kitendo kinachofanywa kinawaathiri wote wawili (au zaidi kama
ni watu wengi). Kiambishi kinachoonyesha kauli hii ni {-an-}. Mifano:
piga pigana
pika pikiana
suka sukana
soma someana
penda pendana
2. Kauli ya kutendesha: Kauli hii huwakilisha dhana ya kusababisha . Mhusika au wahusika
fulani wanasababisha wahusika au mhusika mwingine kutenda kitendo fulani. Viambishi
vya kawaida vya kauli hii ni: {-ish-}, {-esh-}, {-z-}, {-lish-}, (-lesh} na {-sh-}. Mifano:
choka cho-sh-a
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 182 12/11/2019 09:44
183
jaa ja-z-a
toa to-lesh-a
kimbia kimbi-z-a
toboa tobo-lesh-a
tambua tambu-lish-a
jenga jeng-esh-a
kaa ka-lish-a
zaa za-lish-a
lima lim-ish.a
Mzizi Kutendana Kutendesha
pig-
kop-
kos-
wez-
chor-
pit-
ju-
pig-an-a
kop-an-a
kos-an-a
wez-an-a
chor-an-a
pit-an-a
ju-an-a
pig-ish-a
kop-esh-a
kos-esh-a
wez-esh-a
chor-esh-a
pit-ish-a
ju-lish-a
Zoezi
1. Kamilisha jedwali lifuatalo
kutenda kutendana kutendesha
piga
sema
somesha
katana
n g ’o a n a
chora
andikisha
kaa
achana
chimbisha
chota
2. Tumia kitenzi katika kauli iliyoko mabanoni kukamilisha sentensi;
kwa mfano: Mama alim _________ binamu nyumbani kwao. (rudi, tendesha)
Mama alimrudisha binamu nyumbani kwao.
(a) Wachezaji wali______________ uwanjani. (piga, tendana)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 183 12/11/2019 09:44
184
(b) Mwalimu atawa_____________ wanafunzi. (soma, tendesha)
(ch) Nyanya alini_____________ shilingi mia moja. (kopa, tendesha)
(d) Waziri ana______________ katika nyumba ile. (kaa, tenda)
(e) Wazee wali__________________ uwanjani. (jadili, tendana)
(f) Mwalimu mkuu ali _____________ pesa nyingi. (changa, tendesha)
(g) Watoto wali_____________ kazi kwa bidii. (fanya, tenda)
(h) Watu wengi siku hizi wana _________ maisha ya starehe. (penda, tenda)
(i) Mama atam______________ mtoto nguo. (vaa, tendesha)
D. Kuandika
Imla
Imla ni neno linalotumiwa kuelezea hali ambapo mtu anasema au kusoma maneno au kifungu
cha maneno na msikilizaji kuandika. Kwa mfano, mwalimu anaweza kusoma hoja zake kuhusu
suala fulani na wanafunzi kuandika. Kuna mambo kadha ya kuzingatia ili kuweza kuandika
taarifa nzuri.
Kusikiliza kwa makini.
Kuandika maneno au kifungu kilichosomwa kama kilivyo.
Kuhakikisha kuwa hati yako inasomeka vizuri.
Kujitahidi kutobadilisha sehemu yoyote ya kifungu kilichosomwa au hoja zilizotolewa.
Hakikisha kuwa maandishi yako yanaonyesha mpatano au mshikamano fulani.
Unachoandika lazima kionyeshe kushikamana.
Zoezi
Sikiliza taarifa atakayoisoma mwalimu wako kwa mara ya kwanza. Akiisoma mara ya pili, jitahidi
kuandika unayoyasikia.
Utungaji wa kiuamilifu: Kujaza fomu
Fomu ni karatasi yenye maswali fulani ambayo hujazwa ili kutoa habari fulani kuhusu mtu au
kitu fulani. Habari zinazotolewa huwa muhimu ili kumwezesha anayezitaka kufanya uamuzi
ufaao. Pana umuhimu wa kuzijua mbinu za kuijaza fomu ili kuhakikisha kuwa unajaza ipasavyo.
Taarifa zinazotakiwa katika fomu huweza kuhusu maisha ya anayeijaza fomu hiyo kama vile:
mwaka wa kuzaliwa, elimu yake, afya yake n.k. Fomu hutofautiana kutegemea malengo yake;
lakini kuna maswali ya kimsingi ambayo hupatikana katika fomu nyingi.
Mambo ya kuzingatia:
Kwanza ipitie fomu ili uielewe vizuri.
Tambua ni taarifa zipi zinazotakikana.
Hakikisha umejaza kila kitu kinachotakiwa na kwa namna inavyotakiwa.
Tumia hati inayoweza kusomeka; aghalabu fomu nyingi huhitaji kujazwa kwa hati kubwa
iliyo wazi.
Usitoe taarifa ambazo si za kweli au kuandika mambo ambayo hukuulizwa.
Mara nyingi kinachohitajika ni majibu kwa maneno machache. Lakini pale panapohitajika
maelezo zaidi yatolewe kwa njia nzuri.
Baada ya kujaza fomu hakikisha kuwa umeipitia upya kuhakikisha kuwa hukuacha taarifa
muhimu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 184 12/11/2019 09:44
185
Zoezi la kwanza
Jaza fomu ifuatayo kwa usahihi
Fomu ya Usajili
Taarifa za kibinafsi
Majina: Jina la mwisho/ukoo/familia _________________________________
Jina la kati________________________________________________
Majina ya kwanza__________________________________________
Jinsia ___________________________________________________________________
Tarehe ya kuzaliwa ________________________________ Umri ________________
Tarafa___________________________________________ Wilaya _______________
Jina la mzazi/mlezi ________________________________ Anwani ______________
Jina la mama ______________________ Kazi _____________ Anwani______________
Jina la baba _______________________ Kazi _____________ Anwani______________
Ni nani anayelipa karo yako _________________________________________________
Shule ya mwisho kuhudhuria ________________________________________________
Hitimu za kielimu
Matokeo ya jumla _________________________________________________________
Gredi mbalimbali _________________________________________________________
Mwaka__________________________________________________________________
Masuala ya afya
Je una ulemavu wa kimaumbile?______________________________________________
Ikiwa ndiyo eleza__________________________________________________________
Una tatizo la kiafya ______________________ ikiwa ndivyo eleza __________________
Mzio (wa chakula)_________________________________________________________
Ugonjwa sugu ____________________________________________________________
Uoni ___________________________________________________________________
Usikivu _________________________________________________________________
Masuala mengine _________________________________________________________
Michezo
Je, unashiriki katika michezo?____________________ ikiwa ndivyo itaje_____________
Ikiwa la eleza kwa nini _____________________________________________________
Sahihi
Mama/baba/mlezi _____________________________ Tarehe _____________________
Mwanafunzi _________________________________ Tarehe _____________________
Msamiati
Mzio: Hali ya kudhuriwa na aina fulani za chakula au kitu kingine kama vumbi, mbelewele n.k.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 185 12/11/2019 09:44
186
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1
2 3
4
5
6 7 9 8
19
10 11 12
13 14 15
16
17
18
KULIA
2. Maneno yanayotumiwa kwa muda fulani kisha yakatoweka
4. Aliyekuzaa
5. Mwanadamu wa kike
6. Mwizi
9. Mtu anayependa kuchomolea watu mali yao mifukoni
12. Tunu
13. Wafanyakazi wa nyumbani
14. Jipamba au jiremba
16. Aliyekupa kazi
17. Mtu ambaye huchukua mizigo kwa mkokoteni au mwili kwa malipo
18. Yasiyo ya kweli
CHINI
1. Kazi ya mjakazi
3. Fungu la maneno lenye maana ya kipekee, mfano, tia chumvi
4. Shida au matatizo
7. Uongo
8. Kuteua
19. Aliyeajiriwa
10. Bila kucha
15. Kupata kazi ya kufanya
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 186 12/11/2019 09:44
187
Sura ya Kumi na Nane
A. Ufahamu
Runinga ya Mizengwe
Mtaa wa Twaweza ulisiwa ghaya katika jiji la Ngoa. Mtaa huu ulikuwa kwenye upande wa uchejua
wa jiji hilo. Sehemu hizo za mashariki ndizo zilizohodhi mitaa mikubwa walikoishi maskini.
Wengi wao walikuwa vibarua na wafanya kazi katika viwanda vilivyokuwa karibu na mtaa huo.
Licha ya umaskini wao, wakazi wa mtaa wa Twaweza waliishi kwa masikilizano na mapenzi
makubwa. Walijuliana hali na kuingiliana kwa udugu mkubwa. Wakati wa shida walisaidiana
na kutiliana jeki bila ya wivu wala gere.
Siku moja alihamia hapo jamaa mmoja ambaye hakuna aliyelifahamu jina lake. Jamaa huyo
aliingia kwenye nyumba iliyokuwa pembezoni mwa mtaa huo. Alika pamoja na mkewe na
mtoto wao mdogo wa kike wa umri wa takriban miaka saba hivi. Hakuna aliyejua alikotoka au
alikofanya kazi jamaa huyo. Hata mkewe hakufahamika vyema. Tangu wahamie pale, mkewe na
yule msichana mdogo hawakutoka nyumbani. Jamaa mwenyewe ndiye aliyeonekana akitoka kila
alfajiri na kutokomea. Hamna aliyejua alikoelekea. Alirejea jioni mwendo wa saa mbili usiku.
Watu walipomsemesha alijibu kwa maneno machache na kushika hamsini zake. “Huyu jamaa
namna gani?” wakazi wa Twaweza waliulizana.
Kuna sifa nyingine ya kushangaza kumhusu jamaa huyo. Kila wakati alipokuwa nyumbani
ilisikika sauti ya juu kama ya muziki. Sauti hiyo ilichanganyika na zingine kama za watu labda
wanaoimba. Wakazi wa mtaa wa Twaweza waliendelea kushangaa. Hawakujua kilichokuwa
kikiendelea pale, na kama tujuavyo jambo usilolijua ni usiku wa kiza.
Mwezi mmoja baada ya yule jamaa, ambaye sasa wanamtaa walimbatiza Mizengwe kuhamia
Twaweza, mkewe aliondoka. Aliondoka siku moja alfajiri na mapema. Vibarua waliokuwa
wamerauka kwenda kazini mapema ndio waliomwona. Walishangaa ni kitu gani kilichomfanya
arauke jinsi hiyo. Naye kama kawaida yake, Mizengwe aliendelea kuondoka nyumbani asubuhi na
kurudi usiku. Yule msichana mdogo hakuonekana akitoka nyumbani siku zote hizo. Wanamtaa
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 187 12/11/2019 09:44
188
walishangaa msichana yule alikuwa akifanya nini mchana kutwa ndani ya nyumba peke yake.
Siku moja yule msichana mdogo alifanikiwa kuchopoka na kutoka nyumbani alikokuwa
amefungiwa. Alikimbia kwa jirani aliyekuwa karibu. Mama nisaidie, nina njaa. Sijala kitu kwa
siku tatu!” alisema msichana huyo. Mwili wake ulionekana dhaifu kweli. Alikuwa amekonda
kama unyasi kutokana na njaa. Tena alikuwa na vidonda mwilini kote.
Yule jirani alimpakulia chakula alichokuwa nacho na kumkabidhi. Msichana huyo alikula
haraka haraka na kwa hamu kubwa hadi akashiba. Alikula chakula kinachofaa kuliwa na watu
wawili wazima. Kisha akasema kwa sauti ya chini, Asante mama, Mungu atakubariki. Baada
ya kuona ameshiba, yule jirani alimwuliza, Je, unaitwa nani?” “Jamila, alijibu kwa neno moja.
“Je, mamako yuko wapi? Jamila alimwangalia jirani kwa muda kabla ya kusema, Ameondoka!”
Baada ya kusema hayo, yule msichana akaanza kutazama huku na huko kwa woga kama mtu
aliyekumbuka kitu fulani, kisha akachopoka mbio na kurudi nyumbani.
Jioni hiyo Mizengwe alirudi kama kawaida. Alipoingia tu alitambua kuwa binti yake
alikuwa ametoka pale nyumbani. Kwa nini uliondoka nyumbani?” aliuliza kwa sauti ya juu.
“Baba nilikuwa na njaa!” alijitetea Jamila. Aliposikia hivyo, Mizengwe alikuja juu. Hakutaka
kusikiliza sababu zozote. Akachukua mshipi na kuanza kumcharaza na kumpapura binti yake.
Jamila alipiga usiahi mkali. Lakini sauti yake haikusikika huko nje kwa sababu ya sauti nyingine
zilizochanganyika na ile ya mtoto.
Mizengwe aliendelea kumcharaza mwanawe bila ya huruma, ungedhani anapiga ngoma.
Wakati huu yule mwanamke aliyempakulia Jamila chakula alikuwa amewaeleza wanamtaa
kile kisa. Ilikuwa wazi kuwa Mizengwe alikuwa akimtesa mwanawe. Waliamua kuelekea huko
labda watapata ithibati ya kutosha. Walipokaribia ile nyumba, wakasikia sauti za vilio zikitokea
nyumbani mle. Lango la kuingilia nyumba hiyo lilikuwa limefungwa. Wakasimama pale kwa
muda kabla ya kubisha kwa nguvu. Walibisha mpaka Mizengwe akasikia. Alitoka kwa hasira
kama mbogo na kuja langoni.
Mnataka nini? aliuliza kwa hasira kubwa.
“Kuna nini huko?” waliuliza.
“Kwa nini? Mmesikia nini kwani?” aliuliza.
Sauti ya juu ..., walimjibu.
“Ile...ee… ile ile ni runinga yangu. Mimi nina shida ya masikio lazima sauti iwe juu,
alisema Mizengwe. Watu waliridhika na kurudi lakini shingo upande. Mizengwe naye alirudi
chumbani na kufunga mlango ndi kwa hasira.
Lakini mara ile sauti ilianza tena. Sasa ilipanda juu zaidi. Wanamtaa waliamua kurudi.
Wakabisha tena kwa nguvu. Mara hii Mizengwe hakufungua. Wote kwa pamoja wakaupiga
ule mlango vikumbo wakaingia ndani. Watu husema wengi wape usipowapa watachukua kwa
mikono yao. Walielekea moja kwa moja mpaka chumbani.
Walipoingia ndani walipigwa na butwaa. Jamila alikuwa amekaa pale chini akilia kwa uchungu.
Hawakuona runinga yoyote isipokuwa kinanda cha santuri kilichokuwa na vifaa vya kupaazia
sauti ungedhani ni ukumbi wa kuchezea densi. Walikizima kile kinanda mara moja bila kuuliza
mwenyewe ruhusa. Uso na mwili mzima wa Jamila ulikuwa umeenea damu. “Wewe ni baba
wa aina gani? Hii ndiyo runinga? Binti yako ndiye runinga? Unajua uchungu wa uzazi wewe?”
waliuliza kwa uchungu uliochanganyika na hasira kubwa.
Baadhi ya wanamtaa walimchukua Jamila na kumpeleka katika kituo cha afya kilichokuwa
karibu ili apate huduma ya kwanza. Wengine walielekea kituo cha polisi kupiga ripoti. Mizengwe
alichukuliwa siku hiyo hiyo na kutiwa ndani akisubiri kukishwa mahakamani kwa kosa la
kumtesa mtoto. Baadaye ilifahamika kuwa mkewe alitoroka alfajiri ile kutokana na dhuluma
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 188 12/11/2019 09:44
189
alizokuwa akitendewa na mumewe. Mara nyingi yeye na mwanawe walishinda na kulala njaa
pamoja na mateso mengine ya kila aina.
Baada ya siku kadha, Jamila alijiunga na mamake mzazi na kuanza masomo yake yaliyokuwa
yamekatizwa na babake. Maisha yao yalibadilika kabisa. Mizengwe aliishia kufungwa kifungo
cha miaka mitano gerezani kilichoandamana na adhabu kali ya viboko na kazi ya sulubu.
Maswali
1. Toa sifa tatu za wakazi wa mtaa wa Twaweza.
2. Ni kwa nini wanamtaa walishangazwa na mienendo ya familia ya Mizengwe?
3. Unakiri ni kwa nini Mizengwe hakupenda kuongea sana na wakazi wa Twaweza?
4. Baada ya mamake kuondoka, taja matatizo matatu ambayo yalimkumba Jamila.
5. Unakiri ni kwa nini Mizengwe alikuwa akicheza kinanda chake kwa sauti ya juu?
6. Methali, ‘wengi wape na usipowapa watachukua kwa mikono yao inahusianaje na kisa
hiki?
7. Je, adhabu aliyoipata Mizengwe inatufunza nini kuhusu haki za watoto na za kibinadamu
kwa jumla?
8. Tumia misemo ifuatayo katika sentensi ili kuonyesha maana zake:
(a) tiliana jeki (b) shika hamsini (ch) pigwa na butwaa (d) angua kilio
(e) shingo upande (f) piga usiahi
9. Je, ni haki mume kumwadhibu mkewe? Elezea.
10. Eleza maana za maneno haya kama yalivyotumika kwenye kifungu:
(a) uchejua (b) chopoka (ch) gere (d) pembezoni
(e) rauka (f) parura (g) ithibati (h) dhuluma
11. Waeleze wenzako kisa kinachoonyesha ukweli kuwa ‘kitu usichokijua ni usiku wa kiza.
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi simulizi
Ushairi
Ushairi ni neno linalotumiwa kuelezea sanaa inayotambulishwa na muundo na mpangilio maalum
wa sentensi au vifungu, silabi na maneno. Ushairi ni kipera kimojawapo cha fasihi simulizi.
Ushairi wa fasihi simulizi unatofautina na ulioandikwa kwa sababu kadha.
Kwanza, huu unawasilishwa mbele ya wasikilizaji au hadhira fulani.
Pili, tofauti na mashairi ya kuandika, ushairi wa fasihi simulizi unategemea sauti; yaani
unaimbwa au kughaniwa kwa sauti.
Ushairi huu unaweza pia kuambatana na ngoma, kupigwa kwa mikono au ala nyinginezo.
Kwa mfano, mashairi yanayoimbwa huweza kuambatana na vyombo vya kila aina kama dla n.k.
Ushairi wa fasihi simulizi unahusisha makundi yafuatayo:
(a) Nyimbo
(b) Mashairi ya kujibizana au ngonjera
(ch) Shairi
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 189 12/11/2019 09:45
190
CH. Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Kirejeshi amba-
Tazama jedwali hili:
Ngeli Nomino
Kirejeshi
Ma
tumizi
amba-’
i
zi
tembe
tembe
ambayo
ambazo
Tembe ambayo inamezwa ni chungu.
Tembe ambazo zinamezwa ni chungu.
i
i
teknolojia
teknolojia
ambayo
ambazo
Teknolojia ambayo inatumika itasaidia.
Teknolojia ambayo inatumika itasaidia.
u
zi
utambi
tambi
ambao
ambazo
Utambi ambao unauzwa ni mzuri.
Tambi ambazo zinauzwa ni nzuri.
u
u
usingizi
usingizi
ambao
ambao
Usingizi ambao ulilala ni mnono.
Usingizi ambao ulilala ni mnono.
ku
ku
kuroga kuroga ambako
ambako
Kuroga ambako kulirogwa ni kupi? Kuroga
ambako kulirogwa ni kupi?
pa
ku mu
mahali mahali
mahali
ambapo
ambako
ambamo
Mahali ambapo pamejaa ni hapa. Mahali
ambako kumejaa ni huku. Mahali ambamo
mmejaa ni humu.
Zoezi
1. Andika sentensi zifuatazo kwa wingi:
(a) Nyumba ambayo inajengwa ni ya mpwa wangu.
(b) Mahali ambapo pamechafuka patapigwa deki.
(ch) Uchoyo ambao unaonyeshwa ni wa ajabu.
(d) Uto ambao ulivunjika uliniumiza.
(e) Sahani ambayo ililetwa ni mbaya.
(f) Uwezo ambao anao ni mwingi.
(g) Kukimbia ambako alikimbia kulimwokoa.
(h) Mahali ambamo mmefagiliwa mmechafuka tena.
(i) Mvua ambayo ilinyesha iliharibu mimea.
(j) Unywele ambao umekatika ni huu.
2. Tumia kirejeshi amba-’ kwa njia sahihi kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) Nyumba _________ ilianguka imejengwa upya.
Nyumba _________ zilianguka zimejengwa upya.
(b) Mahali _________ pamefunguliwa pameingia wezi.
Mahali _________ pamefunguliwa pameingia wezi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 190 12/11/2019 09:45
191
(ch) Kushiriki _________ ulishiriki kulikusaidia sana.
Kushiriki _________ ulishiriki kulikusaidia sana.
(d) Chai _________ unakunywa imepikwa na Nafula.
Chai _________ unakunywa imepikwa na Nafula
(e) Wimbo __________ utaimbwa utatuliwaza.
Nyimbo _________ zitaimbwa zitatuliwaza.
(f) Kulima __________ unalima hakutafaa bila mvua.
Kulima _________ unalima hakutafaa bila mvua.
(g) Njaa __________ inatuumiza itakwisha.
Njaa _________ inatuumiza itakwisha.
(h) Barua __________ iliandikwa itatumwa leo.
Barua _________ ziliandikwa zitatumwa leo.
(i) Mahali __________ kulifungwa kumefunguliwa tena.
Mahali _________ kulifungwa kumefunguliwa tena.
(j) Ushanga __________ umenunuliwa utafaa nini?
Shanga _________ zimenunuliwa zitafaa nini?
3. Sahihisha matumizi ya kirejeshi amba-’ katika sentensi zifuatazo:
(a) Mwalimu ambao alikuja yuko wapi?
Walimu ambaye walikuja wako wapi?
(b) Kikombe ambalo anatumia kinavuja.
Vikombe ambazo anatumia vinavuja.
(ch) Chakula ambalo wanapika ni cha nani?
Vyakula ambao wanapika ni vya nani?
(d) Mkate ambacho ulikula ulinunua wapi?
Mikate ambavyo ulikula ulinunua wapi?
(e) Mahali ambamo kulichafuka ni kwa Mwangangi.
Mahali ambapo mlichafuka ni mwa Mwangangi.
Mahali ambako palichafuka ni pa Mwangangi.
(f) Baiskeli ambao imeanguka ni ya Paulina.
Baiskeli ambavyo zimeanguka ni za Paulina.
D. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Hotuba
Hotuba ni maelezo (yaliyoandikwa au yasiyoandikwa) yanayotolewa mbele ya watu au kundi
fulani. Maelezo haya yana lengo la kuwasilisha taarifa fulani. Maelezo haya hutolewa na mtu
katika wakati uliopo. Hotuba zinaweza kutolewa sehemu mbalimbali kama shuleni wakati wa
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 191 12/11/2019 09:45
192
kukaribishwa kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza au wakati wa mashindano ya michezo, wakati
wa siku ya wazazi, kwenye mikutano ya kisiasa n.k.
Umuhimu wa hotuba
Hotuba huandikwa au kutayarishwa kwa sababu mbalimbali:
1. Kuwapasha watu habari fulani juu ya jambo fulani kwa mfano kuhusu tatizo au ugonjwa
fulani. Kwa mfano madhara ya dawa za kulevya n.k.
2. Kuwashawishi watu wakubali jambo fulani. Kwa mfano, mtu anayetoa hotuba ili kuwafanya
watu wakubaliane na msimamo wake.
Hatua za kuandika hotuba
1. Jiweke katika hali ya mtu mwingine ambaye ndiye anayetoa hotuba.
2. Hakikisha kuwa umetambua watu watakaokusikiliza ni nani, yaani hadhira yako ni nani.
3. Hadhira yako ndiyo itakayokufanya uteue lugha ya kutumia. Ikiwa wanaokusikiliza ni
watoto, lazima lugha yako iwe rahisi.
4. Unapoanza hotuba yako unaanza kwa salamu. Unaweza kuwataja watu mashuhuri waliopo
hapo.
5. Hakikisha unachokizungumzia kinaeleweka waziwazi.
6. Hotuba yako iwe na mpangilio mzuri; yaani mawazo yako yatiririke vyema; kuanzia
mwanzo mpaka mwisho.
7. Panga mawazo yako vizuri ili hotuba yako ivutie; pia tumia lugha inayowavutia wasikilizaji
wako.
8. Maliza hotuba kwa njia ya kuwavutia wasikilizaji au kuwapa mawaidha ya jinsi ya
kupambana na tatizo fulani walilo nalo.
Zoezi
Umealikwa kama mgeni wa heshima siku ya upandaji miti huko kijijini kwenu. Andika hotuba
kuhusu umuhimu wa kuitunza miti.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 192 12/11/2019 09:45
193
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3
4 5
6
7
8
9
10
11 12 13
14 15 16
17
18 19
20
KULIA
3. Mwanzo wa kufanya kitu
4. Majonzi
7. Hupatikana kwenye shairi
9. Huwa na mishororo, vina na kibwagizo
11. Hutufunza
13. Msukumo
14. Walioajiriwa
16. Chapisho ambalo hutolewa baada ya muda fulani
17. Tunu
18. Tumbuizo
19. Uvunjaji sheria au kanuni
20. Tamko
CHINI
1. Moja kati ya stadi za lugha
2. Dawa za kulevya
5. Kikundi cha watu wa rika moja
6. Mstari katika shairi
8. Bila ya kuona haya
10. Aina ya neno
12. Heshima
15. Kazi
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 193 12/11/2019 09:45
194
Sura ya Kumi na Tisa
A. Ufahamu
Polisi na dhima yao
Sote tulikuwa tumeketi chumbani ndugu alipojitoma ndani ghaa bin vuu huku akihemahema.
“Kuna nini? Mbona umehamanika hivi kama mtu aliyekuwa akikimbizwa, nilimwuliza.
“Wameninyanganya kila kitu, alijibu kwa shida. Kabla hatujamwuliza swali jingine, aliendelea,
nimewaendea polisi huko mjini kuwataka msaada baada ya mkoba wangu kubwakurwa na
wezi, alipumua. Sote tuliendelea kumsikiliza, naye akaendelea, sasa wao badala ya kunisaidia
wameishia kuninyanganya kichache nilichokuwa nimebakia nacho! Nimeshindwa hata kuelewa
tofauti ya watu hawa na hao wezi ikiwa hali ni kama hii, alimalizia ndugu.
Yale maneno ya ndugu yangu yalinichochea kujiuliza maswali kuhusiana na dhima ya polisi
katika jamii zetu. Je, polisi wana dhima gani?
Nilijua kuwa jamii zote ulimwenguni huwa na kanuni na sheria zinazokusudiwa kuzilinda na
kuzihifadhi haki za raia. Katika jamii chache sana, sheria hizi huweza kudhibitiwa na kutekelezwa
na wanajamii wenyewe ambao wanahakikisha kuwa hakuna mtu atakayezivunja au kuzikiuka.
Hata hivyo, katika jamii nyingi za ulimwenguni, jukumu la kuhakikisha kuwa sheria na kanuni
hizo zimefuatwa na kutekelezwa ni la polisi. Polisi wana majukumu mengine mengi fauka ya
jukumu hilo la kimsingi. Huwafuata na kuwabamba wahalifu wanaowasumbua raia, kama
wale waliomwibia ndugu yangu mkoba wake. Aidha polisi huwaandama waendeshaji magari
wanaozikiuka sheria za barabarani na hushika doria katika mitaa na barabara zisizokuwa na
usalama.
Polisi wengine hufanya kazi ofisini, ambako wanachunguza na kutathmini vidokezo
vinavyowasaidia kufumbua tatizo fulani au kukomesha uhalifu. Kwa kawaida, polisi huwashika na
kuwatia pingu wahalifu au watuhumiwa. Baadaye huwashtaki watuhumiwa hao mahakamani ili
waadhibiwe kwa mujibu wa sheria zilizopo. Kazi ya kuchunguza kama pana ushahidi wa kutosha
dhidi ya mtuhumiwa ni ya mahakama. Polisi wazuri huhakikisha kuwa sheria zilizopo zimefuatwa
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 194 12/11/2019 09:45
195
na kutekelezwa vyema. Hawawatii mbaroni wahalifu kwa misingi ya uhalifu wa kudhania tu.
Huhusiana vyema na raia ambao zaidi ya kuwalinda, pia hushirikiana nao kuuangamiza uhalifu.
Kuna aina kadha za polisi kutegemea kazi wanayoifanya. Kwa mfano, kuna makachero au
askari kanzu ambao hawavai mavazi rasmi. Hawa wamefundishwa jinsi ya kufanya uchunguzi
hasa kuhusiana na uhalifu au jinai fulani. Uhalifu unapofanyika, mpelelezi au kachero huchunguza
chanzo, misingi na sababu zake. Hufanya hivi kwa kuwahoji watu walioshuhudia au wenye taarifa
fulani. Kuhoji huku lazima kuwe kwa utu wala sio kwa vitisho na mateso. Wapelelezi hufanya hivi
ili kupata ushahidi wa kuweza kumshtaki anayehusika. Aidha, hufanya hivi ili kupata vielekezi
vya kuwajulisha ni nani aliyehusika. Wanapompata na kumkamata anayehusika, wapelelezi
hufanya uchunguzi zaidi unaodhihirisha kuwa anayehusika ana hatia. Baadaye humwasilisha
mahakamani ili akabiliwe na vyombo vya kisheria.
Hali kadhalika kuna polisi wanaovaa mavazi rasmi na ambao hutambulikana waziwazi.
Mifano ya polisi hawa ni wale wa barabarani au wanaoonekana wakipiga doria mijini. Mavazi
haya huwawezesha watu au raia kuwatambua kwa urahisi na hata kuusaka msaada wao pindi
wanapokumbwa na matatizo. Wapo pia polisi wa kuzima ghasia. Hawa hutumiwa kwa minajili
ya kuzuia fujo. Fujo zinapoenea, huweza kusababisha madhara makubwa kama wizi, uporaji wa
mali na madhara mengine chungu nzima. Kazi ya kimsingi ya polisi wa aina hii ni kukomesha
ghasia au fujo na kuwashika wanaoziongoza na kwa njia hii kudumisha amani.
Polisi wana jukumu muhimu katika jamii, lakini hawawezi kufanikiwa bila ya kuwako na
ushirikiano mzuri na raia wenyewe. Jambo kama hili haliwezi kufanikiwa ikiwa raia wenyewe
wanawatuhumu polisi au uhusiano wao na polisi ni mbaya. Pili, haiwezekani kwa raia kuwaamini
polisi hao ikiwa wanapenda kula rushwa ili kufanya kazi fulani. Nakumbuka malalamiko
tuliyokuwa nayo kijijini siku moja baada ya mwizi aliyewasumbua watu kushikwa na kukabidhiwa
polisi lakini akaachiliwa bila kuchukuliwa hatua yoyote. Watu walidai kuwa aliwahonga wakuu
wa kituo cha polisi ili aachiliwe.
Haikuwa vigumu kutambua chimbuko la hasira ya ndugu yangu baada ya kukumbana na polisi
hao. Pana umuhimu mkubwa wa kuuboresha uhusiano wa kuaminiana kati ya raia na polisi. Ni
muhali kwa polisi kuumaliza uhalifu pekee; lazima pawepo na kutegemeana kukubwa na raia
wenyewe. Kutegemeana huko hakuwezi kuwako ikiwa hakuna kuaminiana katika mahusiano
yao. Ndiyo sote tunahitaji kujirekebisha; tuache kutoa rushwa, nao wenyewe waache kuzipokea
hongo ili pande zote zishirikiane kupambana na uhalifu. Kwa njia hii tutajenga jamii yenye
ushirikiano mzuri kati ya wanajamii tofauti pamoja na kuudhibiti uhalifu.
Sio polisi wote wabaya; lakini pana umuhimu wa hao waovu wachache kuondolewa kwa
kuwa nazi mbovu ni harabu ya nzima, nilimwambia ndugu hatimaye.
Maelezo ya msamiati
alipojitoma : alipoingia ghaa.
umehamanika : umekuwa na wasiwasi; umehangaika.
dhima : jukumu; wajibu.
fauka ya : zaidi ya.
Maswali
1. Taja wajibu mbalimbali wa polisi kulingana na kifungu hiki.
2. Taja aina tatu za polisi waliotajwa kwenye kifungu hiki.
3. Ni nini wajibu wa kikosi cha polisi wa kuzuia ghasia?
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 195 12/11/2019 09:45
196
4. Ni nini wajibu wa askari kanzu?
5. Tumia misemo ifuatayo katika sentensi:
(a) ghaa bin vuu
(b) shika doria
(ch) tia pingu
(d) pora mali
(e) tia kifungoni
(f) toa rushwa
6. Methali nazi mbovu ni harabu ya nzima inahusianaje na mienendo au uwajibikaji wa
polisi?
7. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika kifungu kisha uyatumie katika
sentensi:
(i) bwakura
(ii) haki za raia
(iii) bamba
(iv) makachero
(v) jinai
(vi) fujo
(vii) jukumu
(viii) hoji
(ix) honga
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi simulizi
Tanzu za Ushairi
Nyimbo
Utangulizi
Nyimbo, kama tulivyoona katika sura iliyotangulia, ni sehemu ya ushairi katika fasihi simulizi. Je,
wimbo ni nini? Wimbo ni utungo ambao una mpangilio maalum wa maneno na una mahadhi ya
kupanda na kushuka kwa sauti, yaani sauti yake huenda juu na chini. Nyimbo huweza kuambatana
na ala au vyombo fulani au usiambatane navyo. Nyimbo huweza kuimbwa na mtu mmoja au
watu wengi Kwa mfano: kwaya, bendi, kikundi cha taarabu au kikundi cha ngoma za kienyeji.
Nyimbo huambatana na shughuli mbalimbali kama kufanya kazi, kumlea mtoto, sherehe
za ndoa au harusi, mazishi, siasa n.k.
Umuhimu wa nyimbo
Je, kwa nini watu hupenda kuimba wakati wa shughuli mbalimbali? Je, katika jamii
zetu nyimbo huwa na kazi gani?
Kutumbuiza: Nyimbo huweza kuimbwa kwa ajili ya kutumbuiza watu au kuwafanya
waifurahie hali fulani.
Kuwafariji: Nyimbo zinazoimbwa wakati wa sherehe za mazishi huwafariji waliowa.
Kuwasilisha ujumbe fulani: Watu wanaweza kupitisha ujumbe fulani kwa njia ya kuimba.
Kwa mfano nyimbo za kidini huwa na ujumbe fulani.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 196 12/11/2019 09:45
197
Kuwabembeleza watoto waweze kulala. Kuna nyimbo zinazoimbwa mtoto aliapo ili alale
au aache kulia.
Kuwatia watu moyo wa kufanya jambo fulani; nyimbo zinazoimbwa wakati wa kazi huwatia
watu moyo wa kuifanya kazi fulani.
Nyimbo hutambulishwa na mambo kadha:
(a) Sauti ya mwimbaji au anayeuimba wimbo fulani.
(b) Maneno yaliyoimbwa kuhusu jambo lolote lile.
(ch) Watu wanaoimbiwa au wanaousikiliza wimbo fulani unaoimbwa yaani hadhira.
(d) Muziki wa ala au vyombo ambavyo huandamana na wimbo huo ingawa sio nyimbo zote
ambazo huwa na ala.
(e) Muktadha au msingi wa wimbo huo k.m. sherehe, kazi, ibada, kilio n.k.
Zoezi
a) Je, nyimbo huhusishwa na nini?
b) Kwa nini nyimbo zikawapo?
ch) Taja na ueleze aina zozote tano (5) za nyimbo unazozijua.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -etu, -enu na -ao
Tuliona huko nyuma kuwa mizizi ya vivumishi vimilikishi huweza kuwa katika hali ya umoja au
wingi. Vimilikishi vya umoja ni -angu, -ako na -ake. Vile vya wingi ni -etu, -enu na -ao
Tazama jedwali hili:
Ngeli Nomino
Vimilikishi
Matumizi
-etu -enu
-ao
a
wa
ba
ta
ba
ta
wetu
wetu
wenu
wenu
wao
wao
Bata wao amepotea.
Bata wao
wamepotea.
u
i
mwiko
miko
wetu
yetu
wenu
yenu
wao
yao
Mwiko wetu ulivunjika.
Miko yetu ilivunjika.
u
ya
ulezi
malezi
wetu
yetu
wenu
yenu
wao
yao
Ulezi wenu haufai. Malezi
yenu hayafai.
ya
ya
manukato
manukato
yetu
yetu
yenu
yenu
yao
yao
Manukato yenu yatakwisha.
Manukato yenu yatakwisha.
li
ya
yai
mayai
l
etu
yetu
l
enu
yenu
l
ao
yao
Ya i letu linaliwa.
Mayai yetu
yanaliwa.
ki
vi
kitanda
vitanda
chetu
vyetu
chenu
vyenu
chao
vyao
Kitanda chao kina kunguni.
Vitanda vyao vina kunguni.
1. Tumia nomino mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) ________ chenu kiko wapi?
(b) ________ yenu yamekwisha.
(ch) ________ yao ni mengi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 197 12/11/2019 09:45
198
(d) ________ wetu amepotea.
(e) ________ letu liko wapi?
(f) ________ vyao vilipotea.
(g) ________ wenu analala.
(h) ________ wetu uko wapi?
2. Tumia kimilikishi kilicho kwenye mabano kukamilisha sentensi zifuatazo:
(a) Kiazi ______ kimeoza. (-etu)
Viazi _______ vimeoza. (-ao)
(b) Ugonjwa ______ umepona. (-enu)
Magonjwa ______ yamepona. (-ao)
(ch) Msumari ______ uko wapi? (-etu)
Misumari ______ iko wapi? (-etu)
(d) Farasi _______ ameshinda. (-enu)
Farasi _______ wameshinda. (-ao)
(e) Madhumuni _____ yametimia. (-enu)
Madhumuni _____ yametimia. (-etu)
3. Sahihisha vimilikishi katika sentensi zifuatazo:
(a) Ng’ombe chao amekufa.
(b) Kijiji lake kimechomeka.
(ch) Wazee zenu wako wapi?
(d) Kitoweo lake kimemwagika.
(e) Chungwa chako kimeanguka.
(f) Kiatu yako iko wapi?
(g) Pikipiki wake imeibiwa.
(h) Jembe yako limeazimwa na Mwikali.
(i) Ndoo chake imejaa maziwa.
(j) Mwiko vyake uko kwenye kabati.
Kuakisha
Nukta za dukuduku (...)
Hizi ni alama za nukta zinazoandikwa zikiwa tatu mfululizo. Hutumiwa katika mazingira
mbalimbali ya kimaandishi kama yafuatayo:
1. Kuonyesha kuwa maelezo au maneno yaliyoandikwa yanaendelea ingawa hayajaandikwa;
kwa mfano:
(a) Rais alisema, “Siku hizi kuna watu ambao
(b) Nataka uniletee kitabu, kalamu, wembe…
(ch) Mama aliniuliza, Mariamu, kwa nini…
2. Kuonyesha kuwa maneno yanatanguliwa na mengine ambayo hayajaandikwa; kwa mfano:
(a) …hata ingawa sikujua ataka siku hiyo.
(b) …yaani ni kama vile tu nilivyosema hapo jana.
(ch) …ni mambo muhimu sana katika kujifunza lugha.
3. Kuonyesha kuwa kuna maneno yaliyoachwa katikati ya sentensi; kwa mfano:
(a) Rais alisema, “Mimi ningetaka kuona... kwa hivyo mkiona watu mnaowashuku
mpige ripoti polisi mara moja.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 198 12/11/2019 09:45
199
(b) Kila mwanafunzi anapaswa kuja na… asanteni.
4. Kuonyesha kukatizwa usemi; k.m.
 : Kwa nini hukuja shuleni jana?
 : Mwalimu, jana nilikuwa...
 : Unataka kusema ulikuwa mgonjwa kama kawaida!
 : Siyo hivyo mwalimu lakini...
 : Lakini nini?
5. Kutotaja maneno ambayo yana lugha mbaya, makali au yanayoonyesha utovu wa heshima.
Sentensi ya Kiswahili
Katika mawasiliano ya kila siku, binadamu hutumia maneno. Maneno haya hayatumiki peke
yake. Inabidi yapangwe katika mpangilio maalum ili yaweze kuleta maana. Mpangilio huu wa
maneno kwa kawaida huitwa sentensi.
Sentensi ni nini?
Sentensi ni neno au fungu la maneno lililokamilika kimaana na kisaru. Kwa hivyo kila sentensi
ni lazima ijitegemee kimaana na kisaru. Tazama vifungu hivi vya maneno:
(a) Mwalimu wetu.
(b) Mtu anayekuja.
(ch) Mwizi hatari.
Maneno haya yana maana kimsamiati, yaani tunajua maana ya kila neno lililotumika. Kwa mfano:
tunajua maana ya neno mwalimu au wetu au mwizi au “hatari” n.k. Lakini tukiyaangalia
maneno hayo kwa vifungu kama vile mwalimu wetu au mtu anayekuja au mwizi hatari”
hatupati maana kamili. Yaani hizi si sentensi kwa vile hazijitegemei ingawa kisaru vifungu
hivyo ni sahihi. Ukimwambia mtu mwalimu wetu”, atakuuliza. “Mwalimu wenu amefanyaje?
Ukimwambia mtu anayekuja, atakuuliza. Mtu anayekuja ana nini?” au ukimwambia “Mwizi
hatari” atakuuliza Mwizi hatari yuko wapi?” au maswali mengine kama hayo. Sababu ni kuwa
vifungu hivi vya maneno havijakamilika kimaana. Inabidi viongezwe maneno mengine ili
vikamilike kimaana, yaani ili viwe sentensi kamili; kwa mfano:
(a) Mwalimu wetu anatupenda.
(b) Mtu anayekuja ni raki yangu.
(ch) Mwizi hatari aliuawa jana.
Bila shaka mafungu haya ya maneno sasa yanaleta ujumbe kamili. Ni mifano ya sentensi kamili.
Sentensi huweza kutokea kwa njia mbalimbali. Huweza kutokea kama:
1. Taarifa
Hii ni sentensi inayotoa taarifa ya moja kwa moja na huwa haihitaji jawabu; kwa mfano:
(a) Nungunungu amejicha pangoni.
(b) Kondoo na mbuzi watachinjwa kesho.
(ch) Watoto wa shule hii wana nidhamu sana.
(d) Jana tulikwenda sokoni kununua samaki.
(e) Tunafaa kuhifadhi mazingira yetu.
Sentensi ya aina hii huanza kwa heru kubwa na kuishia kwa kikomo. (au nukta)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 199 12/11/2019 09:45
200
2. Swali
Hizi ni sentensi zinazouliza maswali kuhusu jambo fulani; kwa mfano:
(a) Mama anapika nini leo?
(b) Kwa nini polisi hawakumsaidia kakangu?
(ch) Wamepita wanafunzi wangapi?
(d) Kwa nini unatumia dawa za kulevya?
(e) Kwa nini nyinyi hamtaki kujiepusha na Ukimwi?
(f) Kwa nini makachero hawakufanya upelelezi?
Sentensi za aina hii huanza kwa heru kubwa na kuishia kwa kiulizo.
3. Amri
Hizi ni sentensi zinazotoa amri au zinazoamrisha; kwa mfano:
(a) Tokomea mbali!
(b) Njoo hapa mara moja!
(ch) Funga mlango!
(d) Nenda shuleni!
(e) Fuata sheria!
Sentensi hizi huanza kwa heru kubwa na kuishia kwa nukta (kikomo). Hata hivyo
ikiwa amri inayotolewa ni fupi na yenye ukali zaidi inabidi iishie kwa alama ya hisi (!)
4. Ombi; kwa mfano:
Hizi ni sentensi zinazotoa ombi au rai; kwa mfano:
(a) Nifungulie mlango raki yangu.
(b) Nisaidie ndugu yangu.
(ch) Nenda ukanichotee maji tafadhali.
Sentensi aina hii huanzia kwa heru kubwa na kuishia kwa kitone.
5. Mshangao
Sentensi hizi huonyesha hisia mbalimbali kutokana na huzuni, kustaajabu, kufurahi n.k.
Kwa mfano:
(a) Salaala! Watu wote wameangamia!
(b) Jamani, wezi wanavunja nyumba ya Rehema!
(ch) Kumbe! Sikujua wewe ni mtu mbaya hivyo!
Sentensi ya mshangao huanza kwa heru kubwa na kuishia alama ya hisi.
D. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Maagizo/maelekezo
Kuagiza ni kumtaka mtu afanye jambo fulani; nako kuelekeza ni kuonyesha njia kwa michoro
au maandishi. Basi maagizo au maelekezo ni maelezo yanayomwongoza na kumpa mtu njia ya
kufanya jambo fulani. Bila kuwapo kwa maagizo au maelekezo, hatuwezi kufanya mambo fulani.
Mtu hupewa maelekezo ili kuhakikisha kuwa hayafanyi mambo fulani vibaya au kwa njia
isiyofaa. Kwa mfano wakati wa mtihani, mwanafunzi hupewa maagizo ya kufuata. Maagizo haya
yanamwelekeza kuhusu jinsi ya kujibu maswali, idadi ya maswali ya kujibu, mambo ya kuzingatia
wakati wa mtihani n.k. Ikiwa mwanafunzi atashindwa kuyafuata maagizo aliyopewa, hatafaulu
katika mtihani wake.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 200 12/11/2019 09:45
201
Umuhimu wa maagizo
Kumwongoza mtu kufanya jambo fulani: Maagizo huwa kama kitu cha kumwongoza mtu
anapofanya kazi fulani.
Kuhakikisha kuwa mtu hapotezi wakati: Ikiwa umepewa maagizo, hutapoteza wakati kwa
kufanya mambo yasiyohitajika au ukikiri ufanye nini.
Kumwezesha mtu kuwa na nidhamu fulani: Mtu huwa na nidhamu kwa kufuata maagizo
bila kukosea.
Kuwa na mwelekeo mzuri: Jambo lolote lenye maagizo huwa na mwelekeo mzuri; yaani
linafanyika vyema kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
Kumwepusha mtu na hatari: Maagizo humwezesha mtu kuepukana na hatari fulani. Kwa
mfano maagizo ya barabarani kama ‘USIVUKIE HAPA humsaidia mtembeaji kuepuka
hatari fulani n.k.
Ufuatao ni mfano wa maagizo/maelekezo:
Uokaji wa Biskuti
Unachohitaji
1. Mayai matatu 4. Kikombe kimoja cha sukari
2. Kijiko kimoja cha majarini 5. Kijiko kimoja cha mafuta ya Elianto
3. Kilo moja ya unga wa kuokea 6. Hamira
Uokaji
1. Koroga unga kisha uongeze kilo moja ya sukari. Changanya.
2. Miminia kikombe kimoja cha mafuta ya Elianto kisha ukoroge.
3. Ongeza mayai matatu. Koroga kinyunya hadi kibadilike rangi kuwa manjano.
4. Kata katika vipande mbalimbali kulingana na maumbo unayopenda.
5. Weka kwenye chano yenye shahamu kisha itie kwenye oveni.
6. Oka kwa dakika 20-30 hadi biskuti zibadilike rangi kuwa hudhurungi.
7. Biskuti sasa tayari.
Utungaji wa kiuamilifu: Mahojiano na dayalojia
Dayalojia ni mazungumzo au majibizano baina ya watu wawili au zaidi. Mazungumzo hayo
huweza kuandikwa au kuwasilishwa kwa njia ya maandishi. Siri kubwa ya kuandika mazungumzo
mazuri ni kujifanya mhusika wa mazungumzo yenyewe; yaani jichukulie kama mmoja wa watu
wanaozungumza. Mahojiano ni mazungumzo ambayo huhusisha mtu mmoja kuuliza mwingine
maswali fulani. Anayeuliza maswali ni mhojaji na anayeulizwa ni mhojiwa. Madhumuni ya
kuuliza maswali haya ni kutaka maelezo au taarifa fulani. Kwa kawaida mahojiano huenda karibu
sawa na dayalojia.
Hatua muhimu za kuandika mahojiano
Kukiri kwa makini au kutafakari kuhusu jambo kuu la kuzungumziwa.
Kutayarisha au kuyapanga mawazo yako kwa mantiki, yaani kwa mfufulizo mzuri
unaoyafanya yaeleweka vizuri na kukubalika.
Kuwapanga wahusika kutegemea kazi yao, yaani jinsi wanavyoingiliana katika mazungumzo
yenyewe.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 201 12/11/2019 09:45
202
Vidokezi muhimu
Maelekezo ya kufafanua kama kueleza nani anafanya nini na wapi yaandikwe katika
mabano ili kumwongoza msomaji.
Majina ya wanaosema yawe upande wa kushoto yakifuatiwa na nukta pacha (:)
Alama za mtajo (“ ”) zinazotumiwa katika usemi halisi hazitumiwi katika mazungumzo
lakini alama nyingine za uakishi hutumiwa.
Ni bora kuwa na mazungumzo ya mkato, yaani mzungumzaji mmoja asiyatawale
mazungumzo au dayalojia.
Tumia alama za kuonyesha hisia yaani vihisishi kama: Eboo! Wacha we! Loo! Alaa! Kumbe!
ili kuyatia utamu na uhai mazungumzo na kuyafanya yakaribiane na ukweli.
Mazungumzo yakuze wazo fulani na kwa njia inayoweza kufuatwa na msomaji.
Jitahidi kutumia lugha fasaha na yenye mvuto ili wasomaji wapendezwe na dayalojia yako.
Kumbuka katika maongezi ya kawaida msemaji mmoja anaweza kumkatiza mwingine
anayeongea.
Mfano wa mahojiano
Athari za unywaji pombe
: Daktari ni madhara yapi makuu ya unywaji pombe?
: Kuna mengi.
: Kama yepi?
: Unywaji wa pombe huathiri sehemu ya ubongo inayohusika na maamuzi. Sehemu
hiyo huhusiana na sehemu nyingine za mwili kwa njia ya polepole kuliko ilivyo
kawaida.
: Je, ajali za magari zinazosababishwa na walevi hutokana na hali hii?
: Ndiyo! Mlevi hawezi kuwa na wepesi wa uwazaji na utendaji kama mtu asiye
mlevi.
: Je, kuna madhara mengine?
: Yap o mengine mengi. Kwa mfano, ulevi una athari kubwa kwa ini.
: Ini?
: Ndiyo, pombe huathiri ini kwa kiasi kikubwa. Na ini kama ujuavyo ni kiungo
muhimu, ikiwa kimeathirika matokeo yake ni mabaya. Hiki ni kiungo ambacho
hakiwezi kutibiwa kwa haraka au kupandikizwa kingine kama moyo.
: Ini huathiriwa kwa jinsi gani?
: Huweza kukosa uwezo wa kufanya kazi inavyopasa na hatimaye hata kuishia
kugomea kazi na kusababisha kifo.
: Lo! Kwa hivyo unywaji pombe ni kitu kibaya mno?
: Sio kibaya tu bali ni hatari kwa maisha ya binadamu.
Zoezi
Eleza madhara yanayotokana wa unywaji wa pombe.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 202 12/11/2019 09:45
203
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3 4
5 6
7
8 9 10
11
12
13 14
15
16
17
18
KULIA
4. Waliokuzaa
5. Pahali pa kuthibitisha yaliyopo
8. Ni sawa na tochi
10. Tufaha, maembe, machungwa na papai
11. Kamusi ya lugha mbili
13. Kitabu kinachotoa maana ya maneno
14. Unielezee kisa nami nikueleze kisa
15. Hutumiwa na mtambaji wa hadithi abapoanza kusimulia
16. Rejista
17. Kamusi ya lugha moja
18. Njeo
CHINI
1. Kufanya kuwa na uwezo
2. Aina ya bata
3. Cha kuliwa
6. Hutumika katika Isimujamii
9. Kinyume cha ukanusho
12. Kuwa kwenye jukwaa
13. Kukataa katika sentensi
15 Kiitikio cha hadhira hadithi inapoanza
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 203 12/11/2019 09:45
204
A. Ufahamu
Siri ya jirani
Kwa muda mrefu, sote tulikuwa tukiajabia maendeleo ya jirani yetu. Kwa jina alijulikana kama
Bwa’Koko lakini sote tulimwita Mzee Shabash. Sababu ni kuwa kila ulipokuwa akiongea naye
aliitikia kwa kusema, Shabash!”
Zamani aliishi Mombasa alikofanya biashara, kabla kuamua kurudi kijijini kuanzisha biashara
ya duka hapo karibu na soko. Mwanzo kilikuwa kiduka kidogo tu. Lakini baada ya muda mfupi,
kutokana na bidii zake za mchwa, biashara yake ilichipua haraka kama uyoga. Wafanyabiashara
wengine pale kijijni walijikuta hawana washitiri baada ya wengi wao kuguria kwa Shabash.
Kutokana na uwezo wake wa kifedha, Shabash aliweza kupunguza bei za bidhaa zake mbalimbali
na kwa njia hiyo kuwavuta wanunuzi kama nyuki anavyovutwa na mbelewele ya maua. Wenzake
walianza kulalamika kuwa hakutaka waendelee. Lakini labda kilichowasumbua ni gere au wivu.
Shabash aliipanua biashara yake kwa kuyajenga maduka mengine mawili makubwa. Moja
liliuza vifaa vya ukulima na pembejeo nyingine zinazohusiana na ukulima. Jingine liliuza bidhaa
za kawaida.
Hapo kabla, Shabash hakuhitaji msaidizi katika biashara yake. Lakini baada ya kuipanua
biashara hiyo alilazimika kuandamana na mkewe kila asubuhi kuelekea madukani.
Kadiri miaka ilivyoendelea, ndivyo biashara ya Mzee Shabash ilivyovuta kimo na kujitokeza.
Biashara zake zilianza kuvuta watu kutoka mbali wakasongamana pale kama wadudu penye
nta. Miaka minne baada ya kuanzisha kiduka chake cha kwanza, Shabash alinunua matatu.
Hii ilitumiwa kama gari la usari la pekee kutoka kijijini hadi makao makuu ya wilaya. Wakati
mwingine aliitumia matatu hiyo kubebea mizigo ya maduka yake kutoka maduka ya jumla huko
mjini. Sasa maisha yake yalichukua sura nyingine; maisha yalimnogea na kumchekea wakati
wenzake kijijini walipotokonea kwenye umaskini wa sina sinani.
Sura ya Ishirini
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 204 12/11/2019 09:45
205
Watu walimuonea gere kuyasambaza maneno yao. Wengine walisema kuwa walizituhumu
njia alizozitumia kuipata mali yake. Wengine walimpiga vijembe kuwa walishuku kuwa huenda
alikuwa na hila fulani. Shaka hii ilitokana na ajali mbili zilizohusisha matatu yake. Mara ya
kwanza iliteleza karibu na soko kuu na kuwaua watu wawili. Kesi iliyofuatia ilitupiliwa mbali
na mahakama kuu kwa kutokuwa na misingi mizuri. Siku nyingine alipatikana mwanamume
fulani ameanguka na kufa mbele ya mlango wa duka lake la kuuzia vifaa vya ukulima. Watu
walisema mengi kabla ya kutulia.
Hali ilibadilika muda mfupi baadaye. Ilitokea hivi. Shabash aliwaalika watu nyumbani kwake
kwa karamu. Kwa wengine hii ilikuwa fursa ya kubwia pasi na taahira. Walijua kuwa wakati huo
ngombe kadha watauliwa na kuku wengi watadenguliwa vichwa. Hawakutaka kuikosa abra hii
muhimu ya kuonja nyama za kuku na ngombe.
Baada ya sherehe hiyo, watu walifumukana na kwenda makwao. Siku mbili baada ya karamu,
watu watatu waliokuwako kwenye karamu hiyo walikufa katika mazingira ya kutatanisha. Wote,
mwanamke na wanaume wawili, walilalamika maumivu ya tumbo kisha wakaanguka na kuaga
dunia. Jamaa waliokuwako katika karamu ile walianza kusema. “Ehh, alikuwa na maana gani
aliposimama kabla ya karamu kuanza na kusema: Haya watu ndio hawa…kuleni mshibe!”
Watu walisema kila aina ya maneno, lakini hawakuelekea kukia hatima nzuri hadi siku moja.
Kijana mmoja aliyekuwa mfanyikazi katika mji wa Shabash ndiye aliyeishia kuituliza kiu ya watu
wengi. Kwao huyu ndiye alifumbua kila kitu kwa kudai kuwa Shabash alikuwa akifuga majini
aliyoyatumia katika biashara zake. Alieleza kuwa majini hayo ndiyo yaliyosababisha biashara
yake ikue na kustawi haraka kama uyoga. Lakini yalikuwa na masharti yake. Ilikuwa lazima kila
mwezi pauliwe wanyama kadha katika mji wa Shabash na damu yake kutambikiwa majini hayo.
Siku hizi walikuwa wamekinai shahamu ya nyama ya mbuzi na ngombe. Sasa walitaka watu na
ndio maana Shabash akawaalika watu siku ile na kuyaambia majini hayo kuwa yana uhuru wa
kuchagua na kumla yeyote. Hii ndiyo iliyokuwa siri ya ufanisi wa jirani Shabash.
Mzee Maarifa aliyefahamika kijijini kwa busara aliposikia maneno ya watu aliangua kicheko.
“Nyinyi mmezama kabisa katika lindi la ushirikina? Mtu akifanya kazi kwa juhudi kubwa mnasema
majini? Siri ya ufanisi ni juhudi, si majini. Mkiona vyaelea vimeundwa. Siri ya jirani ni juhudi
tu. Ehh, juhudi ya kujua kuwa haba na haba hujaza kibaba.
Maelezo ya msamiati
kuguria : kuhamia.
mbelewele ya maua : unga wenye mbegu za kiume aghalabu za rangi ya manjano ulio
ndani ya ua.
yalimnogea : yalikuwa mazuri; yalikuwa ya ufanisi.
umaskini wa sina sinani : umaskini mwingi.
walizituhumu : walizitilia shaka, walizishuku.
kubwia pasi na taahira : kula kwa wingi bila kuchelewa au kokosa.
watadenguliwa vichwa : watachinjwa.
abra : nafasi; fursa.
kutambikiwa : kufanyiwa ada fulani ili kutuliza mizimu; kutolewa kama sadaka.
ushirikina : hali ya kuamini mambo ya uchawi, mizimu n.k.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 205 12/11/2019 09:45
206
Maswali
1. Eleza jinsi biashara ya Mzee Shabash ilivyonawiri kiasi cha yeye kuonewa wivu na wafanyi
biashara wengine.
2. Baada ya maendeleo yake, watu walianza kumtuhumu Shabash. Ni matukio gani
yaliyosababisha tuhuma hizi?
3. Unakiri tuhuma kuwa Shabash alifuga majini ni za kweli? Toa sababu zako.
4. Eleza maana ya misemo hii kama ilivyotumika katika kifungu:
(a) toa mleli
(b) miaka na dahari
(ch) piga vijembe
5. Taarifa hii ina mafunzo gani?
6. Eleza maana ya methali hizi kama zilivyotumika kwenye kifungu.
(a) Haba na haba hujaza kibaba.
(b) Ukiona vyaelea vimeundwa.
7. Tumia maneno haya katika sentensi:
(a) kuguria (d) watadenguliwa vichwa (g) wamekinai
(b) washitiri (e) abra (h) kutambikia
(ch) maduka ya jumla (f) ushirikina
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi
Nyimbo
Katika sura iliyopita tuliona kuwa nyimbo hupatikana na kuambatana na shughuli mbalimbali.
Kila shughuli huwa na wimbo tofauti unaohusiana na shughuli hiyo na kuzungumzia suala
fulani. Wimbo unaoimbwa wakati wa harusi sio sawa na wimbo unaoimbwa wakati wa mazishi.
Wimbo wa wakati wa maafa na mazishi huwa na sauti ya chini na upole. Lugha ya wimbo huu
imejaa maneno ya upole na ya kufariji. Wimbo wa harusi kwa upande wake una maneno ya
kufurahisha, kuchangamsha na huweza kuhusisha hata kucheza fulani.
Wimbo unaotumiwa katika shughuli fulani huwa na sifa zake maalum. Kutokana na hali hii
tunapata aina tofauti za nyimbo: nyimbo za harusi, nyimbo za maafa, nyimbo za kisiasa, nyimbo
za watoto, nyimbo za kuwabembeleza watoto walale n.k.
Katika sura hii tutaangalia aina moja tu ya wimbo: wimbo wa kumbembeleza mtoto au
bembelezi. Huu ni wimbo unaoimbwa na mlezi wa mtoto kumbembeleza mtoto alale. Mara nyingi
wimbo huu unaimbwa mtoto anapolia sana na huimbwa kwa sauti ya chini chini. Bembelezi
huweza kuwa na maneno yanayoonyesha chuki aliyo nayo mlezi kuhusu jambo fulani.
Sifa za bembelezi:
Aghalabu baadhi ya maneno hurudiwa au hukaririwa.
Bembelezi hushirikisha matendo, miondoko taratibu (mkono) n.k.
Huimbwa na mlezi wa mtoto.
Huimbwa kwa sauti ya chini, wakati fulani.
Huweza kuwa na maneno yanayoonyesha hisia alizo nazo mlezi kuhusu jambo, hali au
mtu fulani. Kama vile upendo, chuki n.k.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 206 12/11/2019 09:45
207
Mfano
Nyamaa mwana nyamaa
Nyamaa mwana usilie
Ukilia waniliza
Wanikumbusha ukiwa
ukiwa wa baba na mama. . .
Zoezi
Toa mfano wa b-embelezi kutoka jamii yako.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Muundo wa sentensi: Kirai
Muundo wa sentensi: Kirai
Kirai ni fungu la maneno ambalo hufanya kazi pamoja. Kirai hakina huwa na maana lakini si
kamili. Hali hii hutokana na kuwa kirai hakina muundo wa kiima na kiarifu. Muundo wa kiima
na kiarifu ni ule ambao unahusisha mtenda wa jambo au tendo na tendo lenyewe.. Katika kirai
muundo uliopo wa tungo huhusisha neno moja au zaidi ambayo huwekwa kwa mpangilio maalum
ambao huzingatia uhusiano kati ya neno kuu na maneno mengine. Mifano ya virai:
(a) mrefu sana
(b) saa nane kamili
(ch) mtoto mnyenyekevu
(d) mwanamume huyu mwepesi
(e) chini ya meza
(f) mchezaji mwenzetu
Mifano hii inaelezwa kama virai kwa sababu haiwasilishi maana kamili,. Kwa mfano, kuhusu
mrefu sana , tunajiuliza nani?. Kuhusu saa nane kamili kuna nini? au kulifanyika nini? Je,
mtoto mnyenyekevu’ ana nini au kafanya nini au ni wa nani? Tunajiuliza maswali hayo kuhusu
mwanamume huyu mwepesi (kafanya nini?) na mrefu sana (ana nini na ni nani) n.k. Ili maana
kamili iwepo lazima tuongezee maneno mengine. Kwa mfano:
(a) Mwanafunzi mrefu sana ameingia darasani.
(b) Nitasari saa nane kamili
(ch) Mtoto mnyenyekevu amesiwa na mwalimu.
(d) Mwanamume huyu mwepesi ni mwanariadha.
(e) Paka yuko chini ya meza.
(f) Mchezaji mwenzetu amejeruhiwa.
Sehemu zilizopigiwa mistari zimeongezwa ili kutoa maana kamili ya virai. Virai vyenyewe huwa
na kazi mbalimbali. Huu ndio msingi wa kuwepo aina tofauti tofauti ya virai. Kwa mfano, katika
mfano wa kwanza, kinatoa maelezo zaidi kuhusu mwanafunzi. Katika mfano wa b, kinatoa
maelezo kuhusu wakati. Mfano wa c ni wasifu wa mtendaji sawa na ilivyo katika mfano d na
mfano wa f. Katika mfano wa e, ni maelezo ya mahali
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 207 12/11/2019 09:45
208
Sifa za kirai
(a) Hakina muundo wa kiima na kiarifu ambao unahusisha mtendaji na tendo analolitenda.
(b) Uainishaji au upangaji wa virai tofauti hutegemea uhusiano wake na maneno makuu kama
nomino, kitenzi, kielezi, kivumishi n.k.
(ch) Kirai hakikamilishi maana lakini huweza kuwa jibu. Kimsingi, kikisimama peke yake
hakileti maana.
(d) Kirai ni kikubwa kuliko neno lakini ni kidogo kuliko kishazi.
(e) Kirai huweza kutokea upande wa kiima au upande wa kiarifu.
(f) Kirai huweza hata kuundwa na neno moja.
Zoezi
Geuza virai vifuatavyo kuwa sentensi kamili.
(a) Saa moja kamili.
(b) Watu wawili.
(ch) Kama unataka.
(d) Kwa nini?
(e) Ndani ya kikapu.
(f) Katika ubao.
(g) Miaka michache iliyopita.
(h) Jumamosi usiku.
(i) Kwa shoka.
(j) Humu shambani.
(k) ni mwalimu
(l) ana mkate
(m) atanipatia
Kikundi nomino na kikundi tenzi
Sentensi huundwa kwa sehemu mbili kuu Kikundi nomino (KN) na Kikundi tenzi (KT).
Tazama jedwali lifuatalo.
Kikundi nomino (KN) Kikundi tenzi (KT)
Mtoto wangu anakunywa maziwa.
Paka huyu atamshika panya yule.
Shule yetu itafungwa kesho kutwa.
Nyumba yenu ni maridadi sana.
Kiatu chako kimeraruka.
Kikundi nomino (KN) ni neno au fungu la maneno ambalo habari yake inatolewa katika sentensi.
Nacho kikundi tenzi (KT) ni neno au fungu la maneno linalotoa habari kuhusu kikundi nomino
(KN); kwa mfano:
“Mtoto wangu, paka huyu, shule yetu, nyumba yenu”, na “kiatu chako ni vifungu vya
maneno vyenye nomino ambayo habari yake inatolewa katika sentensi. Navyo ndivyo vikundi
nomino (KN). Anakunywa maziwa, atamshika panya yule, itafungwa kesho kutwa, “ni
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 208 12/11/2019 09:45
209
maridadi sana, na “kimeraruka, ni vifungu vya maneno vinavyotoa habari kuhusu vikundi
nomino. Navyo ndivyo vikundi tenzi (KT).
Neno kuu katika kikundi nomino ni nomino au kiwakilishi chake. Nalo neno kuu katika
kikundi tenzi ni kitenzi. Kila sentensi ni lazima iwe na nomino au kiwakilishi cha nomino na
vile vile ni lazima iwe na kitenzi.
Zoezi
1. Tenganisha kikundi nomino (KN) na kikundi tenzi (KT) katika sentensi zifuatazo.
Kwa mfano: Baba yangu atakuja kesho.
Baba yangu KN
atakuja kesho KT
(a) Nyanya yetu ametuletea mananasi.
(b) Kiatu chako kimeraruka.
(ch) Shule yenu itafungwa lini?
(d) Mto huu ulifurika wiki jana.
(e) Watoto saba watapata zawadi kesho.
(f) Runinga nzuri ilinunuliwa wiki jana.
(g) Watoto watundu wamempiga mwanangu.
(h) Kiboko yule atatushambulia.
(i) Nchi yetu imepata maendeleo mengi.
(j) Walimu wetu wanafundisha vyema.
2. Ongeza vikundi tenzi (KT) vifaavyo kwenye vikundi nomino (KN) vifuatavyo ili
kukamilisha sentensi.
(a) Mwalimu yule ……….
(b) Shule hii……………….
(ch) Wachezaji hodari……….
(d) Redio ile……………
(e) Mama yangu ………..
(f) Punda huyu…………..
(g) Mbwa wangu ………….
(h) Yeye ………….
(i) Maua haya ………….
(j) Mdudu mbaya ………..
3. Ongeza kikundi nomino (KN) kwenye vikundi tenzi (KT) vifuatavyo kukamilisha sentensi.
(a) alika jana.
(b) iko mkoani pwani.
(ch) watalima shamba vizuri.
(d) alifagia nyumba vibaya.
(e) ulimwangukia ng’ombe wangu.
(f) ina wanafunzi wengi.
(g) amewasaidia watu wengi.
(h) amepoteza kitabu chake.
(i) atawapa kuku chakula.
(j) wameangua mayai.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 209 12/11/2019 09:45
210
D. Kusoma
Matumizi ya aina mbalimbali za kamusi
Kamusi ni kitabu ambacho kina orodha ya maneno yaliyopangwa kwa mujibu wa alfabeti pamoja
na maana na maelezo yake. Kamusi humsaidia mtu kujua maana ya neno analolitaka pamoja na
kumwonyesha ni maneno yapi yanayofanana na neno hilo.
Kamusi huwa na maelezo yanayotofautiana kutegemea watumiaji wake. Kuna baadhi ya
kamusi ambazo hutumiwa na wanafunzi au watu wanaojifunza lugha, nyingine zinazotumiwa
na wanaoifahamu lugha n.k. Pia, kuna kamusi ambazo zina maelezo mengi zaidi ya maana ya
maneno, kwa mfano: zinazotoa maelezo mengi kuhusiana na jambo fulani. Kuna aina nyingi za
kamusi kutegemea wanaolengwa, ukubwa, eneo au mawanda na idadi ya lugha zinazohusika.
(a) Walengwa wa kamusi
Kamusi hutilia maanani mahitaji ya watumiaji waliokusudiwa. Kwa mfano kuna kamusi
za shule zinazolenga wanafunzi katika shule za msingi, za upili na hata wa vyuo vikuu
ambao wanajifundisha lugha fulani. Kamusi za shule huwa na sifa hizi:
Kamusi za wanafunzi wa shule za msingi huwa na maneno kuanzia 2500. Maelezo
yake yamerahisishwa sana, na aghalabu huambatana na michoro au vielelezo vingi
vya kumsaidia mwanafunzi kulielewa neno fulani pamoja na sentensi za matumizi.
Kamusi za wanafunzi wa shule za upili hadi kukia chuo kikuu huweza kuwa na
maneno yanayokia 50,000. Maneno hayo huelezwa kwa jinsi inayoeleweka na
mtumiaji. Kamusi hizi huwa na vielelezo lakini sio vingi kama katika kamusi za
wanafunzi wa shule za msingi.
Pia, kuna kamusi za kawaida za lugha ambazo huwalenga watumiaji wote wa lugha fulani,
wanaojifunza na wanaoijua lugha hiyo. Mfano mzuri wa kamusi ya aina hii ni Kamusi
Pevu ya Kiswahili.
(b) Eneo au mawanda ya kamusi
Kuna kamusi ambazo hujulikana kama kamusi maalum kwa sababu zinahusika na jambo
fulani. Kamusi za aina hii hujumlisha msamiati wa eneo fulani. Kamusi za aina hii humfaa
mtu anayetaka kujiendeleza katika uwanja maalum Kwa mfano: kujua maneno ya sayansi,
teknolojia, visawe n.k. Msamiati unaopatikana katika kamusi za aina hii ni wa fani maalum
tu. Mfano ni Kamusi ya Visawe, Kamusi ya Teknolojia, Kamusi ya Ufugaji, Kamusi ya
Sayansi, Kamusi ya Fasihi, Kamusi ya ndege, n.k.
(ch) Idadi ya lugha za kamusi
Kamusi inaweza kuwa ya lugha moja, mbili au zaidi. Hapa tutaangalia aina mbili za kwanza:
kamusi ya lugha moja na kamusi ya lugha mbili. Kamusi ya lugha moja hutumia lugha
moja; yaani maneno na maelezo ya maneno hayo pamoja na maana yake huelezwa kwa
lugha hiyo moja. Hii huitwa kamusi wahidiya. Kamusi ya lugha mbili huhusisha lugha mbili,
yaani maneno makuu huwa katika lugha moja na maelezo kuwa katika lugha nyingine.
Kamusi hizi hujulikana kama kamusi thaniya. Mfano wa kamusi kama hii ni A Standard
Swahili-English Dictionary ya F. Johnson.
Zoezi
Eleza manufaa ya kamusi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 210 12/11/2019 09:45
211
E. Kuandika
Utungaji wa kisanii: Vitanza ndimi
Unapotaka kutunga vitanza ndimi unapaswa kuzingatia mambo kadhaa:
Kwanza unaweza kutafuta maneno yenye sauti zinazokinzana.
Jaribu kuyapanga maneno hayo kwa namna inayounda sentensi yenye maana hivi kwamba
maneno yenye sauti zinazokinzana yanabadilishana nafasi.
Angalia kama kuna namna ya kuyabadilisha maneno yenyewe kwa kuzichezea sauti
mbalimbali.
Kumbuka siri kubwa katika vitanza ndimi ni kuleta au kuzua matatizo fulani ya utamkaji;
yaani inahitaji ufundi wa kutamka yale maneno na hasa kwa kasi.
Yapitie maneno uliyoyaandika kwanza polepole halafu kwa kasi ili uangalie athari au
matokeo yake.
Mifano ya vitanza ndimi
1. Baba Ben alibeba pipa akalitupa kwa pupa baharini likamgota papa aliyeruka kwa papara.
2. Nilipomwambia Njenga ajenge jengo la Chengo, alianza kunichenga akisema yeye Njenga
hana uwezo wa kujenga.
3. Tuliibeba mifuko tukaingia kivukoni ili tuvuke kwa kivuko lakini kabla ya kuvuka nikaona
mvuke nikamwambia Mfuke autazame mvuke ufukao kivukoni akasema si mvuke bali ni
moshi unaofanana na mvuke.
4. Sikuifuma fulana kwa mfumo wa mvumo uliovuma Mvumo anakotoka Mwamvumo.
Zoezi
(i) Tunga kitanza ndimi kimoja.
(ii) Mkishirikiana na kujadiliana na mwenzio mmoja, tungeni vitanza ndimi vitatu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 211 12/11/2019 09:45
212
Chemshabongo
Fuata maelezo uliyopewa kukamilisha jedwali.
1 2
3 4
5
6
7
8 9 10
11
12 13
14
15
16 17
18 19
20
CHINI
1. Kuuza na kununua bidhaa na huduma
2. Kutumikia watu au kuwapa msaada
3. Pahali pa kuuzia na kununua vitu mbalimbali
7. Matunda yenye nyama nyeupe tamu kwa ndani na ya rangi ya kijani, nyekundu au
hudhurungi
10. Ndwele
11. Udogo wa mbuzi
13. Chakula
15. Eleza kwa urefu au eleza waziwazi
KULIA
4. Kisunzi
5. Kikao maalum cha mazungumzo
6. Bila kikomo au kusita
8. Mtu aliye na adabu na anayeishi vyema na wenziwe
9. Unyevu ambao hutanda juu ya majani mara nyingi asubuhi
12. Pipi
14. Hali ya kupatanisha
16. Mpira wa miguu
17. A-Z
18. Mwongozo wa matukio katika shughuli fulani
19. Watu wanaokaa katika kijiji fulani
20. Pahali panapobubujika maji.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 212 12/11/2019 09:45
213
Sura ya Ishiri na Moja
A. Ufahamu
Simu na mawasiliano ya binadamu
Mawasiliano kati ya binadamu wanaoishi katika sehemu mbalimbali ni muhimu. Mawasiliano
haya yanaweza kufanyika kwa njia anuwai kama barua, risala, tarakilishi au simu. Baadhi ya njia
hizi ni muhimu, hususan kwa kuukisha ujumbe ambao umeandikwa.
Mawasiliano kwa njia ya simu yana upekee usiopatikana kwenye njia nyinginezo. Kwanza,
simu inamwezesha mtumiaji kuwasiliana kwa njia fasaha na mwenzake aliye mbali. Mtumiaji
ana fursa nzuri ya kuisikia sauti ya mwenzake na kwa njia hii kumhisi karibu. Uhusiano uliopo
wa kihisia katika mawasiliano kwa njia ya simu ni mzito na wa kibinadamu zaidi kuliko kwa
kutumia njia nyinginezo. Wahenga walisema barua ni nusu ya kuonana lakini simu nayo ni
nusu ya kuhisiana.
Njia hii muhimu ya kuwasiliana ilivumbuliwa na mwalimu wa Kimarekani mwenye asili ya
nchi ya Scotland aliyejulikana kama Alexander Graham Bell. Mwalimu huyu aliishi baina ya
mwaka wa 1847 na mwaka wa 1922. Mwalimu huyu aliivumbua njia hii ya kuwasiliana alipofanya
majaribio ya kuona jinsi sauti inavyoweza kutoka sehemu moja hadi nyingine. Alitumia vibapa
vya chuma vinavyotetema. Bell alitambua kuwa kibapa kilichokuwa upande mmoja kikitetema au
kutikisika, kibapa kilichokuwa upande wa pili kilitoa sauti fulani. Huu ndio msingi wa uvumbuzi
ulioishia kuzaa simu kama tunavyoijua leo.
Maendeleo ya simu yamepiga hatua kubwa tangu zama za Bell. Siku hizi, kwa kubofya vidude
vichache, tunaweza kuwasiliana na mtu aliyeko katika sehemu yoyote ile ulimwenguni. Kwa
kurahisisha mawasiliano kiasi hiki, simu imeishia kuufanya ulimwengu kuwa mdogo kuliko
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 213 12/11/2019 09:45
214
ulivyo hasa. Mawimbi ya simu husari sawa na mawimbi ya redio na hutegemea vyombo kama
setilaiti ili kukia lengo lake. Setilaiti huizunguka ardhi na hupokea ishara mbalimbali za simu
kutoka sehemu mbalimbali. Baada ya kuzipokea ishara, vyombo hivi huzikuza ishara zenyewe
kisha kuzielekeza ishara hizo nchi zinazohitajika.
Maungio ya simu yanayodhibitiwa na kompyuta au tarakilishi yanawezesha mawasiliano
kati ya simu moja na nyingine kufanyika. Maendeleo ya simu yamekia ngazi nyingine kwa
kuvumbuliwa kwa simu za mkononi. Hii ni hatua nyingine kutoka simu za kawaida zilizozoeleka
nyumbani, osini na sehemu nyinginezo. Hizi ni simu ambazo tumezoea.
Simu hizi mpya ambazo hujulikana kwa majina tofauti kama kiungambali, simu ya mkononi,
rununu au rununu, humwezesha mtumiaji kuwasiliana na mwenzake popote pale alipo. Simu
hizi hutumia mawimbi ya sauti kwa msaada wa vituo vyenye nguvu vinavyopitisha mawimbi hayo
kwenye setilaiti mbalimbali. Kuvumbuliwa kwa simu hii kumesaidia sana kwa sababu mawasiliano
yamerahisishwa mno. Hii ni simu inayomwezesha mtumiaji kuwasiliana na mwenzake wakati
wa shida kama ajali, ugonjwa na maafa ya aina yoyote.
Licha ya faida zake, simu hii ni ghali sio tu kuinunua bali pia kuitumia. Sio wote ambao wana
uwezo wa kiuchumi wa kuweza kuzinunua simu hizi. Tatizo jingine linalohusishwa na simu hizi
ni uwezekano wa watumiaji wa simu zenyewe kuathiriwa na miale inayofanikisha mawasiliano
yenyewe. Wataalamu wengi wametoa tahadhari kuwa simu hizi zinaweza kuathiri ukuaji wa
mifupa na hata ubongo wa anayehusika. Wataalamu hawa wanawashauri watumiaji kuhakikisha
kuwa simu zenyewe zina vikinga-miale kabla ya kuzitumia. Njia nyingine ni kuhakikisha kuwa
simu zenyewe haziwekwi karibu sana na sikio kwani sikio laweza kuathiriwa vibaya na miale hiyo.
Maswali
1. Taja njia mbalimbali za mawasiliano zilizotajwa kwenye kifungu.
2. Ni kwa nini mawasiliano kwa njia ya simu yana upekee?
3. Je, Alexander Graham Bell alivumbuaje kifaa cha simu?
4. Taja manufaa na hasara za simu za viungambali.
5. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa kwenye kifungu kisha uyatungie
sentensi.
(a) anuwai (ch) vinavyotetema
(b) setilaiti (d) kiungambali
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi: Maigizo
Utangulizi
Maigizo ni neno linalotumiwa kuelezea utanzu mmoja wa fasihi simulizi. Neno hili hutumiwa
kuelezea masimulizi ambayo yanaambatana na vitendo au matendo fulani. Igizo ni tendo
linaloonyesha jambo lililotokea, linalotokea au litakalotokea. Maigizo huwa mbele ya watazamaji
au hadhira.
Katika maisha yetu tunayafanya mambo mengi kwa kuigiza jinsi wengine wanavyofanya;
kwa mfano mtoto hujifunza kwa kuiga vitendo vya mzazi n.k. Ikiwa mtu ataigiza jinsi mkulima
anavyofanya kazi yake, atajifanya analima, kupanda au kuvuna jinsi anavyofanya mkulima wa
kweli.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 214 12/11/2019 09:45
215
Maigizo hufanyika mahali fulani maalum au jukwaani. Maigizo hufanywa au hutendwa
ili kuuwasilisha ujumbe fulani kwa njia ya vitendo. Kwa kawaida igizo linaweza kuandikwa ili
waigizaji waweze kufanya mazoezi lakini hatimaye wataliigiza jukwaani.
Sifa za maigizo
Huandamana na vitendo.
Lugha inayotumika huingiliana sana na lugha ya jamii inayohusika.
Huwasilishwa jukwaani mbele ya watazamaji (yaani hadhira) kwa njia ya usimulizi na
utendaji.
Hadhira hulizingatia igizo kwa masikio yao, macho yao na hisia zao.
Kuna maigizo ambayo hutendwa katika vyombo vya habari kama redio na mengine kwenye
lamu.
Huweza kuandamana na nyimbo.
Huiga mambo yanayopatikana katika jamii.
Zoezi
1. Eleza maigizo ni nini.
2. Taja sifa zozote nne za maigizo.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vimilikishi -etu’, -enu’, -ao
Tazama jedwali lifuatalo:
Ngeli Nomino
Vimilikishi
Matumizi
-etu -enu
-ao
i
zi
bar
ua
bar
ua
yetu
zetu
yenu
zenu
yao
zao
Barua yenu iko wapi? Barua zenu
ziko wapi?
i
i
chumvi
chumvi
yetu
yetu
yenu
yetu
yao
yao
Chumvi yao iko hapa.
Chumvi
yao iko hapa.
u
zi
ufunguo
funguo
wetu
zetu
wenu
zenu
wao
zao
Ufunguo wenu umepotea.
Funguo zenu zimepotea.
u
u
umaskini
umaskini
wetu
wetu
wenu
wenu
wao
wao
Umaskini wetu utakwisha.
Umaskini wetu utakwisha.
ku
ku
kulala
kulala
kwetu
kwetu
kwenu
kwenu
kwao
kwao
Kulala kwetu kutatuumiza.
Kulala
kwetu kutatuumiza.
pa ku
mu
mahali
mahali
mahali
petu
kwetu
mwetu
penu
kwenu
mwenu
pao
kwao
mwao
Mahali
pao
pamejaa.
Mahali kwao kumejaa watu.
Mahali mwao mmejaa watu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 215 12/11/2019 09:45
216
Zoezi
1. Tumia vimilikishi ‘-etu, ‘-enu au ‘-ao katika umoja na wingi kukamilisha sentensi zifuatazo.
(a) Ndege _________ itabeba abiria wengi.
Ndege _________ zitabeba abiria wengi.
(b) Kucheza _________ kutawasaidia.
Kucheza _________ kutawasaidia.
(ch) Kuridhi ka kunanifurahisha.
Kuridhikakunanifurahisha.
(d) Mahali _________ mmechafuka.
Mahali _________ mmechafuka.
(e) Uovu _________ utawapoteza.
Maovu _________ yatawapoteza.
(f) Sukari _________ imekwisha.
Sukari _________ imekwisha.
(g) Uzi _________ utakatika.
Nyuzi _________ zitakatika.
(h) Mahali _________ panafaa sana.
Mahali _________ mnafaa sana.
(i) Chumvi _________ imemwagika.
Chumvi _________ imemwagika.
(j) Kondoo _________ ameuzwa.
Kondoo _________ wameuzwa.
2. Chagua nomino mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo.
(a) ______ zao zimeka. (Umaskini, Barua)
(b) ______ mwenu mna uchafu.(Kulala, Mahali)
(ch) ______ kwenu kuliwafaa.(Mtoto, Kusikiliza)
(d) ______ wao ulivunjika.(Kisu, Uto)
(e) ______ wenu hauwafai.(Utajiri, Kijiko)
(f) ______ wetu amefaulu. (Mchezo, Mwanafunzi)
(g) ______ kwetu kulituokoa. (Uzi, Kutimka)
(h) ______ yao ipo hapa. (Sukari, Mahali)
(i) ______ petu patafungwa. (Runinga, Pahali)
(j) ______ wao atachinjwa. (Mkono,Bata bukuni)
Kuakisha
Kinyota (*)
Hii ni alama ya nyota inayotumika kuashiria jambo fulani katika maandishi. Kwa mfano huweza
kutumika:
a) kuonyesha kuwa maendelezo ya neno fulani yana makosa; kwa mfano:
* kitaabu
* mpiraa
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 216 12/11/2019 09:45
217
* kukuu
* kalaamu
* sae
* kijikeo
b) Kuashiria kuwa mpangilio wa maneno katika sentensi una makosa; kwa mfano:
* Mamangu sokoni leo amekwenda saa sita.
* Kitabu kinakufaa hiki sana.
* Wanafunzi watatia wale sana bidii.
* Kisu cha hiki ni nani?
ch) Kuashiria msomaji kuhusu jambo fulani ambalo maelezo yake yanapatikana sehemu ya
chini ya ukurasa huo.
d) Kuonyesha kuwa sentensi au fungu la maneno lina makosa ya kisaru; kwa mfano:
* Mtoto chetu kinalia.
* Kijiko hiki ni ya nani?
* Mama yangu wananiita.
* Hebu niletee kiatu ile.
D. Kuandika
Utungaji wa kiuamilifu: Taarifa
Taarifa ni maandishi ambayo huwasilisha ujumbe fulani kwa msomaji. Uandishi wa taarifa au
ripoti ni muhimu kwa mwanafunzi sio tu kwa maisha na mazingira ya shuleni bali pia baada
ya shule. Taarifa hupangwa kutegemea wanaohusika, yaani ni nani wanaoisikiliza au kuihitaji
taarifa hiyo. Taarifa huweza kuwa juu ya habari fulani, kwa mfano zinazosomwa redioni au katika
runinga kila jioni.
Mambo ya kuzingatia katika uandishi wa taarifa
1. Weka wazi maelezo au yabainishe kwa kuyapa vichwa vinavyofaa ili kuwaelekeza wasikilizaji
au wasomaji.
2. Maelezo ya taarifa yawe mafupi na rahisi kusomeka na kueleweka.
3. Maelezo yaliyopo kwenye taarifa lazima yahusiane na lengo kuu la taarifa fulani.
4. Usemi unapaswa kuandikwa kwa nafsi ya tatu. Kwa mfano: akaondoka, wakaka, n.k.
5. Taarifa iwe na mtiririko.
6. Isiwe na makosa ya saru na iwe katika Kiswahili sanifu.
7. Hakikisha kuwa alama za uakishaji zimetumiwa vizuri na kisahihi.
Zoezi
Andika taarifa kuhusu umuhimu wa usa shuleni.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 217 12/11/2019 09:45
218
Chemshabongo
Fuata maelezo kukamilisha jedwali.
1 2
3
4 5 6
7
8 9
10 11
12 13
14 15
16
17 18
CHINI
1. Maneno ambayo huibuka wakati fulani katika lugha
2. Mtu anayechukua vitu au mali ya mtu kwa nguvu na aliyejihami kwa silaha hatari
5. Gezageza ndio mji
6. Eusi kama makaa
8. Namna ya kutenda kitu au jambo kwa njia ya kipekee
9. Kwapua
10. Maongezi baina ya watu wawili
12. Mwonekano wa kitu au umbo lake
13. Unyende
15. Weka au simamisha gari, pikipiki au baiskeli mahali
16. Kipengee katika fasihi ambacho huhusisha umbo la nje la fasihi
KULIA
3. Chakula kilichobaki baada ya kuliwa
4. Neno linalotoa maelezo zaidi kuhusu nomino
7. Jicha mahali usionekane
8. Pahali pa kufanyia utati wa kisayansi
11. Zamu wa walinzi kuzunguka sehemu ili kulinda usalama
12. Mtu mwenye bidii na anayefanya kazi kwa bidii
14. Mambo ya dunia
17. Ufafanuzi
18. Nyumba yangu haina mlango
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 218 12/11/2019 09:45
219
A. Ufahamu
Uchafuzi wa mazingira
Mafuta yanayopatikana kwenye fukwe za bahari, moshi wa magari, takataka na bidhaa nyinginezo
zilizotupwa hapa na pale ni vichafuzi vya mazingira. Vichafuzi huathiri afya zetu na kuwaathiri
wanyama pamoja na mimea. Wanadamu wanayachafua mazingira yao kwa kila aina ya bidhaa
mbaya za kikemikali zinazotoka viwandani au kwenye viwanda vya kawi au nguvu. Bidhaa hizo
ni matokeo ya maisha ya siku hizi anayoishi binadamu.
Licha ya ukweli huu, ni muhimu kujua kuwa uchafuzi wa mazingira haukuanza leo. Miaka
na miaka iliyopita, viwanda vimekuwa vikitoa mawingu makubwa ya moshi wenye sumu. Hata
hivyo, uchafuzi wa mazingira umeongezeka maradufu kutokana na kuongezeka kwa viwanda.
Uchafuzi umesambaa ardhini, kwenye anga na majini. Msambao huu unapatikana katika pembe
zote za ulimwengu wetu. Je, kuna aina zipi za uchafuzi?
Moshi kutoka viwandani huichafua hewa au halianga.
Kwanza kuna uchafuzi wa halianga. Huko juu angani kuna tabaka linalojulikana kama ozoni.
Tabaka hili huwa ni aina ya gesi ya oksijeni na linaunda kinga fulani dhidi ya miale ya jua. Miale
hiyo ya jua huweza kusababisha kansa ya ngozi inapomkia binadamu. Hata hivyo, uchafuzi wa
mazingira unaelekea kuliathiri tabaka hili. Vile vile baadhi ya kemikali zinazotumiwa katika friji
au jokofu, au kwenye mikebe ya marashi ya kupulizia na upakiaji bidhaa, huuharibu ukanda huo.
Aina nyingine ya
uchafuzi ni ile
tunayoweza kuiita uchafuzi wa kiajali. Huu ni uchafuzi ambao
hutokea kama ajali, yaani
binadamu hatendi
kimakusudi. Mfano
mzuri ni meli inayovuja
mafuta baharini. Mafuta haya huwaathiri na kuwaua wanyama wanaoishi baharini kama samaki
na ndege na hata kuyaharibu mazingira yenyewe.
Miji mikubwa hukumbwa na uchafuzi mwingine unaohusiana na kuwako kwa idadi kubwa
ya magari. Magari haya hutoa moshi unaochanganya gesi ambazo huungana na nyingine
zinazotolewa na viwanda vikubwa. Mchanganyiko huu unapoungana na maji, husababisha
Sura ya Ishirini na Mbili
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 219 12/11/2019 09:45
220
mvua ya asidi. Mvua hii huweza kuiua mimea, kuathiri majengo na hata kuwaua wanyama wa
pori ambao huenda wakayatumia maji hayo. Magari hutoa moshi uliochanganyika na madini
aina ya risasi ambayo huweza kuathiri siyo tu mazingira bali pia mfumo wa akili wa binadamu.
Uchafuzi mkubwa unaopatikana katika miji na mazingira mengine yetu ni utupwaji ovyo ovyo
wa takataka. Fauka ya hayo, watu hufukia ardhini takataka ambazo huweza kuwa na matokeo
mabaya kwa sababu ya kupenyeza kwenye udongo na maji yanayotumiwa na watu na mimea.
Kila siku tunatupa takataka bila ya kujali wala kubali. Takataka hizi ni kama makopo, mifuko ya
plastiki, mabaki ya sigara au maganda ya matunda. Baadhi ya takataka ni hatari kwa wanyama na
nyingine huweza pia kusababisha majanga kama moto. Aidha, takataka hizi huyafanya mazingira
yetu yaonekane machafu.
Sote tuna jukumu kubwa la kuchangia kuupunguza uchafuzi wa kimazingira. Hatua ya kwanza
ni kuelimishana na kutambua umuhimu wa usa wa mazingira yetu. Tunapaswa kutia takataka
zetu katika vijalala maalum au mahali tunapoweza kuzichoma na kuziteketeza. Njia nyingine ni
kuhakikisha kuwa tunatunza vitu kama mifuko, chupa na kadhalika ambavyo huweza kuundwa
upya na kutumiwa tena. Hali kadhalika, katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwapo na juhudi
za kuwahimiza wenye magari kutumia mafuta ya gari ambayo hayana madini ya risasi. Kwa njia
hii, tutasaidia kuyaboresha mazingira yetu. Vile vile pana umuhimu wa kutilia mkazo utumiaji
wa bidhaa ambazo zinaweza kuoza na kuvunjikavunjika au kusagika na kuwa sehemu ya udongo.
Hatua ya kwanza ya kupambana na uchafuzi wa mazingira ni kujielimisha na kuwajibika. Kila
mmoja akitoa mchango wake tutafanikiwa. Kumbuka kuwa kinga na kinga ndipo moto uwakapo.
Maswali
1. Andika vichafuzi vinne vya mazingira vilivyotajwa katika taarifa hii.
2. Uchafuzi wa mazingira una madhara yapi kwa binadamu, wanyama na mimea?
3. Ni mambo gani yanayofanya uchafuzi wa mazingira kuongezeka kila siku?
4. Eleza jinsi hali ya tabaka la ozoni inavyoweza kusababisha madhara kwa binadamu.
5. Taja aina nne za vifaa vinavyotoa moshi na kuzidisha uharibifu wa mazingira.
6. Kufukia takataka ardhini huwezaje kusababisha uchafuzi wa mazingira?
7. Binadamu anahitajika kufanyaje ili kuzuia uharibifu wa mazingira?
8. Tumia maneno haya katika sentensi ili kuonyesha maana yake kulingana na matumizi
yake kwenye kifungu:
(a) fukwe (b) vichafuzi (ch) kansa
(d) viwanda (e) kuwajibika (f) friji
(g) vijalala (h) halianga
B. Kusikiliza na kuzungumza
Fasihi Simulizi
Vipera vya Maigizo
Maigizo ni kundi pana ambalo linajumlisha aina mbalimbali ambazo hujulikana kama vitanzu
au vipera vya maigizo. Msingi mkuu wa kuzipanga aina hizi ni kuangalia sifa zake za nje pamoja
na malengo yake. Kuna vipera kadha vya maigizo:
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 220 12/11/2019 09:45
221
Ngonjera
Ni maigizo ambapo waigizaji wanawasiliana kwa kutumia beti za mashairi. Wanapowasiliana
kwa mashairi haya wanatenda matendo ambayo yanaufanya ule ujumbe utokeze kwa njia wazi.
Ngonjera huweza kupangwa kwa namna ambavyo mtu mmoja asiyejua jambo fulani anaishia
kulijua. Ni muhimu kukumbuka kuwa ngonjera huingia kwenye kundi la maigizo tu pale
inapotendwa, ikiwa haitendwi basi sio sehemu ya maigizo bali sehemu ya ushairi.
Mfano:
: Mbona ukanifanyiza, kazi kama mimi punda,
Nguo nyingi kunifuza, japo mwili nimekonda,
Umri sijatimiza, ni mtoto bado kinda,
Huoni wanidhulumu?
: Mtu wa miaka kumi, ni mzima sio kinda,
Nakupa makumi kumi, pesa hata ukikonda,
Kelele sitaki mimi, au sivyo nakuponda,
Wewe mtumishi wangu!
: Mwajiri sikia sana, kuna sheria ‘mevunda,
Umemwajiri kijana, ambaye bado ni kinda,
Hiyo ajira ya wana, acha au jela wenda,
Ajira ya watoto ngo!
Zoezi
1. Msichana anatoa malalamishi yapi?
2. Mwajiri anatoa hoja zipi anapojitetea kupinga malalamishi ya Msichana?
3. Kutokana hasa na maelezo ya Msichana na yale ya Mtetezi tunajifunza nini kutokana na
ngonjera hii?
4. Taja sifa tatu za ngonjera zinazojitokeza katika mfano hapo juu.
Vichekesho
Ni maelezo mafupi ambayo hukusudiwa kufurahisha na kuichekesha hadhira. Vichekesho huweza
kuwepo kwa nia ya kuwafanya wasikilizaji wafurahi au kuwajulisha jambo fulani.
1. Kuna mwizi mmoja aliyemwoa mwizi mwenzake halafu watu wakawa wanashangaa
mtoto atakayezaliwa atakuwaje. Mtoto alipozaliwa akawa amefumba mkono wake. Wazazi
wakashangaa. Walipokwenda kwa mjuzi kuwasaidia wakatambua kuwa alikuwa amekunjia
pete ya dhahabu ya mkunga (yaani alipokuwa akizaliwa aliiba pete ya mkunga!).
Majigambo
Maigizo ambapo wanaoigiza hujisifu (kujigamba) kwa sababu ya matendo fulani ya kishujaa au
yasiyokuwa ya kawaida. Kwa mfano mkulima stadi anaweza kujigamba kutokana na kazi yake
ambayo inamletea mazao mengi na sifa.
Mfano
Mimi ni mkulima anayesika
kutoka jimbo hadi jimbo
nishikapo jembe langu
udongo unatetemeka
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 221 12/11/2019 09:45
222
nipandapo mbegu zangu
huchipuka kwa nguvu za ajabu
mimea yangu huipalilia kwa ustadi usio mfano
wakati wa kuvuna
maghala yangu hufurika
kwa mazao mengi ajabu
watu wote wananiogopa
kwa juhudi zangu
mimi ni bingwa wa ukulima
mimi ni shujaa wa ukulima
mimi ni ndiye mkulima asiye mfano
Zoezi
Eleza sifa anazosema anazo mjigambi huyu.
Michezo
Ni maigizo yenye visa virefu; waigizaji huwasiliana kwa njia ya mazungumzo, yaani wao kwa
wao. Michezo inaweza kutungwa na kuigizwa kwa ajili ya sherehe fulani. Kwa mfano: michezo
inayoigizwa wakati wa kufunga shule.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Sentensi sahili
Neno sahili’ huwa na maana ya rahisi’ au ‘-siokuwa ngumu’. Sentensi sahili huwa na muundo
mwepesi au usiokuwa mgumu. Hii ni sentensi ambayo huwa na kiima na kiarifu. Kiima tumeona
ni sehemu inayojaza nafasi ya mtenda. Sehemu hii pia huweza kujaza sehemu ya mtendwa.
Kiarifu ni sehemu inayozungumzia kiima au kutoa maelezo au kuarifu kuhusu kiima. Tuangalie
mfano huu:
(a) Mwalimu ameondoka
Neno mwalimu ni kiima kwa sababu linazungumzia mtenda au nani anayezungumziwa. Neno
au kitenzi ameondoka ni kiarifu kinachoeleza au kutoa taarifa kuhusu kiima, yaani kueleza
mwalimu amefanya nini.
Aghalabu sentensi sahili hudokeza wazo moja na aghalabu huwa na kitenzi kimoja kikuu.
Inawezekana pakawapo na vitenzi vingine vinavyokisaidia kitenzi kikuu. Mifano:
(a) Mwanafunzi anasoma kitabu (Kitenzi kikuu ni kimoja -anasoma)
(b) Yeye ameshinda tuzo (kitenzi kikuu ni kimoja vile vile - ameshinda)
(ch) Mama alikuwa akienda shambani (Kitenzi kikuu ni akienda’; alikuwa ni kitenzi kisaidizi)
(d) Atakuletea (Hapa kiima kinawakilishwa na kiwakilishi nafsi a’)
Upambanuzi wa sentensi sahili
Tunaweza kupambanua sentensi sahili ili kuonyesha muundo wake. Kielelezo cha mstari ndiyo njia
rahisi zaidi inayotumika kupambanua sentensi. Kwa kuzingatia njia hii, sentensi hupambanuliwa
kwa kutenganisha kikundi nomino (KN) na kikundi tenzi (KT) kisha kuonyesha aina za maneno
yanayojenga kila kikundi. Tazama jedwali lifuatalo:
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 222 12/11/2019 09:45
223
Kikundi Nomino (KN Kikundi Tenzi (KT) Muundo (kwa kielelezo cha mstari)
1. Kitabu changu kilipotea jana. KN
(N + V) + KT (T + E)
2. Hawa watoto watundu wameiba kitabu
changu.
KN
(V + N + V) + KT (T + N + V)
3. Ng’ombe wanono watachinjwa kesho. KN
(N +V) + KT (T + E)
4. Ngamia warefu wanabeba mizigo. KN
(N + V) + KT (T + N)
5. Mbwa wakali walibweka bwe! (N + V) + KT
(T + E)
6. Hiki chakula kitamu kitaliwa na nani? KN
(V + N+ V) + KT (T + U + W)
7. Dada yangu amekwenda wapi? KN
(N + V) + KT (T + E)
8. Mishumaa hii imenunuliwa leo. KN
(N + V) + KT (T + E)
9. Gari lako jekundu linapendeza watu sana. KN
(N + V+ V) + KT (T + N +E)
10. Mwalimu wetu amelazwa hospitalini. KN
(N + V) + KT (T + E)
11. Nyimbo zenu zilitupendeza mno. KN
(N + V) + KT (T + E)
12. Barabara hii pana inaelekea wapi? KN
(N + V+ V) + KT (T + E)
13. Lile jambazi hatari lilifungwa gerezani. KN
(V + N + V) + KT (T + E)
14. Wewe muhuni ondoka hapa upesi. KN
(W + V) + KT (T + E + E)
15. Magonjwa haya yalitoka wapi? KN
(N + V) + KT (T + E)
Zoezi
Ukizingatia mifano iliyo hapo juu, pambanua sentensi sahili zifuatazo ili kuonyesha muundo
wake kwa kutumia kielelezo cha mstari.
Kikundi Nomino (KN) Kikundi Tenzi (KT) Muundo (kwa kielelezo cha
mstari)
1. Watoto wake wawili wamesari ngambo.
2. Mwalimu wetu mmoja amehamishwa.
3. Ndovu wale watatushambulia usiku.
4. Kitabu chenu kipya kiko wapi?
5. Jogoo mkubwa alichinjwa jana.
6. Chuo hicho kitafungwa wiki ijayo.
7. Mwandishi shupavu ameandika vitabu maarufu.
8. Mhariri huyu anaandika nini?
9. Baba yako amenunua pikipiki?
10. Ye y e aterejea nyumbani kwao.
11. Mji huo mkubwa unawapendeza watu wengi.
12. Wanafunzi wetu wote wamefaulu.
13. Chakula hiki kimeiva vizuri.
14. Saa yake imeharibika.
15. Maji yenu yanachemka.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 223 12/11/2019 09:45
224
D. Kuandika
Muhtasari: Utangulizi
Muhtasari ni maelezo ambayo yamekusudiwa kuwasilisha mawazo makuu kuhusiana na taarifa
au jambo fulani. Kwa nini ni muhimu kujua jinsi ya kuandika muhtasari au ufupisho? Muhtasari
husaidia kupima jinsi mwanafunzi anavyolielewa jambo.
Sifa za muhtasari
Muhtasari unapaswa kuwa wazi au dhahiri; yaani yaliyomo yaweze kueleweka.
Unapaswa kuwa mfupi; nia ya kuandika muhtasari ni kufupisha, kwa hiyo lazima uwe
mfupi.
Lazima uwe umekamilika; yaani hoja zote muhimu ziwepo. Mtu anayeusoma anapaswa
kuziona hoja zote muhimu.
Ueleze mambo muhimu kwa njia iliyokamilika bila ya kuacha jambo lolote lifaalo.
Lazima uandikwe kwa hati na mtindo unaoweza kusomeka au kueleweka.
Zingatia maagizo uliyopewa kuhusu idadi ya maneno.
Kifungu cha muhtasari
Meno ya Binadamu
Kila mara tunapokula, meno yetu huuma, kutafuna na kusaga chakula tunachokula. Meno
yanatuwezesha kukivunja chakula ili kuuwezesha mwili wetu kukitumia. Ili mwili uweze
kukitumia chakula hicho, pana vitu fulani vinavyokifanyia chakula hicho kazi mpaka kikaweza
kuingia kwenye mwili wenyewe. Hivi hujulikana kama vimengenya. Binadamu ana meno ya aina
nne kuu. Kwanza kuna meno ya mbele au makato ambayo kazi yake ni kuuma au kukata chakula.
Haya yanasaidiana na mengine yanayojulikana kama michonge; yanakata pia lakini yako sehemu
ya nyuma. Michonge hufuatwa na meno mengine yanayosaga chakula na ambayo hujulikana
kama masagego. Masagego hufanya kazi na meno mengine yajulikanayo kama magego. Kazi ya
aina hizi mbili za meno ni kutafuna na kusaga chakula kabisa kabla ya kukimeza. Idadi ya meno
ya mtu mzima ni thelathini na mawili. Bila ya kuwa na meno mazuri binadamu hukabiliwa
na matatizo makubwa wakati wa kula. Meno huweza kuharibika kwa sababu ya kutopigwa
mswaki vizuri na mara kwa mara. Ili kuhakikisha kuwa meno yetu ni mazuri pana umuhimu wa
kudumisha afya nzuri ya meno. Tunafanya hivi kwa kuhakikisha kuwa tunayapiga mswaki kila
baada ya kula na kabla ya kulala. Lazima tuhakikishe tumeyapiga mswaki vizuri bila ya papara
ili kuondoa mabaki ya chakula yanayoweza kuwa chanzo cha viini vinavyoharibu meno. Pili,
lazima tuhakikishe kuwa hatuharibu uzi wa meno, yaani ile nyama inayoshikilia meno hasa
kwa kutia vijiti katikati ya meno baada ya kula. Afya ya meno ni muhimu ili kuhakikisha kuwa
meno yetu yanadumu na kuendelea kutufaidi katika uhai wetu.
Zoezi
Kwa nini ni muhimu kudumisha usa wa meno? (Andika kwa maneno yasiyozidi 20)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 224 12/11/2019 09:45
225
Chemshabongo
Tazama jedwali lifuatalo kisha ujibu swali lililo chini yalo.
O D N X H T H U K U M U K H T Y U J X U X H W D N
E E N P D Q F U E T W T N K O Y X Z J I N A I R C
I P Z Q K U I S M E O A P U D M L Y J Y E A P D K
H Q S M A H O J I A N O P V P Y A A J G K D S W M
U I V H T A U V W P K G W E O C S L Y U Q H W K W
N Y I T I Z L H P U U T B C L K Q C A M K G O O R
Z I D E X K I C R D J J V P E E G W I L R U R C O
B R O G M Z M E U F I S A D I L L D R Y A E M K S
K C K E X D W L T R O D S R W H A E J B H M H U S
G R E M O U E V D Y O Q J B N Y O O Z C M G I W G
A U Z E P K N Z H N S Z G A V A N A A I A V P K W
T S O A L U G H D O E J B J S M E K U S T Y F B O
U H D N T D U U S H I R I K I A N O X F A K F W B
Z W B A T U N A X J Q J K U M U H I M U T F S Z H
I A G Q U K I M Q Y Y U Y C K K G Q A K I R E P S
W J T K A U F E L Q U D K M L G P K Z I Z K I O I
B O Q H A M A N I K A J P P O L I S I Q O A Y Z I
Tafuta maneno yafuatayo kwenye jedwali.
JUKUMU MALALAMIKO POLISI WAPELELEZI GAVANA
TEGEMEANA UMUHIMU RUSHWA VIDOKEZO KACHERO
GATUZI JINAI USHIRILIANO MAHOJIANO UFISADI
HUKUMU ULIMWENGU HAMANIKA MATATIZO
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 225 12/11/2019 09:45
226
Sura ya Ishirini na Tatu
A. Ufahamu
Si urogi, ni ugonjwa
Wanakijiji wa Konyu walika kwa wingi kumsikiliza daktari Rosalia Nyambura aliyehusika
na uenezaji wa habari za Ukimwi mkoani. Watu wote walipoketi na kutulia, daktari alianza
kuongea. “Wenzangu, nina furaha kuka hapa siku ya leo. Ninayo mambo kadha muhimu ya
kuwaeleza. Wengi wenu mmeshasikia neno UKIMWI. Hata hivyo, kama ilivyo kwingineko,
wengi hawaufahamu ugonjwa huu vizuri. Huenda nikiwaambia kuwa baadhi ya wagonjwa wenu
wanaugua Ukimwi hamtakubali.
“Hatutakubali kamwe! Wagonjwa wetu ni wale waliorogwa, akasema Mzee Muragori kwa
ukali mwingi.
Tulia mzee. Sisemi kuwa kila mgonjwa ana Ukimwi. Lakini kabla ya kuamua kama ni kurogwa
usemako, inabidi muwapeleke wagonjwa hospitalini wafanyiwe uchunguzi.
“Uchunguzi wa nini? Uchawi hukabiliwa vyema na waganga wa kienyeji, si madaktari. Dawa
za kienyeji ni mambo yote!” akaropoka Mzee Kajiwe.
Daktari alipoona mambo yanazidi kuharibika akawaita wale wazee wawili pale mbele ya
hadhara. Akawaambia, “Nataka mniambie mambo machache kuhusu wagonjwa wenu. Tuanze
na wewe mzee, daktari akamwambia Mzee Muragori.
: Y   
: A 
: K . N  . B    
,       N. L  .
W  
: N 
: L. H . L      
.
: H 
: B ,     . M  
  K,   M K. L  
  ;       
   . K   
M  M M. L    
 . M     A’, F, N 
W. B     .
: A . N   ,    .
: H   . M   . S 
   C K  .
: N   
: S         .
: A
: B Y   . H     .
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 226 12/11/2019 09:45
227
: V
: M      W,  
M M     . A K
 N. B  ,    
     . T   
  M, S, O, K’  W. N
    .
: L W ,   
: E N   .
: J,    ,   , 
     
  : E
: J,    
: E V  ,    . K 
: N  
 : N
: J,           
: K T   .
: N  
: W  ,     .
: J,        
  : E
: T     
: N. D   
: H   
: L W  K       H   ,
   V D   K,  
 .
: H   U
: A  U  
: H       U.
: L  M  
: P . A U
: S       U. A  
  . I,      
,  , ,    
        
   ,    U.
  : S
: S      . H
     U   .
(A ) N    
  U. U   . U  
      . D  
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 227 12/11/2019 09:45
228
       .
: M   
: A      
   VCT,  V  U, N
 K.
Baada ya maelezo hayo, watu wote walirejea makwao wakiwa wamejifunza mengi kuhusu nduli
huyu mkubwa, yaani Ukimwi.
Maswali
1. Unadhani ni kwa nini watu pale kijijini walikuwa na hamu ya kumsikiliza daktari Rosalia?
2. Wanao Kajiwe na Muragori walikuwa wagonjwa mno. Taja dalili za ugonjwa waliokuwa
nao.
3. Ni tabia zipi za wanao Kajiwe na Muragori zinazoweza kuwa ndizo chanzo cha magonjwa
ya zinaa.
4. Taja majina ya maraki za wanao Kajiwe na Muragori.
5. Mtu akiishi na mgonjwa wa Ukimwi atahitaji kuchukua hatua gani ili amhudumie mgonjwa
huyo bila hatari ya kuambukizwa?
5. Mtu hawezi kuambukizwa Ukimwi ikiwa yeye si asherati. Je, unakubali? Fafanua.
6. Iwapo mtu amekonda sana ni lazima awe na Ukimwi. Ni kweli au si kweli. Fafanua.
7. Eleza mambo muhimu waliyojifunza wanakijiji wa Konyu siku hiyo kuhusu Ukimwi.
8. Toa maana za maneno haya kulingana na vile yalivyotumika kwenye kifungu kisha uyatumie
katika sentensi:
(i) utando (ii) mwana mkembe (iii) usuhuba
(iv) pata jiko (v) majipu (vi) mabebe
(vii) pata jiko (viii) wanaugua (ix) kimanzi (x) nduli
B. Kusikiliza na kuzungumza
Isimujamii: Sajili ya mtaani
Hii ni sajili ambayo hupatikana katika muktadha wa mtaa na si rasmi. Ni sajili ambayo inahusishwa
zaidi na vijana. Muktadha wa mazungumzo na umri wa wanaohusika katika mazungumzo
yenyewe huathiri matumizi ya lugha. Katika maeneo ya mjini inawezekana hata pakawapo na
matumizi ya Sheng
Sifa za sajili ya mtaani
(i) Msamiati unaotumiwa unategemea mada na huenda usiwe msamiati rasmi.
(ii) Matumizi ya lugha isiyokuwa rasmi au sanifu. Lugha ya aina hii haizingatii kanuni rasmi
za matumizi ya lugha
(iii) Matumizi ya maneno ambayo yanaeleweka na wanaohusika katika mazungumzo hayo tu.
Hili huweza kutokana na nia ya kujitambulisha wao kwa wao kama wanakundi fulani au
kwa kutaka kuwa na siri fulani zao
(iv) Kuwepo kwa kuchanganya ndimi au kuchanganya maneno ya lugha tofauti tofauti.
(v) Sifa ya kukatizana wakati wa kuongea au kukatana kauli.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 228 12/11/2019 09:45
229
(vi) Matumizi ya kauli ambazo hazikamiliki kimaana kwa sababu wanaohusika wanaelewa.
(viii) Matumizi ya maneno ya msimu au maneno ambayo huwepo kwa kipindi fulani tu.
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali uliyoulizwa
(Mtaani. Rwechungura, Yamwaka na Mgweno wanakutana njiani.)
: V    Y
: N R. M 
: S .
: H     
: K
: K
: E,    . J     
 ,   
: P,   
: W    ;    .
: H   
: L T .
: H        S  
 
: L  () B  T   
  . W    
’
: L       .
: K 
: Y ;       
 .
: L        
.
: L       ; 
    
: E      (). B   
        .
  : H   (W)
Zoezi
1. Je, ni sifa zipi zinazobainisha sajili iliyotumika katika kifungu hiki?
2. Eleza tofauti zilizoo baina ya sajili hii na ile ya shuleni.
Matamshi bora: Vitate a/h
a h
apa hapa
ama hama
adimu hadimu
ajali hajali
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 229 12/11/2019 09:45
230
Soma vitanza ndimi vifuatavyo ili kujizoeza matamshi fasaha ya sauti hizo.
(a) Tulipohamia mtaa wa Hamers kutoka Amers nilimuuliza Herman kama anahama Hemers
au hahami.
(b) Kasimu alitaka mahadimu wa kuhudumu katika hoteli yake ya Mhadimu Adimu lakini
alijua mahadimu ni adimu na mahadimu wakiwa adimu huenda asipate kamwe mahadimu
wa kuhudumu katika “mhadimu adimu.
CH. Saru na matumizi ya lugha
Upatanisho wa kisaru: Vionyeshi
Tazama jedwali hili:
Ngeli Nomino Vionyeshi Matumizi
‘h-’ ‘-le ‘h-’
a
wa
mzee
wazee
huyu
hawa
yule
wale
huyo
hao
Mzee yule ana mkongojo.
Wazee wale wana mkongojo.
u
i
mti
miti
huu
hii
ule
ile
huo
hiyo
Mti huo una matunda.
Miti hiyo ina matunda.
u
ya
ulezi
malezi
huu
haya
ule
yale
huo
hayo
Malezi yale yalifaa sana.
Malezi yale yalifaa sana.
ya
ya
maji
maji
hayo
haya
yale
yale
hayo
hayo
Maji haya yana nini?
Maji haya yana nini?
li
ya
lengo
malengo
hili
haya
lile
yale
hilo
hayo
Lengo hili litatimizwa.
Malengo haya yatatimizwa.
ki
vi
kisu
visu
hiki
hivi
kile
vile
hicho
hivyo
Kisu hiki kitakukata.
Visu hivi vitakukata.
Zoezi
1. Andika umoja wa sentensi zifuatazo.
Kwa mfano: Vyakula hivi ni vya nani?
Chakula hiki ni cha nani?
(a) Vikapu hivi vina nini? (b) Magonjwa haya yatatibiwa na madaktari wale.
(ch) Matunda yale ni ya nani? (d) Wanafunzi hao wataadhibiwa vikali.
(e) Malezi haya yatanifaa kweli? (f) Maharagwe haya yamenawiri.
(g) Manukato yale yananukia. (h) Wakulima hao watatia bidii.
(i) Mapana haya hayatatosha. (j) Vikombe hivi vina uchafu mwingi.
2. Andika nomino yoyote mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo;
Kwa mfano: _______ hiki ni kizuri sana.
Kitabu hiki ni kizuri sana.
(a) _______ haya yatakuchoma. (b) _______ yale yalimsaidia sana.
(ch) _______ hii ni mitamu sana. (d) _______ hivi ni vya nani.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 230 12/11/2019 09:45
231
(e) _______ hii itapandwa lini? (f) _______ hao watapita mtihani.
(g) _______ lile litaanguka. (h) _______ haya hayakufaa.
(i) _______ hilo halina magurudumu mazuri.
(j) _______ hao watakuuma.
D. Kuandika
Muhtasari/ufupisho
Ujuzi wa kuandika muhtasari au ufupisho ni muhimu sana. Ni muhimu kwa sababu unamwezesha
mwanafunzi kuiwasilisha habari fulani kwa kifupi na njia iliyokamilika. Muhtasari unahusisha
uwezo wa kutambua mambo muhimu na makuu katika kifungu fulani, na kuyawasilisha mambo
hayo kwa lugha yako na inayoonyesha mtiririko mzuri.
Hatua za kuandika muhtasari
Kwanza soma kifungu ulichopewa vizuri.
Jaribu kubainisha au kuelewa ni mambo gani muhimu.
Andika mambo hayo muhimu kama vidokezo fulani.
Acha mambo yasiyokuwa muhimu kama mifano, marudio, mafumbo, methali, n.k.
Chunguza hoja zako kwenye vidokezo ulivyoandika.
Usiongeze kitu ambacho hakipo katika kifungu au habari uliyopewa.
Sasa jaribu kuandika nakala kuunganisha vidokezi vyako.
Hakikisha kuwa unachoandika kinajibu swali uliloulizwa.
Ikiwa hukuambiwa idadi ya maneno katika jibu lako, andika muhtasari wa theluthi moja
ya kifungu ulichopewa.
Tumia viunganishi mbalimbali kama vile ingawa, licha ya, isitoshe, katika jibu lako.
Mfano wa kifungu cha muhtasari
Uongo ni kinyume cha ukweli. Katika dunia hii tuishio, ni watu wachache tu ambao si waongo.
Watu wanapotaka kudanganya au kuwapunja wengine hutumia uongo. Licha ya kuwa uongo
huweza kumsaidia mtu kujiokoa pengine, ni tabia mbaya na si kitu cha kupendelea wala kupendeza
maishani. Uongo hautumiwi na watu waovu na wajinga peke yao, bali hata watu wema huutumia.
Hata hivyo, ni muhimu kujua kuwa uongo ni bahari hatari sana katika dunia hii. Mwongo mmoja
huweza kupoteza na kuangamiza watu kadha wa kadha. Uongo wa wajinga hugunduliwa sana
kuliko ule wa wataalamu. Baadhi ya madhara hutokea duniani kutokana na uongo wa watu
wakubwa kuliko ule wa watu wadogo. Lakini lazima tukumbuke kuwa uongo ni kama giza,
hukimbia mbele ya cheche ndogo ya nuru ya kweli. “Uongo hukimbia kweli ikidhihiri” ni methali
ya Kiswahili ikumbushayo watu udhaifu wa uongo. Uovu mkubwa wa uongo ni kujidanganya
mwenyewe kuwa uongo wako hautagunduliwa, bila ya kujua njia ya mwongo ni fupi.
(Kimenukuliwa na kuhaririwa upya kutoka S. Robert, ‘Uongo Insha na Mashairi).
Zoezi
1. Ni sifa zipi zisizofaa za uongo? (maneno 20)
2. Je, kifungu hiki kinatufunza nini? (maneno 7)
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 231 12/11/2019 09:45
232
Chemshabongo
Tazama jedwali lifuatalo kisha ujibu swali lililo chini yalo.
O B N P J S N B X Y U X C L Z J U C A D I M I K A
S A A T Z W X D T M M N Y A M B U L I K O M N W U
J O B Q G J W H H T A G L Y P X A D P M E S G R W
R K V O M P P I G F W C P K R M J C U A T V E L W
S T Q A W W K B J X D X H Z D B S I A B I F W E V
O M N T A F T I P P S Q Q A G L Y O Z A V A A X D
A L A D T E Q T X E I H W A M S Y L A D H G N V T
F L D Z F X T I V A N D I K I A F N V I W I A I A
O C A J I G A M B A I B T L I Q R U X L A L K H S
L C W S H A G H A L A B A G H A L A K I H I I I H
J I I N A I A O S F M S E N A N G U N K U W J S B
A W U A O A D E O F J R D P B A R U A O S A I I I
P K I N T N H R Z O X I P N X O A G J R I Q J S H
E E P A U Z L V K Z K G V B F H K P C Y K G I H I
B O K U U K U T E N D A V X S E A V F E A J C I H
M I M Y V A V K A T I B A K P Y O Z C Q N X M M X
V F A S I H I S I M U L I Z I S U Q S R G U P N Y
Tafuta maneno yafuatayo kwenye jedwali.
KATIBA DHIBITI ACHANA MUUNDO KUTENDA VIHISISHI
MSENANGU TASHBIHI ADIMIKA WAHUSIKA ANDIKA
MNYAMBULIKO JIGAMBA FASIHI SIMULIZI SHAGHALABAGHALA MABADILIKO
WANAKIJIJI FAGILIWA BARUA VIKATAA
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 232 12/11/2019 09:45
233
A. Ufahamu
Kisa cha Edipode
Kisa cha mfalme Edipode ni maarufu sana nchini Uyunani tangu zamani. Raia wa Uyunani
wanaamini kuwa kila binadamu ana sehemu mbili za maisha yake; sehemu mbaya na sehemu
nzuri. Wanasema kuwa lazima kila mtu azionje sehemu zote mbili katika maisha yake na kwamba
haiwezekani kuepuka jambo hili. Nakumbuka zamani nyanya aliniambia kuwa hata sisi tuliamini
hivyo na ndiyo maana mtoto alipozaliwa alionjeshwa maji ya msubili na asali wakati huo huo.
Maji ya msubili yalinuiwa kumjuza kuwa maisha ya binadamu yana uchungu au shubiri fulani
na lazima aionje. Asali ya nyuki nayo ilimwahidi utamu uliopo pia katika maisha ya ulimwengu.
Tofauti iliyopo kati ya jamii yetu na ya Wayunani ni kuwa, wao waliamini kuwa miungu wao
ndio walioamua maisha yao yatafuata njia gani. Miungu hao ndio waliotabiri maisha ya Edipode
yatachukua njia gani hata kabla ya kuzaliwa kwake. Huu ndio mkondo unaoitwa na wataalam
ujaala, yaani imani katika majaaliwa.
Edipode alikuwa mtoto wa kifalme, babake alikuwa mfalme Laio na mamake malkia Jokasta.
Kabla ya kuzaliwa kwake, miungu walitabiri kuwa mtoto huyu ataishia kumwua babake na
kumwoa mamake mzazi. Utabiri huu uliwatia wazazi wake kihoro kikubwa na walikuwa tayari
kufanya lolote kuzuia usitekelezeke. Alipozaliwa tu walimchukua na kumwagiza mtumishi mmoja
wao aende akamuue mtoto huyo mjalaana. Hawakutaka kushuhudia kitendo cha kinyama cha
kuuliwa kwa mwana wao huyo. Yule mtumishi alimchukua yule mtoto na kuyoyomea naye huko
mbali milimani. Moyo wake uliona ugumu kumwua malaika yule, kwa hiyo aliifunga miguu yake
pamoja na kumwacha huko maporini.
Kwa bahati nzuri, mtumishi wa mfalme wa nchi jirani alimkuta yule mtoto huko milimani,
akamchukua na kumpelekea mfalme pamoja na malkia wake. Walimshukuru sana kwa kumpata
mtoto huyo ambaye walimlea na kumwenzi kwa kila tunu na raha kama mwana wao. Edipode
naye aliwafahamu hao kama wazazi wake.
Sura ya Ishirini na Nne
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 233 12/11/2019 09:45
234
Alipobaleghe na kuwa barobaro mwenye nguvu alianza kuzunguka huku na kule. Ni wakati
huu aliposikia maneno yaliyosemwa na miungu kumhusu. Utamwua babako mzazi na kumwoa
mamako. Yale maneno yalimwudhi sana na kumletea kero kubwa moyoni. Aliwapenda wazazi
wake na wala asingeweza kukiria kitendo kama hicho. Sasa afanye nini? Aliamua kutorokea
nchi za mbali.
Aliondoka kimya kimya kuelekea nchi iliyokuwa upande wa mashariki. Alipokuwa safarini,
alikutana na kundi la watu waliokuwa wakisari. Palikuwa na kigari kizuri kilichovutwa na farasi,
yaani riksho. Kwenye riksho hiyo palikuwa na mtu aliyevalia joho la kifalme. Kundi hili lilimzuia
Edipode njiani na alipojaribu kuongea na mkuu wao wakakosana. Kwa hasira kuu aliuchomoa
upanga wake na kumwua kiongozi huyo mara moja. Aliwaacha hapo na kuendelea na safari
yake. Edipode hakujua kuwa kiongozi huyo aliyemwua alikuwa babake mzazi, Mfalme Laio.
Baada ya safari ya muda alika kwenye nchi iliyokuwa imefunikwa na wingu jeusi la majanga.
Palikuwa na njaa kubwa na lukuki ya magonjwa yaliyokuwa yakiwasumbua raia wa nchi ile.
Edipode alipouliza chanzo cha matatizo yale, alielezwa kinagaubaga. Palikuwa na jinamizi
ambalo lilikuwa limewategea kitendawili kigumu. Jinamizi hilo lilisema kuwa dhiki na matatizo
yaliyokuwako yataendelea kuwako hadi atakapotokea mtu wa kukifumbua. Edipode aliongozana
na watu hadi kwenye lango kuu la kuingia nchini. Huko walilikuta jinamizi kubwa ajabu ambalo
lilikuwa limekingama njiani kama kisiki cha mti mkubwa ajabu.
Lile jinamizi lilimtegea Edipode kile kitendawili kilichowachachafya watu wengi ajabu, “Je,
ni kitu gani ambacho hutembea kwa miguu minne asubuhi, miwili adhuhuri na mitatu jioni?
Edipode hakukawia kujibu kwa kusema, “Binadamu! Anapozaliwa husota, hutembea kwa
miguu na mikono; anapokua huweza kusimama na kutembea kwa miguu miwili, na anapozeeka
hulazimika kuutumia mkongojo. Baada ya kukijibu kile kitendawili tu, lile jinamizi lilitoweka
ghaa bin vuu. Wimbi la furaha liliwasomba raia wote wa nchi hiyo. Walikiria jinsi ya kumtuza
na kumtunuku Edipode aliyewaokoa kutoka tanuri ya majanga yaliyotishia kuwachoma wote.
Waliamua kumtuza kwa kumpa mke wa mfalme wao aliyeondoka kwenda safarini kisha akauliwa
kuko huko. Edipode alipewa mke wa mfalme, Jokasta, ambaye kwa kweli alikuwa mamake mzazi.
Baada ya muda, majanga mengine yaliisibu nchi hiyo tena. Edipode alikuwa tayari kupambana
na yeyote aliyesana majanga hayo. Aliapa hata kumtafuta yeye mwenyewe na kupambana naye
kwa mikono yake iliyojaa nguvu na iliyoshiba siha nzuri. Lakini baada ya uchunguzi ilitambuliwa
kuwa matatizo hayo yalitokana naye Edipode. Kitendo cha kumwua babake na kumwoa mamake
ndicho kilichoisababisha hali hiyo mpya. Edipode alitahayari na kuona fedheha kubwa. Aliamua
kuyatoboa macho yake mwenyewe na kutorokea nchi nyingine alikoishi msituni ambako hakutaka
kuonekana tena.
Maelezo ya msamiati
msubili : mmea unaofanana na mkonge ambao hutoa maji ya rangi ya manjano
ambayo ni machungu sana.
yalinuiwa : yalikusudiwa.
kihoro : huzuni kubwa; simanzi.
usitekelezeke : usitimie; usitokee.
lukuki ya magonjwa : magonjwa mengi.
kilichowachachafya : kilichowashinda; kilichowasumbua; kilichowahangaisha.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 234 12/11/2019 09:45
235
Maswali
1. Raia wa Uyunani walikuwa na imani ipi kuhusu maisha ya binadamu?
2. Mwandishi wa taarifa hii anasema katika jamii yao mtoto alionjeshwa asali ya nyuki na
maji ya msubili. Hii ilikuwa na maana gani?
3. Mtumishi alimuua Edipode huko kichakani. Je, ni kweli? Toa maelezo ya jinsi mambo
yalivyokuwa.
4. Eleza namna Edipode alivyohisi baada ya miungu kumtabiria kuwa atamuua babake na
kumwoa mamake mzazi.
5. Eleza mambo yalivyokuwa huko njiani baada ya Edipode kuamua kutoroka.
6. Kwa nini Edipode alitunukiwa zawadi na wenyeji wa ile nchi iliyokuwa imekumbwa na
majanga? Je, alitunukiwa zawadi gani?
7. Kisa hiki kinaisha kwa huzuni. Ni kwa nini?
8. Ni kwa njia gani hadithi hii inatufunza kuhusu heshima kwa wazazi wetu?
9. Tumia maneno haya katika sentensi:
(i) walitabiri (ii) mjalaana (iii) kumwenzi
(iv) alipobaleghe (v) jinamizi
B. Kusikiliza na kuzungumza
Matamshi bora: Vitate - l/r
Soma maneno haya:
l r
lahanirahani
launi rauni
lea rea
lembaremba
Soma vitanza ndimi vifuatavyo kujizoeza matamshi sahihi ya sauti hizo.
(a) Mimi Mlaha mpenda raha nilikwenda Laha na kuhaha kutafuta raha lakini baada ya
kutafuta raha kila mtaa wa Laha nikaka hoteli ya Bwana Laha Mraha iitwayo ‘Raha Laha
ndipo nilipogundua kuwa huko Laha hakuna raha.
(b) Leah anayelea kwa raha za karaha alinirenga nikawa renge.
(ch) Lemba mwenye kilemba alijiremba urembo wenye ulimbo.
CH. Saru na matumizi ya lugha
(i) Kuakisha
Mstari (________)
Alama ya kuakisha kwa kupigia mstari hutumiwa ili kusisitizia au kupa umuhimu maandishi
fulani. Huweza kutumika ili kuashiria aina fulani za maneno kwenye sentensi. Kwa mfano:
maneno yaliyopigiwa mstari katika sentensi zifuatazo ni vivumishi.
(a) Mtoto yule anacheza.
(b) Nyuki hao watakuumiza.
(ch) Karatasi nyekundu si nzuri.
(d) Mbwa wakali waliwafukuza wezi.
(e) Maji moto huchoma.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 235 12/11/2019 09:45
236
Huweza pia kutumika kuonyesha vitabu, majarida au magazeti kwenye maandishi; kwa mfano:
(a) Gazeti la Daily Nation liko na nani?
(b) Jana niliona picha yangu kwenye gazeti la East African Standard.
(ch) Jarida la Parents linauzwa wapi?
(d) Nimenunua kitabu kiitwacho Ali Baba na Wezi Arobaini.
(e) Mimi hutumia kitabu cha Saru Fafanuzi ili kuelewa saru ya Kiswahili barabara.
(f) Mwalimu wetu alitwambia tununue kitabu kiitwacho Mwenda.
Vile vile alama hii hutumika kuashiria maneno magumu, istilahi maalumu na mambo mengine
mengi.
Kibainishi/ritifaa ( )
Alama hii hutumika katika mazingira mbalimbali ya kimaandishi kama yafuatayo:
1. Kuonyesha tarakimu ambayo haijaandikwa;
Kwa mfano: mwaka ’14 ’18
2. Kuandika kwa kifupi;
k.m. nshaenda (nimeshaenda)
nshaka (nimeshaka)
3. Katika mashairi ili kutosheleza mizani katika mshororo wa ubeti; huonyesha kuwa silabi
(mizani) fulani imedondoshwa. Kwa mfano:
Wasiwasi nondokeya, ondoka enenda zako
Ondoka andama ndiya, nondosheya uso wako
Ondoka! Wanisikiya? Ziwate jeuri zako
Jishughulishe na yako, yangu wayatakiani?
(Abdilatif Abdala, 1971: Sauti ya Dhiki)
4. Kutofautisha sauti /ng’/ na /ng/; kwa mfano:
ng’ombe ngome
ng’ang’ana kanga
ng’ara ngumu
(ii) Upatanisho wa kisaru: Vionyeshi
Tazama jedwali hili:
Ngeli Nomino Vionyeshi Matumizi
‘h-’ ‘-le ‘h-’
i
zi
mashua
mashua
hii
hizi
ile
zile
hiyo
hizo
Mashua hii itazama.
Mashua hizi zitazama.
i
i
mvua
mvua
hii
hii
ile
ile
hiyo
hiyo
Mvua hii itakwisha lini?
Mvua hii itakwisha lini?
u
zi
unywele
nywele
huu
hizi
ule
zile
huo
hizo
Unywele huu umekatika.
Nywele hizi zimekatika.
u
u
uchafu
uchafu
huu
huu
ule
ule
huo
huo
Uchafu huo utafagiliwa.
Uchafu huo utafagiliwa.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 236 12/11/2019 09:45
237
Ngeli Nomino Vionyeshi Matumizi
ku
ku
kuchagua
kuchagua
huku
huku
kule
kule
huko
huko
Kuchagua huku kunafaa.
Kuchagua huku kunafaa.
pa
ku
mu
mahali
mahali
mahali
hapa
huku
humu
pale
kule
mle
hapo
huko
humo
Mahali pale pana siafu.
Mahali kule kuna siafu.
Mahali mle mna siafu.
zi fedha hizi zile hizo hizo Fedha hizi ni chane.
li jua hili lile hilo ua hili ni kali.
vi vita hivi vile hivo Vita hivi havikomi.
1. Andika sentensi hizi kwa wingi.
(a) Nyumba hii ilijengwa juzi.
(b) Mahali hapa hapafai kamwe.
(ch) Barua hiyo ilika jana.
(d) Mvua hii itakwisha tu.
(e) Uzi ule unatakikana haraka.
(f) Kutembea huku ni kubaya.
(g) Mahali mle mna nyoka.
(h) Chai hii ni ya nani?
(i) Ufa huu utazibwa.
(j) Waraka ule unatoka wapi?
2. Chagua nomino mwafaka kukamilisha sentensi.
(a) ___________ hii inavuja. (Ndoo, Uzi)
(b) ___________ huku hakufai. (Kulima, Nyama)
(ch) ___________ hiyo ni ya uzito wa kilo ngapi? (Sukari, Mvua)
(d) ___________ hicho ni kizuri mno. (Mtoto, Kitabu)
(e) ___________ huu umetoka wapi? (Mali, Uchafu)
(f) ___________ hizo zinapendeza. (Nywele, Vioo)
3. Kamilisha jedwali lifuatalo kulingana na mfano uliopewa.
Ngeli Nomino Vionyeshi
‘h-’ ‘-le ‘h-’
pa
k.m.
ku
mu
mahali mahali
mahali
hapa
pale
hapo
u
zi
utepe
tepe
ki
vi
cheti
vyeti
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 237 12/11/2019 09:45
238
Ngeli Nomino Vionyeshi
a
wa
kereng’ende
kereng’ende
ku
ku
kuimba
kuimba
li
ya
nanasi
mananasi
i
zi
eropleni
eropleni
i
i
chai
chai
u
u
uchoyo
uchoyo
u
i
miembe
mwembe
ya
ya
maziwa
maziwa
u
ya
ugonjwa
magonjwa
D. Kuandika
Barua za magazetini
Hizi ni barua ambazo huandikiwa mhariri wa habari. Barua hizi huandikwa na wasomaji wa
magazeti. Huwa na madhumuni mbalimbali.
Kutoa pongezi kwa mhariri au kwa mtu aliyefanya kitendo fulani kizuri.
Kuchua uovu au mabaya fulani ili watu wayajue na labda kuyashughulikia ipasavyo.
Kutoa maoni kuhusu jambo au msimamo fulani.
Kutoa mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali au tatizo fulani.
Sifa za barua za magazetini
Huwa fupi kwa sababu ya nafasi iliyopo kwenye gazeti na pia ili isipoteze muda wa msomaji.
Huandikwa kwa njia wazi ili wasomaji waweze kuielewa na kuyajua maoni ya mwandishi.
Ni muhimu iwe na hoja nzito au sababu wazi ili iwe na nafasi nzuri ya kuchapishwa.
Ni barua rasmi yenye lugha sanifu na inayokubalika.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 238 12/11/2019 09:45
239
Mfano
Wanaochafua mazingira waadhibiwe
Mhariri,
Ni jambo la kukera na kusikitisha kuona uchafuzi wa mazingira unaoendelea kufanyika nchini
mwetu. Kwanza, miti iliyoko kwenye misitu yetu michache inaendelea kukatwa bila ya kuwazia
matokeo mabaya ya kitendo hicho. Kitendo kama hiki kina hatari ya kuiongeza kasi ya nchi hii
kuwa jangwa katika miaka ijayo. Isitoshe, uharibifu wa misitu una madhara makubwa kwa kuwa
misitu ni muhimu kwa kuivuta na kuileta mvua. Tatizo jingine linahusiana na watu wanaolima
katika chemchemi za maji na kwa njia hii kuyachafua maji yanayotegemewa na wakazi wengi
wa maeneo mbalimbali.
Uchafuzi mwingine wa mazingira unatokana na viwanda ambavyo vinaumwaga uchafu
kwenye mito inayopita karibu na viwanda vyao. Uchafu huu hauhatarishi wanyama wanaoishi
mtoni tu bali ni hatari kubwa kwa afya ya watu wanaoyatumia maji hayo.
Isitoshe, kuna uchafuzi unaotokana na watu wanaotupa takataka ovyo; bila ya kuzingatia
usa, licha ya kuwepo na sehemu za kutupa takataka. Hili ni tatizo linaloonekana hata kwenye
sehemu za burudani mijini ambapo watu hutupa vikopo vya soda na karatasi za kila aina ovyo
ovyo. Jambo muhimu ninalowasihi viongozi ni kuhakikisha kuwa zipo njia za kuwaadhibu
wanaohusika katika uchafuzi huu. Wananchi nao hawana budi kujielimisha na kujua kuwa
mazingira sa ni msingi mzuri wa afya zao na maisha yao na pia ya vizazi vyao vijavyo.
Kibao Msanifu
Maji Mazuri Mjini.
Zoezi
Andika barua kwa mhariri wa gazeti la Msemakweli ukilalamika kuhusu wizi unaoendelea
kutendeka katika sehemu unayoishi.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 239 12/11/2019 09:45
240
A. Ufahamu
Tatizo sugu la dawa za kulevya
Suala la watu, vijana na wazima, kutumia dawa za kulevya ni moja kati ya matatizo yanayowakalifu
akili na kuwasumbua watu wengi katika siku za karibuni. Zamani suala kama hili lilionekana
kama kisasili ambacho hakina ukweli wowote lakini siku hizi limekuwa halisi. Katika jamii
yetu hili limekuwa tatizo sugu ambalo linahitaji kushughulikiwa kwa kila njia. Hatuwezi kujitia
hamnazo tena kuhusiana na suala hili. Kwa nini? Kwa kuwa dawa za kulevya zimepenyeza kwenye
taasisi zetu za elimu kuanzia, shule za msingi, za upili, vyuo vya ufundi na vyuo vikuu. Isitoshe,
matumizi yake yamevuka na kuingia viwandani, sokoni na popote wanapotangamana watu wa
kila rika na ukoo almuradi matumizi yake yamesambaa kila mahali.
Dawa za kulevya zinaweza kugawika katika makundi mawili makuu: dawa hasi na dawa sugu.
Katika kundi la kwanza zinaingia dawa zozote ambazo hunywewa, hunuswa au hutumiwa kwa
nia ya kulevya au kumwingiza mtumiaji katika hali ya kujihisi amepanda. Dawa za aina hii huwa
na matokeo hasi kwenye mwili wa anayehusika na hususan akili yake. Baadhi ya dawa zinazoingia
katika kundi hili zinakubalika kijamii ingawa matokeo yake huwa mabaya sana kwenye mwili
wa mtumiaji. Inawezekana jamii ikakubali kuwepo kwake, pamoja na kutumiwa kwake, lakini
matumizi ya kipindi kirefu huwa na matokeo mabaya sana kwa watumiaji. Baadhi ya dawa hizi
ni bidhaa za tumbaku ambazo huwa na aina ya kemikali inayoitwa nikotini. Nyingine ni vileo
kama wiski, bia, divai, miraa au mairungi, gundi ya viatu na bidhaa zinazotokana na petroli.
Hebu sasa tuangalie zile zinazoitwa dawa sugu. Hizi ni dawa ambazo kimsingi zinamchangamsha
mtumiaji na kumfanya apandwe na nishai za ajabu. Dawa hizi hufanya hivi kwa kuzitekenya seli za
ubongo wa anayehusika. Katika kulifanya hili, dawa zenyewe huishia kuziua seli za ubongo huo.
Huu ndio msingi wa mtumiaji kuwa na ustahimilivu fulani wa dawa zenyewe. Ustahimilivu huu
ndio unaomfanya awe kama aliyetawaliwa na dawa hizo. Yaani mtumiaji anavutwa na dawa hizo
na hulazimika kuzitumia ili kuidumisha hali aliyo nayo. Mtumiaji huwa sana hana njia nyingine
ya kujizuia na huishia kuwa mtumwa wa dawa hizo. Baadhi ya dawa sugu ni bangi, afyuni,
heroini, mihadarati na kokeini. Baadhi ya wataalam wanajumlisha miraa katika kundi hili pia.
Ni kawaida kusikia madai kuwa mtu anayetumia dawa za kulevya huonekana kuwa na furaha
kuliko wenzake. Ili kuelewa chanzo cha msisimko na furaha hiyo ya ajabu, lazima tuzijue hatua
anazopitia mtumiaji dawa za kulevya. Kimsingi kuna hatua tatu kuu. Mara tu mtu anapozitumia
dawa za kulevya, dawa hizo huzichangamsha seli za ubongo kwa kiasi kikubwa. Kuchangamshwa
huku kwa seli kunauzuia mwili wa anayehusika kutopata hisia kutoka viungo vingine vya mwili
au musuli za mwili. Matokeo ya hali hii ni kumfanya mtu anayehusika kutenda mambo kupita
kawaida yake. Mathalan, ataonekana kuwa na furaha nyingi, atasoma kupita kawaida, anaweza
kucheza kwa kipindi kirefu na kadhalika. Hali hii inaweza kuitwa hali ya mpumbazo. Mpumbazo
huu unaweza kumdanganya anayehusika kuhisi kuwa ana uwezo usiokuwa wa kawaida. Lakini
hii ni hali ya muda tu ambayo hutangulia kuuliwa na kuharibiwa kwa seli za ubongo.
Mtumiaji anayeingia katika hatua ya pili. Katika hatua hii, mtumizi wa dawa za kulevya
anatoka kwenye ile hali ya mpumbazo. Hatua ya pili hutambulishwa na dalili zifuatazo: uchovu,
kulala kupita kiasi, kutokuwa na hamu ya kazi au mambo mengine, kupuuza masuala ya siha na
afya, usahaulifu, kukosa malengo au shabaha katika kazi yako, kupungukiwa na kumbukumbu,
Zoezi la Marudio III
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 240 12/11/2019 09:45
241
kujitenga na watu wengine na kuwa na hisia za chuki au uhasama na jamaa. Mtumiaji anapokia
hatua hii hutambulikana waziwazi na watu walio karibu naye, wawe jamaa au maraki. Mtumiaji
wa dawa za kulevya huweza tu kunusurika au kuokolewa katika hatua hii. Akipita hatua ya pili
huwa anaingia katika awamu mbaya sana.
Hatua ya tatu ya mtumiaji wa dawa za kulevya huitwa hatua ‘isiyo ya kawaida. Sifa za
kutambulisha mtumiaji aliyeko kwenye ngazi hii ni fadhaa kubwa, unyonge wa mwili, usumbufu
wa kimawazo na uvunjifu mkubwa. Mtumiaji aliyekia ngazi hii huonyesha sifa kadha milele.
Mathalani kujitenga kabisa na jamaa au watu walio karibu naye, kupaliwa kabisa na usingizi,
kuudhika haraka na kuwa na tabia ya kuonyesha uchukivu kwa vita au kupigana, kuchanganyikiwa
kunakotokana na kuharibiwa kwa seli za ubongo, wazimu au kuangukaanguka kama mgonjwa
wa kifafa. Katika ngazi hii, seli za ubongo zinazomsaidia mtu kufanya uamuzi mzuri huwa
zimeharibiwa na dawa zenyewe. Si ajabu basi kuwa mtumiaji anaonyesha tabia za kitoto na huishi
kama mtu aliyeko kwenye ndoto. Hatimaye ubongo unazongwa kabisa kutokana na madhara ya
seli na mtumiaji huweza kushikwa na magonjwa ya kiakili kama wendawazimu.
Mwisho wa mtumiaji wa dawa za kulevya aliyekia ngazi hii ni kufariki baada ya mwili wake
kushindwa kuhimili uzito wa dawa zenyewe. Wengine huishia kujinyonga au kufariki kutokana
na maradhi ya moyo.
Waswahili husema kuwa hadhari kabla ya athari. Njia ya pekee ya kuhakikisha tumejiepusha na
madhara haya ni kuzikwepa dawa za kulevya. Kumbuka uchangamfu ambao unasababishwa na
dawa ni wa kupumbaza na ni wa muda, lakini madhara yake ni ya kudumu. Pumbazo linalotokana
na dawa za kulevya ni la kujidanganya na kuukimbia ukweli wenyewe. Tukumbuke kuwa ni heri
kushika nasaha au mashauri kuliko kuishia kusema laiti ningalijua.
Maswali
1. Dawa za kulevya huweza kugawika katika makundi makuu mangapi?
2. Ni nini maana ya mtu kujihisi amepanda”?
3. Kulingana na kifungu hiki, ni zipi athari za dawa sugu?
4. Kwa mujibu wa kifungu ni ipi njia kuu ya kuyakwepa madhara ya dawa za kulevya?
5. Eleza maana ya nahau zifuatazo kama zilivyotumika katika kifungu hiki:
(a) yanayowakalifu akili (b) kujitia hamnazo
6. Tunga sentensi ukitumia maneno yafuatayo ili kuonyesha maana yake:
(i) fadhaa (b) mathalan (ch) awamu (d) kunusurika (e) tatizo sugu
B. Kusikiliza na kuzungumza
1. Taja tanzu kuu za fasihi simulizi.
2. Taja vipera vya tanzu hizo kuu za fasihi simulizi.
CH. Saru na matumizi ya lugha
1. Chagua nomino mwafaka kukamilisha sentensi zifuatazo.
K.m. _____________ yangu inavuja. (Ndoo, Kikombe) Ndoo yangu inavuja.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 241 12/11/2019 09:45
242
(a) ____________ yake imemwagika. (chai, uji)
(b) _________ kwake kulimwokoa. (kitabu, kukimbia)
(ch) _______________ pako panafaa. (nyuzi, mahali)
(d) __________ zangu zinapendeza. (nyumba, ng’ombe)
(e) _____________ kwako kutakuumiza. (kulala, tunda)
(f) _____________ kutakufaa. (kalamu, kusoma)
2. Weka alama ya kuakisha mahali pafaapo kwenye sentensi zifuatazo.
(a) Mama aliniambia Rehema nenda jikoni ukatupikie chai.
(b) Ni nani yule anampiga mwanangu Maria aliuliza.
(ch) Mimi sitaki kwenda kucheza nilimwambia raki yangu.
(d) Nilisikia mtu akisema Fungua Fungua kisha nikasikia mlio wa bunduki.
3. Badala ya nomino iliyopigiwa mstari, tumia nomino iliyowekwa kwenye vifungo.
K.m. Embe ambalo unakula lina viini vya maradhi. (chakula)
Chakula ambacho unakula kina viini vya maradhi.
(a) Maembe ambayo yameanguka yameliwa na mbuzi.(embe)
(b) Kitabu ambacho unasoma ni cha nani? (vitabu)
(ch) Viroboto ambao wanaruka wanaudhi. (kiroboto)
(d) Miti ambayo imeanguka imeleta hasara. (ukuta)
(e) Manukato ambayo umenunua yako wapi? (mkate)
4. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuandika vitenzi katika kauli ya kutendana na kutendesha.
Kauli ya kutenda Kauli ya kutendana Kauli ya kutendesha
k.m. piga
kata
kaa
kopa
pita
imba
zaa
pigana
pigisha
5. Andika sentensi zifuatazo kwa umoja.
K.m. Tembe ambazo nilimeza ni chungu.
Tembe ambayo nilimeza ni chungu.
(a) Ugali ambao tulikula ulikuwa mtamu.
(b) Nyumba ambazo zilijengwa ni nzuri mno.
(ch) Uchoyo ambao alionyesha ni wa hali ya juu.
(d) Kuta ambazo zilianguka ni hizi.
(e) Kusukumana ambako kunaendelea ni kubaya.
(f) Mahali ambako analala pana kunguni.
(g) Mvua ambayo itanyesha ni kubwa.
(h) Sahani ambazo unaosha ni za nani?
(i) Nyembe ambazo unatumia zina uchafu.
(j) Teknolojia ambayo inatumika ni ya hali ya juu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 242 12/11/2019 09:45
243
Kikundi nomino (KN) Kikundi tenzi (KT)
1.
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
k.m. Mtoto wake
Wanafunzi wawili
Wachuuzi wale
Panya huyu
Wazee
anakunywa maziwa.
atakuja kesho.
alilima shamba zima.
amefungwa gerezani.
watachinjwa wiki ijayo.
Kimeliwa na paka.
6. Chagua msemo mwafaka kukamilisha sentensi.
(a) Nilisikia mbwa wakibweka, kisha ______________ (ghaa bin vu, fofofo) mlango
ukagongwa kwa jiwe na watu watano kuingia wakiwa na silaha.
(b) Ni makosa sana _____________ (kushika doria, kutoa rushwa) kwa mtu yeyote.
(ch) Aliposhikwa na polisi akiiba, ______________ (alipora mali, alitiwa pingu) na
kupelekwa kutiwa korokoroni.
(d) Biashara yangu ilipo_________ (tifua vumbi, toa mleli) nilipiga hatua kubwa
kimaendeleo.
(e) Kwa ____________ wanadamu wamekuwa wakijaribu kuvumbua vitu
vitakavyowasaidia maishani (mikono mitupu, miaka na dahari).
7. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuonyesha kikundi nomino (KN) na kikundi tenzi (KT)
katika kila sentensi.
8. Tumia kimilikishi kilicho kwenye mabano kukamilisha sentensi.
K.m. Mtoto ____________ amekuja. (-ake) Mtoto wake amekuja.
(a) Mzazi ________ yuko wapi? (-ako)
(b) Maradhi ________ yamepona. (-ake)
(ch) Kisu ________ kinanolewa. (-ao)
(d) Yai ________ limevunjika. (-etu)
(e) Mwiko ________ uko wapi? (-enu)
(f) Vikombe ________ vinaoshwa. (-ao)
(g) Manukato ________ yananukia. (-etu)
(h) Limau ________ liko kwenye kabati. (-enu)
(i) Kusoma ________ kutatufaa. (-etu)
(j) Mahali ___________ palifagiliwa. (-ao)
9. Je, sentensi sahili ni sentensi ya aina gani?
10. Pambanua sentensi sahili zifuatazo ukitumia kielelezo cha mstari.
K.m. Watoto wale wanasoma barua. KN
(N + V) + KT (T + N)
(a) Kondoo huyu alinunuliwa jana.
(b) Ngamia wakubwa wameuzwa leo.
(ch) Wanafunzi wote walika mapema.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 243 12/11/2019 09:45
244
(d) Duka lile limefungwa.
(e) Watoto wenu wanacheza uwanjani.
11. Andika sentensi hizi kwa wingi.
K.m. Mkulima huyu anataka nini?
Wakulima hawa wanataka nini?
(a) Mwanafunzi yule amepita mtihani.
(b) Mti huu una matawi makubwa.
(ch) Maziwa yale yamenywewa na paka.
(d) Kizingiti hicho kitakuzuia.
(e) Tawi hili lilianguka jana.
(f) Ndoo ile ina maziwa mengi.
(g) Ukucha huu una uchafu mwingi.
(h) Meli hiyo itabeba nini?
(i) Mahali hapo pana wadudu wengi.
(j) Kutembea huku kunachosha.
D. Kusoma
Soma shairi lifuatalo halafu ujibu maswali yanayofuatia.
Michezo hujenga mwili
Nikianza simulizi, jambo langu la awali,
Ni shime kwa mazoezi, vijana kila mahali,
Ili tupate ujuzi, tujenge viwiliwili,
Michezo hujenga mwili, haraka kwa mazoezi.
Michezo kwa binadamu, ina faida kwa kweli,
Kwa aa ni muhimu, kuhifadhi yako hali,
Tena huwa mahashumu, na sifa kuka mbali,
Michezo hujenga mwili, haraka kwa mazoezi.
Wangapi tunawaona, mabingwa wa jambo hili,
Ambao wamekazana, kwa michezo mbalimbali,
Leo watajwa majina, kwa sifa na nyingi mali,
Michezo hujenga mwili, haraka kwa mazoezi.
Na hiyo michezo bora, kwetu iliyo sahali,
Ni ya mbio na mpira, ambayo twaikubali,
Hima na tufanye ghera, lije kombe na medali,
Michezo hujenga mwili, haraka kwa mazoezi.
Yatosha nilokusanya, msije kuniaili,
Sasa ni shime kufanya, timu zetu ziwe kali,
Ije sifa kwetu Kenya, haya tena mafahali,
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 244 12/11/2019 09:45
245
Michezo hujenga mwili, haraka kwa mazoezi.
Maswali
1. Taja vina vya kati na vya mwisho vya shairi hili.
2. Kwa nini mtunzi wa shairi anasema michezo ni mizuri? Eleza faida nne kuu.
3. Je, shairi hili lina ujumbe gani kwetu?
4. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa.
(a) mahashumu
(b) wamekazana
(ch) sahali
(d) tufanye ghera
(e) kuniaili
E. Kuandika
1. Andika insha inayoanza na kifungu hiki cha maneno:
Nilipozinduka miale ya jua la asubuhi ilikuwa imepenya kupitia dirisha la pekee chumbani.
Niligutuka kuwa alfajiri ilikuwa imewadia tayari. Nilishangaa kwa nini saa yangu haikulia
kama nilivyotarajia. Nilijua lazima nimechelewa. . .
2. Je, mafumbo ni nini? Toa mifano mitatu ya mafumbo unayoyafahamu.
Chemchemi SB1 rvsd FIN.indb 245 12/11/2019 09:45