Anita na Agneto
na
Hadithi Nyingine
Sophy Onura
Anita na Agneto na Hadithi Nyingine
Kimechapishwa na Queenex Publishers Limited
S.L.P. 56049-00200, Nairobi.
Rununu: 0715 808 200, 0727 794 498
Barua pepe: info@queenexpublishers.co.ke,
queenexbooks@gmail.com
Tovuti: www.queenexpublishers.co.ke
©QueenexPublishersLtd
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupigisha chapa,
kutafsiri au kukitoa kitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila idhini kwa
maandishi, ya Queenex Publishers Limited.
ISBN: 978-9966-140-15-9
Anita na Agneto
1
2
Huyu ni Anita na Agneto.
Wao ni wasichana.
Anita na Agneto wanapendana sana.
Wao wameketi na babu yao.
Babu yao anaitwa Mzee Busara.
Babu yao amefurahi sana.
Je, unampenda ndugu yako na dada yako?
3
Huyu ni bwana Neto.
Bwana Neto anakata nyasi.
Anatumia fyekeo kukata nyasi.
Bwana Neto ni baba yake Anita na Agneto.
Je, wewe hutunza mazingira?
4
Huyu ni Karo.
Karo ni mama yake Anita na Agneto.
Karo anapika ugali.
Akimaliza kupika, atawaita Anita na Agneto wale.
Karo anawapenda Anita na Agneto.
Je, wewe huwasaidia wazazi wako nyumbani?
5
Anita na Agneto wanasikiliza hadithi.
Babu anawaambia hadithi tamu.
Wanapenda hadithi za babu yao.
Je, unapenda kusikiliza hadithi?
6
Anita na Agneto wanaenda kwao sasa.
Wana furaha sana.
Wanamwambia babu asante.
Wanasema kwaheri.
Babu ana furaha pia.
Anasema, “Kwaheri ya kuonana wajukuu
wangu.
7
Anita na Agneto wameketi kwenye meza.
Baba yao na mama yao pia wameketi kwenye
meza.
Mama anawapakulia chakula kwenye sahani.
Wanakula kwa furaha.
Familia ya bwana Neto inaishi kwa amani.
Ni vizuri kuishi kwa amani.
Tunafaa tupendane.
8
Nitajua talanta yangu
9
Bi Chapakazi ni mwalimu wangu wa darasa.
Yeye ni mwalimu wa kike.
Ni mrembo kama malaika.
Yeye ni mwalimu safi.
Ni maridadi kama kipepeo.
Chapakazi anazingatia usafi siku zote.
10
Bi Chapakazi ni rafiki yangu sana.
Kama jina lake, anafanya kazi kwa bidii.
Anakuja darasani mapema.
Ana furaha wakati wote.
Huwa anatufundisha vizuri.
Huwa anasema kila mtu ana talanta yake.
Je, unampenda mwalimu wako?
11
Bi Chapakazi anataka tujue talanta zetu.
Talanta zetu ni kama michezo na kuimba.
Bi Chapakazi anajua talanta yake.
Talanta yake ni kuimba.
Bi Chapakazi anapenda kuimba.
Je, unajua talanta yako?
12
Hawa ni wanariadha.
Talanta yao ni kukimbia.
Wamepewa talanta zao na Mungu.
Talanta nyingine ni kama vile kuogelea, kuigiza,
kucheza kandanda na hata kucheza dansi.
Je, unatumia talanta yako vyema?
13
Huyu ni Hamisi Mogaka.
Mogaka ana talanta ya kucheza soka.
Mogaka hufunga magoli mengi.
Ninataka nijue talanta yangu.
Ninataka kuitumia vizuri.
Ninataka kuwa kama Hamisi Mogaka.
Je, unataka kuwa kama nani?
14
Mali ya nchi yetu
15
Wanafunzi wanaingia kwenye basi.
Basi la shule lina rangi ya njano.
Bi Chapakazi anawaongoza wanafunzi.
Wanafunzi wanaenda mahali fulani.
Wanafunzi wana furaha kweli.
16
Tunaenda safari leo.
Safari yetu inaitwa ziara.
Tunaenda kuona wanyama wengi.
Wanaishi katika mbuga ya wanyama.
Tunaenda mbali sana.
Shule yetu iko mbali na mbuga ya wanyama.
Tunaenda mbuga ya Nakuru.
17
Hili ni ziwa Nakuru.
Ziwa hili lina maji mengi sana.
Maji yakiwa mengi pamoja yanaitwa ziwa.
Tunashangaa sana kuona maji haya.
Mwalimu anasema nchi yetu ina maziwa
mengi.
Anasema kuwa maji kama haya ya ziwa ni
mali.
Ziwa ni mali ya nchi yetu ya Kenya.
18
Ziwa Nakuru lina ndege wenye miguu mirefu.
Ndege wenyewe wanapendeza sana.
Ndege hawa wanaitwa flamingo au heroe.
Ndege hao wana shingo ndefu.
19
Safari yetu imekamilika.
Tumeona wanyama wengi na ndege wazuri.
Tunarudi shuleni sasa.
Mwalimu anasema tuyatunze mali ya nchi.
Mali ya nchi ni kama wanyamapori, maziwa
na misitu.
Ninataka kutunza mali ya nchi vizuri.
Tusichafue maji na kuua wanyamapori.
Kwa nini tuwatunze wanyamapori na ndege?
20
Kazi ni kazi
21
Jina langu ni Adili Mpole.
Mimi ni mwanafunzi wa darasa la tatu.
Ninasoma katika shule ya msingi ya Juhudi.
Ninaenda shuleni.
Nina vitabu ndani ya mkoba wangu.
22
Hapa ni darasani.
Mwalimu anafundisha.
Unaona nini?
Shule yetu ina vifaa vya teknolojia.
Vifaa hivi ni kama tarakilishi.
Tunajifunza kutumia tarakilishi.
Je, umewahi kutumia tarakilishi?
23
Huyu ni mwalimu Netto.
Mwalimu Netto anapenda kufundisha.
Mimi napenda somo la sayansi.
Mimi ninataka kuwa daktari.
Daktari anatibu wagonjwa.
Je, wewe unataka kufanya kazi gani ukimaliza
kusoma?
24
Huyu ni mzee Nguva.
Mzee Nguva ni seremala.
Anatumia mbao katika kazi yake.
Anatengeneza viti, meza na vitanda.
Je, mzazi wako anafanya kazi gani?
25
Huyu ni mama Pendo.
Mama Pendo ni mkulima.
Mama Pendo anapalilia kabeji.
Kabeji za mama Pendo ni tamu sana.
Mimi napenda kabeji kwa ugali.
Je, wewe unapenda chakula gani?
26
Hapa ni jikoni.
Mimi namsaidia mama kuosha vyombo.
Ninapenda usafi.
Ninapenda kumsaidia mama.
Mama anasema kuwa ni vizuri kufanya kazi.
Kazi yoyote inahitaji bidii.
Bidii inaleta mafanikio.
Mama anafanya nini?
27
Nchi yetu
28
Hii ni bendera.
Bendera hii ni ya nchi yetu ya Kenya.
Bendera yetu inapendeza.
Je, unaona rangi gani?
Mwambie mwenzako.
29
Hii ni gwaride yetu.
Wanafunzi na walimu wamesimama wima.
Maskauti wanapandisha bendera juu ya mlingoti.
Wanatembea kama wanajeshi.
Leo ni siku ya Ijumaa.
Kila Ijumaa tunapandisha bendera shuleni
mwetu.
30
Angalia jinsi wanafunzi wamesimama.
Hakuna anayepiga kelele.
Bendera ikipandishwa tunasimama wima.
Tunaonyesha heshima kwa nchi yetu.
Tunaipenda nchi yetu.
Sisi ni wazalendo.
Tunaimba wimbo wa taifa.
Tunajivunia kuwa wakenya.
Je, wewe unajua kuimba wimbo wa taifa?
31
Imba wimbo wa taifa
Ee Mungu nguvu yetu
Ilete baraka kwetu
Haki iwe ngao na mlinzi
Na tukae na undugu
Amani na uhuru
Raha tupate na ustawi
Amkeni ndugu zetu
Tufanye sote bidii
Nasi tujitoe kwa nguvu
Nchi yetu ya Kenya
Tunayoipenda
Tuwe tayari kuilinda
Natujenge taifa letu
Ee, ndio wajibu wetu
Kenya istahili heshima
Tuungane mikono
Pamoja kazini
Kila siku tuwe na shukrani
32
Kamusi yangu
amani: hali ya utulivu bila vita
bendera: kitambaa chenye rangi au alama
inayowakilisha nchi
gwaride: sehemu wanakosimama wanafunzi
na penye mlingoti wa bendera ili
kuhutubiwa na walimu
flamingo:ndege mwenye miguu mirefu
myekundu, shingo ndefu na mwili
mweupe wenye wekundu kiasi,
hupatikana kwenye ziwa
kandanda: mchezo wa mpira wa miguu
mbuga: mahali ambapo wanyama wa mwitu
hutunzwa
mlingoti:kipande cha mti au chuma
kilichosimamishwa ardhini ili kushika
bendera
mwanariadha: mtu anayecheza michezo ya
riadha kama kukimbia au kuogelea
riadha: mchezo wa mazoezi kama kukimbia,
kuruka na kuogelea
simama wima: simama sawasawa bila kujipinda
talanta: uwezo wa kufanya jambo fulani
vizuri
tarakilishi: mashine ya elektroniki
33
teknolojia: ujuzi wa sayansi katika matumizi
ya vitu kama tarakilishi
wazalendo: watu wanaoipenda nchi yao
ziwa: sehemu yenye maji mengi
iliyozungukwa na nchi kavu
34
Maswali
1. Babu ya Anita na Agneto anaitwa nani?
2. Bwana Neto anafanya nini?
3. Mama ya Anita na Agneto anafanya nini?
4. Kwa nini Anita na Agneto wanapenda
hadithi za babu yao?
5. Bi. Chapakazi aliwaambiaje wanafunzi?
6. Talanta yako ni ipi?
7. Ziwa ni nini?
8. Kwa nini nchi yetu ni nzuri?
9. Seremala hufanya kazi ipi?
10. Je, ungependa kufanya kazi gani?
11. Je, utawezaje kutunza mali ya nchi?