
4
Licha ya jitihada za kikosi hicho cha askaripori
kuyawinda majitu hayo, jambo lililowashangaza wengi
ni kuwa kila kulipokucha, ng’ombe, mbuzi na kondoo
wao wengi walikuwa wameuliwa. Damu na mifupa
ya mifugo wao ilitapakaa kote kijijini! Kila asubuhi
wanakijiji waliamkia maombolezo. Maombolezo ya
kuwapoteza mifugo na kuwaachia hasara nyingi.
Majitu haya yalitumia mbinu gani? Yalijificha wapi?
Yaliua vipi mifugo yasije yakapatikana na kikosi kile
cha askaripori? Hayo yalikuwa baadhi ya maswali
waliyojiuliza Wanabintuke wasiweze kupata majibu!
Kwa kweli, majitu hayo yalikuwa yameota meno!
Bwana Bintu aliheshimika sana kule kijijini Bintuke.
Katika umri wake wa ujana aliwahi kuwa kamanda
wa vikosi vyote vya polisi katika taifa zima kikiwemo
kikosi cha kuilinda misitu na wanyamapori. Lakini sasa
alikuwa amestaafu. Alikuwa katika awamu yake ya
mwisho ya kujirambia chumvi yake ya kiinuamgongo.
Zama hizo akiwa barobaro, aliviongoza vikosi vyote
kuleta usalama kwenye mataifa yaliyokuwa na matatizo
ya usalama. Uongozini mwake, alifaulu pakubwa na
kusababishia mataifa mengi kupata usalama. Aliweza
kutuzwa zawadi nyingi za ushindi huo akiwa kamanda
mkuu. Hakusifika tu na wanakijiji bali pia alisifika katika
taifa zima. Kutokana na sifa hizo za Bwana Bintu, kikosi
kile cha askaripori kiliamua kumshirikisha kuwasaidia