
79
Fatuma alimfungulia mwanawe ambaye aliingia katika nyumba,
akijiburura polepole. Kama ilivyokuwa mara ya kwanza, alimbebea
zawadi kwa mgongo, ikifungwa kama kifurushi.
“Mama, chukua zawadi yako halafu naomba unipakulie chakula,
nina njaa,” Nuru aliomba.
Fatuma alimpakulia mwanawe wali akaujaza sahani nzima.
Alipozifungua zile zawadi, alishtuka sana. Mlikuwa na mkufu wa
dhahabu, herini, mafuta ya nywele, mafuta ya kujipaka mwili,
manukato, taji la dhahabu, bangili na viatu vya dhahabu.
“Mama, oga sasa halafu uvalie nguo niliyokuletea pamoja na
mapambo hayo,” Nuru alishauri.
Mama alimtii mwanawe. Usiku huo huo alioga kisha akaivalia ile
nguo. Nakuambia Fatuma alipojitazama kiooni, chozi la furaha
lilimtoka. Alikuwa msichana mrembo hata kushinda malkia wa
nchi ile.Alibaki kujitazama pale kiooni kwa muda mrefu.
“Mama, umekuwa maridadi jinsi nilivyopenda. Wazee wa kijiji
wakitambua niko hapa, watanirejesha sehemu nyingine mbaya
kuliko ile ya baridi. Usiogope.Watii mama kwa sababu hii itakuwa
ndiyo mara ya mwisho kwenda kunitupa. Mama, nafanya yote
haya kwa sababu najua ndoto yako. Ulizawidiwa na Mwenyezi
Mungu kunizaa mimi ili ndoto yako itimie kwa hivyo usiwe na
wasiwasi,” Nuru alimshangaza mama.
Siku iliyofuata, wanakijiji wote walikusanyika huku wakiomboleza.
Laana ilikuwa imerejea kijijini. Wazee walimchinja fahali na
kuitolea miungu dhabihu. Siku tatu baadaye, wazee wote
pamoja na Fatuma walifunga safari. Ilikuwa safari ndefu ya siku
nne. Walifika kwenye ukingo wa bahari. Walikuwa na kidau.
Walimweka Nuru ndani ya kidau kisha wakakiachilia kikaelea